1 May 2011



VATICAN CITY — Pope John Paul II moves a step closer to sainthood on Sunday when his successor beatifies him before an expected crowd of several hundred thousand people. Pilgrims from all over the world, many from the pope's native Poland, have flocked to Rome to witness the beatification mass and take part in the biggest event in the Italian capital since the late pope's funeral in 2005.

Groups carrying national flags and singing songs have gathered over the weekend where the ceremony will take place, in St Peter's Square, which is bedecked with posters and photos of the late pope.

Up to 200,000 people attended a prayer vigil on Saturday evening in the Circus Maximus, the huge oval once used by the ancient Romans for chariot races. Some Rome churches threw their doors open all night to give pilgrims a space to pray.

John Paul's successor Pope Benedict XVI will pronounce a Latin formula on Sunday declaring one of the most popular popes in history a "blessed" of the Church.

A place of honor is reserved for Sister Marie Simon-Pierre Normand, a French nun who suffered from Parkinson's disease but whose inexplicable cure has been attributed to John Paul's intercession with God to perform a miracle, thus permitting the beatification to go ahead.

The Vatican will have to attribute another miracle to John Paul's intercession after the beatification in order for him to be declared a saint.

Some 90 official delegations from around the world, including members of five European royal families and 16 heads of state, will attend the beatification.

They include Zimbabwean President Robert Mugabe, who has been widely criticized for human rights abuses in his country. Mugabe is banned from traveling to the European Union, but the Vatican – a sovereign state – is not a member of the bloc.

Coffin on display

Pope John Paul's coffin was exhumed on Friday from the crypts below St Peter's Basilica and will be placed in front of the main altar. After Sunday's beatification mass, it will remain there and the basilica will remain open until all visitors who want to view it have done so.

It will then be moved to a new crypt under an altar in a side chapel near Michelangelo's statue of the Pieta. The marble slab that covered his first burial place will be sent to Poland.

John Paul's beatification has set a new speed record for modern times, taking place six years and one month after his death on April 2, 2005.

While the overwhelming number of Catholics welcome it, a minority are opposed, with some saying it happened too fast.

Liberals in the church say John Paul was too harsh with theological dissenters who wanted to help the poor, particularly in Latin America. Some say John Paul should be held ultimately responsible for the sexual abuse scandals because they occurred or came to light when he was in charge.

Ultra-Conservatives say he was too open toward other religions and that he allowed the liturgy to be "infected" by local cultures, such as African dancing, on his trips abroad.

The pope is being beatified on the day the Church celebrates the movable Feast of Divine Mercy, which this year happens to fall on May 1, the most important feast in the communist world.

The coincidence is ironic, given that many believe the pope played a key role in the fall of communism in Eastern Europe. 

 SOURCE: GMA News

30 Apr 2011



Kuna wapuuzi wanajaribu kutuminisha usanii unaoitwa "kujivua magamba" kwa chama tawala CCM kilichozaa serikali iliyopo madarakani.Lakini hata tukiweka kando ukweli kwamba nyoka anayejivua magamba anakuwa hatari zaidi kuliko awali,porojo hizi za kuchefua za CCM ni miongoni tu mwa jitihada zake kuwapumbaza Watanzania kuhusu matatizo ya msingi yanayotishia uhai wa taifa letu.

Wakati akili za Watanzania zimeelekezwa Samunge "kwa Babu wa Loliondo" na "magamba" ya akina Lowassa,Chenge na Rostam,mafisadi wanaitumia vizuri nafasi hiyo kubaka uchumi wetu kwa kasi ya kimbunga.Hebu angalia habari zifuatazo ambazo ni mwendelezo tu wa mkakati wa kuiflisi Tanzania yetu.

CAG abaini ufisadi wa Sh50 bilioni serikalini

Saturday, 30 April 2011 10:00

Boniface Meena

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), amebaini ufisadi wa Sh50.6 bilioni serikalini ukiwamo wa malipo yanayotia shaka ya Sh15.7 bilioni katika kipindi cha mwaka wa fedha 2009/2010.

Katika ripoti yake ya ukaguzi iliyoishia Juni, 30, 2010, CAG amesema fedha nyingi zilitumika kufanya ununuzi bila kufuata taratibu.

Katika ripoti yake, amesema wizara, idara, wakala na sekretarieti za mikoa, zilitumia fedha katika kipindi cha mwaka 2009/2010 kufanya ununuzi ambao haukuwa kwenye mpango wa mwaka.

Alisema matumizi hayo ni kinyume cha kifungu cha 45 cha Sheria ya Ununuzi ya Umma ya mwaka 2004 kinachozitaka taasisi za ununuzi kuweka mpango wa mwaka kwa lengo la kuepuka ununuzi wa dharura, kupata thamani ya fedha, kupunguza gharama za matumizi na kufanya ununuzi sahihi kwa njia ya kandarasi.

"Ukaguzi umebainisha kwamba katika mwaka wa fedha 2009/2010, taasisi zilizoonyeshwa hapa chini zilifanya ununuzi yenye thamani ya Sh50.6 bila kufuata kifungu cha sheria," imeeleza sehemu ya ripoti hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kati ya fedha hizo, Sh650.7 milioni zilitumika katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, kununulia samani kwa maofisa wanaoishi katika nyumba binafsi

Wizara nyingine ni Nishati na Madini, Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Maliasili na Utalii, Habari, Vijana na Michezo na Tume ya kurekebisha Sheria.

"Ununuzi wa samani kwa maofisa hao ulikuwa si sawa kwa kuwa hawana stahili ya kununuliwa vitu hivyo na ni kinyume cha waraka wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma (Utumishi) Na. C/CA/134/213/01/G/69 wa Januari 30, 2006, unaohusu malipo ya posho ya nyumba na ununuzi wa samani kwa nyumba za Serikali kwa maofisa wenye stahili," imesema ripoti hiyo.

CAG ameeleza pia kuwa eneo jingine ambalo fedha hizo zimetumika vibaya ni matengenezo ya magari ya serikali na taasisi zake ambako Jumla ya Sh176.7 milioni zimeliwa.

Alisema wakati kanuni ya 5 ya Kanuni za Ununuzi wa Umma (mali, kazi, huduma zisizo za ushauri na uuzaji wa mali ya umma kwa zabuni) ya mwaka 2005, ikitaka wizara, idara, wakala na sekretarieti za mikoa kutengeneza magari yake Temesa (Wakala wa Ufundi na Umeme), au kupeleka katika karakana zilizoidhinishwa na wakala huyo, magari mengi yalikuwa yanatengenezwa kwenye karakana binafsi.

"Magari hayo yametengezwa kwenye karakana hizo bila kuwa na kibali kutoka Temesa kama sheria inavyotaka."

CAG amebaini pia kuwa serikali na taasisi zake imetumia Sh13.8 bilioni kulipia mali na vifaa ambavyo hata hivyo, havikupokewa au vilipokewa pungufu.

"Hii ni kinyume na kanuni ya 122 ya kanuni za Ununuzi ya Umma (mali, kazi, huduma zisizo za ushauri na uuzaji wa mali ya umma kwa zabuni) ya mwaka 2005," alisema.

Taarifa hiyo ilisema katika kipindi cha mwaka wa fedha 2009/2010, wizara, idara, sekretarieti za mikoa mitatu zilifanya malipo yenye shaka yanayofikia Sh15.7 bilioni.

Malipo hayo yalikosa viambatanisho ambavyo vingeonyesha taarifa za kina pasipo kuacha shaka yoyote kuhusiana na usahihi wa malipo hayo.

CHANZO: Mwananchi

Mamilioni yafujwa Mambo ya Nje

na Mwandishi wetu

WIZARA Ya Mambo ya Nje na Ushirikinao wa Kimataifa imegumbikwa na ufisadi mkubwa wa upotevu wa mamilioni ya dola katika ubalozi wake wa heshima nchini Israel na ubalozi wa Marekani.

Imebainika kuwa dola za Marekani milioni 615 zimeyeyuka katika ubalozi wake Israel na hivyo jana kuifanya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kumuweka kiti moto Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Hayo yalibainika jana katika kikao cha pamoja cha Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), kilichoketi chini ya mwenyekiti wake, John Cheyo, ambaye alihoji matumizi ya fedha hizo ambayo yalipingana na ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Cheyo, alisema mwaka 2008/2009 imeonekana katika ubalozi huo kupotea kwa kiasi hicho cha fedha hasa katika utoaji wa viza na kutotolewa risiti kwa wahusika.

“Hapa inaonyesha Balozi wa heshima Madam Rinit Hershkovity wa Israel alitumia fedha za serikali vibaya na kamati yetu inahitaji kupata maelezo ya kina inakuaje kiasi cha dola milioni 615 za Marekani kupotea katika mazingira ya kutatanisha.”

“Hii kamati si ya kuchezea hasa katika kudai matumizi ya fedha za walipa kodi wa nchi hii sasa tunahitaji majibu mazuri na hatua zilizochukuliwa juu ya mtu huyu aliyefanya ufisadi wa aina hii,” alisema Cheyo.

Akijibu maswali hayo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya nje na ushirikiano wa Kimataifa, John Haule, alisema serikali ilipogundua ubadhirifu huo ililazimika kuufunga ubalozi huo toka Februari 2, mwaka 2009 na kumtaka balozi huyo kurejesha fedha hizo.

Haule, alisema kwa kuwa yeye ni mgeni katika wizara hiyo amegundua kukabiliwa na changamoto ya kuweka mahesabu sawa ikiwemo kupambana na matumizi mabaya ya fedha za umma.

“Mwenyekiti mimi ni mgeni toka niripoti wizarani; nina siku 21, lakini hivi sasa tumefanikiwa kuufunga ubalozi wa heshima wa Israel; hata hivyo bado ninakiri kuwa nina kazi ya kurekebisha mifumo ya fedha na utendaji wa kazi,” alisema Haule.

Majibu hayo ya Katibu Mkuu Haule, yalimuinua Mbunge wa Kibiti, Abdul Marombwa (CCM), ambaye alitaka kufahamua matumizi ya kiasi cha cha dola za Marekani 7,600,000 zilizotolewa kwa ajili ya kununua jengo la ghorofa sita nchini Marekani kwa kiasi cha dola 10.4 milioni.

Alisema ripoti ya watalaamu ilionyesha kuwa badala ya kufanya kazi hiyo wizara iliagiza kutumika kiasi cha dola milioni 151.0 huku kukiwa hakuna haja ya kufanya hivyo.

“Ripoti hiyo ilibainisha kazi iliyofanyika sio ukarabati bali ni kukata vyumba… sasa kwa hili tunahitaji maelezo ya kina, na hatua zote hizo hakuna kibali kilichothibitisha matumizi ya fedha hizo wala uhalali wa matumizi hayo,” alisema Marombwa.

Hata hivyo hali hiyo ilimfanya katibu mkuu wa wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa kumwachia naibu katibu Mkuu wake kutoa maelezo ya kina kwa kamati hiyo ambaye alisema kuwa hivi sasa wanalazimika kuzifunga balozi nyingi za heshima kutokana kutokuwepo udhibiti.

Kwa mujibu wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), inaonyesha kuwa zaidi ya euro 144,202 hazijalipwa kwa mujibu wa jalada namba TZBR/A.20/11 la Agosti 26, 2009 na kuonyesha kuwa deni hilo bado halijalipwa hadi sasa.

Balozi ambazo zimekumbwa na upotevu wa fedha na kuthibitishwa na CAG ambazo hadi sasa hazijatoa maelezo ya kina kuhusu matumizi yake ni pamoja na Italia waliotakiwa kurejesha kiasi cha sh 6,060,519.00 ambapo wahusika walitakiwa kufanya hivyo.

Mbali na upotevu wa fedha hizo kati ya mwaka 2007/2008 ubalozi ulitakiwa kuwasilisha kibali cha ukaguzi na kufanya matuzi ya sh 517,741,802 zilizotumika kinyume cha sheria




Zaidi mtembelee katika Blogu yake inayopatikana HAPA



By The Associated Press 04/29/11 04:16 PM ET

LONDON -- Tina Lannin, a professional lip reader who was born deaf, caught the private whispers during the royal wedding that television microphones couldn't capture.

Lannin, who has worked for 7 years as a forensic lip reader for police forces and media outlets with O'Malley Communications, picked out comments from Prince William, his bride and Queen Elizabeth II in a partial transcript. Her assessment couldn't be verified.

___

10:20 a.m. – Prince William: "Looking forward to it." To Harry, "shall we go in then?

Prince Harry: "Sure, everyone has arrived."

William (to Bishop): "Make sure everything's alright. It's beautiful the way it is."

10:25 a.m. – William to lady in congregation: "You look very pretty, very pretty."

10:55 a.m. – Michael Middleton to Kate Middleton as they left hotel: "You okay?"

11:00 a.m. – Pippa Middleton to sister Kate: "You look amazing."

Michael Middleton to Kate Middleton as they entered Westminster Abbey: "You okay?"

Kate Middleton to her father: "Yeah."

11:05 a.m. – Kate to Bishop before walking down the aisle: "Yes I suppose so ... I expect I'll be worn out today. Thank you."

Harry to William: "Right, here she is now."

William to Middleton at the altar: "You look lovely ...(unclear)... You look beautiful."

William joking to Michael Middleton: "We're supposed to have just a small family affair."

12:00 a.m. – Queen Elizabeth II to Prince Philip: "It was excellent."

Prince Philip: "Yes?"

12:15 a.m. – William to Kate Middleton: "Alright?"

Kate Middleton: "Yes."

William: "Wish I was out."

Kate Middleton: "I'm beginning to find (unclear)."

William: "Yeah, alright." Hands bouquet to Kate after they climb aboard their carriage, "here you are."

Kate Middleton: "Thank you."

Kate Middleton: "Now, are you happy?"

William: "Yes ... (unclear conversation) ... wave to everybody."

Outside abbey – queen: "I wanted them to take the smaller carriage."

Camilla, Duchess of Cornwall: "It all went very well."

Queen: "Very well."

In wedding carriage – William: "I don't think you should bow quite yet. I think you should just bow your head, okay?"

Kate Middleton: "Okay."

William: "I hope I remember ... It's mad, it's mad! Oh my goodness it ... really loudly here (unclear) these people are clapping."

Kate Middleton: "Did they?"

William: "I think so. I went out here the first (unclear)."

In separate carriage – Prince Charles: "Yeah it looked nice."

Camilla: "Yes, but you have to know how to do it."

In wedding carriage – Kate Middleton to William: "You look happy."

1:30 p.m – On Buckingham Palace balcony, Kate Middleton: "Oh wow."

William: "Alright? You'll be okay?"

Kate Middleton: "Oh I'm fine, thank you."

William: "Yeah! Yeah! There's a lot of people down here." To pageboys, "I know but look up there as well." To his bride: "Okay? Look at me, let's kiss, okay."

William, shouting balcony: "Harry! Your go!"

Kate Middleton: "What's next?"

William: "They want more time I think."

William shouting across balcony, possibly to Camilla: "You could have brought up (unclear) as well."

Camilla: "Oh, very heavy."

William: "Just do a bit of everything. Do you like the balloons (unclear) they go up in the air."

Kate Middleton: "Look at these people."

William: "I want to see the plane, I think I'm (unclear)."

William to Harry: "Okay."

William to pageboys: "...to stop them coming in here, to stop them coming in this side, I mean it's hard."

William to Kate Middleton: "One more." The couple kiss for a second time. "That's it, come on!"

SOURCE: Huffington Post

29 Apr 2011



Baada ya miezi,wiki na masaa,hatimaye ile siku ya kihistoria imewadia.Leo,Ijumaa ya tarehe 29 April 2011,mjukuu wa Malkia Elizabeth wa Pili,Prince William,anafunga ndoa na mchumba wake Kate Middleton,jijini London.Inatarajiwa zaidi ya watu bilioni mbili duniani kote watakuwa wakifuatilia harusi hiyo kwenye runinga zao.

Kwa bahati nzuri,dada yetu Miss Jestina,anatarajia kufuatilia tukio hilo la kihistoria kwa karibu zaidi,na kila kitu kikienda kama kilivyopangwa basi atatuletea up-to-the-minute updates kuhusu tukio hilo la aina yake.Pamoja na mengineyo,anatarajiwa kufanya mahojiano na watu mbalimbali watakaohudhuria shughuli hiyo.

Wakati tunawatakia Prince William na mkewe mtarajiwa Kate ndoa njema na ya amani basi usikose kufuatilia shughuli hiyo ya kihistoria katika blogu ya dada yetu Miss Jestina,live and direct from London hapa Uingereza.

Bonyeza  picha ifuatayo kutembelea blogu ya Miss Jestina





Stay tuned

28 Apr 2011


As Donald Trump tries to leverage his brand with a reality-show campaign for president, surging to the top of the 2012 GOP polls, the past is coming back to bite him. The media establishment has been treating him more as colorful sideshow than serious candidate. But now that it seems The Donald might actually run, it’s time to take a closer look at the darker corners of his empire.

Take John Robbins. When the retired Army officer heard Trump, in a music-filled tent, talk of putting up the tallest building in Tampa, Fla., he wanted in—“because of the Trump name.” But Robbins lost half his $150,000 down payment when the condo project went bankrupt and was “floored” to learn that Trump had merely licensed his gold-plated moniker: “I just don’t see Trump fitting the role of commander in chief. Somebody has to stand up to Mr. Trump.”

Hamed Hoshyarsar invested $54,000 in a condo at the Trump Ocean Resort Baja for one reason: he was a fan of The Apprentice. He lost every dime when the project was never built. “I want to throw up every time I see him,” says the Los Angeles accountant. “I see all these people talking about him being president, and I would never vote for that guy.”

Trump, who exudes a blustery charm, doesn’t miss a beat. “What about the 50 deals that worked out great—are you going to cover that too?” he asks me. Let the record show he has built some fabulous properties—but has also filed for corporate bankruptcy four times, most recently with his casino unit. “I do play with the bankruptcy laws—they’re very good for me” as a way of cutting debt, Trump says.

He says he’s not responsible in lawsuits over the two failed condo projects because his partners were the actual builders—and, his attorney says, such confidential licensing agreements are standard. Besides, says Trump, the buyers are “lucky” because they would have lost more money in a tanking market had the projects been built.

Another venture, Trump University, had to change its name after New York authorities ruled it wasn’t properly licensed; the school is also under scrutiny in Texas, where officials are examining possibly deceptive practices. Tarla Makaeff spent $35,000 to “Learn from the Master,” as a brochure put it, but the marketer says she didn’t get much beyond two “mentors” who were barely available after showing her some properties needing rehab. “I’m just disgusted by their greed,” says Makaeff, who is suing the school.

But Trump, who is countersuing, has a tape of Makaeff calling two staffers “awesome.” “This is really bullshit stuff,” he says, citing customer surveys that rate the school highly.

Trump sells himself as a head-banging businessman who can shake up a dysfunctional Beltway culture. But as pundits belatedly put him under the microscope, they’ll find him all over the political map. While Mitt Romney is typecast as a flip-flopper, Trump declared in 2000 that “we must have universal health care”; now he says Obamacare is unconstitutional. He once pronounced himself “strongly pro-choice” but recently discovered that, guess what, he’s pro-life. Obama was “amazing” and “phenomenal,” Trump wrote in 2009; now, not so much. And while Newt Gingrich is branded an adulterer, Trump conducted a tabloid-frenzy affair with Marla Maples, the second of his three wives.

For now, the press has pushed back hardest on Trump’s strange decision to peddle the birther nonsense. But he knows his customers: polls show roughly half of Republicans don’t believe Obama is a citizen.

Trump is suddenly inescapable, all over the networks, which love Trump because he’s good for ratings and the field is dull. Remember Sarah Palin? Her spokeswoman chided news outlets on Twitter for largely ignoring her last speech.

Trump may be giving his rivals cover by dominating the stage, but if reporters keep turning over rocks, the master showman might be glad he hung onto his day job. 

SOURCE: Newsweek



Kujali "vipaji" vyetu,kutojua vipaumbele vyetu au ufisadi wa kiakili?

Tukiamini takwimu kutoka huko Loliondo kuwa wastani wa wagonjwa wanaofika sehemu hiyo matibabu ni 2000 kwa siku,kwa wiki ni watu 14,000,kwa mwezi ni (wastani) 42000-au tukuze makadirio na kufanya watu 50,000 kwa mwezi,na tunaambiwa "Babu" alianza matibabu kitambo kidogo kabla habari hazijashika moto kwenye mwezi Februari,basi kuna uwezekano takriban watu milioni moja wameshapatiwa tiba na mtumishi huyo wa Mungu. (habari zinasema alianza matibabu tangu mwaka 2009,lakini kwa minajili ya kuamsha tafakuri tufanye alianza mwezi Januari mwaka jana.


Swali moja gumu ambalo nashindwa kabisa kupata jibu lake ni USHUHUDA KUTOKA KWA WALIOPONA.Hivi kweli kati ya watu milioni moja,au kwa kumtendea haki tuseme watu nusu milioni,hakuna hata 100 kati yao wanaoweza kutangaza hadharani kuwa walikuwa na ukimwi kisha wakapona baada ya kupewa kikombe?Vyombo vyetu vya habari vimekuwa bize zaidi kuripoti matukio badala ya kuchunguza ufanisi wa tiba hiyo ya kikombe.


Anyway,hebu soma habari ifuatayo kuhusu namna "Babu" anavyotukuzwa kama VIP flani.Msafara kwenda kwenye msiba wa mwanae ukiongozwa na polisi na maafisa usalama,stahili zinazotolewa kwa viongozi wa juu wa kitaifa kama vile Rais,Makamu wa Rais na Waziri Mkuu.




Babu aenda msibani chini ya ulinzi

MCHUNGAJI Ambilikile Mwasapila anayetoa tiba ya magonjwa sugu huko Samunge Loliondo, juzi jioni aliondoka hapa kwenda Babati, Manyara kuhudhuria mazishi ya mtoto wake huku safari yake hiyo ikiratibiwa na Serikali na akipewa ulinzi mkali wa maofisa usalama na polisi.

Aliondoka Samunge saa 12:20 jioni na gari la Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro akiwa na maofisa hao wa usalama, polisi na wasaidizi wake.Kabla ya kuondoka Samunge, watu mbalimbali walikuwa wamejitolea kumpatia usafiri mchungaji huyo lakini walizuiwa kutokana na sababu za kiusalama.

"Tulikaa kama kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya, tukaona ni busara tuchukue jukumu la kumsafirisha Mchungaji hasa kutokana na sababu za kiusalama," alisema ofisa mmoja mwandamizi wa serikali wilayani hapa.Alisema mchungaji huyo atalindwa akiwa msibani na atakaporejea Samunge.

CHANZO: Mwananchi

TAFAKARI


Niliposoma stori hii almanusura abiria wenzangu kwenye basi wadhani nimepandwa na uchizi kwa kicheko.Yaani mgodi kugundulika shuleni,kisha walimu na wanafunzi kuachana na elimu na kuchangamkia kusaka utajiri kwa kuchimba madini...hahahaha,Lol! (Picha ya juu haihusiani na habari hii bali taswira tu ya wanafunzi wa shule ya msingi).



CHANZO: Tanzania Daima.

What about kujiburudisha na video hii ya Kanye West "Diamond Are Forever"?

Mgodi wa dhahabu waibuka shuleni
• Walimu, wanafunzi waacha masomo, wachimba madini

na Makunga Peter, Bukombe

MGODI mpya wa machimbo madogomadogo ya dhahabu umeibuka katika Shule ya Msingi Nganzo, wilayani Bukombe, mkoani Shinyanga na kufanya viongozi wa wilaya kwa kushirikiana na mwalimu mkuu wa shule hiyo kuufanya kuwa mradi wao wa kujiingizia fedha.

Machimbo hayo yaliyoibuka takriban miezi miwili iliyopita yamesababisha shughuli na masomo katika shule hiyo kusuasua kutokana na walimu na wanafunzi kujiingiza katika shughuli za uchimbaji huku wakisahau kuzingatia masomo hali ambayo imesababisha utoro mkubwa wa wanafunzi.

Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho yalipo machimbo hayo, Boniphace Mashebela, alisema kuwa machimbo hayo madogo kwa sasa yanamilikiwa na kamati ya shule na kijiji lakini yanaendeshwa kwa ridhaa ya Ofisa Elimu wa Shule za Msingi, Fides Munyogwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, Kuruletera Majige, kwa kigezo kuwa machimbo hayo yapo katika eneo la shule.

Mmoja wa wachimbaji wadogo wanaoendesha shughuli za uchimbaji katika eneo hilo, Masamaki Kambale, alisema wao wapo hapo kisheria na si wavamizi kwani wao hufika na kuripoti ofisini kwa mwalimu mkuu pamoja na mtendaji wa kijiji na wao hugawiwa viwanja kabla ya kuzamisha maduwara yao.

Masamaki alisema kuwa kila duara linasajiliwa kwa sh 40,000, ambapo fedha hizo hupewa mwalimu mkuu na mtendaji wa kijiji na pindi duara linapofikia kuanza uzalishaji kila utoapo mifuko 10 ya mawe kati ya hiyo miwili ni mali ya viongozi hao wa wilaya hiyo.

Alisema kuwa kwa upande wa kamati ya shule na mtendaiji wao hutoza ushuru wa sh 1,000.

Kwa upande wake Ofisa Madini wa Wilaya ya Kahama na Bukombe, Medard Msengi, alipotakiwa kutoa ufafanuzi juu ya shutuma hizo alisema mgodi huo mpaka sasa ofisi yake haiutambui na kuomba kuongozana na waandishi wa habari hadi katika eneo hilo kujionea.

Ofisa huyo alipofika alijionea kuwa machimbo hayo yanaendeshwa kinyume cha sheria, kwani kipimo kutoka shimo hadi shimo kinatakiwa kiwe futi 10 kwa 10 lakini hayo yapo futi mbili hadi tatu, hali ambayo inaweza kusababisha maafa ya watu kufunikwa na kifusi wakati wowote wa uchimbaji.

Aidha, alitoa ushauri kuwa ni bora machimbo hayo yakafungwa kwa kuwa yapo katika eneo la shule, hali ambayo inachangia wanafunzi kutosoma vizuri na walimu kukimbilia kufanya biashara hiyo ya uchimbaji, hali ambayo itadhoofisha maendeleo ya elimu katika shule hiyo kwani hayana uataratibu wowote.

Alisema katika eneo hilo hakuna vyoo, hakuna mtaalamu anayetambulika katika ofisi yake ambaye anashughulikia madini katika eneo hilo maarufu kama waangalizi wa madini ili kufanya hali ya usimamizi katika eneo hilo kuwa rahisi na kudhibiti wanafunzi na walimu kufanya kazi hiyo.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe alipoulizwa kwa njia ya simu, alisema kuwa kweli machimbo hayo yapo katika eneo la shule na kuongeza kuwa tayari ameshatoa taarifa kwa mkuu wa wilaya ya maandishi, ila alikanusha kuwa yeye hahusiki katika kuchukua mifuko katika eneo hilo na kuiuza kama inavyosadikiwa

27 Apr 2011


Hatimaye Rais Barack Obama wa Marekani ameamua kuweka hadharani cheti chake cha kuzaliwa baada ya kuandamwa muda mrefu na wapinzani wake wanaomtuhumu kuwa si mzaliwa wa nchi hiyo.

Kasi ya mashambulizi dhidi ya Obama ilishika moto baada ya mfanyabiashara tajiri anayetarajiwa kuwania nafasi ya Urais wa nchi hiyo kwenye uchaguzi mkuu hapo mwakani,Donald Trump,kuungana na kundi la wahafidhina wanaodadisi u-Marekani wa Obama.Kundi hilo linalojulikana kama Birthers,limekuwa likipiga kelele kwa nguvu kuwa Obama ni Mkenya na si Mmarekani,madai ambayo Rais huyo aliyapuuza kwa muda mrefu lakini hatimaye amaeamua kuyakabili.

Akiongea na waandishi wa habari leo asubuhi,Obama alitanabaisha kuwa "ana mambo ya msingi zaidi ya kushughulikia kuliko upuuzi huo (kuhusu uhalisi wa uraia wake)".

"Hatutoweza kufanikiwa iwapo tutayumbishwa,hatuwezi kufanikiwa iwapo tutatumia muda wetu kuchafuana...kama tunazua tu mambo na kujifanya kuwa ukweli ni uongo,hatutoweza kutatua matatizo yetu kama tutawaendekeza wazushi",alisema Obama ambaye alizaliwa Agosti 4 mwaka 1961 huko Honolulu,Hawaii kwa baba Mkenya na Mama Mmarekani Mweupe.

Hata hivyo,dakika chache baada ya cheti hicho cha kuzaliwa kuwekwa hadharani,Trump aliendeleza mashambulizi yake kwa Obama akidai cheti hicho-ambacho bado anakitilia mashaka-kisingwekwa hadharani bila mashambulizi yake kwa Rais huyo.Kadhalika,kundi la Birther limeendelea kuonyesha wasiwasi wake huko baadhi ya wanakundi wakidai cheti hicho ni cha kufoji.

Lakini pengine kwa kugundua kuwa suala la uraia wa Obama halina msingi,Trump alisharukia ajenda nyingine akihoji elimu ya Rais huyo.Tajiri huyo mpenda sifa anamtuhumu Obama kuwa alikuwa "mwanafunzi kilaza" (asiyejimudu kitaaluma) na hakustahili kujiunga na Vyuo Vikuu vye hadhi na heshima kubwa (Ivy League) vya Columbia na Shule ya Sheria ya Harvard.

“Inakuwaje mwanafunzi mbovu anakwenda Columbia kisha Harvard?"Trump alimuuliza mwandishi wa habari wa Associated Press. “Natafakari kuhusu suala hili,na kwa hakika nitalichunguza.Atuonyeshe rekodi zake.” Aliendelea kudai, "kuna maswali kadhaa ambayo hayajajibiwa kuhusu rais wetu".

Baadhi ya wachambuzi wa mambo wanadai kuwa inawezekana Tump ana sukumwa na hisia za ubaguzi wa rangi katika mashambulizi yake dhidi ya Obama,huku kebehi zake dhidi ya elimu ya Obama zikitafsiriwa kama "watu weusi hawastahili kwenda vyuo bora nchi Marekani.



VYANZO: Habari hii imetokana na vyanzo mbalimbali mtandaoni hususan jarida la mtandaoni la Huffington Post.


Ukisikia kimbembe cha zule ndio hiki kinachoikabili CCM kwa sasa.Japo chama hiki tawala ni mahiri sana kwa usanii,lakini ni dhahiri kuwa yanayoendelea sasa ndani ya chama hicho yanaweza kabisa kuwa dalili za mwanzo wa mwisho.Hebu jionee vimbwanga hivi katika stori zifuatazo:


Barua za kuwang’oa kina Lowassa zakamilika
• Yadaiwa ziko mezani kwa Msekwa

na Mwandishi wetu

Barua za makada watatu wanaotuhumiwa kwa ufisadi ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Rostam Azizi, Edward Lowassa, na Andrew Chenge, za kuwataka wajiondoe katika nafasi za uongozi ndani ya chama hicho, ziko tayari.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano umethibitisha kwamba makada hao, waasisi wa mtandao uliomwingiza Rais Jakaya Kikwete madarakani mwaka 2005, wanaweza kupokea barua zao wakati wowote kuanzia leo Jumatano.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, barua hizo ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) iliyomaliza kikao chake hivi karibuni mjini Dodoma.

Inadaiwa makada hao maarufu na wenye ushawishi mkubwa ndani ya nje ya chama hicho tawala, walipewa siku 90 tangu siku ya kikao, wapime wenyewe uzito wa kashfa zinazowakabili na wajiengue kwenye nafasi za uongozi, vinginevyo chama kitawaengua katika kikao kijacho cha NEC.

“Barua za Lowassa, Chenge na Rostam ziko tayari, na suala lao liko mikononi mwa Makamu Mwenyekiti, Pius Msekwa, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Chama. Wiki hii watakabidhiwa,” kilisema chanzo chetu cha habari kutoka ndani ya CCM.

Pamoja na mambo mengine, barua hizo zimeorodhesha tuhuma zao na kurejea maazimio ya NEC yanayowahusu.

Alipohojiwa na Tanzania Daima Jumatano juu ya barua hizo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alithibitisha kwamba tayari barua hizo zimeshaandaliwa. Naye alisema watakabidhiwa barua hizo wakati wowote kuanzia leo Jumatano.

“Kinachofanyika sasa ni utekelezaji wa maazimio ya NEC, si jambo geni. Ninachojua, tulikuwa tunasubiri mapumziko ya Sikukuu ya Pasaka yapite, kila mtu ale Pasaka yake,” alisema Nape.

Wakati barua hizo zikisubiriwa kwa hamu, baadhi ya makada wajumbe wa NEC wamekaririwa na vyombo kadhaa vya habari na katika mazungumzo yasiyo rasmi wakisema hakukuwa na azimio lolote lililopitishwa la kuwataka makada hao wapewe siku 90 za kujiengua. Vilevile, wamekanusha kuwapo kwa azimio lolote la kuwaandikia barua.

Hata hivyo, Nape amekuwa akisema kwa waandishi na katika mikutano ya hadhara kwamba NEC ilitoa azimio hilo. Baadhi ya makada wasiokubaliana na kauli za Nape, katika hali ya kuwaonea huruma au kuwatetea watuhumiwa, wamekuwa wakidai kwamba kauli za Nape zimetoka nje, si ndani ya kikao cha NEC.

Lakini baadhi yao wamekuwa wakidokeza kuwa si rahisi Nape kujitungia maneno makali ya aina hii, huku wengine wakisema anatumwa na wakubwa “kuwashughulikia” kina Rostam.

Katika kujaribu kuthibitisha kwamba Nape anazungumza jambo lisilotokana na maazimio ya NEC, baadhi ya makada wanakumbushia kauli za hivi karibuni za mtangulizi wake, John Chiligati, ambaye amepata kutaja mara kadhaa taarifa zisizosahihi za maazimio ya vikao vya Kamati Kuu na NEC, tofauti na kilichojadiliwa ndani ya vikao hivyo.

Wanasema, kwa mfano, Chiligati alipata kulalamikiwa kwa kutoa taarifa potofu kuhusu maamuzi ya Kamati Kuu kuhusu uamuzi wa ama kuilipa au kutoilipa fidia kampuni ya uzalishaji umeme ya Dowans ambayo inaidai TANESCO shilingi bilioni 94.

Vilevile, wanasema Chiligati aliwahi kutoa maazimio ya kupotosha aliposoma maazimio ya NEC kuhusu utata ulioibuka baada ya kukatwa kwa jina la Hussein Bashe katika kinyang’anyiro cha uteuzi wa mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM kwa jimbo la Nzega katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

Hata hivyo, Nape anasisitiza kuwa kauli yake ni ya chama na inatokana na maazimio ya NEC. Katika mikutano ya hadhara inayodaiwa ni ya kujitambulisha, amekuwa akisisitiza kwamba Lowassa, Rostam na Chenge wametakiwa kujiondoa kwenye ujumbe wa NEC ndani ya siku 90, vinginevyo watang’olewa kwa nguvu.

Ndiye pia aliyesema kwamba wataandikiwa barua za kuwaorodheshea tuhuma zao na kuwataka waondoke kwenye uongozi wa chama. Hata hivyo, hakuna kiongozi hata mmoja aliyesema kama makada hao watavuliwa pia ubunge.

Lowassa ni Mbunge wa Monduli, Chenge anawakilisha jimbo la Bariadi Magharibi, na Rostam Azizi ni mwakilishi wa Igunga.

Wadadisi wa mambo ya siasa wanasema kilichotokea mjini Dodoma ni muendelezo wa minyukano ndani ya CCM na kwamba hoja kuu inayosababisha haya si ufisadi, bali urais katika uchaguzi wa mwaka 2015, hasa kwa kuwa baadhi yao wanasemekana wanatamani kugombea au kuunga mkono baadhi ya wagombea.

Nguvu yao ya kifedha na ushawishi wao ndani ya chama ni baadhi ya mambo yanayoogopwa na washindani wao ndani ya chama tawala. Ingawa wote watatu wamekuwa watu wa karibu sana na Rais Kikwete, habari zinasema kumekuwapo na taarifa za kuchongeana miongoni mwao, zikichochewa na makachero wanaomwaminisha Rais Kikwete kwamba sifa yake iliyopotea mbele ya jamii inaweza kurudi iwapo ataondokana na watatu hao.

Rais Kikwete naye anatumia ushauri huo kama fursa ya kurejesha matumaini ya wananchi kwake na CCM, akitumia kaulimbiu ya kujivua gamba.

Hata hivyo, wachambuzi wa masuala ya kisiasa na wakosoaji wa Rais Kikwete wamesema kujivua gamba kunakofanywa naye ni unafiki mtupu, kwani kama lengo ni kupiga vita ufisadi, naye yu miongoni mwa waliotajwa kwa ufisadi pamoja na Chenge, Rostam na Lowassa.

Baadhi ya makada wamesema kwamba kama CCm inaazimia kuondoa mafisadi, basi kiwaondoe viongozi wote waliopatikana kwa pesa za kifisadi za EPA.

Katika orodha ya viongozi waliofaidika na ufisadi wa EPA, anatajwa pia Rais Kikwete, kwa maelezo kwamba pesa hizo zilitumika kununua kura ili ashinde.

Wanasema hata kuvunja Kamati Kuu na kuingiza wajumbe wengine hakukusaidia kuisafisha, kwani walioingia ni wachafu kama waliotoka, maana historia zao na wasifu wao vinafahamika.

Wengine wanakwenda mbali na kusema kwamba iwapo Rais Kikwete atatekeleza azima yake hii, atakuwa anaandaa anguko lake lisilotarajiwa, maana atakuwa anaongeza idadi ya maadui miongoni mwa watu wanaomjua vema, waliomjenga na kumsaidia hadi hapo alipo


Mafisadi CCM waandaa mamilioni kujisafisha
*Wadaiwa kuandaa vijana kupinga hatua dhidi yao

Na John Daniel

KUNDI la mafisadi wanaokabiliwa na hatihati ya kuvuliwa uongozi na pengine uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamebuni mbinu mpya
kujihami kwa kutumia haramu kwa kuandaa vijana kufanya maandamano kumpinga Rais Jakaya Kikwete na chama chake.

Kundi hilo linapinga vikali uamuzi wa CCM kupitia Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), kuwapa muda wa kujiengua wenyewe kabla ya kufukuzwa baada ya siku 90.

Habari za uhakika kutoka vyanzo vyetu vimeeleza kuwa kundi hilo limepitisha bajeti ya mamilioni ya fedha kwa ajili ya kuwandaa vijana kufanya maandamano kupinga uamuzi wa kuondolewa NEC na hata CCM kwa ujumla, mara tu baada ya kukabidhiwa barua muda wowote kuanzia wiki hii.

"Tayari wameapa kuwa wakiondolewa ni lazima Rais Kikwete naye aondoke kwa kuwa ndiye aliyepitisha maamuzi ya kuwafukuza, wanapanga vijana kwa kuwarubuni kwa fedha haramu ili waandamane mara tu watakapopewa barua.

"Wiki iliyopita walikutana wakapitisha zaidi ya milioni 500 kumshughulikia Bwana mkubwa (Rais Kikwete), wanataka kumchafua ili kummaliza nguvu kuwashughulikia," kilisema chanzo kingine.

Habari hizo zilieleza kuwa mbali na Rais Kikwete anayeelezwa na kundi hilo kukabiliwa na tuhuma na ufisadi, akiwa miongoni mwa watu 11 waliotangazwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa, na familia yake, akiwamo mwanawe Ridhiwan anayedaiwa kuwa mali kuliko kipato chake, pia kundi hilo linasaka kwa udi na uvumba majalada ya mawaziri wanne wa sasa kwa lengo la kuwaunganisha katika tuhuma za ufisadi, kwa kinachoelezwa kuwa ni kampeni ya 'tuchafuke wote'.

"Kati ya fedha hizo sh. milioni 18 zitatumwa katika mikoa 20 kugawiwa vijana ili wafanye maandamano ya kupinga kuondolewa na kuwapakazia wengine wanaotaka waondoke nao kama njia ya kujitakasa.

"Fedha zinazobaki zinatumika kununua mafaili ya watu wengine kutafuta makosa yao ya aina yoyote akiwamo Waziri wa Afrika Mashariki, Bw. Sitta (Samwel) Prof. Mwandosya, (Mark), Dkt. Mwakyembe (Harrison) na Membe au Magufuli," kilisema chanzo chetu.

Ilielezwa kuwa kundi hilo limekuwa likifanya vikao katika maeneo maeneo mbalimbali kwa lengo la kutaka kujisafisha na ufisadi, au kupunguza makali kwa kutaja wengine.

"Mmoja wao amejiandaa kuzungumza na waandishi wa habari kuwapa nyaraka za uongo ili kuwachafua watu wengine, walengwa wakuu ni Rais na familia yake, mawaziri wanne na wengine wadogo," kilisema chanzo kingine.

"Usifikiri hatujui hayo, mbinu zote wanazofanya tunazijua, hatuwezi kupambana na wajinga, tunasubiri tuone mwisho wao, lakini hata ninyi waandishi lazima mjue kuwa Watanzania wanaosoma vitu mnavyoandika wanajua yote," alisema kigogo mmoja wa serikali bila kutoa ufafanuzi.

Mbinu nyingine iliyotajwa mara baada ya uamuzi wa NEC Dodoma ni kuwatumia viongozi wa vyama vya siasa kutoa tuhuma mpya ili ionekane kwamba wameonewa na kupoteza lengo la kuwaondoa.

Pamoja na kwamba hakutaja jina, Chama cha demokrasia na Maendeleo ndicho kimetaja watuhumiwa wapya wa ufisadi, huku Katibu Mkuu wake, Dkt. Slaa akipinga madai ya kutumiwa kufanya hivyo kwa nia ya kuwachafua.

Katika tuhuma hizo, alizungumzia uuzaji wa nyumba za serikali bila kufuata utaratibu zilizoelekezwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa na aliyekuwa waziri wake wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli; Kuhusu fedha za EPA na mahali zilipo zile zilizorejeshwa akielekeza tuhuma hizo kwa Rais Kikwete na John Malecela na Philip Mangula waliodaiwa kuhusika katika wizi wa fedha za EPA, hasa zile zilizoingia katika kampeni ya CCM mwaka 2005.

Katika hatua nyingine kundi hilo la mafisadi wa linadaiwa kuwalenga baadhi ya viongozi wa dini kuwasafisha kwa kutangaza msimamo kuwa wameonewa na hakuna mtakatifu au wao wametolewa kafara.

Majira ilipomtafuta Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Bw. Nape Nnauye kujua kama wana taarifa hizo alikiri na kuongeza kuwa haziwasumbui kwa kuwa mfa maji hakosi kutapatapa.

"Kwanza nilishasema nilipokuwa uwanja wa Manzese, niliwaambia wananchi kuwa mafisadi wamejipanga kumchafua Mwenyekiti wetu na familia yake"

CHANZO: Majira

Diwani matatani kwa kumwita Chiligati fisadi

na Francis Godwin, Iringa

DIWANI wa kata ya Mgama, wilayani Iringa Vijijini, Denis Lupala (CCM), yuko matatani baada ya kumwita Naibu Katibu Mkuu CCM, Tanzania Bara, Kapteni John Chiligati, kuwa ni fisadi na anapaswa kuvuliwa gamba kama Katibu Mkuu aliyepita Luteni Yusuf Makamba na wenzake.

Diwani huyo anadaiwa kutoa kauli hiyo hivi karibuni mkoani Iringa wakati Chiligati na viongozi wengine wapya wa sekretarieti ya CCM taifa alipofanya ziara mkoani humo kwa ajili ya kujitambulisha.

Diwani hayu ambaye tayari ameitwa na sekretarieti ya wilaya na Kamati ya Maadili kujadiliwa kwa utovu kwa Chiligati na viongozi wengine waandamizi wa CCM ambao alipendekeza watimuliwe.

Akithibitisha kuitwa kwenye vikao hivyo, Lupala alisema alipewa barua ya kuitwa kuhusu tuhuma hizo, lakini hakuhojiwa.

‘Kweli waliniita na mwanzoni niliambiwa kikao kitanijadili kwa utovu wa nidhamu niliouonyesha badala yake tulijadili tukio la jukwaa kuanguka wakati Chiligati akihutubia,” alisema diwani huyo.

Hata hivyo alijigamba kuwa alikuwa amejiandaa kupangua hoja zao kwani hadi sasa binafsi hataki Chiligati abaki kwenye nafasi hiyo kwa madai kuwa anapaswa kuvuliwa gamba kama viongozi wenzake aliokuwa nao kwenye sekretarieti iliyopita.

“Nilijipanga vizuri kuwajibu viongozi wa wilaya iwapo wangejaribu kutaka kuniadhibu kwa kumwita Chiligati fisadi. Ni ukweli usiopingika kuwa kati ya watu wanaovuruga CCM Chiligati ni mmojawapo na hana sifa ya kuwa kiongozi ndani ya CC na nasema kuwa niko tayari kuwajibika kwa kusema ukweli dhidi ya Chiligati,” alisema diwani huyo.

Hata hivyo habari zaidi zinasema kuwa diwani huyo anatarajiwa kuitwa wakati wowote kuanzia sasa kujibu tuhuma alizozielekeza kwa Chiligati.

Wakati wa mkutano wa hadhara, diwani huyo wa CCM alipata nafasi ya kuuliza swali na kuanza kumrushia madongo Chiligati kwamba ni fisadi na ajiuzulu nafasi yake.

Pia alitaka Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, Andrew Chenge (Bariadi Mashariki) na Rostam Aziz (Igunga) na wengine kufilisiwa mali zao na kunyang’anywa kadi za uanachama.

Hata hivyo alishindwa kuendelea na hoja yake baada ya baadhi ya wanachama na viongozi wa CCM kuingilia kati na kusitisha swali lake kwa Chiligati.


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.