26 Dec 2008

CHAGUZI NDANI YA CCM HAZIISHIWI VIOJA.RUSHWA IMETAPAKAA MNO NDANI YA CHAMA HICHO KANA KWAMBA NI SEHEMU YA KATIBA YAKE.SIO MATUSI KUAMINI KWAMBA PENGINE INGEKUWA RAHISI ZAIDI KWA CCM KUAHIDI KUENDELEZA LIBENEKE LA RUSHWA KWENYE MANIFESTO YAKE YA 2005 KULIKO AHADI ZA MAISHA BORA,MAHAKAMA YA KADHI,NK MAMBO AMBAYO HADI SASA YAMEENDELEA KUWA AHADI ZISIZOTEKELEZEKA.NI WAZI,RUSHWA HUZAA VIONGOZI WABOVU,MAFISADI NA WABABAISHAJI.HABARI MBAYA NI KWAMBA HAKUNA DALILI ZA KUISHA KWA GONJWA HILO HATARI NDANI YA CHAMA TAWALA.TAASISI ZA UMMA ZA KUKABILIANA NA RUSHWA ZINAISHIA KUALIKWA TU KWENYE CHAGUZI "KUZUIA RUSHWA" NA VIONGOZI WAANDAMIZI WA CHAMA HICHO WAMEISHIA KUPIGA KELELE TU (SINA HAKIKA KAMA NI ZA DHATI) KUHUSU RUSHWA KWENYE CHAGUZI,LAKINI SOTE TUNAJUA KWAMBA KELELE ZA CHURA HAZIMZUII NG'OMBE KUNYWA MAJI.ENEWEI,HEBU CHEKI MKASA HUU HAPA CHINI KISHA SOMA HITIMISHO LANGU BAADA YA HABARI HII:
Zikiwa zimesalia siku 14 kufika siku ya uchaguzi wa viongozi wa ngazi ya taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mambo si shwari katika mchakato wa kumpata mwenyekiti wake. 

Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika mjini Dodoma Januari 7, mwakani ambapo nafasi ya uenyekiti itagombewa na Janet Kahama, Sophia Simba na Joyce Masunga. 

Hali hiyo, ambayo inazidi kuipaka matope CCM, imedhihirika baada ya mgombea wa nafasi ya Janeth Kahama kuwasilisha rasmi malalamiko kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, akimtuhumu mpinzani wake, Sophia Simba kwamba amewahonga wajumbe wote wa Mkutano Mkuu rushwa ya Sh. 100,000 ili wampe kura. 

Mbali na tuhuma za rushwa, Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), anatuhumiwa pia na Kahama kuwa yeye na wapambe wake wamekuwa wakiitumia Ikulu kuwaomba kura wajumbe wa Mkutano Mkuu. 

Kahama, ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM), amewasilisha malalamiko hayo kupitia barua yake yenye kumbukumbu Na. JBK/01/08 ya Desemba 20, mwaka huu, iliyopelekwa kwa Rais Kikwete, Ikulu, jijini Dar es Salaam. 

Nakala ya barua hiyo, ambayo Nipashe inayo, imepelekwa kwa Katibu Mkuu wa UWT Taifa na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba. 

Makamba alipoulizwa na Nipashe juzi jioni kama amepokea nakala ya barua hiyo, alithibitisha kuipokea. 
Simba anadaiwa kutoa hongo hiyo kupitia kadi alizochapisha kwa lengo la kuwatakia heri ya Mwaka Mpya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT Taifa. 

Kadi hizo, ambazo zinadaiwa kusambazwa na Diwani wa Kata ya Ilala, Moshi Kondo, zina picha, jina na saini ya Waziri Simba, kalenda ya Mwaka Mpya wa 2009 na nembo ya CCM. 

Barua hiyo yenye kichwa cha habari kisemacho: `Yah: Malalamiko dhidi ya Mhe. Sophia Simba kugawa vipeperushi mikoani`, Kahama anamueleza Mwenyekiti Kikwete kama ifuatavyo: 

``Kwa heshima ya pekee, nakuomba uhusike na mada ya barua hii kama inavyosomeka hapo juu. Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unavyofahamu, Jumuiya yetu ya UWT hivi sasa ipo katika mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa ngazi ya taifa unaotarajiwa kufanyika mapema mwakani.`` 

``Mimi nikiwa mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa Taifa wa UWT, natambua kuwa wagombea wote tulizuiwa na vikao vya UWT Taifa kutoa vipeperushi vya aina yoyote kwa minajili ya kujinadi kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa UWT.`` 

``Lakini, ajabu ni kwamba, mgombea mwenzangu, Bi Sophia Simba amechapisha kalenda na kadi za `Heri ya Mwaka Mpya` zenye picha yake na nembo ya CCM na kuzisambaza kwa wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa UWT Taifa nchi nzima, ndani zikiwa na kitita cha Sh. 100,000 (kwa kila kadi).`` 

``Mheshimiwa Mwenyekiti, nalazimika kukuandikia waraka huu ili kukupa angalizo juu ya suala hilo hasa ikizingatiwa kuwa Mheshimiwa Sophia Simba ni Waziri katika ofisi yako mwenye dhamana ya Utawala Bora.`` 

``Hivyo hatua yake na nembo ya CCM, inakwenda kinyume na kanuni za uchaguzi za CCM, kipengele cha Miiko ya Kuzingatiwa wakati wa Shughuli za Uteuzi na Uchaguzi`, ibara ya 33 kifungu kidogo cha 14 kinachosema: `Ni mwiko kutumia makaratasi ya kampeni nje ya utaratibu wa chama au kutumia vishawishi vya aina yoyote ile kwa minajili ya kupata kura.`` 

``Je, hatua hii ya Mheshimiwa Simba kuchapisha nyaraka hizo zenye picha yake na nembo ya CCM na kuzitawanya nchi nzima, si uvunjaji wa makusudi wa kanuni hizo za uchaguzi za CCM tena kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa UWT?`` 

``Je hatuoni kwamba hatua yake hiyo ambayo haijakemewa mpaka sasa ni kielelezo kingine cha ubabe na matumizi mabaya ya madaraka yake kama Waziri tena mwenye dhamana ya Utawala Bora? 

Nasisitiza hili kwa sababu Mheshimiwa Simba na wapambe wake wamekuwa wakipita mikoani na kupotosha wapigakura kuwa yeye ndiye chaguo la Ikulu.`` 

``Mheshimiwa Mwenyekiti, nawasilisha kwako waraka huu wenye malalamiko haya ili uweze kujua nini kinaendelea na kuchukua hatua kwani kama kitaachwa, kinaweza kujenga matabaka ndani ya UWT na mpasuko usio wa lazima ndani ya chama chetu, hasa pale hisia za mgombea mmoja kuandaliwa mazingira ya ushindi dhidi ya wenzake zinapoanza kujengwa.`` 

``Naambatanisha moja ya vipeperushi hivyo vya Mheshimiwa Simba vilivyosambazwa mikoani kinyume na utaratibu nilioueleza hapo juu.`` 

Makamba alipoulizwa na Nipashe juzi, licha ya kukiri kupokea nakala ya barua hiyo ya Kahama, alimtaka mwandishi kama ana swali lolote kuhusiana na suala hilo, akamuulize Rais Kikwete kwa vile ndiye aliyeandikiwa barua hiyo. 

``Mtafute Mwenyekiti wa CCM, yeye ndiye aliyeandikiwa barua, aliyeandikiwa ndiye anayejibu. Mimi nimepewa nakala, anayepewa nakala, anaarifiwa tu,`` alisema Makamba. 

Nipashe ilipowasiliana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ikulu, Salvatory Rweyemamu, alisema kwa vile malalamiko ya Kahama yanahusiana na Chama, anayepaswa kujibu suala hilo ni Katibu Mkuu. 

Baada ya Makamba kuulizwa tena, alisema: ``Mimi sina cha kusema, sijaisoma (hiyo barua), sijajua maudhui. 

Nitakapoisoma na kujua maudhui, nitatoa maoni yangu.`` 

Kahama alipoulizwa na Nipashe jana kama barua hiyo ndiye aliyeiandika, hakukiri wala kukanusha, badala yake alisema kwa sasa hawezi kuzungumza lolote kwa vile kipindi hiki ni cha sikukuu ya Krismasi, ambayo yeye kama Mkristo anapaswa kuitukuza. 

``Sina comments (maoni) kabisa kabisa, mpaka nionane na Katibu Mkuu. Pia mimi ni Mkristo na kipindi hiki ni cha Krismasi,`` alisema. 

Naye Diwani wa Kata ya Ilala, Moshi Kondo, alipoulizwa juzi, alikataa kuzungumzia suala hilo, badala yake alimtaka mwandishi akamuulize Simba. 

``Kwani Sophia Simba mimi ni nani kwake?`` alihoji Kondo, ambaye alipojibiwa na mwandishi kuwa ``Simba anadaiwa kuwa ni mtu wake wa karibu``, alisema: ``Nenda kamuulize Simba.`` 

Tangu juzi hadi jana jioni Nipashe ilimtafuta Simba bila kumpata na baadaye kuelezwa na mmoja wa wanafamilia yake kuwa yuko safarini Malaysia. 

CHANZO:Nipashe

WAKATI MAMA KAHAMA AMETUMIA HAKI YAKE YA MSINGI KAMA MGOMBEA NA MWANANCHAMA WA UWT/CCM KUWASILISHA MALALAMIKO YAKE KWA MWENYEKITI WA CCM TAIFA (JK),NADHANI ANGEWEZA PIA KUWASILISHA TUHUMA HIZO POLISI AU TAKUKURU.HIVI KUTOA RUSHWA SI NI KOSA LA JINAI?JE MAMA KAHAMA YUKO MORE CONCERNED NA RUSHWA HIYO KUATHIRI NAFASI YAKE YA KUCHAGULIWA KULIKO UKWELI KWAMBA MTUHUMIWA (SOPHIA SIMBA) SIO WAZIRI TU BALI NI WAZIRI MWENYE DHAMANA YA UTAWALA BORA (ISOMEKE MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA)?


The Afghan chieftain looked older than his 60-odd years, and his bearded face bore the creases of a man burdened with duties as tribal patriarch and husband to four younger women. His visitor, a CIA officer, saw an opportunity, and reached into his bag for a small gift.Four blue pills. Viagra...CLICK HERE FOR FULL STORY


25 Dec 2008


Kiongozi wa mapinduzi hayo,Kapteni Moussa Dadis Kamara,aliyejitangaza kiongozi mpya wa Guinea baada ya kifo cha Rais Lansana Conte.Kwa habari zaidi,BONYEZA HAPA.


HIVI TUNA UHABA MKUBWA SANA WA WATENDAJI NA VIONGOZI WAZURI HADI TUENDELEE KUWANG'ANG'ANIA HATA WALE WALIOKWISHAFANYA MADUDU HUKO NYUMA?KUNA STORI KATIKA GAZETI LA MWANANCHI KUHUSU ALIYEKUWA MKURUGENZI WA MANISPAA YA TEMEKE,JOHN LUBUVA,AMBAYE ALISIMAMISHWA KAZI KUTOKANA NA SAKATA LA UBOMOAJI NYUMBA HUKO TABATA DAMPO.CHA AJABU ETI KWA SASA NI MKURUGENZI WA MANISPAA YA SHINYANGA VIJIJINI.HII SIO TU DHARAU KWA WAKAZI WA MANISPAA HIYO ILIYOLETEWA "MTENDAJI MPYA" BALI PIA NI MUENDELEZO WA HAKA KAMTINDO KA KUNG'ANG'ANIA VIONGOZI WALIOPUNGUKIWA NA SIFA.JE,KUMREJESHA KIONGOZI HUYO MADARAKANI HAKUWEZI KUWA KICHOCHEO KWA VIONGOZI WENGINE KUREJEA MADUDU KAMA YA MWENZAO ALIYEBORONGA,AKAPEWA MAPUMZIKO MAFUPI KISHA AKAREJESHWA MADARAKANI?TANGU LINI ADHABU KWA MAKOSA YA UONGOZI IKAWA KUHAMISHWA KUTOKA TEMEKE NA KUPELEKWA SHINYANGA?HIVI AKILIKOROGA TENA HUKO SHINYANGA ITAKUWAJE?THIS IS NOT ONLY UNFAIR BUT INAKERA NA KUCHUKIZA PIA.


Serikali imeridhia Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA- JKT), liongezewe nguvu kiutendaji na kuwa kampuni ya ulinzi itakayotoa ushindani kwa makampuni binafsi ya ulinzi yanayotoa huduma hiyo kwa kiwango kisichoridhisha. 

Kwa sasa SUMA, imejikita katika ujenzi wa nyumba za serikali, barabara na kutengeneza samani. 

Uamuzi wa JKT kuwa na kampuni ya ulinzi, una lengo la kuajiri vijana wanaohitimu mafunzo ya awali ya kijeshi. 

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Kanali Ayoub Mwakang’ata, alitoa taarifa hiyo jana wakati akihutubia katika kilele cha mafunzo ya Operesheni Uadilifu yaliyokuwa yakifanyika katika Kambi ya 835 JKT Mgambo wilayani Handeni. 

Katika taarifa yake alisema kuwa serikali kwa kushirikiana na Jeshi hilo wameridhia kampuni hiyo kuanza kazi rasmi mapema mwakani. 

Kampuni hiyo imepanga kuboresha huduma za ulinzi kwa kuajiri askari waliopitia Jeshi hilo pekee na kuwasambaza katika maeneo mbalimbali nchini kote wakichuana na makampuni mengine yaliyoko sasa, lakini bila ya kuathiri utendaji wao. 

``Suma JKT itakuwa kampuni ya ulinzi rasmi kuanzia mwakani na itachukua vijana waliohitimu mafunzo ya awali ya kijeshi na si askari wa akiba wa mgambo, mpango huu ni maalumu kwa ajili ya kuwasaidia vijana kama hawa kupata ajira za uhakika baada ya kuhitimu mafunzo haya… na ukweli ni kwamba hatua hii itakuwa ni changamoto kwa vijana wengi wanaomaliza darasa la saba na kidato cha nne kujiunga JKT,``alisema. 

Awali Ofisa Utumishi wa JKT Makao Makuu, Meja Elvis Massawe alipohojiwa kuhusiana na hatua iliyofikiwa hadi sasa na Kitengo hicho cha SUMA alikiri kwamba Ofisi hiyo imeshapokea maombi zaidi ya robo tatu ya vijana waliohitimu katika Jeshi hilo nchi nzima wakisubiri kuajiriwa rasmi. 

Kwa mujibu wa Ofisa huyo ni kwamba Kampuni hiyo mbadala ya ulinzi itachukua askari wa rika mbalimbali bila kujali umri wao na kwamba bado jeshi hilo linapokea maombi ya yawanaotaka kujiunga na kampuni hiyo...

CHANZO: Nipashe

SINA HAKIKA KAMA UMEFANYIKA UTAFITI WA KUTOSHA KUHUSIANA NA MAAMUZI HAYA MAZITO (IT'S PERSONAL KWANI NAMI NI MMOJA KATI YA WALIOPITIA JKT KWA MUJIBU WA SHERIA MIAKA YA 90).NAAMINI TATIZO KUBWA LINALOKWAZWA KUIREJESHA JKT KUWA KAMA YA ENZI HIZO NI PAMOJA NA MIPANGO DHAIFU ISIYOANGALIA MBALI.SIJUI BABA WA TAIFA HUKO ALIKO AKISIKIA JKT INATAKA KUGEUZWA KAMPUNI YA ULINZI ATAJISIKIAJE LAKINI KWA HAKIKA NI JAMBO LINALOTIA SHAKA SANA HASA IKIAZINGATIWA KWAMBA JESHI SIO TAASISI YA BIASHARA.NI VIGUMU KUTUAMINISHA KWAMBA JKT ITAWEZA KUHIMILI USHINDANI WA KIBIASHARA KATIKA SEKTA YA ULINZI BINAFSI ILHALI UFANISI WA VITENGO VYA KIBIASHARA KATIKA JESHI HILO (KWA MFANO SUMA NA MRADI WA KOKOTO KUNDUCHI) WENYE MUSHKELI.

JKT INGEWEZA KUWA KITUO CHA KUZALISHA AJIRA KWENYE SEKTA YA KILIMO NA HATA UJASIRIAMALI IWAPO KUTAKUWA NA MAANDALIZI SAHIHI.MSISITIZO WA JKT NI KUWAANDAA VIJANA KULITUMIKIA TAIFA LAO KWA UZALENDO NA SIO KWENDA KULINDA MALI ZA WATU (INCLUDING MAFISADI).HATA KAMA WAZO LA BIASHARA YA ULINZI NI ZURI BADO KUNA WASIWASI KUHUSU MASLAHI YA VIJANA HAO,JAMBO AMBALO LISIPOANGALIWA KWA MAKINI LINAWEZA KUZAA MAJAMBAZI BADALA YA WALINZI BINAFSI.ULINZI NI TAALUMA NYETI NA ISIPOTENGENEZEWA SERA MAKINI INAWEZA KUZAA MAYHEM KATIKA JAMII.

24 Dec 2008


SAFARI YA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI BADO NI NDEFU NA YENYE VIKWAZO LUKUKI.KATIBA NA SHERIA ZINAZOWATOFAUTISHA VIONGOZI NA WANANCHI WA KAWAIDA ZINATUMIKA KAMA KINGA DHIDI YA MATENDO AMBAYO KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE YANAHUSU UVUNJAJI WA SHERIA.PIA KINGA HIZO ZINAWEZA KUWA KICHOCHEO KIZURI KWA VIONGOZI WAPYA KWANI KAMA WATANGULIZI HAWAKUCHUKULIWA HATUA WALIPOBORONGA (KWA VILE WANA KINGA) THEN KWANINI WALIOPO MADARAKANI WAOGOPE KUBORONGA?HIVI KAMA WENZETU HUKO MAREKANI WANADIRIKI KUMHOJI RAIS MTEULE,IWEJE VIGUMU KWETU KUMHOJI RAIS MSTAAFU?ANYWAY,SOMA STORI HII HAPO CHINI KISHA TUENDELEE NA MJADALA WETU
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, hachunguzwi kwa kosa au tuhuma yoyote ya jinai, imeelezwa. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), katika taarifa yake kwa umma iliyotolewa Dar es Salaam jana, ilisema uvumi kuwa Rais huyo mstaafu anachunguzwa na vyombo vya dola ikiwamo taasisi hiyo, hauna ukweli wowote. 

Tamko la taasisi hiyo limekuja huku kukiwa na uvumi katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa kiongozi huyo anachunguzwa na Takukuru, kutokana na vitendo vingi vya ufisadi vinavyodaiwa kufanywa wakati wa uongozi wake. 

Tayari mawaziri wawili Basil Mramba na Daniel Yona waliowahi kushika nyadhifa nyeti katika Serikali ya Awamu ya Tatu ukiwamo uwaziri wa Fedha, wameshafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 11.7. 

Lakini pia baadhi ya watuhumiwa katika kesi za kuchota mabilioni ya fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu (BoT), ambao wamefikishwa mahakamani, wanadaiwa kufanya wizi huo kati ya mwaka 2004 na 2005 kipindi ambacho Rais Mkapa alikuwa madarakani. 

Ofisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kipwani alisema jana kuwa, taasisi yake haina uwezo wa kumchunguza kiongozi huyo kutokana na Katiba ya nchi kutotoa nafasi hiyo katika Ibara ya 46 (3) ya Katiba ya Tanzania. Kapwani alieleza kuwa taasisi yake inaheshimu Katiba na ina wajibu wa kuilinda na kuheshimu matakwa hayo ya Katiba. 

“Takukuru inawafahamisha wananchi kwamba uvumi huu hauna ukweli wowote, hatumchunguzi kiongozi huyu kwa kosa au tuhuma yoyote ya kijinai,” alisema. “Ni kwa msingi huu, Takukuru imeona ni vyema kuwafahamisha wananchi ukweli dhidi ya uvumi huu. 

Tukumbuke wakati wote kwamba taifa letu lina Katiba ya Nchi ambayo imeweka misingi mikuu ya kuendesha nchi yetu, haki na wajibu wa kila Mtanzania. Katiba kama sheria mama imeweka pia mipaka katika kushughulikia mambo mbalimbali ya nchi na kwa mantiki hii, haina budi kuheshimiwa wakati wote.” 

Kifungu hicho cha Katiba kinaeleza kuwa “Ni marufuku kumshitaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais kwa mujibu wa Katiba hii.” 

Kapwani alisisitiza kuwa Takukuru itaendelea kufanya kazi zake kwa mujibu wa Katiba na sheria ya nchi na sio vinginevyo. Katika siku za karibuni, baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vinaripoti kuwa Mkapa anachunguzwa na Takukuru licha ya kuwa ana kinga ya kutoshitakiwa. 

Vyombo hivyo vimekuwa vikimwandama kwa madai kuwa ufisadi mkubwa umefanyika katika kipindi ambacho alikuwa madarakani. Watu wenye mtazamo huo wamekuwa wanataka kiongozi huyo aondolewe kinga na afikishwe mahakamani kujibu tuhuma mbalimbali za ufisadi. 

Wiki hii, Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo alieleza kusudio la kuwasilisha hoja binafsi katika kikao kijacho cha Bunge kuomba kifungu kinacholinda marais wastaafu kutoshitakiwa kirekebishwe. Mkapa anatajwa katika tuhuma kuhusu ununuzi wa ndege ya Rais, ununuzi wa rada, wizi wa mabilioni ya EPA, uuzaji wa nyumba za serikali, mikataba yenye utata kama ya NetGroup, Alex Stewart na ubinafsishaji wa mgodi wa Kiwira.
CHANZO: Habari Leo

UFAFANUZI HUO WA TAKUKURU HAUWEZI KUZIMA KELELE ZA WANAOTAKA KUMUONA TUHUMA DHIDI YA MKAPA ZINATHIBITISHWA KWENYE VYOMBO VYA SHERIA.PAMOJA NA KUILINDA NA KUIHESHIMU KATIBA,TAKUKURU INA WAJIBU WA KULINDA NA KUTETEA RASLIMALI ZA WATANZANI ZINAZOFUJWA NA MAFISADI.LAKINI TUKIACHANA NA EXCUSE HIYO YA TAKUKURU (WAMESHATOA LUKUKI) THIS IS A WAKE UP CALL KUHUSU HIZI KINGA DHIDI YA VIONGOZI WASTAAFU (NA PENGINE HATA KWA WALIO MADARAKANI).WAKATI WAZO LA KINGA NI ZURI LIKITUMIWA VIZURI,KWA MFANO DHIDI YA WANAOTAKA KUDHALILISHA VIONGOZI KWA SABABU BINAFSI AU KISASI,WAZO HILO NI HATARI KWA VIONGOZI WALIOZITUMIA VIBAYA OFISI ZAO WALIPOKUWA MADARAKANI.MAHALA PEKEE PANAPOWEZA KUMSAFISHA MKAPA NI MAHAKAMANI NA WALA SIO KWA KAULI ZA KULINDANA KAMA HIZO ZA TAKUKURU.

23 Dec 2008


WAKATI Ripoti ya kitaalam ikionyesha namna bora ya kupunguzwa matumizi ya magari ikiwamo ya kifahari maarufu kama mashangingi, serikali imeanza utekelezaji wa mpango mwingine mkubwa wa kuingiza magari mapya 792 kutoka Japan.

Mpango huo mkubwa wa serikali umekuja wakati ripoti ya kitaalamu inayotaka ijipunguzie matumizi yasiyo ya lazima katika ununuzi wa magari ikiwemo ya kifahari ikiwa imewasilishwa mezani kwa Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo tangu Aprili mwaka huu.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye wiki moja iliyopita alitoa angalizo kwa makatibu na manibu makatibu wakuu wa wizara kuhusu kupunguza matumizi ya magari ya kifahari, alinukuliwa na gazeti dada la The Citizen, akisema serikali haiwezi kupiga marufuku ununuzi wa magari hayo wakati imeshaagiza lakini alisisitiza kuwa hiyo itakuwa mzigo wa mwisho kuagizwa na mashangingi kiasi hicho.

Ingawa Pinda hakufafanua, lakini duru huru zaidi za habari kutoka serikalini zilidokeza gazeti hili jijini Dares Salaam jana kwamba, tayari magari 300 yalishaingizwa chini ya mpango huo. "Sehemu kubwa ya magari hayo ni Toyota Pickup, tayari 300 yameingizwa nchini chini ya mpango huo maalumu wa serikali," zilisema duru hizo za habari.

Kwa ufafanuzi zaidi, duru hizo zilisema katika orodha hiyo pia yapo mashangingi Vx na GX ambayo jumla yao ni kati ya 100.

Chini ya mpango huo, duru za habari zilisema gari nyingine ambazo ni nyingi ni pamoja na Toyota Land Cruiser Hard Top ambazo kwa takwimu za kiserikali moja hugharimu kati ya sh 72 hadi 75 milioni.

"Ukiacha Vx na Gx 100, magari mengine mengi katika orodha hiyo ni Toyota Land Cruiser Hard Top na Pickup ndiyo mengi katika orodha hiyo ya magari 792," kilifafanua zaidi chanzo hicho.

Waziri Mkuu Pinda alikaririwa jana na gazeti dada la Mwananchi, The Citizen, katika mahojiano maalum akisema uamuzi wa kuzuia ununuzi wa magari hayo hauwezi kuchukuliwa kwa sasa, kwa kuwa tayari yameshaagizwa na yataanza kuingia nchini hivi karibuni.

“Uamuzi wa kuzuia ununuzi wa magari hayo hauwezi kufanyika sasa kwa kuwa magari 800 tayari yameshaagizwa kutoka kampuni inayoyatengeneza nchini Japan na yanatarajiwa kuanza kuingia nchini hivi karibuni,” alisema Pinda katika mahojiano hayo.

Hata hivyo, Pinda alieleza kuwa katika mwaka wa fedha ujao mambo yatakuwa tofauti kutokana na kuwataka makatibu wakuu kutoagiza magari hayo na fedha zitazopatikana katika zoezi la kuacha kununua magari hayo zinunue matrekta ambayo yatakuwa na matokeo yanayoonekana katika kilimo.

Hakuna mtu anaweza kufa kwa kutopanda gari la kifahari (Toyota Land Cruiser VX, GX) lakini kwa kukosa chakula itakuwa ni tatizo,” alisema Pinda katika mahojiano hayo.

Alisema uamuzi wake huo umekuwa ukiungwa mkono na Rais Jakaya Kikwete, ukiwa umelenga kumkomboa mkulima ambaye amekuwa anatumia jembe la mkono kwa miaka 47 ya uhuru wa nchi hii.

“Magari haya ya kifahari yamekuwa yananunuliwa kutokana na baadhi ya watumishi (wakurugenzi) kutaka kuendana na wakati wa magari ya kifahari yaliyopo sokoni,” alisema Pinda huku akisema serikali sasa inataka kuondokana na dhana hiyo.

Alipoulizwa mbona serikali imeamua kuendelea kununua magari hayo japokuwa yamekuwa yanasemwa kuwa ni mzigo kwa serikali, Pinda alisema wakati anaingia tayari magari yalikuwa yameshaagizwa na hivyo mpango huo utaanzia kwenye bajeti ijayo ya serikali.

Aliongeza kuwa “Nimeongea na makatibu wakuu wiki iliyopita nimewaambia kuhusu suala hili la uagizaji magari ya kifahari, sasa tuachane nalo na badala yake tujikite kwenye kilimo cha kisasa,”

Duru hizo zikieleza kwa kina mpango huo, Ripoti ambayo iko kwa Luhanjo na gazeti hili kufanikiwa kuona nakala yake, inaonyesha namna bora ya serikali kupunguza ununuzi wa magari hasa ya kifahari.

Katika mpango huo, moja ya jambo lililopendekezwa na watalaamu ni kuhakikisha gari la moja aina ya VX au Gx hubadilishwa na kukunuliwa jingine kila baada ya miaka saba tofauti na sasa, ambapo waziri, naibu au makatibu wakuu hubadili magari hayo kila baada ya miaka miwili.

Ripoti hiyo pia inaonyesha orodha ya viongozi wanaopaswa kutumia magari hayo kwa kupunguza viongozi wanaopaswa kutumia Vx na Gx, ambao wanapaswa kutumia ni mawaziri, manaibu, makatibu wakuu na manaibu wao, huku kuanzia wakurugenzi wakipasawa kutumia magari mengine ikiwemo Land Cruiser za kawaida.

Pia kumekuwa na pendekezo la kufuata utaratibu ambao hutumiwa na serikali kama ya Afrika Kusini, Namibia na Botswana ambazo hutumia Kampuni ya Emperial kwa ajili ya usimamizi wa kiteknolojia kwa ajili ya magari yote ya serikali ili kuyaangalia na kudhibiti yasitumike katika shughuli binafsi.

Emperial kwa kutumia teknolojia hiyo huweza kuonyesha hatua ya kila gari kwa kutumia mfumo maalumu wa usalama na pia kuzuia wizi hata wa mafuta katika magari ya serikali ambayo sasa hivi hakuna mfumo wa kuyadhibiti.

CHANZO:Mwananchi

NANI KASEMA MATREKTA KWA WAKULIMA NI MUHIMU KULIKO NYONGEZA YA MASHANGINGI KWA WAHESHIMIWA?EBO?NYIE MNATAKA WAHESHIMIWA WAKAGUE MAENDELEO WAKIWA KWENYE MATREKTA?UHESHIMIWA NI PAMOJA NA KUWA KWENYE GARI LA KIFAHARI.HIZI NDIZO PRIORITIES ZETU ZITAKAZOMWEZESHA KILA MTANZANIA KUWA NA MAISHA BORA HIVI PUNDE TU!



PICHA HIZI ZINAONYESHA UHARIBIFU ULIOSABABISHWA NA VURUGU ZINAZOENDELEA NCHINI UGIRIKI KUFUATIA POLISI KUMUUA MTOTO MMOJA.BAADA YA KUANGALIAPICHA HIZO,HEBU SOMA HABARI IFUATAYO KUHUSU VIFO VYA WATOTO WATATU HUKO KILIMANJARO.
WATOTO watatu wa jamii ya wafugaji wa Kimasai, wameuawa kwa kupigwa risasi na askari polisi waliopo kwenye mazoezi ya kulenga shabaha katika Kijiji cha Embukoi, wilayani Siha, mkoani Kilimanjaro.

Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Embukoi, Peter Pekasi, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 10 jioni, ambapo watoto hao walikuwa wakipita eneo kwenda kusaga nafaka katika mashine iliyo jirani na kijiji hicho.

Mtendaji huyo aliwataja watoto wanaodaiwa kuuawa kuwa ni Lyomo Orkwari (7), Laata Mollel (15) na Samwel Josia(8), wote wakazi wa kijiji hicho cha jamii ya Masai.

Pekasi alisema eneo la tukio limekuwa likitumiwa kwa muda mrefu kama kituo cha kulenga shabaha kwa askari waliopo mafunzoni katika Chuo cha Mafunzo ya Polisi Moshi (CCP) na kuhatarisha maisha yao.

Alisema baada ya tukio hilo walitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ya Siha, Anarose Nyamubi.

Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Lucas Ng’hoboko, alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, alisema hana taarifa kamili za tukio hilo na kuongeza kwamba ametuma maafisa wake eneo la tukio.

“Jamani nimepata taarifa hizo muda mfupi kabla hujaja hapa, nimetuma maofisa wangu eneo la tukio, kwa sasa siwezi kuzungumzia chochote, nitatoa taarifa zaidi baada ya kupata maelezo ya kina kutoka kwa askari wangu,” alisema Ng’hoboko.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Siha, Nyamubi, akizungumza kwa njia ya simu jana, alithibitisha kupata taarifa hizo, lakini hakuwa tayari kuzungumzia kwa undani na kwamba ametuma maofisa wake eneo la tukio.



NA HAITOSHANGAZA IWAPO HAKUNA ATAKAYEWAJIBIKA KWA VIFO VYA WATOTO HAO WASIO NA HATIA.


22 Dec 2008

AISEE,ILE ISHU YA KUMTWANGA GEORGE W BUSH NA KIATU INAENDELEA KUVUTA HISIA.LATEST,JAMAA ALOTENGENEZA VIATU VILIVYOTUMIKA KUMTWANGA BUSH AMEJIKUTA AKIPATA DILI KIBAO,YAANI CHATI NDIO IMESHAPANDA.SINTOSHANGAA TUKISKIA NA HUKO HOME SHOE-SHINER FLANI KAPATA DILI BAADA YA KIATU ALICHOKUWA AKIKIHUDUMIA KUTUMIKA KUMRUSHIA FISADI FLANI....NAJUA HIYO NI PIPE-DREAMING KWA VILE MAFISADI WENYEWE WANALETWA MAHAKAMANI NA MASHANGINGI,WAKIWA LUPANGO WANALAZWA VIP KAMA KEMPINSKI,NA WAKIPATA DHAMANA WANACHUKULIWA NA MA-VOGUE YAO!BACK TO STORI YA IRAQI,KONG'OTA HAPA USOME ZAIDI


Police in Finland believe they have caught a car-thief thanks to a DNA sample taken from a sample of his blood found inside a mosquito. Skip related content

Last June a car was stolen in Lapua, some 380 kilometres (235 miles) north of Helsinki. It was soon found near a railway station in Seinaejoki, about 25 kilometres from where it was stolen.

"A police patrol carried out an inspection of the car and they noticed a mosquito that had sucked blood. It was sent to the laboratory for testing, which showed the blood belonged to a man who was in the police registers," inspector Sakari Palomaeki told AFP.

The suspect, who has been interrogated, has insisted he did not steal the car, saying he had hitchhiked and was given a lift by a man driving the car.

Palomaeki said a prosecutor would decide if the evidence was solid enough for charges to be pressed.

Finnish police said it was rare for them to use insects to solve crimes, although they are interested in everything found at a crime scene.

"It is not usual to use mosquitoes. In training we were not told to keep an eye on mosquitoes at crime scenes," Palomaeki said, laughing.

"It is not easy to find a small mosquito in a car, this just shows how thorough the crime scene investigation was," he added.

SOURCE: Yahoo! News

HOPEFULLY,THE EPA TASK TEAM IS READING.WELL,LET'S NOW TRY MOSQUITOES IF IT'S THAT DIFFICULT TO NAB THE OWNERS OF KAGODA BY USING "CONVENTIONAL" MEANS!AND GOOD NEWS IS,THERE'S NO SHORT SUPPLY OF MOSQUITOES IN TZ.

Photo courtesy of MJENGWA

KURA YANGU INAWAANGUKIA WABABAISHAJI WA TRL.CHEKI "MBELEKO" NYINGINE HII KUTOKA KWA SUMATRA:

HATIMAYE Kampuni ya MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imeiruhusu Kampuni ya Reli (TRL) kuanza kutumia mabehewa yake 23 ya mitumba yaliyokodishwa kutoka Kampuni ya Reli ya India. Awali Sumatra waliizuia TRL kutumia mahehewa hayo kwa madai kwamba hayakuwa na obora unaotakiwa.

Hata hivyo, meneja uhusiano wa TRL, Midrahji Meiz alisema jana kuwa Sumatra sasa imewaruhusu kuendelea kutumia mabehewa hayo baada ya vigezo vilivyokuwa vinahitajika kukamilika.

“Tumesharuhusiwa na Sumatra kuanza kutumia mahehewa hayo na hivi sasa utaratibu unafanyika ili yanze kusafirisha abiria... baada ya utaratibu huo kukamilika tutatoa taarifa rasmi,” alisema Meiz na kuongeza: “Suala la usafiri wa treni ni suala la msingi kabisa na ndiyo maana tunajitahidi kuboresha usafiri huo kila wakati ili abiria wasafiri katika mazingira mazuri.”

Mkurugenzi na mdhibiti wa reli wa Sumatra, Alfred Nalitolela alikiri kuwepo kwa suala hilo na kusema kuwa wameamua kuiruhusu TRL indelee kutumia mabehewa hayo kwa kuwa wamekamilisha marekebisho yaliyokuwa yanahitajika.

“Tulibaini kwamba mabehewa hayo hayana ubora unaostahili kwa matumizi ya reli yetu, na moja ya vitu hivyo ni kiungio kati ya behewa moja na jingine, usambazi wa umeme ndani ya mabehewa, belling, spring, breki ya mkononi na magurudumu,” alisema Nalitolela na kuongeza:

“Tulipokwenda India kukagua mabehewa hayo, tuliwaeleza wafanye vitu hivyo lakini wakaleta mabehewa kabla ya kukamilika kwake ndipo ikabidi tuwakataze kuyatumia mpaka wamalize kuyafanyia marekebisho hayo.”

Alifafanua kwamba baada ya hapo walichukuwa moja ya kiungio cha mabehewa na kuyapeleka katika maabara ya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuyafanyia utafiti kama ni vifaa vipya na kuomba maelezo ya kina.

“Unafahamu katika suala hili lile jumba la behewa ndilo linalotakiwa kuwa mtumba, lakini vifaa vyote vinavyofanya mabehewa hayo yafanye kazi vinatakiwa kuwa vipya, ikiwemo usambaji wa nyaya za umeme ndani ya behewa. Na hicho ndicho tunachokikagua na kukiangalia na kuhakikisha kwamba viko salama kila wakati,” alifafanua Nalitolela.
CHANZO:Mwananchi
JE MWENZANGU KURA YAKO INAANGUKIA WAPI?


KAMPUNI iliyopewa jukumu la kusimamia na kutunza mali za lililokuwa Shirika la Reli Tanzania (RAHCO), imeanza kukatakata injini 27 na mabehewa 19 ili yauzwe kama chuma chakavu.

Mabehewa hayo na injini zake yanadaiwa yalikuwa na hali nzuri, lakini mwekezaji akayakataa wakati anachukua shirika kwa maelezo kuwa hayamfai.

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya mwekezaji Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) kudai kuwa, mabehewa hayo yalikuwa yamechakaa zaidi na hayawezi kutumiwa tena, huku Rahco ikidai kuwa yalikuwa yanafaa kuendelea kutumika.

Tayari zabuni ya kupata makampuni ya kununua vyuma hivyo chakavu imeshafanyika na washindi kupatikana.

Makampuni ambayo yameshinda zabuni yameshaanza kukata mabehewa hayo na injini katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Tabora na Kigoma.

Mwananchi Jumapili wiki hii ilishuhudia baadhi ya mafundi wa kampuni iliyoshinda zabuni wakikata mabehewa yaliyopo katika Stesheni ya Dar es Salaam.

Meneja Uhusiano wa RAHCO, Musita John aliiambia Mwananchi Jumapili kuwa, wameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kushindwa kuzifanyia kazi injini hizo na mabehewa.

Alisema kuwa endapo injini hizo na mabehewa zingefanyiwa ukarabati mdogo zingeendelea kuisaidia kampuni hiyo kupunguza matatizo ya usafiri lakini mwekezaji hakuzikubali.

John alisema wakati mwekezaji anachukua shirika hilo alikuta jumla ya injini 116 na 92 kati yake zilikuwa zinafanya kazi, lakini yeye aliamua kuchukuwa 79 tu na zingine akazikataa kwa madai kwamba hazimfai.

Alisema mbali na injini hizo, pia alikuta jumla ya mabehewa ya abiria 164, yaliyokuwa yanafanya kazi ni 125, lakini yeye aliamua kuchukuwa mabehewa 106 tu na 19 yaliyobaki aliyakataa.

John alifafanua kwamba baada ya mwekezaji huyo kumaliza tathimini ya mali za TRC alizokuta kabla hajaanza kazi waliamua kuziweka katika madaraja mbalimbali, ambapo daraja (A) lilikuwa ni mabehewa na injini yaliyokuwa yanafanya kazi.

Alisema Daraja (B) lilikuwa ni la mabehewa na injini zilizokuwa zinahitaji matengenezo madogo, ingawa yalikuwa bado yanaendelea na kazi ya kusafirisha abiria na mizigo wakati daraja (C) ni yale ambayo alikuta yameondolewa kazini, baada ya kuharibika na kupelekwa kwenye karakana ili yafanyiwe ukarabati, lakini pia aliyakataa kwa madai kwamba hayamfai.

Aliongeza kuwa kulikuwa na daraja (D) ambalo lilihusisha injini na mabehewa yaliyoharibika, yasiyofaa kutumika na daraja E ni yale ambayo yalishakaguliwa na kubainika kwamba, yalishafikia katika kiwango cha vyuma chakavu.

Hata hivyo, habari kutoka ndani ya TRL, zinaeleza kwamba mbali na injini na mabehewa hayo, mali zingine ambazo mwekezaji huyo alizikataa ni vifaa vya ofisini ambavyo hivi sasa pia viko katika orodha ya vitu vinavyouzwa na RAHCO kama vyuma chakavu.

Wakati RAHCO ikiendelea kukatakata injini hizo na mabehewa TRL hivi sasa inadaiwa kuwa katika hali mbaya kutokana na baadhi ya injini zake aina ya ‘73 class’ zilizokodishwa kutoka India kuwa na uwezo mdogo wa kuvuta mzigo, kiasi kwamba wanalazimika kuziunganisha mbili ndipo ziweze kuvuta mzigo ambao ungevutwa na injini moja aina ‘88 class’ za Tanzania alizozikataa.

Meneja Uhusiano wa TRL, Midlajy Maez alipotakiwa kutoa ufafanuzi wake kuhusiana na suala hilo alisema wanaotakiwa kulizunguzia ni RAHCO.

CHANZO:Mwananchi

HIVI KWANINI TUNAENDELEA KUWANG'ANG'ANIA HAWA WABABAISHAJI WA KIDOSI?JIBU JEPESI NI KWAMBA WALIOWAKARIBISHA NI WABABISHAJI WENZAO,SO SIO RAHISI KWAO KUONA UBABAISHAJI ULIOPO.TUNA WAZIRI,NAIBU WAZIRI,KATIBU MKUU,NAIBU KATIKA MKUU,MKURUGENZI,NK,NK,NK WOTE KATIKA WIZARA HUSIKA.HAWA WANALIPWA MSHAHARA NA MARUPURUPU MENGINE KUTOKA KWA WALIPA KODI WA TANZANIA LAKINI SIJUI WANASHINDWA NINI KUCHUKUA HATUA STAHILI DHIDI YA USANII HUU ULIOPEWA JINA LA UWEKEZAJI.MWEKEZAJI GANI AMBAYE ILI ALIPE MSHAHARA KWA WAAJIRIWA WAKE NI LAZIMA APEWE TAFU NA SERIKALI?

KAMA KAWAIDA,JAMAA WATAHARIBU RELI WEE MPAKA IWE TOO MUCH THEN WATAINGIA MITINI,AU MZEMBE FLANI ATAKURUPUKA USINGIZINI NA KUDAI IUNDWE TUME YA UCHUNGUZI (ISOMEKE TUME YA KULA FEDHA ZA VIKAO) LAKINI WAKATI HUO HUDUMA YA RELI YA KATI ITAKUWA IMEKUFA KABISA.CALL IT MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA AS WE ARE APPROACHING 2009!


A Saudi court has rejected a plea to divorce an eight-year-old girl married off by her father to a man who is 58, saying the case should wait until the girl reaches puberty.

The divorce plea was filed in August by the girl's divorced mother with a court at Unayzah, 135 miles north of Riyadh just after the marriage contract was signed by the father and the groom.

Lawyer Abdullar Jtili said:"The judge has dismissed the plea, filed by the mother, because she does not have the right to file such a case, and ordered that the plea should be filed by the girl herself when she reaches puberty."

"She doesn't know yet that she has been married," Jtili said then of the girl who was about to begin her fourth year at primary school.

Relatives who did not wish to be named said that the marriage had not yet been consummated, and that the girl continued to live with her mother.

They said that the father had set a verbal condition by which the marriage is not consummated for another 10 years, when the girl turns 18.

The father had agreed to marry off his daughter for an advance dowry of £5,000, as he was apparently facing financial problems, they said.

The father was in court and he remained adamant in favour of the marriage, they added.

Mr Jtili said he was going to appeal the verdict at the court of cassation, the supreme court in the ultra-conservative kingdom which applies Islamic Sharia law in its courts.

Arranged marriages involving pre-adolescents are occasionally reported in the Arabian Peninsula, including in Saudi Arabia where the strict conservative Wahabi version of Sunni Islam holds sway and polygamy is common.

In Yemen in April, another girl aged eight was granted a divorce after her unemployed father forced her to marry a man of 28.

SOURCE: Daily Mail

21 Dec 2008

There are now more slaves on the planet than at any time in human history. True abolition will elude us until we admit the massive scope of the problem, attack it in all its forms, and empower slaves to help free themselves...CONTINUES HERE

19 Dec 2008


The man accused of masterminding the 1994 Rwanda genocide, Theoneste Bagosora, was jailed for life by an international court yesterday as prosecutors described his conviction as the most significant since Nuremberg.

Bagosora, 67, a former colonel who was the chief of staff in Rwanda's defence ministry, was convicted of genocide, crimes against humanity and war crimes at the end of a five-year trial after judges found that he used the military and an extremist Hutu militia to kickstart the massacre of about 800,000 Tutsis in 100 days.

The international criminal tribunal for Rwanda, sitting in Tanzania, also found Bagosora guilty of responsibility for overseeing individual massacres as well as the murder of Rwanda's prime minister, Agathe Uwilingiyimana, and the killing of 10 Belgian peacekeepers, which prompted the UN to withdraw most of its forces and abandon the Tutsi population to be slaughtered. Lieutenant General Romeo Dallaire, the UN commander in Rwanda, who called Bagosora the "kingpin" behind the genocide, described meeting him as like "shaking hands with the devil".

But the court did not convict Bagosora on the broader charge of conspiracy to commit genocide before the killing, saying that while he created, armed and trained the militia that carried out the massacres and headed an "enemy commission" that vilified Tutsis, that did not demonstrate that he had planned the extermination from the beginning.

"The chamber certainly accepts that there are indications which may be construed as evidence of a plan to commit genocide, in particular when viewed in light of the subsequent targeted and speedy killings immediately after the shooting down [of President Juvénal Habyarimana's plane which unleashed the genocide]," the judgment said. But the tribunal said these preparations were in the context of a war with Tutsi rebels and could not be said beyond doubt to be solely preparations to exterminate civilians.

Once the killings began, the tribunal found that Bagosora was the highest authority in the defence ministry and oversaw control of the military as it murdered opponents and kickstarted the genocide. The court said the killings "formed part of an organised military operation pursuant to orders from superior military authorities". Bagosora said nothing as the verdict was delivered.

Two other army officers on trial with Bagosora, Aloys Ntabakuze and Anatole Nsengiyumva, were also given life sentences for genocide. Prosecutors called them "enemies of the human race". A fourth defendant, Gratien Kabiligi, the former chief of military operations, was acquitted of all charges and released.

Barbara Mulvaney, the lead prosecutor, described the verdicts as historic. "I think it's one of the most important verdicts ever because the body of work, in documents in black and white, in transcripts, in video tapes, lays out the planning and organisation of a genocide," she said. "And it's important to the Rwandan people because it finally puts to rest the claims by some people ... who still deny there was a genocide or deny that it was planned. No one can claim that any more."

But the relevance of the tribunal has been diminished in Rwanda by lengthy trials held outside the country. None of the Hutu leaders on trial have apologised for their role in the genocide, raising fears among some Tutsis that it could happen again.

SOURCE: The Guardian

Watch this tear jecking video about the genocide.WARNING: Contains disturbing images.



18 Dec 2008








Picha kwa hisani ya thread ya Jamii Forums.

Click HERE to read full story.

A polite word of caution: The video is  44.09 mins long.
SOURCE: WSHH

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.