3 Dec 2008


According to tomorrow's New Statesman, Barack Obama was unimpressed by his encounter with David Cameron earlier this year and commented: "What a lightweight!"

According to James Macintyre's report, Cameron's attempt to stress his pro-American and Eurosceptic credentials did not meet with Obama's approval. According to Macintyre's diplomatic sources, the Democratic candidate was "distinctly unimpressed" and labelled Cameron a lightweight.

Macintyre notes that 48 hours earlier Obama had delivered a speech in Berlin stressing "the importance of Europe's role in our security and our future".

Following the meeting with Cameron, Obama apparently asked officials for more information on Tory Euroscepticism. Macintyre also speculates that Cameron's support for the Iraq war – which Obama opposed – did not help the relationship either.

The report is sure to dismay Cameron and damage his attempts to portray himself as a world-class statesman – not to mention relations between Obama's incoming administration and a possible future Tory government.

When Cameron met the then-presidential candidate in July, the two held an hour of discussions, and Obama also met shadow cabinet members William Hague and George Osborne.

Photographs showed the pair looking relaxed and comfortable with each other, and Cameron gave Obama gifts including a box of CDs by some of the Conservative leader's favourite British musicians, among them the Smiths, Radiohead, Gorillaz and Lily Allen, and a copy of Hague's recent biography of the anti-slavery campaigner, William Wilberforce.

A senior Labour source told the Statesman: "Obama will want to work with a united Europe, not the 27 divided nations envisaged by a David Cameron, William Hague and [the Eurosceptic backbencher] Bill Cash vision of Europe. Tory isolationism is the last thing Obama's new foreign policy team will want from London."

1 Dec 2008


People may be tightening their belts to cope with the credit crunch, but their favourite free leisure activity involves whipping off their undies for a quick roll in the hay, a new poll showed on Monday. Skip related content

However the overall figure disguised a stark difference between men and women, with female respondents preferring a good gossip to a good time between the sheets.

According to an online YouGov survey, 37 percent of people rank having sex at the top of their list of activities that don't cost a penny.

That was more than the next three highest options combined -- gossiping with friends (18 percent), window shopping (nine percent) and going to a museum (six percent).

"During the credit crunch our famed British upper lip might not be as stiff as before but other parts still are," said Lisa Power, head of policy at the Terrence Higgins Trust, the sexual health charity that commissioned the poll.

However, while 53 percent of men ranked sex as number one, only 21 percent of women put sex top of their list, with 28 percent saying they preferred gossiping with friends.

It also showed that passion levels may be tied to the cold weather, with 43 percent of Scots rating sex as their favourite free passtime, compared to 35 percent of Londoners.

In a separate study, the Institute for Social and Economic Research at the University of Essex found that declining house prices was increasing the risk of divorce.

The study, published in September, found that "negative house price shocks significantly increase the risk of partnership dissolution".

The YouGov survey interviewed 2,144 people over the Internet between November 21 and 23.

MEANWHILE




French say they need biggest condoms

The French say they need the largest condoms in Europe while Greeks get by on smaller ones, according to a Europe-wide study by a German consultancy that provides advice on condoms. Skip related content

The study by the Singen-based Institute of Condom Consultancy was done by asking 10,500 men in 25 countries to measure their penis and enter the number into a database.

The results show Frenchmen on average claim to need 15.48-cm (6.09-inch) long condoms, about 3 cm longer than Greeks, whose condom-size requirement was the most modest.

Jan Vinzenz Krause, the institute's director, told Reuters Friday the data was collected over a period of eight months.

He did not want to comment on how honest he thought the Frenchmen had been in reporting the data.

The survey was aimed at educating youngsters about the importance of effective contraception.

The institute also offers online condom-size advice and hosts "Pimp Your Condom" -- an annual fair organised in cooperation with the national Aids Trust -- with the aim of educating teens about sexually transmitted diseases.

Krause was in the spotlight in the past when he produced a prototype of the "spray-on condom" -- an aerosol can which contains latex that creates a perfectly fitting condom. But the idea was not developed further.

SOURCE: Yahoo! News

























Presidents and prime ministers, doctors 
and lawyers, scientists and schoolteachers, 
chief executives and trade union leaders, 
religious groups and communities, and 
– critically – people living with HIV, are 
coming together in a brilliant coalition 
that has proved that, with clear targets and 
strong commitment, we can move mountains.”
- UNAIDS Executive Director Peter Piot
2008 World AIDS Day message


Over 300 people have died in Muslim-Christian clashes in the worst sectarian violence in Nigeria since 2004.
Angry mobs burned homes, churches and mosques on Saturday in the central state of Plateau, according to The Associated Press.

Initially a clash between supporters of the region’s two main political parties, the violence was soon divided along ethnic and religious lines.

Tension began when electoral workers did not post the results in ballot centers, causing many locals to assume the election was going to be another fraudulent political event. After riots broke out, a curfew was declared and the governor of Plateau state ordered troops to shoot on sight to enforce the curfew in neighborhoods affected by the violence.

About 7,000 people in conflict areas have left their homes and are seeking refuge in government buildings and religious centers, the Red Cross reported.

Sectarian violence is not new in Plateau, with more than 1,000 people killed in Jos – the state’s capital – in September 2001 due to Christian-Muslim hostility.

This weekend’s sectarian violence was the worst clash in the West African nation since 2004, when as many as 700 died in Plateau and over 100 churches were destroyed. The 2004 violence was said to have been sparked by land disputes between members of the predominantly Christian Tarok tribe and Muslim Hausa-Fulani farmer.

Nigeria is split nearly evenly between a predominantly Muslim north and a Christian south. According to Compass Direct, religious conflicts between Muslims and Christians have claimed more than 10,000 lives since 1999.

SOURCE: EURWEB

WAKATI HAYO YAKIENDELEA HUKO NIGERIA,INAELEKEA BADO KUNA WENZETU HUKO NYUMBANI TANZANIA WANGEPENDA TUONJE HAYO YANAYOWAKUTA WENZETU WA NIGERIA.HEBU SOMA KWANZA STORI HII HAPA CHINI

Waislamu, Wakristo waishika pabaya CCM
NI KATIKA SUALA LA MAHAKAMA YA KADHI, OIC

Na Geofrey Nyang’oro

WAUMINI na dini mbili kuu nchini za Kiislamu na Kikristo wameiweka pabaya serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika kufanya maamuzi kutokana na mvutano mkali unaoendelea, huku pande hizo zikiwa zimeshikilia misimamo mikali kuhusu hoja ya Mahakama ya Kadhi na nchi kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC).

Mjadala kuhusu masuala hayo mawili ulikuwa umepoa, lakini uliibuka hivi karibuni baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk Bernard Membe, kuzungumzia suala la OIC wakati akizungumza na waandishi kuhusu ziara ya rais nje ya nchi.

Baada ya maaskofu kuitahadharisha serikali ya CCM kuwa hawatafanya nayo kazi iwapo itashikilia msimamo huo wa kujiunga na OIC, jana Waislamu nao waliipa serikali mwezi mmoja iwe imeshatoa tamko rasmi kuhusiana na hoja hizo, vinginevyo wataing'oa CCM madarakani kwa kuwa imeshindwa kutekeleza suala hilo, wakidai suala la Mahakama ya Kadhi limo kwenye ilani ya chama hicho tawala.

Kauli hiyo ilitolewa na Waislamu kwenye kongamano la "Hatima ya Elimu ya Uislamu na Urejeshwaji wa Mahakama ya Kadhi," lililofanyika kwenye Ukumbi wa PTA jana jijini Dar es Salaam jana.

Pia kwenye kongamano hilo, Waislamu walimtaka Waziri Membe kuomba radhi au kujiuzulu kutokana na kauli yake ambayo walidai kuwa, inakashifu fedha kutoka OIC kwa madai kuwa ni ya shetani.

Walitoa msimamo huo wakati waumini wa makanisa mbalimbali yaliyo chini ya CCT, KLPT wakiwa wameshatoa tamko lao la nguvu kupinga hatua ya serikali kudhamiria kujiunga na OIC, wakieleza athari ambazo serikali itapata iwapo haitakuwa makini.

"Tuna uhakika kuwa yaliyomo ndani ya OIC ni hatari kabisa, kwani endapo yakikubalika katiba, nchi itakuwa imevunjika na Watanzania watakuwa wameingia katika migogoro itakayoua maridhiano, mshikamano, utengemano na umoja wa kitaifa, " walisema maaskofu hao katika tamko lao.

Rais Jakaya Kikwete pia alitaka waumini wa Kiislamu kuwa na subira na kuiachia serikali itafakari kwa utulivu ili ifanye uamuzi ya hekima utakaojenga na kulihakikishia taifa umoja, amani, utulivu na upendo miongoni mwa raia.

"Tujiepushe na vitendo au kauli ambazo zitawatia watu hofu na kujenga chuki miongoni mwa raia wa nchi yetu wanaopendana na kujenga chuki na kutoaminiana baina ya raia na serikali yao inayowapenda na kuwathamini," alisema Rais Kikwete mwezi uliopita.

Lakini Waislamu jana wakawa na kauli kali wakati wakijadili masuala hayo kwenye kongamano hilo, ambalo pia lilihudhuriwa na baadhi ya viongozi wa Kikristo na kufikia hatua ya kutoa tamko hilo na wameazimia kufanya maandamano makubwa jijini Dar es Salaam ambayo yatakwenda sambamba na mkutano mkubwa wa hadhara utakaofanyika kesho kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja.

Akizungumza kwenye kongamano la jana, Katibu Mkuu wa Baraza la Habari la Kiislamu Tanzania (Bahakita), Sheikh Sadiki Godigodi alisema suluhisho la uwepo wa haki na usawa kwa wote hapa nchini ni urejeshwaji wa Mahakama ya Kadhi pamoja na upatikanaji wa haki ya kielimu kwa Waislamu.

Alisema ukimya wa serikali ya CCM kuhusu Mahakama ya Kadhi unaonyesha kuwa serikali hiyo, ambayo walidai inaongozwa na Jumuiya ya Kikristo (CCT), kutokana na kuonyesha kuipinga dhana hiyo, haina nia ya kutekeleza ilani yake licha ya kwamba suala hilo halina madhara kwa Watanzania wote na ni muhimu kwa dini ya Kiislamu na Uislamu kwa ujumla.

Godigodi alisema kwa sasa Uislamu hapa nchini hautakuwa tayari kudhulumiwa haki zake na hautakuwa tayari kuona mtu yeyote anajitokeza kukwamisha jitihada za kudai haki zao ambazo ni urejeshwaji wa Mahakama ya Kadhi na nchi kujiunga na OIC na kudai kuwa mtu yeyote atakayejitokeza kupinga jitahada hizo, atakuwa anatangaza uadui kati yake na Uislamu.

Sheikh Mustafa Lema kutoka Arusha alisema anashangazwa na serikali ya CCM licha ya kuliweka suala la Mahakama ya Kadhi kwenye ilani ya uchaguzi ya mwaka 2005, imeamua kukaa kimya katika utekelezaji wake.

Alisema Mahakama ya Kadhi ni suala la kiimani katika dini ya Uislamu na wala si la dini ya Kikristo wala serikali, hivyo jambo la msingi linalotakiwa kufanywa na serikali ni kurudishwa kwa chombo hicho.

“Ukimuuliza Mkristo anajua nini kuhusu dini atakupa habari kuhusu maaskofu, mashemasi na wachungaji na mambo yote yanayofanyika ndani ya imani yao, ukimuuliza Mwuislamu yeye atakueleza habari za masheikh, OIC na Mahakama ya Kadhi, hiyo ndiyo imani yao iweje leo Wakristo waje kuipinga Mahakama ya Kadhi ambayo siyo suala la imani yao?” alihoji Godigodi.

“Sisi tunataka Mahakama ya Kadhi ili tuweze kutetea haki zetu, hatuwezi kushughulikia mambo yahusuyo Uislamu ikiwa ni pamoja na mirathi, talaka na mali za Uislamu kama kiwanja cha Chang’ombe,” aliongeza.

Walisema kutokana na serikali ya CCM kuendelea kudhulumu haki za Uislamu na kuwachezea mara kwa mara kwa kushindwa kushughulikia masuala hayo, hawatakuwa tayari kukichagua chama hicho na badala yake watafanya kila linalowezekana kuhakikisha Waislamu wanakitosa chama hicho kwenye chaguzi zijazo.

Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia alisema suala la Mahakama ya Kadhi linapaswa kuanzishwa, lakini akasisitiza uwepo wa elimu ya kutosha katika suala hilo.

Alisema tatizo lililopo ni watu kutojua nini maana ya Mahakama ya Kadhi na kazi zake na kwamba kama watapatiwa elimu ya kutosha na kueleweshwa vema, itaanzishwa kwa amani na utulivu.

Alisema elimu pekee ndiyo itakayokwenda sambamba na mijadala ya uso kwa uso kati ya makundi yote mawili na hivyo kuwezesha uanzishwaji wa mahakama hiyo kuwa wa amani.

“Tatizo linalosababisha watu kupinga ni kutoelewa Mahakama ya Kadhi nini na kazi zake. Hapa inatakiwa elimu kwa wananchi wote kuhusu mahakama hiyo ili kuwaondoa hofu," alisema.

Hata hivyo Mbatia aliwataka Waislamu kuiachia serikali ifanye kazi zake katika kushughulikia hilo kutokana na ukweli kuwa iliahidi kulishughulikia.

Katika kongamano hilo, Waislamu hao walianzisha mchango wa hiari ili kupata Sh2 milioni kwa kwa ajili ya kuendesha zoezi la kufanya kampeni ya kuzunguka nchi nzima kutangaza azma yao ya kukusanya kadi na kuzirudisha kwa CCM kama serikali haitatekeleza suala hilo.

CHANZO: Mwananchi

TATIZO LETU NI KUKURUPUKA KWA WANASIASA AMBAO WAKATI WA CHAGUZI HUTOA AHADI KAMA ZILE ZA KWENYE WIMBO NDIO MZEE WA PROF JAY ILHALI WANAJUA KABISA HAWANA UWEZO WA KUZITEKELEZA.KULIKUWA NA HAJA GANI KWA CCM KUINGIZA KWENYE MANIFESTO YAKE YA 2005 AHADI YA KUPATIA UFUMBUZI SUALA LA MAHAKAMA YA KADHI IWAPO HAIKUWA INAJUA NAMNA YA KUITEKELEZA?NA NANI ALIMTUMA MEMBE KUROPOKA HUKO DODOMA KUHUSU OIC WAKATI MAMBO BAADO KABISA?KAMA ILIVYO RAHISI KWA DEREVA ASIYE MAKINI KUSABABISHA AJALI NDIVYO WANASIASA WASIO MAKINI WANAVYOWEZA KUINGIZA NCHI KATIKA MATATIZO AMBAYO YANAWEZA KABISA KUEPUKIKA.NA KAMA ILIVYO KAWAIDA,WALIOWASHA MOTO HUO WAKO KIMYA KWA SASA KANA KWAMBA SIO WAO WALIOTUFIKISHA HAPA.

27 Nov 2008

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP), amezuia kupelekwa mahakamani aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi. 

Karamagi anatuhumiwa kutumia madaraka vibaya katika kusaini mkataba wa mgodi wa madini wa Buzwagi. 
Imedaiwa kuwa, DPP alichukua hatua ya kuzuia kufikishwa mahakamani kwa Karamagi kutokana na ushahidi dhidi ya tuhuma zinazomkabili kutojitosheleza. 

Kesi dhidi ya Karamagi, ilikuwa iwasilishwe katika Mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kukamilisha kazi yake. 

Habari kutoka ndani ya kikao watendaji wa serikali na wafadhili wanaochangia bajeti ya serikali kilichofanyika Dar es Salaam jana, zilisema kuwa Takukuru walikwisha baini matumizi mabaya ya madaraka katika sakata zima la Buzwagi, lakini DPP akakataa kesi dhidi ya Karamagi isifunguliwe. 

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Mabalozi wote ambao nchi zao zinachangia bajeti kuu ya serikali na Makatibu Wakuu wa wizara mbalimbali. 

Chanzo chetu cha habari kutoka ndani ya kikao hicho, kilieleza kuwa, wafadhili walielezwa kuwa, Takukuru ilipeleka majalada ya kesi mbili kwa DPP, ikiwemo inayowahusu mawaziri wawili wa zamani, Basil Mramba na Daniel Yona ambayo ilitajwa juzi katika Mahakama ya Kisutu pamoja na la Buzwagi. 

Ilielezwa kuwa, liliporudi jalada la mawaziri hao wawili wa zamani, lilipitishwa kwa ajili ya kupelekwa mahakamani, lakini la Buzwagi DPP alisema hakuna ushahidi wa kutosha kuifikisha kesi hiyo mahakamani, hivyo kulifunga. 

Inadaiwa kuwa, uamuzi huo wa DPP, umeikasirisha Takukuru, ambayo ndiyo iliyokuwa ikikusanya ushahidi ili kesi hiyo iweze kufikishwa mahakamani kwa kuanza kusikilizwa. 

Chanzo hicho cha habari cha kuaminika, wafadhili walielezwa kwamba, majalada ya kesi nyingine nne kubwa, zikiwemo zinazoihusu kampuni ya uchimbaji madini ya Meremeta na Deep Green, bado yapo kwa DPP yakisubiri uamuzi wake. 

Pia Mabalozi hao waliwaomba kushawishi nchi za Ufaransa, Uswisi, Afrika Kusini, Mauritius, Hong Kong kutoa ushirikiano ili kesi hizo tatu ziweze kukamilika. 

Ilidaiwa kuwa, nchi hizo zimekuwa hazionyeshi ushirikiano mara maaofisa wa Takukuru wakihitaji taarifa. 

Jitihada za Nipashe za kumpata DPP, Elieza Feleshi jana ziligonga mwamba, kwani baada ya kuwasiliana naye alieleza kuwa, yupo kwenye kikao na kutaka apigiwe baada ya nusu saa. 

Lakini baada ya muda huo kupita na kupigiwa, alipokea msaidizi wake ambaye alieleza kuwa, bado yupo kwenye kikao na hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, kikao hicho kilikuwa bado kikiendelea. 

Nipashe ilipowasiliana na msemaji wa Wizara ya Katiba na Sheria, Omega Ngolle kuhusiana na suala hilo, alisema angeeleza kwa undani suala la jalada la Buzwagi, lakini hakufanya hivyo alipopigiwa simu baadaye. 

Sakata la mkataba wa Buzwagi kusainiwa nje ya nchi kwa mara ya kwanza liliibuliwa Bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, wakati akichangia bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini. 

Zitto alidai kuwa, waziri huyo wa zamani alikwenda kusaini mkataba huo, London nchini Uingereza, kwa kutumia mfumo wa mikataba wa zamani wakati serikali ikiwa inajadiliana na wawekezaji kurekebisha mikataba ya madini nchini. 

Suala hilo alilieleza katika mkutano wa nane wa Bunge mjini Dodoma, ambapo alihoji hatua ya Nazir Karamagi kusaini mkataba huo nje ya nchi. 

Baadaye, Zitto aliwasilisha hoja binafsi bungeni, akiomba kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge, kuchunguza hali hiyo. 

Zitto alieleza kushangazwa na uamuzi wa Karamagi kusaini mkataba wa madini kati ya serikali na kampuni maarufu ya madini hapa nchini ya Barrick Gold Mine kwa ajili ya mgodi ya Buzwagi nchini Uingereza badala ya Dar es Salaam. 

Mbali ya kuhoji uhalali wa Karamagi kusaini mkataba huo, kinyume cha maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete ambaye aliagiza kupitiwa upya kwa mikataba yote mipya ya madini, Zitto alikielezea kitendo hicho kuwa kinaongeza wasiwasi wa kuwepo kwa ushawishi wa rushwa. 

Hata hivyo, hoja hiyo ilitupiliwa mbali na Bunge na hatimaye Zitto aliishia kusimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa kile kilichoelezwa amelidanganya Bunge kuhusiana na madai yake hayo. 

Alipewa adhabu hiyo kwa madai ya kutoa kauli ya uongo Bungeni dhidi ya Karamagi, inayohusu kusaini mkataba na kampuni ya Barrick, juu ya mradi wa Buzwagi, jijini London nchini Uingereza.

CHANZO: Nipashe

26 Nov 2008


Watendaji wa Ifakara wametakiwa kuangalia uwezekano wa kuzungumza na uongozi wa Kanisa Katoliki juu ya ughali wa tiba unaotolewa katika Hospitali yao ya Mtakatifu Francis. Rai hiyo imetolewa na Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wa upokeaji taarifa ya wilaya, mkutano uliofanyika Ikulu Ndogo ya Ifakara juzi. 

Kauli hiyo ilitokana na rai ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini hapo ambao walitoa kilio cha tiba ghali katika hospitali hiyo na kutaka serikali iingilie kati. Hospitali hiyo inayomilikiwa na Kanisa Katoliki inadaiwa kutoa huduma kwa bei ghali baada ya wafadhili wake wakubwa wa Uswisi kujiondoa na kuingia Wataliano. 

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya, Evaristo Ndikilo akichangia hoja ya afya, alisema kwamba kwa upande wao walikuwa wakifikiri kupandisha hadhi kituo chao cha afya kukifanya kuwa hospitali. Hoja hiyo pia ilizungumzwa na Mbunge wa Ulanga Mashariki, Celina Kombani juu ya kuwapo kwa haja ya kupandisha kituo hicho, na kueleza mchakato umeshaanza. Kombani pia ni Waziri wa Tamisemi. 

Mwenyekiti wa Halmadhauri ya Ifakara, Hassan Goagoa, alisema ughali wa hospitali hiyo ambayo inatumika pia na mikoa mingine na shughuli za utafiti, kunatokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji na ingawa walishauriwa kuomba udhamini zaidi wa serikali kwa kuongeza idadi ya vitanda, hali imebaki kwao kama kitendawili. Hospitali ya Ifakara tayari ina vitanda vingi kwa hadhi yake ya kuwa hospitali teule ya rufaa. Rais aliendelea na ziara yake ya Mkoa wa Morogoro ambapo jana alitarajia kuzuru Wilaya ya Kilosa.

CHANZO: Habari Leo

25 Nov 2008

Picha kwa Hisani ya MICHUZI.

Fuatilia latest kuhusu ishu hiyo kwa kuBONYEZA HAPA

UPDATED:
Mramba, Yona waenda rumande kwa ufisadi
*Wakosa dhamana ya Sh7.8bn, waenda rumande na kandambili
James Magai na Paulina Richard

MAWAZIRI wawili waliowahi kuongoza wizara mbalimbali ikiwamo nyeti ya fedha katika serikali ya awamu tatu, Basil Mramba na Daniel Yona wamefikishwa kortini kwa matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Sh11.7 bilioni.

Kufikishwa kizimbani kwa mawaziri hao kunaashiria mwanzo wa utekelezaji wa ahadi ambazo zimekuwa zikitolewa na serikali na watendaji wake kuwa itashughulikia vigogo wote wanaotuhumiwa na ufisadi baada ya wananchi wengi kutoridhishwa na ukubwa wa majina ya watu walioshtakiwa katika kashfa ya wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Ni wiki iliyopita tu wakati Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hoseah alipotangaza kuwa muda mfupi ujao vigogo wanaohusika kwenye kashfa mbalimbali za ufisadi watafikishwa mbele ya mkono wa sheria.

Na hali ilikuwa hivyo jana wakati habari zilipozagaa asubuhi kuwa Mramba na Yonah wangepandishwa kizimbani na hivyo kufanya watu waliopata fununu hizo kujazana mahakama ya Kisutu.

Wawili hao walikuwa wameshafika mahakamanio hapo majira ya saa 2:45 asubuhi, wakiwa kwenye gari aina ya Toyota Land Cruiser VX, lenye rangi ya kijani na mistari ya rangi nyekundu na nyeupe ubavuni lenye namba za usajili T319 ATD.

Lakini namba za gari zilizokuwa katika kisahani cha namba (Plate number) zilikuwa tofauti na zilizokuwa katika vioo vya gari hilo ambazo ni T 562 AJK.

Lakini hawakushuka kwenye gari hilo lililokuwa na vioo vya giza, hadi walipotakiwa kwenda kizimbani.

Mramba na Yona walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana mbele ya Hakimu Hezron Mwankenja saa 5.40 na wakasomewa mashtaka na baadaye kupelekwa rumande kutokana na kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

Vigogo hao walifikishwa mahakamani baada ya uvumi wa tukio hilo kudumu kwa takribani majuma mawili.

Wakati wakiingia mahakamani jana Mramba, ambaye ni mtuhumiwa wa kwanza katika kesi hiyo namba 1200 ya mwaka huu, alisikika akiwahoji waandishi iwapo wamefurahi kufikishwa kwao mahakanai hapo, huku akidai kuwa watapiga picha nyingi sana kwa kuwa huo ni mwanzo tu.

Watuhumiwa hao walipandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka matano ya pamoja, baadaye Mramba akasomewa manane zaidi peke yake, na kufanya akabiliwe na jumla ya makosa 13.

Mwendesha mashtaka ambaye ni wakili wa serikali, Stanslaus Boniface aliyataja makosa yanayowakabili wote kwa pamoja kuwa ni matumizi mabaya ya ofisi kwa kuiruhusu kampuni ya M/S Alex Stewart (Assayers ya Uingereza kuingia mkataba wa kudhibiti madini ya dhahabu kinyume cha sheria.

Boniface alifafanua kuwa kati ya Agosti 2002 na Juni 14, 2004 watuhumiwa wakiwa katika nafasi za uwaziri wa fedha na uwaziri wa Nishanti na Madini waliruhusu kampuni hiyo na mshirika wake, M/S Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation kusaini mkataba wa kudhibiti madini ya dhahabu kinyume cha sheria ya Manunuzi ya Umma na ya Madini.

Katika kosa la pili, Boniface alidai kuwa Mei 28, 2005 watuhumiwa hao walitumia vibaya madaraka yao kuingia mkataba wa nyongeza wa miaka miwili kwa kampuni hiyo kuanzia Juni 14, 2005 hadi 23 Juni 2007 kinyume cha sheria ya Manunuzi ya Umma na ya Madini.

Katika kosa la tatu Boniface alidai kuwa kati ya Machi 28 ,2005 na Mei 28,2005 watuhumiwa wakiwa watumishi wa umma walitumia vibaya madaraka yao kwa kumwalika Dk Enrique Segura wa kampuni hiyo kurasimisha mkataba huo wa nyongeza ya muda kabla ya mazungumzo na timu ya serikali kushughulikia suala hilo.

Boniface aliendelea kuieleza mahakama kuwa katika kosa la nne kati ya Machi 2005 na Mei 28, 2005 watuhumiwa waliachia suala la udhibiti wa madini lifanywe kienyeji bila kumshirikisha mwanasheria wa serikali kama ilivyopendekezwa na timu ya mazungumzo ya serikali, jambo lililosababisha ongezeko la muda wa mkataba huo wa miaka miwili.

Na katika kosa la tano ambalo lilimhusu mshitakiwa wa kwanza, Mramba, Boniface alidai kuwa Oktoba 10 Mramba alitumia vibaya mamlaka yake kwa kudharau ushauri wa Mamlaka ya Mapato (TRA) wa kutotoa msahama wa kodi kwa kampuni ya M/S Alex Stewart (Assayers) Government Busines Corpotion.

Katika kosa la sita ambalo pia linamhusu Mramba peke yake Boniface alidai kuwa kati ya Desemba 18 na 19, 2003 Mramba akiwa Waziri wa Fedha alitumia vibaya mamlaka yake kwa kutoa Tangazo la Serikali (GN) la mwaka 2003 lilitoa msamaha wa kodi kwa kampuni hiyo katika shughuli zake za usambazaji wa bidhaa na utoaji huduma kinyume cha mapekezo yaliyotolewa na TRA.

Boniface alidai kuwa kuanzia kosa la saba hadi la 11 ambayo karibu yote yanafanana ambapo Mramba akiwa waziri wa fedha anadaiwa kutoa msahama wa kodi ya mapato kwa kampuni hiyo ikiwa ni pamoja na kutumia madaraka yake kutoa GN namba 424 /2003 na 497/2004 kati ya Desemba 19, 2003 na Oktoba 15, 2004 kinyume cha mapendekezo ya TRA.

Katika kosa la 12 ambalo linawahusu watuhumiwa wote wawili, Boniface aliendelea kudai kuwa watuhumiwa hao wakiwa mawaziri kwa makusudi na kwa kutokuwa makini waliruhusu makataba ambao uliipa upendeleo kampuni hiyo na kuisababishia serikali hasara ya Sh 11,752,350,148.00.

Na katika kosa la 13 ambalo pia linamhusu Mramba peke yake Boniface alidai kuwa Mramba akiwa waziri wa fedha kati ya 2003 na 2007, alishindwa kuchukua tahadhari katika, kutoa matangazo ya serikali namba GN 23/2003, 424/2003, 497/2004, 498/2004 , 377/2005 na 378/2005 yaliyolenga kusaidi kampuni hiyo kutolipa kodi na hivyo kuisababishia serikali hasara ya Sh11.7 bilioni.

Watuhumiwa wote walikana makosa hayo na mawakili wao kuomba dhamana huku upande wa mashtaka ukisema kuwa hauna pingamizi.

Pamoja na maombi hayo ya dhamana, mmoja wa mawakili wa utetezi Tadayo alimuomba Hakimu Mwankenja atoe masharti nafuu kwa wateja wao akidai kuwa suala hilo limekuwa likipelelezwa kwa zaidi ya miaka mitatu na walitoa ushirikiano ikiwa ni pamoja na kufika mahakamani hapo bila kukamatwa.

“Hivyo hakuna hofu kuwa wanaweza kukimbia,” alisisitiza Tadayo na kumuomba hakimu azingatie sehemu ya pili ya sheria ya dhamana ya watuhumiwa kutoa nusu ya fedha wanazodaiwa kuiba au hati ya mali yenye tahamani sawa na nusu ya fedha hiyo.

Hata hivyo, akitoa masharti ya dhamana Hakimu Mwankenja alitupilia mbali ombi la mawakili hao la kuwataka washtakiwa kuwasilisha hati ya mali na badala yake watoe pesa taslimu Sh3.9 bilioni kila mmoja.

Pia aliwataka wawasilishe hati zao za kusafiria na kutokutoka nje ya Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na kuwa wadhamini wawili waliothibitishwa na mahakama.

Mwankenja aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 2 itakapotajwa tena na kuwataka washtakiwa wapelekwe mahabusu hadi hapo watakapotimiza masharti hayo.

Mara baada ya kesi hiyo kuahirishwa mamia ya watu waliofurika mahakamani hapo kiasi cha kujaa ndani na nje ya ukumbi wa mahakama waliwafuata mlango wa nyuma wa mahakama hiyo lilikokuwa gari walilokwenda nalo mahakamani hapo na kuwasubiria.

Wakati washtakiwa hao wakiingia ndani ya gari hilo na kuondoka mahakamani kupelekwa mahabusu, wananchi waliwazomea kwa kuimba wimbo wa “wezi, wezi hao huku wengine wakitaka hata kuwamwagia mchanga ndani ya gari hilo.

Wakati hayo yakiendele baadhi ya ndugu wa watuhumiwa hao walikuwa wakilia kimyakimya na kujifuta machozi huku wakiwa wameshikilia viatu vya washtakiwa hao mikononi na kuwaangalia wakiondoka na kanda mbili ambazo waliwanunulia mahakamani hapo.

Mapema saa 2: 45 waandishi wa Mwananchi walipofika mahakamani hapo waliwakuta watuhumiwa wakiwa wamekwishafika mahakamani hapo huku wakiwa ndani ya gari aina ya Toyota Landcruiser VX, lenye rangi ya kijani na mistari nyekundu na nyeupe ubavuni lenye namba za usajili T319 ATD.

Lakini namba za gari zilizokuwa katika kisahani cha namba (Plate number) zilikuwa tofauti na zilizokuwa katika vioo vya gari hilo ambazo ni T 562 AJK.

Watuhumiwa hao waliendelea kukaa ndani ya gari hilo na walipoteremka moja kwa moja walipandishwa kizimbani.

Kitendo cha watuhumiwa hao na kuendelea kubaki ndani ya gari hata baada ya kufika mahakamani hapo kiliwashangaza wengi na kufanya wajiulize maswali kuwa iweje wao wasishuke ndani ya gari na kuingizwa katika chumba maalumu cha mahabusu wakati wakisubiri kupandishwa kizimbani kama ilivyo kawaida kwa watuhumiwa wengine.

Mramba alikuwa amevalia kaunda suti yenye rangi ya kijivu na viatu vyeusi, mshirika wake, Yona akiwa amevalia kaunda suti yenye rangi ya khaki na viatu kahawia
CHANZO: Mwananchi

HII INATIA MOYO SANA.LAKINI KIU YA WENGI ITAKIDHIWA KWA MAFISADI WA KAGODA NAO KUWEKWA HADHARANI NA HATIMAYE KUPANDISHWA KIZIMBANI.


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.