18 Sept 2008
18.9.08
Evarist Chahali
FATWA, MICKEY MOUSE, SAUDI ARABIA
No comments

18.9.08
Evarist Chahali
HACKING, SARAH PALIN
No comments

18.9.08
Evarist Chahali
ODD STUFFS
No comments


17 Sept 2008

Katika toleo la wiki hii la gazeti mahiri la Raia Mwema,pamoja na mkusanyiko wa habari na makala motomoto,kuna hababari kuhusu the man of the moment,Nape Nnauye.Kuna wanaodai kuwa huyu jamaa aanashupalia ishu za ufisadi ndani ya UVCCM kwa minajili ya kutafuta umaarufu utakaopelekea apate nafasi ya juu kwenye jumuiya hiyo.Sina uhakika kuhusu hilo lakini binafsi naamini kwamba hata kama malengo yake ya ni kupata umaarufu au uongozi,jitihada zake kuushikia bango ufisadi ndilo lililo muhimu zaidi kuliko motives zake.Na wanaokemea ufisadi,hata kama kwa njia zisizo sahihi,wanapaswa kuungwa mkono badala ya kunyanyaswa.Enewei,habari ya Nape ni hii HAPA na mambo mengine motomoto yanapatikana ndani ya gazeti hili la RAIA MWEMA.
Kigoma.Mwaka 1976.Nyumba kadhaa maeneo na NHC Mnarani zinaonekana zikiwa na magamba (outer cases) ya betri yaliyobandikwa vikaratasi vyenye maandishi ya Kiarabu.Habari zilizozagaa wakati huo ni kwamba pasipo kuweka "kinga" hiyo maafa yangeikumba nyumba husika.Weka usalimike,usiweke uone kitachokutokea.Kwa vile takriban kila nyumba katika mtaa naoukumbuka ilikuwa na "kinga" hizo,haikuwa rahisi kubaini nini kingetokea kwa waliopuuza.Ifakara.Mwaka 1982.Watoto tunaangaliwa kwa karibu na wazazi kwa hofu ya kuchukuliwa na "wanyonya damu" au maarufu kwa jina la mumiani.Nakumbuka nyumba moja iliyokuwa eneo la Kwa Shungu ambayo nadhani mmiliki wake aliamua tu kuiwekea urembo wa msalaba kwa kutumia chokaa ilikuwa ikituhumiwa kwamba ndio kituo cha kukusanyia damu zinazonyonywa na mumiani.Hadi leo sijui kama kuna mtoto au mtu aliyenyonywa damu na mumiani waliodaiwa kuvamia Ifakara.
Tanga.Mwaka 1993.Madereva wanataharishana kuhusu jini la kike linalodaiwa kuonekana nyakati za usiku katika barabara ya Ngamiani.Jini hili linadaiwa kujibadili kama mwanamke mrembo sana,na pindi dereva akithubutu kutoa lifti akidhani "ameopoa mzigo" basi ndio mwisho wake.Pia nyumba moja maeneo ya Makorora ambayo mmiliki wake amefuga mbuzi kadhaa inadaiwa kuhifadhi majini lukuki.Wajuzi wa mambo wanatahadharisha kupita maeneo hayo usiku mkubwa,na wengine wanakwenda mbali zaidi kwa kushauri kwamba hata ukipita mchana usiangalie sana nyumba hiyo,majini yanaweza kukuvuta.Hadi naondoka Tanga mwaka 1995 sikuweza kuthibitisha ukweli au uongo wa habari hizo.
Nyanda za Juu Kusini.Miaka ya hivi karibuni.Taarifa zinatapakaa kwamba kuna biashara ya uchunaji ngozi za binadamu.Inadaiwa kwamba ngozi hizo hutumiwa na waganga kwenye masuala ya baishara.Pia inadaiwa kuwa ngozi hizo zina faida kubwa katika nchi moja jirani.Tarehe 8 mwezi Mei mwaka 2006 Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya inawakumu watu wawili,Dickson Shapwata na Nelson Mwazembe, kunyongwa baada ya kupatikana na tuhuma za kumuua na kumchuna ngozi Marehemu Loti Nzowa mnamo mwaka 2001.
Kanda ya Ziwa.Miaka ya hivi karibuni.Mauaji ya vikongwe wenye macho mekundu yanazidi kushika hatamu.Tuhuma dhidi ya vikongwe hao ni uchawi.Mtani wangu mmoja Msukuma wa Shinyanga ananinong'oneza kwamba amemshauri babu yake aache kuvuta ugoro ili macho yake yasiwe mekundu.Mtani wangu mwingine anadai kwamba vikongwe wenye macho mekundu wanauawa kwa sababu wekundu huo ni matokeo ya wao kukesha wakiwanga usiku.Utani kando,mauaji ya vikongwe bado yanaendelea japo hadi sasa ni vigumu kuelewa kwanini yashamiri Kanda ya Ziwa pekee.
Sehemu mbalimbali Tanzania.Mwaka 2008.Taarifa zinatapakaa kwamba maalbino wanawinda na wanauawa na watu wanaodaiwa kuhitaji viungo kutoka miilini mwa maalbino hao kutengenezea dawa za baishara.Mwandishi wa BBC,VIcky Ntetema,anapata vitisho wakati anatengeneza documentary kuhusu mauaji ya maalbino.Kwa mujibu wa mwandishi huyo,mwaka huu tayari maalbino 25 wameshauawa maeneo ya Mwanza,Shinyanga na Mara.Mwezi Machi mwaka huu,chama cha maalbino mkoani Tanga chatangaza sensa ya maalbino.Mwezi huohuo Serikali mkoani Mwanza inatangaza kuangalia uwezekano wa polisi kuwapatia ulinzi maalbino.
Hii ndio Tanzania yetu ambayo ushirikina unazidi kushamiri.Wapo watakaonipinga lakini ukweli ndio huo.Wanaofuatilia nyendo zisizo rasmi za siasa za nyumbani wanadai kwamba hata baadhi ya wanasiasa wanaosimama majukwaani kukemea mauaji ya vikongwe au maalbino nao wanategemea sana ndumba katika maisha yao ya kisiasa.Wengi tunakumbuka yaliyojiri katika kikao cha Bunge kilichopita ambapo mheshimiwa mmoja alituhumiwa kumwaga ndumba bungeni japo ishu hiyo iliisha kimyakimya.
Kwenye sosholojia ya dini tulifundishwa kwamba kabla ya ujio wa dini za kimapokeo (Ukristo,Uislamu,nk) jamii za Kiafrika zilikuwa zikifuata dini zao za asili (African Traditional Religions-ATRs).Na hadi sasa,dini za asili zina ushawishi mkubwa kwa waumini wa dini za kimapokeo.Tunafahamu Wakristo au Waislam wengi ambao pamoja na kwenda makanisani au misikitini hawasahau kuomba mizimu ya kale.Kwa waliozaliwa na kukulia Dar,sio rahisi sana kuelewa hili nalozungumzia lakini hilo linajulikana sana kwa "wakuja" wenzangu.Sasa,tatizo lipo katika kuchora mstari unaotenganisha dini za asili na ushirikina.Kule kwetu Undambani kuna mababu (wanaitwa "mambuyi" kwa Kindamba) wanaoaminika kufanya miujiza (kutibu,kuepusha ukame/njaa,nk) wanapoombwa kwa dhati.Inaaminika pia kwamba "mambuyi" hao wana uwezo wa kumduru mtu.
Tukirudi kwenye sosholojia ya dini tunaambiwa kuna roho mfu za aina mbili,dead-dead na living-dead.Marehemu wanaokufa na kuenziwa,hubaki kuwa mzimu yenye inayotarajiwa kuleta mema.Marehemu wanaotelekezwa (kwa mfano wanaokufa ajalini na maiti zao kuzikwa na jiji) hugeuka kuwa mzimu yenye uwezo wa kuleta mabaya kwa vile wamesahaulika.Pengine hapa ni vizuri kushauri wazazi kutosahau kutoa "sadaka" ya jina la marehemu babu,bibi,baba,mama au yeyote yule katika ukoo ili kuwaenzi kwa minajili hiyo ya baraka za mbeleni.
Ni vigumu kubashiri iwapo mauaji ya maalbino yatakwisha kwani hata hayo ya vikongwe bado yanaendelea.Tatizo kubwa zaidi linalozikabidili jamii zetu za Kiafrika ni watu kutafuta njia za mkato katika kutimiza malengo au matakwa yao.Ushirikina unashamiri zaidi kwa namna hiyo.Mtu anatafuta dawa ya kufaulu mtihani,anakwenda kwa mganga na kutakiwa apeleke kichwa cha mtu mwenye kipara.Huyu ni mzembe ambaye anataka kupata njia ya mkato ya kufaulu badala ya kusoma kwa bidii.Mheshimiwa flani anataka kurejea bungeni lakini anakabiliwa na upinzani mkali kwa vile hajaonekana jimboni tangu achaguliwe katika uchaguzi uliopita.Anakwenda kwa mganga anaambiwa alete moyo wa albino.Unategemea nini hapo?
Haya ya vikongwe wenye macho mekundu na maalbino ni mwendelezo tu wa ushirikina katika jamii zetu.Yayumkinika kuamini kuwa huko mbele wenye vipara,vitambi,matege,makengeza na pengine hata wenye mustachi wanaweza kuwa wawindwa wa hawa wanaotaka mafanikio kwa njia ya mkato.Mbinde itakuwa pale washirikina hao watakapoanza kuwinda watu wenye fedha nyingi katika akaunti zao ambazo hazikupatikana kihalali!Pengine ndio utakuwa mwisho wa ufisadi.Just thinking aloud!
15 Sept 2008
Came accross this interesting examination of Sarah Palin
Sarah Palin may not have known what the Bush Doctrine was, but we're getting a pretty good idea of what the Palin Doctrine is. Or will be -- because it's still currently under construction. And what is it going to look like? Let's just say, it's going to seem familiar.
According to London's Daily Telegraph, the architects of the Palin Doctrine are a group of people who have been singularly wrong about virtually everything in the last decade -- the neocons, who have been briefing Palin for weeks.
As predicted, the fact that she didn't know anything wasn't a bug, it was a feature. She's perfect for the neocons: likeable on the outside, a blank slate on the inside. To borrow from an old cliché, if Sarah Palin didn't exist, the neocons would have had to invent her.
In fact, this is how one former White House aide describes her: "She's bright and she's a blank page. She's going places and it's worth going there with her."
Of course, the place her neocon mentors hope she's going is the White House. Given their dismal track record, they're smart enough to figure that the American public wouldn't be too keen on letting them in the front door again, so they are trying to sneak in hidden behind Palin's skirt. The Trojan Moose approaches.
The Daily Telegraph details how the neocon talent scouts spotted their political Eliza Doolittle back in the summer of '07. The love connection began, appropriately enough, on a love boat:
"Sources in the McCain camp, the Republican Party and Washington think tanks say Mrs. Palin was identified as a potential future leader of the neoconservative cause in June 2007. That was when the annual summer cruise organised by the right-of-centre Weekly Standardmagazine docked in Juneau, the Alaskan state capital, and the pundits on board took tea with Governor Palin."
So nice to meet you, Governor. And don't forget, cucumber sandwiches and preemptive invasions on the Lido Deck at four!
Not surprisingly, Palin's biggest fan is Bill Kristol, who describes her as the "specter of a young, attractive, unapologetic conservatism" that "is haunting the liberal elites."
Among her other Henry Higginses is neo-neocon Joe Lieberman, who is reportedly helping prep Palin for the big ball -- her debate with Joe Biden.
She's already passed her first test with flying colors: being willing to link 9/11 with Iraq, something not even the president is still willing to do. Last week, she told a group of Iraq-bound soldiers that they were going to "defend the innocent from the enemies who planned and carried out and rejoiced in the death of thousands of Americans."
By George (Bush), I think she's got it! Congratulations, Professor Kristol, your student is coming along just fine.
Of course, the neocons know they already have an ally at the top of the GOP ticket. McCain may have been a reformer on campaign finance, but when it comes to foreign policy, he has always been solidly in the neocon club. He loves to burnish his foreign policy bona fides by talking about how he wanted to fire Donald Rumsfeld months before Bush did. But he doesn't talk a lot about how, in the days immediately after 9/11, he was part of the neocon crowd itching to get into Iraq.
Just a few days after the attack, McCain was already talking about "some other countries" that helped Bin Laden. Countries like Syria, Iran, and...Iraq. And a few weeks later, during an October 18, 2001 appearance on David Letterman, McCain answered a question about how the war in Afghanistan was going by announcing that the invasion of Iraq would be "the second phase" of the war on terror (how prescient of him to know that Saddam wouldn't give up those nonexistent WMD). What's more, he tried to buttress the case for attacking Iraq by claiming that the recent spate of anthrax attacks "may have come from Iraq." Or Fort Detrick.
Six years later, demonstrating how little he's learned from the debacle in Iraq, McCain hired Randy Scheunemann, a neocon darling who helped form The Committee for the Liberation of Iraq in 2002, as his campaign's chief foreign policy advisor.
As TPMMuckraker noted in July, "Of all the hawkish Washington foreign-policy types pushing both before and after 9/11 for war with Iraq -- a war that an overwhelming majority of Americans now considers a mistake -- Scheunemann, though not a marquee name, was among the most energetic and influential. And in the invasion's aftermath, he consistently opposed steps that might have helped stabilize the country."
And now, according to the Daily Telegraph, Scheunemann is briefing Sarah Palin.
McCain's selection of Palin may have been reckless, but it was anything but random. The neocons' view of the world may be disastrous, dangerous, discredited, and deadly -- but it's far from dead. Their patron saint, Dick Cheney, the scowling embodiment of the Neocon Doctrine, had way too much baggage -- and way too low approval ratings -- to mount a run for the White House.
That's why the Palin pick was so brilliant. On the outside, she's exponentially more likable and talented at connecting with people than Cheney ever was. But on the inside, once she graduates from the neocon finishing school, she'll be a complete and total Dick. Cheney. With lipstick.

Mtikila atamka mazito kifo cha Wangwe Na Waandishi Wetu
WAKATI mazingira ya kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime marehemu Chacha Wangwe yakiendelea kuwa tete, Mwenyekiti wa Democratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila, ameibuka na kile alichodai, taarifa za mpango kamili hadi mauaji ya mwanasiasa huyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mchungaji Mtikila alidai mipango ya kumuua marehemu Wangwe ilianza kusukwa mkoani Dodoma na baadaye vikao vya kukamilisha mkakati huo, vilifanyika jijini Dar es Salaam wilayani Kinondoni.
Aliongeza kuwa wahusika baada ya kukamilisha mpango huo na jinsi utakavyotekelezwa, walikwenda nchini Kenya kukodi watu wawili ambao alidai walilipwa sh. milioni 120 kama ujira wa 'kazi' hiyo.
Mchungaji Mtikila alidai kuwa wauaji hao, ndio walioshirikiana na Bw.Deus Mallya ambaye anadaiwa wakati huo alikuwa amejenga uhusiano mzuri na marehemu Wangwe.
Alidai siku ya tukio, marehemu Wangwe hakutaka kusafiri lakini alishinikizwa zaidi ya mara tatu na Bw. Mallya ambaye hadi sasa anashitakiwa kwa kosa la kusababisha ajali na kuendesha gari bila leseni.
"Baada ya kushinikizwa sana, marehemu Wangwe alikubali kuanza safari ambapo Bw. Mallya aliwasiliana na washirika wake ambao muda huo walikuwa eneo la tukio wakiwasubiri," alidai Mchungaji Mtikila na kuongeza kuwa;
"Wakati huo ilikuwa bado mapema hivyo walimshauri apoteze muda japo wa nusu saa, ndipo alipozusha hitilafu ndani ya gari na kurudi gereji na baada ya muda huo kupita ndipo walianza safari kuelekea jijini Dar es Salaam."
Huku akidai kuwa ana ushahidi wa tukio hilo na yupo tayari kutoa ushirikiano kwa Rais Jakaya Kikwete, Mchungaji Mtikila alizidi kueleza kuwa Bw. Mallya aliendelea kuwasiliana na washirika wake hadi walipofika eneo Pandambili, wilayani Kongwa na kusimamisha gari.
"Baada ya kusimamisha gari, washirika wa Mallya walipanda na kumpulizia dawa ya usingizi usoni mara nne na hapo hapo alipoteza fahamu," alieleza Mchungaji Mtikila na kuongeza kuwa baada ya hapo ndipo alipigwa kwa kitu cha ncha kali kisogoni.
"Kwa kuwa Mungu alimpenda sana hakukata roho, aliendelea kuhema ndipo alipopigwa na nyundo na kummalizia kabisa," alidai. Aliongeza kuwa baada ya kutimiza hilo waliweka jiwe kwenye kiongeza mwendo gari likaondoka kwa kasi na lilipindua ili kuonesha kuwa marehemu alikufa kwa ajali lakini muda huo Mallya alikuwa hayuko kwenye gari,"
Alidai kuwa kabla ya kupindua gari hilo, walimfunga marehemu mkanda na kumwibia sh. milioni tisa alizokuwa nazo pamoja na kompyuta yake ndogo 'Lap top' ambayo ilikuwa na nyaraka zake za siri.
Alidai kuwa baada ya kufanikisha mauaji hayo, Bw. Mallya alitoa 'line' yake ya simu ambayo alikuwa akiitumia kuwasiliana na washirika wake na kuitupa. Alidai kuwa hadi anakamatwa simu yake haikuwa na 'line' yoyote.
Kwa mujibu wa Mchungaji Mtikila mauaji hayo yalifanyika kati ya 1.30 hadi saa 2.00 usiku, muda mfupi baada ya kumaliza kuwasiliana na familia yake saa 1.27.
Huku akijata majina ya watu wanaodaiwa kuhusika kwenye mpango huo, alieleza kuwa kipindi cha mchakato wa mpango wa kumuua, Bw. Wangwe, walikuwa wakisafiri kwenda nchini Kenya kusuka mpango huo.
Mchungaji Mtikila alielekeza lawama zake kwa askari wote waliohusika na uchunguzi wa mauaji hayo kwa akidai kuwa hawakusema ukweli hivyo nao wanastahili kuunganishwa kwenye kesi hiyo.
Kutokana na mazingira ya kifo cha marehemu Wangwe kugubikwa na maswali mengi, Mchungaji Mtikila amemuomba Rais Kikwete kuunda tume ya kuchunguza mazingira ya kifo chake kama alivyofanya kwa wafanyabiashara wa madini wa Mahenge, Morogoro ambao wanadaiwa kuuawa na Polisi.
Alidai kwa wadhifa aliokuwa nao marehemu Wangwe katika jamii akiwa Mbunge wa Tarime, Rais ana nafasi ya kuunda tume. "Naupongeza uamuzi wake wa kuunda tume ya kuchunguza vifo vya wafanyabiashara lakini na kwa hili aunde tume na mimi nitakuwa tayari kutoa ushirikiano,"alisisitiza.
Aliongeza kuwa kama Rais hatafanya hivyo, yeye ataleta wataalam wake kutoka nje kufanya uchunguzi kwani ameishafanya mazungumzo na ubalozi wa nchi moja ambao hakuutaja.
Mchungaji Mtikila alidai kuwa atakwenda jimboni Tarime wakati huu wa kampeni ili kuwaeleza wananchi ukweli kuhusu kifo cha marehemu Wangwe. Alisema amesimamisha mgombea kupitia chama chake, Bw. Benson Makanya, ili apate jukwaa la kueleza ukweli kuhusiana na kifo hicho.
Marehemu Wangwe alikufa kwa ajali ya gari iliyotokea eneo la Pandambili mkoani Dodoma Julai 28 mwaka huu lakini tangu kifo chake, yameibuka maswali mengi huku baadhi ya watu wakidai kuwa aliuawa.
Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na madaktari wawili kwa nyakati tofauti ulionesha kuwa hakupigwa risasi bali kifo chake kilisababishwa na ajali ya gari.
14 Sept 2008
14.9.08
Evarist Chahali
IRAN, IRAQ, JOHN MCCAIN, SARAH PALIN, SHIA, THE SURGE
No comments


