23 Apr 2015


Unapoingia mtandaoni kwa minajili ya ku-search kitu, uwezekano mkubwa utaenda kwenye mtambo wa kutafuta habari (search engine) wa Google. Sasa, kwenye mtandao huo, ukiingiza neno pale kwenye kiboksi cha kutafutia habari, wenyewe utaanza kubashiri maneno kulingana na herufi husika zinavyotengeneza neno. Mfano rahisi ni huo pichani juu.Ukitafuta 'What is Tanzania..." kabla hujamaliza, Google itaanza kukupa ubashiri wa unachotafuta. Kitu hicho kinajulikana kama Google autocomplete

Sasa hapa chini ni ramani ya dunia kwa mujibu wa Google autocmplete. Yaani ramani hiyo ya dunia, na kama ilivyogawanywa kwa kila bara ni kwa mujibu wa jinsi watu wanavyo-search habari kuhusu nchi husika. Kwa mfano autocomplete searches nyingi kuhusu Canada ni passport, kwa Brazil ni makahaba...na kwa Tanzania yetu ni SAFARI...Well, sio BIA YA SAFARI bali safari za utalii.


Null


Null



Null

Null

Null

CHANZO: i100


18 Apr 2015

KWA siku kadhaa sasa kumekuwa na mjadala mkali, hususani katika mitandao mbalimbali ya kijamii kuhusu sheria mpya ya kukabiliana na uhalifu wa mtandaoni (Cyber Crime Act 2015).


Kabla ya kuuzungumzia mjadala huo, ningependa kumpongeza Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, kwa kufanya tukio la kihistoria la kuuweka hadharani muswada husika katika mtandao wa kijamii wa Twitter ili ujadiliwe.
Ninatambua kuna uwezekano wa baadhi ya watu kudai haistahili pongezi kwa sababu, kwanza hilo ni jukumu la kila mtendaji wa serikali, na pili, kuleta muswada huo siku chache kabla haujawasilishwa kwa hati ya dharura Bungeni kusingewapa wadau nafasi ya kutosha kuujadili.



Katika hilo la kwanza, ni muhimu tutambue kuwa Tanzania yetu ya sasa imefikia mahala ambapo kiongozi akitimiza wajibu wake anastahili kupongezwa kwani hata asipotimiza wajibu anaolipwa mshahara kuutekeleza hatoathirika. Ni wazi basi, hata kama January angeamua kutouweka muswada huo hadharani, isingemwathiri lolote.



Kuhusu muswada huo kuwasilishwa kwa hati ya dharura, ninaafikiana na wanaolalamikia hatua hiyo kwa sababu licha ya dhamira nzuri na umuhimu wa kuwa na sheria ya kudhibiti uhalifu wa mtandaoni, bado kulikuwa na haja ya wananchi kupewa elimu ya kutosha kuhusu masuala kadhaa, hasa ikizingatiwa kuwa Watanzania wengi bado ni ‘wageni’ katika masuala ya mtandao (wa intaneti.)



Na pengine kabla ya kuingia kwa undani katika kuzungumzia mjadala huo na muswada huo ambao ulipitishwa na bunge na hadi wakati ninaandika makala hii ulikuwa ukisubiri kuidhinishwa na Rais Jakaya Kikwete ili uwe sheria kamili, ni muhimu kuweka wazi msimamo wangu kwamba ninaunga mkono muswada na sheria husika.



Ninaunga mkono kwa sababu kuu tatu: kitaaluma/kitaalamu, kijamii na binafsi. Kwa upande wa kitaaluma/kitaalamu, huko nyuma niliwahi kufanya kazi katika sekta ya usalama, na kwa muda mrefu nimekuwa nikijihusisha na stadi zinazohusu sekta hiyo.



Kwa hiyo, utaalamu na uelewa nilionao, unanisukuma kuunga mkono haja ya, na umuhimu wa kuwa na sheria ya kukabiliana na uhalifu wa mtandaoni.



Kwa kifupi tu, pamoja na faida zake nyingi, mtandao unaweza na umeshaweza kutumika vibaya na kusababisha madhara makubwa.



Pamoja na kurahisisha mawasiliano na kufanikiwa kuiunganisha dunia na kuwa kama kijiji (ninaandika makala hii nikiwa hapa Uskochi, na nikimaliza na kubonyeza ‘send’ inamfikia mhariri wa gazeti hili muda huohuo, tofauti na njia za zamani ambapo ingelazimu kutuma makala hii kwa barua, na kuchukua siku kadhaa njiani), mtandao umekuwa kichaka cha maovu hasa kutokana na teknolojia husika kuwezesha mawasiliano pasipo watu kukutana ana kwa ana.



Kwa mfano, wakati kabla ya ujio wa teknolojia ya mtandao, ilikuwa vigumu kwa ‘mwizi’ kuiba fedha za mwenye akaunti benki bila kufika katika benki husika (au kuziiba wakati mwenye akaunti anaenda kuweka fedha hizo au kuzichukua benki), kwa sasa teknolojia ya mtandao inamwezesha mwizi aliyepo hata mbali na benki au mwenye akaunti kuziiba fedha hizo. Japo pengine hili halijashamiri sana huko nyumbani, ukweli ni kwamba wizi wa aina hiyo umetawala sehemu mbalimbali duniani.



Lakini kiusalama, mtandao umetokea kuwa moja ya nyenzo muhimu za magaidi, ambavyo vikundi maarufu vya kigaidi duniani kama Al-Qaeda, ISIS, Boko Haram na Al-Shabaab, vimekuwa vikiutumia vyema mtandao katika harakati zao dhalimu za ugaidi.



Katika tukio linaloweza kuonekana la kufikirika tu, magaidi wanaweza kutumia mitandao ya kijamii au hata ‘Whatsapp’ kusambaza ujumbe unaoweza kutishia amani na kusababisha madhara makubwa.



Sheria ya kukabiliana na uhalifu wa mtandaoni imekuja wakati mwafaka hasa kwa kuzingatia uwepo wa taarifa zinazoashiria tishio la ugaidi, kufuatilia shambulio la kigaidi lililofanywa hivi karibuni na magaidi wa Al-Shabaab huko Garissa, nchini Kenya na kusababisha vifo takriban 150.



Ninathamini sana haki za raia kuwasiliana pasipo hofu ya serikali au taasisi zake za usalama kuyafuatilia mawasiliano yao, lakini pia ninatambua kuwa ili serikali iweze kutekeleza jukumu lake la kulinda usalama wa raia, inalazimika kufahamu mawasiliano yasiyo na nia nzuri kwa taifa letu.



Katika zama hizi hatari tunazoishi, ni vigumu mno kupata uwiano stahili kati ya uhuru na sheria kwani wahalifu wanaweza kuutumia uhuru huo kwa dhamira mbaya inayoweza kupelekea raia wasiweza kuutumia uhuru wao vyema.



Kijamii, Tanzania yetu imefika mahala pabaya, angalau huko kwenye mitandao ya kijamii. Na kama kuna sehemu inayoweka ushahidi wa wazi kuhusu hicho ninachoongelea, basi ni kwenye mtandao wa kijamii unaohusu picha, Instagram, ambao kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo unavyozidi kuwa uwanja wa matusi na kila lisilopendeza machoni.



Kwa upande wa blogu, licha ya kuwa bado tuna blogu nyingi zinazoitumikia jamii ipasavyo, kumeibuka utitiri wa blogu za ngono na matusi huku nyingine zikijipa uhuru wa kuwachafua watu na kuwasababishia madhara makubwa katika maisha yao. Ilikuwa lazima tufike mahala tuseme ‘sasa yatosha.’ Hakuna uhuru usioambatana na kuzingatia wajibu.



Mwaka jana, binti mmoja wa Kitanzania alikumbana na madhila ya unyanyasaji mkubwa katika mtandao wa kijamii wa Twitter, na siku chache baadaye alikutwa amekufa. Japo hakuna uthibitisho wa moja kwa moja kati ya unyanyasaji huo wa mtandaoni na kifo cha binti huyo, yayumkinika kuhisi kuwa matukio hayo mawili yalikuwa na uhusiano japo hata kama ni wa mbali. Na baada ya tukio hilo la kusikitisha, zilisikika kelele mbalimbali za kuitaka serikali ichukue hatua madhubuti kukabiliana na unyanyasaji wa mtandaoni (cyber bullying).



Sababu yangu ya tatu ya kuunga mkono sheria hiyo ya kupambana na uhalifu wa mtandaoni ni ya binafsi. Baada ya kifo cha binti huyo, nilisimama kidete na baadhi ya wanaharakati wa haki za jamii kuhamasisha mapambano dhidi ya unyanyasaji wa mtandaoni, kosa ambalo ni sehemu ya uhalifu wa mtandaoni.



Katika hali ya kushangaza na kusikitisha, liliibuka kundi lililoanzisha mashambulizi makali dhidi yetu tuliokuwa tukikemea vitendo vya unyanyasaji wa mtandaoni. Binafsi, niliandamwa hadi kiasi cha kuitwa muuaji hadharani, jambo ambalo linaniumiza nafsi hadi muda huu. Nilishindwa kabisa kuelewa kwanini dhamira nzuri ya kukemea maovu igeuke kuwa kosa lililowaudhi watu hao.



Naomba ieleweke kuwa sababu hii ya tatu ni ya binafsi na ningesihi isiangaliwe pekee bali pamoja na hizo mbili niliotaja hapo awali, ili isilete hisia kuwa mimi ni mbinafsi ninayeunga mkono sheria hiyo kwa vile ‘itawakomoa’ waliowahi kuninyanyasa mtandaoni huko nyuma.
Wakati jamii inaweza kuuhitaji muda mrefu kujadiliana kuhusu haja ya kuwa na sheria ya kukabiliana na uhalifu mtandaoni, ni muhimu kukumbuka kuwa wahanga wa uhalifu huo hawana muda wa kusubiri. Waingereza wanasema kumcheleweshea mtu haki yake ni sawa na kumnyima haki hiyo (justice delayed is justice denied).



Wahanga wa uhalifu wa mtandaoni wanastahili haki sawa kama hao wenye hofu kuwa sheria hiyo inaweza kutumiwa na serikali kukandamiza uhuru wa mawasiliano.



Wakati ninatambua mapungufu makubwa ya vyombo vyetu vya dola katika kusimamia na kutoa haki, na hivyo kuelewa vema hofu ya wanaopinga sheria hiyo, ni muhimu pia kutambua kuwa serikali ikiwa na nia ya kuminya haki haihitaji sana kuwa na sheria rasmi.
Tumeshuhudia gazeti la MwanaHalisi likifungiwa kwa kutumia ‘visingizio’ vingine, na wakati huo hatukuwa na sheria ya makosa ya uhalifu wa mtandaoni.



Ni kweli kwamba serikali na taasisi zake zinaweza kuitumia vibaya sheria hiyo kuminya uhuru wa mawasiliano, lakini pia ni muhimu tutambue kuwa serikali hiyohiyo ina sheria nyingine kadhaa, na pengine ‘kali’ zaidi ya hiyo ya kuzuwia uhalifu wa mtandaoni, na ikitaka kuzitumia kuminya uhuru, inaweza kufanya hivyo muda wowote.



Kuna sheria kama ile ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1970 na sheria ya kukabiliana na ugaidi ya mwaka 2002, ambazo zinaipa serikali uwanja mpana tu wa kuzitumia vibaya ikitaka kufanya hivyo.



Kimsingi, mjadala unaoendelea kuhusu sheria hiyo unatokana na suala ambalo nimekuwa nikiliongelea mara kadhaa katika makala zangu: upungufu wa imani ya wananchi wengi kwa serikali yetu. Imefika mahala wananchi wengi hawaiamini serikali, na ndio maana baadhi ya wanaopinga sheria hiyo wanadai imeletwa haraka kwa minajili ya kuisaidia CCM katika uchaguzi mkuu ujao.



Hofu kuwa sheria hiyo inaweza kutumika vibaya ina mantiki, lakini tatizo sio sheria hiyo ambayo kwa hakika imechelewa sana, bali mfumo wa kifisadi unaoathiri nyanja mbalimbali za maisha ya Mtanzania. Hakuna polisi anayeweza kumkamata mtu kwa vile tu kafanya umbeya kwenye ‘Whatsapp’ yake iwapo mfumo tulionao unazingatia sheria na haki.



Kwa bahati mbaya hilo linaweza kutokea kwa sababu baadhi ya polisi wetu wanaofahamika kwa tabia yao ya kupenda rushwa. Je tupuuzie madhila yanayowakumba wahanga wa uhalifu wa mtandaoni hadi tutakapokomesha rushwa kwenye taasisi kama jeshi la polisi au ‘tuue ndege wawili kwa jiwe moja,’ kwa maana ya kuendeleza mapambano dhidi ya mfumo wa kifisadi sambamba na kutumia ipasavyo sheria hiyo mpya kukabiliana na uhalifu wa mtandaoni?



Wakati kwa kiasi kikubwa mjadala kuhusu sheria hiyo unafanywa kistaarabu, na tayari kuna petition imewekwa mtandaoni kumsihi Rais Kikwete asiridhie sheria hiyo, kuna kundi dogo la wanufaika wa uhalifu wa mtandaoni linalojaribu kujificha katika hoja kuwa sheria hiyo ni mbaya.



Na pengine la kusikitisha zaidi ni kuona dhamira nzuri ya Naibu Waziri January Makamba kuuweka hadharani muswada husika ikichukuliwa na baadhi ya ‘wanyanyasaji wa mtandaoni’ kumshambulia yeye binafsi kana kwamba sheria hiyo ni yake binafsi. Tatizo hapa ni kuweka mkazo kwa mtu badala ya suala husika.



Nimalizie makala hii kwa kusisitiza kuwa ninaamini sheria hiyo dhidi ya uhalifu wa mtandaoni ina umuhimu mkubwa kwa usalama wa taifa letu na kwa Watanzania kwa ujumla. Sheria husika haiwalengi raia wema bali wahalifu wa mtandaoni.



Badala ya kuwekeza nguvu nyingi kuhofia madhara yake, ni muhimu kama jamii tujiongoze kistaarabu na kukumbushana wajibu wetu kama raia wema. Tusiwe vigeugeu wa kuilaumu serikali kila tunapokutana na picha za ngono au maiti mtandaoni lakini serikali ikisikia kilio chetu kuhusu haja ya kuchukua hatua kali, na hivyo kuja na sheria kama hiyo ya kukabiliana na uhalifu wa mtandaoni, twaishia kuilaumu pia.


Kwa mujibu wa tovuti ya Bunge letu la Muungano, kama nilivyoi-access saa 11.02 alfajiri kwa saa za hapa Uingereza, marehemu wabunge hawa hapa chini wameendelea kuorodheshwa kwenye tovuti hiyo sio tu kama bado wapo hai bali pia ni wabunge katika majimbo husika.

Ninaamini kabisa kuwa taasisi muhimu kama Bunge ina fungu la kutosha kwa ajili ya huduma zake mbalimbali, ikiwa ni pamoja na tovuti yake. Na hata ingekuwa haina fungu, kufanya marekebisho kwenye tovuti hiyo ni jambo la dakika chache tu, na lisilo na gharama yoyote.

Hakuna ubaya kwa wabunge marehemu kuendelea kuwepo katika tovuti ya Bunge iwapo ukweli kwamba waheshimiwa hao sasa ni marehemu utabainishwa, hususan katika kipengele kinachoonyesha muda wa utumishi wao katika mhimili huo muhimu wa dola.

Pengine hili ni suala dogo lakini kwa hakika Bunge ni moja ya vitambulisho vya taifa letu, na tovuti yake ni njia rahisi kwa Watanzania na wasio-Watanzania kupata habari na taarifa zinazoihusu taasisi hiyo. 

Licha ya kasoro hiyo, nilipofanya search ya majina ya baadhi ya wabunge, hakukuwa na matokeo yoyote.Ukitaka kuhakikisha, tafuta jina la Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete, kwa mfano.








Ni matumaini yangu kuwa Ofisi ya Bunge letu itarekebisha kasoro hii haraka iwezekanavyo

CHANZO: Screenshot za picha kutoka tovuti ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano

14 Apr 2015



Sikiliza Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt Slaa akihojiwa na kitumo kimoja cha redio cha WIBC 93. FM cha Marekani

Bonyeza HAPA kusikiliza

12 Apr 2015

Wakati mitandao mbalimbali ya kijamii ikiendelea mjadala kuhusu sheria ya kudhibiti uhalifu wa mtandaoni (Cyber Crime Act 2015), ukweli mchungu unabaki kuwa uhalifu huo upo, na unaendelea kuwaathiri watu kila siku.

Jamii inaweza kuendelea kubishana hata kwa miaka 100 kama twahitaji sheria hiyo au la, lakini wahalifu wa mtandaoni wanaendelea kutusumbua kila kukicha. Wakati sheria hiyo haiwezi kumaliza kabisa tatizo la uhalifu wa mtandaoni, angalau kwa kiasi flani itasaidia kumfanya mhalifu atafakari mara mbili kuhusu madhara ya uhalifu wake pindi akikamatwa.

Na kama kuna eneo ambalo wahalifu wa mtandaoni hulipendelea zaidi ni wizi wa nywila, au kwa kimombo PASSWORD. Lakini kinachowafanya wahalifu hao kupendelea wizi wa nywila sio kwa vile wakifanikiwa kuiba watakuwa na 'control' ya akaunti yako bali pia ukweli kwamba watu wengi hufanya makosa wakati wanapofungua akaunti mtandaoni kwa kuchagua nywila dhaifu.

Pengine ushamsikia shushushu mmoja maarufu kabisa duniani aitwaye EDWARD SNOWDEN. Kama hujawahi kumsikia, basi ngoja nikuhabarishe.Huyu jamaa alikuwa anafanya kazi kama mchambuzi katika moja ya taasisi kubwa za ushushushu nchini mMarekani, inayojulikana kakma NSA, yaani National Security Agency. Hawa jamaa kazi yao ni kunasa mawasiliano- iwe ya email, simu au njia nyingine yoyote ile. Sasa Bwana Snowden, kwa kukerwa na ukiukwaji wa haki za binadamu uliokuwa unafanywa na mwajiri wake, akaamua kumwaga siri hadharani.Akawapatia wanahabari, hususan wa gazeti la Guardian la hapa Uingereza, data kibao zilizokuwa zikionyesha jinsi NSA ilivyokuwa ikiwapeleleza Wamarekani na watu wengike kibao duniani.

Sasa, kama ilivyo kawaida kwa taasisi za ushushushu, ukiweka hadharani madhambi yao unakuwa adui yao.Hivyo ilimlazimu Bwana Snowden kutoroka Marekani, na kwa sasa amepata hifadhi ya ukimbizi nchini Russia.

Siku nafasi ikiniruhusu nitaelezea kwa kirefu kuhusu mkasa wa shushushu huyu.Ila kwa leo nitazungumzia ushauri alioutoa hivi karibuni kuhusu nywila imara, itakayowapa kibarua wahalifu wa mtandaoni kuihujumu.

Snowden akiongea katika mahojiano na mtangazaji wa televisheni na mchekeshaji, John Oliver, alieleza kuwa nywila za watu wengi ni dhaifu mno kiasi kwamba inamgharimu mhalifu wa mtandaoni chini ya sekunde moja kuhujumu nywila yenye tarakimu nane.

"Nywila yangu ina tarakimu tano," alieleza Oliver. "Huo sio utani.Kwahiyo hiyo ni mbaya,sawa?" Snowden alikubaliana nae kwamba hiyo ni mbaya sana.

Kwahiyo watu wafanyeje kuhusu nywila zao? Wakati pendekezo la Oliver kuwa na nywila kama 'limpbiscuit4eva' lilionekana halifai,Snowden alikuwa na ushauri mzuri.Sahau kuhusu nywila zinazotumia maneno ya kawaida na badala yake tumia maneno marefu (paraphrases) ambayo ni rahisi kuyakumbuka, kwa mfano 'margaretthatcheris110%SEXY.' Mhalifu wa mtandaoni hawezi kuhisi neno kama hilo na wakati huohuo wewe utabaki na kumbukumbu ya neno hilo refu.


Kwa sie tunaotumia Kiswahili, ushauri wangu ni kujaribu kutumia mchanganyiko wa majina ya ndugu katika familia yenu na namba flani, bila kusahau herufi kubwa japo moja na tarakimu zisizo namba au herufi kama vile £ au % au $.

Unaonaje kama baada ya kusoma makala hii ukibadili nywila yako kuwa imara zaidi na hivyo kukuwezesha kukabiliana na jitihada za wahalifu wa mtandaoni kuihujumu nywila yako?



11 Apr 2015



Rais Barack Obama wa Marekani akipeana mkono na Rais Raul Castro wa Cuba, walipokutana katika mkutano wa nchi za Americas jijini Panama City,  Panama.

Tukio hili ni la kihistoria kufuatia uhasama mkubwa kati ya nchi hizo mbili.



10 Apr 2015

Africa is home to some of the richest countries in the world, in part due to its oil-rich soil and human capital. With GDPs going up as high as $594.257 Billion.
According to statistics provided by the International Monetary Fund(IMF), these are currently, according to the figures provided at the time, the Top 10 richest countries in Africa.
1. Nigeria: GDP – $594.257 billion
The most populous country in Africa is a major contender on this list, its manufacturing sector being the third largest in Africa while it contributes a considerable share of the world’s oil. Taking into account this country’s population of 170 million, Nigeria is on track to becoming one of the 20 largest economies in the world by 2020.

2. South Africa: GDP – $341.216 billion
South Africa is popularly known for its mineral resources such as gold and diamond but the Gold Rush ended back in the 19th century. There are more things to look forward to in South Africa besides its jewels. Major cities like Johannesburg and Cape Town offer a unique experiences that can offer scenic routes to mountain ranges by the ocean.

3. Egypt: GDP – $284.860 billion
Egypt has one of the longest histories of any modern country, arising in the tenth millennium BCE as one of the world’s first nation states.

4. Algeria: GDP – $227.802 billion
Oil and gas exports have placed Algeria on this list. Much of its wealth is received from oil deposits deep within the North African soil. Also rich in natural minerals, it is suggested that the ancientRomans collected stones and marbles from quarries in what is now known as Algeria. You can find onyx, red and white marbles, iron, lead, and zinc in large quantities. It’s capital city, Algiers offers rare beauty in the intricate architecture of its most famous buildings.

5. Morocco: GDP – $112.552 billion
Morocco was named the first most competitive economy in North Africa. Tourism, telecoms, textiles and agriculture are Morocco’s biggest biggest money pullers.

6. Sudan: GDP – $112.552 billion
More than once, we have mentioned oil and gas as the main source of income for countries on this list. Sudan also falls into that category but in a more diverse way. It depends on oil but with a third of its GDP contributed by agriculture. Cotton and peanuts constitute its major agricultural exports. You may not notice a “Made in Sudan” tag on the shirt you buy in Khartoum but cotton from Sudan has fueled the textile industry in many parts of the world.

7. Kenya: GDP – $53.40 billion
The capital, Nairobi, is a regional commercial hub. The economy of Kenya is the largest by GDP in Southeast and Central Africa. Agriculture is a major employer; the country traditionally exports tea and coffee and has more recently begun to export fresh flowers to Europe. The service industry is also a major economic driver. Kenya is a member of the East African Community. Compared to other African countries, Kenya enjoys relatively high political and social stability.

8. Angola: GDP – $49.857 billion
Angola has a large deposit of oil and gas resources, diamonds, and bountiful agricultural land. Still recovering from the 27-year civil war that lasted from 1975-2002, Angola has made efforts to revive its economy with heavy oil and agricultural exports. Cities like Luanda are undergoing major reconstruction to make Angola a top African destination.

9. Libya: GDP – $49.341 billion
The Libyan economy depends primarily upon revenues from the oil sector, which accounts for 80% of GDP and 97% of exports. Libya holds the largest proven oil reserves in Africa and is an important contributor to the global supply of light, sweet crude.Apart from petroleum, the other natural resources are natural gas and gypsum.The International Monetary Fund estimated Libya’s real GDP growth at 122% in 2012 and 16.7% in 2013, after a 60% plunge in 2011.

10. Tunisia: GDP – $49.122 billion
Oil, tourism and car manufacturing parts are the name of the game in Tunisia. It is one of the wealthiest countries in Africa so you won’t wander too far into its cities like Tunis before finding a pleasant spot to relax. The city is covered with bits of opulence from as far back as the 12th century. Year-round sunshine and the affordable Tunisian lifestyle have drawn tourists here who now call this place home.


SOURCE: IT NEWS AFRICA

A new infographic has revealed that it takes ten steps for women to make a purchase when shopping. The first being to search the Internet and fashion magazines for inspiration 

Women will then look online to compare prices to ensure they are getting the best deal 

Seeking a second opinion begins by sending a link to friends 

Those seeking a verdict from a wider audience will post an image on social networks 

Eager to be individual 12 per cent will search Instagram to check friends don't own the same outfit 


For one in seven a close female relatives opinion is the one that matters most 


Over half of us will make a special trip to experience a garment in real life 

One in five women will take a fitting room selfie once we have tried on a new outfit

And then we will send them to a friend or partner with our other-half considered the most valuable opinion

Most, two thirds, will complete a purchase in store but 29 per cent will ho home to complete it online

CHANZO; Daily Mail






NIANZE makala hii kwa kuomba radhi kwa makala zangu ‘kupotea’ kwa wiki mbili mfululizo. Hali hiyo ilitokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu.
Pia ningependa kutoa salamu za pole na rambirambi kwa ndugu zetu wa Kenya kufuatia shambulio kubwa la kigaidi lililotokea huko Garissa na kuuwa watu kadhaa.Ugaidi umeendelea kuwa moja ya matishio makubwa kwa usalama wa binadamu.
Wakati tukiungana na majirani zetu wa Kenya katika kipindi hiki kigumu, kuna dalili na sababu kadhaa za kiintelijensia na kimazingira zinazonipa wasiwasi kwamba Tanzania yetu inaweza kukumbwa na shambulio la kigaidi huko mbeleni (Mola aepushie). Hapa chini, ninabainisha dalili/ sababu hizo.
Tukio la ugaidi Garissa, nchini Kenya:
Wiki iliyopita, magaidi wa Al-Shabaab walifanya shambulio kubwa la ugaidi katika mji wa Garissa, uliopo mpakani mwa Kenya na Somalia.Shambulio hilo limepelekea vifo vya watu takriban 150 huku taarifa mbalimbali zikionyesha uwezekano wa kuwepo idadi kubwa zaidi ya waliouawa.
Awali, nilikuwa upande wa watetezi wa serikali ya Kenya na vyombo vya usalama vya nchi hiyo katika lawama kwamba walizembea kuchukua tahadhari. Hoja yangu kuu ilikuwa kwamba kupewa taarifa kuhusu ugaidi ni kitu kimoja, kuweza kuzifanyia kazi taarifa hizo na kuweza kuzuwia ugaidi ni kitu kingine kabisa.
Hata hivyo, utetezi huo umepungua baada ya kupatikana taarifa mbalimbali zinazoashiria mapungufu makubwa ya serikali ya Kenya na taasisi za Usalama nchini humo kukabiliana na tetesi walizopewa kuhusu uwezekano wa shambulio hilo la kigaidi.
Tukiweka kando kilichojiri nchini Kenya lakini tukitilia maanani ukweli kuwa nchi hiyo ilitahadharishwa kabla ya tukio hilo, kwa Tanzania hali ni tofauti. Hadi sasa hakuna taarifa rasmi ya uwezekano wa kutokea shambulio la ugaidi.
Hata hivyo, ni muhimu kutambua kuwa Kenya ina ushirikiano mkubwa zaidi na taasisi za kiusalama za mataifa makubwa zaidi ya Tanzania, hasa ikizingatiwa kuwa Marekani, kwa mfano, ina kituo chake cha kijeshi nchini humo (Manda Bay)
Kwa maana hiyo, tahadhari ya Wamarekani kwa Kenya sio tu kwa maslahi ya Kenya bali ya Wamarekani pia.
Hitimisho: Kwa kufanikiwa kufanya shambulio kubwa kabisa nchi Kenya, ikiwa ni takriban mwaka na nusu baada ya kufanya shambulio jingine la ugaidi kwenye supamaketi ya Westgate jijini Nairobi, magaidi wa Al-Qaeda wanaweza kushawishika kupanua kampeni yao ya uharamia hadi Uganda (ambako tayari kuna tishio kama ninavyoeleza hapo chini) na hata Tanzania (kwa sababu nitazobainisha mbeleni katika makala hii)
Uwezekano wa shambulio la kigaidi Uganda:
Machi 25 mwaka huu, Marekani ilitoa tahadhari kwa Uganda kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi nchini humo. Kama ilivyo kwa Kenya, Marekani ina maslahi yake nchini Uganda ambako inarusha ndege zake za upelelezi (PC 12) kutoka Entebbe, Kwa hiyo usalama kwa Uganda una maslahi kwa Marekani pia.
Hitimisho: Iwapo Al-Shabaab watafanikiwa kutimiza uovu wao kuishambulia Uganda (Mungu aepushe hili), wanaweza kupata motisha wa kutanua zaidi kampeni yao hadi Tanzania hasa kwa kuzingatia kuwa kundi hilo la kigaidi linaziona nchi hizi tatu kama kikwazo kikubwa kwa uhai wake.
Shaka ya ugaidi nchini Tanzania:
Moja ya matatizo makubwa ya kufahamu ukubwa au udogo wa tishio la ugaidi nchini Tanzania ni siasa. Kwa muda mrefu, chama tawala CCM kimekuwa kikiutumia ugaidi kama kisingizio cha kudhibiti vyama vya upinzani na baadhi ya viongozi wake. Kwa minajili hiyo, hata serikali ikitoa taarifa sahihi kuhusu uwezekano wa tishio la ugaidi, kuna uwezekano wa wananchi wengi kudhani hiyo ni siasa tu.
Kana kwamba hiyo haitoshi, mwaka huu Tanzania itafanya uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge hapo Oktoba. Japo haijazoeleka sana, historia inaonyesha kuwa angalau katika uchaguzi mkuu mmoja uliopita zilisikika taarifa za 'tishio la usalama' kutoka kwa nchi jirani. Mbinu hii hutumiwa na vyama tawala kujenga hofu ya kiusalama kwa wapigakura, na kuwaunganisha chini ya mwavuli wa chama kilichopo madarakani. Kwa mantiki hiyo, iwapo kutakuwa na taarifa za tishio la ugaidi, yayumkinika kuhisi baadhi ya wananchi wakatafrisi kuwa ni mbinu tu ya CCM kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.
Lakini tatizo kubwa zaidi kwa sasa ni imani ndogo ya wananchi kwa serikali ya Rais Jakaya Kikwete na nyingi ya taasisi za serikali yake. Uhaba huo wa imani unatokana na mchanganyiko wa hisia za ushahidi wa matukio yaliyopita. Kutokana na kuandamwa mno na kashfa za ufisadi, kumeanza kujengeka imani miongoni mwa Watanzania kuwa serikali yao ni ya kifisadi pia.
Matumizi mabaya ya 'taarifa za kiintelijensia' yamewafanya Watanzania wengi kuwa na hisia kuwa 'taarifa za intelijensia' ni mbinu ya serikali kuwadhibiti. Mara kadhaa, Jeshi la Polisi limekuwa likipiga marufuku maandamano ya kisiasa au kijamii kwa kisingizio cha 'taarifa za kiintelijensia'.
Hivi karibuni, zilipatikana taarifa za mapigano makali kati ya jeshi la polisi wakishirikiana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) dhidi ya 'magaidi' kwenye mapango ya Amboni mjini Tanga. Mchanganyiko wa taarifa za kukanganya na imani haba ya wananchi kwa jeshi hilo vilipelekea tukio hilo kuonekana kama 'mchezo wa kuigiza'.
Lakini licha ya kasoro hizo zinazoihusu serikali na taasisi zake, kuna tatizo jingine linalohusu vyombo vya habari vya nchini. Utitiri wa magazeti ya udaku na uhaba wa uandishi wa kiuchunguzi katika 'magazeti makini' umekuwa ukichangia mkanganyiko katika kubaini ukweli na porojo. Mfano mzuri ni tukio hilo la Amboni ambalo kwa kiasi flani liligeuka kama mfululizo 'series' ya mchezo wa kuigiza, huku magazeti ya udaku yakiwa na 'habari' nyingi zaidi ya 'magazeti makini.'
Hali hiyo yaweza kuwa inachangiwa na mahusiano hafifu kati ya taasisi za dola na vyombo vya habari, sambamba na mazoea ya taasisi hizo kutoa tu taarifa pasipo kuruhusu maswali kutoka kwa wanahabari. Ukosefu wa taarifa sahihi, sambamba na ugumu wa kupata taarifa hizo huchangia 'udaku' kuziba ombwe husika.
Tukiweka kando kasoro hizo hapo juu, hadi sasa kuna mambo yafuatayo ambayo yanaweza kuwashawishi magaidi kuvamia Tanzania.
1. Mgogoro wa muda mrefu kuhusu uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi
Japo hadi muda huu suala hili limeendelea kuwagawa Watanzania kwa njia za mijadala na kwa amani, yayumkinika kuhisi kuwa magaidi wanaweza kulitumia kama kisingizio cha kuishambulia Tanzania.
Cha kutia hofu ni ukweli kwamba si tu suala hili limedumu kwa muda mrefu, hasa baada ya chama tawala CCM kuahidi katika ilani yake ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2005 kuwa itaanzisha mahakama hiyo lakini imeshindwa kufanya hivyo hadi leo, bali pia uamuzi usio wa busara wa kuupeleka bungeni Muswada wa Uanzishwaji Mahakama ya Kadhi kisha kuuondoa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, majuzi Rais Kikwete alikaririwa akidai kuwa serikali haina mpango wa kuanzisha mahakama hiyo, na badala yake jukumu hilo linabaki kwa Waislamu wenyewe. Haihitaji uelewa wa sheria kujiuliza kwamba kama suala hilo lilikuwa la Waislamu wenyewe, lilipelekwa bungeni kwa minajili gani?
Licha ya mjadala huo wa uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi kuendelea kwa amani, mjadala kuhusu suala hilo umewagawa viongozi wa dini (Wakristo na Waislamu) na kwa kiasi flani umerejesha mgogoro kati ya baadhi ya viongozi wa Kiislam na serikali, sambamba na kuleta sintofahamu miongoni mwa baadhi ya wanasiasa.
Yayumkinika kuhisi kuwa magaidi wanaweza kutumia ‘mgogoro’ huo kama kisingizio cha kufanya uovu wao. Na hii ni juu ya malalamiko ya muda mrefu kuwa Waislam wamekuwa wakibaguliwa na serikali huku Wakristo wakionekana kupendelewa. Uzoefu unaonyesha kuwa vikundi vya kigaidi vya kimataifa vina kasumba ya kuteka hoja za ndani ya nchi na kuigeuza yao, kwa kisingizio cha kupigania Uislam.
2. Vitisho bayana kutoka kwa watu wanaodai ni magaidi.
Hivi karibuni ilipatikana video huko nyumbani ambapo mtu mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Kaisi Bin Abdallah alidai kuwa kundi lao limekuwa na mafanikio katika ugaidi wa kudhuru polisi na vituo vya polisi.
Licha ya 'mapungufu kadhaa' katika video hiyo, ambayo yanaweza kutupa imani kuwa ni porojo tu, yawezekana tishio lililo kwenye video hiyo ni la kweli. Na hili ni moja ya matatizo ya kukabiliana na tishio la ugaidi: kuchukulia taarifa kuwa ni za kweli au za kupuuza.
Hofu kuhusu uwezekano wa matukio ya ugaidi nchini Tanzania ilithibitishwa na kauli ya hivi karibuni ya Rais Kikwete kuwa mashambulizi ya hivi karibuni dhidi ya vituo vya polisi katika maeneo mbalimbali nchini humo yana uhusiano na ugaidi, japo hakubainisha iwapo kuna uhusika wa makundi ya kigaidi ya kimataifa au la.
3. Taarifa za kimataifa:
Hadi muda huu hakuna taarifa za moja kwa moja zinazoashiria uwezekano wa tukio la ugaidi nchini Tanzania. Hata hivyo, bado kuna hali ya tahadhari ya wastani kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi.
Wakati serikali ya Canada inaeleza kuwa haina 'ushauri unaohusu taifa (Tanzania) zima, inawashauri raia wake kuchukua tahadhari kubwa kuhusiana na ugaidi.
Kwa upande wake, serikali ya Uingereza inatoa angalizo la jumla tu japo inatahadharisha kuhusu tishio la ugaidi wa Al-Shabaab kwa eneo la Afrika Mashariki (ikiwa ni pamoja na Tanzania). Serikali ya Marekani inatoa ushauri wa jumla tu kwa kurejea matukio ya uvunjifu wa amani huko nyuma.
Hata hivyo, ripoti iliyotolewa Jumamosi iliyopita na taasisi ya HTH Worldwide kuhusu ‘hatari’ (risks) zinazoikabili Tanzania, ugaidi unatajwa kuwa ni tishio la kuaminika, japo uwezekano wa kutokea shambulizi la ugaidi ni wa wastani.
Pengine taarifa ya kuogofya zaidi ni ile iliyobainisha uwepo wa jitihada za kundi la kigaidi la ISIS kutaka kujiimarisha katika eneo la Afrika Mashariki, ikiwa ni pamoja na Tanzania. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ISIS inajaribu kujenga ushirikiano na Al-Shabaab kwa minajili ya kuwa na influence katika eneo la Afrika Mashariki.
Taarifa zaidi za kiintelijensia zinabainisha uwepo wa kikundi cha Al-Hijra nchini Tanzania, ambacho kinatajwa kama ‘tawi’ la Al-Shabaab nchini Kenya. Kwa mujibu wa taarifa hizo, kikundi hicho kinakadiriwa kuwa na wafuasi takriban 1,000.
Inaelezwa kuwa kikundi hicho kinafadhiliwa na Waislamu wa nje wa madhehebu ya Wasalafi (Salafist). Habari zaidi zinabainisha kuwa malengo ya kikundi hicho ni kuanzisha jihadi nchini Kenya na Tanzania. Uwepo wa kikundi hicho unadaiwa kusaidiwa na kikundi kingine cha Al-Muhajiroun ambacho kinatajwa kuwa na mahusiano na kikundi kingine cha kigaidi cha Al-Qaeda.
Kadhalika, majuzi zimepatikana taarifa kutoka Kenya kuhusu mwanamke mmoja wa Kitanzania aliyekamatwa na wenzie wawili Wakenya wakijaribu kwenda Somalia kuwa wenza wa magaidi wa Al-Shabaab.
Tukio hilo linaakisi kinachotokea katika nchi mbalimbali za huku Magharibi ambapo mabinti kadhaa wamekuwa wakitorokea Syria kwenda kuwa 'wenza' wa magaidi wa ISIS.
Vilevile, taarifa zilizopatikana muda mfupi kabla sijaandika makala hii zinaeleza kuwa mmoja wa wahusika wa shambulio hilo la kigaidi nchini Kenya ni Mtanzania. Haihitaji uelewa mkubwa wa intelijensia kutambua kuwa kama baadhi ya Watanzania wenzetu wanaweza kwenda kufanya ugaidi nje ya nchi, wanaweza pia kufanya ugaidi ndani ya nchi.
Hitimisho:
Ni vigumu kwa kuwa na hakika ya asilimia 100 iwapo magaidi watafanya shambulio au la. Kwa upande mmoja, magaidi wana muda wote wanaohitaji kabla ya kutimiza azma yao, yaani wanaweza kusubiri kwa muda mrefu, ilhali vyombo vya dola havina faida hiyo kwani vinatakiwa kuwa makini muda wote.
Kuna msemo maarufu kuhusu ugaidi, kwamba wakati magaidi wanahitaji DAKIKA MOJA TU kutimiza uovu wao, vyombo vya usalama vinahitaji KILA SEKUNDE YA DAKIKA kuwazuia magaidi husika.
Na japo uwepo wa taarifa za uhakika kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi unaweza kusaidia jitihada za kukabiliana na magaidi husika, ukweli mchungu ni kwamba, kuwa na taarifa ni kitu kimoja, uwezo wa kuzitumia taarifa hizo ni kitu kingine.
Wakati huu tunaungana na wenzetu wa Kenya kulaani unyama wa Al-Shabaab, ni muhimu kuchukua tahadhari mahususi ili kuweza kukabiliana na uwezekano wa magaidi hao kushambulia Tanzania.
La muhimu zaidi ni umoja na mshikamano, ambao kwa hakika unapotea kwa kasi, na haja ya haraka kwa serikali kurejejesha imani ya wananchi kwake. Kingine ni umuhimu wa kuweka kando siasa katika masuala nyeti kama haya..
Kubwa zaidi ya yote ni la kitaalamu zaidi. Wakati serikali ya Tanzania imekuwa ikitegemea zaidi misaada ya kimataifa katika kuiimarisha kiuwezo Idara ya Usalama wa Taifa, ni muhimu jitihada za ndani pia zielekezwe katika kuijengea uwezo wa kukabiliana na matishio mbalimbali ya usalama wa taifa letu, ikiwa ni pamoja na hilo la ugaidi.
Kwa uelewa wangu, uwezo wa vitengo vya kuzuwia ugaidi na kitengo cha kupambana na ujasusi unaathiriwa na mapungufu ya kimfumo na kisera, sambamba na nafasi ya maafisa wa Idara hiyo kwenye balozi mbalimbali za Tanzania nje ya nchi 'kubweteka' na hisia ya teuzi zinazodaiwa kufanywa kwa misingi ya undugu, urafiki au kujuana.
Lakini changamoto kubwa zaidi kwa Idara yetu ya Usalama wa Taifa ni kurejesha imani kwa Watanzania. Nimeshawahi kuandika mara kadhaa kwamba kushamiri kwa ufisadi huko nyumbani kunachangiwa na udhaifu wa taasisi hiyo nyeti.
Zama za Idara hiyo ‘kuogopwa’ zimegeuka na kwa kiasi kikubwa taasisi hiyo, ambayo moja ya mafanikio yake makubwa huko nyuma yalikuwa kusimama imara dhidi ya njama na hujuma za utawala wa Makaburu, kwa sasa inaonekana kama sehemu ya mfumo wa kifisadi. Ili Idara yetu ya Usalama wa Taifa iweze kukabiliana na tishio hili la ugaidi inabidi iaminike kwa wananchi.
Mwisho, tishio hili la ugaidi sio la kufikirika. Lipo, na kwa bahati mbaya, mazingira ya kulirutubisha yapo pia. Japo si rahisi kuzuia ugaidi kwa asilimia 100, mikakati madhubuti ya kiintelijensia hususani katika kukabili ugaidi (counterterrorism) inaweza kuwakwaza magaidi kufikiria kuivamia nchi yetu

6 Apr 2015

Twaishi katika dunia ya mfumo dume, na mfumo huo umeota mizizi zaidi katika bara letu la Afrika. Japo jitihada za kitaifa na kimataifa zimeanza kuzaa matunda na sasa twashuhudia taaluma na yandhifa mbalimbali zilizozoeleka kuwa 'za kiume' zikikaliwa na akinamama.

Mfano mmoja wa 'wanawake wanaweza' ni huyu mwanamama, Gladys Sonto Kudjoe, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ushushushu la Afrika Kusini. Hii ni moja ya nyadhifa nyeti kabisa katika taifa lolote lile duniani, kwa sababu ushushushu ndio uti wa mgongo wa taifa (kuna wataokwambia uti wa mgongo wa taifa ni siasa au uchumi...think again!)




Anyway, hapa chini ni wasifu wake (kwa kimombo)

AMB GS KUDJOE

DIRECTOR-GENERAL: STATE SECURITY AGENCY
CURRENT POSITION/S
Ambassador Sonto Kudjoe currently serves as the Director-General of the State Security Agency.  She was appointed into her position in August 2013.
ACADEMIC QUALIFICATIONS 
1981 - 1987: BA and MA Degree in Law.  Specialised in Criminal Law at the Kishinev State University, in the former Soviet Union.

1992 - 1994: Post-graduate Placement Training Programme on the Administration of Criminal Justice and Criminology at the University of Hull, England.
1997: Diploma in Project Management, Damelin, Pretoria.
CAREER / POSITIONS / MEMBERSHIPS / OTHER ACTIVITIES
Prior to her appointment to her current position, Ambassador Kudjoe was with the Department of International Relations and Cooperation (DIRCO), formerly know as the Department of Foreign Affairs.  She has occupied several positions whilst at DIRCO. 
Ambassador Kudjoe held the position of Deputy Director-General: Africa Multilateral.  Her areas of focus whilst in this position dealt primarily with the development and implementation of policies relating to the African Union (AU), the Southern African Development Community (SADC), the New Partnership for Africa's Development (NEPAD), as well as peace and security issues on the African continent. 
Prior to the above position, Ambassador Kudjoe was Deputy Director-General responsible for the Africa Bilateral branch, concentrating on strengthening relations between South Africa and countries on the continent. 
From 2000 to 2002, Ambassador Kudjoe was appointed as the first Chief Director, Africa Multilateral.  Her main responsibilities, amongst others, were the establishment of a new Chief Directorate: Africa Multilateral, the development and implementation of its business plan. 
Between 2002 and 2006, she served as South Africa's Ambassador to Sweden.  She has also served as the country's Ambassador to Egypt for the period 2006 to 2010. 
Ambassador Kudjoe's professional experience also includes working at the former South African Secret Service (SASS) as a Manager responsible for Research, Analysis and Policy Advice on various issues related to Africa.  She has also held the position of Deputy Executive Director at the National Institute for Public Interest Law and Research.



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.