15 Aug 2014

Within 30 years, a futurist believes babies will regularly born in artificial wombs, outside of human bodies. Stock image pictured
Wanasayansi wanataraji kwamba ndani ya miaka 30 ijayo, itawezekana kutengeneza na kutunza ujauzito nje ya tumbo la mama. Teknolojia hiyo inayofahamika kama ectogenesis imekuwa ikifanyiwa kazi katika maabara tangu mwaka 200, na majaribio ya awali yalikuwa ya kutengeneza na kutunza mimba ya panya nje ya tumbo la panya ' wa kike.'

Wakati wanaounga mkono teknolojia hiyo wanadai itapunguza vifo vya watoto wakiwa tumboni kwani itarahisisha kufanya uangalizi na ufuatiliaji, wapinzani wake wanadai kuwa itaingilia utaratibu wa asili wa uzazi. Wengine wanadai kuwa hatua hiyo itaondoa hatua muhimu ya mahusiano kati ya mama na mtoto tangu akiwa tumboni.

Ectogenesis ni makuzi ya kiumbe kichanga (organism) nje ya mwili, na inatokea kwa baadhi ya wanyama na bakteria. Katika kutengeneza na kutunza mtoto nje ya tumbo la mimba, mfuko 'feki' wa uzazi wahitaji 'mrija feki wa uzazi ' (fake uterus) ili kukipatia kiumbe lishe na hewa ya oksijeni. Pia mipira maalum itahitajika ili kuwezesha kiumbe kichanga 'kujisaidia' (kutoa uchafu mwilini). Chupa inayohifadhi 'mimb' itaunganishwa na mitambo itakayofuatilia makuzi ya 'kichanga' na mimba kwa ujumla.

Kwa taarifa kamili BONYEZA HAPA

CHANZO: Daily Mail



Hebu pata picha: unaingia kwenye email yako unakutana na ujumbe kwamba usubiri kwa muda kwa vile 'internet imejaa.' Kama lengo lilikuwa kusoma tu emails zako, yaweza kuwa sio big deal. Lakini kama uliingia kwenye e-mail ili utume CV kwa mwajiri, au utume assignment yako kwa mwalimu/mhadhiri, basi kwa hakika hali hiyo itakuwa na athari kwako.

Taarifa zinaonyesha kwamba kupotea hewani kwa mitandao kunaweza kuwa jambo la kawaida huko mbeleni kufuatia Internet kuanza kuishiwa nafasi.Jumanne wiki hii, makampuni mbalimbali yaliingia hasara kubwa kufuatia kupotea mawasiliano ya internet kutokana na ufinyu wa nafasi.

Mtandao maaarufu wa kuuza na kununua bidhaa, eBay, ulikuwa miongoni mwa wahanga wa tukio hilo la Jumanne, ambapo ulipotea hewani kwa takriban siku nzima na kukwamisha shughuli lukuki zinazofanyika katika mtandao huo wa biashara.

Maelfu kwa maelfu ya wateja walishindwa kuingia kwenye akaunti zao za eBay huku malalamiko mengi yakiwasilishwa na wateja kutaka warerejeshewe fedha walizonunulia bidhaa.

Inaelezwa kuwa chanzo cha tatizo hilo kilikuwa kinachofahamika kama Border Gateway Protocal (BGP). Makampuni yanayotumia internet na mitandao mignine mikubwa hutumia 'barabara' (route map) hiyo yenye mamia kwa maelfu ya 'njia' kupelekeana taarifa kupitia mtandaoni. Video ifuatayo yaelezea kwa undani zaidi:



Katika mazingira ya kawaida, mtu anapotembelea tovuti anategemea mashine zioitwazo 'router' kukumbuka njia salama katika mtandao mpana wa Internet. Hata hivyo 'routers' za zamani zinapata wakati mgumu kumudu teknolojia mpya- kwa mfano simu za kisasa (smartphones) na Tablets ambazo sio tu zina watumiaji wengi bali pia huongeza muda ambao mtumiaji huwa mtandaoni. Hali hiyo imepelekea 'foleni' kubwa mtandaoni na kusabababisha baadhi ya routers kukabiliwa na changamoto ya kumbukumbu (memory) na uwezo wa kuzifanyia kazi data.

Mfano sahihi wa kilichotokea ni pale ubongo wa binadamu unapozidiwa na uwezo wa kukumbuka vitu njiani baada ya safari ndefu.

Ili kukabiliana na tatizo hilo, routers zinabidi kuboreshwa zaidi katika uwezo wa kumbukumbu na kufanyia kazi data.

Wataalamu wanadai kwamba tatizo hilo litazidi kujitokeza huko mbeleni hasa kwa kuzingatia kuongezeka kwa mauzo ya simu za kisasa na Tablets.

CHANZO: Imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza

Endelea kupata habari za teknolojia kwa kutembelea blogu hii, na kwa urahisi zaidi, bonyeza hapo juu kwenye menu palipoandikwa TEKNOLOJIA


Rais Obama na watawala wa Afrika
WIKI iliyopita, viongozi kadhaa wa Afrika walikutana nchini Marekani kuhudhuria ‘Mkutano kati ya Marekani na Afrika’ (US Africa Summit).
Tukiweka kando maelezo ya kisiasa au kidiplomasia kuhusu mkutano huo, lengo halisi lilikuwa kupromoti uwekezaji wa kibiashara wa Marekani barani Afrika.
Kwa hiyo kimsingi, tukio hilo lilikuwa na umuhimu mkubwa zaidi kwa Wamarekani kuliko Waafrika, kwani laiti yaliyoafikiwa yakitimia, basi wao ndio watakaonufaika zaidi.
Lakini kabla ya kujadili kwa undani kuhusu mkutano huo ni vema kuangalia mambo mawili ya msingi. Kwanza, mkutano huo unashabihiana na tukio kubwa la kihistoria lililotokea miaka 130 iliyopita huko Berlin, Ujerumani.
Ninarejea ‘Mkutano wa Berlin’ (The Berlin Conference) kati ya mwaka 1884 na 1885. Mkutano huo uliligawanya Bara letu miongoni mwa mataifa ya Magharibi na hatimaye kutuletea ukoloni.
Tofauti ya msingi kati ya Berlin Conference na US Africa Summit ni kwamba wakati huo wa kwanza uliwakutanisha ‘wakoloni watarajiwa’ pekee, huu wa wiki iliyopita umewahusisha watawala wa Afrika.
Kufanana kwa mikutano hiyo miwili ya kihistoria kupo katika ukweli kwamba yote ililenga kuchuma rasilimali za Bara letu, japo Berlin Conference ilikuwa ni kwa manufaa ya wakoloni pekee ilhali huu wa Marekani unaelezwa kuwa utalinufaisha Bara la Afrika pia (angalau kwa mujibu wa maelezo ya Wamarekani na watawala wetu).
Pili, moja ya sababu kubwa zilizofanya Marekani kuitisha mkutano huo ni kukabiliana na kasi ya China kutumia fursa mbalimbali zilizopo barani Afrika. Mataifa yote hayo mawili, China na Marekani, yanaongoza kiuchumi duniani, na kwa kutambua ‘urahisi wa kuvuna utajiri’ kutoka Afrika ambao kwa lugha ya kistaarabu unaitwa uwekezaji, imekuwa muhimu kwao ‘kuwaweka karibu’ watawala wetu ili kunufaika na utajiri mkubwa tuliojaliwa kuwa nao japo hatuutumii ipasavyo.
Kwa upande mwingine, mkutano huo kati ya Marekani na Afrika unawaweka watawala wetu katika wakati mgumu wa kuchagua ‘nani wa kumtumainia’ wakati wa shida (na kimsingi shida ni sehemu ya maisha ya kawaida katika bara letu: umasikini, maradhi, nk).
Wakati China inafahamika kwa kuweka mbele maslahi yake ya kiuchumi pasi kujali masuala muhimu kama utawala bora na haki za binadamu, Marekani imekuwa mstari wa mbele kuhamasisha masuala hayo mawili (japo tafsiri halisi yaweza kuleta maana tofauti, mifano hai ikiwa ni pamoja na sapoti yake kwa Israel dhidi ya Palestina na ‘majanga’ iliyosababisha huko Iraki, Afghanistan na Libya).
Pengine ni kwa kutambua kuwa China haina muda na masuala ya haki za binadamu na utawala bora, Rais Barack Obama ameonekana kutoyapa kipaumbele masuala hayo.
Lakini kwa kuangalia sera za nje za Marekani ni rahisi kutambua kwamba taifa hilo linafahamu bayana kwamba litapoteza ‘marafiki wengi’ kwa maana ya watawala wetu likiwekea mkazo ajenda hizo hasa ikizingatiwa kuwa tawala nyingi za Afrika ‘zina uhasama wa muda mrefu’ na haki za binadamu na utawala bora.
Lakini wakati Obama na watawala wetu wanausifia mkutano huo kama fursa ya ‘kuikuza Afrika,’ baadhi ya wachambuzi wanaonya kwamba huo ni mwendelezo wa sera zilezile zilizochangia kulifikisha Bara letu hapa tulipo: mafukara wa kupindukia licha ya utajiri mkubwa tulionao, ambao sana unawanufaisha watawala wetu na washiriki wao.
“Angalia waliopo mezani kuelewa kinachoendelea: baadhi ya watawala wa Afrika wenye rekodi mbaya kabisa wakiwa pamoja na waandamizi wa makampuni makubwa ya Marekani,” anaeleza Emira Woods, mtaalam wa sera za nje za Marekani.
Ni vigumu kuikuza Afrika kwa ushirikiano kati ya watu walewale wanaokwaza maendeleo yake – baadhi ya watawala katika Bara hilo wanaoendekeza rushwa na kusigina haki za binadamu – na makampuni makubwa ya kimataifa ambayo baadhi yake yana rekodi chafu linapokuja suala la kusaka faida, na yanathibitisha kauli ya Marehemu Baba wa Taifa kuwa ‘ubepari ni unyama’ (kwa maana ya kujali faida kuliko utu).
Mwandishi mmoja wa Jarida la Foreign Policy anabainisha kwamba kimsingi mkutano huo wa Marekani na Afrika ni marudio ya tukio la kihistoria linalofahamika kama ‘Scramble for Africa,’ ambapo mataifa ya Magharibi yalikuwa ‘yakifukuzana’ kuja kuchuma raslimali katika Bara hilo.
Anaeleza kwamba mkutano huo umefungua milango kwa Marekani kwenda kuvuna mafuta na madini barani Afrika na kupata soko la bidhaa zake.
Hivi msomaji, unafahamu kwamba sentensi iliyopita ndiyo inafanana kabisa na sababu kuu mbili za ujio wa ukoloni barani Afrika: kupata fursa za rasilimali kwa ajili ya mahitaji ya viwanda katika nchi za wakoloni na masoko ya bidhaa za viwanda vyao?
Licha ya Wamarekani wenyewe, inaelezwa kuwa wanufaika wakubwa wa mkutano huo ni tabaka tawala barani Afrika ambalo kwa namna moja au nyingine litatumia fursa hizo za uwekezaji wa Wamarekani kujinufaisha wao wenyewe na washirika wao, na hiyo inatajwa kama moja ya sababu kubwa za watawala wetu kuuona mkutano huo kama ‘fursa muhimu kwa Afrika.’
Lakini kama kuna mtu aliyeelezea vema kuhusu mkutano huo ni mfanyabiashara tajiri wa Kiafrika, Mo Ibrahim. Kauli yake yaweza kuwafanya watawala wetu waliokusanywa na Obama huko Marekani waone aibu.
Anasema Mo Ibrahim,
“Popote uendapo barani Afrika kuna wafanyabiashara wa Kichina, kuna wafanyabiashara wa Kibrazili. Hakuna miongoni mwetu (Waafrika) aliyekwenda Brazil au India au China kuwaambiwa waje wawekeze Afrika. Walijibidiisha wenyewe na wakaja kuwekeza.  Kwanini sasa tuje kuwashawishi ‘Wamarekani wenye umbumbumbu kuhusu bara la Afrika’? Nyie (Wamarekani) ndio mliovumbua Google (tovuti ya kutafuta habari kupitia mtandao wa kompyuta), kwanini msiitumie?”
Afrika tuliyonayo si ile iliyokuwa na jeuri ya kumtimua mkoloni. Yayumkinika kubashiri kuwa laiti tungekuwa na akina Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na wenzake wenye msimamo kama Kenneth Kaunda, Samora Machel, na kadhalika, wangemwambia bayana Obama aje yeye Afrika na si kukusanya viongozi wetu kama kundi la wanafunzi waliopewa  nafasi za masomo nchi za nje.
Naam, kama Wamarekani ni kama mtu anayetaka kuchumbia, sharti yeye aende nyumbani kwa anayetaka kumchumbia. Lakini viongozi wa kizazi hiki hawajali ‘kuuza utu/Uafrika wao’ alimradi kuna ‘faida za uwekezaji’.
Mo anaukosoa mkutano huo katika maeneo makuu mawili: kwanza, ‘jeuri’ ya Obama kukataa mikutano na viongozi mmoja mmoja (bilateral meetings)  licha ya wito kutoka Nigeria, Kenya na Afrika Kusini, na pili, ukweli kwamba  Obama amebakiwa na miaka miwili tu ya urais wake wa Marekani, na hivyo pengine mikakati yake ya ‘kuisaidia’ Afrika ikaishia njiani baada ya yeye kutoka madarakani mwaka 2016.
Sidhani kama mkutano huu utakuwa na manufaa yoyote ya maana kwa mamilioni ya walalahoi wa Afrika. Wakati Rais Kikwete akieleza katika mkutano huo  kuwa moja ya sababu kubwa zinazokwamisha maendeleo makubwa zaidi na ya haraka zaidi ya Afrika ni uzalishaji mdogo na matumizi ya chini mno ya umeme, ukweli wa wazi ni kwamba kikwazo kikubwa ni rushwa inayozidi kuota mizizi na kutapakaa, sambamba na kupuuzia utawala bora na haki za binadamu.
Ni muhimu kwa Kikwete na viongozi wengine wa Afrika kutambua kuwa maendeleo ya kweli katika nchi zao hayataletwa na Wamarekani au Wachina bali wananchi wenyewe. Laiti watawala wetu wangewekeza nguvu katika kuwawezesha wawekezaji wa ndani badala ya kutarajia miujiza kutoka kwa wawekezaji wa nje basi kwa hakika wasingekusanywa na Obama huko Washington DC. Angewafuata kuwaomba nchi yake ipatiwe nafasi za uwekezaji.
Nimalizie makala hii kwa kupongeza uamuzi wa busara wa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya kufikia hoteli yenye gharama nafuu wakati wa mkutano huo kati ya Marekani na Afrika. Uhuru alifikia hoteli ya JW Warriot inayotoza Dola za Kimarekani 339 (takriban sh 560,000) kwa usiku mmoja. Kadhalika, aliwaagiza maafisa alioambatana nao katika msafara wake kuweka makazi katika hoteli za gharama nafuu. 
Sina taarifa kuhusu hoteli aliyofikia Rais wetu Kikwete ila ninachofahamu ni kuwa aliambatana na msafara mkubwa (siku hizi hawaoni umuhimu wa kutufahamisha akina nani wanaambatana na Rais katika ziara zake mfululizo nje ya nchi).



 Kunywa maji ya kutosha 

  1. Increase Your Ejaculate Step 1 Version 2.jpg


  1. Epuka joto kwa sehemu zako za siri
    Increase Your Ejaculate Step 2 Version 2.jpg

  2. ee
  3. Epuka 'nguo za ndani' za kubana
    Increase Your Ejaculate Step 3 Version 2.jpg


  4. Epuka 'kupinda nne'
    Increase Your Ejaculate Step 4 Version 2.jpg

    .


  5. Punguza tendo la ndoa kwa muda ile kurejesha mbegu za kiume 'zilizopotea'
    Increase Your Ejaculate Step 5 Version 2.jpg
    Add caption
  1. Tumia vitamini vya Zinc na Folic Acid
    Increase Your Ejaculate Step 6.jpg


  2. Punguza kunywa soda
    Increase Your Ejaculate Step 7.jpg


  3.  Meza vitamini vya Amino Acid vya aina hizi: L-Arginine, L-Lysine na L-Carnitin Increase Your Ejaculate Step 8.jpg

  4. Jaribu 'vidonge vya asili' viitavyo Horny Goat Weed
    Increase Your Ejaculate Step 9.jpg


  5. Kula matunda na mbogamboga (hasa maharage mekundu, maji ya nazi, apples, wild blueberries, blackberry, cranberry)
    Increase Your Ejaculate Step 10.jpg


    Chua misuli ya 'sehemu yako ya siri' pasipo kufikia 'kileleni'

    1. Increase Your Ejaculate Step 11.jpg

    2. Punguza na hatimaye acha kuvuta sigara (na bangi ni adui mkubwa wa mbegu za kiume)
      Increase Your Ejaculate Step 12.jpg

      • Punguza msongo wa mawazo (stress)
        Increase Your Ejaculate Step 13.jpg

        • Fanya mazoezi mara kwa mara
          Increase Your Ejaculate Step 14.jpg

        • Zingatia ngono salama (maradhi ya zinaa yanaathiri vibaya uzalishaji mbegu za kiume)
          Increase Your Ejaculate Step 15.jpg

          CHANZO: WikiHow

        12 Aug 2014


        Hali nchini Iraki ni tete kufuatia uamuzi wa Rais wa nchi hiyo Fouadi Masoum (I guess wewe kame mie tulikuwa hatumfahamu mtu huyu wala kujua kama Iraki ina rais) 'kumtimua' Waziri Mkuu Nuri al-Maliki, aliyekuwa madarakani kwa miaka minane, na kumteua Haidar al-Abadi kuchukua wadhifa huo.

        Hata hivyo, Maliki sio tu  amegoma kuondoka madarakani bali pia amemwaga wanamgambo na vikosi maalum vya jeshi (special forces) mitaani, na kupelekea kizaazaa cha aina yake.

        Marekani, ambayo ilisaidia kumweka madarakani Maliki mwaka 2003 imempongeza Waziri Mkuu mpya al-Abadi, msaidizi wa zamani wa Maliki, kuashiria kuunga mkono mabadiliko hayo.

        Akihutubia kwa njia ya televisheni (naam, pamoja na vurugu zote nchini Iraki bado televisheni zinafanya kazi) amesema hatua ya Rais kufanya mabadiliko hayo ni ukiukwaji hatari wa Katiba, huku akiambatana na 'wapambe' wake, ameahidi kutatua 'kero' hiyo.

        Mkwe wake, Hussein al-Maliki, ameyaelezea mabadiliko hayo kuwa ni kinyume cha sheria, na kudai yatabadilishwa kortini. "Hatutokaa kimya," alidai.

        Hata hivyo, Marekani imemwonya Maliki kutotumia nguvu za dola kung'ang'ania madaraka.

        Mwislamu wa madehebu ya Shia, Maliki analaumiwa na washirika wake wa zamani huko Marekani na Iran kwa kuwasukuma waumini wa madhehebu ya SUnni katika mapambano yaliyopelekea 'sintofahamu' inayoendelea sasa kwa kikundi cha Sunni cha ISIS kudhamiria kuigeuza nchi hiyo kuwa taifa la Kiislam. Viongozi wengi wa ki-Sunni na Kikurdi wamekuwa wakipiga kelele kuwa Maliki anastahili kuachia ngazi, huku hata baadhi ya viongozi wenzake wa ki-shia wakiwa na msimamo kama huo.

        CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka vyanzo mbalimbali mtandaoni

        11 Aug 2014


        Vacancy
        Governance Advisor
        Irish Aid is the Government of Ireland’s programme of assistance to developing countries operating under the Embassy of Ireland in Tanzania.  The programme focuses on Health, Nutrition and Agriculture, with a strong governance component supporting the achievement of results across the programme.
           
        The Embassy is seeking to recruit a highly motivated and experienced Governance Advisor to join its Development Team.  Reporting to the Senior Governance Adviser and working with the Governance Team and across the other teams at the Embassy, the successful candidate will be expected to contribute to the delivery of a high quality programme.  He/she will have responsibility for management of a number of the governance programme components as well as the provision of strategic input and advice on governance across the Embassy.  The Advisor also will provide support to the team on mainstreaming governance within their areas of responsibility.  

        Candidates applying for the position are expected to have: (i) a post graduate degree in governance,  politics, law, international development, social sciences or other relevant disciplines; (ii) a minimum of four years relevant work experience as well as (iii) knowledge and understanding of the political economy  and governance environment  in Tanzania .  A detailed job description is available on the Embassy of Ireland website www.embassyofireland.or.tz .
        Interested candidates should forward a cover letter together with their most recent Curriculum Vitae and contact details to:[email protected] by 14 August 2014.

                           
        Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba nusura wapigane baada ya kupishana kauli wakati wa mjadala wa ndani ya Kamati Namba Sita inayoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira.
        Habari kutoka ndani ya kamati hiyo inayofanyia vikao vyake katika moja ya kumbi za Dodoma Hoteli zinasema, mvutano huo ulitokea Alhamisi iliyopita na kusababisha Wassira kusitisha kwa muda kikao hicho, kisha kwenda kuwasuluhisha.
        Jana, Wassira licha ya kukiri kutokea kwa mvutano huo, alikanusha taarifa kwamba aliahirisha kikao hicho kwa ajili ya kuwasuluhisha.
        “Kupishana katika masuala haya makubwa ni jambo la kawaida, hivyo mimi sidhani kama ni jambo linalopaswa kwenda mpaka kwenye magazeti maana kila wakati hutokea tofauti hizi na ndiyo maana sisi wenyeviti tupo ili kusimamia mijadala,” alisema Wassira na kuongeza:
        “Lakini kwamba eti hilo jambo lilisababisha kikao kuahirishwa au kusitishwa hapana, kikao kiliendelea na kazi yake baada ya hilo lililoleta na ubishani kumalizwa”.
        Habari zilizolifikia gazeti hili zinasema mvutano huo ulitokea wakati kamati hiyo ilipokuwa ikijadili Sura ya Nne na Tano, hususan suala la uraia wa nchi mbili. Sura ya tano ndiyo inayozungumzia masuala ya uraia.
        “Sophia Simba yeye anataka uraia wa nchi mbili wakati Werema alikuwa akisema hilo jambo haliwezekani kutokea kwa sasa,” kilisema chanzo chetu.
        Kwa mujibu wa taarifa hizo, mvutano huo uliendelea baina ya viongozi hao na ndipo Jaji Werema aliposimama katika mchango wake na kuhoji elimu ya Simba, hivyo kuamsha hasira za waziri huyo ambaye pia alijibu mapigo.
        “AG alipopewa nafasi ya kuzungumzia baada ya mabishano ya muda alihoji shule (elimu) ya Simba kwamba amesoma shule gani akimaanisha kwamba ni mgumu kuelewa, kwa hiyo waziri alikasirika na yeye alianza kujibu mapigo,” kiliongeza chanzo hicho.
        Baada ya kutokea mvutano huo, baadhi ya wajumbe waliingilia kati kusitisha mzozo huo, ndipo Mwenyekiti Wassira alipositisha kikao hicho kwa muda kisha kuwasuluhisha wahusika.
        Walipotafutwa jana kwa nyakati tofauti kuzungumzia mzozo wao, Werema na Simba hawakuwa tayari kubainisha kilichotokea.


        Werema alitaka aachwe apumzike na kwamba mambo ya kamati yaachwe kwenye kamati.
        “Jamani hamtuachi hata tupumzike Jumapili yote hii? Tafadhali bwana niache nipumzike, hayo mambo kama ni ya kamati, yaachwe kwenye kamati,” alisema Werema na kukata simu.
        Simba baada ya kuulizwa alisema: “Heeeee hayo makubwa… I have no comment (sina cha kusema”), kisha alikata simu.
        Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad alisema ofisi yake haikuwa imepata taarifa kuhusu mzozo huo na kwamba angefuatilia ili aweze kufahamu kuhusu kilichojiri.
        “Nina maofisa wa kutosha katika kila kamati, sasa nashangaa kwamba jambo kubwa kama hilo litokee halafu nisipate taarifa, lakini ngoja nifuatilie lakini kwa sasa sina taarifa yoyote,” alisema Hamad.
        Werema
        Juni mwaka huu, Jaji Werema alitaka kumtia adabu Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila bungeni Dodoma baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu kuahirisha kikao cha Bunge, ikiwa ni muda mfupi baada ya Werema na Kafulila kurushiana maneno bungeni.
        Jaji Werema alichukia baada ya Kafulila kumwita mwizi, akijibu mapigo baada ya mbunge huyo kuitwa tumbili na mwanasheria huyo.
        Hali hiyo ilijitokeza baada ya kutofautiana kauli kuhusu mgogoro wa fedha za akaunti ya Escrow kulipwa Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL.
        CHANZO: Mwananchi 
        ANGALIZO: Picha ni kielelezo tu 

        Tuwe wakweli, japo matumizi ya emoji yanaweza kufanya ulichoandika kionekane sio serious lakini kwa hakika emoji zinasaidia kuonyesha mood yako. Sasa sote twafahamu kuwa emoji hutumika zaidi kwenye simu, hasa za kisasa. Je wafanyaje ukitaka kuzitumia mtandaoni, kwenye Twitter au kwingineko?

        Tembelea tovuti hii na utakuta lundo la emoji. Ukishaiona unayotaka, i-copy kisha i-paste kwenye sentensi yako...there you go!

        Endelea kutembelea blogu hii kwa habari mbalimbali ikiwa ni pamoja na za teknolojia. Bonyeza TEKNOLOJIA hapo kwenye main menu utakutana na mengi ya muhimu katika eneo hilo. Karibuni sana


        WIKIENDI iliyopita haikuwa njema kwa mtangazaji Ephraim Kibonde baada ya kutupwa nyuma ya nondo katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar kwa msala wa kudaiwa kugonga gari na kutoa lugha ya matusi, Ijumaa Wikienda lina full stori.
        Mtangazaji Ephraim Kibonde akidhibitiwa na Polisi wa usalama barabarani maeneo ya Mwenge.
        Kwa mujibu wa chanzo chetu makini cha habari ambacho kimeshuhudia sakata hilo mwanzo mwisho, ishu nzima ilianzia maeneo ya Makumbusho ambapo gari alilokuwa akilitumia Kibonde, liligonga kwa nyuma gari jingine na kisha kukimbia.
        “Baada ya kugonga, Kibonde alirudi nyuma kisha kuanza kukimbia ambapo trafiki alitumia gari lililogongwa na Kibonde kumkimbiza,” kilimwaga data chanzo hicho.Chanzo hicho kilifafanua kuwa baada ya polisi kumkimbiza kwa saa kadhaa, walifanikiwa kumkamata maeneo ya Mwenge ambapo trafiki alipanda kwenye gari la Kibonde na kumuamuru arudi eneo la tukio lakini Kibonde hakuwa tayari kurudi ndipo alipoanza kukimbia tena, huku askari aliyemkamata akiwa ndani ya gari.
        Ephraim Kibonde akiwa nyuma ya nondo katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar es Salaam.
        “Inaonekana kulitokea kutoelewana kati ya askari na Kibonde ndipo askari huyo alipowasiliana na wenzie kwa njia ya radio call ili wambananishe na alipofika Ubungo kwenye mataa wakamtaiti na kumpeleka kituoni, Oysterbay,” kilihitimisha chanzo chetu.
        Baada ya kupata maelezo hayo, kachero wa Ijumaa Wikienda alitia timu katika kituo cha Oysterbay ili kutaka kujua mustakabali mzima wa ishu hiyo ambapo alimshuhudia Kibonde akiwa amesimama nyuma ya nondo huku akiwa anaimba ‘nyimbo’ anazozijua mwenyewe.
        Mtangazaji huyo amefunguliwa kesi iliyopewa RB namba OB/RB/13806/20014 KUGONGA NA   LUGHA YA MATUSI.


        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .


        Categories

        Blog Archive

        © Evarist Chahali 2006-2022

        Search Engine Optimization SEO

        Powered by Blogger.