5 Oct 2011



Na Nova Kambota Mwanaharakati,

Mara kwa mara huwa nasema tatizo kubwa la Tanzania yetu ni kupenda kupindisha ukweli, hii imetufanya kuwa watu tusiopenda kufikiri kiasi kwamba tunalambishwa kila linalokuja “tumekuwa madodoki kila uchafu tunasomba”. Naandika hivi kwa nia ya kujenga si kubomoa, naandika hivi kwa mustakabali wa Demokrasia yetu ambayo nathubutu kusema imetikiswa kupita maelezo huko Igunga na tusipokuwa makini Taifa litadondoka siku za usoni.
Kwako Dr Kafumu ambaye umetangazwa kuwa mbunge wa Igunga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), naomba unaposhangilia ushindi wako nikiamini wewe ni msomi na mzoefu katika Nyanja za uongozi wa Taifa hili napenda usome maandishi yaliyo ukutani kisha malizia kwa kuunganisha dots za ushindi wako halafu niambie ikiwa ni kweli unaamini kuwa umeshinda kihalali? Au la niambie kile ambacho kinaitwa “changamoto za uchaguzi Igunga” ni nini kama siyo “mizengwe?”
Kama mchambuzi nisiyeegemea upande wowote nisingependa kutia mwaa mtiririko huu wa hoja zangu kwa hiyo sitaegemea upande wowote bali nitajadili kwa misingi ya hoja ili ikibidi kujibiwa pia nijibiwe kwa misingi ya hoja vivyo hivyo, nataka kuibua hoja zenye mashiko ili zitufikirishe na kutupa majibu ya kisayansi badala ya kumezwa na mawimbi ya watu wenye mkatiko wa mirija ya fikra ambao wamebaki na ushabiki badala ya hoja kiasi kwamba wanatoa majibu ya zamani kwa maswali mapya. Yafuatayo ni mambo manne ambayo yanatia doa ushindi wa Dr Kafumu;
Kwanza Tume Ya Uchaguzi;
Tume ya uchaguzi ya nchi hii haina sifa nzuri na haiwezi kuwa na sifa nzuri mpaka iwe huru, hata I gunga hali ni hivyohivyo tumesikia malalamiko dhidi ya tume hiyo lakini hasa kwa aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa uchaguzi huo ambaye pia ni mteule wa rais na bila shaka kwa kuunganisha mantiki haina shaka kuwa naye ni mwanachama wa CCM au basi anaipenda kimoyomoyo. Uchaguzi wa Igunga ukipimwa kwa mizania hii ya aina ya tume ya uchaguzi tuliyonayo ni vigumu sana kwa mtu mwenye kufikiri kwa mantiki kuridhia matokeo ya uchaguzi huo.
Pili Siasa Uchwara;
Hapa inahitaji moyo mgumu kuyasema lakini kwa vile tangu awali nilishasema kuwa lengo si kufukua makaburi bali kuweka shada la maua juu ya makaburi basi acha niseme hiki ambacho nakiita ni siasa uchwara. Kwanza kabisa jinsi serikali ya CCM ilivyoruhusu kubofywa kwa kile kinachoitwa “kitufe cha udini”, ikumbukwe kuwa hata wakati wa uchaguzi serikali bado ina jukumu la kuilinda katiba na kuhakikisha amani haivurugwi aidha kupitia mirija ya udini wala ukabila, nayasema haya kutokana na baadhi ya viongozi wa dini kuirushia makombora CHADEMA tena wakaenda mbali kwa kutoa wito kwa baadhi ya waumini wa dini Fulani kutompigia kura mgombea wa chamna hiko, lakini cha ajabu hata hiyo hoja ya DC kuvuliwa hijabu imekwama kama gazeti nguli la Mwanahalisi lilivyofunua kuwa Mama Fatuma Kimario uislamu wake una mashaka kutokana na yeye kuwa ni mke halali wa Bw Kimario ambaye ni mkristu wa madhehebu ya Kikatoliki ambapo hata mwanazuoni mashuhuri wa kiislamu nchini Sheikh  Issa Ponda amenukuliwa akisema kuhusu mwanamke au mwanaume wa kiislamu kubadili dini Sheikh Ponda amesema “Hilo ni kosa kubwa sana”.  Lakini cha kusikitisha kuwa wakati haya yote yanatokea CCM walikaa kimya kana kwamba “hawakuliona kosa”, je tukisema kuwa hii ilichangia Wana Igunga kupiga “kura za chuki” dhidi ya CHADEMA tutakuwa tumekosea? Haya ni maswali magumu kuhusu ushindi wa Dr Kafumu.
Jambo la pili ambalo linaangukia kwenye siasa uchwara ni pamoja na vitimbi vya rushwa na vitisho vya “kipuuzi” mfano gazeti la Dira linamtaja mwenyekiti wa mtaa wa Nkokoto huko Igunga Bw Abed Motomoto (CCM) kuwa amekutwa akigawa rushwa “live”kwa wanawake wa mtaa wake kwa lengo la kuwashawishi kumpigia kura mgombea wa CCM (Dr Kafumu), lakini kama hili halitoshi kuna hili la Mh Ismail Aden Rage kupanda na bastola ikining’inia kiunoni halafu tunaambiwa kapewa adhabu ya kulipa laki moja, sasa ladda nitumie fursa hii kumuuliza ndugu yangu Aden Rage kuwa alikuwa anamtisha nani na bastola yake? Au nani kamwambia kuwa ni utamaduni wa kitanzania kuonyeshana vyombo vya moto? Haya ni machache kati ya mengi yanayokinzana na maana ya demokrasia pia kupoteza mantiki nzima ya “uchaguzi huru na wa haki”
Tatu kuchelewesha matokeo;
Hili ni  tatizo linalotia huzuni sana kiasi kwamba nashawishika kuamini kuwa “bado tuna safari ndefu”, nayasema haya kwasababu kwanza idadi ya watu waliojiandikisha ni tofauti sana kwasababu waliopiga kura ni wachache wanaokadiriwa kuwa elfu sitini (60,000) lakini cha ajabu hata kiasi hiki kichache cha kura kimechukua masaa kibao zaidi ya kumi kuhesabu, hiki kama si kiroja ni nini? Au tuamini kuwa kuna lililojificha nyyuma ya pazia hapa?
Nne Matumizi Ya Nguvu;
Nalazimika kuyaandika haya kutokana na tabia inayozidi kukua siku hizi ya polisi kutumia nguvu dhidi ya wananchi , matukio ni mengi lakini hebu tutupie macho kwenye hili sakata la Igunga ambapo nasema kulikuwa na matumizi ya nguvu yasiyo na msingi, mabomu ya machozi ya nini? Watu walitawanywa kwasababu gani? Kwa mamlaka ya nani? Na faida ya nani? Je hii ndiyo demokrasia tunayoitaka? Huu ndiyo tunaouita ushindi halali? Uhalali uko wapi hapa?
Baada ya kuona upungufu huu , sasa tuone nini ambacho Dr Kafumu anaweza kufanya ili kuienzi Demokrasia na kuwapa haki yao Wana Igunga;
1. Awe wa kwanza kulaani matumizi ya nguvu dhidi ya Wana Igunga
2. Awe wa kwanza kuhakikisha Ismail Aden Rage anachukuliwa hatua kali za kimaadili
3.Awe wa kwanza kulaani harakati zozote za wanasiasa kuingiza udini kwenye siasa
4.Awe wa kwanza kuomba radhi kwa niaba ya chama chake kwa kukaa kimya au kushabikia siasa uchwara.
5 Awe wa kwanza ndani ya CCM na Tanzania kukataa ushindi huo na kuitaka Tume kuitisha tena uchaguzi wa jimbo dogo la Igunga , hili lifanywe pasipo kuangalia gharama za zoezi hilo, bali lifanywe ili kuuonyesha Ulimwengu kuwa Dr Kafumu na CCM wameamua kusiamamia misingi ya Demokrasia pasipo kujali gharama za hatua hiyo.
Haya ni mambo ya msingi kwa Dr Kafumu kuyasoma na kuyafanyia kazi, hii itamjengea heshima sio tu ndani ya CCM bali kwa watanzania wote na Ulimwengu mzima. Tafakari! A luta Continua!
  
Nova Kambota Mwanaharakati,
+255717 709618
Wesneday, 5october,2011
Tanzania, East Africa.


Hi, 
There are three benefits with Wanachuo programme East Africa, 
Cost benefits,professional benefits and community benefits 
1.Cost benefits 
In this cost benefit:- 
i.A student can know the exactly price of the product or service ie no need for window shoping,every thing is online. 
ii.Student can be updated with special deals and offers from different product and service providers through his mobile phone 
iii.Students can save minimum of 20% through buying from our discount providers. 
iv. Student can earn points by referring other students in the programme or through buying from our discount providers locations. 

We are in the second phase of developing the professional and community benefits, 
Join the programme its free 
www.wanachuo.com 
Best regards 
Abdalah Kileo

4 Oct 2011


Karibu  Kona ya Mangoma"It's all about East African Flava"
Habari zenu wadau wote... Tunapenda kuchukua nafasi hii ya kipekee kabisa kuwakaribisha katika Libeneke jipya kabisa la KONA YA MANGOMA  Ambapo mtapata kutazama video mpya na nyenginezo nyingi kutoka pande zote Afrika Mashariki yani Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi..Pia tunaomba wasanii wote ambao mnatoa Video mtutumie link kupitia barua pepe hii ([email protected]) ili tuweze wape sapoti ya juu, Kwa pamoja tunaendeleza Muziki wa Afrika. Tunatanguliza Shukrani  zetu za dhati kwenu. Ukiona link hii mpe na mwenzako.


Jina la Blog: Kona ya Mangoma  



Naamini wasomaji wapendwa wa blogu hii mlisoma POST HII niliyomjibu ndugu yangu Omar Ilyas aliyehitimisha kuwa Chadema inahitaji kushindwa ili ishinde

Naam,kwa hakika hicho ndicho kilichojiri jimboni Igunga ambapo licha ya CCM kuwekeza kila aina ya raslimali (halali na za kifisadi) imeibuka na ushindi mdogo tu wa tofauti ya kura takriban 2000.Ni wazi kuwa laiti CUF ingethamini umuhimu wa ushindi kwa vyama vya upinzani-na kumsapoti mgombea wa Chadema- muda huu CCM ingekuwa inahesabu hasara.

Ni rahisi kwa Chadema na wafuasi wake kuvunjika moyo kutokana na kutoibuka washindi katika uchaguzi huo.Lakini kimsingi Chadema imefanya vizuri kuliko ilivyotarajiwa.Unajua,kuna wakati ushiriki tu-na matokeo ya ushiriki huo-ni sawa na ushindi,hususan pale matokeo ya ushiriki huo yanapotoa picha ya kujenga matumaini.

Ni rahisi pia kwa watu kuikebehi Chadema-kama anavyofanya Bwana Nape Nnauye na viongozi wengine kadhaa wa CCM.Ikumbukwe kuwa CCM ililazimika kulamba matapishi yake hadi kufikia hatua ya kushinda uchaguzi huo.Sote tunafahamu kuwa Nnape na wenzie walitupa imani kuwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kabla ya uchaguzi,mtuhumiwa wa ufisadi Rostam Aziz,alikuwa gamba.Na hiyo ndio sababu ya msingi ya kufanyika uchaguzi huo baada ya gamba hilo kuamua kuondoka lenyewe.

Lakini wafuatiliaji wa kampeni za uchaguzi huo watakuwa bado na kumbukumbu za Rostam kupandishwa majukwaani kuiombea kura CCM.Well,hilo sio kosa kwani Rostam bado ni mwanachama wa CCM.Lakini ni kituko kisicho na maelezo kumshirikisha kwenye kampeni hizo mtu anayefahamika kama gamba ndani ya chama hicho.Inadaiwa kuwa Rostam alibembelezwa ashiriki kwenye kampeni hizo kutokana na nguvu zake kubwa za kisiasa jimboni Igunga.

Ni wazi kwa mwenendo huu tusitarajie kusikia magamba mengine ie Edward Lowaasa na Andrew Chenge wakijiuzulu nyadhifa zao kwani wanafahamu fika kuwa bado wanahitajika kwenye chama hicho kama ilivyokuwa kwa Rostam.

Sipati tatizo katika kuhitimisha kuwa Chadema ni kama wameshinda kwa vile katika ucgauzi huo walikuwa kama timu ya soka inayopambana na timu pinzani yenye wachezaji 15 (11 wa kawaida,refarii,kamisaa na washika vibendera wawili).CCM ilipewa kila aina ya sapoti kutoka serikalini,tukiweka kando vitisho vilivyotolewa na mawaziri kwa wapiga kura wa Igunga kuhusu "athari za kuwachagua wapinzani."

Lakini hapa tunazungumzia tuliyosoma magazetini na tuliyasikia redioni au kuyaona kwenye runinga.Kuna nguvu za giza ambazo hazikuweza-na kamwe haitowezekana-kuripotiwa.Hawa ni ndugu zangu wa Idara ya Usalama wa Taifa.Ukweli usiofahamika ni kwamba jamaa hawa ni kikwazo kikubwa sana kwa maendeleo ya demokrasia Tanzania kwani wanafanya kila wawezalo-kwa kutumia usiri wao-kuhakikisha CCM inaibuka na ushindi katika chaguzi mbalimbali.

Sasa kama Chadema imeweza kupata kura zote hizo licha ya vikwazo lukuki ilivyokabiliana navyo jimboni Igunga ni dhahri kuwa laiti chama hicho kikishikamana na kudumisha umoja na mshikamano basi 2015 tunaweza kurejea historia iliyojitokeza nchini Zambia hivi karibuni.

Ni muhimu kutoangalia kushindwa kwa Chadema katika uchaguzi huo pasipo kuhusisha jithada (halali na haramu za serikali,taasisi zake na watumishi wake).Kama Chadema imediriki kupata kura takriban 2000 tu pungufu ya mgombea wa CCM basi kitakwimu na kiuhalisi ni kama wameshinda vile.

Of course najua kuna watakaosema najipa matumaini.Well,mimi si mwanachama wa Chadema na sitegemei kuwa mwanachama wa chama hicho au chama kingine chochote kile huko nyumbani.Kwanza sina sifa ya kuwa mwananchama na pili malengo yangu ya kiajira yananizuwia kujihusisha na chama chochote kile cha siasa.

Basi nimalizie kwa kuipongeza Chadema kwa kumudu kutoa upinzani wa dhati licha ya vikwazo vyote ilivyokabiliana navyo.Uchaguzi huu-na kushindwa kwake-iwe changamoto muhimu ya kuwaandaa kukamata nchi hapo mwaka 2015.Mkiamua kiwa kitu kimoja basi ni dhahiri kuwa yaliyotokea Zabia hivi karibuni yatarudia tena mwaka 2015.

Penye nia pana njia

3 Oct 2011


Wenzetu Zambia wameweza, sie ‘tumerogwa’ na nani?
Evarist Chahali
Uskochi
28 Sep 2011
Toleo na 205
WIKI iliyopita tumeshuhudia wenzetu wa Zambia wakiamua kukipa kisogo chama tawala baada mgombea wa kilichokuwa chama cha upinzani cha Patriotic Front, Michael Sata kuibuka mshindi katika uchaguzi mkuu wa nchini humo.
Sata, anayefahamika pia kwa jina la utani la King Cobra, alimbwaga aliyekuwa Rais na mgombea wa chama tawala cha Movement for Multiparty Democracy (MMD), Rupiah Banda.
Katika mazingira ya kawaida ya siasa za Afrika, yayumkinika kuhitimisha kuwa ni vigumu sana kwa chama cha upinzani kushinda uchaguzi mkuu. Kikwazo kikubwa ni jinsi vyama tawala barani Afrika hutumia kila mbinu kuhakikisha kuwa utawala wao unadumu milele.
Kimsingi, hakuna tatizo kwa chama kimoja kuwa madarakani muda mrefu.Tatizo ni pale uwepo madarakani wa chama hicho unavyozidi kuididimiza nchi husika katika nyanja mbalimbali za maisha.
Kanuni isiyo rasmi ya kisiasa katika bara hili inatanabaisha kuwa ‘chama tawala hakiwezi kushindwa uchaguzi,’ na ikitokea kikashindwa basi labda ni kutokana na sababu kuu tatu.
Kwanza, kuteua mgombea asiyekubalika na wengi ndani ya chama hicho na hivyo kupelekea kura za chuki dhidi yake ambazo zitamnufaisha mpinzani wake mkuu.
Pili, katika sababu inavyoweza kushabihina na hiyo ya kwanza, ni pale chama tawala kinapogubikwa na migogoro isiyoisha na hatimaye baadhi ya waandamizi ndani ya chama hicho kukimfanyia hujuma mgombea wao kwa minajili ya kukomoana.
Sababu ya tatu ni ulevi wa madaraka. Pengine mfano mwepesi ni wa nyoka chatu ambaye akishakula kiumbe mkubwa anakuwa kama mfu. Anajisahau na laiti ukimwona kichakani baada ya mlo huo unaweza kudhani amezimia kama si kufa kabisa.
Sasa, baadhi ya vyama tawala baada ya kuwa madarakani muda mrefu vinafikia hatua ya kujisahau kwanini vipo madarakani.Vinaendesha mambo kwa mtindo wa ‘bora liende.’
Lakini sababu zote hizo hapo juu zinaweza zijitosheleze kukiondoa chama tawala madarakani kwa sababu mara nyingi uwepo madarakani wa chama hicho unazinufaisha taasisi nyingine  zisizo za kisiasa, kwa mfano vyombo vya dola.
Kuna imani kwamba taasisi za usalama kama vile jeshi la polisi, idara za usalama wa taifa na hata jeshi huenziwa vya kutosha na vyama tawala kiasi cha kujenga kile kinachofahamika katika elimu-viumbe (baiolojia) kama symbiotic relationship. Huu ni aina ya uhusiano wa kutegemeana, uhai wa mmoja ni uhai wa mwingine.
Taasisi hizo za dola hujenga au kujengewa imani potofu kwamba pasipo chama tawala kuwepo madarakani basi nazo zinaweza kupoteza uhai wake.Unaweza kujiuliza kwa nini taasisi yenye watu kadhaa ikajazwa imani potofu kirahisi namna hiyo?
Jibu ni kwamba mara nyingi taasisi hizo, kama ilivyo mazoea ya siasa katika nchi mbalimbali za Afrika, huongozwa kibinafsi. Mkuu wa taasisi husika hugeuka kuwa kama mmiliki wake.
Na marais huwa makini katika kufanya teuzi ambapo kigezo kikubwa huwa utiifu wa mteuliwa kwa Rais (sio utiifu kwa mujibu wa sheria na kanuni bali kwa sababu za kibinafsi).
Kwa hiyo, viongozi wa taasisi hizo hugeuka kuwa kama kirefusho (extension) cha matakwa binafsi ya Rais katika taasisi husika. Lengo ni kuhakikisha rais na chama chake wanaendelea kuwepo madarakani; huku taasisi hizo zikipindisha utekelezaji wa majukumu yake kwa manufaa ya chama tawala.
Watendaji katika taasisi hizo huaminishwa kuwa wanachofanya ni kwa mujibu wa sheria zinazoongoza utendaji kazi wao; japo kiuhalisia wanaotekeleza matakwa binafsi ya rais na swahiba yake aliyekabidhiwa jukumu la kuongoza taasisi husika.
Katika mazingira ya kawaida ya siasa zetu, vyama vya upinzani vinapopambana na chama tawala vinakutana na mazingira kama haya ya kinadharia ambapo kesi dhidi ya mtuhumiwa mahakamani inaendeshwa na mshtak ambaye pia ndio hakimu na mwendesha mashtaka. Ni wazi katika kesi ya aina hiyo ni lazima mtuhumiwa ashindwe na mshtaki ashinde.
Au mfano mwingine rahisi (wa kinadharia pia) ni pale timu ya soka inapopambana na timu nyingine yenye wachezaji 15; yaani wachezaji 11 wa kawaida wakisaidiwa na refa, washika vibendera wawili na kamisaa. Haihitaji kuwa na ufahamu wa soka kuelewa timu gani kati ya hizo mbili itaibuka mshindi.
Kwa huko nyumbani, ushindi wa Sata si habari njema kwa chama tawala CCM, chama ambacho hakina maelezo ya msingi ya kwa nini nchi yetu yenye utajiri lukuki inaendelea kuelemewa na lindi la umasikini unaochangiwa zaidi na ufisadi (huku wahusika wakuu wa ufisadi wakiwa ni baadhi ya viongozi wa chama hicho au wanapatiwa hifadhi salama dhidi ya hatua za kisheria).
Yayumkinika kuhisi kuwa CCM wanaombea hali nchini Zambia ichukue mkondo kama ule wa Kenya pale muungano wa wapinzani ulipofanikiwa kuking’oa madarakani chama kikongwe cha KANU. Kwa bahati mbaya (au makusudi) mabadiliko ya kisiasa nchini Kenya yalianza kwa dalili mbaya za vurugu zilizopelekea vifo kadhaa vya wananchi wasio na hatia.
CCM hawakushindwa kutumia mfano wa Kenya kuhalalisha hoja yake mfu kuwa ‘wapinzani wapo kwa ajili ya vurugu tu.’
Sijui sasa watasemaje kuhusu wapinzani kuchukua serikali nchini Zambia tukitarajia yaliyojiri Kenya hayatojitokeza kwa jirani zetu hao tunaounganishwa nao na Reli ya TAZARA (ambayo nayo iko hoi bin taaban kama ulivyo uchumi wetu).
CCM pia wana hoja yao nyingine maarufu kila unapokuja uchaguzi, iwe ni uchaguzi mdogo au uchaguzi mkuu ambapo huwalaghai wapigakura kwamba wasifanye kosa kuwapa madaraka wapinzani ambao hawana uzoefu wa kuongoza.
Hoja hiyo ni fyongo kwa sababu hakuna mwananchi anayehitaji chama chenye uzoefu wa ufisadi. Ni bora kufanya majaribio na chama mbadala cha upinzani - ambacho yawezekana kabisa kikawa makini kwenye utawala wake kwa kuhofia kung’olewa kama mtangulizi wake - kuliko kuking’ang’ania chama kilichoishiwa na uwezo wa kuongoza.
Ukiona chama kikongwe kinaruhusu viongozi wake kupanda majukwaani na silaha waziwazi (kama huko Igunga), basi, ujue tukiendelea kukiweka madarakani tutafika pabaya.
Siichukii CCM; bali nachukizwa sana na jinsi kinavyowafanya Watanzania kama wapangaji katika nchi yao. Kila kukicha ni hadithi za kukera na zisizoleta matumaini, ukiweka kando tuzo lukuki anazotunukiwa Rais wetu mpendwa Jakaya Kikwete huko nje ‘kwa kazi nzuri anayofanya kuongoza taifa letu.’
Ni fahari kuona Rais akipewa tuzo lakini ni matusi makubwa kutoka kwa watoa tuzo hizo pale wanapofumbia macho sababu zinazotufanya tuendelee kuwa masikini wa kutupa. Rais Kikwete anaweza kumaliza uongozi wake akiwa na historia ya kutunikiwa tuzo nyingi zaidi pengine zaidi ya Baba wa Taifa, lakini Watanzania hawatamkumbuka kwa tuzo hizo au picha aliyopiga na rapa 50 Cent; bali aliwafanyia nini katika miaka yake 10 ya utawala.
Mazoea yana athari moja kubwa ya kumfanya mwadamu akubali mabaya kwa vile tu yamekuwepo siku zote. Mazoea kwamba siku zote tumekuwa tukitawaliwa na CCM ni miongoni mwa sababu za takriban kila baya linaloweza kukufanya umlaumu Muumba kwa kukufanya uzaliwe nchini Tanzania.
Kwa hakika, wanaomlaumu Mungu kwa matatizo yetu wanatafuta ugomvi nae tu; kwani ametupa macho ya kuona uhuni tunaofanyiwa,ametupa ubongo wa kutuelewesha kuwa chini ya utawala wa CCM tutaendelea kuwa na maisha bora kwa mafisadi; huku walalahoi wakizidi kudidimia katika lindi la umasikini.
Na  ametupa masikio kusikia jinsi tuliowakabidhi dhamana ya kutuongoza wakitufisadi na kutukejeli kwa anasa zao za safari zisizoisha huko ng’ambo, visenti kwenye akaunti zao Ughaibuni, na utitiri wa mahekalu, magari ya kifahari na mapande makubwa ya ardhi waliyohodhi.
Kama Zambia wameweza, basi, nasi tunaweza pia. Na pengine hakuna namna nzuri ya wapiga kura kutoa pongezi kwa wenzao wa Zambia zaidi ya kuanza na fundisho la kwanza kwa CCM huko Igunga.
Kwa vile uhuni wa mbunge wa CCM Ismail Aden Rage kupanda na bastola kwenye mikutano wa kampeni hautopelekea hatua zozote za kisheria (hadi muda huu ninapoandika makala hii kilichofanyika ni kauli tu ya Waziri wa Mambo ya Ndani kutaka Rage ahojiwe badala ya kukamatwa),adhabu kubwa inaweza kutolewa na wapiga kura wa Igunga kwa kuigaragaza CCM, na kuitumia salamu kuwa kama imewezekana Zambia, Igunga napo inawezekana, na kwa hakika hata 2015 inawezekana kwa mapana zaidi.
Ndio, inawezekana iwapo kila mzalendo mwenye uchungu na Tanzania yetu atakapoamua kuwa IMETOSHA!

30 Sept 2011



Nimetumiwa na mdau Tluway Tsere,nami naiwasilisha kama ilivyo



Habari za asubuhi Ndg. zangu
Tutafakari hii hadithi fupi, kwani mimi sikulala usingizi
jana baada ya kusikia kuwa Tuzo ya Rostam Aziz imekubaliwae
na mahakama kuu. Watakaolipa si Tanesco bali ni sisi watumiaji
wa umeme.
"tutafakari"
.
An airplane was about to crash; there were 5 passengers on board but only 4 parachutes. The first passenger said, " I'm Kobe Bryant, the best NBA basketball player, the Lakers need me, I can't afford to die.... So he took the first pack and left the plane. The second passenger, Hillary Clinton, said, "I am the wife of the former president of the United States, I am also the most ambitious woman in the world and I am a New York Senator and a potential future president." She just took the second parachute and jumped out of the plane. The third passenger, J.K, said: "I'm President of Tanzania, I have a great responsibility being the leader of a nation. And above all I'm the cleverest President in Tanzania's history, so Tanzania's people won't let me die." So he put on the pack next to him and jumped out of the plane. The fourth passenger, the Pope, says to the fifth passenger, a 10 year-old school boy, "I am old and frail and I don't have many years left, as a Catholic I will sacrifice my life and let you have the last parachute." The boy said, "It's OK, there's a parachute left for you. Tanzania's cleverest President has taken my schoolbag."

27 Sept 2011



Natumaini baada ya kuisoma tunaweza kuelewana kwanini ninatofautiana na uchambuzi wa Bwana Ilyas.Katika paragrafu ya kwanza tu,mwandishi ameshahitimisha kuwa Chadema ina safari ndefu ya kushinda kuwa mtawala mbadala.Anaandika "...ili CHADEMA kushinda katika safari ndefu iliyonayo kama mtawala mbadala kinapaswa kushindwa sasa." Hata hivyo,katika makala hiyo hakuna mahala ambapo mwandishi ameweka sababu za kwanini safari hiyo ya Chadema iwe ndefu,au kwanini anaona hivyo.

Pengine jingine linaloweza kuzua taswira tofauti ya mtizamo wa Bwana Ilyas kwa Chadema ni ukweli kwamba kwa ujumla 'uhuni waliofanya Chadema' unaweza kabisa kufunikwa na 'uhuni mwingine mkubwa' uliofanywa na kiongozi wa CCM,Mbunge Ismail Aden Rage kupanda jukwaani akiwa na bastola.Kwa hakika alichofanya Rage ni zaidi ya uhuni,kwani hata kama anamiliki silaha hiyo kihalali,haiingia akilini kwa mbunge huyo kupanda jukwaani akiwa na silaha-na hakufanya jitihada yoyote kuificha.

Na 'uhuni' mwingine wa kuchefua ni ukweli kwamba hadi sasa hatua pekee iliyochukuliwa dhidi ya Rage ni tamko la Waziri wa Mambo ya Ndani kwamba mbunge huyu anastahili kuhojiwa.Hebu pata picha aliyepanda jukwaani angekuwa Mbunge wa Chadema au CUF!Ni dhahiri muda huu angekuwa lupango,na uchunguzi wa kama anamiliki silaha kihalali au la ungefanyika wakati akiwa rumande.

Tukibaki kwenye hoja hiyo hiyo ya 'uhuni' hivi kuna uhuni mkubwa na mchafu zaidi ya ule wa kiongozi mwandamizi wa CCM (na de facto mratibu wa kampeni za chama hicho huko Igunga),Mwigulu Mchemba kutembea na mke wa kada mwenzie wa CCM?Huu sio tu uhuni bali ni ukosefu wa maadili usioelezeka.

Angalau Chadema wanaweza kutoa excuse (ambayo inaweza isikubalike) kuwa chama hicho na viongozi wake si wakomavu wa kisiasa (kwa maana ya uzoefu) lakini tunawezaje kuelezea uhuni wa viongozi wa chama ambacho si tu ni chama tawala lakini pia kina uzoefu unaoweza kuzidi jumla ya umri wa vyama vyote vinavyoshiriki kampeni hizo?

Japo Bwana Ilyas amebainisha kuwa hawezi kutaja "mlolongo wa matukio ambayo yamepelekea baadhi ya watu kuiangalia Chadema kwa jicho la tahadhari badala ya matumaini" kwa hakika shutuma nzito anazoelekeza dhidi ya chama hicho zilipaswa kuambatana na mlolongo huo wa matukio,japo in a point form (yaani kwa kutaja pasipo kufafanua).

Naomba kuweka bayana kwamba two wrongs do not make a right.Hapa ninamaanisha kuwa 'uhuni' wa Rage na wa Waziri (katika kudili na uhuni wa Rage) haupunguzi 'uhuni' wa Chadema.


Lakini pia Bwana Ilyas anakosea kuchukulia tukio hilo lililofanywa na wafuasi wa Chadema wakiongozwa na wabunge wawili tu kuwa ni taswira nzima ya 'uhuni' wa Chadema.Mchambuzi yeyote makini hawezi kuhitimisha kuwa kitendo cha Rage kupanda na silaha jukwaani au kitendo cha Mchemba kutembea na mke wa kada mwenzie wa CCM kuwa ni picha halisi ya nidhamu mbovu ya CCM.

Lakini pia naomba ifahamike kuwa Chadema wanatambua fika mwenendo wa mambo ambapo sheria huonekana zimevunjwa pale tu wapinzani (au walalahoi) wanapokwenda kinyume na taratibu.Bwana Ilyas anafahamu fika kuwa laiti Chadema wangeamua kutoa taarifa kwa vyombo husika kuhusu 'uhuni' wa Mkuu wa Wilaya 'aliyekwidwa' kwa kukiuka taratibu za uchaguzi kusingefanyika lolote.Ushuhuda wa hili ni namna tuhuma za waziwazi za vitendo vya rushwa kwenye mchakato wa ndani wa CCM kupata wagombea wake kwenye nafasi za udiwani na ubunge katika uchaguzi mkuu uliopita ambapo tulishuhudia TAKUKURU ikichezeshwa sandakarawe,na wananchi kumwagiwa mchanga wa macho kwa baadhi ya wahusika kukamatwa.Labda Bwana Ilyas anaweza kutupa takwimu ni watuhumiwa wangapi walikwisha adhibiwa kisheria kutokana na vitendo hivyo.

Siungi mkono matumizi ya nguvu katika kudai haki,lakini ni ukweli usiopingika kuwa mara nyingi tawala dhalimu hazitowi haki pasipo kutumia msuli.Diplomasia ni njia bora zaidi ya kudai haki au kuendesha majadiliano.Lakini kwa  bahati mbaya- na naamini Bwana Ilyas anajua hilo-mara kadhaa diplomasia imekuwa kikwazo katika upatikanaji wa haki kwa haraka.Ndio maana hata Wapalestina walipowasilisha ombi lao la uanachama wa umoja wa mataifa waliweka bayana kuwa WAMECHOSHWA na danadana za haki yao kuchezewa kama privilege flani.

Laiti sheria,kanuni na taratibu zingezingatiwa,Mkuu wa Wilaya mhusika katika tukio hilo asingezifinyanga,na kwa maana hiyo asingekutana na hasira za wana-Chadema wanaodai haki yao.Marehemu Kighoma Ali Malima aliweka wazi mtazamo wake kuhusu namna haki inavyoapaswa kudaiwa.Alisema: "HAKI HAITOLEWI KAMA ZAWADI.INACHUKULIWA AU KUDAIWA,HATA KWA NGUVU INAPOBIDI."

Maandiko Matakatifu ya Waislamu (dini ambayo naamini Bwana Ilyas ni muumini wake yanasema hivi (roughly)  kuhusu jambo baya: "lisemewe vibaya...lichukiwe...na ikibidi liondolewe hata kwa nguvu." (Ninasistiza kuwa nukuu hiyo ni roughly).Sijui kwa Bwana Ilyas kama kuna jambo baya na amelichukia lakini bado lipo,amelikemea lakini linazidi kukua,hatofikia hatua ya kuliondosha hata kwa nguvu ikibidi?

Hicho ndicho kilichofanywa na Chadema.Wlilazimika kumkwida Mkuu wa Wilaya kwa vile aliamua kwa makusudi kupuuza sheria za uchaguzi na haki za vyama vingine vinavyoshiriki kwenye uchaguzi huo mdogo.Ni kweli ingependeza iwapo diplomasia ingetumika,lakini huwezi kuwa na fair play kwenye soka katika mechi ambayo timu pinzani ina wachezaji 15,yaani licha ya wale 11 wa kawaida,pia yumo refa,washika vibendera wawili na kamisaa.Au hakuna haki itakayopatikana katika kesi ambapo mshtaki au mshtakiwa pia anafanya kazi ya uendesha mashtaka,yeye huyhuyo ni mzee wa baraza,na pia ni hakimu/jaji.

Pasipo kuitihumu waziwazi,Bwana Ilyas anaihusisha Chadema na ukabila-yaani Uchagga.Amemtaja Mzee Edwin Mtei na mwenyekiti wa sasa Freeman Mbowe.Kwa makusudi kabisa,amekwepa kutaja safu nzima ya uongozi wa juu wa Chadema unaojumuisha (pasipo kufuatilia mpangilio maalum) Mchaga (Mbowe),Muha (Zitto Kabwe) na Mmbulu (Dkt Slaa).

Busara ndogo tu ingeweza kumsaidia Bwana Ilyas kubaini kuwa ushindi walioupata Chadema katika majimbo mbalimbali kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana haukutokana na ukabila.Je John Mnyika alishinda ubunge huko Ubongo kwa vile kuna Wachagga wengi?Vipi kuhusu Halima Mdee huko Kawe?

Pengine katika kuonyesha chuki yake kwa Chadema,Bwana Ilyas anaituhumu Chadema kuwa iliwezesha Mbowe (Mchagga na Mkristo) kupata uenyekiti kwa kutumia mbinu (ambazo hata hivyo ameshindwa kuzibainisha).Kwani ndugu yangu huyu ambaye ninamheshimu vya kutosha hataki kumwangalia Mbowe kama MTANZANIA na badala yake anaangalia kabila lake (UCHAGGA na dini yake UKRISTO).Huu ni ubaguzi wa waziwazi.Ni sawa kwake kuinyooshea kidole Chadema kwa kujaza Wachagga na Wakristo lakini haoni tatizo kwa kwa CUF au CCM kuwa na idadi kubwa ya Waislam kwenye ngazi za juu za uongozi wa vyama hivyo.

Bwana Ilyas,hivi hata katika karne hii bado unajadili wasifu wa watu kwa vigezo vya dini na kabila,badala ya kuangalia sifa walizonazo kiuongozi?Na kuna ubaya gani kwa chama kujaza watu wa kabila au dini moja ilhali kinawatumika wananchi ipasavyo?Je msukumo wa Chadema uliopelekea serikali ya Rais Jakaya Kikwete kushughulikia bei ya sukari kuna uhusiano gani na ukristo au uchagga?

Bwana Ilyas anaendeleza tuhuma zake dhidi ya Chadema na kudurufu madai kuwa chama hicho kinalea udini.Anadai (nanukuu)"...Kama vile hilo halitoshi, tukielekea katika uchaguzi wa rais na wabunge wa mwaka 2010 ambao CHADEMA ilionyesha muamko mkubwa katika medani za siasa nchini, CHADEMA ama kwa kudhamiria, kutokudhamiria au kwa kulazimika, wakafanya kosa jingine ambalo badala ya kuwanasua katika kiwingu cha ukabila na udini wakajikuta wanajisimika ndani ya wingu la Udini."

Katika uchambuzi fyongo,Bwana Ilyas anadai kuwa Chadema imekuwa ikitafuta uungwaji mono na Kanisa Katoliki.Lakini anajikanganya pale anapoweka wazi kwanini inawezekana kuhisi Chadema na Kanisa Katoliki ni "damu damu" anaposema, "Hili lilikuja ama kutokana na kanisa hilo kama watanzania wengine kuchukizwa na maovu na usaliti wa Chama cha Mapinduzi (CCM)..." Kwa hiyo ni wazi kuwa chuki ya Kanisa Katoliki dhidi ya maovu yaliyokuwa yanafanywa na CCM ilishabihiana na ajenda za kupinga maovu zilizotawala kampeni za Chadema.Huu nao ni udini?

Lakini anageuka tena na kuirushia kombora Chadema kwa kudai "...au kutokana na dalili za uwezekano wa ushindi wa uhakika wa mgombea Urais wa CHADEMA ambaye ni kiongozi wa kiroho na aliyekuwa mtumishi wa ngazi za juu wa chombo nyeti cha kanisa hilo." Hivi Bwana Ilyas anataka kutuambia kuwa hadi leo hafahamu kuwa Dkt Willbrod Slaa si kiongozi wa kiroho?Aua ameamua wka makusudi kuwaiga Daily News na Habari Leo walioamua kumtambulisha Dkt Slaa kama PADRE?

Ni kweli,kiongozi huyo wa Chadema aliwahi kuwa Padre (na upadre si uhalifu kiasi cha kujenga negative connotation) lakini aliamua kuacha nafasi hiyo na kujikitka kwenye siasda.Kuendelea kumwita kiongozi wa kiroho ni sawa na kumtambulisha Kikwete kama kiongozi wa jeshi japo alishaacha uanajeshi zamani hizo.

Bwana Ilyasa anafanikiwa vizuri kuweka tatizo lake la UDINI (ambao ironically anautumia kuishutumu Chadema) anapodai "Kitendo cha viongozi wa kanisa la Katoliki kuanzisha na kuendeleza mpambano mkali wa majukwaani na katika alteri za kanisa kuwashutumu viongozi wa chama tawala cha CCM na serikali yake inayoongozwa na Rais na Mwenyekiti Muislamu, kabla na hata wakati wa uchaguzi huo kilijenga mtazamo wa kuwa kanisa hilo na hivyo wafuasi wake walipaswa kuiepuka CCM na wagombea wake na hivyo kuashiria kuwa CHADEMA ndio chaguo lao."

Naomba kumfahamisha Bwana Ilyas kuwa mtazamo huo ni wa makengeza.Kanisa lilikuwa na linaendelea kukemea maovu bila kujali yanafanywa na muumini wa dini gani.Kwani wakati Kanisa linaikemea CCM kuhusu ufisadi,Waziri Mkuu wa serikali ya CCM hakuna Mkristo?Ina maana Bwana Ilyas anataka kutuaminisha kuwa Kikwete (Muislam) ndio CCM?Au kwa lugha nyingine,tunaposhutumu ufisadi ndani ya CCM tunaushutumu Uislam kwa vile tu mwenyekiti wa chama hicho ni Muislam?Na Bwana Ilyas anasemaje kuhusu Muislam Zitto Kabwe anapokemea ufisadi akiwa ndani ya 'chama cha Wachagga na Wakristo Chadema'?

Bwana Ilyas anaendelea kuuthibtishia umma jinsi udini unavyomkwaza kufanya uchambuzi usio wa kibaguzi kwa kuwashutumu Chadema kumdhalilisha "mwanamama wa Kiislam na hijabu yake." Hapati shida kuepuka kuzungumzia wadhifa wa mwanamama huyo bali inakuwa rahisi kwake kumtambulisha kwa dini yake na vazi lake la kidini.Ni hivi,si Uislam au hijab itakayompendeza Laah pasipo kutenda yale atakayo kama ambavyo si upadre au kutembea na Rozari Takatifu kutakakomfanya Mkristo afikie uzima wa milele.Kama DC huyo alikuwa mcha Mungu halisi basi angefuata maagizo ya kidini ya kutii mamlaka za dunia.Angezingatia taratibu za uchaguzi zinasemaje badala ya kukurupuka na vikao vya kizushi ambavyo kimsingi vililenga kuitengenezea CCM mazingira ya ushindi.

Pamoja na mazingaombe yanayoendelea kuhusu dhana ya kujivua gamba ndani ya CCM, Bwana Ilyas anadiriki kukisifu chama hich akidai kuwa hiyo ni hatua ya kwenda mbele kufuatia matokeo yasiyoridhisha sana katika uchaguzi mkuu uliopita.Ninapenda kuamini kuwa ndugu yangu huyu ana uwezo kubwa wa kujenga hoja lakini amnakwazwa na hisia binafsi.Hilo gamba lililowishavuliwa na CCM ni lipi?Kujiuzulu kwa Rostam Aziz?Ni Rostam huyuhuyu aliyesafishwa na Kikwete kwenye kampeni za uchaguzi mkuu mwaka jana na ambaye leo anatumika kuipigia debe CCM huko Igunga?

Na kama kujivua gamba,vipi mbona Mzee wa Vijisenti Chenge na mwenzie Lowassa bado wapo madarakani huku tukiendelea kusikia kauli za kujikanganya kuhusu suala zima la CCM kujivua gamba?

Nimalizie makala hii kwa kumsihi Bwana Ilyas kwamba ili aweze kuiangalia Chadema vizuri anapaswa kuweka kando hisia zake za udini.Na kama anataka kutumia hoja za udini basi asichelee kuzungumzia pia namna CCM inavyowatumia baadhi ya Waislam kwa manufaa ya kisiasa (na hapa wa kulaumiwa ni Waislam haohao ambao mwaka 2005 waliingizwa mkenge na akina Kikwete kwa kuwaahidi Mahakama ya Kadhi huku dandana zikiendelea hadi leo).

Ushindi wa Chadema ni ushindi kwa kile asiyependa kuona Tanzania ikiendelea kuwa shamba la bibi kwa mafisadi.Chadema,pamoja na Bwana Ilyas kuituhumu kuwa inakumbatia udini na ukabili,imewatumikia vyema Watanzania katika muda mfupi tu ambapo imeweza kuibua ujambazi mkubwa dhidi ya taifa letu (EPA,Richmond,Buzwagi,Deep Green,Meremeta,nk).

Bwana Ilyas anapaswa kutambua pia kuwa laiti Chadema ingekuwa chama cha udini isingepiga kelel kuhusu umafia wa Richmond ambao mhusika mkuu alikuwa Edward Lowassa,mkristo ambaye amekuwa akimwaga mamilioni ya shilingi makanisani.Kadhalika,Chadema ingekalia kimya ufisadi wa Kiwira au namna Ikulu ilivyogeuzwa sehemu ya biashara na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa,Mkatoliki ambaye hakosekani kanisani kila Jumapili.

Na kelele za Chadema kuhusu umuhimu wa marekebisho ya Katiba hazikuangalia maslahi ya Wakristo bali Watanzania kwa ujumla.Kuihukumu kwa hoja mfu za udini,ukabila na uhuni hakuna tofauti na harakati za makusudi za mafisadi kumhukumu kila anayepigania haki ya Mtnzania kuwa ni mhaini,anayetaka kuvuruga amani na utulivu (wa mafisadi kufanya ulafi wa kuifilisi Tanzania,I suppose) na kukwaza harakati za kumpatia Mtanzania ukombozi wa pili.

Kama alivyoniambia msahiliwa mmoja kwenye utafiti vitendo wa kozi yangu kimasomo, "haya mambo ya Ukristo na Uislamu sana sana ni huko mijini tu,ambako napo watu wanatumia dini kama mbinu ya kumudu maisha.Huku vijijini uhaba wa maji haubagui Mkristoa au Muislam.Mgao wa umeme pia hauchagui madhehebu.Kisima cha maji kilichopom msikitini kinahudumia wanakijiji wote pasipo kuuliza kama huyu ni Hamisi au John.Vyama vya ushirika vinapotukopa mazao yetu haviangalii kama flani ni Mkristo au Muislam.Pengne matokeo ya darasa la saba au sekondari yakitoka na Waktisto wengi wamefaulu na watoto wetu wa Kiislam wamefeli ndio kidogo unaweza kusikia watu wanahoji,lakini kimsingi watoto hao,paspo kuangalia madhehebu yao wanasoma katika mazingira magumu kabisa-sakafuni na walimu wao-pasipo kuangalia madhehebu yao-wametawaliwa na manung'uniko."

Tusiwape excuse mafisadi kwa vile tu wanaongozwa na Muislam au Mkristo.Tunaweza kutofautiana katika jinsi tunavyopiga kelele kuhusu ufisadi lakini kimsingi waathirika wa dhambi hiyo ni sote.Lakini kwa vile mafisadi hawana tofauti na wakoloni waliotubagua kwa misingi ya rangi na dini,wataendelea kutumia kete za ukabila na udini kutufarakanisha ili wazidi kutufisadi.Hata hivyo sote tunajua kuwa fedha wanazotufisadi haziendi misikitini au makanisani bali zipo kwenye akaunti zao za vijisenti huku Ughaibuni,huku nyingine zikitumika kuongeza idadi ya mahekalu yao na misururu ya magari yao ya kifahari pamoja na kukuza idadi ya nyumba ndogo zao.Wahanga wao ni mimi na wewe,regardless ya tofauti zetu za kidini au kikabila.

Let's agree to disagree!

26 Sept 2011


Wajuzi wa mambo wanadai kuwa moja ya mambo yanayopunguza ufanisi wa Idara yetu ya Usalama wa Taifa ni tabia iliyoota mizizi ambapo kila kigogo anataka kumpatia mwanae,mpwae,mtoto wa rafiki yake,nk katika ajira ya taasisi hiyo nyeti.Haina ubaya kutoa ajira iwapo mwajiriwa mtarajiwa atakuwa na sifa husika.Lakini uzoefu umeonyesha kuwa kanuni na taratibu zinabemendwa makusudi ili ajira hizo ziende kwa watu wa karibu wa vigogo hao.

Kibaya zaidi ni ukweli kwamba wengi wa watoto wa vigogo wanapopata ajira kwenye taasisi kama hii ambayo msingi wake mkubwa ni uzalendo wa mtumishi husika hujiona kama 'untouchables' flani,wanafanya mambo wapendavyo,usumbufu mtaani kwa zile 'unajua mimi ni nani/nafanya kazi wapi' huku bastola zikiachwa zionekane waziwazi kama Aden Rage.Wengi wa hawa vijana hawafahamu jukumu kubwa walilonalo kwenye kila sekunde ya uhai wa Mtanzania.Don't get me wrong kuwa ninajifanya kuelewa sana mambo haya lakini ukweli ni kwamba taaluma ya ushushushu ni uti wa mgongo wa uhai wa taifa lolote lile duniani.Idara ya Usalama ya nchi ikiyumba,nchi nayo inayumba.Watu wengi hawaelewi umuhimu wa chombo hiki kwa vile kimaadili kinapaswa kufanya kazi zake kwa siri,japo watoto wa vigogo wanaona usiri huo kama kero.

Anyway,nimekutana na tangazo la ajira za ushushusu katika 'Idara ya Usalama' (wa ndani-yaani ya kuzuia ujasusi) ya Uingereza-MI5 au kwa kirefu Military Inteligence,Section 5)-ambalo limewekwa kwenye gazeti la bure la kila siku la METRO.Utaratibu huu ambao sitarajii kuuona ukiigwa na taasisi nyingi za usalama duniani,achilia mbali yetu,unaweza kusaidia sana kufanya zoezi zima la kuajiri (recruitment process) kuwa ya huru,wazi na inayowekea mkazo uwezo,ujuzi na sifa za mwombaji kazi (based on merit(s)).

Hii ni mada nyeti kwahiyo naomba niishie hapa.Ukiwa na swali,usisite kuniuliza (majibu yatategemea swali limeulizwaje).

25 Sept 2011


Mchungaji aliyetibuana na kanisa lake ameanzisha kanisa la Facebook.Mchungaji Mark Townsend (44),ameanzisha kanisa analoliita The Hedge-Church baada ya kuhitilafiana na wazee wa Church of England.

Katika kuchangisha fedha,mchungaji huyo  pia anamiliki tovuti ya kukodisha mchungaji,ijulikanayo kama Rent-a-Rev ambayo inachaji kati ya pauni 40 (Shs 102,029.40) na 150 (shs 382,610.25) kwa ajili ya kufungisha ndoa za wandandoa wa jinsia moja au wa jinsia tofauti,ibada za mazishi na ubatizo,shughuli ambazo zinafanyikia aidha msituni,majumbani au hata kwenye baa.

Kanisa hilo tayari lina waumini 416 na inaaminika kuwa ni la aina yek duniani.Misa na huduma za maombi zinafanyikia mtandaoni na waumini wanatumia ujmumbe wa baraka kila siku kutoka kwa Mchungaji Townsend.

Mwezi ujao,Mchungaji huyo ataendesha ibada ya komunio itakayoonyeshwa moja kwa moja mtandaoni (live streaming).Mark,kutoka eneo la Leominster,Herefordshire,anasema: "Niliamua mwaka jana kuachana na Church of England.Kwa miaka 10 iliyopita nimelitumikia kanisa hilo katika mahusiano ya upendo-chuki (love-hate relationship).Nililazimika kufanya mambo ambayo nilikuwa siyaamini na nilitamani sana mabadiliko.Imechukua mwongo mzima  (kipindi cha miaka 10) kwa dhamira yangu kutimia."

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily Recond la hapa Scotland toleo la jana (Jumamosi,Oktoba 24,2011)

24 Sept 2011


Huwa ninapenda kuwasilisha habari nyingi za kimataifa katika lugha yetu ya taifa Kiswahili.Unajua,tusipokienzi Kiswahili sie wenye lugha sijui nani atakayejihangaisha nacho.Ukienda Twitter ni kimombo kwenda mbele,japo angalau kwenye Facebook Kiswahili bado kinatawala.

Sasa habari ifuatayo ni ya kisayansi zaidi na kuna vitu havitafsiriki Kiswahili (au kama kuna tafsiri basi ni TUKI na BAKITA pekee wanaoweza kutafsiri kwa usahihi).Hivi unaweza kweli kutafsiri kwa Kiswahili maneno haya: Particle physicist,Neutrinos,Theory of Special Relativity,au bricks" of photographic emulsion films interleaved with lead plates?


Habari husika kwa kimombo ni hii



Faster than light particles found, claim scientists

Particle physicists detect neutrinos travelling faster than light, a feat forbidden by Einstein's theory of special relativity
Subatomic Neutrino Tracks
Neutrinos, like the ones above, have been detected travelling faster than light, say particle physicists. Photograph: Dan Mccoy /Corbis
It is a concept that forms a cornerstone of our understanding of the universe and the concept of time – nothing can travel faster than the speed of light.
But now it seems that researchers working in one of the world's largest physicslaboratories, under a mountain in central Italy, have recorded particles travelling at a speed that is supposedly forbidden by Einstein's theory of special relativity.
Scientists at the Gran Sasso facility will unveil evidence on Friday that raises the troubling possibility of a way to send information back in time, blurring the line between past and present and wreaking havoc with the fundamental principle of cause and effect.
They will announce the result at a special seminar at Cern – the European particle physics laboratory – timed to coincide with the publication of a research paper (pdf) describing the experiment.
Researchers on the Opera (Oscillation Project with Emulsion-tRacking Apparatus) experiment recorded the arrival times of ghostly subatomic particles called neutrinos sent from Cern on a 730km journey through the Earth to the Gran Sasso lab.
The trip would take a beam of light 2.4 milliseconds to complete, but after running the experiment for three years and timing the arrival of 15,000 neutrinos, the scientists discovered that the particles arrived at Gran Sasso sixty billionths of a second earlier, with an error margin of plus or minus 10 billionths of a second.
The measurement amounts to the neutrinos travelling faster than the speed of light by a fraction of 20 parts per million. Since the speed of light is 299,792,458 metres per second, the neutrinos were evidently travelling at 299,798,454 metres per second.
The result is so unlikely that even the research team is being cautious with its interpretation. Physicists said they would be sceptical of the finding until other laboratories confirmed the result.
Antonio Ereditato, coordinator of the Opera collaboration, told the Guardian: "We are very much astonished by this result, but a result is never a discovery until other people confirm it.
"When you get such a result you want to make sure you made no mistakes, that there are no nasty things going on you didn't think of. We spent months and months doing checks and we have not been able to find any errors.
"If there is a problem, it must be a tough, nasty effect, because trivial things we are clever enough to rule out."
The Opera group said it hoped the physics community would scrutinise the result and help uncover any flaws in the measurement, or verify it with their own experiments.
Subir Sarkar, head of particle theory at Oxford University, said: "If this is proved to be true it would be a massive, massive event. It is something nobody was expecting.
"The constancy of the speed of light essentially underpins our understanding of space and time and causality, which is the fact that cause comes before effect."
The key point underlying causality is that the laws of physics as we know them dictate that information cannot be communicated faster than the speed of light in a vacuum, added Sarkar.
"Cause cannot come after effect and that is absolutely fundamental to our construction of the physical universe. If we do not have causality, we are buggered."
The Opera experiment detects neutrinos as they strike 150,000 "bricks" of photographic emulsion films interleaved with lead plates. The detector weighs a total of 1300 tonnes.
Despite the marginal increase on the speed of light observed by Ereditato's team, the result is intriguing because its statistical significance, the measure by which particle physics discoveries stand and fall, is so strong.
Physicists can claim a discovery if the chances of their result being a fluke of statistics are greater than five standard deviations, or less than one in a few million. The Gran Sasso team's result is six standard deviations.
Ereditato said the team would not claim a discovery because the result was so radical. "Whenever you touch something so fundamental, you have to be much more prudent," he said.
Alan Kostelecky, an expert in the possibility of faster-than-light processes at Indiana University, said that while physicists would await confirmation of the result, it was none the less exciting.
"It's such a dramatic result it would be difficult to accept without others replicating it, but there will be enormous interest in this," he told the Guardian.
One theory Kostelecky and his colleagues put forward in 1985 predicted that neutrinos could travel faster than the speed of light by interacting with an unknown field that lurks in the vacuum.
"With this kind of background, it is not necessarily the case that the limiting speed in nature is the speed of light," he said. "It might actually be the speed of neutrinos and light goes more slowly."
Neutrinos are mysterious particles. They have a minuscule mass, no electric charge, and pass through almost any material as though it was not there.
Kostelecky said that if the result was verified – a big if – it might pave the way to a grand theory that marries gravity with quantum mechanics, a puzzle that has defied physicists for nearly a century.
"If this is confirmed, this is the first evidence for a crack in the structure of physics as we know it that could provide a clue to constructing such a unified theory," Kostelecky said.
Heinrich Paes, a physicist at Dortmund University, has developed another theory that could explain the result. The neutrinos may be taking a shortcut through space-time, by travelling from Cern to Gran Sasso through extra dimensions. "That can make it look like a particle has gone faster than the speed of light when it hasn't," he said.
But Susan Cartwright, senior lecturer in particle astrophysics at Sheffield University, said: "Neutrino experimental results are not historically all that reliable, so the words 'don't hold your breath' do spring to mind when you hear very counter-intuitive results like this."
Teams at two experiments known as T2K in Japan and MINOS near Chicago in the US will now attempt to replicate the finding. The MINOS experiment saw hints of neutrinos moving at faster than the speed of light in 2007 but has yet to confirm them.
• This article was amended on 23 September 2011 to clarify the relevance of the speed of light to causality.
CHANZO: The Guardian


Setalaiti 'chakavu' yenye ukubwa unaolingana na basi la abiria inatarajiwa kuanguka duniani kutoka angani muda wowote hivi sasa.Awali setalaiti hiyo ya Shirika la Mambo na Anga la Marekani (NASA) ilitarajiwa kuanguka duniani usiku huu (kwa saa za hapa Uingereza ambazo ni masaa mawili mbele huko nyumbani Tanzania) lakini inaelekea itachelewa kutokana na kasi mwendo wake kupungua.

Inaonekana kuwa vumbi linalotoka kwenye setalaiti hiyo linatarajia kuangukia Amerika ya Kaskazini japokuwa bado uwezekano huo ni mdogo.Setalaiti hiyo 'chakavu' ina uzito wa zaidi ya nusu tani (tani moja ni kilo 1000).Awali NASA walieleza kuwa setalaiti hiyo isingeweza kuangukia Amerika ya Kaskazini lakini taarifa zilizopatikana baadaye zimeonyesha kuwa hadi sasa haifahamiki chombo hicho kitaangukia sehemu gani duniani.

"Kuingia (kwa chombo hicho) duniani kunatarajiwa kutokea Ijumaa ya tarehe 23 Septemba (jana kwa saa za hapa), au mapema Jumamosi tarehe 24,mchana kwa saa za Mashariki ya Marekani (masaa matano mbele kwa saa za hapa au masaa saba mbele kwa saa za huko nyumbani)" ilieleza taarifa ya NASA.

NASA inatarajia vipande 26 vya chombo hicho,vyenye jumla ya kilo 532 vitabaki vimefungamana na kuanguka duniani.Vipande vidogo vidogo vya chombo hicho vinatarajiwa kusambaa kwa umbali wa maili 500 katika uso wa dunia.Kutegemea ukubwa wake,vipande hivyo vinatajiwa kuanguka duniani  kwa kasi ya kati ya maili 55 (kilometa 90) kwa saa  na maili 240 (kilometa 385) kwa saa.

Vituo vya rada sehemu mbalimbali duniani vinafuatilia safari ya chombo hicho lakini kuna uwezekano mdogo wa kutabiri vipande vipande vyake vitaangukia wapi.Matarajio ya wanaanga ni kuona vipande vipande vya chombo hicho vikiangukia baharini (na hivyo kuepusha madhara yoyote kwa wanadamu na mali zao).

Habari njema ni kwamba uwezekano wa vipande vipande vya chombo hicho kukuangukia ni takriban 1 kwa trilioni 20 (1:20,000,000,000,000)

NASA wanashauri mtu yeyote atakayeona vipande kutoka katika chombo hicho kutovigusa bali awasiliane na mamlaka husika (polisi kwa Marekani).Kwa mujibu wa mikataba ya kimataifa inayosimamiwa na Umoja wa Mataifa,kila kipande kitakachoanguka popote pale kinapaswa kurekjeshwa kwa mmiliki wake,yaani NASA.

Sasa kwa wale wanaofanya biashara za chuma chakavu wakiona vipande hivyo na kuvifanya dili watakuwa wanajitafutia kesi za bure na NASA na Wamarekani kwa ujumla.Well,hiyo ni changamsha-baraza,lakini ni matumaini yetu sote kuwa kuanguka kwa setalaiti hiyo hakutakuwa na madhara yeyote kwa wanadamu popote pale walipo.

Habari hii imetafsiriwa kwa ufupi kutoka gazeti la Guardian la hapa Uingereza

23 Sept 2011


Hatimaye mfungwa maarufu kuliko wote nchini Tanzania kwa miaka ya hivi karibuni,Bwana Amatus Liyumba ameachiwa huru leo.Haijafahamika kama amemaliza kifungo,au amepewa msamaha wa Rais au muda wa kipindi cha maigizo umekwisha.

Na kwa vile fisadi huyu ameachiwa,je wewe mlipakodi umenufaika vipi na kifungo chake?Sikuwahi kusikia kuwa fedha alizokwiba zilitaifishwa,ikimaanisha kwamba anaweza kabisa kutumia jeuri ya fedha hizo kwa kufuru ya kukufanya utamani angeendelea kuzeekea jela.

Na kwa vile habari za kifungo chake huko jela zilikuwa za siri,hatuna uhakika kuwa alikuwa mfungwa wa kawaida-kwa maana ya kutopewa huduma za ki-V.I.P au hata kuwa analala nyumbani kisha asubuhi anarejea jela.

Anyway,kwa sasa habari ndio hiyo.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.