4 Mar 2010


Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi,Rais Jakaya Kikwete alieleza kwa undani matarajio yake kuhusu ufanisi wa Sheria mpya ya Uchaguzi.Pamoja na mambo mengine,sheria hiyo inatarajiwa kuziba mianya ya rushwa kwa wanasiasa wanaowania uwakilishi wa wananchi katika Bunge.Hata hivyo,pamoja na nia njema na umuhimu wa kuwa na sheria hiyo,ushahidi wa kimazingira unaashiria kuwa itabaki kuwa sheria tu kama zilivyo nyingine nyingi pasipo kuzaa matunda yanayokusudiwa


Tatizo la nchi yetu halijawahi kuwa ukosefu wa sheria bali usimamizi na utekelezaji wake.Mifano ni mingi,lakini kwa vile sheria hii ya Uchaguzi inalenga kudhibiti mianya ya rushwa,ni vema tukaangalia kwanza ufanisi wa sheria nyinginezo zilizopo ambazo kwa hakika zingeaidia sana kupunguza tatizo la rushwa laiti zingetumika ipasavyo.

Kinachokwaza zaidi usimamizi na utekelezaji wa sheria zetu nyingi ni ukosefu wa uzalendo miongoni mwa waliokabidhiwa dhamana ya kuzisimamia na kuzitekeleza.Ni kichekesho kusikia miongoni mwa taasisi zinazotarajiwa kuwa na dhamana ya hali ya juu katika usimamizi na utekelezaji wa sheria hiyo ni TAKUKURU,chombo ambacho wengi wetu tunaamini kuwa kimeshindwa kazi yake.Hivi TAKUKURU iliyoshindwa sio tu kuchukua hatua dhidi ya wezi wa Richmond bali pia kutengeneza ripoti feki ya kuwasafisha watuhumiwa itawezaje kusimamia na kutekeleza sheria hiyo mpya ya uchaguzi?

Ikumbukwe pia kuwa kwa kiasi kikubwa vyombo vyetu vya dola bado vina fikra ya zama za chama kimoja ambapo "madhambi" ya wana-CCM yanachukuliwa kama "ubinadamu" na hivyo vyombo hivyo kusuasua kuchukua hatua zinazostahili.Kwa baadhi ya taasisi za dola,hata kukemea maovu yanayotendwa na baadhi ya vigogo wa CCM ni kama na kuvunja sheria za nchi!

Kwa mwenendo huu,ni dhahiri basi sheria hiyo inaweza kutumika kuvibana vyama vya upinzani huku wana-CCM wakiendeleza libeneke la takrima kana kwamba imehalalishwa.Sheria hii imeletwa na serikali ya CCM ambayo rekodi yake katika mapambano dhid ya rushwa ina walakini mkubwa.Iweje chama kilichounda serikali kiendelee kuwa na mwenyekiti wa kamati yake ya maadili (Andrew Chenge) ambaye ana tuhuma katika suala la rada?

Pengine badala ya kupoteza muda kwa kuja na sheria mpya,ungefanyika mchakato wa kupitia sheria zilizopo na kuhakikisha zinasimamiwa na kutekelzwa ipasavyo.Vinginevyo,itakuwa ni hadithi ileile ya kuja na sheria mpya zenye kuleta matumaini mithili ya kauli-mbiu "mAisha Bora kwa Kila Mtanzania" huku matokeo yake yakibaki sifuri.

3 Mar 2010

NI IDADI INAYOKARIBIA WALIOPIGA KURA MWAKA 2005

na Mwandishi Wetu

WATANZANIA wapatao milioni 8.4 wanashinda na njaa au kulala njaa ili kukabiliana na ukali wa maisha, utafiti umeonyesha.

Kwa mujibu wa utafiti wa Synovate uliofanyika kati ya Septemba na Desemba 2009, wananchi wanaahirisha milo kwa sababu hali ya kiuchumi ya Watanzania milioni 20 imezidi kuwa mbaya.

Mbali na wale waliopunguza bajeti zao (asilimia 43), na wale walioamua kuacha kula baadhi ya milo kwa siku (asilimia 21), watu milioni 11.2 (wanaowakilishwa na asilimia 28 ya wahojiwa), walisema hawajachukua hatua zozote dhidi ya kuongezeka huko kwa gharama za chakula wakati watu milioni 1.6 (asilimia 4) walisema wamekopa kutoka kwenye benki za biashara na hawajui jinsi ya kurejesha mikopo hiyo.

“Idadi ya wale waliosema kuwa hali zao za kiuchumi zimebakia vile vile ilikuwa ni watu milioni 16.8, ambao ni asilimia 42 ya wahojiwa.

“Ni watu milioni 1.4 sawa na asilimia 4 tu ya waliohojiwa, ndio waliosema maisha yao yameboreka, huku watu wengine milioni 2 sawa na asilimia 5 ya waliohojiwa wakisema hawajui,” alisema meneja huduma wa Taasisi ya Synovate, Jane Meela.

Kwa mujibu wa utafiti huo, idadi ya waliosema hali zao za kiuchumi zimekuwa mbaya zaidi ilikuwa kubwa zaidi kwa upande wa wanawake kuliko wanaume, wakati wanaume kidogo walisema hali zao za kiuchumi zilibakia vile vile.

Kwa kuzingatia kipimo cha maendeleo ya jamii, kisiasa na kiuchumi (SPEC), wananchi milioni 17.2 pia wamelazimika kupunguza matumizi yao ya vitu vya nyumbani kutokana na kupanda kwa gharama za mahitaji ya msingi.

Matokeo hayo yalitolewa na meneja utafiti na mawasiliano wa taasisi hiyo, Abdallah Gunda na meneja huduma, Meela, katika mkutano wao na wanahabari uliofanyika juzi jijini Dar es Salaam.

“Makali ya maisha nchini yamefikia hatua mbaya zaidi tangu utafiti wetu uliopita, na mwenendo wa sasa unatisha,” alisema Meela.

Alisema kinachoonekana ni kuwa watu maskini wameendelea kutokomea kwenye umaskini, huku kukiwa na watu wachache tu wanaoona kuwa hali za maisha yao zimekuwa bora.

Meela alisema serikali inahitaji sera na mikakati iliyojengwa na matokeo ya tafiti kama hizo kufanya gharama za maisha ziwe nafuu kwa kila mtu.

Utafiti huo ulihusisha sampuli nasibu za idadi ya watu 2,000 waliopatikana katika mikoa yote 21 ya Tanzania Bara, na visiwa vya Unguja na Pemba.

Alisema matokeo ya sampuli hizo yalipangwa katika jedwali na kufanyiwa upembuzi uliozingatia makadirio ya idadi ya watu milioni 40 nchi nzima ili kupata takwimu zilizokaririwa katika ripoti hiyo.

Matokeo hayo yanaonekana kuakisi hali halisi yakilinganishwa na mwenendo wa hivi karibuni wa mfumuko wa bei za vyakula.

Takwimu za Benki Kuu ya Tanzania (BoT) zinaonyesha kuwa mfumuko wa bei nchini umebaki katika tarakimu mbili.

Rais Kikwete aliingia madarakani kukiwa na nafuu ya mfumuko wa bei, kwani ulikuwa asilimia 5.8.

Hali ilikuwa mbaya zaidi mwaka jana mwezi Agosti, ambapo ulifikia asilimia 18.9, mwezi mmoja tu kabla ya kufanyika kwa utafiti huo wa Synovate.

Kiwango hicho kilishuka hadi kufikia asilimia 17.3 Septemba na kupanda hadi asilimia 18.1 Oktoba, na tangu wakati huo kimekuwa kikishuka na kupanda kati ya asilimia 14.5 na 17 kwa miezi iliyofuatia.

Wachumi wamekuwa wakitumia kigezo hiki kuthibitisha jinsi serikali ya awamu ya nne ilivyoshindwa kuboresha maisha ya mwananchi.

Na wanaharakati wametumia kigezo hiki, na kukithiri kwa ufisadi miongoni mwa vigogo serikalini, kama kielelezo cha Serikali ya Rais Kikwete kushindwa kutimiza ndoto zake za ‘maisha bora kwa kila Mtanzania.’

Naye Gunda alisema tatizo la rushwa na hongo ndilo lililotajwa kuwa sugu kwani linaathiri wengi nchini na lilipewa asilimia 53, likifuatiwa na tatizo la umaskini lililopewa asilimia 42, gharama za vyakula, asilimia 39, uhaba wa chakula na njaa, asilimia 38.

Tatizo la ajira, ukimwi na VVU, maji, kupanda kwa gharama za maisha, afya, umeme, ukame, barabara, elimu, kilimo, kutokuwepo kwa usalama na matumizi ya dawa za kulevya pia vilitajwa kama miongoni mwa matatizo makubwa nchini.

Utafiti huo umebainisha kuwa rushwa na umaskini ni matatizo yanayowaathiri zaidi wanaume kuliko wanawake.

CHANZO: Tanzania Daima


Not every one is blessed with good looks. I for sure wouldn't dare to compare myself to the likes of Brad Pitt or Denzel Washington.However,I'm quite happy and comfortable with my "plain" (or ugly as others would say) looks.When you finish reading the following story, you certainly are going to join me in cherishing whatever looks we have.

A Conservative Party delegate,Lynden Stowe,had to confirm his identity when he was on his way to hear his party Leader David Cameron speak in Manchester.Stowe,who bears stark resemblance to a racist Nick Griffin,leader of a far-right BNP,has had similar experience in the past.In the Manchester incident,he had to show his ID to the police who thought he was the BNP leader.

This episode reminds me of a number of incidents that have been reported by the media about people with huge beards who have were mistaken for Osama bin Laden.Whether or not such incidents had anti-Islam sentiments is for me to judge but being a lookalike to a high profile racist or terrorist is a million times worse than just being plainly ugly.

2 Mar 2010

Japokuwa kutolewa kwa Yanga katika michuano ya kimataifa kunaweza kupokelewa kama habari njema kwa watani wao wa jadi Simba, lakini ukweli unabaki kuwa hiyo ni habari mbaya kwa medani ya soka la kimataifa kwa nchi yetu. Lakini kipigo hicho kinaweza pia kuwa fundisho zuri kwa vilabu vyetu vya soka,hususan Simba na Yanga,vilivyokumbwa na “ugonjwa” wa makocha wa kigeni.

Nimesoma utetezi wa kocha wa Yanga, Kosta Papic, kwenye gazeti la Mwananchi kwamba sababu kuu za kutolewa kwa timu hiyo ni uwanja mbovu, hali ya hewa na matokeo mabaya katika pambano la awali. Kwa ujumla sababu zote hizo si za kitaalamu kwani hata shabiki ambaye hajawahi kucheza chandimu anaweza kukurupuka na sababu kama hizo. Papic anatoa visingizio hivyo huku akielewa fika kuwa havitoi majibu ya kwanini timu yake ilipata matokeo kama hayo (kufungwa) katika mchezo wa kwanza uliofanyika Dar es Salaam.

Je hali ya hewa ya Dar nayo ilichangia Yanga kupoteza mchezo wa awali? Vipi kuhusu uwanja wetu mpya na wa kisasa? Ni dhahiri kuwa alichofanya kocha huyo ni kuamua “kusema chochote” badala ya kukaa kimya. Kufungwa, na hatimaye kutolewa kwa Yanga hakuwezi kutohusishwa na mapungufu ya kocha huyo wa kigeni, na Papic analijua hilo ndio maana akakimbilia kuja na visingizio visivyo na uzito.

Lakini kwa namna flani, kuwalaumu makocha wa kigeni kwa asilimia 100 ni kama kutowatendea haki kwa vile hawakujiajiri wenyewe.Vilabu vyetu, licha ya kuwa ombaomba na kutegemea hisani za wafadhili, ziko tayari kujikakamua na umasikini wao wa kujitakia ili ziwe na “ujiko” wa kocha wa kigeni. La muhimu sio kocha anatoka wapi bali umuhimu wake kwa maendeleo ya timu husika.

Na kwa upande flani angalau makocha wazawa, au wa kutoka nchi jirani, wanaweza kuvumilia “mbinde” zinazotawala kila kukicha katika vilabu vyetu vya soka. Sasa kwa makocha wanaotoka sehemu zenye “tamaduni tofauti” kama Papic,kwa hakika kumudu soka letu inakuwa shughuli pevu.Sote twajua,kwa mfano,jinsi vilabu vyetu vinavyoendekeza “kamati za ufundi” kuliko ushauri wa wataalam wa soka. Sasa kwa kocha “mzungu” mwenye “roho nyepesi”, mambo kama hayo yanaweza kumkimbiza mapema tu.

Ni muhimu sasa kwa Yanga na timu zetu nyingine za soka kutafakari upya “ugonjwa” huu wa makocha wa kigeni. Ikumbukwe kuwa wakati kocha ni sehemu muhimu ya mafanikio ya klabu, wachezaji na mazingira ya soka katika mahala husika ni muhimu pia katika kupata mafanikio. Kwa mfumo wa kibabaishaji unaotawala medani ya soka letu, hata akija kocha mahiri kama Sir Alex Ferguson au Jose Maurinho bado hadithi inaweza kuendelea kuwa kama hiyo ya Yanga huko DRC.

Vilabu vyetu vinapaswa kutengeneza mazingira mazuri hususan kwenye ngazi ya uongozi na kujijengea uwezo wa kujiendesha pasipo kutegemea ridhaa za wafadhili.Ni katika mazingira hayo ndipo vitamudu kufanya usajili wa kutengeneza vikosi vya ushindi visivyo hitaji kusajili na kuacha wachezaji mara kwa mara.Kadhalika,ili kuunda timu ya ushindi ni muhimu kwa vilabu hivyo sio tu kuwa na vikosi visivyobadilika kila msimu bali pia kuwa na walimu (makocha) wanaookaa na wachezaji kwa muda mrefu ili kujenga mshikamano na kuelewana.Vingenevyo,tutaendelea kuwa wasindikizaji tu katika michuano ya kimataifa.


28 Feb 2010

bu
MBUNGE wa Sikonge, Said Nkumba (CCM) juzi jioni alimuacha hoi Waziri Mkuu Mizengo Pinda, pale alipowapa salamu ya shikamoo watoto ili pamoja na wazazi wao wamchague tena kuendelea kuwa mbunge wa jimbo hilo katika uchaguzi mkuu ujao.

Tukio hilo lilitokea wakati Waziri Mkuu alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Sikonge katika mfululizo wa ziara yake ya kuutembelea Mkoa wa Tabora.Kabla ya Waziri Mkuu kuanza kutoa hotuba yake, Nkumba alipewa nafasi ya kuwasalimia wapiga kura wake, ndipo alipoitumia nafasi hiyo kutangaza nia ya kugombea tena ubunge katika uchaguzi mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu.
“Mheshimiwa Waziri Mkuu, wakati ulipokuwa ukiahirisha kikao cha Bunge kilichopita ulisema sasa ni wakati muafaka kwetu kurudi kwa wapiga kura wetu ili kuwapa shikamoo.

“Leo ni siku ya bahati kwani watu wengi wamejitokeza katika mkutano wako huu na mimi naomba kuitumia nafasi hii kutoa shikamoo. “Kwa heshima na taadhima shikamoooni watoto wote mliopo hapa kuanzia mnaonyonya, watoto wa halaiki, watoto mliopo shuleni na shikamooni vijana na wazee wote mliopo hapa,” alisema Nkumba.

“Napenda sasa kutumia nafasi hii kutangaza nia kwamba nitagombea tena ubunge katika Jimbo la Sikonge na naomba wote mniunge mkono,” alisema Nkumba.
Tukio hilo lilimfanya Waziri Mkuu aliyekuwa amekaa jukwaani na viongozi wengine wa kitaifa, mkoa na wilaya, kuvunjika mbavu kwa kicheko.

CHANZO: Habari Leo

Maurice-Edu--001

Rangers have extended their Scottish Premier League (SPL) lead to 10 points after beating their Glasgow arch-rivals Celtic, thanks to a Maurice Edu’s goal seconds from the end of the Old Firm derby.

Well,I still like football though it’s not as much as I used to be back in the days.Although I have never been to a football stadium for ages,but I could describe myself as a Celtic fan if you were to ask me which team I support in Scotland.That has got nothing to do with me being a Catholic but rather it’s largely due to Henrik Larsson,a former Celtic star who was at his peak when I first arrived in Scotland nearly a decade ago.

So am I hurt by today’s results?Not at all.Actually,I’m somehow happy that a scorer of the Rangers’ goal is a Black person.Nothing to do with race but what would you expect in a nation where football colours could inflame a fight.Yes,Edu is an African-American who emerged victorious today after scoring the goal that could as well help Rangers retain their SPL title.

I have always wished I could attend an Old Firm derby but a few people I know in Glasgow have always warned me about potential of violence when the two big guns in Scottish football meet.

Just like like back home where victory for Simba against Yanga,or vice versa,is more important than qualifying for regional competitions,so is to Celtic and Rangers.The two teams’ records in European competitions have generally been dismal.I’m of the opinion that local football success should also translate into performing well in international tournaments.Both Celtic and Rangers are said to be in to difficult financial position,and qualifying for the Champions League would really make a huge difference.But for Rangers fans today,all that matters is their victory against their arch enemies.

Well,although I wish Celtic could have emerge victorious today,I’m a bit consoled by the fact a Black person-Edu-is entered in the Scottish footbal history books.

Big up,Edu!


27 Feb 2010

Pinda(2)

na Mwandishi Wetu, Urambo

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amemmwagia sifa kemkem Spika wa Bunge, Samuel Sitta akisema amejenga Bunge lenye sifa na umakini.

Pinda ambaye majuzi alimmwagia sifa Mbunge wa Igunga, Rostam Azziz (CCM) akiwataka wananchi wake wampime kwa kazi yake ni si kwa maneno ya bungeni, alisema Sitta amekuwa anaongoza Bunge kwa nia nzuri, na kwamba wanaolalamikia kazi yake ni wapotoshaji.

Alikuwa akihutubia wananchi katika Uwanja wa Jamhuri mjini hapa juzi, akasema Sitta ambaye ni Mbunge wa Urambo, amelifanya Bunge lisifiwe hata nje ya nchi.

Katika kusisitiza hili, Pinda alisema: “Hata watu wa nje wanalisifu Bunge letu…wanasema naam, hili ndilo Bunge…Bunge likicharuka kuhusu ufisadi wanasema hata si bure, nani asiyejua ufisadi? Ufisadi si rushwa? Bunge linachofanya ni watu wawe waadilifu.”

Aliwataka Watanzania waungane katika vita dhidi ya rushwa, kwani imesemwa tangu zamani kwamba rushwa ni adui wa haki.

Kwa takribani miaka miwili, Sitta amekuwa na uhusiano mbaya na baadhi ya vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wengi wakiwa wabunge wenzake, kuhusu anavyoliendesha Bunge.

Miongoni mwa walioathirika kwa “kazi nzuri ya Sitta” ni Rostam ambaye pamoja na rafiki yake Edward Lowassa (Monduli – CCM) walihusishwa kinamna na kashfa ya Richmond, ambayo ilisababisha Lowassa kujiuzulu wadhifa wake wa Waziri Mkuu.

Kutokana na msimamo wa Sitta na athari za Kamati ya Mwakyembe, CCM iligawanyika makundi mawili, moja upande wa Sitta jingine likiwa upande wa Lowassa na Rostam.

Uhasama wa makundi hayo uliongezeka na kujikita katika vikao vingine vikuu vya maamuzi vya CCM, kiasi kwamba mwaka jana, wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) walimbana Sitta katika moja ya vikao vyao, wakapendekeza avuliwe uanachama na afukuzwe ubunge, kwa maelezo kuwa anatumia vibaya nafasi yake kwa kuiaibisha CCM.

Sitta aliponea chupuchupu baada ya Rais Jakaya Kikwete kuunda Kamati ya Mwinyi, ambayo kwa muda sasa imekuwa ikihaha kuwapatanisha mahasimu hao; na sasa imefanikiwa kupunguza uhasama wa wazi miongoni mwao.

Katika kikao cha 18 cha Bunge kilichomalizika siku chache zilizopita, Sitta aliwashangaza wananchi alipofunga mjadala wa Richmond, huku akitarajiwa atumie fursa hiyo kuibana serikali itekeleze maagizo 23 ya Bunge kuhusu watu waliojihusisha na kashfa hiyo.

Sitta pamoja na wabunge waliokuwa wamejipambanua kuwa ni wapiganaji vita dhidi ya ufisadi wamelazimika kunywea, licha ya kutambua kuwa maazimio muhimu yaliyomtaka Rais Kikwete kuwajibisha waliokumbwa na kashfa hiyo hayakutekelezwa.

Katika kikao cha NEC kilichoisha hivi karibuni, Sitta aligoma kusuluhishwa na Lowassa na kundi lake, akidai kwamba hana ugomvi binafsi, bali anapambana na ufisadi. Kamati ya Mwinyi imeongezewa muda ili iwapatanishe mahasimu hao.

Mara baada ya kikao cha NEC, Pinda alianza ziara ya wiki sita mkoani Tabora; na alipofika Igunga, alitoa kauli ya kumtetea na kumsafisha Rostam kwa kauli ambayo baadhi ya wachambuzi walidai inalidhalilisha Bunge, kwani ilionekana kana kwamba “maneno ya bungeni” si maneno ya maana kwa wananchi kuyatumia kumpima mbunge wao.

Aliwataka wananchi wa Igunga wampime Rostam kwa kazi zake jimboni, si kwa “maneno ya bungeni;” Bunge lile lile linaloongozwa na Sitta.

Jana Waziri Mkuu alitembelea Wilaya ya Sikonge. Ziara yake mkoani Tabora inatarajiwa kuhitimishwa leo.

CHANZO: Tanzania Daima


26 Feb 2010



Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa TAKUKURU Dr. Edward Hosea akimkaribisha Rais Jakaya Mrisho Kikwete kufungua mkutano mkuu wa Mwaka wa taasisi hiyo.Picha kwa hisani ya MJENGWA

Hivi karibuni,uongozi wa kampuni ya magari ya Toyota ya Japan ulifanya jambo moja la kiungwana kwa kuwaomba radhi wateja wake kutokana na hitilafu za kiufundi katika modeli moja ya magari yake.Japo sakata hilo bado ni bichi hasa kwa vile inaelekea hitilafu hiyo bado haijapatiwa ufumbuzi,na tayari kuna habari za kushuka kwa hisa za kampuni hiyo katika masoko mbalimbali ya mitaji duniani,ni dhahiri hatua ya kuomba radhi imeonyesha kwamba kwa namna flani kampuni hiyo inatambua wajibu wake na inawajali wateja wake.

Majuzi,Rais Jakaya Kikwete alimwaga sifa kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) huku akijigamba kwamba serikali ya awamu ya nne imekuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya rushwa.Binafsi sidhani kama kauli hiyo ya JK inaendana na hali halisi ya utendaji na ufanisi wa TAKUKURU.

Kimsingi,tatizo haliko kwenye taasisi hiyo pekee bali kwenye medani nzima ya utawala bora.Angalia,kwa mfano,kauli za Waziri mwenye dhamana ya Utawala Bora,Mheshimiwa Sophia Simba,wakati wa sakata lililowahusisha wafanyabiashara wawili mashuhuri Bwana Reginald Mengi na Bwana Rostam Aziz.Badala ya kuhamasisha wananchi wanaojitokeza kuwaumbua hadharani mafisadi,Waziri Simba aliamua kuelemea upande mmoja ambapo bila aibu alimkemea Bwana Mengi huku akimlinda Bwana Rostam.

TAKUKURU hiyohiyo inayopongezwa na JK haijafanikiwa kujisafisha na tuhuma za namna ilivyouhadaa umma kuhusu suala la utapeli wa kampuni ya Richmond.Kamati ya Bunge iliyoundwa kuchunguza sakata hilo ilipendekeza Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Dr Edward Hosea,uamuzi ambao uko mikononi wa aliyemteua Hosea,yaani JK mwenyewe.Kwa hali ilivyo,na ukitilia maanani pongezi alozotoa JK kuhusu ufanisi katika mapambano dhidi ya ufisadi,ni dhahiri kuwa Rais hana mpango wa kumwajibisha Dr Hosea.

Nimesema tatizo liko kwenye utawala bora kwa vile hata chama tulichokipa dhamana ya kutuongoza-CCM-kimeendelea kufanya dhihaka linapokuja suala la utawala bora.Hivi inaingia akilini kweli kusikia kuwa Mbunge wa Bariadi,Bwana Andrea Chenge,bado ni mwenyekiti wa kamati ya maadili ya chama hicho tawala licha ya kuhusishwa kwake na tuhuma za ufisadi wa ununuzi wa rada!?Tusisahau kuwa pamoja na mageuzi ya kisiasa ya miaka ya tisini,bado chama tawala kimeendelea kuwa na nguvu pengine zaidi ya serikali,hoja kubwa ikiwa serikali hiyo imeundwa kutokana na ushindi wa chama husika.Kinachopuuzwa ni ukweli kuwa chama hicho hakikuomba ridhaa ya wanachama wake pekee bali Watanzania kwa ujumla.

Ni dhahiri kwamba kunakosekana utashi na udhati wa kupambana na ufisadi.Na kikwazo kikubwa kimeendelea kuwa kuweka mbele maslahi binafsi na ya chama badala ya maslahi ya umma/taifa.Pengine,na kwa hakika,badala ya kutetea mapungufu,ni muhimu kwa CCM na serikali yake kuiga mfano wa kampuni ya Toyota.Imetuangusha sana sio tu kwa kulegea katika mapambano dhidi ya ufisadi bali pia kwa ushiriki wake kwa kuwalinda watuhumiwa wa ufisadi.Laiti chama hicho kingekuwa na dhamira na utashi wa kukabiliana na ufisadi basi ni dhahiri Kamati ya Mwinyi inayoshughulikia mpasuko ndani ya chama hicho (wengine wanadai hakuna mpasuko) ingekuwa na kazi nyepesi tu ya kupendekeza wahusika wafikishwe kwenye vyombo vya sheria ili wasafishwe au waadhibiwe huko.Ikumbukwe kuwa tuhuma zinazowakabili watuhumiwa hao hazijaiathiri CCM pekee bali Watanzania wote kwa ujumla.

Nimalizie kwa kukumbushia usemi wa Kiingereza kwamba To err is human but to rectify is greatness,yaani (kwa tafsiri isiyo rasmi) kukosea ni ubinadamu lakini kujirekebisha ni uungwana.

23 Feb 2010

Angalia "mchemsho" huu  wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Samuel SITTA.Anarusha tuhuma nzito dhidi ya wanaharakati wanaokusudia kuandamana kupinga "mahitimisho ya mjadala wa Richmond bungeni" ilhali katika habari husika ameshindwa kuthibitisha tuhuma hizo.Kibaya zaidi,yeye mwenyewe aliporushiwa tuhuma kama hizo aligeuka mbongo.Hebu soma kwanza habari husika (hasa maneno ya rangi nyekundu)

Salim Said
SPIKA wa Bunge Samuel Sitta amewashukia wana-mtandao wa asasi za kiraia zinazotetea usawa wa jinsia, haki za binadamu na maendeleo ya ukombozi wa Wanawake, akisema wanatia mashaka na kwamba wanaendeshwa na utashi binafsi wa wajanja wachache, huku wenyewe wakisema maandamano yapo palepale.
Wanaharakati hao, walitangaza maandamano makubwa ya amani yatakayoendeshwa nchi nzima kupinga kuvungwavungwa kwa hoja za mikataba ya Richmond, TICTS, TRL, taarifa ya uchafuzi wa mazingira kwa kemikali za sumu katika mgodi wa North Mara na ukiukwaji wa haki za binadamu, Loliondo.
Akizungumza na Mwananchi jana Spika Samuel Sitta alipingana vikali na madai ya wanaharakati hao, kuhusu Bunge na kueleza kwamba mtu yeyote akitaka kupima uwezo na uzuri wa bunge katika maamuzi na kusimamia serikali aangalie rekodi ya kazi za bunge kuanzi mwaka 2005 hadi sasa.
'Mimi sikubaliani na wanaharakati hawa hata kidogo. Maandamano ni haki yao na waandamane, lakini hawawezi kupima kazi za bunge kwa kuangalia kipindi cha mitafaruku ," alisema Spika Sitta.
Spika Sitta alisema kuimarisha Bunge si kazi ya lele mama, bali ni mapambano yanayohitaji ujasiri wa hali ya juu.
"Mimi naamini kwamba bunge letu limeimarika katika kuisimamia serikali ukilinganisha na lilikotoka, wanaharakati wanapaswa kujua pia kuimarisha bunge ni mapambano," alisema Spika.
Kuhusu suala la bunge la mfumo shirikishi wa demokrasia, Spika Sitta alisema hilo ni kinyume na katiba, lakini aliwataka wanaharakati hao wajaribu kujenga hoja.
"Mimi naona mfumo wa demokrasia ya uwakilishi bungeni ni mzuri tu, kwa sababu unapatikana kupitia uchaguzi ambayo ni ridhaa ya wananchi, lakini mfumo shirikishi utapatikana wapi.
"Huwezi kushirikisha mashirika au taasisi hizo katika bunge, kwanza zinamwakilisha nani, kwanza haziwawakilishi wanawake ni utashi tu wa baadhi ya wajanja," alihoji Spika Sitta.
Alisema mitandao hiyo inatia mashaka kwa wahisani kwani baadhi ya taasisi zinakula fedha bila ya kupeleka mrejesho kwa wahusika.
"Mambo yote ya bunge yanajadiliwa hadharani na kila mtanzania anayetaka anasikia, lakini je mambo ya hawa wanaharakati na mitandao yao yanajadiliwa na nani," alihoji Spika Sitta.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Concern for Development Initiatives in Africa (ForDIA), Bubelwa Kaiza alisema ujumbe wao mkubwa katika maandamano hayo, ni kwamba hoja hizo zimevungwavungwa na bunge halitambui nguvu na mamlaka liliyopewa kikatiba, badala yake linafanya kazi kwa maslahi ya vyama vya siaasa na sio wananchi.
"Wapo wanaotaka tusiandamane, lakini huo ni woga wao tu, maandamano yapo palepale nchi nzima, tuna sababu za msingi za kuandamana kwani bunge halikuwajibika katika kushughulikia hoja mbalimbali katika kikao cha 18, badala yake limezivungavunga hoja hizo kwa maslahi ya vyama vyao vya siasa.
"Sisi pamoja na wananchi hatukuridhika kuhusu hoja zile zilivyohitimishwa, hakuna pia aliyewajibishwa, kwa hiyo tunaitaka serikali iachane na mfumo wa demokrasia wakilishi na ianzishe mfumo wa demokrasia shirikishi wa bunge ili wabunge waweze kuwajibika moja kwa moja kwa wananchi," alisema Kaiza.
CHANZO: Mwananchi

Tatizo kubwa linalomkabili Spika wetu Samuel Sitta ni uropokaji,yaani kuongea bila ktafakari athari zinazoweza kusababishwa na matamshi yake.Kama kiongozi mkuu wa chombo chenye dhima ya kutunga sheria za nchi,Sitta alipaswa kutambua kuwa baadhi ya kauli na tuhuma alizotoa dhidi ya wanaharakati ni za kihuni.Na bahati yake ni kwamba wanaharakati hao hawana muda wa kumburuza mahakamani kuthibitisha kashfa alizotoa dhidi yao.

Hivi Spika Sitta anaweza kuuthibitishia umma kuwa mitandao inatia mashaka kwa vile baadhi ya taasisi zinakula pesa bila kurejesha fedha kwa wahusika?Ameyajuaje hayo?Hivi hao wanaotoa fedha zao (wanaofadhili mashirika hayo) wamekuwa wajinga kiasi gani cha kutohitaji taarifa za matumizi ya fedha wanazotoa?

Sitta ni mropokaji kwa vile yeye alipotuhumiwa kukumbatia ufisadi katika ofisi ya Bunge aliwaka kama nini akidai ni njama za mafisadi dhidi yake.Iweje leo akurupuke kuwatuhumu wanamtandao kwa vile tu wameonyesha nia ya kuandamana kupingana na ubabaishaji wa Bunge linaloongozwa na Sitta?

Sitta asijione Mungu-mtu.Kila Mtanzania ana haki kama yeye Sitta kutoa mawazo yake hadharani alimradi havunji sheria za nchi.Kama Sitta anaona Bunge analoongoza limefanya vizuri katika utendaji kazi wake,si lazima kwa kila Mtanzania kuona hivyo au kukubaliana na mtizamo wa aina hiyo.Na ni vigezo vipi anavyoweza kutuonyesha Mheshimiwa Sitta kuwa Bunge lake limewajibika ipasavyo?Huko kutuzuga kwa zaidi ya miaka miwili kuwa yeye na wenzake ni wapambanaji dhidi ya mafisadi kisha kusalimu amri kama kondoo walionyeshewa mvua?

Na hata kama Bunge analoongoza Sitta linawajibika akama anavyotaka tuamini,si ndio kazi yake?Na si kazi ya kawaida kwani kwa mshahara wa mamilioni na kiinua mgongo cha mamilioni mengine kwanini waheshimiwa hawa wasiwajibikie kwa kiwango cha juu?

Sitta anakasirika kwa vile alitangaza kuwa "mjadala umefungwa",na kwa jinsi anavyojihisi ni Mungu-mtu anaona kitendo cha wanaharakati "kuendeleza mjadala" ni kama "wanavunja amri ya Mungu".Katika habari husika hapo juu,Sitta anathibitisha ubinafsi wake kwa kurudiarudia kutumia neno "MIMI".Anaweza kuwa sahihi katika mtazamo wake binafsi,lakini jamii hailazimiki kuafikiana nae wala kushurutishwa kutenda atakayo yeye.





22 Feb 2010

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amewashauri wananchi wa Jimbo la Igunga mkoani Tabora wasimkatae Mbunge wao Rostam Aziz wakati wa uchaguzi mkuu ujao kwa kusikia maneno yanayosemwa bungeni, badala yake wazingatie kile alichowafanyia.

Wakati Pinda anampigia debe Mbunge huyo jana kwenye mkutano wa hadhara katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, baadhi ya wananchi wa jimbo hilo walimwomba Waziri Mkuu amshinikize Mbunge wao abaki jimboni humo, kwa madai kuwa haonekani.

Wananchi hao walitoa ombi hilo ili waweze kupata fursa ya kumweleza kero zao na awaeleze yanayosemwa bungeni kuhusu yeye (Rostam)...ENDELEA



Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.