28 Aug 2010
27 Aug 2010
27.8.10
Evarist Chahali
HUTU, KAGAME, RWANDA GENOCIDE, TUTSI, UNITED NATIONS
No comments
Rais wa Rwanda Paul Kagame amechaguliwa tena kuongoza nchi hiyo baada ya kushinda kwa asilimia 93 katika uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni,lakini kulikuwa na taarifa zilizosambaa kuwa waandishi wa habari na wanasiasa wa vyama vya upinzani wameuawa au kuwekwa jela.Sasa,ripoti iliyovuja (leaked) ya Umoja wa Mataifa inaashiria kuwa jeshi la Rwanda linaweza kuwa limetenda uhalifu wa kivita na kuua makumi ya maelfu ya watu mwishoni mwa miaka ya 90 (late 1990s).
Kagame anaheshimika sana kwa kuleta maendeleo na amani kwa nchi hiyo iliyotiwa kovu na mauaji ya kimbari mwaka 1994 ambapo Wahutu (kabila kubwa nchini humo) waliwaua Watutsi (kabila dogo nchini humo)-na Wahutu wenye msimamo wa wastani- takriban milioni moja.Chini ya Kagame,ambaye ni Mtutsi na kamanda wa zamani wa jeshi,Rwanda sasa ni salama,huku ikitajwa kuwa miongoni mwa zenye rushwakidogo zaidi barani Afrika.Matokeo yake,nchi hiyo imekuwa ikipokea mamilioni ya dola katika misaada ya kimataifa na inaendelea kujijenga.
Lakini,kwa mujibu wa gazeti la New York Times,mmoja wa wapinzani wa Kagame alikutwa amekufa kabla ya uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 8 mwezi huu,huku kichwa chake kikikaribia kutenganishwa na kiwiliwili.Na wapinzani wengine "maarufu ambao waliongea hadharani kumpinga Kagame na pengine kuuweka majaribuni umaarufu wa Rais huyo walizuiliwa kushiriki katika uchaguzi",kwa sababu za kiufundi.Kagame amehalalisha hatua kali alizowahi kuchukua huko nyuma,kwa mujibu wa gazeti hilo,akidai kuwa Rwanda bado haijatulia vya kutosha.
Kwa jinsi gani hali nchi humo haijatulia inabainishwa na katika ripoti ya kamishna wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia haki za binadamu,iliyopatikana na gazeti la Le Monde la Ufaransa kabla haijachapishwa.Ripoti hiyo inabainisha,kwa mujibu wa gazeti la The Guardian la Uingereza,mwaka 1996 wakati vikosi vya Watutsi vikiwakimbiza Wahutu kuelekea Jamhuri ya Kimekrasia ya Kongo (wakati huo Zaire),na mwaka 1998 katika uvamizi wa kudhibiti waasi wa Kihutu,jeshi la Rwanda na washirika wake liliwazingira mamia ya wanaume,wanawake na watoto na kuwachinja kwa kutumia majembe na mashoka.Nyakati nyingine,"wakimbizi wa Kihutu walichinjwa kwa kutumia sime za bunduki,kuchomwa moto au kupigwa nyundo".Matukio hayo,inaeleza ripoti hiyo,ni sawa na mauami ya kimbari.
Serikali ya Rwanda amepinga madai ya ripoti hiyo,na inadaiwa imetishia kuondoa askari wake katika jeshi la kulinda amani huko Darfur na kwingineko,iwapo ripoti hiyo itawekwa hadharani rasmi.Umoja wa Mataifa unaeleza kuwa ripoti ililyovuja ni rasimu (draft) tu.Inasubiriwa kuonwa kama jumuiya ya kimataifa itasalimu amri kwa shinikizo kutoka serikali ya Kagame kuondoa mpambano na kupunguza makali ya lugha katika chapisho timilifu (final version).
Imetafsiriwa kutoka Jarida la Newsweek
| Sheria ni msumeno: Rais Kikwete akisaini kwa mbwembe Sheria ya Gharama za Uchaguzi,ambayo Chadema wanamtuhumu kuikiuka na hivyo wanamwekea pingamizi. |
Geofrey Nyang'oro na Lilian Mazula
SHERIA ni msumeno na sasa imgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete atalazimika kufanya kazi ya ziada isimdhuru baada ya Chadema kumwekea pingamizi rais huyo wa serikali ya awamu ya nne.Kikwete alisaini Sheria ya Gharama za Uchaguzi kwa mbwembwe mapema mwaka huu akitaka itumike mwaka huu, lakini Chadema imeitumia sheria hiyo kumwekea pingamizi, ikidai kuwa mgombea huyo wa CCM ameikiuka.
Katibu mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Kikwete amekiuka sheria hiyo kwa kwa kutangaza ongezeko la mishahara ya wafanyakazi wa sekta ya umma akiwa kwenye mikutano ya kampeni.
"Wanasheria wetu wanashughulikia suala hilo kwa kusaidiana na naibu katibu mkuu, John Mnyika kukamilisha pingamizi hilo na kesho (leo) asubuhi tutawasilisha pingamizi letu kwa msajili wa vyama vya siasa,"alisema Dk Slaa ambaye pia ni mgombea urais kwa tiketi ya Chadema.
Dk Slaa alidai kuwa Kikwete alikiuka kipengele cha 6, sehemu ya 21 (1) cha sheria hiyo inayotoa tafsiri ya mambo yanayokatazwa wakati wa mchakato wa uteuzi wa wagombea na kampeni za uchaguzi.
Alisema Kikwete amekiuka kifungu hicho kwa kutangaza ongezeko la mishahara ya wafanyakazi akiwa katika majukwaa ya kampeni, jambo ambalo linaweza kutafsiriwa na sheria hiyo kuwa ni rushwa ya uchaguzi.
Alieleza kuwa Kikwete amekiuka sheria hiyo kwa kuwa yeye kama mgombea, hana mamlaka ya kuongeza mshahara wa wafanyakazi katika kipindi hiki cha kampeni.
| Dokta Slaa |
"Kwa kutungwa kwa Sheria ya Gharama za Uchaguzi na kusainiwa Julai 17 mwaka huu pamoja na marekebisho yake, tulitegemea kungesaidia kuleta mabadiliko," alisema Dk Slaa ambaye kitaaluma amebobea kwenye sheria.
"Kitendo cha Kikwete kukiuka sheria hiyo kimenishtua sana.
Watanzania tungependa kupewa ufafanuzi; fedha hizo za (mishahara) zimetoka wapi na kwa mamlaka ya nani kwa kuwa wenye mamlaka ya kuidhinisha matumzi ya fedha za umma ni Bunge," alisema Dk Slaa.
Alifafanua kuwa kwa mujibu wa katiba, Bunge ndilo lenye mamlaka ya kuidhinisha matumizi ya fedha ikiwa ni pamoja na ongezeko la mishara kwa wafanyakazi wa umma.
"Kitendo cha serikali kuamuru ongezeko hilo nje ya vikao vya bunge, ni ukiukwaji wa sheria za nchi na ndio mwanya uliosababisha kutoweka kwa fedha za Akaunti ya Madeni ya nje(EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT)," alisema Dk Slaa.
"Sehemu ya tano ya sheria hiyo sura ya 21.-(1) inaweka bayana vitendo vinavyokatazwa wakati wa uteuzi wakati wa kampeni za uchaguzi na inasomeka:
"(a)Kila mtu ambaye kabla au wakati wa kipindi cha kampeni, moja kwa moja au kwa namna nyingine yoyote, kupitia kwa mtu mwingine yeyote au kwa niaba yake, anatoa, anakopesha au anakubali kutoa au kukopesha, au anatoa, anaahidi au kumpatia au anajaribu kumpatia fedha yoyote au kitu chochote chenye thamani,
mpiga kura au kwa ajili ya mtu yeyote kwa niaba ya mpiga kura yeyote au kwa ajili ya mtu mwingine yeyote kwa nia ya kumshawishi kupiga kura, au kuacha kupiga kura au kumrubuni mtu yeyote kutendo hicho kwa niaba ya mpiga kura huyo kupiga kura au kuacha kupiga kura katika kura za maoni au uchaguzi wowote;
"Kikwete alisema yeye mwenyewe hahitaji kura za wafanyakazi, na akasisitiza katika hotuba yake iliyoitoa kwa wazee wa Dar es Salaam kuwa serikali haina uwezo wa kulipa mishahara hiyo na kama wanafanya hivyo kwa kushinikiza kigezo cha kura, yeye hazitaki; leo mishahara imeongezeka, fedha hizo zimetoka wapi?Tunataka utueleze matumizi hayo ya fedha za umma kinyume na utaratibu."
Kwa mujibu wa Dk Slaa mgombea urais anapaswa kulinda katiba na sheria zilizopo, ili kulifanya taifa liendelee kuwa katika hali ya amani na utulivu katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.
Dk Slaa alisema kuwa kitendo cha rais kutumia nafasi hiyo kutangaza mishahara kwenye kampeni ni kujipa upendeleo kwa kushawishi watu kumpigia kura kwa kutumia nafasi aliyonayo.
Dk Slaa pia alitumia fursa hiyo kukemea kitendo cha kufanya maamuzi kwa kukiuka sheria zilizopo akieleza kuwa kufanya hivyo kunaweza kuhatarisha usalama wa nchi.
Dk Slaa pia alienda mbali zaidi na kuituhumu CCM kwamba imekiuka taratibu za uchaguzi kwa kutengeneza mabango yake ya mgombea nchini Canada.
"CCM wametumia Sh1.5 bilioni kutengeneza mabango nje ya nchi kwa kutumia fedha za serikali pia ankara ya malipo "invoice" inaonyesha imeandikwa 'VAT INVOICE' kitu ambacho hakieleweki," alisema Dk Slaa.
Alisema kuwa ni muhimu CCM kutoa ufafanuzi juu ya hilo kwa kuwa ushahidi upo na unaonyesha kuwa kuna mchezo mchafu umeanza kufanywa.
CHANZO: Mwananchi
27.8.10
Evarist Chahali
CYBER WAR, PENTAGON
1 comment
Inaelezwa kuwa vita vya mtandao (cyber war) ni tishio kubwa kwa Marekani kama ilivyo ugaidi.Na katika kujipanga vema kupambana na maadui wa nchi hiyo wanauweza kutumia mtandao kufanya mashambuli,Makao Makuu ya "Wizara" ya Ulinzi,Pentagon,imeanzisha mkakati wa kuajiri vijana wadogo wenye kipaji cha hali ya juu katika kuhujumu mtandao na kuufanya utekeleze matakwa ya mhujumu husika (hacking).
Katika kufanikisha zoezi hilo la kupata makuruta mwafaka,Pentagon ilisimamia shindano la uhujumu huo wa mtandao ambapo hackers vijana kadhaa walishiriki.Kichekesho ni kwamba katika kuonyesha uhodari wake katika fani hiyo,mmoj wa hackers hao alifanikiwa kuhujumu alama alizopewa na wasimamizi wa shindano hilo kabla matokeo hayajatangazwa.
26 Aug 2010
![]() |
| Rostam Aziz |
Katika kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005,mfanyabiashara controversial Rostam Aziz alitumia raslimali zake nyingi kuhakikisha mgombea wa nafasi ya urais kwa tiketi ya CCM,Jakaya Kikwete,anashinda kwa gharama yoyote ile.Na kutokana na utajiri mkubwa alionao pamoja na mbinu zake mbalimbali,mchango wake ulimsaidia sana Kikwete kuingia Ikulu,na sasa ni Rais wetu anayeomba tena ridhaa ya kutuongoza kwa miaka mitano ijayo.
Kati ya mwaka 2005 (baada ya Kikwete kuingia Ikulu) na sasa,Rostam ameibuka kuwa kiumbe mwenye nguvu za kutisha sio tu ndani ya CCM bali kwenye siasa za Tanzania kwa ujumla.Lakini kubwa zaidi katika kipindi hicho ni kwa mfanyabiashara huyo kuhusishwa na tuhuma mbalimbali za ufisadi na Kikwete na serikali yake kushindwa kuwaridhisha Watanzania kwamba "hamkumbatii swahiba wake huyo".Haihitaji kurejea namna Rostam alivyohusishwa na ufisadi wa EPA (Kagoda) na ujambazi wa Richmond.
![]() |
| Jakaya Kikwete |
Mwaka 2010,yaani mwaka huu,Rostam anaelekea kurejea tena ulingoni japo si kwa wazi sana.Ushahidi wa kimazingira unaonyesha kuhusika kwa mfanyabiashara huyo katika kampeni za Kikwete.Vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Rostam vimekuwa vikiendesha kampeni ya chuki dhidi ya mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dokta Wilbroad Slaa,mwanasiasa anayeonekana kuwa tishio kwa mfanyabiashara huyo na vitendo vyake dhidi ya maslahi ya taifa.
![]() |
| Magazeti yanayomilikiwa na Rostam |
Na kama hilo la vyombo vya habari vya Rostam kumuandama Dkt Slaa halitoi mwangaza wa kutosha basi taarifa kwamba mwandishi mwandamizi wa kampuni ya Habari Corporation (inayomilikiwa na Rostam),Muhingo Rweyemamu,anatajwa kuwa mratibu wa kampeni za Kikwete.Itakumbukwa kuwa mwaka 2005,waliokuwa waandishi waandamizi wa Habari Corporation,Salva Rweyemamu na Dokta Gideon Shoo walitumika sana kwenye kampeni hizo.Baada ya kuingia Ikulu,Kikwete "alimzawadia" Salva ukurugenzi wa habari wa Ikulu,nafasi anayoshikilia hadi sasa.
![]() |
| Muhingo Rweyemamu |
Kama alivyo Salva,Muhingo anasifika kwa uwezo wake wa hali ya juu wa kujenga hoja.Kwa bahati mbaya au makusudi,uwezo huo pia unatumika ipasavyo kutengeneza fitna.Wengi watakumbuka namna Dokta Salim Ahmed Salim,mmoja wa wana-CCM waliokuwa wanawania kuchuana na Kikwete,alivyoundiwa zengwe kubwa na kumhusisha na kundi la Hizbu la huko Zanzibar.Inaelekea kuwa mbinu hizohizo zimeanza kutumika dhidi ya Dokta Slaa,na kuna kila sababu ya kuamini kuwa kuna mengi yatakayoibuliwa dhidi yake.
![]() |
| Salva Rweyemamu (kushoto) na Gideon Shoo |
Yayumkinika kuamini kuwa waandishi wa habari wanaotumiwa kumchafua Dokta Slaa na Chadema kwa ujumla wanafanya hivyo kwa minajili ya "kupeleka mkono kinywani".Kubwa zaidi ni sapoti ya Rostam kwa Kikwete.Wakati mwaka 2005 alijibidiisha ili kufanikisha maslahi yake binafsi ya kibiashara (na amenufaika kweli-kwa kuangalia ishu za Kagoda na Richmond/Dowans) safari hii Rostam anahaha kumzuia Dokta Slaa kwa vile anafahamu fika kwamba laiti mwanasiasa huyo wa Chadema anayesifika kwa msimamo wake mkali dhidi ya ufisadi akiingia Ikulu,zama za mafisadi kutumia jeuri yao ya fedha "kuendesha serikali kwa remote control" itakuwa imefikia kikomo.
Kwahiyo,Dokta Slaa na Chadema kwa ujumla wanapaswa kuelewa kuwa safari hii Rostam ana "special mission" ya kuhakikisha "survival (kusalimika) yake.Atatumia kila raslimali aliyonayo kuhakikisha Dokta Slaa haingii Ikulu.Anafanya hivyo akifahamu wazi kuwa rais yeyote mwenye kujali maslahi ya nchi yake "atamkalia kooni" mfanyabisahara huyo na washirika wake.
Hata hivyo,kwa vile si fedha za Rostam au wanahabari wake zitakazopiga kura kwenye uchaguzi mkuu,bali mimi na wewe pamoja na kila Mtanzania aliyechoshwa kuona nchi yetu ikigeuzwa "shamba la bibi",ni muhimu kwa wapiga kura kusema HAPANA.Tusitoe fursa kwa watu wenye maslahi binafsi kuipeleka nchi yetu kwenye maangamizi.Na ni muhimu zaidi kutambua kuwa baadhi ya watu hao wana utata wa kutosha tu kuhusu asili ya mahali walipozaliwa.Hiyo inamaanisha kuwa "wakishaiingiza Tanzania kwenye mtaro",watakuwa na sehemu ya kukimbilia.
KILA MTANZANIA MWENYE KUITAKIA MEMA NCHI YETU ANAPASWA KUPAMBANA NA WAHUNI WA KISIASA WANAOTAKA KUTUWEKEA MADARAKANI VIONGOZI WANAOWAMUDU NA HIVYO KUENDELEA KUTUFISADI KAMA ILIVYOKUWA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA MITANO ILIYOPITA.
INAWEZEKANA,TIMIZA WAJIBU WAKO
26.8.10
Evarist Chahali
UCHAGUZI MKUU
2 comments
Na Frederick Katulanda, Mwanza na Sadick Mtuly
LICHA ya sheria na kanuni za Uchaguzi kuzuia matumizi ya magari ya serikali, msafara wa mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete umetumia magari kadhaa ya serikali katika mikoa ya Mwanza, Geita na Kagera.
Mbali na magari hayo, wakuu wa wilaya waliokuwa wameshiriki msafara wa mwenyekiti huyo wa CCM, walitumia magari yao ya kazi yakiwa yamewekwa namba binafsi huku wakivalia sare za chama hicho.
Ukiondoa magari maalumu ya walinzi wa mgombea huyo ambaye pia ni rais, magari mengine ya wakuu wa wilaya na wakuu wa idara mbalimbali za serikali, yalitumika na kuwekwa namba binafsi.
Kwa mujibu wa habari tulizozipata kutoka vyanzo vyetu zinaeleza kuwa hivi sasa Ikulu ya Dar es Salaam ina upungufu kwa kuwa wafanyakazi wa Ikulu hasa madereva pamoja na wapishi na wagawa vinywaji (waandazi), wanatumika katika kampeni za Rais Kikwete.
Wapishi na waandazi hao wamepelekwa mikoani kulingana na ziara za kampeni.
“Cha ajabu ni kuwa baadhi ya wafanyakazi wa Ikulu hasa madereva, wapishi na waandazi wanatumika katika kampeni za CCM kupitia Rais Kikwete.
“Wamegawanywa katika mikoa tofauti kulingana na ratiba za ziara za kampeni za rais,’’ kilisema chanzo chetu.
Juzi jijini Mwanza Mkuu wa wilaya Ilemela, Serenge Mrengo ambaye alifika majira ya saa 4:35 asubuhi uwanja wa ndege na gari lenye namba za STK 3551 huku wote wawili na dereva wake wakiwa wamevalia sare za CCM, lakini baada ya kusalimiana na viongozi wenzake, aliondoka.
Akiwa wilayani Geita, Mkuu wa wilaya hiyo Philemon Shelutete alitumia gari lake la serikali ambalo lilikuwa limebandikwa namba T 804 BCZ huku akiwa amevalia sare za CCM. Pia gari la Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Benson Katala lilitolewa namba za serikali na kubandikwa namba T 180 BKW.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro alitetea hatua hiyo akisema sio kosa kwa kuwa Kikwete bado ni rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzanania.
Kandoro, alikiri kutumika kwa magari hayo ya serikali na kusema kuwa viongozi hao waliyatumia kumpokea na baadhi yao waliambatana naye katika ziara hiyo kwa kuwa mbali na kuwa mgombea wa CCM pia anayo hadhi ya urais.
“Huyu ni Rais, amekuja kama kiongozi licha ya kwamba anagombea, bado hajavuliwa urais, sasa ma-DC walikuja kama viongozi wa serikali kumpokea rais. Kama kuna mkuu wa wilaya alivaa shati la CCM alivaa kwa sababu ya mapenzi yake kwa chama,” alifafanua Kandoro ambaye alitumia gari binafsi la kiongozi mmoja wa CCM Kanda ya Ziwa.
"Makosa ni kiongozi wa serikali kufanya kazi za chama na sioni kama kuna kiongozi wa serikali ambaye alifanya kazi za chama,"alisema
Msafara wa Kikwete kuambatana na magari ya serikali haukuishia Mwanza na Geita pekee bali pia hata mkoani Kagera ambako magari mengi yalikuwa na namba za STK.
Katika hatua nyingine, uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando umetoa ufafanuzi kwamba uamuzi wake wa kutoa gari la kubebea wagonjwa katika msafara wa mgombea urais wa CCM kuhakikisha usalama wa mgombea huyo.
Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Dk Charles Majinge alisema kwa kawaida jukumu la kutoa magari huwa lipo mikononi mwa uongozi wa mkoa ambao uliomba gari kwao na wao waliamua kutoa gari hilo la wagonjwa namba T 848 AWN.
“Sisi hatutoi ambulance kwa wagombea, ila tulitoa kwa Kikwete kutokana na kuwa ni kiongozi wa nchi. Kutoa magari huwa ni kazi ya uongozi wa mkoa, lakini sisi kama watalaamu wa matibabu tulichukua tahadhari na kuweka gari hilo,” alieleza Dk Majinge.
Alisema kwa vile akiwa jijini Mwanza aliwahi kuanguka, basi waliamua kuchukua tahadhari kuepuka kukosa huduma haraka iwapo jambo hilo lingejirudia akiwa mbali na hospitali ya rufaa.
Akizungumzia gari hilo, Kandoro alisema uwapo wake ni utaratibu wa kawaida katika misafara ya viongozi wa serikali.
“Huu ni utaratibu wa kawaida katika misafara ya viongozi, tumetoa kama utaratibu wa kawaida….unajua huyu ni kiongozi wa nchi, sasa unataka wakija na wagombea wengine wa upinzani nao tuwapatie magari ya wagonjwa, wao ni akina nani?” alieleza na kuhoji Kandoro ambaye pia aligombea kura za maoni kuwania kuteuliwa na CCM kuwa mgombea ubunge Jimbo la Kalenga na kushindwa.
Akizungumza kwa sharti la kutotaja jina gazetini mmoja wa viongozi ambao walikuwa wakishughulika na kuratibu msafara huo alieleza kuwa gari hilo la wagonjwa ni lile ambalo lilitolewa na serikali ya Ujerumani chini ya ushirikiano wa Jiji la Mwanza na Wurzburg.
“Gari hili liliandaliwa kutokana na maofisa wa usalama kuliomba na hili agizo limetolewa katika mikoa yote ambako atafika, kwani katika kampeni anakuwa amekwenda hadi katika wilaya ambazo haina hospitali na ikitokea dharura akimbizwe haraka hospitali huku akiendelea kupatiwa matibabu” alieleza kiongozi huyo wa chama.
Hata hivyo, alisema gari hilo wao kama chama hawakuambiwa wala kuelekezwa kulilipia kwa vile ofisi ya mkoa ilisema watachukua wao katika hospitali ya Bugando, baada ya kuwasiliana na ofisi ya mganga mkuu wa mkoa.
CHANZO: Mwananchi
USHAURI: Imefika wakati sasa kukomesha uhuni huu wa CCM dhidi ya Watanzania hususan wale wasio wanachama wa chama hicho tawala.Matumizi yoyote ya mali za umma zinazogharamiwa na walipakodi pasipo kujali itikadi za vyama zao ni ubadhirifu wa wazi.Haitowezekana kuwa na uchaguzi huru na wa haki iwapo raslimali za taifa zinatumika kwa manufaa ya chama tawala,tena pasipo ridhaa ya walipakodi.Wito wa blogu hii kwa kila mpenda haki na usawa ni kuuweka wazi uhuni huu kwa dunia ili ifahamike mapema kuwa CCM inatengeneza mazingira ya kuhujumu uchaguzi mkuu ujao.
TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA
25 Aug 2010
Hongera nyingi kwako Mzee wa Changamoto Yetu kwa blogu yako kutimiza umri wa miaka miwili.Ama kwa hakika blogu yako ni miongoni mwa sehemu zinazofanya kuweko mtandaoni kuwa ni jambo la muhimu katika maisha yetu ya kila siku.Hekima na filosofia zako zinaamsha tafakuru kubwa,huku ukihakikisha tunamwayamwaya na burudani ya miziki mbalimbali.Kwa hakika,Changamoto Yetu ni miongoni mwa sababu zinazonifanya niendelee kupenda fani ya kublogu.
Kila andiko lililowekwa kwenye blogu yako katka kipindi hiki cha miaka miwili kimekuwa na manufaa makubwa kwa jamii.Ni dhahiri kuwa kila unapoandaa andiko la kuweka bloguni hapo unakuwa na picha ya sie wasomaji wako akilini na hivyo kufahamu maswali,kiu,mshawasha,na matamanio au mahitaji yetu mengine.
Kukupa sifa unazostahili inahitaji chapisho kubwa zaidi ya thesis ya PhD.Naomba pongezi hizi fupi ziwakilishe stahili zako zote kutokana na kazi mwanana unayoifanya kwa jamii.
Again,Hongera Sana na Happy Birthday.
- Body had multiple stab wounds and was decomposing
- Flat owned by private company called New Rodina, which means 'motherland' in Russian
- Acting PM Clegg to be briefed on spy's death today
- Dead man was employed at govt 'listening post'
This is the first picture of the murdered British spy who detectives have said could have been killed up to two weeks ago.The body of Gareth Williams, 31, was discovered stuffed in a large sports bag in his bath in a flat just a few hundred yards from the headquarters of MI6.It is understood Mr Williams had been stabbed, possibly several times, and his body was decomposing when it was found.
Elsewhere in the top-floor flat - in a bizarre ritualistic scene - his mobile telephone and a collection of SIM cards were carefully laid out.Scotland Yard has launched a murder inquiry into the grim find in Pimlico, Central London. Detectives have told local residents today that the murder may have taken place two weeks ago.
Mr Williams was employed as a communications officer at the Government's ' listening post' - better known as GCHQ in Cheltenham, Gloucestershire.But it is thought he was on secondment to the headquarters at MI6, the Secret Intelligence Service, near the flat.MI6 gathers secret information about Britain's overseas enemies, making the spy a possible target of terrorists
![]() |
| Mr Williams was employed as a communications officer at the Government's ' listening post' - better known as GCHQ (pictured) in Cheltenham, Gloucestershire |
Mr Williams was described by neighbours as mild-mannered and a keen cyclist. He joined the University of Cambridge in 2000 to undertake a postgraduate certificate in advanced studies in mathematics but dropped out.
'I'm told the man lived at the top-floor flat but we haven't ever seen him. It's not like you'd tell your neighbours if you were a spy'
A spokeswoman said he was a member of St Catharine's College but left without completing the qualification the next year.The course is described as 'demanding' and normally only accepts students with first-class degrees in physics, mathematics or engineering.He lived in a street where houses sell for more than £1million, and it has been cordoned off at both ends since Monday night. Access is being granted only to residents.
The street remained cordoned off this morning and police officers stood outside No 36, which is divided into three flats.Land Registry documents revealed the block at number 36 is owned by a private company, New Rodina.Its details are hidden because it is registered in the British Virgin Islands and is not listed with Companies House.The word rodina means 'motherland' in Russian and Bulgarian.The property was bought for £675,250 in 2000 with a mortgage from the Royal Bank of Scotland and has been remortgaged twice, in September 2005 and February 2006.
The documents revealed the owner operated through a law firm known as Park Nelson. The firm once occupied a rented office block in Bell Yard, off Fleet Street, but no longer appears to exist.Curtains were drawn in the top-floor flat, where it was believed the attack took place.Public documents revealed that several current and former residents of the freehold block have links to London and Cheltenham.
Police continued to scour the two-floor flat for evidence today and cordons remained in place on the prestigious street where two former home secretaries live.Ex-Tory leader Michael Howard and Sir Leon Brittan are among a host of politicians and bankers who have homes there, residents said.Mr Howard, who lives several doors down the road, was at home when the body was taken away by forensic officers, one resident, Andy Perkins, said.Neighbour Laura Houghton said Mr Williams was an 'extremely friendly' man.The 30-year-old secretary said: 'I have spoken to him only once. I met him in the entrance hall of the set of flats because of a boring plant issue about a year ago.
'He was extremely friendly and had a Welsh accent.'
She said he had an athletic build, and added: 'He was not especially tall. He had medium to short brown hair.'
Mrs Houghton added: 'His windows were always shut and curtains were often closed. I could never tell if anyone was in.
'It was strange that we never saw him come and go. I just assumed he worked away.
'The first I heard of anything happening was when the police knocked on my door and asked me if I had heard anything happening. I told them the walls were so thick that I couldn't hear a thing.
'All they told me was that there had been a serious incident. I'm amazed it's taken this long to all come out.'
A landlady who rented Mr Williams a flat in Cheltenham, said: 'He was polite and mild-mannered and wouldn't hurt a fly. He was forever off on bike rides but never really had friends around.
'Sometimes you could hear tapes whirring from his flat. It must have been audio cassettes he used for work. He never told me what they were.'
Eileen Booth, 73, who lives opposite, said detectives told her the murder may have taken place two weeks ago.She said: 'A few years ago, I would definitely have known who it was that had been killed.
'Detectives came round and asked for our eye colour and height. They said this probably happened two weeks ago.'
Rob Mills, 35, who lives two doors away, said today: 'We've got two children - it's shocking.
'I'm told the man lived at the top-floor flat but we haven't ever seen him. It's not like you'd tell your neighbours if you were a spy.'
Jason Hollands, 41, a City worker, who also lives nearby, said: 'It's truly gruesome - this is a very mixed area of bankers and politicians. I've spoken to the next-door neighbour, who knew nothing.'
![]() |
The one bedroom flat in Cheltenham where Gareth Williams also lived |
The case is being investigated by officers from the Murder Squad with assistance from their counter-terrorist and security service colleagues. No arrests have been made.Forensic teams are continuing to search for clues at the five-storey terraced townhouse.A Met Police spokesman said: 'Officers were called to reports of a suspicious death at 4.40pm on Monday. They attended a top floor flat in Alderney Street and gained entry and found the body of a man in his 30s.'
One resident said: 'My neighbours said it was a stabbing.It sounds like it was really gruesome.'
Scotland Yard said no cause of death was known. A post-mortem examination is due today.
A Downing Street spokesman refused to comment, saying: 'Any potential case is a matter for the police.' Details of the incident will be contained in the Prime Minister's intelligence briefing which will be handed to Deputy Prime Minister Nick Clegg today. David Cameron is also expected to be kept abreast of developments.
A Foreign Office spokesman said: 'There is an ongoing police investigation.
'It is long-standing Government policy not to confirm or deny that any individual works for the intelligence agencies.'
Patrick Mercer, former chairman of the Commons counter-terrorism subcommittee, said: 'This underlines the danger that our outstanding security services have to face on a minute-by-minute basis every single day.'
The last spy to have been killed on British soil was former Russian Federal Security Service officer Alexander Litvinenko in November 2006. He was poisoned with polonium-210.
Bulgarian defector Georgi Markov was killed by an assassin who used an umbrella to fire a ricin pellet into his leg as he crossed Waterloo Bridge in September 1978.A spokesman said the body was yet to be formally identified.A post-mortem examination is due to take place today.
SOURCE: Daily Mail
Subscribe to:
Comments (Atom)




.jpg)















