15 Dec 2011


Call off the search, Mr Perfect does not exist: Poll of 2,000 women failed to find ONE woman who was completely happy with her man



Ladies searching for Mr Right, look away now. The ‘perfect man’, it seems, does not exist.

While many chaps have positive attributes, the majority are deeply flawed.

In fact, in a study of 2,000 women, most ranked their partner as only 69 per cent perfect.

Included in a list of 20 common shortfalls are failing to make an effort with their partner’s friends, criticising their driving and the inability to multi-task.

Other male failings include leaving the toilet door open, watching too much sport and poor personal grooming.

Nikki McReynolds, marketing director for Remington, which commissioned the study, said: ‘It seems women are quite realistic on what they look for from their partner.

‘While they might happily overlook a few common flaws, there are certain behaviours that men just won’t get away with.’ 

The research found a third of women will turn a blind eye to their man watching too much sport – as long as they listen to them when it counts.

'He would be perfect, but he's got a beard'
But one in five women is convinced her mischievous partner only pretends to listen to them, while others believe it’s ‘in one ear and out the other’. 

Thankfully, one in five would forgive leaving the toilet seat up, while the leniency also stretches to those who don’t help with the cooking.

A quarter of women said dodgy dancing was forgivable, but bugbears such as clothes being left on the bedroom floor and snoring can count against men. 

And guys beware: Leaving the toilet dirty, not making an effort with their partner’s family and using her toothbrush are definitely big no-nos.

Leaving out nail clippings, growing a scruffy beard or being too much of a mummy’s boy are other sure fire ways to guarantee ‘imperfection’. 
When asked what would make the perfect man, a good personality came top, followed by a sense of humour and looks.

Miss McReynolds said: ‘The average guy may not be able to compete with the image of a David Beckham, but there are still a number of small changes they can do to make a big difference.’

TOP 20 IMPERFECTIONS IN MEN...

1. Not getting on with her family
2. Using her toothbrush
3. Leaving the toilet dirty
4. Hating her friends
5. Not being good with children
6. Being lazy
7. Having a big bushy beard that you never shave
8. Leaves nail clippings out
9. Driving like a boy racer
10. Being grumpy
11. Being a mummy's boy
12. Using the toilet with the door open
13. Leaving dirty washing on the floor
14. Unkempt facial hair
15. Criticising her driving
16. Burping or farting
17. Not liking dogs
18. Not helping with washing up
19. Watching too much sport
20. Not helping with the cooking

SOURCE: Daily Mail

14 Dec 2011

Whoever wrote the political rulebook needs to start rewriting it. It used to be an iron maxim that voters' most vital organ was neither their head nor their heart, but their wallet. If they were suffering economically, they'd throw the incumbents out. Yet in Britain a coalition presiding over barely-there growth, rising unemployment and forecasts of gloom stretching to the horizon is holding steady in the opinion polls, while in the US Barack Obama is mired in horrible numbers – except for the ones showing him beating all-comers in the election now less than 11 months away. Even though the US economy is slumped in the doldrums, some of the country's shrewdest commentators make a serious case that Obama could be heading for a landslide victory in 2012.

How to explain such a turnaround? In the United States, at least, there is one compellingly simple, two-word answer: Fox News.

By any normal standards, Obama should be extremely vulnerable. Not only is the economy in bad shape, he has proved to be a much more hesitant, less commanding White House presence than his supporters longed for. And yet, most surveys put him comfortably ahead of his would-be rivals. That's not a positive judgment on the president – whose approval rating stands at a meagre 44% – but an indictment of the dire quality of a Republican field almost comically packed with the scandal-plagued, gaffe-prone and downright flaky. And the finger of blame for this state of affairs points squarely at the studios of Fox News.

It's not just usual-suspect lefties and professional Murdoch-haters who say it, mischievously exaggerating the cable TV network's influence. Dick Morris, veteran political operative and Fox regular, noted the phenomenon himself the other day while sitting on the Fox sofa. "This is a phenomenon of this year's election," he said. "You don't win Iowa in Iowa. You win it on this couch. You win it on Fox News." In other words, it is Fox – with the largest cable news audience, representing a huge chunk of the Republican base – that is, in effect, picking the party's nominee to face Obama next November.

This doesn't work crudely – not that crudely, anyway. Roger Ailes, the Fox boss, does not deliver a newspaper-style endorsement of a single, anointed candidate. Rather, some are put in the sunlight, and others left to moulder in the shade. The Media Matters organisation keeps tabs on what it calls the Fox Primary, measuring by the minute who gets the most airtime. It has charted a striking correlation, with an increase in a candidate's Fox appearances regularly followed by a surge in the opinion polls. Herman Cain and Rick Perry both benefited from that Fox effect, with Newt Gingrich, the former House Speaker, the latest: in the days before he broke from the pack, Gingrich topped the Fox airtime chart. Meanwhile, Mitt Romney cannot seem to break through a 20-to-25% ceiling in the polls – hardly surprising considering, as the league table shows, he has never been a Fox favourite.

But it works in a subtler way than the mere degree of exposure. Fox, serving up constant outrage and fury, favours bluster over policy coherence. Its ideal contributor is a motormouth not a wonk, someone who makes good TV rather than good policy. Little wonder it fell for Cain and is swooning now for Gingrich – one of whom has never held elected office while the other messed up when he did, but who can talk and talk – while it has little interest in Romney and even less in Jon Huntsman, even though both have impressive records as state governors. The self-described conservative journalist Andrew Sullivan says that the dominant public figures on the right are no longer serving politicians, but "provocative, polarising media stars" who serve up enough controversy and conflict to keep the ratings high. "In that atmosphere, you need talk-show hosts as president, not governors or legislators."

Fox News and what Sullivan calls the wider "Media Industrial Complex" have not only determined the style of the viable Republican presidential candidate, but the content too. If one is to flourish rather than wither in the Fox spotlight, there are several articles of faith to which one must subscribe – from refusing to believe in human-made climate change, and insisting that Christians are an embattled minority in the US, persecuted by a liberal, secular, bi-coastal elite, to believing that government regulation is always wrong, and that any attempt to tax the wealthiest people is immoral. Those who deviate are rapidly branded foreign, socialist or otherwise un-American.

Some wonder if it was fear of this ultra-conservative catechism that pushed a series of Republican heavyweights to sit out 2012. "The talent pool got constricted," says David Frum, the former George W Bush speechwriter who has been boldest in speaking out against the Foxification of his party. Fox sets a series of litmus tests that not every Republican can or wants to pass.

This affects those who run as well as those who step aside, setting the parameters within which a Republican candidate must operate. What troubles Frum is that it pushes Republicans to adopt positions that will make them far less appealing to the national electorate in November, with Romney's forced march rightward typical. Even if Romney somehow wins the nomination, he won't be "the pragmatic, problem-solving Mitt Romney" of yore, says Frum, but a new Foxified version. It was this process that led the former speechwriter to declare last year: "Republicans originally thought that Fox worked for us – and now we're discovering we work for Fox."

So far, so bad for the Republicans. Why should anyone else care? Because the Fox insistence on unbending ideological correctness turns every compromise – a necessary staple of governance – into an act of treachery. The Republican refusal, cheered on by a Fox News chorus, to raise the US debt ceiling this summer, thereby prompting the downgrading of America's credit rating, is only the most vivid example. The larger pattern is one of stubborn, forced gridlock, paralysing the republic even now, at a moment of global economic crisis.


The problem is compounded by a wilful blindness towards the facts. Ari Rabin-Havt of Media Matters says Fox has created a "post-truth politics", which is happy to ignore and distort basic empirical evidence. To take one example, Fox pundits constantly repeat that "53% of Americans pay all the tax". In fact, 53% pay all the federal income tax – but many, many more pay so-called payroll taxes. It's hard for a nation to make the right policy decisions if the public is misled on the basic facts. And misled they certainly are. A series of surveys has proven that Fox viewers are woefully ignorant of current affairs, the latest study revealing that it is actually better to consume no news than to watch Fox: you end up better informed.

The extremism, anger, paranoia and sense of victimhood that Fox incubates are all unhealthy for the United States. But it's inflicting particular damage on the Republican party, which could well lose a winnable election because of its supine relationship to a TV network. It turns out it is not liberals who should fear the Fox – it's conservatives.

SOURCE: The Guardian

13 Dec 2011


Two weeks ago Nikki Mbishi dropped his debut album “Sauti ya Jogoo”, which surprised many of us. Having heard 4 or 5 hit singles before Jogoo hit the streets, most of us were not certain if Nikki still had enough Punchlines, and most importantlyChapters, in his tank to fill up the 22-track album.
Those who have listened to Sauti ya Jogoo will happily testify “Hakuna Mbishi kama Nikki!”
We have the luxury to hear from two reviewers, Bahati and Ender. What kept them fascinated? What are the strengths of Nikki Mbishi and particularly his debut album? Are there any shortcomings? Is it a classic album? How do they rate Sauti ya Jogoo, lyrically and production-wise?
BAHATI
Sauti ya Jogoo is driven by the adrenaline inside Nikki Mbishi; with well-chosen similes and metaphors patiently sewn together, flowing throughout the album, while Duke Tachez’s production accompanies the energy that sends chills, to both language fanatics and street stories enthusiasts. Each song is like a Chapter, provoking array of emotions, while engaging different subject matters — from stories of political and social activism to those about life.
Nikki’s voice reveals emotions, letting his descriptive lyrics paint-brush the images. This is one of the strengths of this album, apart from Duke’s melodies that serve as soundtracks to every scene. Nikki invites the listener to feel the emotions in his songs for themselves. The emotions are hidden inside the metaphors, something that demands full attention. And it is for this reason the album could be placed in the ‘timeless hip hop album’ category, because no song can be fully understood in one listening session.
The song “Kijusi”, which is my personal favorite, embodies Nikki’s brilliance in story-telling. Nikki raps about teenage pregnancy, a subject that is common, but adds his own twist, by rapping from the perspective of the real victim, whose voice usually goes silent — “kijusi”, the aborted zygote. The emotions captured by the saxophone add to the pain and sorrow in this tragic story. The creativity in this song deserves its rightful recognition. Rap meets poetry, with Nikki rapping and Dannie Sepetu doing Spoken Word on the hook. Whether this rare blend of rap and spoken word in Bongo Hip Hop is intentional or accidental leaves me curious. But it definitely makes the song extra special, creatively.
“Nimezama”, almost like a fast forwarded “Kijusi”, is a story of being born, but still ends up aborted by life. The struggles of a young man, who is trying to make ends meet, ends up in prison, without knowing that what he was doing was actually a crime. This theme of intentional or accidental seems to curve this album’s personality, even with how the songs are positioned; from “Playboy” which directly connects to “Au”, then “Kijusi” that is later followed by “Nimezama”. Just like Nikki’s metaphors that may sound accidentally placed if listened in a hurry, it’s something that creates the mystery and the curiosity, just like how the songs are placed, feeding into the appetite of wanting to listen to the songs again and again, to better understand Nikki’s chain of thoughts, hoping it will help to decipher the mystery.
Sauti ya Jogoo is not exhausted by too many collaborations; something that makes Nikki Mbishi both vulnerable while at the same time giving him an opportunity to prove himself. However, this album legitimizes Nikki Mbishi’s excellence as an emcee. The journey into different emotions in one album, without losing his audience, is one of the highlights of this album. I find myself, having to listen each song carefully, fascinated; as Nikki manages to engage us to listen to his powerful stories. Both his command of Swahili language and its use show how rich the language is, and the special relationship it has in Hip Hop music.
For old school Bongo Hip Hop heads, Sauti ya Jogoo would remind the audience of those good old days, while adding some controversies as it is the norm in Hip Hop. His song “Malimwengu” reminds me of Solo Thang’s “Homa ya Dunia”. While “Punchlines” starts with a controversial line, “Kivipi Nikki wa Pili, wa kwanza hajulikani; wakili unakosa dili, kwa stanza hatulingani”, shots fired or not, again Nikki does a tremendous work of making his audience having to listen bar by bar, metaphor by metaphor, to decipher the puzzle, without boring anyone in the process.
There is a Chapter for everyone in Sauti ya Jogoo, only time will tell as you listen from one track to the next. The only contradiction in the album is, as the last song draws to an end, you would realize your Wait Has Not Been in Vain, because the album delivers both Duke’s composition at the highest level and Nikki Mbishi’s lyrical supremacy. So, what is the message this album seems to communicate to the Bongo Hip Hop scene – it is clear; evolve or become extinct, because the crows of this roaster have just started.

Sauti ya Jogoo is a work of art, a modern day Tanzanian Hip Hop classic. I can honestly testify that, Sauti ya Jogoo is one of the top 10 Hip Hop albums I have listened to this year. And if you are a Hip Hop fan (which I suspect you are since you are reading this), then you know there have been great albums in 2011; which I term “The Year of Hip Hop Resurrection”… No, I did not term it as such as a thought while listening to this album.
Bahati has done a great job explaining what makes this a good album. Still, it remains to be seen if it is going to pass the test of time — that dreaded “replay value”. I personally think it is going to be just fine, because there is a joint for every occasion and everyone on this album. This by itself is a monumental achievement. I have seen great lyricists try to please everyone, resulting in great pool of dog sh*t – I am taking about the Jadakisses of this game.
How did Nikki accomplish this? It is simple. One word: “Production”. The album is versatile in subject matter and flows (I swear the flow on “Malimwengu” reminds me of the old Nigga Jay aka Prof. Jay of Hard Blasters Crew), but the consistency in production and focus on sound is what gels the album together. Nikki has a good ear for beats (something often ignored by most emcees), and it does not hurt to have people like Duke and Den Texas in your arsenal of producers.
This will not be a good review if I do not point out the “shortcomings”. We do not want Nikki, Duke and the whole M-Lab crew to stop improving and striving for perfection.
Two things drag this album a bit. Mind you, these are all very subjective. Firstly, the album is on the long side — 22 tracks of which 18 are actual songs. To their credit, it does not feel that long and this is the testament to the songs that made it. But it still feels songs like “Playboy” are there purely for the commercial aspect of the project. This particular song is not helped by the video as the whole acting out of lines from the song was way too much.
Track sequencing also needs some work. I am not sure who thought starting with love songs to the album titled Sauti ya Jogoo was a good idea. It is not. The song “Au’ is one of my favorites but its placement leaves a lot to be desired. Then again, the same people who did that are more likely to be the ones responsible for placing “Kila Siku” where it is, which I consider a perfect location.
“Chapter” was made to be the first track. I mean, how ill it is to have, “You already know I’m the one, among the best emcees”, as an opening line to a debut album. Plus, the beat has that intro feel. Missed opportunity indeed.
I am aware of the fact that I am really pushing it with the criticism, hence shortcomings being in quotes.
Nevertheless, Nikki has got a very strong debut with Sauti ya Jogoo. The length of the album reminds me of Reasonable Doubt, the feel is like something Common would do.
The Highs:
“Kijusi” is just off the beat and concept. The story-telling execution is an icing; “Future ni Leo”; “Punchlinez”, where Grace kills the hook; “Feedback”. “Au”… I don’t know why Duke wanted to shelf this beat; Nyakati I.
The Lows:
There are no lows really (bearing in mind “Playboy” is blocked).
Cop Sauti ya Jogoo, support Nikki Mbishi and Bongo Hip Hop. Stay tuned for the second part of the review, in which a guest content author will take us through the whole album — track by track!
Related Links:

11 Dec 2011


Ukiangalia picha hiyo juu kwa makini utabaini kuwa suruali ya Rais Kikwete ni kama inaashiria kwamba anaumwa.Of course,nusu ya juu iko kawaida (pengine kwa sababu ya bullet vest kama alikumbuka kuivaa) lakini nusu ya chini inaonyesha kama amekonda.

Inawezekana ni wembamba tu wa miguu ya Rais wetu lakini...well,nakuachia msomaji uhiimishe mwenyewe.


Mmoja ya mabloga ninaowaheshimu,Bwana Nkwazi Mhango (pichani juu) amenishushia tuhuma nzito akidai nimepokea hongo ya mafisadi kama inavyoonekana kwenye baruapepe ifuatayo (BONYEZA PICHA KUIKUZA)

Kama hukuweza kuisoma vizuri basi nainukuu hapa chini


Anonymous has left a new comment on your post "Nova Kambota: VIVA KAMANDA LOWASSA":

Chahali umenisononesha. Umeingiwa na nini hadi unampamba huyu fisadi wa kunuka? Sikuamini kuona naweka shairi langu la kumjibu huyu mtoto changudoa wa maadili wa Lowassa na ukalifuta. Kweli binadamu si viumbe wa kuamini. Hata hii futa kwa maslahi yako. Ila jua legacy uliyokwisha ijenga ina thamani kuliko hiyo hongo ya mabaki ya ufisadi.
Nkwazi Mhango


Publish
Delete
Mark as spam

Moderate comments for this blog.

Posted by Anonymous to Kulikoni Ughaibuni at 11/12/2011 01:16


Lakini cha kusikitisha ni ukweli kwamba baruapepe yenye shairi la Mhango analodai nililifuta (kutokana na hongo ya mafisadi) lilinifikia masaa mawili na dakika 31 baada ya barua pepe ya lawama.Kama ulivyoona katika picha ya hapo juu,Mhango alinitumia braua pepe ya kwanza (ya lawama) saa 7 na dakika 11 usiku kwa muda wa hapa Uingereza (angalia kulia juu kwenye email utaona imeandikwa Sent: Sun 11/12/2011 01.17).

Sasa angalia picha ya email ya shairi la Mhango hapa chini (cha muhimuni ametuma muda gani)

Kama picha inavyoonyesha,shairi la Mhango lilitumwa saa 9 na dakika 48 usiku kwa saa za hapa kama inavvoonekana katika picha hapo juu (kulia juu kuna maandishi kuhusu muda ambapo inasomekana bayana Sent on 11/12/2011 03.48

Anyway,nimekuwa nikimheshimu sana Bwana Mhango (na mmoja wa ushuhuda wa heshima yangu kwake ni makala hii ya Januari MWAKA 2008 isemayo MPAYUKAJI MSEMAOVYO...AU MSEMAKWELI? (bonyeza link kuisoma)

Tangu nianze uandishi wa blogu na makala sijawahi kupata tuhuma nzito kama hizi.Kinachosikitisha zaidi ni ukweli kwamba Mhango anafahamu fika nimetoka wapi katika vita yangu ya jeshi la mtu mmoja (one-man army) dhidi ya ufisadi.Anafahamu pia masahibu yaliyonikumba kutokana na mapambano hayo.Kwa hakika ngepaswa kuwa mtu wa mwisho kabisa kusema hayo aliyosema.Lakini kama alivyoandika mwenyewe,KWELI BINADAMU SI VIUMBE WA KUWAAMINI.

Natumaini baada ya kubaini kuwa alikurupuka kunilaumu kabla ya kuangalia vema kama shairi lake limeshanifikia,atafanya uungwana wa kuniomba samahani.

10 Dec 2011




Kikwete, Lowassa hapatoshi

Saed Kubenea's picture
Na Saed Kubenea - Imechapwa 30 November 2011
Printer-friendly versionSend to friend
HATIMAYE Edward Lowassa ametoka hadharani na kuonyesha kuwa anataka kupimana ubavu na Rais Jakaya Kikwete.
Ameeleza hadharani kuwa Rais Kikwete anahusika kwenye mkataba tata wa Richmond/Dowans; lakini pia, kuwa hafuati taratibu katika kuongoza chama chake.
Lowassa ambaye alikuwa nguzo muhimu katika mbio za urais wa Kikwete mwaka 2005, ameonekana kumgeuka waziwazi swahiba wake huyo kwa kuanika kile wachunguzi wanaita “udhaifu katika uongozi.”
Ndani ya kipindi cha siku nne, Lowassa ametoa kauli tatu nzito zinazoonyesha dhahiri ameamua kufanya mapambano na Kikwete.
Akiwa ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lowassa alinukuliwa akieleza hatua kwa hatua namna kampuni ya kitapeli ya Richmond Development Company (RDC), ilivyopewa zabuni ya kufua umeme wa dharura nchini.
Lowassa alijiuzulu wadhifa wa waziri mkuu mwaka 2008 kufuatia kashfa ya mkataba wa Richmond, kampuni iliyopewa kwa upendeleo zabuni ya kuzalisha umeme wakati haina fedha, haina uzoefu wala fedha za kufanyia kazi hiyo.
Alikiambia kikao cha NEC mjini Dodoma, “Hakuna jambo nililolifanya ambalo wewe Rais Kikwete hukulifahamu au hukunituma” kuhusu Richmond/Dowans.
Alisema, “…Mwenyekiti, natukanwa kwa ufisadi wa Richmond wakati wewe unafahamu yalichosababisha kashfa ya Richmond ni makosa ya watendaji walio chini yangu? Sasa kosa langu ni lipi? Ni kule kukubali kuwajibika kwa ajili ya serikali yangu na chama chetu? Kwa nini nihukumiwe kwa kosa hilo?”
Huku akimtolea macho Kikwete alisema, “Unakumbuka vema jinsi nilivyotaka kuvunja mkataba ule. Nilikupigia simu ukiwa nje ya nchi, lakini ukasema umepata ushauri wa kamati ya makatibu wakuu, ushauri ambao ulisababisha mkataba usivunjwe?”
Lowassa alisema Kikwete anafahamu kila kitu kwa kuwa ni yeye aliyeridhia Rostam Aziz kutafuta mbia baada ya Richmond kushindwa kuleta umeme.
“Uliponitaka ushauri wa mtu wa kutusaidia ili kuondokana na aibu ya Richmond kushindwa kutimiza mkataba wake, nilipokutajia jina la Rostam, haraka ulikubali na kusema, naona hilo ni sawa,” alieleza Lowassa kwa njia ya kumsuta Kikwete.
Hatua ya Lowassa kumuingiza Kikwete kwenye tope la Richmond/Dowans imezima moja kwa moja kauli yake iliyodai, “Siwajui wala siwafahamu wamiliki wa makampuni ya Dowans Tanzania Ltd na Dowans Holdings SA.”
Akihutubia kwenye maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa kwa CCM, tarehe 5 Februari 2011, mjini Dodoma, Kikwete alikana kufahamu wamiliki wa kampuni hiyo na kwamba hajawahi kuwaona wamiliki wake.
Alisema, “Nataka kuuhakikishia umma kwamba, sihusiki na kampuni hii. Siifahamu na wala sijawahi kuwaona wamiliki wake…Ama kweli akutukanae hakuchagulii tusi.”
Kauli ya Kikwete ya kutoitambua Dowans wala wamiliki wake, ilikuwa ni mwendelezo wa kauli kama hizo zilizokuwa zikitolewa na baadhi ya wasaidizi wake, zikilenga kumuondoa kwenye kashfa hiyo iliyomlazimu kuvunja baraza lake la mawaziri.
Akizungumzia kwa undani jinsi Richmond ilivyoingia na jinsi yeye na Kikwete walivyokuwa kitu kimoja kuhakikisha mkataba unasainiwa na kutekelezwa, Lowassa alisema, “Hakuna jambo nililolifanya ambalo Rais Kikwete hukulifahamu.”
Akizungumzia kwa undani suala hilo kwa mara ya kwanza tangu ajiuzulu wadhifa wa waziri mkuu, Februari 2008, Lowassa alisema, “Mwenyekiti kwanza napongeza uamuzi huu wa kurejesha jambo hili katika taratibu za kawaida, lakini napenda kufahamu kwa miezi saba nimetukanwa nikiitwa fisadi, watu wamezunguka nchi nzima kwa fedha za chama, hivi hatukujua kama kuna kamati hizo za maadili?”
Lowassa alikuwa akichangia pendekezo la Kamati Kuu (CC) ya CCM lililotaka kurejeshwa kwa suala la “kujivua gamba” kwenye vikao vya chini vya chama hicho baada ya watuhumiwa, isipokuwa Rostam Aziz, kukataa kuachia uongozi katika chama.
Kikwete alikiambia kikao cha NEC kuwa, uamuzi wa kutaka jambo hilo lirejeshwe kwenye vikao vya chini, umetokana na “taratibu kukosewa.”
Hata hivyo, kiongozi mmoja mwandamizi ndani ya chama hicho aliliambia gazeti hili juzi Jumatatu, uamuzi wa Kikwete kulirejesha suala la kujivua gamba kwenye vikao vya chini ulitokana na hofu ya NEC kujaa wajumbe wengi kutoka kwa kundi la Lowassa.
“Unajua mle NEC, Kikwete hana chake. Mle ndani kuna kundi kubwa la Lowassa, ndiyo maana jamaa ameogopa suala hilo la kuvuana magamba lijadiliwe,” ameeleza kiongozi huyo ambaye ni waziri katika serikali ya Rais Kikwete.
Kanuni za CCM zinaeleza kabla ya tuhuma kufikishwa NEC, sharti wale wanaotuhumiwa wapewe haki na fursa ya kujitetea mbele ya vikao vya kamati ya usalama na maadili.
Akifunga mjadala huo kwa angalizo mwanana, Kikwete aliagiza suala hilo lipelekwe kamati ya maadili ambako alitaka kuwasilishwa ushahidi wa vielelezo na siyo hujuma dhidi ya watuhumiwa.
Wakati Lowassa akishusha tuhuma kwa Kikwete, kiongozi huyo wa nchi alionekana kama amepigwa ngazi. Hakukana hata tuhuma moja miongoni mwa yaliyoelezwa na swahiba wake huyo wa zamani.
Kikwete na Lowassa, wamejitambulisha mara kadhaa kuwa ni marafiki, huku mmoja akisisitiza, “Hatukutana barabarani.”
Haijafahamika mahusiano yao yamefikia wapi kwa sasa baada ya Lowassa kumhusisha mwenzake katika kashfa ya Richmond katika kile wachunguzi wanasema amechukua tabia ya “tufe sote au tukose wote.”
Baadhi ya wachambuzi wa mambo wanasema kauli ya Lowassa ambayo ilitolewa mbele ya viongozi wake wakuu, akiwamo rais mstaafu, Benjamin Mkapa, ililenga kuonyesha udhaifu wa Kikwete ndani ya CCM kwa kuasisi falsafa ya kujivua gamba na kuikimbiza moja kwa moja kwenye CC na NEC, kinyume cha taratibu na kanuni za chama chake.
Kama hiyo haitoshi, juzi Jumapili akiwa mkoani Singida alikokwenda kusimamia harambaee ya kuchangia fedha za ujenzi wa kanisa, Lowassa alinukuliwa akisema, “Kwa vyovyote vile, nitaibuka mshindi dhidi ya vita vya kuvuana magamba.”
Akitiwa moyo na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Dayosisi ya Kati, Ushirika wa Amani, mjini Singida, Eliufoo Sima aliyesema, “suluhu ya mapambano ni kukabiliana nayo,” mwanasiasa huyo alisema, amekuwa akihusishwa na tuhuma ambazo hazina ukweli.
Askofu Sima alisema mapambano katika maisha hayatakwisha na “suluhisho siyo kuyaogopa, isipokuwa kuyatafutia majawabu kwa upole, hekima na utulivu.”
Vita vya magamba viliasisiwa na Kikwete 5 Februari 2011, kabla ya kudakwa na baadhi ya watendaji wa Sekretarieti ya CC ambao kwa miezi saba sasa, wamekuwa wakituhumu Lowassa na wenzake wawili - Rostam Aziz na Andrew Chenge – kuwa mafisadi wanaokidhalilisha chama mbele ya jamii.
Wakati hayo yakiendelea, taarifa kutoka ndani ya CC zinasema kushindwa kwa Rais Kikwete kutekeleza mkakati wake wa kumfukuza Lowassa ndani ya chama chake, kulitokana na upinzani mkali uliotokea kwenye mkutano wa CC.
“Ni kweli kabisa, ndani ya CC, Lowassa alipata uungwaji mkono mkubwa, kiasi ambacho mwenyekiti alilazimika kulipeleka suala hilo NEC. Alipofika NEC na kuona moto umekuwa mkubwa, ndipo alipoamua kuliondoa na kutaka lifanyiwe kazi kwenye vyombo vya chini,” kimeeleza chanzo kimoja cha gazeti hili.
Amesema wajumnbe wa Zanzibar, wakiongozwa na makamu mwenyekiti wa chama hicho visiwani, Amani Abeid Karume, muda wote wa mkutano walisimama imara kuhakikisha Lowassa hafukuzwi kwenye chama.
“Kuna wakati watu kutoka Bara walikuwa wanakaribia kushinda. Lakini baadaye Zanzibar wakapata nguvu pale Karume aliposimama na kusema, shutuma zote hizo hazijafuata taratibu,” ameeleza.



CHANZO: Mwanahalisi

9 Dec 2011



LEO NI SIKU MUHIMU KWANGU KWANI NINATIMIZA MIAKA KADHAA TANGU NIZALIWE.LAKINI SIKU HII NI MUHIMU PIA KWA TANGANYIKA KWANI NAYO INATIMIZA MIAKA 50 TANGU IZALIWE.


NAMSHUKURU MUNGU KWA MEMA YOTE ALIYONIJALIA,ANAYONIJALIA NA NINAYOAMINI ATAZIDI KUNIJALIA.NAWASHUKURU PIA WAZAZI WANGU-BABA MZEE PHILEMON CHAHALI NA MAREHEMU MAMA ADELINA MAPANGO KWA KUNILETA DUNIANI.LICHA YA KUNIZAA,MALEZI BORA NA MWONGOZO WALIONIPATIA TANGU NIZALIWE UMESAIDIA SANA KUNIFIKISHA HAPA NILIPO LEO.

NAWASHURU PIA NDUGU,JAMAA NA MARAFIKI KWA SAPOTI NA SALAMU ZA HERI KWA SIKU HII MUHIMU.SHUKRANI ZA PEKEE KWA MTU MAALUM ALIYENIPIGIA SIMU LEO SAA 6 KAMILI USIKU (KWA SAA ZA TANZANIA) KUNIPA SALAMU ZA BIRTHDAY.MUDA HUO,MIAKA KADHAA ILIYOPITA NDIO MUDA MAMA ALIKUWA ANAJIFUNGUA MIE (NILIZALIWA SAA 6 USIKU),NA KWA KUKUMBUKA KUNIPIGIA SIMU MUDA HUO KUNIPA HEPI BESDEI NI KAMA UMEMWAKILISHA MAMA AMBAYE KIMWILI HATUPO NAYE JAPO KIROHO YUPO NASI.

NIMALIZIE KWA KUSEMA 
HAPPY BIRTHDAY ME...
HAPPY BIRTHDAY TANGANYIKA




7 Dec 2011


Miaka 50 ya Uhuru: Kwa nini bado tu masikini, swali gumu

Evarist Chahali Uskochi

IJUMAA, Desemba 9, mwaka 2011, ni maadhinimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara. Siku hiyo pia ina umuhimu wa kipekee kwangu kwani nami ninatimiza miaka kadhaa tangu nizaliwe.

Kama ilivyokuwa mwaka jana na miaka mingine iliyopita, huwa ninadhimisha siku yangu ya kazaliwa kwa sala, sambamba na kufanya tafakuri ya kina ya wapi nimetoka, nilipo na ninakoelekea. Si kwamba kwa kutofanya sherehe ninapuuza umuhimu wa siku ya kazaliwa bali ninaamini sala na tafakuri ni namna mwafaka zaidi.

Kwa upande wa nchi yetu, miaka 50 ya uhuru inatimizwa huku wengi wa wananchi wakihoji kama tupo huru kweli. Baadhi wanakwenda mbali na kuona haja ya kuwepo uhuru wa pili kwa maana uhuru wa kwanza ulikuwa kuachana na mkoloni ilhali sasa tunasumbuliwa na ‘mkoloni mwingine’ katika taswira ya ufisadi.

Wakati mkoloni anaweza kujitetea leo kuwa alifanya dhuluma, manyanyaso na wizi wa rasilimali zetu kwa vile hakuwa na uchungu na nchi hii, ni vigumu kwa mafisadi kuwa na sababu yoyote ile zaidi ya ulafi wao na kutokuwa na uchungu kwa nchi yetu na watu wake.

Katika wiki ya maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wetu, ripoti iliyopatikana mwishoni mwa wiki inaonyesha kuwa Tanzania ni nchi ya tatu duniani kwa kuombaomba misaada na inashika nafasi ya kwanza barani Afrika. Nchi pekee zinazoitangulia Tanzania ni Iraq na Afghanistan ambazo zimegubikwa na vita kwa miaka mingi.

Lakini kinachosikitisha ni kiwango cha misaada ambacho tumekuwa tukipatiwa - dola za Marekani bilioni 2.811 (zaidi ya shilingi trilioni tatu). Unaweza kujiuliza je, fedha hizo zote zinakwenda wapi na kutuacha tukizidi kuwa masikini?

Huhitaji kufanya hesabu kupata jawabu la swali hilo kwani kwa maisha ya anasa wanayoishi viongozi wetu ni wazi kuwa hata tukipewa mara 10 zaidi ya kiwango hicho itakuwa kazi bure.

Taarifa zinaonyesha kuwa takriban asilimia 20 ya fedha hizo za misaada zinatafunwa na mafisadi. Cha kuvunja moyo zaidi, hakuna dalili kwamba wanaguswa na umasikini wetu au kuona umuhimu wa kutumia rasilimali zetu ipasavyo ili tujikwamue.

Na katika kuthibitisha hilo majuzi tumesikia taarifa kwamba posho za wabunge zimeongezwa hadi kufikia shilingi laki tatu kwa siku, japo kwa sasa kuna utata kuhusu taarifa hizo. Nchi ombaomba mkubwa kuliko zote Afrika na wa tatu duniani lakini yenye matumizi ya anasa kuzidi hata hao wanaotumwagia misaada.

Bado napata shida kuelewa kwa nini mataifa tajiri yanayotupatia fedha hizo za misaada hayaonekani kushtushwa na namna sehemu ya fedha hizo inavyoishia mifukoni mwa mafisadi huku walengwa wakiendelea kuwa masikini.

Au ni kwa vile wengi wa mafisadi wanaweka fedha walizotuibia kwenye benki zilizopo katika nchi hizo zinazotusadia na hivyo, kwa namna moja au nyingine zinakuwa kama zimerejeshwa kwao?

Nimetanabaisha hapo juu kuwa hakuna dalili zozote kwamba viongozi wetu wanaguswa na hali mbaya ya nchi yetu kiuchumi. Lakini jambo ambalo linapaswa kutunyima raha ni ukweli kwamba hali ya uchumi wa dunia ni mbaya. Kwa hiyo, iwapo nchi zinazoendelea kutusaidia licha ya fedha zao kutotumiwa ipasavyo zinaweza kulazimika kupunguza misaada yao kwetu ili kukabiliana na matatizo yao binafsi.

Na si kama viongozi wetu hawafahamu kuhusu hilo hasa ikizingatiwa kuwa wamekuwa wakizurura huko na kule kwa kisingizio cha kusaka misaada (kana kwamba balozi zetu zimefungwa). Wanafahamu vema lakini hawajali kwa vile labda hawapo madarakani kwa maslahi ya nchi na wananchi.

Kwa upande mwingine, yayumkinika kuamini kuwa viongozi hao wanaweza kuombea hali ya uchumi wa dunia izidi kuwa mbaya kwani watakuwa na kisingizio. Wasichotaka kuelewa ni ukweli kwamba mtu mwenye njaa hana cha kupoteza. Kwa hiyo, hali ikizidi kuwa mbaya masikini wa Kitanzania wanaweza kudai haki yao kwa nguvu.

Maana haiingii akilini kusikia Serikali ikidai haina uwezo wa kuboresha maslahi ya watumishi wake lakini inamudu kusikiliza vilio vya wabunge wanaopata mamilioni kila mwezi kwenye mishahara na posho zao. Wengi tunakumbuka vizuri hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa kuhusu tishio la mgomo wa wafanyakazi. Moja ya sababu alizotoa ni kwamba Serikali yake haina uwezo wa kulipa kiwango kinachodaiwa na wafanyakazi hao.

Kama sijakosea, wafanyakazi walikuwa wanaiomba Serikali iwapatie shilingi 315,000 kwa mwezi. Lakini kiwango hicho walichoambiwa ni kikubwa mno, ni zaidi kidogo tu ya kiwango kipya ya posho ya mbunge inayoelezwa kufikia shilingi 300,000 kwa siku.

Ni vigumu kubaishiri mambo yatakuwaje huko mbele lakini miongoni mwa yanayoweza kutabirika ni uwezekano wa Serikali kuishiwa uwezo wa kumudu gharama za anasa za viongozi wetu. Sasa sijui wabunge nao watatishia kugoma pindi posho zao nono zikichelewa kutoka au ikalazimika kuzipunguza.

Pengine hali hiyo ikatokea inaweza kusaidia kwa namna fulani kwani Waswahili wanasema msiba wa wengi ni harusi. Pindi wabunge watakapoonja shubiri inayotawala maisha ya kila siku ya walalahoi labda watafunguka macho na kuanza kuhoji kwa makini kwa nini tuwe masikini licha ya utajiri lukuki wa rasilimali tulionao.

Miaka 50 ya uhuru uliogubikwa na umasikini inakabiliwa na tishio jingine la kiusalama. Majuzi, akaunti ya mke wa Rais, Salma Kikwete, kwenye mtandao wa kijamii wa twitter ilikuwa hacked (yaani ‘iliingiliwa na kutumiwa na mtu asiye na mamlaka ya kufanya hivyo). Yaliyoandikwa kwenye ukurasa wa Mama Salma hayaandikiki hapa lakini kwa hakika ilikuwa ni fedheha hasa pale ilipoonekana kana kwamba mke wa Rais anamkejeli mumewe.

Hivi Kurugenzi ya Teknolojia, Habari na Mawasiliamo (Teknohama) huko Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa wapi kwa takriban saa 24 ambazo akaunti ya mke wa Rais iligeuzwa kituko? Na tukio hili la kukera lilijiri wiki chache tu baada ya akaunti mtandao wa kompyuta ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu kuhujumiwa (hacked).

Ni kweli kwamba ni vugumu kuzuwia hacking kwa asilimia 100 lakini kinachoweza kufanyika kwa watu makini ni kupunguza madhara ya hujuma hiyo kama sio kuzuwia kabisa.

Hivi kama wahuni wa mtandaoni wanaweza kuihujumu akaunti ya twitter ya mke wa Rais kuna usalama kweli kwenye nyaraka nyingine muhimu kwa usalama wa taifa letu? Hivi upungufu kama huu si ishara kuwa watu tuliowakabidhi majukumu muhimu wanazembea?

Tukio hilo linaweza kuonekana dogo na lisilo na madhara makubwa hasa kwa vile idadi ya Watanzania wanaotumia mtandao si kubwa, lakini kama wasemavyo Waingereza, jambo dogo huwa kubwa pindi likiachiwa uhuru wa kukua.

Wakati baadhi yetu tukiadhimisha miaka 50 ya uhuru wetu kuna wenzetu watakuwa wanapiga hesabu ya fedha walizofanikiwa kuchuma katika kile kinachoitwa “maadhimisho kwenye taasisi mbalimbali za umma.” Mamilioni ya shilingi yametumika kwa sherehe zilizosheheni hotuba zilizoelemea kueleza mafanikio badala ya kuwekea mkazo tathmini ya wapi tumetoka, tulipo na tunapoelekea.

Sawa, siku ya kazaliwa ni muhimu kwa anayeadhimisha lakini umuhimu huo unaweza usiwe na maana kama hautolenga kuhakikisha siku kama hiyo inajiri tena na tena huko mbele ya safari. Kama taifa, tulipaswa kufanya mjadala wa kitaifa kuhusu hatima yetu inayotishiwa kwa kiasi kikubwa na kushamiri kwa ufisadi.

Ingependeza sana kama hotuba ya Rais Kikwete katika maadhimisho ya nusu karne tangu tupate uhuru wetu angalau ijumuishe habari njema kwamba sasa anafahamu kwa nini sie ni masikini (swali ambalo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliwahi kujiuliza na hakuwa na jibu).

Hatuwezi kupata tiba ya umasiki wetu kama viongozi wetu hawajui (na hawajihangaishi kujua) kwanini sisi ni masikini licha ya kujaliwa raslimali nyingi.

Ningetamani sana kuona kuwa wakati ninasherehekea siku yangu ya kuzaliwa na nchi yangu inasherehekea miaka 50 ya kuzaliwa kwake, sote tuwe na mengi ya kujivunia tulikotoka na tulipo na pia kuona nuru ya huko mbele tunakoelekea. Kwa bahati mbaya (au kwa makusudi ya baadhi ya watu tuliowakabidhi udereva wa kutufikisha tuendako), safari ya “mwenzangu” Tanzania Bara imetawaliwa na majahili wasiojali kama atafika aendako au ataishia njiani.

Hata hivyo, nimalizie makala yangu kwa kusema HERI YA MIAKA 50 YA KUZALIWA KWA NCHI YANGU (huku nami pia nikijipa heri ya siku ya kuzaliw

3 Dec 2011


1 Dec 2011


Tatizo kuu CCM si mafisadi pekee, bali hata wanaowalea

Evarist Chahali Uskochi

HATIMAYE mchezo wa kuigiza wa “kujivua gamba” umefikia kikomo. Baadhi yetu tulihisi tangu mwanzo kuwa usanii huo haukuwa tofauti na ahadi tamu zinazosheheni kwenye kila ilani ya uchaguzi inayotumiwa na CCM kuombea kura lakini mwisho wa siku ahadi hizo huishia kuwa porojo tu.

Kuna sababu lukuki kwa baadhi yetu kubashiri kwamba kama CCM itafanikiwa kuvua magamba basi chama hicho kitakuwa katika hatari kubwa ya kupoteza uhai wake. Japo magamba yaliyopaswa kuvuliwa na CCM hayakuwa mithili ya yale ya viumbe hai lakini kimsingi kiuhalisia kung’oa gamba la kiumbe kama kobe kunaweza kabisa kupelekea kifo cha kiumbe huyo. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa chama tawala.

Kwa muda mrefu sasa Chama Cha Mapinduzi kimekuwa tegemezi sana kwa watu wenye fedha pasipo kujali watu hao wamepataje fedha hizo. Yayumkinika kabisa kuhitimisha kuwa hata utaratibu usio rasmi kwamba ili kupata nafasi ya uongozi wa kisiasa nchini-hasa kwenye nafasi za udiwani na ubunge-mgombea anapaswa kuwa na mamilioni ya fedha za kununuliwa kura ni matokeo ya CCM kukumbatia wenye fedha, na hatimaye kupelekea uwezo wa kifedha kuwa kigezo muhimu cha ushindi kwa mgombea kuliko uwezo wake kiuongozi.

Lakini sababu kubwa kabisa iliyotengeneza kifo cha ajenda ya magamba tangu siku ya kwanza ni mwasisi wa wazo hilo, yaani Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete. Japo Watanzania tunasifika kwa usahaulifu lakini naamini wengi wetu tunakumbuka jinsi Rais Kikwete alivyopigana kufa au kupona kuwapigia kampenia na kuwatetea kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita, wanasiasa ambao baadaye waliitwa magamba.

Kikwete alisisitiza kwamba wanasiasa hao ni watuhumiwa tu na hawajafikishwa mbele ya vyombo vya sheria na hivyo hakuona ubaya kusimama majukwaani kuwaombea kura. Alikwenda mbali zaidi na kunadi uadilifu na uongozi wao bora, jambo lililoibua hisia kuwa hakuwa anawasaidia tu kupata kura, bali pia alikuwa anawatengenezea kinga pindi zikitokea jitihada za kuwachukulia hatua.

Ni hivi, laiti watuhumiwa hao wa ufisadi (au magamba) wangefikishwa mahakamani wangeweza kabisa kutumia hotuba za Kikwete kwenye kampeni zao kama utetezi wa tuhuma dhidi yao kwani sote tunajua kuwa kama Rais anaamini watu hao ni safi, basi hakuna hakimu au jaji ambaye angediriki kuwa na mtizamo tofauti.

Kwa lugha nyingine, Kikwete alikuwa akiwapatia watuhumiwa hao wa ufisadi kinga dhidi ya mashtaka ndani na nje ya Mahakama. Na kama wasemavyo Waingereza, hukumu ya umma ina nguvu kubwa zaidi ya hukumu halisi inayotolewa mahakamani. Hapa ninamaanisha kwamba “hukumu ya hawana hatia hadi watiwe hatiani” iliyotolewa hadharani na Kikwete kwa watuhumiwa wa ufisadi ilikuwa na nguvu kubwa kwa umma, hasa katika mazingira ya siasa za umungu-mtu wa Rais.

Kama ambavyo mara kadhaa nimeonyesha kutoelewa anayepaswa kubebeshwa lawama katika baadhi ya maamuzi ya Kikwete ni yeye mwenyewe au washauri wake nilipata tabu kumwelewa alipojipa jukumu la “kuwabeba” watuhumiwa wa ufisadi kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita. Haikuhitaji busara kwa Rais Kikwete kutambua kuwa wanasiasa hao waliokuwa wakituhumiwa kwa ufisadi hawakuamka tu ghafla na kujikuta wanatuhumiwa bali kulikuwa na mlolongo wa matukio uliowaingia katika tuhuma hizo.

Angeweza kabisa kuepuka hali ya kuonekana anawatetea na laiti busara zingetumika basi angewaachia jukumu la kuomba kura na kujisafisha kwa umma mikononi mwao. Ndiyo maana miezi michache baadaye alipokurupuka na ajenda ya kuwashughulikia watu hao hao aliowasafisha majukwaani ilikuwa ni dhahiri kuwa usanii huo usingezaa lolote la maana.

Lakini kuna kubwa zaidi lililojiri katika vikao vya CCM vilivyomalizika wiki iliyopita mjini Dodoma. Kwa mujibu wa vyombo vya habari, mmoja wa watuhumiwa wa ufisadi aliweka bayana jinsi Kikwete alivyofanya maamuzi ambayo hatimaye yalisababisha mwanasiasa huyo kuishia kuwa mtuhumiwa wa ufisadi. Kwa lugha nyingine, mwanasiasa huyo alikubali kubebeshwa mzigo wa lawama ambao kimsingi ulipaswa kubebwa na Kikwete.

Wakati usanii wa kujivua magamba unashika kasi kwenye vyombo vya habari kulizuka msamiati mpya wa “mapacha watatu” ambao ulimaanisha wanasiasa watatu waliokuwa wakituhumiwa kwa ufisadi na ambao kimsingi ndio walikuwa walengwa wakuu wa ajenda ya kujivua gamba. Wanasiasa hao ni Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Mbunge wa zamani wa Igunga, Rostam Aziz na Mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge.

Kwa wanaofuatilia kwa karibu harakati za Rais Kikwete tangu aliposhindwa kwenye mchujo wa kupata mgombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka 1985 hadi alipofanikiwa kuingia Ikulu mwaka 1995 ni wazi kuwa “mapacha watatu halisi” ni Kikwete, Lowassa na Rostam ambao kwa pamoja, waliweza kutengeneza mtandao wenye nguvu kubwa uliompa ushindi Kikwete.

Sasa katika mazingira ya kawaida tu, ingewezekanaje Kikwete ambaye kimsingi ndiye mwenye maamuzi ya mwisho ndani ya CCM awasaliti “mapacha wenzie” Lowassa na Rostam? Naomba ieleweke simaanishi kuwa angetaka kwa dhati kufanya hivyo asingeweza.

Nimesema “mazingira ya kawaida” kwa maana ya Kikwete tunayemfahamu sote: mwanasiasa anayeonekana kukumbuka sana fadhila alizofanyiwa na watu waliomsaidia kuingia Ikulu na kiongozi ambaye anachelea sana kuwaadhibu watendaji wake hata pale ambapo kuchelea huko kunaishia kumfanya aonekane kiongozi dhaifu na mwoga wa kuchukua maamuzi magumu.

Laiti Kikwete angetaka “liwalo na liwe” dhidi ya maswahiba zake ambao baadaye alionelea wanapaswa kuchukuliwa hatua ili kuinusuru CCM basi angeweza kabisa kuitumia Idara ya Usalama wa Taifa “kuwaandama” wanasiasa hao kwa minajili ya kuwadhibiti “wasimgeuke au kumdhuru.” Kama ambavyo taarifa za kiintelijensia zinavyosukuma haki za kikatiba za wananchi kuandamana kufinyangwa, basi ingewezekana kabisa kutumia mbinu hiyo kuhakikisha kuwa “magamba yakishang’olewa hayachipui tena.”

Na wala usidhani kwamba kungekuwa na haja ya matumizi ya “mbinu chafu” kuyadhibiti “magamba” bali wahusika wangeweza kukumbushwa “Rais ni nani” kwa njia nyepesi tu ya kile kinachofahamika kama ufuatiliaji wa waziwazi (overt surveillance).

Hii ni mbinu inayotumika kumfikishia ujumbe mlengwa kuwa anafuatiliwa, wafuatiliaji hawajihangaishi kujificha bali wanataka anayefuatiliwa afahamu kuwa anafuatiliwa na hivyo kumdhibiti kufanya jambo lolote lile “baya.”

Kwa hiyo laiti mwasisi wa wazo la kujivua magamba-Rais Kikwete angekuwa na dhamira ya kweli ya kutaka mkakati huo ufanikiwe basi wala kusingekuwa na haja ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, kupita huku na kule akiwahadaa Watanzania kuhusu umakini wa suala hilo.

Sina hakika kama Nape alikuwa anafahamu “ngoma aliyokuwa anaicheza” lakini kilicho dhahiri ni kwamba muda huu anatambua kuwa “hakuna mwenye uwezo au uthubutu wa kumtenganisha Kikwete na watu ambao hakufahamiana nao mtaani (bali wametoka mbali pamoja).”

Lakini kifo cha usanii wa “kujivua magamba” kinaweza kutoa fundisho kwa CCM kuacha mtindo wa kudandia hoja za vyama vya upinzani hususan CHADEMA. Wenye kumbukumbu nzuri watakuwa wanafahamu jinsi CCM ilivyopinga kwa nguvu zote madai ya CHADEMA kuwa chama hicho tawala si tu kinakumbatia mafisadi bali pia kimegeuka kuwa kichaka cha kuwahifadhi mafisadi.

Sasa baada ya kuona kuwa CHADEMA inapata umaarufu mkubwa kutokana na msimamo wake thabiti dhidi ya ufisadi, CCM nayo ikakurupuka na ajenda ya kusaka umaarufu ikisingizia inataka kujisafisha. Lakini hata kama chama hicho tawala kungekuwa na dhamira ya dhati kutekeleza mpango huo ingewawia vigumu kufanikiwa kwa sababu ufisadi na CCM ni kama samaki na maji; ukimtoa samaki majini umemuuwa na ukiwaondoa mafisadi CCM basi umeua chama.

Nimalizie makala hii kwa ushauri wa bure kwa chama tawala. Tatizo la msingi si magamba bali aliyeyawezesha magamba hayo kukomaa. Kama ambavyo ni vigumu kudhibiti malaria kwa kugawa vyandarua na dawa za kukinga au kutibu ugonjwa huo pasipo kuangamiza mazalia ya mbu, ndivyo ambavyo ni vigumu kwa CCM kupambana na mafisadi pasipo kuwabana viongozi ambao si tu wapo madarakani kwa msaada wa mafisadi bali pia uhai wao wa kisiasa umewekwa rehani kwa mafisadi hao.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.