5 Sept 2010
5.9.10
Evarist Chahali
CCM, CHADEMA, LIST OF SHAME
No comments
Pasipo kutarajia,CCM inaweza kulazimika kuuambia umma kwanini mafisadi waliotajwa kwenye List Of Shame (orodha ya mafisadi sugu iliyowekwa wazi na Chadema viwanja vya Mwembeyanga) hawajachukuliwa hatua hadi leo.Kama ambavyo chama hicho tawala kilivyokosa umakini katika kuongoza nchi ndivyo walivyokurupuka na kuwasilisha malalamiko yao NEC wakidai "wametukanwa kwa kuitwa mafisadi".Sijui ni ulevi wa madaraka au ubabaishaji tu kiasi kwamba walisahau kuwa wote waliotajwa katika List of Shame hawajathubutu kwenda mahakamani kama walivyotishia kwa kuogopa "kuwekwa uchi zaidi".Sasa wamejipeleka mahakamani wenyewe kwa kudai tuhuma hizo ni kashfa.Utamu wa stori hii uko kwenye ukweli kwamba ukidai nimekukashifu basi unawajibika kuthibitisha tuhuma nilizotoa dhidi yako sio za kweli.Kibaya zaidi kwa mafisadi waliotajwa,CHADEMA wana ushahidi mzito dhidi ya watajwa.Patamu hapo!
Hebu soma habari husika
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimewasilisha ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) majibu ya utetezi wake kuhusu malalamiko ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa kimeikashifu viongozi wake waandamizi wakati wa uzinduzi wa kampeni huku kikitoa orodha ya mafisadi kama moja ushahidi kwake.
Katika majibu hayo imo orodha ya majina 12 ya watuhumiwa wa ufisadi ambayo iliwahi kutangazwa na Chadema mwaka 2007 katika viwanja vya Mwembeyenga.
Naibu katibu wa Chadema John Mnyika jana aliwaambia waandishi wa habari kuwa wamechukua hatua hiyo ili kuthibitisha kauli zao walizozitoa kwenye uzinduzi wa kampeni zao wiki moja iliyopita katika viwanja vya Jangwani.
“Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015 ya Chadema inaeleza wazi kuwa viongozi wote ambao walishabainisha kuhusika na tuhuma za ufiasadi na ubadhilifu wa mali ya umma ambao serikali imeshindwa kuwafikisha mahakamani, watafiishwa mahakamani ndani ya siku 180, iwapo tutaingia madarakani,” alisema Mnyika.
Alisema watuhumiwa hao wakiwamo marais wastaafu ambao wataondolewa kinga yao na Bunge ili wafikishwe mahakamani.
Mnyika alifafanua kuwa hatua hiyo imelenga katika kujenga uongozi bora na kuimarisha utawala wa sheria hapa nchini.
Kuhusu kutaja orodha ya majina ya mafiasadi kwenye mkutanio huo chama hicho kilisema huo si ukiukaji wa maadili ya uchaguzi kwakuwa tuhuma hizo zipo na wahusika hadi sasa hawajachukuliwa hatua na baadhi yao wanagombea nafasi za uongozi kwenye uchaguzi wa mwaka huu.
Alisema madai yote waliyoyatoa kwenye viwanja hivyo wana ushahidi nayo na mengi ni yale ambayo tayari waliwahi kuyaweka wazi siku za nyuma.
Kwa sababu hiyo, Chadema iliitaka Nec kutupilia mbali malalmiko ya CCM kwa sababu waliwasilisha bila kusoma sheria za maadili.
CHANZO: Mwananchi
Hatimaye watajwa kwenye List of Shame wanaweza kulazimika kuuthibitishia umma kwanini wasiwe jela muda huu wanaopita huku na kule kuomba wachaguliwe tena.
Patamu hapo!!!
5.9.10
Evarist Chahali
CHILE, WEIRD NEWS
No comments
ONE of the trapped Chilean miners is dreading his rescue - his wife has discovered his secret mistress.
Yonni Barrios' wife Marta Salinas and lover Susana Valenzuela were both holding vigils for him
Marta was stunned when she heard Susana shouting his name amid a crowd of miners' loved ones.
Marta, 56, is said to be "horrified" - but is determined not to give up her man to her love rival.
She told friends: "Barrios is my husband. He loves me and I am his devoted wife. This woman has no legitimacy." But Susana said the 50-year-old miner, who she met on a training course five years ago, has been planning to leave his wife for her.
She said: "We are in love. I'll wait for him."
Barrios has been one of the heroes of the landslide drama - using his first-aid training to treat sick colleagues.
He has also vaccinated all 33 men, including himself, against flu and pneumonia. Meanwhile, the captives have been hit with a booze and tobacco ban by Nasa experts helping the rescue.
The space agency's doc James Michael Duncan said: "We need to get their nutrition up before we consider drinking." Two of the smokers have been dropped nicotine patches and gum to deal with their cravings.
But the miners - who may not be drilled out until Christmas - have started eating proper meals of 2,000 calories a day.
Their rations include yoghurt and cereal for breakfast, chicken sandwiches for lunch and jam sarnies for dinner. They each have tea and five litres of water daily.
And yesterday the stranded men had their first hot meal in a month, shredded beef and rice. But they were denied the traditional side dish of beans - to stop them getting wind.
By Guy Adams
She tells lies. She's a lousy tipper. She billed the Republican Party more than $3,000 for the underwear she bought during the last Presidential election, including dozens of Spanx girdles. Oh, and for all the cutesy charm that Sarah Palin projects in public, she's got a nasty habit of bullying staff, losing her temper with friends and family, and, when particularly upset, throwing tin cans at her husband, Todd.
Fresh from a week that seemed to cement her status as the most valuable brand in American conservatism, and saw her both receive top billing at a vast "tea party" rally in Washington, and almost single-handedly alter the direction of a Senate race in her native Alaska, Palin is on the receiving end of a brace of vintage journalistic hatchet jobs from the left and right sides of the political spectrum.
The first, a vast profile of the self-proclaimed "Mamma Grizzly," which covers 18 pages of next month's Vanity Fair, devotes more than 10,000 words to a mixture of revelation, allegation and innuendo regarding both her public and private persona, detailing what it calls her "erratic behaviour," her "pattern of lying," and what the magazine's reporter Michael Gross describes as the "sad, mouldering strangeness" of her everyday existence.
The second comes courtesy of Meghan McCain, the daughter of Palin's former running mate John, whose new book Dirty, Sexy Politics, describes the former Governor of Alaska as a "a time bomb" who is addicted to attention and whose eccentric behaviour brought "drama, stress, complications, panic, and loads of uncertainty," to the 2008 campaign trail.
Like almost everything else that involves Palin – who, despite her habit of avoiding interviews in what she calls the "lamestream media," has still not ruled out a run for the 2012 Presidency – the broadsides are receiving endless attention. As befits an increasingly polarised nation, they are sparking outrage in conservative circles and a mixture of mirth and disbelief in liberal ones. Palin takes issue with the allegation and has responded with an attack on Vanity Fair, calling into question its facts and reporting standards.
In truth, Vanity Fair's article is a curious mixture of un-sourced innuendo and minor revelation which was mostly staggering for its sheer scale. The magazine spent four months trailing the former Alaska governor on the various speaking engagements that have helped her earn $13m since quitting last year.
It alleges she is "warm and effusive in public, and angry in private," that she is paranoid and vindictive towards former friends, and it revels the details of the occasional sense-of-humour failures which inspired the headline: "The Sound and the Fury."
The piece quotes a "friend" of Palin and her husband Todd, who once witnessed a domestic dispute. "They took all the canned goods out of the pantry, then proceeded to throw them at each other," recalls the friend. "As soon as she enters her property and the door closes, even the insects in that house cringe. She has a horrible temper, but she has gotten away with it because she is a pretty woman."
During the campaign, an un-named "aide" is quoted as claiming that Palin "lashed out" at the slightest provocation, sometimes screaming at staff and throwing objects. Asked about her temper, Todd told a staffer: "You just got to let her go through it... Half the stuff that comes out of her mouth she doesn't even mean."
Vanity Fair also claims that Palin signs the autographs in her books with an autopen, requires three hairstylists and make-up artists before public appearances, and despite her principled opposition to immigration, employs an Hispanic housekeeper.
She is also a bad tipper, the article claims. During a recent stay at the Hyatt in Wichita, she gave the bellboy just $5 for seven bags, making her the "all time worst tipper" of the famous people who have stayed there. She also failed to leave money for the maids who cleaned her room.
As suggested by Levi Johnston, the estranged father of her teenage daughter Bristol's child, the magazine also claims that Palin is a lousy and only occasional angler, who exaggerates her interest in fieldsports to win support in conservative circles.
"This whole hunter thing, for Sarah? That is the biggest fallacy," a friend of the family was quoted as saying. "That woman has never hunted. She never helps with the fishing either. It's all a joke." Bristol, by the by, has made several hundred thousand dollars from media appearances, and was this week unveiled as a contestant on the popular US television programme Dancing With the Stars.
The Vanity Fair article wasn't all tittle tattle. It also explored Palin's links to extremist Christians – the "prayer warriors" she often cites in speeches – and explored her somewhat opaque finances. It revealed that Timothy Crawford, treasurer of Sarah-PAC, her political action committee, is being investigated in Ohio for alleged campaign finance misdemeanours, and has refused to respond to a subpoena issued by the state's investigators.
Meanwhile, Palin's famously scant general knowledge may be even more flaky than originally thought. When McCain aides prepared her for television interviews in 2008, they allegedly found that – besides thinking Africa was a country rather than a continent – she had never heard of Margaret Thatcher. Palin now cites Thatcher as one of her all-time heroines.
Responding yesterday, Douglas McMarlin, a spokesman for Sarah-PAC, said: "The article is a collection of lies cobbled together by an outlet without standards. As the message continues to succeed, the messenger will continue to be attacked by yellow journalists seeking to increase sales."
Miss McCain, for her part, has attempted to put a marginally more sympathetic gloss on things. Her book reveals that the Republican inner circle was "waiting for her [Palin] to explode" during the 2008 campaign. She adds: "There was a fine line between genius and insanity, they say, and choosing her as the running mate was starting to seem like a definition of that line."
SOURCE: The Independent
The policeman who found the body of MI6 codebreaker Gareth Williams said it was submerged in ‘fluid’, The Mail on Sunday has learned.An inquest heard last week that the 31-year-old spy was padlocked in a sports hold-all and left in the bath of his two-bedroom flat in Pimlico, Central London.But the disclosure that he was also covered by liquid – not thought to be blood or water – has raised fears that a substance was used to accelerate decay and complicate toxicology tests.
The revelation came as new details emerged of the highly sensitive nature of Mr Williams’s work.A source said he had the highest security clearance available to an intelligence officer and was part of a secretive ‘cell’ that created devices that can steal data from mobiles and laptops.
Now, nearly two weeks after cycling enthusiast Mr Williams was found in his flat, police are apparently no nearer to learning how or when he died.This is despite a post-mortem, a second examination and toxicology tests, the results of which might not be available for weeks.
Sources close to the inquiry say the PC who found the body described it as being in ‘fluid’ when he radioed for assistance. Detectives at the scene are understood to have used the same word in their reports.Immediately after making the discovery at the flat, the PC said: ‘This is a murder scene.’
Mr Williams, from Anglesey, North Wales, worked as a cipher and codes expert for the Government’s eavesdropping centre GCHQ in Cheltenham.He was on a year-long secondment to MI6 which was due to end days after he was found dead.Police and security sources have indicated that the explanation for his death is more likely to be found in his personal life rather than his work.
But speculation that he was the victim of a professional ‘hit’ was given credence last night after further details of his work were disclosed.‘He was involved in some very sensitive projects, known as codeword protected,’ said a security expert.‘This meant that only the people in his cell would know what he was working on, and nobody else in his organisation.
‘You are signed in to these projects and once you finish one you are signed out and you no longer have access to any data or news about what is happening in the project.’Mr Williams – a child prodigy who had a degree in maths at 17 and then a PhD in the subject – was part of a team that created devices which ‘hook’ on to mobiles and laptops. ‘It is an aggressive form of Bluetooth or similar wireless technology,’ said the security expert.
He said such devices would be used by spies on the ground to steal data from the handsets of unsuspecting terrorists, organised criminals or officers from rival intelligence agencies.‘Traditionally, there has been a separation of MI6 and GCHQ,’ said the expert. ‘MI6 has been full of the James Bond types working on the ground and GCHQ is filled with boffins with beards who are doing their scientific stuff. ‘But recently there has been a merger of these agencies’ work and Williams was at the forefront of that. This was why he was on secondment to MI6.’
He added that Mr Williams did similar work when he had stints at the National Security Agency in America.The NSA is the equivalent of GCHQ and has been leading the West’s attempts to intercept communication between Al Qaeda cells. Mr Williams worked for the Special Delivery Team, a unit set up in the NSA to create advanced bugging and intercepting devices.
‘If you just look at Williams’s CV, you know he has worked in some of the most important data-mining centres in the UK and US. His salary is no indication of his rank,’ said the expert.
It has also emerged that before his secondment to MI6, Mr Williams worked briefly for MI5, the domestic security agency. As part of that work, he was sent to Bulgaria on a secret mission.A source close to the investigation said that on August 23 police were asked to check on Mr Williams’s flat as he had not shown up for work. Just before 6pm, a PC went to the Georgian townhouse in Alderney Street, which has been converted into four flats on four floors. Mr Williams had the top one.
The PC could not get into the house so the letting agent, W. A. Ellis, was called and a woman employee arrived with keys.She hovered at Mr Williams’s door as the PC went inside. Within minutes he emerged quickly from the en suite bathroom and escorted the woman back downstairs. He then told her: ‘You stay here. This is now a murder scene.’
This weekend, staff at W. A. Ellis, of Knightsbridge, refused to confirm details.A spokeswoman said: ‘36 Alderney Street is owned by a private company, New Rodina.‘There has been speculation that it is linked to MI6 or that it is a front for MI6. Our clients do not have any links to MI6 whatsoever and are distressed by the death of Mr Williams.’
SOURCE: Daily Mail
Inaudhi na kukasirisha kuona gazeti la serikali,Habari Leo,likijipachika jukumu la kumuua kisiasa mgombea wa Chadema Dokta Wilbroad Slaa kama ambavyo imekuwa ikifanywa na magazeti ya Habari Corporation na Changamoto,na mengineyo yanayofadhiliwa na mafisadi.
Gazeti hilo limeandika kwa kirefu kuhusu anayedaiwa kuwa mume wa mwenza wa sasa wa Dkt Slaa,Josephine Mushumbusi.Ungetegemea gazeti hilo linaloendeshwa kwa fedha za walipa kodi wa Kitanzania pasipo kujali itikadi zao za kisiasa,lingetafakari kwa makini madhara ya habari hiyo.Wanajua sana wanachofanya,na yayumkinika kuamini kuwa serikali inayoongozwa na mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete,imeridhia uchapishaji wa habari za aina hiyo.
Kuna msemo wa busara unaoasa "WANAOISHI KWENYE NYUMBA ZA VIOO WASIRUSHE MAWE".Mantiki ya msemo huo ni kwamba kama una wasifu wenye mawaa ya aina moja au nyingine then si wazo jema kuwachafua watu wengine.Wengi wetu tunafahamu "ishu binafsi" za viongozi wa CCM ikiwa ni pamoja na Kikwete mwenyewe.Hazizungumzwi hadharani kwa kuwatunzia heshima viongozi hao lakini inaelekea katika kutapatapa kwao baada ya kugundua hawamwezi Dokta Slaa kwa hoja,wameamua kuhamia kwenye character assassination.
Majukwaani,Kikwete na CCM yake wanajifanya kuhubiri umuhimu wa kampeni za kistaarabu lakini pembeni wanaruhusu raslimali za umma zitumike kumchafua Dokta Slaa.Kikwete alichukua hatua za haraka pale mtandao maarufu wa Ze Utamu ulipochapisha picha zinazomhusu lakini anaruhusu gazeti la serikali litumike kumwandama Dkt Slaa.
Na kwa kuonyesha unazi,kuna mahala katika habari hiyo ambapo pasi aibu wameandika (nanukuu) "Na wakati Mahimbo akiwa njia panda akishindwa kujua hatima ya ndoa yake, Dk. Slaa, Padri msomi `amelitangazia’ taifa mbele ya mikutano ya kampeni ya chama chake cha Chadema kuwa Josephine ndiye mke wake mtarajiwa..."
Hivi Mhariri wa Habari Leo hafahamu kuwa Dkt Slaa sio Padri bali aliwahi kushika nafasi hiyo na kuiacha?
Blogu hii inamshauri Kikwete akemee mkakati huu mufilisi wa character assassination.Wengi wanafahamu kwa undani maisha ya Kikwete tangu akiwa Waziri,na wanajua vema maisha yake binafsi ndani na nje ya nchi.Asijivunie vyombo vya dola kumlinda pindi kibao kitapogeuzwa upande wake.Ni bora Dokta Slaa anayetangaza hadharani kuhusu uhusiano wake na Josephine kuliko kashfa lukuki zinazohifadhiwa kuhusu viongozi wa CCM kwa vile tu tunawaheshimu na tuna mambo muhimu zaidi ya kuzungumzia kuliko maisha binafsi ya viongozi wetu.
I repeat: Those who live in glass houses shouldn't throw stones!!!
4 Sept 2010
Dr_Slaa
TAFADHALI UKISHASOMA SAMBAZA KWA MWENZIO.BONYEZA HAPO JUU KULIA PALIPOANDIKWA "<>SHARE" KISHA CHAGUA NJIA YA KUSAMBAZA.
Tunafahamu kuwa mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete,ni mahiri sana katika kutoa ahadi.Wakati wa kampeni zake za kuwania urais kwa mara ya kwanza mwaka 2005 alitoa rundo la ahadi ambazo hata angekuwa na uwezo wa kutekeleza basi ingebidi awe rais wa milele.Kwa makusudi,badala ya kufanya marejeo ya ahadi zake lukuki za 2005,Kikwete ameendelea kutoa ahadi zaidi akijaribu kuwaghilibu Watanzania kuwa safari hii akipewa madaraka atazitekeleza.Swali la msingi ni kipi kilichomzuia kuzitekeleza katika kipindi hiki (2005-2010) na kipi kitamwezesha kutekeleza ahadi hizo katika awamu ijayo (2010-2015).
Alipokuwa kwenye kampeni zake huko mikoani aliahidi (bila aibu) kuwa tatizo la umeme sasa litakuwa historia.Last time aliposema hayo,walikuja matapeli wa Richmond.Sijui safari hii watakuja wasanii gani "kuvuna wasichopanda".Angekuwa na busara,angewaeleza Watanzania kwanini umeme umeendelea kuwa tatizo sugu nchini.Ufumbuzi wa tatizo hilo hauwezi kupatikana kwa ahadi zaidi ya zilizokwishatolewa.Kikwazo kikubwa katika upatikanaji wa ufumbuzi wa tatizo la umeme ni maslahi binafsi na ufisadi.Kuna watu wanaoombea Tanzania iwe kizani kila siku ili wauze jenereta zao.Kuna wengine wanaotaka umeme uendelee kuwa tatizo ili wapate fursa ya kutengeneza dili za kifisadi kama za IPTL,Richmond na Dowans.Na Kikwete anawajua sana watu hao lakini hana nia wa kuwachukulia hatua.Ikumbukwe kabla ya kuukwaa urais,Kikwete alishawahi kuwa Waziri wa Nishati!!!
Kadhalika,katika mwendelezo wa ahadi,Kikwete ameahidi kuleta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la maji jijini Dar es Salaam.Utadhani kwamba tatizo hilo halikuwepo wakati wa utawala wake,au limeanza majuzi.Na kama hiyo haijatosha,akaahidi tena kuwa daraja la Kigamboni litajengwa kwa vile zabuni ya kumpata mkandarasi imeshakamilika.Kwanini iwe baada ya kumchangua tena na sio alipochaguliwa 2005?Haihitaji hata elimu ya chekechea kutambua kuwa ahadi hizi ni hewa.ZITAENDELEA KUWA AHADI TU.
Ukimsikiliza kwa makini utagundua kuwa Kikwete hayuko serious na anachoongea.Pengine ni kwa vile anafahamu kuwa hahitaji kuwa serious kupata tena nafasi ya urais.Pengine ni tatixo la upeo tu.Hata hivyo,kumlaumu JK ni kumwonea kwa vile kama ilivyokuwa Desemba 2005,come Oktoba this year HATAJICHAGUA MWENYEWE KUWA RAIS BALI ATATEGEMEA KURA ZA WATANZANIA.Mwaka 2005 waliompigia kura na kumpa ushindi wa kishindo wanaweza kuwa na excuse kwa kudai walikuwa HAWAMJUI VEMA.Five years later,naamini kila Mtanzania anafahamu udhaifu wa kiongozi huyu.Kumrejesha tena Ikulu kwa miaka mingine mitano ni kosa ambalo litawagharimu sana Watanzania.
Ikumbukwe kuwa kama atarejea tena madarakani,kuna uwezekano mkubwa wa kuendesha nchi kwa mtindo wa BORA LIENDE kwa vile hiyo itakuwa awamu yake ya mwisho kwa mujibu wa Katiba.Kama ameweza kuwapuuza Watanzania katika kipindi hiki cha miaka mitano inayoisha huku akielewa fika kuwa itambidi awabembeleze tena wampigie kura mwaka huu,kwanini basi asiwapuuze zaidi kwa vile hatagombea tena urais hapo 2015?
Ni muhimu kwa Watanzania kutambua kuwa tusipoziba ufa tutajenga ukuta.Ufa wetu kwa sasa ni Kikwete na CCM yake.Tukiwarejesha tena madarakani hapo Oktoba tutakuwa tumejichimbia kaburi refu.Tuweke kando ushabiki wa vyama vya siasa na tuangalie maisha yetu na hatma ya taifa letu.Tusifanye mzaha kwa kuendekeza kauli "JINI LIKUJUALO HALIKULI LIKAKWISHA" (i.e. Bora Kikwete na CCM kwa vile tunawajua kuliko hao akina Dkt Slaa na Chadema tusiowajua).Problem is,jini hili safari hii litatumaliza na kutukomba kila kitu.Wameiba mabilioni ya EPA,wametutapeli na Richmond,Dowans,IPTL,Kiwira,Meremeta,Tangold,nk na hawajatosheka.Tukiwarejesha tena madarakani watatukomba kila kitu.
Bahati nzuri Mungu si Athumani.Ametuonea huruma na kumwibua mkombozi Dokta Wilbroad Slaa.Hii ni nafasi adimu,na ndio maana nguvu za giza zimekuwa zikimwandama.CCM wanajua bayana kuwa Dkt Slaa ana dhamira ya dhati kuwatumikia Watanzania.Hawampingi kwa vile ni mwanasiasa wa upinzani bali wanahofia atawafungua macho waliolala,na pia atawapora mtaji wao- yaani masikini wanaonunuliwa kwa pishi za mchele na sukari huku wakiahidi maisha bora "hewa".
Kama wewe si fisadi basi unapaswa kuwa na NIA,SABABU na UWEZO wa kumtosa JK na CCM yake hapo Oktoba.Maisha Bora ya Kweli (na sio ya kuzugana) Yanawezeka,Ila tu sio kwa wazushi hawa waliopo madarakani bali kupitia kwa Dokta Slaa na CHADEMA.
Kwa mujibu wa blogu ya Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua (mwanahabari mahiri Ansbert Ngurumo),Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa alionekana Ikulu siku ya Alhamisi majira ya saa 9 alasiri ambapo inaelezwa alikutana na Rais Jakaya Kikwete,mgombea wa CCM ambaye amelalamikiwa na Chadema kwa kukiuka Sheria y Gharama za Uchaguzi.Awali,Tendwa alisema kuwa angetoa "hukumu" keshokutwa (Jumatatu).
Kwa hakika,haihitaji utaalam wowote kuhusisha tukio hilo (la Tendwa kukutana na Kikwete) na pingamiz la Chadema.Na haihitaji ujuzi wa sheria kubashiri matokeo ya "hakimu kukutana faragha na mshtakiwa" siku chache kabla ya hukumu.
Wengi wetu tunafahamu Tendwa atasema nini hiyo Jumatatu.Most likely,ameshafanya maamuzi ila kinachoshughulikiwa sasa ni usanii wa lugha ya utoaji wa maamuzi hayo.Na ni katika hilo ndio maana inamlazimu awasiliane na JK ili "ajenge mazingira ya hukumu ya haki".Katika mazingira tuliyonayo ambapo Msajili wa vyama vya siasa ni kama kibaraka wa CCM,haiwezekani kabisa kiongozi huyo kutoa maamuzi ya haki yatakayokiathiri chama hicho.
Na dalili za "usanii" zimeonekana tangu Chadema wawasilishe malalamiko yao.Hivi Tendwa anaweza kuwaambia Watanzania kwanini imchukue takriban wiki nzima kutoa maamuzi kuhusu malalamiko ya Chadema?Je hiyo pekee sio dalili ya uzembe na kutowajibika ipasavyo?Awali aliwaeleza waandishi wa habari kuwa angetoa maamuzi Jumatatu lakini hakueleza kwanini itachukua muda wote huo kutoa maamuzi hayo muhimu kwa mustakabali wa demokrasia nchini mwetu.Jibu jepesi ni kwamba hana ubavu wa kutoa maamuzi kabla ya kupata ridhaa ya CCM.Na kwa vile CCM ndio watuhumiwa,ni dhahiri maamuzi ya Tendwa yataelemea kuipendelea CCM.
Nafahamu kuna wataosema "aah,sasa kelele za nini wakati maamuzi hayajatolewa?" Wana haki ya kusema hivyo lakini wanapaswa pia kutambua vema mapungufu ya Katiba yetu yanayomfanya mgombea wa chama tawala kuwa na advantage kubwa dhidi ya wagombea wengine kutokana na ukweli kwamba Katiba inampa rais nguvu kubwa mno.
Kikwete ameendelea kupuuza malalamiko ya Chadema kwa kuzidi kutoa rushwa ya ahadi katika mikutano yake ya kampeni.Sote tumemsikia akiwazuga wapigakura huko Mbagala kuhusu daraja la Kigamboni na ahadi nyingine hewa ya huduma ya uhakika kwa maji jijini Dar es Salaam.Huyu mtu hana aibu kwa sababu ahadi anazotoa sasa zinatoa picha ya mgombea anayeomba idhini ya kuingia madarakani kwa mara ya kwanza na sio aliyekuwa rais wetu kwa miaka mitano iliyopita.Kama tangu 2005 hadi leo ameshindwa kuwezesha ujenzi wa daraja hilo la Kigamboni,kwanini tumwamini kuwa ataweza katika mhula wake wa mwisho (2010-2015) hasa ikizingatiwa kuwa kipindi hicho cha pili kitatumika zaidi kwa yeye kujitengenezea mazingira ya "kustaafu kwa amani"?
Jeuri ya Kikwete inasababishwa na ufahamu kuwa Chadema,na vyama vingine vya upinzani,havina mahala pa kukimbilia pindi wasiporidhishwa na mwenendo wa kampeni za Kikwete na CCM kwa ujumla.Anafahamu kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa,Mahakama na taasisi nyingine za kusimamia uchaguzi na sheria nza nchi kwa ujumla,ziko mikononi mwa CCM.Hata hivyo,wapinzani hawapaswi kukata tamaa kwa vile nchi yetu kama masikini wa kutupwa inategemea sana misaada ya wafadhili.Japo kuwapigia magoti wafadhili kunaweza kutafsiriwa kama "kuegemea kwenye ukoloni" lakini tufanyeje kama nchi yetu inaendeshwa kiholela.Binafsi,nina matumaini makubwa kuwa nchi wafadhili zinafuatilia kwa karibu mwenendo wa kampeni za vyama vya siasa nchini na hazitasita kuchukua hatua mwafaka pale CCM itakapotumia ubabe wake kulazimisha ushindi.
Hata hivyo,wakati we keep on hoping for the best and expecting the worst,Tendwa afahamu kuwa he wont get away with this issue as easily as he might think.Blogu hii inaamini kuwa Chadema ni chama makini na chenye rekodi nzuri ya ufuatiliaji mambo.Ni katika mantiki hiyo basi blogu hii inatarajia kuwa Chadema hawatamruhusu Tendwa kufanya uhuni wa aina yoyote ile katika maamuzi yake.Ni heri uchaguzi uvurugike lakini haki ipatikane.Kutoa fursa ya sheria za nchi kupindishwa kwa namna watawala wanavyotaka ni hatari sana hasa tukizingatia ulevi wa madaraka unaowakabili viongozi wengi wa "dunia ya tatu".
Kama alivyoandika Ngurumo katika blogu yake,nami narejea kumkumbusha Tendwa kuwa HATUDANGANYIKI!
3 Sept 2010
Wenye busara zao wanatuusia kuwa pindi ukiwa unaishi kwenye nyumba ya vioo then sio wazo jema ku-entertain kurusha mawe.Mantiki ya msemo huo ni kwamba kama una ishu zenye utata katika maisha yako then sio wazo jema kuanza kushupalia ishu za watu wengi lest flani akakugeuzia kibao.
Lakini usemi huo umeonekana hauna maana kwa Katibu Mkuu wa CCM,Yusuph Makamba,ambaye kwa siku kadhaa sasa ameamua "kuvalia njuga maisha binafsi ya Dokta Wilbroad Slaa" na kuligeuza suala la ndoa ya mgombea huyo wa Chadema kuwa ajenda ya uchaguzi.
Pengine ni dharau au ujinga,Makamba alijisahau kuwa wakati anamnyooshea kidole Dkt Slaa,yeye mwenyewe (Makamba) alikuwa na doa linaloweza kabisa kumpeleka jela.Kwa mujibu wa taarifa zilizozagaa mtandaoni,Makamba anatuhumiwa kumbaka mwanafunzi wakati akiwa mwalimu mkuu wa shule moja na hatimaye kufukuzwa ualimu.
Hizi ni tuhuma nzito sana kwani licha ya kumtia doa Makamba kama mwanasiasa,ni suala linaloweza kumpeleka jela endapo victim wake atajitokeza hadharani,na kupatiwa msaada wa kisheria.Lakini tukiweka ishu za kisiasa kando,hapa kuna suala la binti asiye na hatia ambaye inadaiwa alibakwa na mtu aliyekabidhiwa dhamana ya kumpatia elimu na mwongozo katika maisha yake,mwalimu wake,lakini akaishi kubakwa.
Blogu hii inatoa ombi maalum kwa yeyote yule anayeweza kuipatia taarifa za uhakika kuhusu binti huyo anayedaiwa kubakwa na Makamba.Lengo si kumkomoa mtuhumiwa bali kuhakikisha sheria inachukua mkondo wake as well as kutoa reminder kwa watu wengine wanaotumia vibaya dhamana walizokabidhiwa,iwe mashuleni,makazini au hata katika ngazi ya familia.
Je unamfahamu binti anayedaiwa kubakwa na Makamba?Kama jibu ni ndiyo basi tafadhali sana tuwasiliane kwa barua pepe kwa anuani hii [email protected].
1 Sept 2010
31 Aug 2010
31.8.10
Evarist Chahali
URBAN PULSE
No comments
Mwezi Juni mwaka huu tuzo maarufu ya kimataifa iitwayo Ashden Awards iilitolewa kwa wahusika kadhaa duniani zikiwepo nchi za Afrika Mashariki. Tuzo hiyo hutolewa na shirika maalum lililoundwa na duka maarufu la matajiri wa Uingereza yaani Sainsbury Kutoka katika Ashden Trust Charity ambapo mlezi wake akiwa ni Prince Charles. Lengo lake ni kusaidia kurekebisha na kuboresha mazingira duniani . Tuzo ya mwaka huu ilitolewa kwa watafiti na wabunifu waliotengeneza zana za kutengeneza umeme kutokana na nguvu asilia za jua yaaani Solar Energy.
Ingawa wabunifu walitoka mataifa mbalimbali ya Marekani, Asia na Afrika washindi pia walihusisha Kenya, Uganda na Tanzania.
Umeme Jua, Bio gas( Gas Itokayo kwenye kinyesi cha ng'ombe) ni zana ambayo itawasaidia watu maskini hasa wanaotoka nchi kama yetu Bongo vijijini.
Baada Ya Mafanikio makubwa la movie ya £ovely Gamble Urban Pulse wakishirikiana na Msanii/ Mhariri Freddy Macha Wamepewa mzigo mwingine wa kutengeneza documentary ambayo itakuwa hewani tarehe 2 sept 2010 na kurushwa katika tv za hapa ukerewe na mabara mengine ya ulaya.
Hivyo basi utawala wa Urban Pulse Unawaletea trailer ya documentary hiyo hapo juu.
Baada ya uzinduzi tutawapatia kipindi chote
Asanteni sana
Urban Pulse Creative
30 Aug 2010
Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kimewasilisha rasmi pingamizi dhidi ya mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Jakaya Kikwete kwa madai ya kukiuka Sheria ya Gharama za Uchaguzi (iliyosainiwa na Kikwete kama Rais).Imedaiwa kuwa Kikwete amenongeza mishahara ya watumishi wa umma kinyume cha taratibu,na inatafsiriwa kuwa ni rushwa.
Stay tuned!
Kwa mujibu wa mwana-Jamii Forums
30.8.10
Evarist Chahali
USALAMA WA TAIFA
1 comment
Nimekutana na habari hii huko Jamii Forums,nami naiwasilisha kama ilivyo:
If it's true,hivi hii sio local version yetu ya Watergate?
Dola kuishughulikia CHADEMA
DAWATI LA HATUDANGANYIKI limepokea taarifa za kuaminika kutoka vyanzo vyake kuwa kuwa mara tu baada ya mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CHADEMA, siku ya Jumamosi tarehe 28 Agosti 2010 wakuu wa Idara ya intelejensia walikutana na timu ya Kampeni ya CCM kwa ajili ya kutoa mlisho nyuma, na kupanga mikakati ya kuikabili CHADEMA, na yafuatayo yalijiri:-
a)Idara ililazimika kutolea ufafanuzi sababu zilizopelekea shauri wake wa kutaka matangazo ya TBC ya mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za CHADEMA kurejeshwa mara moja baada ya kukatizwa. Walieleza kuwa ilitokana na maelfu ya wananchi waliohudhuruia mkutano huo kuwa wa kwanza kugundua kukatishwa kwa matangazo hayo na kuamua wenyewe, bila ya kushawishiwa na kiongozi yeyote kuchukua hatua kali sana dhidi ya TBC. Viongozi wa CHADEMA walistukia tuu mkutano ukitaka kuvurugika kwa wananchi kudai vikali kurejeshwa kwa matangazo hayo. Ilielezwa kuwa kuvurugika kwa mkutano ikwa sababu ya kukatishwa kwa matangazo ya chombo cha umaa kama TBC iimeelezwa kuwa ingekuwa ni aibu kubwa kwa Serikali na TBC.
b)Idara ilitoa taarifa kuwa licha ya umati wa watu waliohudhuria kutofikia ule wa mkutano wa uzinduzi wa CCM, lakini kwa kuwa umati huo kila mtu alijinyanyua kutoka atokako na kuja Jangwani kwa ajili ya CHADEMA tofauti na maandalizi makubwa ya usafiri, fedha, burudani za kila aina, viburudisho n.k yaliyofanywa na CCM kuwafikisha watu kwa maelfu Jangwani. Hizo ni dalili mabaya na ni tishio kubwa kwa CCM. Na ikaamuliwa kuwa iandaliwe mikakati ya kuwakatisha tamma wananchi wenye mapenzi na CHADEMA.
Mkakati :- Ilamuliwa kuwa upandikizwe mgogoro baina ya viongozi wa CHADEMA na mgombea wake Dr W. Slaa; na kuwachonganisha na wapiga debe wao akina Marando, Shibuda, Mpendazoe n.k kwa nia ya kuwakatisha tamaa wenye mapenzi na CHADEMA na wote wanaotarajia kuwapigia kura wagombea wa CHADEMA.
Iliamualiwa kwa kuwa wananchi wanampenda sana Dr W Slaa, zisambazwe habari kuwa aelewani na Mwenyekiti wake Ndg Freeman Mbowe kwa sababu Dr Slaa sio kutoka kabila la wachagga. Ilikubaliwa kuwa taarifa hizo zianze kusambazwa wiki inayoanzia Jumatatu ya tarehe 30 Agosti 2010. Na tathmini ifanyike kujua mafanikio yake wakati zinatungwa mbinu mpya.
Iliamuliwa kuwa magazeti ya New Habari Corporation ikiwemo Mtanzania, Rai n.k yaanze kutumika kwa kazi hiyo wakati waandishi zaidi wa kufanya kzai hiyo wakitafutwa.
Ili wananchi wenye mapenzi mema na CHADEMA waweze kusadiki taarifa zitakazosambazwa ilikubaliwa kuwa magazeti yatakayotumika yaanze kwanza kwa kipindi kifupi kuandika habari njema kuhusu CHADEMA na wagombea wake; na baada ya mashabiki wake kuyaamini magazeti na vyombo hivyo vya habari ndipo kazi ya kuisamabaratisha CHADEMA ianze rasmi.
Ili kutekeleza mipango hiyo waandishi wa gazeti la Mtanzania walipatiwa maelekezo ya kurekebisha kichwa cha habari na maudhui ya habari za uzinduzi wa CHADEMA zilizochapishwa tarehe 29/8/2010, kwa lengo hilo.
Vyombo vya habari vya Serikali ya ikiwemo magazeti ya Daily News na Habari Leo na TBC na redio za TBC vilielekezwa kuanza mara moja kazi ya kuipamba CHADEMA kama chama na watu wa fujo mbele ya jamii makakati amabo unadaiwa kufanikiwa sana kuisambaratisha CUF mwaka 2005, wakati Mkuu wa chombo kimoja cha dola alipodai siku moja kabla ya upigaji kura wamekamata shehena ya majambia yenye rangi za bendera za CUF
c)Pingamzi la CHADEMA dhidi ya Jakaya Kikwete mkutano ulikubaliana kuwa kuaniza sasa idara ihakikishe kuwa inamgeuzia kibao Dr Slaa na kusambaza habari kwa wafanyakazi na umma kuwa DR Slaa anapinga wafanyakazi kuongezwa mishahara ndio maana CHADEMA inamuwekea pingamizi mgombe wa CCM Jakaya Kikwete kwa kitendo cha kuwaongezea mishahara watumishi wa umma katika kipindi hiki cha kampeni.
Dawati litaendelea kuwahabarisha!!!!!!!
If it's true,hivi hii sio local version yetu ya Watergate?
30.8.10
Evarist Chahali
NIGERIAN SCAMS
1 comment
From Lt. Gen. Peter Olu
From:
NATIONAL SECURITY ADVISER
Add to Contacts
OFFICE OF THE NATIONAL SECURITY ADVISER
TO THE PRESIDENT FEDERAL REPUBLIC OF NIGERIA
GET BACK TO ME AT YOUR EARLIEST CONVENIENCE
Dear Sir/Madam,
I am Lt. Gen. Peter Olu, National Security Adviser to the New President Dr Goodluck Jonathan Federal Republic of Nigeria. I decided to contact you because of the prevailing security report reaching my office and the intense nature of policy in Nigeria. This is to inform you about our plan to send your fund to you via cash delivery. This system will be easier for you and for us. We are going to send your contract part payment of US4.1 Million to you via diplomatic courier service.
Note: The money is coming on two security proof boxes. The boxes are sealed with synthetic nylon seal and padded with machine. This fund was brought to us from America; it was meant for our Local AFEM market. But since the money was not used, I will use my position as the National Security Adviser to the President to send this fund to you.
The boxes are coming with a Diplomatic agent who will accompany the boxes to your house address. All you need to do now is to send to me
Your full name
Your house address
Your age
Your marital statue
Your identity such as, international passport or driver license
Your contact phone and fax numbers,
The Diplomatic attached will travel with it. He will call you immediately he arrives your airport. I hope you understand me.
I will let you know by the special grace of God when the boxes are airlifted.
Note: The diplomatic does not know the original contents of the boxes. What l declared to them as the contents is Sensitive Photographic Film Material. I did not declare money to them please. If they call you and ask you the contents please tell them the same thing OK, I will let you know how far I have gone with the arrangement. I will secure the Diplomatic immunity clearance certificate that will be tagged on the boxes to make it stand as a diplomatic consignment.
This clearance will make it pass every custom checkpoint all over the world without hitch. Confirm the receipt of this message and send the requirements to me immediately you receive this message. If you need more information about this, I will give you the details how to contact the diplomat for more information on how to carry out the plan.
I need you response because the boxes are schedule to leave as soon as we hear from you. Reply me immediately you receive this message via Email ([email protected]) Call me on my direct phone: (+234-8063619571) or Fax: (234-8029402741)
Best Regards,
Lt. Gen. Peter Olu
28 Aug 2010
28.8.10
Evarist Chahali
CHADEMA
No comments
Bonyeza HAPA kupata up-to-the-minute updates za uzinduzi wa kampeni za Chadema katika viwanja vya Jangwani.
Subscribe to:
Posts (Atom)



















.jpg)