10 Mar 2012


FRIDAY, MARCH 9, 2012

Mamlaka ya Urais yawezeshe uwajibikaji kumaliza mgogoro wa Serikali na Madaktari


Jana tarehe 8 Machi 2012 asubuhi nilitoa tamko kwa niaba ya CHADEMA la kutaka kauli ya haraka ya Rais Jakaya Kikwete ya kutengua uteuzi wa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hadji Mponda na Naibu Waziri wa wizara husika Dk. Lucy Nkya kutokana na udhaifu wao mkubwa wa kiongozi waliouonyesha katika kushughulikia mgogoro wa madaktari ambao umedumu kwa muda wa takribani miezi miwili. 

Nilieleza kusitikitishwa na ukweli kwamba Rais Kikwete toka mgogoro utokee hajatumia ipasavyo mamlaka yake ya kikatiba kwa mujibu wa ibara ya 34 na 35 na tarehe 5 Februari 2012 aliahidi kwamba atazungumzia kwa kina suala la mgomo wa madaktari lakini badala yake akalizungumza kwa ufupi tarehe 29 Februari 2012 katika hotuba yake kwa taifa bila kuchukua hatua za msingi hali inayoashiria ombwe la uongozi. 

Nilieleza kuwa iwapo Rais Kikwete haitatoa kauli viongozi wakuu wa CHADEMA wataeleza hatua za ziada ambazo chama kitachukua kuiwajibisha serikali. Jioni Serikali ilieleza kuwa leo Rais angezungumza na wazee wa Dar es salaam, na leo imetolewa taarifa kuwa atazungumza nao kesho.

Jana usiku na leo asubuhi masuala kadhaa yameendelea kuhusu mgogoro huu, mosi; hukumu ya mahakama ya kazi, pili; uamuzi wa serikali na wadau wake kufanya propaganda dhidi ya madaktari tatu; uamuzi wa serikali kufanya mawasiliano na uongozi wa madaktari.

Mkakati wa kufanya propaganda hautaisaidia Serikali badala yake iwekeze katika mawasiliano na uongozi wa madaktari kabla ya Rais kuzungumza ili Rais atoe kauli baada ya kuchukua hatua za msingi ikiwemo za kuwezesha uwajibikaji wa viongozi waliotajwa na pia kuanza kushughulikia madai ya madaktari na yale yanayohitaji kuingizwa kwenye bajeti kuwe na makubaliano ya utekelezaji. 

Izingatiwe kwamba matatizo ya Wizara ya Afya pamoja na udhaifu wa kiutendaji yalichangiwa pia na ufinyu wa bajeti, na bajeti husika iliandaliwa na serikali na kupitia kwenye baraza la mawaziri ambalo Rais ni mwenyekiti wake kabla ya kuletwa bungeni na wengine tuliipinga tukitaka fedha zitoke kwenye matumizi mengine ya anasa na kuelekezwa kwenye huduma muhimu za kijamii. 

Pia; kutokana na matatizo katika serikali kwenye wizara mbalimbali yenye madhara ya kiuchumi, kisiasa na kijamii katika taifa tunasisitiza umuhimu wa Rais Kikwete kulivunja baraza la mawaziri ili kufanya mabadiliko ya kimsingi ya kuongeza uwajibikaji kama ilivyoazimiwa pia na kamati kuu ya CHADEMA katika mkutano wake wa tarehe 3 na 4 Machi 2012.

Tarehe 7 na 8 Machi 2012 Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa mara nyingine tena alitoa taarifa kinyume na kauli za awali za tarehe 9 Februari 2012 ambazo badala ya kushughulikia vyanzo vya mgogoro vimeendeleza mgogoro na kusababisha mgomo mwingine wa madaktari wenye athari kubwa kwa wananchi.

Ndio maana nikatoa kauli ya kumtaka Waziri Mkuu kuweka wazi kwa umma taarifa ya uchunguzi uliofanywa na serikali kuhusu tuhuma dhidi ya viongozi wakuu na watendaji waandamizi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, na kushughulikia madai ya msingi ya madaktari. 

Aidha, pamoja na kuunganisha nguvu za pamoja kuhakikisha mgomo unakwisha ili kuepusha athari zaidi kwa umma, ni muhimu hatimaye tathmini huru ikafanyika kuhusu matokeo ya mgogoro na mgomo toka ulipoanza mpaka sasa ikiwemo kueleza wazi idadi ya vifo vilivyotokea na madhara yaliyojitokeza katika hospitali za umma tofauti na kauli potofu iliyotolewa bungeni tarehe 3 Februari 2012 na Waziri husika.

Rais Kikwete alipaswa kabisa kuchukua hatua kuiongoza serikali kufanya maamuzi ya msingi mara baada ya matokeo ya kikao kati ya ujumbe wa Serikali ulioongozwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda na wanataaluma wa kada ya afya sanjari na mkutano kati ya madaktari na wawakilishi wa kada nyingine za sekta ya afya katika utumishi wa umma vilivyofanyika tarehe 9 Februari 2012; kwa kuzingatia pia ushauri tuliotoa tarehe 10 Februari 2012.

Kwa upande mwingine, jana nilirudia kutoa mwito tuliotoa tarehe 30 Januari 2012 kwa TUGHE, MAT na kamati ya muda ya madaktari kuendelea kutoa ushirikiano unaostahili kwa chama, kambi rasmi ya upinzani na wadau wengine ili kuweza kuunganisha nguvu ya pamoja katika kushughulikia madai ya msingi ya madaktari yenye kuathiri sekta ya afya nchini na maisha ya wananchi kwa ujumla. 

Naendelea kuwashukuru wanaharakati kwa kuunganisha nguvu katika kutaka uwajibikaji wa viongozi wa serikali katika kushughulikia mgogoro na madaktari na kinaitaka Serikali kuacha vitisho na matumizi makubwa ya vyombo vya dola kwa madaktari na makundi mengine katika jamii yanapotumia uhuru wa kikatiba kwa kukusanyika, kujadiliana na kuhoji kuhusu uwajibikaji wa serikali na viongozi wake kwa kuzingatia ibara za 8, 18 na 20 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Rais Kikwete anapaswa baada ya mawasiliano yanayoendelea kutoa hotuba yenye kuleta matumaini badala ya kurudia tena maelezo yasiyoridhika kama yale yaliyotolewa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda tarehe 9 Februari 2012 na 7 na 8 Machi 2012 kuhusu namna ambavyo imeshughulikia mgogoro huu na madai ya madaktari, watumishi wengine wa umma katika sekta ya afya nchini pamoja na uboreshaji wa huduma katika hospitali, zahanati na vituo vya afya nchini.

Narudia kutoa rai kwa wananchi kuendelea kuunga mkono madai ya msingi ya madaktari ili kuhakikisha kwamba hospitali za umma nchini zinakuwa mahali salama kwenye huduma bora za kulinda maisha ya wananchi hususan wasio na uwezo wa kudumu gharama za matibabu katika hospitali binafsi za ndani na nje ya nchi. 

Pamoja na madai ya maslahi ya madaktari ambayo ni kwa maslahi ya umma, madaktari wanataka pia serikali ichukue hatua za kuboresha huduma za afya. Serikali inaingia gharama kubwa kupeleka baadhi ya watanzania wengi wao wakiwa viongozi kwenda kutibiwa nje ya nchi huduma katika hospitali za umma zinazidi kuzorota kutokana na ukosefu wa madawa, vifaa tiba na wataalamu wa kutosha katika hospitali za umma. 

Aidha, serikali inashindwa kuipa kipaumbele sekta ya afya kwa kisingizio cha kutokuwa na uwezo wakati ambapo inafanya matumizi mengine ya anasa kwa kiwango kikubwa kama ilivyokuwa katika maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru. Serikali inachelewa kushughulikia madai ya posho za madaktari kama nyongeza ya posho ya kulala kazini (on call allowance) na posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi (risk allowance) wakati huo huo serikali hiyo hiyo inazungumzia nyongeza ya fedha katika matumizi mengine ya serikali yasiyokuwa ya lazima. Serikali ishughulikie vyanzo vya migogoro ya kijamii badala ya matokeo.

MTEMBELEE MHESHIMIWA MNYIKA KATIKA BLOGU YAKE INAYOPATIKANA http://mnyika.blogspoti.com.PIA UNAWEZA KUMFUATA TWITTER www.twitter.com/jjmnyika NA UKURASA WAKE WA FACEBOOK NI http://www.facebook.com/pages/John-Mnyika/113913842009362




BBC News presenter Simon McCoy 'caught sleeping at his desk live on air'

BBC breakfast news anchor Simon McCoy was apparently caught out living the dream today, as he slept at his desk while at work, prompting a few red faces at the BBC and some light-hearted jibes from co-host Martine Croxall.

Simon McCoy BBC News sleeps live on air Simon's co-anchor Martine looked uncomfortable as he apparently napped live on air (Picture: BBC)
McCoy, who has been a BBC News anchor since 2004, was seen napping on his desk during a live bulletin on the rolling digital news channel just before 8.30am.
The 50-year-old presenter was caught resting his head on his desk during the broadcast, while Martine Croxall appeared to look slightly uncomfortable in her upright position next to him.
After realising cameras were trained on him and that he was live on air, the presenter quickly sat up, but he appeared tired and bleary-eyed as he did so. 
As viewers flocked to social media sites to share their thoughts on the amusing incident, Simon insisted that he hadn't been sleeping; merely joking around in the studio.
Simon McCoy BBC News sleeps live on air Martine and Simon are regular co-hosts on the morning programme on BBC News 24 (Picture: BBC)
He tweeted: 'It was a long desk head-banging that wasn't meant to be picked up in the BBC1 opt!!'
'I was not asleep! Had just been told The Queen wanted me to cover her NEXT visit...' he later wrote, apparently exasperated at the attention his 'nap' was receiving.
Simon McCoy BBC News sleeps live on air As he realised he had been caught out, McCoy quickly assumed a more vertical position (Picture: BBC)
But McCoy's co-host Martine later appeared to confirm that he had indeed been catching 40 winks, tweeting: 'Intravenous cafeine now being administered to @simonmccoy'.
She added: 'There's no such thing as an incident-free shift with @simonmccoy, have you noticed?! x'
And in a stunning act of clairvoyance, Martine had predicted yesterday that there would be some sort of incident during her shift with Simon the following day.
She tweeted: '@simonmccoy is only ever a step away from mischief.' 



SOURCE: Metro

9 Mar 2012

Wednesday, 07 March 2012 19:31

Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa
ATHIBITISHA YUKO HOSPITALINI, ASEMA ASINGEPENDA KUELEZEA KWA UNDANI KUHUSU AFYA YAKE  
Ramadhan Semtawa
UTATA umegubika afya ya Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa baada ya taarifa mbalimbali kueleza kuwa yuko hospitalini nchini Ujerumani kwa matibabu.Takriban juma moja sasa kumekuwa na taarifa mbalimbali zikizungumzia afya ya Lowassa lakini hakukuwa na taarifa rasmi kutoka chanzo chochote kati ya Serikali, familia yake au Bunge kuzungumzia afya ya Mbunge huyo wa Monduli.

Jana, Lowassa akizungumza na mwandishi wetu kwa simu alisema kwamba yuko hospitali, bila kufafanua kuwa ni nje au ndani ya nchi, wala kueleza kinachomsibu.

Mahojiano hayo kati ya Lowassa na mwandishi wetu yalikuwa kama ifuatavyo:

Swali: Asalaam alaykum Mheshimiwa Lowassa.
Jibu: Waalaykum Salaam.

Swali: Mimi naitwa... (jina la mwandishi) kutoka gazeti la Mwananchi. Kwanza pole kwa matatizo ya kiafya yanayokusumbua.
Jibu: Ahsante.

Swali: Nimekupigia pamoja na kukupa pole, nilitaka kujua unaendeleaje na matibabu?
Jibu: Niko hospitalini kwa sasa naomba niache mambo mengine tutaongea baadaye.

Swali: Lakini, ni matibabu gani hasa unayopata?
Jibu: ... (akimtaja mwandishi) naomba niache niko hospitalini sasa hivi mambo mengine tuongee baadaye.

Lowassa alitoa majibu hayo majira ya saa nane mchana na alipopigiwa tena saa 10.20 jioni, alijibu kama ifuatavyo:

Swali: Naam, Mheshimiwa Lowassa nimekupigia tena mimi... (mwandishi akajitambulisha).
Jibu: ... Unataka nikuambie nini tena? Nilishakwambia niko hospitalini niache!

Swali: Sawa, natambua uko hospitalini, lakini wewe ni kiongozi ambaye umewahi kuwa Waziri Mkuu, hivyo Watanzania wangependa kujua maendeleo ya afya yako kutokana na utata ulioibuka na kama je, umelazwa hapo hospitalini au uko katika matibabu ya kawaida?
Jibu Niache, ninachokwambia niko hospitalini sasa unataka nini tena? Nisingependa kuzungumzia afya yangu kwa undani.

Bunge

Akizungumzia suala hilo juzi, Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashillilah alisema ofisi hiyo haijapata maombi rasmi ya mbunge huyo kwenda nje kwa ajili ya matibabu.

Dk Kashillilah alisema kwa utaratibu, Ofisi ya Bunge inashirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa ajili ya kuwapeleka wabunge wanaoumwa nje ya nchi baada ya kupata rufaa ambayo inatokana na ushauri wa kitaalamu wa madaktari wa ndani.

Alisema hadi juzi, hakuwa akijua aliko Lowassa na kama ana matatizo ya kiafya kama inavyozungumzwa au la: “Mimi ndiyo Ofisi ya Bunge na ndiyo nakwambia hatujapata maombi ya kutaka mheshimiwa Lowassa apelekwe nje ya nchi.”

Mtendaji huyo mkuu wa Bunge alisema wapo baadhi ya wabunge ambao huwa wanakwenda nje kwa vipindi maalumu kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa kawaida wa afya baada ya matibabu lakini, katika orodha hiyo Lowassa hayumo.

“Tunao utaratibu wa baadhi ya waheshimiwa wabunge kwenda nje kwa mujibu wa ratiba zao kwa ajili ya kufanyiwa uangalizi wa kawaida wa afya zao. Lakini, hadi sasa (juzi) katika orodha hiyo mheshimiwa Lowassa hayumo,” alisema Dk Kashillilah.

Hata hivyo, kwa mujibu wa nafasi yake ya utumishi serikalini aliyokuwa nayo, Lowassa anaweza kupata matibabu nje ya nchi kwa kupitia utaratibu wa Serikali bila ya kuhusisha Bunge.

Juhudi za kupata Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda au Naibu wake, Dk Lucy Nkya zilishindikana kutokana na simu zao kufungwa na kutopatikana ofisini.

CHANZO: Mwananchi

8 Mar 2012


Tanzania nchi ya vituko na viporo vya utatuzi wa kero

Kitendawili bila majibu kwa mgomo wa madaktari
Arumeru wanausalama walinda ‘usalama wa rushwa’
MIONGONI mwa habari zilizogusa hisia za wengi wiki iliyopita ni tishio la madaktari kuwa ifikapo Jumatano hii (Machi 7)  watarejea kwenye mgomo iwapo viongozi wawili wa Wizara ya Afya, Waziri Dk. Haji Mponda na Naibu wake, Dk. Lucy Nkya hawatakuwa wameng’olewa kwenye nyadhifa hizo.
Ni vigumu kuelewa kwa nini Rais Jakaya Kikwete anaendelea kuwalinda Mponda na Nkya, lakini uzoefu unapaswa kutukumbusha kuwa ni nadra kwa watawala wetu kusikia vilio vya watawaliwa, isipokuwa nyakati za uchaguzi.
Kimsingi, kilichofanywa na Serikali hapo awali kuwashawishi madaktari kusitisha mgomo wao na kurejea kazini ni sawa na kuahirisha tatizo pasipo kujihangaisha namna ya kulikabili litaporejea tena.
Msimamo wa madaktari hao ulikuwa wazi kwa Serikali, ambapo pamoja na kutaka watimiziwe madai ya kutaka kuboreshewa maslahi na mazingira yao ya kazi, walitamka bayana viongozi wanne wa Wizara ya Afya waondolewe madarakani.
Lakini kabla ya Serikali kuamua kukaa chini na madaktari, ilishajichanganya kwa kujaribu kutumia ubabe kama njia ya kumaliza mgomo. Awali, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alitoa tishio kwamba daktari atakayegoma kurejea kazini, angekuwa amejifukuzisha kazi huku ikiahidiwa kwamba madaktari kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wangeziba pengo kubwa lililojitokeza.
Pengine kwa kutambua kuwa katika siku za hivi karibuni kauli za Pinda zimekuwa kama za mtu anayesema kwa minajili ya kusikia tu sauti yake mwenyewe, madaktari walipuuza tishio hilo na nguvu kazi iliyoahidiwa kutoka jeshini ikiishia kuwa kituko kama si utani mbaya (bad joke).
Baada ya kugundua kuwa ‘imeshikwa pabaya’ ndipo Serikali kupitia Pinda ikajirudi na kuwaahidi madaktari kuwa ingetimiza matakwa yao. Na siku chache baadaye, ikatangaza kuwasimamisha kazi Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Blandina Nyoni na Mganga Mkuu wa Serikali, Deo Mtasiwa.
Japo uamuzi huo wa kuwasimamisha kazi Nyoni na Mtasiwa ulipokewa na kueleweka vizuri, bado inaniwia vigumu kuelewa kwa nini Mponda na Nkya walisalimika na wanaendelea kukumbatiwa hadi leo.
Kwa kiasi kikubwa, kusita kwa Serikali kuchukua hatua dhidi ya Waziri huyo na Naibu wake ndio kumesababisha kurejea tena kwa sakata hili la mgomo. Lakini kingine kinachokera zaidi ni ukweli kwamba japo Nyoni na Mutasiwa wamesimamishwa kazi, hakuna taarifa zozote kutoka serikalini kuhusu hatua zaidi dhidi yao.
Yayumkinika kuhisi inasubiriwa ‘upepo utulie’ kabla watendaji hao hawajapangiwa madaraka mengine. Ndio Tanzania yetu ilivyo.
Kilio cha madaktari na tishio lao la mgomo ni dalili tu ya tatizo kubwa linalohitaji dhamira ya dhati ya Serikali kulishughulikia. Asilimia kubwa ya watumishi wa umma wanakabiliwa na matatizo kama hayo yanayowasibu madaktari, kubwa zaidi likiwa maslahi na mazingira ya kazi duni.
Lakini kilio cha watumishi wa umma ni mithili ya ‘tone kwenye bahari’ ukilinganisha na hali ngumu ya maisha inayowakabili asilimia kubwa ya Watanzania. Cha kusikitisha zaidi ni kukosekana kwa dhamira ya dhati kwa upande wa Serikali kuboresha maisha ya Mtanzania, awe mtumishi wa umma au sekta binafsi, aliyejiajiri au mkulima, na kila kundi katika jamii.
Mara zote nimekuwa nikiamini kuwa kikwazo kikubwa cha maendeleo yetu si kukosekana kwa sera nzuri na mipango mizuri, au mawazo mazuri. Kinachotukwaza zaidi ni kutokuwapo nia ya kutekeleza sera, mipango au mawazo hayo, sambamba na usimamizi mbovu pale tunapojaribu kuitekeleza.
Rais Kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005 sio tu aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania bali pia alibainisha kuwa suala hilo (la maisha bora) linawezekana. Na hakuwa anatania (angalau kwenye ukweli wa mambo) kuwa maisha bora yanawezekana katika nchi iliyojaliwa kila aina ya utajiri japo tunaendelea kuwa masikini wa kutupa huku tukiwa nchi ya tatu kwa kupokea misaada mingi zaidi duniani (mbele ya Iraq na Afghanistan).
Rais Kikwete hajajihangaisha kupima ufanisi wa dhamira yake ya kuwaletea maisha bora Watanzania, lakini ninachokumbuka kuna wakati kauli mbiu hiyo ya maisha bora kwa kila Mtanzania ‘ilikarabatiwa’ na kuongezwa vikorombwezo kama ‘maisha bora hayawezi kushuka kutoka mbinguni.’ Unaweza kujiuliza kwa nini kaulimbiu hiyo ilipotolewa mara ya kwanza haikuwa ‘maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana lakini hayawezi kushuka kutoka mbinguni.’
Kwa kutathmini dhamira hiyo ya Kikwete tangu aitangaze hadi leo hii, yayumkinika kuhitimisha kuwa ilikuwa ni porojo tu za kutaka kura za Watanzania. Ninasema hivyo kwa sababu ni rahisi kupata idadi ya safari za Rais kwenda nje ya nchi kuliko kuwa na takwimu sahihi za uboreshwaji wa maisha ya Mtanzania. Hapa ninazungumzia takwimu halisi za mtaani na sio kauli za kisiasa za akina (Waziri wa Fedha) Mustafa Mkulo kuwa uchumi unakua.
Hivi kuna ugumu gani kujifunza kutoka kwa majirani zetu wa Rwanda, taifa lililojitutumua na kutoka kwenye mauaji ya kimbari na kuibuka kuwa moja ya mifano adimu ya mafanikio ya kiuchumi barani Afrika.
Nchi hiyo ambayo sasa inafananishwa na economic tigers wa Kusini Mashariki mwa Asia (kwa mfano Malaysia) imepiga hatua kubwa katika kupunguza umasikini huku uchumi wake ukikua kwa kasi.
Rwanda imediriki kufika ilipo sasa kwa sababu Rais Paul Kagame yupo makini, sio kufanya safari za kuzunguka dunia, bali kuhakikisha kuwa nchi yake inapiga hatua kimaendeleo. Sidhani kama Wanyarwanda watakuwa na tatizo iwapo Kagame ataamua ‘kushindana na Kikwete kufanya safari za nje ya nchi’ kwa sababu uchumi unaokua nchini humo unaweza kumudu gharama kubwa zinazotokana na safari za aina hiyo.
Kwa bahati mbaya, shinikizo la madaktari kuitaka serikali iboreshe maslahi na mazingira yao ya kazi linakuja wakati tunaelekezea kwenye msimu mwingine wa kuteketeza fedha katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki.
Na dalili za awali za uteketezaji fedha za umma ni taarifa za uwepo wa makachero wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na wenzao wa Idara ya Usalama wa Taifa kwenye mchakato wa CCM kupata mgombea wake kwenye uchaguzi huo.
Licha ya ukweli kwamba taasisi hizo sio za kisiasa na hivyo hazikupaswa kuwepo kwenye shughuli hiyo ya ndani ya CCM, uwepo wao ambao umegharimiwa na fedha za umma haukuweza kuzuia utoaji na upokeaji wa rushwa.
Siwezi kuilaumu sana TAKUKURU kwa vile kuwepo au kutokuwepo kwake hakuna faida kwa Mtanzania zaidi ya kumwongezea hasira na mzigo wa kugharamia uendeshaji wa taasisi hiyo butu. Lakini nina swali au changamoto kwa Idara ya Usalama Taifa; hivi haioni kama inajidhalilisha inapotuma maofisa wake kwenda kwenye chaguzi za ndani za CCM, kisha rushwa ikamwagwa kana kwamba ni halali, na hatimaye maofisa hao wakarejea ofisini kuripoti tu jinsi rushwa ilivyotawala?
Zamani, sio tu kuwa uwepo wa maofisa Usalama wa Taifa ulitosha kuwatisha wahalifu (kwa mfano hao wanaomwaga rushwa kwenye michakato ya uchaguzi ya CCM) lakini ilikuwa sio rahisi kubaini uwepo wao (na hivyo kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi).
Lakini siku hizi imekuwa kama desturi kusikia wakijazana kwenye vinyang’anyiro vya kupata wagombea wa CCM lakini wakiishia kuwa watazamaji tu kwani rushwa imeendelea kuwa turufu muhimu kwa wanachama wa chama hicho tawala kumudu kupata kura za kutosha.
Fedha zinazotumika kugharimia uwepo wa wanausalama hawa zingeweza kuelekezwa kwenye maeneo mengine muhimu, na hilo licha ya kupunguza migongano kati ya serikali na watumishi wake na wananchi wengine kwa ujumla, ingesaidia pia kuepusha aibu ya wanausalama hao kuwa waangalizi wa namna rushwa inavyofanikisha ushindi wa wanaowania kuteuliwa.
Tutashuhudia katika kampeni za uchaguzi huo mdogo wa Arumeru Mashariki jinsi Serikali itakavyotapanya fedha za Watanzania (pasipo kujali ukweli si kila mlipakodi wa nchi yetu ni mwana-CCM) kuhakikisha inashinda uchaguzi huo. Tutashuhudia pia nyenzo za umma (kama magari) zikitumika kisiasa na kuwabebesha Watanzania mzigo wasiostahili. Chama kinachopata wagombea kwa njia ya rushwa hakina njia nyingine ya kuomba kura zaidi ya kutoa rushwa.
Ni mazingira haya ya serikali yetu kumudu gharama zisizo muhimu (kama safari mfululizo za Rais Kikwete nje ya nchi na matumizi makubwa ya fedha za umma kwenye shughuli za kisiasa za CCM), yanayofanya vilio vya madaktari (na watumishi wengine wa umma pamoja na wananchi kwa ujumla) kuwa sio tu vya msingi bali pia vya lazima.





BONYEZA ORODHA HIYO HAPO JUU KUANGALIA ORODHA KAMILI NA NYINGINEZO




I didn't forget about your birthday; I just wanted to help prolong the celebration.

I didn't really forget your special day, I just figured you deserved more than one.

Even though this message comes to you a little late, the wish it brings for happiness is good on any day date.

Happy belated birthday.





6 Mar 2012

Usiniite mnafiki,au mpindisha maneno.Uthibitisho kuwa hata Rais Jakaya Kikwete hana imani na TAKUKURU upo katika habari ifuatayo (ANGALIA MAANDISHI MEKUNDU)


Rungu la Kikwete lilimwokoa Siyoi
Monday, 05 March 2012 09:17

Rais Jakaya Kikwete
NAPE, WASSIRA WADAIWA KUSIMAMA KIDETE ATOSWE, JK AKATUMIA 'RUNGU' KUZIMA HOJA,WABUNGE WOTE CHADEMA KUHAMIA ARUMERU
Joseph Zablon, Dar na Moses Mashalla, Arusha 

USHINDI wa Siyoi Sumari kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki, unadaiwa kuitesa Kamati Kuu (CC) ya chama hicho, baada ya baadhi ya wajumbe kukuna vichwa kuhusu mbinu na mikakati ya kutengua ushindi alioupata katika duru ya pili dhidi ya William Sarakikya.

Katika Mkutano Mkuu wa jimbo hilo uliofanyika, Februari 20 ulimchagua Siyoi ambaye ni mtoto wa aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, marehemu Jeremiah Sumari kwa kura 361, akifuatiwa na Sarakikya aliyepata kura 259. Hata hivyo, CC ya CCM iliyoketi Februari 27, iliagiza kurejewa kwa upigaji kura kati ya wagombea hao.
Katika duru hilo la pili la uchaguzi uliofanyika Machi Mosi mwaka huu, Siyoi alipata ushindi wa kishindo wa kura 761 na kumtupa mbali mpinzani wake, Sarakikya aliyepata kura 361. 

Juzi katika kikao hicho cha CC, ushindi huo wa mara ya pili wa  Siyoi uliipasua tena kamati hiyo kuu yenye mamlaka ya juu ya uamuzi ndani ya chama hicho, baada ya baadhi ya wajumbe kudaiwa kutaka atoswe na apitishwe Sarakikya kutokana na tuhuma za matumizi makubwa ya fedha wakati wa kampeni.

Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka katika kikao hicho cha CC, vilifafanua kwamba waliosimama kidete kutaka Siyoi atoswe ni Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira.

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, Nape alipinga Siyoi kurejeshwa akizingatia matukio mbalimbali ya tuhuma za matumizi makubwa ya fedha yaliyokuwa yakifanywa na baadhi ya watu ili wamchague mgombea huyo, kitu ambacho hakikupaswa kuvumiliwa. 

Hoja hiyo ya Nape iliungwa mkono na Wassira ambaye naye alitaka Siyoi atoswe kutokana na tuhuma hizo za matumizi makubwa ya fedha kutoka kwa baadhi ya wapambe wake waliotaka mgombea huyo achaguliwe.


Lakini inadaiwa kuwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alisema kikao hicho kisingeweza kumkata Sumari kwa sababu tu ya tuhuma hizo za rushwa zilitolewa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), mkoani humo.


Chanzo kingine kilimnukuu mwenyekiti huyo akisema kwamba, Arusha ni mkoa wenye siasa za aina yake hivyo ni muhimu kuwa makini kwani siku za nyuma kuliwahi kuibuka tuhuma za rushwa kwa wabunge wa CCM kukamatwa lakini, mahakama ikawaachia huru.

Chanzo hicho kiliongeza kwamba, Rais Kikwete alisisitiza kuwa hata tuhuma za rushwa zilizotolewa zilikuwa zikigusa wengine kwani iliwahi kupendekezwa kwamba Elishalia Kaaya ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC), ndiye apitishwe na wengine wang'olewe. 

Katika kikao hicho, Rais Kikwete pia alinukuliwa akihoji kuwa endapo Siyoi angekatwa jina kungekuwa na uhakika wa chama kushinda kwa kumsimamisha Sarakikya? Hakupata jibu kama mgombea huyo wa pili angeweza kushinda kiti hicho.

Hata hivyo, chanzo hicho kilisema baada ya mwenyekiti kutumia rungu kumpitisha Siyoi alimpa angalizo: “Basi na wewe usiende kutamba huko mitaani kwamba umeangusha watu, fanya kampeni, ushinde jimbo tuangalie mambo mengine mbele.”

Ilielezwa zaidi kwamba Rais Kikwete aliungwa mkono na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, aliyeeleza kuwa haoni sababu ya kumwondoa Siyoi katika kinyang'anyiro hicho kwani ushindi wake ulikuwa mkubwa. 


Chanzo na Kwa habari Kamili: Mwananchi

5 Mar 2012


ngoma inaitwa AGAIN and AGAIN,
msanii ni SEMY PAGE toka kundi la Macube rymers,akiwa amemshirikisha msanii BIG BOSS
ngoma imetengenezwa kwenye studio za M LAB producer akiwa Kanye Mujwahuki
hii ni nyimbo yake ya kwanza kama solo artist baada ya kutoka na ngoma ya kundi iliyokwenda kwa jina la HIRA.



Picha,Caption na Track kwa hisani ya DJ CHOKA

Mahojiano mafupi na msanii Linah akizungumzia (japo kwa ufupi) kuhusu historia yake kimuziki, maendeleo katika muziki wa kizazi kipya na ziara yake hapa Marekani kwa mwaka 2012.


3 Mar 2012

Waishi na fisi kwa miaka 44 sasa
Friday, 02 March 2012 20:44


Wakazi wa Kijiji cha Chela, Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga Mussa Serikali (kushoto), Doi Lukondya (katikati) na Matandalwa Lukondya wakiwa wamewashikilia fisi nyumbani wanaowafuga kwa ajili shughuli za burudani kama walivyokutwa hivi karibuni.
Na Shija Felician, Kahama
FAMILIA moja katika Kijiji cha Chela, Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga imesimulia jinsi inavyoishi na fisi kwa miaka 44 sasa.Kijiji cha Chela ndiko alikozaliwa Waziri wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige na fisi hao walionekana hadharani wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipofika katika kijiji hicho akiwa katika ziara mkoani Shinyanga wiki iliyopita. 

Familia inayofuga fisi hao ni ile inayounda kikundi cha burudani ya ngoma za jadi ambacho ni maarufu katika Kanda ya Ziwa kikijulikana kwa jina la Bununguli na kwamba fisi hao ni moja ya nyenzo za kufanikisha kazi yao.
Mmoja wa wanafamilia wanaomiliki ngoma hiyo, Lukondya Mabiti Jinoja anasema aina ya fisi wanaofuga wanajulikana kama nhawa kwa lugha ya Kisukuma na kwamba fisi wa aina hiyo wana maumbo makubwa kuliko wale waitwao mbitimululu wenye maumbile madogo yasiyovutia.

Alisema ingawa fisi hao wameanza kuwatumia na kuonekana hadharani siku za karibuni, familia yake imeanza kuishi na wanyama hao tangu mwaka 1968.

“Ni miaka mingi inafikia 44 au 45 na katika muda wote huo tumejifunza mbinu mbalimbali za namna ya kuwakamata na tumefanikiwa kuishi nao kwa muda wote bila kupata madhara yoyote,” anasimulia Jinola.
Jinoja ambaye ni Mwenyekiti wa Bununguli, alisema wakati wa maonyesho ya burudani za ngoma, fisi hao hutumika kunogesha na kuvutia umati wa watazamaji wa ngoma hizo.

Wanawakamataje?
Jinola anasema mara nyingi ukamataji wa fisi hao hufanywa kwa kutumia mbinu za kijadi ambazo hata hivyo, hakutaka kuziweka wazi.

“Hawa mafisi hukaa kwenye mapango, kwa hiyo sisi huenda tukiwa kundi kubwa kuwavizia taratibu na tukiwakaribia huwa tunawavamia, tukiwakamata tu huwa tunawahifadhi kwenye masanduku yetu makubwa na kuwafungia, kisha huyabeba hadi nyumbani tunakowafuga,” alisema Jinola.

Alisema fisi hufugwa kama ilivyo wanyama wengine ambao ni mbwa au paka na kwamba baada ya kuishi nao kwa siku kadhaa, huzoeana nao na baadaye huwa wapole wasiokuwa na madhara kwa binadamu.Hata hivyo, Jinoja alisema changamoto kubwa waliyonayo ni uwezo wa kuwalisha kwani fisi mmoja ana uwezo wa kula kati ya kilo mbili hadi nne za nyama kwa siku moja kulingana na ukubwa wake.

“Natumia wastani wa kilo 16 za nyama kila wiki kuwalisha fisi wangu wanne, ni kazi kubwa kweli lakini tunajitahidi kadri tunavyoweza,” alisema.Hata hivyo, alisema baada ya familia hiyo kufanikisha mpango wa kuishi na fisi hao sasa wameweka mikakati wa kufuga chui siku zijazo.


CHANZO: Mwananchi


Pata Windows 8 (ya majaribio) kwa KUONYEZA HAPA

1 Mar 2012

Wazee wa iliyokuwa Jumuia ya Afrika Mashariki wakiwa wamekaaa katikati ya jiji la Dar es Salaam wakijadili malipo yao yaliyocheleweshwa na serikali hadi leo.…

Nimekutana na picha hiyo hapo juu kwenye mtandao wa Global Publishers.Kwa kweli imenisikitisha sana kuona wazee wetu waliotumikia taifa letu kwa uadilifu wakihangaishwa miaka nenda miaka rudi kupewa mafao yao ya utumishi katika iliyokuwa Jumuiya ya Nchi za Afrika Mashariki.

Hazipiti wiki kadhaa kabla ya kusikia Rais wetu yuko kiguu na njie kwenda nje ya nchi huku akiambatana na msururu wa watu kwenye msafara.Watendaji wengine wa serikali wanatumia magari ya thamani kubwa huku ofisi zao zikisheheni samani kutoka ng'ambo.Matumizi ya viongozi wetu hayaendani kabisa na umasikini wetu.Mabilioni yalitapanywa mwezi Disemba mwaka jana katika maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru.Hivi fedha hizi zisingeweza kumaliza adha inayowakabili wazee wetu hawa?

Jamii inayopuuza wanyonge (kwa mfano wazee hawa) ni kama inasaka ugomvi usio wa lazima na Muumba.Kosa la wazee hawa ni lipi hadi wahangaishwe kiasi hiki?Chonde chonde viongozi wetu-hususan Rais Kikwete-waoneeni huruma wazee wetu hawa.Wanachodai sio posho za vikao kama za wabunge bali ni jasho lao halali.Wenzao wa Uganda na Kenya walishalipwa stahili zao zote.Kama wao waliweza kwanini sie tushindwe?

Kama hakuna polisi anayetaka kuua, je, kuna raia anayependa kuuawa?

KWA mara nyingine tena, Watanzania tumeshuhudia unyama wa Jeshi la Polisi ambao wiki iliyopita waliwapiga risasi na kuwaua raia mjini Songea. Kosa pekee la wananchi hao ni kutumia haki yao ya kikatiba kuandamana.
Ni rahisi kuwalaumu askari waliofyatua risasi zilizoua iwapo tutapuuza kanuni za utendaji kazi wa watumishi wa vyombo vya dola. Ifahamike kuwa moja ya kanuni muhimu kwa askari ni nidhamu kwa uongozi wa juu, sambamba na kutekeleza amri na maagizo ya viongozi pasipo kuhoji.
Kwa hiyo ni muhimu kuyaangalia matukio yanayowahusisha watendaji wa vyombo vya dola na utekelezaji wa ‘amri halali’ zinazotolewa na viongozi husika. Kwa vyovyote vile, askari walioua huko Songea hawakufanya hivyo kwa vile walikuwa na hamu ya kuua au wasingeua usalama wao ungekuwa hatarini bali walikuwa wanatekeleza amri ‘halali’ za viongozi wao.
Suala jingine linalostahili kupigiwa mstari ni mtiririko wa amri kutoka kwa viongozi kwenda kwa watekelezaji, sambamba na mawasiliano kati ya ngazi za chini za vyombo vya dola (kwa mfano polisi) na makao makuu yao.
Katika mazingira ya kawaida tu, pindi hali ya usalama inapochafuka hadi kufikia hatua ya kumhusisha Kamanda wa Polisi wa Mkoa, ni dhahiri kwamba ‘wakubwa’ makao makuu ya Jeshi la Polisi walifahamishwa kila kinachoendelea katika eneo la tukio.
Kwa hiyo basi wakati tunaelekeza lawama zetu kwa polisi walioua Songea tusisahau kudadisi juu ya nani aliyetoa amri kwa askari hao.
Taarifa zilizopo hadi sasa ni kwamba zaidi ya wananchi 50 wameshafikishwa mahakamani kutokana na ‘vurugu’ hizo za Songea. Lakini wakati hilo likitokea, tunaambiwa kuwa ni askari wanne tu waliokamatwa kwa ‘tuhuma za kutumia risasi za moto.’
 Kwa nini wananchi ambao wenzao waliouawa wawe wameshafikishwa mahakamani kwa ‘kosa la kufanya vurugu’ lakini walioua waishie kukamatwa tu.
Na kuna uhakika gani kama wamekamatwa kweli ilhali hata majina yao hayajawekwa hadharani? Na hata kama madai hayo ni kweli (kuwa askari hao wamekamatwa) kuna uwezekano gani wa haki kutendeka katika mazingira ya polisi kukamata polisi wenzao waliokuwa wanaotekeleza amri ‘halali’ ya jeshi hilo?
Kingine kinachovunja moyo na kuchukiza ni mkanganyiko katika kauli za uongozi wa jeshi hilo. Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma, Michael Kamhanda, alinukuliwa akidai kuwa askari hao walikamatwa na wanaendelea kuhojiwa ili kujua kama kulikuwa na uzembe katika utekelezaji wa majukumu yao.
Kadhalika alisema kuwa (namnukuu); “Kwa kuwa tukio hilo limehusisha vifo, hatuwezi kuacha hivi hivi tu ni lazima tujiridhishe kuwa askari hao hawakufyatua risasi kwa uzembe.”
Lakini katika kile kinachoweza kutafsiriwa kama ‘hukumu imeshatolewa juu ya nani alikuwa sahihi na nani mkosaji,’ Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Kamishna Paul Chagonja, alizungumza na vyombo vya habari na kuhitimisha kuwa ‘maandamano hayo hayakuwa ya amani bali ya kihuni kwani yalilenga kuvamia ofisi za serikali ikiwemo Ikulu ndogo na Ofisi ya Mkuu wa mkoa.’
Kamanda Chagonja alitetea polisi akisema; "Usifikirie polisi hawana akili. Haiwezekani watu wazima na akili zao wenye mafunzo wafyatue ovyo risasi za moto kwa raia. Hakuna askari anapenda kuua raia...lakini watu wanavamia Ikulu, ofisi ya mkuu wa mkoa, magari ya polisi hapo kuna amani kweli?"
Jambo la kutilia shaka ni kwamba, Chagonja huyo huyo ndiye kiongozi wa msafara uliotumwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema kwenda Songea kuchunguza tukio hilo. Sasa kulikuwa na haja gani ya kupelekea timu hiyo ilhali imeshathibitika kuwa waandamanaji walikuwa wahuni tu (na pengine ilikuwa sahihi kwa polisi kuwaua baadhi)?
Chagonja anasema tusifikiri kuwa polisi hawana akili lakini kauli zake zinaonyesha ni kwa kiwango gani yeye mwenyewe ana matatizo katika kuushirikisha ubongo wake na mantiki. Hivi busara ndogo tu isingemwelekeza kuwa wakati mwafaka wa yeye kutoa hukumu ni baada ya kukamilika kwa uchunguzi huo?
Kulikuwa na haja gani ya kuwatia mbaroni askari wanne ilhali sio tu walikuwa wanatekeleza maagizo ya uongozi wa Jeshi la Polisi bali pia walikuwa wanakabiliana na wahuni?
Japo Kamanda Chagonja anatusihi tusifikiri polisi hawana akili, lakini kila mwenye akili timamu anaweza kubaini nani asiye na akili katika kukurupuka huko kwa kiongozi wa ngazi za juu katika Jeshi la Polisi, kutoa hukumu kabla hata hajaanza uchunguzi wa tukio husika.
Kimsingi, Jeshi letu la Polisi limegeuka na baadhi ya matukio yakionyesha kuwa limeanza kuwa na dalili za awali za kundi la maharamia. Siku zote wamekuwa waoga kuchukua hatua dhidi ya wahalifu wakubwa (hususan mafisadi wanaosababisha ugumu wa maisha-ambao kwa namna fulani unachangia haja ya kudai haki kwa njia ya maandamano inapobidi) lakini sio tu wepesi wa kudhibiti wananchi wasio na hatia, bali wana vidole vyenye kiu ya kufyatua risasi (trigger happy).
Kila mara tunalikumbusha Jeshi la Polisi kuwa maandamano ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania. Hiyo kanuni ya kidikteta ya kutaka waandamanaji waombe kibali ni kinyume cha Katiba yetu inayoruhusu uhuru wa kukusanyika. Kinachopaswa kufanyika ni kwa waandamanaji kulifahamisha tu jeshi hilo kuhusu maandamano na sio kuomba ridhaa yao.
Jukumu la polisi sio kujifanya watabiri kwa intelijensia zao zenye shaka na kuhitimisha kuwa maandamano yatasababisha uvunjifu wa amani bali wanapaswa kushirikiana na waandaaji wa maandamano kuhakikisha yanafanyika kwa amani na utulivu.
Nimeandika intelijensia zenye shaka (za ovyo ovyo)’ kwa sababu zinaonekana kuwa na ‘ufanisi’ tu kwenye kuminya haki za wananchi lakini hazitumiki kukamata majambazi wanaobaka uchumi wetu kila kukicha. Jeshi la Polisi linaloshindwa kufanya intelijensia ya kubaini wala rushwa ndani yake litawezaje kudai lina intelijensia dhidi ya wananchi wasio waajiriwa wake?
Tatizo kubwa linalolikabili Jeshi la Polisi ni kasoro za kufikiri sawasawa miongoni mwa viongozi wake wa ngazi za juu katika suala la haki za binadamu. Unaposikia Mkuu wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi hilo anapuuza mauaji ya raia na kuhitimisha kuwa ni wahuni tutegemee nini kwa askari wa ngazi za chini?
Kwa wadhifa wake, Chagonja ndiye mwenye dhamana kubwa ya kuwapatia askari wake uelewa wa haki za binadamu. Sasa kama mtu mwenye dhamana ya kuwafundisha kazi watendaji wake, anaongoza kwa mfano wa kupuuza haki za raia kuishi ni wazi tutaendelea kushuhudia polisi wakiendelea kuua, na kisha ‘kujibaraguza’ kwa kuunda tume ‘za kizushi’ ambazo zitatoa hukumu kabla ya kuanza uchunguzi rasmi.
Kwa asili, Watanzania ni watu wenye kuenzi sana amani japo baadhi ya wanasiasa wanatulaghai kuwa hayo ni matokeo ya wao kuwepo madarakani. Laiti mtu kama Chagonja angetumia faida hiyo ya ‘upole’ wa Watanzania angeweza kuliepusha Jeshi la Polisi na gharama zisizo na msingi, kuandaa operesheni kubwa (kana kwamba wanaenda vitani) kwa kuhakikisha kila maandamano yanapatiwa ulinzi na polisi na kuwakumbusha waandamanaji na viongozi wao juu ya umuhimu wa kukamilisha shughuli yao kwa amani.
Na si kwamba polisi hawana uzoefu katika kusikindikiza maandamano kwa amani lakini tatizo ni mtazmao wa baadhi yao wenye mwelekeo wa kiharamia, kwamba kila maandamano ni chanzo cha vurugu. Chagonja anasema hakuna polisi anayetaka kuua lakini hasemi kama kuna Mtanzania anayependa kuuawa.
Damu za wananchi wanaouawa pasipo hatia huku vifo vyao vikiombolezwa na akina Chagonja kwa kuwaita wahuni hazitapotea bure. Kila anayeingilia jukumu la Mwenyezi Mungu kutoa uhai wa mwanadamu mwenzie, atambue kuwa kuna siku atawajibika kwa mauaji hayo.
Hayo madaraka yanayowatia jeuri polisi kuua watu wasio na hatia yatawatokea puani, kwa njia moja au nyingine. Kwa vile kama mwananchi wa kawaida anakumbana na kila ugumu kupewa haki yake akiwa hai ni wazi hao wanaouawa pasipo hatia hawawezi kupata haki hiyo kwa sasa.
Lakini kwa vile maandiko matakatifu yanatufundisha kuwa mshahara wa dhambi na mauti, basi kwa hakika kila anayetoa amri ya kuua au kufyatua risasi atawajibika huko mbele ya haki kwani kila nafsi itaonja mauti.
Nimalizie makala hii kwa kulikumbusha Jeshi la polisi kuwa halina uwezo wala nguvu ya kuua kila Mtanzania anayetimiza haki yake ya kikatiba kuandamana.
Wanaweza kuua watu kadhaa kwa muda fulani, na wanaweza kuua watu wengi kwa muda mwingi lakini kamwe hawawezi kuua watu wote. Na kama ambavyo walionyanyaswa na mfumo dhalimu wa kibaguzi huko Afrika Kusini walimudu kupambana na silaha za hali za juu la polisi wa makaburu, yawezekana kabisa siku moja wananchi waliochoshwa kuuawa na polisi wetu watachukua hatua mkononi kwa staili ya ‘akuanzae mmalize.’


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.