21 Jul 2015




Juzi nilipatiwa uthibitisho wa kitu nilichokwishaambiwa awali: Idara yetu ya Usalama wa Taifa iliandaa operesheni dhidi ya mtu aliyepaswa kuja Tanzania kumzika baba yake. 

Nilipata taarifa kuhusu kinachoendelea katika Idara hiyo masaa kadhaa baada ya kutangaza kuwa baba yangu, Mzee Chahali amefariki. Afisa mmoja wa Idara hiyo alinipa ushauri kuwa nisije huko nyumbani kwa sababu kuna hujuma dhidi yangu. Kuthibitisha kuwa taasisi hiyo ni ya kibabaishaji, nilipata taarifa hizo muda mfupi tu baada ya maandalizi ya operesheni hiyo, and guess what, mie nipo Uingereza. Sasa kama mie nisiye na hatia yoyote na masikini nisiye na fedha za kuhonga, jiulize, ni wauza unga wangapi wenye mamilioni ya kuhonga  wanaopewa taarifa huko nyumbani kutoka katika Idara hiyo na taasisi nyingine za dola.

Sijawahi kuficha kuwa nilikuwa mtumishi wa taasisi hiyo. Nilikuwa mtumishi mwaminifu kwa takriban miaka 15 hadi mwaka 2008 nilipoamua kuachana nayo. Sijawahi kutamka nini kilichonifanya kuchukua uamuzi huo, lakini kwa kifupi maisha yangu yalikuwa hatarini baada ya kuzushiwa kosa ambalo ni sawa na uhaini. Kwa kifupi, ukiwa mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa ya nchi yeyote ile, kosa la 'kutumikia Idara ya Usalama wa Taifa ya nchi nyingine' ni kile kwa kimombo kinaitwa 'treasonable offence,' yaani kosa la kihaini. Kwanini nilizushiwa hilo, hiyo ni hadithi nyingine, ila sijawahi kuitumikia taasisi nyingine ya Usalama wa Taifa  zaidi ya hiyo ya nchi yangu.

Mwaka 2002, Idara hiyo ilinipatia skolashipu ya kuja kusoma shahada ya uzamili (Masters) huku Uingereza. Baada ya kumaliza shahada hiyo, niliomba ruhusa ya kusoma shahada ya uzamifu (PhD). Lakini kwa vile shahada ya uzamili niliyosoma haikuwa ya kiutafiti (research-based), ilinilazimu kusoma shahada nyingine ya uzamili (MRes) ambayo ni ya kiutafiti, na nilipomaliza nilijiunga na shahada ya uzamifu. Hayo yote yalifanyika kwa ruhusa ya taasisi hiyo.

Matatizo yangu na Idara hiyo yalianza Oktoba mwaka 2006, baada ya mie kuchapisha makala iliyokuwa ikimkemea aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, Edward Lowassa, kuhusu taarifa za vyombo vya habari vya huko nyumbani kuwa alikuwa akijaribu kuzima mjadala wa skandali ya Richmond. Mmoja wa Wakurugenzi katika Idara hiyo alinipigia simu ya vitisho akinituhumu kuwa 'ninawasidia wapinzani,' 'ninaikosoa serikali ilhali mie ni mtumishi wake (kwa wakati huo),' na kubwa zaidi, kuhoji iwapo ninaitumikia Idara ya Usalama wa Taifa ya nchi nyinyingine. Kadhalika, press secretary wa Lowassa alisambaza makala kali kunikemea

Walinileta huku kusoma stadi za siasa, sasa mie kupevuka kifikra kuhusu vikwazo vya siasa yetu katika maendeleo ya taifa letu ikawa kosa. Uzalendo ulinishinda, ndio maana ikanilazimu kukosoa maovu mbalimbali yaliyokuwa yanawaumiza walalahoi wa Tanzania. Kichekesho ni kwamba kile nilichoandika 2006 na kushambuliwa vikali, ndicho kilichotokea miaka miwili baadaye, na kulazimisha Lowassa kujiuzulu. Na hakuna aliyenipongeza.

Mwaka 2008 nilikuja huko nyumbani kwa miezi kadhaa kumuuguza marehemu mama yangu. Nikidhani kuwa watumishi wenzangu katika Idara hiyo walikuwa wakielewa kilichokuwa kikinisibu wakati huo, wakanisumbua vya kutosha, na hatimaye njia pekee niliyobakiwa nao ilikuwa kuondoka huko nyumbani - japo baba alikuwa taabani kutokana na kifo cha mkewe aliyedumu nae kwenye ndoa kwa miaka 53. Na niliporudi huku, usumbufu ukaendelea: vitisho na upuuzi mwingine. Kwa ushauri wa taasisi za hapa, na kwa kuzingatia kuwa maisha yangu yalikuwa hatarini, nikaamua kuachana na taasisi hiyo. So ukiangalia hadi hapo, sikuwa nimefanya kosa lolote la kustahili kusumbuliwa kiasi hiki.

Kuhusu tukio la majuzi, masaa kadhaa baada ya kutangaza kuwa baba yangu amefariki, nililetewa taarifa ya uwepo wa operesheni maalum dhidi yangu, na aliyenipa taarifa hiyo alinisihi nisije huko nyumbani. Nimeambiwa kuwa Idara hiyo iliweka maofisa wake airport ili 'kunipokea.' Lakini baada ya kutoniona, walituma maafisa watatu, wawili wanaume na mmoja mwanamke, kwenda Ifakara 'kushirikiana nasi kwenye mazishi.' Wahuni hawa hata hawana ubinadamu.

Sijui wametumia kiasi gani cha fedha za walipakodi kukesha macho airport kunisubiri, na sijui hadi sasa washatumia kiasi gani huko Ifakara kuendeleza operesheni yao fyongo. Hawa wahuni hawataki kujifunza. Mwaka juzi, mwezi Februari, walituma watu kuja kunidhuru hapa Uingereza. Kwa vile Idara hiyo inaiendeshwa kishkaji, nadhani walituma wababaishaji walioishia kudakwa na mashushushu wa hapa Uingereza, ambao baadaye waliwafahamisha Polisi hapa Glasgow kuwa nichukue tahadhari muhimu. Na tangu wakati huo nimekuwa nikiishi na uelewa kuwa kuna mtu flani, siku flani atajaribu kunidhuru. Sio rahisi kuishi namna hiyo lakini sio impossible.Na hili tukio la majuzi limekuwa kama 'wake-up call' kwamba hujuma hizo dhidi yangu bado zipo hai.

Nilipokuwa mtumishi wa taasisi hiyo, niliitumikia kwa uadilifu mkubwa, na nilifanya kazi katika vitengo mbalimbali.Lakini kubwa zaidi, hadi ninaondoka huko nyumbani kuja huko kimasomo, nilikuwa Mkuu wa Kanda ya Kiintelijensia katika moja ya kanda zake jijini Dar. Huo si wadhifa mdogo, na ninakumbuka nilipowaambia maafisa wangu kuwa nakwenda Uingereza kimasomo, wapo walioniuliza 'sasa bosi unataka nini zaidi ya hiki ulichonacho sasa?' Japo wakati huo nilikuwa na shahada moja kutoka UDSM, dhamira yangu siku zote ilikuwa kukamata udaktari wa kitaaluma, na nilipopewa skolashipu kuja huku kimasomo, sikufikiria mara mbili.

Enough about that. Laiti Idara yetu ya Usalama ingekuwa na vipaumbele mwafaka basi ingehangaika na wahalifu waliokimbilia kwenye siasa na kuwadhibiti au ingehangaika na tishio la usalama wa taifa letu katika biashara ya madawa ya kulevya. Wanazidi kujaza mafaili kwenye masjala yao yenye majina ya wauza unga lakini wapo bize na watu kama sie tusio na hatia.

Wengi wenu mnanifahamu kama 'mropokaji' lakini kwa vile nilikula kiapo cha utiifu, hata siku moja sijawahi kuropoka kuhusu mambo mbalimbali niliyoshuhudia au kushiriki wakati nikiwa mtumishi wa taasisi hiyo. Sasa kwanini niendelee kuonekana adui? 

Hiyo operesheni fyongo ya mwaka juzi ilinishtua, lakini hii ya majuzi imenichukiza. Ushauri wangu pekee kwa Idara hiyo ni wa aina mbili: kwanza, fedha za Watanzania zinazopotezwa kufuatilia watu wasio na makosa zielekezwe katika kuimarisha uwezo wa Idara hiyo kupambana na wahalifu halisi wanaotishia usalama wa taifa letu, eg mafisadi , wauza unga, majangili, nk. Lakini pili, nimewashauri pia kwamba fedha zinazotumika kutufutilia akina sie' zielekezwe kwenye mafunzo ya maofisa wanaokabidhiwa majukumu ya aina hiyo. Walijaribu kuja kunidhuru hapa UK wakaishia kuumbuka. Na sasa wamejaribu kunishughulikia huko nyumbani, wameishia kupata hasara ya bure. Lakini wahuni hawa hawana uchungu na fedha wanazotumia kwa operesheni fyongo kwa vile hazitoki mfukoni mwao.

Sikupenda kzungumzia suala hili hadharani lakini imenilazimu kufanya hivyo hasa baada ya kufahamishwa kuwa familia yangu huko Tanzania inaishi kwa hofu baada ya kufahamishwa kuwa kuna watu wapo Ifakara kwa 'nia mbaya' dhidi yangu. Ninatambua hii ni vita ya sisimizi (mie) na tembo (Idara hiyo) lakini cha kutia matumaini ni vitu viwili: siku zote Mungu husimama na wanaonyanyaswa, na pili, mafunzo aliyopitia tembo ndio aliyopitia sisimizi. Hapa ni suala la akili ya nani iko mbele ya mwenzie, na ninaamini kuwa kamwe operesheni hizo fyongo hazitofanikiwa. Mlinifunza 'constant vigilance of an officer.' For your information, kwa hakika ninaitumia vizuri sana. This is a battle of wits...and sadly for you, I am still winning.

Sijaandika haya kusaka huruma ya mtu flani au taasisi hiyo. Nimeamua tu kuweka rekodi bayana. 

Asanteni kwa kuchukua muda wenu kunisoma

MESSAGE SENT AND DELIVERED.

18 Jul 2015

MOGADISHU: Kiongozi wa kikundi cha kigaidi cha Al-Shabaab jana Ijumaa alitoa ujumbe wa sikukuu ya Idd Elf Fitr ambapo alitoa wito wa  kupata  magaidi wapya ili 'kuondoa maumivu ya Waislamu' katika eneo la Afrika Mashariki.

Katika taarifa ambayo inaonyesha dhamira ya magaidi hao kusambaza ubaradhuli wao, kiongozi huyo, Ahmed Diriye, ambaye pia hujulikana kama Ahmed Umar Abu Ubaidah, alizionyooshea kideole Kenya, Ethiopia, Djibouti na Uganda.

"Majambia ya Mujahidina yameshatolewa kibindoni na mashambulizi dhidi ya maadui yanaendelea...na tunawataka wapiganaji wetu kuongeza mashambulizi dhidi ya makafiri," alisema katika taarifa iliyowekwa kwenye tovuti ya Waislam wenye msimamo mkali.

"Tunasema kwa jamaa zetu wapendwa wanaoishi kwenye maeneo yaliyo chini ya ukoloni wa Kenya kwamba sisi jamaa zenu hatotuacha kuja kuwasaidia."

"Mnapaswa kufahamu kuwa jihadi ndio njia pekee ya kujikomboa wenyewe kutoka katika unyanyasaji na udhalilishaji mnaokabiliana nao, kwahiyo mharakishe kujiunga na jihadi...na kuyakomboa maeneo yenu kutoka kwa Wakristo."

Diriye alipongeza shambuli la kigaidi katika chuo kikuu cha Garissa, Kaskazini Mashariki mwa Kenya, ambao magaidi wanne wa kikundi hicho waliwaua watu 148, wengi wao wakiwa wanafunzi. Wengi wa magaidi hao walikuwa Waislam kutoka nchini humo.
"Tunawapongeza ninyi na na Waislamu wengini duniani kwa operesheni ya kijasiri katika chuo kikuu cha Garissa," alisema kiongozi huyo wa magaidi, akieleza kuwa shambulio hilo lilikuwa la kulipiza kisasi kwa 'mauaji yaliyoidhinishwa na serikali ya Kenya dhidi ya mashehe na utekaji vijana wa Kiislam' kwenye maeneo ya pwani ya nchi hiyo.ambaye wakazi wake wengi ni Waislam.

"Muda wa Wakristo kufanya unyama bila kuwajibishwa umefikia kikomo," alisema. " Tunaswali kwako Mola kuodnoa maumivu ya Waislam katika Afrika Mashariki nzima - Ethiopia, Uganda na Djibouti."

"Hatotoacha jitihada za kuwasaidia, na milango ya mafunzo katika makambi yetu ipo wazi kuwapokea na makazi yetu yapo wazi kuwakaribisha."

Al-Shabaab, jina lenye maana 'vijana' kwa Kiarabu, waliibuka wakati wa mapambano makali dhidi ya majeshi ya Ethiopia, ambayo yaliingia nchini Somalia mwaka 2006 katika uvamizi ulioongozwa na Marekani kuung'oa utawala wa Muunganowa Korti za Kiislam ambao wakati huo ulikuwa ukitawala mji mkuu wa Mogadishu.

Magaidi wa Al-Shabaab wameendelea kufanya mashambulizi ya mara kwa mara, yenye malengo ya kupina madai kuwa kikundi hicho kinakaribia kushindwa kwenye operesheni inayoendeshwa na majeshi ya Somalia na yale ya Umoja wa Afrika, mashambulizi ya ndege ndogo zinazojiendesha zenyewe (drones) yanayofanywa na Marekani dhidi ya viongozi wa kikundi hicho, sambamba na wapiganani wanaotoroka kutoka katika kundi hilo la kigaidi.
Wakati hivi sasa kundi hilo la kigaidi linaungwa mkono na kundi jingine la kigaidi la kimataifa, Al-Qaeda, hisia zimekuwa zikiongezeka kwamba kundi hilo la Somalia linaweza kuhamisha utiifu wake kutoka kwa Al-Qaeda na kuelekea kwa kundi jingine hatari kabisa la kigaidi kimataifa la Dola ya Kiislam (Islamic States) au ISIS (kama linavyofahamika kwa kifupi).

Wakati flani, Al-Shabaab ilikuwa sumaku ya kuvuatia wapigania vijana wapiganaji kutoka mataifa mbalimbali, lakini mkakati wao kuwavutia wapiganaji wa kigeni umeathiriwa na kushamiri kwa ISIS huko Syria na Iraq, sambamba na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe ndani ya Al-Shabaab.

CHANZO: Imetafsiriwa kutoka tovuti ya eNCA



14 Jul 2015


Nitakuwa siwatendei haki kwa kusema ASANTE au SHUKRANI pekee. Kwa hakika ni vigumu sana kupata neno/ maneno sahihi yenye kuonyesha shukrani za dhati kwa wema mkubwa uliofanyiwa. Labda niseme hivi: nawaombea Mwenyezi Mungu awabariki sana kwa upendo mkubwa na sapoti kubwa kabisa mliyonipatia mie na familia ya Marehemu Mzee Philemon Chahali.

Ninyi sasa ni familia ya Mzee Chahali kwa sababu wengi wenu mlishirikia kumfanyia sala/dua ili apone lakini bahati mbaya akafariki, na mkajitokeza kwa wingi wenu kumlilia kwa salamu zenu za rambirambi lukuki. Sidhani kama kuna upendo mkubwa zaidi ya huo. 

Kitu kimoja nina hakika nacho ni kwamba japo sasa ni marehemu, Mzee Chahali ametuacha akithamini sana upendo wenu usiomithilika. Dua/sala alipokuwa anaumwa na salamu za rambirambi zitoka kwa zaidi ya watu 850 kwa ujumla wenu. Inawezekana idadi ni kubwa zaidi ya hiyo kwa sababu nilishindwa kuhesabu watu wote.

Historia fupi ya marehemu Mzee Chahali ni kama ifuatavyo, Alizaliwa Ifakara tarehe 22/11/1930 na kupata elimu yake katika zama za Ukoloni, kitu kilichomfanya athamini sana elimu kwa sie wanae. Baadaye alifunga ndoa na marehemu mama yetu Adelina Mapngo, ndoa iliyodumu hadi mama alipofariki Mei 2008, ikiwa imedumu kwa miaka 53. Katika uhai wake, baba na mama walijaaliwa kupata watoto tisa, japo mmoja alitangulia mbele ya haki na kwa sasa tumebaki wanane, wanaume sita na wanawake wawili.

Moja ya mafanikio makubwa katika maisha ya marehemu baba ni kuwa mmoja wa mapostamasta wa kwanza wazalendo baada ya uhuru. Kwangu binafsi, moja ya legacies za baba ni kunifanya nipende habari. Kwa kawaida, alipokuwa akitoka kazini alikuja na rundo la magazeti, aliyasoma kisha kutusimulia kilichomo katika magazeti hayo. Vilevile alihakikisha hakosi kusikia taarifa ya habari ya Redio Tanzania zama hizo, na vituo vya redio vya kimataifa kama vile BBC Swahili , Sauti ya Ujerumani na Voice of Amerika kila ilipowezekana. Ile tabia ya kusoma/kusikikia habari kisha kutusimulia hatimaye ilihamia kwangu ambapo kwa hakika ninashindwa kujizuwia kukutana na habari kisha nisiishirikieshe jamii aidha katika blogu hii au kwenye makala za Raia Mwema au kwenye tweet au Facebook.

Baada ya ujio wa televisheni, Mzee alikuwa akitumia muda mwingi kufuatilia habari. Na kila mara nilipompigia simu alikuwa akiniulizia kuhusu habari za kimataifa. Hofu yake kubwa ilikuwa katika maeneo mawili. Kwanza alikuwa anapata wasiwasi sana akiona kwenye TV kuhusu matishio ya ugaidi yanayozikabili nchi za Magharibi ikiwa pamoja na hapa Uingereza ninapoishi. Kingine ilikuwa ni wasiwasi wake kuhusu athari zinazoweza kujitokeza kutokana na makala zangu magazetini hasa pale nilipoonekana nina msimamo mkali. Baba alipatwa na hofu kubwa aliposikia kwamba kwa wakati flani maisha yangu yalikuwa hatarini kutokana na tishio lililotoka huko nyumbani. Nilijitahidi sana kumpa matumaini lakini kwa hakika alikuwa na hofu kubwa hasa kila nilipokosa kufanya mawasiliano nae japo kwa siku chache.

Miongoni mwa vitu ninavyobaki ninasikitika kwa maana ya 'kumwangusha' marehemu baba ni, kwanza, kutotimiza lengo lake la mie kuwa padre. Nilipomaliza darasa la saba nilichaguliwa kujiunga na seminari ya Kasita huko Morogoro lakini pia nilikuwa nimefaulu kujiunga na sekondari ya serikali. Nikafuata moyo wangu, sikwenda seminari nikajiunga na sekondari ya serikali. Hilo lilimuumiza sana baba, lakini kwa bahatio nzuri alifanikiwa kumshawishi mdogo wangu wa kike na kumwingiza kwenye usista ambao anautumikia hadi leo.

Kingine ni faragha kidogo, ila kwa kifupi, ilinigharimu miaka kadhaa kabla sijamfahamisha nilikuwa ninafanya kazi gani nilipokuwa mtumishi wa umma huko Tanzania. Nilipomjulisha na kumfahamisha kwanini sikumweleza mapema, alinielewa. Lakini hapohapo nikawa nimemwanzishia hofu mpya akidhani kuwa kazi hiyo ilikuwa ya roho mkononi. Na hata aliposikia kuwa 'nimeachana na kazi hiyo,' baba alifanya sala kwenye simu kumshukuru Mungu akinieleza kuwa ilikuwa ikimyima amani rohoni.

Mzee Chahali alifariki tarehe 8/7/15 kutokana na mchanganyiko wa maradhi lakini kubwa likiwa tatizo la moyo. Hata hivyo, baada ya mkewe wa miaka 53- marehemu mama - kufariki mwaka 2008, mzee aliyekuwa na takriban miaka 10 zaidi ya mama, alishindwa kabisa kukabiliana na ukweli kuwa mkewe amemtangulia. Mara kadhaa nilipoongea nae alikuwa akimkumbuka mkewe na kutamani kuwa nae. Kimsingi, marehemu baba na marehemu mama walikuwa zaidi ya mke na mume. Walikuwa marafiki pia hasa kwa vile Mzee Chahali alikuwa mkimya sana na mwenye marafiki wachache. 

Sijui niwaelezeje kuhusu kifo hiki kilivyoniathiri binafsi. Baada ya mama kututoka, mzazi pekee tuliyebakiwa nae alikuwa baba. Sasa tumabaki yatima. Kwa hakika inauma sana.  Lakini yote ni kazi yaMungu.

Mzee Chahali amezikwa kwa heshima zote, ambapo kwa mji wetu wa kidini sana, misa ya mazishi kuendeshwa na Askofu ni heshima kubwa sana, na kwa hakika tunalishukuru sana jimbo la Mahenge kwa kumthamini Mzee wetu kiasi hicho.

Lajkini sijui kama leo hii ningekuwa katika nafasi ya kuandika makala hii bila sapoti yenu kubwa mno. Kila nilipotupa jicho Facebooka au Twitter nilikuta rundo la salamu za kumwombea dua/sala baba alipokuwa mgonjwa, na rundo kubwa zaidi baada ya kuwatangazia taarifa za msiba. Ninawashukuru sana sana sana. Nawaombea kwa Mwenyezi Mungu awabariki mno na awazidishie upendo wenu.

Jana nilibandika Makala Maalumu ya Sauti lakini kwa kutambua kuwa si kila mmoja ana muda au access ya kuskiliza audio filela takriban dakika 30 nikaona ni bora niziwasilishe tena salamu hizi za shukrani kwa maandishi.

Ninaomba mniruhusu nisimtaje kila mmoja wenu kwa sababu sio tu mpo wengi sana bali pia ukweli kwamba shukrani za dhati huwa moyoni. Naweza kujibaraguza hapa na sante zangu nyiiingi lakini moyoni nina mawazo mengine. Ila kwa hakika Mungu ndo shahidi wangu. Ninathamini mno mchango wenu wa hali na mali katika kumuuguza baba na kushiriki katika mazishi yake kwa njia ya rambirambi.

ASANTENI SANASANA SANA. SINA MANENO SAHIHI YA KUWAAMBIA LAKINI NINAWAOMBEA BARAKA TELE KUTOKA KWA MWENYEZI MUNGU.

Mwisho, Pumziko la Milele Bwana Mungu ajmjaalie Mzee Chahali, na mwanga wa milele amwangazie apumzike kwa amni, Ameni

ASANTENI SANA

8 Jul 2015

Ufuatao ni waraka kutoka kwa Chama cha DP kinachoongozwa na Mchungaji Christopher Mtikila kumpiga mwania nia ya Urais Edward Lowassa

KATIKA UCHAGUZI MKUU HUU
TUSIRUHUSU MAFISADI WALICHEZEE TAIFA
Edward Lowasa ni balaa kwa Taifa!

Democratic Party (DP) inatarajia kufikisha Mahakamani chama cha
CCM pamoja na wanachama wake sita, Edward Lowasa na wengine,
kwa mujibu wa Ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Tanzania, kwa kosa kubwa sana la kuvunja Katiba na Sheria za Nchi kwa kuanza kampeni ya Uchaguzi kabla ya wakati unaopasa kwa mujibu wa Sheria.

1. Tunao ushahidi mzito unaothibitisha kwamba Edward Lowasa na
wenzake walianza kampeni ya urais ndani ya chama chao kabla ya
wakati, na kwamba chama chao kiliwapa adhabu ya kutofanya siasa
kwa miezi 12. Lakini safari hii Lowasa ameanza kampeni ya urais
Arusha kwa mkutano mkubwa sana wa hadhara wa kampeni haramu
na kumwaga rushwa ya kutisha!

2. Kama ni wadhamini alipaswa kuwapata katika ofisi za chama chake, katika mikoa nane (8) tu Tanganyika na mikoa miwili tu Unguja na Pemba, wadhamini 45 tu katika kila mkoa. Lakini Edward Lowasa amefanya mikutano nchi nzima, ya kuwaahidi maelfu ya wananchi katika kila mkutano wa hadhara, mambo atakayofanya kama wakimpa kura zao awe Rais! Hii ndiyo kampeni halisi, ambayo ni ukiukaji wa Katiba na Sheria za Nchi! Uchaguzi Mkuu unaendeshwa na Sheria, hivyo ni lazima Sheria ichukue mkondo wake dhidi yake kwa kuivunja.

3. Edward Lowasa amevunja Katiba ya Nchi na Sheria ya kiwango cha
fedha kinachoruhusiwa kutumika katika shughuli halali za Uchaguzi,
kiasi kwamba CCM na Taasisi zote za uchunguzi wa kifedha nchini,
upelelezi wa Jinai na Usalama wa Taifa ni mlazima wanayo kazi muhimu sana ya kupata ukweli kuhusu haya mabilioni ya fedha yanayomwagwa nchini na fisadi Edward Lowasa, ameyapata wapi na kwa namna gani, kumehusika ‘’Money laundering’ au la, kama mapato ya mapesa hayo yote ni halali, na kama mapato hayo yote yalilipiwa kodi inayopasa kwa ajili ya Taifa.

Ni marufuku kabisa tena ni makufuru Edward Lowasa kuruhusiwa
kugombea urais, kwa sababu amevunja Katiba ya Nchi na Sheria na
Kanuni za Uchaguzi. Sifa mojawapo ya kustahili kugombea uongozi wa nchi yoyote ni maadili mema na uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na
taratibu za Utawala wa Sheria
4. Edward Lowasa, kwa kujimilikisha maeneo nchi nzima kwa kutumia kifisadi Uwaziri wake wa Ardhi, ameliweka Taifa katika hatari kubwa ya mmwagiko wa damu baina ya wakulima na wafugaji, baada ya kueneza nchi nzima makundi ya ng’ombe wake, na kusababisha mapigano makali ya mara kwa mara kila mahali nchini kati ya wafugaji wake na wakulima. Kwa sababu ya uovu huu hata katika kampeni yake haramu Lowasa ameshindwa kusema lolote juu ya kilimo, ingawa ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi yetu na ndiyo shughuli inayotunza uhai wa asilimia 95 ya wananchi!

Kwa kuwaingilia wakulima katika ardhi yao, kuwaua ovyo, kuwaonea
kiasi cha kufisha matumaini yao katika kilimo, kumeifanya kauli mbiu ya “Kilimo kwanza” kuwa porojo tu ya kisanii!

5. Edward Lowasa ni mwiko kabisa kupewa kugombea urais, kwa
sababu siyo tu aliutumia kifisadi Uwaziri wa Ardhi akajitajirisha na
kujipatia maeneo makubwa ya ardhi nchini kote, bali alitumia kifisadi
zaidi uwaziri wa nchi katika ofisi ya Waziri Mkuu, katika uagizaji wa
mashangingi ya Wabunge, mawaziri, wakuu wa Mikoa na Wilaya.

6. Edward Lowasa alikemewa mnamo mwaka 1995 na Mwalimu Nyerere anayeenziwa na CCM lama “Baba” yao, alipotaka kugombea urais, kwa sababu alikuwa fisadi papa, wala hakuweza kujitetea kwavile utapeli wote aliojitajirishia ulikuwa mezani. Leo baada ya mabiashara haramu mengi na kulipora sana Taifa kukiwa ni pamoja na utapeli wa “kununua mvua Thailand” na kuliibia Taifa mabilioni ya fedha kwa kutumia kampuni hewa ya RICHMOND, huyu ni fisadi-nyangumi. Ni mlemavu wa rushwa tu wa kununuliwa na mapesa machafu anayomwaga Lowasa, anayeweza kumruhusu fisadi Edward Lowasa agombee urais.

Sifa za mtu wa kukugombea Urais zimeelezwa bayana na Mwenyezi
Mungu katika Kumbukumbu la Torati 17:15-20, ambazo Edward
Lowasa hana hata mojawapo! Lowasa awali alikemewa na Mwalimu
Nyerere ambaye CCM wanamuenzi kama “Baba” yao, kuwa hafai kabisa kuwania urais, kwa sababu alikuwa fisadi papa, kama alivyomtangaza hata Reginald Mengi pale alipolazimika kujiuzulu Uwaziri Mkuu kwa ajili ya wizi kwa kampuni hewa ya Richmond, lakini leo akiwa fisadi la kutisha zaidi kuliko papa eti anataka urais!
Si ajabu kwamba magabacholi yalioipora vibaya sana Nchi hii kama Sigh Setti na hata Nazir Karamagi wote wamo katika genge la Edward
Lowasa! Si ajabu hata fisadi Reginald Mengi leo kuungana na fisadi
Lowasa yakizingatiwa machafu yake yeye mwenyewe, na kuhusika kwa Mengi na mauaji ya Chacha Wangwe, pamoja na mpango wa Chadema
wa kumwua Mchungaji Mtikila, waraka feki wa kujaribu kuupotosha
ukweli ukatangazwa kwa ITV yake.

Katika uwaziri wake katika ofisi ya Waziri Mkuu, na katika Uwaziri wakewa Ardhi na Uwaziri Mkuu, Lowasa alifanya ufisadi ambao katika nchi kama China zenye uchungu na maslahi ya mataifa yao angekuwa wa kupigwa risasi hadharani, lakini katika nchi yetu anatafuta urais!

7. Edward Lowasa AFYA yake imempiga marufuku kugombea Urais!
Kwa ajili ya kila ajira duniasni kote, moja ya mashart makuu ni lazima mwombaji awe na afya iliyo bora, ndiyo sababu ni lazima ajira ya kila mwombaji itegemee taarifa ya kitaalamu ya madaktari, inayothibitisha kwamba hana dosari kiafya. Sharti hili ni la lazima kwa sababu:
a. Majukumu yote atakayopewa mwajiriwa atayatekeleza kikamilifu
kwa kutumia viungo vya mwili wake, kwahiyo viungo vyake vyote
ni lazima viwe katika hali iliyo imara kwa ajili ya kazi.

b. Hata kama kwa uthibitisho wa kitaalamu wa madaktari mwajiriwa
anazo akili nzuri kichwani mwake, akiwa na hitilafu katika viungo
vingine vya mwili wake huathiri afya ya akili zake na uwezo wa
utendaji wa akili zake.

c. Kazi ya Rais ni ngumu sana, kwa sababu ni pamoja na kusimamia
shughuli zote za maendeleo ya nchi nzima, na matatizo yote
yanayowatokea wananchi wote kila walipo, na kusimamia
utekelezaji wa majukumu yote ya watendaji wote katika Taifa,
hivyo kwamba maamuzi sahihi yanatokana na afya bora yenye
kuhakikisha uwezo unaopasa wa kiakili wakati wote

d. Hitilafu katika afya hudhoofisha uwezo wa kifikira na kusababisha
maamuzi mabovu, ambayo huleta athari mbaya sana kwa Taifa. Na
udhaifu huo huathiri mpaka maadili na hata uzalendo wa huyo
kiongozi mdhaifu. Kwa mfano akipatikana Rais anayeishi kwa
matumaini, kwa hofu ya kupoteza uhai kabla hajaweka sawa
mambo yake na ya familia na jamii yake atatumikia maslahi yake
zaidi kuliko Taifa, tatizo hilo la afya likawa limelikosesha Taifa
kipaumbele, na kuliangamiza kimaendeleo!
e. Wanaowania kugombea urais ni lazima wachunguzwe kwa makini
sana afya zao, kwa sababu kukifanyika makosa akatawazwa
mwenye hitilafu za kiafya, atakwenda kuwa mzigo mzito sana kwa
Taifa, hususan ugharamiaji wa utunzaji wa uhai wake ndani na nje
ya nchi, kukosekana na umakini anaopasa kuwa nao kwa ajili ya
dhamana kubwa aliyopewa n.k.

Kutokana na AFYA yake kuwa dhaifu sana hata kwa kumwona kwa
macho tu, kabla ya uchunguzi wa kitaalamu ni kwamba Edward Lowasa hawezi kabisa kugombea Urais. Kwani amekosa sifa muhimu sana ya afya bora, ambayo ni ya lazima kwa mtu yeyote anayestahili kupewa dhamana kubwa sana ya kuliongoza Taifa. Pengine hata kugombea urais kwenyewe anatafuta kutokana na hitilafu ya kiafya, iliyosababisha udhaifu katika kufanya maamuzi, hivyo amejikuta kwa bahati mbaya anagombea asichokiweza kabisa.

Ni lazima wagombea wote wa Urais, wa Ubunge na hata wa Udiwani
wachunguzwe kwa makini afya zao kabla ya kupewa kugombea, na hata kuchunguzwa tena katikati ya muhula wa utumishi wao, kama kweli tunalithamini na kuliheshimu Taifa.

Sifa za urais ni wito au uhanga kwa ajili ya Nchi ambao ni zaidi ya
maadili ya kizalendo, maono, vipawa na AFYA BORA. Ni dhana potofu
sana kwamba sifa ya urais ni kushabikiwa na umati wa watu! Kwa
sababu wengi hufuata mapesa na husombwa hata na magari ili umati
wa kishabiki tu upatikane. Lakini kumpenda mtu huwa lazima kuwe na sababu, wakati ushabiki ni pepo mchafu au ‘psychological deficiency’.





4 Jul 2015

Kwa niaba ya familia ya Mzee Philemon Chahali, ninaomba kuwashukuru nyote mnaoungana nasi kumwombea dua/sala ili apone. Hatuna cha kuwalipa bali kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu awabariki kwa upendo wenu. Pia kwa vile hali ya baba bado si ya kuridhisha, tunawaomba tuendelee na dua/sala zaidi. Wanasema 'penye wengi Mungu yupo' basi ni matumaini yetu kuwa ushirikiano huu katika sala/dua utapelekea kupona kwa Mzee Chahali. Again, asanteni sana, na Mungu awabariki sana.

Tangu nipate taarifa za kuumwa kwa baba, nimepunguza kujishughulisha na 'kelele' zangu kuhusu masuala mbalimbali yanayoikabili Tanzania yetu. Sijafanya hivyo kwa maana ya kupuuzia masuala hayo bali kichwa changu kimetawaliwa na suala la afya ya baba yangu kwani ndo mzazi pekee niliyebakiwa naye baada ya kufiwa na mama mwaka 2008.

Hata hivyo, leo nimelazimika kuandika makala hii baada ya kufanya maongezi na jamaa yangu mmoja huko Tanzania ambaye katika nafasi yake kikazi, anafahamu mambo mengi yanayojiri 'nyuma ya pazia.'

Alichoniambia kimenishtua sana. Ni kuhusu kampeni zinazoendelea mtandaoni zinazomhusisha mtoto mdogo anayejiita DOGO JEMBE. Pia kampeni hizo zinatumia hashtag #IkuluSio.

Huyo jamaa yangu, pengine kutokana na majukumu yake kikazi au ufuatiliaji tu, amenionyesha ushahidi unaothibitisha kuwa kampeni hiyo inaendeshwa na mtangaza nia mmoja wa CCM. Kwahiyo tofauti na picha inayojengwa na DOGO JEMBE kuwa yupo upande wa maslahi ya Watanzania, kimsingi mtoto huyo anatumiwa tu na mwanasiasa huyo anayetaka urais. 

Kwa mujibu wa jamaa yangu huyo anayefanya kazi katika taasisi moja 'nyeti' huko nyumbani, kosa la msingi lililofanywa na waandaaji wa kampeni hiyo ni kwenye kitu kinachofahamika kama IP Address ambayo kwa lugha nyepesi ni anwani ya mlolongo wa namba zinazotenganishwa na nukta ambao unaitambua kompyuta katika mtandao. 'Mtaalam' huyo amefanikiwa kubaini kuwa posts za kampeni hiyo zinatoka kwa IP address ya mdogo wa mwania nia fulani. Amenitumia screenshots zenye uthibitisho kuhusu suala hilo.

Amenijulisha pia kuwa taasisi anayoitumikia inafahamu bayana kuhusu 'uhuni' huo, na hii unaisoma hapa kwa mara ya kwanza, usishangae ukikutana na breaking news hii katika vyombo vya habari katika siku chache zijazo. Inaelekea kuna 'wakubwa' hawajapendezwa na mbinu hiyo ya kuwahadaa Watanzania kwa kisingizio cha kumsaka Rais bora.

Kilichomkera, kinachonikera, na ambacho pengine nawe Mtanzania kitakukera ni kitendo cha mwania huyo kuwafanya Watanzania wapumbavu. Kwanini nasema hivyo? Kwanza ni 'kosa' la kumtumia mtoto mdogo kuvuta hisia za watu, kuwaaminisha kuwa lengo ni kupigania maslahi ya taifa kwa kuamsha tafakuri ya nani hasa anatufaa kuwa Rais wetu ajaye, ilhali ukweli ni kwamba kampeni hiyo ina lengo la kumpigia debe mwania nia huyo.

Kumtumia mtoto huyo mdogo kwa minajili ya kisiasa hakuna tofauti na kile kinachoitwa CHILD LABOUR, yaani kuwatumikisha watoto. Sasa hapo tu yatupasa kutambua kuwa child labour ni ukiukwaji wa haki za binadamu, na kwa minajili hiyo, mwania nia anayesaka urais kwa kukumbatia ukiukwaji wa haki za watoto/binadamu HAFAI.

Pili, hadaa, usanii, na uhuni mwingine wa kisiasa ndivyo miongoni mwa vitu vilivyotufikisha hapa. Sasa kama katika hatua hizi za awali tu za kuwania kupitishwa na chama kuwania urais mwanasiasa anaanza kukumbatia vitu kama hivyo, huhitaji kuwa mwenye uelewa mkubwa wa kisiasa kubaini kuwa mwania nia huyo hafai hata ujumbe wa nyumba kumi, achilia mbali urais.

Tatu, japo watoto wana haki ya kikatiba na kidemokrasia kuzungumzia kuhusu hatma ya taifa letu ikiwa ni pamoja na Uchaguzi Mkuu ujao, hiyo sio excuse kwa wamasiasa yeyote yule kutumia haki hiyo ya watoto kwa manufaa yake binafsi. Angekuwa jasiri, angejitokeza mwenyewe hadharani badala ya kujikampenia kwa kutumia child labour.

Kwa mujibu wa jamaa yangu huyo ambaye kwa ninavyomfahamu hana kambi yoyote hasa kwa vile majukumu yake kikazi yanamzuwia kujihusisha na siasa, kuna data nyingine ambazo zinaihusisha moja kwa moja kampeni hiyo na mwania nia huyo.

Japo nipo katika wakati mgumu kutokana na kuzorota kwa afya ya Mzee Chahali lakini afya ya Tanzania yetu ni muhimu pia kama afya ya mzazi wangu, na nimeshindwa kukaa kimya baada ya kuletewa ushahidi kuhusu 'uhuni' huu. 

Amenieleza kuwa kauli ya Dogo Jembe kuwa 'Ikulu sio ya baba yako' ilimlenga Makongoro Nyerere kwa vile yeye ni mtoto wa Nyerere, na kauli kuwa 'Ikulu sio hospitali' illimlenga Lowassa kwa vile mwania nia huyo amedaiwa kuwa afya yake sio nzuri japo haijathibitishwa. 


Lakini pengine hata bila kupata 'ufunuo' huu, ilipaswa tujiulize NANI ANAYEFADHILI KAMPENI HII YA KISASA KABISA?

Kwa mtizamo wa jamaa yangu huyo, kosa jingine la kampeni hiyo ni kwamba imejitengenezea 'ufupi wa maisha' kwa maana kwamba ipo siku Dogo Jembe atalazimika kuwashawishi tena Watanzania kuwa 'mtaka nia flani ana sifa za dogo jembe, na ndio anafaa kuwa Rais,' na hapo all hell will break loose kwa sababu kila mwenye akili timamu atabaini nani alikuwa behind kampeni hiyo.

Anyway, ningetamani kuandika kwa kirefu lakini wito wangu kwa Watanzania wenzangu ni mdogo tu: AKILI ZA KUAMBIWA, CHANGANYA NA ZA KWAKO. Tumeshwahi kuhadaiwa huko nyuma, tumeshaona matokeo ya hadaa hizo, chonde chonde, tusirejee tena makosa hayo. Kama katika kuwania tu kupitishwa na CCM, mwanasiasa yupo radhi kutumia mtoto mdogo kuwahadaa Watanzania, je akifanikiwa kuingia Ikulu itakuwaje? Ni muhimu pia kutambua kuwa mwanasiasa ambaye yupo desperate mno kuingia Ikulu lazima atakuwa na ajenda zake binafsi,

Nimalizie kwa kuwashukuru tena nyote mnaojumuika nasi kumfanyia dua/sala Mzee Chahali, na ninawashukuru sana, na kuwaombea Mungu awabariki sana. 



25 Jun 2015

NIANZE makala hii kwa kuomba radhi kutokana na kushindwa kuwaletea makala katika toleo lililopita. Hiyo ilitokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu. Ninaomba pia kutumia fursa hii kuwatakia ndugu zangu Waislamu mfungo mwema wa mwezi Mtukukufu wa Ramadhani.
Katika makala ya hii nitaendelea kuzungumzia kinyang’anyiro cha Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu. Na zaidi nitaelemea katika nafasi ya urais, hususan mchakato unaoendelea ndani ya chama tawala, CCM, ambapo hadi wakati ninaandaa makala hii, makada 37 wa chama hicho wameshajitokeza kuomba ridhaa ya chama hicho kuwapitisha kuwania nafasi hiyo.
Lakini kabda sijaingia kwa undani, pengine ni muhimu tukumbushane kuwa wakati idadi ya makada 37 (ambayo huenda ikaongezeka) ni ya kihistoria, suala la kushtua zaidi ni ukweli kwamba miongoni mwao ni pamoja na Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na mawaziri kamili saba, bila kujumuisha manaibu waziri.
Nimekumbushia suala hili kwa sababu ni vigumu kufahamu serikali yetu muda huu inaendeshwaje, hasa ikizingatiwa kuwa Rais Jakaya Kikwete nae amekuwa katika safari za mara kwa mara nje ya nchi (wakati ninaandika makala hii yupo nchini India).
Ukiondoa Makamu wa Rais, ambaye anakuwa kaimu Rais wakati Rais anapokuwa nje, licha ya majukumu ya kiwaziri, Waziri Mkuu na hao mawaziri wengine pia ni wabunge. Katika hili ni vigumu kufahamu wanamudu vipi kugawa muda wao kwa majukumu yao ya kiserikali, kiubunge na hayo ya kuwania kuteuliwa kuwania nafasi ya Urais.
Hata hivyo, si vigumu kudhani kwamba kwa muda huu, akili na nguvu kubwa kwa makada wote waliotangaza nia zitakuwa zimeelekezwa kwenye kinyang’anyiro cha Urais. Kwa kiasi gani hilo linaathiri utumishi wao kwa umma, ni vigumu kwa sisi wengine kufahamu.
Nikirejea kwenye suala la makada wa CCM kutangaza nia zao kuwania urais, jina lililosikika zaidi wiki iliyopita lilikuwa la Jaji Mkuu wa zamani, Augustino Ramadhan. Japo jina lake lilishawahi kutajwa huko nyuma kama mmoja wa watu ‘wanaoweza kuokoa jahazi,’ lakini kwa kiasi kikubwa habari zilizosikika huko nyuma zilionekana kama tetesi tu pasi uthibitisho.
Angalau mara mbili, gazeti hili la Raia Mwema lilibeba habari zilizohusu uwezekano wa Jaji Ramadhani kugombea urais kwa tiketi ya CCM.

Binafsi, kwanza ninaheshimu uamuzi wa Jaji Ramadhani kwani ni haki yake ya Kikatiba kuchukua uamuzi huo. Hata hivyo, tayari kuna baadhi ya wananchi walioshtushwa kumsikia Jaji huyo akielezea kuwa amekuwa mwanachama wa CCM tangu miaka ya sitini.
Kwanza ninadhani alipitwa tu kutoa kauli hiyo kwa sababu CCM iliundwa mwaka 1977 baada ya TANU na ASP kuungana. Kwahiyo, hakukuwa na CCM miaka ya sitini.
Jaji huyo alieleza kuwa alijiondoa CCM mwaka 1992 kufuatia mabadiliko ya sheria, ambapo mfumo wa vyama vingi uliruhusiwa na hiyo kupelekea watumishi wa umma kutoruhusiwa kuwa wanachama wa vyama vya siasa.
Japo Jaji Ramadhan anasema alijiondoa CCM wakati huo, kuna wanaokwenda mbali zaidi na kutaka uthibitisho katika suala hilo. Sote tunaijua Tanzania yetu, na kwa hakika tunawafahamu vema viongozi na wanasiasa wetu. Ni kwa mantiki hiyo, kuna wanaotaka uthibitisho kuwa kweli Jaji huyo alijiondoa CCM na kutokuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa katika utumishi wake, ikiwa ni pamoja na Ujaji Mkuu.
Na kauli hiyo ya uana-CCM wake, kwa namna flani, imerejesha tena suala la hukumu iliyotolewa na Jaji huyo kwa kushirikiana na majiji wengine dhidi ya kesi ya Mchungaji Christopher Mtikila aliyetaka mahakama itamke kuwa sheria inayozuwia mgombea binafsi ni kinyume cha Katiba.
Pasi kuingiza kiundani katika kesi na hukumu hiyo, binafsi ninaichukulia hukumu hiyo kuwa moja ya hiba (legacies) kuu za utumishi wa Jaji Ramadhani.
Kwa baadhi yetu tunadhani Jaji huyo angebaki shujaa kwa demokrasia kwa sababu mfumo wa sasa unaolazimisha wawania nafasi mbalimbali za uongozi ikiwa pamoja na urais kuwa wanachama wa vyama vya siasa unatupunja fursa ya kupata viongozi wa kisiasa wazalendo lakini wasiotaka kujihusisha na vyama vya siasa.
Hata hivyo, ili kumtendea haki, ni muhimu kutambua kuwa hukumu hiyo haikuwa maamuzi binafsi ya Jaji Ramadhani bali licha ya kuwahusisha majaji wengine pia, ilikuwa ni ya kisheria na sio hisia binafsi.
Lakini kwangu, licha ya dalili zinazoonekana wazi kuwa kana kwamba CCM imeshapata mgombea wake urais kufuatia uamuzi wa Jaji Ramdhan kutangaza nia, nina wasiwasi kidogo kuhusu ufanisi wake.
Kubwa zaidi ni ukweli kwamba Idara ya Mahakama, ambayo licha ya Jaji Ramadhan kuitumikia muda mrefu bali pia aliwahi kuwa mkuu wake kwa maana ya ujaji mkuu, imeendelea kuwa moja ya taasisi sugu kwa rushwa. Takribani kila ripoti inayotolewa kuhusu tatizo la rushwa katika taasisi mbalimbali za serikali nchini mwetu, Idara ya Mahakama haikosekani, na tena ikishika nafasi za juu.
Mara baada ya kuchukua fomu kuomba CCM imteue kuwania Urais, Jaji Ramadhan aliwaambia waandishi wa habari kuwa atatumia uzefu wake kupambana na ufisadi. Swali la msingi: uzoefu upi? Huohuo ulioshindwa ukiondoa Idara ya Mahakama katika orodha ya taasisi zinazoongoza kwa rushwa?
Kwa upande mwingine, Jaji Ramadhan alikuwa mjumbe wa ‘Tume ya Warioba’ iliyokusanya maoni kuhusu mabadiliko ya Katiba. Sote twakumbuka yaliyomsibu Jaji Joseph Warioba na baadhi ya wasaidizi wake kupigania sio tu kazi nzuri iliyofanywa na tume yao bali pia mustakabali wa Katiba mpya.
Kwanini Jaji Ramadhani amekuwa kimya sana katika suala hilo? Je ukimya wake ulitokana na kufahamu kuwa siku moja angeomba kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM?
Na katika hilohilo, kwa vile mapendekezo ya Tume hiyo iliyomshirikisha Jaji Ramadhani yalikuwa muungano wenye muundo wa serikali tatu, je kwa vile CCM ambayo jaji huyo anaiomba ridhaa ya kumteua awe mgombea wake ina msimamo wa serikali mbili kama ilivyo sasa, hilo si tatizo angalau kimsimamo na kimtizamo?
Hadi muda huu, Jaji Ramadhani ni Rais wa Mahakama ya Afrika kuhusu haki za binadamu. Sihitaji kuorodhesha matukio lukuki ya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Tanzania lakini miongoni mwa matukio makubwa ni pamoja na ukatili unaofanywa na Jeshi la Polisi na rushwa (naam, rushwa sio tu adui wa haki bali pia inachangia ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu).
Je Jaji Ramadhani amekuwa wapi wakati ukiukwaji wa haki za binadamu ukiendelea kushamiri na kuwa kama umehalalishwa na Katiba yetu? Ni nani anaweza kusimama hadharani na kuwaambia Watanzania kuwa ‘Urais wa Jaji Ramdhani katika Mahakama ya Haki za Binadamu Afrika umechangia hili na lile katika kutetea au kudumisha haki za binadamu nchini Tanzania’?
Niwe mkweli, binafsi ninamwona Jaji Ramadhani kama Rais Kikwete alipojitambulisha mwaka 2005 kuwania urais na hatimaye kushindwa nafasi hiyo.
Alionekana mtu mwadilifu, aliyeitumikia nchi kwa muda mrefu, na pengine kubwa zaidi, msafi (asiye na kashfa). Sifa hizo zinalingana na tunazosikia kuhusu Jaji Ramadhan. Je, kwa mfano, kuwa msafi ni sawa na kuwa na uwezo wa kuongoza nchi?
Lakini la mwisho kuhusu kada huyo ni taarifa za awali kuwa amekuwa akiombwa na baadhi ya wana-CCM kuwania nafasi ya urais (kuna wanaodai kuwa ndio mtu pekee anayeweza kumudu ‘kumzuia’ Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa asiingie Ikulu, na wengine wanasema Jaji huyo ndio ‘msafi zaidi’ kuliko makada wengine wanazowania nafasi hiyo).
Swali la msingi: je hao waliomwomba (kama ni kweli) hawafanyi hivyo kwa maslahi yao binafsi? Na je, kumwomba huko (kama ni kweli) hakutopelekea urais wa Jaji Ramadhan (iwapo atashinda) ukaishia kuwa kama ‘deni la kwa wanamtandao’ lilivyouandama utawala wa Rais Kikwete?

Nimalizie makala hii kwa kuwakumbusha tena Watanzania wenzangu kuwa ni muhimu tujiulize na kuwauliza wawania urais maswali magumu ili tusije kuishia kujiulaumu huko mbeleni.
Nchi yetu ipo katika wakati mgumu; umasini wa kupindukia huku ufisadi ukizidi kuimarika, uhaba mkubwa wa uzalendo, utovu mkubwa wa maadili ya uongozi ikiwa na pamoja na uhuni katika matumizi ya fedha za umma, shilingi inayporomoka kama ipo kwenye mashindano ya marathoni na kadhalika.
Tunahitaji rais ambaye si tu anajua matatizo yetu bali pia ana uzalendo na uwezo wa kukabiliana nayo. Hatuhitaji Rais msafi lakini mwoga wa kupambana na maharamia wanaoibomoa nchi yetu kila kukicha.
Hatuhitaji mtu anayeahidi kupambana na rushwa ilhali hana mfano japo mmoja wa jinsi alivyowahi kupambana na rushwa.

-

24 Jun 2015






IT'S SPORAH CUSTOM HANDMADE WIGS... Finest Quality Handmade Custom Made Wig In Any Shade Or Length To Suit Your Style. 

Add caption

Meet the host at the Sporah Treasure Launch, Award winning Voxafrica UK Sports 360 Presenter Mr. Adesope Olajide
Meet the Co-Host, The Former model Irene Major and the wife of Canadian oil tycoon Sam Mail. 

Irene Major and Vox Africa TV presenter Adesope ready for the day.

WELCOMING THE GUESTS!








INTRODUCING LIVE PERFORMANCE
Add caption
Add caption
Add caption
Chipper Inter Performing LIVE at The Sporah Treasure Launch. 

Team Sporah making sure  that everyone is taken care.of







WELCOMING SPORAH 




And Irene Major had a question for Sporah "WHY HAIR? Why she decided to branch into hair business as a talk show queen.

Sporah talking about the Drive behind SPORAH TREASURE.




Kwa picha zaidi BONYEZA HAPA

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.