17 Dec 2008

SOMA HABARI HII KISHA ANGALIA UCHAMBUZI WANGU
MLOLONGO wa matukio ya kufikishwa mahakamani kwa waliokuwa viongozi waandamizi katika Serikali ya Awamu ya Tatu pamoja na watuhumiwa wa wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), unaonekana kuwatisha viongozi wa Kanisa Katoliki na sasa wameanza kupanga mikakati ya kuliepusha taifa na hali ya machafuko.

Askofu Mkuu Msaidizi wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Methodius Kilaini, juzi aliiambia Tanzania Daima Jumatano katika mahojiano maalumu yaliyofanyika ofisini kwake kuwa, matukio yanayotokea sasa hapa nchini yanatisha kwa sababu yanaweza kuhatarisha amani iliyopo.

Alisema matukio ya kukamatwa kwa baadhi ya Watanzania wakiwa na mabilioni ya fedha zinazoweza kununua vijiji au mkoa, kufikishwa mahakamani kwa viongozi wastaafu wa serikali wakihusishwa na ufisadi na matumuzi mabaya ya madaraka wakiwa watumishi katika ofisi za umma, viongozi wa juu serikali kujiuzulu na matukio mengi ya mauaji ya kikatili, ni mambo yasiyokuwa ya kawaida na ya hatari.

Alisema kwa kutambua hali inayolikabili taifa, Kanisa Katoliki limeamua kuweka mikakati ya kulinusuru taifa na machafuko, itakayoongozwa na sala maalumu ya kuomba amani iendelee kutawala nchini.

“Kutokana na mambo haya mazito kutoka hapa nchini, tuna jukumu la kuhakikisha tunaiombea nchi yetu ili amani iliyopo iimarike kwa vile mlolongo wa matukio haya yasiyo ya kawaida yanaweza kuhatarisha amani iliyopo.

Sisi Kanisa Katoliki tumepiga kelele tumechoka, wenye jukumu la kuongea sana ni viongozi wa vyama vya siasa na mashirika ya kijamii. Sasa tumeamua kuanza na silaha kubwa zaidi ambayo ni sala, tumewaambia waumini wetu waanze utaratibu maalumu uliotolewa na Baraza la Maaskofu (TEC) wa kusali sala maalumu ya kuliombea taifa amani, ambao utafuatwa na waumini wote Wakatoliki,” alisema Askofu Kilaini.

Alisema pamoja na kusali, kanisa lina jukumu la kuishauri serikali juu ya mwenendo wa mambo nchini, pamoja na kukemea maovu, uvunjaji wa maadili, tabia za ushirikina zinazokithiri, mauaji ya kikatili ya mtu mmoja mmoja na ya koo na mambo mengine ya kifisadi yanayofanywa na baadhi ya viongozi ambao ni waumini wa makanisa au misikiti.

Hata hivyo, alisema si wajibu wa kanisa kuwakataa waumini wake wanaohusishwa na matukio ya ufisadi nchini kwa sababu kuwafukuza kundini si kuwasaidia, bali ni wajibu wa kanisa kuwaelimisha na kuwajenga watu katika maadili mema.

“Sisi si polisi au mahakama, kwa hiyo hatuna jukumu la kumtaja mtu binafsi hadharani au kanisani, kama muumini anashiriki katika mamabo ya kifisadi, tunalo jukumu la kumrekebisha au kumkemea, lakini si kumtaja hadharani.

“Lakini ifahamike kuwa yanapotokea matukio makubwa nchini kama haya ya ufisadi na serikali ikachukua hatua au kutochukua hatua, ni lazima kanisa lizungumze.

Hata hivyo hatua iliyokwishachukuliwa na serikali ya kuwafikisha watuhumiwa wa EPA na wengine waliotumia madaraka vibaya mahakamani wakati wakiwa madarakani ni nzuri, ila ieleweke kuwa kanisa halisemi kuwa watuhumiwa wamekwisha, haliwezi kusema hivyo.

“Kanisa linathamini na kutambua hatua za awali zilizokwisha kuchukuliwa na serikali za kuwafikisha watuhumiwa mahakamani, hatujui wapo wangapi, tunavuta subira kusikiliza kazi ya vyombo vya uchunguzi inayoendelea ili kuwafikisha wote mahakamani,” alisema Kilaini.

Akizungumzia mauaji ya albino, alisema kanisa linasikitishwa na hali inayoendelea nchini ya mauaji ya albino, vitendo ambavyo ni vya kikatili na ukiukwaji wa haki za binadamu vinavyoweza kuvunja umoja wa kitaifa.

Alisema mauaji ya albino yanakera, yanaitia aibu nchi na kuikosesha heshima machoni pa jumuiya ya kimataifa. Kwamba dunia inawashangaa Watanzania wanaishi karne ipi.

Alisisitiza kuwa matukio ya mauaji ya albino yameichafua nchi kiasi cha wageni kuiona Tanzania kama mahali pasipofaa kuishi.

“Wageni nao wanaanza kuogopa kuja kwani albino wakiisha nchini watafuata kundi jingine la watu, na kwa mtiririko huo, baadaye Watanzania wote wataanza kuuana. Serikali inatakiwa ilitangaze suala hili kuwa janga la kitaifa.

“Kama taifa tunapaswa kuchukua hatua madhubuti kupambana na kukomesha mauaji haya kwa vile tunakoelekea ni kubaya, wakimaliza albino, watawataka wenye kipara, baadaye watu weusi au wa kabila fulani, tukifika hapo ni vita ya wenyewe kwa wenyewe.

“Kanisa linaitaka serikali kutumia mbinu zozote, kutoa elimu kwa raia wake ikiwezekana kuanzia kwenye shule za msingi na sekondari juu ya madhara ya mauaji hayo. Kanisa linaiomba serikali iunde idara maalumu ya usalama wa taifa, makachero watumwe vijijini kuangalia kazi inayofanywa na waganga wa kienyeji, wachunguze kazi zao, wanavyopiga ramli na kupata ufumbuzi wa chimbuko na misingi ya mauaji hayo,” alisema Askofu Kilaini.

Akizungumza sababu ya kanisa kuchukua hatua ya kuanzisha mkakati wa kuomba ili kunusuru taifa na hali yoyote ya uvunjifu wa amani, alisema, imetokana na hofu ambayo kanisa limeipata baada ya kuwapo kwa ongezeka kubwa la matukio ya ajabu ambayo kwa kipindi cha miaka mingi hata kabla ya uhuru hayakuwahi kutokea.


KAMA MKATOLIKI,NAKUBALIANA NA KAULI YA KIONGOZI WANGU WA DINI MHASHAMU KILAINI.LAKINI KAMA MCHAMBUZI (MCHANGA) WA STADI ZA SIASA,NAOMBA KUTOAFIKIANA NAE KATIKA MAENEO YAFUATAYO.

KWANZA,KANISA KATOLIKI LINAPASWA KUKUBALI KWAMBA HALIJAFANYA VYA KUTOSHA KUPAMBANA NA MAOVU NDANI YA JAMII.NA KATIKA HILO,SIO KANISA PEKEE LINALOWEZA KUTUPIWA LAWAMA BALI TAKRIBAN MADHEHEBU YOTE HUKO NYUMBANI.TUNAWEZA KWENDA MBALI ZAIDI KWA KUANGALIA BAADHI YA MAMBO YANAYOWEZA KUWA SABABU KUU YA "UOGA" WA BAADHI YA VIONGOZI WA DINI KUKEMEA MAUMI MENGINE KATIKA JAMII.WENGI WETU TUNAFAHAMU "UCHAFU" WA BAADHI YA VIONGOZI HAO,NA JAPO KANISA LIMEKUWA LIKISISITIZA KUFUATA MAFUNDISHO YA VIONGOZI NA SIO MATENDO YAO,UKWELI UNABAKI KWAMBA NI VIGUMU KUTENGANISHA MANENO NA VITENDO VYA MSEMAJI.HIVI INALETA MAANA KWELI.KWA MFANO,MTUMISHI WA MUNGU ANAYEBANJUA AMRI YA SITA (MZINZI) KISHA AKAHUBIRI KUHUSU DHAMBI YA UZINZI?NI DHAHIRI MJUMBE WA YESU ANAPASWA KUISHI KAMA YESU MWENYEWE.YAYUMKINIKA KUSEMA KWAMBA LAITI MITUME WETU WASINGEKUWA WASAFI KATIKA MATENDO YAO,LEO HII TUSINGEKUWA WAUMINI WA DINI ZETU.

TUKIREJEA KWENYE HABARI HIYO HAPO JUU,SIJAMWELEWA VIZURI MHASHAMU KILAINI ANAPOSEMA "matukio yanayotokea sasa hapa nchini yanatisha kwa sababu yanaweza kuhatarisha amani iliyopo".JE ANAMAANISHA KWAMBA AMANI ITAHATARISHWA KUTOKANA NA TUKIO KAMA KUWAFIKISHA WATUHUMIWA WA UFISADI MAHAKAMANI?KWANINI SUALA HILO LISIWE KIGEZO CHA KUREJESHA IMANI YA WANANCHI ILIYOPOTEA KUTOKANA NA HISIA KWAMBA MAFISADI WANALINDWA?AMANI HAIWEZI KUHATARISHWA KWA KUWACHUKULIA HATUA MAFISADI,REGARDLESS YA NAFASI ZAO KATIKA JAMII.KWA NAMNA FLANI KAULI HIYO YA MHASAHAMU KILAINI INASHABIHIANA NA ILE ILIYOWAHI KUTOLEWA NA MKURUGENZI WA TAKUKURU,BW EDWARD HOSEA,KWAMBA WATUHUMIWA WOTE WA EPA WAKISHTAKI NCHI ITAYUMBA.

SITAKI KUINGIA KWA UNDANI KUHUSU DHANA KUWEPO KWA AMANI HUKO NYUMBANI,KWA SABABU DHANA HIYO NI TETE.JE AMANI NI KUTOKUWEPO KWA VITA PEKEE?JE KUNA AMANI KWA VILE WENYE VIPARA,VITAMBO,MAWOWOWO,ETC HAWAWINDWI KAMA MAALBINO?JE KUNA AMANI WAKATI IDADI YA WASIO NA UHAKIKA WA MLO WA KESHO NI KUBWA ZAIDI YA WALE WENYE UHAKIKA HUO?SIKU CHACHE ZIJAZO NITAINGIA KWA UNDANI KUANZISHA MJADALA KUHUSU DHANA YA AMANI NCHINI TANZANIA.LAKINI TUNALOWEZA KUHOJIM KWA SASA NI IWAPO MATUKIO YANAYOZUNGUMZWA NA MHASHAMU KILAINI YANAWEZA KUHATARISHA AMANI (KAMA TUNAKUBALIANA KUWA AMANI HIYO IPO,IN THE FIRST PLACE).

MHASHAMU KILAINI ANASEMA "Kanisa Katoliki limeamua kuweka mikakati ya kulinusuru taifa na machafuko, itakayoongozwa na sala maalumu ya kuomba amani iendelee kutawala nchini".NATAKA KUAMINI KWAMBA MKAKATI HUU WA KANISA UMEKUWEPO KWA MUDA MREFU ILA SASA UNAIMARISHWA.KINYUME CHA HIVYO ITAMAANISHA KWAMBA KANISA LIKO OUT OF TOUCH NA HALIJALI MADHILA YANAYOWAKUMBA WENGI WA WAUMINI WAKE.SI KWELI KWAMBA MATATIZO YANAYOIKABILI TANZANIA YAMEANZA MAJUZI KIASI CHA KANISA KUSHTUKA NA KUJA NA MKAKATI HUO,BALI MATATIZO HAYO YAMEKUWEPO KWA MUDA MREFU SASA.HATA MAUAJI DHIDI YA ALBINO HAYAJAANZA MWAKA HUU KIASI CHA KANISA KUSHTUKA WAKATI HUU TUNAPOELEKEA MWISHONI MWA MWAKA.

LAKINI TWENDE MBELE ZAIDI NA KUJADILI IWAPO MKAKATI HUO WA SALA UNAWEZA KUWA NA MAFANIKIO.TUNAFAHAMU KWAMBA BAADHI YA WATUHUMIWA WA UFISADI NI WAKRISTO WANAOHUDHURIA KANISANI KILA JUMAPILI.TUAMINI PIA KWAMBA MAHUBIRI MENGI HUKO KANISANI YANASISITIZA UPENDO NA KUPINGA VITENDO VYA KIFISADI.SASA KWA VILE VITENDO HIVYO SIO TU VIMEENDELEA BALI VIMESHIKA HATAMU TO ANA EXTENT YA KULIFANYA KANISA KUJA NA MKAKATI MPYA,NI DHAHIRI KWAMBA SALA PEKEE HAZIWEZI KULETA MABADILIKO YA MAANA.HAWA MAFISADI TUNAOJUMUIKA NAO MAKANISANI WANAPASWA KUWEKWA "KITIMOTO" HATA KAMA KUFANYA HIVYO NI KINYUME NA TARATIBU ZA KANISA.VIONGOZI WETU WA DINI WANAPASWA KUWAITA WAUMINI WAO WANAOTUHUMIWA NA UFISADI NA KUWAAMBIA (KATIKA LUGHA YA KIROHO) KWAMBA MATENDO YAO YANAMKERA MUNGU (NA MUNGU TUNAYEMZUNGUMZIA HAPA NI YULE TULIYEAMBIWA WAKATI WA KAMPENI KWAMBA "ANA CHAGUO LAKE KATIKA UCHAGUZI MKUU WA 2005").

NADHANI WENGI WETU BADO TUNA KUMBUKUMBU NAMNA ASKOFU LAIZER WA KKKT ALIVYOTUMIA MIMBARI YAKE KUMSAFISHA LOWASSA (REJEA MAKALA HII KATIKA JARIDA LA RAIA MWEMA).VIONGOZI WENGI WA DINI WAMEKUWA MASHABIKI WA WANASIASA,PENGINE KWA MASLAHI YAO BINAFSI BADALA YA YALE YA WAUMINI WAO AMBAO NDIO WANAOONJA JOTO YA JIWE KILA KUKICHA KUTOKANA NA MADUDU YA BAADHI YA WANASIASA HAO.NAKUMBUKA LECTURE MMOJA PALE MLIMANI (UDSM) WAKATI NASAKA SHAHADA YANGU YA KWANZA AMBAPO MHADHIRI MMOJA,DR MAX MMUYA,ALIELEZA KWAMBA FORCES KUU ZA KUWEZA KUBADILI TABIA,MAAMUZI NA MATENDO YA WANASIASA NA TAASISI ZA DINI NA WAHISANI.VIONGOZI WA DINI WAKTITISHI KUMTENGA KIONGOZI FISADI LAZIMA ATABADILIKA KWANI ANAJUA KESHO KUNA KIFO.WAHISANI WAKITISHIA KUNYIMA MSAADA BASI HATA WATUHUMIWA WA ANBEM WATAFIKISHWA MAHAKAMANI.KWA KIFUPI,MADHEHEBU YA DINI NCHINI YAMETUANGAUSHA WAUMINI WAKE KATIKA VITA DHIDI YA UFISADI.

TUREJEE KWENYE HABARI HUSIKA.MHASHAMU KILAINI ANASEMA "Sisi Kanisa Katoliki tumepiga kelele tumechokawenye jukumu la kuongea sana ni viongozi wa vyama vya siasa na mashirika ya kijamii. Sasa tumeamua kuanza na silaha kubwa zaidi ambayo ni sala...".HIVI KAMA KANISA LIMECHOKAM KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI LITAWEZA KWELI KWENYE MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI YANAYOLENGWA KUWASAIDIA WAUMINI WAKE WAUFIKIE UZIMA WA MILELE?THIS IS SHEER IRRESPONSIBILITY!KANISA HALIPASWI KUCHOKA,SIO TU KWENYE KUPIGA KELELE DHIDI YA UFISADI BALI PIA KWENYE KILA JAMBO LITAKALOWASAIDIA WAUMINI WAKE KUUONA UFALME WA MBINGU.KUDAI KUWA JUKUMU LA KUPIGA MAKELELE LIMEACHWA KUONGELEWA NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA NA MASHIRIKA YA KIJAMII NI TUSI KWA WAUMINI WA KANISA HILO.KWANI HAKUNA WAKATOLIKI MIONGONI MWA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA NA VYAMA VYA KIJAMII?KAMA WAPO,WAPI WATAPATA MWONGOZO WA KIROHO WA KUWAPA UJASIRI WA KUKEMEA MAFISADI KAMA SIO KANISANI?TANGU LINI KANISA LIKACHOKA?HIVI YESU ANGECHOKA KATIKA MISSION YAKE YA KUMKOMBOA MWANADAMU TUNGEKUWA NA AKINA MHASHAMU KILAINI?SALA PEKEE PASIPO KUPIGA KELELE HAZIWEZI KULETA MABADILIKO KWANI HIYO HAINA TOFAUTI NA KWA MWANAFUNZI KUSALI SANA LAKINI BILA KUJISOMEA KISHA AKATEGEMEA KUFAULU MTIHANI.SALA ZIENDANE NA MAKELELE ZAIDI YA KUKEMEA UFISADI.

MHASHAMU KILAINI AMEJITAHIDI KUNYAMBULISHA MAJUKUMU YA KANISA KWA WAKATI HUU (ACTUALLY,KWA MUDA WOTE) NA HAPO NDIPO ANAPOZUA CONTRADICTION KUBWA ZAIDI KWANI MAJUKUMU HAYO HAYATATEKELEZEKA IWAPO KANISA LITAKUWA LIMECHOKA.BY THE WAY,UCHOVU UNAOZUNGUMZIWA HAPA NI ULE UNAOSHABIHIANA NA KUKATA TAMAA AU UVIVU,NA VYOTE HIVYO NI MIZIZI YA DHAMBI.TUTAMUANIJE MHASHAMU KILAINI KWAMBA BAADA YA KUCHOKA KUPIGA MAKELELE KANISA HALITACHOKA PIA KUISHAURI SERIKALI?

MWISHO,NAUNGANA NA MHASHAMU KILAINI JUU YA UMUHIMU WA KUTANGAZA MAUAJI YA ALBINO KUWA NI JANGA LA KITAIFA.NAAFIKIANA NAE PIA KWAMBA SERIKALI INAPASWA KUZI-MOBILIZE TAASISI ZA USALAMA ZIONGEZE NGUVU ZAO KUKABILIANA NA JANGA HILO.KAMA INAFANYWA HIVYO KATIKA KUKABILIANA NA UJAMBAZI AU KUDHIBITI WAKIMBIZI,KWANINI ISIANZISHWE OPERESHENI MAALUMU DHIDI YA MAUAJI YA ALBINO?



Videos tu.tv
INTRO (T.I.):Life is an interesting journey; you never know where itll take you. Peaks and valleys, twists and turns, you can get the surprise of your life. Sometimes on the way to where you going you might think, this is the worst time in my life.But you know what, at the end of the road through all the adversity, if you can get where you wanted to be, you remember whatever dont kill you make you stronger, and all of the adversity was worth it. On your way to the top youll do anything. But how do you get your life back when you get there yeah thats my dilemma

A web developer has made thousands of dollars from George Bush after registering the lapsed domain name for his presidential library. 

George Huger bought the domain GeorgeWBushLibrary.com for just $10 (£6.60) after the web developers for the library website failed to renew it.

He then sold the domain back to the Bush family and their contractors for a whopping $35,000 (£23,000) - a 3,500% return on his investment.

GeorgeWBushLibrary.com is the official website for the presidential library of Mr Bush, located on the campus of Southern Methodist University in Dallas, Texas.

Jonathan Robinson, chief operating officer at domain registrar NetNames said opportunist speculators are so quick to pounce, "that brands, businesses and even former presidents can be at risk".

But internet and domain law expert Adam Taylor, principal at Adlex Solicitors, says there were several other options available.

He said: "It surprises me that they paid the $35,000 on the face of it. There are a whole range of options here."

Mr Taylor said the usual course in a case like this is to seek recovery of the domain name through arbitration under the "uniform domain name dispute resolution policy".

This protects rights owners where domain names have been registered and used in bad faith.

Court is also a possibility if it could be proven Mr Huger was misrepresenting himself as connected with the library, if he infringed a registered trade mark or if he broke the US laws on cybersquatting.

Mr Taylor added: "It looks to me as though there's a possibility the web development company paid it off their own back, perhaps out of embarrassment.

SOURCE: Sky News

16 Dec 2008



Chati ya Muntadhar al Zaid,mwandishi aliyemtupia viatu Rais Bush imepanda ghafla.Tayari charity organization moja huko Libya imetangaza kutoa tuzo kwa mwandishi huyo.

15 Dec 2008

Hii ni kwa mujibu wa mujibu wa Jamii Forums.For developing stories FUATILIA HAPA.

He had been hunted, kidnapped, and told he was filming his own execution. But CNN correspondent Michael Ware had no plans to leave Iraq. Now, it won’t leave him...CLICK HERE FOR THE FULL STORY.


14 Dec 2008

Makamu Wa Pili wa Rais wa TFF,"Ustaadh" Ramadhan Nassib (mbele kulia) akishangilia baada ya kushinda nafasi hiyo dhidi ya mpinzani wake Damas Ndumbaro katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika leo jijini Dar.Ila Ustaadh,mbona TFF sasa iko chini ya Yanga tupu?Tenga alikuwa Pan (mtoto wa Yanga),Nyamlani ni Yanga na wewe ndio kama vile.....just kidding!Big up,man.You made it.At least jamaa kadhaa wanaweza kusema "tuna mshkaji TFF...!!!".Picha na habari  kwa hisani ya MICHUZI

13 Dec 2008

Watanzania wengi wanapenda habari.Na siku hizi vyombo vya habari viko vya kumwaga.Hata hivyo,upatikanaji wa habari za uhakika bado ni tatizo.Kwanza,wanahabari wengi wa huko nyumbani wanapendelea zaidi kuripoti habari badala ya kuleta habari iliyochunguzwa.Leo hii ukitoka ughaibuni na vizawadi viwili vitatu kisha ukaitisha press conference na kudai unataka kuanzisha mradi flani,kesho yake habari hizo zitaripotiwa kama ulivyotaka.Na kama hiyo press conference itaambatana na makulaji na vinywaji basi si ajabu habari hiyo ikawa ukurasa wa kwanza.Of course,kuna exceptions kwenye magazeti kama This Day,Kulikoni,Raia Mwema,Mwanahalisi na mengine machache.

Tatizo la pili katika upitakanaji wa habari liko katika mafungu mawili.Kwanza,japo magazeti ni mengi,wenye uwezo wa kununua bado si wengi sana.Bei ya wastani ya gazeti ni shilingi 400.Ukizingatia ugumu wa maisha,ni vigumu kutoa kiasi hicho kwa gazeti ambalo ukishasoma linakuwa halina matumizi mengine ya muhimu.Pili,upatikanaji wa habari kwa njia ya runinga na redio bado ni mgumu katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.Nilipokuwa Ifakara hivi karibuni,nilibaini kwamba ili uweze kukamata matangazo ya vituo vyote vya televisheni ni lazima uwe na "ungo".Sasa unaweza ku-imagine ni watu wangapi wenye uwezo wa kumudu gharama za kununua na ku-install satellite dish.

Pamoja na "chengachenga" za hapa na pale,redio imeendelea kuwa tegemeo la wengi hasa vijijini.Na ukipta hapa na pale utakuta wazee wetu nyakati za jioni wakisikiliza matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC au Deutsche Welle.Na kupitia matangazo hayo ndipo mzee wangu mmoja niliyeongea nae kwa simu jioni ya leo alipata habari kwamba kuna wawekezaji kadhaa "walioingizwa mkenge" na tapeli mmoja,Bernard Madoff,katika kile kinachofahamika kama Ponzi Scheme.Mzee huyo aliniuliza inakuwaje "wazungu" wenye uelewa mkubwa wa mambo waliweza kuhadaika na kushiriki "upatu" huo?Sikua na jibu kwa vile habari yenyewe ilikuwa bado ngeni kwangu.Kama mwenzangu nawe hujaipata,BONYEZA HAPA kuisoma kwa undani.

The crisis in Somalia is getting worse as a force of Islamic militants, led by a hardline wing known as al-Shabab, seizes more territory, threatening the fragile transitional government. The Ethiopian troops that are backing the government are likely to leave the country soon, and experts warn this may lead to the government's collapse and the potential of Somalia becoming a safe haven for terrorists.

"They're expanding their reach,"said Jeniffer  Cooke,head of the Africa program at the Center for Strategic and International Studies in Washington. "They've seized a number of key port towns - Merka, Kismayo - and are really driving the chaos that is engulfing Mogadishu at this point."

There has been no real central Somali government since 1991. Only U.S. aid and the presence of Ethiopian troops who invaded in 2006 have kept the current transitional government in Mogadishu from collapse.

Although Ethiopia has announced it would pull out of Somalia by the end of the year, the government has hinted it could delay the move. Still, a withdrawal could prompt African Union peacekeepers to follow suit. 


U.S. State Department spokesman Sean McCormack says Washington is trying to avert a collapse in Somalia. "We're trying to work through the international system, that is trying to find a way that you can have a responsible international force in Somalia to help provide some security and therefore some stability," McCormack said. "And allow some of these weaker institutions to start to take hold in a positive way."

The concern in Washington is that if the militant al-Shabab takes control of Somalia the country could become a launching ground for terrorists.

Joint Chiefs of Staff Chairman Admiral Michael Mullen spoke about the danger at a news conference Wednesday."I am concerned about the potential for a safe haven in Somalia as I am in Yemen. I try to pay a lot of attention to the evolution of potential safe havens, these two in particular and specifically to the one in Somalia," Mullen said. "So, I'm extremely concerned about that."

The United States considers the multi-clan al-Shabab a terrorist group. 

It practices a harsh form of Islamic law as seen in this recent video of a beheading released by the militants. Its propaganda videos, and its terror tactics have led some to believe the group may have ties to al-Qaida. 

"Whether or not the links are direct, we don't know," Cooke stated. "There have been former al-Qaida operatives within Mogadishu responsible for the bombings in Dar Es Salaam and in Kenya in 1998, but certainly there's a potential there, a very strong potential for increasing support and linkage with al-Qaida."

Cooke and other experts say the prospect of further violence and a deepening humanitarian crisis in Somalia could become a major problem for the incoming Obama administration. 

SOURCE: VoA

Kwenye uchambuzi makini,vitu kama laana,nuksi au bahati mbaya huwa havileti maana yoyote.Lakini katika maisha yetu kijamii tunafahamu kuwa jambo likiandamwa na kutofanikiwa linaweza kuhusishwa na laana au bahati mbaya.Na kama kuna sekta ambayo imekuwa ikiandamwa na matatizo kwa muda mrefu huko nyumbani basi ni usafiri.

Ukiangalia usafiri kuanzia kwenye cities hadi vijijini utabaini kwamba kadri unavyozidi kwenda chini (city ikiwa juu na kijiji chini) ndivyo matatizo yanavyozidi kuongezeka.Matatizo ya daladala jijini Dar ni "cha mtoto" ukilinganisha na namna ya kufika sehemu iitwayo Tanganyika Masagati (sijui kama ushawahi kuisikia).
Na hata hapo Dar,kero ya usafiri inazidi kuongezeka kadri unavyoelekea kwenye vitongoji vya jiji hilo.Ushawahi kufika Pemba Mnazi?Mara kwa mara tunasikia mipango mipya ya kuboresha usafiri,hasa jijini Dar.Tulisikia kuwa vipanya vingekuwa phased out lakini wajuzi wa mambo walishajua kuwa hilo ni changa la macho kwa vile wamiliki wengi wa vipanya hivyo ndio haohao wanaotuzuga kwenye media kuwa vipanya ni kero.Wanajuaje kero za vipanya ilhali wao wanazungushwa na ma-VX au Vogue yao yenye viyoyozi?
Tukiachana na usafiri wa barabara,wa majini ndio wa roho mkononi zaidi.Na hapa sizungumzii meli au boti pekee.Angalia pale Kigamboni!Au kama unadhani pale ndio kiboko cha matatizo basi jaribu kwenda kivuko cha Mto Kilombero!Nilipokuwa huko hivi karibuni nilihabarishwa kwamba kivuko kipya kilichotarajiwa kutatua kero katika eneo hilo kiliishia kusomwa na maji.Kisa?Bila shaka fisadi flani kanunua kivuko mtumba.Kama kawaida,hakuna aliyewajibika hadi leo.

Hapo feri jijini Dar nako ni ngonjera kila siku.Mara sijui kuna daraja litajengwa,mara sijui kuna nini kitafanyika.Kama kawaida yetu,tunasubiri litokee janga flani kisha ndio mabwana mipango wetu waje na mipango mipya ya kujali maisha yetu.Vivuko vingi huko nyumbani ni sawa majeneza yanayoelea.Hakuna la muhimu tulilojifunza kutokana na janga la Mv Bukoba,na sijui hata kama policy makers wetu wanakumbuka janga hilo.
Usafiri wa reli ndio balaa.Zamani za kale,ukiwa ndani ya treni ya Tazara ungeweza kujiskia kama uko kwenye treni ya nchi zilizoendelea.Siku hizo tulikuwa tunasafiri na watalii kibao.Si unajua reli ya Tazara inakatiza katika hifadhi ya Selous,kwahiyo kwa wenzetu wanaotafuta vivutio safari hiyo ilikuwa ni kuua ndege wawili kwa jiwe moja:kufikishwa waendako na kupata uhondo wa wanyama mbugani.Hivi sasa Tazara iko dhoful khal,inakaribia kukata kauli.Mara ya mwisho niliposafiri kwa Tazara,jamaa mmoja Mzambia alinieleza bayana kuwa wanasubiri tu kifo cha shirika hilo.
Huko Reli ya Kati ndio habari mbaya zaidi.Hivi inaingia akilini kweli kwa mtu anayejiita mwekezaji kuwa anapewa fedha na serikali kulipa mishahara ya watumishi?Huyu ni m-babaishaji tu.Watu pekee wanaofahamu sababu za kwanini hadi leo TRL bado iko mikononi kwa wababaishaji hao wa kidosi ni Watanzania wenzetu wachache wanaoendela kuamini kwamba ipo siku TRL itasisima na kujiendesha yenyewe.Wajuzi wa mambo wanaiona TRL kama kipofu anayetafuta sindano kwenye chumba chenye kiza totoro,huku sindano hiyo ikiwa haipo humo!

Kitu pekee kitachowakimbiza Wahindi hao ni janga.Kwanza tukubaliane kwamba kama wangekuwa hawapati faida katika huduma yao mbovu wasingeendelea kuwepo hadi leo.Si unawajua Wahindi linapokuja suala la faida?Yes,janga ndio itawakimbiza wadosi hao.Mungu aepushe janga hilo lakini likitokea la kutokea na kisha tukaishia kumlaumu Mungu,atatuadhibu vikali.Hawa wababaishaji hawajafanya matengenezo ya reli,wanasafirisha abiria kwenye mabehewa ambayo hata ng'ombe hawastahili kupanda,na ratiba zao ni za bahati nasibu.Yayumkinika kuhitimisha kuwa mazingira hayo ni sawa na a catastophy in the making.And once that happens,God forbid,hawa jamaa wataingia mitini just like wawekezaji wababsiahji wengine wanavyotukimbia baada ya kuukamua uchumi wetu.Na huwezi kuwalaumu kwani hata mwenye nyumba ambaye anaacha mboga yake jikoni pasipo kuhofia nyau,hawezi kuwalaumu paka wakikwiba mboga hiyo kukidhi njaa zao!

Hatuwezi kuuzungumzia usafiri wa anga pasipo kutaja AIR TANZANIA.Uongozi mmoja umeupisha mwingine one times too much,nembo zimebadilishwa mara lukuki,mgogoro mmoja umeupisha mwingine,lawama za wasafiri ndio usiseme!Hivi Waethiopia ni wachawi kwa namna walivyoweza kuifanya Ethiopian Airlines kuwa moja ya mashirika ya ndege ya mfano barani Afrika?Vipi kuhusu watani zetu na Kenyan Airways yao?Sisi tunashindwa nini?Hivi kuna ugumu gani wa kukodi ndege,kutoa huduma ya kuridhisha,kutumia itakayopatikana kununua ndege zaidi na kisha kutanua safari katika maeneo mbalimbali duniani?
Tatizo kubwa la Air Tanzania,or whatever its current name is,ni ufisadi.Na chanzo cha ufisadi huo ni hao wanaofanya teuzi pasipo kuzingatia rekodi.Hivi hawa viongozi wa sasa wa ATC wana sifa stahili za kulitoa shirika ICU na kulirejesha angani?Majuzi David Mattaka aliruka kimanga alipoulizwa iwapo ndege za shirika hilo zimepigwa stop kutoa huduma (kutoa non-existent huduma?) kabla ya kukiri muda mfupi baadaye kwamba habari hiyo ni ya kweli.Hivi background ya mtu huyu inaleta matumaini yoyote ya kufufuka kwa ATC?Na hapo sizungumzii maisha yake binafsi (hapa sio mahala pake).

Sababu kubwa ya nuksi,mikosi na bahati mbaya zinazoiandama sekta ya usafiri huko nyumbani ni uksefu wa uzalendo.Hilo linaanzia kwa hao wanaofanya uteuzi wa kuongoza taasisi zinazotoa huduma za usafiri wa angani,majini,barabara na reli.Pia uteuzi usiozingatia rekodi kwenye mamlaka zinazosimamia sekta hiyo ni tatizo jingine la msingi.Takriban maeneo yote yaliyoguswa katika uchambuzi huu yana Waziri,Naibu Waziri,Katibu Mkuu,Naibu Katibu Mkuu,Mkurugenzi Wizarani na Mkurugenzi shirikani,mameneja lukuki,Wenyeviti na wajumbe wa bodi ambao vikao vyao ni about posho tu na sio maendeleo ya shirika husika,na mlolongo mwingine wa watendaji.Sasa hapo inahitajika domino effect top to down.Waziri akiweka mbele uzalendo na uwajibikaji hao wote chini yake watatimiza majukumu yao.Lini tutapata Waziri ambaye ataapa kuwa lazima AIR TANZANIA itarudi hewani,TRC itafufuka kutoka katika wafu,TAZARA itapata uhai mpya,vivuko vinakuwa na maana ya vivuko,na hatua nyingine nyingi.Na isiishie kuapa tu kwani waheshimiwa wneig tu huapa lakini huishia kufisadi nchi na viapo vyao.

Uzalendo ni kuweka maslahi ya nchi mbele badala ya maslahi binafsi,Uzalendo ni kuchagua watu wenye sifa na uwezo na sio ku-recycle watendaji wenye sifa zisizostahili personally na professionally.It can be done,if wenzetu wakiamua ku-play their part....au just kusema YES WE CAN!

12 Dec 2008


Demonstrations against the killing were seen in cities across the continent with left-wing radicals and other sympathisers taking to the streets.

In Spain, 11 protesters were arrested and several police officers injured when clashes took place in Madrid and Barcelona.

In Copenhagen, 32 people were arrested when their protest in support of the Greek protests turned violent.

In neighbouring Turkey, about a dozen left-wing protesters daubed red paint over the front of the Greek consulate in Istanbul.

Around 150 people belonging to a Danish underground movement took to the streets, throwing bottles and paint bombs at buildings, police cars and officers. In Moscow and Rome, protesters threw petrol bombs at Greece's embassies.

Journalists came under attack for the first time in the riots, with a Russian news crew assaulted by a mob of about 50 youths, some of them reportedly drunk.

A correspondent and a cameraman for Russian television channel NTV were injured in the confrontation, which happened while they filmed clashes in Exarchia, a crucible of student radicalism.

In Athens, around 40 youths threw stones at riot police near university buildings in the volatile Exarchia district where 15-year-old Alexis Grigoropoulos was shot dead on Saturday.They were met with volleys of tear gas and three arrests were made, police said. Overnight, students hurling petrol bombs and stones again battled riot police in Athens, in a continuation of the worst riots to have hit Greece in more than 30 years.

There were similar clashes in the northern city of Thessaloniki, where more than 80 shops and 14 banks were damaged, with students continuing to occupy university campuses.Despite the turmoil that has rocked Greece since Grigoropoulos was killed, embattled Prime Minister Costas Karamanlis said he would fly to Brussels to attend a European Union summit. His conservative government has a parliamentary majority of just one seat.

Corruption scandals and attempts at economic reform have made Mr Karamanlis' administration deeply unpopular, but he has so far resisted calls to resign and call early elections.Epaminondas Korkoneas, 37, the police officer accused of shooting the teenager, has been charged with voluntary homicide and "illegal use" of his service weapon. He was ordered to remain in custody by an Athens magistrate.

His partner, Vassilios Saraliotis, 31, was charged with being an accomplice and will also remain in custody. The pair have been held since Sunday.Under questioning by a magistrate, Mr Korkoneas said he had acted out of self defence when a group of youths began throwing firebombs and other objects while threatening to kill him and his partner.His lawyer said the bullet which killed Grigoropoulos showed signs of having bounced off a hard surface, indicating that the boy was killed as a result of an accidental ricochet.

Greece has a history of clashes between the police and left-wing, anarchist groups.A student uprising in 1973 helped bring an end to the country's military dictatorship a year later.But the scale of this week's violence has left the country in deep shock as Greeks count the cost of the destruction.

The Athens Chamber of Commerce said 435 businesses had been hit during the violence, with 37 completely gutted, estimating the damage at GBP 44 million (50 million euros).Under the headline "Greece in self-destruct mode" the conservative daily newspaper Kathimerini said in an editorial: "This is a country with a state that is in a shambles, a police force in disarray, mediocre universities that serve as hotbeds of rage instead of knowledge and a shattered health care system. It is also on the brink of financial ruin."


11 Dec 2008


SALAAM ZA MWAKA MPYA

 

Uongozi na wafanyakazi wa

MwanaHALISI,

hata ndani ya kifungo cha

siku 90 cha gazeti hili,

tunayo furaha kukutakia

heri katika sherehe za msimu huu

zinazoambatana na

kuaga mwaka huu na kukaribisha

Mwaka Mpya.

Tumetambua na kuthamini

upendo na ujasiri wako katika kutetea

uhuru wa mawazo na uhuru wa

habari; na tunaahidi

 kuendelea kutenda kwa mujibu wa

uhuru, haki na wajibu

mara baada ya kurejea ulingoni. 

Heri ya Mwaka Mpya – 2009


Saed Kubenea

Mkurugenzi Mtendaji

Hali Halisi Publishers


Na Simon Mhina
Kada machachari wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema kauli ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusuf Makamba, kwamba mjadala juu ya mafisadi wa Akauti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ufungwe, inaashiria kuwakumbatia mafisadi. 

Mwanasiasa huyo chipukizi ambaye yupo katika kipindi cha mapambano na makada wenzake ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), kutokana na kuvuliwa uanachama kwa kupinga mradi wa Jengo Jipya la Umoja huo, alisema hatua ya Makamba kuweka mizengwe mapambano dhidi ya ufisadi inawavunja moyo watendaji wa serikali ambao wapo mstari wa mbele kushughulikia tatizo hilo. 

Nape ambaye bado ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), alisema kauli ya Makamba ni sawa na ya mtu anayeogopa kivuli chake. 

Hata hivyo, Nape katika mazungumzo na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, alisema kimsingi Makamba hana uwezo wala madaraka ya kuzuia mjadala juu ya mafisadi. 

Nape alisema ingawa hana uhusiano wowote na watu wanaopiga makelele juu ya ufisadi, lakini anafikiri wanafanya hivyo kutokana na machungu makubwa ya umasikini wanayopata Watanzania kutokana na mafisadi. 
Alihoji: ``Hivi Mzee Makamba mafisadi wakisemwa vibaya yeye anakerwa na nini? 

Hivi kinachomkera ni kipi, mafisadi waliopora fedha za wavuja jasho au wavuja jasho wanaopiga makelele juu ya mafisadi kuwaibia?`` 

Alisisitiza kuwa katika hali ya kawaida, hakuna Mtanzania ambaye atanyamazia ufisadi kutokana na uzito wake. 

Nape alihoji tena: ``Ina maana Mzee Makamba anajua idadi ya mafisadi wote nchini?`` 

Akifafanua, alisema kazi ya kuwashughulikia wahalifu hao ipo chini ya serikali na vyombo vyake vya dola na sio jambo la kisiasa. 

Wakati huo huo, Mbunge wa Moshi Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Philimon Ndesamburo, amesema chama chake `kitafunga mdomo` kuhusu ufisadi, iwapo Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, atakamatwa na kufikishwa mahakamani. 

Alisema Mkapa ni hazina kubwa ya mafisadi nchini na siku akifikishwa kortini janga hilo litakuwa limefikia tamati. 

``Chadema hatutaacha kupiga kelele juu ya ufisadi kama anavyosema Makamba hadi hapo Mkapa ambaye ni hazina ya mafisadi atakapopelekwa kortini, mambo yote yaliyofanyika yalikuwa chini ya utawala wake na alikuwa anayajua na alishiriki, lazima akamatwe,``alisema Ndesamburo. 

Mbunge huyo alisema mafisadi ndani ya CCM na serikali yake, hawajamalizika hivyo lazima waendelee kusakwa. 
Alisema asilimia 10 tu ya mafisadi wote nchini ndio wamekamatwa, lakini asilimia 90 akiwemo `baba lao` bado wapo mitaani. 

Ndesamburo alisema japokuwa Makamba amelenga kuwasaidia baadhi ya mafisadi, lakini kwa hili anatakiwa aone aibu. 

``Yaani wakati huu ambao Rais Jakaya Kikwete ameridhia watu waliokuwa mawaziri wafikishwe Mahakamani yeye anasimama kutetea ufisadi, namuomba angalau aone aibu, hata kama amelambishwa asali,`` alisema. 

Kuhusu Operesheni Sangara, Ndesamburo alisema itaendelea kwa nguvu zote licha ya Makamba kuibeza, kwa vile inalenga kuwafumbua macho Watanzania. 

Alisema operesheni hiyo si uchochezi wala nguvu ya soda, bali Makamba ametoa shutuma hizo, baada ya kushindwa kujibu hoja zinazotolewa na Chadema. 

Makamba alinukuliwa katika vyombo vya habari jana akisema kwamba mjadala wa EPA kwa sasa umefungwa kwa kuwa watuhumiwa wote wamefikishwa kortini. 

Hata hivyo, ukweli ni kwamba bado watuhumiwa wengine wakiwamo wamiliki wa Kagoda Agriculture Ltd hawajafikishwa kortini. 

CHANZO: Nipashe

Scientists believe successful tests in monkeys could prove a step towards a new type of drug to combat HIV.

The journal Nature reports infected animals survived almost twice as long after a single treatment to raise immune response to the virus.

An independent expert said multiple doses were possible, and might eliminate the virus.

Current antiretroviral drugs must be taken for life, giving HIV the opportunity to build up resistance.

Although millions of people without HIV cannot currently receive them, modern antiretroviral drugs have transformed the life expectancy of people with the infection.

However, scientists are constantly looking for alternative ways to keep the virus in check.

One option is being tested in the US on macaque monkeys infected with "simian immunodeficiency virus" - their equivalent of HIV.

One of the features of HIV is its ability to shut down or impede the body's own methods for clearing viral infections.

In particular, it manages to activate a signalling system in the body's immune cells - which then actually holds back the body's immune response.

The latest treatment works by blocking that signalling system, which has the effect of boosting the function of "killer" immune cells.

The blocking antibody was injected once into nine animals who had developed AIDS after SIV infection, all of whom lived on average almost twice as long as other monkeys who did not receive the treatment.

The treated monkeys had clear signs of more active immune systems and reduction of the amount of virus circulating in their blood, both signs that they were tackling the disease more efficiently.

While the virus was not fully controlled in any of the monkeys, the scientists said that more than one dose was possible, and that it could be used in combination with antiretroviral drugs.

Long wait

Dr Rama Amara, who led the research, said: "It is important to note that this therapy was effective without antiretroviral drugs and in monkeys with severe AIDS.

"It is critical to induce protective immune responses targeting the mutated virus for developing a successful immune therapy to control HIV infection."

Another of the researchers said that the treatment also offered potential against other chronic infectious diseases such as hepatitis C and TB.

Professor Thomas Lehner, an immunologist from King's College London, said that the findings were "very interesting", and that the drug showed potential for human treatment.

He said: "It's possible that multiple doses could eliminate the virus, although the present experiment has not shown that.

"It's my understanding that some groups are already working to test this in humans, and although the safety of the drug is a concern, I see no reason why that should be a problem.

"It's most likely that we will see it used alongside antiretroviral therapy."

Dr Ade Fakoya, from the International HIV/AIDS Alliance, said that the research was "an important avenue" to pursue, particularly as it had managed to extend the lifespan of the monkeys.

However, he said: "There's a long process of many years before this basic research is translated into actual research with the HIV virus in humans and then identifying a way to be able to actively block this on a large enough scale for it to be another useful tool in HIV treatments."

SOURCE: BBC


9 Dec 2008





Pichani juu ni dada SOPHIA RWANGA mara baada ya kukamata nondo yake ya  MSc in Geospatial Information Systems hapo University of Aberdeen.Picha zifuatazo hapo chini ni shamrashamra za mahafali hayo katika chuo hiki kilichoanzishwa mwaka 1495,the third oldest in Scotland,and the fifth oldest in the UK.




CLICK HERE FOR THE WHOLE LIST


WASHINGTON — The first sign of cracks in President-elect Barack Obama's foreign policy team of rivals emerged on Monday as his choices for secretary of state and U.S. ambassador to the United Nations visited the State Department.

As Secretary of State-pick Hillary Rodham Clinton and U.N. envoy-choice Susan Rice separately visited the diplomatic agency's headquarters in Washington's Foggy Bottom neighborhood, persons familiar with the transition said that Rice wants to install her own transition team inside the department.

Such a move by an incoming U.N. ambassador is rare, if not unprecedented, because the job is based at the United Nations in New York, where Rice already has a small transition staff, the sources familiar with the incoming administration.

The push by Rice, an early Obama supporter whose position the President-elect wants to elevate to a cabinet post, is also a signal that she intends to use her influence with the new president to play a more significant role than previous U.N. envoys, they said. The transition sources spoke on condition of anonymity to discuss internal deliberations.

Officials with Clinton's transition team declined to comment on the matter, and aides to Rice could not immediately be reached. State Department officials declined to comment on issues related to the transition.

It was not clear if Clinton and Rice _ who had strained relations during the Democratic primaries because of Rice's steadfast backing of Obama _ saw each other at the State Department as Clinton left the building shortly after Rice arrived.

During the presidential campaign, some Clinton aides saw Rice's early decision to back Obama as a betrayal because of her previous role as a high State Department official during President Bill Clinton's administration. Rice's desire to place her own team in Washington could fuel speculation that those tensions will carry into the new administration.

The officials could not say if Clinton's team had formally objected to Rice's plan, or even if Rice would be able to install a separate transition team inside the State Department. But they noted that dueling transition teams could complicate the handover by blurring lines of authority.

Technically, the job of U.N. envoy falls under the authority of the secretary of state, although some previous U.N. ambassadors have held cabinet rank. The last U.N. ambassador to be part of the president's cabinet was Richard Holbrooke, who had a famously icy relationship with then-Secretary of State Madeleine Albright during the Clinton administration.

Albright, who was President Clinton's first ambassador to the United Nations, was a mentor to Rice. But the two had a falling out when Albright, America's first female secretary of state, lined up behind Hillary Clinton for the Democratic presidential nomination and Rice backed Obama.

Hillary Clinton, meanwhile, was to dine Monday evening with the nation's current and second female secretary of state, Condoleezza Rice, at Rice's apartment in the exclusive Watergate complex. The two Rices are not related and Condoleezza Rice said on Sunday that she thought Clinton would do a great job.

Also Monday, Clinton was to meet privately with Sen. John Kerry, D-Mass. and the incoming chairman of the Senate Foreign Relations Committee, according to a Democratic official. Kerry, once a contender for the secretary of state job, will oversee Clinton's confirmation. Kerry has pledged to hold "swift and fair" confirmation hearings.


8 Dec 2008


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, ameonya kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinaweza kusambaratika ikiwa uadui uliopo ndani yake unaoendelezwa na makundi hautadhibitiwa. 

Membe alisema uadui huo unasababishwa na vitendo kama vile hujuma za kuangushana katika kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika chama hicho. 

Waziri huyo alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam. 

Membe, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya CCM, alisema ni dhana potofu kuamini kuwa uadui wa aina hiyo unasababishwa na vyama vya upinzani. 

``Maadui wapo ndani, ni wenzetu sisi wenyewe, tunakaa nao lakini wanashiriki kupanga kuangushana, majungu yamekithiri hiyo ni kielelezo cha ugonjwa wa chama kusambaratika,`` alionya Membe ambaye pia ni Katibu wa Idara ya Mambo ya Nje ya CCM. 

Membe, alisema uzoefu ywa miaka miwili aliopata tangu ateuliwe kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, umemuonyesha kuwa vyama vingi vilivyotawala kwa muda mrefu vinaweza kuondoka madarakani kutokana na udhaifu uliopo, na si nguvu ya upinzani. 

``Mara nyingi sana vyama tawala vinajiua vyenyewe, si kwa sababu ya upinzani,`` alisema Mbunge huyo wa Mtama,. 

`` Tunapotafunana, kutoaminiana, kama CCM na jumuiya zake hatushikamani, tukagawanyika, hatuwezi kuwa chama imara, tutameguka,`` alisema. 

Membe alisema machafuko yanayotokea baada ya chaguzi barani Afrika, yanachochewa na kasumba ya kutokukubali matokeo. 

Alisema hali hiyo inawafanya watu wengine kuingia msituni ama kufikia hatua ya kufanya mapinduzi ya kijeshi. 

Alitoa mfano kuwa katika kipindi cha takribani miaka 50, viongozi 32 barani Afrika, waliuawa kutokana na mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa katika nchi zao na kwamba vyama vilivyopo madarakani, vina fursa nyingi za kufanikisha kubaki katika uongozi. 

Kwa mujibu wa Membe, baadhi ya fursa hizo ni kueleweka kwa sera zake, uwepo wa viongozi bora na jumuiya imara. 

Wakati Membe akitoa tahadhari hiyo, baadhi ya wajumbe wa mkutano huo nusura wapigane hadharani, kutokana na tofauti za kuwaunga mkono wagombea katika nafasi mbalimbali za UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam. 
Hali hiyo ilijitokeza jana asubuhi, kabla ya Membe kuwasili kufungua mkutano huo. 

Taarifa za ndani zilidai kuwa kundi linalomuunga mkono mmoja wa wagombea wa uenyekiti, lilipanga njama za kuhujumu uchaguzi huo ili kutoa fursa kwa `mtu wao` kushinda. 

Miongoni mwa hujuma hizo, ni kusimamishwa kwa wajumbe zaidi ya 10, ili wasishiriki kupiga kura. 
Hata hivyo, baada ya kugundulika, baadhi ya vijana kutoka wilaya za Kinondoni, Ilala na Temeke, waligoma kuingia ukumbini. 

``Hatuingii ukumbini kama wenzetu waliosimamishwa hawatapewa vitambulisho, hatukubali kuburuzwa,`` walisikika baadhi yao wakisema. 

Hakuna kiongozi yeyote wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, aliyekuwa tayari kuzungumzia suala hilo, isipokuwa wanachama wengine wa umoja huo walisikika wakilalamikia kundi walilodai kwamba liliongozwa na mmoja wao. 

Baadaye, taarifa zilieleza kuwa vijana waliozuiwa kupiga kura, waliruhusiwa na kupewa vitambulisho.

CHANZO: Nipashe

WAKITAHARIDHISHANA WENYEWE INAKUWA SALAMA,MAANA KAZI HIYO IKIFANYWA NA WACHAMBUZI WA SIASA WANAISHIA KUNYOOSHEWA VIDOLE WAKITUHUMIWA KWA UCHOCHEZI.

JAPO MEMBE ANASTAHILI PONGEZI KWA KUJITOA MHANGA KUSEMA HAYO ALOSEMA NDANI YA CHAMA KILICHOZOWEA KUSIFIWA TU HUKU CRITICISM YA AINA YOYOTE IKITAFSIRIWA KUWA NI MITHILI YA UHAINI,ALIPASWA PIA KUONGELEA NAMNA CCM INAVYOJIMALIZA KWA KUKUMBATIA MFUMO  USIO RASMI AMBAPO ASIYE NA FEDHA HAWEZI KUSHINDA CHAGUZI YOYOTE YA CHAMA HICHO.RUSHWA IMEKITHIRI MNO NDANI YA CHAMA HICHO KIKONGWE.

MADHARA YA MUDA MFUPI (IMMEDIATE) YA RUSHWA KATIKA CHAGUZI HIZO NI NI PAMOJA NA UWEZEKANO WA KUPATA VIONGOZI WASIO NA SIFA STAHILI NA AMBAO WANAWEZA KUTOWAJIBIKA IPASAVYO KWA VILE WANAJIONA KAMA WAMENUNUA UONGOZI NA WANA HAKI YA KUFANYA MAMBO WAPENDAVYO.MADHARA YA MUDA MREFU (LONG TERM) NI REPRODUCTION YA MAFISADI.CCM NDIO CHANZO KIKUBWA CHA VIONGOZI WA NGAZI MBALIMBALI NCHINI.KWA MAANA HIYO,CHAMA HICHO KIKIZEMBEA KAMA SASA NA KUACHIA VIONGOZI WAPATIKANE KWA NJIA YA RUSHWA BASI TAIFA NALO LITAENDELEA KUPATA SUPPLY KUBWA YA VIONGOZI WALIONUNUA CHAGUZI AMBAO HAWATASHINDWA KULIFISADI TAIFA.

HABARI MBAYA NI KWAMBA HAKUNA DALILI YA CCM KUPAMBANA NA RUSHWA KATIKA CHAGUZI ZA CHAMA HICHO.NA KIKWAZO KIKUBWA CHA JITIHADA HIZO NI HIZI SIASA MUFILISI ZA MITANDAO.KWAMBA,UKIJITAHIDI KUSIMAMIA HAKI UTALIPULIWA NA WALE WANAOJUA UMEFIKAJE HAPO ULIPO.NDIO MAANA WANASIASA MAKINI HUJITAHIDI SANA KUEPUKA MAKUNDI YA KUSAIDIA USHINDI KWA VILE KUJIHUSISHA NAYO HUMGEUZA MWANASIASA HUSIKA KUWA MTUMWA WA MAKUNDI YA AINA HIYO.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.