13 Nov 2008

They lecture the rest of us on the evils of discrimination in the workplace. But those in charge of the Equality and Human Rights Commission don't seem to be following their own advice. 

Female staff at the superquango are paid less than the men, it was revealed yesterday. The gap between the average pay of the sexes runs at more than 15 per cent, figures given to MPs showed. 

They mean that a typical female employee of the £70million-a-year equality body gets £85 a week less than a typical male worker. 

The organisation also pays its white staff more than blacks, by a margin of more than 6 per cent, and able-bodied employees more than disabled workers. 

The commission, headed by Labour activist Trevor Phillips, has been scathing about the shortcomings of other employers when it comes to women's pay. 

In September it published a report accusing bosses of being wedded to old-fashioned ways of working that are unfair to women. 

The pay gap between men and women in the workforce in general, in terms of average hourly earnings, is 17.2 per cent. 

It was this figure which led one of the commission's governors, Margaret Prosser, to declare that full-time women workers 'are cheated of £330,000 over the course of their lifetime'. 

Equalities minister Maria Eagle told MPs that the commission's salary figures covered the average of total earnings and did not take into account the effects of part-time working. 

She said no figures for hourly rates of pay were available because the commission was still 'harmonising' pay rates inherited from the equality quangos it took over last year. 

She said: 'These new rates have now been agreed with trade unions and staff have been consulted. It is expected that these new arrangements will be implemented shortly.' 

The commission, which started work in October last year, employed 518 staff this spring. It pays its male employees an average of £33,366.96. 

The average salary for its women staff is £28,920.48, an amount £4,446.48 or 15.4 per cent lower. 

The figures compare with average pay of £23,750 for all workers, men and women, in the economy as a whole. 

Black and ethnic minority staff at the commission average £29,035.12, or 6.1 per cent below the £30,803.91 average paid to white employees. Disabled staff get an average of £29,784.07, which is 2.7 per cent below the £30,598.81 average paid to able-bodied employees. 

The figures provoked outrage among critics of the commission. Tory MP Philip Davies, whose parliamentary question drew the details from ministers, said: 'Given that this organisation is always banging on about the faults of employers, it is astonishing to find that it is paying men more than women. 

'To lecture everybody else about doing something they can't do themselves is hypocrisy beyond belief.' 

He added: 'Since their top man is black, there must be real discrepancies lower down in the organisation for them to end up paying blacks less than whites.' 

Ruth Lea, economic adviser to the Arbuthnot Banking Group, said: 'This is a reality check. If the commission is paying its male staff more on average than it pays to its female staff, it must think they are worth more on average. It is one of life's little ironies.' 

SOURCE: Daily Mail

12 Nov 2008

MKURUGENZI wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah, amesema kuwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote wa ufisadi kwa pamoja kunaweza kusababisha nchi kuyumba.

Hoseah alisema hayo katika siku ambayo hakukuwa na mtuhumiwa yeyote katika sakata la wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) aliyefikishwa mahakamani baada ya wafanyabiashara 20 kupandishwa mfululizo kizimbani kuanzia Jumatano iliyopita hadi juzi.

Akitoa mada kwenye semina iliyohusisha vyuo vikuu tisa nchini iliyofanyika kwenye Hoteli ya Blue Pearl jijini, mkurugenzi huyo wa Takukuru alisema: "Tukiwapeleka wote mara moja mahakamani, nchi inaweza 'ikaparalyse' (ikapooza) ni lazima kuwe na 'stability' (kutoyumba), tufanye kwa kuwa ni sahihi," alisema Hoseah.

Akitoa mada katika semina hiyo iliyowahusisha wajumbe wa kamati za maadili kutoka vyuo hivyo, Hoseah alieleza kuwa, mapambano dhidi ya rushwa kubwa yanapaswa kufanyika kukiwa na utashi wenye nguvu wa kisiasa, mikakati sahihi ya kiuchumi pamoja na kuzuia rushwa.

Alisema kuwa watuhumiwa wa rushwa kubwa wana nguvu kutokana na fedha nyingi wanazomiliki, kiasi cha kuweza kuhatarisha usalama wa watu wengine kwa kutumia vibaya fedha zao.

Dk Hoseah ni kigogo wa tatu kuzungumzia uwezo wa mafisadi na hatari ya kuwashughulikia bila ya umakini baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kulieleza bunge kuwa, kushughulikia watu wenye uwezo wa kifedha ni kazi ngumu, kama ilivyoelezwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Ali Hassan Mwinyi kuwa mafisadi ni hatari.

Watuhumiwa katika kashfa hiyo ya EPA wanadaiwa kuchota fedha hizo katika kipindi cha mwaka 2005/06 wakisingizia kupewa au kulipa madeni na makampuni ya nje yaliyokuwa yakiidai serikali. Watuhumiwa hao wanadaiwa kuchota Sh133 bilioni.

Pamoja na kilio cha wananchi kuwa wote waliochota fedha hizo wapandishwe kizimbani, Rais Jakaya Kikwete alitoa maagizo kuwa wale ambao wangeshindwa kurejesha fedha walizochota kabla ya Oktoba 31, ndio waliotakiwa kufikishwa mahakamani.

Na watuhumiwa hao 20 waliofikishwa mahakamani hadi sasa wamekuwa wakipandishwa kizimbani kwa nyakati tofauti na wengi wameshtakiwa kwa makosa tofauti, wakipandishwa mmoja mmoja na wakati mwingine kuunganishwa na wenzao na kwa mahakimu tofauti.

Akitoa mada yake jana, Dk Hosea alisema Takukuru peke yake haiwezi kumaliza tatizo la rushwa nchini bila kuwepo ushirikiano kutoka kwa taasisi za elimu, mashirika mbalimbali na wananchi.

Aliongeza kuwa, mapambano dhidi ya rushwa, kubwa na ndogo yanapaswa kuwashirikisha wananchi wote, huku akielezea Watanzania kuwa ni waoga kutokana na kukosa ufahamu wa masuala mbalimbali yanayowahusu.

Hoseah alisema kuwa katika mapambano ya rushwa ni vema kuzuia rushwa na kwamba uadilifu ndiyo njia bora ya kulitokomeza tatizo hilo.

Alisema moja ya kasoro za Tanzania ni kuwa na taasisi nyingi dhaifu, zisizo na uwezo zinazofanya kazi zake bila ya uwazi, hali aliyoielezea kuwa inakaribisha rushwa.

"Moja ya kasoro za Tanzania ni kuwa na taasisi dhaifu, zisizo na uwazi... lazima tufanye kazi kuzipa nguvu kwa kurejesha maadili," alisema Hoseah.

Aliongeza kuwa, ndani ya serikali pia uadilifu upo chini na kueleza kuwa kuwa kutokana na hali hiyo ni vema wananchi wakaacha kulalamika badala yake kutafuta ufumbuzi wa tatizo kwa kushiriki kurejesha maadili na kupambana na rushwa.

Alisema kuwa Watanzania wengi wamekuwa wakilalamikia tatizo la rushwa huku wakishinikiza Takukuru ichukue hatua bila wao kushiriki katika mapambano hayo ambayo alisema kuwa ni ya kila mmoja.

Mkurugenzi huyo wa Takukuru alisema kuwa katika kutilia maanani umuhimu wa kuongeza jitihada za kuzuia na kupambana na rushwa nchini, wameanzisha mkakati maalumu wenye lengo la kurejesha uadilifu nchini.

"Tunataka kurejesha maadili, lengo ni kuzuia rushwa, jukumu letu ni kuwawezesha watu wafahamu na kushiriki katika mapambano hayo," alisema.

Kwenye Mahakama ya Kisutu, hali jana ilikuwa shwari baada ya siku nne za purukushani za kupandisha kizimbani watuhumiwa hao 20, ambao kati yao ni wawili tu waliopata dhamana kutokana na mahakama kuweka masharti magumu, anaripoti James Magai na Paulina Richard.

Hadi majira ya alasiri jana, hakuna mtuhumiwa hata mmoja mpya kwenye kesi hiyo ambaye alikuwa amefikishwa mahakamani hapo.

Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Inspekta Charles Kenyela, aliwaambia waandishi wa habari kuwa hadi mchana huo hakuwa na taarifa za kuwepo kwa watuhumiwa wengine ambao wangepandishwa kizimbani.

Mpaka sasa ni wamiliki wa kampuni 10 tu kati ya 22 zinazodaiwa kuchota fedha hizo ambao walikuwa wameshafikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, akiwemo mfanyabiashara maarufu mwenye asili ya Kiasia, Jayatkumar Chantubhai Patel, ambaye anajulikana zaidi kwa jina la Jeetu Patel.

Tofauti na siku nyingine jana hali ilionekana kuwa tulivu mahakamani hapo huku kukiwa na pilikapilika chache za baadhi ya ndugu wa watuhumiwa katika kashfa hiyo ya EPA ambao walikuwa wakishughulikia dhamana za watuhumiwa hao.

Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Elieza Feleshi, hakutaka kuwaambia waandishi kama kuna watuhumiwa zaidi ambao wangefikishwa mahakamani jana na badala yake alisema aulizwe msemaji wa Wizara ya Sheria na Katiba.

Hata hivyo, msemaji huyo, Omega Ngole alijibu kwa ufupi kuwa hawawezi kusema ni lini watuhumiwa wanapelekwa mahakamani na badala yake taratibu zinapokamilika na DPP kujiridhisha, wahusika hufikishwa mahakamani.

“Hivyo ninachoweza kukuambia ni kwamba, tumwache DPP afanye kazi, kama kuna watu wa kuwapeleka mahakamani akishajiridhisha atawapeleka,” alisema Ngoe.

Wamiliki wa makampuni waliofikishwa mahakamani mpaka sasa ni Johnson na Mwesiga wanaomiliki kampuni ya Kernel, Ketan Chohan, Jeetu Patel na Amit Nandy (Bina Resort na Itoh), Bahati Mahenge, Manase Mwakale, Davis Kamungu, Godfrey Mosha na Edah Nkoma Mwakale (Changanyike Residential Compelex Ltd)

Wengine ni Rajabu Farijala, Japhet Lema na Rajabu Malanda (Mibale Farm), Rajabu Farijala na Rajabu Malanda (Money Planner), Japhet Lema (Njake Enterprises) na Ajay Somani na Jay Somani (Liquidity Services).

Wengine ni Jeetu Patel na ndugu zake wanaomiliki kampuni za Bencon International Ltd, Maltan Mining Ltd na Navy Cut Tobacco (T) Ltd.

CHANZO: Mwananchi

HAYO NDIO MATUNDA YA PhD YA HOSEA KATIKA KUPAMBANA NA RUSHWA AU NDIO APPLICATION YA THEORY FLANI YA KULINDA UHALIFU INAYODAI KWAMBA UKIFUTA KABISA UHALIFU KWENYE JAMII BASI VYOMBO VYA KUPAMBANA NA UHALIFU VITAKUWA HAVINA KAZI YA KUFANYA?MBONA VITA YA SOKOINE DHIDI YA WAHUJUMU UCHUMI HAIKUYUMBISHA NCHI?


A British car dealer has found one way around the looming recession -- by offering a buy-one-get-one-free offer on new cars, a report said Saturday. 

Online car broker Broadspeed.com, based in Colchester near London, offered customers two Dodge Avenger SXT saloon cars, complete with leather seats and air conditioning, for 20,000 pounds (24,450 euros, 31,300 dollars).

The dealership based in Colchester near London has just sold the last of the cars.

Managing director Simon Empson told the Guardian newspaper: "It was amazing. We had been trying to sell those cars online at half price for nearly a month and they were selling, but it was nothing special.

"But when we made the deal two-for-one, we got 22,000 customers.

"The very first call I had was from a father who was going to buy the two cars, have one himself and give the other to his son."

The number of new cars sold in Britain in October fell by nearly a quarter compared with the same period a year ago, the biggest decline since 1991.

SOURCE: Yahoo! News



A BBC Radio presenter has been sacked following a 'racist' call to a taxi firm, in which she requested a 'non-Asian' driver.

Sam Mason told the operator that 'a guy with a turban would freak her daughter out' insisting they send an English driver instead.

The ex-glamour girl, 40, called the firm to order a taxi for her 14-year-old daughter off-air, while presenting her BBC Bristol radio show.

After the operator branded her request 'racist', Mason insisted, claiming it wasn't the first time she had made the request.

She said: 'A guy with a turban is going to freak her out. She's not used to Asians.'
When the operator said it would not be possible to carry out her wishes, she said: 'You've managed it before.'

Mason, who has previously battled alcohol addiction, claimed she wasn't racist but insisted she was looking out for her daughter's interest.

Mason said: 'If it were me I wouldn't care if it had two heads, but it's my little girl we are talking about.'

After the operator refused to book a car, Mason complained before hanging up.

The operator said: 'We would class that as being racist. We can't just penalise the Asian drivers and just send an English one.'

She later called back before a manager accepted the booking.

Mason said: 'I work at the BBC. I'm far from racist and that uneducated woman has no right to call me one.'

The BBC were alerted to the conversation after it was recorded and sent to the Sun newspaper. 
The mother-of-one was subsequently suspended and fired 24 hours later.

A BBC spokesman said: 'Although Sam Mason's remarks were not made on-air, her comments were completely unacceptable and, for that reason, she has been informed that she will no longer be working for the BBC with immediate effect.'

SOURCE: Daily Mail


Serikali imewataka wanafunzi wote wa vyuo vya elimu ya juu nchini kuingia madarasani mara moja ifikapo saa moja asubuhi leo. Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe alisema sera ya uchangiaji huduma za jamii ikiwamo elimu, halikwepeki katika mazingira haya ya kiuchumi. 

“Sera yoyote ile haiwezi kubadilishwa mara moja bila ya majadiliano ya kina yanahusisha wadau wote,” alisisitiza Profesa Maghembe, katika kujibu madai ya wanafunzi hao wanaopinga sera ya uchangiaji elimu ya juu hasa suala la mikopo wakitaka kulipwa asilimia 100. 

Waziri huyo wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi alisema matatizo yote ya kiutendaji katika utekelezaji wa sera ya elimu yatatafutiwa ufumbuzi. “Itaundwa kamati itakayowashirikisha wadau wote mkiwamo wanafunzi,” alisema Profesa Maghembe, ingawa hakufafanua hatua zitakazochukuliwa endapo wanafunzi watakataa kutii agizo hilo la kurejea madarasani leo. 

Akiahirisha Bunge mjini Dodoma Ijumaa iliyopita, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema hivi sasa serikali inabeba gharama za kuchangia elimu ya juu, na haitawezekana kutoa mikopo kwa asilimia 100. “Kwa hali ya kawaida, hii mikopo ilitakiwa ilipiwe riba kwa wanafunzi, lakini kwa sasa serikali inabeba mzigo huo. 

Hatuna uchaguzi mwingine, bali kuendelea kuchangia gharama za elimu ili wanafunzi wengi zaidi wapate elimu ya juu,” alisema Pinda bungeni na kuongeza: “Napenda nirudie kusema kwamba serikali wakati wote itakuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanafunzi wanapata kile wanachostahili kujiendeleza kielimu. 

Naomba nitamke kuwa wanafunzi wale wanaotaka wanafunzi wote kupewa mikopo asilimia 100 haiwezekani.” Awali, jana wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani wameendelea kusisitiza kuendelea na mgomo leo baada ya Mkurugenzi wa Elimu ya Juu kutotokea chuoni hapo. 

Akihutubia wanafunzi waliokusanyika kwa shauku katika Ukumbi wa Nkrumah kusubiri tamko la serikali, Rais wa Serikali ya Wanafunzi (DARUSO), Anthony Machibya alidai amepata taarifa kuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu pamoja na wasaidizi wake waliitwa Ikulu na Rais kwenda kujadili matatizo yao. 

“Profesa Mukandala ameondoka kimya kimya na wasaidizi wake wameenda Ikulu kujadili mgomo wetu, nimepigiwa simu na Karani wake, kwa hiyo tusikate tamaa tuendelee na msimamo wetu mpaka tuone hatima yetu,” alisema Machibya na kuongeza kuwa mgomo utaendelea kama kawaida hawatarudi nyuma. Aidha, magari matatu yakiwa na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), yalikuwa yakirandaranda katika maeneo ya chuo hicho tangu juzi na jana kuhakikisha usalama wa mali na watu unakuwapo.

CHANZO: Habari Leo


VIONGOZI wa Nchi za Maziwa Makuu wamesema ipo haja ya kupeleka majeshi kwa ajili ya kurejesha amani eneo la Kivu lililopo Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ambako kwa sasa hali ya usalama si shwari kutokana na mapigano yanayoendelea. 

Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam jana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe ambaye alisema uamuzi huo ulitolewa na viongozi wa nchi hizo na kuungwa mkono na wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika. 

Alisema hatua hiyo inatokana na hali ya siasa ilivyo Kaskazini Mashariki mwa DRC kuwa mbaya kufuatia mashambulizi yaliyoanzishwa na kundi la waasin wanaoongozwa na Bw. Laurent Nkunda. 

"Mashambulizi hayo yamesababisha athari kubwa kwa wananchi, kiasi cha watu wengi kukimbia makazi yao hivi karibuni. Pamoja na kuwepo makubaliano mengi ya awali, Laurent Nkunda na kundi lake bado hawaheshimu makubaliano hayo," alisema Bw.Membe. 

Alisisitiza kuwa kwa hali ilivyo sasa nchini DRC viongozi wa Umoja wa Afrika (AU) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Umoja huo, Rais Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na viongozi wengine kadhaa wamekuwa wamekifanya mikutano ya dharura ili kuona jinsi gani wanaweza kumaliza mapigano yanayoendelea na kurejesha amani. 

Pia alisema maamuzi mengine yaliyotolewa na viongozi hao ni SADC kupeleka haraka wataalamu wa jeshi kusaidia kuangalia mipaka ya DRC na nchi jirani. 

Vile vile SADC iwe na ujumbe katika timu ya upatanishi iliyoanzishwa na wakuu wa nchi za Maziwa Makuu ambapo Rais Mstaafu wa Naijeria, Jenerali Olesegun Obassanjo na Rais Mstaafu wa Tanzania, Bw. Benjamin Mkapa wa Tanzania wamechaguliwa kuwa wajumbe wa timu hiyo. 

Alipoulizwa kuna tofauti gani kati ya Bw. Nkunda na aliyekuwa muasi wa Komoro, Kanali Mohamed Bakar, Bw. Membe alisema hawana tofauti kwa sababu wote ni waasi. 

"Hakuna tofauti kati ya hawa wawili kwani Kanali Bakari aliiasi Serikali yake Nkunda naye ni muasi ndio maana tunamtaka asitishe mapigano na tunakoelekea akiendelea kukaidi kuna hatari ya AU kupeleka majeshi ya kumdhibiti," aliongeza. 

Kuhusu hali ya kiasa nchini Zimbabwe, Bw.Membe alisema bado juhudi za kutafuta suluhu kuhusiana na muskabali wa nchi hiyo unaendelea.

CHANZO: Majira

NI WAKATI WA VITENDO ZAIDI KULIKO MANENO.

11 Nov 2008

The startling case of an AIDS patient who underwent a bone marrow transplant to treat leukemia is stirring new hope that gene-therapy strategies on the far edges of AIDS research might someday cure the disease.

The patient, a 42-year-old American living in Berlin, is still recovering from his leukemia therapy, but he appears to have won his battle with AIDS. Doctors have not been able to detect the virus in his blood for more than 600 days, despite his having ceased all conventional AIDS medication. Normally when a patient stops taking AIDS drugs, the virus stampedes through the body within weeks, or days.

"I was very surprised," said the doctor, Gero Hütter.

The breakthrough appears to be that Dr. Hütter, a soft-spoken hematologist who isn't an AIDS specialist, deliberately replaced the patient's bone marrow cells with those from a donor who has a naturally occurring genetic mutation that renders his cells immune to almost all strains of HIV, the virus that causes AIDS.

The development suggests a potential new therapeutic avenue and comes as the search for a cure has adopted new urgency. Many fear that current AIDS drugs aren't sustainable. Known as antiretrovirals, the medications prevent the virus from replicating but must be taken every day for life and are expensive for poor countries where the disease runs rampant. Last year, AIDS killed two million people; 2.7 million more contracted the virus, so treatment costs will keep ballooning.

While cautioning that the Berlin case could be a fluke, David Baltimore, who won a Nobel prize for his research on tumor viruses, deemed it "a very good sign" and a virtual "proof of principle" for gene-therapy approaches. Dr. Baltimore and his colleague, University of California at Los Angeles researcher Irvin Chen, have developed a gene therapy strategy against HIV that works in a similar way to the Berlin case. Drs. Baltimore and Chen have formed a private company to develop the therapy.

Back in 1996, when "cocktails" of antiretroviral drugs were proved effective, some researchers proposed that all cells harboring HIV might eventually die off, leading to eradication of HIV from the body -- in short, a cure. Those hopes foundered on the discovery that HIV, which integrates itself into a patient's own DNA, hides in so-called "sanctuary cells," where it lies dormant yet remains capable of reigniting an infection.

But that same year, researchers discovered that some gay men astonishingly remained uninfected despite engaging in very risky sex with as many as hundreds of partners. These men had inherited a mutation from both their parents that made them virtually immune to HIV.

The mutation prevents a molecule called CCR5 from appearing on the surface of cells. CCR5 acts as a kind of door for the virus. Since most HIV strains must bind to CCR5 to enter cells, the mutation bars the virus from entering. A new AIDS drug, Selzentry, made by Pfizer Inc., doesn't attack HIV itself but works by blocking CCR5.

About 1% of Europeans, and even more in northern Europe, inherit the CCR5 mutation from both parents. People of African, Asian and South American descent almost never carry it.

Dr. Hütter, 39, remembered this research when his American leukemia patient failed first-line chemotherapy in 2006. He was treating the patient at Berlin's Charité Medical University, the same institution where German physician Robert Koch performed some of his groundbreaking research on infectious diseases in the 19th century. Dr. Hütter scoured research on CCR5 and consulted with his superiors.

Finally, he recommended standard second-line treatment: a bone marrow transplant -- but from a donor who had inherited the CCR5 mutation from both parents. Bone marrow is where immune-system cells are generated, so transplanting mutant bone-marrow cells would render the patient immune to HIV into perpetuity, at least in theory.

There were a total of 80 compatible blood donors living in Germany. Luckily, on the 61st sample he tested, Dr. Hütter's colleague Daniel Nowak found one with the mutation from both parents.

To prepare for the transplant, Dr. Hütter first administered a standard regimen of powerful drugs and radiation to kill the patient's own bone marrow cells and many immune-system cells. This procedure, lethal to many cells that harbor HIV, may have helped the treatment succeed.

The transplant specialists ordered the patient to stop taking his AIDS drugs when they transfused the donor cells, because they feared the powerful drugs might undermine the cells' ability to survive in their new host. They planned to resume the drugs once HIV re-emerged in the blood.

But it never did. Nearly two years later, standard tests haven't detected virus in his blood, or in the brain and rectal tissues where it often hides.

The case was presented to scientists earlier this year at the Conference on Retroviruses and Opportunistic Infections. In September, the nonprofit Foundation for AIDS Research, or amFAR, convened a small scientific meeting on the case. Most researchers there believed some HIV still lurks in the patient but that it can't ignite a raging infection, most likely because its target cells are invulnerable mutants. The scientists agreed that the patient is "functionally cured."

Caveats are legion. If enough time passes, the extraordinarily protean HIV might evolve to overcome the mutant cells' invulnerability. Blocking CCR5 might have side effects: A study suggests that people with the mutation are more likely to die from West Nile virus. Most worrisome: The transplant treatment itself, given only to late-stage cancer patients, kills up to 30% of patients. While scientists are drawing up research protocols to try this approach on other leukemia and lymphoma patients, they know it will never be widely used to treat AIDS because of the mortality risk.

There is a potentially safer alternative: Re-engineering a patient's own cells through gene therapy. Due to some disastrous failures, gene therapy now "has a bad name," says Dr. Baltimore. In 1999, an 18-year-old patient died in a gene therapy trial. Even one of gene therapy's greatest successes -- curing children of the inherited "bubble boy" disease -- came at the high price of causing some patients to develop leukemia.

Gene therapy also faces daunting technical challenges. For example, the therapeutic genes are carried to cells by re-engineered viruses, and they must be made perfectly safe. Also, most gene therapy currently works by removing cells, genetically modifying them out of the body, then transfusing them back in -- a complicated procedure that would prove too expensive for the developing world. Dr. Baltimore and others are working on therapeutic viruses they could inject into a patient as easily as a flu vaccine. But, he says, "we're a long way from that."

Expecting that gene therapy will eventually play a major role in medicine, several research groups are testing different approaches for AIDS. At City of Hope cancer center in Duarte, Calif., John Rossi and colleagues actually use HIV itself, genetically engineered to be harmless, to deliver to patients' white blood cells three genes: one that inactivates CCR5 and two others that disable HIV. He has already completed the procedure on four patients and may perform it on another.

One big hurdle: doctors can't yet genetically modify all target cells. In theory, HIV would kill off the susceptible ones and, a victim of its own grim success, be left only with the genetically engineered cells that it can't infect. But so far that's just theory. All Dr. Rossi's patients remain on standard AIDS drugs, so it isn't yet known what would happen if they stopped taking them.

In 1989, Dr. Rossi had a case eerily similar to the one in Berlin. A 41-year-old patient with AIDS and lymphoma underwent radiation and drug therapy to ablate his bone marrow and received new cells from a donor. It is not known if those cells had the protective CCR5 mutation, because its relation to HIV hadn't been discovered yet. But after the transplant, HIV disappeared from the patient's blood. The patient died of his cancer 47 days after the procedure. Autopsy tests from eight organs and the tumor revealed no HIV.








Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Khalid Mohamed maarufu kama TID, amekata rufaa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kupinga adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja jela alichohukumiwa mwaka huu. 

Rufani hiyo ya msanii huyo ambaye tangu ahukumiwe kifungo hicho amekwishatumikia adhabu hiyo kwa miezi minne, itaanza kusikilizwa leo na Jaji Robert Makaramba; kwa mujibu wa habari zilizotolewa na ofisa mmoja wa mahakama hiyo. 

TID alihukumiwa kwenda jela mwaka mmoja kutokana na kutiwa hatiani kwa kosa la kushambulia na kumjeruhi kichwani na mkononi kijana aliyefahamika kwa jina la Ben Mashibe. Msanii huyo alimjeruhi Mashibe kichwani na mkononi kwa kutumia chombo cha kuwekea majivu ya sigara ‘ash tray’ na alisomewa mashtaka hayo mara ya kwanza Julai 10, mwaka huu mbele ya Hakimu Hamisa Kalombola wa Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni. 

Mwendesha Mashtaka wa kesi hiyo, Inspekta Nyagabona alidai TID alitenda kosa hilo Julai 2, mwaka jana saa sita na nusu usiku katika Hoteli ya Slipway iliyopo Msasani Dar es Salaam. TID mwenye umri wa miaka 26, alitiwa hatiani na Hakimu Kalombola baada ya hakimu huyo kuridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi wanne walioletwa mahakamani na upande wa mashitaka

10 Nov 2008

Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

MKURUGENZI wa kampuni ya Shivacom Tanzania, Bw. Tamir Sonaiya ametoa jumla ya sh. milioni 400 kwa Umoja wa Vijana ya CCM (UVCCM) kwa ajili ya kugharamia Mkutano Mkuu wa Umoja huo unaotarajiwa kufanyika kabla ya Desemba 15, mwaka huu. 

Kati ya fedha hizo sh. milioni 150 zitakuwa ni posho za wajumbe 1,000 wa mkutano huo ambapo kila mmoja atalipwa sh. 50,000 na kiasi cha milioni 250,000 zimetumika katika kutengenezea fulana, mikoba, kofia na bendera za chama kwa ajili ya mkutano huo. 

Fedha hizo zilikabidhiwa jana makao makuu ya CCM mjini hapa mbele ya Rais Jakaya Kikwete. 

Akikabidhi fedha hizo, Bw. Sonaiya alisema kuwa ameamua kujitolea kusaidia chama chake kwa kuwa yeye ni kada mwaminifu wa CCM na vifaa vyote alivyotoa vimetengenezwa kutoka katika kiwanda chake. 

Kwa upande wa Rais Kikwete alimpongeza Mkurugenzi huyo kwa kujitolea fedha hizo na kuwataka makada wengine wa CCM wenye uwezo kusaidia chama hasa kwa wakati huu wa kuelekea uchaguzi Mkuu ambapo fedha nyingi huhitajika ili kugharamia maandalizi ya mikutano hiyo. 

“Kinachosumbua sana kwenye mikutano ni namna ya kupata fedha za kuhudumia mikutano hiyo hivyo kwa hatua iliyofanywa na Umoja wa Vijana itasaidia kuondokana na tatizo la fedha lililokuwa likiwakabili katika maandalizi ya mkutano wao,” alisema Rais Kikwete. 

Fedha hizo zimepatikana kupitia uhamasishaji uliofanywa na kamati iliyoteuliwa na Baraza Kuu la Umoja huo kwa ajili ya kufanya maandalizi ya mkutano huo ikiwa chini ya Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Willium Ngeleja, Waziri wa Mambo ya Ndani, Bw. Laurence Masha na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bw. Willium Lukuvi.

CHANZO: Majira













MVUTANO mkali uliibuka jana katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa NEC- CCM kuhusu mwenendo wa baadhi ya wabunge wa chama katika mambo mbalimbali yaliyolihusu taifa na chama hicho. Tanzania Daima Jumapili imedokezwa.

Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho vililieleza gazeti hili kuwa mvutano huo uliibuka baada ya baadhi ya wajumbe wa kikao hicho ambao si wabunge kuwashangaa wenzao ambao wamekuwa wakiibua hoja zenye mwelekeo wa kuishambulia serikali na wale wanaoendeleza hoja zenye mwelekeo wa kuchochea udini.

Habari hizo zilieleza kuwa wajumbe wa kikao ambao si wabunge walionyesha dhahiri kuchukizwa na hatua ya baadhi ya wajumbe ambao ni wabunge ya kuanza kuwachimba viongozi wa kitaifa wa chama hicho kwamba inahatarisha umoja wa chama hicho.

Sambamba na taarifa za kuwepo mjadala mkali kuhusu hoja hizo, taarifa nyingine zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa wakakti Bunge likisubiri hatua zitakazochukuliwa na serikali dhidi ya gazeti lake la Habari Leo, baada ya kufichua njama za kundi dogo la wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kusuka zengwe la kumpinga hadharani Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, kuhusu hatua alizozichukua dhidi ya wezi wa EPA, chama hicho kimeanzisha uchunguzi wa kuwabaini wabunge waliodaiwa kuhusika katika mpango huo.

Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka ndani ya chama hicho, vimedokeza zaidi kuwa hatua hiyo ina nia ya kutaka kuthibitisha kilichoandikwa na gazeti hilo la serikali kama ni kweli au ni uongo na uchochezi, kama ilivyodaiwa juzi bungeni na Mbunge wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka.

Sendeka, mmoja wa wabunge machachari ndani ya CCM, juzi akitumia kanuni ya Bunge namba 68, alieleza masikitiko yake kuhusu habari iliyoandikwa katika ukurasa wa kwanza wa gazeti la Habari Leo kuwa ilikuwa ya uchochezi na kuitaka serikali ichukue hatua kama ilizochukua kwa gazeti la MwanaHalisi, ambalo limefungiwa miezi mitatu, kwa madai ya kuchapisha habari ya uchochezi kuhusu kuwepo mpango wa kumng’oa madarakani Rais Kikwete, ifikapo mwaka 2010.

Habari iliyochapishwa na Habari Leo ilieleza kuwa kuna kundi la wabunge ambalo kwa makusudi lilikusudia kuwasilisha hoja hiyo bungeni, lakini mkakati huo ulizimwa na habari iliyochapishwa na gazeti hilo kabla ya kundi hilo kuwasilisha linachokiamini kuwa Rais Kikwete hajachukua hatua stahiki katika kulishughulikia suala la wezi wa EPA.

“CCM imeshitushwa na hoja hiyo kuletwa bungeni, kuomba serikali ichukue hatua dhidi ya gazeti la Habari Leo wakati taarifa hiyo inaelezwa na walioitoa kuwa ni kweli tupu. Sasa chama kimeamua kufanya uchuguzi ili kije na majina ya wabunge waliokuwa na mpango huo na mahala walipoendeshea vikao hivyo ili kuuthibitishia ulimwengu kwamba habari hiyo ni sahihi na kwamba kuna wabunge waliopanga kumdhalilisha rais,” kilisema chanzo chetu hicho cha habari.

Juzi Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Serikali ya Daily News na Habari Leo, Isaac Mruma, alikaririwa akieleza kuwa habari iliyoandikwa na gazeti analolisimamia ni sahihi na ya kweli.

“Kwanza napenda kusema kuwa tuna uhakika na tulichokiandika kuwa ni kweli, kwani chanzo chetu cha habari ni cha kuaminika,” alisema Mruma.

Alipoulizwa ni kwanini walichapisha habari hiyo upande mmoja bila kupata maelezo ya upande wa pili, yaani bungeni au kwa wabunge waliotuhumiwa, Mruma alisema taarifa hiyo waliipata usiku, hivyo walishindwa kuwatafuta wahusika, licha ya kwamba waliwajua kupitia chanzo chao cha habari.

Alisema kutokana na hali hiyo, waliamua kuyaondoa majina ya wabunge wote waliokuwa wakitajwa kuhusika katika mpango huo wa kumpinga Rais Kikwete, kuhusu namna alivyoeleza jinsi suala la EPA litakavyoshughulikiwa, wakati akilihutubia taifa hivi karibuni.

Mruma aliwataka wabunge kutambua kwamba gazeti la Habari Leo ni chombo cha serikali na lina dhamana ya kuchukua tahadhari kwa kuandika jambo lolote linaloonekana kwa namna moja ama nyingine kujaribu kuiyumbisha serikali au rais aliye madarakani.

Habari zaidi kutoka mjini hapa ambapo kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kinaendelea, zilieleza kuwa huenda suala la habari hiyo likaibua mjadala mzito katika kikao cha NEC kinachoendelea leo mjini hapa.

Akiwasilisha maelezo yake juzi bungeni, Sendeka alisema habari hiyo iliyokuwa na kichwa kisemacho ‘Kundi la wabunge CCM lasuka zengwe la EPA, ilikuwa na lengo la kuleta mtafaruku na uchochezi kati ya wabunge wa CCM na serikali.

Hoja ya Sendeka iliungwa mkono na Spika Samuel Sitta, ambaye alieleza kushangazwa kwake na habari hiyo kutoa maelekezo kwa serikali kufuatilia suala hilo na kupelekewa taarifa.

Kwa upande wake serikali, ilisema tayari ilishaanza kulishughulikia suala hilo kwa kuwahoji wahusika.

CHANZO: Tanzania Daima

9 Nov 2008


UTATA umegubika mchakato wa zabuni nyeti ya matengenezo ya mfumo wa usalama ndani ya Benki Kuu Tanzania (BoT), ambayo imetolewa kwa Kampuni ya Siemens ya Afrika Kusini.

Kuibuka kwa utata huo kumekuja wakati Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu akiwa katika mipango ya kuisafisha benki hiyo na tuhuma mbalimbali, ikiwemo ya ufisadi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Nyaraka ambazo gazeti hili inazo, zinaonyesha utata huo umeibuka kutokana na malalamiko kutoka kwa Kampuni ya ESS ya Afrika Kusini, ambayo haijaridhishwa na taratibu za mchakato zilivyofanyika.

Kwa mujibu wa nyaraka hizo, ESS inaonekana kulalamikia hatua ambayo imeita kuwa ni kuwepo mawasiliano kabla, kati ya watendaji wa Siemens na baadhi ya watu ndani ya Bodi ya Zabuni ya BoT.

Mawasiliano hayo yalinaswa katika barua pepe kati ya mwakilishi wa Simens nchini Julai 29,2008, akifahamisha viongozi wake kufanya mawasiliano na mtu mmoja muhimu ndani ya BoT.

Sehemu ya barua hiyo inasomeka, " Nimeweza kuzungumza na mtu mmoja wa kuaminika ndani ya BoT, na amesema zipo zabuni mbili tofauti, ila sisi tutapatiwa moja tu ya utengenezaji mfumo wa usalama."

Barua hiyo, iliandikwa Julai wakati mshindi wa zabuni alipatikana Oktoba 28, ambapo ESS kama mmoja wa washiriki, alifahamishwa.

Utata mwingine katika zabuni hiyo unatokana na kile kinachoelezwa kwamba, Siemens ilishiriki katika uwekaji mfumo huo katika ujenzi wa jengo la ghorofa 18 maarufu kama Twin Towers na lile la Gulioni Zanzibar, ambayo yanachunguzwa.

"Sasa ikitokea ukaguzi wa Twin Towers umeonyesha kulitumika mabilioni bila kuangalia Value for money (thamani ya pesa kwa kitu), itakuaje?" kilihoji chanzo kimoja.

Siemens katika mkataba huo wa miaka miwili iliomba zabuni kwa sh 3.4 bilioni, hata hivyo, makampuni mengine kwa mujibu wa nyaraka za BoT yako juu zaidi.

Hata hivyo, akizungumzia utata huo ofisini kwake jijini Dar es Salaam wiki iliyopita, Gavana Ndulu, alisema hadi sasa ana imani kwamba, mchakato wa zabuni hiyo ulifuata taratibu husika.

Kwa mujibu wa Profesa Ndulu iwapo atabaini kuna tatizo lolote ikiwemo ukiukwaji wa mkataba huo hatasita kuisitisha.

Profesa Ndulu alisema dai la kwamba Siemens ilijenga Twin Towers ni kweli, lakini akabainisha kuwa hata kampuni nyingine ambayo ni pamoja na ESS na Group 5, pia zilishiriki katika ujenzi huo na pia ziliomba zabuni hiyo.

Profesa Ndulu alisema kabla ya kushirikisha kampuni hizo tatu ambazo zote zilishiriki katika uwekaji wa mfumo wa usalama kwa ngazi tofauti, ilibidi bodi itafute mwongozo kutoka Mamlaka ya Zabuni (PPRA), ambayo ilithibitisha hakuna tatizo.

Mwananchi Jumapili ilifanikiwa kuona nakala ya baraka za PPRA kwa BoT, ikieleza kuwa hakuna matatizo kwa makampuni hayo kushiriki ili mradi vigezo vizingatiwe.

"Najibu moja baada ya jingine, unanijua sifichi kitu na sipendi kupindisha mambo, kuhusu Siemens kushiriki katika Twin Towers, ni kweli, lakini hata ESS na Group 5 walishiriki kwa ngazi tofauti, Group 5 ndiyo wanaojenga jengo hilo, lakini pia wameshiriki," alisema Profesa Ndulu na kuongeza;

"Kama ni kigezo hicho, tusingeruhusu hata ESS na Group 5, kampuni hizi mbili na Siemens zote zimeshiriki katika Twin Towers, ndiyo maana kabla ya zabuni tukaenda PPRA kupata ufafanuzi, wakaruhusu," alisema.

Akifafanua kuwepo mawasiliano kati ya watu ndani ya bodi na Siemens, alisema hadi sasa hajaona tatizo kwani ni kweli zabuni zilikuwa mbili, lakini BoT ikaamua yenyewe kuchukua kazi moja ya kushughulikia uendeshaji wa mambo mbalimbali na kuacha hilo la ukaratabati mfumo wa usalama.

"Ni kweli, zabuni zilikuwa mbili, tulipoona wenyewe tunayo idara ya kuangalia mambo mbalimbali ikiwemo usafi na ununuzi wa vifaa, tukaamua tuipunguzie gharama kwa benki kwa kuipa zabuni kampuni moja, lakini pia si kwamba tunamwachia peke yake, wapo vijana wetu mahiri wanashirikiana nao," alifafanua.

Profesa Ndulu alisema hajaona tatizo katika hatua hiyo kwani zabuni ilitangazwa Juni na mawasiliano yamefanyika Julai, huo ni utaratibu wa kawaida kwa sababu kuna vitu ambavyo kampuni zote zinapaswa kuelezwa baada ya zabuni kufunguliwa.

"Sasa kusema kwamba zabuni ambayo itatolewa kwa ajili ya kugombaniwa ni ya usalama si uendeshaji, si tatizo ndicho tulichoeleza kwa kampuni zote," alifafanua.

Profesa Ndulu alisema ingawa haingii wala kuruhusiwa kuingilia mambo ya zabuni, lakini amekuwa akiuliza na kupatiwa taarifa za mara kwa mara kwa lengo la kuangalia utaratibu wa kutekelezwa kwa kuzingatia taratibu za kisheria.

"Mimi sitaki watu wapindishe mambo hata kidogo, nitasimamia sheria na kanuni, ndiyo maana huwa wakati mwingine nataka ufafanuzi wa mambo mbalimbali," alisisitiza Gavana Ndulu.

BoT katika kipindi cha kuanzia mwaka 2000 imekuwa na matatizo mbalimbali, ambayo hata hivyo, chini ya uongozi wa Profesa Ndulu amekuwa akijaribu kuisafisha na tuhuma hizo.

Baadhi ya mambo aliyoahidi kuyashughulikia ni kuchunguza mchakato wa ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo jijini Dar es Salaam na lililoko Zanzibar, kupitia ajira za watumishi wa BoT ambaye ametekeleza kwa kiasi kikubwa.

CHANZO: Mwananchi

8 Nov 2008


US President-elect Barack Obama would never have become the British Prime Minister because of "institutional racism" in the Labour Party, the head of Britain's equality watchdog has claimed. Skip related content

Trevor Phillips (pictured above), chairman of the Equality and Human Rights Commission, told The Times: "If Barack Obama had lived here I would be very surprised if even somebody as brilliant as him would have been able to break through the institutional stranglehold that there is on power within the Labour Party."

He said the Conservative Party had made more progress when it came to its selection procedures than Labour.

He said: "The parties and unions and think-tanks are all very happy to sign up to the general idea of advancing the cause of minorities but in practice they would like somebody else to do the business. It's institutional racism."

He added that he opposed all-black shortlists but said "positive action" was needed by all parties.

His views were supported by Adam Afriyie, Conservative MP for Windsor, who said he did not believe he would see a black PM in his lifetime.

But Sadiq Khan, Labour MP for Tooting, disagreed and predicted a black or Asian Labour PM would be elected in his lifetime.

A Labour Party statement in response to Mr Phillips said it continually reviewed its procedures to ensure its elected positions reflected British society.

A spokesman for the party said it has a "proud record of promoting ethnic minority candidates".

SOURCE: Yahoo! News


SERIKALI kwa mara nyingine imeingilia kati na kuamua kulipa mishahara ya wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), baada ya mwekezaji wake kushindwa kulipa mishahara ya mwezi uliopita.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alitangaza uamuzi huo bungeni jana, alipokuwa akijibu swali la papo kwa hapo la Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Mamuya (CCM), aliyetaka kujua mpango wa serikali katika kuhakikisha mwekezaji huyo anaiendesha kampuni hiyo kwa ufanisi na kama alikuwa akijua kuwa hadi jana wafanyakazi wa kampuni hiyo walikuwa hawajalipwa mishahara yao ya mwezi uliopita.

“Serikali imelichukua tena tatizo hilo na tunalifanyia kazi. Ninaahidi kuanzia sasa wafanyakazi hawa hawatakosa tena mishahara, tutajaribu kuona kama hiyo nyongeza tutaweza kuilipa,” alisema Pinda.

Agosti, mwaka huu, tatizo la wafanyakazi kukosa mishahara lilipotokea kwa mara ya kwanza, Waziri Mkuu ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kuokoa jahazi na hadi jana na juzi alikuwa akihaha kuhakikisha wafanyakazi hao wanalipwa mishahara yao ya Oktoba.

“Hadi juzi nilikuwa nahangaikia suala hili, ahadi ya serikali ilimalizika Agosti na tulitarajia uongozi wa TRL ungeendelea kulipa viwango vipya vya mishahara kuanzia Oktoba kama tulivyokubaliana, lakini kwa bahati mbaya wameshindwa na tunalazimika tena kulipia mishahara ya wafanyakazi hao hadi Novemba,” alisema Pinda.

Hii ni mara ya tatu kwa serikali kulazimika kuiokoa kampuni hiyo, baada ya uongozi wake kushindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi.

Miezi mitano tangu mwekezaji alipolichukua shirika hilo wakati huo likiitwa Shirika la Reli Tanzania (TRC), serikali iliingia mfukoni na kutoa fedha za walipa kodi zaidi ya sh bilioni tatu kuikopesha TRL kwa ajili ya kulipa mishahara ya wafanyakazi.

Septemba, mwaka huu, TRL ilikwama tena kulipia viwango vipya vya mishahara na serikali iliamua kulipa mishahara ya mwezi huo kwa ahadi kwamba kuanzia Oktoba mwekezaji angeweza kuendelea kulipa wafanyakazi wake bila matatizo.

Kampuni hiyo imeshindwa tena kulipa mishahara ya mwezi uliopita. Serikali kwa mara ya tatu sasa inajikuta ikilazimika kuingia tena mfukoni kuokoa jahazi.

Juzi wafanyakazi wa TRL walitangaza kuanza mgomo baridi, huku wakisubiri hatua zinazochukuliwa na mwekezaji kuikoa kampuni hiyo. Mbali na sula la TRL, Waziri Pinda pia alizungumzia suala la kuvuja kwa mitihani aliposema serikali inaliangalia kwa umakini Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kwani ndipo penye tatizo.

Serikali inajitahidi kuangalia namna bora ya kulisimamia kwani ni aibu kwa taifa kukaa na kuulizana maswali juu ya uvujaji wa mitihani. Amewataka wazazi na wanafunzi wanaotafuta mitihani kuacha kuendekeza tabia hiyo ya aibu.

“Natoa rai kwa wazazi kuwa tusikubali na tuwe wa kwanza kutoa taarifa tunapoona watoto wana mitihani ya kununua,” alisema Pinda.

Jibu hilo la Waziri Pinda lilitokana na swali la Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya (CUF), aliyetaka kujua mpango wa serikali katika kukabiliana na tatizo la kuvuja kwa mitihani na uchapishaji wa vyeti feki vinavyosambazwa mashuleni na kusababisha kushuka kwa kiwango cha elimu nchini.

Akizungumzia hali ya kiuendeshaji ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), Pinda alikiri kwamba kwa sasa kampuni hiyo iko taabani, hali iliyosababisha serikali ilazimike kufanya mazungumzo na shirika moja nchini China, lengo likiwa ni kuinusuru ATCL katika hali hiyo mbaya.

Akijibu swali la Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro, aliyeitaka serikali ichukue jukumu la kununua vitabu vya kiada kwa shule za msingi na sekondari na kuvisambaza badala ya jukumu la sasa la kutumia wakandarasi, Waziri Pinda alisema utaratibu wa sasa ni kwamba serikali inatoa fedha kwa halmashauri, nazo zinatumia wakandarasi ambao wengine si waaminifu.

“Wakandarasi mara nyingine hununua vitabu vya mitaani vinavyokuwa katika kiwango cha chini, hivyo tumekubaliana na wizara tutafute utaratibu mzuri wa upatikanaji wa vitabu,” alisema.


CHANZO: Tanzania Daima

KUMWOKOA MWEKEZAJI KILA ANAPOKWAMA SIO UFUMBUZI,BALI UAHIRISHAJI WA UFUMBUZI,WA TATIZO.NI MUHIMU KUJIULIZA HUYU MWEKEZAJI ATAENDELEA KUOKOLEWA HADI LINI,AND WHAT'D HAPPEN IF HATOOKOLEWA!







These pics are so lovely that no wonder we keep on hearing bull***t LIKE THIS.

Na Daniel Mjema, Dodoma
SERIKALI imekiri kuwa gazeti lake la Habari Leo liliandika habari ya uchochezi na kuliahidi Bunge kuwa italichukulia hatua zinazostahili gazeti hilo.

Hatua hiyo ya serikali inafuatia agizo la Bunge kwamba ilichukulie hatua kali gazeti hilo kwa kuchapisha habari za uchochezi dhidi ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), serikali na Rais Jakaya Kikwete.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo baada Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, kulalamika kuhusina na kitendo cha gazeti hilo la serikali kuchapisha habari hiyo.

Awali mbunge huyo aliomba mwongozo wa Spika jana kuhusiana na habari hiyo akisema kuwa ni nzito na ya uchochezi kuliko iliyoandikwa na gazeti la MwanaHALISI lililofungiwa miezi mitatu hivi karibuni na waziri huyo.

Habari hiyo iliyochapwa Jumatano wiki hii katika toleo namba 636 ilikuwa na kichwa cha habari likichosema ‘Kundi la wabunge wa CCM lasuka zengwe la EPA” na kuelezea njama za wabunge hao wa CCM kumpinga Rais kuhusu hatua zake dhiti ya watuhumiwa wa EPA.

Ole Sendeka alisema habari hiyo ni ya uchochezi mkubwa, hasa inapodai kuwa zipo njama za wabunge wa CCM za kumpinga Rais Jakaya Kikwete kuhusu uamuzi wake katika sakata la kashfa ya fedha za EPA.

Mbunge huyo alisema gazeti hilo limejenga hoja kuonyesha kwamba wabunge hao wa CCM wamekuwa wakitumiwa na watu waliopo nje ya Bunge kupinga maamuzi ya Rais baada ya kuagiza kuwa watuhumiwa wafikishwe kortini.

Ole Sendeka alisema habari hiyo ni nzito na ya uchochezi kuliko ile ya gazeti la MwanaHALISI, kwa sababu inawagombanisha wabunge hao na Serikali pamoja na Rais na kutaka mwongozo wa Spika ni hatua gani zitachukuliwa.

Baada ya maelezo hayo, Spika Samwel Sitta aliungana na Mbunge huyo na kusema kuwa hata yeye alishtuka sana aliposoma habari hizo na kuongeza kuwa huo ni mchezo mchafu ambao serikali inapaswa kuuchukulia hatua kali.

“Hata mimi nilishtuka sana niliposoma habari hiyo, kwa kweli ni mchezo mchafu sana, ingekuwa imeandikwa na gazeti hovyo hovyo hivi tusingeshangaa sana, lakini hili ni gazeti la Serikali,” alisema Sitta.

Sitta ambaye alionekana kukerwa na habari hiyo aliongeza kusema kuwa: “Linapokuwa limechapisha gazeti la Serikali, hili ni jambo zito sana, hivyo naagiza wahusika waliotajwa na gazeti hilo waandike malalamiko rasmi kwa waziri husika”.

Spika alisema pamoja na wahusika ambao ni wabunge wa CCM, kuwasilisha malalamiko hayo na kupeleka kwa waziri nakala za gazeti hilo, Bunge litafuatilia kujua hatua zilizochukuliwa dhidi ya chimbo hicho cha habari cha serikali.

Mara baada ya maelezo hayo , Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika, ambaye ndiye aliyelifungia gazeti la MwanaHALSI alisimama na kukiri kuwa gazeti hilo la serikali kuandika habari hizo za uchochezi.

Hata hivyo, alisema kuwa wizara yake imekwishachukua hatua kwa kuwaandikia wahusika kuwataka wajieleze kuhusu ukweli wa habari hiyo na baada ya kupokea maelezo hayo serikali itachukua hatua zinazostahili.

Pamoja na maelezo hayo, Spika alimweleza waziri huyo kuwa ni vyema taarifa ya jinsi serikali ilivyolishughulikia suala hilo iwasilishwe katika ofisi ya Spika ili naye aishirikishe Kamati ya Bunge ya Maadili.

Mwezi mmoja uliopita serikali ililiufnugia kwa miezi mitatu gazeti la MwanaHALISI kwa maelezo kwamba limeandika habari ya uchochezi iliyokuwa na kichwa kisemacho: ‘Njama za kungoa Kitwete zafichuka’, ambayo ilieleza kwamba ndani ya CCM kuna watu wanataka kumzuia Rais Kikwete asigombee urais tena kipindi cha pili.

Waziri husika alisema serikali imechukua hatua kwa sababu gazeti hili imeandika habari yenye lengo la kumchonganisha Rais na mtoto wake aliyedaiwa kutumiwa na kundi la baadhi ya vigogo wa CCM wanaotaka kumwengua ili asigombee kipindi cha pili.

Hatua ya waziri huyo kulifungia gazeti hilo kilipingwa na wadau mbali mbali wa habari na kufuatiwa na maandamano ya amani ya wahiri wa vyombo vya habari nchini hadi katika ofizi za wizara hiyo wakiwa wameziba midomo na gundi ya karatasi au plasta.

CHANZO: Mwananchi


7 Nov 2008


Barack Obama's motorcade had an unexpected occurrence while ferrying the president-elect to a security briefing at Chicago FBI headquarters Thursday morning.

As the motorcade pulled onto Van Buren, towards the Loop, a couple in a tan sedan tried to drive around the heavily-armed line of vehicles, wrote pool reporter P.J. Hufstutter of the Los Angeles Times:

The SUV cut the car off immediately, and the security team aimed their weapons at the car. The driver and passenger in the sedan stopped, and looked stunned -- until the male driver appeared to understand what was happening (your pool reporter could see him mouth "Obama"). The motorcade continued on. The sedan remained stopped, near the side of the road. [...] Some of the drivers here in Chicago do not seem to understand that a) the Chicago police car at the end of the president-elect's motorcade is serious about having traffic pull over when the officers flash their lights and hit their sirens, and b) it's not a great idea to jump ahead of traffic by trying to cut around the black SUV filled with five heavily-armed secret service CAT members.


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.