4 Mar 2010
3 Mar 2010
Meela alisema serikali inahitaji sera na mikakati iliyojengwa na matokeo ya tafiti kama hizo kufanya gharama za maisha ziwe nafuu kwa kila mtu.
Utafiti huo ulihusisha sampuli nasibu za idadi ya watu 2,000 waliopatikana katika mikoa yote 21 ya Tanzania Bara, na visiwa vya Unguja na Pemba.
Alisema matokeo ya sampuli hizo yalipangwa katika jedwali na kufanyiwa upembuzi uliozingatia makadirio ya idadi ya watu milioni 40 nchi nzima ili kupata takwimu zilizokaririwa katika ripoti hiyo.
Utafiti huo umebainisha kuwa rushwa na umaskini ni matatizo yanayowaathiri zaidi wanaume kuliko wanawake.
CHANZO: Tanzania Daima
Not every one is blessed with good looks. I for sure wouldn't dare to compare myself to the likes of Brad Pitt or Denzel Washington.However,I'm quite happy and comfortable with my "plain" (or ugly as others would say) looks.When you finish reading the following story, you certainly are going to join me in cherishing whatever looks we have.
A Conservative Party delegate,Lynden Stowe,had to confirm his identity when he was on his way to hear his party Leader David Cameron speak in Manchester.Stowe,who bears stark resemblance to a racist Nick Griffin,leader of a far-right BNP,has had similar experience in the past.In the Manchester incident,he had to show his ID to the police who thought he was the BNP leader.
This episode reminds me of a number of incidents that have been reported by the media about people with huge beards who have were mistaken for Osama bin Laden.Whether or not such incidents had anti-Islam sentiments is for me to judge but being a lookalike to a high profile racist or terrorist is a million times worse than just being plainly ugly.
2 Mar 2010
2.3.10
Evarist Chahali
No comments
Japokuwa kutolewa kwa Yanga katika michuano ya kimataifa kunaweza kupokelewa kama habari njema kwa watani wao wa jadi Simba, lakini ukweli unabaki kuwa hiyo ni habari mbaya kwa medani ya soka la kimataifa kwa nchi yetu. Lakini kipigo hicho kinaweza pia kuwa fundisho zuri kwa vilabu vyetu vya soka,hususan Simba na Yanga,vilivyokumbwa na “ugonjwa” wa makocha wa kigeni.
Nimesoma utetezi wa kocha wa Yanga, Kosta Papic, kwenye gazeti la Mwananchi kwamba sababu kuu za kutolewa kwa timu hiyo ni uwanja mbovu, hali ya hewa na matokeo mabaya katika pambano la awali. Kwa ujumla sababu zote hizo si za kitaalamu kwani hata shabiki ambaye hajawahi kucheza chandimu anaweza kukurupuka na sababu kama hizo. Papic anatoa visingizio hivyo huku akielewa fika kuwa havitoi majibu ya kwanini timu yake ilipata matokeo kama hayo (kufungwa) katika mchezo wa kwanza uliofanyika Dar es Salaam.
Je hali ya hewa ya Dar nayo ilichangia Yanga kupoteza mchezo wa awali? Vipi kuhusu uwanja wetu mpya na wa kisasa? Ni dhahiri kuwa alichofanya kocha huyo ni kuamua “kusema chochote” badala ya kukaa kimya. Kufungwa, na hatimaye kutolewa kwa Yanga hakuwezi kutohusishwa na mapungufu ya kocha huyo wa kigeni, na Papic analijua hilo ndio maana akakimbilia kuja na visingizio visivyo na uzito.
Lakini kwa namna flani, kuwalaumu makocha wa kigeni kwa asilimia 100 ni kama kutowatendea haki kwa vile hawakujiajiri wenyewe.Vilabu vyetu, licha ya kuwa ombaomba na kutegemea hisani za wafadhili, ziko tayari kujikakamua na umasikini wao wa kujitakia ili ziwe na “ujiko” wa kocha wa kigeni. La muhimu sio kocha anatoka wapi bali umuhimu wake kwa maendeleo ya timu husika.
Na kwa upande flani angalau makocha wazawa, au wa kutoka nchi jirani, wanaweza kuvumilia “mbinde” zinazotawala kila kukicha katika vilabu vyetu vya soka. Sasa kwa makocha wanaotoka sehemu zenye “tamaduni tofauti” kama Papic,kwa hakika kumudu soka letu inakuwa shughuli pevu.Sote twajua,kwa mfano,jinsi vilabu vyetu vinavyoendekeza “kamati za ufundi” kuliko ushauri wa wataalam wa soka. Sasa kwa kocha “mzungu” mwenye “roho nyepesi”, mambo kama hayo yanaweza kumkimbiza mapema tu.
Ni muhimu sasa kwa Yanga na timu zetu nyingine za soka kutafakari upya “ugonjwa” huu wa makocha wa kigeni. Ikumbukwe kuwa wakati kocha ni sehemu muhimu ya mafanikio ya klabu, wachezaji na mazingira ya soka katika mahala husika ni muhimu pia katika kupata mafanikio. Kwa mfumo wa kibabaishaji unaotawala medani ya soka letu, hata akija kocha mahiri kama Sir Alex Ferguson au Jose Maurinho bado hadithi inaweza kuendelea kuwa kama hiyo ya Yanga huko DRC.
Vilabu vyetu vinapaswa kutengeneza mazingira mazuri hususan kwenye ngazi ya uongozi na kujijengea uwezo wa kujiendesha pasipo kutegemea ridhaa za wafadhili.Ni katika mazingira hayo ndipo vitamudu kufanya usajili wa kutengeneza vikosi vya ushindi visivyo hitaji kusajili na kuacha wachezaji mara kwa mara.Kadhalika,ili kuunda timu ya ushindi ni muhimu kwa vilabu hivyo sio tu kuwa na vikosi visivyobadilika kila msimu bali pia kuwa na walimu (makocha) wanaookaa na wachezaji kwa muda mrefu ili kujenga mshikamano na kuelewana.Vingenevyo,tutaendelea kuwa wasindikizaji tu katika michuano ya kimataifa.
28 Feb 2010
28.2.10
Evarist Chahali
No comments
Tukio hilo lilitokea wakati Waziri Mkuu alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Sikonge katika mfululizo wa ziara yake ya kuutembelea Mkoa wa Tabora.Kabla ya Waziri Mkuu kuanza kutoa hotuba yake, Nkumba alipewa nafasi ya kuwasalimia wapiga kura wake, ndipo alipoitumia nafasi hiyo kutangaza nia ya kugombea tena ubunge katika uchaguzi mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu.
“Mheshimiwa Waziri Mkuu, wakati ulipokuwa ukiahirisha kikao cha Bunge kilichopita ulisema sasa ni wakati muafaka kwetu kurudi kwa wapiga kura wetu ili kuwapa shikamoo.
“Leo ni siku ya bahati kwani watu wengi wamejitokeza katika mkutano wako huu na mimi naomba kuitumia nafasi hii kutoa shikamoo. “Kwa heshima na taadhima shikamoooni watoto wote mliopo hapa kuanzia mnaonyonya, watoto wa halaiki, watoto mliopo shuleni na shikamooni vijana na wazee wote mliopo hapa,” alisema Nkumba.
“Napenda sasa kutumia nafasi hii kutangaza nia kwamba nitagombea tena ubunge katika Jimbo la Sikonge na naomba wote mniunge mkono,” alisema Nkumba.
Tukio hilo lilimfanya Waziri Mkuu aliyekuwa amekaa jukwaani na viongozi wengine wa kitaifa, mkoa na wilaya, kuvunjika mbavu kwa kicheko.
28.2.10
Evarist Chahali
No comments
Rangers have extended their Scottish Premier League (SPL) lead to 10 points after beating their Glasgow arch-rivals Celtic, thanks to a Maurice Edu’s goal seconds from the end of the Old Firm derby.
Well,I still like football though it’s not as much as I used to be back in the days.Although I have never been to a football stadium for ages,but I could describe myself as a Celtic fan if you were to ask me which team I support in Scotland.That has got nothing to do with me being a Catholic but rather it’s largely due to Henrik Larsson,a former Celtic star who was at his peak when I first arrived in Scotland nearly a decade ago.
So am I hurt by today’s results?Not at all.Actually,I’m somehow happy that a scorer of the Rangers’ goal is a Black person.Nothing to do with race but what would you expect in a nation where football colours could inflame a fight.Yes,Edu is an African-American who emerged victorious today after scoring the goal that could as well help Rangers retain their SPL title.
I have always wished I could attend an Old Firm derby but a few people I know in Glasgow have always warned me about potential of violence when the two big guns in Scottish football meet.
Just like like back home where victory for Simba against Yanga,or vice versa,is more important than qualifying for regional competitions,so is to Celtic and Rangers.The two teams’ records in European competitions have generally been dismal.I’m of the opinion that local football success should also translate into performing well in international tournaments.Both Celtic and Rangers are said to be in to difficult financial position,and qualifying for the Champions League would really make a huge difference.But for Rangers fans today,all that matters is their victory against their arch enemies.
Well,although I wish Celtic could have emerge victorious today,I’m a bit consoled by the fact a Black person-Edu-is entered in the Scottish footbal history books.
Big up,Edu!
27 Feb 2010
27.2.10
Evarist Chahali
No comments
na Mwandishi Wetu, Urambo
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amemmwagia sifa kemkem Spika wa Bunge, Samuel Sitta akisema amejenga Bunge lenye sifa na umakini.
Pinda ambaye majuzi alimmwagia sifa Mbunge wa Igunga, Rostam Azziz (CCM) akiwataka wananchi wake wampime kwa kazi yake ni si kwa maneno ya bungeni, alisema Sitta amekuwa anaongoza Bunge kwa nia nzuri, na kwamba wanaolalamikia kazi yake ni wapotoshaji.
Alikuwa akihutubia wananchi katika Uwanja wa Jamhuri mjini hapa juzi, akasema Sitta ambaye ni Mbunge wa Urambo, amelifanya Bunge lisifiwe hata nje ya nchi.
Katika kusisitiza hili, Pinda alisema: “Hata watu wa nje wanalisifu Bunge letu…wanasema naam, hili ndilo Bunge…Bunge likicharuka kuhusu ufisadi wanasema hata si bure, nani asiyejua ufisadi? Ufisadi si rushwa? Bunge linachofanya ni watu wawe waadilifu.”
Aliwataka Watanzania waungane katika vita dhidi ya rushwa, kwani imesemwa tangu zamani kwamba rushwa ni adui wa haki.
Kwa takribani miaka miwili, Sitta amekuwa na uhusiano mbaya na baadhi ya vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wengi wakiwa wabunge wenzake, kuhusu anavyoliendesha Bunge.
Miongoni mwa walioathirika kwa “kazi nzuri ya Sitta” ni Rostam ambaye pamoja na rafiki yake Edward Lowassa (Monduli – CCM) walihusishwa kinamna na kashfa ya Richmond, ambayo ilisababisha Lowassa kujiuzulu wadhifa wake wa Waziri Mkuu.
Kutokana na msimamo wa Sitta na athari za Kamati ya Mwakyembe, CCM iligawanyika makundi mawili, moja upande wa Sitta jingine likiwa upande wa Lowassa na Rostam.
Uhasama wa makundi hayo uliongezeka na kujikita katika vikao vingine vikuu vya maamuzi vya CCM, kiasi kwamba mwaka jana, wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) walimbana Sitta katika moja ya vikao vyao, wakapendekeza avuliwe uanachama na afukuzwe ubunge, kwa maelezo kuwa anatumia vibaya nafasi yake kwa kuiaibisha CCM.
Sitta aliponea chupuchupu baada ya Rais Jakaya Kikwete kuunda Kamati ya Mwinyi, ambayo kwa muda sasa imekuwa ikihaha kuwapatanisha mahasimu hao; na sasa imefanikiwa kupunguza uhasama wa wazi miongoni mwao.
Katika kikao cha 18 cha Bunge kilichomalizika siku chache zilizopita, Sitta aliwashangaza wananchi alipofunga mjadala wa Richmond, huku akitarajiwa atumie fursa hiyo kuibana serikali itekeleze maagizo 23 ya Bunge kuhusu watu waliojihusisha na kashfa hiyo.
Sitta pamoja na wabunge waliokuwa wamejipambanua kuwa ni wapiganaji vita dhidi ya ufisadi wamelazimika kunywea, licha ya kutambua kuwa maazimio muhimu yaliyomtaka Rais Kikwete kuwajibisha waliokumbwa na kashfa hiyo hayakutekelezwa.
Katika kikao cha NEC kilichoisha hivi karibuni, Sitta aligoma kusuluhishwa na Lowassa na kundi lake, akidai kwamba hana ugomvi binafsi, bali anapambana na ufisadi. Kamati ya Mwinyi imeongezewa muda ili iwapatanishe mahasimu hao.
Mara baada ya kikao cha NEC, Pinda alianza ziara ya wiki sita mkoani Tabora; na alipofika Igunga, alitoa kauli ya kumtetea na kumsafisha Rostam kwa kauli ambayo baadhi ya wachambuzi walidai inalidhalilisha Bunge, kwani ilionekana kana kwamba “maneno ya bungeni” si maneno ya maana kwa wananchi kuyatumia kumpima mbunge wao.
Aliwataka wananchi wa Igunga wampime Rostam kwa kazi zake jimboni, si kwa “maneno ya bungeni;” Bunge lile lile linaloongozwa na Sitta.
Jana Waziri Mkuu alitembelea Wilaya ya Sikonge. Ziara yake mkoani Tabora inatarajiwa kuhitimishwa leo.
CHANZO: Tanzania Daima
26 Feb 2010
23 Feb 2010
23.2.10
Evarist Chahali
BUNGE, SAMUEL SITTA, UFISADI
No comments
Salim Said
SPIKA wa Bunge Samuel Sitta amewashukia wana-mtandao wa asasi za kiraia zinazotetea usawa wa jinsia, haki za binadamu na maendeleo ya ukombozi wa Wanawake, akisema wanatia mashaka na kwamba wanaendeshwa na utashi binafsi wa wajanja wachache, huku wenyewe wakisema maandamano yapo palepale.
Wanaharakati hao, walitangaza maandamano makubwa ya amani yatakayoendeshwa nchi nzima kupinga kuvungwavungwa kwa hoja za mikataba ya Richmond, TICTS, TRL, taarifa ya uchafuzi wa mazingira kwa kemikali za sumu katika mgodi wa North Mara na ukiukwaji wa haki za binadamu, Loliondo.
Akizungumza na Mwananchi jana Spika Samuel Sitta alipingana vikali na madai ya wanaharakati hao, kuhusu Bunge na kueleza kwamba mtu yeyote akitaka kupima uwezo na uzuri wa bunge katika maamuzi na kusimamia serikali aangalie rekodi ya kazi za bunge kuanzi mwaka 2005 hadi sasa.
'Mimi sikubaliani na wanaharakati hawa hata kidogo. Maandamano ni haki yao na waandamane, lakini hawawezi kupima kazi za bunge kwa kuangalia kipindi cha mitafaruku ," alisema Spika Sitta.
Spika Sitta alisema kuimarisha Bunge si kazi ya lele mama, bali ni mapambano yanayohitaji ujasiri wa hali ya juu.
"Mimi naamini kwamba bunge letu limeimarika katika kuisimamia serikali ukilinganisha na lilikotoka, wanaharakati wanapaswa kujua pia kuimarisha bunge ni mapambano," alisema Spika.
Kuhusu suala la bunge la mfumo shirikishi wa demokrasia, Spika Sitta alisema hilo ni kinyume na katiba, lakini aliwataka wanaharakati hao wajaribu kujenga hoja.
"Mimi naona mfumo wa demokrasia ya uwakilishi bungeni ni mzuri tu, kwa sababu unapatikana kupitia uchaguzi ambayo ni ridhaa ya wananchi, lakini mfumo shirikishi utapatikana wapi.
"Huwezi kushirikisha mashirika au taasisi hizo katika bunge, kwanza zinamwakilisha nani, kwanza haziwawakilishi wanawake ni utashi tu wa baadhi ya wajanja," alihoji Spika Sitta.
Alisema mitandao hiyo inatia mashaka kwa wahisani kwani baadhi ya taasisi zinakula fedha bila ya kupeleka mrejesho kwa wahusika.
"Mambo yote ya bunge yanajadiliwa hadharani na kila mtanzania anayetaka anasikia, lakini je mambo ya hawa wanaharakati na mitandao yao yanajadiliwa na nani," alihoji Spika Sitta.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Concern for Development Initiatives in Africa (ForDIA), Bubelwa Kaiza alisema ujumbe wao mkubwa katika maandamano hayo, ni kwamba hoja hizo zimevungwavungwa na bunge halitambui nguvu na mamlaka liliyopewa kikatiba, badala yake linafanya kazi kwa maslahi ya vyama vya siaasa na sio wananchi.
"Wapo wanaotaka tusiandamane, lakini huo ni woga wao tu, maandamano yapo palepale nchi nzima, tuna sababu za msingi za kuandamana kwani bunge halikuwajibika katika kushughulikia hoja mbalimbali katika kikao cha 18, badala yake limezivungavunga hoja hizo kwa maslahi ya vyama vyao vya siasa.
"Sisi pamoja na wananchi hatukuridhika kuhusu hoja zile zilivyohitimishwa, hakuna pia aliyewajibishwa, kwa hiyo tunaitaka serikali iachane na mfumo wa demokrasia wakilishi na ianzishe mfumo wa demokrasia shirikishi wa bunge ili wabunge waweze kuwajibika moja kwa moja kwa wananchi," alisema Kaiza.
CHANZO: Mwananchi






