27 Apr 2009

Neighbours of a woman who ended up in court for her noisy love-making were savouring peace and quiet today after she was locked up accused of breaking her anti-social behaviour order.

Caroline Cartwright, 48, was remanded in custody until May 5 charged with three breaches of her Asbo in just 10 days. The four-year order was imposed by magistrates in Sunderland on April 17 and prevented Cartwright 'making excessive noise' anywhere in England
...continue


Judges could be forced to bow to Sharia law in some divorce cases heard in Britain.

An EU plan calls for family courts across Europe to hear cases using the laws of whichever country the couple involved have close links to. That could mean a court in England handling a case within the French legal framework,or even applying the laws of Saudi Arabia to a husband and wife living in Britain...
continue

As many as one in five British couples sleep in separate beds. According to a recent survey, snoring, tossing and turning, and talking in your sleep were cited as the main irritants, with ever more stressful careers and lives that demand a good night's rest making us increasingly reluctant to put up with them. But does choosing to sleep apart sound the death knell of intimacy? ...continue

Facebook messages, texts and internet addresses will all be logged and stored under new laws proposed by the Home Secretary today.Jacqui Smith said phone and internet providers would be legally obliged to retain records of customers' calls and internet usage.

However, the proposed plans fell short of a widely-predicted centralised database containing email, phone and web data.The information, to be stored for a year at a cost of £2bn, would be available to police in the event of criminal investigations...continue

MOJA YA MAENEO KOROFI KATIKA BARABARA KUU WILAYANI KILOMBERO.UNGETEGEMEA VIONGOZI WA WILAYA HIYO WAELEKEZE NGUVU ZAO KWENYE KU-ADDRESS SHIDA ZA WANANCHI (KAMA HIYO YA BARABARA) BADALA YA KUTAKA KUUZA ARDHI YAO.HUU NI UNYAMA USIOKUBALIKA HATA CHEMBE.ANYWAY,2010 IS COMING.I HOPE UKATILI HUU WA VIONGOZI WABABAISHAJI UTAKUWA SABABU TOSHA YA KUWAPIGA CHINI KWENYE UCHAGUZI.

na Mwandishi Wetu, Kilombero

KIJIJI cha Namwawala, kilichopo Kata ya Idete, Tarafa ya Ifakara, Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, kiko hatarini kuuzwa kwa mwekezaji, huku viongozi wanaosimamia mpango huo wakidai ni agizo kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.

Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka katika kijiji hicho, zilidai kuwa baadhi ya viongozi wa wilaya na mkoa, wanasimamia uuzaji wa ekari zaidi ya 3,384, sawa na asilimia 95 ya ardhi ya kijiji chote, kwa ajili ya mwekezaji anayetarajia kuanzisha mashamba ya miwa na kiwanda cha sukari.

Hivi sasa, kijiji hicho kimeunda kamati kufuatilia mambo manne ya msingi ambayo ni kuthibitisha kauli ya viongozi wao kwamba Rais Kikwete ameamuakuchukua ardhi hiyo, na kama ardhi inayochukuliwa ni asilimia 95 ya eneo lote la
kijiji.

Mambo mengine ni, Mkurugenzi Mtendaji Kilombero kuanza kuthaminisha mali zao bila taarifa rasmi na kutaka wasomewe waraka unaoelekeza Rais Kikwete kutoa agizo la kuchukua ardhi na kumpa mwekezaji.

Kamati hiyo ambayo inadaiwa kuishi kwa kutishiwa na baadhi ya viongozi wilayani humo, inaundwa na Mwenyekiti Zuberi Kapindijega, Kenani Haule (Katibu), wakati wajumbe ni Johson Msuya na Godfrey Lwema.

Akizungumza na Tanzania Daima kutoka mjini Ifakara jana, Kapindijega, alisema baada ya viongozi wa wilaya na kata kupita kwa wananchi na kuwataka waanze kufanya tathimini ya mali zao na kujiandaa kuhama, walifikisha barua yao kwa Rais Kikwete jijini Dar es Salaam wakitaka ufafanuzi wa mpango huo.

“Januari 31 kwenye mkutano wa mapato na matumizi ya kijiji, iliibuka hoja ya wanakijiji kutaka kujua hatma ya ardhi yetu, ndipo mwenyekiti wa kijiji alitusomea waraka aliodai wa rais, ambao umetumika katika kuchukua asilimi 95 ya ardhi hiyo. Kutokana na mazingira na mfumo uliotumika kufikisha waraka huo wa rais kwetu, tunahisi kuna mchezo
mchafu.

“Kwa hofu hiyo na kwa kuwa kila tunaloliuliza jibu ni moja tu la rais kaamua kuchukua ardhi yake, ndiyo maana tumeamua kuja kuonana na wewe mwenyewe Mheshimiwa Rais,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo kwenda kwa rais iliyoandikwa Februari 13 na Tanzania Daima kupata nakala yake.

Hata hivyo, katika majibu ya rais kwa viongozi hao wa tume yalitolewa kwa barua iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, F. Mwaipaja, Februari 16, viongozi hao walitakiwa kuwasiliana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, na Mkuu wa Mkoa na kama hawataridhishwa, wanaweza kuonana na rais.

Kutokana na barua hiyo kutoka kwa rais, viongozi wa tume hiyo walibisha hodi katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero kwa barua waliyoiandika Februari 20 nakufuatiwa na nyingine ya Februari 27, ambazo pia Tanzania Daima nakala zake inazo.

Hata hivyo, ofisi hiyo ya mkuu wa wilaya, ilijibu barua hiyo kupitia kwa Katibu Tawala, E Mmbaga, akidai kuwa ameagizwa na DC Evarist Evarist Ndikilo awajulishe wajumbe hao wa tume kwamba amepokea barua hizo.

“Aidha mnafahamishwa kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itawasiliana na SUDECO, Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), Serikali ya Kijiji (Namwawala) pamoja na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W), wanafanya tathmini ya fidia. Mnaombwa mvute subira kwani matokeo ya mawasiliano hayo, mtajulishwa,” ilisema barua hiyo.

Baada ya majibu hayo, tume hiyo pia ilifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, na kuwasilisha barua yao Machi 6, mwaka huu kutaka kupata ufafanuzi wa kuuzwa kwa ardhi ya kijiji chao.

Ofisi ya mkoa kupitia kwa Kaimu Katibu Tawala, L. Msuya, iliahidi katika barua yenye kumb namba CD/148/06/87, kwamba italishughulikia suala hili kwa makini.

“Kumbukeni kwamba mmeshafikisha malalamiko yenu kwenye ofisi ya rais na sasa mmerudishwa kwa Mkuu wa Mkoa, kwa hiyo suala hili linatakiwa lishughulikiwe kwa umakini sana.
Mnatakiwa mvute subira wakati mkuu wa mkoa anafanya uchunguzi wa kina ili kupata ufumbuzi wa kudumu,” ilisema barua hiyo.

Hata hivyo, akizungumzia malalamiko ya tume hiyo, DC wa Kilombero, jana alikaririwa na moja ya vyombo vya habari vya kila siku kwamba wajumbe wa tume hiyo ni wachochezi na kutoa amri wakamatwe mara moja.

Uchunguzi wa Tanzania Daima umebaini kuwa, hali ya kijiji hicho si shwari kwani wananchi wanashindwa kuendelea kufanya shughuli za maendeleo kwa hofu ya kuhamishwa, huku baadhi ya viongozi wakitofautiana kuhusu mpango huo unaodaiwa kuendeshwa kiujanja ujanja kwa kutumia jina la rais.


THIS IS BECOMING PERSONAL!TATIZO LA WILAYA YETU (NA JIMBO LA KILOMBERO KWA UJUMLA) NI KAMA HATUNA MBUNGE.KUNA JAMAA ANAITWA LIGALAMA.I JUST CANT UNDERSTAND WHAT THIS GUY HAS BEEN DOING!BADALA YA VIONGOZI KUWEKEZA NGUVU ZAO KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO WAO WANAENDEKEZA USHKAJI NA WAWEKEZAJI....NA HAIHITAJI UTAFITI KUFAHAMU KUWA KICHOCHEO KIKUBWA HAPO NI RUSHWA NA UFISADI KWA UJUMLA.

26 Apr 2009


KUNA kila dalili kuwa taifa halielekei pazuri hasa baada ya siku za hivi karibuni kuibuka matukio kadhaa ambayo kwa kiasi kikubwa yameishtua jamii kiasi cha kuhoji taifa linakoelekea.

Matukio ya kiongozi wa nchi kudhalilishwa kwenye mtandao wa kompyuta, malumbano ya wabunge juu ya kuvuja kwa siri za serikali na kuanikwa kwa mishahara yao pamoja na hatua ya Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, kutaja majina ya watu anaowatuhumu kuwa mafisadi ‘papa’ hadharani.

Kutokea kwa matukio hayo katika kipindi hiki ambacho taifa linaelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika mwakani kumeelezwa ni mambo ambayo kwa kiasi kikubwa yanaweza kuliyumbisha taifa.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii wanayaona matukio hayo kama ni mapambano ya hatari yanayowahusisha baadhi ya wafanyabiashara na vigogo wa siasa ambao katika siku za hivi karibuni wamekuwa wakitumia njia mbalimbali kuhakikisha wanafanikisha mikakati ya kuongoza.

Tukio la Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, kuwataja baadhi ya wafanyabiashara na wanasiasa maarufu hapa nchini kuhusika na kashfa za ufisadi limezua mtafaruku miongoni mwa jamii ambapo baadhi ya watu wanaiona hatua hiyo ni mapambano ya hadharani baina ya pande hizo mbili.

Mapambano hayo ambayo katika siku za hivi karibuni yamefikia hatua mbaya kiasi cha kuanza kuhusisha uandishi wa habari usiozingatia maadili ya fani ya habari umeonekana kutumika kwa ajili ya kukashfu na kudhalilisha utu wa baadhi ya walengwa.

Vita ya pande hizo mbili vinaonekana kuanza kushika kasi na kuna habari kuwa baadhi ya wafanyabiashara waliotajwa na Mengi wamejipanga kujibu mashambulizi hayo kwa gharama zozote zile.

Wakati mapambano hayo yakionekana ni ya pande mbili wanasiasa, wafanyabiashara na wananchi mbalimbali wamejikuta ama wanaunga mkono upande mmoja au mwingine hali inayozidisha utete wa vita hivyo.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii wamebainisha kuwa hali hii ya sasa imekuja hasa baada ya ufisadi wa EPA, Meremeta, Richmond na kadhalika ambao ulisababisha baadhi ya viongozi akiwemo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowasa kujiuzulu.

Kujiuzulu kwa viongozi hao na kufikishwa mahakamani kwa baadhi ya watuhumiwa walioshiriki katika kashfa hizo na za matumizi mabaya ya madaraka kumechochea vita dhidi ya ufisadi huku baadhi ya wananchi wakitaka pia Rais wa mstaafu, Benjamini Mkapa, naye aondolewe kinga ili aweze kujibu tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka.

Hatua ya Mengi kujitokeza hadharani na kutaka majina ya watu anaowatuhumu kwa kashfa za ufisadi na baadhi ya wabunge kuwachachamalia watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi nako kumezidisha joto na hofu ya mapambano hayo.

Wakati mawazo ya watu yakiwa bado katika mzozo huo, limetokea tukio jingine la kusikitisha katika mtandao ambapo kiongozi wa nchi amejikuta akidhalilishwa kwa picha zisizofaa mbele ya jamii.

Tukio hilo kwa kiasi kikubwa linaonyesha ukosefu wa ustaarabu na maadili kwa baadhi ya watu ambao wameamua kutumia vibaya teknolojia ya kisasa hususan upashanaji habari kwa kutumia mtandao.

Jambo hilo kwa kiasi kikubwa limekuwa likihusishwa na mbinu za kuchafuliana majina hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi na kubainishwa kuwa kama hatua za haraka za kuwakamata wanaohusika na mitandao hiyo zisipochukuliwa kuna hatari ya viongozi wengi zaidi kudhalilishwa kupitia mambo mbalimbali.

Moja kati ya tukio la udhalilishaji wa viongozi ni hatua ya kijana mmoja kuamua kumpiga kofi Rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, katika sherehe za Maulid zilizofanyika kwenye Ukumbi wa Daimond Jubilee, Dar es salaam.

Sakata jingine ambalo limeonekana kuwagawa zaidi Watanzania na wanasiasa ni kauli ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma, kuwa kuanzia sasa wabunge na watendaji wote watakaovujisha siri za serikali watashughulikiwa ipasavyo.

Kauli hiyo ambayo ilionekana kumlenga Mbunge wa Karatu Dk. Wilbrod Slaa (CHADEMA) na baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wakitumia nyaraka mbalimbali zinazodaiwa kuwa za siri kuiumbua serikali sasa watakumbana na mikono ya sheria endapo watakutwa na nyaraka hizo.

Kauli hiyo imeonekana kupingwa na wananchi wengi kwa madai kuwa sasa serikali inataka kuwa ya kidikteta hasa kwa kuficha nyaraka za ufisadi uliofanywa au unaofanywa na viongozi waliopo na waliomaliza muda wao madarakani.

Baadhi ya wananchi wamekuwa wakiihusisha kauli hiyo kama ni njama za kuficha uovu ambao umekuwa ukipoteza fedha nyingi za Watanzania kupitia rasilimali mbalimbali.

Mshangao huo wa wananchi uliongezeka zaidi pale baadhi ya wabunge walimshutumu hadharani Dk. Slaa kwa kubainisha vipato wanavyovipata wabunge na kutaka fedha hizo zipunguzwe ili zitumike kwa maendeleo ya wananchi.

Baadhi ya wabunge walimtuhumu Dk. Slaa kwa kutaka kujitafutia umaarufu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu ujao jambo ambalo limepingwa vikali na wananchi wanaoonekana kukubaliana na ushauri wa Dk. Slaa.

Matukio haya kwa kiasi kikubwa kwa namna moja au nyingine yanaonyesha kuliweka taifa katika sehemu mbaya na iwapo kama hatua za kurekebisha baadhi ya mambo hazitachukuliwa kuna kila dalili za kutokea mpasuko mkubwa miongoni mwa jamii.

Naye Rahel Chizoza anaripoti kutoka Dodoma kuwa sakata la wizi wa nyaraka za serikali na kuwekwa hadharani kwa mishahara minono na marupurupu wanayopata wabunge kulikoibuliwa na Mbunge wa Karatu Dk. Wilbrod Slaa (CHADEMA), hivi karibuni limechukua sura mpya baada ya baadhi ya wabunge kuonyesha kumchukia mbunge huyo.

Hali hiyo imejitokeza jana kwenye semina ya maboresho ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma iliyoendeshwa kwa wabunge ambao baadhi yao walionyesha hali ya kumbeza mbunge huyo aliposimama kwa ajili ya kuchangia hoja.

Hali hiyo ilisababisha mwenyekiti wa semina hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Mpwapwa, George Lubeleje, kuingilia kati na kuwasihi wabunge kupunguza minong’ono.

“Hivi hizi nyaraka zinazodaiwa kuwa ni za siri, kwa nini zinawekwa kwenye makabati ya serikali, naomba Katibu Mkuu aniambie kama ni halali kwa nyaraka za wizi kuwepo katika kabati za serikali,” alihoji Dk. Slaa

CHANZO:Tanzania Daima

25 Apr 2009


DECI....DECI...DECI.NDIO GUMZO HUKO NYUMBANI.LAKINI KUNA MENGI YANAYOHITAJI TAFAKURI PANA KUHUSU SUALA HILO.TRULY YOURS NIMEJARIBU KUCHANGANUA SUALA HILO KWA UNDANI KIDOGO.ANGALIA HAPO JUU KULIA KWENYE SECTION YA AUDIO USIKIE UCHAMBUZI HUO.NIRUSHIE BARUA-PEPE TUENDELEZE MJADALA KWA MANUFAA YA TAIFA.NA KAMA NIMECHEMSHA,USISITE KUNIKOSOA.
KARIBUNI SANA!!!



MZALENDO MMOJA AMENITUMIA UJUMBE UFUATO KWENYE E-MAIL,NAMI NAOMBA KUUWASILISHA KAMA ULIVYO:


Kuna habari kwamba mmoja wa wafanyabiashara aliyetajwa na Mkurugenzi wa IPP Bwana Reginald Mengi amenunua hisa nyingi za umiliki wa kituo cha kurusha matangazo ya Television.

Mfanya biashara huyo inasemekana ni yule aliyetumia mtindo huohuo kununua hisa za kampuni iliyokuwa inatoa gazeti lilikuwa maarufu kabla ya mwaka 2005 na sasa si maarufu tena.

Mfanyabiashara huyo ambaye ana hisa kwenye kampuni moja ya simu za mikononi inasemekana ana mpango wa kutumia minara ya kampuni hiyo ya simu ili kusambaza matangazo ya kituo hicho nchi nzima kwa urahisi na bila gharama kubwa.

Kwa vile kampuni yake ndiyo yenye mtandao mkubwa hapa nchini basi itakuwa ni rahisi kwake kusikika nchi nzima kuzidi vyombo vyote vya habari.

Iwapo mpango huo utatekelezwa basi mfanyabiashara huyo atakuwa anaongoza kusikika eneo kubwa nchini.

Bwana Mengi ina ITV na Redio zake tabidi avute bidii ya kasi kwa sababu yeye hataweza kuwa na mtandao mkubwa kama hiyo TV.

Wenu mtafuta habari

24 Apr 2009


Boniface Meena na Mkinga Mkinga

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Reginald Mengi jana aliamua kujitoa muhanga alipotangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia ambao anadai kuwa ni mafisadi papa wanaoiba mabilioni ya fedha za wananchi na kutaka wachukuliwe hatua kwa madai kuwa wataiyumbisha na kuitingisha nchi.

Kati ya wafanyabiashara waliotajwa na Mengi, wawili wamefunguliwa mashtaka ya tuhuma za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), wengine wakiwa wameshatajwa kwenye kashfa mbalimbali, zikiwemo za zabuni ya utoaji umeme wa dharura ya Richmond Development na uuzwaji wa jengo la Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye anamiliki kampuni ya IPP yenye kampuni mbalimbali zikiwemo za habari na vinywaji, alitaja wafanyabiashara hao watano akisema kuwa ndio papa kwa ufisadi lakini akasema idadi ya mafisadi wanaofilisi nchi hawazidi 10.

"Wanaotuhumiwa kuwa mafisadi papa wanahusishwa na karibu kila kashfa kubwa hapa nchini zikiwepo kashfa za Richmond, EPA, Dowans, helikopta na magari ya jeshi, ndege ya rais, rada, NSSF, Bahati Nasibu ya Taifa, mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma na kadhalika," alidai Mengi katika mkutano wake na waandishi wa habari alioufanya kwenye ofisi yake jijini Dar es salaam.
>
Kati ya wafanyabiashara hao watano ambao Mengi alidai ni mapapa wa ufisadi, wamo Rostam Aziz, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel), ambao Mwananchi ilipata nafasi ya kuzungumza nao kuhusu tuhuma hizo za Mengi.

Hata hivyo, Mengi hakuwa tayari kutoa vielelezo kuthibitisha madai yake, lakini akasema iwapo watamshtaki mahakamani na wafanye hivyo kwa kuwa huko ndiko haki inakopatikana.

Mengi alirusha tuhuma nyingi kwa watu hao ambao alidai kuwa wamecharuka baada ya Rais Jakaya Kikwete kuamua kupambana nao na hivyo wameamua kupambana na yeyote anayemsaidia mkuu huyo wa nchi katika vita hiyo.

"Jitihada kubwa za Mhe. Rais za kuleta maendeleo na maisha bora kwa kila Mtanzania zinazoofishwa na wizi mkubwa wa rasilimali za taifa. Bado Watanzania wengi wanaandamwa na umaskini mkubwa; hawajui hata mlo mmoja kwa siku utatoka wapi," alidai Mengi ambaye pia alitoa taarifa ya maandishi aliyoisaini.

"Cha kusikitisha ni kuwa pale Mtanzania mwema mwenye uwezo anaposaidia jamii kuondokana na umasikini, mafisadi wanapiga kelele kuwa misaada ya aina hiyo ina agenda. Wanapinga kwa kuwa wanataka Watanzania wafe na njaa na matatizo mengine."

Mengi alikwenda mbali zaidi na kudai mafisadi anaowatuhumu wanaweza wakaunga mkono matatizo yanayotokana na Deci, taasisi inayoendesha mchezo wa kuchangisha fedha na kulipa maradufu na Watanzania kubakia "wakifukuzana na wachungaji bila ya kujiuliza ni kina nani hasa wanachochea vurugu".

Wakiongea na Mwananchi, watu hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi hawakutaka kujibu kwa kirefu na badala yake walimtuhumu mwenyekiti huyo mtendaji wa IPP kuwa ana wivu, fitina chuki na ambaye ameshindwa kuendesha nyumba na biashara zake, huku mwingine akieleza kuwa anatumia haki yake ya kidemokrasia ya kutoa maoni yake.

"Mengi... (si mstaarabu)," alisema Manji ambaye anamiliki kampuni ya Quality Group. " Biashara zake zimemshinda ndio maana anazungumza ovyo." Rostam Aziz, ambaye ni mbunge wa Igunga anayejishughulisha na biashara mbalimbali za miradi mikubwa ya ujenzi, uchimbaji na habari, alimuelezea Mengi kama mtu ambaye analingana kwa umri na baba yake mzazi na hivyo hawezi kubishana naye.

Lakini akasema: "Mengi amejaa chuki, wivu na fitina. Sina cha kumsaidia isipokuwa kumuombea Mungu ili amsaidie kwa kumpuuzia hayo maana ni adhabu kwa nafsi yake mwenyewe. Kwa malezi niliyopata, siwezi kubishana na mzee."

Jeetu Patel naye alisema haoni busara kujibizana na Mengi na kwamba alichofanya mwenyekiti huyo wa Chama cha Wafanyabiashara Wenye Viwanda (CTI) ni kutumia haki yake ya kidemokrasia ya uhuru wa kuongea.

“Hayo ni matatizo yake," alisema Patel, ambaye anakabiliwa na kesi ya tuhuma za wizi wa fedha za EPA. "Amewaita waandishi kuzungumza nao... sikumsikia lakini ninachoweza kusema ni kwamba anatumia uhuru wake wa kujieleza.>
"Binafsi sijui chochote kuhusu hizo tuhuma za Mengi dhidi yangu, ila anayo haki ya kusema chochote. Nina mambo mengi ya kufanya hivyo sioni kama itanisaidia kwenye biashara zangu za kila siku kuanza majibizano na Mengi."

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mengi alidai kuwa watu hao aliowataja si tu kwamba wanaiba rasilimali za Tanzania, bali pia wanaiba muda wa Watanzania.

"Badala ya kutumia muda katika shughuli za maendeleo, tunajikuta tukitumia muda mwingi kupambana nao na hawatingishiki," alidai Mengi. "Badala yake wanatumia fedha walizotuibia kuanzisha magazeti ya kujenga kiburi cha kutudharau, kututukana na kutunyanyasa. Inakuwa kesi ya mwizi kumkimbiza na kumpiga aliyeibiwa.

"Hata sasa hivi, mafisadi papa wanaendelea kutumia uwezo wao wa kiuchumi uliotokana na wizi wa rasilimali za nchi yetu kushawishi na kupata miradi mikubwa mikubwa kwa kutumia majina tofauti tofauti huku wakipuuza kabisa kelele za wananchi kuhusu ufisadi wao.

Alisema ni muhimu wananchi wakajiuliza hawa mafisadi wanapata wapi ujasiri wa majigambo, dharau na nguvu za kutukana na kunyanyasa watu.

Alisema mafisadi papa ni lazima wajue kwamba iwapo wapambanaji wa ufisadi watapata madhara kwa njia yoyote hapa nchini au nje ya nchi, wananchi wa Tanzania watawawajibisha.

"Ni lazima Watanzania wote tuone kwamba sasa tumefika mahali pa kusema imetosha," alidai Mengi.

CHANZO:Mwananchi

22 Apr 2009


Na Waandishi Wetu

VURUGU kubwa zimeibuka katika Makao Makuu ya taasisi ya Development of Entrepreneurship for Community Initiative (Deci), wanachama wake walipokuwa wakigombea kuingia ndani ya ofisi hizo kuorodhoresha majina yao kwa ajili ya kung’oa mbegu walizopanda.

Kati msongamano wa wanachama waliokuwa wakigombea kuingia ndani ya ofisi za taasisi hiyo jana; baadhi ya watu walianguka chini, kumi kati yao walipoteza fahamu na saba walinusurika kufa baada ya kutumbukia kwenye kisima cha maji kilichopo katika eneo hilo.

Mashuhuda wa tukio hilo waliliambia gazeti hili kuwa watu hao walianza kusukumana kwenye lango la kuingilia ndani ya ofisi hizo, muda mfupi baada ya kufunguliwa na kukaidi amri ya kufuata foleni iliyotolewa na muhudumu wa Deci.

Walisema baada ya wanachama hao kukaidi amri hiyo, walijazana kwenye mlango wa kuingilia ndani ya ofisi hizo na ndipo walinzi wa kampuni binafsi wanaolinda ofisi hizo walitumia nguvu kuwarudisha nyuma wanachama hao bila mafanikio.

“Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya walifunga mlango wa kuingilia na shughuli za taasisi hiyo kusimamishwa kwa muda,” alisema mmoja wa mashuhuda.

Alisema ofisi zilisitishwa kuanzia saa 3:00 hadi saa 4:05 zilipofunguliwa baada ya kuwasili kwa askari polisi kutoka Kituo cha Magomeni.

Polisi hao wakiwa na silaha waliwasili kwenye ofisi hizo na kuingia ndani kupitia katika mlango uliokuwa umezingirwa na umati wa watu, ili waweze kuwalazimisha kufuata foleni.

Hata hivyo, zoezi hilo lilizidi kuwa gumu bada ya watu hao kuendelea kusukumana mlangoni hapo licha ya polisi kuingia ndani ya ofisi hizo na wahudumu wa Deci kutangaza kuwa wanachama waliopanda mbegu zao Machi mosi hadi 10, mwaka huu kuwa ndio wanatakiwa kuingia kupata huduma.

Kutokana na vurugu kuongezeka, ofisi hizo zilifungwa tena saa 7:45 mchana na kuwataka wanachama waondoke hadi kesho saa 2:00 asubuhi.

Hata hivyo muhudumu aliyekuwa anatoa taarifa kwa wanachama hao aliwataka kutofuata ratiba iliyoandaliwa na taasisi hiyo awali ya kuwahudumia waliopanda mbegu zao Februari. Badala yake aliwataka waliopanda mbegu zao kuanzia Machi mosi hadi 5, mwaka huu ndio watatakiwa kwenda kujiorodhesha leo.

Mmoja wa wanachama waliotumbikia kwenye kisima, Getruda Moto aliliambia Mwananchi kuwa akiwa na wenzake, alishituka baada ya mbao alizokuwa amesimamia juu yake zikizama.

“Mimi nilikuwa nimesimama pembeni, lakini kuna watu walikuja na kukanyaga mbao iliyogusa kwenye mgomba, ndipo ikatengua mbao zilizoegeshwa kwenye kisima hiki na mimi pamoja na wenzangu kutumbukia,” alisema Moto.

Hata hivyo alisema mara baada ya kuokolewa alifarijiwa na wanachama wenzake, wakimtaka asiilaumu Deci, bali serikali ambayo ndiyo chanzo cha yote hayo.

“Usiilaumu Deci hii haikudhamiria kufanya haya bali ni serikali iliyoifunga na kusababisha yote haya” alisema mama mmoja ambaye jina lake halikupatikana.


Mchungaji wa Kanisa la Sharoom Gospel la Yombo Buza, Kamiliusi Macha ambaye ni mmoja wa wanachama wa Deci aliilalamikia serikali kwa kutoweka ulinzi wa kutosha katika eneo hilo linalokusanya umati mkubwa wa watu.

“Hapa walitakiwa kuwepo askari wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU), ndiyo wangeweza kuwalazimisha wanachi kupanga foleni na hali hii ya wanachama ya kujazana mlangoni isingekuwapo,” alisema Macha.

Akizungumzia kampuni hiyo alisema kwa sasa inakatisha tamaa kwani taarifa zake ni za kutatanisha. Ofisi hizo pia ziligubikwa na kila aina ya vituko baada ya vibaka kuibuka na kuwaibia watu simu za mkononi pamoja na risiti zao za Deci.

Mwanachama mmoja aliporwa risiti zote za Deci zenye thamani ya Sh 200,000 akiwa nje ya makao makuu ya ofisi hizo. Mwanachama huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini alisema aliporwa karatasi hizo alizokuwa amezishika mkononi na kuachiwa karatasi ya ratiba.

Alisema mara baada ya kuporwa stakabadhi hizo alikwenda kituo cha polisi cha Urafiki kutoa taarifa, lakini alipofika huko aliambiwa arudi katika ofisi za Deci ambako angepewa barua ya utambulisho.

Hata hivyo juhudi za kupata barua hiyo zilishindikana baada ya watendaji wa Deci kukataa kufungua mlango wa ofisi hizo kwa madai kuwa muda wa kufanya kazi ulikuwa umemalizika.

“Nifungulieni mimi nimeibiwa naomba mnisaidie, nimeshaenda polisi nimeambiwa nije huku mniandikie barua,” alilalamika bila mafanikio baada ya sauti kutoka ndani ya ofisi hizo ikidai muda wa kazi umeisha.

Mwenyekiti wa kamati ya dharura ya wanachama wa Deci, Mchungaji Isaack Kalenge alifika katika ofisi hizo na kuwatangazia wanachama juu ya mkutano wao utakofanyika Jumamosi wiki hii kuanzia saa 7:00 katika viwanja vya Jangwani na kuwataka wanachama wote kufika bila kukosa.

Kabla ya kufika katika ofisi hizo mkutano aliokuwa ameuitisha na waandishi wa habari Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo, ulivunjwa na maofisa wa maelezo kwa kushirikiana na maafisa usalama, baada ya mchungaji huyo kutoa kauli iliyodaiwa kumdhihaki Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Mkutano huo ulivunjwa baada ya mchungaji huyo kusema kuwa kauli ya Waziri Mkuu kuwa Deci ina Sh1.8 bilioni katika akaunti yake badala ya 54bilioni zilizotajwa na viongozi wa taasisi hiyo, ni ya kuropoka na kupotosha umma.

Kauli hiyo iliwaudhi maofisa wa maelezo hivyo kumtaka aache kuongea habari za viongozi wa taasisi hiyo, hata wa serikali badala yake kusoma maandishi aliyoyaandika katika karatasi yake.

“Wewe siyo kiongozi wa Deci hivyo unatakiwa kuzungumzia masuala yako binafsi kwa kuwa ni mwanachama wa taasisi hiyo, si kumdhihaki na kumtukana Waziri Mkuu,” alisikika kiongozi mmoja wa maelezo na kuamsha kelele kutoka kwa waandishi waliokuwepo katika mkutano huo.

Hata hivyo mchungaji huyo aliitaka serikali kupitia Wizara ya Fedha kuwajengea wananchi mazingira ya kupata fedha zao.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alimtaka mchungaji huyo kufuata utaratibu uliowekwa na jeshi hilo kabla ya kufanya mkutano wake Jumamosi ijayo kwa kuwa kufanya hivyo bila kibali ni kukiuka Sheria namba 322 ya Jeshi la Polisi iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2002.

Katika tawi la Deci lililopo maeneo ya Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaam umati mkubwa wa wanachama ulikusanyika huku ukiulalamikia utaratibu wa kujiandikisha majina na kuacha risiti mpaka siku ya kurudishiwa fedha zao.

Mwananchi lilishuhudia washiriki hao wakizozana na baadhi ya viongozi wa tawi hilo na kuwalazimu kubadili uamuzi huo kwa kubandika tangazo ambalo lilikuwa linaonyesha utaratibu wa malipo kwa waliopanda mbegu kuanzia Oktoba mwaka jana mpaka Aprili, mwaka huu.

“Hatutaki kabisa kuacha risiti hapa kwani ikifika siku ya malipo mtaturuka. Tunasema hatutaki, nyie tuambieni siku ya kuja kuchukua fedha zetu, tutakuja na risiti zetu,” walisema washiriki hao.

Wakati hayo yakiendelea Deci katika taasisi nyingine ya Malingumu Investment iliyopo maeneo ya Ukonga karibia na lilipo tawi la Deci wanachama wake walionekana wakiendelea kupanda kama kawaida.

Mwananchi lilifika eneo hilo saa tisa alasiri ilikuta wanachama wa taasisi hiyo wakigombania kuingia ndani, huku wakiwa wanazuiwa na walinzi wa kampuni binafsi waliokuwa wakilinda eneo hilo.

CHANZO: Mwananchi
Baadhi ya washiriki hao walikuwa na nia ya kung’oa mbegu zao kwa kuhofia taasisi hiyo kufungiwa kama ilivyofungiwa Deci.



KWA MFANO KATINA GAZETI LA SANI KUNA HABARI KWAMBA MWANANCHI MMOJA ALIYEPANDA MBEGU ZENYE THAMANI YA SHS MILIONI 20 "AMEPARALAIZI" (AMEPOOZA)UPANDE MMOJA WA MWILI WAKE BAADA YA HABARI KUWA HUENDA MBEGU YAKE HIYO IKAWA "IMEOZA ARDHINI".....KIBAYA ZAIDI NI KWAMBA MBEGU HIZO (SHS MILIONI 20) ZILIKUWA NI FEDHA ZA URITHI WA FAMILIA,NA "MPANDA MBEGU" HUYU ALITUMIA TU NAFASI YAKE KAMA MWEKA HAZINA WA FUNGU HILO AKIAMINI MBEGU ZINGEZAA FAIDA NA KISHA ANGEREJESHA KIWANGO HICHO......



Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.