14 Sept 2008

Let me make a confession:Until when Hillary Clinton withdrew from the Democrat presidential campaign,and eventually endorse Barack Obama,I strongly believed that the latter's nomination could lead to another 4 yrs of a Republican in the White House ie a win for John McCain.It's not that I didnt want to see Obama making history by becoming the first Black president of the US of A,but I was rather scared of  the Republican dirty tricks (known in Bongo as "Siasa za Majitaka") on an easy target as Obama.I imagined how the GOP smear machine would assassinate Obama's character,bearing in mind how they successfully made John Kerry's bid to the White House a nightmare.

Perhaps I was wrong.Obama is now on the verge of making history.Given the unpopularity of Bush's presidency,the Dem's road to victory should have been easier.Unfortunately,the Republicans certainly know the odds against them.As I have always suspected,when the going gets tough in politics,any option on the table could be usefull.Of recent,McCain has been accussed of lies and deception,a possible sign that all might not be going well for the GOP candidate.And it seems he will soon receive support from same old groups that focuses on producing emotional rather than rational responses from voters.

HERE they come! (CLICK TO READ THE STORY)



Rais Jakaya Kikwete amewataka Watanzania kutambua kuwa njia pekee itakayowakwamua kiuchumi na kuwaletea maisha bora ni kujishughulisha na shughuli mbalimbali za maendeleo na si kukaa tu vijiweni na kulalamika. 
Kauli hiyo aliitoa jana wakati akijibu malalamiko ya wananchi wa kijiji cha Nyumba ya Mungu, kilichopo katika kata ya Lang`ata, tarafa Msitu wa Tembo, wilayani Simanjiro, ikiwa ni siku yake ya kwanza ya ziara yake ya kikazi mkoani Manyara. 

Wananchi hao waliokuwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali, walimweleza Rais Kikwete kuwa bado wanashindwa kuishi maisha bora kama walivyokuwa wametarajia na badala yake wanakabiliwa na matatizo sugu ya kupata huduma bora ya afya na mitaji ya biashara na ukosefu wa ajira. 

Rais Kikwete alielezwa hayo na wananchi wa kijiji cha Lemkuna, muda mfupi kabla ya kuzindua bonde la umwagiliaji la kijiji hicho, ambapo pia walilalamikia bei kubwa ya pembejeo za kilimo na umbali wa upatikanaji wake, hasa mbolea. 

Akizungumza mara baada ya kuwasikiliza wananchi hao, Rais Kikwete, aliwaeleza kuwa wanapaswa kujiajiri wenyewe kupitia utaratibu wa kupata mikopo na kujiunga kwenye vikundi vya kuweka na kukopa (SACCOS) ili waweze kuanzisha miradi ya maendeleo. 

``Jamani msitarajie maisha bora kama yatadondoka kutoka juu, utaratibu uliopo ni wa mikopo tuliyoianzisha ili muweze kufanya shughuli za maendeleo, awamu ya kwanza imekwishapita wengine wamepata wengine hawajapata ila tutaendelea kuhakikisha kuwa mikopo zaidi inatatolewa ili wale ambao hawajapata waweze kupata`` alisema. SOURCE:ippmedia.com

Kauli hiyo inashabihiana na hii iliyotolewa na Waziri Mkuu wa zamani,Edward Lowassa

2007-05-10 15:55:28 
Na Radio One Habari

Waziri Mkuu, Mheshimiwa Edward Lowassa amesema maisha bora kwa kila Mtanzania hayawezi kuja kwa kukaa vijiweni na kunywa kahawa bali kwa kufanyakazi kwa bidii na hasa kuendeleza kilimo. 

Amefafanua kuwa maisha bora kwa kila Mtanzania yanayosemwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ni matokeo ya kazi na hayaji kwa kukaa vijiweni kutwa nzima kunywa Kahawa na kutaka wananchi wa Pwani wafanye kazi kwa bidii kujiletea maendeleo. 

Akihutubia mkutano wa hadhara kijijini Maneromango Wilayani Kisarawe Mkoani Pwani Waziri Mkuu amesema watu wa mkoa huo lazima wabadili pato la mwaka la kila mtu ili liwe kubwa kama katika mikoa mingine. 

Aidha ameagiza mashambapori yaliyopo Kisarawe na wilaya nyingine Mkoani Pwani yaorodheshwe, yapelekwe Wizara ya Ardhi ili hatimaye yafikishwe kwa Rais yatwaliwe na kuwagawia vijana wafanye kazi za kilimo. 
Waziri Mkuu anakamilisha ziara yake ya siku sita ya Mkoa wa Pwani leo kwa kutembelea Wilaya ya Bagamoyo. 
SOURCE: Radio One


13 Sept 2008

Moja ya mambo hatari sana ambayo kwa kiasi kikubwa ni kama yamefumbiwa macho huko nyumbani ni matangazo yaliyotapakaa kwenye magazeti na mitaani kuhusu tiba ya Ukimwi.Waganga wengi wa jadi,wa kweli na "wasanii",wamekuwa wakijitangaza kuwa wanatibu ugonjwa huo hatari.Ni vigumu kupata takwimu sahihi za watu wanaopoteza maisha kwa kufuata tiba hizo badala ya ARVs,lakini yayumkinika kuamini kuwa utapeli wa aina hii inagharimu maisha ya waathirika wengi.Nimekutana na habari ya usanii kama huo uliokuwa ukiendelea nchini Afrika ya Kusini.Kibaya zaidi ni kwamba mtu aliyesimamia shughuli hiyo,Matthias Rath, alikuwa akijigamba kuwa mkombozi wa Afrika na dunia dhidi ya Ukimwi.Simulizi kamili ya video iko HAPA

12 Sept 2008

Suala la Health and Safety ni miongoni mwa vipaumbele vikubwa kwa hawa wenzetu wa nchi zilizoendelea.Lakini inapofikia hatua ya kung'oa kwa makaburi in the name of health and safety,yayumkinika kuamini kuwa hawa wenzetu nao wakati mwingine wana maamuzi as if vichwani mwao kuna mapovu badala ya ubongo.Hebu soma KIOJA HIKI CHA HAPO LONDON

Kama kioja hicho hakijakuchekesha,vipi kuhusu hiki cha Mmasai aleyekwenda Mombasa kwa matarajio ya kudaka mwanamama mtalii mzungu amuoe lakini akajikuta akiishia kuwa msusi!Bingirika na kioja hiki HAPA

Ama kweli wenzetu wako serious na siasa zao.Kama kutokea kwenye kipindi cha televisheni cha mapishi kumemng'oa madarakani aliyekuwa Waziri Mkuu wa Thailand,Samak Sundarajev,sijui ingekuwa ishu kama ya Richmond huyu mwanasiasa angeepuka kitanzi.In a bigger picture,effectiveness ya Mahakama za Katiba ingeweza kuwa nyenzo muhimu sana kwa uwajibikaji wa viongozi wetu na maamuzi/matendo yao.Habari kamili kuhusu mkasa huu BONYEZA HAPA

Nani kasema vibaka na wezi wanaenda likizo mwezi wa toba?Hebu cheki kituko hiki kilichojiri ndani ya msikiti.Kwa mujibu wa gazeti la Dar Leo,JESHI la Polisi (huko nyumbaniTanzania) linamsaka mwanaume mmoja ambaye hakuweza kufahamika jina lake mara moja kwa tuhuma za kumpa Baraka Rwambow (22), futari yenye dawa za kulevya kisha kumpora pikipiki yake katika msikiti wa Tambaza. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Kanda Maalum Dar es Salaam, Jamal Rwambow amesema kuwa tukio hilo limetokea jana saa 11 jioni, msikiti wa Tambaza. 
Amesema kijana huyo alikodiwa Kimara Temboni na mtu anayemfahamu kwa sura ili ampeleke msikiti wa Tambaza kwa ajili ya kuswali swala ya magharibi. Amesema kuwa baada ya kufika msikitini hapo mtu huyo aliingia ndani kuswali na baada ya kutoka alimpa dereva wa pikipiki futari hiyo ambapo alikataa na alimbembeleza akaamua kula. Baada ya kula mtu huyo alianza kulegea na mwishowe alimuomba mteja wake huyo amuendeshe ili waweze kurejea nyumbani ambapo mteja huyo aling'oa pikipiki na kwenda moja kwa moja Salender Club na kumtupa kijana huyo akiwa hajitambui. 

Walinzi waliokuwepo jirani walimuokota mtu huyo na kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi.Polisi wanaendelea kumsaka mtu huyo na pikipiki hiyo aina ya Royck.

Ama kweli dunia haijaishiwa vituko.Hebu tumwangalie na huyu nae.Jana dunia iliungana na Wamarekani kuadhimisha mwaka wa saba wa mashambulizi ya kigaidi ya September 11,2001.Licha ya kusababisha majonzi na kubadili mwenendo wa mambo ulimwenguni,tukio hilo lilizaa mashujaa kadhaa:kwa mfano watu waliojitolea mhanga kuokoa maisha ya wenzao na wale walionusurika kufa katika majengo yaliyoshambuliwa.Kumbe kuna "wasanii" walioona nafasi ya kujichukulia ujiko wa kuwa mashujaa wa September 11 hata kama hawakuwepo mahala pa tukio.Mfano ni HUYU SHUJAA FEKI WA 9/11.

11 Sept 2008

Sidhani kama kuna ubishi kwamba Kanye West ana kipaji cha hali ya juu katika muziki,both as a rapper and a producer.Sasa sijui ni yale ya mgema akisifiwa tembo hulitia maji au ni matokeo ya ile ajali ambayo almanusura ichukue uhai wake,lakini something is wrong with Kanye.Hebu angalia HAPA kasheshe aliyoizua leo huko Los Angeles Airport.

Hapa chini kuna kazi mbili za msanii huyo.Ya kwanza ni wimbo wake mwenyewe wa Through The Wire na ya pili ya ni production yake kwa The Game katika wimbo Dreams.




Wakati Waamerika na wapenda amani wengine duniani wanakumbuka mashambulizi ya kigaidi yaliyotokea siku kama leo mwaka 2001,kibosile wa polisi wa Devon&Cornwal hapa Uingereza,Colin Terry,ameadhimisha siku hiyo kiaina kwa kuvaa sanamu la Osama bin Laden.Kitendo hicho kimezua kimbembe na tayari wapo wanaotaka awajibishwe pengine kwa vile afande huyo pia ni mwandamizikatika eneo lake  kwenye mapambano dhidi ya ugaidi.Habari zaidi iko HAPA


10 Sept 2008

Jana niliongelea kidogo kuhusu The Big Bang Theory,na hofu zilizojitokeza kwamba huenda leo,Jumatano,ingekuwa mwisho wa dunia.Well,experiment hiyo inaendelea huko kwenye underground tunnel lililosambaa mpakani mwa Uswisi na Ufaransa na hakuna dalili kwamba dunia itafikia tamati leo!Hata hivyo,hofu ya Big Bang imepelekea mwisho wa dunia huko India.Well,sio kwa nchi nzima bali kwa binti mmoja ambaye aliamua kujitoa uhai wake baada ya kuwa traumatized na taarifa za vyombo vya habari kuhusu uwezekano wa mwisho wa dunia kutokana na experiment ya Big Bang.Pengine tutasikia mengi pindi experiment hiyo itapomalizika.Habari kamili kuhusu binti wa India ni hii HAPA

Pamoja na kuchukua sabbatical leave ya lazima katika uandishi wa makala katika gazeti la Raia Mwema,blogu hii itaendelea kuwaletea kinachojiri kila wiki katika jarida hilo mahiri huko nyumbani.Miongoni mwa habari zilizochukua uzito wa juu katika toleo la wiki hii ni pamoja na kauli ya Spika wa Bunge la Muungano,Samuel Sitta,kwamba amejiandaa vya kutosha kufuatia taarifa kwamba watuhumiwa wa ufisadi wameingiza sumu huko Bongo kwa lengo la kuwadhuru Sitta na Mbunge wa Kyela,Dr Harrison Mwakyembe.Sidhani kama inahitaji kujumlisha mbili na mbili kupata jawaba as to akina nani watakuwa the usual suspects wa unyama wa aina hii.Zaidi BONYEZA HAPA kusoma habari hiyo na nyingine motomoto.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.