24 Mar 2009


NAKUOMBA SOMA HABARI MBILI ZIFUATAZO KISHA TUJADILI DHANA YA KULAZIMISHA UWAJIBIKAJI.KWA KIFUPI,KATIKA HABARI YA KWANZA,PAMOJA NA MAMBO MENGINE,DR SLAA ANAONYESHA KUWA CHADEMA INA USHAHIDI WA KUTOSHA KUIHUSISHA CCM NA WIZI WA EPA.KATIKA HABARI YA PILI,MWANASHERIA TINDU LISSU ANAMTAKA MKUU WA MKOA WA SINGIDA,MHESHIMIWA KONE,AOMBE RADHI HADHARANI KUTOKANA NA MADAI KUWA ALIWATUKANA HADHARANI BAADHI YA WANANCHI ANAOWAONGOZA.MJADALA UTAKAOFUATA BAADA YA HABARI HIZO UNAANGALIA MANTIKI YA DR SLAA NA CHADEMA KUENDELEA KUTUELEZA KWAMBA WANA USHAHIDI WA KUTOSHA UNAOIHUSISHA CCM NA UFISADI WA EPA,LAKINI KIONGOZI HUYO NA CHAMA CHAKE WAMEKUWA KANA KWAMBA WANATINGISHA KIBERITI VILE...KWA MAANA KWAMBA KAMA USHAHIDI UPO,KWANINI WASIFUNGUE KESI MAHAKAMANI KWA NIABA YA WANANCHI BADALA YA KUENDELEA KUDAI USHAHIDI TUNAO,USHAHIDI UPO...IRONICALLY,TINDU LISSU,MWANASHERIA ANAYEWATETEA BAADHI YA WAKAZI WA SINGIDA DHIDI YA MH. KONE,SIO TU NI MWANASHERIA WA CHADEMA BALI PIA NI MIONGONI MWA VIONGOZI WAANDAMIZI WA CHAMA HICHO.

ANYWAY,HEBU SOMA KWANZA HABARI HUSIKA

Chama tawala chaambiwa kuacha kutisha wananchi kuhusu ufisadi

Na Mussa Juma, Same.

KATIBU mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amemtaka katibu mwenezi wa CCM, John Chiligati, kuacha vitisho dhidi ya upinzani, akisema kuwa wataendelea kufichua ufisadi uliotanda kwenye chama hicho tawala.

Chiligati alivionya vyama vya upinzani kuwa visitumie ufisadi kama ngazi ya kujipatia umaarufu, huku akionya kuwa kuendelea kuishutumu CCM kunaweza kuhatarisha amani kwa sababu kama watu milioni nne watachukia (akimaanisha wana-CCM), hakutakuwa na amani.

Lakini Dk Slaa, mmoja wa wabunge ambao wamesimama imara katika kufichua na kupiga vita ufisadi, alisema hakuna ubishi kuwa CCM imeingia madarakani kwa kuchotewa fedha kutoka Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) na kama kinapinga, basi kiende mahakamani. Kauli hiyo ilitolewa jana na Dk Slaa wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika kata ya Hedaru na Makayanya wilayani Same na baadaye kukutana na waandishi wa habari.

Dk Slaa alisema Chadema ina ushahidi wa maandishi jinsi CCM ilivyokuwa inachotewa fedha za EPA kupitia kampuni ya Kagoda, hivyo kama inaona inapakwa matope, inaweza kwenda mahakamani kulalamika na sio kutoa vitisho kupitia vyombo vya habari.

“Tunamshangaa sana Chiligati na tunamuomba aache vitisho. Tunao ushahidi hadi muhtasari wa kikao kilichoongozwa na rais mstaafu kikielezea jinsi walivyokuwa wanajichotea fedha za EPA na pia ujumbe mfupi kutoka kwa katibu mkuu wa CCM kwenda Benki Kuu kuomba fedha hizo. Sasa wanaposema hawahusiki na EPA tunawashangaa,” alisema Dk Slaa.

CHANZO: Mwananchi
HABARI YA PILI :


RC atakiwa kuwaomba radhi wananchi

na Deogratius Temba

MKUU wa Mkoa wa Singida, Vincent Parseko Kone, ametakiwa kuitisha mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kisasida, Wilaya ya Singida na kuomba radhi kwa wanachi na mwenyekiti wa kijiji hicho, kwa kuwatukana hadharani na kuwalipa fidia ya sh milioni moja.

Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Mwenyekiti wa kijiji hicho, Ramadhani Mwankumbi, kutoa taarifa kuwa anakusudia kumfikisha mkuu huyo wa mkoa mahakamani kutokana na kumtukana hadharani wakati akiwa katika mkutano wa hadhara kijijini hapo.

Kwa mujibu wa barua aliyoandikiwa jana, Mkuu wa mkoa huyo, kutoka kwa Kampuni ya uwakili ya M/S TUNDU A.M. LISSU Advocates, yenye kumbukumbu namba TAML/SDG/RSM/KSSD/09/01, na kusaniwa na wakili wa kujitegemea Tindu Lissu, ilieleza Februari 24, mwaka huu, mkuu huyo wa mkoa alienda katika kijiji hicho na kutumia cheo chake kwa lengo alilodai kuwa ni kukagua mradi wa kilimo cha umwagiliaji. Badala ya kutembelea mradi huo, kama alivyodai, aliomba kumwona Mwenyekiti wa Kijiji Mwankumbi, na kuanza kumfokea mbele ya wanakijiji wenzake, viongozi wa mkoa na wananchi wengine wengi kwa madai kuwa ameshirikiana na mtu mwingine aitwaye, Josephat Isango, kumchafulia jina lake.

“Mteja wetu alipoomba nafasi ya kujieleza juu ya tuhuma ulizokuwa unamrushia ulikataa na badala yake ulianza kumtukana matusi mazito, baada ya kumtukana ukaondoka na kurudi Singida,” ilieleza sehemu ya barua hiyo. Pia barua hiyo ilieleza kisheria maneno hayo, ambayo yalitolewa na mkuu huyo wa mkoa ni kosa na ni kashfa dhidi ya mteja wao, na yamemdhalilisha, kumnyanyasa, kumvunjia heshima aliyokuwa nayo mbele ya wanakijiji waliomchagua na kumpa dhamana.

“Maagizo kutoka kwa mteja wetu ni kukutaka wewe Parseko Kone, utembelee tena Kijiji cha Kisasida na kuitisha mkutano wa hadhara wa wanakijiji wote na uwaombe radhi hadharani kwa maneno ambayo sisi tutakuelekeza.

“Aidha, tunakuagiza ufanye ziara ya mkutano huo wa kuomba radhi ndani ya siku 14, kutokea leo (jana), pia mteja wetu anadai umlipe sh milioni moja kama gharama za ufuatiliaji kwetu,” ilieleza barua hiyo.

Lissu, alidai kuwa mkuu huyo wa mkoa, endapo atashindwa kufanya hivyo, au kupuuza kutekeleza matakwa yao watamfungulia kesi ya madai katika mahakama watakayoichagua wao. Aliongeza pia kama Kone atashindwa kutekeleza madai yao, hawatasita kumdai fidia zaidi ya fedha na nafuu nyinginezo za kisheria dhidi yao.

Mwishoni mwa wiki iliyopita Kone alizungumza na Tanzania Daima, alikanusha tuhuma hizo zinazomkabili na kudai kuwa alikwenda katika kijiji hicho kukagua mradi wa umwagiliaji na hakumtukana kiongozi yeyote.


MLOLONGO WA KULALAMIKA,KUTOA VITISHO AU HATA KULIA HAUWEZI KUKOMESHA UFISADI AU KUWAKUMBUSHA WAJIBU BAADHI YA VIONGOZI WANAOJIONA MIUNGU WATU.DR SLAA NA CHADEMA WAMEKUWA WAKITUAMINISHA KWAMBA CCM INAHUSIKA MOJA KWA MOJA KATIKA KUFANIKISHA UJAMBAZI WA EPA.JAPO NAFAHAMU KUWA HUKUMU YA UMMA INA MADHARA ZAIDI YA HUKUMU YA MAHAKAMA ZA KISHERIA,SOTE TUNAJUA NAMNA HUKUMU YA UMMA INAVYOWEZA KUPINDISHWA NA ZAWADI ZA KHANGA,FLANI,KILO YA SUKARI,NK KAMA VIVUTIO WAKATI WA UCHAGUZI.

NGOJA NIFAFANUE KAMA HUJANIELEWA VIZURI.YAYUMKINIKA KUAMINI KUWA CHADEMA INAPOITUHUMU CCM KWENYE MIKUTANO YA HADHARA KWAMBA CHAMA HICHO TAWALA KINA MAHUSIANO NA UFISADI/MAFISADI INATARAJIWA KUWA WANANCHI WATATOA HUKUMU DHIDI YA CCM (HUKUMU YA UMMA) WAKATI WA UCHAGUZI.HILO LINAWEZEKANA KATIKA MFUMO HURU WA DEMOKRASIA,NA MIFANO HAI NI NAMNA HUKUMU YA UMMA ILIVYOFANYA KAZI KATIKA CHAGUZI HUKO HISPANIA MWAKA 2004 NA MAREKANI MWAKA JANA.KATIKA CHAGUZI ZINAZOFANYIKA KATIKA MAZINGIRA YA DEMOKRASIA HURU,HASIRA ZA WAPIGA KURA (AU KURIDHISHWA KWAO) NI MIONGONI MWA MAMBO MUHIMU KATIKA KU-DETERMINE MATOKEO YA UCHAUZI HUSIKA.

SASA SOTE TUNAJUA MAZINGIRA YA CHAGUZI NYINGI ZA "DUNIA YA TATU".KANUNI ISIYO RASMI KUHUSU CHAGUZI ZETU INADAI KWAMBA CHAMA TAWALA HAKIWEZI KUSHINDWA UCHAGUZI.KIKISHINDWA BASI AIDHA KILIZEMBEA KUTUMIA MBINU ZAKE ZA AWALI ZA KUBAKI MADARAKANI AU KILIPIGIWA KURA ZA CHUKI NA WAFUASI WAKE AU KULITOKEA MPASUKO NDANI YA CHAMA TAWALA AMBAO ULIZAA MAKUNDI MAWILI YENYE TAKRIBAN NGUVU SAWA,KILA MOJA LIKIFAHAMU MBINU SAFI NA CHFU ZA KUSHINDA CHAGUZI,NK.WAPO WANAOAMINI KUWA HATA KANU YA MOI HAKIKUSHINDWA UCHAGUZI WA 2002 KWA VILE WAPIGA KURA WALIKUWA WAMEICHOKA (WHICH WAS TRUE i.e. kweli walikuwa wameichoka) BALI NI UTEUZI MBOVU WA MGOMBEA UHURU KENYATA.

VINGI VYA VYAMA TAWALA KATIKA NCHI ZA TATU HUSHIKILIA DOLA KWA MAANA HALISI YA KUSHIKILIA,YAANI WANAITUMIA IPASAVYO KUHAKIKISHA UTAWALA UNAENDELEA MILELE.HAKUNA DHAMBI KWA CHAMA KUWA MADARAKANI MUDA MREFU AS LONG AS KINAWAHUDUMIA WANANCHI IPASAVYO.KWA BAHATI MBAYA,U-KING'ANG'ANIZI WA BAADHI YA VYAMA TAWALA KATIKA NCHI ZA DUNIA YA TATU HAUTOKANI NA MAPENZI YAO KWA NCHI AU WANANCHI BALI HOFU YA KUADHIBIWA KWA MADHAMBI YALIYOWAFANYWA WAKATI VYAMA HIVYO VIKIWA MADARAKANI.KADRI MADHAMBI YANAVYOZIDI KUONGEZEKA NDIVYO KADRI VYAMA HIVYO VINAVYOZIDIWA NA HOFU YA NINI KITATOKEA PINDI VIKITOLEWA MADARAKANI,NA MATOKEO YAKE NI KUTUMIA KILA NJIA KUHAKIKISHA VINATAWALA MILELE.NA KWA VINASHIKILIA DOLA,HILO LINAKUWA SIO JAMBO GUMU.

KWAHIYO,KAMA DR SLAA,CHADEMA NA WENGINEO WANADHANI KELELE KUWA CCM INAHUSIKA KATIKA WIZI WA EPA ZITAFANIKISHA KUPATIKANA KWA HUKUMU YA UMMA KATIKA UCHAGUZI WA 2010 AU BAADAYE,THEY REALLY NEED TO THINK AGAIN.KUFANYA HIVYO NI SAWA NA KUTARAJI KUWA HUYO RC ANAYETUHUMIWA KUWATUKANA WANANCHI ANGEAMUA YEYE MWENYEWE KWA HIARI YAKE KUOMBA RADHI BADALA YA KULAZIMISHWA KUFANYA HIVYO (KAMA ANAVYOTAKIWA NA WAKILI LISSU).NAMNA PEKEE YA CHADEMA,ET AL WANAWEZA KUFANIKIWA KATIKA TUHUMA ZAO DHIDI YA CCM NI KWENDA MAHAKAMANI WAKIWA NA USHAHIDI WANAODAI KUWA NAO.

KUITAKA CCM IENDE MAHAKAMANI (INAPOTUHUMIWA KUWA NA UHUSIANO NA MAFISADI) NI SAWA NA KUMTAKA MTU UNAYEMTUHUMU KUTEMBEA NA MKEO/MUMEO (KUTEGEMEA JINSI YAKO MSOMAJI) AENDE POLISI/MAHAKAMANI.....KWA KIFUPI,ATAENDELEA KUKUIBIA NA HATOTIA MGUU POLISI/MAHAKAMANI.COMMON SENSE INATUELEZA KUWA MWENYE TUHUMA NDIO ANAYEPASWA KUWA NA UHARAKA WA KUZIDHIBITISHA AU KUWA NA DHAMIRA YA KUZITOKOMEZA KABISA.MTUHUMIWA ANAWEZA KUWA NA UHARAKA HUO IWAPO ANAONA ZINAMCHAFULIA JINA.LAKINI WHAT IF TUHUMA DHIDI YA MTUHUMIWA NI ZA KWELI?BADO TUTATEGEMEA MTUHUMIWA AJIEPELEKE KWENYE HUKUMU YAKE?

NAHISI CHADEMA WANACHELEA KWENDA MAHAKAMANI SIO KWA VILE WANAHOFIA KUTOPATA HAKI BALI WANAZITUMIA TUHUMA HIZO KUWA MTAJI WA KISIASA.NA-HYPOTHESIZE KUWA CHAMA HICHO KITAZITUMIA TUHUMA HIZO KWENYE KAMPENI ZAKE ZA UCHAGUZI MKUU WA 2010 KIKIAMINI KUWA ZITAKISAIDIA KUPATA USHINDI KWA HUKUMU YA UMMA DHIDI YA CCM.JAPO LOLOTE LINAWEZEKANA KATIKA SIASA,NA MBINU HIYO YA CHADEMA INAWEZA KUFANIKIWA,WAZOEFU WA SIASA WANAWEZA KUAFIKIANA NAMI KWENYE HYPOTHESIS YANGU YA PILI KUWA MKAKATI HUO HAUTOFANIKIWA.KINACHONIPELEKA KUAMINI HIVYO NI UZOEFU KUHUSU NAMNA CCM INAVYOELEWA UDHAIFU WA MPIGA KURA WA KITANZANIA,FAIDA ZA KILOJISTIKI ZINAZOELEMEA UPANDE WA CHAMA TAWALA,MILKI NA SAPOTI YA DOLA BILA KUSAHAU "MBINU CHAFU."

UCHAGUZI MKUU WA 2010 UNAWEZA KABISA KUPITA NA CCM KUIBUKA KIDEDEA HUKU CHADEMA IKIWA "IMEDODEWA" NA USHAHIDI WAKE DHIDI YA CCM.HILO SIO BAO LA KISIGINO BALI NI MITHILI YA KIBAKA KUKUPORA KISHA ANAKUPIGIA KELELE KUWA WEWE NDIO MWIZI....(AND WE ALL VERY WELL KNOW MOB JUSTICE HUKO NYUMBANI ZILIVYO...WATU WAKISKIA UKELELE WA MWIZI,MWIZI HAWAULIZI ILIKUWAJE.NI KIPIGO TU....PASIPO KUJUA KUWA WANAYEMPIGA NDIO ALOPORWA NA KIBAKA).

BONYEZA HAPA kusoma kimbwanga hiki.

23 Mar 2009


KADA maarufu wa Chama cha Mapinduzi, Nape Nnauye, amesema malumbano yanayoendelea sasa nchini ni ishara kwamba mafisadi wamejipanga kuifanya nchi isitawalike.

Nape alitoa kauli hiyo jana alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu hali ya kisiasa nchini, hususani malumbano yanayoendelea sasa kati ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.

Bila kutaja majina ya watu, Nape alisema chimbuko la malumbano hayo aliyoyaita ya kipuuzi ni kashfa nzima ya kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, iliyosababisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na aliyekuwa Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha, kujiuzulu.

Huku akiwa makini kuchangua maneno ya kuzungumza, Nape alisema malumbano hayo yanaonyesha kuna baadhi ya watu hawakuridhika na taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Mwakyembe, hivyo kuna ulazima wa hoja hiyo kurudishwa tena bungeni ili kukata mzizi wa fitna.

“Kuna kila dalili kuwa mafisadi wamejipanga kuhakikisha nchi haitawaliki, ndiyo maana mijadala isiyo na kichwa wala miguu inaibuka kila kukicha hata kwa mambo ambayo yamekwishaamuliwa na chombo kikubwa kama Bunge,” alisema.

Katika kuthibitisha kauli yake, Nape alisema ana taarifa za siri kuwa kuna baadhi ya mafisadi wamekuwa wakifanya mikutano ya faragha ambapo pamoja na mambo mengine, wamepanga kuhakikisha nchi haitawaliki kwa kuibua hoja na mijadala kupitia baadhi ya vyombo vyao vya habari.

“Tunakoenda ni kubaya, ila naamini serikali iko imara na CCM kama chama tawala, tutaomba tulizungumze kwenye vikao vyetu kwa nia njema ya kuliokoa taifa linalovurugwa na watu wachache wenye fedha,” alisema Nape.

Nape alisema ili kuhakikisha Tanzania haiyumbishwi, aliwataka wananchi kupuuzia mjadala wa sasa kwa madai kuwa hauna tija na una lengo la kuhatarisha amani na utulivu uliopo nchini.

Kuhusu mjadala wa ununuzi wa mitambo ya kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans iliyorithi kutoka Kampuni ya Richmond, kada huyo wa CCM alisema anashangazwa na uamuzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kuomba kibali cha Bunge au kamati zake.

“Kwani TANESCO wanapoenda kununua transfoma na vifaa vingine, wanaomba kibali cha Bunge? Kama si hivyo, kwa nini wanataka kuhalalisha ununuzi wa mitambo ya Dowans kupitia kamati za Bunge? Hata hivyo, Bunge lilishatoa msimamo wake juu ya hilo, kama kuna mtu hakuridhika, alirudishe bungeni na si kuwagawa Watanzania kwa mijadala isiyoisha na vitisho,” alisema Nape.

Mwanasiasa huyo machachari aliwataka mafisadi kutambua kuwa hata wakiibua mijadala ya kuwagawa Watanzania kama ilivyo sasa, hakutabadili ukweli kwamba Richmond na hata mrithi wake Dowans, ndio waliolifikisha taifa hapa lilipo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Maswa, John Shibuda, alisema malumbano yanayoendelea sasa kati ya Dk. Mwakyembe na Rostam kumetokana na upepo wa kisiasa ambao wakati mwingine huleta tija katika kukuza demokrasia.

Hata hivyo, Shibuda ambaye hupenda kuzungumza kwa mafumbo, alisema mjadala huo umejikita kwenye hila na visa vya kufunika mema na mazuri ya mtu.

“Mimi naona hayo ni mapepo ya kisiasa na mtenguko wa fikra ambao umeleta mng’atuko dhidi ya dhulma, lakini ni mjadala wa heri kwa maana kuwa unawafanya watu kutoa manung’uniko yao, bila hivyo hali ingekuwa mbaya siku moja, kwa hiyo naona mjadala uendelee,” alisema Shibuda.

Mbunge wa zamani wa Morogoro Vijijini, Semindu Pawa (CCM), aliiambia Tanzania Daima jana kuwa, mjadala huo sasa umechacha na kuwataka waandishi wa habari kuachana nao.

“Mimi sitaki kusema nani yuko sahihi, lakini nasema mjadala huo umechacha, umepitwa na wakati, wanahabari mkiacha tu, hautausikia tena, lakini naweza kusema wanahabari ndio mnaoukuza, waacheni,” alisema Semindu Pawa.

Mwishoni mwa wiki, Dk. Mwakyembe alijibu tuhuma zinazomhusisha na kumiliki kampuni binafsi ya kuzalisha umeme kuwa ni kazi mahususi inayofanywa na majeruhi wa vita ya ufisadi, ambao waliumizwa na matokeo ya kazi ya Kamati Teule ya Bunge ya kuchunguza mkataba wa Kampuni ya Richmond, ambayo yeye alikuwa mwenyekiti wake.


Hatua ya Mwakyembe kujibu tuhuma hizo, ilikuja baada ya magazeti mawili ya kila siku, (si Tanzania Daima) kuchapisha habari zinazomhusisha yeye na umiliki wa hisa 1,000,000 zenye thamani ya jumla ya sh bilioni 1.5 katika Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd.

Mbali ya habari hizo kuandikwa katika magazeti hayo mawili; moja la binafsi na jingine la serikali, nyaraka kadhaa zinazomhusisha Mwakyembe na kampuni hiyo, zimesambazwa katika mtandao wa intaneti.

Taarifa hizo pia zinamtaja Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya TANESCO, kuwa miongoni mwa wanahisa wa kampuni hiyo binafsi ambayo wakati fulani Mwakyembe alipata kuwa mtendaji mkuu wake.

Taarifa hizo zinajaribu kujenga hoja zinazojaribu kumuondolea Mwakyembe uhalali wa kuendelea kudai kupambana na ufisadi ndani na nje ya Bunge ilhali yeye mwenyewe akionekana kuwa na ukwasi mkubwa unaotiliwa shaka.

Pia zinaonyesha kuwa, Mwakyembe licha ya kuwa na hisa nyingi katika kampuni hiyo, ameisaidia katika mambo mbalimbali ambayo hata hivyo hayakufafanuliwa, wakati akiwa katika wadhifa wa mtendaji mkuu.

Kwa mujibu wa uchunguzi wetu, lengo kuu la kusambaza nyaraka hizo ni kujaribu kumnyoshea kidole Mwakyembe na kujaribu kumuondolea uhalali wa kuendelea kupigania sekta ya nishati ilhali yeye mwenyewe akijua kuwa na maslahi.

Mwakyembe ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alisema kuwa katika Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd, hakuwezi kukamsababishia akaingia katika mgogoro wowote wa kimaslahi kutokana na ukweli kwamba, kampuni hiyo iliyosajiliwa kwa Wakala wa Usajili wa Makampuni (BRELA), bado ipo katika hatua ya awali ya mradi ambao bado haujaanza kuzalisha.

Alipotakiwa kueleza ni kwa nini wakati alipoteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyoichunguza Richmond kuanzia Oktoba mwaka juzi na kuwasilisha ripoti yake mwaka jana, hakueleza lolote kuhusu kuwa na kampuni ya kuzalisha umeme, Mwakyembe alisema asingeweza kufanya hivyo wakati mkakati wao wa kikampuni ukiwa katika hatua ya mradi tu.

‘‘Kwa mujibu wa sheria ya makampuni, majina yanakuwapo mpaka hapo kampuni itakapoanza ‘ku-take off’ (kuanza kazi). Sikuweza kuitaja kuwa ni sehemu ya makampuni yangu, kwa kuwa bado ilikuwa katika hatua ya mradi,” alisema Mwakyembe.

Mwanasiasa huyo alikwenda mbele zaidi na kuwaeleza wanahabari hao ambao miongoni mwao walionekana dhahiri kukabiliana naye kwa njia ya malumbano kuwa, hata wakati akiandikisha mali anazomiliki chini ya sheria ya viongozi kutangaza mali wanazomiliki, hakuitaja kampuni hiyo ya Power Pool kwa sababu hizo hizo za kutoanza kwake kazi.

Akifafanua tuhuma hizo dhidi yake, alimgeukia mbunge mwenzake wa CCM, Rostam Aziz na kumtuhumu kuwa nyuma ya habari zote mbaya zinazoandikwa dhidi yake.

Huku akilitaja jina la Rostam mara kadhaa, Mwakyembe alisema ni jambo ambalo haliingii akilini kwa mtu ambaye amechafuka kuamua kutumia maji taka kujisafisha.


WALA TUSINGEFIKA HAPA TULIPO IWAPO SHERIA INGEFUATA MKONDO WAKE.VINARA WALIOTUINGIZA MKENGE KWENYE UTAPELI WA RICHMOND HAWAJACHUKULIWA HATUA BAADA YA KUJIUZULU,NA SASA WAMEPATA JEURI YA KUTAKA KUTULIZA MARA YA PILI KWA KUTUUZIA MITAMBO MITUMBA ILEILE ILE YA RICHMOND a.k.a DOWANS.HUU MTINDO WA KULINDANA UTALIPELEKA TAIFA MAHALA PABAYA.

HOWEVER,LET IT BE KNOW TO MAFISADI AND THOSE WHO SHIELD THEM THAT IF THEY TURN OUR BELOVED COUNTRY INTO ANOTHER MADAGASCAR THEY TOO WOULDNT BE SAFE!

22 Mar 2009


Tanzania has condemned the forced resignation of Madagascar President Marc Ravalomanana and said it does not recognise the regime of his successor, Andry Rajoelina...MORE

SOURCE: Guardian



As the public electricity power supply utility, Tanesco struggles with bail-out plans in order to avoid major power shedding expected to hit the nation by September this year, fresh details have emerged showing how the cash-strapped company missed a $300million power deal due to greed and battle for the control of big money running into billions of shillings.

According to details from the financier - Barrick Tanzania - the project was suspended early in January this year after Tanesco - Tanzania Electricity Supply Company - failed to adhere to the financing conditions issued in order to ensure that the billions are not swindled by some corrupt top officials within the state-owned company.

Barrick Tanzania had agreed to finance the $300million Mnazi bay power project, which could have produced 300megawatts, and forestalled the looming power crisis.

According to inside information, Barrick Tanzania, being one of the potential clients of the proposed deal, was approached by Tanesco and Artumas through a Power Purchasing Agreement (PPA).

Under this arrangement, Barrick, as a prospective client was to consider the possibility of investing in a generating company, TanGen, and recover its investment through sale of power under the Power Purchase Agreement.

It is through this arrangement that Barrick Tanzania was ready to give the needed billions to finance the stalled project.

Investigations conducted by The Guardian on Sunday have established that earlier, Barrick Tanzania, being alarmed by the financial mismanagement within Tanesco, gave the latter a condition that the two should open a joint venture account in order to manage the Sh390billion($300million).

But for unknown reasons, Tanesco flatly rejected the proposal, insisting that it should be given full mandate to control the $300million.

However, the move was strongly rejected by Barrick which among other things questioned the intention of Tanesco of declining to operate a joint venture account with the financier.

A senior official from Barrick Tanzania who declined to be named citing the sensitivity of the current power debate told The Guardian on Sunday this week: ``I am surprised, they (Tanesco) are crying to buy $50million Dowans plants while they have failed to utilise a $300million deal from us…This is a shame.

``We were surprised to hear that Tanesco management wasn`t ready to agree with a very simple condition they were being given by Barrick…And this led us to think that perhaps there were hidden motives about our money.``

After failure to agree on how to manage the billions which is close to the company`s annual revenue collections, Barrick Tanzania`s management decided to stop financing the project, casting a bleak future on the country`s energy sector.

Surprisingly on February 21, this year, while tabling the financial recovery plan of Tanseco before the parliamentary committee responsible for overseeing all publicly owned corporations, the Company`s Managing Director, Dr. Idris Rashidi, told the committee that he wasn’t aware why Barrick Tanzania pulled out of the project.

``This has come as a surprise to us because we banked our hopes on this project…we were shocked to learn that the financier had pulled out of the
project, `` the MD told the committee, indicating that he wasn’t aware why Barrick had pulled out at the final stages.

But contacted for comment, the Minister for Energy and Minerals, William Ngeleja said: ``I have already started a process to rescue the project…It is true that the negotiations hit a snag recently, but I am working on it.

``I have organised a meeting on March 25 at my office that will involve all concerned parties - Barrick, Tanesco and Artumas - to discuss how to rescue the plan.``

The Minister went on: ``You know that in any deal there`s always disagreement about contentious issues but that can be sorted out…I will ensure that the country gets the 300 megawatts electricity as planned.”

The revelations come after three weeks of a verbal wrangle between prominent leaders, focused on accusations and counter-accusations over an alleged hidden agenda on the proposed 60bn/- Dowans takeover, a situation that has opened the floodgates of mudslinging politics.

The two parliamentary committees - the one led by legislator Kabwe and the other chaired by fellow legislator William Shelukindo - have strongly differed on the Dowans deal, raising a heated debate during the past few weeks.

The company currently purchases about 59 percent of its power from private producers, which according to financial details eats up to 83 percent of the total revenue collected annually.

With dilapidated infrastructure built mainly during the 1970s, the company`s power supply capacity is estimated at 595 megawatts.

This year, the actual demand is 787 megawatts - creating a deficit of 192 megawatts.

According to available details, the company has only 670,000 customers.

Last year, the company planned to increase its customer base by about 100,000, but the target couldn’t be reached due to financial straints.

Still, based on the current economic growth, demand for electricity is estimated to increase by 15 percent annually, while the production capacity continues to dwindle due to various technical and non-technical factors.

Since there are no comprehensive power generating plans in 2010, the power deficit will surge to 300 megawatts, putting the country at risk of facing an even worse phase of power rationing.

Currently, the state-owned company needs about $200m for major repairs on its dilapidated infrastructure, but so far there’s nowhere to get the money from.

Just two years ago, the company borrowed $300m from a consortium of local banks at 10 percent interest per annum, but almost 80 percent of that money was spent on settling outstanding debts.

Currently according to the inside details, Tanesco is on the brink of collapse due to the heavy costs of operations, largely attributed to capacity charges.

In 2004, the company paid 43/- to private power producers for every 100/- it collected in revenue. By 2006, when dubious government deals were made with private companies, that figure had more than doubled, to 104/- for every 100/- collected, according to the parliamentary committee presentation.

In 2007/08, the company spent 83/- for every 100/- it collected to foot the bill of power generated by private producers, but this year, the figures will soar even higher - to 106/- for every 100/- collected, according to the financial recovery plan seen by The Guardian on Sunday.

In other words, 83 percent of the total revenue collected by the state-owned utility company will go to private power producers, leaving the company in dire financial straits.

Over the past two years, the company`s revenue collection has spiked by 122 percent, reaching 437bn/-, a year up from 196bn/- in 2006.

Today, the company`s electricity loss - meaning the amount of energy lost when transmitted from point A to point B - is 24 percent, a staggering amount when compared to countries like South Africa where that loss is below 4.5 percent.


That's according to the News of The World.


Na Khamis Mkotya

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imesema orodha ya majina ya watumishi wasio waaminifu kwenye kitengo cha kudhibiti mapato bandarini (TISCAN), bado haijawasilishwa Makao Makuu kama ilivyoahidiwa na Rais Jakaya Kikwete. Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Elimu kwa Walipa Kodi, Protus Mmanda, alisema Menejimenti ya TRA chini ya Kamishna Mkuu, Hary Kitillya, inayasubiri majini hayo kuweza kuchukua hatua stahili.

Mmanda alisema, watumishi wote wa TRA watakaotajwa kwenye orodha hiyo watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zote za nidhamu, ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi kama Rais alivyoagiza. Machi 2, mwaka huu, Rais Kikwete alifanya ziara ya ghafla bandarini kukagua utekelezaji wa maagizo yake kuhusu ufanisi katika utendaji kazi wa bandari ya Dar es Salaam, hasa kuhusu mrundikano wa makontena. Katika ziara hiyo, Rais alionyesha kukerwa na baadhi ya watumishi wa TISCAN ambao wamekuwa wakishirikiana na wafanyabiashara wakubwa kuwaonyesha mbinu za kukwepa kodi, vitendo vinavyolisababishia taifa hasara. Rais Kikwete alisema, orodha ya watumishi wanaoendekeza mchezo huo mchafu anayo na kumtaka Kamishna Mkuu wa TRA, kuwafukuza kazi watumishi hao atakapokabidhiwa majina.

Orodha ya majina hayo bado haijafika kwetu, tunaendelea kusubiri sijui yatakuja lini, maana mimi kwa wadhifa wangu siwezi kwenda Ikulu kuuliza majina hayo yataletwa lini. “Labda kwa kuwa nyinyi waandishi wa habari mnakutana na Salva Rweyemamu, (Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu) muulizeni hayo majini yatakuja lini, lakini sisi huku hatuwezi kuuliza, hadi hapo yatakapoletwa,” alisema. Mmanda alisema kuwa, wakati majina hayo yanasubiriwa, TRA imechukua hatua kadhaa zinazolenga kuweka mfumo mzuri wa utendaji, ikiwa ni pamoja na kufanya mabadiliko kwa baadhi ya maofisa wake.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, TRA imeshafanya mabadiliko kwa kuwahamisha idara baadhi ya maofisa wake, wanaoonekana kuwa na chembe za ukosefu wa maadili kama hatua za awali za kutekeleza maagizo ya Rais. “Hatuwezi kukaa tu bila kufanya tathimini yoyote juu ya utendaji kazi wetu, kwa sababu tunasubiri majina kutoka kwa Rais. Baadhi ya hatua tulizochukua ni pamoja na kufanya mabadiliko katika baadhi ya idara zetu. “Tumefanya marekebisho pale palipostahili, mahala palipokuwa na watumishi wazembe wasiokuwa waadilifu tumewaondoa na kuweka watumishi wengine,” alisema Mmanda, ingawa hakutaja idara na maofisa wake walioguswa na zoezi hilo.

Mkurugenzi huyo alisema, hatua nyingine zilizochukuliwa ni pamoja na kurahisisha taratibu za usajili wa magari, kuondoa kero ya muda mrefu ambayo imekuwa ikilalamikiwa kuhusu uchelewashaji wa usajili wa magari. Kwa mujibu wa Mmanda, taratibu zote za usajili wa magari yanayoingizwa nchini hivi sasa zitafanywa na ofisi moja, ili kuondoa usumbufu kwa watu, tofauti na zamani ambako taratibu hizo zilikuwa zikishughulikiwa na ofisi zaidi ya moja. Alisema kuwa, utaratibu huo mpya pia utasaidia kuondokana na watu wa ‘kijiweni’ maarufu kwa jina la ‘vishoka’, ambao wamekuwa wakiwatapeli watu kwa kisingizio cha kuwasaidia katika taratibu za usajili wa magari.

CHANZO: Mtanzania


21 Mar 2009


THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

CONTROVERSY surrounds the mysterious disappearance of a large consignment of local currency notes with a value running into millions of Tanzanian shillings, as it was being airlifted into the country from Germany on a Qatar Airways flight.

Sources within the Bank of Tanzania (BoT) have confirmed the apparent large-scale theft which was discovered on arrival at the Julius Nyerere International Airport in Dar es Salaam early last week.

It has yet to be established exactly at what point the consignment of bank notes got stolen whether it was in Germany, where the notes were manufactured; in Doha, where the flight made a stopover; or at the final JNIA destination in Dar es Salaam.

According to THISDAY findings, the consignment contained crisp new bank notes of 10,000/- denomination. However, the exact number of such notes involved � and hence the total value of the package � could not be immediately verified.

’’The consignment arrived at the airport in Dar es Salaam on the evening of Monday, March 9. But because the following day was a Maulid holiday, it could not be dealt with until Wednesday, March 11. That’s when it was discovered that the notes were gone,’’ said an informed BoT source.

It is understood that besides the new 10,000/- notes, the consignment also contained a substantial amount of old local currency notes that had long been removed from circulation.

Said the source: ’’The old notes were under audit query...during an earlier auditing exercise, the auditors wanted to know why these notes had not been returned for so many years since being sent to the printers overseas because of various technical problems.’’

But it remains unclear of what use the old notes long out of circulation were expected to be at this moment in time, or whether the government or central bank has received or is expecting any compensation from the company manufacturing the notes.

The discovery of a consignment of defective Tanzanian currency notes with a total value of 3.5bn/- back in 2001, led to serious repercussions including the launch of an official investigation by the then Prevention of Corruption Bureau (PCB).

However, no arrests or prosecutions were ever made.

The notes were printed by the German company Glesecke & Devrient Gmbh, on behalf of the Bank of Tanzania (BoT). They were of 1,000-shilling denomination, amounting to a total value of $3,237,492.

Following this scandal, the government vetoed central bank plans to award another print order to the same German firm, while the defective notes were said to have been quietly withdrawn from circulation.


SOURCE: ThisDay

The first black chief executive of a FTSE 100 Index company was appointed when insurer Prudential named Tidjane Thiam as its next boss...MORE

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.