13 Dec 2008

Kwenye uchambuzi makini,vitu kama laana,nuksi au bahati mbaya huwa havileti maana yoyote.Lakini katika maisha yetu kijamii tunafahamu kuwa jambo likiandamwa na kutofanikiwa linaweza kuhusishwa na laana au bahati mbaya.Na kama kuna sekta ambayo imekuwa ikiandamwa na matatizo kwa muda mrefu huko nyumbani basi ni usafiri.

Ukiangalia usafiri kuanzia kwenye cities hadi vijijini utabaini kwamba kadri unavyozidi kwenda chini (city ikiwa juu na kijiji chini) ndivyo matatizo yanavyozidi kuongezeka.Matatizo ya daladala jijini Dar ni "cha mtoto" ukilinganisha na namna ya kufika sehemu iitwayo Tanganyika Masagati (sijui kama ushawahi kuisikia).
Na hata hapo Dar,kero ya usafiri inazidi kuongezeka kadri unavyoelekea kwenye vitongoji vya jiji hilo.Ushawahi kufika Pemba Mnazi?Mara kwa mara tunasikia mipango mipya ya kuboresha usafiri,hasa jijini Dar.Tulisikia kuwa vipanya vingekuwa phased out lakini wajuzi wa mambo walishajua kuwa hilo ni changa la macho kwa vile wamiliki wengi wa vipanya hivyo ndio haohao wanaotuzuga kwenye media kuwa vipanya ni kero.Wanajuaje kero za vipanya ilhali wao wanazungushwa na ma-VX au Vogue yao yenye viyoyozi?
Tukiachana na usafiri wa barabara,wa majini ndio wa roho mkononi zaidi.Na hapa sizungumzii meli au boti pekee.Angalia pale Kigamboni!Au kama unadhani pale ndio kiboko cha matatizo basi jaribu kwenda kivuko cha Mto Kilombero!Nilipokuwa huko hivi karibuni nilihabarishwa kwamba kivuko kipya kilichotarajiwa kutatua kero katika eneo hilo kiliishia kusomwa na maji.Kisa?Bila shaka fisadi flani kanunua kivuko mtumba.Kama kawaida,hakuna aliyewajibika hadi leo.

Hapo feri jijini Dar nako ni ngonjera kila siku.Mara sijui kuna daraja litajengwa,mara sijui kuna nini kitafanyika.Kama kawaida yetu,tunasubiri litokee janga flani kisha ndio mabwana mipango wetu waje na mipango mipya ya kujali maisha yetu.Vivuko vingi huko nyumbani ni sawa majeneza yanayoelea.Hakuna la muhimu tulilojifunza kutokana na janga la Mv Bukoba,na sijui hata kama policy makers wetu wanakumbuka janga hilo.
Usafiri wa reli ndio balaa.Zamani za kale,ukiwa ndani ya treni ya Tazara ungeweza kujiskia kama uko kwenye treni ya nchi zilizoendelea.Siku hizo tulikuwa tunasafiri na watalii kibao.Si unajua reli ya Tazara inakatiza katika hifadhi ya Selous,kwahiyo kwa wenzetu wanaotafuta vivutio safari hiyo ilikuwa ni kuua ndege wawili kwa jiwe moja:kufikishwa waendako na kupata uhondo wa wanyama mbugani.Hivi sasa Tazara iko dhoful khal,inakaribia kukata kauli.Mara ya mwisho niliposafiri kwa Tazara,jamaa mmoja Mzambia alinieleza bayana kuwa wanasubiri tu kifo cha shirika hilo.
Huko Reli ya Kati ndio habari mbaya zaidi.Hivi inaingia akilini kweli kwa mtu anayejiita mwekezaji kuwa anapewa fedha na serikali kulipa mishahara ya watumishi?Huyu ni m-babaishaji tu.Watu pekee wanaofahamu sababu za kwanini hadi leo TRL bado iko mikononi kwa wababaishaji hao wa kidosi ni Watanzania wenzetu wachache wanaoendela kuamini kwamba ipo siku TRL itasisima na kujiendesha yenyewe.Wajuzi wa mambo wanaiona TRL kama kipofu anayetafuta sindano kwenye chumba chenye kiza totoro,huku sindano hiyo ikiwa haipo humo!

Kitu pekee kitachowakimbiza Wahindi hao ni janga.Kwanza tukubaliane kwamba kama wangekuwa hawapati faida katika huduma yao mbovu wasingeendelea kuwepo hadi leo.Si unawajua Wahindi linapokuja suala la faida?Yes,janga ndio itawakimbiza wadosi hao.Mungu aepushe janga hilo lakini likitokea la kutokea na kisha tukaishia kumlaumu Mungu,atatuadhibu vikali.Hawa wababaishaji hawajafanya matengenezo ya reli,wanasafirisha abiria kwenye mabehewa ambayo hata ng'ombe hawastahili kupanda,na ratiba zao ni za bahati nasibu.Yayumkinika kuhitimisha kuwa mazingira hayo ni sawa na a catastophy in the making.And once that happens,God forbid,hawa jamaa wataingia mitini just like wawekezaji wababsiahji wengine wanavyotukimbia baada ya kuukamua uchumi wetu.Na huwezi kuwalaumu kwani hata mwenye nyumba ambaye anaacha mboga yake jikoni pasipo kuhofia nyau,hawezi kuwalaumu paka wakikwiba mboga hiyo kukidhi njaa zao!

Hatuwezi kuuzungumzia usafiri wa anga pasipo kutaja AIR TANZANIA.Uongozi mmoja umeupisha mwingine one times too much,nembo zimebadilishwa mara lukuki,mgogoro mmoja umeupisha mwingine,lawama za wasafiri ndio usiseme!Hivi Waethiopia ni wachawi kwa namna walivyoweza kuifanya Ethiopian Airlines kuwa moja ya mashirika ya ndege ya mfano barani Afrika?Vipi kuhusu watani zetu na Kenyan Airways yao?Sisi tunashindwa nini?Hivi kuna ugumu gani wa kukodi ndege,kutoa huduma ya kuridhisha,kutumia itakayopatikana kununua ndege zaidi na kisha kutanua safari katika maeneo mbalimbali duniani?
Tatizo kubwa la Air Tanzania,or whatever its current name is,ni ufisadi.Na chanzo cha ufisadi huo ni hao wanaofanya teuzi pasipo kuzingatia rekodi.Hivi hawa viongozi wa sasa wa ATC wana sifa stahili za kulitoa shirika ICU na kulirejesha angani?Majuzi David Mattaka aliruka kimanga alipoulizwa iwapo ndege za shirika hilo zimepigwa stop kutoa huduma (kutoa non-existent huduma?) kabla ya kukiri muda mfupi baadaye kwamba habari hiyo ni ya kweli.Hivi background ya mtu huyu inaleta matumaini yoyote ya kufufuka kwa ATC?Na hapo sizungumzii maisha yake binafsi (hapa sio mahala pake).

Sababu kubwa ya nuksi,mikosi na bahati mbaya zinazoiandama sekta ya usafiri huko nyumbani ni uksefu wa uzalendo.Hilo linaanzia kwa hao wanaofanya uteuzi wa kuongoza taasisi zinazotoa huduma za usafiri wa angani,majini,barabara na reli.Pia uteuzi usiozingatia rekodi kwenye mamlaka zinazosimamia sekta hiyo ni tatizo jingine la msingi.Takriban maeneo yote yaliyoguswa katika uchambuzi huu yana Waziri,Naibu Waziri,Katibu Mkuu,Naibu Katibu Mkuu,Mkurugenzi Wizarani na Mkurugenzi shirikani,mameneja lukuki,Wenyeviti na wajumbe wa bodi ambao vikao vyao ni about posho tu na sio maendeleo ya shirika husika,na mlolongo mwingine wa watendaji.Sasa hapo inahitajika domino effect top to down.Waziri akiweka mbele uzalendo na uwajibikaji hao wote chini yake watatimiza majukumu yao.Lini tutapata Waziri ambaye ataapa kuwa lazima AIR TANZANIA itarudi hewani,TRC itafufuka kutoka katika wafu,TAZARA itapata uhai mpya,vivuko vinakuwa na maana ya vivuko,na hatua nyingine nyingi.Na isiishie kuapa tu kwani waheshimiwa wneig tu huapa lakini huishia kufisadi nchi na viapo vyao.

Uzalendo ni kuweka maslahi ya nchi mbele badala ya maslahi binafsi,Uzalendo ni kuchagua watu wenye sifa na uwezo na sio ku-recycle watendaji wenye sifa zisizostahili personally na professionally.It can be done,if wenzetu wakiamua ku-play their part....au just kusema YES WE CAN!

12 Dec 2008


Demonstrations against the killing were seen in cities across the continent with left-wing radicals and other sympathisers taking to the streets.

In Spain, 11 protesters were arrested and several police officers injured when clashes took place in Madrid and Barcelona.

In Copenhagen, 32 people were arrested when their protest in support of the Greek protests turned violent.

In neighbouring Turkey, about a dozen left-wing protesters daubed red paint over the front of the Greek consulate in Istanbul.

Around 150 people belonging to a Danish underground movement took to the streets, throwing bottles and paint bombs at buildings, police cars and officers. In Moscow and Rome, protesters threw petrol bombs at Greece's embassies.

Journalists came under attack for the first time in the riots, with a Russian news crew assaulted by a mob of about 50 youths, some of them reportedly drunk.

A correspondent and a cameraman for Russian television channel NTV were injured in the confrontation, which happened while they filmed clashes in Exarchia, a crucible of student radicalism.

In Athens, around 40 youths threw stones at riot police near university buildings in the volatile Exarchia district where 15-year-old Alexis Grigoropoulos was shot dead on Saturday.They were met with volleys of tear gas and three arrests were made, police said. Overnight, students hurling petrol bombs and stones again battled riot police in Athens, in a continuation of the worst riots to have hit Greece in more than 30 years.

There were similar clashes in the northern city of Thessaloniki, where more than 80 shops and 14 banks were damaged, with students continuing to occupy university campuses.Despite the turmoil that has rocked Greece since Grigoropoulos was killed, embattled Prime Minister Costas Karamanlis said he would fly to Brussels to attend a European Union summit. His conservative government has a parliamentary majority of just one seat.

Corruption scandals and attempts at economic reform have made Mr Karamanlis' administration deeply unpopular, but he has so far resisted calls to resign and call early elections.Epaminondas Korkoneas, 37, the police officer accused of shooting the teenager, has been charged with voluntary homicide and "illegal use" of his service weapon. He was ordered to remain in custody by an Athens magistrate.

His partner, Vassilios Saraliotis, 31, was charged with being an accomplice and will also remain in custody. The pair have been held since Sunday.Under questioning by a magistrate, Mr Korkoneas said he had acted out of self defence when a group of youths began throwing firebombs and other objects while threatening to kill him and his partner.His lawyer said the bullet which killed Grigoropoulos showed signs of having bounced off a hard surface, indicating that the boy was killed as a result of an accidental ricochet.

Greece has a history of clashes between the police and left-wing, anarchist groups.A student uprising in 1973 helped bring an end to the country's military dictatorship a year later.But the scale of this week's violence has left the country in deep shock as Greeks count the cost of the destruction.

The Athens Chamber of Commerce said 435 businesses had been hit during the violence, with 37 completely gutted, estimating the damage at GBP 44 million (50 million euros).Under the headline "Greece in self-destruct mode" the conservative daily newspaper Kathimerini said in an editorial: "This is a country with a state that is in a shambles, a police force in disarray, mediocre universities that serve as hotbeds of rage instead of knowledge and a shattered health care system. It is also on the brink of financial ruin."


11 Dec 2008


SALAAM ZA MWAKA MPYA

 

Uongozi na wafanyakazi wa

MwanaHALISI,

hata ndani ya kifungo cha

siku 90 cha gazeti hili,

tunayo furaha kukutakia

heri katika sherehe za msimu huu

zinazoambatana na

kuaga mwaka huu na kukaribisha

Mwaka Mpya.

Tumetambua na kuthamini

upendo na ujasiri wako katika kutetea

uhuru wa mawazo na uhuru wa

habari; na tunaahidi

 kuendelea kutenda kwa mujibu wa

uhuru, haki na wajibu

mara baada ya kurejea ulingoni. 

Heri ya Mwaka Mpya – 2009


Saed Kubenea

Mkurugenzi Mtendaji

Hali Halisi Publishers


Na Simon Mhina
Kada machachari wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema kauli ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusuf Makamba, kwamba mjadala juu ya mafisadi wa Akauti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ufungwe, inaashiria kuwakumbatia mafisadi. 

Mwanasiasa huyo chipukizi ambaye yupo katika kipindi cha mapambano na makada wenzake ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), kutokana na kuvuliwa uanachama kwa kupinga mradi wa Jengo Jipya la Umoja huo, alisema hatua ya Makamba kuweka mizengwe mapambano dhidi ya ufisadi inawavunja moyo watendaji wa serikali ambao wapo mstari wa mbele kushughulikia tatizo hilo. 

Nape ambaye bado ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), alisema kauli ya Makamba ni sawa na ya mtu anayeogopa kivuli chake. 

Hata hivyo, Nape katika mazungumzo na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, alisema kimsingi Makamba hana uwezo wala madaraka ya kuzuia mjadala juu ya mafisadi. 

Nape alisema ingawa hana uhusiano wowote na watu wanaopiga makelele juu ya ufisadi, lakini anafikiri wanafanya hivyo kutokana na machungu makubwa ya umasikini wanayopata Watanzania kutokana na mafisadi. 
Alihoji: ``Hivi Mzee Makamba mafisadi wakisemwa vibaya yeye anakerwa na nini? 

Hivi kinachomkera ni kipi, mafisadi waliopora fedha za wavuja jasho au wavuja jasho wanaopiga makelele juu ya mafisadi kuwaibia?`` 

Alisisitiza kuwa katika hali ya kawaida, hakuna Mtanzania ambaye atanyamazia ufisadi kutokana na uzito wake. 

Nape alihoji tena: ``Ina maana Mzee Makamba anajua idadi ya mafisadi wote nchini?`` 

Akifafanua, alisema kazi ya kuwashughulikia wahalifu hao ipo chini ya serikali na vyombo vyake vya dola na sio jambo la kisiasa. 

Wakati huo huo, Mbunge wa Moshi Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Philimon Ndesamburo, amesema chama chake `kitafunga mdomo` kuhusu ufisadi, iwapo Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, atakamatwa na kufikishwa mahakamani. 

Alisema Mkapa ni hazina kubwa ya mafisadi nchini na siku akifikishwa kortini janga hilo litakuwa limefikia tamati. 

``Chadema hatutaacha kupiga kelele juu ya ufisadi kama anavyosema Makamba hadi hapo Mkapa ambaye ni hazina ya mafisadi atakapopelekwa kortini, mambo yote yaliyofanyika yalikuwa chini ya utawala wake na alikuwa anayajua na alishiriki, lazima akamatwe,``alisema Ndesamburo. 

Mbunge huyo alisema mafisadi ndani ya CCM na serikali yake, hawajamalizika hivyo lazima waendelee kusakwa. 
Alisema asilimia 10 tu ya mafisadi wote nchini ndio wamekamatwa, lakini asilimia 90 akiwemo `baba lao` bado wapo mitaani. 

Ndesamburo alisema japokuwa Makamba amelenga kuwasaidia baadhi ya mafisadi, lakini kwa hili anatakiwa aone aibu. 

``Yaani wakati huu ambao Rais Jakaya Kikwete ameridhia watu waliokuwa mawaziri wafikishwe Mahakamani yeye anasimama kutetea ufisadi, namuomba angalau aone aibu, hata kama amelambishwa asali,`` alisema. 

Kuhusu Operesheni Sangara, Ndesamburo alisema itaendelea kwa nguvu zote licha ya Makamba kuibeza, kwa vile inalenga kuwafumbua macho Watanzania. 

Alisema operesheni hiyo si uchochezi wala nguvu ya soda, bali Makamba ametoa shutuma hizo, baada ya kushindwa kujibu hoja zinazotolewa na Chadema. 

Makamba alinukuliwa katika vyombo vya habari jana akisema kwamba mjadala wa EPA kwa sasa umefungwa kwa kuwa watuhumiwa wote wamefikishwa kortini. 

Hata hivyo, ukweli ni kwamba bado watuhumiwa wengine wakiwamo wamiliki wa Kagoda Agriculture Ltd hawajafikishwa kortini. 

CHANZO: Nipashe

Scientists believe successful tests in monkeys could prove a step towards a new type of drug to combat HIV.

The journal Nature reports infected animals survived almost twice as long after a single treatment to raise immune response to the virus.

An independent expert said multiple doses were possible, and might eliminate the virus.

Current antiretroviral drugs must be taken for life, giving HIV the opportunity to build up resistance.

Although millions of people without HIV cannot currently receive them, modern antiretroviral drugs have transformed the life expectancy of people with the infection.

However, scientists are constantly looking for alternative ways to keep the virus in check.

One option is being tested in the US on macaque monkeys infected with "simian immunodeficiency virus" - their equivalent of HIV.

One of the features of HIV is its ability to shut down or impede the body's own methods for clearing viral infections.

In particular, it manages to activate a signalling system in the body's immune cells - which then actually holds back the body's immune response.

The latest treatment works by blocking that signalling system, which has the effect of boosting the function of "killer" immune cells.

The blocking antibody was injected once into nine animals who had developed AIDS after SIV infection, all of whom lived on average almost twice as long as other monkeys who did not receive the treatment.

The treated monkeys had clear signs of more active immune systems and reduction of the amount of virus circulating in their blood, both signs that they were tackling the disease more efficiently.

While the virus was not fully controlled in any of the monkeys, the scientists said that more than one dose was possible, and that it could be used in combination with antiretroviral drugs.

Long wait

Dr Rama Amara, who led the research, said: "It is important to note that this therapy was effective without antiretroviral drugs and in monkeys with severe AIDS.

"It is critical to induce protective immune responses targeting the mutated virus for developing a successful immune therapy to control HIV infection."

Another of the researchers said that the treatment also offered potential against other chronic infectious diseases such as hepatitis C and TB.

Professor Thomas Lehner, an immunologist from King's College London, said that the findings were "very interesting", and that the drug showed potential for human treatment.

He said: "It's possible that multiple doses could eliminate the virus, although the present experiment has not shown that.

"It's my understanding that some groups are already working to test this in humans, and although the safety of the drug is a concern, I see no reason why that should be a problem.

"It's most likely that we will see it used alongside antiretroviral therapy."

Dr Ade Fakoya, from the International HIV/AIDS Alliance, said that the research was "an important avenue" to pursue, particularly as it had managed to extend the lifespan of the monkeys.

However, he said: "There's a long process of many years before this basic research is translated into actual research with the HIV virus in humans and then identifying a way to be able to actively block this on a large enough scale for it to be another useful tool in HIV treatments."

SOURCE: BBC


9 Dec 2008





Pichani juu ni dada SOPHIA RWANGA mara baada ya kukamata nondo yake ya  MSc in Geospatial Information Systems hapo University of Aberdeen.Picha zifuatazo hapo chini ni shamrashamra za mahafali hayo katika chuo hiki kilichoanzishwa mwaka 1495,the third oldest in Scotland,and the fifth oldest in the UK.




CLICK HERE FOR THE WHOLE LIST


WASHINGTON — The first sign of cracks in President-elect Barack Obama's foreign policy team of rivals emerged on Monday as his choices for secretary of state and U.S. ambassador to the United Nations visited the State Department.

As Secretary of State-pick Hillary Rodham Clinton and U.N. envoy-choice Susan Rice separately visited the diplomatic agency's headquarters in Washington's Foggy Bottom neighborhood, persons familiar with the transition said that Rice wants to install her own transition team inside the department.

Such a move by an incoming U.N. ambassador is rare, if not unprecedented, because the job is based at the United Nations in New York, where Rice already has a small transition staff, the sources familiar with the incoming administration.

The push by Rice, an early Obama supporter whose position the President-elect wants to elevate to a cabinet post, is also a signal that she intends to use her influence with the new president to play a more significant role than previous U.N. envoys, they said. The transition sources spoke on condition of anonymity to discuss internal deliberations.

Officials with Clinton's transition team declined to comment on the matter, and aides to Rice could not immediately be reached. State Department officials declined to comment on issues related to the transition.

It was not clear if Clinton and Rice _ who had strained relations during the Democratic primaries because of Rice's steadfast backing of Obama _ saw each other at the State Department as Clinton left the building shortly after Rice arrived.

During the presidential campaign, some Clinton aides saw Rice's early decision to back Obama as a betrayal because of her previous role as a high State Department official during President Bill Clinton's administration. Rice's desire to place her own team in Washington could fuel speculation that those tensions will carry into the new administration.

The officials could not say if Clinton's team had formally objected to Rice's plan, or even if Rice would be able to install a separate transition team inside the State Department. But they noted that dueling transition teams could complicate the handover by blurring lines of authority.

Technically, the job of U.N. envoy falls under the authority of the secretary of state, although some previous U.N. ambassadors have held cabinet rank. The last U.N. ambassador to be part of the president's cabinet was Richard Holbrooke, who had a famously icy relationship with then-Secretary of State Madeleine Albright during the Clinton administration.

Albright, who was President Clinton's first ambassador to the United Nations, was a mentor to Rice. But the two had a falling out when Albright, America's first female secretary of state, lined up behind Hillary Clinton for the Democratic presidential nomination and Rice backed Obama.

Hillary Clinton, meanwhile, was to dine Monday evening with the nation's current and second female secretary of state, Condoleezza Rice, at Rice's apartment in the exclusive Watergate complex. The two Rices are not related and Condoleezza Rice said on Sunday that she thought Clinton would do a great job.

Also Monday, Clinton was to meet privately with Sen. John Kerry, D-Mass. and the incoming chairman of the Senate Foreign Relations Committee, according to a Democratic official. Kerry, once a contender for the secretary of state job, will oversee Clinton's confirmation. Kerry has pledged to hold "swift and fair" confirmation hearings.


8 Dec 2008


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, ameonya kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinaweza kusambaratika ikiwa uadui uliopo ndani yake unaoendelezwa na makundi hautadhibitiwa. 

Membe alisema uadui huo unasababishwa na vitendo kama vile hujuma za kuangushana katika kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika chama hicho. 

Waziri huyo alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Mkoa wa Dar es Salaam. 

Membe, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya CCM, alisema ni dhana potofu kuamini kuwa uadui wa aina hiyo unasababishwa na vyama vya upinzani. 

``Maadui wapo ndani, ni wenzetu sisi wenyewe, tunakaa nao lakini wanashiriki kupanga kuangushana, majungu yamekithiri hiyo ni kielelezo cha ugonjwa wa chama kusambaratika,`` alionya Membe ambaye pia ni Katibu wa Idara ya Mambo ya Nje ya CCM. 

Membe, alisema uzoefu ywa miaka miwili aliopata tangu ateuliwe kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, umemuonyesha kuwa vyama vingi vilivyotawala kwa muda mrefu vinaweza kuondoka madarakani kutokana na udhaifu uliopo, na si nguvu ya upinzani. 

``Mara nyingi sana vyama tawala vinajiua vyenyewe, si kwa sababu ya upinzani,`` alisema Mbunge huyo wa Mtama,. 

`` Tunapotafunana, kutoaminiana, kama CCM na jumuiya zake hatushikamani, tukagawanyika, hatuwezi kuwa chama imara, tutameguka,`` alisema. 

Membe alisema machafuko yanayotokea baada ya chaguzi barani Afrika, yanachochewa na kasumba ya kutokukubali matokeo. 

Alisema hali hiyo inawafanya watu wengine kuingia msituni ama kufikia hatua ya kufanya mapinduzi ya kijeshi. 

Alitoa mfano kuwa katika kipindi cha takribani miaka 50, viongozi 32 barani Afrika, waliuawa kutokana na mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa katika nchi zao na kwamba vyama vilivyopo madarakani, vina fursa nyingi za kufanikisha kubaki katika uongozi. 

Kwa mujibu wa Membe, baadhi ya fursa hizo ni kueleweka kwa sera zake, uwepo wa viongozi bora na jumuiya imara. 

Wakati Membe akitoa tahadhari hiyo, baadhi ya wajumbe wa mkutano huo nusura wapigane hadharani, kutokana na tofauti za kuwaunga mkono wagombea katika nafasi mbalimbali za UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam. 
Hali hiyo ilijitokeza jana asubuhi, kabla ya Membe kuwasili kufungua mkutano huo. 

Taarifa za ndani zilidai kuwa kundi linalomuunga mkono mmoja wa wagombea wa uenyekiti, lilipanga njama za kuhujumu uchaguzi huo ili kutoa fursa kwa `mtu wao` kushinda. 

Miongoni mwa hujuma hizo, ni kusimamishwa kwa wajumbe zaidi ya 10, ili wasishiriki kupiga kura. 
Hata hivyo, baada ya kugundulika, baadhi ya vijana kutoka wilaya za Kinondoni, Ilala na Temeke, waligoma kuingia ukumbini. 

``Hatuingii ukumbini kama wenzetu waliosimamishwa hawatapewa vitambulisho, hatukubali kuburuzwa,`` walisikika baadhi yao wakisema. 

Hakuna kiongozi yeyote wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, aliyekuwa tayari kuzungumzia suala hilo, isipokuwa wanachama wengine wa umoja huo walisikika wakilalamikia kundi walilodai kwamba liliongozwa na mmoja wao. 

Baadaye, taarifa zilieleza kuwa vijana waliozuiwa kupiga kura, waliruhusiwa na kupewa vitambulisho.

CHANZO: Nipashe

WAKITAHARIDHISHANA WENYEWE INAKUWA SALAMA,MAANA KAZI HIYO IKIFANYWA NA WACHAMBUZI WA SIASA WANAISHIA KUNYOOSHEWA VIDOLE WAKITUHUMIWA KWA UCHOCHEZI.

JAPO MEMBE ANASTAHILI PONGEZI KWA KUJITOA MHANGA KUSEMA HAYO ALOSEMA NDANI YA CHAMA KILICHOZOWEA KUSIFIWA TU HUKU CRITICISM YA AINA YOYOTE IKITAFSIRIWA KUWA NI MITHILI YA UHAINI,ALIPASWA PIA KUONGELEA NAMNA CCM INAVYOJIMALIZA KWA KUKUMBATIA MFUMO  USIO RASMI AMBAPO ASIYE NA FEDHA HAWEZI KUSHINDA CHAGUZI YOYOTE YA CHAMA HICHO.RUSHWA IMEKITHIRI MNO NDANI YA CHAMA HICHO KIKONGWE.

MADHARA YA MUDA MFUPI (IMMEDIATE) YA RUSHWA KATIKA CHAGUZI HIZO NI NI PAMOJA NA UWEZEKANO WA KUPATA VIONGOZI WASIO NA SIFA STAHILI NA AMBAO WANAWEZA KUTOWAJIBIKA IPASAVYO KWA VILE WANAJIONA KAMA WAMENUNUA UONGOZI NA WANA HAKI YA KUFANYA MAMBO WAPENDAVYO.MADHARA YA MUDA MREFU (LONG TERM) NI REPRODUCTION YA MAFISADI.CCM NDIO CHANZO KIKUBWA CHA VIONGOZI WA NGAZI MBALIMBALI NCHINI.KWA MAANA HIYO,CHAMA HICHO KIKIZEMBEA KAMA SASA NA KUACHIA VIONGOZI WAPATIKANE KWA NJIA YA RUSHWA BASI TAIFA NALO LITAENDELEA KUPATA SUPPLY KUBWA YA VIONGOZI WALIONUNUA CHAGUZI AMBAO HAWATASHINDWA KULIFISADI TAIFA.

HABARI MBAYA NI KWAMBA HAKUNA DALILI YA CCM KUPAMBANA NA RUSHWA KATIKA CHAGUZI ZA CHAMA HICHO.NA KIKWAZO KIKUBWA CHA JITIHADA HIZO NI HIZI SIASA MUFILISI ZA MITANDAO.KWAMBA,UKIJITAHIDI KUSIMAMIA HAKI UTALIPULIWA NA WALE WANAOJUA UMEFIKAJE HAPO ULIPO.NDIO MAANA WANASIASA MAKINI HUJITAHIDI SANA KUEPUKA MAKUNDI YA KUSAIDIA USHINDI KWA VILE KUJIHUSISHA NAYO HUMGEUZA MWANASIASA HUSIKA KUWA MTUMWA WA MAKUNDI YA AINA HIYO.

7 Dec 2008


The Commission for Human Rights and Good Governance (CHRAGG) is now set to conduct an indepth study on the causes behind the spate of killings of albinos and people with other related skin disorders, the Commission’s Chairman, Judge Amir Manento, has announced. 

Judge Manento told reporters in Dar es Salaam yesterday that the killings were an ugly blot on the country’s image, and it was important that all stakeholders joined in to fight the vice, but that a thorough investigation on the motives behind the killings needs to be done to facilitate its elimination. 

The Commission, he said, takes the albino killings seriously, and that it was high time a lasting solution was found soon. The Acting CHRAGG Executive Secretary, Ms Mary Massay, told reporters that the Commission was currently raising funds for the countrywide study. 

“We are serious about this … the commission will soon carry out a special investigation on the killings and their impact on society … in the next two years we will hopefully be in a position to deal decisively with this national shame,” Ms Massay said. On the state of human rights in the country, Judge Manento said that available statistics show that Dar es Salaam Region was leading with many acts of abuse being recorded. Though small geographically, the region is home to the country’s largest concentration of people in comparison to other urban settings in the country. He cited the increasing number of street children, rapes, criminal killings among many other examples of human rights abuses. He commended the government for addressing the issue with the seriousness it deserved, but said there were still many areas in which people feel still need more action taken to curb abuses of individual rights and freedoms. 

Judge Manento said many of the complaints the Commission had received so far were levelled against the police and prisons departments, old age and related retirement benefits and the job market. Beginning this year (on December 10), Tanzanians will for the first time celebrate - and consecrate the day – as an annual anniversary. This year’s theme is ‘Justice and Dignity for us all’

SOURCE: Daily News

SO WE ACTUALLY HAVE THE COMMISSION FOR HUMAN RIGHTS AND GOOD GOVERNANCE?LEAVE THE HUMAN RIGHTS STUFF ASIDE,WHAT'S THE COMMISSION DONE SO FAR IN FIGHTING UFISADI?ISN'T THAT PART AND PARCEL OF GOOD GOVERNANCE?OK,MAY BE IT'S CONDUCTING A 10-YEAR STUDY ON THAT BEFORE IT COULD DEAL DECISIVELY WITH THAT MATTER.

DOES IT REALLY MAKE ANYSENSE WHEN YOU HEAR THAT THE COMMISSION IS NOW SET TO CONDUCT AN INDEPTH STUDY ON THE CAUSES OF THE KILLINGS OF ALBINOS,AS IF THIS PROBLEM STARTED A FEW MONTHS AGO!THESE GUYS COULDN'T EVEN AFFORD TO SAY WHAT SHOULD BE DONE WHEN THEY ARE BUSY SOLICITING FUNDS FOR THE STUDY OR DURING THE 2 YEAR TIME WHEN THE STUDY IS BEING CARRIED OUT,IF IT WILL AT ALL!

THE KILLINGS NOT ONLY VIOLATE THE BASIC HUMAN RIGHTS,WHICH THE COMMISSION WAS CREATED TO OVERSEE,BUT ALSO INDICATE THAT THOSE ASSIGNED WITH THE TASK OF PROTECTING CITIZENS HAVE FAILED TO DELIVER,WHICH TRANSLATES INTO POOR GOVERNANCE.


A Dutch-operated container ship outran pirates off the coast of Tanzania this weekend, an official with the International Maritime Bureau said Sunday.

The incident took place "very far out to sea," showing that Somali-based pirates are extending their reach further and further, Noel Choong of the IMB's Piracy Reporting Center told CNN.

"Earlier attacks were on ships off the coast of Somalia, then off the coast of Kenya, and now this was 450 nautical miles off Dar es Salaam," he said, tracing the southward expansion of the pirates' area of operations.

The ship, which Choong declined to name, came under attack from rocket-propelled grenades, starting a fire on board, he said. The crew was able to put out the fire and escape by increasing speed.

The ship and crew are now out of danger, he said, following the incident at 11:42 GMT Saturday.

Piracy has become increasingly common in the Gulf of Aden and the Indian Ocean this year. So far, pirates have attacked almost 100 vessels off Somalia's coast and successfully hijacked nearly 40, according to the center.

Those hijacked vessels include an enormous oil tanker, a chemical tanker, and a ship laden with Soviet-era arms including tanks. The pirates normally hold the ships for ransom.

A luxury cruise ship carrying more than 1,000 passengers and crew successfully outran pirates off the coast of Yemen last weekend.

The IMB has tracked at least 11 incidents of actual or attempted piracy near the Tanzanian coast this year.

A multinational fleet, including vessels from the U.S., NATO member states, Russia and India, has been patrolling the Indian Ocean waters near the Gulf of Aden, which connects the Red Sea and the Arabian Sea. Around 20,000 oil tankers, freighters and merchant vessels pass along the crucial shipping route each year. Watch anti-piracy vessels patrol the region. »

In a recent interview provided to CNN, a pirate leader claimed attacks on shipping would continue as long as life in Somalia remained desperate.

"The pirates are living between life and death," said the pirate leader, identified by only one name, Boyah. "Who can stop them? Americans and British all put together cannot do anything."

SOURCE: CNN


UTATA wa zilipo fedha zilizorejeshwa na kampuni zilizoiba fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), umeendelea kuigubika nchi, baada ya kubainika kuwa fedha hizo hazijaingizwa kwenye mfuko ulioelekezwa na Rais Jakaya Kikwete wakati akilihutubia Bunge, Agosti 21 mwaka huu.

Fedha hizo ambazo ni zaidi ya sh bilioni 70, zilitakiwa ziende Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB), ambapo zingefunguliwa dirisha maalumu, lenye jukumu la kutoa mikopo kwa wakulima ambao kwa miaka mingi wamekosa fursa hiyo.

Uchunguzi wa Tanzania Daima Jumapili, umebaini kuwa fedha hizo zimehifadhiwa katika akaunti maalumu ambayo mpaka hivi sasa maelezo yake bado yamegubikwa na utata, kwa sababu kila ofisa wa Wizara ya Fedha na Uchumi aliyeulizwa juu ya akaunti hiyo, ameshindwa kutoa jibu linaloeleweka.

Tangu awali baadhi ya watu walionyesha wasiwasi wao kuhusu urejeshaji wa fedha hizo kama ni kweli zimerejeshwa au ilikuwa mbinu ya kisiasa ya serikali kutaka kuzima joto la wananchi, wapinzani na wahisani waliotaka fedha hizo zirejeshwe na watuhumiwa wafikishwe katika mikono ya sheria.

Watu hao waliweka wazi msimamo wao kuwa fedha hizo hazikurejeshwa bali ilikuwa ni janja ya serikali ili waweze kupata misaada kutoka kwa wafadhili ambao awali walitishia kutochangia bajeti ya serikali mpaka majibu sahihi na hatua za wizi wa EPA zichukuliwe.

Shinikizo hilo inadaiwa ndilo lililomfanya Rais Jakaya Kikwete kuamua kutengua uteuzi wa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Daudi Ballali, pamoja na kuunda timu ya uchunguzi chini ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, baada ya mkaguzi wa nje, Ernst & Young, kuthibitisha kuwapo kwa wizi katika akaunti hiyo, unaofikia kiasi cha sh bilioni 133.

Mkurugenzi wa Benki ya Rasilimali (TIB), William Mlaki, hivi karibuni alikaririwa na vyombo vya habari kuwa fedha hizo hadi sasa hawajazipokea.

Alisema inawezekana serikali inajiandaa kuwapelekea fedha hizo ambazo Rais Jakaya Kikwete alishaweka wazi dhamira ya serikali yake kuzipeleka TIB ili ziwasaidie wakulima.

“Mpaka sasa fedha za EPA, bado hazijaingia kwetu na si jukumu letu kuulizia fedha hizo zitakuja lini, kazi yetu ni kuzipokea na kuratibu zoezi la utoaji mikopo kwa wakulima,” alikaririwa Mlaki.

Kauli hiyo ya Mlaki, inazidisha utata kuhusu ukweli wa urejeshaji wa fedha za EPA ambazo uchotwaji wake unahusishwa na matumizi ya uchaguzi mkuu uliopita.

Inadaiwa kuwa mbinu za kuchota fedha hizo, zilifanywa na viongozi wa juu wa Serikali ya Awamu ya Tatu kwa kushirikiana na mwanasiasa na mfanyabiashara maarufu nchini ili zikisaidie Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu uliopita.

Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni, tena kwa nyakati tofauti, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba na Mkurugenzi wa Uchumi na Fedha, Amos Makala, wamekanusha chama chao kuhusishwa na wizi huo.

Mfanyabiashara huyo ndiye anayeaminika alikuwa mmiliki halali wa Kampuni ya Kagoda Agriculture Limited iliyochota sh bilioni 40, lakini hadi hivi sasa hajafikishwa mahakamani au kutajwa mbele ya umma.

Kutotajwa kwa mfanyabiashara huyo kunatokana na ukweli kuwa ndiye anayejua siri yote ya Kagoda na viongozi waliomuagiza kuzichota fedha hizo na hata matumizi yake pamoja na kujua nani kapata kiasi gani na kwa kazi gani.

Kwa hali ilivyo, Kagoda ndiyo kampuni inayoonekana kuitikisa nchi kama wamiliki wake watatajwa na kufikishwa mahakamani, kwani hawatakubali kushitakiwa peke yao bila kuwataja viongozi waliowatuma kufanya wizi huo.

Hali hiyo ndiyo iliyomfanya aliyekuwa Waziri wa Fedha, Zakhia Meghji, kutoa ufafanuzi kwa umma kuwa fedha zilizochotwa zilitumika kwa mambo ya usalama na si ufisadi kama ambavyo baadhi ya wanasiasa, akiwemo Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa, walivyokuwa wakisema.

Msumari wa moto juu ya utata wa urejeshwaji wa fedha za EPA na ufisadi hivi karibuni ulishindiliwa na mfanyabiashara maarufu nchini na mwachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jafar Sabodo, ambaye alisema serikali inafanya mchezo wa kuigiza na haina nia thabiti ya kutatua matatizo ya rushwa.

Sabodo ambaye ni rafiki wa karibu wa marehemu Mwalimu Nyerere na mfadhili wa mfuko wa taasisi ya Mwalimu Nyerere na CCM, alifikia hatua ya kusema yuko tayari kukisaidia chama chochote cha upinzani katika uchaguzi ujao, kuiangusha CCM madarakani, kwa madai kuwa imeshindwa kuondoa tatizo la rushwa nchini.

Wachambuzi wa masula ya siasa wanadai kupandishwa mahakamani kwa mawaziri wawili ya serikali iliyopita Basil Mramba (Fedha) na Daniel Yona ((Nishati na Madini), ni mpango wa kuwasahaulisha wananchi juu ya mwenendo wa kesi ya EPA, hasa kuendelea kufikishwa mahakamani kwa watuhumiwa wengine.

Mpango huo uliasisiwa kutokana na joto la wananchi kutaka wamiliki wa Kampuni ya Kagoda inayohusishwa na wafanyabiashara, wanasiasa maarufu na wakongwe nchini, kuzidi kushika kasi kiasi cha kumfanya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuweka bayana kuwa joto hilo likizidi, wamiliki wake watajulikana.

Wadadisi hao wanaendelea kubainisha kuwa mpango huo kwa kiasi fulani, umefanikiwa, kwani watu walihamisha macho na masikio yao kutoka EPA na kuhamia kwa Yona na Mramba, ambao wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salam kwa kosa la kuisababishia hasara serikali ya zaidi ya sh bilioni 11.7, kwa kutoa misamaha ya kodi kiholela katika sekta ya madini.

Wakati wingu zito likiwa limetanda kuhusu mahali zilipo fedha za EPA, kuna tetesi kwamba fedha hizo ndizo zilizotumika kulipa madai ya walimu ambao miezi miwili iliyopita walitishia kugoma nchi nzima kushinikiza kulipwa fedha zao za malimbikizo zinazofikia sh bilioni 16.


6 Dec 2008


December 1st was World Aids Day, an occasion marked each year by different activities including rallies, speeches, free and voluntary blood screening for the Aids virus in order to sensitise and mobilise people towards HIV/Aids eradication. 

As usual, the media people made it colourful with photographs, interviews and stories that were published in newspapers, TV screens and broadcasted by various radio stations in the country. 

One thing the media personnel did not do on the very day was to tell their audience the status of journalists with regard to the spread of HIV/Aids amongst themselves. 

Health authorities report that the prevalence of HIV/Aids among the Tanzanian population averaged at 7 per cent. 

However, this percentage may not be useful to journalists if they themselves are not participants in the free voluntary testing going on throughout the country, so they can be in the front line to take the test and publicly give testimonies as to their status and experiences. 

Last week`s meeting in Nairobi, Kenya from November 27-29 that was attended by journalists living with HIV from Tanzania, Kenya, Uganda and Ethiopia flagged off this important process in the region. 

Tanzania was represented at the workshop by the author of this article, Zephania Musendo, Kenya had two participants, Evelyn Simaloy and Lucy Maroncha. 

From Ethiopia were Ermeyas Mekonen and Tamerat Yemane and from Uganda came Elvis Basudde and David Musengeri. 

It was the first meeting of its kind to be held in Eastern Africa with the express purpose of bringing together journalists living with HIV/Aids in order to establish a network for sensitisation, mobilisation and action against the spread of HIV/Aids at the work places of journalists and beyond. 

The gist of the meeting was to work together on regional initiatives to promote a vibrant media fully engaged in the response to HIV/Aids. 

Journalists from the region shared experiences as victims of the HIV/Aids scourge. 

Panos Eastern Africa, which is working to support the establishment of a network of Journalists Living With HIV/Aids (JLWHA) was represented by Paul Banoba, Health Communications Regional Programme Co-ordinator, Paul Kimuwe, Programme Assistant and Metsehate Ayenekulu. 

The proceedings of the meeting and interactions of the participants were just as interesting as valuable. 

Serious deliberations started on November 27, when participants were introduced to the JLWHA project-their own project. 

It was amplified that journalists themselves must take the lead in testing and expounding on the HIV/Aids message of treatment, care and prevention. Surely, the testimonies given by the participants went a long way to confirm that they were ready for the task. 

Panos` Paul Banoba told the participants that South Africa had made some headway in establishing a network for journalists living with HIV/Aids. He therefore, urged the Eastern Africa region to follow suit and catch up with South Africa. 

The participants immediately positively took up the challenge. 

This is what they unanimously agreed to realise; that at the end of the meeting they would cascade information back to their media organisations and communities, raise the voices of people living with HIV/Aids, influence media houses to publish more stories on HIV/Aids, publicise the initiative to others, remain active and share HIV/Aids stories with other members. 

They also vowed to communicate within country and at regional levels, ask Panos to lead the progress of engaging members and communicate with journalists living with HIV/Aids until networks are established. 

They did not stop at that. Most importantly, they also charted means of realising those objectives. 

They said they would sensitise and identify more journalists to cover HIV/Aids and TB care and support programmes. They resolved to enrol more members and produce more feature articles on HIV/Aids. 

They would also introduce education programmes on HIV/Aids at work places and organise press conferences and briefings. 

The participants said they would establish links with national Aids programmes and Panos as stakeholders. 

In the end, they anticipated improved coverage of HIV/Aids and TB stories, reduced stigma on the victims in the Eastern Africa communities as well as increased support from editors in expanded focus on HIV/Aids stories and finally reach their ultimate goal of establishing networks of journalists living with HIV/Aids in their home countries as the end result. 

Panos Eastern Africa Executive Director, Luther Anukur, who officiated at the workshop`s closing ceremony had this to say; ``We are celebrating the birth of something new- the Network of Journalists Living with HIV/Aids which is very much needed.`` 

he added; ``Our commitment to do what participants of this meeting have resolved-to support the network to take off.`` 

Though Anukur admitted that this was a challenging task they were starting, he expressed optimism. 
``One day we will have the dream come to pass,`
SOURCE: Ippmedia.



MBUNGE wa Jimbo la Buchosa, Samwel Chitalilo ameingia katika mkasa mpya baada ya kudaiwa kumshambulia Mabula Matulanya, ambaye ni mlinzi wa ghati la ofisi ya kivuko cha Nyakaliro Kome, linalomilikiwa na serikali.

Mlinzi huyo anadai alishushiwa kipigo hicho na mbunge huyo kwa kushirikiana na washirika wake wawili mara baada ya kummulika tochi Chitalilo wakati akiwa kwenye haja ndogo karibu na mlango wa ofisi ya kivuko hicho, ambalo ni eneo la lindo lake.

Akizungumza na gazeti hili, mlinzi huyo alidai kuwa, shambulizi hilo lilimkumba Oktoba 10 mwaka huu majira ya saa 3:00 usiku wakati alipoingia kazini kwake kumpokea lindo mlinzi mwenzake. Muda mfupi baada ya kukabidhiwa lindo hilo, alihisi kuwepo kwa mtu katika eneo la ofisi na hivyo kumulika eneo hilo kwa tochi.

Alisema kitendo cha kumulika tochi ndicho kilichomponza na kumsababishia kupata kipigo kutokana na mbunge huyo kukasirika, akidai kuwa alidhalilishwa kwa kumulikwa na tochi wakati akiwa kwenye haja ndogo na kwamba yeye kama mbunge hapaswi kufanyiwa hivyo.

“Nilimulika nikidhani pengine anaweza kuwa mwizi katika lindo lango... sikujua kama ni mbunge na wala sikuwa natambua kama alikuwa katika baa ya jirani akinywa pombe. Nilikuwa kazini, lakini licha ya kumueleza yote hayo nilishikwa na watu wake wawili na kuanza kushambuliwa na mbunge huyo kwa ngumi na mateke,” alidai.

Alidai kuwa baada ya kipigo hicho alikwenda katika kituo cha polisi cha Nyakalilo kutoa taarifa ambapo baadaye, Chitalilo, akiwa na wapambe hao wawili (majina tunayo), walimfuata na kuendelea kumshambulia akiwa kituoni hapo mbele ya mgambo wa kituo anayejulikana kwa jina moja la Shimo.

Alidai baada ya kuzuiwa na mgambo huyo, mbunge huyo na wapambe wake waliamua kupiga simu kituo kikubwa cha polisi ambako walitoa maelekezo kwa askari wa zamu aliyemweka ndani na kesho yake kuchukuliwa na polisi wa kituo kikuu cha wilaya ambao walimwandikisha maelezo.

"Lakini walininyima PF3 kwa ajili ya matibabu jambo ambalo limefanya nitibiwe kienyeji na kupona pasipo kumchukulia hatua yoyote mbunge huyo," alidai mlinzi huyo na kuomba vyombo vya usalama vimsaidie ili aweze kuchukua hatua dhidi ya mbunge huyo kwa vile ameshambuliwa akiwa kazini.

Naye Mbunge Chitalilo, alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu mkasa huo, alikiri kuwepo kwa shambulio hilo na kusema kuwa mlinzi huyo alishambuliwa na wananchi waliokuwa jirani kutokana na yeye kulalamika kudhalilishwa kwa kumulikwa wakati akiwa anakojoa.

“Sikiliza suala hili, mimi nilishalisamehe, polisi kwa kuwaomba wamfutie mashtaka mlinzi huyo kwa vile watu wengi waliniomba samahani... alinidhalilisha kwa kunimulika makusudi licha ya kujua nilikuwa mimi... alishambuliwa na watu ambao nilifanya kazi ya kuwatuliza, sasa mimi kosa langu ni kumsamehe?” alihoji.

Hata hivyo, mbunge huyo alimsihi mwandishi kuachana na habari hizo kwa vile hazina maana katika jamii na kumtaka kufuatilia masuala ya maendeleo katika jimbo lake.

Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Jamal Rwambow, hakuweza kupatikana kulitolea ufafanuzi jambo hilo kutokana na kuwa katika ukaguzi wa vituo vya polisi jijini Mwanza, ziara ambayo amekuwa akiifanya kwa lengo la kutambua na kubaini matatizo ya jeshi lake mkoani hapa.

CHANZO: Mwananchi

THIS GUY IS A FRAUD.LAKINI HAYA NDIO MATOKEO YA KUANGALIA HAIBA YA MGOMBEA (NA VIJISENTI VYAKE) WAKATI WA KAMPENI YA UBUNGE BADALA YA KUPIMA UWEZO WAKE.HUYU MTU ANA TUHUMA ZA KUFOJI CHETI CHA SHULE,ANADAIWA KUWALIZA WATU FLANI WALOMKOPESHA FEDHA KWA AJILI YA BIASHARA YAKE,NA SASA KITUKO HIKI!MBUNGE GANI MAKINI ATAKOJOA OVYO?KWANI ANGEKWENDA KUJISAIDIA MSALANI ANGEMULIKWA TOCHI NA HUYO MLINZI?HUU NI UHUNI WA KISIASA UNAOHITAJI ADHABU KALI COME 2010.

LAKINI MKASA HUU UNATUSAIDIA KUONYESHA NAMNA HAKI ILIVYO NA TAFSIRI TOFAUTI KATI YA WALALAHOI NA WAHESHIMIWA.MLINZI ALIYEKWENDA KUDAI HAKI YAKE AMEISHIA KUSWEKWA NDANI,MHESHIMIWA ALIYETUHUMIWA KWA SHAMBULIO YUKO HURU AKIJIGAMBA KWA "KUMSAMEHE" VICTIM WAKE!

5 Dec 2008


Picha (for illustrative purpose only) kwa hisani ya MWANAKIJIJI.

MAPIGANO ya koo katika wilaya ya Tarime mkoani Mara, yameingia katika sura mpya baada ya kubainika watu wanaodaiwa kuwa askari wastaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kutumia silaha, sare za Jeshi hilo na mbinu mbalimbali ili kuhakikisha koo wanazotoka zinashinda. 

Baada ya kugundulika kwa matumizi hayo ya vifaa vya JWTZ, Polisi mkoa wa Mara imeanzisha operesheni kali na limewafanikiwa kukamata bunduki tatu, risasi 56 na sare mbalimbali za Jeshi, ambazo zimekuwa zikitumiwa na baadhi ya watu katika mapigano ya koo za Wairegi na Wanyabasi wilayani Tarime. 

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Bw. Deusdedit Kato, alisema jana kuwa silaha hizo ndizo zilizotumika katika mapigano hayo juzi na kuua watu wawili kwa risasi. 

Alisema ingawa bado haijathibitishwa kuwa wamiliki wa silaha hizo kinyume cha sheria ni askari wastaafu wa JWTZ, lakini kuna ukweli huo kutokana na taarifa za awali na wamekuwa pia wakiendesha mafunzo kwa vijana hili kumudu mapambano hayo ya koo. 

Alisema katika operesheni hiyo inayoendeshwa na Polisi, limeweza kukamata bunduki mbili aina ya shotgun namba 979256 na 85084 na risasi 56 zinazomilikiwa kinyume cha sheria nyumbani kwa Bw. Samwel Range wa kijiji cha Magoto ambaye alikimbia kabla ya kukamatwa. 

Kamanda Kato alisema katika upekuzi huo, pia polisi walikamata sare za JWTZ kama vile half sack (2), kit bags (6), suruali za JWTZ (2), suruali za JKT (2) na shati aina ya kombati moja ya JWTZ ambazo zimekuwa zikitumiwa katika mapigano ya koo na matukio mengine ya uhalifu. 

Alisema katika upekuzi mwingine uliofanyika nyumbani kwa Bw. Samwel Magabe, askari hao wa Polisi walikamata bunduki nyingine aina ya shotgun 978862 CAR 151 ambayo pia inasadikiwa kutumika katika mapigano ya koo hizo mbili katika kata ya Nyamwaga. 


Kamanda Kato ambaye pia ni Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Mkoa (RCO) wa Mara, alisema pia viongozi wawili wa kijiji cha Magoto wamekatwa baada ya kudaiwa kuchochea mapigano hayo ya koo. 

Aliwataja viongozi hao kuwa ni Bw. Gabriel Matiku, ambaye ni Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho na Bw. Charles Chacha, Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho na hivi sasa wanahojiwa na Polisi Tarime kabla ya kufikishwa mahakamani. 

“Vita hii ya koo katika wilaya ya Tarime, kwa kweli inatuumiza vichwa kwani baadhi ya viongozi pia wanahusika, sasa lazima tufanye uchunguzi na hatutashindwa kuwachukulia hatua viongozi wote wanaodaiwa kuwa wachochezi,” alisema Kamanda Kato. 

Katika mapigano hayo ambayo kwa sasa yameanza kudhibitiwa na polisi waliosambazwa katika vijiji vya Nyamwaga na Magoto, watu wawili waliuawa kwa kupigwa risasi na kutajwa kuwa ni Bw. Girasi Marwa na Bw. Samwel Chacha wote wakazi wa Nyamwaga kutoka koo ya Wairegi. 

Wilaya ya Tarime imekumbwa na vita vya koo kwa muda sasa na watu kadhaa kuuawa kwa mishale, kukatwa mapanga, kuchomwa moto na wengine kupigwa risasi, huku mali na nyumba zikiteketezwa kwa moto kwa kuhusisha koo za Wakira, Waanchari na Warechoka katika kata za Susuni na Sirari, wakati mapigano kama hayo pia yamekuwa yakiibuka katika kata ya Bumera kwa kuhusisha koo za Wahunyaga na Wamera. 

Chanzo kikuu cha mapigano hayo kimekuwa kikitajwa kuwa ni wizi wa mifugo, mipaka ya ardhi na kilimo cha bangi.

CHANZO:Majira

MAUAJI YA DHIDI YA ALBINO YAMESHINDWA KUDHIBITIWA,NA HAKUNA ANAEWAJIBIKA.MAPIGANO YA KOO HUKO TARIME YAMEKUWA YAKIENDELEA KWA MUDA MREFU SASA NA ENEO HILO LIMEGEUKA MITHILI YA ENEO LISILOTAWALIKA LA MPAKA KATI YA PAKISTAN NA AFGHANISTAN.AGAIN,HAKUNA ANAYEWAJIBIKA KUTOKANA NA MAPIGANO HAYO HUKO TARIME.NA KAMA KAWAIDA YETU,TUNASUBIRI MOTO UWE NJE YA UWEZO WA ZIMAMOTO NDIO TUANZE KUUZIMA KWA MIKONO. 

4 Dec 2008


MAUAJI ya albino yanaendelea kutikisa, na safari hii kwa kutumia silaha kali, licha ya serikali kuanza operesheni maalum ya kupambana na uovu huo baada ya mlemavu wa ngozi anayefahamika kama Ezekiel John, 47, kuuawa kwa risasi na watu wasiojulikana ambao walitoweka na mkono wake wa kulia.

Mlemavu huyo wa ngozi aliuawa wakati akiwa nyumbani kwake.

Kamanda wa polisi mkoani Kigoma, Abdihaki Rashid alisema katika taarifa yake jana kuwa watu hao walivamia nyumbani kwa marehemu na kumpiga risasi mgongoni, na baadaye kumkata mkono ambao walitoweka nao.

“Tukio hilo lilitokea juzi, katika Kijiji cha Muyama wilayani Kasulu na askari waliokwenda kufanya uchunguzi wa awali katika eneo la tukio hawajarudi, hivyo watakaporejea tutatoa taarifa za kina zaidi,” inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Mauaji ya albino yametapakaa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa yakihusishwa na imani za kishirikina na tayari watu wengi wenye ulemavu wa ngozi wameshauawa kikatili na watu wasiojulikana ambao hukata viungo vya albino na kutoweka navyo.

Serikali imepeleka askari wa kikosi maalum cha kupambana na ukatili huo, lakini taarifa za kuuawa kwa albino zinaendelea kumiminika, huku polisi wanne wakiripotiwa kuwekwa ndani kwa tuhuma za kuwaachia wauaji wa albino baada ya kuhongwa fedha.

Mwanzoni mwa wiki hii watu waliokuwa wamejifunika sura zao walimvamia mwanafunzi wa darasa la tatu mwenye ulemavu huo, Mateso Dunia, 13 na kumuua kikatili.

Mtoto huyo wa darasa la tatu alikuwa mkazi wa Kijiji cha Gunihuna kilicho katika Kata ya Iponya wilayani Bukombe. Hilo lilikuwa tukio la pili wilayani humo kwa mtoto albino kuuawa tangu mauaji hayo ya kikatili yanayohusishwa na imani za uchawi yaanze Kanda ya Ziwa.

Tukio hilo lilitokea siku chache baada ya jeshi hilo kuwakamata polisi wanne ambao wanatuhumiwa kupokea rushwa kutoka kwa wauaji wa albino na kuwaachia huru.

Mwanafunzi huyo albino aliuawa juzi majira ya saa 6:00 wakati akiwa anarudi nyumbani na wenzake. Walikuwa wakitoka kuangalia video.

Hata hivyo baadaye miguu miwili ya albino ilikamatwa kwa mganga wa jadi ambaye alikimbia kabla polisi hawajamfikia.

Katika hatua nyingine taarifa hiyo ilisema kwamba, katika Kijiji cha Munyange, Polisi wakiwa katika doria ya kawaida, waliwakurupusha watu waliodhaniwa kuwa ni majambazi na kukimbia.

Taarifa hiyo ilifafanua kwamba watu hao wakiwa katika harakati za kukimbia, walidondosha mabomu mawili ya kutupa kwa mkono.

CHANZO: Mwananchi

HIVI JAMII ITAENDELEA KUWA WATAZAMAJI WA UKATILI HUU HADI LINI?HII NI AIBU KUBWA KWA TAIFA LETU KWANI LICHA YA KUONEKANA KITOVU CHA UKATILI DHIDI YA WALEMAVU (WA NGOZI) TUNAONEKANA KAMA KITUO CHA USHIRIKINA USIOTHAMINI UHAI WA BINADAMU WENZETU.INGEKUWA NCHI ZA WENZETU,KUNA MTU ANGEWAJIBIKA LAKINI KWETU NI BUSINESS AS USUAL AS IF NOTHING IS HAPPENING,WAZIRI WA MAMBO YA NDANI ANAPASWA KUWAJIBIKA KWA HILI.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.