28 Apr 2009



YAH,WANASEMA NI SUALA LA MTIZAMO: KUSEMA GLASI IKO HALF EMPTY AU HALF FULL.HABARI MBILI ZIFUATAZO ZINADHIHIRISHA MANTIKI YA MSEMO HUO.

Na Boniface Meena

UMAARUFU wa Rais Jakaya Kikwete unaonyesha kuendelea kuporomoka, kwa mujibu wa ripoti ya matokeo ya utafiti uliofanywa na taasisi ya Mpango wa Utafiti wa Elimu ya Demokrasia nchini (Redet).

Ripoti hiyo pia inaonyesha kuwa utendaji kazi wa Rais Kikwete, ambaye aliingia madarakani mwaka 2005 kuongoza serikali ya awamu ya nne, umeshuka kwa asilimia 28 mwaka jana ukilinganisha na matokeo ya utafiti ya mwaka 2006.

Pamoja na kushuka kwa asilimia hiyo, utafiti huo umeonyesha kuwa wananchi waliohojiwa wanaridhika zaidi na utendaji wa Rais Kikwete, kuliko wanavyoridhishwa na utendaji kazi wa baraza lake la mawaziri ambalo utendaji wake umekubaliwa na asilimia 18 tu.

Kwa mujibu wa utafiti huo, watu wanaoridhika sana na utendaji kazi wa Kikwete ni asilimia 39.5 tu kulinganisha na asilimia 69 iliyoonyesha kuridhika naye sana mwaka 2006.

Akitoa taarifa ya utafiti huo jana kwa waandishi wa habari, mtafiti mkuu wa Redet, Dk Benadetha Killian alisema kuwa ukilinganisha takwimu za Oktoba 2006 na Oktoba 2007, asilimia ya wale wahojiwa ambao wanasema wanaridhika sana na utendaji kazi wa Rais Kikwete imepungua kutoka asilimia 69 Oktoba 2006 hadi asilimia 44 mwezi Oktoba 2007 na sasa imefikia asilimia 39.5 hadi Novemba mwaka jana.

Dk. Killian alisema kuwa ukichambua undani wa mwenendo huo utaona kwamba wakati idadi ya wanaosema wanaridhika sana iliteremka kwa tofauti ya asilimia 23, kati ya mwaka 2006 na 2007, kasi ya kutoridhika sana imepungua ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2007/08 wakati idadi ya wahojiwa ambao walisema wanaridhika sana ilipungua kwa tofauti ya asilimia 4.5 tu.

Kwa mujibu wa Dk. Killian, ukusanyaji wa maoni kwa ajili ya utafiti huo ulifanyika katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani na sampuli ilichaguliwa katika ngazi tatu ambazo ni wilaya na vijiji/mitaa na katika kila ngazi sampuli ilipatikana kwa kutumia mtindo wa sampuli nasibu.

"Katika kila wilaya, watafiti walitakiwa kuchagua vijiji viwili (kwa maeneo ya shamba) au mitaa miwili (kwa maeneo ya mjini) kwa kutumia njia ya sampuli nasibu. Katika kila wilaya, jumla ya watu 50 walichaguliwa kwa ajili ya kuhojiwa, 25 kutoka kila kijiji/mtaa," alisema.

"Na kati ya watu 50 waliohojiwa katika kila wilaya, 25 walitakiwa wawe wanawake na wengine 25 wawe wanaume na uchaguzi wote wa wahojiwa ulifanyika kwa kutumia njia ya sampuli nasibu."

Alisema ukiacha masuala mengine ya utendaji wa mawaziri, waliohojiwa walitakiwa kutoa tathimini yao kuhusu utendaji kazi wa Rais Kikwete katika kipindi cha takriban miaka mitatu ya utawala wake kwa kutoa maoni yao kama wanaridhika sana, wanaridhika kiasi au hawaridhiki.

Dk. Killian alisema kati ya wote waliohojiwa, asilimia 39.5 walisema wanaridhishwa sana na utendaji wa Rais Kikwete, asilimia 39.0 walisema wanaridhika kiasi na asilimia 19.3 walisema hawaridhiki na utendaji kazi wa mkuu huyo wa nchi.

Alisema hata hivyo kwa ujumla, matokeo ya utafiti wa Novemba mwaka jana yanaashiria kwamba, utendaji kazi wa Rais Kikwete bado unaonekana kuridhisha idadi kubwa ya watu pale ambapo makundi mawili ya wahojiwa yanapojumlishwa pamoja yaani wale wanaosema wanaridhika sana asilimia 39.5 na wale wanaosema wanaridhika kiasi asilimia 39 ikiwa inafanya idadi hiyo ya wahojiwa wote kufikia asilimia 78.5.

Dk Killian alisema sababu za kuridhika au kutoridhika na utendaji kazi wa serikali ya Rais Kikwete ni kutoridhishwa na ahadi yake ya kuboresha hali ya maisha. Asilimia 31.0 ya waliohojiwa walisema ameshindwa kuboresha hali ya maisha, wakati asilimia 24 walisema hajatimiza ahadi na asilimia 12.2 walisema hafuatilii utekelezaji wa ahadi zake.

"Sababu nyingine zilizotolewa na wahojiwa ni kuchagua viongozi wasiofaa asilimia 10.8, ameshindwa kupambana na rushwa asilimia 8.0, lakini pamoja na kwamba utafiti huu ulifanywa kipindi ambacho "vigogo" walikuwa wanapelekwa mahakamani kuhusiana na tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi na wengine kutuhumiwa na wizi wa fedha za akaunti ya madeni ya nje (EPA), ni asilimia 6 tu ndiyo waliotaja moja kwa moja suala hili kama sababu ya kutoridhishwa au kuridhishwa kiasi na utendaji kazi wa rais," alisema.

Alisema sababu za wananchi kutoridhika na utendaji wa serikali iliyo madarakani ni kutofuatilia utekelezaji asilimia 30.7, serikali kujihusisha na rushwa asilimia 29 na inapitisha mikataba mibovu asilimia 10.0.

Utafiti huo pia unaonyesha kuwa bunge ndio linaongoza kwa kutoridhisha wananchi baada ya asilimia kubwa ya waliohojiwa kueleza kuwa hawaridhishwi na taasisi hiyo ya kutunga sheria.

Bunge limeonekana kutoridhisha wengi tofauti na taasisi za serikali kama polisi, taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini, serikali za mitaa na kadhalika.

Dk. Killian alisema bunge linaongoza kwa kuwa na asilimia kubwa ya kiwango cha kutoridhika ambacho ni asilimia 77.4, ikifuatiwa na serikali za mitaa asilimia 75.6 wakati baraza la mawaziri linashika nafasi ya tatu kwa asilimia 63.

Kwa upande wa utendaji kazi wa Rais Amani Abeid Karume wa Zanzibar, utafiti unaonyesha kuwa asilimia 44 tu ya wote waliohojiwa wanaridhika sana, wakati asilimia 24 wanaridhika kiasi na asilimia 26 walisema hawaridhiki.

Alisema kiwango cha utendaji wa Rais Karume kimeonekana kupanda kwa asilimia 9 ukilinganisha na utafiti wa Oktoba 2007 wakati asilimia 35.5 tu ilimkubali baada ya kuporomoka kutoka asilimia 47.8 aliyopata kipindi cha hadi Oktoba 2006 na baadaye kupanda kutoka asilimia 35.5 Oktoba 2007.

CHANZO: Mwananchi



Nyota ya Kikwete Bado Yang'ara
na mwandishi Wetu


Watanzania walio wengi, zaidi ya asilimia 80, bado wana imani na Rais Jakaya Kikwete, kuliko miaka minne iliyopita alipochaguliwa kuwa Rais. Pia asilimia kubwa ya Watanzania inaridhishwa na utendaji kazi wa Rais na Serikali yake.

Kura ya maoni iliyoendeshwa na taasisi ya uchunguzi inayojitegemea ya REDET kuhusu utendaji wa Serikali ya Kikwete katika miaka mitatu iliyopita ya uongozi wake, inaonyesha kuwa asilimia 83.7 ya Watanzania wana imani naye.

Kundi hilo la Watanzania wanaothibitisha kuwa na imani na Rais Kikwete likigawanywa katika makundi ya ulinganisho wa imani, asilimia 50 inasema ina imani sana kwa kiongozi huyo, asilimia 33.7 inasema ina imani kiasi cha kutosha kwake.

Asilimia hiyo ni kubwa kuliko ile ya ushindi wa urais mwaka 2005, alipochaguliwa kwa kishindo ambapo alichaguliwa kwa asilimia 82. Hakuna mwanataaluma yeyote wa REDET ambaye alikubali kuzungumza na gazeti hili kuhusu kura hiyo ya maoni licha ya kupatikana kwa nakala ya matokeo ya utafiti huo.

Lakini habari zinasema matokeo kamili ya kura hiyo yanatarajiwa kutangazwa rasmi wiki ijayo na uongozi wa REDET. Kubwa zaidi katika ripoti hiyo, ni ukweli kuwa asilimia ya Watanzania wenye kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais Kikwete bado iko juu.

Utafiti huo wa kisayansi na wa kina uliofanyika katika sehemu mbalimbali za nchi mijini na vijijini unaonyesha kuwa asilimia 78 ya Watanzania wanaridhishwa na utendaji kazi wake. Matokeo ya kura hizo yamethibisha kwa mara nyingine, ukweli ambao umebakia bila kubadilika kuhusu imani ya wananchi kwa Rais Kikwete na utendaji wake tangu alipoingia madarakani.

Kura zote za maoni ambazo zimefanyika tangu wakati huo, zimekuwa zikionyesha kuwa kiwango cha imani ya wananchi wake na kwa utendaji kazi wake kimebakia kwenye eneo la asilimia 80. Kura hizo pia zinaonyesha kuwa imani ya wananchi kwa wasaidizi wake wakuu ni ya juu.

Zinaonyesha pia kuwa asilimia 82.7 wana imani na Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Shein akiwa nyuma ya Rais kwa asilimia moja, wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda anavutia asilimia 84. Utafiti huo pia unathibitisha kuwa wananchi kiasi cha asilimia 70 wana imani na Baraza la Mawaziri, wakati asilimia 66 wana imani na wakuu wa mikoa. Imani ya wananchi inashuka kidogo kwa Bunge ambalo lina asilimia 65.

Katika namna ambayo pia itakipa nguvu na kuifurahisha CCM, asilimia ya Watanzania ambao wanasema wanaridhishwa na utendaji kazi wa chama hicho ni 72.8 wakati asilimia 75.6 wanasema wana imani na chama hicho. Matokeo hayo yatakifurahisha chama hicho kwa sababu asilimia hiyo kubwa ya kukubaliwa na Watanzania imebakia ya kiwango hicho hicho kwa karibu miaka 17 tangu kuanzishwa kwa vyama vya upinzani nchini.

Mwaka 1992 wakati CCM na serikali zilipoongoza mageuzi ya kuingia katika mfumo wa vyama vingi, ilikuwa baada ya uchunguzi uliothibitisha kuwa ni asilimia 20 tu ya Watanzania waliokuwa wanataka mfumo wa vyama vingi. Kwa namna moja au nyingine, asilimia hiyo imebakia na kujithibitisha mara nyingi kupitia njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupitia uchaguzi mkuu ambao umefanyika tangu wakati huo na hasa uliopita uliomwingiza Rais Kikwete madarakani mwaka 2005. Kwa upande wa vyama vya upinzani, asilimia ya Watanzania ambayo inasema haina imani na vyama hivyo inabakia juu kwa asilimia zaidi ya 31.



CHANZO: HabariLeo



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































27 Apr 2009


KUNA MAMBO YANAYOTOKEA HUKO NYUMBANI YANAKERA KUPITA MFANO.HIVI HAWA WATANZANIA WENZETU WALIOKABIDHIWA DHAMANA YA KUTUONGOZA (TUKIAMINI KABISA KUWA WANA UPEO MZURI TU WA KUTAFAKARI MAMBO) WANAWEZAJE KUONGEA MAMBO YA AJABU NAMNA HII?ANYWAY,HEBU SOMA KWANZA HABARI HUSIKA KISHA TUENDELEE KUJADILI



* Waziri Sophia Simba asema Mengi kachemsha
*Mkuchika naye asema wanamchunguza

Ramadhan Semtawa na Leon Bahati

MAWAZIRI wawili, Sophia Simba na George Mkuchika jana walimshambulia mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi ambaye wiki iliyopita alitangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia, akisema ni mafisadi waliokubuhu.

Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Mkuchika, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo walisema mfanyabiashara huyo wa jijini Dar es salaam "amechemsha".

Mengi alitangaza majina ya wafanyabiashara hao Alhamisi iliyopita akisema ni kati ya watu wasiozidi 10 ambao alidai wanaifilisi nchi na kutaka wadhibitiwe mapema kabla hawajaitingisha na kuiyumbisha nchi. Hata hivyo, Mengi, ambaye alidai katika taarifa yake kuwa juhudi za Rais Jakaya Kikwete zinakwamishwa na watu hao, hakueleza jinsi watano hao wanavyoitafuna nchi zaidi ya kusema kuwa wanatorosha fedha wanazozipata 'kifisadi'.

Jana, kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam mawaziri hao wawili walitoa kauli za kumshambulia mwenyekiti huyo mtendaji wa makampuni ya IPP, kauli ambazo zinadokeza mtazamo wa serikali katika mjadala unaoendelea wa vita dhidi ya ufisadi na vinara wake.

Waziri Simba, ambaye wizara yake pia inawajibika katika vita dhidi ya ufisadi, alisema: "Kakosea... watoto wa mjini wanasema kachemsha." Simba alitoa msimamo huo jijini Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kufungua semina ya wadau wa vyama vya siasa kuhusu namna ya kuiboresha Sheria ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995.

Simba alisema Mengi hana mamlaka hayo ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Kabla ya kujibu swali kuhusu kitendo cha Mengi, ambaye anamiliki televisheni ya ITV na kituo cha redio cha Radio One Stereo, kutaja majina ya watu hao aliowaita
mafisadi papa, Simba alihoji: " Hapa kuna mtu wa ITV?." Baadaye alisema: "Sikilizeni, kwanza kitendo alichokifanya Mengi si sahihi, kakosea hawezi kuhukumu watu, mamlaka hayo anatoa wapi?"

Simba, huku akionekana kama mtu ambaye alikuwa akitafuta jukwaa kuzungumzia suala hilo, alisema Mengi amekosea kwa kuwa baadhi ya watu aliowataja wana kesi mahakamani."Anahukumu watu," alisema. "Kuna mtu kama Jeetu (Patel) ana kesi mahakamani (EPA), sasa unapokuja kusema ni fisadi wakati mahakama haijathibitisha, unakuwa na maana gani.

"Kwanza kwanini awatuhumu wafanyabiashara wenzake tu, ina maana si ana nia mbaya nao."

Alisema Mengi amechukua uamuzi huo kama vile serikali, wakati serikali ipo siku zote na imekuwa ikifanya kazi zake kwa umakini kwa kufuata misingi ya sheria.

"Serikali ipo na inafanya kazi kwa misingi ya sheria, sasa yeye kukaa na kutangaza watu nasema si sahihi kabisa. Mahakama pekee ndiyo inaweza kumtia mtu hatiani, lakini huwezi kuhukumu watu kama hakuna mamlaka."

Waziri Simba, ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), alisema Mengi hapaswi kutumia vyombo vyake vibaya. "Asitumie vyombo vyake kufanya atakavyo yeye. Huwezi kukaa katika chombo chako na kuanza kuhukumu watu. Kila mtu akifanya hivyo itakuaje," alihoji.

Akiongea na Mwananchi baada ya kupata taarifa za kauli ya Simba, Mengi alisema: "Namuombea kwa Mwenyezi Mungu na kwa maskini wa Tanzania ili wamsamehe kwa sababu hajui anenalo." Mengi hakutaka kuzungumza zaidi kuhusu hatua hiyo ya Mama Simba.

Naye Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali itamchukulia hatua za kisheria Mengi iwapo itabainika alikiuka taratibu na kanuni za nchi kwa kutangaza majina ya watu anaowatuhumu kwa ufisadi
.

Mkuchika alisema jijini Dar es Salaam jana kwa sasa serikali inafanya uchunguzi juu ya suala hilo na itatumia mikanda ya video pamoja na maelezo ya kimaandishi aliyoyatoa Mengi siku alipokutana na waandishi wa habari.

"Tumekusudia kupata ule mkanda wa video, pia tusome maelezo yake ya kimaandishi... tukigundua kuna mahala ambapo sheria haikuzingatiwa, (Mengi) atachukuliwa hatua," alisema Mkuchika.

Mkuchika alisema serikali imepokea malalamiko mengi kutoka kwa watu wengi, wakishutumu hatua iliyochukuliwa na Mengi, ambaye pia anamiliki viwanda vya vinywaji.

Bila kutaka kuwataja majina, Mkuchika alisema miongoni mwa walalamikaji, wapo walioeleza kuwa vyombo vya habari vya mfanyabiashara huyo havikuwatendea haki watuhumiwa waliotajwa kuwa ni mafisadi wakuu.

Alisema ni kutokana na vyombo hivyo kuwataja majina watuhumiwa bila ya kuwapa fursa ya kujibu madai dhidi yao. Waziri Mkuchika alipotakiwa kueleza siku ambayo uchunguzi huo utakamilika, alijibu wananchi wanapaswa kuwa watulivu kwa sababu serikali ikimaliza kuchunguza, itawatangazia yale waliyobaini.

Hii ni mara ya pili katika kipindi cha miezi takribani mitatu kwa Mengi kuingia katika mvutano na serikali baada ya kuvutana mapema mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kutokana na kutangaza kuwa kuna mipango ya kumfilisi na kumuua.

Mengi pia amewahi kujikuta katika malumbano na watendaji wa serikali hasa na waziri wa zamani wa nchi, ofisi ya rais (utawala bora), Wilson Masilingi alipotoa tuhuma kuwa suala la utoaji zabuni ya ununuzi wa hoteli ya Kilimanjaro, hivi sasa inajulikana kama Kilimanjaro Kempiski, kulikuwa na kitu alichokiita "mchezo mchafu". Suala hilo liliamsha malumbano makali, lakini liliishia hewani.

Katika tuhuma za wiki iliyopita, Mengi aliwahusisha wafanyabiashara hao watano na kashfa za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development (LLC) na uuzwaji wa jengo la Mfuko wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye kituo chake cha televisheni cha ITV kiliwahi kuendesha mchezo mkubwa wa bahati nasibu ya Jackpot Bingo, pia aliitaja Bahati Nasibu kuwa katika tuhuma hizo, pamoja na mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma.


CHANZO: Mwananchi


HALAFU TUKISEMA UFISADI NI MIONGONI MWA SERA ZA CCM TUTAITWA WACHOCHEZI?CHADEMA WALIPOTOA LIST OF SHAME CCM,KAMA KAWAIDA YAKE,IKAJA JUU KUDAI HIZO NI POROJO ZA KISIASA.WENGINE WAKAENDA MBALI ZAIDI NA KUTISHIA KUWAPELEKA AKINA SLAA MAHAKAMANI KWA MADAI YA "KASHFA".HADI LEO HAKUNA HATA MMOJA WAO ALIYEKWENDA MAHAKAMANI,NA SANASANA BAADHI YA WATUHUMIWA HAO KWA SASA WAKO MAHAKAMANI WAKITUHUMIWA KUHUSU YALEYALE YALOTAJWA KWENYE LIST OF SHAME.


TATIZO LA MAWAZIRI WOTE WAWILI SIO MANJI AU THE PATELS.NI MR UNTOUCHABLE.HUYU AKIGUSWA BASI NDIO KAMA UMEPIGA LUMUMBA,HQ YA CCM.HAIHITAJI UPEO WA JUU KUBAINI KUWA WANACHOONGEA MAWAZIRI HAO WAWILI NI SAWA NA SELF-DENIAL.YAANI TUKIMJUA MWIZI TUSIMUITE MWIZI MPAKA AFIKISHWE MAHAKAMANI?TUTAMFIKISHAJE HUKO PASIPO KUMTUHUMU IN THE FIRST PLACE?


NA KWANINI ALALAMIKE WAZIRI SIMBA NA MKUCHIKA NA SIO HAO WALIOTAJWA NA MENGI?WAMETUMWA AU WANATUMIWA?WASITUFANYE WATOTO KUHUSU HABARI ZA HAO MAPAPA WA UFISADI KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA VILE HILO HALIWEZEKANI.KWANI KUNA SABABU NYINGINE INAYOSABABISHA KUSUASUA KUWATAJA WAMILIKI WA KAGODA ZAIDI YA UKWELI KUWA AMONG THE WAMILIKI NI MR UNTOUCHABLE?


AH,SIJUI MAMBO HAYA YATAENDELEA HADI LINI!

Neighbours of a woman who ended up in court for her noisy love-making were savouring peace and quiet today after she was locked up accused of breaking her anti-social behaviour order.

Caroline Cartwright, 48, was remanded in custody until May 5 charged with three breaches of her Asbo in just 10 days. The four-year order was imposed by magistrates in Sunderland on April 17 and prevented Cartwright 'making excessive noise' anywhere in England
...continue


Judges could be forced to bow to Sharia law in some divorce cases heard in Britain.

An EU plan calls for family courts across Europe to hear cases using the laws of whichever country the couple involved have close links to. That could mean a court in England handling a case within the French legal framework,or even applying the laws of Saudi Arabia to a husband and wife living in Britain...
continue

As many as one in five British couples sleep in separate beds. According to a recent survey, snoring, tossing and turning, and talking in your sleep were cited as the main irritants, with ever more stressful careers and lives that demand a good night's rest making us increasingly reluctant to put up with them. But does choosing to sleep apart sound the death knell of intimacy? ...continue

Facebook messages, texts and internet addresses will all be logged and stored under new laws proposed by the Home Secretary today.Jacqui Smith said phone and internet providers would be legally obliged to retain records of customers' calls and internet usage.

However, the proposed plans fell short of a widely-predicted centralised database containing email, phone and web data.The information, to be stored for a year at a cost of £2bn, would be available to police in the event of criminal investigations...continue

MOJA YA MAENEO KOROFI KATIKA BARABARA KUU WILAYANI KILOMBERO.UNGETEGEMEA VIONGOZI WA WILAYA HIYO WAELEKEZE NGUVU ZAO KWENYE KU-ADDRESS SHIDA ZA WANANCHI (KAMA HIYO YA BARABARA) BADALA YA KUTAKA KUUZA ARDHI YAO.HUU NI UNYAMA USIOKUBALIKA HATA CHEMBE.ANYWAY,2010 IS COMING.I HOPE UKATILI HUU WA VIONGOZI WABABAISHAJI UTAKUWA SABABU TOSHA YA KUWAPIGA CHINI KWENYE UCHAGUZI.

na Mwandishi Wetu, Kilombero

KIJIJI cha Namwawala, kilichopo Kata ya Idete, Tarafa ya Ifakara, Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, kiko hatarini kuuzwa kwa mwekezaji, huku viongozi wanaosimamia mpango huo wakidai ni agizo kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.

Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka katika kijiji hicho, zilidai kuwa baadhi ya viongozi wa wilaya na mkoa, wanasimamia uuzaji wa ekari zaidi ya 3,384, sawa na asilimia 95 ya ardhi ya kijiji chote, kwa ajili ya mwekezaji anayetarajia kuanzisha mashamba ya miwa na kiwanda cha sukari.

Hivi sasa, kijiji hicho kimeunda kamati kufuatilia mambo manne ya msingi ambayo ni kuthibitisha kauli ya viongozi wao kwamba Rais Kikwete ameamuakuchukua ardhi hiyo, na kama ardhi inayochukuliwa ni asilimia 95 ya eneo lote la
kijiji.

Mambo mengine ni, Mkurugenzi Mtendaji Kilombero kuanza kuthaminisha mali zao bila taarifa rasmi na kutaka wasomewe waraka unaoelekeza Rais Kikwete kutoa agizo la kuchukua ardhi na kumpa mwekezaji.

Kamati hiyo ambayo inadaiwa kuishi kwa kutishiwa na baadhi ya viongozi wilayani humo, inaundwa na Mwenyekiti Zuberi Kapindijega, Kenani Haule (Katibu), wakati wajumbe ni Johson Msuya na Godfrey Lwema.

Akizungumza na Tanzania Daima kutoka mjini Ifakara jana, Kapindijega, alisema baada ya viongozi wa wilaya na kata kupita kwa wananchi na kuwataka waanze kufanya tathimini ya mali zao na kujiandaa kuhama, walifikisha barua yao kwa Rais Kikwete jijini Dar es Salaam wakitaka ufafanuzi wa mpango huo.

“Januari 31 kwenye mkutano wa mapato na matumizi ya kijiji, iliibuka hoja ya wanakijiji kutaka kujua hatma ya ardhi yetu, ndipo mwenyekiti wa kijiji alitusomea waraka aliodai wa rais, ambao umetumika katika kuchukua asilimi 95 ya ardhi hiyo. Kutokana na mazingira na mfumo uliotumika kufikisha waraka huo wa rais kwetu, tunahisi kuna mchezo
mchafu.

“Kwa hofu hiyo na kwa kuwa kila tunaloliuliza jibu ni moja tu la rais kaamua kuchukua ardhi yake, ndiyo maana tumeamua kuja kuonana na wewe mwenyewe Mheshimiwa Rais,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo kwenda kwa rais iliyoandikwa Februari 13 na Tanzania Daima kupata nakala yake.

Hata hivyo, katika majibu ya rais kwa viongozi hao wa tume yalitolewa kwa barua iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, F. Mwaipaja, Februari 16, viongozi hao walitakiwa kuwasiliana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, na Mkuu wa Mkoa na kama hawataridhishwa, wanaweza kuonana na rais.

Kutokana na barua hiyo kutoka kwa rais, viongozi wa tume hiyo walibisha hodi katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero kwa barua waliyoiandika Februari 20 nakufuatiwa na nyingine ya Februari 27, ambazo pia Tanzania Daima nakala zake inazo.

Hata hivyo, ofisi hiyo ya mkuu wa wilaya, ilijibu barua hiyo kupitia kwa Katibu Tawala, E Mmbaga, akidai kuwa ameagizwa na DC Evarist Evarist Ndikilo awajulishe wajumbe hao wa tume kwamba amepokea barua hizo.

“Aidha mnafahamishwa kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itawasiliana na SUDECO, Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), Serikali ya Kijiji (Namwawala) pamoja na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W), wanafanya tathmini ya fidia. Mnaombwa mvute subira kwani matokeo ya mawasiliano hayo, mtajulishwa,” ilisema barua hiyo.

Baada ya majibu hayo, tume hiyo pia ilifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, na kuwasilisha barua yao Machi 6, mwaka huu kutaka kupata ufafanuzi wa kuuzwa kwa ardhi ya kijiji chao.

Ofisi ya mkoa kupitia kwa Kaimu Katibu Tawala, L. Msuya, iliahidi katika barua yenye kumb namba CD/148/06/87, kwamba italishughulikia suala hili kwa makini.

“Kumbukeni kwamba mmeshafikisha malalamiko yenu kwenye ofisi ya rais na sasa mmerudishwa kwa Mkuu wa Mkoa, kwa hiyo suala hili linatakiwa lishughulikiwe kwa umakini sana.
Mnatakiwa mvute subira wakati mkuu wa mkoa anafanya uchunguzi wa kina ili kupata ufumbuzi wa kudumu,” ilisema barua hiyo.

Hata hivyo, akizungumzia malalamiko ya tume hiyo, DC wa Kilombero, jana alikaririwa na moja ya vyombo vya habari vya kila siku kwamba wajumbe wa tume hiyo ni wachochezi na kutoa amri wakamatwe mara moja.

Uchunguzi wa Tanzania Daima umebaini kuwa, hali ya kijiji hicho si shwari kwani wananchi wanashindwa kuendelea kufanya shughuli za maendeleo kwa hofu ya kuhamishwa, huku baadhi ya viongozi wakitofautiana kuhusu mpango huo unaodaiwa kuendeshwa kiujanja ujanja kwa kutumia jina la rais.


THIS IS BECOMING PERSONAL!TATIZO LA WILAYA YETU (NA JIMBO LA KILOMBERO KWA UJUMLA) NI KAMA HATUNA MBUNGE.KUNA JAMAA ANAITWA LIGALAMA.I JUST CANT UNDERSTAND WHAT THIS GUY HAS BEEN DOING!BADALA YA VIONGOZI KUWEKEZA NGUVU ZAO KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO WAO WANAENDEKEZA USHKAJI NA WAWEKEZAJI....NA HAIHITAJI UTAFITI KUFAHAMU KUWA KICHOCHEO KIKUBWA HAPO NI RUSHWA NA UFISADI KWA UJUMLA.

26 Apr 2009


KUNA kila dalili kuwa taifa halielekei pazuri hasa baada ya siku za hivi karibuni kuibuka matukio kadhaa ambayo kwa kiasi kikubwa yameishtua jamii kiasi cha kuhoji taifa linakoelekea.

Matukio ya kiongozi wa nchi kudhalilishwa kwenye mtandao wa kompyuta, malumbano ya wabunge juu ya kuvuja kwa siri za serikali na kuanikwa kwa mishahara yao pamoja na hatua ya Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, kutaja majina ya watu anaowatuhumu kuwa mafisadi ‘papa’ hadharani.

Kutokea kwa matukio hayo katika kipindi hiki ambacho taifa linaelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika mwakani kumeelezwa ni mambo ambayo kwa kiasi kikubwa yanaweza kuliyumbisha taifa.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii wanayaona matukio hayo kama ni mapambano ya hatari yanayowahusisha baadhi ya wafanyabiashara na vigogo wa siasa ambao katika siku za hivi karibuni wamekuwa wakitumia njia mbalimbali kuhakikisha wanafanikisha mikakati ya kuongoza.

Tukio la Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, kuwataja baadhi ya wafanyabiashara na wanasiasa maarufu hapa nchini kuhusika na kashfa za ufisadi limezua mtafaruku miongoni mwa jamii ambapo baadhi ya watu wanaiona hatua hiyo ni mapambano ya hadharani baina ya pande hizo mbili.

Mapambano hayo ambayo katika siku za hivi karibuni yamefikia hatua mbaya kiasi cha kuanza kuhusisha uandishi wa habari usiozingatia maadili ya fani ya habari umeonekana kutumika kwa ajili ya kukashfu na kudhalilisha utu wa baadhi ya walengwa.

Vita ya pande hizo mbili vinaonekana kuanza kushika kasi na kuna habari kuwa baadhi ya wafanyabiashara waliotajwa na Mengi wamejipanga kujibu mashambulizi hayo kwa gharama zozote zile.

Wakati mapambano hayo yakionekana ni ya pande mbili wanasiasa, wafanyabiashara na wananchi mbalimbali wamejikuta ama wanaunga mkono upande mmoja au mwingine hali inayozidisha utete wa vita hivyo.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii wamebainisha kuwa hali hii ya sasa imekuja hasa baada ya ufisadi wa EPA, Meremeta, Richmond na kadhalika ambao ulisababisha baadhi ya viongozi akiwemo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowasa kujiuzulu.

Kujiuzulu kwa viongozi hao na kufikishwa mahakamani kwa baadhi ya watuhumiwa walioshiriki katika kashfa hizo na za matumizi mabaya ya madaraka kumechochea vita dhidi ya ufisadi huku baadhi ya wananchi wakitaka pia Rais wa mstaafu, Benjamini Mkapa, naye aondolewe kinga ili aweze kujibu tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka.

Hatua ya Mengi kujitokeza hadharani na kutaka majina ya watu anaowatuhumu kwa kashfa za ufisadi na baadhi ya wabunge kuwachachamalia watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi nako kumezidisha joto na hofu ya mapambano hayo.

Wakati mawazo ya watu yakiwa bado katika mzozo huo, limetokea tukio jingine la kusikitisha katika mtandao ambapo kiongozi wa nchi amejikuta akidhalilishwa kwa picha zisizofaa mbele ya jamii.

Tukio hilo kwa kiasi kikubwa linaonyesha ukosefu wa ustaarabu na maadili kwa baadhi ya watu ambao wameamua kutumia vibaya teknolojia ya kisasa hususan upashanaji habari kwa kutumia mtandao.

Jambo hilo kwa kiasi kikubwa limekuwa likihusishwa na mbinu za kuchafuliana majina hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi na kubainishwa kuwa kama hatua za haraka za kuwakamata wanaohusika na mitandao hiyo zisipochukuliwa kuna hatari ya viongozi wengi zaidi kudhalilishwa kupitia mambo mbalimbali.

Moja kati ya tukio la udhalilishaji wa viongozi ni hatua ya kijana mmoja kuamua kumpiga kofi Rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, katika sherehe za Maulid zilizofanyika kwenye Ukumbi wa Daimond Jubilee, Dar es salaam.

Sakata jingine ambalo limeonekana kuwagawa zaidi Watanzania na wanasiasa ni kauli ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma, kuwa kuanzia sasa wabunge na watendaji wote watakaovujisha siri za serikali watashughulikiwa ipasavyo.

Kauli hiyo ambayo ilionekana kumlenga Mbunge wa Karatu Dk. Wilbrod Slaa (CHADEMA) na baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wakitumia nyaraka mbalimbali zinazodaiwa kuwa za siri kuiumbua serikali sasa watakumbana na mikono ya sheria endapo watakutwa na nyaraka hizo.

Kauli hiyo imeonekana kupingwa na wananchi wengi kwa madai kuwa sasa serikali inataka kuwa ya kidikteta hasa kwa kuficha nyaraka za ufisadi uliofanywa au unaofanywa na viongozi waliopo na waliomaliza muda wao madarakani.

Baadhi ya wananchi wamekuwa wakiihusisha kauli hiyo kama ni njama za kuficha uovu ambao umekuwa ukipoteza fedha nyingi za Watanzania kupitia rasilimali mbalimbali.

Mshangao huo wa wananchi uliongezeka zaidi pale baadhi ya wabunge walimshutumu hadharani Dk. Slaa kwa kubainisha vipato wanavyovipata wabunge na kutaka fedha hizo zipunguzwe ili zitumike kwa maendeleo ya wananchi.

Baadhi ya wabunge walimtuhumu Dk. Slaa kwa kutaka kujitafutia umaarufu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu ujao jambo ambalo limepingwa vikali na wananchi wanaoonekana kukubaliana na ushauri wa Dk. Slaa.

Matukio haya kwa kiasi kikubwa kwa namna moja au nyingine yanaonyesha kuliweka taifa katika sehemu mbaya na iwapo kama hatua za kurekebisha baadhi ya mambo hazitachukuliwa kuna kila dalili za kutokea mpasuko mkubwa miongoni mwa jamii.

Naye Rahel Chizoza anaripoti kutoka Dodoma kuwa sakata la wizi wa nyaraka za serikali na kuwekwa hadharani kwa mishahara minono na marupurupu wanayopata wabunge kulikoibuliwa na Mbunge wa Karatu Dk. Wilbrod Slaa (CHADEMA), hivi karibuni limechukua sura mpya baada ya baadhi ya wabunge kuonyesha kumchukia mbunge huyo.

Hali hiyo imejitokeza jana kwenye semina ya maboresho ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma iliyoendeshwa kwa wabunge ambao baadhi yao walionyesha hali ya kumbeza mbunge huyo aliposimama kwa ajili ya kuchangia hoja.

Hali hiyo ilisababisha mwenyekiti wa semina hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Mpwapwa, George Lubeleje, kuingilia kati na kuwasihi wabunge kupunguza minong’ono.

“Hivi hizi nyaraka zinazodaiwa kuwa ni za siri, kwa nini zinawekwa kwenye makabati ya serikali, naomba Katibu Mkuu aniambie kama ni halali kwa nyaraka za wizi kuwepo katika kabati za serikali,” alihoji Dk. Slaa

CHANZO:Tanzania Daima

25 Apr 2009


DECI....DECI...DECI.NDIO GUMZO HUKO NYUMBANI.LAKINI KUNA MENGI YANAYOHITAJI TAFAKURI PANA KUHUSU SUALA HILO.TRULY YOURS NIMEJARIBU KUCHANGANUA SUALA HILO KWA UNDANI KIDOGO.ANGALIA HAPO JUU KULIA KWENYE SECTION YA AUDIO USIKIE UCHAMBUZI HUO.NIRUSHIE BARUA-PEPE TUENDELEZE MJADALA KWA MANUFAA YA TAIFA.NA KAMA NIMECHEMSHA,USISITE KUNIKOSOA.
KARIBUNI SANA!!!



MZALENDO MMOJA AMENITUMIA UJUMBE UFUATO KWENYE E-MAIL,NAMI NAOMBA KUUWASILISHA KAMA ULIVYO:


Kuna habari kwamba mmoja wa wafanyabiashara aliyetajwa na Mkurugenzi wa IPP Bwana Reginald Mengi amenunua hisa nyingi za umiliki wa kituo cha kurusha matangazo ya Television.

Mfanya biashara huyo inasemekana ni yule aliyetumia mtindo huohuo kununua hisa za kampuni iliyokuwa inatoa gazeti lilikuwa maarufu kabla ya mwaka 2005 na sasa si maarufu tena.

Mfanyabiashara huyo ambaye ana hisa kwenye kampuni moja ya simu za mikononi inasemekana ana mpango wa kutumia minara ya kampuni hiyo ya simu ili kusambaza matangazo ya kituo hicho nchi nzima kwa urahisi na bila gharama kubwa.

Kwa vile kampuni yake ndiyo yenye mtandao mkubwa hapa nchini basi itakuwa ni rahisi kwake kusikika nchi nzima kuzidi vyombo vyote vya habari.

Iwapo mpango huo utatekelezwa basi mfanyabiashara huyo atakuwa anaongoza kusikika eneo kubwa nchini.

Bwana Mengi ina ITV na Redio zake tabidi avute bidii ya kasi kwa sababu yeye hataweza kuwa na mtandao mkubwa kama hiyo TV.

Wenu mtafuta habari

24 Apr 2009


Boniface Meena na Mkinga Mkinga

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Reginald Mengi jana aliamua kujitoa muhanga alipotangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia ambao anadai kuwa ni mafisadi papa wanaoiba mabilioni ya fedha za wananchi na kutaka wachukuliwe hatua kwa madai kuwa wataiyumbisha na kuitingisha nchi.

Kati ya wafanyabiashara waliotajwa na Mengi, wawili wamefunguliwa mashtaka ya tuhuma za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), wengine wakiwa wameshatajwa kwenye kashfa mbalimbali, zikiwemo za zabuni ya utoaji umeme wa dharura ya Richmond Development na uuzwaji wa jengo la Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye anamiliki kampuni ya IPP yenye kampuni mbalimbali zikiwemo za habari na vinywaji, alitaja wafanyabiashara hao watano akisema kuwa ndio papa kwa ufisadi lakini akasema idadi ya mafisadi wanaofilisi nchi hawazidi 10.

"Wanaotuhumiwa kuwa mafisadi papa wanahusishwa na karibu kila kashfa kubwa hapa nchini zikiwepo kashfa za Richmond, EPA, Dowans, helikopta na magari ya jeshi, ndege ya rais, rada, NSSF, Bahati Nasibu ya Taifa, mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma na kadhalika," alidai Mengi katika mkutano wake na waandishi wa habari alioufanya kwenye ofisi yake jijini Dar es salaam.
>
Kati ya wafanyabiashara hao watano ambao Mengi alidai ni mapapa wa ufisadi, wamo Rostam Aziz, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel), ambao Mwananchi ilipata nafasi ya kuzungumza nao kuhusu tuhuma hizo za Mengi.

Hata hivyo, Mengi hakuwa tayari kutoa vielelezo kuthibitisha madai yake, lakini akasema iwapo watamshtaki mahakamani na wafanye hivyo kwa kuwa huko ndiko haki inakopatikana.

Mengi alirusha tuhuma nyingi kwa watu hao ambao alidai kuwa wamecharuka baada ya Rais Jakaya Kikwete kuamua kupambana nao na hivyo wameamua kupambana na yeyote anayemsaidia mkuu huyo wa nchi katika vita hiyo.

"Jitihada kubwa za Mhe. Rais za kuleta maendeleo na maisha bora kwa kila Mtanzania zinazoofishwa na wizi mkubwa wa rasilimali za taifa. Bado Watanzania wengi wanaandamwa na umaskini mkubwa; hawajui hata mlo mmoja kwa siku utatoka wapi," alidai Mengi ambaye pia alitoa taarifa ya maandishi aliyoisaini.

"Cha kusikitisha ni kuwa pale Mtanzania mwema mwenye uwezo anaposaidia jamii kuondokana na umasikini, mafisadi wanapiga kelele kuwa misaada ya aina hiyo ina agenda. Wanapinga kwa kuwa wanataka Watanzania wafe na njaa na matatizo mengine."

Mengi alikwenda mbali zaidi na kudai mafisadi anaowatuhumu wanaweza wakaunga mkono matatizo yanayotokana na Deci, taasisi inayoendesha mchezo wa kuchangisha fedha na kulipa maradufu na Watanzania kubakia "wakifukuzana na wachungaji bila ya kujiuliza ni kina nani hasa wanachochea vurugu".

Wakiongea na Mwananchi, watu hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi hawakutaka kujibu kwa kirefu na badala yake walimtuhumu mwenyekiti huyo mtendaji wa IPP kuwa ana wivu, fitina chuki na ambaye ameshindwa kuendesha nyumba na biashara zake, huku mwingine akieleza kuwa anatumia haki yake ya kidemokrasia ya kutoa maoni yake.

"Mengi... (si mstaarabu)," alisema Manji ambaye anamiliki kampuni ya Quality Group. " Biashara zake zimemshinda ndio maana anazungumza ovyo." Rostam Aziz, ambaye ni mbunge wa Igunga anayejishughulisha na biashara mbalimbali za miradi mikubwa ya ujenzi, uchimbaji na habari, alimuelezea Mengi kama mtu ambaye analingana kwa umri na baba yake mzazi na hivyo hawezi kubishana naye.

Lakini akasema: "Mengi amejaa chuki, wivu na fitina. Sina cha kumsaidia isipokuwa kumuombea Mungu ili amsaidie kwa kumpuuzia hayo maana ni adhabu kwa nafsi yake mwenyewe. Kwa malezi niliyopata, siwezi kubishana na mzee."

Jeetu Patel naye alisema haoni busara kujibizana na Mengi na kwamba alichofanya mwenyekiti huyo wa Chama cha Wafanyabiashara Wenye Viwanda (CTI) ni kutumia haki yake ya kidemokrasia ya uhuru wa kuongea.

“Hayo ni matatizo yake," alisema Patel, ambaye anakabiliwa na kesi ya tuhuma za wizi wa fedha za EPA. "Amewaita waandishi kuzungumza nao... sikumsikia lakini ninachoweza kusema ni kwamba anatumia uhuru wake wa kujieleza.>
"Binafsi sijui chochote kuhusu hizo tuhuma za Mengi dhidi yangu, ila anayo haki ya kusema chochote. Nina mambo mengi ya kufanya hivyo sioni kama itanisaidia kwenye biashara zangu za kila siku kuanza majibizano na Mengi."

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mengi alidai kuwa watu hao aliowataja si tu kwamba wanaiba rasilimali za Tanzania, bali pia wanaiba muda wa Watanzania.

"Badala ya kutumia muda katika shughuli za maendeleo, tunajikuta tukitumia muda mwingi kupambana nao na hawatingishiki," alidai Mengi. "Badala yake wanatumia fedha walizotuibia kuanzisha magazeti ya kujenga kiburi cha kutudharau, kututukana na kutunyanyasa. Inakuwa kesi ya mwizi kumkimbiza na kumpiga aliyeibiwa.

"Hata sasa hivi, mafisadi papa wanaendelea kutumia uwezo wao wa kiuchumi uliotokana na wizi wa rasilimali za nchi yetu kushawishi na kupata miradi mikubwa mikubwa kwa kutumia majina tofauti tofauti huku wakipuuza kabisa kelele za wananchi kuhusu ufisadi wao.

Alisema ni muhimu wananchi wakajiuliza hawa mafisadi wanapata wapi ujasiri wa majigambo, dharau na nguvu za kutukana na kunyanyasa watu.

Alisema mafisadi papa ni lazima wajue kwamba iwapo wapambanaji wa ufisadi watapata madhara kwa njia yoyote hapa nchini au nje ya nchi, wananchi wa Tanzania watawawajibisha.

"Ni lazima Watanzania wote tuone kwamba sasa tumefika mahali pa kusema imetosha," alidai Mengi.

CHANZO:Mwananchi

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.