17 Mar 2009


By Mkinga Mkinga

The Government is assessing the impact of the global financial crisis on the Tanzanian economy.

The deputy minister for Finance and Economic Affairs, Mr Omar Yusuf Mzee, told The Citizen yesterday by phone that officials from his ministry had been dispatched to regions to talk to stakeholders on problems facing them as a result of the global financial crisis.

"I am in Kigoma on a similar mission and my colleague [deputy minister Jeremiah Sumari) is in southern regions," he said.

The assessment is aimed at collecting crucial information on the crisis. He said his tour would take him to Kigoma, Tabora, Singida and Dodoma regions while Mr Sumari would visit Lindi and Mtwara regions to gather similar information.

"We need to know the real picture when we call stakeholders to a national meeting to discuss the crisis.During the meeting we will focus on how we can help businesses which have been affected," he said.

He said a national roundtable with chief executive officers of various firms to discuss the situation would be held soon after completing the assessment.

Bank of Tanzania (BoT) Governor Benno Ndulu, did not say what the Government could do to shore up businesses amid the crisis.

"I cannot say that the Government will offer stimulus packages to affected businesses. But we are aware of the situation and we are planning something for our local entrepreneurs," he said. Prof Ndulu said BoT was closely following the developments.

He noted that so far there was no indication that local banks would face difficulties in the near future as a result of the global crunch.

"People should go on with their activities; there is no need to worry as we are closely following the developments here and abroad. In case of any serious problem, we will issue an alert immediately," he said.

Recently, Finance and Economic Affairs minister Mustafa Mkulo did not rule out direct Government intervention, as members of the business community called for a state plan to save them from collapse.

He said during the forthcoming roundtable meeting, the Government would discuss with CEOs and draw up a joint strategy to deal with the problem.

"Our intervention will be within the limitations of the budget and it is my hope, as the Finance minister, that our engagement will be effected as soon as possible. It should be before the conclusion of the budget proposals," he said.

"If employers are thinking of retrenching workers, this will be discussed to see the best way in which the Government could assist," said Mr Mkulo.
Many countries are offering stimulus packages to private companies.

Such countries include the United States where the financial crunch started, sending financial institutions crumbling.The ministry has dispatched its team to regions at a time when businesses are calling for quick plans to remedy the situation.

The Association of Tanzania Employers (ATE) has confirmed that it had received urgent appeals for assistance from three companies. ATE executive secretary Aggrey Mlimuka warned of difficult times ahead unless the Government intervened.

The Tanzania Horticultural Association bemoans a 50 per cent business slump.It has urged the Government to support the small-scale growers and supply chains using a portion of the money that President Jakaya Kikwete pledged to give to agriculture.

It has also asked for the rescheduling of loans through commercial banks with BoT's intervention.
SOURCE: The Citizen

EACH REGION HAS A REGIONAL COMMISSIONER,REGIONAL ADMINISTRATIVE SECRETARY,REGIONAL PLANNING OFFICER,etc,etc,...AND SO ARE THE DISTRICTS.DOES THIS DECISION TO DESPATCH OFFICIALS FROM THE MINISTRY SUGGEST THAT THOSE AT REGIONAL/MUNICIPAL/DISTRICT LEVEL HAVE NO IDEA ABOUT THE GLOBAL FINANCIAL CRISIS THAT THEY CAN'T FURNISH THE GOVERNMENT WITH THE DATA NEEDED FOR THE ECONOMIC ASSESSMENT,OR THEY ARE TOO DUMB TO TALK TO STAKEHOLDERS IN THEIR RESPECTIVE ADMINISTRATIVE AREAS, OR IT IS ALL ABOUT THE NOTORIOUS PER DIEM SYNDROME AT THE TIME WHEN WE SERIOUSLY NEED TO KEEP OUR EXPENDITURE IN CHECK...!?

16 Mar 2009












KIPINDI CHA INSIDE AFRICA CHA CNN WIKI HII KINA SEGMENT KUBWA KUHUSU TANZANIA.MOJA YA YALIYONIVUTIA KATIKA KIPINDI HICHO NI MAHOJIANO KATI YA RIPOTA WA CNN,DAVID MCKENZIE, NA MSANII WETU NAKAAYA SUMARI.MWANADADA ALIJIELEZA CONFIDENTLY.I WISH NINGE-RECORD VIDEO LAKINI KWA SABABU ZILIZOKUWA NJE YA UWEZO WANGU NILIAMBULIA PICHA HIZO HAPO JUU.UKIPATA WASAA UNAWEZA KUCHEKI VIDEO YA SEGMENT HIYO KWENYE TOVUTI YA CNN-INSIDE AFRICA PINDI WATAKAPOIWEKA (HADI MUDA HUU BADO HAIJAWEKWA).PENGINE BAADA YA KUANGALIA SEGMENT NZIMA UNAWEZA KUBAKI NA MASWALI,LIKE I DID, KUHUSU ASSESSMENT YA RIPOTA HUYO WA CNN KUHUSU MWENENDO WA UCHUMI WETU.



13 Mar 2009


BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), limeibua upya hoja za kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na Jumuiya ya nchi za Kiislamu Duniani (OIC), kwa kuitaka serikali kutafakari kwa kina na hekima juu ya kuridhia kuanzishwa kwa vyombo hivyo.

Kuibuka tena kwa hoja hizo kumekuja miezi michache baada ya Rais Jakaya Kikwete kufunga mijadala hiyo iliyokuwa ikielekea kuwagawa wananchi kwa misingi ya kidini.

Hoja hizo zimeibuliwa juzi kwenye Baraza la Maulid na Naibu Katibu Mkuu wa Utawala wa Bakwata, Suleiman Lolila, ambaye aliitaka serikali iangalie upya na kwa hekima na kama inawezekana iharakishe masuala hayo mawili.

“Tunaipongeza serikali kwa hekima kubwa na jitihada inayoitumia katika kushughulikia masuala ya Mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na OIC, Waislamu wanangoja kwa hamu na shauku kubwa ridhaa ya serikali, Inshallah, tunaiombea serikali ipate wepesi katika masuala haya maridhawa.

“Tunawaomba Waislamu wadhamirie kwa dhati katika suala hili la OIC na mahakama ya kadhi kwa kutokuruhusu mwanya wowote wa mifarakano miongoni mwetu, kwani mifarakano itakaribisha mgawanyiko na utengano miongoni mwa jamii,” alisema Lolila.

Naibu Katibu Mkuu huyo, akisoma risala ya Bakwata mbele ya Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, alisema ili kuridhiwa kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na OIC kuna hitaji utulivu wa hali ya juu miongoni mwa waumini wa dini zote mbili (Waislamu na Wakristo) ili kuipa serikali nafasi ya kufanya maamuzi ya busara kwa lengo la kuimarisha umoja wa kitaifa miongoni mwa jamii.

Suala la uanzishwaji wa mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na OIC, mwishoni mwa mwaka jana lilizua mjadala mpya nchini, baada ya kufika bungeni na kutishia kuwagawa wabunge kwa itikadi za kidini.

Oktoba mwaka jana katika hotuba yake, Rais Kikwete, hakutaka kuweka wazi ni lini Tanzania itaridhia kujiunga na OIC pamoja na uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, na badala yake aliwatuliza wananchi kwa kuwaambia wavute subira wakati serikali ikilifanyia kazi suala hilo kwa masilahi ya umma.

Rais Kikwete aliweka bayana kuwa ni mapema mno kuanza kutoa uamuzi wa masuala hayo, kwa kuwa bado utafiti haujakamilika pamoja na serikali kutotoa uamuzi wa mwisho, hivyo hakuna sababu kwa wananchi kulumbana.

11 Mar 2009


Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi amepigwa kofi na mmoja wa watu waliohudhuria Baraza la Maulid wakati akihutubia katika ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam jana.Mwinyi, ambaye alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika Baraza hilo, alikutwa na masaibu hayo baada ya kijana aliyefahamika kwa jina la Ibrahim Said (26) kwenda jukwaani akajifanya fundi na kumpiga kofi la nguvu Rais mstaafu.

Kijana huyo aliyekuwa miongoni mwa umati uliohudhuria baraza hilo, aliinuka wakati Rais mstaafu akizungumzia masuala ya Ukimwi na kwenda hadi jukwaani na kujifanya anarekebisha vyombo vya kupaza sauti vikiwemo na vya televisheni alivyokuwa akitumia kuhutubia.Kijana huyo ambaye alikuwa amevalia suruali ya khaki na shati jeupe, alitumia sekunde kadhaa kujifanya kutengeneza vifaa hivyo akiwa mbele ya Mwinyi na ghafla alimzaba kibao. Kitendo hicho kilisababisha viongozi waliokuwa jukwaani, kusimama ghafla na wanausalama kuingilia kati na kumkata mtama kijana huyo katika juhudi za kumdhibiti asiendelee kuleta madhara.

Miongoni mwa watu waliokuwa katika jukwaa kuu ni pamoja Sheikh Mkuu Mufti Issa Shaaban Simba, Kaimu Mufti Suleiman Gorogosi na Waziri Mkuu mstaafu, Rashidi Kawawa ambao wote walibaki katika mshangao. Baada ya wanausalama kumdhibiti kijana huyo waumini walimwagika na kuanza kumtwanga kwa ngumi na mateke na hivyo wanausalama ikabidi wabadili majukumu na kuanza kumhami. Kutokana na hekaheka hizo shughuli za hotuba zilisimama kwa dakika kama nne.

Pamoja na vurumai hizo, wanausalama walifanikiwa kumuingiza kijana huyo katika gari aina Land Cruiser yenye namba za usajili T 531 AUB na kuondolewa katika viwanja vya Diamond Jubilee na kufikishwa Kituo cha Polisi cha Selander Bridge. Kwa mujibu wa Polisi ambaye hakutaka kutaja jina lake kituoni hapo, alisema katika kumhoji, kijana huyo (Said) alijitambulisha kuwa ni mkazi wa Mabibo Farasi, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa hizo zilizopatikana kituoni hapo, Said ni mzaliwa wa Mkoa wa Dar es Salaam aliyehitimu kidato cha Sita mwaka juzi katika Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Tabora. Kijana huyo katika maelezo yake, amejitambulisha kuwa ni Mwalimu wa masomo ya ziada katika Kituo cha Ngome Kongwe, kilichoko Mabibo. Hata hivyo, haikuweza kufahamika sababu za kijana huyo kufanya kitendo hicho kutokana na waandishi kushindwa kupata nafasi ya kuzungumza naye.

Awali, kabla ya kijana huyo kumpiga kofi kiongozi huyo mstaafu wa kitaifa, Mwinyi alikuwa akiwaasa Waislamu kuepukana na ngono zembe zinazochangia ongezeko la Ukimwi. Alisisitiza kwamba ugonjwa huu umekaa mahali pabaya na kuwasihi waumini kuwa ni jukumu la kila mmoja kujilinda. Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Mufti Gorogosi, alisema amekuwa akimuona kijana huyo katika mikutano ya dini.

"Hata jana (juzi) katika Maulid usiku alikuwepo, hivyo nashindwa kuelewa kama ana akili nzuri au la," alisema Gorogosi. Alimwomba Rais mstaafu awasamehe Waislamu kwa tukio hilo. Wakati huo huo, Joseph Lugendo anaripoti kwamba Mwinyi amewataka viongozi wa dini nchini kujenga daraja la upendo, baina ya waumini wa dini tofauti badala ya kugeuka kuwa kuta zenye kuwagawa Watanzania katika misingi ya dini.

Aliwataka viongozi hao, wakiwamo masheikh na mapadri, kujenga daraja la upendo na masikilizano baina ya waumini wa dini mbalimbali, ili kuendeleza amani na mshikamano uliopo nchini. Akihutubia mkesha wa Maulid ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (SAW) usiku wa kuamkia jana Dar es Salaam, Mwinyi alionya viongozi hao wasigeuke kuwa kuta zisizopenyeka zitakazogawa Watanzania kwa misingi ya dini zao.

"Tupo hapa Waislamu na wasio Waislamu kwa kuwa ushirikiano Tanzania ni jadi na mila yetu, sisi huungana kusherehekea siku zote, Waislamu husherehekea na Wakristo siku ya Pasaka na Krismasi na wao hutuunga mkono kwenye Idd zote."Hili ni jambo jema linaloondoa chuki baina ya dini na kuleta mshikamano, mimi napendezwa sana na mwenendo huu na ninatoa mwito kwa mapadri na masheikh kuliendeleza," alisema Mwinyi.

Alisema hawezi kuisemea dini ya Kikristo kwa kuwa haifahamu, lakini miongoni mwa mafunzo yao ni kuwa na subira na kusamehe na kuongeza kwamba mafundisho yao (Wakristo), yamewataka anayepigwa kofi shavu moja ageuze na lingine lipokee kofi la pili. "Huu ni mfano wa kuepusha shari. Lakini na sisi Waislamu pia Mungu katutaka kuwatendea mema na uadilifu ambao hawakupigana nasi wala hawakututoa majumbani kwetu, hakika Mungu huwapenda waadilifu," alisema Mzee Mwinyi huku akinukuu baadhi ya aya kuongeza nguvu katika hoja yake hiyo.

Alisema msingi wa kuishi kwa amani, huanzia katika kaya mpaka jamii na ndio uliosababisha Tanzania kuwa kisiwa cha amani kilichozungukwa na nchi zenye vurugu na kutaja kuwa dini zimechangia kuunda msingi huo. Hata hivyo, alisema kauli hiyo haina maana kuwa nchi zisizo na amani hazina dini, bali malezi ya Watanzania yaliyotekelezwa na viongozi waliotangulia, pia yamechangia sehemu ya amani iliyopo. "Wazee wetu walitandika zulia la utamaduni wa kuishi kwa amani, upendo na utulivu ... katika hali hii ya utu uzima wangu, inanituma kuwausia vijana, tutunze utulivu huu.

"Katu tusiruhusu uondoke tusiwape wenzetu sababu ya kutupa majina mabaya, ya mjahidina na magaidi, vijana nakuusieni tena tusitoe mwanya huo, tumekuwa tukipewa majina na maadui wa nje. "Wanasema dini yetu ni ya fujo, ni wakati wa kushikamana na si wa kulumbana na kama mnajadiliana si mbaya ila kuwepo na staha, heshima na pasiwepo kejeli, ubabe wala dharau dhidi ya dini nyingine," alisema Mwinyi.


CHANZO: Habari Leo


AJALI HUTOKEA,LAKINI LINAPOKUJA SUALA LA ULINZI WA VIONGOZI AJALI ZINAPASWA KUZUIWA KWA GHARAMA YOYOTE ILE.TULISIKIA YALIYOJIRI MBEYA HIVI KARIBUNI AMBAPO KUNDI LA WANANCHI WALIURUSHIA MAWE MSAFARA WA RAIS JK.KWA MTAZAMO MPANA,TUKIO HILO LINGEWEZA KUTAFSIRIWA KAMA SEHEMU YA MAPUNGUFU KATIKA ENEO ZIMA LA ULINZI WA VIONGOZI WETU.NASEMA HIVYO KWA VILE KUNA WATU WENYE JUKUMU LA KUHAKIKISHA USALAMA WA NJIA AU ENEO ATAKALOPITA KIONGOZI,NA NI KWA UHAKIKA KUTOKA KWAO ONLY,NDIPO MSAFARA AU ZIARA YA KIONGOZI ITAENDELEA KAMA ILIVYOPANGWA.THANKS GOD,HAYO MAWE HAYAKUMDHURU YEYOTE,NA PENGINE LA KUSHUKURU ZAIDI NI KWAMBA YALIKUWA MAWE TU NA SIO SILAHA.
SASA TUNASIKIA MZEE MWINYI NAE AMEKUMBWA NA ZAHAMA KAMA INAVYOELEZWA KATIKA HABARI YA HAPO JUU NA PICHANI HAPO CHINI.INAFAHAMIKA KWAMBA ULINZI WA VIONGOZI HUWA MGUMU ZAIDI KWENYE MIKUSANYIKO AU MIKUTANO YA HADHARA LAKINI KWA KAWAIDA UGUMU HUO UNAPASWA KUWA CHANGAMOTO YA MAFANIKIO YA SHUGHULI NZIMA YA KIONGOZI HUSIKA.TUNAPASWA KUMSHUKURU MUNGU KWAMBA ALICHOPIGWA NACHO MZEE MWINYI NI KIBAO TU,LAKINI KAMA TUKIENDELEA NA "BUSINESS AS USUAL" KUNA SIKU ITAKUWA TINDIKALI AU KITU KINGINE CHENYE MADHARA.KAMA MTU HUYO ALIWEZA KUPIGA KIBAO,NI DHAHIRI KWAMBA ANGEWEZA HATA KUCHOMA KISU AU KURUSHA RISASI.KUMKATA MTAMA MHUSIKA WAKATI AMESHAFANYA MADHARA NI SAWA NA KUSOMA RAMBIRAMBI YENYE MANENO MAZURI WAKATI MTU AMESHAPOTEZA UHAI:INALIWAZA LAKINI HAISAIDII.

(Aliyemzaba kibao Mzee Mwinyi akidhibitiwa baada ya tukio.Wajuzi wa mambo ya ulinzi wa viongozi wanaweza kuafikiana nami-kutokana na picha hii-kwamba kuna mapungufu LUKUKI.Picha ya tukio kwa hisani ya MICHUZI Jr)

NI ISHARA NYINGINE KWAMBA KUNA MAPUNGUFU MAHALA FLANI.YAYUMKINIKA KUHISI KWAMBA MAPUNGUFU HAYO NI MATOKEO YA MAZOWEA.KUNA WATU WANATEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA MAZOWEA,KWAMBA KWA VILE JANA ILIFANYIKA HIVI BASI HATA LEO ITAFANYIKA HIVYOHIVYO.DHANA YA "HOPE FOR THE BEST EXPECT THE WORST" INAONEKANA KAMA POROJO TU KWA WANAOENDEKEZA MAZOWEA.

TUSIFIKE MAHALA TUKALEWESHWA NA "AMANI NA UTULIVU".KUNA MENGI YANAYOJIRI HUKO MITAANI YANAYOASHIRIA KWAMBA KIWANGO CHA FRUSTRATIONS KWENYE UMMA KINAONGEZEKA.FOR THAT MATTER,KUNA UMUHIMU MKUBWA WA KUENDESHA MAMBO KULINGANA NA HALI HALISI BADALA YA KUONGOZWA NA HISIA AU IMANI ZISIZOZINGATIA REALITY.

IT CAN BE DONE...BUT IF AND ONLY IF SOMEONE OUT THERE PLAYS THEIR PART.



10 Mar 2009

The winner of a pancake-eating contest has dropped dead while accepting his prize for gorging on 43 of the banana and cream stuffed desserts. Boris Isayev, 48, from west Russia died on stage moments after winning the competition to mark the end of Butter Week.

The contest, which took place in the town of Chernyakhovsk, was part of festivities to celebrate Maslenitsa, the last week before the period of Lent starts. According to local traditions, meat, fish, dairy products and eggs are forbidden during Lent, as well as dancing and parties.Witnesses described Mr Isayev as "the most active participant in the contest" adding that he "ate all the types of pancakes on offer and won fairly".

The witness added: "He had really enjoyed the pancakes but then he started foaming at the mouth and went down like a sack of stones.

"People have fainted during the contests before."

Medics tried to revive Mr Isayev after he collapsed while collecting his prize on stage. The exact cause of death is not clear but doctors believe he choked after a piece of pancake got lodged in his throat. Celebrations are said to have continued after Mr Isayev's body was taken away in an ambulance.


SOURCE: Sky News

8 Mar 2009

Bonyeza HAPA kwa habari na video.

5 Mar 2009

SAKATA la ununuzi wa mitambo ya ufuaji umeme wa dharura ya kampuni ya Dowans Tanzania Limited, jana lilimgusa spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta na kuamua kutoa tamko kali la kuitahadharisha serikali dhidi ya azma yake ya kutaka kuinunua mitambo hiyo yenye utata.

Spika Sitta pia ameonya kuwa mkasa wa kampuni tata ya Richmond Development (RDC) LLC uliotikisa kiasi cha kusababisha Edward Lowassa awajibike kwa kujizulu wadhifa wake wa waziri mkuu, lisifufuliwe upya kwa kutumia Dowans, ambayo ilirithishwa mkataba wa miaka miwili wa kufua umeme wa dharura.


Richmond ilishinda zabuni ya kufua umeme wa dharura kwa njia iliyojaa utata kabla ya matatizo ya usajili wake kuzua maswali mengi na kusababisha Dowans warithishwe mkataba huo mwaka 2006.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Sitta alieleza nafasi ya Bunge katika kuisimamia na kuishauri serikali katika utekelezaji wa majukumu yake, huku akitaka ushauri wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini wa kuizuia serikali isinunue mitambo hiyo uheshimiwe.

Sitta pia alisema Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma haikustahili kufuatwa katika kutaka ushauri kuhusu suala hilo kwa kuwa suala hilo lipo kwenye Kamati ya Nishati na Madini na kwamba kama kuna sababu mbadala, wasi ililazimika kuliwasilisha upya kwa kamati hiyo.

"Naitahadharisha serikali juu ya athari zinazoweza kujitokeza iwapo itaamua kuendelea na mchakato wa ununuzi wa mitambo ya Dowans kwa kupuuza ushauri uliotolewa na Kamati ya Nishati na Madini," alisema Spika Sitta.

Alisema: "Isisahaulike kwamba Dowans ni kampuni iliyopatikana kwa kurithishwa mradi na kampuni ya Richmond katika mazingira yenye utata ambao hadi leo ni kitendawili."

Spika Sitta alifafanua kuwa uhalali wa utaratibu wa Richmond kumkabidhi mradi Dowans ulitiliwa mashaka na kamati teule ya Bunge, na kuongeza kuwa Dowans na Richmond ni kama kitu kimoja.

"Dowans na Richmond ni mtu na binamu yake na si vigumu kukubali kuwa bado wao ni wabia hadi sasa: Pamoja na yote mkasa wa Richmond haufai kufufuliwaaa upya kupitia Dowans," alisisitiza Sitta.

Aliongeza kuwa kama kweli Tanesco na serikali inazo Dola 69 milioni za Kimarekani (sawa na Sh90 bilioni za Kitanzania) ambazo ni bei ya mtambo wa Dowans, ingezitumia fedha hizo kama sehemu ya malipo ya kununua mitambo mipya. Alisema Tanesco ingetafuta ushauri kutoka Mamlaka ya Ununuzi Serikalini (PPRA) ili taratibu za dharula zitumike kununua mitambo mipya kukabiliana na "dharula inayotabiriwa".

Sitta alihoji mantiki itakayotumiwa na Tanesco kutaka kununua mitambo ambayo inamilikiwa na kampuni ambayo imeishtaki kwenye Baraza la Usuluhishi ambalo makao yake makuu yako Paris, Ufaransa.

"Gharama za mitambo na gharama za kuikodi haviwezi kuepukwa kuwa ni sehemu ya shauri lililo Paris," anasema Sitta. "NI kwa mantiki ipi kesi baina yao iendelee na hapo hapo mdaiwa (Tanesco) anunue mitambo kutoka kwa mdai (Dowans.

"Tanzania ilikuwa ikilipa Dowans shilingi za Kitanzania milioni 152 kwa siku (Dola 120,000) sawa na Dola 42 milioni kwa mwaka).

"Pamoja na yote, mkasa wa Richmond haufai kufufuliwa upya kupitia Dowans. Tanesco/serikali waelekeze nguvu zao katika njia mbadala za kulipatia taifa umeme wa dharura, badala ya njia hii ya Dowans iliyojaa utata."

Kuhusu mvutano kati ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Mashirika ya Umma na ile ya Nishati na Madini, Spika Sitta amsema si sahihi kwa kamati yoyote ya Bunge isiyo ya sekta husika, kutoa maoni yake hadharani na kuishawishi jamii kwamba Bunge lina ushauri unaopingana kuhusu suala husika.

"Si sahihi kwa Kamati yoyote ya Bunge isiyo ya sekta kutoa maoni yake hadharani na kujenga taswira kwa umma kwamba, Bunge lina ushauri unaokinzana kuhusu suala lililo mbele yake. Kamati nyingine, haina budi kupitisha ushauri na maoni yake kwenye kamati ya kisekta," alisema Sitta.

Zitto Kabwe, ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, alikaririwa na vyombo vya habari akieleza msimamo wa kamati yake kuunga mkono Shirika la Umeme (Tanesco), kuinunua mitambo ya Dowans kwa maelezo kuwa hatua itasaidia kulinusuru taifa katika janga kubwa la kukosa umeme na kwamba sheria ya manunuzi si msahafu, hivyo inaweza kubadilishwa.

Lakini Kamati ya Nishati na Madini, ambayo mwenyekiti wake ni William Shelukindo, inapinga hatua hiyo ikieleza kuw ainakiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma, inayokataza serikali kununua vitu ambavyo tayari vimetumika.

Alisema ushauri kwa serikali kuhusu Tanesco kununua au kutonunua mitambo ya Dowans ulikwishatolewa kwa Wizara ya Nishati na Madini na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini Desemba 14 mwaka uliopita.

"Huo ndiyo ushauri rasmi na sahihi wa Bunge ninaoutambua. Kwa msingi huo hoja ya kuzikutanisha Kamati hizi mbili (ya Nishati na Madini na ya Hesabu za Mashirika ya Umma) ili kurejea uamuzi au maoni yaliyokwishatolewa na Kamati inayohusika, haina msingi," alisema Sitta.

Alisema mkondo rasmi wa ushauri kwa serikali uliokusudiwa kwenye Ibara ya 63 (2) ya katiba ikisomwa na pamoja na kanuni za Bunge za mwaka 2007 ni kupiti Bunge zima au kamati zake za kisekta kila kamati na sekta yake.

Wakati Spika Sitta akibainisha msimamo wake na wa Bunge, mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba ameunga mkono ununuzi wa mitambo hiyo huku akisema kauli ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa jana inaweza kukwamisha mchakato wa ununuzi wa mitambo hiyo.

Lipumba alisema katika mfumo wa utawala bora wakati kamati za bunge zinazohusika na mambo hayo na bodi za mashirika zipo, rais hapaswi kujiingiza mapema katika mijadala.

“Katika mfumo wa utawala bora ambao una kamati za bunge zinazohusika na sekta ya umeme na manunuzi, kwa rais kujiingiza kunaweza kuwa ni kikwazo cha mchakato mzima wa ununuzi wa mitambo,” alisema Profesa Lipumba.

Alifafanua kuwa, sheria ya manunuzi ya Serikali ina upungufu kwa kuwa inalazimisha ununuzi wa mitambo mipya, jambo ambalo haliwezekani kwa nchi zinazoendelea kama Tanzania.

“Ununuzi wa mitambo ya kibiashara katika sekta ya biashara huwezi kulazimisha ununuzi wa mitambo mipya hususan katika nchi zinazoendelea kama ya kwetu. Jambo la msingi ni kuangalia uwezo wa mitambo katika kufanya kazi na si kwamba ni mipya au mikongwe,” alifafanua Lipumba na kuongeza:

“Sheria yetu ya manunuzi ni nzuri na inafaa sana kwa kununua vitu vya huduma za serikali, kama magari na vifaa vingine.”

Aliitaka Tanesco kuwa wazi kwa kuwa ni wao waliosema mitambo hiyo hawaitaki hivyo kuamuwa kuvunja mkataba na Dowans iweje leo wanageuka na kusema mitambo hiyo ni mizuri na kuitaka serikali iinunuwe.

“Tanesco walituambia kuwa mitambo hiyo hawaitaki na walivunja mkataba na Dowans, sasa inakuaje leo wanageuka na kusema kwamba mitambo hiyo ni mizuri na inunuliwe kwa ajili ya kuzalishia umeme? Tunahitaji uwazi zaidi kutoka Tanesco,” alihoji Profesa Lipumba.

Naye Stephen Menad ambaye ni mshauri wa masuala ya nishati na mazingira, alisema hakuna kitu kipya kwenye mitambo hiyo ya Dowans hivyo isinunuliwe na badala yake itafutwe mipya ili kuondoa mvutano baina ya wananchi na serikali.

Mussa Hassan, mkazi wa jijini Dar es Salaam ambaye ni mfanyabiashara, alisema ni aibu kwa serikali kula matapishi na kwamba viongozi wasisahau yaliyotokea wakati mitambo ya Richmond ilipokuja na mwisho wake kuwaweka pabaya viongozi waliokuwa serikalini.

Anthony Chambi, ambaye ni mfanyabiashara katikati ya jiji la Dar es Salaam, alisema hataki kusikia kuhusu mitambo hiyo kwa kuwa tayari ilishaiabisha serikali. Alisema anasikia kuna kesi Ufaransa kuhusu mitambo hiyo kitu kinachomshangaza kwa nini serikali inataka kununua mitambo ambayo ina kesi.
CHANZO: Mwananchi
BIG UP,MHESHIMIWA SPIKA.
BINAFSI HADI MUDA HUU SIELEWI HAO WANAOTAKA MITAMBO YA DOWANS INUNULIWE WANA AJENDA GANI!NACHANGANYWA ZAIDI NAPOSIKIA WATU KAMA ZITTO KABWA NA PROFESA LIPUMBA NAO WAKIPIGA DEBE MITAMBO YA DOWANS INUNULIWE.HUU NI UNAFIKI WA MCHANA KWEUPE.WHY?BECAUSE KUNUNUA MITAMBO HIYO NI KUHALALALISHA UJAMBAZI WA DOWANS NA KAKA YAKE RICHMOND.HIVI INAINGIA AKILINI KWELI PALE TAPELI ANAPOKUUZIA MALI FEKI KISHA UKAMKALIA KOONI MPAKA AKAKIRI KUWA KWELI ALICHOKUUZIA NI FEKI,HALAFU UKAISHIA KUONGEZA FEDHA KUNUNUA MALI HIYO FEKI!?
I WOULD ONLY SUPPORT MATUMIZI YA MITAMBO YA DOWANS LAITI INGEKUWA IMETAIFISHWA (NA SIJUI KWANINI HADI MUDA HUU HAIJATAIFISHWA...WE MISS YOU BABA WA TAIFA).ETI AKINA KABWE WANASEMA TUWEKE MBELE UTAIFA KWANZA!UTAIFA KWANZA KWA MANUFAA YA AKINA RICHMOND?HAWA WAMEINGIZWA MKENGE NA VITISHO VYA TANESCO KUWA ETI NCHI IKO HATARINI KUINGIA KIZANI!YALEYALE YA RICHMOND!
WIZI MTUPU!

Picha kwa hisani ya Mjengwa
MWAKA 2006,MANISPAA YA TEMEKE ILITANGAZA AZMA YAKE YA KULIBORESHA SOKO LA TEMEKE.LAKINI KATIKA HALI YA KUSTAAJABISHA,KUNA TAARIFA KWAMBA SASA SOKO HILO LIMEUZWA KWA MWEKEZAJI.KWA MWENENDO HUU,SI AJABU SIKU YA SIKU MTU AKAAMKA NA KUKUTA MTAA ANAOISHI UMEUZWA KWA MWEKEZAJI.

4 Mar 2009

A controversial Italian doctor known for his work allowing post-menopausal women to have children has claimed in an interview to have cloned three babies who are now living in eastern Europe.

"I helped give birth to three children with the human cloning technique," Severino Antinori, a prominent gynaecologist, told Oggi weekly in an interview to appear Wednesday."It involved two boys and a girl who are nine years old today. They were born healthy and they are in excellent health now."He did not provide proof of his claims, but said cells from the three fathers, who were sterile, allowed the cloning to be carried out.

The women's egg cells were impregnated in a laboratory through a method called "nuclear transfer," he said.Antinori, who became famous after allowing a 63-year-old woman to have a child in 1994, said "respect for the families' privacy does not allow me to go further."He added that the method used was "an improvement" over the technique used to clone Dolly the sheep in 1996.

Reminded by the journalist that such cloning is prohibited in heavily Catholic Italy, the doctor said he preferred to "speak of innovative therapies" or "genetic recoding" rather than cloning.Two weeks ago, Antinori sparked controversy by announcing that he would artificially impregnate a woman whose husband is in an irreversible coma following a brain tumour.It would be the first procedure of its kind in Italy if successful.
SOURCE: AFP

3 Mar 2009

RAIS Jakaya Kikwete amesema ana majina ya watu wa kitengo cha maktaba cha Bandari ya Dar es salaam wanaofanya ufisadi unaolikosesha taifa mamilioni ya fedha na kuahidi kuyakabidhi kwa wahusika ili washughulikiwe. Kikwete alisema hayo jana baada ya kufanya ziara ya kushitukiza kwenye Bandari ya Dar es salaam kukagua utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa Januari 15 mwaka huu kwa wakuu wa Mamlaka ya Bandari (TPA).

Alisema kitengo cha maktaba kimekuwa kikifanya mchezo mchafu bandarini hapo kwa kushirikiana na wasafirishaji na kwamba, vibarua vya watu wa kitengo hicho viko hatarini.

“Waambieni watu wa kitengo cha maktaba kuwa mchezo wao unajulikana na orodha ya majina yao inajulikana, lakini bado kuwaumbua tu,” alisema Kikwete baada ya kumaliza ziara yake.

“Ndugu zangu sitawataja hadharani wala kwenye magazeti, bali nitakachofanya nitawaletea orodha ya majina, muwafukuze kazi. Kama wameshindwa kazi tutaleta watu wengine ambao wako tayari kufanya kazi kwa uaminifu.”

Alisema watu hao wamekuwa wakiwasiliana na wasafirishaji na kufanya ujanja wakati wa kujaza fomu za makontena yanayoingia nchini kwa kuandika mizigo tofauti na ile iliyomo ndani ya makontena hayo, ili yasipitishwe katika mashine ya uchunguzi ...ENDELEA

CHANZO: Mwananchi

HIVI KAMA MAJINA YA MAFISADI YANAJULIKANA (NA KINACHOSUBIRIWA NI "KUWAUMBUA") KWANINI WASICHUKULIWE HATUA?WAZIRI MWENYE MAMLAKA NA BANDARI YUKO WAPI NA ANAFANYA NINI?MKURUGENZI NA BODI YA BANDARI WANAFANYA NINI?NA,HIVI HATUA MWAFAKA DHIDI YA MAFISADI NI KUWAUMBUA AU KUWAFIKISHA MBELE YA VYOMBO VYA SHERIA?

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.