8 Jun 2011



SIASA NA HARAKATI

Dr. Asha-Rose Migiro (Tanzania)
Prof. Attahiru Jega (Nigeria)
Babatunde Fashola(Nigeria)
Johnson-Sirleaf (Liberia)
Goodluck Jonathan (Nigeria)
Jacob Zuma (South Africa)
John Githongo (Kenya)
Julius Malema (South Africa)
Kah Wallah (Cameroon)
Kofi Annan (Ghana)
Nana Rawlings (Ghana)
Nelson Mandela (South Africa)
Paul Kagame (Rwanda)
Robert Mugabe (Zimbabwe)
Salva Kir (South Sudan)
Wael Ghonim (Egypt)

FILAMU

Chiwetel Ejiofor (Nigeria)
Djimon Hounsou (Benin)
Genevieve Nnaji (Nigeria)
Idris Elba (Sierra Leone)

SAYANSI NA TEKNOLOJIA
 
Cheikh Modibo Diara (Mali)
Mark Shuttleworth (South Africa)
Dr. Rashika el Ridi (Egypt)
Dr. Thebe Rodney Medupe (South Africa)

FASHENI NA MITINDO
 
Alek Wek (Sudan)
Alphadi (Niger)
Iman (Somalia)
Liya Kebede (Ethiopia)
Oluchi Onweagba (Nigeria)

WATUNZI WA VITABU NA WASHAIRI 

Chimamanda Ngozi Adichie (Nigeria)
Chinua Achebe (Nigeria)
Lebo Mashile (South Africa)
Ngugi wa Thiong'o (Ethiopia)
Wole Soyinka (Nigeria)

UTAMADUNI NA DINI 

Bishop Desmond Tutu (South Africa)
Dr. John Sentamu (Uganda)
Otumfuo Osei Tutu II (Ghana)

WANAWAKE WENYE USHAWISHI 

Ayaan Hirsi Ali (Somalia)
Bineta Diop (Senegal)
Bisi Adeleye-Fayemi (Nigeria)
Dambisa Moyo (Zambia)
Graça Machel (Mozambique)
Helen Zille (South Africa)
Ory Okolloh (Kenya)
Dr. Precious Moloi – Motsepe (South Africa)
Souhayr Belhassen (Tunisia)
Professor Wangari Maathai (Kenya) 

Dr. Frannie Léautier (Tanzania)

BIASHARA NA FEDHA 


Aliko Dangote (Nigeria)
Arnold Ekpe (Nigeria)
Arumna Oteh (Nigeria)
Chris Kirubi (Kenya)
Prof. Chukwuma Soludo (Nigeria)
Cyril Ramamphosa (South Africa)
Donald Kaberuka (Rwanda)
Evelyn Oputu (Nigeria)
Fred Swaniker (Ghana)
Jean-Louis Ekra (Côte d'Ivoire)
Jim Ovia (Nigeria)
Mehdi Houas (Tunisia)
Mike Adenuga (Nigeria)
Mo Ibrahim (Sudan)
Mohamed El-Arian (Egypt)
Moïse Katumbi (Congo)
Naguib Sawiris (Egypt)
Ngozi Okonjo-Iweala (Nigeria)
Nicky Oppenheimer (South Africa)
Oby Ezekwesili (Nigeria)
Phuthuma Nhleko (Swaziland)
Salimo Abdula (Mozambique)
Sam Jonah (Ghana)
Stellah Kinonzo (Kenya)
Sanusi Lamido Sanusi (Nigeria)
Tdjane Thiam (Côte d'Ivoire)
Thierry Tanoh (Côte d'Ivoire)
Tokyo Sexwale (South Africa)
Tony Elumelu (Nigeria)
Trevor Manuel (South Africa)
Vincent Le Guennou (Côte d'Ivoire)
Wale Tinubu (Nigeria)

WANAHABARI 

Alain Foka (Cameroon)
Amadou Ba (Senegal)
Branko Brkic (South Africa)
Emna Ben Jemaa (Tunisia)
Ferial Haffajee (South Africa)
Isha Sesay (Sierra Leone)
 Ndesanjo Macha (Tanzania)
Nduka Obaigbena (Nigeria)
Tariq Ramadan (Egypt)
Trevor Ncube (Zimbabwe)

MUZIKI

Aliune “Akon” Thiam (Senegal)
Angelique Kidjo (Benin)
Hamada “El Général” Ben Amor (Tunisia)
Nneka Egbuna (Nigeria)
Youssou N'Dour (Senegal)

MICHEZO 

Danny Alexander Jordaan (South Africa)
Didier Drogba (Côte d'Ivoire)
Haile Gebreselassie (Ethiopia)
Roger Milla (Cameroon)
Samuel Eto'o (Cameroon)

CHANZO: Headturner






Mafisadi CCM wageuka mbogo

Na Jabir Idrissa - Imechapwa 01 June 2011

SASA ni piga ni kupige ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wanakataa kujiuzulu, MwanaHALISI limeelezwa.

Taarifa zinasema walipoitwa mbele ya viongozi wakuu wa chama hicho – makamu mwenyekiti Pius Msekwa na katibu mkuu, Wilson Mukama - wanaoitwa na CCM kuwa “watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini,” walishikilia msimamo kuwa hawawezi kujiuzulu kwa kuwa hawana hatia.

Wanaotakiwa kujiuzulu na viongozi wakuu wa CCM ni Edward Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge. Mkutano wa kuwashawishi wajiuzulu, ulifanyika Alhamisi na Ijumaa wiki iliyopita katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Lumumba, Dar es Salaam.
Taarifa zinasema katika mkutano huo, Msekwa na Mukama waliomba Lowasa ajiuzulu ili kukiokoa chama hicho, lakini yeye alipinga kwa hoja kuwa hana hatia.

MwanaHALISI lilipowasiliana na Msekwa kutaka kufahamu kilichojadiliwa katika mkutano wake na viongozi hao, haraka alisema, “…Umetoa wapi habari hizo?”

Alipoelewa ni vyanzo vya ndani ya chama na serikali, Msekwa alisema, “Hayo ni mambo ya ndani ya chama. Hatuwezi kuyaleta magazetini.”
Lowassa alipoulizwa juu ya kuwapo kwa kikao hicho, alisema ni kweli wamekutana. Hata hivyo, alisema hawezi kueleza walichojadili kwenye vyombo vya habari.

Rostam hakupatikana kueleza upande wake. Hata hivyo, MwanaHALISI limeelezwa na mtoa taarifa wake kuwa mbunge huyo wa Ingunga alitoka kwenye ukumbi wa mkutano akiwa amenuna na kuvurumisha “maneno makali.”

Anasema Rostam alitoka pale akiwa amenuna na kusema yeye hana hatia yoyote na kwa hiyo hastahili kushambuliwa. Amesema yote yanayotokea sasa yanatokana na uadui wa siasa za urais wa mwaka 2005 na ule wa 2015.


Hili linatokea wakati uongozi wa juu wa chama hicho ukishindwa kukabidhi barua ya kuwataka watuhumiwa hao wajiuzulu.
Kuchelewa kwa utekelezaji wa maazimio ya kuwawajibisha Lowassa, Rostam na Chenge kumezaa majungu na umbeya. Hivi sasa taarifa zinasema, Mukama anadaiwa kugoma kuandika barua ya kuwataka watuhumiwa hao kuachia nafasi zao za ujumbe wa Halmashauri Kuu ya taifa (NEC) wanazozishikilia.

Baada ya Mukama kugoma kuandika barua hizo kwa hoja kuwa kilichoamuriwa na NEC hakifahamu kwa kuwa alikuwa hajateuliwa, ndipo Nape Nnauye, katibu wa itikadi na uenezi alipoandika barua hizo na kuzipeleka kwa Msekwa.

Naye Msekwa alizipokea barua na kuzirekebisha. Akazirejesha kwa Nape ili azipeleke kwa Mukama kuzisaini. Mukama akagoma. Zikapelekwa kwa mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, ambaye taarifa zinasema, “amezifungia kabatini.”

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya kikao hicho, Lowassa alifika Lumumba saa nne asubuhi. Mazungumzo kati yake, Msekwa na Mukama inakadiriwa yalichukua takribani saa moja.

Katika mazungumzo hayo, Msekwa ananukuliwa akimweleza Lowassa “unatakiwa ujiuzulu nyadhifa zako za uongozi katika chama ili kutekeleza maagizo ya NEC na falsafa ya chama ya kujivua gamba.”

Akijibu hoja hiyo, mtoa taarifa anasema Lowassa alijibu, “Kuhusu Richmond (kampuni feki ya kufua umeme wa dahurula), ukweli unafahamika…Katika hili, mimi sina makosa. Rais anafahamu hilo na kila mmoja anajua hivyo.”

Anasema Lowassa alisema kama kuwajibika kwa makosa yaliyotokana na Richmond tayari amefanya hivyo kwa niaba ya chama chake na serikali pale alipoamua kujiuzulu wadhifa wake wa uwaziri mkuu.
Anasema mbali na kueleza hilo, Lowassa alisikika akisema, “nilikutana na Rais Kikwete. Aliyonieleza si haya.”

Alisema Rais Kikwete alimweleza kuwa hakuna maazimio yoyote ya NEC yaliyomtaka kujiuzulu. Akahoji, “Sasa nimwamini nani, ninyi mnaotaka nijiuzulu au rais aliyesema hakuna azimio kama hilo?”

Habari zinasema mara baada ya Lowassa kuwaeleza viongozi wake msimamo juu ya mazungumzo yake na Kikwete, ndipo Msekwa aliposikika akisema, “Lowassa acha mbio za urais.”

Naye Lowassa hakumkawiza Msekwa. Alijibu, “Lini nimetangaza kugombea urais? Lakini hata kama ninataka kufanya hivyo, ni haramu kugombea nafasi hiyo? Je, kuna mliowaandaa?”

Ni kauli hiyo ya Lowassa, iliyomshutua Msekwa na kusema, “Hapana. Hapana. Hakuna tuliyemuandaa…Haya mambo ya urais yatatuvuruga.”
Akihitimisha hoja zake kabla ya kumalizika kwa mkutano huo, mtoa taarifa anasema Lowassa alikitaka chama chake kuisaidia serikali kutekeleza wajibu wake kwa wananchi, badala ya kufanyia kazi kile alichoita, “majungu ya wanasiasa.”

Naye Chenge taarifa zinasema aliwaambia viongozi aliokutana nao kuwa yeye si fisadi na hafahamu maana ya ufisadi. Akataka kama tuhuma wanazomtuhumu wanaweza kuzithibitisha wamfikishe mahakamani ili aweze kujitetea. Hakuna maelezo ya ziada.

Hata hivyo, watu waliokaribu na kiongozi huyo wanasema, Chenge amejipanga kuhakisha kwamba hang’oki katika kiti chake cha NEC; ikibidi kuondolewa kwa nguvu ametishia kuondoka CCM na kujiunga na upinzani.

Kwa upande wa Rostam Aziz, taarifa zinasema alitakiwa kujiuzulu ujumbe wa NEC kwa tuhuma za kuingiza nchini kampuni feki ya Richmond na baadaye Dowans.

Mtoa taarifa anasema, mara baada ya kuelezwa tuhuma hizo, Rostam alihoji, “Haya ni maamuzi ya NEC?” Naye Msekwa akajibu, “NEC imetaka chama kijivue gamba kuanzia ngazi ya taifa hadi chini kwa kuondoa watu wote wanaotuhumiwa ufisadi.”

Habari zinasema, katika mazungumzo kati ya viongozi hao na Rostam, hakuna mahali popote ambapo Msekwa na Mukama walitaja ushiriki wa mbunge huyo wa Igunga, katika wizi wa fedha za umma kupitia kampuni ya Kagoda Agriculture Limited.

Kampuni ya Kagoda ni miongoni mwa makampuni 22 yaliyothibitika kuchota mabilioni ya shilingi kwenye akaunti ya madeni ya nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Gazeti hili limeshindwa kufahamu mara moja kilichosababisha Msekwa na wenzake kushindwa kumweleza Rostam ushiriki wake katika Kagoda. Hata hivyo, kwa zaidi ya miaka minne sasa, CCM imekuwa ikituhumiwa kunufaika na fedha za EPA hasa Sh. 40 bilioni zilizoibwa na Kagoda.

Wakati suala hilo likichukua sura hiyo, taarifa zilizofikia gazeti hili zinasema baadhi ya vigogo wa chama hicho wamepanga kupeleka hoja katika vikao vijavyo vya (CC) na (NEC) kushinikiza kufukuzwa ndani ya chama hicho wanaoitwa, “wasaliti ndani ya chama.”

Wanaopangiwa mkakati wa kufukuzwa ni spika wa zamani wa Bunge, Samwel Sitta na mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe wanaotuhumiwa kuanzisha Chama cha Jamii (CCJ) wakati wakiwa bado wanachama na viongozi wa CCM.

Wengine ni Nape Nnauye, Victor Mwambalaswa na Daniel Porokwa.
Habari kutoka ndani ya CCM zinawanukuu makada mawili; rais mstaafu, na mjumbe mmoja wa NEC wakitaka chama chao kuwafukuza waasisi wa CCJ kwa kukosa uaminifu.

MwanaHALISI limeelezwa na aliyekuwa naibu katibu mkuu wa CCJ, Dickson Ng’hily kwamba Sitta na Mwakyembe waliokuwa waanzilishi wa chama hicho, walimkatiza masomo yake nchini Afrika Kusini ili kusaidia kupatikana usajili wa chama hicho.

Ng’hily ambaye mahojiano yake yatachapishwa kikamilifu katika toleo lijalo amesema, aliyemwingiza yeye CCJ ni Sitta na Dk. Mwakyembe na anasikitishwa na hatua ya viongozi hao kutaka kuficha ukweli.

“Hawa watu ndio waanzilishi hasa wa CCJ. Mimi na Makonda tulipewa jukumu la kutafuta usajili wa chama. Lakini naona wenzangu wameamua kuficha ukweli kwa maslahi binafsi. Hii si sahihi,” ameeleza.

Ng’hily anaonyesha nyaraka za muhtasari wa vikao walivyoshiriki viongozi wakuu wa CHADEMA, John Mnyika, Anthony Komu na Tundu Lissu kuwa ni miongoni mwa watu walioshiriki katika majadiliano ya kuunganisha nguvu kati ya CCJ ya Sitta na CHADEMA.

“Tulikubaliana kama CCJ itakosa usajili, basi mheshimiwa Sitta atagombvea urais kupitia CHADEMA. Lakini kama tutafanikiwa kusajili chama chetu, basi Sitta angegombea urais kupitia CCJ na CHADEMA wangetuunga mkono,” anaeleza Ng’hily.

Kuibuka kwa Ng’hily kuelezea ushiriki wa Sitta na Dk. Mwakyembe katika kuanzisha na kusimamia usajili wa CCJ kumekuja wiki tatu baada ya Fred Mpendazoe kumtaja Nape Nnauye kuwa ni miongoni mwa waanzilishi wa kwanza wa CCJ.

Mpendazoe aliuambia mkutano mkubwa wa hadhara mjini Njombe kuwa yeye, Sitta na Mwakyembe ndio walianzisha CCJ; bali yeye alitangulia kutoka CCM ili kurahisisha usajili wa chama hicho. Wenzake walikuwa wamfuate baadaye.

CHANZO: Mwanahalisi


Ndugu. Kwa mara nyingine nawakilisha ombi la kunisaidia kutangaza (wakati wowote upatapo nafasi) kuhusu Dada mdogo RENATHA BENEDICTO ambaye tumepoteana kwa takriban miaka 12 sasa.

Renatha alikuwa mwanafunzi wa shule ya Sekondari Kibasila jijini Dar kati ya mwaka 1998 - 2001 na baada ya hapo alienda Songea TTC kujiunga na masomo ya ualimu. Pia alikuwa kati ya wahanga wa ajali mbaya ya Tawfiq iliyotokea tarehe kama ya leo mwaka 1999 ambapo alikuwa msaada mkubwa saana kuokoa maisha yangu. (Maelezo kamili yako http://changamotoyetu.blogspot.com/2009/04/namtafuta-renatha-benedicto.html)

Niliwasiliana naye kwa miaka miwili iliyofuata mpaka alipoenda chuoni Songea nami nikaondoka nchini mwaka 2003 na kwa miaka mingi sasa nimekuwa nikijitahidi saana kumtafuta bila mafanikio. Naomba kama anaweza kusoma ama kuna anayesoma na kumfahamu anisaidie kuwasiliana naye.

Email yangu ni [email protected]

NATANGULIZA SHUKRANI



7 Jun 2011


Ama kwa hakika Rais Jakaya Kikwete anaweza kabisa kushinda tuzo ya kuiongozi mbabaishaji aliyepindukia.Hivi inahitaji rocket science kwa mkuu wa nchi kufahamu majina ya viongozi wa dini wanaojihusisha na uuzaji wa madawa ya kulevya,kisha akayakalia majina hayo hadi kwenye halfa ya kidini na kulalamika BADALA YA kuchukua hatua stahili?Hata askari mgambo angeweza kuchukua hatua katika tuhuma kama hii kwa kuliripoti kwa vyombo vya dola.

Kikwete ni mbabaishaji,period.Nasema hivyo kwani hii si mara yake ya kwanza kukurupuka na kauli zake tunazoweza kabisa kuziita za kizushi akidai anawafahamu wahalifu.Mwaka 2006,mara tu baada ya kuukwaa urais kwa nguvu za wanamtandao (ambao baadhi yao leo wanaitwa magamba),Kikwete alifanya kituko kwa kudai sio tu anawafahamu wala rushwa bali anawafahamu kwa majina.Badala ya kuchukua hatua stahili,yeye akatoa deadline kuwa wajirekebishe la sivyo watamwona mbaya.

Ni dhahiri wala rushwa waliamua kumpuuza,na yeye mwenyewe ameamua kupuuza deadline hiyo kwani hadi leo hajaigusia tena.Ukidhani kuwa labda amejifunza lolote kuhusu tabia hiyo ya uropokaji,baadaye alifanya ziara Bandarini Dar na kudai tena kuwa anawafahamu watu wanaosaidia kukwepa ushuru bandarini hapo,na kwamba atawasilisha majina kwa wahusika ili wachukuliwe hatua.Kwa vile ubabaishaji uko damuni kwake,hakuweza kuwasilisha majina hayo wala kuchukua hatua stahili.

Sasa sijui ni kucnganganyikiwa au mwendelezo wa ubabaishaji,safari hii kakurupuka tena na uzushi mwingine akidai kuwa baadhi ya viongozi wa dini wanashiriki kwenye biashara haramu ya madawa ya kulevya.Hivi jamani,Rais mzima anasubiri hadi aalikwe kwenye sherehe ya kidini ndio atangaze kuwa anafahamu viongozi wa dini wanaojihusisha na uhalifu?Ina maana Kikwete hajui majukumu yake kama Rais wa Tanzania ni pamoja na kulinda sheria sambamba na kuchukua hatua dhidi ya wanaovunja sheria (including wazungu wa unga)?

Lakini safari hii,ubabaishaji wake unaweza kumtokea puani baada ya viongozi wa dini kumpa masaa 48 (hadi muda huu yatakuwa yamebaki kama 24 hivi) kuwataja hadharani viongozi hao wa dini anaodai wanashiriki katika biashara ya madawa ya kulevya.Na wamemtega vizuri kwelikweli kwa kumwambia aidha ataje majina hayo ndani ya masaa 48 au jamii imhukumu kuwa ni mnafiki na mzushi.

Soma habari husika hapa chini

JK awapasha viongozi wa dini
• Asema wapo wanaouza dawa za kulevya
na Stephano Mango, Songea

RAIS Jakaya Kikwete, amewaonya viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini kuacha tabia ya kushiriki biashara ya kuuza dawa za kulevya na badala yake washirikiane na viongozi wa serikali kuidhibiti biashara hiyo haramu.

Alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga wakati wa ibada maalumu ya kupewa daraja la uaskofu na kusimikwa kwa askofu wa jimbo hilo, Mhashamu John Ndimbo, katika kanisa la kiaskofu la Mtakatifu Killian iliyohudhuriwa pia na Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamini Mkapa.

Alisema baadhi ya viongozi hao wamekuwa wakishiriki kufanya biashara hiyo ya dawa za kulevya kwa kuwatumia vijana ambao huwafanyia mipango ya kuwatafutia hati za kusafiria (Passport) kwenda nchi za nje.

Badala yake Rais Kikwete amewataka viongozi hao nchini kuikemea biashara hiyo na kujenga uhusiano mzuri na vyombo vya dola katika kuhakikisha biashara hiyo inakomeshwa kwa kuwafichua wahusika wanaoifanya ili wachukuliwe hatua za kisheria.

“Inasikitisha sana na kutisha, biashara hii haramu sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu, taifa letu litaharibika tusipokuwa makini katika hili kwani baadhi yenu tumewakamata.

“Kwa kauli zenu kemeeni jambo hili kwa kuelimisha jamii hususan vijana waweze kuepuka na matumizi ya dawa hizi,” alisema Rais Kikwete

Chanzo: Tanzania Daima

Maaskofu CCT wampa Rais Kikwete saa 48 kuwataja Viongozi wa Dini "wauza unga"
06/06/2011

L-R: Kadinali Pengo, Rais Kikwete, Askofu John Ndimbo (picha: C.Sikapundwa)Katika taarifa ya habari iliyosomwa leo saa mbili usiku kupitia kituo cha runinga cha ITV, imetamkwa kuwa Maaskofu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania, CCT, wamempa Rais Kikwete saa 48 za kuwataja kwa majina viongozi wote wa Dini anaowatuhumu kuhusuka na biashara haramu ya madawa ya kulenya "unga".

Maaskofu hao wamesema endapo Rais atashindwa kufanya hivyo, basi itachukuliwa kwamba siyo mkweli.

Agizo la CCT lilitolewa na Mwenyekiti wake taifa, Askofu Peter Kitula jijini Dar es Salaam katika mkutano na waandishi wa habari linasema, “Tunampa saa 48 rais awataje kwa majina viongozi hao ambao yeye anadai wanajihusisha na kuuza dawa na kama atashindwa kufanya hivyo tunamtafsiri ni mwongo na mzushi... Tunasikitishwa na kushangazwa kwa kauli hiyo na tunamheshimu kama kiongozi wa nchi, hivyo tunampa masaa hayo awataje kwa majina” alisema Kaimu Mwenyekiti wa CCT, Askofu Mokiwa akichangia hoja.

Kauli ya Rais kuhusu viongozi wa dini kuhusika na biashara ya madawa ya kulevya inanukuliwa kuwa ilitamkwa siku ya Jumapili, Juni 5, 2011 wakati akiwa aalipowahutubia waumini wa Kanisa Katoliki la Jimbo la Mbinga wakati wa ibada maalumu ya kuwekwa wakfu na kupewa daraja la uaskofu na hatimaye kusimikwa kuwa Askofu wa jimbo la Mbinga, Mhashamu John Ndimbo.

Misa hiyo ilifanyika katika Kanisa la Kiaskofu la Mtakatifu Killian na kuhudhuriwa na Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa pamoja na mkewe, Anna Mkapa.

Rais Kikwete amenukuliwa na vyombo vya habari (1), (2), (3), (4), (5), (6) ... kuwa alisema ,“Inasikitisha sana na kutisha biashara hii haramu sasa inawavutia hata watumishi wa Mungu, Taifa letu litaharibika tusipokuwa makini katika hili, baadhi yenu tumewakamata,”... “Kauli zenu kemeeni jambo hili kwa kuelimisha jamii hususani vijana waweze kuepuka na matumizi ya madawa ya kulevya.”

Kwamba, baadhi ya viongozi hao wamekuwa wakishiriki kufanya biashara ya madawa ya kulevya kwa kuwatumia vijana ambapo huwafanyia mipango ya kuwatafutia hati na pasi za kusafiria kwenda nchi za nje kufanya biashara hiyo. Rais akawataka viongozi wa dini nchini kuikemea biashara hiyo na kujenga uhusiano mzuri na vyombo vya dola katika kuhakikisha biashara hiyo inakomeshwa kwa kuwafichua wahusika wanaoifanya ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Wakahoji, ikiwa Rais anawafahamu viongozi wa dini wanaohusika na biashara ya kuuza "unga" iweje ashinde kuwachukulia hatua za kisheria ikiwemo kuwakamata na kufunguliwa mashitaka?

Walisema viongozi wa dini wanalo jukumu la kutetea na haki mbalimbali za wananchi, na kuionya Serikali pale inapokosea.

CHANZO: Wavuti



Nuru The Light!!!

Jestina George had an opportunity to interview Artist  Fashion Blogger Nuru the Light and she gave us the full deets on her latest single ‘MUHOGO ANDAZI. Enjoy!!!!

JG: Why did you choose to pursue a music career?

NURU: IV BEEN SINGING SINCE THE AGE OF FOUR, I USED TO STAND WITH THE FAMILY CHOIR IN THE CHURCH AND SING. MY GRANDFATHER CANALI/MCHUNGAJI MAGOKE WAS A MAN OF GOD AND LIVED BY THE NAME OF GOD, SO BEING AROUND THAT WITH THE CHOIR I STARTED SINGING AT A VERY YOUNG AGE IT WAS AT 16YEARS OF AGE THAT I SIGNED A RECORD DEAL WITH STOCKHOLM RECORDS AND MY ARTIST NAME THEN WAS DANUMA.SO PROFESSIONALLY I STARTED AT 16 TO GO ON TOUR AND TRAVELLED ALOT PLUS ALL THAT COMES WITH THE JOB.

JG: How has the journey been since you started doing music?

NURU: AM GLAD THAT I STARTED YOUNG BECAUSE IT GAVE ME THE TOOLS, BOTH GOOD AND BAD THAT COMES WITH THIS JOB. AND ALSO A CHANCE TO MAKE MISTAKES SO THAT TODAY I CAN SAY I KNOW BETTER IN TERMS OF SIGNING A GOOD DEAL AND LOOK OUT FOR MYSELF. AT 16 I WAS JUST HAPPY TO BE SIGNED BUT TODAY I WOULDNT SETTLE FOR JUST THAT.

THE JOURNEY HAS BEEN BOTH GOOD AND BAD BUT THEN AGAIN I DONT KNOW IF I WOULD HAVE IT ANY OTHER WAY BUT AT THE SAME TIME IV LEARNED ALOT ALONG THE WAY, BOTH AS A WOMAN AND AN ARTIST.

IV BEEN LIED TO, PROMISED THINGS THAT NEVER HAPPEN, SOME EVEN TAKEN MY MONEY, TRUSTED THE WRONG PEOPLE BUT AT THE END OF THE DAY IT MADE ME STRONG SO THAT TODAY I CAN STAND UP FOR MYSELF, AS OPRAH ALWAYS TELLS HER GUESTS "SIGN YOUR OWN CHECKS!"

JG: What inspires you as a singer?

NURU: LIFE INSPIRES ME NOT JUST MINE BUT OTHERS ASWELL. SINGING IS MY PASSION, IS A WAY OF LIVING AND ITS SOMETHING THAT GOD BLESSED ME WITH.

MY VOICE IS A GIFT AND AM NOT GONNA LET GOD DOWN BY NOT USING IT....

JG: How long have you been singing for and how have you evolved as an artist?

NURU: IV BEEN SINGING SO LONG BUT EVOLVING AS AN ARTIST HAS ALOT TO DO WITH HOW YOU SEE YOURSELF. MY VOICE IS MY TOOL AND JUST AS YOUR BODY YOU HAVE TO TAKE CARE OF IT.

SMOKING, DRINKING, DRUGS AND SOME FOOD DESTROYS WHAT YOU HAVE IF YOU ARE NOT CAREFUL BUT TO ME TAKING LESSONS,LISTENING AND WORKING WITH OTHER ARTISTS AND ALWAYS LEARNING NEW THING MAKES ME EVOLVE AS AN ARTIST.

JG: What are your views on the Tanzanian entertainment industry today?

NURU: OUR TANZANIAN MUSIC INDUSTRY NEEDS MORE PEOPLE INVOLVED CAUSE AS OF RIGHT NOW FEW PEOPLE CONTROL THE MUSIC INDUSTRY AND THAT IS WHAT MAKES US NOT TO MOVE FORWARD. WE NEED MORE VARIETY RATHER THAN TWO VIEWS AND HOW TO RUN THINGS. WE NEED RISK TAKERS WHO ARE WILLING TO TAKE A CHANCE.,.,INSHALLAH WE WILL SEE...

JG: What are the best and worst parts of being an artist in Tanzania, though you live in Europe?

NURU: THE WORST IS THAT PEOPLE DON'T SEE YOUR VIEW OR GET IT RIGHT AWAY..THEY ARE SO USED IN DOING SOMETHING IN ONE WAY THAT IS WHY SO IT TAKES TIME TO CONVISCE THEM. SOMETIMES THEY DONT RESPECT SUDDEN ASPECTS LIKE TIME IS MONEY AND PROFFESIONALISM WHEN IT COMES TO WORK.

FOR EXAMPLE IF I AM NOT PRESENT IN TANZANIA MY WORK GOES VERY SLOW BECAUSE AM NOT THERE TO PUSH EVERYBODY WHILE THEY ARE ALREADY PAID AND THATS VERY SAD. THE GOOD PART IS THAT IN EUROPE I CAN LIVE MY LIFE AND GO ON WITHOUT THINKING THE PAPS ARE THERE.

I CAN GO TO A CLUB AND GO WILD WITHOUT SAYING OH GOSH, HERE AM JUST NURU AS OPPOSE TO NURU THE LIGHT OR NURU THE SINGER. AT MY WORK PEOPLE DONT EVEN KNOW THAT I SING AND AM OK WITH THAT.

JG: Would you say the bad economy crisis the world is currently facing as affected you directly as a singer?

NURU: IT HASNT REALLY AS A SINGER MAYBE ON A PERSONAL LEVEL BUT THE MUSIC INDUSTRY IS GONNA LIVE BECAUSE WHEN PEOPLE ARE SAD OR GOING THROUGH A HARD THING IN LIFE MUSIC ALWAYS HELPS SO IN THE LONG RUN IT HASN'T EFFECTED ME MUCH WHICH I THANK GOD FOR THAT.

JG: How many videos have you made till date? Name them if you can please

NURU: MORE THAN TEN VIDEOS BUT AM JUST GONNA NAME THE SWAHILI VERSIONS

WALIMWENGU
MSELA
KWANINI
"MUHOGO ANDAZI"
WAS FEAUTERED IN CHEGES VIDEO, MORACKA, AND QUICK ROCKA CALLED BULLET WHICH I WAS A LEAD GIRL.., FUN TIMES

JG: Tell us what inspired the concept for your latest single ‘MUHOGO ANDAZI’ and also tell us a bit about the video?

NURU: HAHAHAAHAHAHA THE SONG CAME ABOUT AS A JOKE, WE WERE IN THE STUDIO N BOB SAID NURU WE SHOULD CALL THE SONG MUHOGO ANDAZI AND I WENT LIKE HAHAHAAHA WE MJINGA NINI, UTANIITAJE MM ANDAZI AND THEN I STARTED SINGING CAUSE THE MELODY JUST CAME TO ME AND I SANG WE MUHOGO WEE AND HE ANSWERED ANDAZI WE AND THATS THE STORY OF HOW IT ALL STARTED. THIS SONG HAS ITS ON HISTORY BECAUSE SO MANY THINGS HAPPENED WHILE RECORDING LIKE COMPUTER DIED ON US WHILE RECORDING..,


Nuru at the studio recording "MUHOGO ANDAZI"

JG: How long did it take to shoot the video?

NURU: THE VIDEO TOOK 4HOURS ONLY TO SHOOT BECAUSE I ALWAYS COME PREPARED ON MY VIDEO SHOOT AND OTHERS.

JG: Tell us about the team behind the video, Who wrote the ‘Muhogo Andazi’, who produced it and who was your glam squad ? Who are you wearing? We’re style spotting already and we spot Chichia London, are we right?

NURU: THE SONG WAS RECORDED AT AT SHAROBARO RECORDS IN MAGOMENI AND BOB JUNIOR MR CHOCOLATE FLAVOUR PRODUCED THE SONG AND WROTE MOST OF THE LYRICS BUT MELODIES AND HARMONIES THAT WE DID BOTH ME AND HIM.

THE TEAM BEHIND WAS VISUAL LAB WITH ADAM JUMA AS A VIDEO DIRECTOR WHO CAME WITH HIS CREW AND MAKE UP PEOPLE BUT I DID MY MAKE UP ALL BY MYSELF SINCE I KNEW EXACTLY WHICH KIND OF LOOK I WANTED FOR THE SHOOT. I WORE MAC FOUNDATION AS A BASE AND I DONT HAVE ANYTHING ELSE EXCEPT THAT AND THE RED LIPS OFFCOZ.

I WORE TWO DRESSES BY CHICHIA LONDON AND TWO DRESSES FROM H&M. I WORE A COPPAR BRACELET/NECKLACE AND BANGLES FROM MADE BY AFRICA ANOTHER TANZANIAN BRAND MAKING GOOD STUFF. AND MR CHOCOLATE FLAVOUR WORE HIS YOUTHFULL SWAGG.,


Nuru at the shoot of her new video 'MUHOGO ANDAZI"

JG: Wow! You did a great job with the make up, now our favourite part, Talk us through wardrobe for the music video.

NURU: WHEN IT COMES TO MY WARDROBE FOR THE VIDEO I USUALLY PUT TOGETHER EVERYTHING THE NIGHT BEFORE AND I EAN EVERYTHING, FROM THE ACCESSORIES,TO SHOES,UNDERWEAR AND THE ACTUAL DRESS OR PANTS. I DO SO BECAUSE I WANNA COME PREPARED AND IT SAVES A LOT OF TIME WHEN YOU ARE IN LOCATION AND IT'S STRESS FREE. FOR THIS ONE IT WAS VERY EASY SINCE I KNEW AM WEARING CHICHIA AND MY LONG GREEN MAXI DRESS AND I WAS GOOD TO GO WHICH YOU ALL CAN SEE. YA ANOTHA THING DO YOU KNOW THAT I DID MY MAKE UP ON THE WAY TO LOCATION USING A SIGHT MIRROR OF THE CAR HAHAHAAHAH...,AND HOW GREAT IT TURNED OUT TO BE..,

JG: What should we look forward to next from Nuru?

NURU: AM NOT JUST A SINGER AM ALSO A FASHION BLOGGER, SO YOU SHOULD EXPECT A LOT MORE FROM ME CAUSE THERE IS MORE COMING INSHALLAH!!

JG: Do you have a message for our readers and your fans?

NURU: MY MESSAGE TO ALL THE READERS IS THAT WE AS BLACK WOMEN SHOULD LEARN TO LOVE YOURSELF,TO SUPPORT EACH OTHER, LOVE ONE ANOTHER AND BE GREAT ROLE MODELS TO OUR CHILDREN,THE TIME FOR A CHANGE HAS COME THAT WHEN YOU SEE YOUR FELLOW SISTER TRYING TO MAKE IT LEND HER A HAND AND WALK WITH HER AND TELL HER GO FOR IT BECAUSE SHE IS WORTH IT. AHSANTE!

Check out the video "MUHOGO ANDAZI" BELOW":

THANK YOU FOR YOUR TIME NURU & WE WISH YOU ALL THE BEST!!

JG



XOXOXOXOXOXO


For more on Nuru visit her blog NURU THE LIGHT

Chanzo: Miss Jestina

6 Jun 2011



Utawala wa Rais Jakaya Kikwete unaendelea na jithada zake za kutaka kuifanya Tanzania isitawalike baada ya jeshi lake la polisi kuendeleza ubabe dhidi ya viongozi wa Chadema.

Katika matukio yanayoweza kuingizwa kwenye vitabu vya historia (chafu),jeshi hilo maarufu zaidi kwa ubabe kuliko uwezo wake kukabiliana na uhalifu limewatia mbaroni Mwenyekiti wa taifa wa Chadema,Freeman Mbowe,na Mbunge maarufu wa chama hicho Zitto Kabwe.Wakati Mbowe,ambaye pia ni Kiongozi Mkuu wa Upinzani Bungeni (wadhifa unaomfanya kuwa Waziri Mkuu Kivuli) alikamatwa kwa madai ya kukiuka taratibu za dhamana katika kesi inayomkabili huko Arusha,Zitto alikamatwa kwa madai ya kuzidisha muda wa kuhutubia mkutano wa hadhara.

Tangu Tanzania iridhie uwepo wa mfumo wa vyama vingi vya siasa,mahusiano kati ya vyombo vya dola na vyama hivyo yamekuwa mabaya na ya ounevu kupindukia.Tatizo la wazi ni vyombo hivyo vinavyoendeshwa kwa fedha za walipa kodi pasipo kujali itikadi zao za kisiasa kuendelea kutekeleza majukumu yake kana kwamba ni matawi ya chama tawala.Wakati jeshi la polisi ndilo linaloongoza kwa kuwanyanyasa wapinzani,taasisi nyingine za dola kama Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania pia kwa nyakati mbalimbali zimeonyesha kuweka mbele unazi wa kisiasa na kuipendelea CCM.

Lakini licha ya kushamiri kwa vitendo vya ukatili dhidi ya wanasiasa wa vyama vya upinzani,kuibuka kwa Chadema kama ngome kuu ya upinzani kumekuwa mithili ya pilipili inayowawasha polisi kiasi cha kuwaandama viongozi wa chama hicho kila kukicha.

Ni dhahiri kuwa matendo haya yana baraka za Rais Kikwete kwani laiti angemwamuru rafiki yake Said Mwema,Inspekta Jenerali wa Polisi,kuhakikisha jeshi la polisi sio tu linawapa heshima viongozi wa upinzani bali pia lizingatie haki zao za kibinadamu,ni dhahiri tusingeshuhudia manyanyaso kama hayo waliyopewa Mbowe na Zitto.

Kikwete na jeshi lake la polisi wanapaswa kutambua kuwa kadri wanavyotumia nguvu nyingi kuwadhibiti Chadema ndivyo wanavyozidisha huruma ya Watanzania kwa chama hicho.Mtu yeyote mwenye akili timamu hatoshindwa kubaini kuwa unyanyasaji unaofanywa na jeshi la polisi dhidi ya chama hicho unalenga kukipunguzia nguvu katika jitihada zake za kupambana na ufisadi unaolelewa na serikali ya Kikwete na chama chake cha CCM.

Uzoefu unaonyesha kuwa tunaweza kulilaani jeshi la polisi hata kila sekunde lakini hiyo haitopelekea jeshi hilo lililosheheni mbumbumbu wa sheria za haki za binadamu kubadili utendaji kazi wao wa ovyo ovyo.Tunahitaji kwenda mbali zaidi ya kulaumu na kulaani pekee.

Ni muhimu basi kwa Chadema kuchukua hatua za kisheria dhidi ya jeshi la polisi.Kwa vile mahakama zetu nazo zinaendeshwa kisiasa,basi pengine ni muhimu kujaribu kufungua mashtaka ya aina hiyo katika mahakama za kimataifa.

Tetesi zinadai kuwa tawi la serikali ambalo kikatiba lina jukumu la kutafsiri ya sheria (Mahakama) chini ya uongozi wa Jaji Mkuu Othman Chande linaendesha shughuli zake "kishkaji" na tawi la serikali lenye jukumu la kusimamia sheria,yaani serikali kwa maana ya Executive branch.Tetesi hizo zinapigia mstari hoja kuu mbili.Kwanza,Jaji Mkuu Othman ni kaka wa Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa Othman Rashid,ambaye pia ni rafiki wa karibu wa Kikwete,kama alivyo IGP Mwema.Sasa ukiwa na kaka wawili kwenye nafasi nyeti kama hizo,na ambazo kikatiba zinapaswa kufanya kazi zake kwa kuzingatia mgawanyiko wa mamlaka (separation of powers),ni wazi kuwa nchi inaendeshwa kama kampuni ya mtu binafsi.

Kwa upande mwingine,Jaji Mkuu alikuwa miongoni mwa waalikwa kwenye semina elekezi iliyofanyika majuzi jijini Dodoma.Yayumkinika kuhisi kuwa ushiriki wa Jaji Mkuu kwenye semina hiyo kumepelekea Mahakama kumezwa na Serikali (Executive),na si aabu Mahakama ikawa inatekeleza majukumu yake kwa maelekezo ya serikali.Changanya hali hiyo na hizo teuzi za kufahamiana...!!!

All in all,ni lazima ukatili wa jeshi la polisi sio tu ulaaniwe kwa nguvu zote bali pia ukomeshwe kwa hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi yake.Na kwa vile mahakama za ndani ndio hivyo tena zishakuwa kama matawi ya CCM,kuna haja ya kutafuta haki kwenye mahakama za kimataifa.

Mwisho,Kikwete na watendaji wake,na jeshi lake onevu la polisi wanaweza kuwatupa ndani viongozi wa vyama vya upinzani kadri watakavyo...kwa muda flani, lakini kamwe hali hiyo haitaendelea milele.Kama ameshindwa dikteta Hosni Mubarak ataweza Kikwete?Tawala dhalimu zinaweza kudhani kuwa ubabe na uonevu ni silaha muhimu za ustawi wake lakini ukweli ni kwamba vitendo hivyo huharakisha uchimbaji kaburi la kuzika tawala za aina hiyo.

Ni muhimu kwa kila mpenda haki na usawa kukemea kwa nguvu zote uhuni huu wenye lengo moja tu: kudhoofisha mapambano yanayoongozwa na Chadema dhidi ya ufisadi unaolelewa na serikali ya Kikwete na CCM yake.Kadhalika,kashkash dhidi ya Chadema inamsaidia Kikwete na CCM yake kupooza mvurugano unaoendelea ndani ya chama hicho ambao umesababishwa na mgongano wa kimaslahi ya kifisadi.

Enough is enough!

3 Jun 2011

Mwana blogger wa wiki hii ni Evarist Chahali wa Kulikoni Ughaibuni

Leo tumepata bahati ya kufanya mahojiano na Evarist Chahali waKulikoni Ughaibuni na kwenye Twitter anapatikana kwa jina la Chahali. Toka nimefahamu hii blog mimi personal nimekua nikiifuatilia na nilipokea email kutoka kwa wasomaji wake wapenzi wanaoifuatilia na kupendekeza kama tutaweza kufanya mahojiano naye lakini hata mimi nilikua nina mpango wa kumwandikia ili tufanye mahojiano naye. Nilikua natamani sana mahojiano haya ili watu ambao hawajawahi kuiona hii blog yake wapate kuifahamu. Ni blog yenye mambo mengi sana na anajadili mambo yake vizuri sana, kwa upana na kama inavyotakiwa (Tell it like it is). Kama hujawahi kuisoma blog yake basi usiache kuingia na kuisoma. Asante sana Evarist kwa kukubali kufanya mahjiano na sisi unaweza kutuambia kidogo kuhusu blog yako?
Jina la blogu yangu la Kulikoni Ughaibuni lilitokana na swali la msingi nililokuwa nikijiuliza mara kwa mara nilipofika hapa Uingereza kwa mara ya kwanza. Kwamba “kulikoni wenzetu wanaweza hili lakini sie tushindwe?” Yaani kwa mfano, kulikoni ninapokwenda tawi la benki hapa ninyenyekewe kama mfalme lakini kwetu iwe kama manyanyaso japo ni fedha zangu na za wateja wengine ndizo zinaipa uhai benki husika?Au, kulikoni Waingereza, kwa mfano, waweke mbele zaidi maslahi ya nchi yao kuliko maslahi ya kisiasa au kibinafsi? Kwahiyo, kimsingi hiyo ndio maana halisi ya jina la blogu yangu. Blogu hii ina-focus zaidi kwenye masuala ya siasa (hususan za Tanzania) pamoja na social justice. Mimi ni mwanaharakati wa mtandaoni (e-Activist) na Kuliko Ughaibuni ndio kama “ofisi” yangu. Malengo ya blogu ni kuhabarisha, kufundisha, kukosoa na kuburudisha jamii. Natumia Kiswahili japo nyakati nyingine huwa naweka posts kwa lugha ya Kiingereza japo ni nadra.
Je, wewe kazi yako ni kublog tu au hii ni kama kazi ya muda tu au hobby?
Hapana. Mimi nina shughuli nyingine zinazoniwezesha kumudu maisha. Moja ya shughuli hizo ni uanafunzi wa shahada ya uzamifu katika stadi za siasa (PhD in Political Studies). Kwangu, kublogu ni zaidi ya hobby kwani ninaamini sana katika kupashana habari, kuelimishana, kukosoa na kuburudisha pia. Ila napenda kukiri kuwa nina hobby ya kuandika, na siwezi kupitisha siku pasipo kuandika kitu fulani, iwe ni mtandaoni au kwenye makabrasha yangu.
Jinsi gani unaanza kublog na kwa nini?
Nilianzisha blogu yangu mwezi April mwaka 2006.Wakati huo nilikuwa naandika makala kwenye magazeti ya Mtanzania na Kulikoni. Kwahiyo lengo la awali la blogu yangu lilikuwa kuifanya iwe mahala pa kuwawezesha wasomaji kusoma makala hizo, hasa kwa vile magazeti hayo yalikuwa hayapatikani mtandaoni. Lakini kwa vile makala hizo zilikuwa zinatoka mara moja tu kwa wiki, ilinilazimu niwe naandika habari nyingine pia katika blogu zaidi ya makala hizo.
Nini changamoto unazozipata kwa kuwa na blog?
Kwa uapnde mmoja blogu hii imeniwezesha kutengeneza marafiki mbalimbali, lakini pia imenitengenezea maadui, hususan kutokana na msimamo wangu mkali kuhusu suala la ufisadi. Suala la uandishi limenigharimu sana kimaisha kwani nilishawahi kupoteza ajira sehemu flani baada ya wenye mamlaka kutopendezwa na maandiko yangu. Changamoto nyingine ni ukweli kwamba Watanzania wengi wanapenda zaidi picha kuliko habari au uchambuzi. Pengine hili linaeleza kwanini licha ya blogu yangu kuanzishwa mwaka 2006 bado imetembelewa na chini ya watu laki tano. Wakati najibu maswali haya idadi ya waliotembelea ni watu 406660 tu. Hata hivyo, cha muhimu kwangu sio mamilioni ya wasomaji bali hata wasomaji wachache ambao wanaweza kufanyia kazi ninachojaribu kuishawishi jamii yetu hususan katika vita dhidi ya ufisadi
Unafanya nini wakati ukiwa hushughulikii hii blog yako?
Again, kama nilivyojitambulisha hapo awali,kwa upande mmoja mimi ni mwanafunzi (kwa sasa ninasoma part-time) na pia ninafanya shughuli nyingine za kimaisha ambazo nisingependa kuziweka hadharani japo ni shughuli halali (sio ufisadi,lol!).
Ni mara ngapi unafikiri juu ya blog yako wakati uko mbali na kompyuta?
Kwa kweli ni vigumu kusema ni mara ngapi lakini blogu yangu ni sehemu muhimu ya maisha yangu na ninajitahidi kuipa attention mara kadhaa kwa siku
Ni nani wasomaji wa blog yako?
Kwa hakika ni vigumu kujibu swali hili lakini nadhani wasomaji wakuu wa blogu hii ni pamoja na wasomaji wa safu yangu katika jarida la Raia Mwema (safu yangu inafahamika kama “Raia Mwema Ughaibuni”). Pengine wasomaji wengine wakuu ni watu wanaofahamu msimamo wangu katika vita dhidi ya ufisadi.Na labda wasomaji wengine ni kila anayependa kusoma uchambuzi wa habari na matukio kuliko kuangalia tu picha.
Je ni mitandao gani mingine ambayo unatumia ili iweze kukusaidia kuitangaza blog yako ili iwafikie wasomaji walengwa wa blog yako? Mfano Twitter au Facebook
Posts zangu zinachapishwa pia huko Facebook, Twitter na LinkedIn. Kadhalika, kuna nyakati huwa nasambaza baadhi ya posts kwa bloga wenzangu, sambamba na kutuma kwenye kumbi za mtandaoni kama Jamii Forums
Nini hasa ni changamoto kubwa wakati unatengeneza post ya kuweka kwenye blog yako na kwanini?
Changamoto yangu kubwa ni kuwa sahihi katika kila ninachoposti kwenye blogu yangu. Kwa uzoefu wa hapa Uingereza na nchi nyingine za Magharibi, kuandika kitu mtandaoni pasipo kuwa na uhakika nacho kunaweza kusababisha matatizo makubwa kisheria. Lakini changamoto nyingine ni lugha. Watu wengi ninaofahamiana nao tangu nifikie hapa Uingereza takriban miaka 10 iliyopita hawafahamu kiswahili. Sasa inawawia vigumu kwao kuelewa ninachoandika japokuwa nimeweka Google Translator kwenye blogu yangu. Miongoni mwa malengo yangu ya baadaye ni kuanzisha version ya kiingereza ya blogu hiyo ili kukidhi matakwa ya wasomaji waiofahamu Kiswahili
Unafanya nini iwapo kuna wakati huna la kuandika kwenye blog yako?
Huwezi kuamini lakini haijawahi kunitokea hata mara moja kukosa cha kuandika. Nilibainisha hapo mwanzo kuwa nina hobby ya kuandika. Hobby yangu nyingine ni kusoma. Hakuna siku ninayopitisha bila kusoma, iwe riwaya, blogu, habari mtandaoni au chochote kile. Hobby nyingine ni habari kwa maana ya zinazotangazwa radioni au kwenye runinga au mtandaoni. Kwahiyo hivyo ni vyanzo vyangu muhimu vya kupata vitu vya kuandika kwenye blogu yangu. Kingine kinachonisaidia sana kupata habari ni maongezi na watu wa kada tofauti za maisha.
Je ni nini mkakati wako na blog yako kwa ujumla?
Lengo la muda mfupi ni kuwa na tovuti kamili. Lengo la muda mrefu ni kuwa na taasisi ya habari, uchambuzi na utafiti. Baadhi ya rafiki zangu huwa wananiona kituko ninapowaambia kuwa malengo yangu ya baadaye sana ni kuanzisha “think tank” au policy institute (yaani taasisi ya sera).Actually, mmoja wa rafiki zangu hao alinipachika jina la one-man think tank, na nimelitundika jina hilo kwenye profile yangu ya Twitter.
Je ni bora kupata ukweli au uchunguzi wa jambo unalotaka kuliandika kwenye blog yako wewe mwenyewe au kupitia mtu mwingine?
Ni vigumu kwa mimi au blogger mwingine kuwa ndio chanzo pekee cha habari. Kwangu, cha muhimu sio kuwa chanzo cha habari bali usahihi na umuhimu wa habari husika.
Ni jambo gani bora blogger anaweza kutoa kwa wasomaji wake?
Kufundisha,kuhabarisha,kukosoa na/au kuburudisha. Hayo ndio malengo yangu makuu ya blogu yangu,na ninaamini yanaendana na dhima ya vyombo mbalimbali vya habari.
Ni jinsi gani (mtu) anaweza kuelezea style ya yako unavyo blog?
Disgustingly critical.Uandishi wangu unaweza kumkera msomaji anayeangalia tu “upinzani” au “ukosoaji” wangu..Kama mwanastadi wa taaluma ya siasa,msimamo wangu kitaaluma umeelemea zaidi kwenye critical thinking,wanachoita thinking about thinking.
Ni nini imekuwa mkakati wako kwa ajili ya kujenga kujulikana kwa mwenyewe na blog yako?
Binafsi sipendi kujulikana. Mimi ni mtu down-to-earth sana. Ningependa zaidi maandiko yangu yaeleweke na pengine kufanyiwa kazi kuliko mimi binafsi au blogu yangu kujulikana. Na kama kujulikana,basi makala zangu magazetini zingeweza kufanya kazi hiyo kwa ufanisi zaidi,lakini hiyo sio priority yangu kabisa.
Kila mtu ana post anayoipenda au anayoichukia. Je wewe ni post ipi unaipenda sana na kwanini? Na ni post ipi unaichukia sana na kwanini?
Binafsi naamini katika kupenda kila ninachokifanya. Napenda kazi zangu. Maana kama mie mhusika nisipopenda ninachofanya nitarajie nini kutoka kwa jamii? Lakini kwa minajili ya kujibu swlai lako,post iliyogusa hisia za wengi ni hii http://www.chahali.com/2010/09/chaguo-la-mungu-mafanikio-ya-kikwete.html Niliandika post hii wakati wa kampeni za Uchaguzi,na moja ya mambo ya kupigiwa mstari ni kwamba ilinukuliwa na aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema Dokta Willibroad Slaa katika ukurasa wake wa Facebook.Sijawahi kuchukia post yoyote niliyoandika kwa vile siamini kwamba kuchukia kitu ni njia bora ya kukirekebisha.Badala ya kuandika kiitu kisha nikakichukia,mie nakwepa kabisa kuandika kitu cha aina hiyo.
Je ni bloggers wapi ambao wewe unawaangalia na kufuata nyayo zao? Na kwanini?
Kuna bloga gwiji anaitwa Ndesanjo Macha. Huyu ndiye aliyenifundisha kublogu japo si kama tuliwasiliana. Nilitembelea blogu yake, nikafuata maelekezo yake ya namna ya kuanzisha blogu, na hatimaye Kulikoni ughaibuni ikazaliwa. Blogger mwingine ni mwanaharakati mwenzangu, Mwalimu Nkwazi Mhango wa Canada (ambaye pia huandika makala magazetini kwa jina la Mpayukaji Msemaovyo). Kufuata nyayo, well, mie sio mfuasi. Si kwamba ni mbishi kufuata walionitangulia bali naamini katika kufuata njia sahihi. Kwahiyo labda niseme nafuata nyayo za uandishi wa blogu katika namna inavyostahili badala ya kufata nyayo za mtu.You never know, unaweza kufuata nyayo zikakupeleka porini (I’m just kidding). Huwezi amini, lakini kila siku ninajitahidi kupitia takriban kila blogu ya Watanzania wenzangu kupitia Google Reader kwenye kompyuta au kwenye simu yangu. Nathamini kila kazi ya bloga wenzangu japo nitakuwa sitendi haki nisipowataja watu kama Michuzi “Mkubwa naMdogo”,Subi, Maprofesa Mbele na Masangu, Haki Ngowi, Abdallah Mrisho,Mubelwa, Jestina George, Dinahicious na wadogo zangu DjChoka, Sarah (Angalia Bongo) na Faith Charles Hillary (Candy1) na wengineo (kutowataja haimaanishi kuwa siwathamini). Pia nathamini sana kazi iliyotukuka ya Maxence Melo wa Jamii Forums.
Hebu tuambie ni watu gani umewahi kukutana nao wakati ukisughulikia post za kuweka kwenye blog yako?
Kukutana na watu physically hapana. Hilo halijatokea bado. Kukutana na watu through mtandao, hao ni wengi. Kama nilivyobainisha awali, moja ya faida ya kublogu ni kufahamiana na watu mbalimbali. Nimetengeneza marafiki kadhaa (na maadui pia) kupitia fani ya kublogu.
Je unafikiria kuwa unadaiwa na mtu akiyeacha comment/s kwenye blog yako?
Deni kubwa ni pale mtu anapoacha ushauri, ambapo nalazimika kuufanyia kazi. Deni jinginie ni uvumilivu pale mtu anapoamua kuacha comment kwa lugha ya matusi. Inataka moyo kumezea kashfa au matusi lakini I’m not just a grown up kid but thick-skinned too.
Je kunadhamani kujibu comment iliyoachwa kwenye blog yako wakati ukijua kuwa huyo aliyeiandika labda hatarudi kusoma jibu lake tena?
Huwezi jua,labda atarudi.Wanasema bora uamini Mungu yupo ili ukifa na kukuta hayupo you’ll have nothing to lose.Imagine unakufa wakati hukuamini existence ya Mungu, then unafika huko waendapo wafu na kukutana naye mlangoni...Ni salama kuamini kuwa anayeacha comment atarejea,na inapendeza kwa msomaji kuona umethamini comment yake na kuijibu (kama inastahili kujibiwa).
Je, umewahi kufikiria kuacha kupost comment ambayo iko negative kwako na ukijua hamna mtu atakayejua?
Hilo hutokea mara kadhaa.Kuna waungwana flani tulipishana lugha siku za nyuma wanapenda kunitumia comments zisizostahili kuchapishwa bloguni. Hey,my blog is like my home,and I reserve the right to welcome or deny someone kuingia humo. Lugha chafu haina nafasi kabisa katika blogu yangu.
Je unazitreat tofauti au unafikiri watu wanaoacha comment kwenye blog yako na kuacha majina yao yaonekane wazi wanastaili comments zao kujibiwa au hata kuacknowledge kuwa umeona maoni yao?
Mie ni muumini mkubwa wa uhuru.Msomaji ana uhuru wa kuandika jina lake anapoacha comment au kubaki anonymous.Cha muhimu kwangu sio jina la mtoa comment bali umuhimu wa comment yake.Mara nyingi napenda kutoingilia uhuru wa wasomaji kuacha comments zao bloguni kwangu.Kwahiyo napendelea zaidi kutochangia comments unless kuwe na umuhimu wa kufanya hivyo.
Je, unafikiria ni makosa kucomment kwenye blog yako kwa kutumia jina lingine?
Kama una jina lako halisi, na comment unayotoa ni yako binafsi, sioni umuhimu wa kutumia jina la mtu mwingine. Hilo ni kosa kisheria.I think the word for that is identity fraud. Lakini si kosa kutumia nickname au kutotumia jina kabisa kwa maana ya kubaki anonymous.
Je unazichukulia comments zote sawa unazotumiwa kwenye blog yako bila kujali maoni uliachwa?
Kwa hakika ninaheshimu comments zote,except zinazochafua hewa ie za matusi, kashfa, nk.Kwa vile uandishi wangu umetawaliwa zaidi na kukosoa, kamwe sichukizwi na mie mwenyewe kukosolewa. Naamini kujifunza kutokana na constructive criticism.
Je, unaamini comments kwenye blog yako zilizoandikwa kwa urefu sana zinahitaji kuzawadiwa zaidi kuliko zile zilizoandikwa kwa ufupi tu?
Inategemea kama urefu huo wa comment unaendana na uzito wa kilichomo. Comment ya mstari mmoja iliyojaa mantiki ni muhimu zaidi kuliko comment ya nusu ukurasa au ukurasa mzima iliyosheheni “hewa tupu”.Lakini kimsingi, ninazi-treat comment zote kwa uzito unaostahili.
Je wewe ni mtu ambaye uko rahisi kukata tamaa?
Hapana. Kukata tamaa is only for losers.Maisha ni mapambano.Vikwazo katika maisha ni sehemu muhimu ya maisha, na wakati mwingine vinatusaidia kujipanga upya. Hakuna mahala katika cheti cha kuzaliwa cha mwanadamu palipoandikwa kuwa life will treat you fairly. By the way, kukata tamaa hakujawi kumsaidia mwanadamu yeyote kufikia malengo yake. Kuna tofauti kati ya kukata tamaa na kuachana na jambo. Kama mtu anaona hawezi kitu flani basi ni vema akaachana nacho kuliko kupoteza muda kisha kukata tamaa na kuishia kuachana nacho mbeleni. Kila sekunde ni sawa na muujiza usiojirudia maishani. So it’s now or never.
Je unaedit picha zako ili ziwavutie sana wasomaji?
Kama ku-edit kwa minajili ya zionekane kwa ufasaha, jibu ni yes. Lakini kama editing kwa minajili ya kupachika kichwa cha mwarabu kwenye mwili wa mswahili, hapana. Mie nina allergy na photoshopping hususan kwenye uwasilishaji habari kwa umma.
Je unaepuka kuweka post ambazo ziko very controversy kwasababu ya kuogopa watu hawatakubaliana na wewe au huna hizo post?
Bahati nzuri mimi sio mwoga. Nilisoma Tabora Boys High School, enzi hizo ikiwa ni mchepuo wa kieshi, nilipomaliza nikaenda jeshini mwaka mzima kwa mujibu wa sheria. Na baadaye nikapita maeneo flani ya “nusu-jeshi” (paramilitary). Uzoefu huo umeondoa kabisa kitu kinachoitwa uoga. Kwa upande mwingine, kama mwanafunzi wa zamani wa sosholojia, natambua kuwa hakuna kitu kinachoweza kuafikiwa na wote. Kadhalika, natambua umuhimu na uwepo wa mitizamo tofauti. Kwahiyo kabla ya kuandika chochote kile bloguni kwangu huwa natafakari kwa makini kwa kutumia mizani hizo, sambamba na uzoefu wangu binafsi
Je unajisikia vizuri zaidi ukiweka post kwenye blog yako na ukapata maoni ya watu zaidi ya 20 au ukipata maoni ya mtu mmoja mashuhuri tu.
Kwangu,one useful comment is more important than 100 worthless comments. Of course, inapendeza kuona watu wakichangia topic flani lakini what if michango yenyewe ni kwa minajili ya kuandika tu? Nina tabia ya ku-track wanaotembelea blogu yangu kwa kutumia njia mbalimbali zinazopatikana kwa bloggers. Na mara kadhaa ninaona watu wanaotumia muda mwingi tu kwenye blogu yangu lakini hawaachi comment. Hilo sio tatizo kwani angalau kuna mtu amesoma na huenda akafanyia kazi alichokisoma.
Je unasema blog yako kuwa inamafanikio iwapo unapata watu wengi wa kusoma au unapata watu wengi wakuacha comment kwenye blog yako?
Kwangu, mafanikio ya blogu sio idadi ya watu wanaoacha comment au kuitembelea.Mafanikio ni pale ninachoandika kinapochangia jambo flani kwenye jamii. Kama mtu mmoja atatembelea blogu na kuona kitu cha maana, kisha kafanyia kazi kwa manufaa ya jamii, hayo ni mafanikio makubwa kuliko kutembelewa na watu milioni moja wanaopita bloguni “kuosha macho”.
Je blog yako unatumia jina lako kamili au unablog kwa kutumia kivuli kingine na watu wanasoma na kuenjoy blog yako lakini hawajui wewe ni nani?
Ninatumia jina langu kamili la Evarist Chahali. Tatizo ni kwamba nina majina mawili, moja “la kiofisi” (official) na jingine “la mtaani”. Unajua katika baadhi ya mila unapozaliwa unapewa jina la kuzaliwa na kisha unabatizwa (kwa sie Wakristo). Sasa kwa niliokutana nao masomoni au kazini wananifahamu zaidi kwa jina la Evarist, lakini kwa marafiki wa mtaani wananifahamu zaidi kwa jina la Jimmy. Sasa inatokea baadhi ya hao marafiki zangu wa mtaani kuhangaika kufahamu kuwa Evarist wa Kulikoni Ughaibuni ndiye huyohuyo Jimmy wa mtaani. Anyway, sichoki kuwaelimisha na taratibu tatizo hilo linazidi kupungua. Zamani hizo, niliwahi kuandika makala kwenye magazeti “ya udaku” ya Sanifu, Kasheshe na Komesha. Huko nilianzisha safu ya nyota (unajimu “wa kizushi”) na nilikuwa natumia jina bandia la “Ustaadh Bonge”. Mpaka leo baadhi ya marafiki zangu wachache wanaendelea kutumia jina hilo la utani. Lakini kwa sasa natumia jina langu kamili na halisi katika maandiko yangu yote.
Ni nini baadhi ya malengo yako ya mwaka huu kwa ajili ya blogu yako au unaonaje mwenyeew kwa kipindi cha mwaka mmoja ua mitano toka sasa hivi blog ya itakuaje?
Kama nilivyojibu hapo awali, malengo ya muda mfupi ni kuwa na tovuti kamili ya habari, na malengo ya muda mrefu ni kuwa na taasisi kamili ya habari,sambamba na uanzishwaji wa think tank. Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu, ninataraji blogu yangu itakuwa tovuti kamili.
Je upi ujumbe wako kwa wale watu wanaotaka kuanza kublog?
Ujumbe wangu ni mwepesi tu. Kama Michuzi aliweza, na mimi nimejaribu, kwanini isiwe wewe? Kuanzisha blogu ni kitu rahisi tu palipo na nia. Na kama kuna yeyote anayetaka kuanzisha blogu lakini anakwama kwa namna moja au nyingine, basi namkaribisha kwa mikono miwili kumsaidia katika hilo na hata kumfanyia promosheni ya blogu yake kwenye blogu yangu.
Je kwa maoni yako ni lengo gani kubwa kwa mwanablogger?
Kama nilivyojibu hapo awali,lengo ni kuhabarisha, kufundisha, kukosoa na kuburudisha. Haya ni malengo yangu makuu japo ninatambua kuna wanaoanzisha blogu kwa minajili ya kuweka maisha yao hadharani. Hilo sio kosa lakini ukifungua mlango unapaswa kutambua sio hewa safi tu itakayoingia bali pia hewa chafu, nzi, hata nyoka, nk. Lakini, hey, kila mtu ana uhuru wa kufanya apendacho...kula ile kitu roho inapenda.
Watu wengi wanafikiria kublog kwa ajili ya kupata hela. Je ni nini baadhi ya vidokezo kwa watu wanaofikiria kufanya hivyo? Je, ni ukweli upi wa baadhi ya matarajio yanayohusina na nini kinaweza kufanywa na nini hakiwezi kufanywa wakati wa kublog?
Ni kweli kuna wenye mawazo hayo.Kwa mtizamo wangu, money isn’t everything. Naomba nifafanue: kichaa anaweza kuokota tiketi ya bahati nasibu akawa milionea. Pengine anaweza kutumia utajiri wake kutibu ukichaa wake lakini label ya ukichaa haitamwondoka licha ya fedha zake. Jambazi anaweza kupora fedha na akapata utajiri wa ghafla. Lakini label ya ujambazi itaendela kuwepo, kama si akilini basi mioyoni mwa watu. Na kuna wanaopata fedha kwa kuuza utu wao. Na wote hao wanaweza kupoteza fedha na utajiri wao kama mzaha vile.Kwa huyo kichaa anaweza kuzimalizia kwenye matumizi ya kiendawazimu. Kwa jambazi anaweza pia kuzitapanya kwa vile hakuzitolea jasho kihivyo. Kwa upande mwingine, vitu kama elimu vinaendelea kubaki milele maishani unless mwenye elimu akatwe kichwa, which means death. Nikilipwa mamilioni kwa kublogu ilhali mamilioni ya Watanzania wenzangu wakitarajia nitumie elimu yangu kusaidiana nao kuitengeneza Tanzania bora, nitabaki kuwa msaliti. Sintokuwa tofauti na huyo kichaa au jambazi aliyefuma utajiri.Ndio,fedha ni muhimu kwa minajili ya kumudu maisha lakini kuna tuzo kubwa maishani zaidi ya fedha. Na kama bloga,tuzo kubwa kwangu sio udhamini mnono wa blogu yangu bali michango wake katika jamii yetu.
Asanteni kwa mahojiano haya.
Tunashukuru sana hapa Tanzania Blog Award kwa kufanya mahojiano na sisi na tunakutakia mafanikio mengi katika blog yako.
If you or someone you know would be great for our Weekly Blogger Interview, please [email protected] and tell us!

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.