8 Oct 2010

Image and video hosting by TinyPic


Urban Pulse Creative ikishirikiana na Aset Inapenda kuwataarifu wadau wote wa Music wa bongo Flava na Hip Hop kuwa imeandaa tamasha maalum linaloitwa URBAN TOUR ambapo msanii Diamond kutoka bongo anayetamba na kibao chake cha Mbagala atakuwepo hapa ukerewere kuanzia mwezi wa November mwaka huu. Wasanii wengine ni Pamoja na First lady wa Urban Pulse Mish Ze Fyah Sis UK Artist anayetamba na single yake Freedom na I don't give a damn.



Tamasha Hili ni kwa ajili ya kuchangia Vita Dhidi ya Malaria Afrika. Diamond ni ambassador wa Malaria Tanzania na ndiye atakekuwa akiwakilisha.
Shows Hivi zitafanyika tarehe 6th Nov Milton keynes, 12th Nov London and 27th Nov Birmingham.
Stay tune kwa habari zaidi.

Asanteni,

Urban pulse Creative.

Katika toleo la wiki hii la jarida la Raia Mwema nazungumzia kuhusu tuzo ya milenia,msaada tuliopewa na Waingereza baada ya kuridhishwa kwao na "nidhamu na matumizi yetu" na sifa alizomwaga Obama kuhusu "utawala bora".Cheki makala hiyo hapa bila kusahau makala na habari nyingine motomoto ndani ya jarida hilo maridhawa.

6 Oct 2010

BABA BABA BABA HUYO BABA BABA BABA BABA BABA HUYO...TUMBA TUMBA TUMBA TUMBA HILO TUMBA TUMBA HILO TUMBA TUMBA HILO...KIKWETE HOYEEEE...NILISEMA WALA RUSHWA NAWAJUA KAMA WAPIGA TUMBA ILA NAWAPA MUDA WA KUJIREKEBISHA...AKINA CHAHALI WANAOHOJI KUHUSU DEADLINE KWANINI HAWAHOJI PIA KUHUSU DEADLINE YA KUJIFUNZA KUPIGA TUMBA? (ACTUALLY,NIKIREJEA IKULU  NTAMSHTAKI HUYU KIJANA HUKO KIBEREGE KWA MZEE MAGU%^&£$%^)


NIMEISHIWA NA AHADI SASA.NGOJA NIJARIBU HII: NAWAAHIDI WATANZANIA KUWA MKINICHAGUA TENA NITAHAKIKISHA KILA MTANZANIA ATAKUWA NA TUMBA YAKE NYUMBANI AMBAYO UKIPIGA TU UNAPATA MAISHA BORA...SI NILIWAAMBIA KUWA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA YANAWEZEKANA?

UFISADI OYEEE,TUMBA OYEEEE

MIE NI ZAIDI YA MORIS NYUNYUSA.ACTUALLY,ZILE NGOMA ZA ULE WIMBO WA TAARIFA YA HABARI YA RADIO TANZANIA NI KAZI YANGU.MCD (BADO YUPO TWANGA?)  NA ALI JAMWAKA AJIRA YENU MASHAKANI.

HUYU ZUMA ANATAKA KULETA HABARI ZA VUVUZELA,HAJUI KAMA MIE MTOTO WA MJINI.AI NEMA NEMA,AI NEMAA AAA,AI NEMA NEMA USIPONEMA LEO UTANEMA LINI

NEMA MWANANGU NEMA
SITAKI WATANZANIA WANIKUMBUKE KWA EPA,KAGODA NA RICHMOND PEKEE.NATAKA PIA WAELEWE KUWA MIE MIE KWA KUYARUDI NDIO MWENYE,IWE ENZI ZA NZAWISA,MAYENU AU HATA MSONDO....SHALO SHALO TINA TINA,YAANI SHAA MTU MZIMA (HEHEHEEE NGWEA NA JAY MO MPO?HATA MIE BONGOFLAVA NAZIJUA PIA.SI MNAWAONA WANABONGOFLEVA KWENYE KAMPENI ZANGU?)

UWEZEKANO WA JAKAYA KIKWETE KUMALIZIA MAUMIVU YAKE YA KUBWAGWA NA DOKTA SLAA (KAMA HAWATACHAKUACHUA KURA) KWENYE UALIMU KATIKA CHUO CHA SANAA BAGAMOYO NI MKUBWA (HOME BOY COMES BACK HOME....DON'T FORGET KIKWETE NI MKWERE).TUSICHOWEZA KUWA NA UHAKIKA NACHO NI WHETHER ATAKUWA MWALIMU WA KUPIGA NGOMA (TUMBA) AU DANSI STUFFS HE FANCIES KAMA PICHA ZA HAPO JUU ZINAVYOONYESHA

HAPPY RETIREMENT MR SOON-TO-BE EX-PRESIDENT



Chanzo: Wandima









Tukiwa tunaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu Tanzania ambao utafanyika October 31, 2010, Watanzania wazalendo wanachama na wapenzi wa Chadema mnaombwa kuchangia kwa dhati harakati za Chadema ili tuweze kuwafikia Wananchi wengi zaidi katika kila kona ya Tanzania tukitafuta ridhaa yenu ya kuweza kujenga nchi yetu; nchi yenye usawa, uzalendo, maadili na uwajibikaji katika miaka mitano ijayo.

CHANGIA CHADEMA KUPITIA BANK:
CRDB BANK
CHADEMA - M4C
Account Number: 0J1080100600

National Microfinance Bank [NMB]
CHADEMA
Account Number: 2266600140

Unaweza kuweka pesa kupitia tawi lolote la Benki hizi Tanzania.


CHANGIA CHADEMA KUPITIA SMS (MESEJI):
Tuma neno:

"CHADEMA" kwenda namba 15710
"NAJIUNGA" kwenda namba 15710
"SLAA" kwenda namba 15710

Unaweza kutuma meseji mara nyingi kadri unavyoweza na kila ujumbe utagharimu TZS 350/= tu.
HII NI KWA MITANDAO YA ZAIN, TIGO NA VODACOM TU.

CHANGIA KUPITIA M-PESA:
Kwa watakaotaka kuchangia kwa M-Pesa wanaweza kutumia namba zifuatazo:

0758 223 344
0764 776 673


CHANGIA KUPITIA ZAP:
Kwa watakaotaka kuchangia kwa ZAP wanaweza kutumia namba hii:

0789 555 333

"Ndugu Zangu Watanzania, tunawaomba kwa dhati kabisa tushikamane, tushirikiane bila kujali itikadi zetu kuchangia harakati hizi, tunawashukuru sana. - Dr. Wilbroad Peter Slaa"

CHAGUA MABADILIKO YA KWELI. CHAGUA CHADEMA.









Kwa hisani ya SUBI

4 Oct 2010

France


France


Sweden


Germany

Add caption


3 Oct 2010




Blogu hii inapenda kutoa salamu za pongezi kwa mpambanaji na mwanaharakati mahiri,Mwalimu Nkwazi Mhango (a.k.a Mpayukaji Msemaovyo) mwenye makazi yake nchini Kanada kwa kutuletea mpambanaji mwingine wa kiume.Ujio wa mwanaharakati huyu mchanga unaweza kuwa dalili njema hasa kwa vile tupo kwenye mchakato wa kuwatimua mafisadi wanaofakamia keki ya taifa letu kama hawana akili nzuri.

Naungana na Mwalimu Nkwazi na familia yake kumtakia kijana wetu afya njema na kila mafanikio ili pindi muda utapowadia ajumuike nasi katika harakati zetu za kupigania usawa katika jamii.

1 Oct 2010

"Ufisadi Oyeee.Tupeni tena miaka mitano tuwakwangue kabisa".Of course ni unatarajia nini hapo?

Mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete akiendelea na ngwe ya kuwatetea rafiki zake.Alianza na Lowassa,akaenda kwa Mramba,kisha kwa Mzee wa Vijisenti Chenge,na sasa kwa "baba lao" Rostam Aziz.Ama kweli Tanzania bila ufisadi inawezekana!

Wakati "ndege wenye manyoya yanayofanana wakiruka pamoja",Dokta Slaa anaendelea na darasa la kuwahamasisha wenye uchungu na nchi yao kufanya kila liwezekanalo kuwang'oa "ndege hao"


Wananchi mjini Songea wakimsikiliza Rais Mtarajiwa kwa makini
Picha zote kwa hisani ya Jamii Forums

30 Sept 2010

UTITIRI WA AHADI ZA KIKWETE NI KAMA UTAMU WA PIPI HIZO ANAZOMPATIA MTOTO HUYO PICHANI.PIPI NI TAMU KADRI INAVYOYEYUKA MDOMONI LAKINI SIO TU HAIDUMU BALI HAIONDOI NJAA.

Hebu soma kwanza nukuu hii hapa chini kisha utaelewa kwanini nimeweka kichwa cha habari hicho hapo juu

MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amesema moja ya kazi kubwa itakayofanywa na serikali yake katika kipindi cha miaka mitano ijayo ni kumsaidia mkulima wa Tanzania aweze kulima kwa kutumia trekta badala ya jembe la mkono.
Rais Kikwete aliyasema hayo alipokuwa akiwahutubia wakazi wa kata ya Lyabukande, jimbo la Solwa wilayani Shinyanga katika moja ya mikutano yake ya kampeni iliyofanyika jana.
“Katika miaka mitano ijayo iwapo mtatupa ridhaa ya kuendelea kuongoza nchi hii, tumepanga kumsaidia mkulima ili aweze kuboresha kilimo chake kwa kumwezesha kulima kwa trekta badala ya jembe la mkono alilolizoea enzi na enzi,” alieleza Rais Kikwete.
Alisema iwapo mkulima atasaidiwa katika kilimo chake, ataweza kujikomboa kutokana na umasikini na kumuwezesha kuwa na maisha bora kama ambavyo sera ya CCM inavyoelekeza.
CHANZO: Majira

Sio siri,inaudhi,inakera na inachukiza.Hivi huyu Jakaya Kikwete siye aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu mwaka 2005 hadi leo hii?Ofkozi,jibu ni ndiyo.Sasa hizi habari za kusema atamsaidia mkulima kuondokana na jembe la mkono kwanini ziwe leo na sio mwaka 2005 au 2006 au 2007 au 2008 au 2009 au hata mapema mwaka huu?



Kwa kweli kama kuna Watanzania bado wanajishauri kuhusu wampigie au wamnyime kura Kikwete basi utitiri wa ahadi anazoendelea kutoa,huku nyingi zikiwa ni marejeo ya alizotoa wakati wa kampeni zake za mwaka 2005 ni sababu moja kati ya maelfu ya sababu ya kustaafisha urais kwa kumyima kura.Tena huyu hapaswi kushindwa kwa tofauti ya kura chache bali stahili yake ni kile kiitwacho anguko la pua.

Hakuna maelezo mengine zaidi ya kuamini kuwa Kikwete anawafanya Watanzania ni wapumbavu maana vinginevyo asingediriki kuongea upuuzi kama huu wa kuahidi kuwakomboa wakulima eti akipewa miaka mingine mitano ilhali hii anayomaliza ameitumia zaidi kuzurura huko nje ya nchi.Na kwa angalizo tu,huyu mtu amezowea sana kusafiri,sasa kwa vile amelazimika kukaa nchini kwa zaidi ya miezi miwili sasa basi wapiga kura mkirogwa tu kumrejesha atafanya utalii wake kwa hasira,perhaps on weekly basis badala ya monthly basis kama tulivyozowea.

Badala ya kuwaomba msamaha wakulima kwa kuwapuuza kwa muda wote aliokuwa madarakani yeye anakuja na hadithi mpya kuwa anadhamiria kuwatoa kwenye kilimo cha jembe la mkono.Hayo matrekta hewa yatanunuliwa kwa fedha zipi ilhali priority ya serikali yake ni ununuzi wa magari ya kifahari na samani za bei mbaya kwa watawala?

Na wakulima wakishapatiwa matrekta,je ziada ya mazao yao itauzwa wapi ilhali vyama vya ushirika vimeendelea kuwa taasisi maalum za kuwafisadi wakulima?Kama kweli alikuwa na nia ya kuona mkulima anaondokana na jembe la mkono kwanini basi zile fedha "zilizorejeshwa" na mafisadi wa EPA hazikutumiwa kwa dhamira hiyo?Lakini kwa kuonyesha kuwa anawazuga tu wakulima,alipotangaza "stimulus package" ya kisanii,waliopewa kipaumbele ni wafanyabiashara huku wakulima wakisahaulika.

Naomba nisiandike zaidi.Kikwete ni mbabaishaji na hana jipya.Haihitaji majini ya Sheikh Yahya kufahamu kuwa ahadi alizokwishatoa hadi sasa zinahitaji awe rais wa maisha ili atekeleze japo nusu ya ahadi hizo.Haiwezekani kutoa ahadi kila kukicha ilhali kuna lundo la ahadi zinazosubiri utekelezaji.

Chonde chonde Watanzania,kumbukeni kuwa kama Kikwete ameweza kufanya masihara katika awamu yake ya kwanza huku akijua fika kuwa mwishoni mwa awamu hiyo angesimama tena majukwaani kuomba ridhaa ya kuchaguliwa tena,pata picha awamu yake ya pili ambapo hatohitaji tena kura itakuwaje!Tafakari maneno haya kwa makini sana kwa sababu pindi mtu huyu akirejea Ikulu basi sote tumeliwa.Kidogo kilichobaki kitakombwa na kukwanguliwa kabisa.Na kwa namna ufisadi ulivyoshamiri katika awamu yake ya kwanza basi yayumkinika kubashiri kuwa pindi akichaguliwa tena (God forbid) basi si ajabu Watanzania kushtukia nchi yetu imeshauzwa na hatuna pa kwenda.

Bahati nzuri,katika uchaguzi wa mwaka huu hatuna tena tatizo lililokuwa likitukwaza hata kufikiria mbadala wa CCM.Zama hizo tulikuwa tunasema "sasa tusipoichagua CCM tukichague chama gani ilhali vyama vyenyewe ni bora ya hiyo CCM".Mwaka huu Mungu amesikiliza kilio chetu na kutupatia ufumbuzi mapemaaa.Tumeletewa Dokta Wilbroad Slaa,mwanasiasa ambaye kwa hakika amejidhihirisha bayana kuwa ana uchungu wa dhati kwa Tanzania na Watanzania.


TANZANIA BILA UFISADI INAWEZEKANA.TANZANIA BILA MAFISADI WANAOLINDWA NA KUPIGIWA KAMPENI NA KIKWETE INAWEZEKANA PIA.MPE KURA YAKO DOKTA SLAA NA MPATIE WABUNGE WA KUTOSHA WA KUUNDA SERIKALI NDOGO YA UFANISI NA YA UKOMBOZI WA MTANZANIA.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.