26 Dec 2010





Kwa mara ya kwanza kabisa,nalazimika kumpongeza Mbunge wa Monduli kwa tiketi ya CCM,Edward Lowassa.Tuweke kando ishu nyingine ambazo blogu hii zimepelekea kumshutumu kiongozi huyo mara kwa mara,hadi kufikia hatua ya aliyekuwa Mwandishi wake wa habari (Press Secretary),Bwana Said Nguba,kutoa comments bloguni hapa kumtetea bosi wake wa wakati huo (Lowassa).

Majuzi,Lowassa alitoa wito kwa chama chake cha CCM na Chadema wakae pamoja kutafuta mwafaka kuhusu sakata la umeya wa Arusha.Waziri Mkuu huyo wa zamani alifanya kile kiongozi yoyote anayejali maslahi ya umma anachopaswa kufanywa kwa kuweka kando itikadi za kisiasa na badala yake kutilia mkazo umuhimu wa kupata mwafaka katika sakata hilo la umeya wa Arusha.Lowassa alionya kwamba kama hatua za haraka na za makusudi hazitachukuliwa basi kuna hatari ya kuzalisha 'Ivory Coast nyingine ndani ya Tanzania yetu' akirejea hali tete inayozidi kusumbua katika taifa hilo la Afrika Magharibi baada ya Rais aliyemaliza muda wake na kushindwa uchaguzi mkuu kugoma ''kuachia ngazi".

Lakini wakati baadhi yetu tukivutiwa na uzalendo wa Lowassa,akaibuka mmoja wa wanasiasa wenye rekodi nzuri ya kubwatuka na "kusema ovyo",Katibu Mkuu wa CCM,Yusuph Makamba.Kiongozi huyo mwenye rekodi ya uropokaji alimvaa Lowassa akidai amekosea kusema aliyosema kwani hayo yalipaswa kujadiliwa kwenye vikao vya chama hicho tawala.Sina hakika kama Makambaanatumia kilevi cha aina yoyote lakini mchemsho huu wa safari hii unapaswa kuwa "wake up call" kwa (Mwenyekiti wa Taifa wa CCM),Rais Jakaya Kikwete,kwamba Makamba anastahili kupatiwa msaada wa kuchunguzwa akili yake.Ni mpuuzi asiye na mfano ambaye kwake usalama wa wakazi wa Arusha una umuhimu mdogo kulinganisha na taratibu za chama hicho tawala.Angalizo aloloyoa Lowassa kuwa Arusha inaweza kugeuka Ivory Coast halikuweza kuingia kwenye ubongo wa Makamba,sio kwa vile haelewi umuhimu wa political consensus bali kwa vile kwa akili yake nayohisi ina mapungufu kitendo cha CCM kukaa kitako na Chadema ni sawa na kuvunja Amri ya Mungu.

Mpuuzi huyu amesahau kuwa mgogoro mkubwa wa kisiasa visiwani Zanzibar ulimalizwa baada ya CCM na CUF kuweka mbele maslahi ya taifa na kukaa pamoja kutafuta mwafaka wa kudumu.Na kwa tunaokumbuka kauli za kitoto za Makamba katika nyakati tofauti za jitihada za CCM na CUF kutafuta mwafaka huko Zanzibar,yayumkinika kuamini kuwa suluhu hiyo isingepatikana laiti mwanasiasa huyo "angepewa rungu" la kupitisha maamuzi ya mwisho.

Kwa akili yenye mapungufu ya Makamba,vyama vya upinzani ni mithili ya wanyama wasiopaswa kuwepo nchini.Ni sahihi kusema kuwa laiti CCM ingekuwa ile ya Baba wa Taifa,basi Makamba asingepewa hata fursa ya kuwa Mjumbe wa Nyumba Kumi.Inakuwaje kiongozi wa kitaifa wa chama tawala haoni umuhimu wa kutafuta ufumbuzi wa haraka wa matatizo yanayoendelea huko Arusha?Haihitaji PhD ya Siasa kutambua kuwa anayemlea Makamba ni Kikwete ambaye anakiendesha chama hicho kwa mtindo wa "bora liende".Na Kikwete asipoamka kutambua kuwa CCM inazidi kujiweka mbali na wananchi,si ajabu chama hicho kichovu kikamvunjikia kabla hajamaliza muda wake hapo 2015.Mwenyekiti gani asiye na ujasiri wa kumwambia Katibu wake kuwa achunge mdomo wake?

Enewei,tuweke kando tofauti zetu na tusapoti mawazo ya busara ya Lowassa kuhusu umuhimu wa kutafuta suluhu huko Arusha.Sambamba na hilo,tumpuuze Makamba na pengine tumshauri aruhusu ubongo wake uwe na mawasiliano na mdomo wake kabla hajaropoka jambo lolote lile.

24 Dec 2010


Majuzi,msomaji mmoja wa blogu hii alinitumia maoni ambapo pamoja na mambo mengine aliashiria kuwa nina chuki dhidi ya Rais Jakaya Kikwete.Msomaji huyo aliyejitambulisha kuwa mkazi wa hapa Glasgow alidai (namnukuu) "...I know you hate JK because whatever happens to him you have a negative view, even a tyre puncture...",yaani kwa Kiswahili,"najua unamchukia JK kwa vile chochote kinachotokea kwake wewe una mtizamo hasi,hata pancha ya tairi".Hii ndio mitizamo ya Watanzania wenzetu ambao licha ya kubahatika kuwa nje ya nchi,hususan nchi zilizoendelea kama hapa Uingereza,bado wana mitizamo mgando ambayo kwa kiasi kikubwa imechangia kutufanya hata miaka 49 baada ya uhuru kutamani mkoloni arejee.

Yah,huwezi kuwalaumu wanaotama mkoloni arejee japo mie si mmoja wao.Hivi tunawezaje kuelezea namna Watanzania wanavypelekeshwa kama watoto wadogo tena yatima siku chache tu baada ya Kikwete na CCM yake kupita huku na kule kuahidi neema,only for madudu and more madudu kuibuka kila kukicha?Unajua,angalau mkoloni alipotupelekesha alikuwa na excuse (japo isiyokubalika) kwamba yeye hakuwa Mtanganyika,na hakuwa na uchungu na nchi yetu.Na kwa wanaokumbuka vizuri somo la historia wanafahamu bayana kuwa ujio wa mkoloni ulikuwa kwa minajili ya kuendeleza nchi zao za asili,yaani kukwapua raslimali zetu kwa ajili ya viwanda vyao,kupata masoko ya bidhaa zao na eneo la makazi kwa nguvukazi ya ziada katika nchi hizo za wakoloni.Sasa ondoa neno mkoloni kisha weka neno FISADI,na yayumkinika kuhitimisha kuwa angalau mkoloni alikuwa na ajenda ya maendeleo huko kwao japo at our expense.Mafisadi nao wana ajenda za maendeleo pia,ila ni katika kutunisha akaunti zao kwenye mabenki ya hukohuko kwa wakoloni,kuongeza idadi ya nyumba ndogo zao (isomeke ufuska au uzinzi),kuongeza idadi ya mahekalu yao na magari ya kifahari,na sasa ajenda mpya ya kuimarisha himaya zao kwa kutumbukiza kila mwanafamilia na ndugu wa karibu kwenye siasa ili pindi baba akiondoka madarakani basi mwana amrithi kuzuia uwezekano wa baba mtu kukaliwa kooni kwa madudu aliyofanya akiwa madarakani.

Nimelazimika kuandika makala hii sio kwa minajili ya kumjibu huyo msomaji wangu wa hapa Glasgow bali ni baada ya kusoma toleo la mtandaoni la gazeti la Mwananchi ambapo kuna habari kuwa Tanesco wametangaza tena mgao wa umeme nchi nzima.Hivi sio majuzi tu shirika hilo lilitangaza mwisho wa mgao wa umeme?Tuwe wakweli,hivi uhuni huu wa Tanesco,ambao mie natafsiri kuwa ni uhuni wa serikali iliyopo madarakani,utaendelea hadi lini?So far,hakuna taarifa za wazi kuhusu athari za mgao wa umeme lakini haihitaji sayansi ya roketi au dissertation ya quantum physics kumaizi kwamba mgao huo una madhara makubwa mno kwa uchumi wa taifa na kwa maisha ya walalahoi kwa ujumla (vigogo licha ya kunufaika na ufisadi unaowawezesha kuuza jenereta kila mgao unapotangazwa lakini pia hawaathiriki kwa vile majumbani na maofisini kwao kuna jenereta zinazoendeshwa na fedha za kodi za walalahoi).

Hatuwezi kuilaumu Tanesco pekee kuhusiana na uhuni huu kwani ni siri ya wazi kuwa shirika hilo na sekta ya nishati kwa ujumla vimegeuzwa kitegauchumi kizuri kwa mafisadi.Majuzi tu tumesikia majambazi wa Richmond wakijiandaa kurejeshewa fedha walizotuibia ambapo watalipwa fidia ya mabilioni kwa mgongo wa binamu zao wa Dowans.Hatuwezi kumwepusha Kikwete na CCM yake na ufisadi huu kwa vile licha ya madudu hayo kushika hatamu wakati wa utawala wake,sasa tunafahamu kuwa amekuwa akiwakingia kifua mafisadi wasichukuliwe hatua za kisheria (thanks to nyaraka za siri za kidiplomasia zilizovujishwa na mtandao wa WikiLeaks).Kwa wale ambao hawajabahatika kusoma habari hizo,kuna nyaraka kutoka ubalozi wa Marekani hapo Dar zilizobeba maongezi kati ya bosi wa Takukuru Edward Hoseah na afisa ubalozi wa Marekani ambapo Hoseah alinukuliwa akieleza bayana kwamba Kikwete alishinikiza baadhi ya mafisadi wasichukuliwe hatua.Japo bosi huyo wa Takukuru amejaribu kuruka kimanga na kukana tuhuma hizo,kila mwenye akili timamu anafahamu kuwa ufisadi unashamiri Tanzania kwa vile Kikwete ameshindwa kuwachukulia hatua mafisadi papa licha ya madaraka lukuki aliyorundikiwa na Katiba.

Baadhi yetu tuliwaasa Watanzania wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita majuzi kwamba kuirejesha tena madarakani serikali ya Kikwete ni sawa na kumwaga chumvi kwenye kidonda kibichi,na matokeo yake ndio haya.Wakati tunaelekea mwezi wa pili tangu Kikwete atangazwe mshindi,hakuna lolote la maana lililokwishafanyika kuashiria kuwa kiongozi huyo ana ajenda mpya tofauti na zile zilizotawala miaka mitano iliyopita,kubwa ikiwa na kushamiri kwa ufisadi na uimarishaji himaya za mafisadi huko nyumbani.

Sawa,makosa yameshafanyika kwa kumrejesha Kikwete na CCM yake madarakani lakini hiyo isiwe sababu ya kuendelea kunung'unika kimoyomoyo huku nchi yetu ikizidi kuteketea.Umefika wakati Watanzania wasikubali kupelekeshwa namna hii.Kwanini Kikwete asibanwe kuhusu tatizo la umeme licha ya ahadi zake za mara kwa mara kuwa tatizo hilo lingekuwa historia?Au alimaanisha kuwa tatizo hilo litaendelea kuwa la kihistoria?

Nimesikia taarifa za mpango wa Chadema kuandaa maandamano ya nchi nzima kupinga kuongezwa bei ya umeme.Yaani licha ya mgao wa kila kukicha bado Tanesco wanataka kuongeza bei?Yayumkinika kuhisi kuwa wazo hilo la ongezeko la bei ya umeme ni la kifisadi lenye lengo la kupata fedha za kuwafidia mafisadi wa Richmond/Dowans.Ni muhimu kwa kila Mtanzania mzalendo kuunga mkono mpango huo wa maandamano ya amani ili kufikisha ujumbe kwa Kikwete na serikali yake kuwa Watanzania wamechoka kupelekeshwa.Hata hivyo,kama maandamano ya kuwapongeza wabunge wa upinzani yalizuiliwa na polisi,sidhani kama serikali itaridhia maandamano hayo ya kupinga ongezeko la bei ya umeme.

Mwisho,tuna choices mbili tu:kuchukua hatua sasa kabla hatujafika mahala ambapo hata tukichukua hatua itakuwa sawa na kutwanga maji kwenye gunia,au tusubiri kusoma rambirambi kuhusu nchi yetu hapo 2015.

22 Dec 2010



Picha kwa Hisani ya Mjengwa

Japo haipendezi kuona jeshi la polisi likitumia nguvu kubwa kuzuwia haki ya kikatiba ya wananchi kuandamana au kugoma kwa amani,lakini nashawishika kutowaonea huruma wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma kufuatia kichapo walichopewa na askari wa FFU.Hivi sio hawa wana UDOM waliochangisha fedha kwa ajili ya kampeni za Jakaya Kikwete?Na sio hawa waliotoa tamko la kukemea haki ya kikatiba ya wabunge wa Chadema kususisa hotuba ya Kikwete huko Bungeni?

Najua si vyema kutoa lawama za jumla kwani si kila mwana-UDOM aliafiki wazo la kujikomba kwa Kikwete lililopelekea wanafunzi hao kuchangia fedha zao za ngama ili kumwezesha mwanasiasa huyo aliyekuwa mgombea wa CCM arejee madarakani.

Na kama tulivyoandika baadhi yetu wakati wa kampeni za uchaguzi wakati tunaonya madhara ya kuirejesha CCM madarakani,haijachukua muda kwa  Kikwete na serikali yake kuwalipa fadhila wasomi hao wa Dodoma.

Majuzi nilimsuta mwanahabari mkongwe Dunstan Tido Mhando baada ya kupata taarifa kuwa serikali imemtosa ubosi wa TBC.Nilimsuta kwa vile naamini wakati Tido anaombwa na WALIOMUOMBA kuja kuendesha TBC alikuwa anafahamu fika kuwa aidha anapanda mchicha au bangi,na mavuno yangekuwa mchicha au bangi,respectively.Ukikubali kutumiwa lazima ukubali kitachotekea itapojiri "expiry date" yako.

Sasa tunashuhudia kundi jingine la walioingizwa mkenge.Hawa wasomi watarajiwa wa UDOM walijikomba kwa Kikwete na CCM na kuchangia kampeni zake,sijui wakitarajia kuwa pindi mwanasiasa huyo akirejea Ikulu angewapatia muujiza gani sijui!

MLIPANDA BANGI SASA MNATARAJIA KUVUNA MPUNGA?

17 Dec 2010



So the infamous Dunstan Tido Mhando is gone!I was a bit shocked to learn that,not because he did or did not deserbe the boot,but rather the fact the the guy had been running TBC as if it were an extension of the CCM-owned Radio Uhuru.You wouldn't blame him,would you?He had to serve his masters in the government who shamelessly disregard the fact that state-run bodies are funded by all Tanzanian taxpayers (minus mafisadi,of course) regardless of their politicwl affiliations.

Tido has simply been used and abused.I'm sorry to say this but anyone,journalists included,who allow themselves to be used by some unscrupulous politicians could find themselves deemed useless once their service is no longer required.We all are aware of how,for instance, our artists attract inexplicable attention from our politicians come elections,only to hear the same cries of "tumesahauliwa" after the elections.Our ever important politicians can't afford to be seen sorrounded by a bunch of wana bongoflava.They had afterall done their job and got paid,so no more reasons for them to hang around with such important people in our society.

Of course we could blame such selfish crooks who never shy away from taking for a long ride whoever willing to attend to their needs but I think the latter deserve a share of such blames simply because they wouldnt be on the receiving end of such dirty games had they resisted being manipulated in the first place.Njaa?kujikomba?Blind faith?or sheer stupidity?

Back to poor Tido,he just reaped what he had sewn.I simply don't get it when I hear some people suspecting that his removal would bring TBC back to the 'Radio Tanzania era'.What they overlook is the fact that before he took the TBC post,Tido was working with one of the best,and hugely transparent,media house in the world,The British Broadcasting Corporation (BBC).Some people.Some of us expected that Tido would have brought "the BBC effect" to Tanzanian media but you and I know how he fared.Of course,I understand it wouldn't have been easy for him to transform an exceedingly biased,pro-ruling party state-owned media into an independent,fair and balanced organisation but at least he could have tried.Praising him for allowing opposition parties candidates to take part in "Jimbo kwa Jimbo" is totally missing the point.Why?Because that's actually what a public funded media organisation is supposed to do.Let us not forget what TBC behaved when Chadema inaugurated their general election campaign.And who was TBC's top boss when that was happening?

Rumour has it that Tido was brought to TBC by a certain bigwig who's currently not in the government.If such rumours are true,then why should we feel sorry for someone who got the job not on merit but rather because someone out wanted Tido at the helm of TBC for the bigwig's personal interests to be realised?

I just hope Tido has learned a lesson that political conmen would never hesitate to use and abuse anyone who is willing to be manipulated.For these cons,any tesource is like a condom: needed before and during sex,but something to disposed of immediately after the act.It's my hope that a decorated professional like him would never again allow any politician to take him for a stepping stone.There were some rumours that a certain fisadi who's aspiring to vie for the presidency in 2015 was planning to recruit Tido as his proposed TV/radio chief.If the rumours eventually turn out to be true in the future,and Tido grabs the offer,then we surely haven't seen the end of saddening chapters in Tido's professional life.

16 Dec 2010

Soma stori yake HAPA

15 Dec 2010

NIMETUMIWA NA WADAU,NAMI NAIWASILISHA

Kwanza napenda kukusalimu sana na kukupa hongera sana kwa kazi ambayo umeendelea kuifanya katika blog site yako big up sana...Tulikua tunaomba ututambulishie hii trak yetu mpya ni ya X-mas and New year special. Natanguliza shukurani zangu kwako. Asante sana.



UMABE GENERAL MANAGER: AZMA MPONDAPRODUCED BY: KITA
STUDIO: RAMA RECORDS
PROJECT AND DESIGN: FREDY NJEJE
COUNTRY:TANZANIA
+255712738888
MAY GOD BLESS U ALL!! PAMOJA SANA.
EMAIL: [email protected] &[email protected]
WEBSITE:  http://umabeartscompany.blogspot.com

Tunatanguliza shukurani
 Zetu....

12 Dec 2010



Majuzi kulifanyika uzinduzi wa kitabu kinachoelezea wasifu wa Rais Jakaya Kikwete.Tukio hilo linaelekea kuwa na uzito wa kipekee kwani baadhi ya picha zilionyesha sehemu kubwa ya familia ya mkuu huyo wa nchi ilihudhuria uzinduzi huo.Sina hakika kuhusu kilichomo kwenye kitabu hicho lakini yayumkinika kuamini kuwa laiti wasifu huo ungegusia masuala kama "Wanamtandao na mchango wao katika ushindi wa Kikwete 2005",au "Uswahiba kati ya Kikwete,Lowassa na Rostam Aziz na jinsi unavochangia kufilisika kwa Tanzania", au "wasifu wa wateuliwa mbalimbali wa Kikwete na namna wanavyohusiana nae",nk isingekuwa rahisi kwa Rais Kikwete kujitokeza kwenye uzinduzi huo.

Mwandishi wa kitabu hicho ni Profesa Julius Nyang'oro.Wakati mwingine najiuliza kama baadhi ya maprofesa wa aina hii wameishiwa na mada za muhimu kwa jamii na badala yake wanageukia kujikomba kwa watawala kwa kuandika wasifu mithili ya pambio.Unaweza kunilaumu kwa kutoa tuhuma kabla sijasoma kilichomo katika kitabu hicho.Hata hivyo,huhitaji upeo wa juu kubashiri yaliyomo katika kitabu hicho,maana laiti ingekuwa ni wasifu wa Kikwete huyu ambaye utawala wake umetuzalishia msamiati wa "ufisadi",sambamba na kugubikwa na ishu za Kagoda,EPA,Dowans,Richmond na uzururaji njeya nchi,basi si mkulu huyo wala wanafamilia yake wangetia mguu kwenye uzinduzi huo.

Sasa sijui Profesa Nyang'oro kajaza nini kwenye wasifu huo!Mamia ya ahadi za Kikwete na kisha kuichambua moja baada ya nyingine ( kwa mtizamo chanya usiomuudhi mtawala) au ni hadithi za namna Jakaya alivyozaliwa katika familia ya kawaida,akajiendeleza pasipo makeke,akashika hatamu za uongozi lakini akiendelea kuwa "mtu wa watu" na hatimaye akapata urais ( bila kutaja mchango wa wanamtandao) na ameendelea kuwa mwenye upendo na upole sio kwa walalahoi pekee bali hata mafisadi.

Huenda wasifu huo pia ukagusia udaktari wa falsafa (wa heshima) wa Rais Kikwete.Inawezekana atapomaliza miaka yake 10 hapo 2015 (na kama hatafanya mbinu za kutaka aongezewe muda madarakani) ataweka historia nyingine ( on top ya ile ya kumpiku Vasco da Gama kwa safari) ambapo atakuwa kiongozi pekee aliyezawadiwa shahada nyingi za uzamifu kuliko mwingine duniani.Sijui mpaka sasa ana PhD ngapi,ila nakumbuka ile ya Uturuki,nyingine sijui ya Uganda kama sio Kenya,hii ya juzijuzi Dodoma na Muhimbili nao wamemzawadi shahada ya Afya ya Jamii.


Na kwa vile utawala wa Kikwete umetawaliwa na usanii wa namna flani,yayumkinika kuhisi kuwa hizo PhDs zinatolewa baada ya wahusika "kupigwa somo" au "kupewa kilicho chao".Ungeweza kuhisi kuwa ilikuwa hivyo hata Profesa Nyang'oro,lakini "mnyonge mnyongeni haki yake mpeni" hapo itakuwa mtu tu kaamua kujikomba.

Na kama ilivyozoeleka,wanahabari wetu (pamoja na baadhi ya mabloga) walichokumbuka ni picha za tukio na maelezo ya picha hizo (captions) tu,utadhani kwa kuangalia picha hizo msomaji atapata summary ya jumla ya kilichomo katika kitabu hicho.Hapa "simpigi mtu dongo" ila natoa changamoto kwa wenzetu mliobobea kwenye picha,mkumbuke kuwa picha pekee si habari kamili.Hivyo,inapowezekana mtupatie habari zaidi ya picha husika.Ni ushauri tu,tena wa bure buleshi.

Nakumbuka mwaka 2005 kulikuwa na kitabu cha wasifu wa Kikwete.Nahisi hapa katikati kuna waliojipendekeza na kuja na wasifu mwingine.Sasa tuna wasifu huu "mpya" kutoka kwa Profesa Nyang'oro na huenda hapo 2015 kutakuwa na wasifu mwingine wa "miaka 10 ya mafanikio ya kihistoria chini ya utawala wa Jakaya Kikwete".Mtu mmoja wasifu kibao!

Enewei,hiyo ndio Tanzania yetu.Na ukiwa na kiongozi mpenda sifa basi wajanja hawachelewi kumpamba kwa sifa hii au ile.Na kwa vile hawagusii yale yatakayomfanya mtawala atambue kuwa "hajafunga zipu" basi kwa upande mmoja watoa sifa hao wanapata wanachotegemea kupata (sifa,hela,kupiga picha na rais,kualikwa ikulu,na pengine kuzawadiwa U-DC) na kiongozi mpenda sifa anaendelea kuamini yeye ni chaguo la Mungu ndio maana sifa zinaendelea kumiminika kumhusu yeye.



WAKATI biashara ya magogo ikiendelea kutikisa vichwa vya viongozi wa serikali, imebainika kuwa mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, kada wa CCM, wakuu wa polisi na maafisa wa Takukuru ndio wanaomiliki vibali vya kuvuna magogo katika msitu wa serikali wa Sao Hill ulio wilayani Mufindi.Biashara ya magogo ambayo ilishamiri mwaka 2005/06 ilipigwa marufu baada ya kuonekana kasoro kwa wasafirishaji magogo nje ya nchi ambao walionekana kukiuka masharti ya leseni zao na wiki iliyopita Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alisema marufuku hiyo inaendelea kwa kuwa ni kinyume cha sheria za nchi.
Lakini msimamo huo wa Waziri Maige utakuwa mgumu kuutekeleza baada ya Mwananchi kubaini kuwa wanaomiliki vibali vya kuvuna magogo ni baadhi ya viongozi wa serikali ambao badala ya kuvitumia kwa malengo waliyoombea, wamekuwa wakivikodisha kwa wafanyabiashara.

Baadhi ya vigogo mbao majina ambayo yamo kwenye orodha watu wanaomiliki vibali hivyo ni pamoja na Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Cyril Chami, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera, Uratibu na Bunge-, William Likuvi, mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Evalista Kalalu, mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita na wengine waliotumia majina ya jamaa zao.

Wengine ni Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene na kampuni ya Rombo Green View inayomilikiwa na mmoja wa mawaziri wa zamani katika serikali za awamu tofauti. Katika orodha hiyo pia yamo majina ambayo ubini wake unafanana na baadhi ya viongozi kama vile Selemani KIKWETE, Aneth P. Msekwa na Juma Abdallah Zombe.

Hata hivyo, haikufahamika mara moja kama watu hao wana uhusiano wa moja kwa moja na watu ambao majina yao ya ubini yanafanana na ya viongozi wa serikali.Vyanzo vyetu vya habari vimebainisha kuwa vigogo walioficha majina yao wanafahamika na kwamba itakapohitajika watatajwa hadharani na raia wema walioapa kuwa tayari kufanya hivyo.
Habari za kiuchunguzi zimebaini kuwa kuwepo kwa watumishi hao wa serikali katika biashara ya magogo kumezua mgogoro mkubwa wa kimaslahi kati yao na wavunaji wadogo wanaolalamika kupunjwa kwenye mgao wa vitalu vya uvunaji.

Uchunguzi umebaini kuwa mgao wa kitaifa unaelekeza meneja mradi wa Sao Hill kugawa magogo yasiyozidi mita za ujazo (cubic metre) milioni moja kwa mwaka.Hata hivyo, katika hali inayoweka mashaka, mgao huo unaonekana kuwapendelea zaidi vigogo hao wanaotumia nyadhifa zao kupata vibali bila kuwa na sifa za kupata mgao huo, huku wengine wanaonufaika wakitajwa kuwa ni baadhi ya wawekezaji wakubwa.Imeelezwa kuwa masharti yaliyowekwa na serikali kwa kila kibali ni kwamba lazima muombaji awe na vifaa kama malori makubwa ya kukokota magogo (break down), mashine zenye uwezo mkubwa wa kuchana magogo na lazima muomba kibali awe ameajiri wataalamu toka chuo cha misitu kinachotambuliwa na serikali, masharti ambayo Mwananchi imedokezwa kuwa hayajatekelezwa na vigogo hao.

Katika kipindi ambacho Rais Jakaya Kikwete amewataka mawaziri na wasaidizi wao kuwa tayari kutoa habari kwa wananchi, katibu mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk Ladslaus Komba hakuweza kuzungumzia suala hilo kila mara Mwananchi ilipowasiliana naye kuanzia Jumatano iliyopita.Badala yake, katika simu zote sita alizopigiwa kati ya Jumatano na jana jioni, Dk Komba alipokea lakini baada ya mwandishi kujitambulisha na kueleza kile anachotaka kufahamu kutoka kwake, alijibu:
"Kwa sasa niko kwenye kikao nitakutafuta baadaye.Hata hivyo, hakutekeleza ahadi hiyo hata mara moja.

Katika moja ya simu hizo, Dk Komba alisema: “Kuna kitu hapa nakinukuu, naomba unipe muda nitakujulisha.”
Hata hivyo alipotafutwa baadaye simu yake ilikuwa haipatikani.
Hata alipofuatwa ofisini kwake, katibu muhtasi wake alieleza kuwa Dk Komba alikuwa ameenda kikazi nje ya ofisi na kumtaka mwandishi amsubiri.

Mmoja wa vigogo waliotajwa kwenye orodha ya mgao wa magogo, WaziriLukuvi alikiri kupokea mgao huo, lakini akasema aliomba kwa ajili ya ujenzi wa shule za sekondari zilizo jimboni kwake Isimani na si kwa nia ya biashara.

Kwenye mgao huo, Lukuvi amepewa kibali cha kuvuna magogo yenye mita za ujazo 1,000, kulingana na orodha iliyobandikwa kwenye ubao wa matangazo wa Sao Hill Mufindi. Katika  orodha hiyo Lukuvi ni mtu wa 564.
“Ni kweli niliomba na nikapewa kibali cha kuvuna magogo. Lakini, si kwa nia ya biashara bali kwa ajili ya kupata mbao za ujenzi wa sekonda zilizopo jimboni kwangu, ikiwemo ile iliyoungua moto ya Idodi,” alisema.

Mbunge wa jimbo la Kibakwe, George Simbachawene alipoulizwa kuhusu suala hilo alikiri kuomba mgao wa uvunaji magogo katika msitu huo, lakini akasema lengo lake si kwa ajili ya kufanya biashara bali ni ujenzi wa madarasa.
"Ni kweli niliomba wala sibishi, lakini si kwa ajili ya kufanya biashara. Ilikuwa ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya shule zetu zilizo katika halmasahauri yetu, kwa sababu kununua mbao zikiwa zimeshaandaliwa ni gharama kuliko kuomba kuvuna magogo na kuchana mwenyewe," alisema Simbachawene.

Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni jitihada za kumpata Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Cyril Chami na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita zilishindikana.

Taarifa zinasema kuwa licha ya kujipatia vibali vinavyotolewa bure na Wizara ya Maliasili na Utalii, wamekuwa hawavitumii kwa uvunaji bali huvikodisha kwa wavunaji wadogo kwa gharama ya Sh5 milioni hadi Sh7 milioni kwa kibali kimoja huku ikielezwa kuwa wapo wanaomiliki vibali zaidi ya 10 na wanavitumia kwa majina tofauti.
Hali hiyo imefanya wavunaji wadogo kupunjwa mgao wa uvunaji magogo tofauti na ilivyokuwa kabla ya watumishi hao wa umma na vigogo kuvamia sekta hiyo.

Hivi sasa wavunaji wadogo zaidi ya 400 wanaambulia mgao kiduchu na wengine kukosa kabisa, hivyo wengi wamelazimika kufunga viwanda vyao kutokana na kukosa malighafi.
“Kama watoa vibali ndio wahusika katika biashara hii je, haki itatendeka kwa wavunaji wadogo?,” kilihoji chanzo kimoja.

9 Dec 2010



JAMAA mmoja ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Joseph, leo asubuhi alikutwa na kamera yetu akiwa ameanguka katika Barabara ya Forest mjini Morogoro, pembezoni mwa uzio wa Hospitali Kuu ya Mkoa wa Morogoro, akidai kwamba alikuwa ametokea katika hospitali hiyo na kwamba hali yake ilikuwa imezidi kuwa mbaya.

Akizungumza na mtandao huu, Joseph alisema: "Nimetoka humu ndani (hospitali) kutibiwa na baada ya kupewa dawa niliruhusiwa kurudi nyumbani, nilipofika hapa nimezidiwa na njaa pamoja na ukali wa dawa hizo na kujikuta nikiishiwa nguvu na kuanguka.

Kama kuna mtu ana shilingi elfu moja anisaidie nikanunue walau uji," alisema Joseph huku akionekana akitetemeka kwa njaa pamoja na ukali wa dawa hizo.



Alipoulizwa anasumbuliwa na ugonjwa gani alidai ni homa ya matumbo (typhoid) iliyoambatana na homa kali.

Mwandishi wetu alimpatia kiasi hicho cha fedha ambapo pia baadhi ya watu waliokuwa eneo hilo walimuunga mkono mpiga picha wetu kwa kumuongezea kiasi cha fedha na baadaye kumwinua hadi kwenye mgahawa uliopo jirani na Shule ya Sekondari ya Morogoro.

Baada ya kupata hudumu hizo, Joseph alizinduka na kauli yake ya kwanza ilikuwa ni kuushukuru mtandao huu na wananchi wengine kwa kumpatia msaada huo.

Picha na Habari kwa Hisani ya Global Publishers



WAKATI HALI IKIWA HIVYO KWA MLALAHOI HUYU,GAZETI LA Mwananchi LILIRIPOTI HABARI IFUATAYO.ISOME KISHA ULINGANISHE NA HABARI HIYO YA KUSIKITISHA HAPO JUU,KISHA TAFAKARI KUHUSU MIAKA 49 YA UHURU WETU

Mashangingi ya mawaziri yazua utata 
Sunday, 28 November 2010 21:05

Sadick Mtulya

WAKATI mawaziri na manaibu wawaziri wakikabidhiwa magari mapya, baada ya kuapishwa Jumamosi iliyopita, serikali imeibuka na kusema sio mapya ni ya zamani.Kauli hiyo inaibua utata kutokana na kuwa baada ya kuapishwa viwanja vya Ikulu na Rais Jakaya Kikwete, kila waziri alikabidhiwa dereva mpya na gari jipya aina ya Toyota GX V8, badala ya gari aina ya Toyota VX V8 iliyokuwa ikitumiwa na mawaziri waliopita.

Ununuzi wa Toyota GX V8 mpya, unashiria serikali bado haijawa tayari kuunga mkono msimamo wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambaye amekuwa akisikika akitaka kusitishwa ununuzi wa magari ya kifahari ili kupunguza matumizi ndani ya serikali.

Toyota GX V8 moja huuzwa kati ya Sh210 milioni hadi Sh240 milioni, hukuToyota VX V8 moja inauzwa sio chini ya Sh180 milioni.Akizungumza na Mwananchi jana, Katibu Mkuu wa iliyokuwa Wizara ya Miundombinu, Omari Chambo, alisema magari hayo sio mapya na kwamba, yaliyotumiwa na mawaziri waliopita.Rais Jakaya Kikwete ameigawanya iliyokuwa Wizara ya Miundombinu na kuwa wizara mbili; Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Uchukuzi.

“Yale magari sio mapya, yalikuwepo. Kwanza uliyaona au unasema tu, hamjayachunguza vizuri jamani, fanyeni uchunguzi,’’ alisema Chambo na kukata simu.
Mawaziri wote na baadhi ya manaibu walikabidhiwa magari hayo (GX V8), huku manaibu wengine wakikabidhiwa VX V8.Sababu ya baadhi ya manaibu mawaziri kukabidhiwa VX V8 badala ya GX V8, ni kutokana na kutokamilishwa kwa taratibu za kutokamilika.

Mmoja wa manaibu mawaziri (jina tunalo), alikabidhiwa VX V8 iliyokuwa ikitumiwa na aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifungo na Uvuvi, John Magufuli, ambaye sasa ni Waziri wa Ujenzi.Gazeti moja la kila siku (si Mwananchi) limeeleza kuwa ununuzi wa magari hayo, umegharimu serikali Sh9.3 bilioni na kwamba, takwimu za iliyokuwa Wizara ya Miundombinu zinaonyesha kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwaka wa fedha wa 2005/06 magari makubwa ya kifahari yapatayo 6,000 yalikuwa yamenunuliwa na serikali kwa gharama inayokadiriwa kufikia Sh160 bilioni.

Miongoni mwa magari hayo ni Toyota Land Cruiser (VX/ GX V8, Prado) yapatayo 1,655, Nissan Patrol na Land Cruiser 885, Mitsubishi Pajero 400 na mengineyo.

Tangu kipindi cha serikali ya awamu ya tatu chini ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, kumekuwepo na mjadala kuhusu matumizi makubwa ya serikali hasa katika ununuzi wa magari ya kifahari kutokana na kuendeshwa kwa gharama kubwa.Wadau wengi wanataka viongozi watumie magari ya kawaida kama ilivyo kwa nchi ya Kenya na Rwanda




Leo ni siku yangu ya kuzaliwa.Kwanza sina budi kumshukuru Muumba kwa kunileta duniani tarehe 9 Desemba miaka thelathini na kitu iliyopita (30 plus yrs ago).Pili,nawashukuru wazazi wangu wapendwa,Baba Mzee Philemon Chahali na Mama mpendwa Marehemu Adelina Mapango (Mungu Akulaze Mahali Pema Peponi Amen).Tatu,nawashukuru wanafamilia wenzangu katika familia yetu-kaka na dada na wadogo zangu.Na nne nawashukuru wale woote nilio/ninaofahamiana nao katika muda wote huo.

Makala hii sio kwa ajili ya kuzungumzia birthday yangu.Kwa bahati nzuri (au mbaya?) tarehe ya siku yangu ya kuzaliwa inarandana na tarehe ya Uhuru wa Tanzania.Inapendeza kusherehekea siku ya kuzaliwa inayoambatana na tukio jingine muhimu la kihistoria.Lakini historia pekee sio muhimu kama haina manufaa stahili kwa jamii husika.

Wakati tunaadhimisha miaka 49 ya uhuru wa Tanzania tunalazimika kujiuliza mara mbili mbili umuhimu wa uhuru huo.Je uhuru wetu uliishia tu kwenye kumwondoa mkoloni au ulipaswa kutuweka huru katika nyanja zote?Naamini hilo la pili ndilo dhamini na maana halisi ya uhuru: uhuru wa kupata huduma tunazostahili (elimu,afya,maji,barabara,umeme,maji,nk),uhuru wa kuchagua na kukataa viongozi kwa njia halali (sio uchakachuaji),uhuru wa habari pamoja na uhuru wa kutoa maoni hata kama habari na maoni hayo hayawapendezi watawala),uhuru wa kuabudu pasipo kuwa kikwazo kwa waumini wa imani tofauti,uhuru wa kuishi ikiwa ni pamoja na kuepusha vifo vinavyoepukika (ajali zinazochangiwa na ufisadi wa polisi trafiki,ukosefu wa madawa unaochangiwa na ufisadi kwenye misaada/manunuzi kwenye sekta ya afya),uhuru wa kuishi bila kubaguliwa (mafisadi vs walalahoi,vigogo vs makabwela,watawala vs watawaliwa,nk),na KILA UHURU ambao ni HAKI ya msingi kwa mwanadamu.

Japo haipendezi kuzungumizia,ukweli mchungu ni kwamba miaka 49 ya uhuru wetu inatuacha na maswali mengi kuliko majibu.Na kama mzaha mbaya,siku chache kabla ya kusherehekea umri huu tumeshuhudia namna uchaguzi mkuu uliojaa kasoro lukuki na uchakachuaji ukitupatia "serikali mpya" (denti yuleyule lakini katika yuniformu mpya...ni dhahiri kuwa kama denti huyo ni "kichwa panzi" yunifomu hizo mpya hazitomsaidia lolote kimasomo).Na siku chache zilizopita tumeshindiliwa msumari wenye kutu katika kidonda kibichi pale kampuni ya Dowans "iliposhinda" kesi dhidi ya Tanesco (serikali) na sasa inastahili kulipwa mabilioni ya shilingi.Hiyo ndio salamu ya happy birthday kutoka kwa mafisadi.Tukio hilo halina tofauti na vitendo vya vibaka (hususan mitaa ya Mwananyamala karibu na hospitali kama unatokea Mwananyamala Kwa Kopa) ambapo vibaka wanakupiga roba ya mbao kisha wanakupigia ukelele wa "mwiz,mwizi".Kuporwa uporwe,na kipigo ukipate.Naam,ndivyo Dowans na wamiliki wake mafisadi wanavyotutenda.Huu ni ubakaji wa hadharani tena mchana kweupe.

Anyway,mie nasherehekea birthday yangu kibinafsi.Kama kuna mafanikio au mapungufu yaliyojiri katika miaka thelatini na kitu tangu nizaliwe yanabaki kuwa masuala binafsi.Lakini kwa vile Tanzania ni yetu sote,hatuna budi kusherehekea birthday yake kwa kufanya tafakuri kuhusu mantiki nzima ya "kuzaliwa" na kuwepo kwake.Ni kwa namna hiyo tu ndipo tutaweza kuendelea kusherehekea siku kama ya leo kwa "amani na utulivu" (tukumbuke mwenye njaa hana amani kama ilivyo kwa mgonjwa asiyeweza kupewa tiba stahili,au msafiri asiyeweza kufika aendako kwa vile barabara hazipitiki,au mlipakodi anayekwamishwa kimaisha na mgao usioisha wa maji na umeme,au mlalahoi asiye na haki mbele ya matakwa ya vigogo na mafisadi).

Happy birthday to me.Happy birthday Tanzania

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.