30 Mar 2009


LONDON, England (CNN) -- Leading British Cabinet minister Jacqui Smith's political future is in doubt after her husband admitted to paying for adult movies with taxpayers' money.

The home secretary's husband, Richard Timney, has apologized for the "embarrassment" he caused his wife, while she has promised to repay the money spent, including the £10 ($14) charge for the two films, the British Press Association reported.

According to British media reports, Smith had not seen the videos and was "mortified" that they had "mistakenly" been paid for using her MP's expense account.

Timney, who Smith pays £40,000 ($56,000) a year to be her office manager, submitted an expense claim last June for a £67 ($95) Virgin Media bill for television services in the couple's family home in Redditch, Smith's constituency, The Guardian newspaper reported.

It reported the bill included two adult films, at a cost of £5 ($7) each, as well as two viewings of the heist movie "Ocean's 13" and one of "Surf's Up," a children's film about a penguin.

The revelations could not come at a worse time for Smith, who is already being investigated by the Parliamentary Commissioner for Standards over her decision to claim at least £116,000 ($164,000) in second-home allowances for her family home since becoming an MP.

She has claimed the second-home allowance for her family home while living with her sister in London. Smith designated her sister's house as her "main" residence, allowing her to claim the money for her family home.

Conservative and opposition leader David Cameron described the latest news as "deeply embarrassing" for Smith.

He said Smith had "questions to answer," PA reported.

"I do not think this individual thing is the issue. I think she has got some questions to answer about the second home issue. It does seem to me pretty incredible to claim that the home where her family is, that is not her main home.

"I think this goes to a deeper problem, which is the second home allowance for MPs. The prime minister has ordered a review but he has sort of kicked it into the long grass.

"The review doesn't start until September, it is not going to report until after the next election. That is hopeless. We have got to get on with it."

Prime Minister Gordon Brown defended Smith.

"The home secretary is doing a great job and I do not think this issue should be allowed to detract from everything she is doing to ensure we protect the public and keep our neighborhoods safe," he said.

"She has done the right thing by taking steps to rectify the mistake that was made as soon as she became aware of it.

"This is very much a personal matter for Jacqui. She has made her apology, her husband has made clear that he has apologized."

Last week Brown ordered a review of the complex and opaque system of MPs' pay and allowances.

29 Mar 2009

A retired US police chief said he was robbed by “probably the dumbest criminal in Pennsylvania” at a police officers’ convention attended by 300 narcotics officers.

John Comparetto said that as he came out of a stall in the men’s room, a man pointed a gun in his face and demanded money.

Mr Comparetto gave up his money and mobile phone. But when the man fled, Mr Comparetto and some colleagues chased him.

They arrested 19-year-old Jerome Marquis Blanchett of Harrisburg as he was trying to leave in a taxi.

When a reporter asked Mr Blanchett for comment as he was led out of court, he said: “I’m smooth.”

About 300 police from Pennsylvania and Ohio were attending the narcotics officers’ convention near Harrisburg.


SOURCE: AP
Well,may be he's not the dumbest criminal ever...Look at the list below according to the Daily Mirror:
1: A stupid armed robber held up a petrol station in Vancouver and then returned to ask the cashier for directions. The 22-year-old man was chased by cops at 100mph after holding up staff at knifepoint but got lost and so pulled into a petrol station for help unaware it was the same one he had just robbed.

2: Dozy Californian thief Claud Gipson-Reynolds stole a fire engine and then radioed for help when it got stuck in the mud. Drunk Gipson-Reynolds called for a tow truck on the vehicle's radio – and was surprised when cops turned up instead. He said: "I could probably get on that show, World's Dumbest Criminals. I was pretty intoxicated at the time. My thinking was not the best." Sure was…

3: Brainless burglar John Pearce was left dangling upside down from the window of a house he was breaking into for an hour after getting his foot stuck. Home owner Paul Ives said: "He must be the world's dumbest thief." Pearce admitted a charge of burglary with intent to steal at Dartford magistrates.

4: A not so clever thief obviously didn't consider how easy it would be to spot him when he stole the prototype of a unique high-performance sports car worth £2m. The British-built Delfino Feroce, which has a maximum speed of 150mph, was being driven from a film studio when it was stolen from outside a flat in Fulham, west London
5: Dim-wit joyriders smiled for a speed camera as they raced past in a car they had just pinched. Police later used the photograph in court which clearly showed the teenage louts - nicknamed Dumb, Dumber and Dumbest by cops - turning round to make sure the camera got their best side. Police could not believe their luck when they found the speed trap picture - taken three hours before the Escort was torched.

6: Yob Andrew Kellett was slapped with an Asbo banning him from posting films of his antisocial antics on YouTube. Kellett, 23 - who calls himself Mr Chimp - was seen taking part in high speed car chases and boasting of 140mph speeds. In one of 80 clips, a car drives from a petrol station without paying, in another a wheelie bin is blasted with a firework and a third shows a man taking drugs. He said: "I'm not Britain's dumbest criminal - I'm just misunderstood."

7: Dopey burglar Peter Addison made it easy for police to track him down - by scrawling his name on a wall at the crime scene. The 18-year old wrote "Peter Addison was here" with black marker pen as he and friends raided a campsite for underprivileged children and went on a drunken wrecking spree. And when police tracked him down he did them another favour, by wearing a T-shirt he had stolen from the site to prove they had the right man.

8: Two would-be car thieves had their plans scuppered when they couldn't understand how to drive a manual. After holding up the owner at gunpoint the duo then spent several minutes trying to fathom out how to drive the Honda Accord to make good their escape in Georgia, U.S. However, before they could drive off police arrived and arrested them.

9: Germany's dumbest criminal was jailed for four years after he attempted to rob a bank wearing a mask that he couldn't see out of. He had to lift up his mask so he could demand money from the cashier which allowed cops to identify him.

10: Dim thieves stole presents from under a Christmas tree at a council's offices only to find out they were fake. Despite the boxes being unbelievably light and when shaken, would make no sound, they still made off with them thinking they had got their hands on a festive haul.

(Picha kwa hisani ya KENNEDY)

Gazeti la Majira limepotea mtandaoni kwa muda mrefu sasa,na kwa akina sie tunaotegemea habari za nyumbani kupitia nakala za kielektroniki za magazeti husika mkombozi wetu mkuu amebaki Mr Kennedy.Na ni kwa kupitia tovuti yake ndipo nilikutana na version isiyopendeza ya habari kuhusu ajali iliyomhusisha Mzee wa Vijisenti,Andrew Chenge,na kupelekea vifo vya akinadada wawili.

Gazeti la Majira lilidai kuwa marehemu hao ni "machangudoa waliokuwa wanatokea Maisha Club".Sijui vyanzo (sources) vyao vya habari husika ni vipi lakini mwandishi yeyote mwenye busara angepaswa kujiridhisha kuhusu identity halisi ya marehemu hasa kwa vile tunazungumzia watu waliopoteza maisha.Hivi mwandishi huyo atajisikiaje iwapo baada ya uchunguzi itagundulika kuwa marehemu hao hawakuwa machangudoa?In fact,magazeti kadhaa yameripoti maelezo ya ndugu za marehemu yanayoeleza kwamba mmoja wao alikuwa mfanyabishara na mwingine mfanyakazi wa hoteli jijini Mwanza.

Pengine haikuwa nia ya mwandishi kuwa-describe marehemu hao kama changudoa (labda kutokana na haraka ya kuwahisha habari kwa mhariri) lakini taswira ya haraka iliyopatikana kutoka katika habari hiyo ni ujenzi wa matabaka:kigogo (mzee wa vijisenti) kagonga fukara (changudoa).By the way,hata hata kama hao mabinti wangekuwa machangudoa as suggested by the Majira reporter bado haiondoi haki yao ya kuwa hai muda huu!

Kingine ambacho hakihusiani na uandishi japo kinahusu tukio hilo la kusikitisha ni namna Jeshi la Polisi linavyoonekana "kubabaika" katika kushughulikia ajali hiyo.Kwa mujibu wa vyombo vya habari,Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Suleiman Kova,ameunda TUME MAALUM ya kuchunguza ajali hiyo eti kwa "kuzingatia uzito wa tukio hilo".Chenge ni Mtanzania kama mie na wewe,na kama amehusika na ajali basi sheria za uslama barabarani zifanye kazi yake.Sijui ni madereva wangapi walalahoi wanaopata "bahati" kama ya Chenge ya kuundiwa tume!

Kamanda Kova anadai kuwa tume hiyo imeundwa ili "kusiwepo mwanya wowote ,taratibu zote zitafuatwa bila kujali nani na wala nafasi aliyonayo....na kuleta uwazi na utawala bora" (kwa mujibu wa gazeti la Majira) na pia amenukuliwa na gazeti la Mwananchi akisema kuwa "hapa bwana hakuna mchezo wala hakuna kuangalia vyeo wala nani ni nani...".Hivi matamshi kama hayo (iwapo kesi itapelekwa mahakamini) hayawezi kutumiwa na wakili wa Chenge kudai "ameonewa kwa vile Kamanda Kova alishadai hawataangalia vyeo-which directly points to Chenge ambaye licha ya kuwa ex-minister,pia ni munge na kigogo wa CCM?"

Kama nilivyoandika jana,tuendelee kuwapa polisi benefit of doubt kwa matarajio kwamba wanafahamu bayana kuwa tukio hilo linaangaliwa na Watanzania wengi kama kipimo cha haki sawa kwa wote (huku wakiwa na kumbukumbu ya kesi ya marehemu Ditto).

SHAHIDI katika kesi ya kuomba na kupokea rushwa ya sh 600,000 inayomkabili Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Mbelekese, wilayani Iramba, Singida, Iddi Mughenyi, juzi alipata kipigo kutoka kwa mwanasheria wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwenye viwanja vya Mahakama ya Wilaya ya Iramba, kwa madai kuwa alimgeuka katika ushahidi alioutoa mahakamani hapo.

Mtuhumiwa alipata kipigo kutoka kwa mwanasheria huyo aliyetambulika kwa jina moja la Mchumi, kwa madai kwamba alimgeuka katika ushahidi aliuotoa mahakamani hapo.

Tukio hilo la aina yake limedaiwa kutokea muda mfupi baada ya Mughenyi kutoa ushahidi katika kesi namba 14/2009 inayomkabili ofisa mtendaji huyo.

Akizungumza kwa njia za simu kutoka Iramba, mmoja wa watumishi wa mahakama hiyo ambaye hakutaka kutajwa jina, alisema kuwa kuna kila dalili kuwa ushahidi uliotolewa na shahidi huyo haukumridhisha mwanasheria Mchumi, kwa madai kwamba ulikuwa kinyume cha walivyokubaliana.

“Idd Mughenyi ni shahidi wa upande wa TAKUKURU kwenye kesi hiyo ambayo Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Mbelekese anatuhumiwa kuomba na kupokea rushwa, lakini juzi aliposimama kizimbani aliikana taasisi hiyo, kitendo ambacho kinawezekana kilimuudhi mwanasheria huyo ambaye ndiye alikuwa mwendesha mashtaka katika kesi hiyo,” alifafanua mtumishi huyo wa mahakama.

Aidha, mtumishi huyo alisema baada ya kesi hiyo kuahirishwa na kutoka nje ya mahakama, ndipo Mchumi alipomweka chini ya ulinzi shahidi huyo na kumtaka apande kwenye gari ili waende ofisi za TAKUKURU Wilaya ya Iramba.

Alisema kutokana na shahidi huyo kugoma kupanda gari kwa madai ya kutofahamu kosa, ndipo mwanasheria huyo alipoanza kumpiga makofi hadi kumuumiza kwenye jicho la upande wa kushoto na kumchania shati.

Alibainisha tukio hilo lilishuhudiwa na baadhi ya mahakimu, na kuongeza kuwa waliwaamru askari kwenda kuamua ugomvi huo, kisha kuwapeleka kituo cha polisi.


RUSHWA NI RUSHWA,IWE NDOGO AU KUBWA.LAKINI INGEPENDEZA ZAIDI KUONA TAKUKURU IKITUMIA MISULI MINGI KWENYE RUSHWA KUBWA NA UFISADI SAMBAMBA NA HIZO RUSHWA NDOGO.MAPAPA WA KAGODA NA RICHMOND (achana na yule Mdosi aliyepandishwa kizimbani) BADO WANAPETA URAIANI SAMBAMBA NA MAFISADI WA RADA.

28 Mar 2009

(Photo credit:JIJI LA DAR)

Mayor threatens legal action against street name changers

SEBASTIAN MRINDOKO
Dar es Salaam

A TOP local government official in Dar es Salaam has roundly rebuked the ongoing trend of people clandestinely changing street names in the city without following proper channels, including getting the blessing of the City Fathers.

According to the Mayor of the Ilala Municipality, Abuu Jumaa, legal action will certainly be taken against such people once sufficient proof is obtained.

Referring specifically to a query by THISDAY on the name-change applied to one of the city’s most historically famous thoroughfares Kisutu Street, now apparently going by the name of ’PRAMUKH SWAMI’, Mayor Jumaa stated unequivocally:

’’My office has never received an official application to change the Kisutu Street name into an Indian name. Therefore, such an action is an insubordination to the city authority.’’

The mayor’s statement is a direct contradiction of that made last year by the former deputy mayor of the same Ilala Municipality, Mohamed Yakoub, who asserted in an interview with THISDAY that the Kisutu Street name-change had been given a formal stamp of approval.

’’All the (Ilala) municipality legal procedures were properly followed in changing the name of not only Kisutu Street, but also some other streets around the city centre,’’ Yakoub said.

But according to current mayor Jumaa, there are no records whatsoever showing the change of the traditional Kisutu name to ’PRAMUKH SWAMI.’

THISDAY last year ran a series of articles on the increasing trend of various streets within Dar es Salaam’s central business district, suddenly acquiring bizarre-sounding new names in highly mysterious circumstances.

It has been noted that skepticism is on the rise amongst members of the general public over the supposed ’secrecy’ shrouding the whole exercise, with open suggestions that corruption at certain local government levels may be involved.

The Dar es Salaam City Director, Bakari Kingobi, has conceded in the past that such street name changes could very easily cause confusion particularly for tourists who may be trying to find their way around the metropolis using officially-approved city maps.

According to Kingobi, only the city authorities have the mandate to administer such street name changes.

’’There is only one city authority - not two - responsible for administering such name-changes to the city streets. Anyone who tries to do so without informing this city authority, is violating the law and is liable for prosecution,’’ he said.

Speaking to THISDAY yesterday, Ilala Municipality mayor Jumaa said it amounted to sacrilege for anyone to change a street name on the basis of racial, tribal, or religious beliefs.

’’There are some basic criteria used to endorse suggestions for street name changes. Bias of any sort is not one of them,’’ he asserted.

He also said streets with traditionally famous names like Kisutu should be left alone, while anyone wanting to recommend a street name to suit their own needs should look for streets with no names at all � of which apparently there are still many.

According to Jumaa, the municipal authorities will seek explanations from the local government authorities regarding the Kisutu Street name-change in particular.

Any official found to have been responsible for wrongdoing in the whole episode will be taken to task through legal channels, he added.

SOURCE: ThisDay


Aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge (61), amewekwa chini ya ulinzi katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar es Salaam, kwa zaidi ya saa saba baada ya kuhusishwa na ajali ya gari na bajaj ambayo imeua watu wawili. Waliokufa ni wanawake wawili ambao ndugu amejitokeza na kudai kuwa wote ni wageni, waliwasili juzi Dar es Salaam kutoka Mwanza na mmoja alikuwa njiani kwenda Zanzibar kuolewa. Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, ajali hiyo ilitokea saa 10 alfajiri usiku wa kuamkia jana wakati Chenge akiendesha gari namba T 512 ACE aina ya Toyota Hilux na kuigonga bajaj hiyo namba T 736 AXC iliyokuwa na abiria hao wawili wanawake.

Chanzo hicho kilidai kuwa baada ya ajali hiyo, Chenge alikwenda kwanza nyumbani kwake na kuripoti kituoni hapo saa moja asubuhi jana na kuwekwa chini ya ulinzi na kuhojiwa hadi saa saba mchana, huku nje akisubiriwa na ndugu zake. Gazeti hili lilimshuhudia mbunge huyo wa Bariadi Magharibi akiingizwa kwenye gari la Polisi namba PT 0217 na kwenda eneo la tukio karibu na shule ya msingi ya Oysterbay katika makutano ya barabara za Karume na Haile Selassie, ambako alieleza namna ajali hiyo ilivyotokea.

Wakati mbunge huyo akitolewa katika kituo cha Polisi, kulitokea vurugu baina ya ndugu zake na waandishi wa habari, ndugu hao wakitaka kuzuia Chenge kupigwa picha, hali iliyosababisha kusukumana na kurushiana maneno makali. “Ninyi mmezidi kumwonea huyu kwani ni lazima mumpige picha ndio muuze? Hebu tokeni hapa,“ alisikika mwanamke ambaye alikuwa mstari wa mbele kusukuma waandishi, huku akilia na almanusra wapigane na mmoja wa wapigapicha waliokuwa kazini.

Hata hivyo, vurugu hizo zilimalizika baada ya waandishi kuwazidi nguvu ndugu hao na kung’ang’ania kumpiga picha mbunge huyo ambaye awali alikuwa akifunikwa magazeti na nduguze, lakini aliyatoa na kupisha waandishi wampige picha vizuri. Akiwa katika eneo la tukio, Chenge alimwelezea Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Peter Kivuyo, namna ajali hiyo ilivyotokea na alidai ilitokea baada ya bajaj hiyo kutaka kupita gari jingine kwa kasi.

“Bajaj ile ilikuwa inataka kupita gari jingine lililokuwa likitoka Morogoro Stores, bahati mbaya kukawa na gari lingine linakuja, ile bajaj ikabana upande wangu na mimi nilikuwa katika mwendo wa kati ya kilometa 80 hadi 100 kwa saa,“ alidai Chenge. Alidai kuwa baada ya kuona bajaj ile inakwepa gari la mbele wasigongane uso kwa uso, alirudi upande wa kulia ndipo alipoigonga ubavuni kushoto. "Gari la nyuma lingesimama, dereva wake angeweza kueleza vizuri, ila baada ya ajali nikasikia watu wanaita 'Chenge! Chenge!’ nikajua niko salama, nikashuka,“ alidai.

Aliendelea kudai kuwa aliposhuka, alikuta abiria wawili wanawake wakiwa bado wanapumua ingawa kwa shida, lakini walipofika trafiki hali zao zilizidi kuwa mbaya na katika kipindi hicho chote, dereva wa bajaj alikuwa haonekani. Naye askari wa usalama barabarani aliyefika katika ajali hiyo, Mustafa Salum, alimweleza Kivuyo juu ya tukio hilo, ambapo alisema alipata taarifa za ajali hiyo saa 10.30 alfajiri na alipofika eneo la tukio, alikuta tayari abiria hao wawili wameshafariki dunia. “Niliipeleka miili ya marehemu hospitali ya Mwananyamala, ila kwa mujibu wa watu waliokuwa eneo la tukio, waliowaona marehemu hao wawili katika ukumbi wa Maisha Club,“ alisema.

Naye kaka wa mmoja wa marehemu hao, January Constantine, alisema alipata taarifa za kifo cha dada yake, Beatrice Constantine (34) asubuhi na alikwenda kutambua mwili wake hospitalini, lakini kutokana na alivyopondeka alimtambua kwa alama za mwili. Alisema dada yake ni mfanyabiashara na mkazi wa Mwanza na kwamba aliwasili Dar es Salaam, akiwa na rafiki yake huyo na ilikuwa aondoke jana alfajiri kwenda Zanzibar kwa ajili ya harusi ya rafiki yake huyo. Gazeti hili lilishuhudia gari la Chenge kwa mbele likiwa na damu, nywele na mabaki ya ubongo ambao unasadikiwa kuwa wa mmoja wa marehemu hao. Polisi pia iliokota kipande cha fuvu la mtu katika eneo la tukio.

Gari hilo lilikuwa na stika ya Bima ambayo ilikatwa Juni 6, 2006 na kumaliza muda wake Juni 6, mwaka juzi. Naye Theopista Nsanzugwanko anaripoti kuwa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu Dar es Salaam, Suleiman Kova, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema mmiliki wa bajaj hiyo ni Zuwena Nassoro na anatakiwa kuripoti katika kituo chochote cha Polisi huku wakiwa wanamshikilia Chenge Oysterbay ili kuisaidia Polisi. Alisema uchunguzi wa tukio hilo unafanywa chini ya Kivuyo na wataalamu mbalimbali ili kuondoa dhana ya upendeleo kwa kuwa Chenge ni mtu maarufu.

Chenge (62) alijiuzulu uwaziri wa miundombinu Aprili 20 mwaka jana, kutokana na kashfa ya rushwa ya dola milioni moja kutoka kampuni kubwa ya uuzaji vifaa vya kijeshi duniani ya BAE Systems. Alijiuzulu baada ya kudaiwa kupokea rushwa ili kuwezesha ununuzi wa rada ya kijeshi ya pauni milioni 20 za Uingereza na kwamba fedha hizo ziliwekwa katika akaunti yake ya kisiwa cha Jersey.

Baada ya kujiuzulu, alikaririwa akisema pamoja na tuhuma hizo, mapenzi kwa nchi yake na chama chake, ndivyo vilimlazimisha achukue uamuzi huo na kuongeza kuwa fedha zilizokutwa katika akaunti yake hiyo hazina uhusiano wowote na BAE Systems. Tuhuma hizo za rushwa zilichochea kelele pale alipohojiwa na waandishi wa habari na kujibu kuwa fedha anazotuhumiwa nazo ni 'vijisenti (fedha kidogo)'.

CHANZO: HabariLeo

I SMELL DITOPILE-LIKE ADMINISTRATION OF JUSTICE......KWA UBINADAMU WA KAWAIDA TU,GARI LAKO LIKIHUSIKA KATIKA AJALI INAYOPELEKEA HATARI YA MAISHA YA MAJERUHI PRIORITY INAKUWA KWENYE KUOKOA MAISHA YA MAJERUHI HAO (KWA MUJIBU WA HABARI HII MZEE WA VIJISENTI ALIKWENDA ZAKE NYUMBANI HADI SAA 1 ASUBUHI ALIPORIPOTI KITUO CHA POLISI NA KUHOJIWA KWA MASAA 7-(DOES IT REALLY MATTER HOW LONG THE INTERROGATION LASTED WHEN TWO PEOPLE HAD ALREADY LOST THEIR LIVES?).

ANYWAY,LET'S GIVE THE POLICE A BENEFIT OF DOUBT HOPING THAT THIS TIME HAKUTAKUWA NA USANII KAMA KATIKA ISHU YA MAREHEMU DITO.

27 Mar 2009


DNA tests on Alfie Patten, the 13-year-old boy who was alleged to have become a father when he was just 12, show that he not the baby girl’s actual dad.

The 300-pound test was conducted on him after half a dozen boys claimed to have slept with schoolgirl pal Chantelle Stedman, 15.

Although Alfie was convinced he was the dad after a single night of unprotected sex with Chantelle, the DNA test proved the 4ft-tall pupil was not the father of her seven-week-old tot Maisie Roxanne.

According to The Mirror, Chantelle had told her half-sister Jodie O’Neill, 17, that her daughter’s father could have been one of the boys she slept with at her parents’ home in Eastbourne, East Sussex.

The paper further reveals that the teen girl also said that her mother Penny had ordered her to keep saying that she has been a virgin when she slept with Alfie.
SOURCE: ThisIs50.com


Brazil’s President Luiz Inácio Lula da Silva on Thursday blamed the global economic crisis on “white people with blue eyes” and said it was wrong that black and indigenous people should pay for white people’s mistakes.

Speaking in Brasília at a joint press conference with Gordon Brown, the UK prime minister, Mr Lula da Silva told reporters: “This crisis was caused by the irrational behaviour of white people with blue eyes, who before the crisis appeared to know everything and now demonstrate that they know nothing.”

He added: “I do not know any black or indigenous bankers so I can only say [it is wrong] that this part of mankind which is victimised more than any other should pay for the crisis.”

Mr Brown appeared to distance himself from Mr Lula da Silva’s remarks. “I’m not going to attribute blame to any individuals,” he said.

Mr Brown was visiting Brazil as part of a five-day tour of Europe, the US and South America in preparation for the G20 summit to take place in London next Thursday. He made a joint appeal with Mr Lula da Silva for the world’s biggest economies to provide $100bn to boost global trade.

“I’m going to ask the G20 summit next week to support a global expansion of trade finance to reverse a slide in world trade,” Mr Brown said.

Mr Lula da Silva also spoke out strongly against raising trade barriers in response to the global crisis. “I compare protectionism to a drug,” he said. “Why do people use drugs? Because they are in crisis and they think the drug will help them. But its effects pass quickly.”

The two leaders’ remarks demonstrate the desire each will have to secure the other’s support during the G20 meeting.

Brazil – which has long campaigned unsuccessfully to be given a permanent seat on the United Nations Security Council – will argue for a bigger voice for Brazil and other emerging nations in multilateral organisations such as the International Monetary Fund and the Financial Stability Forum, a group of central banks and national supervisory authorities established in 1999.

Brazil is one of many nations calling for increased regulation of global financial markets and greater powers for multilateral regulators.

It will also call for a resumption and conclusion of the Doha round of talks at the World Trade Organisation.

In return for supporting such initiatives, Mr Brown will expect Brazil to endorse calls for fiscal stimulus in a bid to mitigate the impact of the global crisis, such as the proposed $100bn in trade finance.


SOURCE: FT


KWA MTU YEYOTE MWENYE AKILI TIMAMU,HATA AKIAMSHWA USINGIZINI AU AKIWA BWII KWA ULEVI,HAIINGII KICHWANI KUSIKIA HOJA ZA KIFISADI ZA KUNUNUA MITAMBO ILIYONGIZWA NCHI KITAPELI NA MAJAMBAZI WA RICHMOND NA HATIMAYE KURITHISHWA KISANII KWA WENZAO WA DOWANS.TUKIRUHUSU HILI LITOKEE,KUNA MAHALA ITAFIKA NCHI YETU NAYO ITAUZWA NA KISHA TUTATAKIWA KUINUNUA BACK....


Tausi Mbowe na Elias Msuya

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk Wilbroad Slaa ameitaka serikali kuitaifisha mitambo ya Kampuni ya kuzalisha umeme ya Dowans badala ya kujadili manunuzi yake.

Dk Slaa aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada yakutopa taarifa ya kamati kuu kilichokutana kwaajili ya kuandaa mkutano wa baraza kuu.

Alisema kuwa mitambo ya Dowans ilirithiwa kutoka kwenye kampuni ya Richmond ambayo ilibainika bungeni kuwa ni ya kifisadi kwahiyo hakuna haja ya kuinunua tena bali kuitaifisha.

“Msimamo wangu siku zote ni kutaifishwa kwa mitambo ile na siyo kuinunua. Naishangaa serikali, kutaka kuinunua mitambo ya Dowans wakati mitambo ile ilishabainishwa Bungeni kuwa ni ya kifisadi. Kama mtu umekamata kitu chako cha wizi utakinunua tena?" alihoji

Akizungumzia malumbano kati ya Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, Dk Slaa alisema,

“Mradi wa kuzalisha umeme nimeushughulikia kwa miezi minane. Nilikwenda hadi kijiji cha Kisesida mkoni Singida ambako ndiko kampuni mbili za Power Pool East Africa ya Dk Mwakyembe na wenzake na Wind East Africa ya Rostam Aziz zimewekeza.

Kampuni ya Power Pool East Afrika ni ya wazalendo na imeshalipa fidia kwa wakazi wa kijiji cha Kisesida lakini ile ya Wind East Africa haijafanya hivyo, badala yake inabebwa na kiongozi wa ngazi za juu mkoani ambaye amekuwa akiwakejeli wanakijiji wa Kisesida. Ndiyo maana kuna kuwa na malumbano kati ya Rostam Aziz na Dk Mwakyembe,” alisema Dk Mwakyembe.

Akizungumzia tatizo la mgawo wa umeme ambalo litangazwa na Tanesco hivi karibuni, Dk Slaa alisema,"Baada ya kubainika kwa kashfa ya Richmond, Rais Kiwete alitangaza kuwa suala la mgawo wa umeme litakuwa historia katika nchi hii, sasa mgawo huu unatoka wapi tena? nendeni mkamwulize,” alisema Dk Slaa.

Aidha alimshangaa Rais Kikwete kwa kuendelea kumwacha madarakani Mkurugenzi wa Tanesco, Idriss Rashid wakati anatuhumiwa kwa ufisadi.

"Dk Rashid (PICHANI JUU) alihusishwa na ufisadi alipokuwa Gavana wa Benki kuu. Tumeshatoa vilelezo vyote kuthibitisha jinsi alivyoshiriki kwenye ununuzi wa rada na ndiyo maana sasa hivi anashirkiana na Dowans ili kununua mitambo yake kiufisadi. Tunashangaa kwanini Rais Kikwete hamchunguzi, wala kumwajibisha. Eti wanasema Serikali ya Uingereza inachunguza, wakati si kweli. Uingereza wanachunguza ushiriki wa BAE system siyo watu wetu,” alisema Dk Slaa.



CHANZO: Mwananchi
IT MAKES A LOT OF SENSE,DOESN'T IT?UNAMKAMATA KIBAKA NA MALI YAKO,BADALA YA KUMKWINDA AKUREJESHEE NA HATIMAYE KUMFIKISHA POLISI ETI UNAKUBALI AKUUZIE ALICHOKUIBIA!IT COULD ONLY HAPPEN IN TANZANIA,I SUPPOSE!

26 Mar 2009


YAANI HADI INATIA KIZUNGUZUNGU.HEBU SOMA HABARI IFUATAYO KISHA TUSHIRIKIANE KUJIBU MASWALI NILIYOWEKA BAADA YA HABARI HII

Bunge mradi wa ulaji

na Mwandishi Wetu

WAKATI baadhi ya wabunge wakiendelea kulumbana kupitia katika vyombo vya habari kuhusu masuala mbalimbali yanayogusa maslahi ya taifa,imebainikawamekuwa wakichuma mamilioni ya fedha kupitia katika malipo yao halali ya mishahara, posho na fedha nyingine zisizotokana na malipo yao rasmi wanayostahili.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano umethibitisha pasipo shaka kwamba, fedha ambazo wabunge wamekuwa wakichuma kwa njia mbalimbali kwa kutumia nafasi zao za uwakilishi, zinaweza zikawa sababu mojawapo muhimu ya kuibuka kwa makundi yanayosigana ndani ya Bunge na hususan miongoni mwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, gazeti hili limefikia hatua ya kutilia shaka kwamba, mzozo wa hivi karibuni, kati ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe na mwenzake wa Igunga, Rostam Aziz, kwa kiwango kikubwa unakuzwa kutokana na sababu za maslahi binafsi zaidi kuliko madai ya uzalendo na maslahi ya taifa.

Shaka hiyo ya Tanzania Daima Jumatano inatokana na ukweli kwamba, wabunge hao wawili ambao wote wawili ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kwa namna moja au nyingine wamepata kuwa au wanayo maslahi ya wazi na ya moja kwa moja katika sekta ya nishati.

Kauli ya hivi karibuni ya mmiliki wa Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd, Mohammed Al Adawi, kukiri kwamba aliwekeza katika sekta ya nishati kwa ushawishi wa Rostam sambamba na ile ya kubainisha kuwa kampuni ya mbunge huyo ilipata kuingia katika zabuni ya kutaka kufanya kazi za ujenzi katika mradi wa kuzalisha umeme wa dharura, ni ushahidi wa wazi wa namna mwanasiasa huyo alivyo na maslahi ya moja kwa moja katika sekta ya nishati.

Kama ilivyo kwa Rostam, taarifa za hivi karibuni, zilizothibitishwa na Mwakyembe mwenyewe
kuwa ni mmoja wa wakurugenzi waanzilishi wa Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd yenye malengo ya kuzalisha umeme wa upepo kutoka mkoani Singida, ni ushahidi kwamba naye anayo maslahi ya moja kwa moja katika sekta ya nishati.

Kuingia kwa Rostam na Mwakyembe katika sekta ya nishati, kwa kiwango kikubwa kunaonyesha namna wabunge, hususan wale wa CCM walivyojizatiti kutumia fursa zao za kisiasa kujinufaisha kiuchumi, nyuma ya kivuli cha uwekezaji
kupitia sheria ya soko huria.

Kama hiyo haitoshi, mzizi wa fitina kuhusu ukweli kwamba Bunge limekuwa likitumiwa kama kiota cha wanasiasa kuvuna mamilioni, zilithibitishwa mkoani Kilimanjaro juzi na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilibrod Slaa ambaye alisema mshahara anaolipwa mbunge kwa mwezi unafikia sh. milioni saba, hiyo ikiwa mbali na posho nyingine.

Dk. Slaa alitaja kiwango hicho cha mshahara wake wakati akihutubia wakazi wa mji mdogo wa Hedaru, wilayani Same katika mfululizo wa mikutano ya Operesheni Sangara inayoendeshwa na CHADEMA.

Wakati Dk. Slaa akibainisha ukweli huo, uchunguzi wa Tanzania Daima Jumatano umebaini pia kuwa wabunge wanaweza kujikusanyia mamilioni ya shilingi kwa kuhudhuria vikao mbalimbali vya kamati za kudumu za Bunge, semina na safari za ndani na nje ya nchi.

“Ndugu zangu, afadhali msijue mshahara anaolipwa Dk. Slaa kama mbunge, mkijua nalipwa shilingi ngapi mnaweza hata kunipiga mawe,” alisema Dk. Slaa wakati akihutubia mkutano huo na kuitikiwa na sauti za wananchi wakimtaka ataje mshahara wake.

“Mnataka kuujua mshahara wangu, ninalipwa sh milioni saba kwa mwezi. Haki iko wapi? Mimi nalipwa milioni saba, na posho yangu kwa siku ni sh 135,000. Haya ni malipo makubwa mno, fedha ninayopata kwa siku inaweza kuzidi hata mshahara wa mwezi mzima wa polisi. Muulizeni yule polisi pale analipwa shilingi ngapi msikie.

“Juzi nimetaja posho za wabunge na kusema zipunguzwe, lakini Spika wa Bunge analalamika eti naingilia haki na madaraka ya Bunge, sasa leo nasema ninalipwa jumla ya shilingi milioni saba kwa mwezi, acha posho za bungeni. Kweli hii ni haki?” alisema Dk. Slaa.

Alisema kuwa akiwa raia huru, ana haki ya kutaja kwa hiari yake kiwango cha mshahara wake, hasa pale anapoona kuwa kulipwa kiwango hicho ni kutowatendea haki mamilioni ya Watanzania maskini wanaolipa kodi zao wakitegemea serikali iwakomboe kutoka kwenye lindi la umaskini.

Dk. Slaa alisema wabunge wengi wa CCM akiwamo Spika wa Bunge, Samuel Sitta, hawawezi kuunga mkono hoja hiyo kwa vile wapo bungeni kwa ajili ya kutafuta maslahi yao binafsi.

“Wafanyakazi wengi na Watanzania wanateseka kwa mishahara midogo na maisha duni, mamilioni haya ya fedha kwenda mifukoni mwa watu ni aibu kwa nchi na CHADEMA tunasema hapana, fedha hizi ziende katika masuala ya kusaidia jamii na kuongeza mishahara ya walimu, polisi, mahakimu na watendaji wengine,” alisema Dk. Slaa huku akishangiliwa na mamia ya wakazi wa Hedaru waliohudhuria mkutano huo.

Alirejea kauli yake ambayo amekwishakaririwa akiitoa mara kadhaa kuwa Spika Sitta, anapaswa kujiuzulu nyadhifa alizonazo katika CCM, ili awe huru kuliongoza Bunge kwa maslahi ya Watanzania badala ya kushinikizwa na maslahi ya chama chake.

Dk. Slaa alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba, kushangazwa na hatua ya Rais Jakaya Kikwete kuendelea kuwateua wabunge wa CCM kuwa wajumbe katika bodi za mashirika ya umma.

Akizungumza wiki iliyopita katika mkutano uliondaliwa na Jukwaa la Wahariri, Prof. Lipumba alisema, hatua hiyo ya Rais Kikwete mbali na kuwahalalishia wabunge ulaji, inazoretesha utendaji wao katika kuyasimamia ipasavyo mashirika hayo ambayo utendaji wake wa kazi unapaswa kusimamiwa na taasisi hiyo muhimu ya dola.

Wakati hali ikiwa hivyo katika mishahara ya wabunge, Tanzania Daima Jumatano limebaini kuwa wabunge wamekuwa wakilipwa mamilioni ya fedha wakati wanapokutana na baadhi ya taasisi za umma ambazo kamati za Bunge zinazisimamia shughuli zake.

Taarifa za hivi karibuni ambazo gazeti hili limezipata zinaonyesha kuwa, Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (Tanesco) lilitumia jumla ya sh milioni 16 kwa ajili ya kulipa posho na usafiri wabunge kutoka majimboni mwao, pamoja na makatibu wawili waliohudhuria kikao cha dharura kilichowakutanisha Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Kamati ya Bunge ya Kamati ya Nishati na Tanesco.

Taarifa kutoka ndani ya ofisi ya Bunge, zinaeleza kuwa licha shirika hilo kuwa na hali mbaya kifedha, lililazimika kuingia gharama hizo baada ya ofisi ya Bunge kuitaka Wizara ya Nishati na Madini kuwagharamia wabunge hao kwa sababu Bunge halikuwa na fedha katika kikao chake cha Desemba mwaka jana.

Katika hali ya kushangaza, habari za wanakamati hao wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kulipwa posho na gharama zao nyingine na Tanesco wakati wakihudhuria kikao hicho zimewafanya wabunge, Katibu wa Bunge na Spika kutofautiana.

Spika Sitta, jana alilithibitishia Tanzania Daima Jumatano kuwa, wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini walilipwa posho na gharama za usafiri kwa sababu Bunge halikuwa na fedha wakati Waziri wa Nishati na Madini, Ngeleja alipotaka kukutana na kamati hiyo ili kupata ushauri.

Lolote linaweza kutokea kutegemea na nani amewaita, kama wameitwa kusaidia jambo ambalo halimo kwenye utaratibu wa Bunge wanalipwa na aliyewaita. Na katika hili ilikuwa hivyo, ninalifahamu vizuri sana, waziri aliomba kukutana na kamati wakati muda wa Bunge ukiwa umepita, Katibu wa Bunge alimuandikia akimueleza kuwa Bunge halina fedha ila kama wizara yake inaweza, basi ilipe posho na gharama za wabunge hao kusafiri hadi Dar ili aweze kukutana
nao.

“Hivyo ndivyo ilivyokuwa, sasa mimi sijui kama ililipa wizara, Tanesco au nani, la msingi hawakulipwa na Bunge, na kama wabunge ambao ni wanakamati wanakanusha hili, ni watu wa ajabu kwa sababu sijui wanaogopa nini kueleza ukweli,” alisema Spika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo (CCM), alipozungumza na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani, alikana kupokea senti tano kutoka Tanesco wakati wakihudhuria kikao hicho na kueleza kuwa, kamati yake iliitwa na Spika na malipo yalifanywa na Bunge.

Hatukumuomba mtu hela, sielewi lolote, sisi tuliitwa na Spika na malipo yetu yalishughulikiwa na Bunge,” alisema Shellukindo na kusisitiza kuwa, kanuni za Bunge zinaeleza wazi kuwa wabunge wanapokuwa katika vikao vilivyo na baraka za Spika, iwe bungeni au nje ya Bunge, posho na gharama zao nyingine zinalipwa na Bunge na si taasisi nyingine yoyote.

Alipoulizwa kuhusu hilo, Waziri wa Nishati na Madini, Ngeleja alieleza kuwa Tanesco ililazimika kulipa gharama hizo kwa wabunge licha ya kikao hicho kufanyika kwa ridhaa ya Spika, baada ya Bunge kueleza kuwa halikuwa na fedha kwa ajili ya kulipa posho na gharama za usafiri kwa wabunge.

Wakati wanasiasa hao wakivutana kuhusu mfumo huo wa ulipaji posho, Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashillilah, alipotafutwa na Tanzania Daima Jumatano
ili kutoa ufafanuzi wa jambo hilo, alieleza kuwa wabunge wote wanapokuwa katika shughuli za Bunge, ikiwamo vikao vya kamati za kudumu za Bunge, posho na gharama
zao nyingine zinalipwa na ofisi ya Bunge, na si vinginevyo.

Alisisitiza kuwa, Tanesco haiwezi kuliwalipa posho wabunge wakiwa katika kikao cha kamati ya kudumu ya bunge na kuongeza kuwa katika utumishi wake ndani ya taasisi hiyo, hajawahi kuona fedha za Tanesco zikitolewa kwa ajili ya kulipa posho wa wabunge.

CHANZO: Tanzania Daima

MHESHIMIWA SPIKA ANASEMA WABUNGE WA KAMATI HUSIKA WALILIPWA NA TANESCO.WAZIRI NGELEJA NAE ANATHIBITISHA HILO.MBUNGE SHULIKINDO ANAKATAA TAARIFA KUWA WALILIPWA JAPO SENTI TANO,NA KATIBU WA BUNGE ANAWEKA BAYANA TARATIBU ZA MALIPO KWA WANAKAMATI ZA BUNGE.
JE NANI MKWELI NA NANI ANAONGOPA?
JE ANAYEONGOPA ANAFANYA HIVYO KWA SABABU GANI?
SHERIA NA TARATIBU ZINASEMAJE KUHUSU KUONGOPA KWA AINA HIYO?
NA ADHABU GANI INATOLEWA KWA KOSA LA AINA HIYO?

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.