Showing posts with label USANII WA KISIASA. Show all posts
Showing posts with label USANII WA KISIASA. Show all posts

25 Feb 2013


Majuzi serikali imezindua 'mpango kabambe' ambapo MAWAZIRI na watendaji wa wizara mbalimbali watakaokuwa wazembe, watachekechwa na kubaki wale ambao utendaji kazi wao ni bora, baada ya kuzinduliwa kwa mpango maalumu wa kupima utendaji wa kazi wa viongozi.

Pichani ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt Shukuru Kawambwa ambaye licha ya matokeo mabaya ya Kitano cha nne amegoma kujiuzulu, akionekana waziwazi kuchekewa na Rasi Kikwete,makamu wake Dkt Bilal na Waziri Mkuu Pinda. Kwnaini tusidhani kuwa mpango huo kabambe ni usanii tu?

26 Jun 2010

Sijui ni ukosefu wa mawasiliano au uzembe tu,au pengine ni mkakati wa makusudi wa kutoa kauli zinazotofautiana ili baadaye iwe rahisi "kuziruka kimanga",lakini ni dhahiri kuwa mmoja kati ya viongozi hawa anatudanganya.Wakati Waziri wa Sheria na Katiba Mathias Chikawe akirejea ahadi kama ya mwaka 2005 (wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu) kuhusu uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi,Makamu Mwenyekiti wa CCM Pius Msekwa anasema bayana kuwa suala hilo halipo (labda Waislamu wenyewe walishughulikie "kivyao").Hebu soma kwanza hapa chini

Kwa mujibu wa Gazeti la Tanzania Daima: SERIKALI imesema Mahakama ya Kadhi itaanza katika mwaka wa fedha 2010/11 baada ya jopo la wanazuoni wa Kiislamu wanaoziangalia na kuzihuisha sheria za Kiislamu kukamilisha kazi hiyo.

Jambo hilo lilibainishwa jana bungeni na Waziri wa Katiba na Sheria Mathias Chikawe wakati akisoma hotuba ya makadirio ya matumizi ya wizara yake kwa mwaka 2010/2011 ambapo ameliomba Bunge limuidhinishie kiasi cha sh bilioni 116.8

Alisema kuwa jopo hilo linaziangalia na kuzihuisha sheria za Kiislamu zinazohusiana na ndoa, mirathi na urithi kwa madhumini ya kuziorodhesha ili zitambuliwe chini ya sheria za dini ya Kiislamu (Islamic Law resstatment act).

Aliongeza kuwa jopo hilo lilianza kazi hiyo baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kukutana na Mufti, Sheikh Mkuu, Issa Bin Shaaban Simba, na kukubaliana kuwa waanzishe mchakato wa Mahakama ya Kadhi.

Lakini Gazeti la Majira linaripoti kwamba:

Katika hatua nyingine, Bw. Msekwa amefafanua sababu za ilani ya CCM mwaka huu kutohusisha kipengele cha uanzishwaji wa Mahakam ya Kadhi kama ilivyokuwa mwaka 2005.

Alisema kuwa ahadi hiyo iliyotolewa 2005 tayari utekelezaji wake umekamilika.

Katika ilani hiyo, kifungu namba 108(b) CCM iliahidi kulipatia ufumbuzi suala la kuanzishwa mahakama ya kadhi Tanzania bara, ambalo limekamilika kwa kukabidhi wenye dini yenyewe wahusike katika uanzishwaji wa mahakama hiyo, kwa kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siyo ya kidini.

"Serikali inaweza kukubali au kukataa, ndiyo maana ya kulipatia ufumbuzi lakini watu wanalitafsiri vibaya kuwa
serikali kupitia kifungu hicho imekubali kuanzishwa kwa mahakama hiyo wakati sivyo," alisema Bw. Msekwa.

Alibanisha kuwa serikali ilifanyia kazi kupitia Tume ya Kurekebisha sheria ambayo ilishauri kwamba haitakuwa sahihi kwa mahakama ya kadhi kuundwa na serikali kwa kuwa ni suala linalohusu taratibu za dini ya kiislamu.

Aliongeza kuwa baada ya serikali kupata ushauri huo ilifanya uamuzi kwamba haitaunda mahakama ya kadhi lakini kwa kuwa suala hilo linahusu taratibu za dini la kiislamu, waislamu wapo huru kuunda mahakama hiyo ndani ya taratibu za dini yao.

16 Feb 2010


Pamoja na kuwa moja ya nchi maskini kabisa duniani, Tanzania yetu bado inaendelea kusifika kwa mambo kadhaa. Ukiachia mbali vivutio vya asili kama Mlima Kilimanjaro, utitiri wa wanyama huko Selous, Mikumi na kwingineko, na “utajiri” wa madini kama Tanzanite,dhahabu, almasi na madini mengineyo,nchi yetu pia inasifika kwa watu wenye uwezo wa kuongea.

Ndio maana jirani zetu wanapenda kututania kuwa “nyie Watanzania iko maneno mingi” wakimaanisha tunaongea sana. Na pengine mahala mwafaka pa kuthibitisha uwezo wetu wa kuongea ni katika vikao vya bunge letu tukufu. Laiti yote yanayoongewa katika vikao hivyo yangekuwa yanatafsiriwa kwa vitendo, basi kwa hakika tungekuwa mbali sana.

Lakini licha ya sifa hiyo ya kuongea sana, Watanzania tuna sifa nyingine ya usikivu na kuamini kirahisi kila tusikiacho hata kama ni “wizi mtupu”. Ndio maana basi watu wenye akili na busara zao walidanganyika kwamba miongoni mwa wabunge wa CCM kuna kundi la WAPIGANAJI DHIDI YA UFISADI.Kundi hilo lililojipatia umaarufu usiostahili linadaiwa kuwa chini ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta.

Na kwa katika kile kinachoweza kutafsiriwa kwamba ni jitihada za kujiongezea sifa za “upambanaji” , Spika Sitta na wabunge wawili kutoka vyama vya upinzani,Dr Wilbroad Slaa (Chadema) na John Cheyo (UDP) walichapisha kitabu walichokipa jina “BUNGE LENYE MENO”. Si lengo la makala haya kurejea yaliyomo katika kitabu hicho, lakini kwa kifupi ni mwendelezo wa sifa tulizonazo Watanzania: maneno meeeengi lakini vitendo SIFURI.

Sijui Sitta wa “wapiganaji” wenzie walikuwa na mawazo gani kurefusha mjadala wa ujambazi wa Richmond kwa takriban miaka miwili lakini tukashuhudia wakilamba matapishi yao walipounga mkono kile kinachoitwa “utekelezaji wa serikali wa maazimio ya bunge kuhusu suala la Richmond”.Kwanini hawakuiunga mono serikali tangu siku ya kwanza badala ya kuwazuga Watanzania kwa muda wote huu?

Binafsi siamini kabisa kuwa Spika Sitta ni mpambanaji dhidi ya ufisadi.Ni usanii tu ambao unaelekea kuwa moja ya sifa muhimu za wanasiasa wetu.Sitta atakuwaje kamanda wa vita dhidi ya ufisadi ilhali ndiye aliyemfungia Zitto Kabwe alipohoji ufisadi wa Buzwagi?Je sio Sitta huyohuyo aliyetishia kumpeleka Dr Slaa kwenye vyombo vya sheria pale (Slaa) alipoibua ufisadi wa EPA?

Spika Sitta,akisaidiwa na vyombo vyetu vya habari vinavyosifika kwa umahiri wa kukariri kikasuku kila kinachosemwa na wanasiasa (badala ya kwenda mbali zaidi na kuchambua kauli hizo), alitambua vema kuwa Watanzania wengi wanahitaji wanasiasa watakaoungana nao kupambana na ufisadi.Kwa lugha nyingine,alifahamu fika kuwa mapambano dhidi ya ufisadi ni mtaji maridhawa kisiasa na ungeweza kuimarisha nafasi yake.

Na kwa vile anafahamu kuwa Watanzania ni wasikivu sana hata kama wanadanganywa,akawa anapita huku na kule akijigamba kwamba “kamwe hatatishwa na wanaomwandama kisiasa kutokana na msimamo wake thabiti wa kupiga vita ufisadi”. Sitta, na wasanii wenzake waliotuhadaa kuwa ni “wapiganaji dhidi ya ufisadi” walibinafsisha ajenda ya vita dhidi ya ufisadi kiasi kwamba “kila aliyeonyesha dalili ya kutamani MAJIMBO YAO alionekana anasukumwa na umahiri ya akina Sitta katika kupambana na ufisadi”.Yaani hawakubinafisha tu hoja ya ufisadi bali wamegeuza majimbo yao kuwa mali zao za urithi ambazo hazipaswi kuguswa na Mtanzani mwengine yeyote yule.

Na Sitta anadai atawania tena kiti cha Uspika katika bunge lijalo.Kuna dalili kuwa anaweza kurejea bungeni kwa vile ametumia vema nafasi yake ya uspika kujiimariusha jimboni kwake Urambo.Lakini kama bunge lijalo litakuwa na wabunge wanaowajali wapiga kura wao basi ni dhahiri Sitta atabaki kuwa historia tu.Hatastahili hata unaibu Spika,pamoja na naibu wake wa sasa Anne Makinda,viumbe wawili waliotumia vibaya sana madaraka yao na kuendesha taasisi hiyo kwa utashi wao huku wakitumia kanuni zilizopitwa na wakati kuwaokoa mawaziri wazembe walioshindwa kutoa majibu sahihi kwenye mijadala bungeni.

“Wapiganaji feki wa ufisadi” wametuchezea shere.Upande mmoja wao ni sehemu ya mfumo wa kifisadi unaoshamiri kwa kulindana,na hawana jeuri ya kujitenga nao kwa vile ni wabinafsi.Lakini kwa upande mwingine wanataka tuwaone wao ni wenzetu,wanaguswa na matatizo yetu na wana uchungu wa dhati na nchi yetu.Wasanii hawa wanatuona sie wajinga tusiojua kuwa mishahara yao minono ni ushahidi tosha kuwa wanaishi dunia nyingine kulinganisha na walimu,madaktari,manesi,wakulima na walalahoi wengine.Wanarefusha vikao vya bunge ili posho zao nonoi ziendelee kutunisha akaunti zao.

Spika Sitta na wasanii wengine waliotudanganya kuwa wao ni wapiganaji dhidi ya ufisadi hawana sababu hata moja ya kuwaacha majambazi wa Richmond wakisafishwa na pasipo kuchukuliwa hatua yoyote.Kuna baadhi yetu tulikuwa tukifahamu tangu mwanzo kuwa hakutakuwa na hatua yoyote dhidi ya Lowassa,Karamagi,Msabaha,Mwanyika ,Hoseah na wengineo waliohishwa na ufisadi huo.Tulifahamu hivyo kwa vile kimsingi,ufisadi huo-kama ilivyo kwenye ishu za EPA,Kiwira,na kwingineko-ni matokeo ya ushirika wa kijambazi uliobuniwa na kufanikishwa kwenye korido za utawala za CCM.Kuwachukulia hatua watuhumiwa hawa kungeweza kabisa kupelekea vigogo wengine kuadhiriwa hadharani.

Hiyo haimaanishi kuwa kuadhirishwa kwa vigogo hao ni kosa,bali ni muhimu kwetu kuelewa kuwa mtandao huu wa kifisadi uliundwa kwa madhumuni ambayo mpaka sasa bado yana umuhimu kwa wahusika.Kwa lugha nyepesi.mfumo wa kifisadi ni matokeo ya moja kwa moja ya kundi la WANAMTANDAO.Na kama walivyoshirikiana kuingizana madarakani,wanaendelea kulindana ili Mtandao huu uendelee kututawala.

Na Watanzania tuna sifa nyingine ya ziada:UPOLE. Ungetarajia kusikia wananchi wakiandamana kupinga majambazi wa Richmond “kuachiwa huru na Bunge” huku wakihakikishiwa kuwa “kuna siku watarejea madarakani”. Yaani tumetapeliwa,tukachezewa akili kwa zaidi ya miaka miwili na sasa tunashuhudia majambazi wakisafishwa bungeni lakini hakuna tumetulia kana kwamba Katiba inatuelekeza tufanye hivyo!Ama kweli hiyo ndio amani na utulivu-sio kwako na kwangu bali AMANI KWA WANAOTAFUNA NCHI YETU NA UTULIVU KWA AKAUNTI ZAO ZILIZESHEHENI MAMILIONI YA FEDHA ZA KIFISADI.

Habari njema kwa mafisadi ni dalili kuwa wengi wao watarejea tena madarakani baada ya uchaguzi mkuu hapo Oktoba.Na habari njema zaidi kwao,ni kuwepo kwa kila ishara kuwa chama kinacholea ufisadi,CCM,kitaunda serikali ya awamu ya tano huku kikilindwa na idadi kubwa ya wabunge.Japo baadhi yetu tungependa kuona mabadiliko lakini ni muhimu kwetu kuwa wakweli kwa nafsi zetu.Hakuna dalili ya CCM kushindwa uchaguzi mkuu ujao kwa vile mazingira yaliyopo yanakwaza mabadiliko ya aina yoyote ile.

Hata hivyo,kama wewe Mtanzania umechoshwa na ufisadi,kulindana,ahadi hewa na ubabaishaji mwingine,una nafasi ya pekee ya kutimiza hasira zako kwa kuinyima kura CCM.Vinginevyo,hali sio tu itaendelea kuwa mbaya bali tunaweza kufika mahala watu wakalazimisha mabadiliko yatakayopelekea kutuathiri sote.Ni muhimu kwako mpiga kura kujisuta kwa makosa uliyofanya 2005 na huko nyuma,lakini kufanya kosa si kosa bali kurejea kosa.Ni mwaka huu au ndio tumeumia milele.Timiza wajibu wako.


13 Oct 2009


Hivi mwenzangu unapoiangalia CCM kwa mtazamo wa kawaida tu (yaani usiohisha uchambuzi wa kitaaluma) unaielezeaje?Pengine huafikiani na mtizamo wangu wa “kawaida” na kitaaluma kwamba pamoja na hadi lukuki za kuwakomboa Watanzania kutoka kwenye lindi la umasikini,chama hicho hakijaonyesha dhamira ya dhati kutimiza ahadi hizo.

Naamini kuwa baadhi ya ahadi hizo zilikuwa za dhati,hususani ile ya kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.Naamini hivyo kwa vile ni dhahiri kwamba chama hicho kilikuwa kinatambua hali ngumu inayowakabili Watanzania baada ya miongo kadhaa ya utawala wake.Kwa kutambua tatizo,CCM ilileta dalili za matumaini kwamba sio tu inataka kuendelea kutawala lakini pia inataka kuwa chachu ya mabadiliko.Japo chama hicho kinafahamika kwa usugu wa kukiri mapungufu ya utendaji wake,uamuzi wake kugusia maeneo yanayowakera wananchi ilikuwa ishara ya kutambua mapungufu katika awamu zilizotangulia na kudhamiri kufanya marekebisho.

Binafsi nilitarajia kwamba kama ilivyokuwa mwaka 2005 ambapo CCM “ilikiri mapungufu yake kiaina” kwa kuahidi kuboresha maisha sambamba na kukabili chanzo kikuu cha kuzorota/kudidimia kwa maendeleo (rushwa),basi safari hii pia kingepata ujasiri wa kutueleza bayana kwamba kumekuwa na mapungufu makubwa zaidi katika utekelezaji wa ahadi hizo.

Ni nani asiyejua kuwa kiwango cha rushwa kinazidi kupaa siku hadi siku?Ni nani asiyejua kuwa rushwa na uhujumu mwingine wa uchumi umechukua sura mpya kwa kuzaa tabaka “jipya” la mafisadi?Ni nani pia asiyejua kuwa kwa kiasi kikubwa ahadi ya maisha bora kwa kila Mtanzania imekuwa na maana zaidi kwa mafisadi kuliko walalahoi?Ni dhahiri kwamba Watanzania wenzetu kama wamiliki wa kampuni ya Kagoda wanaishukuru CCM kwa ukarimu na huruma yake to an extent that inaona aibu kuwataja hadharani.Matapeli wa Richmond (achana na yule Mhindi aliyegeuzwa mbuzi wa kafara mahakamani) wanaishukuru sana CCM kwa huruma yake kwao ambapo kila kikao cha bunge kinazugwa kuwa “taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya kamati ya Mwakyembe itatolewa katika kikao kijacho”,na porojo nyingine kama hizo.

Kinachokera sasa sio tu madudu yanayoendelea kufanywa na CCM bali hizi kauli za kukera kwamba eti chama hicho kimeweka rekodi ya mapambano ya rushwa kuliko nyakati yoyote ile.Hii ni sawa na kuwasanifu Watanzania.Ni mithili ya kuwafanya wajinga,wasioona madudu yanayoendelea,wasiosikia maumivu ya vibano wanavyopewa na mafisadi,na wasiofahamu kuwa watuhumiwa kadhaa wa ufisadi hawajaguswa hadi leo (na hakuna dalili kuwa wataguswa licha ya ahadi kuwa kuna kesi tatu kubwa zitafunguliwa hivi karibuni....na kila mara tunaambiwa “hivi karibuni).”

Ni kweli kwamba hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi hazipaswi kuchukuliwa kutokana na utashi wa watu flani bali kwa kuzingatia sheria na kanuni.Lakini utashi ni muhimu katika kuchukua hatua,na hapa hatuzungumzii utashi wa wananchi wasio na uwezo wa kuuamua,kwa mfano “Chenge na tuhuma za vijisenti vyake huko Jersey hastahili kuwa kwenye kamati ya maadili ya CCM.”Kwanza kuwa na utashi wa kufanya jambo jema si dhambi,kama CCM inavyotaka kutuaminisha.Kuwa na utashi wa kuchukua hatua dhidi ya mafisadi ndio itapelekea chama hicho kuwatenga mafisadi inaowakumbatia,na hivyo kuwa rahisi kwake kuchukua hatua dhidi yao.Utashi unapaswa kuepukwa ni kama ule wa wanamtandao unaoendelea kuwaangalia wana-CCM wasio wanamtandao kuwa mithili ya wahaini.

Mamlaka husika zinapozembea kuchukua hatua sahihi halafu tunaishia kuambiwa kuwa hatua haziwezi kuchukuliwa kwa utashi wa watu flani...jibu jepesi ni kwamba matatizo yetu hayawagusi wanaotuongoza.Wanaona tunapiga kelele zisizo na msingi,ndio maana kwao haki za binadamu za mafisadi ni muhimu zaidi kuliko za walalahoi walio wengi.

Hivi kweli CCM inataka kutuzuga kuwa haifahamu kwamba Watanzania wengi wangependa kuona wahusika “halisi” wa utapeli wa Richmond wakifikishwa mahakamani badala ya kile tunachoelezwa kuwa “walijiuzulu kwa maslahi ya taifa”?CCM haijui kwamba kwa kuendelea kuminya taarifa kuwa nani anamiliki Kagoda ni mithili ya kuwapuuza Watanzania?Au CCM haifahamu kuwa kuwaachia mzigo Waingereza kudili na vijisenti vya ujambazi wa rada ni kukwepa majukumu?

Au chama hicho kinapotulaghai kwamba tumwache mhusika mkuu wa ufisadi katika mgodi wa Kiwira apumzike kwa amani ni sawa na kuruhusu kila mtu aibe kisha aachwe apumzike kwa amani?Kwanini basi vibaka wanajazana magerezani ilhali wezi wakubwa wanatetewa kwa nguvu zote?

Watanzania wana kila sababu ya kuiadhibu CCM hapo mwakani.Kinachofanywa na chama hicho kinapodai kuwa “kimeweka rekodi ya kupambana na rushwa” ni mithili ya vibaka wanaokuibia kisha wanakupigia ukelele wa mwizi na kupelekea wewe mwathiriwa wa uporaji huo kushushiwa kipigo kitakatifu huku kibaka “akiyeyuka kiulaini.”Badala ya kukiri kwamba kasi yao ya kupambana na ufisadi ni ndogo, wao wanatukejeli kuwa wameweka rekodi!Halafu bado tutegemee lolote kutoka kwa wababaishaji hawa?

Hakuna haja ya kubishana au kupigiana kelele nao.Dawa yao ni hapo mwakani.Kama unataka kuendelea kuona mafisadi wakitetewa huku wanaowapinga wakikemewa basi irejeshe CCM madarakani hapo mwakani.Kama unadhani maisha bora yaliyoahidiwa 2005 yamepatikana zaidi ya matarajio yako basi hutofanya kosa kutoa kura ya ndio kwa chama hicho.

Tukiendeleza mazowea tutazidi kuumia.Kuna wanaodhani kwamba Tanzania haiwezi kuwa kisiwa cha amani pasipo utawala wa CCM.Wanachosahau kuwa hata hao CCM ni Watanzania wenzetu japo wanawathamini zaidi wageni (wawekezaji) kuliko sie wenye nchi.Wanasahau pia kuwa wingi wa wabunge wa CCM unakwaza jitihada wa wapambanaji kama akina Dokta Slaa kuwakalia kooni wababaishaji waliojazana chini ya utawala wa CCM.

Atakayenuna na anune lakini nchi hii ni yetu sote na kila Mtanzania ana haki ya kudai haki yake.Tukiruhusu kuendelea kwa ngojera za “tunaendelea na mchakato wa blah blah blah” au “kesi kadhaa zkubwa zitapelekwa mahakamani hivi karibuni...” na hadithi nyingine kama hizo basi tutaendelea kuwa watu wa kulalamika kila siku japo ni sie wenyewe tunaoweza kukomesha usanii wa kisiasa wa aina hiyo.Kama imewezekana Ghana basi hata kwetu inawezekana.Si kweli kwamba chama mbadala kitashindwa kutupeleka tunakostahili kwenda hasa ikizingatiwa kuwa hakuna uwezekano wa chama hicho mbadala kupata idadi kubwa ya wabunge zaidi ya CCM,which means itakuwa rahisi kukidhibiti iwapo kitaonyesha dalili za kurejea madudu ya CCM.

Kusanya hasira zako lakini usipigane bali pugie kura ya kujiletea maisha yako bora wewe mwenyewe kwa kuwaondoa wanaokwaza uwezekano huo.Ifike wakati tusema tumechoshwa na ahadi na maneno matamu (na mengine si matamu bali ya dharau kama hayo ya kudai wameweka historia ya kupambana na rushwa wakati wanajua waziwazi kuwa wamekuza rushwa kupindukia).

It can be done if you play your part.

Inawezekana ukiamua kutimiza wajibu wako.


8 Oct 2009




Manji, Jeetu wagombea matrekta

• Homa ya Kilimo Kwanza

na Mwandishi Wetu

WAFANYABIASHARA wawili maarufu hapa nchini wenye asili ya Kiasia, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel, maarufu kwa jina la Jeetu Patel, wanadaiwa kuingia katika mzozo mkubwa wa kibiashara wakati wakigombea kupata zabuni ya mradi wa kuingiza nchini na kusambaza matrekta, wenye thamani ya zaidi ya sh bilioni 50.

Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano limezipata kutoka vyanzo vyake vya habari vya kuaminika zimeeleza kuwa, Manji na Patel ambao wanadaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika kuomba zabuni hiyo, sasa wanawindana huku wakitishana kumalizana kibiashara.

Baadhi ya watu wa karibu na wafanyabiashara hao mabilionea waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti katika siku za karibuni walieleza kuwa, kumekuwa na jitihada za chini kwa chini zinazofanywa na wapambe wao kuvujisha katika vyombo vya habari mbinu zao wanazotumia kupata zabuni kubwa za serikali.

Mfanyabiashara mmoja maarufu ambaye yuko karibu na wafanyabiashara hao, alilieleza gazeti hili kuwa, mabilionea hao sasa wamekuwa mahasimu baada ya kuzidiana ujanja katika zabuni hiyo ambapo kila mmoja anatishia kutoa siri za kibiashara za mwenzake.

“Sasa wanatishana, kila mmoja anatishia kutoa siri za mwenzake kibiashara. Wote wanapata tenda kubwa kutoka serikalini, wanavyozipata wanajua wao. Kinachotushangaza kila mmoja anasema atamuanika mwenzake,” alisema mfanyabiashara huyo aliyeomba jina lake lisitajwe.

Taarifa za ndani kutoka kwa watu walio karibu na Manji, zinadai kuwa mfanyabiashara huyo hakufurahishwa na jinsi mchakato wa upatikanaji zabuni hiyo ulivyoendeshwa, na sasa anakusudia kuvujisha katika vyombo vya habari taratibu zilizokiukwa katika mchakato wa utoaji wa zabuni hiyo.

Zinadai kuwa, Manji anajiandaa kuweka wazi jinsi sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004 ilivyokiukwa wakati wa mchakato wa utoaji zabuni hiyo.

Katika mradi huo, Jeetu ambaye anatajwa kuwa mwakilishi wa Kampuni ya Escort hapa nchini, yenye makao makuu yake nchini India, ambayo imeshinda zabuni hiyo, anadaiwa kuwashawishi maofisa wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ambalo limekabidhiwa jukumu la kuutekeleza mradi huo na serikali, kuipatia kampuni hiyo.

Habari hizo zimedai kuwa, Jeetu alifanikisha mpango huo baada ya kuwaunganisha maofisa kadhaa wa ngazi za juu wa JKT na watendaji wakuu wa Escort walioko India, ambao baada ya kuhakikishiwa kupewa zabuni hiyo, waliwaalika maofisa kadhaa wa JKT kwenda nchini humo kwa ajili ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa kazi ya kusambaza matrekta hapa nchini.

Taarifa zaidi zilidai kuwa, tayari baadhi ya viongozi wa juu wa JKT wamekwisha safiri hadi India kusaini mkataba huo.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa, Manji anapinga hatua ya viongozi wa JKT kwenda kusaini mkataba huo nchini India, ikizingatiwa kuwa baadhi ya watendaji wa serikali wamekwishalalamikiwa kwa kusaini mikataba inayohusu miradi ya kitaifa nje ya nchi.

Aidha, inadaiwa kuwa, baadhi ya habari zinazotarajiwa kusambazwa zitakuwa zinahoji ukiukwaji wa taratibu kwa kutoa zabuni hiyo pasipo kuitangaza kama sheria ya manunuzi ya umma inavyoelekeza, licha ya Baraza la Mawaziri kuujadili mradi huo na kutoa baraka kwa JKT kuutekeleza.

Kwa upande wa Jeetu, taarifa zinadai kuwa, anajiandaa kujibu tuhuma za aina yoyote zitakazotolewa katika vyombo vya habari, zikiwa na lengo la kuichafua Kampuni ya Escort au zinazohusu upatikanaji wa zabuni hiyo.

Baadhi ya maofisa wa serikali waliozungumza na Tanzania Daima Jumatano kuhusu suala hilo walieleza kuwa, serikali ina taarifa kuhusu jambo hilo na inalifuatilia kwa karibu ili kuhahakisha hakuna taratibu zinazokiukwa katika utekelezaji wa mradi huo.

Mmoja wa maofisa wa ngazi za juu serikalini aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake alieleza kuwa, anafahamu kuwa Serikali ya India ilitoa mkopo usiokuwa na riba, wa zaidi ya sh bilioni 50 kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kununulia matrekta, wakati Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed Shein, alipofanya ziara nchini humo mapema mwaka huu, kwa sharti la kulipwa katika kipindi cha miaka 10.

Alisema sharti jingine lililotolewa katika kutoa mkopo huo, linaitaka Serikali ya Tanzania kuhakikisha inanunua matrekta hayo kutoka kampuni za India na si vinginevyo.

Ofisa huyo alisema, serikali iliamua kuikabidhi JKT jukumu la kusimamia utekelezaji wa mradi huo ili kuondoa mazingira yoyote ya kutokea udanganyifu katika kuutekeleza.

Hata hivyo, alieleza wasiwasi wake iwapo kuna taarifa za baadhi ya maofisa wa JKT waliokabidhiwa jukumu la kusimamia utekelezaji huo, kuzungumza na mwakilishi wa Kampuni ya Escort hapa nchini (Jeetu), kisha wakaipa kampuni anayoiwakilisha zabuni hiyo bila kufuata taratibu.

“Hili jambo linaweza kuharibu kabisa sifa ya JKT kama litakuwa kweli, kwa sababu itakuwa ni kashfa kubwa kwa jeshi kukiuka taratibu za manunuzi ya umma. Ingawa kuna imani kuwa si rahisi mambo ya kijeshi kuchunguzwa, lakini hili liko wazi mno kwa sababu ni zabuni iliyo wazi iliyokuwa ikifuatiliwa na wafanyabiashara wengi, hivyo hao hao wanaweza kuwa wametoa siri za taratibu kukiukwa,” alisema ofisa huyo.

Waziri mmoja aliyezungumza na gazeti hili hivi karibuni, alisema suala hilo lilizungumzwa katika Baraza la Mawaziri na kupatiwa baraka zote za kulitekeleza. Aliongeza kuwa, anaamini hakuna taratibu zilizokiukwa.

Hata hivyo, alionya kuwa Baraza la Mawaziri linazo taarifa za mfanyabiashara mmoja maarufu kufanya mpango wa kutoa taarifa za uongo kuhusu mchakato wa upatikanaji zabuni hiyo kwa sababu ya kisasi cha kukosa zabuni hiyo.

Tanzania Daima Jumatano lilipowasiliana na Ofisa Habari wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Nadhifa Omary, ili kupata ufafanuzi wa suala hilo, alisema jambo hilo linaweza kuzungumziwa na waziri tu kwa sababu ya unyeti wake.

Alieleza zaidi kuwa, hawezi kulizungumzia kwa sababu yuko nje ya ofisi kwa mapumziko, hivyo hana maelezo ya kina ya kulitolea ufafanuzi.

Alipoulizwa, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga, Dk. Hussein Mwinyi, alisema analifahamu vizuri suala hilo na alilihakikishia gazeti hili kuwa, hakuna utata wowote katika utekelezaji wa mradi huo, isipokuwa linaweza kufanywa ajenda ya kuchafuana na watu ambao wana malengo binafsi na mradi huo.

“Ninalijua vizuri jambo hilo, tenda zilitangazwa na zikafunguliwa, nakuhakikishia. Mimi mwenyewe niliona kampuni kama 11 hivi zilizoomba zabuni hiyo, sasa kama kuna mtu anasema kulikuwa na kasoro, ni mambo ya wafanyabiashara kutaka kuchafuana tu kwa malengo binafsi waliyonayo katika mradi huo,” alisema.

Naye Manji alipotafutwa kupitia simu yake ya kiganjani ili kuzungumzia suala hilo, kwa mara kadhaa ilikuwa ikipokelewa na wasaidizi wake na kueleza ameweka utaratibu wa kutoongea na waandishi wa habari mpaka inapobidi.

CHANZO: Tanzania Daima

NILIWAHI KUANDIKA HUKO NYUMA KWANZA HUU WIMBO WA "KILIMO KWANZA" HAUNA TOFAUTI NA USANII WA "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA."NGONJERA ZA KISIASA ZINAZOHANIKIZWA NA KAULI-MBIU MWANANA HAZIWEZI KUMKOMBOA MTANZANIA KATIKA LINDI LA UMASIKINI UNAOMKABILI.BADALA YAKE,JITIHADA KUBWA ZINAHITAJIKA KATIKA KUPAMBANA NA UFISADI NA MAFISADI,VIKWAZO VIWILI VIKUU VYA MAENDELEO YETU.HILO HALIWEZEKANI CHINI YA UTAWALA WA CCM KWA VILE CHAMA HICHO NI KITALU MWAFAKA KWA MAZALISHO NA HIFADHI YA UFISADI NA UFISADI.

HAWA WAHINDI WAMEGEUZA TANZANIA KAMA SEHEMU YA MAJARIBIO YA KILA MADUDU YANAYOWAJIA KICHWANI.WAMENABAKA UCHUMI WETU HUKU TULIOWAKABIDHI DHAMANA YA KUULINDA WANAENDELEA KUWANYENYEKEA KUTOKANA NA NJAA YAOYA TENI PASENTI.

MWAKA WA HUKUMU 2010 UNAKARIBIA.USIREJEE MAKOSA YA 2005,PLEEEEEZ!

6 Oct 2009


NILIWAHI KUBASHIRI HUKO NYUMA KWAMBA KADRI 2010 INAVYOSOGEA NDIVYO TUTAVYOZIDI KUSHUHUDIA VITUKO.LEO HII MAKAMBA NAE AMEJIUNGA KATIKA VITA DHIDI YA UFISADI!HIVI SI BINADAMU HUYU ALIYEWATAKA WATANZANIA KUACHANA NA MIJADALA YA UFISADI KWA VILE BAADHI YA WAHUSIKA WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI?

HEBU MSIKIE ALIVYOGEUKA KINYONGA KATIKA HABARI HII HAPA CHINI:

Makamba ahimiza mapambano dhidi ya ufisadi

na Jacob Ruvilo, Kigoma

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusufu Makamba, amesema ufisadi unapaswa kupigwa vita na kila Mtanzania mzalendo, kwani umechangia kwa kiasi kikubwa kudidimia maendeleo ya nchi.

Makamba alisema hayo juzi kwenye semina ya viongozi wa CCM Jimbo la Kigoma Mjini iliyofanyika katika viwanja vya Lake Tanganyika.

Alisema suala la watu kujipatia mali kinyume cha utaratibu na kuhujumu nchi havina uhusiano wowote na CCM, kwani watuhumiwa wote hawakuagizwa na chama kufanya hivyo, bali ni hulka zao binafsi.

Makamba alifafanua kuwa suala la muumini wa dhehebu fulani kwenda kinyume na maadili au amri ya vitabu vya dini, hapaswi kulaumiwa sheikh au mchungaji, badala yake ni muumini husika ambaye mwisho wa siku ndiye atakayepata adhabu kwa Mungu.

Aidha, Makamba alisema suala la vyama vya upinzani kushika bango na kuidhihaki CCM kuwa ni mafisadi kutokana na viongozi wachache wasio waaminifu, halina maana, bali suala la umoja na mshikamano katika kupinga mafisadi hao ni jukumu la watu wote, ikiwamo CCM.

Mbali na hilo, Makamba alikemea baadhi ya viongozi wa chama hicho kutumia uwezo wao wa fedha kutoa rushwa ili kupita katika chaguzi mbalimbali kuwa ni moja ya upatikana wa viongozi mafisadi na wasiofaa kwa jamii.

Alisema Tanzania haikuandaliwa kutawaliwa na wenye nacho na kwamba hali hiyo inaweka tabaka la mwenye nacho na asiyenacho, hali ambayo isipoangaliwa kwa umakini suala la rushwa litabaki kuwa ndoto.


TATIZO LETU WATANZANIA NI UWEPESI WETU KUAMINI KILA KINACHOAHIDIWA.MWAKA 2005 MAKAMBA NA CCM YAKE WALITAMBUA HILO NA KUJA NA AHADI LUKUKI IKIWEMO ILE MAARUFU YA KULETA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.SASA WANASEMA KWAMBA SUALA LA MAISHA BORA LILIANZA ZAMA ZA MWALIMU NYERERE,PENGINE KATIKA KUKWEPA KUTUELEZA HAYO MAISHA BORA WALIYOAHIDI ILIKUWA NI KWA MAFISADI PEKEE AU...?MAANA KAMA SUALA HILO LILIASISIWA NA NYERERE BASI WANGETAMKA BAYANA WAKATI ZA KAMPENI ZA 2005 BADALA YA KUIFANYA KAULI-MBIU MUHIMU ILIYOWAZUGA WATANZANIA NA KUTOA USHINDI MKUBWA KWA CCM.

NI MUHIMU KWA WAPIGA KURA KUTAMBUA KUWA WANASIASA WETU WANAWEZA KUAHIDI LOLOTE ILI WAPATE KURA KAMA ILIVYOSANIFISHWA KWENYE WIMBO WA "NDIO MZEE" WA PROFESA JAY.

TUSIREJEE MAKOSA YA 2005,PLEEEEZ!

17 Sept 2009


HIZI SIO HARAKATI ZA SIASA BALI NI UTOTO.NA UTOTO HUU UNAENDELEA KWA VILE CHAMA TAWALA KINA IMANI YA KUTOSHA KUWA WANAOCHEZEWA SHERE (WAPIGA KURA) BADO WAKO USINGIZINI,NA KINACHOENDELEA (UTOTO HUO) NI SAWA NA NJOZI.

HEBU SOMA HII,KISHA TAFAKARI:

Makamba amfuata Spika Sitta Urambo, ampigia magoti

*ASEMA HANA UGOMVI NAYE, ASEMA ALIKUWA MLEZI WA NDOA ZA WANAYE

Na John Dotto, Tabora

KATIKA kile kilichoelezwa kwamba, ni kujisafisha mbele ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, CCM imesema ipo pamoja naye katika kutekeleza majukumu yake kama Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa CCM, Yusufu Makamba; ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kuondoa utata uliotokana na maazimio ya Halmashauri Kuu ya chama hicho ulioonyesha kuwa wabunge wanaopiga kelele dhidi ya ufisadi, wanakichafua chama na serikali yake.

Akizungumza na viongozi wa CCM wilaya ya Urambo kwenye mkutano wa ndani uliohudhuriwa na Spika Sitta, Makamba, alitumia muda mwingi kumsifia Sitta kwamba ni mtu muelewa, asiyetetereka na wala kuyumbishwa na mtu yeyote na kwamba anachokifanya ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho.

Makamba aliwaambia wanaCCM hao kwamba, hana chuki na Sitta, kwani hata alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alimkaribisha katika ndoa za wanawe na akapewa nafasi ya kuzungumza kama baba mlezi, heshima ambayo alisema hataisahau katika maisha yake.

Alisema wana CCM wanatakiwa kupuuza maneno ya watu wanaodai chama kina mgogoro na Spika, kwasababu hakuna kitu kama hicho na yote anayoyatekeleza kwenye Bunge ni kwa niaba ya chama chake.

Hata hivyo, baada ya kikao cha NEC, Makamba alikuwa mstari wa mbele kudai kuwa kikao kile kina uwezo wa kumuhoji mbunge yoyote hata Sitta kama anakwenda tofauti na chama.

Makamba alinukuliwa akisema NEC ni mama na akina Spika ni watoto hivyo ina mamlaka ya kuhoji mienendo yao.

Mara baada ya kikao cha NEC, Sitta alifanya ziara mkoani Tabora na kulalamika kwamba, CCM makao makuu wamewakataza viongozi wa chama hicho mkoani kumpokea.

Hatua ya Makamba kwenda Urambo kuhutubia na Sitta, inatafsiriwa kama njia ya kuweka mambo sawa na kufuta makovu ya huko nyuma baina yake na Spika.

Kwa upande wake, Sitta alimshukuru Makamba kwa kutembelea jimboni kwake na mkoa wa Tabora kwa ujumla.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika baada ya kikao cha ndani kumalizika, Makamba aliwahakikishia wananchi wa Urambo kwamba CCM kipo pamoja na mbunge wao Sitta, ndiyo maana wanatekeleza ahadi zote ikiwemo ujenzi wa barabara ya Urambo Kaliua mpaka Tabora Mjini.

Akizungumzia suala la ufisadi, Makamba alisema kuwa wanaCCM wote kuanzia ngazi ya matawi wanapaswa kuungana na wabunge wanaopiga vita ufisadi, kwani vita dhidi ya rushwa ni ya wanaCCM wote.

Alisema anakerwa na watu wanaosema CCM ni chama cha mafisadi kwani ufisadi wa mtu mmoja si wa CCM na akatoa mfano kuwa dhambi ya Mkatoliki mmoja si dhambi ya Askofu Kilaini wala kanisa lote.

Makamba alimaliza ziara yake jana mkoani Tabora na juzi alipokuwa akizungumza na viongozi wa CCM wakiwemo makatibu wote wa wilaya za Tabora kwenye ukumbi wa mikutano wa CCM mkoa, aliwalaumu viongozi hao kukaa kimya wakati wapinzani wanakishambulia chama hicho kwa kukipakazia maneno machafu.

Aliwataka waamke na kukipigania chama na kuacha kukaa kimya na kusubiri makao makuu ama Makamba kujibu mashambulizi.

Baada ya kikao cha Nec kilichofanyika Dodoma mwezi uliopita, Makamba na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chilligati kwa nyakati tofauti walisema CCM imeunda kamati ya watu watatu, inayoongozwa na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi kuwachunguza wabunge wenye tabia ya kuishambulia serikali nje ya vikao vya chama.

Habari za ndani ya kikao hicho ambazo baadaye zilivuja kwa vyombo vya habari, zilieleza kuwa Nec ilimweka kitimoto Spika Sitta kwa madai kuwa anaruhusu mijadala inayokichafua chama na serikali, huku baadhi ya wajumbe wakishinikiza anyang'anywe kadi ya CCM kwa madai kuwa anawapa uhuru bungeni watu wanaoishambulia serikali kwa ufisadi.

Hata hivyo, mwanzoni mwa wiki hii baada ya hotuba ya Rais, Chilligati alisema chama hicho hakina ugomvi wala uadui na wabunge wake wanaoongoza vita dhidi ya mafisadi nchini.

Kabla ya hapo, Mwenyekiti wa Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita ambaye alisemekana kumwandama Spika Sitta katika kikao cha NEC na akamwita faru aliyejeruhiwa anayetakiwa kumalizwa kabla hajasababisha madhara zaidi, naye alibadili msimamo na kuwaunga mkono wapiganaji wa ufisadi pamoja na Spika Sitta kwamba, wanatekeleza ilani ya CCM, hivyo wanastahili kuungwa mkono.

Mabadiliko haya ya siasa ndani ya chama hiki tawala na mfululizo wa matukio ya aina hiyo likiwemo la Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile ambaye amekaririwa katika vyombo vya habari akisema hana ugomvi na Mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe, anayesemekana kuwa ni hasimu wake kisiasa.

CHANZO: Mwananchi


NA HAWA NDIO TUNAOTARAJIA WAREJEE KUTUTAWALA 2010!

8 Sept 2009


RAIS Jakaya Kikwete leo ataanza staili mpya ya kuwasiliana moja kwa moja na wananchi kwa njia ya simu na barua pepe, akisikiliza hoja, kujibu maswali na kupata maoni yao juu ya mustakabali wa nchi , Ikulu imesema jana.

Kikwete, ambaye alizungumza na taifa kwa mara ya mwisho Juni 11 alipozungumza na wazee wa mkoani Dodoma, atafanya mazungumzo hayo ya dakika 90 kwa njia ya televisheni kuanzia saa 2:30 usiku wakati atakapopokea simu na kusikiliza maswali, ushauri, maoni na kujibu moja kwa moja.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais inaeleza kuwa katika staili hiyo ya aina yake, Rais Kikwete pia atapokea ushauri kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu (sms) kutoka kwa watazamaji na ujumbe wa barua pepe, ikiwa ni mpango wa kusikiliza matarajio ya wananchi katika jitihada zao za kuboresha maisha yao kwa kujiletea maendeleo.

"Rais atatumia aina mpya ya kuwasiliana na wananchi kwa kusikiliza hoja zao, kwa kujibu maswali yao, kusikiliza ushauri wao na kupata maoni juu ya mambo yanayohusu mustakabali wa nchi yetu, serikali yetu na maendeleo yetu," inaeleza taarifa hiyo.

"Mazungumzo hayo yatakachukua muda wa dakika 90 kuanzia saa mbili unusu usiku (saa 2:30 usiku) hadi saa nne kamili usiku."

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, chini ya mpango huo rais atazungumza moja kwa moja kupitia vituo vya redio na televisheni vya Shirika la Utangazaji (TBC) na vyombo vingine vya utangazaji nchini.

Kurugenzi hiyo ya Mawasiliano Ikulu, ilifafanua kwamba "mbali na TBC, televisheni nyingine za ITV, TVZ, Mlimani TV, Tumaini TV na Channel Ten zinatarajiwa kuonyesha mazungumzo hayo".

Taarifa ya kurugenzi hiyo imevitaja vituo vitakavyotangaza moja kwa moja mazungumzo hayo kuwa ni TBC-Taifa, Sauti ya Tanzania Zanzibar (STZ), Radio Mlimani, Radio Clouds, Radio Tumaini, na Radio Uhuru.

Ikulu pia imetaja namba zitakazotumika kwa ajili ya maswali, maoni, hoja, ushauri utakaotolewa moja kwa moja kupitia TBC. Namba hizo ni +255-22-2772448, +255-22-2772452 na +255-22-2772454.

Pia kwa watakaotaka kutuma ujumbe mfupi wa simu watatakiwa kutuma kwenda namba 0788-500019, 0714-591589 na 0764-807683, huku wale watakaotaka kutumia barua pepe watatuma kwenda anuani ya [email protected].

Hii ni mara ya kwanza kwa Rais Kikwete kutumia aina hiyo ya mazungumzo na wananchi baada ya viongozi wengine waliomtangulia kutumia hotuba za mwisho wa mwezi kwa kupitia redio na televisheni na pia mikutano na wazee au na waandishi wa habari.

Kikwete anaanza utaratibu huo akionekana kufuata nyayo za aliyekuwa Rais wa Philippines, hayati Gloria Macapagal Arroyo, ambaye amekuwa alikuwa na utaratibu wa kuruhusu wananchi kupiga simu na kuuliza maswali.

Lakini Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ana utaratibu tofauti. Kiongozi huyo wa muda mrefu wa Uganda ana kawaida ya kuingilia mijadala inayoendeshwa moja kwa moja na vituo vya redio na kujibu tuhuma dhidi ya serikali yake au kutoa ufafanuzi.

Rais wa Marekani, Barack Obama husikiliza maoni, ushauri na kujibu maswali ya wananchi kupitia barua pepe.

Utaratibu huo mpya utamfanya rais apokee maswali ya aina tofauti na kumuwezesha kujua kero hasa za wananchi tofauti na vilio vya wanasiasa, hali ambayo itafanya muda wa dakika 90 kuwa mfupi kuweza kukidhi utashi.

Katika hotuba yake ya Juni 11, Rais Kikwete alizungumzia athari za mtikisiko wa uchumi na kutangaza mpango mkubwa wa kutenga Sh1.7 trilioni kwa ajili ya kunusuru uchumi.


CHANZO: Mwananchi

HIVI MPAKA LEO KIONGOZI WETU HAJUI MUSTAKABALI WA TAIFA LETU HADI AOMBE MAONI KUTOKA KWA WANANCHI?HIZO DAKIKA TISINI ZINATOSHA KWELI KUMFAHAMISHA KUWA NCHI INAELEKEA PABAYA?
JE INA MAANA ZIARA ZA KILA KUKICHA ZA VIONGOZI WETU HAZIJAFANIKIWA KUWAFAHAMISHA KERO ZA WANANCHI NI ZIPI?
NAULIZA HAYO KWA VILE HUU NI MWAKA WA 4 TANGU AWAMU YA NNE IINGIE MADARAKANI.SASA KAMA HADI LEO HAWAFAHAMU KINACHOIANGAMIZA TANZANIA....
LAKINI KUBWA ZAIDI YA KWAMBA LICHA YA UFINYU WA MUDA ULIOTOLEWA KWA WAULIZA MASWALI/ATOA USHAURI,NA LICHA YA UKWELI KWAMBA UTARATIBU HUO UNAWAPENDELEA WACHACHE WENYE ACCESS NA SIMU AU KOMPYUTA (KUTUMA BARUA-PEPE),KUNA UHAKIKA GANI KUWA KERO ZITAKAZOTOLEWA ZITAFANYIWA KAZI?KAMA USHAURI WA KITAALAM WA KAMATI YA AIKNA MWAKYEMBE KUWA WASHIRIKI WA UTAPELI WACHUKULIWE HATUA NA HADI LEO "BADO WANAPETA" KERO NA VILIO VYA WALALAHOIKWENYE SIMU/SMS/E-MAIL ZITABADILISHA KITU GANI?
KADRI 2010 INAVYOJONGEA NDIVYO KADRI VITUKO VINAVYOONGEZEKA.NA TUTASHUHUDIA MENGINE MENGI.

26 Jun 2009


Hili ndio "BUNGE LENYE MENO"!Juzijuzi mbunge mmoja wa CCM kaomba Mungu alilaani Baraza la Mawaziri kwa kushindwa kutimiza majukumu yake.Mwingine kadai serikali ina ugonjwa na inahitaji maombezi (na kwa kawaida magonjwa yanayohitaji maombezi ni yale yasiyotibika kama vile ukimwi,nk).Jana mbunge mwingine wa chama hicho tawala amewafananisha mawaziri na mbwa.Na pengine moja ya mambo yatakayokumbukwa zaidi katika historia ya bunge letu tukufu ni jinsi kikao hiki cha bajeti kinavyoonekana "mwiba mkali" kwa mawaziri,at least according to walio mahiri katika kuripoti pasipo kusoma kati ya mistari (reading between the lines).

Sina maneno ya huruma kwa baadhi ya wabunge hawa wa CCM.Ni wanafiki wanaohangaika kutumia vizuri nafasi hizi za mwisho mwisho kujitengenezea mazingira ya kurejea bungeni hapo mwakani.Lakini ili haki itendeke,ni vema kuwatofautisha wanafiki hawa kwa makundi.Kuna kundi la wabunge waliojitokeza mapema (kabla hata ya joto la uchaguzi wa mwakani halijaanza kupanda) kukemea ufisadi na vitendo vingine vinavyokwaza maendeleo ya taifa letu.Sio siri kwamba wabunge kama Selelii,Kimaro,Killango,Mwambalaswa,Mwakyembe na wengineo wamejitokeza kuwa sauti adimu ndani ya CCM dhidi ya ufisadi.Na tunafahamu vituko wanavyofanyiwa na watu walewale wanaopaswa kuwaunga mkono.

Kundi la pili ni la wababaishaji walio njia panda; upande mmoja hawana nia ya dhati ya kupambana na ufisadi au pengine ni sehemu ya mfumo unaodumisha ufisadi,upande mwingine wanafahamu fika kwamba miongoni mwa ajenda za uchaguzi mkuu ujao ni ufisadi na namna wawakilishi wetu walivyoshiriki katika mapambano dhidi ya ufisadi.

Pia kuna makundi mengine mawili: la kwanza linajumuisha wababaishaji wanaokwenda bungeni kwa vile tu ndio mahala pao pa kuchuma shs 7,000,000/= za mshahara kiulaini.Hawachangii hoja,hawaongei lolote japo si mabubu,wapo wapo tu.Kuwepo au kutokuwepo kwao bungeni hakutambuliki kwa vile wanaongeza tu idadi ya wabunge.Kundi la pili ni la watetezi wa ufisadi.Hawa ni wepesi wa kuomba mwongozo wa Spika kila maslahi yao au ya wadau wenzao wa ufisadi yanapoguswa.Nadhani mmesikia "Dokta" Mzindakaya alivyotumia Maandiko Matakatifu kutetea ufisadi .Ila hawa wanaocheza na vitabu vya Mungu,nadhani ndio wanaostahili kulaaniwa zaidi kwani wamevigeuza kama manifesto za usanii wao wa kisiasa!

Uzuru wa makundi haya mawili ya mwisho-la tatu na la nne-ni kwamba angalau yanajumuisha wabunge tunaofahamu wanaposimamia.Aidha ni wazembe na mabubu wasioongea (aidha kwa aibu ya kuongea,au "heri mie sijasema",au uzembe tu) au ni watetezi wa mafisadi.Hawa si wanafiki as such kwa vile wameji-identify kwetu kuwa ni viumbe wa namna gani.

Tofauti kati ya makundi hayo ni ndogo mno contrary to inavyosomeka na kusikika kwenye vyombo vya habari.Hapa nataka kuzungumzia makundi mawili ya mwanzo-la kwanza na la pili.Hawa wote ni wana CCM,na kwa namna yoyote ile hawawezi kujitenganisha na matatizo yanayosababishwa na chama hicho tawala.Na hili si la kufikirika kwa sababu tayari wengi wa wabunge wa kundi la kwanza wamekuwa wakikumbana na kadhia mbalimbali kutokana na msimamo wao dhidi ya ufisadi,na guess what,kadhi hizo ni kutoka kwa wenzao ndani ya CCM.

Mawaziri wanaolaaniwa na kufikia hatua ya kuitwa mbwa wanatoka CCM pia.Hii sio vita ya wenyewe kwa wenyewe kama inavyoweza kutafsiriwa kiuzembe.Huu ni unafiki,period.CCM isingefika hapo ilipo laiti "wapambanaji hawa" wangekuwa na mkakati wa dhati wa kuleta mabadiliko ya kweli.Wanachofanya muda huu ni cha kibinafsi zaidi kuliko kitaifa.Wanaweza kurudi bungeni hapo mwakani baada ya wapiga kura wao "kuzugika" na CVs za wawakilishi wao tangu 2005 hadi 2010.Kurudi kwao bungeni kutapelekea CCM kuendelea kuwa yenye wabunge wengi bungeni,na hivyo kupelekea kuendelea kwa haya tunayopigia kelele kila siku.

Siamini kama kuna mkakati kwa Selelii na wenzake kuleta mageuzi ndani ya CCM.So far,kelele zao hazijasaidia kukitenganisha chama hicho na ufisadi,implying that kelele zao zimebaki kuwa kelele tu.Wana options mbili: waendelee kupiga kelele lakini wabaki kuwa sehemu ya chama kinachohusishwa na ufisadi au wajondoe ndani ya chama hicho na hivyo kubainisha kuwa kuwa kwao ndani ya CCM ilikuwa ni sehemu tu ya maisha yao ya kisiasa lakini cha muhimu zaidi kwao ni Tanzania na ustawi wa Tanzania.Yes,si lazima kuwa mbunge wa CCM ili kupata fursa ya kupigania maslahi ya taifa.Mifano hai ipo;Dkt Slaa,Zitto Kabwe,nk sio wabunge wa CCM,lakini sote tunafahamu michango yao katika kupambana na ufisadi.

Unafiki wa wabunge hao wa CCM unasababishwa na kitu kimoja kisicho na msingi: UBINAFSI WA KISIASA.Ni hivi,kwa CCM,umoja na mshikamano ndani ya chama hicho ni muhimu zaidi kuliko umoja na mshikamano wa taifa.Na hilo ni matokeo ya chama hicho kuamini kwamba ni chenyewe tu kinachoweza kudumisha mshikamano na umoja wetu.Kwa lugha nyingine,kimebinafsisha uwezo,dhamira,jitihada na nguvu za Watanzania zaidi ya milioni 35 ambao si wanachama wa chama hicho (takwimu za karibuni zinaonyesha idadi ya wanachama wa CCM ni takriban milioni 4 tu).Japo ni kweli kwamba chama hicho kimetoa uongozi uliosaidia kudumu kwa amani na mshikamano huo,Watanzania wenyewe ndio waliofanya kazi ya msingi zaidi kufanikisha hilo.Upendo na upole wetu (ambao mara nyingi umeishia kutumiwa vibaya na wanasiasa walafi) ndio sababu kuu ya kwanini tumeendelea kubaki kisiwa cha amani (kwa maana ya kutokuwa vitani).

Ni ubinafsi wa kisiasa unaopelekea CCM kuweka mbele maslahi ya kisiasa badala ya maslahi ya taifa.Sote tumeshuhudia mara kadhaa wabunge wa chama hicho tawala wakiitisha vikao "vya kuwekana sawa" kila zinapojiri hoja nzito bungeni.Kuwekana sawa kwa maslahi ya nani?Hivi cha muhimu ni hoja ipite tu au ipite ili ilete mabadiliko chanya kwa wananchi?

Lakini ili upate mfano sahihi zaidi kuhusu ubinafsi wa wabunge hawa ni pale Dkt Slaa alipotamka bayana kwamba mishahara ya wabunge ni mikubwa mno kulinganisha na hali halisi ya uchumi wetu.Kwa umoja wao (huku wakipata sapoti kutoka kwa wabinafsi wengine waliojificha kwenye vyama vya upinzani) walimzomea Dkt Slaa na kumzongazonga kana kwamba kawatukana.Hivi ina maana wabunge hawa wanaotuzuga kuwa wanatetea maslahi yetu hawaelewi kuwa wakati wao wanazawadiwa takriban shilingi 7,000,000/= mwezi (wastani wa shilingi laki 230,000/= kwa siku sawa na takriban shs 10,000/= kwa saa) takriban Watanzania 36,000,000 wanaoishi kwa chini ya shilingi 3000/= kwa siku?

Hadi kufikia tamati yake na mabiloni kadhaa kutumika,kikao hiki cha bajeti kitashuhudia kila aina ya vituko kutoka kwa wanafiki hawa.Ukidhani hizo dua dhidi ya mawaziri na "matusi" ya kuwaita mbwa ndio hatua kali kabisa,subiri usikie "makombora" zaidi.Na kama kawaida ya vyombo vyetu vya habari,kurasa zitapambwa na maneno mazito kama "Bunge moto juu","Wabunge wachachamaa",na ubabaishaji mwingine kama huo.Lakini pamoja na yote hayo,makadirio ya wizara za mawaziri wanaoombewa dua mbaya na kuitwa mbwa yatapitishwa na wabunge haohao wanaotuzuga kuwa "wana hasira na mawaziri".

21 Feb 2009

ULE MCHEZO WA KUIGIZA KUHUSU "KUTOWEKA" KWA LIYUMBA BADO UNAENDELEA.LATEST EPISODE INAHUSU TAKUKURU KUTANGAZA DONGE NONO KWA ATAYEFANIKISHA KUKAMATWA KWA NDUGU LIYUMBA.

Na Boniface Meena

TAASISI ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini(Takukuru) imetangaza kutoa donge nono kwa mtu yeyote atakayefanikisha kukamatwa kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi (DPA) wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba ambaye hadi hivi sasa hajulikani halipo.

Wakati Takukuru ikifikia hatua hiyo, tayari kuna wananchi ambao wametoa taarifa kwenye baadhi ya vyombo vya habari kuwa wanaweza kutoa taarifa za alipo Liyumba. Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani alisema wameamua kutangaza doge nono ambalo hakulitaja ni kiasi gani cha fedha ili wananchi wasaidie kupatikana kwa Liyumba. Alisema Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru Dk Edward Hoseah ,anakaribisha watu ambao wanaweza kutoa taarifa au kusaidia alipo Liyumba ili aweze kukamatwa.

"Kuna wananchi tumesikia wako tayari kuisaidia Takukuru, tunawakaribisha na Dk Hoseah anawakaribisha ili waweze kutusaidia na donge nono litatolewa kwa atakayesaidia kukamatwa kwa Liyumba," alisema Kapwani.

Wakati Takukuru ikifikia maamuzi hayo Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imesema kama Takukuru itahitaji msaada wa Wizara hiyo kumtafuta Liyumba iko tayari kutoa msaada huo.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili Waziri wa Wizara hiyo, Lawrance Masha alisema wakipewa maombi ya kumtafuta Liyumba, watasaidia kumtafuta kwa kuwa wote ni Serikali. "Juzi nilitoa tamko kuwa hatujaletewa maombi ya kumtafuta, lakini Takukuru wakituletea tutafanya hivyo, kwa kuwa sisi ni Serikali," alisema Masha.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilifuta dhamana ya Liyumba Februari 19 na kutoa amri ya kuwakamata wadhamini wake ambao walikamatwa siku hiyohiyo na baadaye kuachiwa. Wadhamini hao ni wafanyakazi wa BoT Benjamin Nduguru (mhasibu wa benki hiyo) na Agaterus Oto (Afisa Usalama wa ndani wa benki hiyo).

Hata hivyo, licha ya mahakama kufuta dhamana kuwakamata wadhamini hao, ilitoa amri ya kumtafuta na kumkamatwa Liyumba.Liyumba pamoja na aliyekuwa Meneja Miradi wa BoT, Deogratius Kweka wameshitakiwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia vibaya madaraka yao katika mradi wa ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo na kuisababishia hasara serikali jumla ya Sh221 bilioni.

Liyumba alipewa dhamana na Hakimu Mkaazi wa Kisutu, Hadija Msongo kwa kutumia hati ya nyumba yake iliyoko Mbezi Juu, jijini Dar es Salaam yenye thamani ya Sh800 milioni, ambayo hata hivyo ililalamikiwa na upande wa mashitaka kwamba imetolewa katika mazingira tata kwa kuwa haijafikisha kiwango cha Sh50 bilioni walizotakiwa kutoa

Juzi Wakili wa serikali, Prosper Mwangumila aliileza mahakama kwamba, Liyumba bado hajapatikana. Hakimu alisema amri ya kumkamata Liyumba bado inaendelea na ya kuwakamata wadhamini imesitishwa hadi kesi itakapotajwa Februari 24, mwaka huu.

Katika hatua nyingine Mawakili wanaomtetea mtuhumiwa huyo waliulalamikia upande wa mashitaka kwa kitendo chake cha kuwanyanyasa ndugu wa mtuhumiwa huyo ambapo walidai kuwa uliwanyang’anya baadhi ya mali zao.

Mmoja wa mawakili hao wa utetezi, Majura Magafu aliiomba mahakama kutoa amri ya kuutaka upande wa mashitaka kuacha kuinyanyasa familia ya Liyumba na kwamba warudishe gari ya mmoja wa wadhamini ambayo waliikamata. Akijibu hoja hiyo, Hakimu Msongo aliutaka upande wa utetezi kama una maombi yoyote kuyapeleka kwa utaratibu wa mahakama kwa kuwa juzi haikuwa tarehe ya kesi.

Wakati akitoa dhamana hiyo Februari 17, mwaka huu, Hakimu Msongo alisema mshitakiwa huyo, atakuwa nje kwa dhamana ya Sh882 milioni wakati mahakama inajiridhisha na hati nyingine zilizopingwa na upande wa mashitaka. Alisema mshitakiwa atatakiwa kutimiza masharti ya dhamana ya kiasi kilichobaki cha Sh54,417,344,800.23 endapo mahakama itabaini kuwa hati hizo zina kasoro.

Hata hivyo baada ya kutolewa maamuzi hayo Wakili wa serikali Justus Mulokozi alisema hawajaridhika na maamuzi yaliyotolewa na kwamba watakaa kuyajadili na kuyatolea maamuzi. Upande wa mashitaka ulipinga kupokelewa kwa hati 10 kati ya 11 zilizowasilishwa mahakamani hapo na upande wa utetezi kwa madai kuwa zina kasoro, zikiwemo za kuwa na mali zisizokuwa za kudumu kama mbuzi, ng’ombe na kuku.

Siku mbili baada ya mtuhumiwa huyo kuachiwa huru na mahakama kutokana na kutimiza masharti, mahakama ilitoa amri ya kukamatwa tena jambo lilosababisha wadhamani wake kushikiliwa kwa muda na kisha kuachiwa.

Liyumba na Kweka walipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza , Januari 27, mwaka huu kwa tuhuma za kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia hasara serikali kiasi cha Sh 221 bilioni. Kweka bado hajapata dhamana.



TATIZO KUBWA LA VYOMBO VYETU VYA HABARI NI KURIPOTI HABARI AU MATUKIO BADALA YA KWENDA NDANI ZAIDI NA KUCHUNGUZA YALIYOJIFICHA KATI YA MISTARI.KWA MFANO,KWANINI HATUJIULIZI SABABU WA WADHAMINI WA LIYUMBA KUKAMATWA KISHA KUACHIWA?JE WADHAMINI HAO NAO "WAKITOWEKA" SI ITAMAANISHA "KIFO CHA ASILI" CHA KESI HIYO?

HIVI HATUWEZI KUJIULIZA SABABU ZA HAKIMU KUTOA DHAMANA KWA MSHTAKIWA JAPO DHAMANA HIYO ILIKUWA NA MAPUNGUFU?NAFAHAMU NI HAKI KWA MSHTAKIWA KUPATIWA DHAMANA LAKINI SHARTI ATIMIZE MASHARTI YA DHAMANA HIYO.

WIZI MTUPU!

20 Feb 2009

Picha kwa hisani ya KENNEDY.
HUU NI USANII WA MCHANA MWEUPE.UNFORTUNATELY,VYOMBO VYETU VYA HABARI VIMEKUWA MAKINI ZAIDI KATIKA KURIPOTI MATUKIO BADALA YA KUYAFANYIA UCHUNGUZI HABARI.WELL,HII NDIO BONGO BWANA.


PENGINE UTASEMA NI MAPEMA MNO KUWA PESSIMIST,LAKINI YAYUMKINIKA KUAMINI KWAMBA NI VIGUMU SANA KWA MTUHUMIWA MWENYE UWEZO WA KIFEDHA KUHUKUMIWA KWA KOSA LOLOTE ALILOTENDA,HATA KAMA KUNA USHAHIDI WA WAZIWAZI.


HIVI INAINGIA AKILINI KWELI KWAMBA TUHUMA DHIDI YA LIYUMBA NI PAMOJA NA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA KATI YA MWAKA 2001 HADI 2006?KAMA HUJAELEWA MANTIKI YA SWALI LANGU NI KWAMBA HUU NI MWAKA 2009.SO,INA MAANA MATUMIZI HAYO MABAYA HAYAKUWEZA KUGUNDULIKA KWA KIPINDI CHOTE HICHO CHA MIAKA MITANO?HIVI BENKI KUU HAIFANYIWI UKAGUZI WA MAHESABU KILA MWAKA?IF SO,KWANINI WAKAGUZI HAO WASIULIZWE KUHUSU TAARIFA ZA MWAKA 2001-2006?OK,TUACHANE NA WAKAGUZI.VIPI KUHUSU INTERNAL SECURITY NDANI YA BENKI KUU?HAWA WATU WANALIPWA KWA AJILI YA KAZI GANI IWAPO FEDHA ZILIKUWA ZIKITUMIKA KWA MIAKA MITANO MFULULIZO PASIPO WAO KUSHTUKA.


PENGINE JIBU LA SWALI HILO LA MWISHO LINAWEZA KUPATIKANA KWENYE TAARIFA KWAMBA MMOJA YA WADHAMINI WA LIYUMBA NI AFISA USALAMA WA BENKI HIYO.DOES THIS MAKE ANY SENSE?AFISA USALAMA WA BENKI ANAMDHAMINI MTUHUMIWA ANAYAYESHTAKIWA KWA UBADHIRIFU WA FEDHA KATIKA BENKI HIYOHIYO!?


HAYA TWENDE KWENYE SUALA ZIMA LA DHAMANA.KAMA LIYUMBA ALIKUWA HAJATIMIZA MASHARTI YOTE YA DHAMANA KWANINI BASI HAKIMU ALITOA DHAMANA HIYO?INAELEZWA KWAMBA DHAMANA ILIYOTOLEWA ILIKUWA NA MAPUNGUFU YA MAMILIONI KADHAA.HALAFU ETI KWA USANII,WAENDESHA MASHTAKA WALINUKULIWA WAKIDAI HAWAJARIDHISHWA NA DHAMANA HIYO.


HUU NI MCHEZO WA KUIGIZA.NA NDIO MAANA UKISOMA MAGAZETI KADHAA UTAGUNDUA STORI ZINALINGANA.HII BUZZ IS MOST LIKELY ENGINEERED BY SOMEONE WHO'S BEHIND ALL THIS FRAUD.WANATANGAZA KWA SAUTI KUWA LIYUMBA KATOWEKA (JAPO TUNAAMBIWA ETI PASSPORT YAKE ILIKUWA IMEZUILIWA) ILI BAADAE WATANZANIA WASAHAU KAMA WALIVYOSAHAU KUHUSU BALLALI,MAJAMBAZI WA RICHMOND,MAFISADI WA KAGODA,NK.

WANAFANYA HIVI KWA VILE WANAFAHAMU BAYANA KUWA WATANZANIA NI WAPOLE,HAWAKAWII KUSAMEHE NA KUSAHAU MABAYA.

HII NDIO BONGO YETU!AU KAMA WANAVYOSEMA SIKU HIZI, WIZI MTUPU

7 Dec 2008


UTATA wa zilipo fedha zilizorejeshwa na kampuni zilizoiba fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), umeendelea kuigubika nchi, baada ya kubainika kuwa fedha hizo hazijaingizwa kwenye mfuko ulioelekezwa na Rais Jakaya Kikwete wakati akilihutubia Bunge, Agosti 21 mwaka huu.

Fedha hizo ambazo ni zaidi ya sh bilioni 70, zilitakiwa ziende Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB), ambapo zingefunguliwa dirisha maalumu, lenye jukumu la kutoa mikopo kwa wakulima ambao kwa miaka mingi wamekosa fursa hiyo.

Uchunguzi wa Tanzania Daima Jumapili, umebaini kuwa fedha hizo zimehifadhiwa katika akaunti maalumu ambayo mpaka hivi sasa maelezo yake bado yamegubikwa na utata, kwa sababu kila ofisa wa Wizara ya Fedha na Uchumi aliyeulizwa juu ya akaunti hiyo, ameshindwa kutoa jibu linaloeleweka.

Tangu awali baadhi ya watu walionyesha wasiwasi wao kuhusu urejeshaji wa fedha hizo kama ni kweli zimerejeshwa au ilikuwa mbinu ya kisiasa ya serikali kutaka kuzima joto la wananchi, wapinzani na wahisani waliotaka fedha hizo zirejeshwe na watuhumiwa wafikishwe katika mikono ya sheria.

Watu hao waliweka wazi msimamo wao kuwa fedha hizo hazikurejeshwa bali ilikuwa ni janja ya serikali ili waweze kupata misaada kutoka kwa wafadhili ambao awali walitishia kutochangia bajeti ya serikali mpaka majibu sahihi na hatua za wizi wa EPA zichukuliwe.

Shinikizo hilo inadaiwa ndilo lililomfanya Rais Jakaya Kikwete kuamua kutengua uteuzi wa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Daudi Ballali, pamoja na kuunda timu ya uchunguzi chini ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, baada ya mkaguzi wa nje, Ernst & Young, kuthibitisha kuwapo kwa wizi katika akaunti hiyo, unaofikia kiasi cha sh bilioni 133.

Mkurugenzi wa Benki ya Rasilimali (TIB), William Mlaki, hivi karibuni alikaririwa na vyombo vya habari kuwa fedha hizo hadi sasa hawajazipokea.

Alisema inawezekana serikali inajiandaa kuwapelekea fedha hizo ambazo Rais Jakaya Kikwete alishaweka wazi dhamira ya serikali yake kuzipeleka TIB ili ziwasaidie wakulima.

“Mpaka sasa fedha za EPA, bado hazijaingia kwetu na si jukumu letu kuulizia fedha hizo zitakuja lini, kazi yetu ni kuzipokea na kuratibu zoezi la utoaji mikopo kwa wakulima,” alikaririwa Mlaki.

Kauli hiyo ya Mlaki, inazidisha utata kuhusu ukweli wa urejeshaji wa fedha za EPA ambazo uchotwaji wake unahusishwa na matumizi ya uchaguzi mkuu uliopita.

Inadaiwa kuwa mbinu za kuchota fedha hizo, zilifanywa na viongozi wa juu wa Serikali ya Awamu ya Tatu kwa kushirikiana na mwanasiasa na mfanyabiashara maarufu nchini ili zikisaidie Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu uliopita.

Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni, tena kwa nyakati tofauti, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba na Mkurugenzi wa Uchumi na Fedha, Amos Makala, wamekanusha chama chao kuhusishwa na wizi huo.

Mfanyabiashara huyo ndiye anayeaminika alikuwa mmiliki halali wa Kampuni ya Kagoda Agriculture Limited iliyochota sh bilioni 40, lakini hadi hivi sasa hajafikishwa mahakamani au kutajwa mbele ya umma.

Kutotajwa kwa mfanyabiashara huyo kunatokana na ukweli kuwa ndiye anayejua siri yote ya Kagoda na viongozi waliomuagiza kuzichota fedha hizo na hata matumizi yake pamoja na kujua nani kapata kiasi gani na kwa kazi gani.

Kwa hali ilivyo, Kagoda ndiyo kampuni inayoonekana kuitikisa nchi kama wamiliki wake watatajwa na kufikishwa mahakamani, kwani hawatakubali kushitakiwa peke yao bila kuwataja viongozi waliowatuma kufanya wizi huo.

Hali hiyo ndiyo iliyomfanya aliyekuwa Waziri wa Fedha, Zakhia Meghji, kutoa ufafanuzi kwa umma kuwa fedha zilizochotwa zilitumika kwa mambo ya usalama na si ufisadi kama ambavyo baadhi ya wanasiasa, akiwemo Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa, walivyokuwa wakisema.

Msumari wa moto juu ya utata wa urejeshwaji wa fedha za EPA na ufisadi hivi karibuni ulishindiliwa na mfanyabiashara maarufu nchini na mwachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jafar Sabodo, ambaye alisema serikali inafanya mchezo wa kuigiza na haina nia thabiti ya kutatua matatizo ya rushwa.

Sabodo ambaye ni rafiki wa karibu wa marehemu Mwalimu Nyerere na mfadhili wa mfuko wa taasisi ya Mwalimu Nyerere na CCM, alifikia hatua ya kusema yuko tayari kukisaidia chama chochote cha upinzani katika uchaguzi ujao, kuiangusha CCM madarakani, kwa madai kuwa imeshindwa kuondoa tatizo la rushwa nchini.

Wachambuzi wa masula ya siasa wanadai kupandishwa mahakamani kwa mawaziri wawili ya serikali iliyopita Basil Mramba (Fedha) na Daniel Yona ((Nishati na Madini), ni mpango wa kuwasahaulisha wananchi juu ya mwenendo wa kesi ya EPA, hasa kuendelea kufikishwa mahakamani kwa watuhumiwa wengine.

Mpango huo uliasisiwa kutokana na joto la wananchi kutaka wamiliki wa Kampuni ya Kagoda inayohusishwa na wafanyabiashara, wanasiasa maarufu na wakongwe nchini, kuzidi kushika kasi kiasi cha kumfanya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuweka bayana kuwa joto hilo likizidi, wamiliki wake watajulikana.

Wadadisi hao wanaendelea kubainisha kuwa mpango huo kwa kiasi fulani, umefanikiwa, kwani watu walihamisha macho na masikio yao kutoka EPA na kuhamia kwa Yona na Mramba, ambao wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salam kwa kosa la kuisababishia hasara serikali ya zaidi ya sh bilioni 11.7, kwa kutoa misamaha ya kodi kiholela katika sekta ya madini.

Wakati wingu zito likiwa limetanda kuhusu mahali zilipo fedha za EPA, kuna tetesi kwamba fedha hizo ndizo zilizotumika kulipa madai ya walimu ambao miezi miwili iliyopita walitishia kugoma nchi nzima kushinikiza kulipwa fedha zao za malimbikizo zinazofikia sh bilioni 16.


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.