Showing posts with label JAKAYA KIKWETE. Show all posts
Showing posts with label JAKAYA KIKWETE. Show all posts

24 Jul 2013


WAKATI taifa likiwa katika maombolezo ya vifo vya mashujaa wetu saba waliouawa huko Darfur, Sudan, wakitumikia kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani nchini humo, Jeshi letu la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lilifanya tukio linalostahili pongezi nyingi, japo huenda ni wananchi wachache tu wenye taarifa nalo.
Jumapili iliyopita jeshi hilo lilianza kutumia rasmi mtandao wa kijamii wa twitter likitumia ‘handle’ @jw_tz. Hatua hiyo ni ya kimaendeleo na inaonyesha kuwa jeshi letu limedhamiria kwenda na kukumbatia teknolojia ya kisasa ya mawasiliano.
Mtandao wa twitter na pengine mitandao ya jamii kwa ujumla, bado ni suala geni kwa Watanzania wengi. Na licha ya ugeni huo, ukweli kwamba umiliki na upatikanaji wa huduma ya kompyuta bado ni ‘anasa’ wanayomudu watu wachache unafanya matumizi ya twitter (na mitandao mingine ya kijamii) kutokuwa suala muhimu au maarufu kwa jamii yetu.
Hata hivyo, mitandao ya kijamii hivi sasa imekuwa sehemu muhimu ya mawasiliano; huku ikibadili kwa kiasi kikubwa upatikanaji na kupashana habari. Wakati kwa muda mrefu mawasiliano kati ya mtu na mtu yamekuwa yakitegemea aidha neno la mdomo (kwa maana ya watu kukutana au kwa njia ya barua) au magazeti na redio, na kwa kiasi fulani runinga, mitandao ya jamii na teknolojia ya mawasiliano kwa ujumla imetokea kuwa njia ya haraka ya mawasiliano katika jamii.
Ukitaka kupata mfano wa umuhimu wa teknolojia hiyo ya mawasiliano, ni jinsi ziara ya kihistoria ya Rais wa Marekani Barack Obama huko nyumbani Tanzania, hivi karibuni, ilivyoripotiwa in real time (kadri matukio yalivyokuwa yakitokea) badala ya kusubiri gazeti la kesho au ripoti za redioni au kwenye runinga.
Kadhalika, kwa kutumia mtandao wa twitter, wananchi wamekuwa wakiendesha kampeni mbalimbali, na ya hivi karibuni kabisa ni ile inayohamasisha kupinga kodi ya sim card ambapo inatumia hashtag #NoSIMcardTax.
Iwapo Serikali itasikiliza kilio cha wananchi na kusitisha au kufuta kodi hiyo, basi kampeni hiyo ya mtandaoni (hususan huko twitter) itastahili pongezi kubwa.
Pamoja na pongezi zangu kwa hatua hiyo ya JWTZ kujiunga na mtandao wa twitter, bado taasisi hiyo inakabiliwa na changamoto kubwa; hususan kutumia ipasavyo mtandao huo kama nafasi kwa jeshi hilo kuupasha umma habari stahili.
Kwa mfano, juzi Rais Jakaya Kikwete aliwaongoza Watanzania kutoa heshima zao za mwisho kwa miili ya wanajeshi wetu waliouawa Darfur, na katika mazingira mwafaka, tungetegemea akaunti ya twitter ya JWTZ ingetulea tukio hilo ‘live’ lakini haikuwa hivyo. Siwalaumu kwa vile pengine ni ugeni tu katika matumizi ya teknolojia hiyo.
Licha ya ujio huo wa JWTZ huko twitter, mtandao huo wa kijamii unatumiwa pia na baadhi ya viongozi wetu wa serikali na wanasiasa, japo idadi yao ni ndogo. Rais Kikwete ni miongoni mwa viongozi hao; huku akiweka historia ya kuwa mmoja wa marais wachache wa Afrika wanaotumia mitandao ya kijamii.
Miongoni mwa mawaziri wachache wanaotumia mtandao wa twitter ni Mheshimiwa Lazaro Nyalandu (@LazaroNyalandu), Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii. Uwepo wake katika mtandao huo umenisaidia kumfahamu katika namna ambayo pengine Watanzania wengi hawaifahamu.
Nyalandu amekuwa mfano bora wa jinsi inavyostahili na inavyowezekana kuweka maslahi ya nchi mbele ya maslahi ya kiitikadi. Lilipotokea tukio la milipuko ya mabomu jijini Arusha, Waziri Nyalandu alishiriki kikamilifu kuufahamisha umma kuhusu hatua mbalimbali zilizokuwa zikifanyika kuwasaidia majeruhi.
Na japo Nyalandu ni Mbunge wa CCM, kamwe hajawahi ku-tweet mambo ya kiitikadi, na badala yake tweets zake zimekuwa zikihusu masuala ya Tanzania na Watanzania, badala ya masuala ya CCM.
Kingine kinachopendeza kuhusu Naibu Waziri huyo ni usikivu kwa hoja mbalimbali zinazowasilishwa kwake kupitia mtandao huo. Kama ilivyo kwa Naibu Waziri mwingine, Januari Makamba (@JMakamba), Nyalandu huwasiliana na wananchi waliopo twitter kwa heshima na unyenyekevu mkubwa, kiasi yaweza kuwa vigumu kudhani ni mtu mwenye dhamana kubwa serikalini.
Ni kwa sababu hiyo, kupitia mtandao wa twitter Jumapili iliyopita nilimtumia ombi Waziri Nyalandu kumsihi awasilishe kilio cha msanii Johnson Nguza (Papii Kocha) ambaye, pamoja na baba yake Nguza Viking na kaka zake wawili, wanatumikia kifungo kirefu jela kwa kosa la kubaka.
Mwishoni wa wiki, blog mbalimbali zilichapisha barua iliyoandikwa na msanii huyo (Papii Kocha) kwenda kwa Rais Kikwete akiomba msamaha kwa yeye na familia yake, na kumwomba Rais awatoe gerezani.
Nina sababu mbili za msingi za kuguswa na suala la ‘Babu Seya’ na wanae ambao wamekuwa gerezani kwa takriban miaka 10 sasa. Kwanza, japo kuna msemo maarufu kwenye kila jela kuwa ‘kila mfungwa hana hatia’ (yaani amefungwa kwa kuonewa), tangu Nguza na wanae walipokamatwa na hatimaye kufungwa nimebaki na hisia kuwa sheria ilipindishwa dhidi yao.
Mengi yameshasemwa huko mitaani kwamba kesi hiyo ilisababishwa na visasi binafsi dhidi ya msanii huyo na wanae. Ikumbukwe kuwa katika nchi zetu masikini kuna ‘haki za aina mbili,’ kwa wanyonge ambao wanaweza kwenda jela kwa kusingiziwa tu, na kwa vigogo ambao ni kama wana kinga ya kudumu ya kisheria.
Sababu ya pili ya kumwomba Waziri Nyalandu amfikishie Rais Kikwete ujumbe wa Papii Kocha ni ya kibinadamu zaidi. Tuweke kando hisia kuwa kifungo cha Nguza na wanae ni sheria kufuata mkondo au kupindishwa.
Kama binadamu, na hasa katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan, unajiskiaje ukisoma barua ya kutoa majonzi kutoka kwa kijana mfungwa anayezeekea jela akiomba msamaha kuhusu hukumu ambayo tangu mwanzo wafungwa hao wamekuwa wakidai ni ya uonevu tu dhidi yao?
Ndio, huko jela ‘kila mfungwa hana hatia’ (yaani wafungwa wengi hudai wamefungwa kwa kuonewa hata kama walikamatwa red-handed wakifanya makosa).Lakini katika mazingira ya kawaida, ni wafungwa wangapi waliopo jela kwa takriban miaka 10 na wanaendelea kusisitiza kuwa walifungwa kwa uonevu na wanaomba hukumu dhidi yao ziangaliwe upya au wasamehewe?
Laiti ukisoma barua hiyo ya Papii Kocha (na amekuwa akiandika barua kama hiyo mara kadhaa) usipolengwa na machozi basi utakuwa na ‘moyo mgumu’ kweli.
Lakini hata tukiweka kando huruma ambayo baadhi yetu tunayo kwa Nguza na wanae, katika ubinadamu tu, msanii huyo na wanae wameshatumikia adhabu ndefu (bila kujali walitenda kosa au la), na adhabu waliyokwishapata inatosha kutoa fundisho kwao na kwa jamii kwa ujumla. Hivi sisi kama jamii tutaathirika vipi iwapo Nguza na wanawe wakisamehewa?
Kama nilivyotarajia, ‘mtu wa watu’ Naibu Waziri Nyalandu alinijibu juzi akisema kwa tweet (namnukuu) “copy that...” akimaanisha amesikia ombi langu na atalifanyia kazi.
Licha ya imani yangu kwa Nyalandu, nina imani pia kuwa Rais Kikwete atasikiliza ujumbe huo kutoka kwa mteuliwa wake. Vilevile ukweli kuwa huu ni Mwezi Mtukufu, na nina hakika Rais amefunga pia, roho ya huruma itamsukuma kusikiliza kilio cha mara kwa mara kutoka kwa Papii Kocha, kaka zake na baba yao.
Mwisho, ninaomba kila Mtanzania mwenye kuamini katika kuwasamehe waliotukosea (ikiwa ni pamoja na wanaotajwa kuwa wahanga wa makosa yaliyofanywa na ‘Babu Seya na wanawe) atajumuika nami kuwaombea msamaha wasanii hao.
Maandiko Matakatifu katika Surat Al I’mran 155 ya Kurani Tukufu na Marko 11:25 ya Biblia Takatifu ni baadhi za aya lukuki zinazotusisitiza kuhusu msamaha.



20 Jul 2013







Na katika video hii, Lipumba anakiri kuwa alimsaidia JK katika kampenzi za uchaguzi mkuu uliopita...kwa kigezo cha dini

18 Jul 2013

BLANTYRE (MaraPost)—Tanzania has maintained that it still owns half of Lake Malawi, reiterating that the border between the two countries runs in the middle of the disputed lake.

Tanzania’s foreign affairs and international cooperation, Mkumbwa Ally on Tuesday told that country’s Daily News Dodoma will not change its position on the matter.

“We didn’t expect anything new or different; neither are we going to change our position. Our position is that the border runs in the middle of Lake Nyasa [Malawi].

“The mediation team is gathering information, then they will give their statement, then each side will decide to take it further if they do not agree with the mediation team’s judgment,” Ally is quoted as saying.

The African Forum for Former Heads of State delegation are scheduled to leave for Tanzania next week on a fact-finding mission regarding the wrangle over sovereignty of Lake Malawi.

Former Mozambican President Joachim Chissano and Thabo Mbeki of South Africa on Sunday met President Joyce Banda and her entourage at Kamuzu Palace in Lilongwe on the same mission.

The Malawi leader told the two mediation team being led by Chissano to reach an agreement on the matter by this September or else the matter should go to the International Court of Justice (ICJ).

She said the longer the matter is taking to be resolved, the more strains are rising, mostly along the lake shores bordered with Tanzania.

President Banda also said her government will not bow down to “entertain any interim agreement” on usage of the waters of the lake with Tanzania “until the sovereignty issue is amicably resolved” through the Sadc forum.
Banda notified Chissano and Mbeki that Malawi owns the entire lake except for a portion ceded to Mozambique in 1954 for mutually beneficial reasons.

Malawi, which sits to the west of Africa’s third-largest lake, claims the entire northern half of the lake while Tanzania, to the east, says it owns half of the northern area. The southern half is shared between Malawi and Mozambique.-MARAPOST.
CHANZO: The Maravi Post
This content was copied from www.maravipost.com


Salem-News.com (Jul-16-2013 16:02)

The FDLR Speaks Out

There is much speculation and rumors about this group of rebels and what their purpose is

(WASHINGTON DC) - The Eastern part of the Democratic Republic of Congo is a hot bed for armed rebel groups engaged in a geostrategic power struggle for the control of minerals and territory. One such group is the FDLR which is a rebel group from Rwanda that fled after the 1994 genocide made up of primarily Hutu refugees.

This group is considered an enemy to Rwandans and the current ruling party in Rwanda seeks to exterminate this group. A few international actors have called for the Government of Rwanda to negotiate with this enemy group in order to bring about peace and stability in the region but President Kagame of Rwanda has stated that he will not bow to this pressure.

There is much speculation and rumors about this group of rebels and what their purpose is. Some have returned to Rwanda to seek forgiveness and be repatriated back into society. President Kagame has granted this on occasion for former FDLR members and even included some of the members into government positions.

This reporter was able to reach a representative for the FDLR in Europe who was willing to answer a few questions:

JF: What is the goal of the FDLR? You have lived in exile for nearly twenty years.
FDLR: To liberate Rwanda from RPF Dictatorship, restore democracy and promote reconciliation.
JF: Is it true that the FDLR is working with FARDC and the UN forces in Eastern DRC as reported by the Government of Rwanda?
FDLR: No, FARDC has Tanzanian and the entire SADC under UN forces behind them. They don’t need FDLR.
JF: Why is Rwanda accusing the FLDR of collaborating with FARDC and the UN forces and have even sent a letter to the UN regarding this matter?
FDLR: they lost an "Element of surprise" on assault on Goma. Last time they walked in. This time they met a different FARDC. They know FDLR as tactically proficient soldiers, so they can’t believe FARDC could pull something like that.

The speculation that continues about the FLDR was also reported in a publication that reviewed the UN GoE leaked report that the FDLR is splintering apart. The report by Afroamerica.net stated that.
According to the UN Experts’s leaked report, “the FDLR suffers from internal divisions and a weak hierarchy that lacks the capability to command and control the organization’s entire operations. The movement’s leadership is divided between hardliners such as Mudacumura who want to continue the armed struggle, and moderates belonging to younger generations.”

On July 16, 2013 the FLDR released a press statement reporting that this information is not accurate and that they continue to be a strong and viable force in Eastern DRC. They stated in part that: “In response to the article on the site afroamerica.net dated July 5, 2013, the Democratic Liberation of Rwanda, FDLR forces acronym, would like to inform the public, the international community in general and the Rwandan community in the diaspora and inside Rwanda in particular the FDLR still exist, and they are stronger now, more than they have ever been before.

The FDLR is organized in several divisions, within some of which are inside Rwanda, and two others one based in South Kivu and the other in North Kivu. Each one of these divisions has its own well trained operational staff, and these divisions are combined under one joint command led by General MUSENYERI Achilles.

The FDLRs are fine and well-structured from high to lowest level, and their armed wing, the Force Combattantes Abacunguzi (FOCA) has a strong insightful command, led by the commander of the FOCA. The command is determined more than ever, to force the dictatorial power of the RPF Inkotanyi led by General Paul Kagame and his click to accept the democratic system in the country, and the freedom of the Rwandan people, in all its diversity, to express themselves freely, and choose their own leaders.”

The FDLR addressed talks with Kagame in this press statement by stating:

“The FDLR has firmly supported the proposal of the head of the Tanzanian government and the Minister of Foreign Affairs of Belgium to encourage the dictatorial government of General Paul Kagame to accept negotiations with them to find a lasting peace in our country and consequently in the whole Great Lakes region OF Africa. One has to notice that these Belgian and Tanzanian officials have not made this suggestion if they were not convinced that our organization is real, fine and strong.

In conclusion, the FDLR urge all forces of the Rwandan opposition whatsoever from inside the country or outside Rwanda to stand, walk and act as one in order to reach a brighter output.

The combination of efforts is appropriate to fight against the common evil that is the dictatorial system of the RPF and its President.”

The fight in the Great Lakes region of Africa rages on and each rebel group has made statements that they are stronger than ever. Time will tell which groups survive and which groups change names and re-form into other groups. The FDLR has been a constant in the region for nineteen years and desires to return home. They have stated that they are willing to negotiate with President Kagame but Kagame made it clear that he is not willing to engage in talks with them.
____

17 Jul 2013





NIANZE kwa kutoa salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa askari wetu saba mashujaa waliouawa huko Darfur, Sudan wakiwa sehemu ya jeshi la kimataifa la kulinda amani nchini humo. Damu ya askari hao haijapotea bure kwani kilichowapeleka huko ni kusaka amani, na kama tujuavyo sote, kila dini inasisitiza amani. Kwa hiyo ni matarajio yetu kuwa Mwenyezi Mungu atazimpumzisha roho zao kwa amani.
Pili, niwatakie mfungo mwema wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan wasomaji wote wa gazeti hili la Raia Mwema. Kila Ramadhan ni ushahidi mzuri kuwa Watanzania tuna umoja na udugu, licha ya tofauti zetu za kiimani, kwani wengi tusio Waislam tunawaunga mkono ndugu hao.
Na tatu, ningependa kukipongeza Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa ushindi wao katika uchaguzi wa madiwani katika kata zote nne huko Arusha.
Itakumbukwa uchaguzi huo uliahirishwa baada ya kutokea shambulio la bomu katika mkutano wa kuhitimisha kampeni za CHADEMA kuwania viti hivyo vya udiwani.
Lakini hata kabla ya kutokea janga hilo la kusikitisha, uchaguzi huo ulivuta hisia za Watanzania wengi hasa kutokana na ushindani mkubwa uliojitokeza kati ya CHADEMA na CCM.
Kama kuna kubwa tulilojifunza katika uchaguzi huo ni ukweli kwamba matumizi ya fedha, ubabe, vitisho na hadaa yanaweza kushindwa kuwarubuni wapiga kura wanaolewa wanataka nini. Japo uchaguzi huo ulikuwa wa ngazi ya kata tu, lakini matokeo yake yanaweza kuwa na maana kubwa zaidi, kwa CHADEMA na CCM, kwani kuna uwezekano, hata kama ni mdogo, wa matokeo hayo kujiakisi kwenye chaguzi nyingine, na pengine hata uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Lakini kati ya picha mbaya zilizojitokeza katika uchaguzi huo ni namna chuki inavyokua kati ya CCM na CHADEMA. Japo hadi muda huu hakuna maendeleo ya maana katika uchunguzi wa chanzo cha bomu la Arusha katika mkutano wa CHADEMA, yayumkinika kuhisi chuki hizo za kisiasa zinaweza kuwa miongoni mwa sababu kuu za tukio hilo la kinyama.
Na kwa kuthibitisha chuki hiyo, vifo vya Watanzania wanne vilivyotokana na shambulio hilo vilionekana kama ‘vimetokea nchi nyingine,’ tulishuhudia Bunge likishindwa angalau kuahirisha kikao cha bajeti japo kwa saa chache tu kuwakumbuka marehemu na majeruhi.
Kadhalika, tukio hilo liligeuzwa turufu muhimu kwa baadhi ya wanasiasa ‘hamnazo’ wa CCM ambao walidai CHADEMA wanahusika kwa minajili ya kusaka huruma ya wapigakura.
Kibaya zaidi, hata Rais Jakaya Kikwete naye hakuona haja ya kwenda Arusha kuhani misiba ya waliouawa kinyama na hadi leo hajaona umuhimu huo.
Kana kwamba haitoshi, majuzi ubalozi wa Marekani huko nyumbani umeliumbua Jeshi la Polisi kwa kubainisha kuwa wapelelezi wa Shirika la Upepelezi la nchi hiyo FBI hawapo Arusha kupeleleza tukio hilo, tofauti na taarifa za awali za jeshi hilo. Sijui polisi wetu walikuwa wanataka kumhadaa nani.
Kimsingi, ushindi wa CHADEMA katika uchaguzi huo wa ngazi ya kata una umuhimu mkubwa kwa chama hicho kwa sababu wafuasi wake wamekuwa wakipewa wakati mgumu na CCM pamoja na vyombo vya dola. Hali hiyo imekuwa ikijitokeza takriban katika kila chaguzi.
Pasi aibu, Jeshi la Polisi limekuwa likiwanyanyasa CHADEMA kana kwamba jeshi hilo ni sehemu ya kikundi cha ulinzi cha CCM kinachofahamika kama Green Guard.
Na ni suala hilo la Green Guard ambalo ndio dhima ya makala hii. Majuzi, Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alieleza dhamira ya chama chake kuanzisha kikosi cha ulinzi, Red Brigade, kwa ajili ya ulinzi wa mikutano ya chama hicho.
Kauli hiyo ya Mbowe imezua mzozo mkubwa huku Rais Kikwete akikemea hadharani, Jeshi la Polisi likiapa kupambana na dhamira hiyo ya CHADEMA, na muda mfupi kabla ya kuandaa makala hii, Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, amenukuliwa akidai ataifuta CHADEMA iwapo wataanzisha kikosi cha ulinzi.
Kati ya ‘upinzani’ wote huo dhidi ya Red Brigade, ulionigusa ni ule wa Rais Kikwete. Binafsi, hainiingii akilini kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM hafahamu chama chake kina kikundi cha ulinzi kama hicho wanachotaka kuanzisha CHADEMA. Kikwete hafahamu kikosi hicho, kinaitwa GREEN GUARD.
Nisiume maneno, kama Rais Kikwete, ambaye pia Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, hafahamu chama chake kina kikosi cha ulinzi kiitwacho Green Guard basi yayumkinika kusema haistahili kuendelea kuwa kiongozi wa juu wa chama hicho.
Bila kujali suala la vyama vya siasa kuwa na vikosi vya ulinzi ni sahihi au la, ukweli kwamba kwa muda mrefu tu CCM imekuwa na Green Guard, CUF nayo imekuwa na Blue Guard, na si Kikwete, Jeshi la Polisi wala Tendwa, waliokemea suala hilo, lakini ghafla CHADEMA kutangaza ina nia ya kufuata ‘mkumbo’ huo inakuwa nongwa, basi nchi yetu imekosa mwelekeo.
Huu sio upendeleo au uonevu bali ni ubabaishaji. Ukisikiliza kwa msingi hoja za CHADEMA kuhusu dhamira yao ya kuwa na kikosi chao cha ulinzi kama wenzao wa CCM na CUF, utaafikiana nao mara moja. Sio siri Jeshi la Polisi sio tu limeshindwa kukipatia chama hicho ulinzi unaostahili bali pia limekuwa mstari wa mbele kuwapiga, kuwanyanyasa na hata kushindwa kuzuia vifo vya wana-CHADEMA.
Ifahamike kuwa Katiba ya nchi inatoa ruhusa kwa raia kupatiwa ulinzi na kujilinda inapobidi. Sasa kama polisi sio tu hawataki kuwalinda CHADEMA bali pia wanashiriki kuwanyanyasa, chama hicho kifanye nini?
Niliwahi kuandika mfululizo wa makala huko nyuma kuhusu kampeni ya chuki inayoongozwa na baadhi ya viongozi waandamizi wa CCM (nikawataja Steven Wassira, Mwigulu Nchemba, Nape Nnauye, Spika Anne Makinda na Naibu wake Job Ndugai). Katika makala hizo nilibainisha angalau Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Kikwete amekuwa akiepuka kauli za chuki dhidi ya wapinzani, hususan CHADEMA.
Lakini kwa kushindwa kwenda kuwapa pole waathirika wa shambulio la bomu katika mkutano wa CHADEMA Arusha, na kauli yake ya majuzi kuituhumu CHADEMA kuhusu wazo la chama hicho kuanzisha Red Brigade, ilhali CCM anayoongoza Kikwete nayo ina Green Guard, naanza kushawishika pengine akina Wassira, Nape, Mwigulu na wengineo wanaomwaga sumu ya chuki dhidi ya CHADEMA wana idhini ya Mwenyekiti wao.
Nihitimishe makala hii kwa kumsihi Rais Kikwete atafakari upya mwenendo wa chama chake katika siasa hizi za chuki dhidi ya CHADEMA. Badala ya kukimbilia kudhibiti matokeo, ni vema kuchunguza chanzo cha ‘tatizo’ (yaani kwa nini CHADEMA ‘inaisumbua’ CCM).
Badala ya kudhani kuwa uungwaji mkono wanaopata CHADEMA ni matokeo ya chama hicho ‘kuhamasisha vurugu’ au ‘kufanya nchi isitawalike,’ ni rahisi tu kwa Kikwete na CCM kubaini kwamba turufu kubwa ya CHADEMA ni utambuzi wa matatizo yanayomkabili Mtanzania hivi sasa, na kushauri njia mwafaka za kuyatatua. Na matatizo makubwa zaidi ni ufisadi na umasikini, licha ya utajiri mkubwa wa rasilimali katika nchi yetu.
Mfano mwepesi, mwananchi wa kawaida tu hahitaji uelewa wa juu wa utendaji kazi wa vyombo vya dola kutambua kuwa haiwezekani kilo 150 (zaidi ya gunia la lumbesa) za dawa za kulevya ziweze kupita kwenye mipaka yetu na kukamatwa Afrika Kusini kama hakukuwa na msaada wa vigogo fulani. Na kama kawaida, si Waziri, Naibu wake, IGP au kiongozi yeyote yule mwenye dhamana aliyechukuliwa hatua kuhusiana na skandali hiyo inayochafua sifa ya Tanzania kimataifa. Je, kuzubaa huko kuwajibishana katika tukio kama hilo si hatua muhimu ya kuwapa CHADEMA pointi a bure?
Niihadharishe CCM kuwa chuki na hujuma zake dhidi ya CHADEMA zinarahisishia safari ya chama hicho kuingia Ikulu mwaka 2015. Hivi sasa, CHADEMA inavuna wafuasi wengi sio tu kwa sababu wanakihurumia chama hicho kwa jinsi kinavyonyanyaswa kila kukicha, lakini pia wanakerwa kuona ajenda pekee ya CCM sasa hivi ni kuidhibiti na pengine ‘kuichinja’ CHADEMA. Huu ni mithili ya mpambano kati ya babu mtu mzima mwenye ‘miguvu’ tele (CCM) dhidi ya mjukuu wake ‘dhaifu’ (CHADEMA). Sote tunajua uungwaji mkono wa wapenda haki utaelekezwa upande gani.



9 Jul 2013


Nimeshalaumiwa mara kadhaa kuwa nina chuki binafsi na Rais Jakaya Kikwete kutokana na maandiko yangu yanayomkosoa mara kwa mara. Hata hivyo, ukweli ni kwamba sio tu kuwa namheshimu Kikwete kama Rais wangu lakini pia nina mapendo ya dhati kwa nchi yangu ya asili, yaani Tanzania. 

Ni kwa sababu hiyo ndio maana nimeshtushwa sana na kauli za kibabe- au za KIHUNI, kwa lugha mwafaka-za Rais wa Rwanda, Paul Kagame, dhidi ya  Rais wetu Kikwete na nchi yetu kwa ujumla. So far, Rais Kikwete ameepuka malumbano na Kagame, lakini inaelekea Mnyarwanda huyo anadhani ukimya wa Kikwete ni uoga kwake, au labda anatafsiri kuwa anadharauliwa.

Ni jukumu la kila Mtanzania kusimama kidete na Rais wetu katika suala hili kwani sio tu ni dhihaka dhidi yake bali taifa letu kwa ujumla. Tuweke kando tofauti zetu na tuwe kitu kimoja.Ifike mahala tumwambie Kagame na Rwanda kuwa IMETOSHA, ENOUGH IS ENOUGH. 

Soma habari husika hapa chini:

I will Just Wait For You At the Right Place And I will Hit You, Rwandan General Paul Kagame Threatens Tanzanian Jakaya Kikwete

by AFROAMERICA NETWORK on JULY 3, 2013


President Jakaya Kikwete and  General Paul Kagame: Good  old days
President Jakaya Kikwete and General Paul Kagame: Good old days
“Those people [Tanzanian President Jakaya Kikwete] you just heard siding with Interahamwe and FDLR  and urging negotiations… negotiations?  Me, I do not even discuss this topic, because I will just wait for you [Tanzanian President Jakaya Kikwete] at the right place and I will hit you! He[Tanzanian President Jakaya Kikwete]  did not deserve my answer. I did not waste my time answering him…It is well known. There is a line you cannot cross, there is a line, a line that you should never cross. It is impossible…”
It is in these ominous terms that the Rwandan dictator General Paul Kagame threatened to get even with Tanzanian President Jakaya Kikwete, while addressing Rwandan Youth on June 30, 2013 during a summit called “Youth Konnect”“, sponsored by his wife, Janet Kagame.

Relations between Tanzanian President Jakaya Kikwete and Rwandan leaders have soured in the last weeks. On several occasions Rwandan leaders called the Tanzanian President “a genocide and terrorist sympathizer”, “ignorant”, “arrogant”, and “mediocre leader”. The relations have deteriorated following the recommendation by President Jakaya Kikwete of open negotiations between Rwandan, Ugandan and Congolese leaders and their respective armed opposition in order to bring durable peace and security  in the African Great Lakes region.
Then, General Paul Kagame, while addressing a closed door meeting with his close aides, called the Tanzanian President “4Bs”, which in Rwandan language means “an opportunist, attention seeker, arrogant and contemptible person.”
The latest public threats by  General Paul Kagame against the physical person of the Tanzanian President are arguably the most serious sign of how worse the relations among the two countries and the their leaders have become. According to sources in Kigali, General Kagame has also been frustrated by the attention Tanzanian President has been receiving from World powers. Until a few years ago, Rwanda and its dictator was the darling of the West. The attention from the West has since dwindled.
The upcoming days and months promise to be full of anticipation and sursprises in the Great Lakes Region of Africa.

26 May 2013


MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameibua suala zito akikihusisha chama chake na “kumnusuru” Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu uliopita.

Tanzania Daima limefahamishwa kuwa Profesa Lipumba alitoboa siri hiyo katika Msikiti wa Idrissa, Kariakoo, jijini Dar es Salaam, alikokwenda kuswali swala ya Ijumaa, miezi kadhaa iliyopita.

Kwa mujibu wa video ya tukio hilo, ambayo gazeti hili lina nakala yake, Profesa Lipumba alikaribishwa kuzungumza na waumini hao mara baada ya utangulizi uliotolewa na Imamu wa msikiti huo, Sheikh Ali Basaleh, aliyemtaka awaeleze Waislamu hali ya kisiasa nchini kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Huku akisisitiza juu ya umuhimu wa mshikamano wa kiimani, Profesa Lipumba alianza kwa kuzungumzia matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2010, na ushindani mkali wa kisiasa uliokuwapo.

Alisema hawaoni matunda ya jitihada walizofanya kumnusuru Rais Kikwete asishindwe, kwani hata chini ya uongozi wake, Waislamu wameendelea kutothaminiwa.

“Ninyi masheikh mnajua vizuri zaidi hali ya kisiasa ilivyokuwa, kwamba ilibidi zifanyike juhudi za makusudi ili kuokoa jahazi. Lakini pamoja na kuliokoa jahazi, hali halisi inaonyesha mpaka sasa hakuna matunda yoyote yaliyopatikana, na tupo katika mtihani mgumu zaidi,” alisema.

Katika hali ambayo inasemekana ushindi wa Rais Kikwete ulipatikana kwa mbinu, huku wengine wakiituhumu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa ilimnusuru mgombea wa CCM, kauli hii ya Profesa Lipumba inadokeza kwamba anajua mkakati zaidi wa kazi ya Tume ya Uchaguzi.

Katika hali isiyo ya kawaida, Profesa Lipumba anaonekana kuhamasisha Waislamu kujipanga akisema “wenzetu wameanza kujipanga” kuelekea 2015.

“Kwahiyo kama Waislamu tunataka kupata haki zetu, kama tunataka kuishi kama raia wa daraja la kwanza katika nchi yetu, lazima tujipange kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015; na sisi tuanze kujipanga kwa sababu wenzetu wameanza kujipanga, vinginevyo tutaendelea kubaki maskini na raia wa daraja la nne katika nchi yetu wenyewe.

“Mwaka 2010 wakati mshindi wa uchaguzi wa rais alipotangazwa, mimi nilikwenda kwenye hafla ya kutangazwa matokeo, na nilikwenda makusudi tu, siyo kwamba uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, ila nilikwenda makusudi kwa kujua hali ya kisiasa ilivyokuwa wakati huo.

“Huku nilikutana na Sheikh Basaleh. Nilipokutana naye, alinipongeza; sijui kama yeye anakumbuka, akaniambia ‘umeweka mbele imani yako na umekuwa mwelewa wa mambo.’”

Hata hivyo, licha ya Profesa Lipumba kuwaambia Waislamu wajipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu, hakusema wajipange kupitia chama kipi.

Lakini alisisitiza kwamba uchaguzi ujao ni zaidi ya siasa au rais yupi anafaa, bali maslahi, hasa ya rasilimali nyeti zinazopatikana katika ukanda wa Pwani ya Mashariki, eneo ambalo alisema linakaliwa zaidi na watu wenye imani ya Kiislamu.

Katika moja ya kauli zake, Profesa Lipumba alisema kwamba kuna chama kimoja kinataka kuchukua madaraka ya nchi, lakini kinasaidiwa na mataifa ya magharibi, yasiyoenzi wala kuthamini imani ya Kiislamu.

Kwa muda sasa, zimekuwapo tetesi kwamba CCM imekuwa inafanya siasa za udini dhidi ya vyama vya upinzani, hasa inapoona maslahi yake yapo hatarini.

Mwaka 2010 makada kadhaa wa CCM walitumia mitandao ya simu kuchonga (spoofing) ujumbe wa simu ulioshambulia mgombea mmoja wa upinzani, ukimhusisha na imani yake.

Kauli ya Lipumba imethibitisha pia minong’ono iliyokuwapo muda mrefu kuwa baadhi ya kura za Profesa Lipumba zilipotelea kwa Rais Kikwete.

Katika uchaguzi huo, Lipumba alitangazwa kushika namba ya tatu, nyuma ya Rais Kikwete na Dk. Willibrod Slaa wa CHADEMA.

Alipoulizwa kuhusu ziara yake msikitini na kauli aliyotoa, Profesa Lipumba alikiri kwamba alikwenda kuzungumzia hali ya kisiasa nchini. Hata hivyo alisema inawezekana video hiyo imechakachuliwa kwa kuungaunga vipande vya matamshi wanavyovitaka badala ya hotuba nzima.

Hata hivyo, video iliyotazamwa na waandishi wa habari hii, ambayo nakala yake imetunzwa na gazeti hili, haionekani kukatwakatwa.

Katika tukio hilo, Sheikh Baseleh ndiye anayeanza kuzungumza huku akisoma kipande cha gazeti lililomnukuu Waziri wa Uwezeshaji na Uwekezaji, Dk. Mary Nagu, akizungumzia mchakato wa katiba, kwamba Tume ya Katiba “haitazingatia maoni ya wachache”, na kwamba mambo ya dini yasiingizwe kwenye katiba.

Katika ufafanuzi wake, Sheikh Basaleh anasema Dk. Nagu alizungumza mambo haya mbele ya waumini wa Kanisa la Chang’ombe kwenye uzinduzi wa kwaya; na kwamba miongoni mwa mambo ambayo yanaitwa ya kidini yasiyotakiwa kuingizwa kwenye katiba ni Mahakama ya Kadhi Mkuu.

Baadaye anamkaribisha Profesa Lipumba, ambaye naye katika hotuba yake, pamoja na mambo mengine, anakosoa msimamo wa serikali kutaka Waislamu waanzishe mahakama yao ya kadhi, akisema mahakama ni chombo cha dola ambacho hakipaswi kuwa nje ya mfumo wa serikali.

Mara baada ya Profesa Lipumba kuhitimisha hotuba yake, Sheikh Basaleh alimkaribisha Sheikh Musa Kundecha, ambaye naye alisisitiza kauli ya Profesa Lipumba kuwataka Waislamu wajipange kwa ajili ya 2015.

Vile vile alifafanua kuwa “wachache” waliozungumzwa na Dk. Nagu ni Waislamu, kwani zilishatoka taarifa katika kituo cha TBC kuwa idadi ya wasiokuwa Waislamu nchini ni asilimia 52.

“Mimi sijaiona hiyo video ila nimeisikia tu kuwa ipo inauzwa mitaani na makanisani, lakini inawezekana waliorekodi wamenichakachua maana imekuwa siku nyingi kidogo tangu niende kuongea pale Msikiti wa Idrissa. Yamewezekana wameungaunga vipande wanavyovitaka ili kunipaka matope mimi na CUF kuwa tuna udini,” alifafanua Profesa Lipumba.

Alipotakiwa akutane na waandishi wa habari hii ili waiangalie kwa pamoja video hiyo ili kujua ukweli kama ni video halisi au ya kuchakachua, Profesa Lipumba alisema waandishi waende kumwona Naibu Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano ya Umma, Abdul Kambaya.

Alipopigiwa simu, Kambaya hakutoa ushirikiano kwa waandishi. Badala yake aliwashambulia kuwa wana ajenda ya siri dhidi ya CUF, akisema wanafuatilia na kuona makosa ya viongozi wa CUF tu na kufumbia macho vitendo vya wanasiasa wengine wanapokwenda makanisani.

“Nyie waandishi wa Tanzania mmezidi, yaani ninyi mnaona matendo ya viongozi wa CUF tu, wengine wakienda makanisani mbona hawafuatiliwi? Mbona hamumfuatilii Lowassa akienda makanisani? Au mbona hamsemi Dk. Slaa akienda kanisani? Sasa Profesa akienda msikitini kuongea na Waislamu wenzake kuna kosa gani? Sasa ninyi andikeni chochote,” alifoka na kukata simu.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Tanzania Bara, Julius Mtatiro alipotakiwa kuzungumzia video hiyo, alikataa katakata na kuwashauri waandishi wawasiliane na ama Profesa Lipumba mwenyewe au Kambaya.

Itakumbukwa kuwa kumekuwepo tuhuma dhidi ya Rais Kikwete na CCM kuwa mwaka 2010 waliendesha propaganda chafu za udini zenye lengo la kuwagawa Watanzania hususan Wakristo na Waislamu kwa manufaa yao ya kisiasa.

Mwelekeo huo wa kisiasa wa Rais Kikwete na CCM unadaiwa kutokana na hatua ya viongozi wa Kanisa Katoliki nchini kupitia Idara ya Uchungaji kutoa waraka maalumu uliowataka Watanzania kuchagua viongozi waadilifu.

Waraka huo haukuifurahisha CCM, ambayo imekuwa inagubikwa na tuhuma nyingi za ufisadi. Makada na viongozi wa CCM walijaribu kuupinga kwa kuupotosha, wakisema unaingiza mambo ya dini katika siasa.

Kanisa Katoliki lina utaratibu wa muda mrefu wa kutoka nyaraka kuelekeza waamini na wananchi juu ya mambo ya msingi katika jamii.

Katika hali hiyo, Rais Kikwete na CCM wanadaiwa kukimbilia kwa viongozi wa Kiislamu na kuwaomba wawaunge mkono kwa kuwajaza maneno ya uongo, kwamba Wakatoliki walikuwa wamewaagiza waumini wao kupigia kura wagombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Inadaiwa waliwafitinisha zaidi kwa kuwaeleza kuwa aliyekuwa mgombea kiti cha rais wa CHADEMA katika uchaguzi huo, Dk. Willibrod Slaa ambaye ameshawahi kuwa Padri, alikuwa ametumwa na Kanisa Katoliki ili kuendeleza utawala wa Kikristo nchini.

Propaganda hizo hazikuishia kwa viongozi na waumini wa Kiislamu tu, bali zilielekezwa pia kwa viongozi na wafuasi wa CUF ambao walirubuniwa na kushawishiwa kumpigia kura “Muislamu mwenzao” Rais Kikwete, huku wakiahidiwa kuwa mwaka 2015 Waislamu wa CCM nao watampigia kura mgombea wa CUF kwa hoja kuwa CCM watakuwa wamesimamisha mgombea Mkristo.

Licha ya madai hayo ya udini kuwa wazi kwa muda mrefu, lakini wakati wote Rais Kikwete na CCM wamekuwa wakikanusha tuhuma hizo na kuziita kuwa uongo na uzushi.


CHANZO: Tanzania Daima

8 May 2013

















Watakaosema Rasi Jakaya Kikwete ni miongoni mwa vyanzo vya matatizo ya udini yanayotusumbua sasa wanaweza kuwa sahihi. Mtandao ulioasisiwa mwaka 1995 kwa minajili ya kumwingiza Kikwete Ikulu na kufanya kazi kwa nguvu hadi mwaka 2005 ulichangia sana kuleta siasa za mifarakano. Nani aasiyejua jinsi Mtandao wa Kikwete ulivyofanikiwa kumchafua Dkt Salim Ahmed Salim hadi akaonekana kana kwamba ni adui wa Watanzani hususan huko Zanzibar?

Mwaka 2010 wakati Kikwete anawania kurejea Ikulu kwa mara nyingine, tulishuhudia kila aina ya uhuni ambapo vitu muhima kama dini vilitummika kwa minajili ya kisiasa, kubwa likiwa kumzuwia Dkt Willbrod Slaa asiingie Ikulu. CCM iliruhusu kuhususha kazi ya zamani ya Dkt Slaa, yaani upadre, ni uthibitisho tosha kuwa Cahdema ni chama cha Kikatoliki. Kikwete aliyafahamu hayo lakini akakaa kimya, kwani alijua yangemsaidia kumwingiza tena Ikulu.

Lakini tuweke lawama pembeni kidogo. Tatizo kubwa la Kikwete ni uzembe wa kuruhusu kuzungukwa na maharamia hatari kabisa kwa Tanzania yetu.Uzembe hauna excuse. Lakini kuna nyakati unaweza kuona picha halisi ya Kikwete pasi maharamia hao.Hebu msomaji angalia picha hizo hapo juu kwa makini.Yah, kuna wanaosema Kikwete ni msanii mzuri-yaani mtu anayejua kutumia fursa vizuri kufikisha ujumbe anaotaka yeye.

Honestly, katika picha hizo hapo juu ninamwona Mtanzania mwenzetu ambaye ana uchungu na ameguswa na yaliyowakumba hao aliokwenda kuwatembelea. The pictures are so genuine to an extent unaweza kujiuliza is this the same JK tunayemlaumu kila siku?

I know, kuna watakaohisi sifa hizi ninazompa JK ni kwa vile yupo na Wakristo. No.Mie ninaangalia utu wa huyu kiongozi wetu kama unavyojionyesha kwenye picha hizo.Wanasema picha zinaweza kuwakilisha maneno 1000.Mie nasema picha hizo hapo juu zimewakilisha maneno mengi sana...japo pia zinaweza kuzua maswali kwamba kama Kikwete ni mtu wa kujali kiasi hikli kwanini basi anaruhusu hao maharamia wanaomzunguka waipeleke nchi yetu kwenye korongo nene?




27 Jan 2013












Na wakati hayo yanatokea, Rais wetu mpendwa alikuwa Makao Makuu ya Shirika La Soka Duniani (FIFA) huko Uswisi na alipata fursa ya kupiga picha na Kombe la Dunia. Ikumbukwe pia kuwa Uswisi ndipo kulikohifadhiwa mabilioni yetu yaliyoporwa na mafisadi.


26 Aug 2012


13 Jul 2012


Takriban wiki moja baada ya Naibu Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Dkt Asha-Rose Migiro, kurejea nyumbani Tanzania baada a kukitumikia chombo hicho cha kimataifa kwa kipindi cha miaka mitano, vyanzo vya habari ndani ya Umoja huo vinadokeza kuwa utendaji kazi dhaifu na kushindwa ku-fit katika 'taasisi hiyo kubwa na ngumu' ndio sababu zilizopelekea Mtanzania huyo kunyimwa fursa ya kurefusha mkataba wake wa kazi.

"Wadhifa wa Naibu Katibu Mkuu ni mgumu na wenye mahitaji mengi; unahitaji mtu mwenye uzoefu wa kuongoza Sekretariaeti (ya Umoja huo).Changamoto kubwa kwake ilikuwa kutofahamu siasa za chombo hicho na kutengeneza 'marafiki' (alliances)," kilieleza chanzo kimoja kwa Vox Media kupitia maongezi ya simu.

Imefahamika kuwa Dkt Migiro alijaribu kulishawishi Kundi la Afrika (Africa Group),linalounda asilimia 28 ya wanachama wote wa Umoja wa Mataifa,kuomba limsaidie 'kumpigia debe' ateuliwe tena,ombi ambalo lilikataliwa.

"Hakuwa maarufu miongoni mwa wanadiplomasia, kwahiyo hakuna aliyemsikliza. Pia ukumbuke kuwa uteuzi wake ulipingwa sana," kilieleza chanzo hicho.

Jijini Dar es Salaam, mjumbe mwandamizi wa zamani wa Sekretarieti ya chama tawala CCM  aliyewahi kufanya kazi na Dkt Migiro kabla hajateuliwa kushika wadhifa huo wa Umoja wa Mataifa alieleza kuwa uteuzi huo katika chombo hicho cha kimataifa ulitokana na ukaribu wa Dkt Migiro na Rais Jakaya Kikwete.

Inafahamika kuwa Rais Kikwete na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon walijenga urafiki katika kipindi wote wawili walipokuwa mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa mataifa yao.

Ilipofika wakati kwa Ban Ki-moon kuomba kura kushika wadhifa wake wa sasa, Tanzania ilikuwa mstari wa mbele kumsapoti,na kura ya Kikwete ilisaidia Migiro kuteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu.

Lakini Ki-moon alipoamua hivi karibuni kufanya mapitio ya timu yake nzima kwa minajili ya kukabiliana na upinzani mkubwa dhidi ya timu hiyo, ililazimika Dkt Migiro 'atoswe' kutokana na "utendaji kazi dhaifu na ukosefu wa uzoefu unaohitajika kwa watendaji wa ngazi za juu katika Umoja wa Mataifa."

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka Vox Media.Shukrani za pekee kwa mdau @mactemba kwa kunitumia kiungo (link) cha habari hii.

2 Jun 2012

 
AKIRI TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA KUWA BOMU, ASEMA LISIPOTATULIWA LITALETA MACHAFUKO BARANI AFRIKA

Peter Saramba na Mussa Juma, Arusha
RAIS Jakaya Kikwete amekiri kuwa ukosefu wa ajira kwa vijana ni tatizo kubwa na kwamba lisipotafutiwa ufumbuzi wa kudumu linaweza kusababisha vurugu, machafuko na uasi wa umma, hata kwa nchi zinaoongozwa kwa misingi ya kidemokrasia, kama inavyotokea sasa katika nchi za Kiarabu.

Onyo hilo la Rais Kikwete linafanana na lile ambalo limekuwa likitolewa mara kwa mara na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, lakini, linapingana na kauli ya Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka ambaye Machi 21 mwaka huu, alimjibu Lowassa akisema, "Kitendo cha wanasiasa kuendelea kusema tatizo la ajira kwa vijana ni bomu linalosubiri kulipuka, siyo kweli."

Jana akifungua mkutano wa mwaka wa Magavana wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) Jijini Arusha, Rais Kikwete alisema moja ya sababu kuu ya machafuko yanayoshuhudiwa sasa kwenye ukanda wa nchi za Kiarabu, ni matokeo ya ukosefu wa ajira kwa vijana na watu kukata tamaa.

“Siyo kweli kwamba machafuko yanayoshuhudiwa kwenye nchi za Kiarabu ni matokeo ya Serikali za nchi hizo kukaa madarakani kwa kipindi kirefu kama wengi wanavyodhani. Ukweli ni kwamba hayo ni matokeo ya ukosefu wa ajira na watu kukata tamaa ya maisha,” alisema Rais Kikwete.

Alisema bila kutafutia ufumbuzi wa haraka, tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana ambao wengi hukimbilia mijini kusaka hali bora ya maisha, hata nchi zenye kuongozwa kidemokrasia, zinaweza kukumbwa na machafuko na uasi wa umma.

Rais alitumia fursa hiyo kuishukuru Denmark kwa kutoa fedha za kusaidia Mfuko wa Ajira kwa Vijana barani Afika, akisema ni moja ya mapendekezo kadhaa yaliyotolewa na kamati maalum ya kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya kiuchumi barani Afrika ambayo yeye na Rais wa AfDB, Dk Donald Kaberuka, walikuwa wajumbe.

Mapema Rais wa Ivory Coast, Allasane Ouattara aliyehudhuria mkutano huo aliunga mkono kauli hiyo ya Rais Kikwete kwa kusisitiza kuwa vijana lazima wawekewe mazingira mazuri na kuwezeshwa kukabiliana na kumudu changamoto za kiuchumi, kitamaduni na kiteknolojia wanazokabiliana nazo.

“Lazima wasaidiwe na wawekewe mazingira bora ya kupata fursa za ajira na kujiajiri, bila kufanya hivyo ni kukaribisha matatizo na machafuko yanayotokana na ongezeko la mahitaji na kukata tamaa katika miji yetu inayokua kila kukicha kutokana na ongezeko la vijana wanaosaka ajira na maisha bora,” alisema Rais Ouattara.

Rais Ouattara aliyetumia muda mwingi kumshukuru Rais Kikwete na viongozi wenzake wa Kiafrika kwa kusaidia upatikanaji wa amani nchini mwake alitaja changamoto kadhaa zinazokabili Bara la Afrika, kuwa ni mabadiliko ya tabia nchi, ukame, uhaba wa chakula na ukosefu wa amani kwa baadhi ya sehemu.

Mambo mtambuka 
Ili kukabiliana na tatizo hilo, Rais Kikwete alitaja mambo kadhaa yanayopaswa kufanyika ikiwa ni pamoja na kukuza na kuboresha sekta ya kilimo kwa kuongeza uwekezaji na kuacha kutegemea kilimo cha mvua badala yake itumie fursa ya vyanzo vingi vya maji.

“Bara la Afrika linaweza kuzalisha mazao ya kilimo na kujitosheleza kwa chakula na kubakisha ziada ya kuuza nje hadi kuwa ghala la chakula duniani iwapo uwekezaji katika sekta ya kilimo utapewa kipaumbele,” alisema Rais Kikwete.

Kuhusu miundombinu, Rais Kikwete aliipa changamoto AfDB kuongeza juhudi katika ufadhili na udhamini wa miradi ya maendeleo barani Afrika, ikiwemo miradi ya miundombinu aliyosema ni moja ya changamoto zinazokwaza maendeleo ya Afrika.

Alisema pamoja na kukwaza mawasiliano kwa njia ya barabara, reli na anga, uduni wa miuondombinu pia huchangia bei kubwa ya bidhaa na huduma katika nchi za Kiafrika kutokana na gharama kubwa ya usafirishaji.

Rais Kikwete alisema uwepo wa miundombinu ya uhakika siyo tu itawahakikishia wakulima vijijini soko na bei ya uhakika kwa mazao na bidhaa zao, lakini pia itapunguza kasi ya watu kuhamia mijini inayozikabili miji mingi barani Afrika.

Akizungumzia uwekezaji katika nyanja ya uchumi mdogo, Rais alisema  uwekezaji huo ndiyo njia pekee ya kuboresha na kuinua uchumi wa watu wa kawaida huku ikitumia vema soko lake la ndani kwa kutumia bidhaa zinazopatika barani humo badala ya kuendelea kutumia fedha nyingi kuagiza bidhaa kutoka nje, hata zile zinazopatikana nchi jirani.

Rais Kikwete alisema ili kupiga hatua kimaendeleo, Afrika kupitia AfDB na wahisani wengine wa ndani na nje lazima iwekeze katika ujenzi na uboreshaji wa miuondombinu ambayo ni nyenzo muhimu kimaendeleo.

Kuhusu sekta ya utali, alisema licha ya  Afrika kujaliwa vivutio vingi vya utalii, sekta hiyo bado haichangii kikamilifu uchumi wa bara hilo kutokana na kukabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo miundombinu mibovu, ukosefu wa safari za ndege za kimataifa na bei kubwa ya safari ndege chache za kimataifa zinazofanya safari zake barani Afrika.


Lowassa na ajira
Novemba 15, mwaka jana akiwa katika harambee ya ujenzi wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Makasa, Parokia ya Nyakato, Mwanza, Lowassa alionya kuhusu tatizo hilo na kulitaka Kanisa lisaidie kujenga vyuo vya ufundi.

Alitoa takwimu akisema utafiti wa mwaka 2006, ambao hata hivyo, hakusema ulifanywa na taasisi gani, ulionyesha kuwa tatizo hilo kwa sasa limekuwa na kufikia asilimia 15 huku likigusa zaidi vijana wenye umri wa miaka kati ya 15 hadi 24 ambao ndiyo nguvukazi ya taifa.

Novemba 29, mwaka huo wa jana akiwa harambee ya ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Usharika wa Amani Sabasaba, Singida, Lowassa alionya tena kuhusu tatizo hilo la ajira. 

Mwezi Machi mwaka huu akiwa katika sherehe za uzinduzi wa Jimbo jipya la Kanisa Katoliki Ifakara alirejea kisema: “Nawaomba maaskofu katika miradi yenu mlipe kipaumbele suala la tatizo la ajira kwa vijana.... hili kama tulivyosema ni bomu linalosubiri kulipuka...”

Hata hivyo, kauli hiyo mpya ya Lowassa, ilijibiwa na Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Gaudensia Kabaka Machi 21 akisema, "Siyo kweli  kudai Serikali hayaijafanya kitu, wanakuwa hawaitendei haki na kuongeza kwamba, utafiti uliofanywa na wizara yake kwa kushirikiana na Taasisi ya Takwimu ya Taifa (NBS), unaonyesha kuwa tatizo hilo limepungua kwa asilimia 1.2.

CHANZO: Mwananchi

22 Apr 2012




JK alinda mawaziri
•  ASISITIZA WAACHWE, UPEPO HUU UTAPITA

na Mwandishi wetu

WAKATI taarifa ya Kamati ya wabunge wa CCM chini ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, juzi iliridhia mawaziri wote wanaokabiliwa na tuhuma za ubadhirifu kwenye wizara zao wajiuzulu, jana Rais Jakaya Kikwete aliwasili nchini akitokea Brazil akiwa na msimamo tofauti.

Taarifa zinasema kumekuwa na mazungumzo baina ya Rais Kikwete na Pinda yaliyolenga kunusuru serikali yao lakini walitofautiana kuhusu hatua inayopaswa kuchukuliwa dhidi ya mawaziri waliotakiwa kujiuzulu.

Msimamo wa Pinda inadaiwa kuwa anataka mawaziri wanaokabiliwa na tuhuma waondoke ili kuleta uwajibikaji serikalini, lakini Rais Kikwete amesema mawaziri hao waachwe waendelee na kazi zao, kwa kuwa suala hili ni la upepo tu, liachwe litapita.

Tanzania Daima Jumapili limeelezwa kuwa rais anakataa shinikizo hilo kwa madai serikali haipaswi kuyumbishwa yumbishwa.

Miongoni mwa mawaziri wanaopaswa kuondoka ni Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo; Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Cyril Chami na naibu wake, Lazaro Nyalandu; Waziri wa Tawala wa Mikoa na Serikali za Mitaa, George Mkuchika na naibu wake, Aggrey Mwanri; Waziri wa Afya, Dk. Haji Mponda na naibu wake, Lucy Nkya na Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu.
Wengine ni Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja na Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige.

Habari zinasema Rais Kikwete na Pinda walitofautiana juu ya hatua dhidi ya mawaziri hao, hivyo kuwafanya baadhi ya mawaziri kutamba mitaani kuwa hawang’oki madarakani kwa sababu tayari bosi wao ameonyesha kutounga mkono tuhuma zinazoelekezwa kwao na wabunge wa upinzani na CCM.

Habari hizi zinasema pia kwamba Pinda amekuwa hafurahishwi na msimamo wa ‘bosi’ wake, hasa katika kushindwa kutoa uamuzi mgumu.

Zinadai kuwa rais amekuwa na tabia ya kuacha upepo uchukue nafasi yake wakati Pinda anataka baadhi ya watu wawajibike bila kujali nyadhifa zao au ukaribu na kiongozi mkuu wa nchi ili kurejesha imani ya serikali kwa wananchi.

Pinda inadaiwa amekuwa akitaka maamuzi magumu yafanyike, kwakuwa yeye ndiye anayesulubiwa na maswali pamoja na hoja za wabunge wawapo bungeni.
Baadhi ya wabunge waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili, wameweka wazi kuwa kama Rais Kikwete ataamua kuwalinda na kuwatetea mawaziri wake basi watawaondoa kwa mkakati tofauti utakaomlazimisha rais kukubaliana na hoja za wabunge.

Baadhi ya wajumbe waliozungumza na gazeti hili waliweka wazi hatua hiyo inahitaji muda na mipango madhubuti na wao wapo tayari kufanya hivyo, kwani nchi inazidi kudidimia kwenye umaskini huku watu wake wakikosa huduma muhimu za kijamii.

Walisema kwa muda mrefu wamekuwa wakiwalalamikia watendaji wa serikali na chama tawala lakini rais amekuwa mgumu wa kuyashughulikia matatizo hayo.

Wanasema rais ndiye kikwazo kikubwa cha maendeleo ya chama chao na serikali, hasa kwa kuwateua mawaziri, wakurugenzi na maofisa wengine bila kuangalia uwezo wao wa kiutendaji.

“Kaka kwenye Bunge la Februari kuna mbunge alitoa kauli kuwa kama tunaona mambo hayaendi serikalini tupige kura ya kutokuwa na imani na rais, watu walimshambulia. Sasa tunaona umuhimu wa kauli yake ile,” alisema mbunge mmoja.

Tanzania Daima Jumapili, limedokezwa makada wa CCM wameanza kuingiwa na hofu ya kubomoka kwa chama chao hasa baada ya makada wenzao kuanza kujiunga na vyama vya upinzani.
Wanasema wakati makada wa chama hicho wakiendelea kukihama uongozi wa CCM hauonekani kuchukua hatua zinazostahiki dhidi ya viongozi wanaochangia wananchi wakose imani na chama tawala.

Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe, aliweka wazi kuwa wabunge wa CCM ni lazima wakemee ubadhirifu kwakuwa Tanzania si mali ya CCM.

Mbunge huyo alikwenda mbali kwa kumtaja Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo, kuwa ni mwizi, mwongo na mbadhirifu wa mali za umma.

Mawaziri wasuasua kuwasilisha barua
Hadi jana Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema hajapokea barua ya kujiuzulu kutoka kwa waziri yeyote huku akiweka wazi kuwa kesho atatoa taarifa kamili juu ya jambo hilo.

Juzi vyombo vya habari vilipata taarifa kutoka kwenye kikao cha wabunge wa CCM kuwa baada ya wabunge kuzituhumu baadhi ya wizara kukithiri kwa ubadhirifu mawaziri wake wameamua kujiuzulu.

Taarifa hizo zilidokeza kuwa mawaziri hao walishinikizwa kuachia nyadhifa zao ili kukinusuru chama na serikali dhidi ya hasira za wananchi wanaokerwa na ufisadi.

Chami atoboa siri
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami, amejitetea kuwa wizara yake haimlindi Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Charles Ekelege, kama alivyotuhumiwa na baadhi ya wabunge.
Alisema amesononeshwa na taarifa ya ukaguzi wa CAG juu ya TBS iliyotolewa kwa waheshimiwa wabunge bila yeye mwenyewe au wizara kupewa nakala kwa kipindi cha wiki nzima.

Alisema kuwa baada ya kusikia kuwa waheshimiwa wabunge wengi wanayo taarifa hiyo na hata naibu wake kukiri bungeni kwamba taarifa imetoka wakati yeye hana nakala, alikwenda kwa Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashillilah na kuiomba nakala ya taarifa hiyo.

Alibainisha kuwa baada ya kufanya ufuatiliaji katika ofisi ya CAG ilikiri kuigawa kwa wabunge na kusahau kuipeleka kwa wizara hiyo ambayo ndiyo inayohusika.

“Hapa wasomaji wapime wenyewe. Inawezekanaje taarifa ya CAG iliyoandikwa kutokana na takwimu zilizotolewa na wizara yangu, iwafikie wabunge huku wizara yangu itakayotakiwa kuifanyia kazi taarifa yenyewe haipewi nakala, eti kwa kughafilika?

“Ni ukweli ofisi ya CAG walighafilikiwa, au jambo hili limesukwa ili kuniaibisha mimi mbele ya Watanzania, rais aliyeniteua na hasa wapiga kura wangu wa Moshi Vijijini?” alihoji.

Nundu ajitetea
Naye Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu, alisema tuhuma dhidi yake zilizoelekezwa na baadhi ya wabunge, hazina ukweli na zimelenga kumchafua.

Alisema kilichoelezwa na Kamati ya Miundombinu ni uongo na uzushi, kwani nyaraka walizozitumia kuorodhesha tuhuma dhidi yake si halali.

Kuhusu kuingilia utendaji wa Mamlaka ya Bandari kwa masilahi binafsi,  alisema si kweli, akaongeza kuwa kinachomponza ni kuipinga kampuni inayotetewa na menejimenti isipewe zabuni ya kufanya upembuzi yakinifu peke yake na kwenda kukopa na baadaye iruhusiwe kujenga gati namba 13 na 14.

“Wanasema namtaka mwekezaji  ambaye makubaliano yanaonyesha atamiliki gati hilo kwa miaka 45. Nachelea kusema ni uongo na uzushi,” alisema Nundu.

Mkuchika apata kigugumizi
Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika, alipoulizwa juu ya suala hilo alishindwa kukubali wala kukataa iwapo ataandika barua ya kujiuzulu. Alimtaka mwandishi amuulize Katibu wa Kamati ya Uongozi.


CHANZO: Tanzania Daima

UPDATE:


 
Picture

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 

Gazeti la Tanzania Daima la leo Jumapili Aprili 22, 2012 lina habari katika ukurasa wake wa mbele yenye kichwa cha habari ‘JK alinda Mawaziri’, inayodai kumekuwa na mazungumzo baina ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri MkuuMhe Mizengo Pinda kuhusu hatua inayopaswa kuchukuliwa dhidi ya mawaziri waliotakiwa kujiuzulu.

Habari hiyo imedai kuwa Mhe. Pinda anataka mawaziri wanaokabiliwa na tuhuma waondoke ili kuleta uwajibikaji serikalini, lakini, imeendelea  kudai habari hiyo, “Rais Kikwete amesema mawaziri hao waachwe waendelee na kazi zao, kwa kuwa suala hilini la upepo tu, liachwe litapita”.

Tunachukua nafasi hii kuweka bayana kwamba habari katika hilo gazeti la Tanzania Daima Jumapili si za kweli, bali ni za uzushi na upotoshaji mkubwa.

Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi nchini Brazil, amerejea jana Aprili 21, 2012 jioni. Hajaonana wala kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu, Mhe. Pinda.

Hivi sasa Mhe. Rais anasubiri kupata taarifa rasmi  kutoka Bungeni Dodoma.

Mhe Rais anawasihi wananchi wasiamini habari hizo za upotoshaji zilizomo kwenye gazeti hilo la Tanzania Daima Jumapili.

Pia ametoa rai kwa wanahabari wasitoke nje ya mstari wa weledi katika kutekeleza kazi zao ili kuendelea kulinda heshima zao binafsi, vyombo wanavyofanyia kazi pamoja na taaluma yenyewe.

Mwisho

Imetolewana:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
22 Aprili, 2012


Source: SUBI

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.