20 Aug 2009


Labda CCM imekaa madarakani kwa muda mrefu mno hadi imefikia hatua ya kusahau wajibu wake. Pengine ni matokeo ya mafisadi kushika hatamu ndani ya chama hicho, au pengine ni CCM imesharidhika kwamba Watanzania wamezowea kunyanyaswa, kupuuzwa na kuchezewa kama watoto wadogo pasipo kuchukua hatua yoyote.

Najiuliza hivyo baada ya kusoma habari kwamba chama hicho tawala “kimechimba mkwara mzito” kwa baadhi ya viongozi na wanachama wake wanaodiriki kunyooshea vidole ufisadi na mafisadi.Ungetegemea CCM ingekuwa mstari wa mbele kuhamasisha mapambano dhidi ya ufisadi na mafisadi kwa vile so far ndio kikwazo kikubwa katika utekelezaji wa kauli-mbiu Maisha Bora kwa Kila Mtanzania. Lakini kwa vile mafisadi ni watu muhimu sana kwa chama hicho, jaribio lolote la kuwakemea ni sawa na kusigina katiba ya CCM.

Kana kwamba kushindwa ku-meet matarajio ya wapigakura (waliokipa dhamana chama hicho mwaka 2005 kututawala tena) sio jambo linaloinyima CCM usingizi, chama hicho kimeanza kuonyesha dalili za udikteta tukirejea kauli zake nzito za hivi karibuni. Siku chache zilizopita, kiongozi mkongwe na miongoni mwa waasisi wa CCM,Kingunge Ngombale Mwiru,aliwakemea viongozi wa Kanisa katika lugha inayoweza kutafsiriwa kuwa ni ya kidikteta,alipoonyesha dhahiri kukerwa na kitendo cha viongozi wa dini kutumia uhuru wao wa kikatiba kutoa maoni yao kuhusu hatma ya taifa letu.Na sasa tunaambiwa kwamba chama hicho kimeamua kuwafunga midomo wabunge wake wanaojaribu kuwakemea mafisadi, sambamba na kunyamazisha kelele dhidi ya tuhuma zinazomwandama Benjamin Mkapa, Rais wa Awamu ya Tatu.

CCM imefikia hatua ya kulitukana Bunge la Jamhuri ya Muungano na kulifananisha na kikundi cha vichekesho cha Ze Komedi.Jaribu ku-imagine kauli kama hiyo ingetoka kwa mtu kama Dkt Wilbroad Slaa au Zitto Kabwe! Ni dhahiri watu kama George Mkuchika, anayechanganya majukumu yake ya u-Katibu Mwenezi wa CCM na u-Waziri wa Habari, au Yusuph Makamba wangekurupuka na vitisho kuwa “wapinzani wanaikosea heshima Katiba ya Jamhuri.” Kulilinganisha Bunge na Ze Komedi kwa vile tu limejikongoja kuruhusu sauti zisizopendeza masikioni mwa mafisadi na watetezi wao ni kitendo kinachoashiria utovu wa nidhamu wa hali ya juu.

Bunge la Jamhuri ya Muungano ni taasisi nyeti na inayopaswa kuenziwa na kuheshimiwa na kila Mtanzania including hao wanaoifananisha na kikundi cha vichekesho. Kama unadhani kauli ya “Bunge ni mithili ya Ze Komedi” haina uzito, tafakari upya. Mtu anapokufananisha na mchekeshaji (comedian) anafikisha ujumbe kwamba hupaswi kuchukuliwa seriously. Kauli na matendo yake pia yanapaswa kuchukuliwa kama mambo yasiyopaswa kupewa umuhimu au kutekelezwa kwa vile ni ya “kusukuma muda” tu. Japo vichekesho vingi huwa na ujumbe uliofichika katika maneno au matendo ya kuchekesha, mara nyingi kauli au matendo hayo hayapaswi kuchuliwa seriously.

Kwa CCM kulifananisha Bunge na Ze Komedi inatueleza kwamba taasisi hiyo yenye jukumu la kutunga sheria za nchi haistahili kuchukuliwa serious katika kauli, maamuzi na matendo yake. Lakini hilo si geni kwa vile hata maamuzi ya baadhi ya kamati za Bunge, kama ile ya Mwakyembe, yameendelea kupuuzwa katika kile kinachothibitisha kuwa CCM imekuwa ikiliona Bunge kama genge la wachekeshaji,with exception of wabunge kama Kingunge,Serukamba,Mkuchika ,Lowassa,Rostam,Karamagi,Chenge na “wateule wengine wachache” wenye umuhimu wa kipekee kwa chama hicho.

La kusikitisha ni kwamba bado mamilioni ya Watanzania wenye akili zao timamu wataipigia kura CCM hapo mwakani irejee madarakani kuendeleza nyodo kama hizi.Na hicho ndicho kinawapa jeuri watu kama Mkuchika kusema lolote pasi hofu ya kukigharimu chama hicho ushindi hapo mwakani.CCM inajivunia knowledge yake kuhusu Watanzania kwamba ni kama wamezowea kupuuzwa (wao na baadhi ya wawakilishi wao wachache wanaopiga kelele Bungeni kutetea maslahi ya walalahoi),kunyanyaswa,kuburuzwa na kudanganywa kama watoto wadogo.

La kusikitisha zaidi ni namna uongozi wa juu (with exception of Makamba na Mkuchika wanaofahamika bayana wanaoelemea upande gani kati ya watetezi na wapinzani wa ufisadi) walivyo kimya japo kila siku wanasikika majukwaani wakiahidi Maisha Bora kwa Kila Mtanzania. Taarifa za vyombo vya habari kuhusu yaliyojiri kwenye vikao vya juu vya chama hicho zinatuthibitishia bayana kuwa uongozi wa juu wa CCM hauna dhamira ya dhati ya kukomesha ufisadi kwa vile badala ya kuwakemea wanaowakwaza wapambanaji dhidi ya ufisadi wanadaiwa kuleta ngonjera za “kujadili mambo ndani ya chama.”Yaani wanataka kutuambia hawajui kuwa ndani ya chama kuna watu kama Lowassa, Rostam, Chenge na wengineo ambao kwa namna yoyote hawako tayari kuruhusu mjadala huru dhidi ya ufisadi kwa vile wao ni watuhumiwa?

Ungetarajia busara za watu kama Mzee Ali Hassan Mwinyi ziwafumbue macho CCM kwamba kuzuia demokrasia katika kujadili mambo yanayowakera na kuwaumiza Watanzania kutapelekea kifo cha mende kwa chama hicho. Lakini pengine wanafahamu nguvu za mafisadi ndani ya chama hicho, na hivyo kuhofia kuwaudhi katika kipindi hiki ambacho CCM inawahitaji mafisadi more than ever ili iendelee kututawala.Wanatupuuza kwa vile wanajua hatuna jeuri ya kuwaadhibu kwa madhambi yao.

They could be right, though! However, they fooled us in 2005.They possibly will fool us again in 2010, but let them rest assured that they will never fool us forever. They are simply buying time to finish digging their own graves.


14 Aug 2009


Kingunge Ngombale Mwiru ni mkingwe,kiumri,kisiasa na kimadaraka.Japo umri si kigezo muhimu cha kuwa na busara,ukongwe katika fani flani unatarajiwa kuambatana na busara.Lakini hali si hivyo kwa Kingunge.Kuna nyakati baada ya kifo cha Nyerere baadhi ya watu walitarajia kuwa Kingunge angefanikiwa kuendeleza mema ya Mwalimu hasa kwa vile tuliaminishwa kwamba mwanasiasa huyu (Kingunge) ana damu ya Ujamaa kiasi cha kuachana na mambo ya imani ya kidini.Tuliambiwa dini ya Kingunge ni Ujamaa.

Pamoja na mapungufu ya hapa na pale,Nyerere anaendelea kukumbukwa kwa jitihada zake za kujenga jamii yenye kukaribia usawa na kuchukia unyonyaji.Sijui Kingunge akifa tutamkumbuka kwa lipi zaidi ya kuzeekea kwake kwenye siasa pasipo tija na hili jukumu jipya alilojipachika la u-Baba wa Taifa wa Mafisadi.Kingunge ni mnafiki mkubwa kwa vile wakati anadai kuwa viongozi wa kanisa "wangeufyata" laiti Mwalimu angekuwa hai,sijui yeye Kingunge angemwambia nini anaposimama kidete kutetea mafisadi.

Haya ndio madhara ya kuviacha vikongwe madarakani hadi vinapoteza uwezo wa kufikiri.Na huyu ni mshauri wa kiongozi wa nchi!Kama uwezo wake binafsi wa kufikiri umefikia kikomo atawezaje kumshauri mtu mwingine,achilia mbali kiongozi wa nchi?

Kwanini adai waraka wa kanisa utawagawa Watanzania lakini akae kimya pale chama chake cha CCM kilipocheza karata-tatu ya kisiasa kilipoahidi (katika manifesto yake ya uchaguzi 2005) uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kwa Waislam?Binafsi,sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama ya kadhi iwapo mambo flani muhimu yatazingatiwa,lakini kwa uendeshaji wa mambo kwa mtindo wa zima moto,au pata potea,ni dhahiri uamuzi huo wa mahakama ya kadhi unaweza kulipeleka pabaya taifa.Narudia,tatizo sio uanzishwaji au kuwepo kwa mahakama hiyo,bali ni ubabaishaji wa viongozi wetu katika kushughulikia uanzishwaji na uwepo wake pasipo kuathiri umoja wa kitaifa.

Na kikongwe huyu (Kingunge) mbona yuko kimya hadi leo baada ya chama chake kusuasua katika utekelezaji wa ahadi hiyo ya uanzishwaji wa mahakama ya kadhi?Kama uamuzi wa CCM kutaja katika manifesto yake juu ya suala hilo ulikuwa hatari (kwa mujibu wa wanaodhani hivyo),kitendo cha chama hicho kurushiana mpira kila kinapoulizwa na waahidiwa (Waislam) kuhusu utekelezaji ni cha hatari zaidi.

Tatizo la Kingunge kuhusu waraka wa kanisa haliko kwenye kile anachodai "kuijua vizuri nchi yetu" bali wasiwasi wake kwamba pindi waraka huo ukitekelezwa kwa vitendo basi yeye na mafisadi anaowatetea watakuwa katika wakati mgumu.Kwa lugha nyingine,Kingunge anatetea maslahi ya tabaka alilomo na analoliwakilisha (mafisadi).

Hivi ni lini umewahi kumsikia Kingunge akikemea ufisadi?Hivi Kanisa lingetoa wapi wazo la kujana waraka huo laiti kikongwe hiki cha siasa kingesimama kidete kuendeleza harakati za Mwalimu kupambana na unyonyaji?Badala ya kutueleza yeye anafanya nini kuhakikisha nchi inakwenda vizuri anakimbil;ia kukosoa wengine kuwa wanataka kuipeleka nchi pabaya.

Halafu inakera zaidi kumskikia babu huyu akijifanya kama yeye ndio mwenye hatimili ya historia,mwelekeo na chochote kuhusu Tanzania.Eti anakemea wenzake "wanaodakia hoja pasipo kujua vema tumefikaje hapa..."Tumefika hapa tulipo kwa sababu ya watu kama Kingunge,wanafiki waliojifika kwenye ngozi wa kondoo wakati wa Mwalimu kumbe ni mbwa mwitu wa kifisadi waliokuwa wakisubiri Mwalimu aondoke kwenye ulingo wa siasa kisha watufisadi.

Kingunge ni mtu hatari sana,na asipodhibitiwa ataiingiza nchi katika machafuko.Kishajizeekea,hajali litakalotukumba kwa vile ashachuma vya kutosha na anamsubiri Muumba amrejeshe mbele ya haki (na huko atakuwa na maswali lukuki ya kujibu atapokutana na Mwalimu).Ni muhimu kwa wanaomlea kikongwe huyu wakamhurumia kwa kumpatia pumziko haraka,la sivyo "atazidi kulikoroga".

Mungu ibariki Tanzania na waangamize mafisadi na watetezi wao,hususan wale wanaotaka ligi
na wachunga kondoo wako.

11 Aug 2009


Kuna tamasha kubwa la kimataifa linaloendelea jijini Glasgow.Wenyewe wanaliita World Pipe Band Championships.Ni mashindano ya bendi za kupuliza filimbi kama zile za brass band (pipes).Kumejitokeza mgogoro wa kiplomasia baada ya Wakala ya Mipaka ya Uingereza (UK Border Agency) kuwanyima viza wanabendi ya kupuliza filimbi kutoka Pakistan.Licha ya bendi hiyo inayojulikana kama Lahore Piping Band,msafara wa wafanyabiashara kutoka Pakistan nao umenyimwa viza.Kinachochochea zaidi songombingo hilo ni ukweli kwamba Glasgow na Lahore ni miji pacha (twin cities).

7 Aug 2009



Kwa mfumo wa tarehe za "kwetu" tunaanza na tarehe kisha mwezi,tofauti na wenzetu wa kwa Obama ambao wanaanza na mwenzi kisha tarehe.Yaani,kwa hapa,na kama ilivyo huko nyumbani TZ,ni tarehe 07/08/09 japo kwa wenzetu wa US itaandikwa 08/07/09.Basi,leo mchana kulikuwa na tukio adimu katika uhai wa wengi.Kama inavyoonekana pichani juu,kuna muda saa na kaelnda ilisomeka 1-2-3-4-5-6-7-8-9,yaani saa 12 na dk 34 na sekunde 56 tarehe 7 mwezi wa nane mwaka 2009 (12:34:56 7/8/9).Ulikumbuka kuhusu tukio hili?

MHAMASISHA VITA DHIDI YA MAFUA YA NGURUWE NAYE AAMBUKIZWA....


Na the funny side ya "maadhimisho" hayo ni habari hapa Uingereza kwamba jamaa aliyetumika katika tangazo la "Wizara" ya Afya katika runinga kuhamasisha jamii dhidi ya mafua ya nguruwe (swine flu) nae ameambukizwa ugonjwa huo.Msanii Davidi McCusker (pichani juu).Hata hivyo,lililo dhahiri ni kwamba maambukizo hayo hayana mahusiano na ushiriki wa msaanii huyo David McCusker katika tangazo hilo.

6 Aug 2009


IMMIGRANTS who come to live and work in Scotland could have a better chance of earning full UK citizenship, it was revealed yesterday.

The Home Office unveiled plans for an Australian-style points systems for foreigners who want to settle in Britain.

Workers from overseas will receive extra points based on their skills and qualifications. Once they have enough points, they will be able to move to Britain permanently.

It also emerged yesterday that extra points will be given to migrants who settle in parts of the UK where population is set to fall - such as Scotland.

The move would build on the Fresh Talent Initiative, set up by former first minister Jack McConnell to let foreign students stay after graduation.

A Home Office spokesman said: "There are parts of the country where spaces in the workforce aren't being filled by UK residents and could very easily be filled by hard-working migrants."

Scottish Secretary Jim Murphy last night said he was "pleased" at the move.

He added:"Our need for a growing population is ranked alongside the need to recruit to occupations where we have a shortage."

SNP MP Pete Wishart gave the plans a cautious welcome. He said:"The Home Office must demonstrate the new points based immigration system is fit for Scottish purpose.

"Scotland's population and immigration requirements are completely different from the rest of the UK and this has to be recognised when points are added up."



Na Awila Silla, Singida

RAIS Jakaya Kikwete ametangaza vita dhidi ya askari wa usalama barabarani ili waweze kufanya kazi kwa kufuata sheria na kanuni za nchi.

Kikwete alitoa kauli hiyo nzito mkoani Singida alipozungumzia kero kubwa ya ajali nchini ambayo alisema inakwamisha juhudi za serikali kuleta maendeleo kwa wananchi.

"Na nyie watu wa usalama barabani manaendekeza urafiki na madereva wa nini badala ya kukagua gari mnazunguka nyuma ya gari na makonda kufanya nini? huku umeona kabisa gari bovu na dereva hana leseni, nawambia, safari hii naanza na nyie," alisema Rais akionyesha ukali

"Msinilazimishe sana niendelee kufoka kila siku wimbo umekuwa huo huo nimechoka jamani , Wizara mnafanya nini fanyeni kazi yenu fukuzeni hawa watu kama hawataki kufuata sheria warudi nyumbani kufua au wakafanye kazi nyingine" alisisitiza .

Mbali ya kauli hiyo nzito pia alisema haoni sababu ya kuendelea kufoka kuhusu baadhi ya matatizo ya ajali na badala yake aliitaka pia Wizara ya Mambo ya Ndani kuchukua hatua mathubuti kutatua matatizo hayo.

Alisema jukumu la sasa kwa Wizara hiyo ni pamoja na kuweka mpango mkakati wa utaratibu mpya wa sheria ya usalama barabarani juu utoaji leseni kwa madereva na kufanya marekebisho ya adhabu ambazo alisema zimepitwa na wakati.

Rais alisema hatua ambazo zinaweza kuchukuliwa chini ya wizara hiyo ni unyang'anywaji wa leseni bandia kwa madereva wasio na taaluma au wanaokiuka sheria na masharti ya usalama barabarani.

Kutokana na hilo aliitaka Wizara hiyo kuongeza ukali na kuondoa urafiki na ulegevu kwenye mambo yanayozuika ili kuboresha usalama wa barabara na kulinda uhai wa watu.

Akifafanua juu ya hilo Kikwete alisema licha ya matatizo mengi yanayojitokeza kwenye miundombinu hiyo, lakini utafiti unaonyesha kuwa asilimia kubwa ya ajali nyingi inatokana na matatizo ya kibinadamu ikiwemo uzembe wa madereva hao.

Kwa mujibu wa utafiti huo takribani asilimia 88 ya vifo hivyo kwa mwaka vilisababishwa na uzembe wa madereva,ulevi wa kupindukia na mwendo kasi.

Katika hatua nyingine alitoa mfano wa kusikitishwa na ajali mbaya ya basi la Kampuni ya Mohamedi iliyotokea hivi karibuni Wilayani Korogwe mkoani Tanga na kusababisha vifo vya watu vya zaidi ya watu 28,jambo alilokemea kutohitaji lisikia tena.

Alisema badala ya serikali kufanya ubinadamu mwema kwa wananchi lakini imekuwa ikilazimika kutuma salamu za rambirambi kwa vifo vinavyotokana ama kusababishwa na uzembe wa wachache huku ikiwa na majukumu mengi hatua aliyosema kuwa imechangia kuzorotesha maendeleo.

Aidha ametaja sababu nyingine kuwa ni pamoja na mashindano ya uendeshaji baina ya magari unaotokana na matajiri wa magari hayo hususani wa mabasi kutaka madereva hao kufika mapema kwenye vituo lengwa kwa kile kinachodaiwa cha kuwapa takrima ama posho nzuri nje ya mshahara anaopata.

Rais Kikwete alisema hayo jana kwenye uzinduzi wa miradi mikuu 3 ya barabara iliyofanyi kwenye eneo la Kititimo yenye urefu wa km 224 ya mikoa ya Singida, Manyara na Arusha (Singida, Babati na Minjingu) iliyoko kwenye mchakato wa ujenzi kwa kiwango cha lami kwa miaka 3.

CHANZO: Mwananchi

KATIKA KUMSAIDIA MHESHIMIWA RAIS,AMBAYE PIA NI AMIRI JESHI MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NA USALAMA,KIINI CHA TATIZO NI RUSHWA NA UFISADI.LAITI AHADI ZA 2005 ZA KUPAMBANA NA RUSHWA ZINGETIMIZWA NI DHAHIRI TATIZO LA AJALI ZINAZOSABABISHWA NA TRAFIKI KUTOTEKELEZA MAJUKUMU YAO IPASAVYO (BAADA YA KUSHIKISHWA KITU KIDOGO) LINGEPUNGUA KWA KIASI KIKUBWA.

RAIS ALIKASIRISHWA NA UFISADI KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM NA KUELEZA KUWA ANAWAJUA WAHUSIKA NA ANGEWASILISHA MAJINA YAO KWA MAMLAKA HUSIKA ILI WACGHUKULIWE HATUA.YOU AND I KNOW WHAT TRANSPIRED....JUST LIKE ALIVYOSEMA 2006 ANAWAJUA WALA RUSHWA NA KUWAPA MUDA WA KUJIREKEBISHA...SOUNDS LIKE AN UNDEFINITE DEADLINE.

KUFOKA AU KUONGEZA UKALI HAKUWEZI KUWA UFUMBUZI WA AJALI ZA KILA KUKICHA,ESPECIALLY PALE UKALI WENYEWE UNAPOKUWA NI MITHILI YA KUTEKELEZA WAJIBU TU.YEAH,KWANI WANAOKARIPIWA HAWANA MASIKIO AU MACHO YA KUMAIZI KUWA KUFOKA NA UKALI KWA RAIS HUKO NYUMA HAKUJABADILI CHOCHOTE?

4 Aug 2009


Mkutano mwingine wa Bunge umamilizika huko Dodoma huku danadana ziliendelea kuhusu ufisadi wa Richmond.Wakati Watanzania wakiendelea kumwagiwa "changa la macho",gazeti la Mwananchi linaripoti kuwa Mwanasheria Mkuu,Johnston Mwanyika,ambaye anahusishwa kwa karibu na ufisadi huo,anatarajiwa kustaafu kabla ya kuanza kwa kikao kijacho cha Bunge.Na akistaafu ndio habari imekwisha!Kama unabisha,jiulize kwanini uamuzi wa Lowassa,Msabaha,Karamagi na Chenge ndio ulikuwa mwisho wa kuhusishwa kwao na tuhuma zote zinazowakabili.Yaani mtu anaiba,au anawezesha wizi,au kwa lugha mwafaka ANAFISADI kisha anajiuzulu!Kwa lugha nyingine,anahitimisha utumishi wake uliotukuka kwa heshima zote.


Kwa wale wanaotarajia jipya kwenye kikao kijacho cha Bunge hapo Novemba wanapoteza muda wao.Ngonjera zitakuwa zilezile za "Bunge kuwaka moto kuhusu Richmond","Wabunge wampania Masha","Ngeleja kuwekwa kitimoto",na uzushi mwingine.Kikao kitaanza,wahehimiwa watalambishwa mamilioni yao ya mishahara (huku Watanzania wenzao waliokodoshwa kwa wahindi wa TRL wakizungungushwa kila kukicha na wawekezaji hao feki),na hatimaye kikao kitafikia ukingoni kwa ahadi kuwa "ishu x,y na z zitajadiliwa katika kikao kijacho"


Na bado itapojiri 2010 utaskia watu wazima na akili zao wamefungiwa baa au shuleni (na mgombea mmoja) ili wasinunuliwe na mgombea mwingine!Wawakilishi wetu wanafahamu kuwa hata wakizembea namna gani bado siasa itaendelea kuwa shughuli yenye mvuto mkubwa miongoni mwa wananchi kuliko jambo lolote lile.


Halafu tunaambiwa eti tuna BUNGE LENYE MENO!Labda ya plastiki!

31 Jul 2009


Ushaskia kuhusu political conmanship?Hebu soma kwanza habari ifuatayo kisha tujadili




Spika Sitta aomba ulinzi zaidi, adai nguvu ya mafisadi inahatarisha maisha yake

Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muuangano wa Tanzania sasa anahofia maisha yake kutokana na vitisho vya mafisadi

Spika Sitta aomba ulinzi zaidi, adai nguvu ya mafisadi inahatarisha maisha yake

Kizitto Noya, Dodoma na Boniface Meena

SPIKA wa Bunge Samuel Sitta ameiomba Serikali kumwongezea ulinzi kwa kuwa mafisadi wameongeza nguvu ya vita dhidi yake.

Spika Sitta alisema hayo alipokuwa akizungumzia tuhuma dhidi yake, zilizoripotiwa jana na baadhi ya vyombo vya habari (sio Mwananchi) kuwa anafanya njama kuchoma nyaraka za Bunge.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Spika anadaiwa kula njama ili kuchoma ofisi ya mhasibu wa Bunge ili kuharibu nyaraka muhimu zinazomhusisha na ubadhirifu wa fedha za Bunge.

Lakini Spika Sitta alijibu tuhuma hizo bungeni akisema taarifa hizo zina mkono wa wabaya wake, wenye lengo la kumchafua katika utendaji wake.

“Hivi kama kweli nataka kuficha faili la Bunge nani anaweza kunizuia humu ndani?” alihoji Spika Sitta na kuongeza:

“Hizi ni taarifa za wabaya wangu, wanachofanya ni kuziweka kwenye internet kwanza halafu wanazisambaza kwenye vyombo vyao maalum, magazeti manne; gazeti la Tazama, Tanzania Daima na mengine mnayoyaona," alisema Spika na kuongeza:

“Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba mnipe ulinzi zaidi, hii vita ni ngumu na kubwa sasa. Ulinzi mnaonipa naona hautoshi,” alilalamika Spika Sitta na kuwaponda wanaomwandama kuwa hata iweje, ataendelea kushinda ubunge jimboni kwake na kuwa Spika kama bado atakuwa hai mwakani.

Alifafanua kuwa fedha wanazopeleka maadui zake jimboni kwake Urambo zinasaidia kuimarisha maendeleo, lakini hazitomng’oa madarakani.

"Wananchi wangu wanajua ninachokifanya jimboni kwangu, hata wakipeleka pikipiki bado nitashinda," alisema Sitta.

Mara kwa mara Spika Sitta amekuwa akidai kwamba anaandamwa na mafisadi ambao wanataka aache kufichua maovu yao.

Spika Sitta alisema hayo muda mfupi baada ya kumaliza kutoa mwongozo kwa mbunge wa Micheweni (CUF), Shoka Khamis Juma, kwamba chama fulani kina tabia ya kununua shahada za kura wakati wa chaguzi.

Katika mwongozo wake, Spika alimtaka mbunge huyo kufuta kauli yake bungeni kwa kuwa ushahidi aliotoa kuthibitisha kauli hiyo ni dhaifu.

“Madai ya Shoka ni tuhuma kama tuhuma zozote zinazotolewa na wanasiasa wengine,” alisema.

Akifafanua kuwa Shoka ameshindwa kuthibitisha tuhuma zake kwa kuwa ametoa ushahidi wa magazeti ambayo sio yote yanaweza kuaminika.

“Magazeti yanaweza kuwa chanzo cha taarifa kwa wabunge katika kuchangia hoja zao, lakini sio kigezo pekee cha kumwezesha Spika kutoa mwongozo,” alisema Sitta na kuendelea:

“Hivyo mheshimiwa Shoka hawezi kulindwa na kifungu namba 63 (2), kwa mantiki hiyo namtaka kwa kanuni namba 63 (1) afute kauli yake humu bungeni kabla ya kumalizika kikao hiki cha Bunge”.

Juni 12 mwaka huu mbunge huyo wa CUF alitamka bungeni alipokuwa akiuliza swali la nyongeza kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimekuwa na tabia ya kuiba shahada za kupigia katika maeneo ambayo kinaona hakiungwi mkono.

Naibu Spika Anne Makinda ambaye alikuwa anaongoza kikao cha Bunge siku hiyo, alimtaka mbunge huyo athibitishe kauli yake, naye alifanya hivyo Juni 17, mwaka huu kwa kuwasilisha kwa Spika nakala za magazeti yaliyoripoti uchaguzi wa Jimbo la Busanda.

Hata hivyo, Spika Sitta alisema kwa kuwa hakuna ushahidi wa hukumu kuhusu tuhuma hizo, madai ya Shoka ni tuhuma kama tuhuma zingine zinazotolewa na wanasiasa majukwaani, hivyo kumtaka afute madai yake.




CHANZO: Mwananchi

Nadhani sasa kuna umuhimu wa kuangalia kama Spika huyu wa Viwango na Spidi bado anastahili kuendelea na wadhifa wake ambao ni wa nne kitaifa.Natoa hoja hiyo kwa vile kuna kila dalili kuwa Spika Samwel Sitta sasa anaogopa kivuli chake mwenyewe.




Ni hatari kwa kiongozi wa kitaifa kama Spika kutoa madai mazito namna hiyo pasipo kuwa na uthibitisho wowote.Hivi hao mafisadi wanaohatarisha maisha yake ni akina nani?Nauliza hivyo kwa vile kwa mujibu wa maelezo yake inaonyesha anawafahamu hata kwa majina.Sasa tunapokuwa na kiongozi wa kitaifa ambaye pindi maisha yake yanapokuwa hatarini (kama unaamini anachosema) anakimbilia kuomba aongezewe ulinzi hadharani,then hapo kuna mushkeli.



Ni hatari zaidi kumsikia Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,taasisi tukufu yenye jukumu la kutunga sheria za nchi,akiuliza bila aibui wala uoga "Hivi kama kweli nataka kuficha faili la Bunge nani anaweza kunizuia humu ndani?” You can't be serious,Mzee wa Spidi na Viwango!Yaani unatuambia kuwa kwa wadhifa wako unaweza kuficha nyaraka muhimu za Taifa (mfano faili la Bunge) na hakuna mwenye uwezo wa kukuzuia?Nadhani unatafsiri vibaya madaraka yako.Uspika ni nafasi inayoongozwa kwa taratibu na sheria,za nchi na za Bunge unaloongoza.Sasa unapotuambia kuwa hakuna wa kukuzuia ndani ya Bunge kuficha faili (ukijiskia kufanya hivyo) unatuaminisha kuwa aidha huelewi mipaka ya kazi yako,au unadhani Uspika ni kuwa juu ya sheria za nchi na Bunge,au kulewa madaraka.



Tukiwa hapohapo kwenye hoja yako ya "hakuna wa kukuzuia...",na tukiamini kuwa ni kweli hakuna wa kukuzuia,je utalalamika kuwa mafisadi wanakuwinda wakikuzushia zengwe kwamba umeficha nyaraka muhimu zaidi ya faili la Bunge?Sawa utasema wanakuandama lakini ushawapa hoja kwamba "ukitaka kuficha faili la bunge hakuna wa kukuzuia".Well,wao wanaweza kuja na tuhuma kubwa zaidi ya kuficha faili.Laiti busara zingetumika,ungeishia tu kukanusha tuhuma za kwamba una mpango wa kuchoma moto ofisi za bunge,na sio kukurupuka kudai una uwezo wa kuficha faili la bunge pasipo kuwapo wa kukuzuwia.



Ni rahisi kwa Spika kuomba aongezewe ulinzi (kwa kigezo kuwa ulinzi alionao sasa hautoshi) kwa vile gharama za kuongezewa ulinzi zitabebwa na walipa kodi na si kutoka mfukoni mwa Spika.Hoja hii ya Spika Sitta pia inaweza kufanya tujiulize iwapo licha ya nafasi yake ya Uspika,Mheshimiwa Sitta pia ni mtaalam wa mambo ya ulinzi wa viongozi,na review aliyofanya katika protection anayopewa hivi sasa imempelekea kuhitimisha kuwa ulinzi alionao hautoshi.Hii ni sawa na kuwadharau professionals wenye jukumu hilo,ambao naamini wangetambua mapungufu hayo kabla hata ya Spika Sitta kutamka hadharani.



Lakini twende mbali zaidi kwenye hili la "ulinzi alionao Spika hautoshi"Je anaweza kututhibitishia japo tukio moja linaloashiria kutotosha kwa ulinzi alionao hivi sasa?Yaani kutuhumiwa kuwa anataka kuchoma moto ofisi za bunge, na "maadui zake kumwaga fedha jimboni kwake" vimekuwa matishio ya kiusalama yanayotosheleza kufikia uamuzi wa kumuongezea ulinzi?



Kichekesho ni kwamba wakati Spika akimtaka Mbunge wa Cuf (Mheshimiwa Shoka Hamis Juma) afute kauli yake kwa kuwa "ushahidi aliotoa-katika madai kuwa kuna chama flani kinanunua shahada wakati wa chaguzi-ni dhaifu",yeye mwenyewe anafanya kilekile cha kutoa madai dhaifu kuwa nguvu ya mafisadi inahatarisha usalama wake ilhali hajaweza kutoa uthibitisho wowote zaidi ya "kauli za kisiasa" kuwa maadui zake wanapeleka pesa jimboni kwake ili asirejee bungeni.Ana uhakika gani kuwa hao anaowaita maadui zake si wananchi wenye dhamira ya kuleta maendeleo katika jimbo hilo pasipo kuwa na ajenda za kisiasa?Au Spika Sitta anataka kutuambia kuwa ni yeye tu aliye na hatimiliki ya kupeleka misaada katika jimbo hilo?Jamani,yaani hadi maendeleo ya jimbo yanafanywa kuwa mithili ya maamuzi ya mtu binafsi!?



Kuna mengi ya kujadili kuhusu kauli za Spika Sitta,lakini lililo wazi ni kwamba nafasi anayojipachika ya ukinara wa mapambano dhidi ya ufisadi ni sawa na political conmanship.Kwa lipi hasa?Sio Sitta huyu aliyempa "kifungo" Zitto Kabwe kwa "kosa" la kumkalia kooni Karamagi kuhusu Buzwagi?Sio Spika Sitta huyu aliyetishia kumfungulia mashtaka Dkt Wilbroad Slaa pale mbunge huyo wa Karatu aliposhikilia bango kuhusu ishu za ufisadi?Ni lipi alilofanya Samweli Sitta,kama Spika wa Bunge la Jamhuri au Mbunge wa Urambo linaloweza kumjumuisha kwenye kundi la vinara wa mapambano dhidi ya ufisadi?Yaani Watanzania wenzake kutamani jimbo la Urambo imekuwa ufisadi?Au mtu kutamani nafasi ya uspika imekuwa ufisadi?



Lakini kwa vile siasa zetu kwa sasa zinaruhusu mambo ya ajabu kabisa kutokea,kauli hizi za Spika Sitta hazitawahangaisha wenye dhaman ya uchambuzi wa kauli hatari kama hizi na kuchukua hatua za haraka.Ni business as usual,kauli imetolewa,siku imepita,and life goes on!



Na kwa vile magazeti yetu yako bize zaidi kuripoti habari badala ya kuchambua mantiki ya habari husika,yayumkinika tutasikia makubwa zaidi ya kauli hizi za wanasiasa wanaoogopa vivuli vyao wenyewe.Na kwa vile kilio,kicheko,kuchafua hewa na hata kukoroma kwa mwanasiasa kunatosha kuwa leading news kwenye magazeti yetu,basi tutarajia vimbwanga zaidi.



Trust me,tutashuhudia vituko vingi zaidi na zaidi kadri siku zinavyoyoyoma kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010.By the way,si ndio tunaelekea kile kipindi cha usanii wa kisiasa ambapo watu wazima hupiga magoti majukwani na wengine kutoa shikamoo hata kwa watoto wadogo alimradi wahakikishiwe kura?




30 Jul 2009


Tume huru inayochunguza uhusika wa Uingereza katika vita ya Iraki imetangaza kuwa itamhoji Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair.


Atakayenuna na anune,lakini ni dhahiri kuwa Rais wetu mstaafu ( wa awamu ya tatu),Benjamin William Mkapa,amekuwa akiandamwa na tuhuma za ufisadi wakati akiwa jengo takatifu la Ikulu.Hoja kubwa ya wanaomtetea Mkapa ni maneno kama "Mwacheni Mzee wetu apumzike".

Ni wazo zuri kutosumbua wazee wetu,lakini ingeleta maana kama wazee wote,na si Mkapa pekee,wangekumbukwa katika "maombi" hayo kuwa waachwe wapumzike.Mbona "busara" hizo hazijatumika kuwakumbuka wazee (halisi) wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki?Wamesumbuliwa,wamezungushwa,wametishiwa FFU,na kufanyiwa kila aina ya vituko...tofauti na Mkapa-ambaye hajaomba atetewe au ajitetee-wastaafu hao wanadai stahili yao halali.Hawakutumia ofisi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kununua japo vifusi vya kokoto au kuanzisha chama cha kuweka na kukopa,tofauti na Mkapa ambaye pamoja na mambo mengine anayetuhumiwa kujiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei ya kishkaji na pia kuhusishwa na kuanzisha benki.

Hivi njia bora zaidi ya kumwacha Mkapa apumzike ni kwa wanasiasa kumsafisha katika tuhuma za ufisadi zinazomkabili au kwa mahakama-chombo chenye mamlaka ya kikatiba kutoa haki-kufanya kazi hiyo?Wanasiasa wetu ni wavivu wa kufikiri.Wao ni binadamu,kwa maana hiyo leo wapo kesho hawapo-aidha kiuhai au kimadaraka.Utetezi wao leo unaweza kabisa kuondoka pindi nao watakapoondoka.Uzuri wa taasisi-kama mahakama-ni kwamba inastahili kuwepo kwa muda mrefu au hata milele ikibidi.Na hata ikibadilishwa,misingi yake itaendelea kuwepo.Kwa mantiki hiyo,namna pekee ya "kumwacha Mkapa apumzike" ni kumburuza mahakamani kisha haki itendekee huko.Kupuuza ushauri huu kunaweza kupelekea mzee huyo kuburuzwa kwa nguvu kwenda kujibu tuhuma zake wakati watetezi wake wa sasa hawako madarakani au nao wakiwa wanakabiliwa na tuhuma za kujibu.Hebu chukua mfano mwepesi kama huu.Unadhani Charles Taylor huko aliko anakumbuka flani aliyekuwa anamtetea?Hapo ni kila mtu anabeba mzigo wake.

Sawa,Tanzania sio Uingereza.Na ni kweli kwamba sio kila wafanyalo Waingereza lazima sie pia tulifanye.Lakini mfano wa Blair kufikishwa kwenye tume hiyo ya vita ya Irak inapswa kuwa changamoto nzuri kwa mamlaka zetu kuangalia umuhimu wa kuzingatia sheria na taratibu badala ya kuendekeza ushakaji na kubebana.By the way,si kila mtuhumiwa anayefikishwa kwenye vyombo vya sheria lazima aonekane ana hatia.

Mzee wetu Mkapa hatoweza kupumzika hadi sheria itakapochukua mkondo wake kumsafisha au kumtia hatiani.Kuzembea kufanya hivyo ni kuiachia "mahakama ya umma" (court of public opinion) kumhukumu pasipo kumpatia nafasi ya kujitetea.Na kwa vile mahakama hiyo ya umma haina utaratibu wa kukata rufaa pindi hukumu ikishatolewa,tuhuma dhidi ya Mkapa zitaendelea kuwepo hadi hapo......God knows!Kama wanaomtetea wanampenda kwa dhati (au hata kinafiki) basi ni vema wakamwepusha na hatari ya kuburuzwa mahakamani akiwa na mkongojo wake,say miaka 20 au zaidi kutoka sasa.

Binafsi siamini kuwa wanaomtetea Mkapa wanafanya hivyo kwa vile wanamheshimu sana au wanaamini kuwa tuhuma hizo ni uzushi.Badala yake,wanachelea kwamba wakiruhusu sheria ichukue mkondo wake,kesho wao nao watajikuta wakikabiliwa na hali hiyohiyo kama ya Mkapa.Waadilifu hawaogopi sheria bali wanaiheshimu na kuilinda,lakini wenye mapungufu kwenye maadili yao huiogopa sheria kama kirusi cha mafua ya nguruwe (japo huitumia kuwakandamiza wabaya wao).

Naamini pia kuwa ipo siku Mkapa na watuhumiwa wengine wa ufisadi watafikishwa kwenye vyombo vya sheria.Inaweza kuwa sio kesho au mwaka kesho lakini siku hiyo itafika.Na hapa nazungumzia mahakama za kidunia na sio ile ya kwenye wimbo niupendao wa "na kila mtu atatoa habari zake mwenyewe mbele ya Mungu,siku hiyo itafika...."

Kuendeleza ushkaji katika mambo yanayopaswa kushughulikiwa kisheria kunaweza pia kusambaza kirusi cha "ah mbona yule fisadi anatetewa na kusafishwa,what's wrong with me kufisadi pia?Si nami nitatetewa kama fisadi X..."Hapo tunafanya reproduction ya ufisadi katika jamii.Yayumkinika kuhisi kuwa kwa namna watuhumiwa wa ufisadi wa EPA,Richmond na maskandali mengine wanavyoendelea kuogopwa,tayari mafisadi hao wameshaambukiza virusi vya ufisadi kwa Watanzania wengine chungu mbovu.Thing is,kama wenye maamuzi wameamua kuhalalisha visivyo halali,then visivyo halali vinageuka kuwa halali.

Na kama kuna mzembe ataona wazo langu la kuchukua hatua dhidi ya Mkapa ni ukosefu wa nidhamu,then they can simply shove it up kunakostahili.


Kizitto Noya, Dodoma


SASA ni wazi kwamba sakata la Richmond limeingia katika hatua nyingine baada ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ofisi Rais kutangaza kwamba, Rais Jakaya Kikwete hahusiki kwa namna yoyote na kashfa hiyo ambayo inaendelea kulitikisa taifa kwa muda sasa.

Hatua ya Rais Kikwete kutotaka kuhusishwa na kashfa hiyo ya Richmond kunazidi kuibua maswali mengi kutoka kwa wananchi kwamba, ni nini hatima ya mjadala huo ambao unazidi kupamba moto kila kukicha nje na ndani ya Bunge.

Wakati Rais Kikwete akijivua kutoka katika sakata hilo, Kamati ya Nishati na Madini imetoa maazimio ya kupinga jinsi serikali inavyotekeleza maazimio ya Bunge kuhusu ripoti ya Richmond. Jana jioni Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, ilitoa taarifa ikimuepusha rais na kashfa hiyo.

"Tumepata kusema huko nyuma, na tunapenda kusisitiza kwa mara nyingine kuwa, Rais hana mkono katika Richmond na hata Ripoti ya Bunge iliyotolewa kufuatia uchunguzi katika suala hilo la Richmond, haikumhusisha Rais Kikwete," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa ya Ikulu, imetolewa huku Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba akidai kwamba, Rais Kikwete anahusika na Richmond kwa kuwa maamuzi yalifanyika chini ya serikali anayoiongoza.

Habari kutoka Dodoma zinadai kuwa kutokana na kusuasua kwa utekelezaji wa maazimio ya Bunge kutaka maafisa wa serikali waliohusika kwa njia moja au nyingine na mchakato wa kampuni hiyo kupewa zabuni Tanesco, wachukuliwe hatua.

Kundi mojawapo la wabunge limeeleza kutoridhishwa na ripoti ya serikali iliyotolewa bungeni hivi karibuni kuwasafisha. Kundi hilo limepanga kumchukulia hatua kubwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye ndiye kiongozi mkuu wa serikali bungeni, kutokana na kuwanusuru maafisa waliotuhumiwa kuhusika na kashfa hiyo.

Wakati kamati hiyo ikitoa msimamo huo, wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walikutana jana usiku katika Ukumbi wa Pius Msekwa kutafakari sakata hilo.

Ingawa tangazo la Mwenyekiti wa Bunge, Job Ndugai jana mchana halikueleza agenda za kikao hicho, vyanzo huru vya habari vililidokeza gazeti hili kuwa wabunge hao wangejadili ripoti ya Richmond na kuweka mkakati wa kuinusuru serikali.

Mjumbe wa Kamati ya Nishati na Madini ambaye hakutaka kutajwa gazetini akihofia kuvunja Kanuni za Bunge kwa kutoa siri za vikao, alisema kamati haikuridhishwa na ripoti ya serikali hasa katika suala la kuwasafisha Mkurugenzi wa Takukuru, Dk Edward Hoseah na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika.

"Kamati haikubaliani na ripoti hiyo hasa pale iliposema Dk Hoseah na Mwanyika hawana hatia. Tumekuwa na vikao kwa siku mbili jana (juzi), leo (jana) na bado tunaendelea kesho (leo),”alisema.

Alisema mapendekezo ya kamati ya Bunge kuhusu Richmond yalijitosheleza kimaamuzi na serikali ilitakiwa kuyatekeleza tu na sio kuendesha uchunguzi mwingine.

"Uchunguzi ulishafanywa na Bunge, serikali ilitakiwa kutekeleza tu. Ilikuaje ifanye tena uchunguzi kwa muda zaidi ya ule uliopangwa na Bunge badala ya kufanya utekelezaji?" alihoji.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, William Shelukindo na Makamu wake, Dk Harrison Mwakyembe hawakupatikana jana kuzungumzia suala hilo na simu zao za mikononi kutopatikana kabisa.

Mjumbe wa kamati iliyoundwa na Bunge kuchunguza suala la Richmond, Habib Mnyaa alikiri kuwa na taarifa ya kamati ya kisekta kukutana na kujadili ripoti hiyo, lakini akaeleza kuwa kikao hicho kilichokaa juzi na jana, kinamalizika leo.

"Kikao kimekuwapo, lakini hakijafikia maamuzi hayo unayosema," alisema Mnyaa akirejea hoja ya mwandishi wa habari aliyetaka kuthibitisha taarifa kwamba, kikao hicho kimejenga hoja ya kutokuwa na imani na serikali katika suala la Richmond.

Hata hivyo, habari nyingine zinadai kuwa kamati hiyo leo inatarajia kumweka kiti moto Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja ili awaeleze ni kwanini serikali imeshindwa kutekeleza mapendekezo ya Bunge.

Hata hivyo, mjumbe mwingine, Lucas Selelii alilieleza gazeti hili kuwa vikao vyote vilivyojadili Richmond, vimemaliza kazi na kuwasilisha hoja zake kwa spika wa Bunge Samuel Sitta ambaye leo atatoa mwongozo bungeni.

"Mjadala wa Richmond umemalizika na mambo yote kesho (leo) yako hadharani. Kamati ya kisekta imekaa na kuandaa taarifa ambayo amekabidhiwa spika wa Bunge leo (jana). Kikubwa jamii ijue kwamba, kamati iko makini, haimwonei wala kumpendelea mtu," alisema Selelii.

Alipotakiwa kuthibitisha kama amepokea hoja za kamati hiyo kuhusu Richmond na kwamba ataruhusu mjadala wake bungeni leo, Spika Sita alisema: "Haijanifikia bado".

Alifafanua kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini anatarajia kuwasilisha hoja za Kiwira na Richmond kesho, siku ambayo pia wenyeviti wa kamati za Miundombinu, Ardhi, Maliasili na Mazingira watawasilisha hoja zao.

Alibanwa zaidi aeleze kama endapo angeipata jana jioni angekuwa tayari kuiwasilisha leo kama ilivyoelezwa, alijibu:

"Hata kama nitaipata sasa, siwezi kuitable kesho (leo) kwani nahitaji muda kuisoma na kuielewa".

Awali mbung wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alisema suala la Richmond limeanza kuligawa taifa na njia pekee ya kuirudishia jamii imani na serikali, ni Rais kwa mamlaka ya kuwa mkuu wa nchi kuunda jopo la majaji kupitia upya hoja zote na kutoa maamuzi.

"Suala hili limeonekana kuigonganisha mihimili mikuu miwili ya dola, Bunge na Serikali, dawa yake sasa ili liishe, ni Rais kama mkuu wa nchi nasisitiza, mkuu wa nchi sio serikali kuunda tume ya majaji wapitie Maazimio ya Bunge, utekelezaji wa serikali na watoe maamuzi," alisema.

Alisema: "Inavyoonekana kila upande unavutia kwake, wakati Bunge likitaka serikali itekeleze mapendekezo yake ndani ya miezi mitatu, serikali imetumia karibu mwaka na nusu na bado inakuja na majibu ya kubabaisha.
CHANZO: Mwananchi

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.