Tarehe 6 ya mwezi ujao,Waingereza watapiga kura katika Uchaguzi Mkuu.Kura za maoni zinaonyesha kuwa hakuna chama kitakachopata ushindi wa kutosha kuunda serikali peke yake (hung parliament).Vyovyote itakavyokuwa,kuna mambo kadhaa mbayo Watanzania wanaweza kujifunza katika uchaguzi huu hasa kwa vile nasi tutakuwa na uchaguzi hapo Oktoba mwaka huu.
Kubwa zaidi ni namna wagombea wanavyohangaika kuwabembeleza wapiga kura.Unajua kuna kijitabia cha baadhi ya wanasiasa huko nyumbani ambao sijui ni ulevi wa madaraka au dharau kwa wapiga kura,hawajihangaishi hata kidogo kuwaonyesha wapiga kura kuwa ajira zao zinategemea ridhaa za wapiga kura hao.Pengine ni jeuri ya uwezo wao wa kununua kura katika jina la takrima au kudumisha chama.
Yani hapa ukiangalia kwenye runinga namna Waziri Mkuu wa sasa,Gordon Brown,anavyopelekeshwa na wapiga kura kwa maswali mazito kana kwamba utawala wake ulikuwa mbovu kupindukia,unapata picha kuwa kwa hawa wenzetu GOOD IS NOT ENOUGH,THEY WANT EVEN BETTER (Ubora tu hautoshi,wanataka ubora zaidi).Na si kwamba Brown na Labour yake hawajafanya mambo ya maana kwa Waingereza bali watu hawa hawapendi 'kuangushwa' kwa aina yoyote ile.
Na jingine linalovutia katika kampeni hizi ni namna wapiga kura wanavyozipa manifesto za vyama umuhimu mkubwa na pengine mwelekeo wa nani watampigia kura.Kwetu,manifesto ni sawa na waraka unaokumbukwa wakati wa chaguzi na 'kinga' ya kujitetea pale mambo yanapokwenda mrama.Wengi tunafahamu namna akina Makamba wanavyotumia manifesto ya CCM kujibu shutuma mbalimbali zinazoelekezwa kwa chama hicho tawala.Hilo sio kosa bali tatizo ni kwamba utetezi huo mara nyingi hauendani na hali halisi.Kwa mfano haitoshi kusema manifesto ya CCM inatamka bayana kuhusu 'chuki' yake dhidi ya rushwa huku in practice hadi leo hatufahamu Kagoda ni mdudu gani.Matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno,so Waswahili say.
Manifesto ya CCM kwenye uchaguzi wa mwaka 2005 iliweka bayana dhamira yake ya kupata ufumbuzi wa suala la mahakama ya kadhi lakini hadi leo suala hilo linapigwa danadana.Utafiti wangu wa shahada ya uzamili kuhusu harakati za vikundi vya waislam nchini Tanzania (unaoelekea ukingoni) ambao umegusia kwa undani suala hilo unaashiria kuwa 'kupuuzia' kero (grievances) kama hiyo ya mahakama ya kadhi na suala la OIC yana potential ya kusababisha matatizo huko mbeleni.Tatizo haliwezi kutatuliwa kwa kuliepuka bali kulikabili.We have to solve difficulties before they become problems (tunapaswa kutatua ugumu kabla haujawa tatizo).
Ni matumaini ya wapiga kura wa Tanzania kuwa watatumia haki zao za kidemokrasia kwa busara zaidi kuchagua wagombea wanaoweza kuwatumikia kwa dhati.Zama za ushabiki wa vyama zimepitwa na wakati hasa kwa vile kitakachowakomboa Watanzania kutoka kwenye lindi la umaskini na ufisadi sio ushabiki bali ufanisi wa chama.
Ujumbe kutoka kwa Executive Producer Baraka Baraka (na video ya interview hapo chini)
Kwa mara nyingine tena ningependa kuwatolea Intavyu siku tuliyotembelea rasmi na world service radio katika studio zetu za Urban Pulse hapa Mjini kusoma UK tukiwa na Presenter Fred Ili kujadili Movie ya £ovely Gamble.
Pia aliweza kukutana na baadhi ya wanatimu wa lovely gamble na pia utapata comments za Steve Kanumba mwenyewe jinsi anaitwa siku hizi.
Pia unaweza kuangalia trailer ya movie inayosubiriwa kwa hamu sana Tanzania 28.4.10 club Billcanaz na hapa mji wa kusoma UK 29.5.10
BARAKA BARAKA
EXECUTIVE PRODUCER
BUZZIE PRODUCTION UK.
Kama nilivyoahidi siku chache zilizopita kuwa blogu yako ingekuletea mahojiano mengine exclusive kutoka kwa mmoja wa Watanzania wanaotuwakilisha vema,leo natimiza ahadi hiyo kwa kuwaletea exclusive interview na msanii mahiri wa Bongoflava,anayefahamika kama Mzee wa Commercial.Huyo si mwingine bali ni Ambwene Yesaya,au AY kama anavyofahamika na wengi.Kama ilivyokuwa katika mahojiano ya Mwana FA,interview hii itapatikana pia katika sura ya Kiingereza (English version).Tuaanza kwanza na WASIFU wa AY kabla ya kuingia kwenye mahojiano kamili.Pata vitu:
MSANII TANGU UTOTONI:
AY alianza kijihusisha na fani ya muziki tangu udogoni.Alipokuwa shule ya msingi alishiriki katika mashindano mbalimbali ya kutafuta vipaji na pia alitumbuiza katika hafla mbalimbali.Mwaka 1996 akiwa high school aliunda kundi la S.O.G lililojumisha wasanii watatu (akiwemo AY) na walirekodi albamu yao ya kwanza mwaka 2000.
KUKUA KISANII:
Mwaka mmoja baadaye,AY aliamua kufanya kazi za kisanii peke yake (solo) na kufyatua albamu yake ya kwanza iliyokwenda kwa jina ‘Raha Kamili’.Wimbo wa kwanza kutambulisha albamu hiyo, ‘Raha Tupu’ ulipata mafanikio makubwa na kukamata chati za vituo vya radio na runinga,na hatimaye kumtambulisha rasmi AY katika anga za muziki nchi Tanzania.
‘Machoni Kama Watu’, single ya pili (kutoka katika albamu ya ‘Raha Kamili’) iliyomshirikisha Lady Jaydee ilifanya vizuri sana kwenye chati mbalimbali za muziki na ulisaidia sana kupaisha mauzo ya albamu hiyo katika soko.
KUJIIMARISHA KISANII:
Mwaka 2005,AY alitoa albamu yake ya pili aliyoipa jina ‘Hisia Zangu’, na ‘Yule’, single ya kwanza kutoka katika albamu hiyo, ilikamata chati mbalimbali za muziki.Katika albamu hii,AY aliwashirikisha wasanii mbalimbali maarufu katika Afrika Mashariki ikiwa ni pamoja na Prezzo,Tattuu na Dexu Vultures (wote kutoka Kenya) na msanii Maurice Kirya kutoka Uganda.Hii ilisaidia sana kumtangaza zaidi AY nje ya mipaka ya Tanzania.Single yake ya pili, ‘Binadamu’,ilifanya vizuri sana ukanda mzima wa Afrika Mashariki na hatimaye kuteuliwa kugombea Tuzo za Kora,jambo lililoandika historia kwani AY ni msanii wa kwanza wa kiume kutoka Tanzania kuteuliwa kugombea Tuzo hiyo.
KUJIKITA ZAIDI KATIKA MUZIKI
Umaarufu wa AY ulizidi kuongezeka hasa baada ya kutoa albamu hiyo ya pili,na sasa alitambulika kama mmoja wa wasanii mahiri wa Afrika Mashariki.Mwaka 2006 alifanikiwa kupata mkataba wa kutangaza kinywaji (kikali) cha ‘Konyagi’ ambacho ni maarufu ndani na nje ya Tanzania.Mkataba huo ulichangia AY kutambulika zaidi kupitia matangazo ya kinyaji hicho,na ulifungua njia kwa makampuni mengine,kama Coca Cola,Vodacom,Celtel (sasa Tigo) na Kilimanjaro Lager kuingia mikataba na msanii huyo.
STAILI:
Staili ya muziki wa AY ni hip-hop inayozungumzia ishu na maisha ya Mwafrika hivi sasa.Maudhui hayo yanawasilishwa kwa ucheshi lakini pia yanaburudisha.Muziki wa AY unawagusa watu wa rika lote.
TUZO:
Msanii huyo amefanikiwa kuteuliwa katika/kushinda tuzo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania.Tuzo hizo ni pamoja na
1 Mwaka 2005 aliteuliwa kugombea Tuzo ya Kora katika kundi (category) ya Msanii Bora wa Kiume kwa Afrika Mashariki na Kati.Wimbo ulioteuliwa ni ‘Binadamu’.
2 Mwaka 2006 aliteuliwa kugombea Tuzo za Kisima (nchini Kenya) katika kundi la Msanii Bora wa Kiume kutoka Tanzania.
3 Mwaka 2007 aliteuliza kugombea Tuzo za Kilimanjaro (Kilimanjaro Music Awards) katika kundi la single bora ya hip-hop.
4 Mwaka huohuo aliteuliwa tena kugombea Tuzo za Kisima (nchini Kenya) katika kundi la video bora ya hip-hop kutoka Tanzania.
5 Mwaka 2007 uliendelea kuwa wa mafanikio kwa AY baada ya kuteuliwa pia kugombea Tuzo za Lulu ya Afrika (Pearl of Afrika) katika kundi la single bora ya hip-hop kutoka Tanzania.
6 Mwaka 2008 AY aliteuliwa kugombea Tuzo za Kilimanjaro katika kundi la collaboration (ushirikiano wa msanii zaidi ya mmoja) bora.
7 Mwaka huohuo,msanii huyo aliteuliwa tena kugombea Tuzo za Lulu ya Afrika katika kundi la msanii bora wa kiume kutoka Tanzania.
8 Katika mwaka huo,Akon-msanii maarufu duniani kutoka Marekani,alikiri hadharani kuwa anavutiwa na staili ya muziki wa AY na akamtabiria kuwa anaweza kabisa kuwa msanii kutoka Afrika atakayefanya vizuri katika anga za muziki kimataifa.
9 Mwaka huu,AY ameteuliwa kugombea tuzo kadhaa ikiwa ni pamoja na Tuzo za Muziki za Kilimanjaro (kundi la video bora na wimbo bora wa mahadhi ya Reggae),Tuzo za Teen Extra za nchini Kenya (kundi la video bora,msanii bora wa mwaka,collaboration bora ya Afrika,wimbo bora wa mwaka Afrika Mashariki,wimbo bora wa hip-hop, na msanii bora wa kiume).
10 Na hivi karibuni AY alishinda kuwa msanii bora wa Afrika Mashariki katika Tuzo za Teenez nchini Kenya.
MAFANIKIO:
Hadi sasa msanii huyo ameshajikusanyia Tuzo sita.Pia vibao vyake 14 vimefanikiwa kukamata chati mara katika ukanda wa Afrika Mashariki.Kibao chake kinachonyanyasa zaidi ni King and Queens (Wafalme na Malkia),na kimepelekea kumpatia tuzo na umaarufu zaidi kimataifa.Wakati mahojiano haya yanafanyika,wimbo wake ‘Habari Ndio Hiyo’ ulikuwa unakamata nafasi ya 10 katika chati za muziki kwa Afrika (Radio Express-Africa Chart).AY amefanikiwa kuwa msanii pekee wa Kitanzania aliyefanya collaboration nyingi zaidi na wasanii wa nje ya Tanzania ikiwa ni pamoja na Chameleone na Ngoni (Uganda),Amani,Nameless na Juacali (Kenya), P Square na J. Martini (Nigeria) na wengineo.
Uzinduzi wa albamu za AY umekuwa wa kihistoria na wenye mafanikio makubwa chini ya udhamini wa Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) na ulifanyika wakati wa matamasha ya wasanii wa kimataifa kama vile Fat Joe,Eve,Shaggy,nk nchini Tanzania.Kadhalika msanii huyo alikuwa miongoni mwa wasanii walioshiriki tamasha kubwa la kuhamasisha vita dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi (Music Against HIV/AIDS) liliodhaminiwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).Pia ameshiriki Coke Side of Life Tour kwa Afrika Mashariki,Tamasha la Vijana la Afro Arab nchini Uganda,Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar (Zanzibar International Film Festival),na Tamasha la Sauti za Busara.Kadhalika,AY amewahi kualikwa kutumbuiza wakimbiki kutoka Burundi na Rwanda kwa udhamini wa Shirika la Kimataifa la Wakimbizi (UNHCR),alitumbuiza katika sherehe za kuukaribisha mwenge wa Olimpiki nchini Tanzania,na mwaka jana alialikwa kutumbuiza katika Tuzo za Muziki za MTV barani Afrika nchini Kenya.Vilevile,msanii huyo ameshatumbuiza katika nchi mbalimbali duniani ikiwa ni pamoja na eneo la Afrika Mashariki,Rwanda,Burundi,Dubai,Afrika Kusini,Marekani na Uingereza.
NINI KIPYA?
Hivi karibuni AY amezindua tovuti yake inayopatikana katika anuani www.ay.co.tz. Pia single yake ya ‘Binadamu’ itakuwa miongoni mwa nyimbo katika albamu inayoandaliwa na kampuni ya kimaifa ya muziki,Warner Music (Africa).Kadhalika,msanii huyo ameingia mkataba wa kutangaza kinywaji (kikali) cha Waragi nchini Uganda sambamba na mkataba na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.Kwa sasa anandaa ushirikiano na wasanii wa kimataifa kama J. Martin wa Nigeria na wengineo kutoka Afrika Kusini na Marekani.
JE WAJUA?
Kwamba jina halisi la AY ni Ambwene Yesaya?
Staili ya AY ni ‘simple and casual’?
AY alizaliwa Julai 5 na nyota yake ni Kansa?
Rangi aipendayo zaidi ni bluu?
Scent (harufu ya perfume au manukato) aipendayo ni DKNY?
Na msanii anayemvutia zaidi duniani ni Dr Dre?.
MAHOJIANO KAMILI YANAFUATA (BONYEZA) HAPA CHINI . KULIKONI UGHAIBUNI (K.U): Kwanza blogu hii inatoa shukrani kwa kukubali ombi la kufanya mahojiano haya maalum. Pili, hongera sana kwa kuteuliwa na hatimaye kushinda Tuzo za Teneez Kenya 2010.Wasomaji wangependa kufahamu kwanini unajulikana kama Mzee wa Commercial
A.Y: Producer P.Funk ndio alianza kuniita hiyo baada kuwa kila nikienda Bongo Records alikuwa anaweka beats za aina tofauti na tukawa tunaflow na artists wengine so akaona kila beat naenda nayo na wengine walikuwa wanashindwa katika beats nyingine so akawa ananiita mzee wa commercial ila kwa sasa nimekuwa wa commercial ya muziki wa biashara na biashara kwa ujumla.
K.U: Laiti AY asingekuwa Mzee wa Commercial (yani usingekuwa msanii) unadhani leo angekuwa nani (katika fani gani)?
A.Y: nilikuwa na ndoto sana ya kusomea urubani na naamini ningeendelea nadhani ndoto yangu ingetimia coz nikiamua kufanya kitu naakikisha nimekifanikisha
K.U:Kitu gani kilichokusukuma kuingia kwenye fani ya muziki?
A.Y: kutokana na kusikiliza nyimbo za wasanii wengine wa nje na kuona mbona naweza kujitahidi nikafanya kama wao.
K.U: Kabla hatujagusia mafanikio yako kisanii ,nini hasa kimekuwezesha kubaki kwenye chati kwa kipindi kirefu kiasi hiki?
A.Y: bidii,nidhamu na malengo katika kazi,naipenda kazi yangu na najifunza kila siku na kukubali kuwa kila kitu kinaweza kubadilika
K.U: Tuje kwenye mafanikio yako kisanii.Licha ya kuweka historia kwa kuwa Mtanzania wa kwanza wa kiume kuteuliwa kugombea tuzo za Kora na baadaye tuzo za Kisima,kuna mafanikio gani mengine unayoyahusisha na fani ya muziki?
A.Y:Ni mengi. (Zaidi angalia wasifu hapo juu)
K.U: Miongoni mwa vilio vya wanamuziki wa Tanzania ni suala la ‘wadosi’.Kama msanii mwenye mafanikio makubwa umewezaje kupambana na suala hilo?
A.Y: hili nimeliongelea sana na sasa sihusiki nao kwa sasa naweza kusema ni tatizo sugu na linaweza kumalizika au kupungua ila naona wengi wenzangu wanaendelea kufanya biashara isiyo kuwa transparent
K.U: Nilidokezwa na Mwana FA kuhusu kampuni yako inayoshughulikia usimamizi na usambazaji wa muziki ijulikanayo kama Unity Entertainment.Wasomaji wangependa kufahamu japo kwa ufupi kuhusu wazo,maendeleo na ufanisi wa mradi huu.
A.Y:(angalia wasifu hapo juu) mpaka sasa kampuni yangu imekuwa na ni wakala wa wasanii wengi ukanda huu wa afrika mashariki kama mwana fa,shaa,nameless,j.martins wa nigeria ambae nimemleta kwenye new campaign ya zain,p.square,amani,chidi benz na wengine wengi wa afrika
K.U:Tuje kwenye ushiriki wako na hatimaye kujitoa kwenye kundi la East Coast Team.Sababu zipi zilipelekea wewe kujiengua?
A.Y: kutofautiana misimamo na malengo
K.U: Wakati ukiwa na kundi la East Coast kulikuwa na beef na wasanii wa Temeke.Je unadhani beefs zinasaidia au kudumaza maendeleo ya wasanii? (nauliza hivyo kwa sababu wakati mwingine baada ya kufifia kwa beef -kama hiyo yenu-baadhi ya wasanii nao wanafifia)
A.Y: zipo zinazojenga na zipo zinazobomoa
K.U: Je makundi (kama ilivyokuwa East Coast) yanaficha udhaifu wa wasanii dhaifu na kudumaza umahiri wa wasanii bora?(nauliza hivi kwa vile baadhi ya wana-East Coast ‘walipotea’ muda mfupi baada ya wewe na Mwana FA kujitenga):
A.Y: ni kweli kabisa,makundi mengi yakivunjika ndio mnapata ukweli kuwa nani anaweza na nani hawezi kujimanage
K.U: Unatambulika kama mwakilishi bora kabisa wa Tanzania kwenye tuzo mbalimbali za kimataifa (Kora,Kisima na sasa hii ya hivi karibuni ya Teneez 2010 huko Kenya ambapo umeibuka mshindi).Wasomaji wangependa kufahamu nini siri ya mafanikio yako?
A.Y: ni kama nilivyokwambia ni bidii na nidhamu na malengo bila hivyo huwezi kwenda mbali.na si hizo tu pia nimekuwa nominated kwa mtv awards 2009 (best hip hop artist nikiwa na jay z,kanye west na m.i)kili awards (2 categories),extra teneez awards (1category) na tuzo za Ghana zinaitwa moma (5categories-artist of the year- Africa,best male,collaboration,east African song,hip hop artist) nawaomba watanzania waweze kuvote online na kwa simu kwa walio Tanzania niweze kunyakua tuzo hizo,unaweza kugogle then upate informations
K.U: Kumekuwepo malalamiko kutoka kwa baadhi ya wasanii kuhusu baadhi ya tuzo za hapo nyumbani hususan suala la upendeleo na mapungufu katika upangaji makundi (categories).Nini mawazo yako katika suala hili?
A.Y:zingine naweza kusema kweli na kuna wakati wasanii wanatakiwa kukubali matokeo maana ukikubaki kuingia katika mashinda jua kuna kushinda na kushindwa
K.U: Ukiwa kama msanii uliyedumu kwenye fani kwa muda mrefu,unaonaje maendeleo ya bongoflava ndani na nje ya Tanzania?
A.Y: inazidi kwenda mbele na kwa sasa wanaoipeleka mbele si wengi so nawaomba wenzangu tuongeze bidii na kutengeneza network zaidi ndani na nje ya nchi
K.U: Baadhi ya kazi zako zimetengenezwa na producers wa nje ya Tanzania.Je kuna tofauti yoyote kati ya kazi zako zinazotengenezwa na producers wa nyumbani na hizo zinazotengenezwa nje?
A.Y: ni ladha hazifanani,napenda sana kuchange plava mara kwa mara kwa audio na hata video
K.U: Swali linaloshabihiana na hilo lililopita.Je kufanya kazi na producers wa nje kunaweza kumsaidia msanii kufanya vyema katika nchi anayotoka producer huyo?
A.Y: sana tu mfano mzuri ni mimi mwenyewe na producer naofanya nao na nafurahi kuona wasanii wengine wa tz wameanza kufuata nyao zangu kwa kuanza kusafiri kurecord sehemu mbali mbali na kushirikiana na wasanii wa nje maana soko limeanza kuwa la afrika na si vile zamani kuwa la kibongo tu,angalia hata charts za redio records nyingi za nje na ndani zinaingia kwa pamoja
K.U: Umewahi kushiriki kwenye fani ya filamu (ambapo ulihusika kwenye filamu ya Girlfriend).Je una mpango wa kuendelea na fani hiyo huko katika siku za usoni?
A.Y:bado sijafikiria kwa kweli kama nitafanya movie
K.U:Vipi kuhusu umodo hasa ushiriki wako kwenye matangazo mbalimbali ya biashara.Je una mpango wa kuwa full-time model licha ya muziki?
A.Y:hapana ila muda wote huwa wananunua image au sauti yangu kwa ajili ya products zao au campaign zao.
K.U: Unawezaje kumudu majukumu yote hayo (muziki, umodo, biashara) pasipo kuathiri ufanisi wako?
A.Y:na masomo pia,nasomea business administration ktk chuo cha Learn IT,mi ni mtu wajukumu tangu zamani sana so najua kuhandle pressure zote na huwa naishi kwa ratiba maalumu ambazo naziweka kwa simu na calendar yangu.
K.U: Umefanikiwa sana kuteka soko la bongoflava katika eneo la Afrika Mashariki.Nini mipango yako ya baadaye kutanua mafanikio hayo maeneo mengine ya Afrika na nje ya bara hilo?
A.Y:Nimeanza kupata bookings za S.A,DJIBOUTI,NIGERIA na ZAMBIA na pia Ethiopia so nazidi kusogea zaidi.pia natoa wimbo wangu mpya niliomshirikisha J.MARTINS kutoka Nigeria so najua itanijenga zaidi.
K.U:Kwa uzoefu wako,na kwa kuzingatia mafanikio unayopata nje ya mipaka ya Tanzania,unadhani ni jambo gani linalopelekea wasanii wengine wengi wa hapo nyumbani kushindwa kufanya vizuri kwenye anga za kimataifa?
A.Y: wengi ni wagumu kujifunza,kufanya networking.maana vile wengine wengi wa nje ya tz wanavyojituma ndio maana natumia style wazotumia wao.
K.U: Moja ya mambo yanayoisumbua Tanzania kwa sasa ni ufisadi lakini wasanii wengi wa bongoflava wamekuwa wakikwepa kuzungumzia suala hili kwenye tungo zao.Je ni sahihi kuyumkinisha kuwa mnaistarehesha jamii kwa vibao vyenu ‘vikali’ lakini mnawatenga kwa kutolipa kipaumbele suala la ufisadi kwenye tungo zenu?
A.Y: sidhani kama ukiimba ufisadi utaisha, nilichongundua ni kuwa watu hawaipendi nchi yetu ndio maana tunawafumbia macho wanaofanya ufisadi na tuna ile hulka ya kulalamika tu then hakuna hatua tunazochukua ndio maana ktuna matatizo mengi sugu tunayalalamikia tu halafu tunanyamaza
K.U: Nini mipango yako ya baadaye katika fani ya sanaa?
A.Y:kuna surprise kubwa nitawatangazia muda si mrefu naakika nitasogea/tutasogea kisanaa
K.U: Mwisho,una ujumbe gani kwa mashabiki wako na wapenzi wa bongoflava kwa ujumla?
A.Y: tuthamini na kuvipenda vya kwetu kwanza kabla ya vya wengine cz hata wao mnaona jinsiwanavyosupport vya kwao kwanza hata kama ni vibaya ila ni vyao na wanavipush sana mpaka wengine wanavikubali..
Blogu hii inakushukuru sana kwa kutumia muda wako kujibu maswali haya mengi.Pia inakutakia kila la heri na mafanikio katika shughuli zako.Na ni matarajio ya blogu na wasomaji wake kuwa tutapata fursa nyingine ya kuongea huko mbeleni.Asante sana.
ANGALIZO KUTOKA KWA AY: Nyimbo zangu na video zangu zitaanza kupatikana very soon online kupitia moja ya kampuni kubwa duniani,pia May hii nafungua duka la nguo mchanganyiko lipo sinza madukani.karibuni sana na kwa mawasiliano tutaweza kuwasiliana katika email yangu ya [email protected]. Na hapa chini ni wasifu wa kampuni ya Unity Entertainment
Waungwana,ni MwanaFA hapa..i dont usually do this kwenye blogs na sites (ku'post maoni) but naona nichangie this time since naona concerns zimekuwa za kistaarabu hapa na zina lengo la kujua tu na si vinginevyo...
Yes,nimefanya masters degree ya finance,Coventry University,ilianza January 2009 na ikamalizika January 2010,natakiwa kufanya mahafali aidha July ama November(kwa jinsi ntakavyoamua)...
Sichukui maoni yeyote kati ya haya vibaya,na pengine yanamaanisha kitu nilichofanya sio kidogo mpaka kufika mahali waungwana wanashindwa kuamini nimeweza kukifanya...
NB: na yes,nikijaliwa uhai na uwezo wa kuhudhuria mahafali ntawaletea picha...
Wasalaam...nawasilisha!!
KULIKONI UGHAIBUNI: Asante Mwana FA kwa hope ufafanuzi huu.
This day last year,at 1400,I received my miracle from the Lord.Two months earlier,I was introduced to a Houston,TX-based powerful woman of God,Apostle Esther.She taught me that when praying,I should ask the Lord for receiving,rather than seek for, my miracle because it was already there.She also gave recommended the ever powerful Psalm 91 to read every day for a number of days.And guess what,as she assured me,I eventually got something that has people waiting for up to a decade to get it, if they at all are successful.God is really Great,and this particular miracle is a living example.I would also like to thank Christha, the woman whose love and care comes only second to my mother's,for introducing me to the Apostle,and for her tirelessly efforts in praying with me.Praise the Lord,Ameen.For Christa,I dedicate the following video (though I know you don't fancy secular music).
Majuzi Rais Jakaya Kikwete alimteua Doug Pitt,mdogo wa staa wa filamu Brad Pitt,kuwa balozi wa heshima (goodwill ambassador) kusaidia kuitangaza Tanzania hususan kwenye sekta ya utalii.Kwa kuzingatia wasifu wa Doug,na umuhimu wa kuitangaza nchi yetu,uteuzi huo unastahili pongezi za kutosha.Hat hivyo,ili Doug awe na umuhimu kwa Tanzania,au uteuzi wake uzae matunda yanayotarajiwa,kuna mambo kadhaa tunayopaswa kuyaangalia kwa makini
Kwa hakika hatuna kisingizio cha kwanini nchi yetu inahitaji nguvu za ziada (kama akina Doug) katika kujitangaza.Tuna kila aina ya utajiri na vivutio ambavyo laiti tungejibidiisha kuvitangaza kwa bidii basi huenda tungekuwa mbali sana kimaendeleo.Kwa mtizamo wangu,kikwazo kikubwa ni uhaba wa uzalendo.Baadhi ya wateule wanaopaswa kuwajibika ipasavyo kulitangaza taifa letu na raslimali zake wako bize zaidi kuangalia maslahi yao binafsi badala ya kufanya kile wanacholipwa mshahara kukifanya.
Lakini kama unadhani hilo ni tatizo dogo basi kuna suala la mazingira yanayopaswa kuboreshwa ili jitihada za Doug ziweze kuwa na maana au zilete ufanisi unaotarajiwa.Kwa mfano,Doug anaweza kuhamasisha watalii waje kwa wingi Tanzania,lakini kwa ufisadi unaoendelea kila kukicha katika sekta ya umeme,ni dhahiri kuwa watalii watakaoitikia wito wa Doug wanaweza kuhisi 'wameingizwa mkenge' baada ya kukutana na adha za mgao wa umeme ambao unazidi kuzoeleka kwa Watanzania wengi.Danadana zinaendelea kuhusu kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo sugu la umeme.Na kikwazo kikubwa katika kupatikana ufumbuzi huo ni wahusika kutanguliza maslahi yao binafsi badala ya yale ya taifa.Ni katika mazingira hayo ndipo matapeli wa Richmond na Dowans walifanikiwa kutufisadi.
Kwa Watanzania walio nje watakubaliana nami kwamba kwa hawa wenzetu,'holidays' ni suala lenye umuhimu wa kipekee katika kalenda na ratiba zao.Ni matarajio ya wengi kwamba holidays walizozihangaikia kwa muda mrefu zitaacha kumbukumbu nzuri maishani mwao,na sio kugeuka 'holidays from hell'.
Kuna tatizo jingine katika suala la udokozi.Pale Mwalimu Nyerere International Airport panahitaji tahadhari kubwa ili mizigo ya msafiri itoke eneo hilo salama.Sasa kama kweli tunataka jitihada za akina Doug ziwe na maana ni vema tukafahamu kuwa pasipo kudhibiti wahuni hawa wa airport ambao inaonekana dhamira yao kuu ni kutoa 'karibu Tanzania ya majonzi' tutaishia kukimbiza watalii badala ya kuwafanya wawashiwishi ndugu na jamaa zao nao waende Tanzania kutalii.Wadokozi wengine mahiri wako Posta.Kwa vile mawasiliano yetu bado si ya kisasa sana,umuhimu wa Posta unabaki kuwa mkubwa,na si ajabu kwa baadhi ya potential watalii kutumia huduma hiyo kabla ya kwenda Tanzania,au wakati wakiwa hapo.Sasa it seems as if baadhi (au pengine most) ya watumishi wa Posta wana 'allergy' na kitu chochote chenye address ya ng'ambo.Ni lazima wafungue na wakikuta chochote 'wanakitaifisha'.
Tuna matatizo ya miundombinu.Tumeruhusu wahuni wa TRL wafanye usanii wao pasipo kuleta mabadiliko yoyote ya muhimu zaidi ya kuandika historia ya kuwa wawekezaji wa kwanza kusaidiwa na serikali kulipa mishahara ya wafanyakazi wao.Ni dhahiri kuwa laiti waliosaini mkataba wa wababaishaji hao angekuwa mzalendo wa dhati angetambua kuwa wangekuja kuikongoroa zaidi Reli ya Kati kuliko walikvyoikuta.Je watalii wakitaka kutumia usafiri wa treni kutalii inakuwaje?Huko TAZARA nako hadithi ni ileile.Na hii ni njia muhimu kwa mtalii anayetaka 'kuifaidi' hifadhi ya Selous.
Kuna tatizo la barabara zetu.Na hapa kuna suala la barabara za msimu ambazo kupitika kwake kunatarajia msimu wa mwaka.Nyingi ya barabara hizi hufanyiwa ukarabari pale tu panapokuwa na ujio wa kiongozi.Uelekeo wa kule kwetu Ifakara tuna hifadhi ya msitu asilia,lakini kufikika kwake ni mbinde msimu wa masika.
Kwa kifupi,nachojaribu kupigia mstari hapa ni umuhimu wa kuboresha mazingira yatakayopelekea watalii kuhitimisha kuwa hawakufanya makosa kukubali ushauri wa Doug kuitembelea Tanzania.Pasipo mazingira bora basi tunaweza kuteua mabalozi Hollywood nzima lakini itakuwa kazi bure.
Na jingine la muhimu zaidi ni manufaa ya ujio wa watalii kwa Watanzania.Sote tunashuhudia jitihada za kuvutia wawekezaji na mwitikio wao lakini pia sote twafahamu namna uwekezaji ulivyoshindwa kuwa na manufaa kwa Watanzania walio wengi.Makampuni ya madini yanazidi kumaliza raslimali zetu huku sie wenye utajiri huo tukibaki na mashimo matupu.Sasa Doug anaweza kulivalia njuga suala la kuhamasisha watalii,nao wakaitikia wito lakini kitakachopatikana kikaishia kwenye ununuzi wa ma-vogue,ujenzi wa mahekalu au kuongeza idadi ya nyumba ndogo za mafisadi.
Ndio maana basi,pamoja na kupongeza uteuzi wa Doug Pitt kuwa balozi wa hisani wa Tanzania huko Marekani,ni muhimu kuwekeza zaidi katika uzalendo utakaopelekea kuzalisha akina Doug wa ndani (na hakutokuwa na gharama ya kuwafuata ng'ambo) na, cha muhimu zaidi,kuchangia maendeleo ya taifa letu 'changa'.
Dressed to kill.Our sisters looking good.Picture courtesy ofMiss Jestina's Blog.(1st left ).
'SOS' Appeal!
Yea,I normally blog about politics and such stuffs,but,well,there's no harm in touching some other issues that make the world go around.I'm talking about fashion.If you happen to visit as many blogs each day as I do you certainly would appreciate that our sisters are doing quite an excellent job in blogging about different stuffs in our lives,especially fashion.However,unfortunately,most of them tend to 'forget' including men's fashion trends in their blogs.They justifiably could 'defend' themselves by arguing that it's not up to them to make sure that we look as good as they normally do.But,honestly,when you have the likes of me whose taste for fashion is as good as a blind man in a dark alley,that spells trouble,and calls for an urgent need for help.Arguably,I'm not an exceptional case as there's probably a whole bunch of guys out there who seriously need help.So,come on sisters,we all know that if what a man dresses pleases you it certainly would please the rest of the world.Could you kindly please think of us,at least once a month, when you keep your audience posted about latest fashion trends?
Picha zote hapo juu zinaonyesha maadhimisho ya 'Siku Ya Bangi Kitaifa' (National Weed Day) almraaduf '4/20' (April 20) nchini Marekani.ANGALIA HAPA kwa habari kamili na picha zaidi
Hapa chini kuna habari ambayo kama ni ya kweli basi hatma ya nchi yetu iko mashakani.Lakini kabla hujaisoma,angalia picha ifuatayo na inaweza kukusaidia kukupa uelewa wa namna tulivyofika tulipo.
KUMBE Rais Jakaya Kikwete hakusoma sheria aliyosaini kwa mbwembe. Sasa baada ya kugundua kasoro zake anataka ikarabatiwe kwa njia ya kanuni, MwanaHALISI limeelezwa.
Hilo liligundulika katika mkutano wa wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wenyeviti na makatibu wa wilaya uliomalizika wiki iliyopita mjini Dar es Salaam.
Taarifa za ndani zinasema, bila aibu na hasa kwa ujasiri wa kiongozi mkuu wa nchi, Rais Kikwete alimuuliza Philip Marmo, waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, maana ya baadhi ya vifungu katika sheria hiyo.
Lakini katika hali ambayo haikutegemewa, Marmo alijibu kana kwamba anamkejeli rais, jambo ambalo lilistua wajumbe wa kikao hicho cha juu cha utekelezaji wa sera za chama.
MwanaHALISI limeelezwa kwamba Rais Kikwete alistushwa na kifungu cha sheria kinachotaka mgombea kuwasilisha katika ofisi za msajili, taarifa ya fedha atakazotumia.
Kifungu hicho kinatoa siku saba kabla ya siku ya mwisho ya NEC kutangaza majina ya wagombea.
Kifungu kingine kinachodaiwa kumstua kinahusu idadi ya wajumbe wa kampeni. Kwa CCM, yenye hata vikundi vya ngoma na nyimbo kama ToT, kuweka timu ndogo kunaweza kupunguza shamrashamra na kuathiri kampeni.
Kwa mujibu wa mtoa taarifa, ilikuwa baada ya rais kupitia maeneo hayo, alimuuliza Waziri Marmo iwapo kile alichokuwa akifafanua kimetokana na sheria iliyopitishwa.
Naye Marmo, akiongea kwa sauti ya unyenyekevu alijibu, “…hiki ndicho ulichosaini.”
Kwa kauli ya Marmo, Rais Kikwete alionekana kustuka na kusema, kama hali ni hivyo, basi sheria itakuwa imeingilia hata mchakato wa wagombea ndani ya vyama, kimeeleza chanzo chetu.
Taarifa zinamnukuu rais akihoji kwa nini “sheria imekwenda mbali mno” na kuagiza papohapo kuwa wahusika waangalie ambapo sheria inaingiliana na watengeneze kanuni zitakazoleta nafuu.
Rais amenukuliwa akimwagiza Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutengeneza “kanuni vizuri” ili kuondoa mwingiliano unaoleta ugumu wa utekelezaji.
Hoja ya maelekezo ya sheria mpya ya gharama za uchaguzi ilikuwa moja ya ajenda za kikao cha NEC, wenyeviti na makatibu wa CCM wilaya kutoka kote nchini.
Tarehe 17 Machi mwaka huu, Rais Kikwete alisaini hadharani na kwa mbwembwe Sheria ya Gharama za Uchaguzi, ikulu Dar es Salaam ambapo hafla hiyo ilihudhuriwa na majaji, wabunge, viongozi wa serikali na vyama vya siasa, mabalozi na waandishi wa habari.
Hata hivyo, sheria hii imekuwa ikilalamikiwa na vyama vya siasa na wanaharakati, kabla na baada ya kusainiwa kuwa itakuwa ya udhibiti kwa wenye msimamo tofauti na watawala.
Aidha, siku tatu baada ya sheria hiyo kusainiwa, mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa alitupa kombora kwa kusema sheria aliyosaini rais ilikuwa na vipengele ambavyo havikujadiliwa bungeni na kwamba “viliingizwa kinyemela.”
Ubishi wa Mwanasheria Mkuu wa serikali, Jaji Frederick Werema kwamba hakukuwa na chochote kilichofanywa kinyemela ndio umekuza hoja ya Dk. Slaa na kufanya achimbue zaidi kshfa hiyo.
Katika kufukua, Dk. Slaa amekwenda hadi kwenye kumbukumbu za bunge (Hansard) na kuthibititisha kuwa Kifungu 7 (3) ambacho kimo katika sheria aliyosaini rais hakikujadiliwa bungeni na hivyo hakikurekodiwa katika hansard.
Mtunga sheria huyo kutoka Karatu amesema pia kuwa chochote kilichojadiliwa bila kuamuliwa na bunge kilikuwa kinatarajiwa tu katika kanuni au fafanuzi za au ainisho za maneno na taratibu lakini siyo katika vifungu vya sheria.
Katika majibu yake kwa kauli za Dk. Slaa, Jaji Werema alitetea serikali na kuthibitisha kuwa kifungu hicho kiliwekwa na waziri Marmo.
Dk. Slaa amesema katika andishi maalum, “Hakuna mwenye mamlaka, hata rais hana mamlaka hayo, sembuse waziri.
“Baada ya mjadala katika Kamti ya Bunge zima, maneno yakikubaliwa ndiyo hayo yanaingia kwenye sheria na serikali haina mamlaka ya kwenda kuyarekebisha inavyotaka. Ndiyo maana ya kusema ‘kifungu kimepitishwa,’ ” ameeleza Dk. Slaa.
Akiweka msisitizo, Dk. Slaa anasema, “Kitendo cha kuchomeka kinyemela ni kitendo kibaya sana na kinapaswa kulaaniwa, kwa sababu, kwa utaratibu huu wataalam wanaweza kuipeleka nchi pabaya kwa kupenyeza jambo lolote wanalotaka wao hata kama halijajadiliwa au limekataliwa na Bunge.”
Dk. Slaa anafafanua hatua ya serikali ya kuingiza mambo kinmyemela katika sheria kuwa ni kosa la jinai na kusema hata kifingu walichochomeka kinyemela kina madhara makubwa.
Kifungu kilichoongezwa na serikali kinataka timu ya kampeni kukaguliwa na watendaji wa serikali ya CCM.
“Kampeni ndiyo inayobeba mikakati na siri yote ya uchaguzi. Haiingii akilini kabisa kuwa serikali (pengine unayotaka kuiondoa kwenye uchaguzi ambayo ndio haki ya msingi ya kila mgombea) ndiyo inaweka mkono wake kwenye udhibiti wa mikakti hiyo,” anafafanua Dk. Slaa.
Anasema kuweka kifungu kama hicho ni “wenda wazimu, kwa mtu yeyote aliyefikiria jambo hilo, au anaandika tu kutoka mezani na au hajui maana halisi na majukumu yake.”
Kutokana na kuibuka kwa kashfa hii, serikali sasa imeamua sheria hiyo irejeshwe bungeni ili kufanyiwa marekebisho yanayostahili.
Naye Dk. Slaa tayari ametoa pendekezo: “Namna pekee ya kuepukana na athari hiyo ni kwa serikali kukiri imefanya makosa, na ndio ustaarabu bila kutafuta visingizio.”
Anasema serikali iwasilishe kwenye Mkutano wa 19 wa Bunge hili ulioanza jana, kitu kinachoitwa “Miscellaneous Amendment” – marekebisho ya sheria mbalimbali – na au ikichelewa sana katika Bunge la Bajeti.
Wachunguzi wa mambo wanasema Rais Kikwete atakuwa amesikitishwa sana na hatua ya wasaidizi wake ya “kumchomekea” vitu ambavyo baadaye vinamomonyoa hadhi yake kama mkuu wa nchi.
Miongoni mwa wanaotajwa kuwa wamempotosha au wameshindwa kumsaidia rais, ni pamoja na Jaji Werema ambaye ametetea uingizaji kinyemela kipengele ambacho hakikujadiliwa bungeni.
Mwingine anayetajwa ni waziri Marmo ambaye ambaye nduye hasa ametajwa kubuni na kuingiza maneno ya kifungu kinacholaaniwa.
Ni dhahiri unapokutana na kitangulizi 'http://...' unafikiri kuwa kinachofuata ni anuani ya tovuti flani.Lakini je 'http://' (kifupisho cha Hypertext Transfer Protocal)bado ina umuhimu katika mazingira ya sasa ambapo unaweza kuitambua anuani ya tovuti hata bila kitangulizi hicho? .
Wanateknolojia wa Google Chrome hawadhani kama kitangulizi hicho bado ni muhimu na wameamua kukificha katika toleo jipya la browser hiyo.
Hata hivyo,ufumbuzi huo sio rahisi kama inavyoonekana kwani unaweza kuficha kitangulizi hicho unapoandika anuani ya tovuti lakini bado kipo.Pia inatarajiwa kuwa maendeleo hayo yanaweza kuzua mkanganyiko kwa baadhi ya watumiaji wa intaneti.
Makala hii imetafsiriwa (katika tafsiri isiyo rasmi) kutoka mtandao wa Mashable
Kuna busara moja inayotuasa kuwa mpuuzi husema kwa vile anajiskia kusema (hata kama ni upuuzi) ilhali mwenye busara husema tu pale anapokuwa na kitu cha kusema (ikimaanisha kama hana cha kusema,au haoni umuhimu wa kusema kitu,atakaa kimya. Busara zaidi zinatuasa kuwa makini na tunayosema hadharani kwa vile mara nyingi jamii humtambua zaidi mtu kwa kauli zake.Sema upuuzi,utaonekana mpuuzi.Sema ya busara,utaonekana mwenye busara.Sasa kuna huyu msomi,Dokta Benson Bana,ambaye licha ya kuwa mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam,ni mkuu wa idara ya Sayansi za Siasa na Uongozi na pia ni Mwenyekiti Mwenza wa REDET.Yayumkinika kusema Dkt Bana amekuwa mahiri zaidi wa kutoa kauli zisizoendana na wasifu wake kitaaluma kuliko umahiri wa wa usomi wake
Na leo,kwa mujibu wa habari katika gazeti la Mwananchi,msomi huyo 'amelipuka' tena kwa kauli kwamba tuhuma zilizokithiri dhidi ya ufisadi zinaweza kusababisha taifa kukosa viongozi wazuri wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba.Huhitaji kuwa na hata asilimia moja ya kiwango cha elimu ya Dkt Bana kutambua kuwa tuhuma zilizotapakaa kuhusu ufisadi ni matokeo ya kuwepo kwa ufisadi.Msomi huyu anaishi Tanzania lakini yaelekea hafahamu mazingira yanayomzunguka,na hilo linaleta wasiwasi mkubwa kuhusu mchango wa wanataaluma katika maendeleo ya nchi yetu.
Katika habari hiyo Dk Bana aliwataka watu "waaache siasa chafu za kuhubiri na kudai kuwa watuhumiwa wa ufisadi hawafai kupewa kura au kuchaguliwa katika nafasi mbalimbali za uongozi kana kwamba wameshathibitika".Huu ni zaidi ya ubabaishaji wa kitaaluma,na kwa kiasi flani inaaibisha Udaktari wa Filosofia tunaohenyea akina sie.Kwanza,Dkt Bana amepata wapi mamlaka ya kuwataka wananchi waache kulalamikia ufisadi?Usomi hautoi mamlaka ya kuizuia jamii kulalamikia maovu yanayoisumbua.Pili,kwa mtizamo wa msomi huyu,kwa vile tuhuma za ufisadi hazijathibitika basi watu wakae kimya hadi 'miujiza itapotokea kwa watawala wetu kuamua kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mafisadi'!Hii ni sawa na kuingiliwa ndani na kibaka halafu ukakaa kimya kwa vile tu wewe sio chombo cha sheria.Ukifanya hivyo,hata hao polisi watakuona mpumbavu na unawapotezea muda.La kufanya ni kumdhibiti kibaka au kupiga kelele kuwashtua majirani wakusaidie kumdhibiti.
Binafsi,pamoja na kuheshimu uhuru wa kutoa mawazo,nadhani tatizo kubwa la Dkt Bana ni tabia yake ya 'kusema chochote' hata kama hana cha kusema.Inaelekea aidha hafahamu athari za tabia hiyo au anapuuza tu.Matokeo yake ni kuonekana mbabaishaji wa namna flani.Si lazima jina lake lionekane magazetini au kusikika radioni kama hana la muhimu kuieleza jamii.Eti anatuasa kuwa "si vizuri kwa watu kunyimwa kura kwa sababu ya kutuhumiwa kwa ufisadi hadi hapo watakapothibitika na kutaka wanasiasa waache kuhukumu wenzao bila kosa".Kwanini hajiulizi inakuwaje watu hao wanatuhumiwa ufisadi in the first place?Kwanini ni wao na si Dokta Bana,kwa mfano?
Hivi lipi lililo muhimu zaidi kwa Tanzania kama taifa: kukosa viongozi bora kwa vile wanatuhumiwa kwa ufisadi au kupata viongozi bora watakaowajibika kulitumikia taifa kupambana na ufisadi?Wasiwasi wa Dkt Bana ulipaswa kuwa kwenye athari za ufisadi kwa jamii na sio tuhuma za wananchi dhidi ya mafisadi.Ni mlevi tu atakayeshindwa kuelewa kuwa kinachoumiza Watanzania kwa sasa ni UFISADI na sio TUHUMA DHIDI YA MAFISADI.
Mwanataaluma huyu anaongoza taasisi ya REDET ambayo mara imekuwa ikishutumiwa kwa upendeleo inapotoa taarifa za kura zake za maoni (opinion polls) kuhusu CCM na vyama vingine vya siasa.Sina hakika kuwa matokeo ya kura hizo huwa 'yanapikwa' ili kuridhisha watawala lakini kinachozua maswali dhidi ya polls hizo ni kutoendana na hali halisi na dalili za upendeleo.
Wito wangu kwa Dkt Bana ni huu: wakati mwingine jaribu kuitendea haki taaluma yako kwa kukaa kimya pale usipokuwa na cha kuongea.Kwa kufanya hivyo,utawatendea haki pia wasomi wenzako,taasisi unazoongoza na fani nzima ya usomi.Ni muhimu pia unapotoa matamshi mazito ukajitahidi kutumia theories za kusapoti matamshi hayo badala ya kutoa hisia zenye mwelekeo wa kijiweni.
Tanzania leads the list of East African states that have lost billions of dollars to money laundering, tax evasion, government graft and other illegal operations, according to a report by a US-based financial watchdog group.
The report “Illicit Financial Flows from Africa: Hidden Resources for Development,” by Global Financial Integrity, states that the country has lost $8.9 billion over the past four decades through the illicit means. Kenya lost $7.3 billion while Uganda lost $6.4 billion over the same period.
The three East African countries thus lost a total of $22.6 billion, money that would be sufficient to wipe out their combined outstanding external debt while leaving several billion dollars available for fighting poverty and spurring economic growth.
The study points out that the impact of these losses is felt most acutely by the poorest Africans. The illicit outflow of money also “drains hard currency reserves, heightens inflation, reduces tax collection, cancels investment and undermines free trade,” the study says.
Tanzania is ranked 13th among the top 15 countries with cumulative illicit outflows after Angola, Republic of Congo, Cameroon, Côte d’Ivoire, Ethiopia, Gabon, Ghana, Madagascar, Mozambique, Nigeria, South Africa and Sudan. Zambia and Zimbabwe take the 14th and 15th positions respectively.
Already, Global Financial Integrity has started collecting signatures to petition the G20 Transparency at the G20 summit this June. The organisation is looking for 100,000 signatures from all over the world to forward to Canadian Prime Minister Stephen Harper, the current president of the G20. “Our goal is to show him the names of 100,000 people from all over the world who support ending banking secrecy, increasing financial transparency, and finally attacking the root causes of poverty.”
The report says: “So long as illicit capital continues to haemorrhage out of poor African countries over the long term at a rapid pace, efforts to reduce poverty and boost economic growth will be thwarted as income distribution becomes ever more skewed, leading to economic and political instability.”
Tanzania’s Finance and Economy Minister Mustafa Mkulo told The EastAfrican from Dodoma that in order to reverse this situation, the country has set up a Financial Intelligence Unit within the ministry to join international community in fighting money laundering and financing of terrorism.
“This problem indeed exists. At regional level, within the East African Community and the Southern African Development Community, we have seen this problem thrive for a long time and decided to jointly act against it,” he said. (See related story, “Will electronic tax registers stem the tide of pilfering?”)
The report says that the figure for Uganda likely understates the true volume of illicit outflows. It notes that civil strife in the Great Lakes region during parts of the 1970-2008 study period resulted in “incomplete and poor quality data” for Uganda, Rwanda, Burundi and Congo.
In all cases, adds the study that encompassed all of Africa, actual losses due to systematic looting are likely to be far greater than the study estimates.
Researchers Dev Kar, a former senior economist at the International Monetary Fund, and Devon Cartwright-Smith, an economist at Global Financial Integrity, note that their figures do not take account of proceeds from smuggling and some of the ways in which trade and services are mis-priced by commercial swindlers.
The actual totals might be more than double the $22.6 billion listed in the report for the three East African countries if those other sorts of illicit outflows were included in the computations, a Global Financial Integrity spokeswoman told The EastAfrican.
Bribery and theft involving government official accounts for only a three per cent share of the money that moves across borders illicitly, the study says.
“Criminal proceeds generated through drug trafficking, racketeering, counterfeiting and more are about 30 to 35 per cent of the total,” the study adds. “The proceeds of commercial tax evasion, mainly through trade mis-pricing, are by far the largest component at some 60 to 65 per cent of the global total.”
Trade mis-invoicing, described in the report as “a significant problem for Kenya,” involves the overpricing of imports and the underpricing of exports on Customs documents, the study explains.
For Africa as a whole, total illicit outflows are said to have amounted to at least $854 billion across the 39 years encompassed in the study.
The top five countries with the highest outflow measured were: Nigeria ($89.5 billion) Egypt ($70.5 billion), Algeria ($25.7 billion), Morocco ($25 billion), and South Africa ($24.9 billion). Most of that money has gone into Western financial institutions, the study says.
“This massive flow of illicit money out of Africa is facilitated by a global shadow financial system comprising tax havens, secrecy jurisdictions, disguised corporations, anonymous trust accounts, fake foundations, trade mis-pricing and money laundering techniques,” Mr Kar and Mr Cartwright-Smith write. “The impact of this structure and the funds it shifts out of Africa is staggering.”
The researchers argue that the existing global financial system, shaped by liberalisation and deregulation of financial markets, has ended up generating ever-rising illicit flows and losses in government revenues. Economic growth without credible reform could lead to more, not less, capital flight, as the increase in incomes would simply finance the increased accumulation of foreign assets.
According to the United Nations’ Millennium Development Goals, $348 billion will be needed to cover MDG costs by 2010 and $529 billion by 2015. The United Nations report World Economic Situation and Prospects 2010 notes that a large gap still separates Africa from its MDGs.
By all accounts, official donor aid commitments will probably fall well short of the required funding of MDGs, leaving open the serious possibility that related targets will recede even further.
Nimefarijika sana kuona mahojiano niliyofanya na msanii mahiri wa Bongoflava,Hamis Mwinjuma a.k.a Mwana FA,yamechapishwa katika tovuti ya kimataifa ya muziki wa hip-hop,Hip-Hop-Dance.Net.Pamoja na kuwapatia wasomaji wa blogu hii nafasi ya kuwafahamu Watanzania wenzetu wanaotangaza jina la nchi yetu kwa namna moja au nyingine,dhumuni jingine la mahojiano hayo lilikuwa kutangaza vipaji vinavypatikana nchini kwetu. Japo mahojiano hayo yanaelekea kuzua mjadala mwingine ambao binafsi nautafsiri kama uhuru wa mawazo,ninaishukuru sana tovuti ya Hip-Hop-Dance kwa "kutoa shavu" kwa mahojiano hayo hasa kwa vile Mtanzania mwenzetu mmoja aliamua kuyabania licha ya kumpa ombi ayaweke "kiwanjani" kwake.Again,naamini alifanya hivyo kwa kutumia uhuru wake kuchagua nini kinastahili kuwepo hapo kwake.
Kuhusu suala la elimu ya Mwana FA,ninaomba kumtetea,sio kwa vile nilimhoji,bali kwa sababu naamini anastahili zaidi pongezi kuliko criticism.Naomba niweke wazi kuwa Mwana FA hakuomba mahojiano hayo bali ni mimi niliyemwomba (na namshukuru sana kwa kukubali ombi hilo).Pili,kama alivyosema mwenyewe,mtu haihitaji kuwa na Masters ili aweze kufanya vizuri kwenye bongoflava.Alichukua uamuzi wa kujiendeleza kimasomo kwa vile,kwa mujibu wa maeleoz yake nayoafikiana nayo,fani ya muziki (hasa wetu) haitoi mwamana wa mafanikio katika maisha.Kwa amaan nyingine,alimua kuongeza elimu yake kama hatua ya kimaendeleo mbali na mafanikio yake katika Bongoflava.
Na hata kama angekuwa anadanganya kuhusu elimu yake (which he absolutely doesn't) ingemsaidia nini wakati tayari ana jina kubwa ndani na nje ya nchi yetu?Nadhani baadhi ya wasomaji wanaomtaka "aeleze ukweli" wanapaswa kwanza "kueleza uongo wake" kabla ya kumtaka aseme "ukweli".Nasema hivyo kwa maana kama nasema jina langu ni Evarist,halafu mtu anasema hilo sio jina langu ,basi ni muhimu kwake kuthibitisha jina langu halisi ni nani.
Binafsi,kama mwanafunzi,nimekumbana na zahma kama hiyo ya Mwana FA.Nimekuwa napokea barua pepe na hata SMS za watu wanaoulizia lini namaliza shule.By the way,shule huwa haimalizwi bali mtu anahitimu hatua moja na anaweza kuendelea na hatua nyingine.Kadhalika,katika mfumo wa elimu ya juu hapa,mwanafunzi anaweza kuahirisha kozi yake pale atapoona umuhimu wa kufanya hivyo.In my case,majibu yangu kwa watu wanaoniuliza kistaarabu ni kuwa kuchelewa kumaliza kozi yangu kumesababishwa na A,B,C na kadhalika kisha nawafahamisha hatua niliyofikia.Kwa wale wanaouliza kwa minajili ya "kudhani nauhadaa umma kuhusu elimu yangu" jibu langu huwa jepesi: Mind your own damn business.
Kuna wanaojiuliza inakuwaje mtu atoke IFM na kuja kufanya Masters University of Coventry,nawasihi wafanye utafiti kidogo kwenye mfumo wa elimu ya Uingereza,na pengine hata huko nyumbani.Inawezekana kabisa kupata admission kwenye vyuo vya hapa kwa kigezo cha "sifa linganifu" (equivalent qualifications).Ni kama ambavyo baadhi ya wanafunzi wanavyojiunga na MBA pale Mzumbe au kwingineko baada ya kumaliza masomo ya stashahada kutoka IFM,Nyegezi,Ustawi wa Jamii (pale Sayansi),nk.Kwa kifupi,mifumo mingi ya elimu duniani iko so "accommodating" kwa watu wenye nia ya dhati ya kujiendeleza kitaaluma.
Nimalizie kwa kutoa shukrani kwa wote wanaoendelea kutoa mawazo yao kuhusu mahojiano hayo.Sipingani na mawazo yoyote bali huu ni mchango na mtazamo wangu binafsi (ambao pia unaweza kuwa si sahihi kwa mujibu wa mitizamo mingine).Huo ndio uhuru wa mawazo,alimradi tunatumia lugha za kiungwana na "hatutiani vidole machoni".Kwa Mwana FA,hizi ndio changamoto za Tanzania yetu.
Stay tuned for the next interview na Mtanzania mwingine anayetuwakilisha vilivyo.Can you make a wild guess?Au una pendekezo lolote?
SIRI ya kuchelewa kwa posho za askari polisi mwezi Febuari mwaka huu imefichuka baada ya kudaiwa kuwa maafisa watatu wa jeshi hilo walitoweka na hundi ya malipo hayo yanayofikia Sh3 bilioni.
Baadhi ya maofisa wa polisi waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti wiki hii, walielezea mazingira ya wizi huo na kusisitiza kuwa ngazi ya juu ya jeshi hilo imekuwa ikificha taarifa hizo, kwa hofu ya kuchafua sifa ya chombo hicho cha dola.
Wakizungumza kwa sharti la kutotajwa majina yao gazetini, walisema fedha hizo ziliibwa na maofisa hao watatu baada ya kubadili maelezo kwenye hati ya malipo na kuielekeza katika akaunti za mmoja wao.
Mwananchi: Tanesco yapoteza umeme wa Sh 100 bilioni kwa mwaka
Sadick Mtulya
MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (Cag), Ludovick Utouh amesema kuwa upo uwezekano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kufilisika baada ya kubaini kuwa kila mwaka linakabiliwa na upotevu wa Sh 100 bilioni.
Alisema fedha hizo zinapotea wakati wa kusambaza nishati hiyo kutoka kwenye vyanzo vyake hadi kwa watumiaji.
Utouh alieleza kwenye ripoti yake, ambayo gazeti hili lina nakala yake amebaini shirika hilo limepata hasara ya Sh Sh48 bilioni mwaka uliopita kutokana na ununuzi wa umeme kutoka katika kampuni binafsi, ikiwemo IPTL kufuatia mgawo mkubwa uliojitokeza Septemba na Oktoba, mwaka jana.
Ripoti hiyo ya Cag iliyowasilishwa Aprili 6, mwaka huu katika kikao baina ya watendaji wakuu wa Tanesco na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Masharika ya Umma (Poac) kilichofanyika katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam.
Kutokana na hali hiyo, Poac iliiagiza Tanesco kuhakikisha inafanya jitihada za kujinasua katika hali hiyo.
SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta, jana alilazimika kuahirisha kikao cha Bunge kwa muda wa dakika 45 kutokana na hitilafu ya mitambo ya mawasiliano ndani ya jengo hilo jipya la Bunge.
Spika Sitta alifikia hatua hiyo baada ya kuingia ukumbini, majira ya saa 2.59 na kuanza kusoma dua kama kawaida, ingawa alilazimika kukatisha tena baada ya kipaza sauti chake kutofanya kazi.
Jambo hilo lilisababisha Spika kuendesha dua kwa sauti ya chini huku baadhi ya wabunge wakipigwa na butwaa.
WATU kadhaa waliotangaza au kuonesha nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ukiwemo ubunge wanadaiwa kutoa rushwa yakiwemo majeneza.
Kisheria kipenga cha kuanza kampeni za kuwania urais, ubunge na udiwani hakijapulizwa na hata kampeni za ndani ya vyama hazijaruhusiwa.
Kampeni hizo haramu zimekuwa zikifanyika hadharani katika mikusanyiko ya watu inayohusu mambo ya kijamii zaidi kuliko siasa na mbaya zaidi imebainika kuwa wagombea hao wamekuwa wakivizia misiba, wakati jamii ikiomboleza kuondokewa na ndugu au jamaa, wao wanafikiria kura za waombolezaji.
Kutokana na hali hiyo ambayo imeonekana kwa wanaotangaza nia za kugombea ubunge kupitia vyama mbalimbali, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imebainisha mwishoni mwa wiki kwamba inafahamu kuwepo kwa vitendo hivyo na imeanza kuwafuatilia wanasiasa hao.
Mkurugenzi wa Idara ya Elimu kwa Umma wa Takukuru, Mary Mosha alibainisha hayo alipokuwa anatoa mada kwenye semina ya kujadili mbinu sahihi za kuripoti habari za uchaguzi mkuu, inayowashirikisha waandishi waandamizi na wahariri wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) inayochapisha magazeti ya Daily News, Sunday News, HabariLeo na HabariLeo Jumapili.
Mwandishi Wetu
Aprili 14, 2010 Ni fedha za stimulus package alizozitetea Kikwete bungeni
Gavana BoT aruka kiunzi, amtupia mpira msaidizi wake
SAKATA la matumizi yenye kutia shaka ya fungu la fedha lililopitishwa na Bunge kwa ajili ya kuhami uchumi, maarufu kama stimulus package , sasa limemrudia Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Beno Ndulu, ambaye baada ya baadhi ya kampuni za ununuzi wa pamba kukosa mgawo huo katika mazingira yanayozua maswali zilimtaarifu naye akawajibu kuwa Serikali haina fedha.
Hata hivyo, wakati Gavana akitoa majibu hayo kuwa “Serikali haina fedha” si fedha zote Sh. trilioni 1.7 zilizoidhinishwa na Bunge la Tanzania ndizo zilizotumika katika mpango huo wa kunusuru uchumi uliotikiswa baada ya uchumi wa dunia kuyumba.
Wiki hii Gavana Ndulu amekwepa kuzungumzia suala hilo, akidai kwamba kwa sasa linashughulikiwa na mtu maalumu chini yake anayepaswa kutafutwa kuzungumzia suala hilo.
Raia Mwema ilipozungumza na Profesa Ndulu, ambaye alieleza kuwa yuko mkoani Mwanza kwa ajili ya mkutano, alisema masuala ya ‘‘stimulus package’’ yamekabidhiwa mtu maalumu ndani ya benki hiyo, na kwamba si yeye anayeweza kuyazumngumzia.
“Haya masuala ya stimulus package tumempa mtu maalumu ambaye ni mkuu wa kitengo cha sera na utafiti, mimi siwezi kuyazungumzia,” alijibu Ndulu hata alipotakiwa kujibu yale yanayomhusu moja kwa moja katika sakata hilo pia hakuwa tayari kuzungumzia.
Uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwa fedha zilizokwishakutumika ni sehemu tu ya Sh trilioni 1.7 zilizopitishwa na Bunge, ambazo ni takriban Sh bilioni 870.8. Fedha hizo Sh bilioni 870.8 kwa mujibu wa taarifa zilizopo ndizo zilizokwishakutolewa na Benki Kuu (BoT), chombo ambacho kimepewa mamlaka ya kutoa fedha hizo.
Kwa mujibu wa utaratibu wa BoT, fedha hizo hutolewa kutoka benki hiyo kwenda katika benki ambazo zilikopesha kampuni zinazostahili kufidiwa, ambazo zimeathiriwa na mtikisiko wa uchumi duniani.
Nipashe: Sungusungu wawavua nguo walimu na kuwachapa viboko
NA ANCETH NYAHORE
14th April 2010
Walimu watatu wa kike na mke mmoja wa mwalimu wa kijiji cha Sakasaka, tarafa ya Kisesa wilayani Meatu, wamevuliwa nguo na kucharazwa viboko na walinzi wa jadi sungusungu wa kijiji hicho kwa madai ya kutohudhuria mkutano uliokuwa umeitishwa na jeshi hilo.
Imedaiwa kuwa walimu hao walishindwa kwenda kwenye mkutano huo kwa sababu ni wajawazito jambo ambalo sungusungu hao walipinga na kuwalazimisha wavue nguo kuthibitisha kama kweli ni wajawazito mbele ya mkutano huo.
Tukio hilo la aina yake na udhalilishaji kijinsia, lilitokea AprilI 7, mwaka huu kati ya saa na 4:00 na 5:00 asubuhi kijijini hapo.Katibu wa Chama cha Walimu (CWT) wa wilaya ya Meatu, Baraka Owawa, aliiambia Nipashe kuwa walimu hao walikamatwa na sungusungu hao na kuanza kuwapiga, kuwavua nguo kwa madai ya kutohudhuria mkutano.Owawa alisema walimu hao hawakuwa na jinsi yoyote ya kukabiliana na sungusungu hao bali walitii amri hiyo ya askari hao wa jadi kunusuru maisha yao.
Mara baada ya walimu hao kufanyiwa unyama huo, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Julius Mtuli, alitoa taarifa kwa uongozi wa juu wilayani hapa ikiwemo polisi na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Meatu na timu maalum kuundwa kwenda kijijini hapo kufuatilia suala hilo.