21 Oct 2009


DANADANA KUHUSU SUALA LA RICHMOND IMEZIDI KUENDELEA.BINAFSI SIDHANI KAMA SUALA HILI LITAPATIWA UFUMBUZI UNAOSUBIRIWA NA WATANZANIA WENGI.KUPATA UFUMBUZI,KWA MAANA YA KUWEKWA BAYANA UKWELI WA UTAPELI NA UJAMBAZI HUO UTAMAANISHA WATU MUHIMU KUPOTEZA NYADHIFA ZAO.SIO KWAMBA HILO NI BAYA BALI HALIWEZEKANI KATIKA MAZINGIRA YA SIASA ZETU ZA KUJIKOMBA,KUOGOPANA NA BORA LIENDE.


PENGINE HII NI SABABU NYINGINE MUHIMU KWA WAPIGAKURA KUIHOJI CCM COME THE 2010 ELECTION.HEBU SOMA KWANZA HAPA CHINI:


Mazingaombwe tupu Richmond


• Shellukindo anuna, akataa kuulizwa maswali

na Deogratius Temba

KWA mara nyingine tena, serikali jana ilishindwa kuwasilisha maelezo ya utekelezaji wa maazimio 23 ya Bunge kuhusu hatma ya kashfa ya Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.

Licha ya kauli thabiti iliyotolewa na Mwenyekiti wa kamati hiyo, William Shellukindo mwanzoni mwa wiki kwa waandishi wa habari kuwa, serikali ingetoa maelezo hayo kwa kamati yake jana, hali ilikuwa tofauti baada ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kutotokea katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam, ambako kamati mbalimbali za Bunge zinaendelea na vikao vyake.

Kwa mujibu wa ratiba mpya ya vikao vya kamati hiyo vinavyoendelea katika ofisi hizo, jana kamati ilipanga kupokea taarifa hiyo na kuanza kuijadili kwa muda wa siku mbili, baada ya wiki iliyopita kuahirishwa kwa kile kilichoelezwa kuwa Waziri Ngeleja alikuwa nje ya nchi.

Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano lilizipata kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini zilieleza kuwa, walipokea ombi la serikali la kuahirishwa kwa mjadala huo ili ijipange sawasawa.

Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo alieleza kuwa, serikali katika ombi lake kwa kamati, iliitaka kuliweka suala hilo pembeni hadi baadaye itakapoarifiwa, na ilitaka kuendelea na ratiba zake nyingine kama zilivyopangwa.

“Ni kweli leo (jana) tulikuwa tuipokee taarifa ya serikali kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge, lakini haya ni masuala yanayoihusu serikali zaidi, wameomba tuendelee na kazi nyingine, wanaweza kuiwasilisha kesho (leo) au keshokutwa (kesho),” alisema mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo aliyeomba jina lake lisitajwe kwa sababu si msemaji.

Alieleza zaidi maelezo kamili ya kuahirishwa kwa upokeaji maelezo ya serikali yanaweza kutolewa na mwenyekiti wa kamati hiyo, Shellukindo, ambaye ndiye aliyepokea ombi hilo la serikali.

Shellukindo alipoulizwa kuhusu hali hiyo, aligeuka mbogo kwa waandishi wa habari kwa kuwataka wasimuulize maswali kuhusu Richmond. Kwa ukali aliwataka waulize maswali yanayohusiana na kampuni ya kuzalisha umeme wa gesi ya Songas, ambayo ilikuwa ikijadiliwa na kamati yake jana.

“Nataka kuwaeleza tulichozungumza na watu wa Songas, lakini nikimaliza nitakaribisha maswali ambayo yatahusiana tu na suala hili la Songas, nje ya hapo sitajibu,” alisema Shellukindo.

Msimamo huo wa Shellukindo uliwafanya waandishi wa habari waliokuwa na shauku ya kutaka kujua sababu za serikali kushindwa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji maazimio ya Bunge ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa na watu wengi, kushikwa na butwaa na kushindwa kuuliza maswali kwa muda.

Baada ya dakika chake, Shellukindo ambaye alionekana kutokuwa katika hali ya kawaida, alieleza kuwa kamati yake imezungumza na uongozi wa Kampuni ya Songas kuhusu utengenezaji wa mashine ya kuzalisha umeme wa megawati 20 iliyoharibika wiki iliyopita na upatikanaji wa gesi nchini.

Hata hivyo katika hali ambayo haikutarajiwa na waandishi wa habari, wakati Shellukindo akiendelea kutoa maelezo, wajumbe wa kamati walianza kusimama mmoja mmoja na kuondoka na walipoulizwa sababu ya kuondoka katika kikao hicho, walidai kuwa wana majukumu mengi ya kufanya.

Kabla ya Shellukindo kuanza kuongea na waandishi wa habari, Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe ambaye ni kinara wa kashfa hiyo, alisimama na kutoka nje. Mwakyembe amekuwa hazungumzi lolote na waandishi tangu kuanza kwa vikao vya kamati hiyo.

Awali Tanzania Daima Jumatano lilielezwa kuwa, taarifa hiyo haitawasilishwa kwa kamati hiyo ikiwa jijini Dar es Salaam kwa sababu za kiusalama na badala yake itawasilishwa mjini Dodoma.

Taarifa hizo zilieleza kuwa, wajumbe wa kamati ya Shellukindo watapata nafasi ya kuijadili wakiwa Dodoma na endapo watairidhia wataruhusu serikali iiwasilishe bungeni katika mkutano wa 17, utakaokuwa ukiendelea. Mkutano huo unatarajiwa kuanza Oktoba 27.

Taarifa nyingine zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa, serikali ina hofu kuwa, iwapo itaitoa taarifa hiyo kwa kamati ya Shellukindo mapema, inaweza kuvuja na kutoa mwanya kwa baadhi ya watuhumiwa wa Richmond kujipanga namna ya kujisafisha au kupoteza baadhi ya vielelezo.

Mmoja wa viongozi wa serikali aliyezungumza na gazeti hili katika eneo la ofisi ndogo za Bunge jana, alisema serikali imekuwa ikisita kuiwasilisha taarifa yake kwa kamati hiyo kwa sababu inaweza kuvuja na kuvuruga mwenendo wa mambo.

“Hofu yetu ni kwamba, serikali ikiwasilisha taarifa hii mapema, hadi kufikia siku ya kuijadili bungeni itakuwa imezagaa mno, taarifa kuenea si jambo jema, watuhumiwa wanaweza kujipanga, inatakiwa iwe ya kushtukizia,” alisema ofisa huyo.

Katika mjadala huo uliokamiwa na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo, wajumbe pamoja na mambo mengine wataangalia kama serikali imejibu maswali na maagizo ambayo Bunge liliipa serikali.

Wakati Bunge likitaka watu zaidi waliohusika wawajibishwe, tayari mmoja wa wawakilishi wa Kampuni ya Richmond, Naeem Adam Gire, ameshafikishwa katika Mahakama ya Kisutu, Dar es Salaam Januari 13, mwaka huu na kusomewa mashtaka matano ya makosa ya jinai.

CHANZO: Tanzania Daima

MAAMUZI YA KUIPA TENDA RICHMOND HAYAKUFANYIKA KWENYE KIJIWE CHA KAHAWA BALI KWENYE OFISI NYETI.SASA KWANINI KILA ALIYEHUSIKA KWENYE MAAMUZI HAYO ASIWEKWE HADHARANI?JIBU JEPESI NI KWAMBA KUFANYA HIVYO KUNAWEZA KUPELEKEA "KUISOGEZA 2010 KABLA YA MUDA WAKE" (READ BETWEEN THE LINES,PLZ).

19 Oct 2009


I would like to understand a few things about this Miss EA Schengen competition (as there seems to be a lot of Miss competitions popping up with the notion of empowering young women). For anyone who can help, please do share your knowledge. Earlier attempts to speak to Mr. Charles Gadi were futile, as he hung up on me, upon me saying I did not recognise what the company was. Most importantly, we would like to know who is behind the organisation. What is their background? Who is training the girls? What do these individuals do for life? The girls competiting are required not to have "poor behaviour or they will be disqualified". Are the organisers, trainers etc squeaky clean? Will their background impart "beauty, culture and purity" to the girls? Do you really, really know who is working with your daughters and sisters? DO YOU??

So my questions;

1. What kind of organisation is this? Is it an individuals company or an NGO? What is the registration number if anyone knows, and when was it registered. Who is on the board?

2. On the website, the contact is not clear, there is only an e-mail and phone number but no physical address.

3. What kind of health (or any other) insurances are in place for young girls participating in this event?

4. The organisation aims to encourage people to visit East African countries etc. Is this encouraging East Africans in the diaspora to go back to their own countries, or they are targeting Europeans? If so, how is this being marketed to them?

5. One of the entry requirements is; girls must be single and have no children. Why specifically single? Is this a discrimination on young girls who might have boyfriends? Does it make them improper to serve the community?

6. I see there are only 2 sponsors, one travel company and a restaurant. Are they the main sponsors of the event? Do they provide the presents for these young girls? I believe, it is important to have transparency, and it would be encouraging to see the companies put forward what they are actually sponsoring, so that come the time their word will be legally binding (mainly to the participating girls). I would hate to see naive young girls being exploited.

7. Does the company provide psychological support to young girls who might be vulnerable to insults that will no doubt pop in different blogs whereby the individual has decided to market. It is one thing to claim to build confidence in young girls, it is another when individuals elsewhere try and knock young girls' confidence. A proper organisation should have these things in place.

8. On that note, a concerned parent has recently called the organiser, Mr. Gadi in relation to the pictures and more importantly to a "bongoflava" cheap $2 video (NOTE: $2 is a compliment), which consists of lyrics that arent pleasant to a parent, with videos of the young girls pictures flashing. He has been asked to remove them, the singer has been requested to remove them. In reply Mr. Gadi said "Maybe I will do", "I will see what I can do" or "They are 18 years, they can decide what they want". I believe on this note, an organiser creating a reputable organisation, promoting positivity for the girls, shows a lack of understanding and respect to a concerned parent and our beautiful african culture. I believe the organiser has a family, and needs to think like a family man. So if anyone else knows who is running this organisation, it will be wise to share it, so they can be contacted, perhaps they might show sense and discuss as grow ups.

9. It may be neccessary to contact the different ambassadors to understand their involvement in this event, and whether they endorse the carefree nature of dealing with parents as shown by this particular organiser.

10. For parents who have young girls competiting for these events, it is important you ask questions and make sure your children's interests are best served. Where will your girls be staying? How are they funding their travelling costs? Will these costs be recouped regardless of whether they win or lose?

Food For Thought for parents: What do you want your young girls to achieve from this? Is it attention? Fame? Material things? If helping the community, is parading on stage and being viewed as an object what your daughter is about? In terms of modelling, in Europe there are a lot of very genuine modelling companies with clear procedures on how they are run. My word is, ask questions, talk to your friends, advise them and do the right and sensible things for your young daughters and sisters.

Best of Regards,

Denis

Defunkadelic

(Please feel free to contact me in private and in confidence. I am accessible on the e-mail (and my mobile no. is available on request via e-mail), I will be happy to speak out when you do not dare, where neccessary, you can always rely on the rule of law).

17 Oct 2009


By GAUTAM NAIK and MARK SCHOOFS

Researchers from the U.S. Army and Thailand announced last month they had found the first vaccine that provided some protection against HIV. But a second analysis of the $105 million study, not disclosed publicly, suggests the results may have been a fluke, according to AIDS scientists who have seen it.

The second analysis, which is considered a vital component of any vaccine study, shows the results weren't statistically significant, these scientists said. In other words, it indicates that the results could have been due to chance and that the vaccine may not be effective.

The additional data were available to the researchers on Sept. 24 when they announced the trial results, but they chose not to disclose them, said Jerome Kim, a scientist with the U.S. Army who was involved in the study. News of the second analysis was first reported on the Web site of Science magazine, but the story didn't provide specific data. Full details of the trial are to be aired at an AIDS meeting in Paris that starts Oct. 19.

The incomplete disclosure raises the question of whether the Army, the Thai government and the U.S. National Institutes of Health -- which helped fund the study -- rushed to give a positive spin to what may turn out to be another inconclusive AIDS-vaccine effort.

"We thought very hard about how to provide the clearest, most honest message," Dr. Kim said. "We stand by the fact that this is a vaccine with a modest protective effect." He called the trial results "complex."

Anthony Fauci, director of the National Institute of Allergy and Infectious Diseases, the part of the NIH that oversees AIDS research, declined to comment.

The study was criticized as pointless by some AIDS scientists when it was launched three years ago because it combined a failed vaccine with one widely thought to have little chance of success. It was the largest HIV vaccine trial ever conducted, with more than 16,000 participants in Thailand.

Some AIDS researchers and activists who have learned of the additional data still think the vaccine shows promise and should be investigated further. But they worry that not disclosing the study transparently will cause people to conclude the vaccine trial was a failure and undermine support for more research.

"I would have preferred to have seen both results straight up. It might spring back on them, and that would be unfortunate," said Mitchell Warren, executive director of the AIDS Vaccine Advocacy Coalition in New York.

About 33 million people were living with HIV world-wide in 2007, according to the latest United Nations statistics. About two million people died from AIDS that year. There have been more than 100 HIV vaccine trials since 1987. None had succeeded until the latest Thai trial.

The results announced last month were based on a "modified intent to treat analysis," which includes virtually everyone who enrolled in the study, regardless of whether they ended up getting the full course of the vaccine. It is a good stand-in for the real world, where people don't always follow instructions properly. By this measure, the vaccine tested in Thailand reduced by 31% the chance of infection with HIV, the AIDS-causing immunodeficiency virus.

But the result was derived from a small number of actual HIV cases: New infections occurred in 51 of the 8,197 people who got the vaccine, compared with 74 of the 8,198 volunteers who got placebo shots. Statistical calculations showed there was a 3.9% probability that chance accounted for the difference. In drug and vaccine trials, anything above a 5% probability of a chance result is deemed statistically insignificant.

The second analysis is called "per protocol" and adheres strictly to how the trial was designed by only including the study participants who got the full regimen of vaccine shots at the right time. Because it excludes study participants who didn't get the full vaccine regimen, it usually provides corroboration to the looser "intent to treat" findings.


Two AIDS scientists, who have seen the "per protocol" analysis, said it indicates there is a 16% chance the study results were a fluke -- a far greater probability than is considered statistically acceptable. This analysis included 86 people who received either the vaccine or a placebo and were infected. The "per protocol" analysis also showed that the supposed effectiveness was lower, at 26.2%. Dr. Kim, of the U.S. Army, declined to comment on the data. It isn't clear why the vaccine was seemingly ineffective among participants who followed the guidelines to the letter.

These anomalous results sparked discussion last week at a meeting of the Center for HIV-AIDS Vaccine Immunology in Durham, N.C. The group is made up of a team of universities and academic medical centers established by the NIH to help vaccine design and development.

"I think in general it's best to lay out as much data as possible," said Barton Haynes, director of the center and an HIV vaccine expert at Duke University, who was at the meeting. "This is a very difficult situation for everyone, and we'll have to wait until all the data are released so we can drill down into it."

When drug or vaccine trials results are disclosed, it is common for investigators to simultaneously provide "per protocol" and "intent to treat" data. For example, when Merck & Co. announced the details of its failed HIV vaccine trial in 2007, the Whitehouse Station, N.J., company provided both sets of statistics at the same time.

In September, the AIDS Vaccine Advocacy Coalition published a report in anticipation of the Thai results that noted: "The safest route is to report both PP [per protocol] and ITT [intent to treat] and to analyze the difference."

In January 2004, a group of 22 scientists in article in the journal Science noted that one component of the Thai vaccine, a primer dose made by Sanofi Pasteur, a division of Sanofi-Aventis SA of France, was poor at triggering an immune response. They also pointed out that trials of the second component of the Thai vaccine, a booster component now licensed to Global Solutions for Infectious Diseases, of South San Francisco, Calif., had been proven "to be completely incapable of preventing or ameliorating HIV-1 infection."

They added: "One price for repetitive failure could be crucial erosion by the public and politicians in our capability of developing an effective AIDS vaccine collectively."



16 Oct 2009





Far-right Dutch politician Geert Wilders sparked angry protests today as he declared that Islamic culture is inferior to Christianity.The MP was met by angry Muslim protesters when he arrived in the UK after winning a court battle to enter the country.Around 40 demonstrators gathered near the Houses of Parliament as Mr Wilders, whose film Fitna criticises the Koran as a 'fascist book', arrived in central London.Brandishing banners saying 'Sharia is the solution, freedom go to hell' and 'Geert Wilders deserves Islamic punishment', the protesters were held back by police...READ MORE



A black adviser to police on race issues has accused officers of 'horrendous harassment' as he revealed he has been stopped by officers more than 100 times.Ken Hinds, 50, attacked the Metropolitan police for 'racial profiling' as he revealed he had been repeatedly stopped in the past two decades.And he said other people have suffered similarly disproportionate treatment while driving, on the street and at Tube and railway stations

Mr Hinds of Edmonton, north London, sits on the force's Black Independent Advisory Group and is chairman of a monitoring group for stop and search in Haringey.
Earlier this week he won an apology and £22,000 compensation from British Transport Police (BTP) after he was handcuffed as he watched a black youth being arrested at Seven Sisters Tube station in 2004...READ MORE



Picha kwa hisani ya vyanzo mbalimbali mtandaoni.


MBUNGE wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge jana alinguruma ndani ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, alipowataka Watanzania kuacha kutafuta mchawi aliyeua mashirika ya umma, akisema kuwa mengi yalikufa yakiwa mikononi mwao na si mwa wageni.

Chenge, mwanasheria mkuu wa zamani wa serikali, ametoa kauli hiyo wakati wananchi wengi wakilalamikia mikataba mibovu ya uwekezaji na uendeshaji mashirika ya umma kuwa ndiyo iliyochangia baadhi kufa na mengine kuwa katika hali mbaya.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati akichangia Taarifa ya Utekelezaji wa Moboresho ya Shirika la Bima (NIC), Chenge alisema makaburi mengi ya mashirika ya umma yamechimbwa na Watanzania wenyewe.

"Leo (jana) wakati tunamalizia kuadhimisha miaka kumi ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, shirika hili la Bima lilikuwa moja ya malengo yake," alisema Chenge akirejea NIC ambayo ilikua na kutapakaa nchi nzima kabla ya kuanguka kiuchumi kiasi cha kusababisha serikali kuingilia kati na kuitengenezea muundo mpya.

"Lakini shirika hili leo liko hoi; kwa vyovyote vile serikali haiwezi kusimamia shirika hili kwa asilimia 100, lazima likabidhiwe kwa sekta binafsi, lakini Watanzania tumekuwa ni watu wa kupenda kupiga kelele hasa tunapoamua kubinafsisha. Mashirika haya tumeyaua wenyewe wala si wageni."

Chenge alisema: "Watanzania hatupaswi kutafuta mchawi wa mashirika yetu haya. Sisi wenyewe ndiyo tumeyaua na makaburi mengi leo hii yanaonekana."

Alifafanua kwamba, umefika wakati sasa Watanzania wakaachana na dhana ya kulalamika na badala yake wafanye kazi kwa bidii, huku pia akiitaka serikali iondoe dhana ya kuendesha mashirika kijamaa, akitolea mfano uwekaji wa kiwango cha chini cha bei na kutaka bei ya soko ishike hatamu.

Hata hivyo, alionyesha wasiwasi na Kikosi Kazi kinachofanya marekebisho kutokana na kukosa bodi na kuongeza: "Napata shaka kidogo, chombo ambacho kinaandaa taarifa halafu chenyewe pia ndio kijitathmini, nafikiri inapaswa kuundwa bodi."

Akichangia katika kikao hicho cha Kamati ya Fedha na Uchumi, Mbunge wa Tabora Mjini, Juma Kaboyonga aliitaka serikali kuharakisha ununuzi wa nyumba za NIC ambazo thamani yake ni Sh31.7 bilioni.

Mbunge huyo ambaye kitaaluma ni mchumi alisema serikali haipaswi kucheza na NIC, hivyo ni lazima itafute fedha hizo ili kuliwezesha shirika kwenda kwa kasi zaidi.

Kaboyonga alidai kuwa kumekuwa na hujuma dhidi ya NIC na kuhoji kwamba "kama mashirika binafsi yanaweza, vipi NIC ya serikali ishindwe".

Alisema: "Ipo dhana kwamba mashirika ya serikali hayana wenyewe, lakini mimi nasema yana wenyewe na wenyewe ni wananchi, lazima NIC iangaliwe, iwezeshwe na ipewe mtaji."

Akijibu hoja mbalimbali, Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremia Sumari alisema serikali imepanga kuendeleza huduma nafuu na zenye ubora kutokana na kuamini NIC inaweza kujiendesha kwa faida zaidi.

Sumari alisema uamuzi huo wa serikali kupanga kutoa huduma bora na za gharama nafuu haumaanishi kuwa nchi inarejea kwenye ujamaa, bali ni kuangalia uwezo wa shirika na mahitaji ya Watanzania.

Kuhusu mtaji na mpango wa kununua nyumba za NIC kwa Sh31.7 bilioni, alisema hilo liko katika hatua nzuri na za mwisho na kuongeza: "Lakini hadi sasa nyumba hizi ni za serikali, kuna mahitaji ya nyumba kwa watumishi wetu kama waheshimiwa majaji n.k."

Dk Abdallah Kigoda, ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo, alisema katika majumuisho yake kuwa kuna umuhimu wa serikali kulipatia shirika kiasi hicho cha fedha.

Alisema:" Sioni tatizo kwa serikali kutoa au kukopa Sh31.7 bilioni kuokoa shirika kubwa la umma kama hili, nafikiri kuna umuhimu wa kulipatia kiasi cha fedha kwa sasa."

NIC iko katika kipindi cha mageuzi baada ya kuwepo mvutano kati ya serikali na bunge, hasa tathmini ya mali ambayo awali ilikuwa Sh18 bilioni, lakini Kamati ya Fedha ikaikataa na kutaka ifanyike upya.

Tathmini mpya iliyoonyesha kuwa thamani ya mali za NIC ni Sh31.7 bilioni ilikubaliwa na mwezi Februari, Rais Jakaya Kikwete aliunda Kikosi Kazi kilicho chini ya Balozi Charles Mutalemwa kufanya mageuzi ya shirika hilo.

Hadi Februari wafanyakazi waliokuwa nje ya ajira wakati huo walilipwa malimbikizo ya mishahara yao kwa jumla ya Sh1.90 bilioni.

CHANZO: Mwananchi

MBONA MAMBO!?


NDUGU YANGU Mpayukaji Msemaovyo anasema:

Naitwa Mchumiatumbo mwana wa Tapeli.

Ingawa wakati naandika waraka huu vijana wenzangu wapatao 166 wamo wakimenyeka toka Mwanza hadi Butiama, kama ishara ya kumbukizi ya safari yako adhimu ya ukombozi ukiliungua mkono marehemu azimio la Arusha, mimi sitafanya hivyo.

Nina sababu. Kwanza mimi ni mnafiki wala mjamaa kama wewe. Nina roho nyepesi hasa nionapo vitu kama pesa madaraka na sifa.

Mimi ni mbabaishaji na muongo; au msanii kama washikaji wasemavyo. Ni fisadi through and through. Ninanuka kiasi cha kutostahili hata kukaribia kaburi lako achia mbali nyumba yako, wanao, mkeo, watu wako hata taifa lako. Nisingependa walevi na wazinzi kufagia makaburi ya mitume mwalimu. Hivyo, kwanza nakuwa mkweli kwa nafsi yangu na kwako na umma wako.

Tatu, nitaunga mkono azimio lipi iwapo ninaoona wamenizunguka wakiwaibia watu wako ni wale wale walioliua azimio la Arusha? Nitaadhimisha vipi iwapo miiko ya uongozi na usawa wa binadamu vimetoweka na nafasi yake kuchukuliwa na ufisadi, ujambazi wa mchana, ubabaishaji na uongo?

Nne, mwalimu, sitaki kujidanganya na kukudanganya. Kile ulichopigania kwa sasa hakuna. Ulipigania uhuru na maendeleo. Sasa kuna utumwa na kuporomoka. Ulitekeleza ujamaa na kujitegemea. Sasa tuna uhujumaa na kujimegea. Ulipigania mstakabali wa nchi toka kwa wakoloni wawe wavumbuzi, wamisionari na watawala. Sasa mstakabali huo umo mikononi mwa wawekezaji, na wafadhili wa makuadi wao. Ulipigania ardhi ya Tanzania kabla haijaingia mikononi mwa vijifalme vya kifamilia. Nitakuenzi kwa udhu upi iwapo kila nipitapo Loliondo nakaribishwa kwenye falme za kiarabu utadhani hapa ni uarabuni?

Nitapata wapi mshipa wa kukuenzi wakati nakung’ong’a? Je mwalimu una habari? Yale madini uliyosema vizazi vijavyo vingeyaendeleza na kufaidika nayo yaliuzwa na jamaa yako Tunituni uliyempigia debe usijue jizi.

Tano, mwalimu siwezi kukuenzi wakati nakuchukia na kukudharau. Ningekupenda na kukuheshimu ningeshika urithi wako na kuheshimu wosia wako wa kupendana na kutohujumiana. Nakumbuka wakati ukianga dunia ulikuwa ukiwalilia watanzania wako baada ya kugundua makosa uliyofanya kuwaweka mikononi mwa nunda wala watu. Nami ni mmojawapo.

Je una habari mkoani mwako watu wameishamiminiwa risasi za moto kutokana na kukatiza kwenye ardhi ya mwekezaji na si mtanzania? Una habari mkoani mwako uchafuzi wa mazingira unatishia maisha ya ndugu zako? Hapa kweli nina sababu ya kukuenzi? Je kukuenzi ni matendo au maneno mwalimu?

Ingawa ukiwa kuzimu bado unaliletea sifa taifa langu, sifichi wala kuchelea kukwambia kuwa waliohai wanaliletea aibu na fedheha baada ya kulibinafsisha huku wakibinafsisha hata akili na roho zao. Mwalimu nilikufahamu sana . Ulikaa madarakani kwa kitambo kirefu ukiacha nyuma familia isiyo na ukwasi zaidi ya utu. Uliowawezesha wamefikia hata kuchukua ule mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira uliozawadiwa na rafiki yako Mao Tse Tung.

Mwalimu, vinyamna mwitu na mbwa hawa walitutenda kweli. Walitudanganya kuwa uwekezaji ndiyo sera na njia pekee ya kutukomboa tusijue walikuwa wakimaanisha kinyume. Wengine walituahidi maisha bora kwa wote tusijue wote ni wao washirika zao, watoto zao na wake zao hata nyumba ndogo zao. Tupo msambweni mwalimu wakati huu tunapozidi kuuzana na kuhadaana. Je unaweza kuamini kuwa kwa sasa hakuna tofauti ya polisi na kibaka? Nina ushahidi. Juzi polisi aliuawa kama kibaka na wananchi wenye hasira na kukata tamaa huku polisi tena wakubwa wakiwapiga risasi wafanyabiashara wakidai ni vibaka!

Wakati wa uongozi wako matupinkele au zeruzeru kwa lugha rahisi walikuwa salama. Baada ya kuingia pepo la utajiri usioulizwa ulivyopatikana, maskini hawa wanatolewa kafara na wanganga njaa wa kienyeji. Hivyo ndugu zetu hawa wanauawa hata zaidi ya swala mwalimu na hawana mtetezi zaidi ya vijikesi viwili vitatu vya kuondolea lawama. Tembo kwa sasa wana ulinzi madhubuti zaidi ya ndugu hawa.

Zama zako uliongoza. Uongozi ulikuwa utumishi wa umma na si uchumia tumbo na utumikishaji na uhujumu wa umma. Ikulu ilikuwa mahali patakatifu siyo pa deal. Uongozi ulikuwa uongozi na si uongo kama sasa. Siasa ilikuwa baraka si balaa kama sasa.

Wale watoto wa wachunga mbuzi na maskini wa kunuka uliowatoa kwenye umaskini na kuwasomesha sasa ni matajiri wa kutupwa. Yupo mpumbavu mmoja jizi aliyewahi kuita shilingi bilioni moja vijisenti ukiachia mbali wengine uliowaachia laana kuwa walikuwa wamejilimbikizia chumo la wizi. Na kweli maneno yako hayakuanguka. Kwani wezi wenzao waliwabeba na kuwakweza hatimaye tamaa zao na upofu vikawadondosha.

Mwalimu sitakuenzi,. Siwezi kujidanganya na kuidanganya dunia. Nitakuenzije iwapo kipato changu kinatokana na rushwa, uwekezaji, uuzaji mihadarati, uongo, ahadi hewa, uhujumu na mengine mengi yapinganayo na dhamira ya dira yako mwalimu?

Hivi kweli panya anaweza kumuenzi paka zaidi ya kufaidi ‘uhuru’ baada ya paka kuondoka? Je nune aweza kuishi nje ya kinyesi cha ng’ombe zizini? Si haki nune kuwa mwalimu wa usafi wakati mlo wake na makazi yake ni kwenye uchafu hata anenepe na kunawiri vipi.

Mwalimu naogopa kuja Butiama au kusimama mbele ya kadamnasi ya maadhimisho yako na kukupamba wakati nilisha kuvua nguo. Naogopa. Maana mama Maria hata wanao wananijua. Inawezekana nikakulamba uchogo na kukupaka mafuta kwa mgongo wa chupa kiasi cha kumkera mmojawapo akaamua kunizodoa na nikazidi kudhalilika ingawa niliishadhalilika muda mrefu.

Mwalimu ulikuwa na akili inayochemka. Yangu mimi ni bongolala. Ulikuwa msafi na mwadilifu. Mie ni mchafu sina mfano. Mkeo hakuwa akitumia ofisi yako kuubia umma. Mie wangu nami wote tu wezi. Nikiiba huku yeye anaibia kule. Hata watoto nimewaingiza. Nataka hata ikibidi wawe marais kama siyo mawaziri. Je hapa mwalimu nitakuwa na cha kukuenzi?

Mwalimu ulileta elimu bure kwa wote. Mie nashabikia kuchangia gharama ingawa kimsingi hakuna gharama za kuchangia zaidi ya kutunisha mfuko wa walaji wakubwa. Ulipigania ardhi. Mie natamani niwe rais niiuzie mbali nipate changu nifiche ughaibuni. Mwalimu ulichukia wafanya biashara wezi. Mie hawa ndiyo washitili wangu.

Mwalimu ulisisitiza usawa wa binadamu. Mie naamini binadamu si sawa wala si mfano wa Mungu kama wachungaji wasemavyo. Usawa ni mambo ya kizamani. Kwangu, heshima ya binadamu haitokani na ubinadamu wake bali pochi lake. Hukusikia wahenga wakisema mwalimu kuwa aso kitu si mtu bali kinyama mwitu? Mtu chake bwana. Kwa imani yangu mie si mfano wa Mungu bali mfano wa shetani kutokana na uroho na roho mbaya vyangu. Mungu si mwizi wala muongo wala mbabaishaji kama mimi mwalimu.

14 Oct 2009


Na Fredy Azzah

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, amesema kashfa za ufisadi zinazowakabili baadhi ya viongozi wake, zimekiumbua chama hicho pamoja na serikali yake.

Akiwahutubia wanafunzi wa matawi ya CCM ya vyuo vikuu vilivyopo jijini Dar es Salaam, wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere jana, alisema ufisadi ambao umewakumba wengi umesababishwa na tabia ya viongozi kulindana na kutosimamia kikamilifu maadili ya uongozi yaliyoainishwa ndani ya katiba ya CCM.

Alisisitiza kuwa tabia hiyo ni kinyume na misingi ambayo Baba wa Taifa, aliwaachia Watanzania....ENDELEA

WAKATI HUOHUO

WASOMI na wanazuoni nchini, wamesema nchi haina dira na kwamba kuna mpasuko mkubwa ambao usiposhughulikiwa mapema, nchi inaweza kuingia kwenye machafuko.

Wakizungumza juzi katika baraza lililopewa jina la Mbongi, lililoandaliwa na Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Julius Nyerere, walisema mpasuko hiyo ni pamoja na ya udini, ukabila, ukanda, matatizo ya vitambulisho Zanzibar pamoja na hofu ya kuvunjika muungano...ENDELEA

CHANZO: Mwananchi


Police recoup £1.4m from criminals in last two weeks as war on crime profits gathers pace



Oct 12 2009 by Rebekah Oruye, Birmingham Mail



WEST Midlands Police is driving home the message that crime does not pay after confiscating £1.4 million from criminals in the past two weeks.

In addition, nearly £100,000 in cash was seized from a car on the M6 in Birmingham, believed to have been intended for criminal use.

Det Chief Insp Simon Wallis, head of the force’s economic crime team, said: “This money has been taken from those who think crime is an easy way to make money.

“It brings West Midlands Police to a total of £15 million seized from criminals in the last 18 months.

“On many of these occasions through financial investigation and the confiscation process we are able to trace monies and give them back to victims. In cases where money is transferred abroad, it still is able to be retrieved. Crime does not pay. We will investigate those involved in criminality to ensure that they do not enjoy their ill gotten gains.”

Among the success stories for the police is the near £900,000 seized from Walsall conman Mponjoli Malakasuka, who had been stealing and exporting high powered luxury cars.

Malakasuka, aged 36, from the Yew Tree estate, was ordered to pay back the money in one month or face an additional four years in jail. He was originally sentenced to three-and-a-half years in July 2008 for conspiracy to steal.

Malakasuka had used a variety of sophisticated methods to steal prestige vehicles which he then exported out of the UK to Tanzania and Kenya. The cars were stolen both through car key burglaries and a variety of identity fraud and fake hire purchase agreements.

The cars included Mercedes Benz S320 CDi and Porsche Cayenne cars. In all over £300,000-worth of vehicles were stolen.

At the time of his arrest police discovered Malakasuka to be living a life of luxury in his four-bed house. At his address were pictures of luxury houses in Tanzania into which officers believed he had invested his fraudulent cash.

The court accepted the houses in Tanzania were proceeds of his criminality. Financial investigators were also able to show thousands of pounds passing through in excess of 70 bank accounts in the UK and Tanzania including one account which alone had £350,000. Det Sgt Jonathan Jones, who led the investigation for the Economic Crime Team, said: “This has been a great investigation, as not only have we stopped fraud and theft, but we have now recovered the profit that this man made from his criminality.”

In a separate case a money launderer from Birmingham was ordered to pay back more than £450,000 of his criminal profit.

Barrington Fulcott, aged 48, from Kingstanding, was told to pay £450,386 at the hearing in Birmingham Crown Court.

He was given six months to return the cash, or face an extra four years in prison. Fulcott was originally sentenced to 42 months in prison in February 2008 in relation to three counts of money laundering.

He had gathered considerable wealth from his criminal activity which had allowed him to purchase five properties in the West Midlands and begin the development of a large home in St Annes, Jamaica.


13 Oct 2009


WAKATI TUNAADHIMISHA KIFO CHA MWASISI WA TAIFA LA TANZANIA,MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE,TUNAPASWA PIA KUTAFAKARI MAMBO KADHAA AMBAYO KWA KIASI KIKUBWA HAYAKUPATA FURSA YA KUJADILIWA WAKATI WA UHAI WA NYERERE,NA KUYAJADILI BAADA YA KIFO CHAKE INAWEZA KUTOA TAFSIRI POTOFU YA UTOVU WA NIDHAMU.

MENGI YAMEONGELEWA KUHUSU MCHANGO WA NYERERE KATIKA HARAKATI ZA UHURU WA TANGANYIKA,NA NDOTO YAKE YA UMOJA ILIYOZAA TAIFA LA TANZANIA KWA KUUNGANA NA ZANZIBAR,PAMOJA NA MCHANGO WA TANZANIA KATIKA MAPAMBANO YA UHURU KUSINI MWA BARA LA AFRIKA.

BAADHI YA MISINGI ALIYOJENGA NYERERE BADO IPO LICHA YA JITIHADA KUBWA ZA "WANAFUNZI WAKE" KUIBOMOA.WATANZANIA BADO TUNASIFIKA KWA NAMNA TUNAVYOTHAMINI UNDUGU WETU (USHAHIDI UKIWA NENO "NDUGU" KABLA YA MAJINA YETU JAPO WAWAKILISHI WETU BUNGENI WANAITWA WAHESHIMIWA).

KAMA KATUNI YA KIPANYA INAVYOONYESHA HAPO JUU,NYERERE PIA ALITUFANYA TUWE WAPOLE KUPITA KIASI.UPOLE HUO ZAMA ZA CHAMA KIMOJA ULIIMARISHWA NA SHERIA ZILIZOTULAZIMISHA KUAMINI KUWA KIONGOZI YUKO SAHIHI WAKATI WOTE.MADHARA YA IMANI HIYO NI HUJUMA INAYOFANYA NA BAADHI YA WANASIASA KUAHIDI MAMBO WASIYOWEZA KUTEKELEZA LAKINI KWA VILE WATANZANIA NI WAPOLE,NA WANAOAMINI KILA ASEMACHO KIONGOZI,WAMEENDELEA KUTUTAWALA NA SI AJABU WAKAENDELEA KUTUTAWALA ZAIDI.WANAFAHAMU KUWA WANAOWATAWALA HAWANA JEURI YA KUHOJI AHADI ZISIZOTEKELEZEKA ACHIULIA MBALI VITENDO VYA UFISADI VINAVYOFANYWA NA WATEULE WA VIONGOZI HAO.

PAMOJA NA HESHIMA YANGU KUBWA NILIYONAYO KWA BABA WA TAIFA,NALAZIMIKA KUMLAUMU KWA UZAZI NA KULEA TABAKA AMBALO LEO HII TUNALIITA MAFISADI.SIAMINI KABISA KUWA BAADHI YA WANAFUNZI WA MWALIMU WALIKURUPUKA GHAFLA KUWA MATAJIRI KUPINDUKIA HUKUN WAKIKUMBATIA WAGENI NA MARAFIKI ZAO.NAAMINI KUWA WATU HAWA HAWAKUWAHI KUWA WAJAMAA JAPO WALIIMBA NA KUCHEZA UJAMAA MAJUKWAANI WAKIWA NA MWALIMU.

TUMWANGALIE MTU KAMA KINGUNGE NGOMBALE MWIRU.HUYU ALIKUWA SWAHIBA WA MWALIMU NA TULIAMBIWA KUWA DINI YAKE NI UJAMAA.HIVI KWELI KINGUNGE AMEBADILIKA GHAFLA KUWA MTETEZI WA MAFISADI AU ALIKUWA ANAMZUGA TU MWALIMU ZAMA ZA UTAWALA WAKE?

BAADHI YA MADUDU TUNAYOSHUHUDIA LEO YALIANZA ZAMA ZA MWALIMU.KULIKUWA NA KIJITABIA CHA MTU AKIHARIBU HAPA ANAHAMISHIWA PALE,KAMA AMBAVYO AKINA MATTAKA WALIVYOSHINDWA KUIOKOA TRC LAKINI WAKAPELEKWA BIMA.SI KWELI KWAMBA NYERERE HAKUENDEKEZA URAFIKI,MAANA ISINGEKUWA HIVYO BASI ASINGEMPIGIA DEBE MKAPA,RAIS AMBAYE BAADA YA KUTOKA IKULU AMEACHA WATANZANIA WENGI WAKISHANGAA KWA NAMNA ALIVYOTUMIA FURSA HIYO KUJITAJIRISHA (REJEA ISHU YA KIWIRA).

BAADHI YA WACHAMBUZI WA SIASA ZA AFRIKA WANAMTUHUMU MWALIMU KUWA WAKATI ANASTAAFU MWAKA 1985 ALIACHA TAIFA LIKIWA KATIKA HALI MBAYA SANA KIUCHUMI.KUNA WANAODAI KWAMBA UAMUZI WA KUNG'ATUKA UNAOPIGIWA MSTARI KAMA MFANO WA KUIGWA ULIKUWA MATOKEO YA KUKWEPA MAJUKUMU.WAPO WANAOKWENDA MBALI ZAIDI NA KUDAI KWAMBA MWALIMU ALIPASWA KUWAOMBA MSAMAHA WATANZANIA KWA KULIFIKISHA TAIFA LILIPOFIKA WAKATI ANASTAAFU.

HATA SIASA YA UJAMAA NAYO IMEZUA MJADALA KWA BAADHI YA WACHAMBUZI WA SIASA.KUNA WANAOONA KUWA NYERERE ALIKUWA MUUMINI PEKEE WA ITIKADI HIYO HUKU AKIWA AMEZUNGUKWA NA KUNDI LENYE BAADHI YA MATAPELI WA KISIASA WALIOKUWA WANAMUUNGA MKONO JAPO NAFSINI MWAO WALIKUWA NA MAWAZO TOFAUTI.NA MFANO UNAOREJEWA MARA NYINGI NI UAMUZI WA KUUA AZIMIO LA ARUSHA MARA BAADA YA MWALIMU KUTOKA MADARAKANI NA KULETA AZIMIO LA ZANZIBAR.

TATIZO JINGINE LA UJAMAA LIKO KWENYE UKWELI KWAMBA ULIKUWA MITHILI YA JARIBIO,AMBALO KWA KIASI KIKUBWA HALIKUFANIKIWA HADI MWALIMU ANAONDOKA MADARAKANI.KUTOKUFANIKIWA HUKO KULICHANGIWA NA NAMNA UJAMAA ULIVYOSAMBAZWA,AMBAPO MATUMIZI YA NGUVU YALIKUWA JAMBO LA KAWAIDA.REJEA NAMNA OPERESHENI VIJIJI VYA UJAMAA ILIVYOWAATHIRI BAADHI YA WATANZANIA KWA KUONDOLEWA MAHALA WALIPOJIJENGA NA KUPAZOWEA NA KUPELEKWA "UGENINI."HOJA HAPA SI KWAMBA WAZO LA UJAMAA LILIKUWA ZURI AU BAYA BALI KAMA LILIKUWA LINATEKELEZEKA HASA IKIZINGATIWA KWAMBA TANZANIA ILIKUWA TEGEMEZI KIUCHUMI TANGU ILIPOPATA UHURU WAKE 1961.

KUDHANI KWAMBA MAFISADI WALIIBUKA GHAFLA NI KUKWEPA KUDADISI CHANZO CHA TATIZO.MAFISADI WENGI NI TABAKA LILILOIBUKA MIAKA YA MWISHO WA HARAKATI ZA UHURU NA BAADA YA KUPATIKANA UHURU.NI KIKUNDI CHA WARASIMU WALIOTUELEKEZA NAMNA YA KUFANYA JAPO WAO WENYEWE HAWAKUFANYA HIVYO.TABAKA HILI LILIKUWA LINASUBIRI MWALIMU AONDOKE MADARAKANI LIANZE "KUFANYA VITU VYAKE",AND SURE THEY DID!

NYERERE ALIZUNGUKWA NA LUNDO LA WANAFIKI.KISICHO NA HAKIKA NI KAMA ALIFAHAMU UNAFIKI WAO NA KUWAVUMILIA AU WALIMZIDI AKILI.YOTE MAWILI HAYAMTOI LAWAMANI KWA VILE PINDI KIONGOZI ANAPOCHAGUA WASAIDIZI WENYE MAPUNGUFU,AIDHA KWA KUTOJUA AU KWA MAKUSUDI,NI LAZIMA ABEBE LAWAMA KWA UTEUZI MBOVU.

UJAMAA,REGARDLESS YA KUWA ITIKADI YA MAJARIBIO,UNGEWEZA KUZAA MATUNDA MEMA IWAPO UNGEGUSA KILA MTANZANIA PASIPO KUJALI NAFASI YAKE KATIKA JAMII.NI DHAHIRI KUWA LAITI HILO LINGETIMIA BASI TUSINGESHUHUDIA AWAMU YA PILI (BAADA YA NYERERE) IKIENDESHA TAIFA KWA MTINDO WA LAISSEZ FAIRE (BORA LIENDE) NA AWAMU YA TATU IKITUAMINISHA UJIO WA ZAMA ZA UWAZI NA UKWELI HUKU WATU WANAUZIANA MGODI WA KIWIRA KWA BEI YA KISHKAJI.YA UFISADI KILA MMOJA WETU ANAFAHAMU HALI ILIVYO.

KWA VILE MIE NI MKRISTO,NA KWA VILE MILA ZETU ZINAKATAZA KUWASEMA VIBAYA MAREHEMU,BASI NAUNGANA NA WATANZANIA WENZANGU KUMTAKIA MWALIMU PUMZIKO LA MILELE NA MWANGA WA MILELE,APUMZIKE KWA AMANI,AMINA.HATA HIVYO,KAMA SIE WAKATOLIKI TUNAVYOAMINI KUWA ROHO ZA MAREHEMU ZIKO "HAI" TUKIZIKUMBUKA KWA SALA,BILA SHAKA MWALIMU ANAJUTA KUCHAGUA "MARAFIKI" AMBAO BAADA YA KUONDOKA KWAKE WAMEGEUZA TANZANIA KUWA SHMBA LA BIBI,WANACHUMA WATAKAVYO,WANAKWIBA WATAKAVYO,LAKINI KWA VILE ALITUGEYUZA WAPOLE NA WAGUMU KUDAI HAKI ZETU,TUNAENDELEA KUVUMILIA MACHUNGU.

MWISHO,KWA VILE LAWAMA PEKEE HAZIWEZI KUSAIDIA KUTUFIKISHA TUENDAKO,JUST LIKE MAKALA NDEFU ZA KUMBUKUMBU YA MWALIMU ZISIVYOWEZA KUWAKWAMUA WALALAHOI,NI MUHIMU KUITUMIA SIKU HII KUJIULIZA SWALI HILI MUHIMU.JE NYERERE NA WAPIGANIA UHURU WENZAKE WALIPAMBANA NA MKOLONI KWA MINAJILI YA KUMUONDOA MTU MWEUPE NA KUMUWEKA MKOLONI MWEUSI (MAFISADI,et al)?

ANGALAU MKOLONI ALIKUWA NA EXCUSE YA KUTUNYONYA NA KUTUPELEKESHA.HAKUWA MTANZANIA,HAKUWA NA UCHUNGU NA NCHI HII,NA HAKUFIKISHWA ALIPOFIKIA KWA JITIHADA ZA WATANZANIA.LAKINI MAFISADI NI WATANZANIA WENZETU,WANALAZIMIKA KUWA NA UCHUNGU NA NCHI YETU KWA VILE KWA VYOVYOTE VILE BAADHI YA WAATHIRIKA WA UFISADI WAO NI NDUGU ZAO WA MBALI (WA KARIBU WAMESHATENGENEZEWA ULAJI SOMEWHERE).

NJIA BORA YA KUMUENZI MWALIMU NI KUREKEBISHA PALE ALIPOKOSEA (KWA MFANO KUWALEA VIONGOZI WALIOMZUGA KUWA NI WAJAMAA LAKINI WAKAGEUKA MAFISADI MARA BAADA YA KUONDOKA KWAKE) NA KUIANGALIA TANZANIA KAMA NCHI YETU SOTE NA SI YA WATEULE WACHACHE (AMBAO MARA NYINGI HAWATAKI KUSIKIA SAUTI TOFAUTI NA YAO UNLESS IWE NI VIGEREGERE AU MAKOFI YA PONGEZI).TUMUENZI MWALIMU KWA KUKATAA NCHI YETU KUWA SHAMBA LA BIBI HUKU WAWEKEZAJI UCHWARA WAKIJA NA BRIEF CASES TUPU NA KUONDOKA WAKIWA MAMILIONEA.TUKATAE WEZI KAMA WA KAMPUNI YA KAGODA NA MATAPELI KAMA WA RICHMOND,NA UJAMBAZI KAMA WA MEREMETA,TANGOLD,NK KUENDELEA HUKU WAHUSIKA WAKITUPUUZA KWA KUGOMA KUTUELEZA UKWELI.


BONYEZA PICHA KUIKUZA NA KUSOMA STORI



Hivi karibuni niliandika makala flani kuhusu milipuko ya mabomu huko Mbagala, jijini Dar es Salaam. Kwa kutambua kuwa blogu yangu haina idadi kubwa ya wasomaji (japo nawathamini sana wachache wanaotumia muda wao kuitembelea) niliamua kuisambaza makala hiyo kwa bloga wenzangu wawili ambao “nyumba” zao hupata “wageni” wa kutosha kila siku.

Kwa bahati mbaya, bloga hao waliamua kuiweka makala hiyo kapuni.Siwalaumu,kwa sababu kadhaa. Kwanza, blogu ni mali ya mmiliki, na hilo linampa haki ya kuchagua nini kiwepo kwenye blogu yake na nini kisiwepo.Pili, kila bloga ana mtazamo wake kuhusu mambo mbalimbali yanayotuzunguka, iwe siasa, dini au nyanja nyingine za maisha ya binadamu. Kwa maana hiyo, kama ataletewa makala inayokinzana na mtazamo huo, ana haki ya kuipuuza. Kuna sababu nyingine za kibinafsi lakini sidhani kama zina umuhimu sana.

Makala husika (isome hapa) haikuwa ya matusi, kashfa au utovu wa nidhamu kwa watawala japo ilikuwa ikizungumzia uzembe na kutowajibika kwa baadhi ya viongozi wetu unavyohusika na janga hilo la milipuko ya mabomu.Nilishauri katika makala hiyo kwamba wakati umefika kwa Watanzania kudai haki zao hasa pale zinapopuuzwa makusudi. Kwamba ripoti ya milipuko ya kwanza inaozea katika makabrasha ya Wizara husika, kisha mlipuko mwingine unatokea lakini hakuna anayewajibika, jambo linalohitaji shinikizo la kudai haki na uwajibikaji.

Naamini kwamba laiti makala hiyo ingechapishwa laiti ingekuwa ya kumsifia kiongozi flani au kukumbushia tarehe yake ya kuzaliwa. Au laiti ingekuwa ni tangazo binafsi. Yote hayo ni mazuri kwa vile ni huduma kwa umma. Hata hivyo, harakati tunazohangaika nazo wengine kuboresha future ya nchi yetu ni muhimu pia na hazipaswi kupuuzwa.

Ni rahisi kwangu kuhitimisha kwamba kinachokwanza makala za aina hiyo kuchapishwa ni uoga wa mabloga husika wakihofia kuwaudhi watawala. Japo huo ni uhuru wao kibinadamu, madhara yake kwa jamii ni makubwa kwa vile historia inaonyesha kwamba uoga ni kitalu mwafaka kwa ushamiri wa tawala dhalimu.

Lengo langu si kulaumu bali kushauriana.Kukimbilia kuweka picha za kiongozi akihutubia au akirejea Dar akiwa bukheri wa afya lakini kuchelea kujumuisha maelezo kwamba pia alikumbwa na dhahama ya kiafya ni kutowatendea haki wasomaji wetu. Hapa narejea tukio lililotokea jijini Mwanza hivi karibuni ambapo baadhi ya wenzetu walitonyesha “picha nzuri” za JK lakini “wakabania” maelezo kuhusu mkasa uliomkumba wa kushindwa kuendelea na hotuba yake katika kile kilichoelezwa kuwa “uchovu wa safari.”

Ushirikiano wetu jumuiya iliyojibebesha dhamana ya kuujulisha umma kuhusu mambo mbalimbali usiishie kwenye yanayopendeza machoni pekee bali pia yale yanayoudhi au kukera.


Hivi mwenzangu unapoiangalia CCM kwa mtazamo wa kawaida tu (yaani usiohisha uchambuzi wa kitaaluma) unaielezeaje?Pengine huafikiani na mtizamo wangu wa “kawaida” na kitaaluma kwamba pamoja na hadi lukuki za kuwakomboa Watanzania kutoka kwenye lindi la umasikini,chama hicho hakijaonyesha dhamira ya dhati kutimiza ahadi hizo.

Naamini kuwa baadhi ya ahadi hizo zilikuwa za dhati,hususani ile ya kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.Naamini hivyo kwa vile ni dhahiri kwamba chama hicho kilikuwa kinatambua hali ngumu inayowakabili Watanzania baada ya miongo kadhaa ya utawala wake.Kwa kutambua tatizo,CCM ilileta dalili za matumaini kwamba sio tu inataka kuendelea kutawala lakini pia inataka kuwa chachu ya mabadiliko.Japo chama hicho kinafahamika kwa usugu wa kukiri mapungufu ya utendaji wake,uamuzi wake kugusia maeneo yanayowakera wananchi ilikuwa ishara ya kutambua mapungufu katika awamu zilizotangulia na kudhamiri kufanya marekebisho.

Binafsi nilitarajia kwamba kama ilivyokuwa mwaka 2005 ambapo CCM “ilikiri mapungufu yake kiaina” kwa kuahidi kuboresha maisha sambamba na kukabili chanzo kikuu cha kuzorota/kudidimia kwa maendeleo (rushwa),basi safari hii pia kingepata ujasiri wa kutueleza bayana kwamba kumekuwa na mapungufu makubwa zaidi katika utekelezaji wa ahadi hizo.

Ni nani asiyejua kuwa kiwango cha rushwa kinazidi kupaa siku hadi siku?Ni nani asiyejua kuwa rushwa na uhujumu mwingine wa uchumi umechukua sura mpya kwa kuzaa tabaka “jipya” la mafisadi?Ni nani pia asiyejua kuwa kwa kiasi kikubwa ahadi ya maisha bora kwa kila Mtanzania imekuwa na maana zaidi kwa mafisadi kuliko walalahoi?Ni dhahiri kwamba Watanzania wenzetu kama wamiliki wa kampuni ya Kagoda wanaishukuru CCM kwa ukarimu na huruma yake to an extent that inaona aibu kuwataja hadharani.Matapeli wa Richmond (achana na yule Mhindi aliyegeuzwa mbuzi wa kafara mahakamani) wanaishukuru sana CCM kwa huruma yake kwao ambapo kila kikao cha bunge kinazugwa kuwa “taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya kamati ya Mwakyembe itatolewa katika kikao kijacho”,na porojo nyingine kama hizo.

Kinachokera sasa sio tu madudu yanayoendelea kufanywa na CCM bali hizi kauli za kukera kwamba eti chama hicho kimeweka rekodi ya mapambano ya rushwa kuliko nyakati yoyote ile.Hii ni sawa na kuwasanifu Watanzania.Ni mithili ya kuwafanya wajinga,wasioona madudu yanayoendelea,wasiosikia maumivu ya vibano wanavyopewa na mafisadi,na wasiofahamu kuwa watuhumiwa kadhaa wa ufisadi hawajaguswa hadi leo (na hakuna dalili kuwa wataguswa licha ya ahadi kuwa kuna kesi tatu kubwa zitafunguliwa hivi karibuni....na kila mara tunaambiwa “hivi karibuni).”

Ni kweli kwamba hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi hazipaswi kuchukuliwa kutokana na utashi wa watu flani bali kwa kuzingatia sheria na kanuni.Lakini utashi ni muhimu katika kuchukua hatua,na hapa hatuzungumzii utashi wa wananchi wasio na uwezo wa kuuamua,kwa mfano “Chenge na tuhuma za vijisenti vyake huko Jersey hastahili kuwa kwenye kamati ya maadili ya CCM.”Kwanza kuwa na utashi wa kufanya jambo jema si dhambi,kama CCM inavyotaka kutuaminisha.Kuwa na utashi wa kuchukua hatua dhidi ya mafisadi ndio itapelekea chama hicho kuwatenga mafisadi inaowakumbatia,na hivyo kuwa rahisi kwake kuchukua hatua dhidi yao.Utashi unapaswa kuepukwa ni kama ule wa wanamtandao unaoendelea kuwaangalia wana-CCM wasio wanamtandao kuwa mithili ya wahaini.

Mamlaka husika zinapozembea kuchukua hatua sahihi halafu tunaishia kuambiwa kuwa hatua haziwezi kuchukuliwa kwa utashi wa watu flani...jibu jepesi ni kwamba matatizo yetu hayawagusi wanaotuongoza.Wanaona tunapiga kelele zisizo na msingi,ndio maana kwao haki za binadamu za mafisadi ni muhimu zaidi kuliko za walalahoi walio wengi.

Hivi kweli CCM inataka kutuzuga kuwa haifahamu kwamba Watanzania wengi wangependa kuona wahusika “halisi” wa utapeli wa Richmond wakifikishwa mahakamani badala ya kile tunachoelezwa kuwa “walijiuzulu kwa maslahi ya taifa”?CCM haijui kwamba kwa kuendelea kuminya taarifa kuwa nani anamiliki Kagoda ni mithili ya kuwapuuza Watanzania?Au CCM haifahamu kuwa kuwaachia mzigo Waingereza kudili na vijisenti vya ujambazi wa rada ni kukwepa majukumu?

Au chama hicho kinapotulaghai kwamba tumwache mhusika mkuu wa ufisadi katika mgodi wa Kiwira apumzike kwa amani ni sawa na kuruhusu kila mtu aibe kisha aachwe apumzike kwa amani?Kwanini basi vibaka wanajazana magerezani ilhali wezi wakubwa wanatetewa kwa nguvu zote?

Watanzania wana kila sababu ya kuiadhibu CCM hapo mwakani.Kinachofanywa na chama hicho kinapodai kuwa “kimeweka rekodi ya kupambana na rushwa” ni mithili ya vibaka wanaokuibia kisha wanakupigia ukelele wa mwizi na kupelekea wewe mwathiriwa wa uporaji huo kushushiwa kipigo kitakatifu huku kibaka “akiyeyuka kiulaini.”Badala ya kukiri kwamba kasi yao ya kupambana na ufisadi ni ndogo, wao wanatukejeli kuwa wameweka rekodi!Halafu bado tutegemee lolote kutoka kwa wababaishaji hawa?

Hakuna haja ya kubishana au kupigiana kelele nao.Dawa yao ni hapo mwakani.Kama unataka kuendelea kuona mafisadi wakitetewa huku wanaowapinga wakikemewa basi irejeshe CCM madarakani hapo mwakani.Kama unadhani maisha bora yaliyoahidiwa 2005 yamepatikana zaidi ya matarajio yako basi hutofanya kosa kutoa kura ya ndio kwa chama hicho.

Tukiendeleza mazowea tutazidi kuumia.Kuna wanaodhani kwamba Tanzania haiwezi kuwa kisiwa cha amani pasipo utawala wa CCM.Wanachosahau kuwa hata hao CCM ni Watanzania wenzetu japo wanawathamini zaidi wageni (wawekezaji) kuliko sie wenye nchi.Wanasahau pia kuwa wingi wa wabunge wa CCM unakwaza jitihada wa wapambanaji kama akina Dokta Slaa kuwakalia kooni wababaishaji waliojazana chini ya utawala wa CCM.

Atakayenuna na anune lakini nchi hii ni yetu sote na kila Mtanzania ana haki ya kudai haki yake.Tukiruhusu kuendelea kwa ngojera za “tunaendelea na mchakato wa blah blah blah” au “kesi kadhaa zkubwa zitapelekwa mahakamani hivi karibuni...” na hadithi nyingine kama hizo basi tutaendelea kuwa watu wa kulalamika kila siku japo ni sie wenyewe tunaoweza kukomesha usanii wa kisiasa wa aina hiyo.Kama imewezekana Ghana basi hata kwetu inawezekana.Si kweli kwamba chama mbadala kitashindwa kutupeleka tunakostahili kwenda hasa ikizingatiwa kuwa hakuna uwezekano wa chama hicho mbadala kupata idadi kubwa ya wabunge zaidi ya CCM,which means itakuwa rahisi kukidhibiti iwapo kitaonyesha dalili za kurejea madudu ya CCM.

Kusanya hasira zako lakini usipigane bali pugie kura ya kujiletea maisha yako bora wewe mwenyewe kwa kuwaondoa wanaokwaza uwezekano huo.Ifike wakati tusema tumechoshwa na ahadi na maneno matamu (na mengine si matamu bali ya dharau kama hayo ya kudai wameweka historia ya kupambana na rushwa wakati wanajua waziwazi kuwa wamekuza rushwa kupindukia).

It can be done if you play your part.

Inawezekana ukiamua kutimiza wajibu wako.


10 Oct 2009


SOMA KAULI ZA BABU HUYU HAPA CHINI KISHA UELEWE KWANINI NATOA WITO AONEWE HURUMA KWA KUPUMZISHWA.

Ahofia wabunge wengi CCM kutorudi Bungeni
Na Keneth Goliama, Mbeya

MBUNGE wa kuteuliwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kingunge Ngombale Mwiru, amewashutumu viongozi wanaounda makundi ndani ya chama hicho na kuwaita waliochanganyikiwa.

Mbunge huyo aliapa kuwa matajiri wasipewe kipaumbele katika uongozi, kwani watu wakishakuwa na fedha wanajiingiza katika siasa kufanikisha malengo yao ya kibiashara.

Kingunge ambaye pia ni Naibu Kamanda UVCCM Taifa,aliyasema jana wakati akiwaapisha Makamanda wa Mkoa wa Mbeya kwenye ukumbi wa Mkapa.

Aliwataka makamanda hao kufanya kazi ya kuwashauri vijana na sio kuwaingiza vijana katika makundi yaliyopo ndani ya chama hicho.

Kingunge alisema kauli za baadhi ya viongozi kuwa, wabunge wengi wa CCM hawatarudi katika ubunge mwaka 2010 ni kweli kwa sababu kunahitajika mabadiliko katika uongozi ndani ya chama.

Hata hivyo, alisema wabunge hao wapya ni faraja kwa CCM kwa sababu watakuwa ni wakutoka ndani ya chama hicho.

Aliongeza licha ya Mkoa wa Mbeya ni mingoni mwa mikoa ambayo ilitoa watu waliokuwa mstari wa mbele kugombea uhuru , lakini sifa hiyo imeharibiwa na viongozi wachache.

Kingunge alisema baadhi ya viongozi mkoani hapa wanauhasama wa kugombea madaraka na kwamba sasa ugomvi huo unakiharibia chama.

Akiunga mkono jitihada za vijana wa mkoa huo kupambana na mafisadi, Kingunge aliwataka wasiache kutetea haki yao kwa sababu vijana ndio wenye nguvu katika maendeleo ya jamii na siasa.

Kingunge aliwaasa wanachama hao kukataa kurubuniwa na watu wenye fedha kwani kukubali kufanya hivyo ni kuua chama.

Baadhi ya viongozi wamefanikiwa kuwarubuni vijana kwa fedha ili waweze kujinufaisha wenyewe na kuharibu siasa mkoani hapa, alisema Kingunge

Alikionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa, hakijui siasa ndio maanakimejaa matatizo matupu na uchaguzi wao ni ovyo na kwamba hakina uwezo wa kupewa kuongoza dola.

CHANZO: Mwananchi

HIVI ALIYECHANGANYKIWA NI NANI KATI YA KINGUNGE NA HAO ANAOWAITA "WAMECHANGANYIKIWA."MAJUZI,MTETEZI MAHIRI WA MAFISADI,YUSUPH MAKAMBA NAE ALITOA TAMKO LINALOSHOBIHIANA NA HILI LA KINGUNGE,MWANASIASA ALIYETUZUGA ENZI ZA MWALIMU KUWA NI MFUASI MAHIRI WA UJAMAA ONLY KUIBUKA MTETEZI MAHIRI WA MAFISADI.LEO,MIEZI MICHACHE KABLA YA UCHAGUZI MKUU,NAE ANAJITUTUMUA KUKEMEA MAFISADI!?HUKU NI KUCHANGANYIKIWA KUNAKONASIBISHWA NA KUZEEKA VIBAYA.

9 Oct 2009


From its politics to its economy to its environment and way of life, California is like a patient on life support. At the start of summer the state government was so deeply in debt that it began to issue IOUs instead of wages. Its unemployment rate has soared to more than 12%, the highest figure in 70 years. Desperate to pay off a crippling budget deficit, California is slashing spending in education and healthcare, laying off vast numbers of workers and forcing others to take unpaid leave. In a state made up of sprawling suburbs the collapse of the housing bubble has impoverished millions and kicked tens of thousands of families out of their homes. Its political system is locked in paralysis and the two-term rule of former movie star Arnold Schwarzenegger is seen as a disaster – his approval ratings having sunk to levels that would make George W Bush blush. The crisis is so deep that Professor Kevin Starr, who has written an acclaimed history of the state, recently declared: "California is on the verge of becoming the first failed state in America." WRITES The Observer's Paul Harris.



Na Ramadhan Semtawa

RAIS Jakaya Kikwete aliweka hadharani matokeo ya uchunguzi wa vipimo vya afya yake, yanayoonyesha kuwa kiongozi huyo wa nchi ana afya njema baada ya tatizo la kuishiwa nguvu akiwa jukwaani mjini Mwanza Oktoba 4, kuibua mjadala.

Lakini vipimo hivyo vinaonyesha kuwa tatizo pekee linalomsumbua Rais Kikwete ni maumivu ya shingo ambayo yanatokana na kuumia nyakati za ujana au utoto.

Afya ya Rais Kikwete ilizuia mjadala baada ya kuishiwa nguvu akihutubia kwenye Uwanja wa Kirumba mjini Mwanza na kulazimika kubebwa na wasaidizi wake hadi chumba kidogo cha uwanjani hapo na ilielezwa baada ya rais kuzinduka kuwa tatizo hilo lilitokana na uchovu baada ya safari ndefu kati ya New York, Marekani na Dar es salaam na baadaye Arusha na Mwanza.

Pamoja na uchovu huo kuhusishwa na safari ndefu ya Rais Kikwete taarifa iliyopokelewa kutoka Radio Jamaica jana jioni zinasema kuwa rais atakwenda nchini Jamaica kwa ziara ya kikazi itakayoanza Novemba 24 na kumalizika Novemba 26.

Na jana daktari wa rais, Peter Mfisi alirejea tena kauli hiyo akisema uchovu, hasa wa safari, ndio uliosababisha kiongozi huyo wa nchi kuishiwa nguvu jukwaani, huku kukiwa na habari kuwa ataenda Jamaica mwezi ujao kwa safari ya kikazi.

Hii ni mara ya kwanza kwa Ikulu kuweka hadharani vipimo vya uchunguzi wa afya ya Rais Kikwete, ambaye pia aliwahi kuishiwa nguvu siku ya mwisho ya kampeni zilizomuingiza Ikulu, na kuanguka akiwa jukwaani.

Daktari wa rais, Peter Mfisi aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa vipimo hivyo ni pamoja na cha damu kwa ajili ya kuangalia virusi vya Ukimwi ambacho huchukuliwa kila baada ya miezi sita.

"Nimekuja kufafanua afya ya mheshimiwa rais kutokana na tukio la Oktoba 4, 2009 (la kuishiwa nguvu jukwaani) pale Mwanza. Tukio hilo limesababisha mshtuko kwa watu wengi na kuendelea kuwa jambo linalozua mjadala kuhusu hali ya afya ya mheshimiwa," alisema daktari huyo.

"Naelewa sababu ya wananchi kuwa na hofu na kuwepo kwa mjadala miongoni mwao. Tatizo pekee ambalo limekuwa likimsumbua rais mara kwa mara ni maumivu ya shingo yanayotokana na kuumia utotoni na wakati wa ujana.

"Baadhi ya pingili za uti wa mgongo sehemu ya shingoni ziliathirika kutokana na kuumia huko na humsababishia maumivu. Mara nyingi matatizo hayo huwapata wanamichezo na wanajeshi."

Dk Mfisi aliongeza kusema: "Tumekuwa tunamfanyia mheshimiwa rais uchunguzi wa damu yake kwa vipimo mbalimbali vinavyotumika kutambua maradhi mbalimbali yanayohusu damu yenyewe na mwili mzima wa mwanadamu. Tumekuwa tunafanya hivyo hapa nchini na hata nje kwa nia ya kulinganisha matokeo yetu na kwa vipimo ambavyo sisi tunavyo.

"Matokeo ya uchunguzi wetu yameonyesha mheshimiwa rais yuko salama, hana maradhi ya damu au kisukari, wala Ukimwi au wingi wa mafuta (Cholestrol), kiwango cha madini, tezi la kibofu wala shingo, au ya ini, au ya homoni mbalimbali zilizoko mwilini na mengine."

Dk Mfisi alifafanua kwamba, uamuzi huo wa kutoa vipimo hivyo umetokana na ridhaa ya rais mwenyewe.

"Ni ridhaa ya mheshimiwa rais mwenyewe... kutokana na kiapo changu cha udaktari na maadili yangu ya kazi, siruhusiwi kutoa hadharani undani wa habari yoyote inayohusu mgonjwa ninayemtibu bila ridhaa yake," alisema Dk Mfisi.

Kwa mujibu wa daktari huyo, baada ya Rais Kikwete kuishiwa nguvu jukwaani, alichukua vipimo muhimu wakati akiwa kwenye chumba maalumu uwanjani hapo kama ilivyo kawaida na kwamba vipimo hivyo vimeshafanyiwa uchunguzi.

Alifafanua kwamba matokeo ya vipimo vilivyochukuliwa siku ya tukio la Mwanza yalionyesha shinikizo la damu (BP) lilikuwa kati ya 130 kwa 85 (vipimo vya kitaalamu), kitu ambacho ni cha kawaida kwa mtu mwenye umri kama wa Rais Kikwete.

"Mapigo ya moyo wake yalikuwa ni 76 kwa dakika ambayo pia ni ya kawaida; sukari kwenye damu ilikuwa 5.5 ambayo nayo ilikuwa ya kiwango cha kawaida; joto la mwili lilikuwa nyuzi 37.5 ambalo ni la kawaida," alifafanua Dk Mfisi.

"Mheshimiwa Rais pia hakuwa na kiungo chochote kilichoonekana kutetereka, jambo ambalo lilithibitisha kuwa hakupata kiharusi. Mheshimiwa Rais hakuwa na matatizo yoyote ya kiafya ambayo yangeweza kuhusishwa kuwa chanzo cha tukio lile (la Mwanza)."

Hata hivyo, Dk Mfisi alisema baada ya kurejea Dar es Salaam alijaribu kuwasiliana na madaktari wenzake wa ndani na nje ya nchi ambao wamekuwa wakishirikiana nao katika kuchunguza na kufuatilia afya ya Rais Kikwete.

"Wote hao baada ya kuwasimulia kilichotokea na matokeo ya vipimo nilivyomfanyia mheshimiwa rais, kwa tafakuri zao hawakuwa na wasiwasi wowote kuwa tukio hilo lilisababishwa na jambo jingine lolote isipokuwa uchovu," alisisitiza daktari huyo wa rais.

Aliongeza kwamba mmoja wao alimuona rais siku moja kabla ya kuondoka New York ambako alipata nafasi ya kumchunguza afya ya mkuu huyo wa nchi.

Dk Mfisi, akitoa mtiririko huo wa vipimo mbalimbali na matokeo alisema: " Blood Pressure (shinikizo la damu), tunafuatilia kwa karibu sana msukumo wa damu, mwenyewe tunampa mashine ya kujipima kila siku na anafanya hivyo, kwa jumla presha yake iko kwenye viwango vya kawaida.

"Aidha, uzito wake wa mwili unaendana ipasavyo na urefu wake, mheshimiwa Rais ni mtu mwenye mazoea ya kufanya mazoezi na yuko makini katika chakula anachokula."

Daktari huyo wa rais aliweka bayana kwamba, wanahusika kwa ukamilifu na kuelekeza kuhusu chakula anachokula na kuongeza kwamba "ana nidhamu ya kujipima pamoja na mazoezi na chakula."

Kuhusu moyo, Dk Mfisi alisema tayari walishamfanyia rais vipimo vya kitaalamu vinavyofahamika kama ECHO na ECG na vingine, na kwamba matokeo yameonyesha hakuna tatizo lolote.

Akizungumzia ubongo, alisema mwaka jana Rais Kikwete alifanyiwa uchunguzi wa afya ya ubongo wake katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kutumia kipimo cha CT-Scan na matokeo yake yalionyesha kwamba, hakuwa na tatizo pia.

Dk Mfisi alisema Rais Kikwete aliwahi kufanyiwa uchunguzi wa ini, figo, bandama na kongosho kwa kutumia kipimo cha mionzi (ultra sound), uchunguzi ambao ulibaini viungo vyote hivyo viko salama.

"Kila mwaka tunapomfanyia uchunguzi wa afya ya mheshimiwa rais, tumekuwa tunafanyia uchunguzi wa viungo vyake muhimu vya tumboni kama vile ini, figo, bandama na kongosho na kwa kupima damu yake kwa vipimo vyote muhimu," aliongeza Dk Mfisi.

Kuhusu mfumo wa njia ya chakula, ambayo huhusisha koromeo la chakula, tumbo, utumbo mdogo, Dk Mfisi aliweka bayana kwamba matokeo ya uchunguzi yameonyesha hakuna tatizo lolote.

Alisema mwaka 2007 walimfanyia kipimo cha kitaalamu cha colonoscopy mjini Paris, Ufaransa, kuchunguza hali ya afya ya utumbo mkubwa na kwamba matokeo ya uchunguzi yalionyesha kuwa hana matatizo yoyote.

Alisema daktari aliyemfanyia rais kipimo hicho aliwaambia kuwa mkuu huyo wa nchi hahitaji kufanyiwa kipimo kama hicho tena mpaka baada ya miaka saba na kwamba daktari huyo alimtania rais kwa kusema kuwa "angefurahi kuazima utumbo" wake.

Kuhusu tezi la shingo, Dk Mfisi alisema kuwa akiwa mjini New York katika safari yake ya juzi, Rais Kikwete alifanyiwa uchunguzi wa afya ya tezi la shingo pamoja na kiwango chake cha utoaji wa homoni, matokeo yaliyoonyesha hakuna tatizo, hali kadhalika uchunguzi wa tezi la kibofu ulionyesha hana tatizo.

Dk Mfisi alisema rais hana tatizo la macho, masikio na pua na kwamba uvaaji miwani wa Kikwete haumaanishi kuwa ni maradhi.

"Tunapofanya uchunguzi wa macho ukiacha ile ya kuchunguza uwezo wa kuona, tunaangalia presha ya macho na hali ya viungo vya nje na ndani, mheshimiwa Rais hana matatizo yoyote," alisema.

CHANZO: Mwananchi

WAKATI DR MFISI AKITOA MAELEZO HAYO,MHADHIRI MWANDAMIZI KATIKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM DR HAJI SEMBOJA AMENUKULIWA NA JARIDA LA RAIA MWEMA AKIELEZA KUWA URAIS NI ASASI NA SI MTU BINAFSI.

Urais si Kikwete binafsi, ni mfumo wa kitaasisi. Ni wazi kuwa Rais amesema yeye ndiye hakuzingatia ushauri wa wataalamu wake kutokana na kuwaondolea lawama. Ameamua kuwalinda kwa kubeba lawama, lakini ukitazama jambo hili kwa upana wake wasaidizi wake walipaswa kutambua tangu awali kuwa urais ni system nzima Ikulu hata mlinzi wa getini. Kwa hiyo, wasaidizi ndiyo wenye kuamua na si kila kitu kifanywe na Rais kama ambavyo wanasema sasa watajaribu kumpunguzia ratiba,” ALISEMA DR SEMBOJA NA KUSISITIZA KWAMBA“Sidhani kama ni sahihi kukubali kuwa Rais ndiye alikataa ushauri, kwa taratibu za kimfumo Rais anapangiwa kila kitu ni kama anaamriwa hivi. Kwa tukio hili ameamua tu kuwa na nidhamu ya kuwalinda wasaidizi wake, namwombea afya njema lakini ni muhimu tuzingatie kuwa wengi walioamua kufanya kila kitu wenyewe walipata matatizo, Ikulu sasa ifanye kazi kama Ikulu.”

BINAFSI NAAMINI TATIZO NI LA KIMFUMO ZAIDI.KUNA TAASISI ZENYE MAMLAKA NA WAJIBU WA KUPANGA RATIBA ZA RAIS SAMBAMBA KWA KUZINGATIA UHALISIA,USALAMA NA MAMBO MENGINE KAMA HAYO.KWA WENZETU WANAOZINGATIA KANUNI NA TARATIBU ZA KITAASISI,SI RAHISI KWA RAIS KUJIAMULIA MAMBO YAKE MWENYEWE PASIPO KUZINGATIA USHAURI WA KITAALAM.SI RAHISI,KWA MFANO,BARACK OBAMA KUJIAMULIA KWENDA MAHALA FLANI KINYUME NA USHAURI WA U.S. SECRET SERVICE.UBISHI WA RAIS KAMA BINADAMU HAUNA NAFASI KATIKA UFANISI WA TAASISI INAYOZINGATIA TAALUMA NA MAADILI.IKUMBUKWE KWAMBA LAITI RAIS AKING'ANG'ANIA KUFANYA ZIARA MAHALA FLANI KINYUME NA USHAURI WA WASAIDIZI WAKE KISHA AKAPATWA NA JANGA,WATAKAOBEBA LAWAMA NI WASAIDIZI HAO NA SI RAIS.LAKINI PIA KUNA SUALA LA FEDHA ZA WALIPA KODI ZINAZOTUMIWA NA TAASISI HUSIKA KUILINDA ASASI YA URAIS NA BINADAMU ALIYEKABIDHIWA DHAMANA YA URAIS.NI DHAHIRI KWAMBA RAIS AKIPUUZA USHAURI WA WA TAASISI HUSIKA INAMAANISHA PIA UPOTEVU WA FEDHA ZA WALIPA KODI.



UTENDAJI WA AINA YA ZIMAMOTO,AU VIBAYA ZAIDI,KULENGA SHABAHA BAADA YA RISASI KUFYATUKA,UTATUGHARIMU HUKO MBELENI.LEO HII TUSINGEHITAJI DAKTARI WA RAIA KUWEKA HADHARANI TAARIFA NYETI ZA AFYA YA JK LAITI TAASISI HUSIKA ZINGEMLAZIMISHA JK KUFUATA USHAURI WA KITAALAMU KUHUSIANA NA RATIBA AU ZIARA ZAKE.TUSISUBIRI JAMBO LITOKEE NDIPO TUANZE KUTOA MAELEZO YA KITAALAMU. BY THE WAY,TAARIFA HIYO YA DAKTARI WA RAIS INAWEZA KUZUA MJADALA USIO NA TIJA KUHUSU MANTIKI YAKE.JAPO NI VEMA KUTOA UFAFANUZI KATIKA MASUALA YANAYOZUA UTATA (I WISH NA KWELI ISHU YA KAGODA INGEKUWA HIVYO) LAKINI KUNA UWEZEKANO WA "WABISHI" KUHOJI KAMA DAKTARI WA RAIS WA AFRIKA ANAWEZA KUTOA TAARIFA "MBAYA" DHIDI YA BOSI WAKE!

KWA SASA,MAMLAKA HUSIKA ZINAWEZA KUFARIJIKA BAADA YA KUPATA UTETEZI KUTOKA KWA JK.LAKINI NI VEMA ZIKATAMBUA KUWA JUKUMU LAO SI KUMWOGOPA MHESHIMIWA BALI KUFANYA KAZI ZAO KWA KUZINGATIA MAADILI NA TAALUMA.JK KAMA MTU ANAWEZA KUTOZINGATIA USHAURI WA MAMLAKA HIZO,LAKINI JK KAMA RAIS HARUHUSIWI KUJIAMULIA MAMBO YANAYOWEZA KUATHIRI ASASI YA URAIS.UOGA NA KUJIKOMBA NI MAMBO YASIYO NA NAFASI KATIKA PROFESSIONALISM.


8 Oct 2009

Mambo mengine huku Ughaibuni ni vituko vitupu.Kuna watu wanafuga majoka makubwa na kuyalea kama watoto wao,kuna wanaofuga panya mithili ya paka,na wengine wamegeuza tumbili kuwa watoto wa kambo.Na matunzo wanayopewa mbwa na paka hayatofautiani sana na anasa wanazofaidi watoto wa wabaka-uchumi wetu (mafisadi).

Kuna vijibwa flani vimekuwa kwenye chati kwa muda mrefu kutokana na kushebedukiwa na watu maarufu.Nadhani ushakiona ki-chihuahua cha Paris Hilton,kijibwa kidogo mithili ya paka.Sasa imeibuka fasheni mpya ya “kitimoto pimbi”,yaani nguruwe wadogo kupindukia.

Jioni hii kipindi cha Live From Studio Five katika kituo cha runinga cha Channel Five kimezungumzia fasheni hiyo mpya ambayo kwa hakika inaweza kuzua songombingo na maustaadhi pindi ikitua Bongo,almaaruf kwa ku-copy na ku-paste mengi ya yanayojiri anga hizi.



Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.