Showing posts with label EDWARD LOWASSA. Show all posts
Showing posts with label EDWARD LOWASSA. Show all posts

24 May 2012




Uamuzi mgumu na ujasiri wa kisiasa

Evarist Chahali
Toleo la 240
23 May 2012
WIKI iliyopita, Rais wa Marekani, Barack Obama, aliingia kwenye vitabu vya historia ya taifa hilo kwa kuwa kiongozi wa kwanza kuunga mkono ndoa za watu wa jinsia moja. Kwa muda mrefu Obama alikuwa aidha akipinga suala hilo nyeti au kuchelea kuweka wazi msimamo wake.
Tayari suala hilo la ndoa za jinsia moja limezua mgawanyiko mkubwa wa kimtizamo ingawa kura mbalimbali za maoni zinaonyesha kuwa msimamo huo ‘mpya’ wa Obama hautoathiri kwa kiasi kikubwa maamuzi ya wapigakura katika uchaguzi mkuu wa Marekani unaotarajiwa kufanyika Novemba mwaka huu.
Kwa mujibu wa kura za maoni za hivi karibuni, takriban asilimia 60 ya Wamarekani wanasema kitendo cha Obama kuunga mkono ndoa za mashoga hakitowashawishi kumpigia au kutompigia kura.
Lakini moja ya makundi ambayo yanaonyesha kuguswa na suala hilo ni Wamarekani Weusi. Kama ilivyo kwetu Waafrika, Wamarekani Weusi wamekuwa wapinzani wakubwa si tu wa ndoa, bali hata uhusiano wa kawaida wa watu wa jinsia moja. Mara kadhaa wasanii wengi wa muziki wa kufokafoka (hip-hop/rap), ambao ni maarufu kwa Wamarekani Weusi, wamekuwa wakilaumiwa kwa tungo zao zenye kuonyesha bayana upinzani dhidi ya ushoga.
Kwa mujibu wa gazeti la New York Times, baadhi ya viongozi wa makanisa ya Wamarekani Weusi wameeleza bayana kuwa hawamuuingi mkono Obama katika suala hilo, huku wengine wakitishia kutompigia kura katika uchaguzi mkuu ujao.
Japo Obama anaendelea kuungwa mkono na kundi hilo (la Wamarekani Weusi) huku akionekana kuwa ni ‘mwenzao’, kura za maoni zinaonyesha kuwa asilimia 49 inampinga katika msimamo wake kuhusu ndoa za mashoga kulinganisha na asilimia 43 ya Wamarekani Weupe.
Obama mwenyewe amekiri kuwa anafahamu bayana msimamo wake huo utawaudhi baadhi ya wanaomuunga mkono. Lakini akizungumza katika mahojiano maalumu na kituo cha luninga cha ABC cha Marekani, Rais huyo alieleza kuwa inamwia vigumu kuendelea na ‘sintofahaumu’ katika ‘ubaguzi’ dhidi ya mashoga ilhali Wamarekani kadhaa anaowaongoza wamo kwenye kundi hilo.
Alifafanua kuwa kama mzazi, alikuwa anapata wakati mgumu kutokuunga mkono ndoa za mashoga ilhali wanae Sasha na Malia wana  baadhi ya marafiki zao ambao wazazi wao ni mashoga.
Kadhalika, alieleza kuwa ilikuwa inamsumbua pia kuendelea kutokuunga mkono ndoa za mashoga huku baadhi ya makundi muhimu katika nchi hiyo, kwa mfano, wanajeshi wanaolitumikia taifa hilo kwa uadilifu mkubwa, yakijumuisha mashoga.
Lengo la makala hii si kumuunga mkono au kumpinga Obama katika msimamo wake huo kwa ndoa za mashoga bali kupigia mstari nafasi ya ujasiri katika uongozi.
Kama alivyokiri mwenyewe kuwa anafahamu bayana uamuzi wake wa kutangaza hadharani msimamo wake kuhusu ndoa za mashoga utawakera wengi, na pengine kumgharimu katika uchaguzi mkuu ujao, lakini Obama ameweza kufanya ujasiri wa kusimamia kile anachokiamini.
Japokuwa kuna baadhi ya wachambuzi wa siasa wanaotafsiri hatua hiyo ya Obama kama kigeugeu-kwa maana alishawahi kuwa mpinzani wa ushoga- huku wengine wakidai hatua hiyo ni ‘janja yake’ tu kusaka kura za mashoga, jambo la msingi hapa ni ukweli kwamba amediriki kuweka kando uoga (huku akijua madhara) na kuweka wazi wapi anasimamia katika suala hilo.
Kwa upande fulani, uamuzi huo unaweza kumnufaisha dhidi ya mpinzani wake mtarajiwa kutoka chama cha Republicans, Mitt Romney, ambaye kama ilivyo kwa wahafidhina wengi, suala la ushoga ni kama laana.
Sasa, kwa vile moja ya misingi muhimu ya taifa la Marekani ni uhuru wa mtu kufanya apendacho alimradi havunji sheria, sambamba na kupinga ubaguzi wa aina yoyote ile, Obama na wanaomuunga mkono wanaweza kuutumia upinzani wa Romney dhidi ya ndoa za mashoga kama mfano hai wa jinsi mgombea huyo (mtarajiwa) na chama chake cha Republicans walivyobobea kwenye ‘ubaguzi na kuminya uhuru’  wa Wamarekani.
Kwa mtizamo wangu, ujasiri alionyesha Obama (bila kujali kama naafikiana au ninapingana naye katika suala la ndoa za mashoga) ninaulinganisha na kauli za hivi karibuni za aliyekuwa Waziri Mkuu na Mbunge wa sasa wa Monduli (CCM), Edward Lowassa. Naomba niweke wazi kuwa ninaamini wasomaji wengi wa makala hizi wanafahamu fika msimamo wangu dhidi ya Lowassa, hususan kuhusiana na tuhuma za ufisadi. Lakini msimamo huo haumaanishi nichelee kumuunga mkono pale anapoonyesha ujasiri wa kisiasa.
Kwa muda mrefu sasa, Lowassa amejitokeza kuwa mmoja wa wanasiasa wachache ndani ya CCM wanaoeleza waziwazi mapungufu ya chama hicho na jinsi yanavyoliathiri taifa kwa ujumla. Lakini kama ilivyozoeleka, msimamo huo (ambao hapa ninauita ujasiri) umemfanya mwanasiasa huyo aonekane kama kiumbe hatari kabisa kwa ustawi na uhai wa chama hicho tawala.
Majuzi, Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, alinukuliwa akimpinga Lowassa kutokana na kauli yake katika mkutano wa hadhara huko Mto wa Mbu, Arusha, kuwa tatizo la CCM ni uongozi kuacha kusimamia misingi. Katika majibu yake kwa Lowassa, Mukama alimtaka mbunge huyo wa Monduli kushughulikia matatizo jimboni kwake kwanza.
Kuna wanaotafsiri kuwa msimamo wa Lowassa kukikosoa chama chake ni sehemu tu ya mikakati yake ya kuwania urais mwaka 2015. Lakini wanaofikiria hivyo wanapaswa kumtendea haki mwanasiasa huyo hasa kwa vile hajatangaza kuwa atagombea urais katika uchaguzi mkuu ujao. Kadhalika, ni muhimu kutanua upeo wetu na kuzichambua kauli za Lowassa pasipo kuzihusisha zaidi na malengo yake ya baadaye ya kisiasa.
Kimsingi, tukiweka kando hisia za ‘unafiki wa kisiasa’, anayoongea Lowassa kuhusu CCM ni ya kawaida sana kwa maana kwamba kila Mtanzania mwenye uwezo wa kufikiri anaelewa ‘mchango wa CCM katika kukwaza maendeleo ya nchi yetu.’
Kama chama tawala, CCM haiwezi kujinusuru dhidi ya shutuma kwamba inachangia sana kukwaza jitihada za kulikwamua taifa kutoka kwenye lindi la umasikini unaochangiwa zaidi na vitendo vya ufisadi.
Kwamba Lowassa ni mmoja wa wana-CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi si sababu ya kumfanya mwanasiasa huyo kutozungumzia suala hilo. Na hata hizo tuhuma dhidi yake zinaweza kukosa nguvu kwa vile CCM yenyewe imeshindwa kuchukua hatua zozote dhidi yake.
Makala hii haina maneno ya kuitia moyo CCM katika msimamo wa baadhi ya viongozi wake wanaokerwa na kauli za Lowassa, hasa ikizingatiwa kuwa anachofanya mwanasiasa huyo ni kuwakilisha tu mtizamo wa Watanzania wengi (ikiwa ni pamoja na wana-CCM) dhidi ya chama hicho tawala. CCM inaweza hata kumtimua Lowassa lakini isipojirekebisha, kuna kila dalili kuwa itang’olewa madarakani huko mbeleni.
Japo ninaelewa msimamo wa Mukama kwamba kama kiongozi wa CCM Lowassa anapaswa kuongelea matatizo ya chama hicho kwenye vikao vya ndani, kimsingi hilo ni moja ya vyanzo vya matatizo yanayosababisha watu kama Lowassa kuamua kuweka hadharani matatizo hayo.
Ni hivi, kama chama hicho kina matatizo, kisha yanazungumzwa kwenye vikao vya ndani na hayapatiwi ufumbuzi, kwa nini basi kiongozi asishawishike kuyaongelea matatizo hayo hadharani?
Halafu kuna suala la maslahi ya taifa dhidi ya maslahi ya chama. Kwa vile CCM ni chama tawala, kila inachofanya au kuzembea kufanya kinaligusa taifa moja kwa moja. Kwa mantiki hiyo, wakati Mukama anaweza kuyaona matatizo ya CCM kuwa ni suala la kichama, kiuhalisi matatizo hayo si tu yanaligusa taifa bali pia ni suala la kitaifa. Na kwa vile Tanzania ni yetu sote, basi ni sahihi na halali kwa kila Mtanzania, ikiwa ni pamoja na Lowassa, kuyaongelea matatizo yanayolisumbua taifa letu pasi uoga wa kumuudhi mtu flani.
Naomba kuhitimisha makala hii kwa kurejea kuweka bayana msimamo wangu kuwa lengo halikuwa kuunga mkono msimamo wa Obama kuhusu ndoa za mashoga wala kugeuka muungaji mkono wa Lowassa (japo vyote si dhambi).
Makala hii imelenga kuwapongeza wanasiasa hao kwa ujasiri wa kuweka wazi misimamo yao hata pale kufanya hivyo kunapoweza kuwaingiza matatizoni. Kinyume cha ujasiri ni uoga na unafiki, na sote tunafahamu kuwa kiongozi mwoga na/au mnafiki si tu hawezi kusimamia yale anayoamini lakini pia ni kikwazo katika jitihada za kuleta mabadiliko muhimu kwa anaowaongoza.


9 Mar 2012

Wednesday, 07 March 2012 19:31

Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa
ATHIBITISHA YUKO HOSPITALINI, ASEMA ASINGEPENDA KUELEZEA KWA UNDANI KUHUSU AFYA YAKE  
Ramadhan Semtawa
UTATA umegubika afya ya Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa baada ya taarifa mbalimbali kueleza kuwa yuko hospitalini nchini Ujerumani kwa matibabu.Takriban juma moja sasa kumekuwa na taarifa mbalimbali zikizungumzia afya ya Lowassa lakini hakukuwa na taarifa rasmi kutoka chanzo chochote kati ya Serikali, familia yake au Bunge kuzungumzia afya ya Mbunge huyo wa Monduli.

Jana, Lowassa akizungumza na mwandishi wetu kwa simu alisema kwamba yuko hospitali, bila kufafanua kuwa ni nje au ndani ya nchi, wala kueleza kinachomsibu.

Mahojiano hayo kati ya Lowassa na mwandishi wetu yalikuwa kama ifuatavyo:

Swali: Asalaam alaykum Mheshimiwa Lowassa.
Jibu: Waalaykum Salaam.

Swali: Mimi naitwa... (jina la mwandishi) kutoka gazeti la Mwananchi. Kwanza pole kwa matatizo ya kiafya yanayokusumbua.
Jibu: Ahsante.

Swali: Nimekupigia pamoja na kukupa pole, nilitaka kujua unaendeleaje na matibabu?
Jibu: Niko hospitalini kwa sasa naomba niache mambo mengine tutaongea baadaye.

Swali: Lakini, ni matibabu gani hasa unayopata?
Jibu: ... (akimtaja mwandishi) naomba niache niko hospitalini sasa hivi mambo mengine tuongee baadaye.

Lowassa alitoa majibu hayo majira ya saa nane mchana na alipopigiwa tena saa 10.20 jioni, alijibu kama ifuatavyo:

Swali: Naam, Mheshimiwa Lowassa nimekupigia tena mimi... (mwandishi akajitambulisha).
Jibu: ... Unataka nikuambie nini tena? Nilishakwambia niko hospitalini niache!

Swali: Sawa, natambua uko hospitalini, lakini wewe ni kiongozi ambaye umewahi kuwa Waziri Mkuu, hivyo Watanzania wangependa kujua maendeleo ya afya yako kutokana na utata ulioibuka na kama je, umelazwa hapo hospitalini au uko katika matibabu ya kawaida?
Jibu Niache, ninachokwambia niko hospitalini sasa unataka nini tena? Nisingependa kuzungumzia afya yangu kwa undani.

Bunge

Akizungumzia suala hilo juzi, Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashillilah alisema ofisi hiyo haijapata maombi rasmi ya mbunge huyo kwenda nje kwa ajili ya matibabu.

Dk Kashillilah alisema kwa utaratibu, Ofisi ya Bunge inashirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa ajili ya kuwapeleka wabunge wanaoumwa nje ya nchi baada ya kupata rufaa ambayo inatokana na ushauri wa kitaalamu wa madaktari wa ndani.

Alisema hadi juzi, hakuwa akijua aliko Lowassa na kama ana matatizo ya kiafya kama inavyozungumzwa au la: “Mimi ndiyo Ofisi ya Bunge na ndiyo nakwambia hatujapata maombi ya kutaka mheshimiwa Lowassa apelekwe nje ya nchi.”

Mtendaji huyo mkuu wa Bunge alisema wapo baadhi ya wabunge ambao huwa wanakwenda nje kwa vipindi maalumu kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa kawaida wa afya baada ya matibabu lakini, katika orodha hiyo Lowassa hayumo.

“Tunao utaratibu wa baadhi ya waheshimiwa wabunge kwenda nje kwa mujibu wa ratiba zao kwa ajili ya kufanyiwa uangalizi wa kawaida wa afya zao. Lakini, hadi sasa (juzi) katika orodha hiyo mheshimiwa Lowassa hayumo,” alisema Dk Kashillilah.

Hata hivyo, kwa mujibu wa nafasi yake ya utumishi serikalini aliyokuwa nayo, Lowassa anaweza kupata matibabu nje ya nchi kwa kupitia utaratibu wa Serikali bila ya kuhusisha Bunge.

Juhudi za kupata Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda au Naibu wake, Dk Lucy Nkya zilishindikana kutokana na simu zao kufungwa na kutopatikana ofisini.

CHANZO: Mwananchi

10 Dec 2011




Kikwete, Lowassa hapatoshi

Saed Kubenea's picture
Na Saed Kubenea - Imechapwa 30 November 2011
Printer-friendly versionSend to friend
HATIMAYE Edward Lowassa ametoka hadharani na kuonyesha kuwa anataka kupimana ubavu na Rais Jakaya Kikwete.
Ameeleza hadharani kuwa Rais Kikwete anahusika kwenye mkataba tata wa Richmond/Dowans; lakini pia, kuwa hafuati taratibu katika kuongoza chama chake.
Lowassa ambaye alikuwa nguzo muhimu katika mbio za urais wa Kikwete mwaka 2005, ameonekana kumgeuka waziwazi swahiba wake huyo kwa kuanika kile wachunguzi wanaita “udhaifu katika uongozi.”
Ndani ya kipindi cha siku nne, Lowassa ametoa kauli tatu nzito zinazoonyesha dhahiri ameamua kufanya mapambano na Kikwete.
Akiwa ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lowassa alinukuliwa akieleza hatua kwa hatua namna kampuni ya kitapeli ya Richmond Development Company (RDC), ilivyopewa zabuni ya kufua umeme wa dharura nchini.
Lowassa alijiuzulu wadhifa wa waziri mkuu mwaka 2008 kufuatia kashfa ya mkataba wa Richmond, kampuni iliyopewa kwa upendeleo zabuni ya kuzalisha umeme wakati haina fedha, haina uzoefu wala fedha za kufanyia kazi hiyo.
Alikiambia kikao cha NEC mjini Dodoma, “Hakuna jambo nililolifanya ambalo wewe Rais Kikwete hukulifahamu au hukunituma” kuhusu Richmond/Dowans.
Alisema, “…Mwenyekiti, natukanwa kwa ufisadi wa Richmond wakati wewe unafahamu yalichosababisha kashfa ya Richmond ni makosa ya watendaji walio chini yangu? Sasa kosa langu ni lipi? Ni kule kukubali kuwajibika kwa ajili ya serikali yangu na chama chetu? Kwa nini nihukumiwe kwa kosa hilo?”
Huku akimtolea macho Kikwete alisema, “Unakumbuka vema jinsi nilivyotaka kuvunja mkataba ule. Nilikupigia simu ukiwa nje ya nchi, lakini ukasema umepata ushauri wa kamati ya makatibu wakuu, ushauri ambao ulisababisha mkataba usivunjwe?”
Lowassa alisema Kikwete anafahamu kila kitu kwa kuwa ni yeye aliyeridhia Rostam Aziz kutafuta mbia baada ya Richmond kushindwa kuleta umeme.
“Uliponitaka ushauri wa mtu wa kutusaidia ili kuondokana na aibu ya Richmond kushindwa kutimiza mkataba wake, nilipokutajia jina la Rostam, haraka ulikubali na kusema, naona hilo ni sawa,” alieleza Lowassa kwa njia ya kumsuta Kikwete.
Hatua ya Lowassa kumuingiza Kikwete kwenye tope la Richmond/Dowans imezima moja kwa moja kauli yake iliyodai, “Siwajui wala siwafahamu wamiliki wa makampuni ya Dowans Tanzania Ltd na Dowans Holdings SA.”
Akihutubia kwenye maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa kwa CCM, tarehe 5 Februari 2011, mjini Dodoma, Kikwete alikana kufahamu wamiliki wa kampuni hiyo na kwamba hajawahi kuwaona wamiliki wake.
Alisema, “Nataka kuuhakikishia umma kwamba, sihusiki na kampuni hii. Siifahamu na wala sijawahi kuwaona wamiliki wake…Ama kweli akutukanae hakuchagulii tusi.”
Kauli ya Kikwete ya kutoitambua Dowans wala wamiliki wake, ilikuwa ni mwendelezo wa kauli kama hizo zilizokuwa zikitolewa na baadhi ya wasaidizi wake, zikilenga kumuondoa kwenye kashfa hiyo iliyomlazimu kuvunja baraza lake la mawaziri.
Akizungumzia kwa undani jinsi Richmond ilivyoingia na jinsi yeye na Kikwete walivyokuwa kitu kimoja kuhakikisha mkataba unasainiwa na kutekelezwa, Lowassa alisema, “Hakuna jambo nililolifanya ambalo Rais Kikwete hukulifahamu.”
Akizungumzia kwa undani suala hilo kwa mara ya kwanza tangu ajiuzulu wadhifa wa waziri mkuu, Februari 2008, Lowassa alisema, “Mwenyekiti kwanza napongeza uamuzi huu wa kurejesha jambo hili katika taratibu za kawaida, lakini napenda kufahamu kwa miezi saba nimetukanwa nikiitwa fisadi, watu wamezunguka nchi nzima kwa fedha za chama, hivi hatukujua kama kuna kamati hizo za maadili?”
Lowassa alikuwa akichangia pendekezo la Kamati Kuu (CC) ya CCM lililotaka kurejeshwa kwa suala la “kujivua gamba” kwenye vikao vya chini vya chama hicho baada ya watuhumiwa, isipokuwa Rostam Aziz, kukataa kuachia uongozi katika chama.
Kikwete alikiambia kikao cha NEC kuwa, uamuzi wa kutaka jambo hilo lirejeshwe kwenye vikao vya chini, umetokana na “taratibu kukosewa.”
Hata hivyo, kiongozi mmoja mwandamizi ndani ya chama hicho aliliambia gazeti hili juzi Jumatatu, uamuzi wa Kikwete kulirejesha suala la kujivua gamba kwenye vikao vya chini ulitokana na hofu ya NEC kujaa wajumbe wengi kutoka kwa kundi la Lowassa.
“Unajua mle NEC, Kikwete hana chake. Mle ndani kuna kundi kubwa la Lowassa, ndiyo maana jamaa ameogopa suala hilo la kuvuana magamba lijadiliwe,” ameeleza kiongozi huyo ambaye ni waziri katika serikali ya Rais Kikwete.
Kanuni za CCM zinaeleza kabla ya tuhuma kufikishwa NEC, sharti wale wanaotuhumiwa wapewe haki na fursa ya kujitetea mbele ya vikao vya kamati ya usalama na maadili.
Akifunga mjadala huo kwa angalizo mwanana, Kikwete aliagiza suala hilo lipelekwe kamati ya maadili ambako alitaka kuwasilishwa ushahidi wa vielelezo na siyo hujuma dhidi ya watuhumiwa.
Wakati Lowassa akishusha tuhuma kwa Kikwete, kiongozi huyo wa nchi alionekana kama amepigwa ngazi. Hakukana hata tuhuma moja miongoni mwa yaliyoelezwa na swahiba wake huyo wa zamani.
Kikwete na Lowassa, wamejitambulisha mara kadhaa kuwa ni marafiki, huku mmoja akisisitiza, “Hatukutana barabarani.”
Haijafahamika mahusiano yao yamefikia wapi kwa sasa baada ya Lowassa kumhusisha mwenzake katika kashfa ya Richmond katika kile wachunguzi wanasema amechukua tabia ya “tufe sote au tukose wote.”
Baadhi ya wachambuzi wa mambo wanasema kauli ya Lowassa ambayo ilitolewa mbele ya viongozi wake wakuu, akiwamo rais mstaafu, Benjamin Mkapa, ililenga kuonyesha udhaifu wa Kikwete ndani ya CCM kwa kuasisi falsafa ya kujivua gamba na kuikimbiza moja kwa moja kwenye CC na NEC, kinyume cha taratibu na kanuni za chama chake.
Kama hiyo haitoshi, juzi Jumapili akiwa mkoani Singida alikokwenda kusimamia harambaee ya kuchangia fedha za ujenzi wa kanisa, Lowassa alinukuliwa akisema, “Kwa vyovyote vile, nitaibuka mshindi dhidi ya vita vya kuvuana magamba.”
Akitiwa moyo na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Dayosisi ya Kati, Ushirika wa Amani, mjini Singida, Eliufoo Sima aliyesema, “suluhu ya mapambano ni kukabiliana nayo,” mwanasiasa huyo alisema, amekuwa akihusishwa na tuhuma ambazo hazina ukweli.
Askofu Sima alisema mapambano katika maisha hayatakwisha na “suluhisho siyo kuyaogopa, isipokuwa kuyatafutia majawabu kwa upole, hekima na utulivu.”
Vita vya magamba viliasisiwa na Kikwete 5 Februari 2011, kabla ya kudakwa na baadhi ya watendaji wa Sekretarieti ya CC ambao kwa miezi saba sasa, wamekuwa wakituhumu Lowassa na wenzake wawili - Rostam Aziz na Andrew Chenge – kuwa mafisadi wanaokidhalilisha chama mbele ya jamii.
Wakati hayo yakiendelea, taarifa kutoka ndani ya CC zinasema kushindwa kwa Rais Kikwete kutekeleza mkakati wake wa kumfukuza Lowassa ndani ya chama chake, kulitokana na upinzani mkali uliotokea kwenye mkutano wa CC.
“Ni kweli kabisa, ndani ya CC, Lowassa alipata uungwaji mkono mkubwa, kiasi ambacho mwenyekiti alilazimika kulipeleka suala hilo NEC. Alipofika NEC na kuona moto umekuwa mkubwa, ndipo alipoamua kuliondoa na kutaka lifanyiwe kazi kwenye vyombo vya chini,” kimeeleza chanzo kimoja cha gazeti hili.
Amesema wajumnbe wa Zanzibar, wakiongozwa na makamu mwenyekiti wa chama hicho visiwani, Amani Abeid Karume, muda wote wa mkutano walisimama imara kuhakikisha Lowassa hafukuzwi kwenye chama.
“Kuna wakati watu kutoka Bara walikuwa wanakaribia kushinda. Lakini baadaye Zanzibar wakapata nguvu pale Karume aliposimama na kusema, shutuma zote hizo hazijafuata taratibu,” ameeleza.



CHANZO: Mwanahalisi

26 Nov 2011


MKUU NIMEFURAHISHWA NA LOWASSA KUANZA KUANIKA UKWELI KUHUSU RICHMOND KWA KWELI NAONA ANAFANYA KILE NILICHOWAHI KUTABIRI KWENYE MAKALA YANGU YA "LOWASSA SEMA NENO MOJA TU" SASA KWA KULIONA HILO NIMEAMUA KUMTUNGIA SHAIRI HILO HAPO CHINI NAOMBA LITUNDIKE KWENYE BLOG YAKO WADAU WALISOME......


Kalamu yangu nashika, shairi nakutungia
Kamanda umeongea, kiwingu umeondoa
Hukutaka kusinzia,makosa kuyarudia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Mwananchi nimesoma, la jana nilinunua
Machoya yakatuama, dukuduku umetoa
Uliyosema Dodoma, Kwakweli yanavutia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Richmond kupasua, mapema uligundua
Kikwete ukamwambia, mkataba kuondoa
Rais akakataa, nini alitegemea?
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Nape akashikilia, lile asilolijua
Mikoani kaambaa, uzushi kang’ang’ania
Jinalo kulichafua, wewe ukavumilia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Mapema nilitabiri, falsafa nikapinga
Magamba sikukariri, kuvuana sikuunga
Ukweli niliukiri, mantiki iso kunga
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Beti sita nakomea, kalamu naweka chini
Mengi nimeongelea, soma tena kwa makini
Yatazidi kutokea,kusini kaskazini
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa.

Shairi limetungwa na Nova Kambota Mwanaharakati,
+255717 709618
Tanzania, East Africa
Jumamosi, November 26, 2011


9 Oct 2011


Tuipende,tuichukie lakini ukweli unabaki kuwa CCM ndio chama tawala.Kwa mantiki hiyo kila Mtanzania,including sie tusiokuwa wananchama wa chama chochote kile cha siasa tunalazimika kuwa na interest na hali ya mambo ndani ya chama hicho.Afterall,tofauti zetu za kiitikadi hazimaanishi uadui kama unavyohubiriwa na akina Nape.Sote ni Watanzania,na iwe CCM,Chadema,CUF,nk vyote ni vyombo tu vya kutushirikisha katika siasa za nchi yetu kwa namna moja au nyingine.

Anyway,niende kwenye mada.CCM inakabiliwa na changamoto kubwa katika kumpata mgombea wake anayetarajiwa kumrithi Rais Jakaya Kikwete atakapomaliza muda wake mwaka 2015.Naomba kuorodhesha changamoto hizo kama ifuatavyo

MGOMBEA KUTOKA ZANZIBAR

Japo Katiba ya Jamhuri ya Muungano na ile ya CCM hailazimishi utamaduni usio rasmi wa kupokezana nafasi ya mgombea urais kati ya CCM Bara na Zanzibar,yayumkinika kuamini kuwa baada ya miaka 20 (1995-2015) ya CCM Zanzibar kutotoa mgombea kwenye nafasi ya Urais wa Muungano upande huo utakuwa unatarajia kuwa sasa ni zamu yao.Baada ya Rais Mzanzibari Ali Hassan Mwinyi,alikuja M-Bara Benjamin Mkapa aliyetawala kwa miaka 10 kabla ya kurithiwa na M-Bara mwingine Jakaya Kikwete ambaye kufikia mwaka 2015 atakuwa ametawala kwa miaka 10.

Kwa vile katika utamaduni mwingine usio rasmi ndani ya CCM mgombea atakayepitishwa mwaka 2015 (na ikitokea akashinda) anaweza kuwa madarakani kwa miaka 10 (kwa maana kuwa anatarajiwa kupitishwa tena mwaka 2020-kama ilivyokuwa kwa Mwinyi,Mkapa na sasa Kikwete), Wazanzibari wakikubali mgombea ajaye wa CCM atoke Bara itamaanisha wakose nafasi kwa miaka 30 mfululizo.

Tofauti na ccm Bara ambapo uongozi wake una sauti kuliko wanachama,kwa Zanzibar wanachama na viongozi wa kawaida wana influence kubwa ndani ya chama hicho.Wakati uongozi wa CCM Zanzibar unaweza kuridhia mgombea ajaye ataoke Bara,ni vigumu kuhisi wanachama na viongozi wa kawaida wakakubali miaka mingine 10 pasipo Mzanzibari mwenzao kushika urais kupitia CCM.

Iwapo CCM Bara watashinikiza lazima mgombea atoke Bara basi Wazanzinari wanaweza kutumia turufu ya "tunatoka nje ya Muungano" na hili linaweza kuzua sokomoko kubwa.

MGOMBEA/RAIS MUISLAM KISHA MKRISTO (na vice versa)

Utamaduni mwingine ndani ya CCM ni kuzungusha nafasi ya urais (au mgombea wa urais) kati ya Waislam na Wakristo.Baada ya miaka kadhaa ya utawala wa Mwalimu Nyerere ikaja zamu ya Muislam Mwinyi,ambaye naye alirithiwa na Mkristo Mkapa,kabla ya ujio wa Muislam Kikwete.Katika mambo ambayo CCM inapaswa sifa nyingi ni pamoja na umakini wake katika kudili na ishu nyeti ya dini (japo wanasiasa mufilisi wameanza kutumia udini kwa minajili ya kusaka mafaniko yao binafsi kisiasa).Chama hicho kimejitahidi sana kuzingatia ukweli wa mgawanyo wa kiimani miongoni mwa Watanzania ambapo Waislam na Wakristo wanatengeneza takriban robo mbili za wakazi wote wa nchi yetu (robo nyingine ni wanaofuata imani nyingine pamoja na wapagani)..

Sasa,kwa kuzingatia ukweli kuwa Kikwete ni Muislam,inatarajiwa mgombea urais wa CCM mwaka 2015 awe Mkristo ili kudumisha utamaduni huo usio rasmi.Iwapo mgombea huyo atatoka Bara,haitokuwa vigumu kumpata.Tatizo ni iwapo mgombea atatakiwa kutoka Zanzibar.Kama tujuavyo,takriban asilimia 99 ya Wazanzibari ni Waislam,na hali ni kama hiyo kwenye uongozi wa CCM visiwani humo.Uwezekano wa kumpata mgombea urais kutoka Zanzibar ambaye ni Mkristo ni mgumu pengine kuliko uwezekano wa Gaddafi kuwa mgombea urais wa Marekani kuchuana na Rais Barack Obama hapo mwakani.

Kwa mantiki hiyo,kama changamoto ya kwanza itapatiwa ufumbuzi,yaani CCM kufanikiwa kupata mgombea wake kutoka Zanzibar,tatizo litabaki kwenye changamoto ya pili,yaani kupata mgombea Mkristo kutoka visiwani humo.

CHAGUO LA KIKWETE

Ni wazi Rais Kikwete angependa kupata mrithi atakayeweza kumpa amani baada ya kustaafu.Baada ya kuonjesha ladha ya 'ujeuri' pale baadhi ya vigogo wa chama hicho wanapodaiwa kutaka kumng'oa kwenye kiti cha uenyekiti wa chama hicho kwa kigezo cha kutenganisha kofia ya urais na uenyekiti wa CCM,yayumkinika kuamini kuwa asipokuwa makini kumpata mrithi atakayehakikisha anakula pensheni yake bila usumbufu wala hofu ya kukumbana na yaliyomkuta Chiluba...

Lakini Kikwete kulazimisha chaguo lake kutategemea namna atakavyoweza kumpromoti kuanzia sasa.Wachambuzi wengi wa siasa zetu wanafahamu kuwa Kikwete hana sauti kubwa ndani ya chama hicho.Kimsingi,mtu kama Edward Lowassa ana nguvu takriban mara mbili ya alizonazo Kikwete ndani ya chama hicho.Nguvu pekee ya mwenyekiti huyo ni kutoka kwa watu wa Idara ya Usalama wa Taifa ambao licha ya kumpatia dossiers zenye "machafu" ya viongozi wenzie wa CCM,pia wanaweza kulazimisha matakwa ya Kikwete yakatimia kwa mbinu chafu za kiintelijensia.Hilo linafanyika sehemu nyingi tu duniani ambapo siasa na intelijensia zimefunga ndoa isiyo rasmi.

Lakini hili la mashushushu kuingilia siasa za ndani ya CCM linategemea zaidi siasa za ndani za Idara ya Usalama wa Taifa.Wajuzi wa mambo wanafahamu mgogoro wa chini chini ndani ya Idara hiyo kuelekea mchakato wa CCM kumpata mgombea wake mwaka 2005.Tofauti za kimaslahi miongoni mwa viongozi waandamizi wa Idara hiyo zilitishia kwa kiasi kikubwa jina la Kikwete kupitishwa,na hata alipofanikiwa kupitishwa na hatimaye kushinda urais baadhi ya viongozi waandamizi wa Idara hiyo walijikuta majeruhi.

LOWASSA NA 'PIGA UA' YAKE

Mpende au mchukie, lakini Edward Lowassa ameendelea kuwa mwanasiasa mwenye nguvu na ushawishi mkubwa ndani na nje ya CCM.Licha ya uwezo wake mkubwa wa kifedha,Lowassa amewasaidia viongozi wengi wa CCM kuwepo madarakani,iwe kwa misaada ya kifedha au kimkakati.

Japo hajaweka msimamo wake hadharani,wachunguzi wengi wa siasa wanaamini kuwa ndoto za mwanasiasa huyo kumrithi Kikwete bado zipo hai.Inaaminika kuwa chanzo cha ndoto hizo ni mkataba usio rasmi kuwa Kikwete angemwachia Lowassa jahazi la kuongoza Tanzania baada ya kumaliza miaka yake 10 ya Urais.Mahesabu yalikwenda vizuri hadi pale ilipoibuka skandali ya Richmond iliyopelekea Lowassa kuachia ngazi.Laiti hilo lisingetokea basi muda huu wala nisingeandika makala hii kwa vile ingekuwa wazi kuwa Lowassa ndiye Rais ajaye baada ya Kikwete.

Kinachomsaidia Lowassa ni jinsi anavyotumia kila nafasi ipasavyo kuhakikisha jina lake linaendelea kuwa masikioni mwa Watanzania.Mwanasiasa huyo yupo radhi hata kuwaunga mono wanasiasa wa vyama vya upinzani alimradi kufanya hivyo kunamweka karibu zaidi na wapiga kura.

Kadhalika,pamoja na kuhusishwa na ufisadi,Lowassa anakubalika kama mtu anayemudu kufanya anachoamini,jambo linalomtofautisha na Rais Kikwete ambaye anaelemewa zaidi na kutaka kuwafurahisha watu wake wa karibu.Lowassa yupo tayari aonekane mbaya ndani ya CCM lakini aishie kuonekana mkombozi kwa Watanzania.

Na katika kumtendea haki,Lowassa ana 'u-Sokoine' wa namna flani.Hasiti kutoa maamuzi na anaweza kusimamia maamuzi yake.Laiti mwanasiasa huyu asingekuwa na mawaa ya ufisadi basi Tanzania ingeweza kupata carbon copy ya Sokoine.

Kuna wanaomwona Lowassa kama mwanasiasa anayeweza kubadilika kwa sababu kuu mbili.Kwanza,utajiri mkubwa alionao unaweza kabisa kumshawishi asitumie madaraka yake kuendeleza utaratibu wa kuifanya Tanzania kuwa shamba la bibi.Japo utajiri sio kigezo cha fisadi kutotamani fedha zaidi lakini madaraka kama ya Urais yanaweza kumfanya mtu apate huruma kwa anaowaongoza.Kikwete ana huruma lakini tatizo ni kwamba huruma yake kwa mafisadi ni kubwa ziadi ya ile aliyonayo kwa walalahoi.Hilo halina mjdala na mwenyewe anajua hilo.

Kingine kinachoweza kumpa faida Lowassa ni network yake ambayo inaweza kabisa kupenya Zanzibar kuwashawishi wamuunge mkono.Ukichanganya na advantage nyingine kwamba yeye ni Mkristo (ambayo inamfanya awe eligible kwa mujibu wa changamoto ya pili hapo juu),

Lakini pengine faida nyingine aliyonayo mwanasiasa huyu ni ukaribu wake na Idara ya Usalama wa Taifa,ambayo penda usipende itacheza nafasi muhimu kwa mgombea mwana-CCM yeyote anayetaka kumrithi Kikwete.Japo sina hakika kwa sasa ukaribu huo upo katika hali gani lakini unaweza kuwa na faida kubwa kwake.

Kubwa zaidi ya yote ni ukweli kwamba Lowaasa anamfahamu Kikwete in and out.Kwa mantiki hiyo,anaweza kumwandama Kikwete hata atakapomaliza muda wake wa Urais.Na kwa vile by then Kikwete hatokuwa na nguvu za kutosha ukilinganisha na hali ilivyo sasa ambapo yeye ni mkuu wa nchi, yayumkinika kuamini kuwa angependa kuwa na maadui wachache wenye nguvu na uwezo wa kumwangamiza.Kikwete anaweza kujikuta anakabiliwa na mzimu uleule ambao yeye na wanamtandao wenzake walimsababishia Rais Mkapa.

Inafahamika kuwa Kikwete na timu yake waliweka wazi kwa Mkapa kuwa laiti asingepitishwa basi aidha angegombea (na pengine kushinda) kupitia tiketi ya chama cha upinzani.Sasa ukizingatia Kikwete hakuwa karibu kihivyo na vyama vya upinzani kwa wakati huo,ukaribu wa Lowasaa kwa wapinzani unaweza kulifanya tishio la aina hiyo kuchukuliwa kwa uzito mkubwa.Ikumbukwe kuwa nafuu pekee kwa Kikwete atakapostaafu ni kwa CCM kubaki madarakani kwani kuna kila dalili kuwa kama chama cha upinzani kikishinda basi anaweza kabisa kupandishwa kizimbani kujibu tuhuma lukuki za ufisadi.

Je CCM wanawezaje kukabiliana na changamoto hizi?Moja ya njia mwafaka ni kujaribu kuiga utaratibu wa siasa za uchaguzi nchini Marekani ambapo wananchama wenye nia ya kuwania kupitishwa kugombea urais wanatangaza dhamira zao mapema.Pamoja na faida ya kumfanya mwanachama mwenye dhamira hiyo kufahamika vema kwa wapiga kura,utaratibu huo unaambatana na hatari zake.Kwa mwananchama kujitambulisha hadharani mapema anaweza kuwapatia maadui zake wa kisiasa ammunition ya kutosha kumteketeza mapema,na ikifika wakati wa kupiga kura za kumpitisha mgombea anaweza kuwa amekwisha kabisa.

Anyway,kwa leo naomba kuishia hapa.Nitaendelea na mada hii wakati mwingine

10 May 2011



Kwa walioamini usanii wa CCM kuwa imeamua kujivua magamba wahesabu wameliwa.Sio tu ukweli kwamba joka linalojivua magamba linakuwa hatari zaidi bali pia ufahamu wetu wengi kuwa joka likijivua magamba haligeuki kuwa mjusi.Na kama baadhi ya wanasiasa wa upinzani walivyoelezea suala hilo la magamba,tatizo la CCM ni mithili ya kansa ya damu.Dawa yake pekee ni kifo,and sure will CCM die,sio kwa vile kimezeeka vibaya bali kwa sababu ni mkusanyiko wa walafi,waroho,majambazi,matapeli na mabazazi wa kisiasa.Putting it bluntly,ushirika wa wachawi kamwe hauwezi kudumu.Let's wait and see!

VIONGOZI wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameshindwa kuwaondoa katika chama hicho wale wanaowaita watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, imefahamika.

Viongozi ambao waliotajwa kuwa wanatakiwa kujiondoa kwenye uongozi au chama ndani ya siku 90 kwa kuwa ni “mafisadi wanaochafua sura ya chama mbele ya jamii,” ni Edward Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge.

Kinyume na majigambo ya viongozi wa juu wa chama hicho, kuwa sharti watuhumiwa hao waondolewe kwenye vikao vya maamuzi, hadi sasa chama kimeshindwa kuwapa barua za kuwajulisha juu ya suala hilo.

Katibu Mkuu Wilson Mukama, katibu wa itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara, John Chiligati wamekuwa wakishindilia kuwa “mafisadi lazima waondoke.”

Hata hivyo, Mukama aliwaambia waandishi wa habari juzi Jumatatu, jijini Dar es Salaam, “…hakuna mahali popote katika maazimio ya NEC panapotaja siku 90.”

Alisema, “Kama ni muda basi ni pale mwenyekiti wetu aliposema NEC ijayo. NEC hukutana kila baada ya miezi minne na kwa hiyo kama ni siku, basi ni 120 na siyo 90,” alieleza Mukama akijibu swali la mmoja wa waandishi waliotaka kufahamu ni lini chama hicho kitaandika barua na kukabidhi watuhumiwa.

Kauli ya Mukama kwamba hakuna mahali ambapo NEC imeagiza Lowassa, Rostam na Chenge waondoke ndani ya chama katika muda wa siku 90 zijazo, imekuja wiki moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kukutana kwa faragha na Lowassa.

Taarifa za ndani ya chama na kutoka baadhi ya viongozi wa CCM, zinasema mazungumzo ya viongozi hao wawili yalijikita katika kile kilichoitwa “kujivua gamba” na kwamba Lowassa anamtuhumu Nape kusambaratisha chama chao kwa kuendeleza tuhuma katika mikutano ya hadhara.

Lowassa na Kikwete walikutana ikulu jijini Dar es Salaam, 25 Aprili 2011 baada ya kushindwa kukutana mjini Dodoma, 3 Aprili 2011 kama ambavyo Kikwete alikuwa ameahidi.

Katika mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari, Mukama alisema, “NEC ilitoka na maazimio 26. Azimio mojawapo linasema chama kiendelee na mapambano yake dhidi ya ufisadi na kwamba watuhumiwa wakitafakari, wajipime na kuchukua hatua.”

Alisema, “Sehemu ya hotuba ya mwenyekiti wakati akifunga mkutano ilisema tunatambua athari ya kukosekana maadili katika chama na tuendelee kupambana; na katika hili hakuna ajizi. Viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajitafakari, wajipime na wachukue hatua,” alisema Mukama akinukuu kauli ya mweneykiti wa CCM, Rais Kikwete.

Alipoulizwa ni watuhumiwa gani wa ufisadi kwa kuwa chama hicho hakijawahi kuwa na orodha yake, badala yake orodha inayofahamika kwa wengi ni ile iliyotolewa na kiongozi mkuu wa upinzani nchini, Dk. Willibrod Slaa, Mukama alisema, “…CCM ni taasisi kubwa yenye mfumo wake na miongozo yake; hivyo haitegemei orodha ya CHADEMA.”

Mukama alikuwa akijibu swali la Manyerere Jackton wa New Habari House. Alitaka kufahamu vigezo vinavyotumika kutambua mafisadi; na iwapo wataweza kumwondoa Kikwete ndani ya chama hicho kwa vile naye ametajwa katika orodha ya Dk. Slaa ya tarehe 15 Septemba 2007.

Hata hivyo Mukama aliendelea kushikilia kuwa chama chake hakiwezi kufuata orodha za vyama vingine, hasa CHADEMA.

Kwa upande mwingine Lowassa amenukuliwa akimtaka Kikwete kumdhibiti Nape kwa kuwa “anakivuruga chama” kwa hatua yake ya kusisitiza kuwa NEC ilipitisha maamuzi ya kuwataka wajiuzulu, wakati akijua fika kwamba hilo si kweli.

“Mkutano kati ya Lowassa na rais ulikuwa mfupi sana. Lowassa alimueleza Bwana Mkubwa (rais Kikwete), jinsi asivyofurahishwa na mwenendo wa Nape hasa jinsi anavyowatuhumu ufisadi. Alimsihi Rais Kikwete kumweleza hilo katibu wake mwenezi, Nape…,” ameeleza mtoa taarifa.

Kikwete, taarifa zinasema, alimhakikishia Lowassa kuwa “…hakuna lolote litakalotokea,” kauli ambayo imethibitishwa na Mukama katika mazungumzo yake na wahariri.

“Yule bwana (Lowassa) alimuuliza Kikwete, mnataka kunipa barua kwa kosa lipi? Nimefanya nini? Nini ambacho wewe hukifahamu,” anasema mtoa taarifa wa MwanaHALISI.

Gazeti hili limejulishwa na vyanzo vyake vya ndani ya serikali kuwa uamuzi wowote utakaochukuliwa na Lowassa, unaweza kuzidisha mgawanyiko ndani ya CCM.

Mara baada ya Lowassa kukutana na Kikwete, taarifa zinasema mbunge huyo wa Monduli alikutana na kufanya mazungumzo marefu na Peter Kisumo, mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya chama hicho.

Katika mazungumzo yao, Lowassa alionya kuwa CCM kiko hatarini kupasuka kutokana na kauli za Nape na mwenzake John Chiligati juu ya ufisadi na watuhumiwa wake.

“Huyu bwana anaua chama. Nakuhakikishia mzee Kisumo, hawa watu wakiendelea kunishutumu bila sababu, nitatoka hadharani na kujibu mapigo,” anaeleza mtoa taarifa akimnukuu Lowassa katika mazungumzo yake na Kisumo.

Naye Kisumo anaripotiwa kumhoji Lowassa, “Mbona ninyi marafiki wawili mnataka kusambaratisha chama?” Naye Lowassa alijibu, “Kheri iwe hivyo…”

Mwandishi wa gazeti hili alimtafuta Lowassa ili kuthibitisha walichojadili na Kikwete, lakini simu yake iliita bila kupokelewa.



10 Apr 2011




Habari zilizopatikana kutoka Dodoma kwenye kikao cha CCM chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete zinaeleza kuwa baadhi ya viongozi waadamizi wa chama hicho wamevuliwa madaraka.Kwa mujibu wa vyanzo vya mtandaoni,waliokumbwa na panga la Kikwete ni pamoja na maswahiba wake wakuu kisiasa,Edward Lowassa na Rostam Aziz.Wengine wanaotajwa kwa mujibu wa habari hizo ni "Mzee wa Vijisenti" Andrew Chenge na "mgosi" Yusuph Makamba.

Ningependa kuichambua habari hii kwa kirefu lakini nasubiri kwanza tamko rasmi la CCM.Hata hivyo,tukiamini kuwa habari hizo ni sahihi,kuna uwezekano ya yafuatayo kutokea:

Kwanza,ni muhimu kufahamu watu kama Lowassa na Rostam wametoka wapi.Hawa walikuwa vioungo muhimu kwa ushindi wa Kikwete mwaka 2005.Wanaowajua vema wanawa-describe kwa mlolongo huu:Lowassa-mwanasiasa haswa (simaanishi kuwa ni mwanasiasa mwadilifu),Rostam-bwana fedha,na Kikwete-mtawala.Wajuzi wa siasa chafu wanaeleza kuwa ushirikiano huo wa watu hawa watatu ulitumia kila aina ya mbinu kuhakikisha Kikwete anaingia Ikulu hapo 2005.Na ikawa hivyo,baada ya viongozi hao wakuu wa "Mtandao" kufanikiwa kupenya takriban kila kundi la jamii;kutoka viongozi wa dini hadi wakuu wa taasisi za dola,kutoka wanahabari hadi wasanii.

Pasipo kuuma maneno,ushirika huu usio mtakatika wa Lowassa,Rostam na Kikwete ni mithili ya joka lenye vichwa vitatu.Sasa iwapo ni kweli kuwa Kikwete kaamua kubaki kichwa pekee kwenye joka hilo basi yayumkinika kubashiri kuwa uhai wa joka hilo nao uko matatani.

Pili,kwa kufuata mlolongo wa nilichoandika hapo juu,inaelezwa kuwa Lowassa ndiye aliyefanya kazi kubwa zaidi ya kutengeneza serikali ya Kikwete.Ikumbukwe kuwa japo wote wawili walishashika nyadhifa mbalimbali serikali kabla ya 2005,Lowassa alikuwa amejijenga zaidi kiuchumi na kisiasa ukilinganisha na Kikwete.Kadhalika-na hapa nafafanua kwanini niliandika hapo juu kuwa Lowassa ni mwanasiasa haswa(japo simaanishi ni mwanasiasa mwadilifu)-ni ukweli kuwa mwanasiasa huyo ana ushawishi wa kisiasa zaidi ya Kikwete.Japo wote wawili ni wapenda umaarufu (populists),wakati Kikwete amekuwa akitumia zaidi turufu ya "tabasamu la muda wote" na "kuwa karibu na watu",Lowassa amekwenda mbali zaidi na kujifanya anayafahamu matatizo ya wananchi na kuyatolea ufumbuzi mapema (ndio maana licha ya kulazimika kujiuzulu kutokana na ufisadi wa Richmond bado kuna wanaomwona kama mwajibikaji).Kwa kifupi,Lowassa ni mwepesi wa kuchukua maamuzi (hususan yale yatayopelekea yeye kuonekana kama "Sokoine flani hivi"),Kikwete ni mzito wa maamuzi (huku walio karibu naye wakidai tatizo sio uzito wa maamuzi bali hajui vipaumbele vyake).

Inaaminika kuwa Lowassa ana ufuasi mkubwa ndani ya CCM na serikalini kwa ujumla.Kwa mujibu wa wajuzi wa mambo,faida aliyonayo Lowassa ndani ya chama hicho ni uwezo wa kifedha,ambapo inaelezwa kwamba amewasaidia viongozi mbalimbali wa CCM kiuchumi na kuwawezesha kuwepo walipo leo.Kadhalika,akiutumia vema urafiki wake na Kikwete, na nafasi yake kama Waziri Mkuu kabla ya skandali ya Richmond,aliweza kutengeneza "mtandao ndani ya mtandao",kwa maana ya kuwaweka madarakani watu wenye utiifu kwake zaidi kuliko CCM au Kikwete.Inaelezwa wateuliwa wengi kwenye nafasi za kiserikali na kichama ngazi za mikoa na wilaya ni wafuasi wa Lowassa,kwa mfano ma-RC na ma-DC,na wenyeviti na makatibu wa CCM mikoani na wilayani.

Swali la muhimu ni je,kuondoka kwa Lowassa katika wadhifa mmoja kutazuwia nguvu na ushawishi wake kwa wafuasi wake,wengi wao wakiwa ni watu walio madarakani kutokana na fadhila za mwanasiasa huyo?

La tatu ni ukweli kuwa Lowassa anataka urais hapo 2015.Na hilo halikuanza jana au juzi bali wajuzi wa mambo wanaeleza kuwa kulikuwa na makubaliano rasmi kati ya Kikwete na Lowassa kuwa wangepokezana uongozi maara baada ya Kikwete kumaliza miaka yake 10.Japo suala la Richmond lilizua mfarakano wa aina flani kati ya wawili hao lakini ukweli unabaki kuwa "heshima" aliyotoa Kikwete kwa Lowassa kwa kutomtimua bali kusubiri ajiuzulu mwenyewe iliwaacha wawili hao wakiendelea na urafiki wao japo si kama ilivyokuwa mwanzoni.

Haifahamiki kama Kikwete bado anaheshimu "makubaliano" yake na Lowassa kuhusu "kupokezana kijiti cha urais hapo 2015" lakini hiyo haimzuwii Lowassa kuamini kuwa "piga au" lazima achukue nafasi hiyo.Of course,kuna majina kama Bernard Membe (mtu anayetajwa kuuweka uhusiano na Lowassa katika wakati mgumu kwa vile yeye na Lowassa "picha hazipandi" ilhali yeye na Kikwete ni "damu damu",na Kikwete na Lowassa ndio hivyo tena "hawakufahamiana mtaani" kama ilivyowahi kutamkwa hadharani ) lakini turufu ya Lowassa haitegemei sana baraka za Kikwete bali ushawishi na nguvu yake ndani ya CCM,sambamba na uwezo wake mkubwa wa kifedha (alizitoa wapi....waulize TAKUKURU).Na ana faida nyingine kubwa ambayo ni uswahiba wake na Rostam,mfanyabiashara mwenye asili ya kiasia anayetajwa kuwa na nguvu zaidi ya Kikwete-kutokana na utajiri wake unaoweza kumfanya kuwa mtu tajiri kuliko wote Tanzania.Kadhalika,inaelezwa kuwa Rostam ni mjuzi wa mbinu chafu hususan kwa kutumia fedha zake na "njaa" za wanaohitaji chochote kutoka kwake.

Jingine,ambalo linaweza kuwa si la msingi sana japo lina umuhimu wa aina flani ni ukweli kwamba Lowassa na Rostam wana siri muhimu kumhusu Kikwete na urais wake kwa ujumla.Njia pekee kuwadhibiti wawili hao kwa kutumia Idara ya Usalama wa Taifa.Katika siasa zetu za "ovyo ovyo" ni rahisi tu kwa rais kuiamuru taasisi hiyo imfanyie kazi zake binafsi badala ya zile za kikatiba.Hilo linawezekana zaidi kutokana na nafasi ya Rais kama consumer wa taarifa zote za kishushushu.

Nisingependa kutabiri matokeo kabla ya taarifa kamili ya CCM lakini tukiamini habari zilizopo na ikathibitika kuwa ni kweli basi nachobashiri ni mwanzo wa mwisho wa chama hicho tawala.Naomba unielewe vizuri: tatizo la msingi sio kutimuliwa kwa Lowassa na Rostam bali ukweli kuwa USHIRIKA WA WACHAWI HAUDUMU.Sambamba na hilo ni ukweli mwingine kuwa JOKA LENYE VICHWA VITATU HALIWEZI KUWA HAI MUDA MREFU PINDI VICHWA VIWILI VIKIKATWA.

Lakini la muhimu kuliko yote ni manufaa kwa Watanzania kutokana na mabadiliko hayo ndani ya CCM.Kwa kifupi,ukiacha vichwa vikubwa vya habari kwenye magazeti yetu,mabadiliko hayo hayana manufaa yoyote kwa masikini wasio na hakika ya mlo wao wa kesho,wanafunzi wanaokaa sakafuni kwa uhaba wa madawati,akina mama wanaoletewa bajaj za kuwawahisha hospitali wakiwa wajawazito japo wabunge wanapewa mashangingi ya uheshimiwa,nk nk nk.Wa kuondoka na CCM kama chama kilichopo madarakani.Wanapoondoana ndani kwa ndani haimsaidii Mtanzania wa kawaida.

17 Mar 2011


"Tiba ya Babu" imeibua kila aina ya vimbwanga.Nikianza kuviorodhesha vimbwanga hivyo basi tutakesha kwani kila kukicha kuna mapya.Mara tusikie wagonjwa waliotoroka mahospitalini "wamefumaniana" na madaktari waliotorokwa na wagonjwa hao,huku wote-wagonjwa na madaktari wakiwa kwenye foleni kusbiri "tiba ya Babu"

Lakini siui kama msomaji mpendwa umebaini "mpasuko wa kimtizamo" kati ya maswahiba wawili maarufu,Rostam Aziz na Edward Lowassa.Wakati Rostam alinukuliwa akiiponda "tiba" hiyo,swahiba wake-Lowassa-sio tu alitinga kwa "Babu kupata kikombe" bali pia inaelezwa amewalipia wapiga kura wake gharama za usafiri kwenda kupata "tiba" hiyo.

Je hii ni dalili ya mwanzo ya mpasuko kati ya wanasiasa hawa ambao majina yao ni kama synonymous na ufisadi?Au wanatuzuga tu mind games?You decide

Rostam aponda tiba ya Mchungaji Loliondo
Tuesday, 15 March 2011 21:22

Shija Felician, Igunga
WAKATI Watanzania wengi wakimiminika kwenda wilayani Loliondo, mkoani Arusha kupata dawa inayodaiwa kutibu magonjwa sugu, Mbunge wa Igunga (CCM), Rostam Aziz ameibuka na kusema tiba hiyo haina lolote akidai kwamba ndugu zake watano wameitumia lakini hawajapona.

Akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru wapigakura uliofanyika kwenye Viwanja vya CCM wilayani Igunga, Tabora mbunge huyo alisema haiamini dawa hiyo kwa kuwa ana ushahidi kwa ndugu zake hao ambao anadai kwamba wanaendelea kuugua kisukari licha ya kutumia dawa hiyo siku saba zilizopita.

Aliwataka wale watakaokwenda Loliondo ambao wanatumia dawa za hospitalini kuendelea kuzitumia badala ya kuzipuuza na kuzitupa... “Ndugu zangu wananchi wa Igunga, mimi mjomba wangu Hassan mnamfahamu karibu wote hapa mjini ni mgonjwa wa siku nyingi wa kisukari. Ameshakunywa dawa hiyo lakini mpaka sasa ni mgonjwa kama mnavyomuona sasa hiyo dawa inaponyesha nani?”

Hata hivyo, aliwataka wananchi wote wenye imani juu ya dawa hiyo waende huku akiwasisitizia kutopuuza ushauri wa madaktari kwani.

Wakati Rostam akipinga dawa hiyo, wilayani Kahama, mamia ya wafanyabiashara wamefunga shughuli zao na kukimbilia Loliondo kwa Mchungaji Mwasapile kunywa dawa hiyo huku baadhi ya waliorejea baada ya kuinywa wakidai kuwa hali zao sasa ni nzuri.

Wafanyabiashara hao wengi wao wanaondoka kwa siri wakidai wanakwenda Dar es Salaam katika shughuli zao, lakini siri imefichuka baada ya baadhi yao kuoneka katika runinga wakiwa katika foleni wakisubiri kupatiwa huduma hiyo.

Mbali ya kuzungumzia suala hilo la tiba ambalo limegusa hisia za wananchi wengi wa Afrika Mashariki, mbunge huyo aliwapa pole wananchi wa Igunga ambao nyumba zao zimeezuliwa na upepo uliosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha wiki iliyopita ambazo ziliathiri kaya 19. Aitoa msaada wa Sh500,000 kwa kila kaya iliyokumbwa na maafa hayo.
CHANZO: Mwananchi

Lowassa apata kikombe Loliondo
Tuesday, 15 March 2011 23:47

Waandishi Wetu

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa juzi alipata tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapile katika Kijiji cha Samunge, Tarafa ya Sale, Loliondo, mkoani Arusha.Lowassa alifika katika eneo hilo mchana akiwa na viongozi kadhaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Serikali kisha kupata kikombe kimoja chenye dawa kinachotolewa na mchungaji huyo kwa ajili ya tiba.

Tofauti na viongozi wengine, Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), Jimbo linalopakana na Kijiji cha Samunge, alikwenda huko akiwa na viongozi mbalimbali wakiwamo viongozi wa dini na baadhi ya wapigakura wake.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Lowassa alithibitisha kwenda Loliondo na kuwataja viongozi wa dini alioambatana nao katika msafara wake kuwa ni Askofu Msaidizi wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini, Dk Frederick Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Dayosisi ya Kaskazini Kati (Arusha), Mchungaji John Nangole.

Katika ramani ya utendaji kazi ya KKKT, Jimbo la Masai Kaskazini ndipo kilipo Kijiji cha Samunge ambako ni makazi ya Mchungaji Mwasapile.“Ni kweli, nimekwenda pale na wapigakura wangu pamoja na viongozi wa dini, Msaidizi wa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Dk Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Mchungaji Nangole,” alisema Lowassa na kuuliza: “Kwani hiyo nayo ni habari jamani?”

Baada ya Lowassa kufika katika kijiji hicho akiwa na ujumbe wake, aliongoza moja kwa moja hadi kwa Mchungaji Mwasapile na kuzungumza naye kisha akapata kikombe cha tiba na kuondoka.

Kabla ya Lowassa kwenda kupata tiba, amekuwa akitoa msaada wa nauli kwa wagonjwa mbalimbali wa jimbo lake kwenda kwa mchungaji huyo ambaye dawa yake inadaiwa kutibu magonjwa ya saratani, kisukari, pumu, shinikizo la damu na Ukimwi.Lowassa ni miongoni mwa wanasiasa maarufu nchini ambao wameshafika kwa mchungaji huyo kupata tiba hiyo wakiwamo mawaziri, naibu mawaziri, wabunge, wakuu wa mikoa na wilaya.
CHANZO: Mwananchi

29 Jan 2011


Katika siku za hivi karibuni,gazeti la Tanzania Daima limeonekana kama linafanya juhudi za wazi kuiweka profile ya Edward Lowassa machoni na masikioni mwa wasomaji wa gazeti hilo.

Ukidhani observation hii ni ya majungu,basi nakushauri uanze na habari zilizo kwenye toleo la kesho Jumapili (mbalo tayari lipo mtandaoni katika tovuti ya gazeti hilo) kisha fanya assessment yako Jumapili ijayo,na nyingineyo.

Je hizi ni sehemu ya kampeni za kumrithi Kikwete 2015?

Nimechokoza tu udadisi,hitimisho nakuachia wewe msomaji

24 Jan 2011



Kwa hakika inachosha kila unapoingia mtandanoni na kukutana na episode mpya ya sakata la Dowans.Tangu mwanzo ilishabainika Rais Jakaya Kikwete yuko upande gani katika ishu ya ujambazi wa waziwazi (daylight robberies) ulioshamiri kwenye sekta ya nishati.Lakini si vibaya kujikumbusha tumetoka wapi na uhusika wa Kikwete katika ufisadi unaokaribia kuadhimishwa kitaifa kwa tuzo kubwa ya mabilioni ya shilingi kwa kampuni ya kijambazi ya Dowans.


Muda si mrefu baada ya Kikwete kuingia madarakani,aliendeleza mlolongo wa porojo zake za kuwaletea Watanzania maisha bora kwa kulipatia ufumbuzi tatizo sugu la nishati ya umeme.Na hapo tunaweka kando uhusika wa Kikwete katika mkataba mwingine wa kitapeli unaoiwezesha kampuni ya IPTL kulipwa mamilioni ya shilingi hata wasipoipatia Tanesco mchango wa umeme katika gridi zake.

Huku baadhi ya Watanzania wakiendelea kuamini kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu,aliwaahidi kuwa tatizo la umeme litakuwa historia pindi itapowasili mitambo ya umeme kutoka nchini Marekani.Na hatimaye mitambo hiyo ikawasili kwa mbwembwe ikiwa imekodiwa dege kubwa la mizigo.Picha zikapigwa,wahusika katika radio,runinga, magazeti na blogu wakaripoti.

Lakini kama wasemavyo waswahili kuwa za mwizi arobaini,mitambo hiyo ikabaki kuwa mitambo tu.Kumbe sio tu ilikuwa bomu bali hata kampuni iliyopewa dili na Kikwete-RICHMOND HIYO- nayo ilikuwa bomu.Actually,ilikuwa ni kampuni yenye ofisi kwenye brifukesi.

Kikwete akaufyata kana kwamba si yeye aliyeutangazia umma kuwa mitambo feki ya richmond ingekuja kumaliza tatizo la upatikanaji wa nishati ya umeme.Lakini kwa vile Kikwete hakuwa peke yake kwenye dili hilo,swahiba wake wa karibu,na Waziri wake Mkuu kwa wakati huo,Edward Lowassa,akaamua kulivalia njuga suala hilo na kuanzisha jitiahada za makusudi kuzuwia mjadala wowote kuhusu utapeli huo.Katika harakati hizo,blogu hii ilikumbwa na zahma pale mwandishi wa habari wa Lowassa,Said Nguba alodiriki kuandika comments kali hapa bloguni akinishambulia Truly Yours baada ya mie kumkemea Lowassa kuhusu jitihada zake za kuzuwia mjadala wa Richmond Bungeni. 

Kadhalika,msimamo wangu na wa blogu hii kuhusu suala hilo ilipelekea kupewa karipio kali kutoka kwa aliyekuwa mwajiri wangu wakati huo huku bosi aliyenipigia simu kuwasilisha karipio hilo akihoji nimekuja Uingereza kusoma au kuandika habari za uchochezi.Kichwa maji huyu alijifanya haelewi kuwa mie nilikuwa najinyima muda wangu wa masomo ili kufanya kile mwajiri wangu alipaswa kukifanya in first place,na laiti angefanya basi leo hii tusingekuwa tunajadili malipo kwa mrithi wa Richmond,yaani kampuni ya kiharamia ya Dowans.Kwa sababu za kimaadili,siwezi kumtaja mwajiri huyo. 

Ofkoz,Nguba na bosi huyo walikuwa wanatekeleza tu wajibu wao uliokuwa unawawezesha kupeleka mikono yao kinywani.Hata hivyo,kile kile nilichokiasa kwenye makala iliwasukuma wazushi hao kunikaripia,kilitokea miaka miwili baadaye: Lowassa alilazimika kujiuzulu baada ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dr Harrison Mwakyembe kuchunguza sakata hilo la Richmond kukamilisha kazi yake.

Kufupisha habari,baadaye Richmond ikarithishwa kwa jambazi mwingine Dowans.Na muda wote huo Kikwete akaendelea kuuchuna kana kwamba kinachotokea hakihusiani na maamuzi yake finyu.Baadaye mjadala wa Richmond ukarejeshwa tena bungeni lakini kwa vile wahusika walishajipanga vyema kuukabili,na kwa vile CCM ilishajitambulisha kuwa ni kichaka cha mafisadi,mjadala huo ukamalizwa kishkaji.Hakuna aliyewajibishwa,na Watanzania kama kawaida yao wakaendelea na maisha yao kana kwamba hakuna fedha zilizoibiwa.

Kelele za hapa na pale zilikuwepo,lakini kimsingi zilikuwa kama kelele za kutimiza wajibu tu (talking for sake of hearing own voice).Ni katika kipindi hicho pia kukazuka mjadala nini kifanyike kuhusu mitambo feki ya Dowans.Baadhi ya wenzetu,kwa mfano Mbunge Zitto Kabwe,walishauri mitambo hiyo itaifishwe.Wengine wakasisitiza kuwa kutaifisha pekee hakutoshi pasipo kuwawajibisha waliotuingiza mkenge katika suala hilo.Wakati wote huo Kikwete aliendelea kujifanya bubu na kiziwi kuhusu ishu hiyo.

Lakini kabla kidonda hakijapona,zikasikika habari kuwa Mahakama moja ya Kimataifa imeipa ushindi Dowans na serikali kuamuriwa ilipe mabilioni kama fidia.Kichekesho,or rather matusi,ni ukweli kwamba habari kuwa serikali imeshtakiwa na Dowans zilifanywa siri.Na kama kuongeza uzito wa matusi,viumbe waliopaswa kuwa watetezi wa umma kupinga malipo kwa majambazi wa Dowans-hapa namaanisha Waziri wa Nishati William Ngeleja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Werema- wakaibuka kuwa watetezi wa Dowans.Uchizi,kulewa madaraka,sintofahamu au sheer ufisadi!!!???Yani mshtakiwa anakuwa bize kuhalalisha hukumu dhidi yake?Kwanini basi nguvu wanayotumia mafisadi hawa baada ya hukumu kutolewa haikutumika kuhakikisha wanashinda kesi husika (assuming kulikuwa na kesi kweli,maana kuna tetesi kuwa mahakama yenyewe ilikuwa katika mfumo wa mlo wa jioni hapo Movenpick).

Back to Rais wetu Kikwete.Ameendelea kuuchuna hadi majuzi.Awali,alipotuhumiwa kuwa ndio mmiliki wa Dowans,mpambe wake Salva Rweyemamu akakurupuka na kauli chafu kabisa dhidi ya mwakilishi wa umma,Dkt Willibrod Slaa,aliyeamua to call a spade a spade kwa kubainisha kwamba Kikwete ndiye Dowans.Siku chache baadaye Kikwete akamjibu Dkt Slaa kwa vitendo: akaagiza askari wake (through IGP Said Mwema) wapige hadi kuua wananchi wasio na hatia huko Arusha.

Lakini,again za mwizi arobaini.Juzi tumefahamishwa bayana kuwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichokaa chini ya uenyekiti wa Kikwete kimeridhia malipo kwa Dowans.Huhitaji japo short course ya uchambuzi wa siasa kutambua kuwa laiti Kikwete angekuwa upande wa wananchi na hivyo kupinga malipo kwa kampuni hiyo ya kifisadi,Kamati Kuu isingethubutu kuridhia malipo hayo.Kwa hiyo at last Kikwete ameweza kuibua sura yake aliyoficha mchangani kwa ukimya wa kuzungumzia suala la Dowans,na ametujulisha bayana kuwa kamwe hawezi kukata mkono unaomlisha.Hawezi kuamuru Dowans isilipwe ilhali yeye ni mhusika mkuu katika ujio wa Richmond iliyorithiwa na Dowans.


Nihitimishe kwa kutoa wito kwa Kikwete na washirika wake wa Dowans kuwa sasa tumechoshwa na drama hii.Wameshaamua kujilipa,wajilipe.Hakuna haja ya kuendeleza mchezo huu mchafu wa kuigiza.In fact,hakukuwa na haja kwa CCM kutoa tamko la kuridhia malipo hayo kwani walishaamua mapema kuwa watailipa Dowans.Kwanini wasiilipe wakati inawadai fadhila?Actually,kwanini wasijilipe wakati wao ndio wamiliki wa kampuni hiyo?Wanasaini mikataba fyongo kwa makusudi ili baadaye waivunjue kisha wajishtaki mahakamani na kudai fidia,na hatimaye wajilipe.Yaleyale ya kununua bima ya moto kisha mnunuzi wa bima hiyo anachoma moto alichokiwekea bima,na kuishia kulipwa mara 1000 ya gharama halisi bima husika.

Sio kama nimechoka kupiga kelele dhidi ya ufisadi bali katika ishu hii ya Dowans naona kama kelele zetu zinamaliza sauti bure.Kwenda Mahakama Kuu kuzuwia malipo kwa Dowans ni wazo zuri,only if we forget nani anayewateua majaji tunaowapelekea kesi hiyo.Mnadhani kasi ya Kikwete kuteaua majaji ni coincidence tu?Anaweza kuwa dhaifu katika kuitumikia Tanzania ipasavyo lakini yuko makini sana katika kuhakikisha maslahi yake binafsi na ya washkaji zake hayaathiriwi kwa namna yoyote ile.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.