24 Apr 2010

This day last year,at 1400,I received my miracle from the Lord.Two months earlier,I was introduced to a Houston,TX-based powerful woman of God,Apostle Esther.She taught me that when praying,I should ask the Lord for receiving,rather than seek for, my miracle because it was already there.She also gave recommended the ever powerful Psalm 91 to read every day for a number of days.And guess what,as she assured me,I eventually got something that has people waiting for up to a decade to get it, if they at all are successful.God is really Great,and this particular miracle is a living example.I would also like to thank Christha, the woman whose love and care comes only second  to my mother's,for introducing me to the Apostle,and for her tirelessly efforts in praying with me.Praise the Lord,Ameen.For Christa,I dedicate the following video (though I know you don't fancy secular music).

23 Apr 2010

Majuzi Rais Jakaya Kikwete alimteua Doug Pitt,mdogo wa staa wa filamu Brad Pitt,kuwa balozi wa heshima (goodwill ambassador) kusaidia kuitangaza Tanzania hususan kwenye sekta ya utalii.Kwa kuzingatia wasifu wa Doug,na umuhimu wa kuitangaza nchi yetu,uteuzi huo unastahili pongezi za kutosha.Hat hivyo,ili Doug awe na umuhimu kwa Tanzania,au uteuzi wake uzae matunda yanayotarajiwa,kuna mambo kadhaa tunayopaswa kuyaangalia kwa makini 
Kwa hakika hatuna kisingizio cha kwanini nchi yetu inahitaji nguvu za ziada (kama akina Doug) katika kujitangaza.Tuna kila aina ya utajiri na vivutio ambavyo laiti tungejibidiisha kuvitangaza kwa bidii basi huenda tungekuwa mbali sana kimaendeleo.Kwa mtizamo wangu,kikwazo kikubwa ni uhaba wa uzalendo.Baadhi ya wateule wanaopaswa kuwajibika ipasavyo kulitangaza taifa letu na raslimali zake wako bize zaidi kuangalia maslahi yao binafsi badala ya kufanya kile wanacholipwa mshahara kukifanya.

Lakini kama unadhani hilo ni tatizo dogo basi kuna suala la mazingira yanayopaswa kuboreshwa ili jitihada za Doug ziweze kuwa na maana au zilete ufanisi unaotarajiwa.Kwa mfano,Doug anaweza kuhamasisha watalii waje kwa wingi Tanzania,lakini kwa ufisadi unaoendelea kila kukicha katika sekta ya umeme,ni dhahiri kuwa watalii watakaoitikia wito wa Doug wanaweza kuhisi 'wameingizwa mkenge' baada ya kukutana na adha za mgao wa umeme ambao unazidi kuzoeleka kwa Watanzania wengi.Danadana zinaendelea kuhusu kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo sugu la umeme.Na kikwazo kikubwa katika kupatikana ufumbuzi huo ni wahusika kutanguliza maslahi yao binafsi badala ya yale ya taifa.Ni katika mazingira hayo ndipo matapeli wa Richmond na Dowans walifanikiwa kutufisadi.

Kwa Watanzania walio nje watakubaliana nami kwamba kwa hawa wenzetu,'holidays' ni suala lenye umuhimu wa kipekee katika kalenda na ratiba zao.Ni matarajio ya wengi kwamba holidays walizozihangaikia kwa muda mrefu zitaacha kumbukumbu nzuri maishani mwao,na sio kugeuka 'holidays from hell'.

Kuna tatizo jingine katika suala la udokozi.Pale Mwalimu Nyerere International Airport panahitaji tahadhari kubwa ili mizigo ya msafiri itoke eneo hilo salama.Sasa kama kweli tunataka jitihada za akina Doug ziwe na maana ni vema tukafahamu kuwa pasipo kudhibiti wahuni hawa wa airport ambao inaonekana dhamira yao kuu ni kutoa 'karibu Tanzania ya majonzi' tutaishia kukimbiza watalii badala ya kuwafanya wawashiwishi ndugu na jamaa zao nao waende Tanzania kutalii.Wadokozi wengine mahiri wako Posta.Kwa vile mawasiliano yetu bado si ya kisasa sana,umuhimu wa Posta unabaki kuwa mkubwa,na si ajabu kwa baadhi ya potential watalii kutumia huduma hiyo kabla ya kwenda Tanzania,au wakati wakiwa hapo.Sasa it seems as if baadhi (au pengine most) ya watumishi wa Posta wana 'allergy' na kitu chochote chenye address ya ng'ambo.Ni lazima wafungue na wakikuta chochote 'wanakitaifisha'.

Tuna matatizo ya miundombinu.Tumeruhusu wahuni wa TRL wafanye usanii wao pasipo kuleta mabadiliko yoyote ya muhimu zaidi ya kuandika historia ya kuwa wawekezaji wa kwanza kusaidiwa na serikali kulipa mishahara ya wafanyakazi wao.Ni dhahiri kuwa laiti waliosaini mkataba wa wababaishaji hao angekuwa mzalendo wa dhati angetambua kuwa wangekuja kuikongoroa zaidi Reli ya Kati kuliko walikvyoikuta.Je watalii wakitaka kutumia usafiri wa treni kutalii inakuwaje?Huko TAZARA nako hadithi ni ileile.Na hii ni njia muhimu kwa mtalii anayetaka 'kuifaidi' hifadhi ya Selous.

Kuna tatizo la barabara zetu.Na hapa kuna suala la barabara za msimu ambazo kupitika kwake kunatarajia msimu wa mwaka.Nyingi ya barabara hizi hufanyiwa ukarabari pale tu panapokuwa na ujio wa kiongozi.Uelekeo wa kule kwetu Ifakara tuna hifadhi ya msitu asilia,lakini kufikika kwake ni mbinde msimu wa masika.

Kwa kifupi,nachojaribu kupigia mstari hapa ni umuhimu wa kuboresha mazingira yatakayopelekea watalii kuhitimisha kuwa hawakufanya makosa kukubali ushauri wa Doug kuitembelea Tanzania.Pasipo mazingira bora basi tunaweza kuteua mabalozi Hollywood nzima lakini itakuwa kazi bure.

Na jingine la muhimu zaidi ni manufaa ya ujio wa watalii kwa Watanzania.Sote tunashuhudia jitihada za kuvutia wawekezaji na mwitikio wao lakini pia sote twafahamu namna uwekezaji ulivyoshindwa kuwa na manufaa kwa Watanzania walio wengi.Makampuni ya madini yanazidi kumaliza raslimali zetu huku sie wenye utajiri huo tukibaki na mashimo matupu.Sasa Doug anaweza kulivalia njuga suala la kuhamasisha watalii,nao wakaitikia wito lakini kitakachopatikana kikaishia kwenye ununuzi wa ma-vogue,ujenzi wa mahekalu au kuongeza idadi ya nyumba ndogo za mafisadi.

Ndio maana basi,pamoja na kupongeza uteuzi wa Doug Pitt kuwa balozi wa hisani wa Tanzania huko Marekani,ni muhimu kuwekeza zaidi katika uzalendo utakaopelekea kuzalisha akina Doug wa ndani (na hakutokuwa na gharama ya kuwafuata ng'ambo) na, cha muhimu zaidi,kuchangia maendeleo ya taifa letu 'changa'.

22 Apr 2010

Dressed to kill.Our sisters looking good.Picture courtesy of Miss Jestina's Blog.(1st left ).

'SOS' Appeal!

Yea,I normally blog about politics and such stuffs,but,well,there's no harm in touching some other  issues that make the world go around.I'm talking about fashion.If you happen to visit as many blogs each day as I do you certainly would appreciate that our sisters are doing quite an excellent job in blogging about different stuffs in our lives,especially fashion.However,unfortunately,most of them tend to 'forget' including men's fashion trends in their blogs.They justifiably could 'defend' themselves by arguing that it's not up to them to make sure that we look as good as they normally do.But,honestly,when you have the likes of me whose taste for fashion is as good as a blind man in a dark alley,that spells trouble,and calls for an urgent need for help.Arguably,I'm not an exceptional case as there's probably a whole bunch of guys out there who seriously need help.So,come on sisters,we all know that if what a man dresses pleases you it certainly would please the rest of the world.Could you kindly please think of us,at least once a month, when you keep your audience posted about latest fashion trends?

21 Apr 2010







Picha zote hapo juu zinaonyesha maadhimisho ya 'Siku Ya Bangi Kitaifa' (National Weed Day) almraaduf '4/20' (April 20) nchini Marekani.ANGALIA HAPA kwa habari kamili na picha zaidi

20 Apr 2010

Hapa chini kuna habari ambayo kama ni ya kweli basi hatma ya nchi yetu iko mashakani.Lakini kabla hujaisoma,angalia picha ifuatayo na inaweza kukusaidia kukupa uelewa wa namna tulivyofika tulipo.






KUMBE Rais Jakaya Kikwete hakusoma sheria aliyosaini kwa mbwembe. Sasa baada ya kugundua kasoro zake anataka ikarabatiwe kwa njia ya kanuni, MwanaHALISI limeelezwa.

Hilo liligundulika katika mkutano wa wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wenyeviti na makatibu wa wilaya uliomalizika wiki iliyopita mjini Dar es Salaam.

Taarifa za ndani zinasema, bila aibu na hasa kwa ujasiri wa kiongozi mkuu wa nchi, Rais Kikwete alimuuliza Philip Marmo, waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, maana ya baadhi ya vifungu katika sheria hiyo.

Lakini katika hali ambayo haikutegemewa, Marmo alijibu kana kwamba anamkejeli rais, jambo ambalo lilistua wajumbe wa kikao hicho cha juu cha utekelezaji wa sera za chama.

MwanaHALISI limeelezwa kwamba Rais Kikwete alistushwa na kifungu cha sheria kinachotaka mgombea kuwasilisha katika ofisi za msajili, taarifa ya fedha atakazotumia.

Kifungu hicho kinatoa siku saba kabla ya siku ya mwisho ya NEC kutangaza majina ya wagombea.

Kifungu kingine kinachodaiwa kumstua kinahusu idadi ya wajumbe wa kampeni. Kwa CCM, yenye hata vikundi vya ngoma na nyimbo kama ToT, kuweka timu ndogo kunaweza kupunguza shamrashamra na kuathiri kampeni.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa, ilikuwa baada ya rais kupitia maeneo hayo, alimuuliza Waziri Marmo iwapo kile alichokuwa akifafanua kimetokana na sheria iliyopitishwa.

Naye Marmo, akiongea kwa sauti ya unyenyekevu alijibu, “…hiki ndicho ulichosaini.”

Kwa kauli ya Marmo, Rais Kikwete alionekana kustuka na kusema, kama hali ni hivyo, basi sheria itakuwa imeingilia hata mchakato wa wagombea ndani ya vyama, kimeeleza chanzo chetu.

Taarifa zinamnukuu rais akihoji kwa nini “sheria imekwenda mbali mno” na kuagiza papohapo kuwa wahusika waangalie ambapo sheria inaingiliana na watengeneze kanuni zitakazoleta nafuu.

Rais amenukuliwa akimwagiza Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutengeneza “kanuni vizuri” ili kuondoa mwingiliano unaoleta ugumu wa utekelezaji.

Hoja ya maelekezo ya sheria mpya ya gharama za uchaguzi ilikuwa moja ya ajenda za kikao cha NEC, wenyeviti na makatibu wa CCM wilaya kutoka kote nchini.

Tarehe 17 Machi mwaka huu, Rais Kikwete alisaini hadharani na kwa mbwembwe Sheria ya Gharama za Uchaguzi, ikulu Dar es Salaam ambapo hafla hiyo ilihudhuriwa na majaji, wabunge, viongozi wa serikali na vyama vya siasa, mabalozi na waandishi wa habari.

Hata hivyo, sheria hii imekuwa ikilalamikiwa na vyama vya siasa na wanaharakati, kabla na baada ya kusainiwa kuwa itakuwa ya udhibiti kwa wenye msimamo tofauti na watawala.

Aidha, siku tatu baada ya sheria hiyo kusainiwa, mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa alitupa kombora kwa kusema sheria aliyosaini rais ilikuwa na vipengele ambavyo havikujadiliwa bungeni na kwamba “viliingizwa kinyemela.”

Ubishi wa Mwanasheria Mkuu wa serikali, Jaji Frederick Werema kwamba hakukuwa na chochote kilichofanywa kinyemela ndio umekuza hoja ya Dk. Slaa na kufanya achimbue zaidi kshfa hiyo.

Katika kufukua, Dk. Slaa amekwenda hadi kwenye kumbukumbu za bunge (Hansard) na kuthibititisha kuwa Kifungu 7 (3) ambacho kimo katika sheria aliyosaini rais hakikujadiliwa bungeni na hivyo hakikurekodiwa katika hansard.

Mtunga sheria huyo kutoka Karatu amesema pia kuwa chochote kilichojadiliwa bila kuamuliwa na bunge kilikuwa kinatarajiwa tu katika kanuni au fafanuzi za au ainisho za maneno na taratibu lakini siyo katika vifungu vya sheria.

Katika majibu yake kwa kauli za Dk. Slaa, Jaji Werema alitetea serikali na kuthibitisha kuwa kifungu hicho kiliwekwa na waziri Marmo.

Dk. Slaa amesema katika andishi maalum, “Hakuna mwenye mamlaka, hata rais hana mamlaka hayo, sembuse waziri.

“Baada ya mjadala katika Kamti ya Bunge zima, maneno yakikubaliwa ndiyo hayo yanaingia kwenye sheria na serikali haina mamlaka ya kwenda kuyarekebisha inavyotaka. Ndiyo maana ya kusema ‘kifungu kimepitishwa,’ ” ameeleza Dk. Slaa.

Akiweka msisitizo, Dk. Slaa anasema, “Kitendo cha kuchomeka kinyemela ni kitendo kibaya sana na kinapaswa kulaaniwa, kwa sababu, kwa utaratibu huu wataalam wanaweza kuipeleka nchi pabaya kwa kupenyeza jambo lolote wanalotaka wao hata kama halijajadiliwa au limekataliwa na Bunge.”

Dk. Slaa anafafanua hatua ya serikali ya kuingiza mambo kinmyemela katika sheria kuwa ni kosa la jinai na kusema hata kifingu walichochomeka kinyemela kina madhara makubwa.

Kifungu kilichoongezwa na serikali kinataka timu ya kampeni kukaguliwa na watendaji wa serikali ya CCM.

“Kampeni ndiyo inayobeba mikakati na siri yote ya uchaguzi. Haiingii akilini kabisa kuwa serikali (pengine unayotaka kuiondoa kwenye uchaguzi ambayo ndio haki ya msingi ya kila mgombea) ndiyo inaweka mkono wake kwenye udhibiti wa mikakti hiyo,” anafafanua Dk. Slaa.

Anasema kuweka kifungu kama hicho ni “wenda wazimu, kwa mtu yeyote aliyefikiria jambo hilo, au anaandika tu kutoka mezani na au hajui maana halisi na majukumu yake.”

Kutokana na kuibuka kwa kashfa hii, serikali sasa imeamua sheria hiyo irejeshwe bungeni ili kufanyiwa marekebisho yanayostahili.

Naye Dk. Slaa tayari ametoa pendekezo: “Namna pekee ya kuepukana na athari hiyo ni kwa serikali kukiri imefanya makosa, na ndio ustaarabu bila kutafuta visingizio.”

Anasema serikali iwasilishe kwenye Mkutano wa 19 wa Bunge hili ulioanza jana, kitu kinachoitwa “Miscellaneous Amendment” – marekebisho ya sheria mbalimbali – na au ikichelewa sana katika Bunge la Bajeti.

Wachunguzi wa mambo wanasema Rais Kikwete atakuwa amesikitishwa sana na hatua ya wasaidizi wake ya “kumchomekea” vitu ambavyo baadaye vinamomonyoa hadhi yake kama mkuu wa nchi.

Miongoni mwa wanaotajwa kuwa wamempotosha au wameshindwa kumsaidia rais, ni pamoja na Jaji Werema ambaye ametetea uingizaji kinyemela kipengele ambacho hakikujadiliwa bungeni.

Mwingine anayetajwa ni waziri Marmo ambaye ambaye nduye hasa ametajwa kubuni na kuingiza maneno ya kifungu kinacholaaniwa.

CHANZO: Mwanahalisi.



19 Apr 2010

Ni dhahiri unapokutana na kitangulizi 'http://...' unafikiri kuwa kinachofuata ni anuani ya tovuti flani.Lakini je 'http://' (kifupisho cha Hypertext Transfer Protocal)bado ina umuhimu katika mazingira ya sasa ambapo unaweza kuitambua anuani ya tovuti hata bila kitangulizi hicho? . 
Wanateknolojia wa Google Chrome hawadhani kama kitangulizi hicho bado ni muhimu na wameamua kukificha katika toleo jipya la browser hiyo.

Hata hivyo,ufumbuzi huo sio rahisi kama inavyoonekana kwani unaweza kuficha kitangulizi hicho unapoandika anuani ya tovuti lakini bado kipo.Pia inatarajiwa kuwa maendeleo hayo yanaweza kuzua mkanganyiko kwa baadhi ya watumiaji wa intaneti.

Makala hii imetafsiriwa (katika tafsiri isiyo rasmi) kutoka mtandao wa Mashable

Kuna busara moja inayotuasa kuwa mpuuzi husema kwa vile anajiskia kusema (hata kama ni upuuzi) ilhali mwenye busara husema tu pale anapokuwa na kitu cha kusema (ikimaanisha kama hana cha kusema,au haoni umuhimu wa kusema kitu,atakaa kimya. Busara zaidi zinatuasa kuwa makini na tunayosema hadharani kwa vile mara nyingi jamii humtambua zaidi mtu kwa kauli zake.Sema upuuzi,utaonekana mpuuzi.Sema ya busara,utaonekana mwenye busara.Sasa kuna huyu msomi,Dokta Benson Bana,ambaye licha ya kuwa mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam,ni mkuu wa idara ya Sayansi za Siasa na Uongozi na pia ni Mwenyekiti Mwenza wa REDET.Yayumkinika kusema Dkt Bana amekuwa mahiri zaidi wa kutoa kauli zisizoendana na wasifu wake kitaaluma kuliko umahiri wa wa usomi wake

Na leo,kwa mujibu wa habari katika gazeti la Mwananchi,msomi huyo 'amelipuka' tena kwa kauli kwamba tuhuma zilizokithiri dhidi ya ufisadi zinaweza kusababisha taifa kukosa viongozi wazuri wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba.Huhitaji kuwa na hata asilimia moja ya kiwango cha elimu ya Dkt Bana kutambua kuwa tuhuma zilizotapakaa kuhusu ufisadi ni matokeo ya kuwepo kwa ufisadi.Msomi huyu anaishi Tanzania lakini yaelekea hafahamu mazingira yanayomzunguka,na hilo linaleta wasiwasi mkubwa kuhusu mchango wa wanataaluma katika maendeleo ya nchi yetu.

Katika habari hiyo Dk Bana aliwataka watu "waaache siasa chafu za kuhubiri na kudai kuwa watuhumiwa wa ufisadi hawafai kupewa kura au kuchaguliwa katika nafasi mbalimbali za uongozi kana kwamba wameshathibitika".Huu ni zaidi ya ubabaishaji wa kitaaluma,na kwa kiasi flani inaaibisha Udaktari wa Filosofia tunaohenyea akina sie.Kwanza,Dkt Bana amepata wapi mamlaka ya kuwataka wananchi waache kulalamikia ufisadi?Usomi hautoi mamlaka ya kuizuia jamii kulalamikia maovu yanayoisumbua.Pili,kwa mtizamo wa msomi huyu,kwa vile tuhuma za ufisadi hazijathibitika basi watu wakae kimya hadi 'miujiza itapotokea kwa watawala wetu kuamua kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mafisadi'!Hii ni sawa na kuingiliwa ndani na kibaka halafu ukakaa kimya kwa vile tu wewe sio chombo cha sheria.Ukifanya hivyo,hata hao polisi watakuona mpumbavu na unawapotezea muda.La kufanya ni kumdhibiti kibaka au kupiga kelele kuwashtua majirani wakusaidie kumdhibiti.

Binafsi,pamoja na kuheshimu uhuru wa kutoa mawazo,nadhani tatizo kubwa la Dkt Bana ni tabia yake ya 'kusema chochote' hata kama hana cha kusema.Inaelekea aidha hafahamu athari za tabia hiyo au anapuuza tu.Matokeo yake ni kuonekana mbabaishaji wa namna flani.Si lazima jina lake lionekane magazetini au kusikika radioni kama hana la muhimu kuieleza jamii.Eti anatuasa kuwa "si vizuri kwa watu kunyimwa kura kwa sababu ya kutuhumiwa kwa ufisadi hadi hapo watakapothibitika na kutaka wanasiasa waache kuhukumu wenzao bila kosa".Kwanini hajiulizi inakuwaje watu hao wanatuhumiwa ufisadi in the first place?Kwanini ni wao na si Dokta Bana,kwa mfano?

Hivi lipi lililo muhimu zaidi kwa Tanzania kama taifa: kukosa viongozi bora kwa vile wanatuhumiwa kwa ufisadi au kupata viongozi bora watakaowajibika kulitumikia taifa kupambana na ufisadi?Wasiwasi wa Dkt Bana ulipaswa kuwa kwenye athari za ufisadi kwa jamii na sio tuhuma za wananchi dhidi ya mafisadi.Ni mlevi tu atakayeshindwa kuelewa kuwa kinachoumiza Watanzania kwa sasa ni UFISADI na sio TUHUMA DHIDI YA MAFISADI.

Mwanataaluma huyu anaongoza taasisi ya REDET ambayo mara imekuwa ikishutumiwa kwa upendeleo inapotoa taarifa za kura zake za maoni (opinion polls) kuhusu CCM na vyama vingine vya siasa.Sina hakika kuwa matokeo ya kura hizo huwa 'yanapikwa' ili kuridhisha watawala lakini kinachozua maswali dhidi ya polls hizo ni kutoendana na hali halisi na dalili za upendeleo.

Wito wangu kwa Dkt Bana ni huu: wakati mwingine jaribu kuitendea haki taaluma yako kwa kukaa kimya pale usipokuwa na cha kuongea.Kwa kufanya hivyo,utawatendea haki pia wasomi wenzako,taasisi unazoongoza na fani nzima ya usomi.Ni muhimu pia unapotoa matamshi mazito ukajitahidi kutumia theories za kusapoti matamshi hayo badala ya kutoa hisia zenye mwelekeo wa kijiweni.


.

Tanzania leads the list of East African states that have lost billions of dollars to money laundering, tax evasion, government graft and other illegal operations, according to a report by a US-based financial watchdog group.


The report “Illicit Financial Flows from Africa: Hidden Resources for Development,” by Global Financial Integrity, states that the country has lost $8.9 billion over the past four decades through the illicit means. Kenya lost $7.3 billion while Uganda lost $6.4 billion over the same period.


The three East African countries thus lost a total of $22.6 billion, money that would be sufficient to wipe out their combined outstanding external debt while leaving several billion dollars available for fighting poverty and spurring economic growth.

The study points out that the impact of these losses is felt most acutely by the poorest Africans. The illicit outflow of money also “drains hard currency reserves, heightens inflation, reduces tax collection, cancels investment and undermines free trade,” the study says.

Tanzania is ranked 13th among the top 15 countries with cumulative illicit outflows after Angola, Republic of Congo, Cameroon, Côte d’Ivoire, Ethiopia, Gabon, Ghana, Madagascar, Mozambique, Nigeria, South Africa and Sudan. Zambia and Zimbabwe take the 14th and 15th positions respectively.

Already, Global Financial Integrity has started collecting signatures to petition the G20 Transparency at the G20 summit this June. The organisation is looking for 100,000 signatures from all over the world to forward to Canadian Prime Minister Stephen Harper, the current president of the G20. “Our goal is to show him the names of 100,000 people from all over the world who support ending banking secrecy, increasing financial transparency, and finally attacking the root causes of poverty.”

The report says: “So long as illicit capital continues to haemorrhage out of poor African countries over the long term at a rapid pace, efforts to reduce poverty and boost economic growth will be thwarted as income distribution becomes ever more skewed, leading to economic and political instability.”

Tanzania’s Finance and Economy Minister Mustafa Mkulo told The EastAfrican from Dodoma that in order to reverse this situation, the country has set up a Financial Intelligence Unit within the ministry to join international community in fighting money laundering and financing of terrorism.

“This problem indeed exists. At regional level, within the East African Community and the Southern African Development Community, we have seen this problem thrive for a long time and decided to jointly act against it,” he said. (See related story, “Will electronic tax registers stem the tide of pilfering?”)

The report says that the figure for Uganda likely understates the true volume of illicit outflows. It notes that civil strife in the Great Lakes region during parts of the 1970-2008 study period resulted in “incomplete and poor quality data” for Uganda, Rwanda, Burundi and Congo.

In all cases, adds the study that encompassed all of Africa, actual losses due to systematic looting are likely to be far greater than the study estimates.

Researchers Dev Kar, a former senior economist at the International Monetary Fund, and Devon Cartwright-Smith, an economist at Global Financial Integrity, note that their figures do not take account of proceeds from smuggling and some of the ways in which trade and services are mis-priced by commercial swindlers.

The actual totals might be more than double the $22.6 billion listed in the report for the three East African countries if those other sorts of illicit outflows were included in the computations, a Global Financial Integrity spokeswoman told The EastAfrican.

Bribery and theft involving government official accounts for only a three per cent share of the money that moves across borders illicitly, the study says.

“Criminal proceeds generated through drug trafficking, racketeering, counterfeiting and more are about 30 to 35 per cent of the total,” the study adds. “The proceeds of commercial tax evasion, mainly through trade mis-pricing, are by far the largest component at some 60 to 65 per cent of the global total.”

Trade mis-invoicing, described in the report as “a significant problem for Kenya,” involves the overpricing of imports and the underpricing of exports on Customs documents, the study explains.

For Africa as a whole, total illicit outflows are said to have amounted to at least $854 billion across the 39 years encompassed in the study.

The top five countries with the highest outflow measured were: Nigeria ($89.5 billion) Egypt ($70.5 billion), Algeria ($25.7 billion), Morocco ($25 billion), and South Africa ($24.9 billion). Most of that money has gone into Western financial institutions, the study says.

“This massive flow of illicit money out of Africa is facilitated by a global shadow financial system comprising tax havens, secrecy jurisdictions, disguised corporations, anonymous trust accounts, fake foundations, trade mis-pricing and money laundering techniques,” Mr Kar and Mr Cartwright-Smith write. “The impact of this structure and the funds it shifts out of Africa is staggering.”

The researchers argue that the existing global financial system, shaped by liberalisation and deregulation of financial markets, has ended up generating ever-rising illicit flows and losses in government revenues. Economic growth without credible reform could lead to more, not less, capital flight, as the increase in incomes would simply finance the increased accumulation of foreign assets.

According to the United Nations’ Millennium Development Goals, $348 billion will be needed to cover MDG costs by 2010 and $529 billion by 2015. The United Nations report World Economic Situation and Prospects 2010 notes that a large gap still separates Africa from its MDGs.

By all accounts, official donor aid commitments will probably fall well short of the required funding of MDGs, leaving open the serious possibility that related targets will recede even further.


15 Apr 2010


Nimefarijika sana kuona mahojiano niliyofanya na msanii mahiri wa Bongoflava,Hamis Mwinjuma a.k.a Mwana FA,yamechapishwa katika tovuti ya kimataifa ya muziki wa hip-hop,
Hip-Hop-Dance.Net.Pamoja na kuwapatia wasomaji wa blogu hii nafasi ya kuwafahamu Watanzania wenzetu wanaotangaza jina la nchi yetu kwa namna moja au nyingine,dhumuni jingine la mahojiano hayo lilikuwa kutangaza vipaji vinavypatikana nchini kwetu. Japo mahojiano hayo yanaelekea kuzua mjadala mwingine ambao binafsi nautafsiri kama uhuru wa mawazo,ninaishukuru sana tovuti ya Hip-Hop-Dance kwa "kutoa shavu" kwa mahojiano hayo hasa kwa vile Mtanzania mwenzetu mmoja aliamua kuyabania licha ya kumpa ombi ayaweke "kiwanjani" kwake.Again,naamini alifanya hivyo kwa kutumia uhuru wake kuchagua nini kinastahili kuwepo hapo kwake.


Kuhusu suala la elimu ya Mwana FA,ninaomba kumtetea,sio kwa vile nilimhoji,bali kwa sababu naamini anastahili zaidi pongezi kuliko criticism.Naomba niweke wazi kuwa Mwana FA hakuomba mahojiano hayo bali ni mimi niliyemwomba (na namshukuru sana kwa kukubali ombi hilo).Pili,kama alivyosema mwenyewe,mtu haihitaji kuwa na Masters ili aweze kufanya vizuri kwenye bongoflava.Alichukua uamuzi wa kujiendeleza kimasomo kwa vile,kwa mujibu wa maeleoz yake nayoafikiana nayo,fani ya muziki (hasa wetu) haitoi mwamana wa mafanikio katika maisha.Kwa amaan nyingine,alimua kuongeza elimu yake kama hatua ya kimaendeleo mbali na mafanikio yake katika Bongoflava.

Na hata kama angekuwa anadanganya kuhusu elimu yake (which he absolutely doesn't) ingemsaidia nini wakati tayari ana jina kubwa ndani na nje ya nchi yetu?Nadhani baadhi ya wasomaji wanaomtaka "aeleze ukweli" wanapaswa kwanza "kueleza uongo wake" kabla ya kumtaka aseme "ukweli".Nasema hivyo kwa maana kama nasema jina langu ni Evarist,halafu mtu anasema hilo sio jina langu ,basi ni muhimu kwake kuthibitisha jina langu halisi ni nani.

Binafsi,kama mwanafunzi,nimekumbana na zahma kama hiyo ya Mwana FA.Nimekuwa napokea barua pepe na hata SMS za watu wanaoulizia lini namaliza shule.By the way,shule huwa haimalizwi bali mtu anahitimu hatua moja na anaweza kuendelea na hatua nyingine.Kadhalika,katika mfumo wa elimu ya juu hapa,mwanafunzi anaweza kuahirisha kozi yake pale atapoona umuhimu wa kufanya hivyo.In my case,majibu yangu kwa watu wanaoniuliza kistaarabu ni kuwa kuchelewa kumaliza kozi yangu kumesababishwa na A,B,C na kadhalika kisha nawafahamisha hatua niliyofikia.Kwa wale wanaouliza kwa minajili ya "kudhani nauhadaa umma kuhusu elimu yangu" jibu langu huwa jepesi: Mind your own damn business.

Kuna wanaojiuliza inakuwaje mtu atoke IFM na kuja kufanya Masters University of Coventry,nawasihi wafanye utafiti kidogo kwenye mfumo wa elimu ya Uingereza,na pengine hata huko nyumbani.Inawezekana kabisa kupata admission kwenye vyuo vya hapa kwa kigezo cha "sifa linganifu" (equivalent qualifications).Ni kama ambavyo baadhi ya wanafunzi wanavyojiunga na MBA pale Mzumbe au kwingineko baada ya kumaliza masomo ya stashahada kutoka IFM,Nyegezi,Ustawi wa Jamii (pale Sayansi),nk.Kwa kifupi,mifumo mingi ya elimu duniani iko so "accommodating" kwa watu wenye nia ya dhati ya kujiendeleza kitaaluma.

Nimalizie kwa kutoa shukrani kwa wote wanaoendelea kutoa mawazo yao kuhusu mahojiano hayo.Sipingani na mawazo yoyote bali huu ni mchango na mtazamo wangu binafsi (ambao pia unaweza kuwa si sahihi kwa mujibu wa mitizamo mingine).Huo ndio uhuru wa mawazo,alimradi tunatumia lugha za kiungwana na "hatutiani vidole machoni".Kwa Mwana FA,hizi ndio changamoto za Tanzania yetu.

Stay tuned for the next interview na Mtanzania mwingine anayetuwakilisha vilivyo.Can you make a wild guess?Au una pendekezo lolote?

Nimekuletea habari sita zilizopelekea nijiulize swali hilo hapo juu:TUNAELEKEA WAPI kama Taifa?Tutafakari pamoja...

Mwananchi: Polisi waibiana Sh3 bilioni za posho

Salim Said
SIRI ya kuchelewa kwa posho za askari polisi mwezi Febuari mwaka huu imefichuka baada ya kudaiwa kuwa maafisa watatu wa jeshi hilo walitoweka na hundi ya malipo hayo yanayofikia Sh3 bilioni.

Baadhi ya maofisa wa polisi waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti wiki hii, walielezea mazingira ya wizi huo na kusisitiza kuwa ngazi ya juu ya jeshi hilo imekuwa ikificha taarifa hizo, kwa hofu ya kuchafua sifa ya chombo hicho cha dola.

Wakizungumza kwa sharti la kutotajwa majina yao gazetini, walisema fedha hizo ziliibwa na maofisa hao watatu baada ya kubadili maelezo kwenye hati ya malipo na kuielekeza katika akaunti za mmoja wao.
MwananchiTanesco yapoteza umeme wa Sh 100 bilioni kwa mwaka



Sadick Mtulya
MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (Cag), Ludovick Utouh amesema kuwa upo uwezekano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kufilisika baada ya kubaini kuwa kila mwaka linakabiliwa na upotevu wa Sh 100 bilioni.
Alisema fedha hizo zinapotea wakati wa kusambaza nishati hiyo kutoka kwenye vyanzo vyake hadi kwa watumiaji.
Utouh alieleza kwenye ripoti yake, ambayo gazeti hili lina nakala yake amebaini shirika hilo limepata hasara ya Sh Sh48 bilioni mwaka uliopita kutokana na ununuzi wa umeme kutoka katika kampuni binafsi, ikiwemo IPTL kufuatia mgawo mkubwa uliojitokeza Septemba na Oktoba, mwaka jana.

Ripoti hiyo ya Cag iliyowasilishwa Aprili 6, mwaka huu katika kikao baina ya watendaji wakuu wa Tanesco na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Masharika ya Umma (Poac) kilichofanyika katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam.

Kutokana na hali hiyo, Poac iliiagiza Tanesco kuhakikisha inafanya jitihada za kujinasua katika hali hiyo.



Tanzania Daima: Mitambo jengo jipya la Bunge yakwama


na Kulwa Karedia, Dodoma

SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta, jana alilazimika kuahirisha kikao cha Bunge kwa muda wa dakika 45 kutokana na hitilafu ya mitambo ya mawasiliano ndani ya jengo hilo jipya la Bunge.
Spika Sitta alifikia hatua hiyo baada ya kuingia ukumbini, majira ya saa 2.59 na kuanza kusoma dua kama kawaida, ingawa alilazimika kukatisha tena baada ya kipaza sauti chake kutofanya kazi.

Jambo hilo lilisababisha Spika kuendesha dua kwa sauti ya chini huku baadhi ya wabunge wakipigwa na butwaa.

Habarileo: Wagombea watarajiwa wadaiwa kuhonga majeneza 

WATU kadhaa waliotangaza au kuonesha nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ukiwemo ubunge wanadaiwa kutoa rushwa yakiwemo majeneza.

Kisheria kipenga cha kuanza kampeni za kuwania urais, ubunge na udiwani hakijapulizwa na hata kampeni za ndani ya vyama hazijaruhusiwa.

Kampeni hizo haramu zimekuwa zikifanyika hadharani katika mikusanyiko ya watu inayohusu mambo ya kijamii zaidi kuliko siasa na mbaya zaidi imebainika kuwa wagombea hao wamekuwa wakivizia misiba, wakati jamii ikiomboleza kuondokewa na ndugu au jamaa, wao wanafikiria kura za waombolezaji.

Kutokana na hali hiyo ambayo imeonekana kwa wanaotangaza nia za kugombea ubunge kupitia vyama mbalimbali, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imebainisha mwishoni mwa wiki kwamba inafahamu kuwepo kwa vitendo hivyo na imeanza kuwafuatilia wanasiasa hao.

Mkurugenzi wa Idara ya Elimu kwa Umma wa Takukuru, Mary Mosha alibainisha hayo alipokuwa anatoa mada kwenye semina ya kujadili mbinu sahihi za kuripoti habari za uchaguzi mkuu, inayowashirikisha waandishi waandamizi na wahariri wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) inayochapisha magazeti ya Daily News, Sunday News, HabariLeo na HabariLeo Jumapili.

Raia Mwema: Utata mpya waibuka 'EPA namba mbili'

Mwandishi Wetu
Aprili 14, 2010
Ni fedha za stimulus package alizozitetea Kikwete bungeni
Gavana BoT aruka kiunzi, amtupia mpira msaidizi wake




SAKATA la matumizi yenye kutia shaka ya fungu la fedha lililopitishwa na Bunge kwa ajili ya kuhami uchumi, maarufu kama stimulus package , sasa limemrudia Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Beno Ndulu, ambaye baada ya baadhi ya kampuni za ununuzi wa pamba kukosa mgawo huo katika mazingira yanayozua maswali zilimtaarifu naye akawajibu kuwa Serikali haina fedha.

Hata hivyo, wakati Gavana akitoa majibu hayo kuwa “Serikali haina fedha” si fedha zote Sh. trilioni 1.7 zilizoidhinishwa na Bunge la Tanzania ndizo zilizotumika katika mpango huo wa kunusuru uchumi uliotikiswa baada ya uchumi wa dunia kuyumba.

Wiki hii Gavana Ndulu amekwepa kuzungumzia suala hilo, akidai kwamba kwa sasa linashughulikiwa na mtu maalumu chini yake anayepaswa kutafutwa kuzungumzia suala hilo.

Raia Mwema ilipozungumza na Profesa Ndulu, ambaye alieleza kuwa yuko mkoani Mwanza kwa ajili ya mkutano, alisema masuala ya ‘‘stimulus package’’ yamekabidhiwa mtu maalumu ndani ya benki hiyo, na kwamba si yeye anayeweza kuyazumngumzia.

“Haya masuala ya stimulus package tumempa mtu maalumu ambaye ni mkuu wa kitengo cha sera na utafiti, mimi siwezi kuyazungumzia,” alijibu Ndulu hata alipotakiwa kujibu yale yanayomhusu moja kwa moja katika sakata hilo pia hakuwa tayari kuzungumzia.

Uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwa fedha zilizokwishakutumika ni sehemu tu ya Sh trilioni 1.7 zilizopitishwa na Bunge, ambazo ni takriban Sh bilioni 870.8. Fedha hizo Sh bilioni 870.8 kwa mujibu wa taarifa zilizopo ndizo zilizokwishakutolewa na Benki Kuu (BoT), chombo ambacho kimepewa mamlaka ya kutoa fedha hizo.

Kwa mujibu wa utaratibu wa BoT, fedha hizo hutolewa kutoka benki hiyo kwenda katika benki ambazo zilikopesha kampuni zinazostahili kufidiwa, ambazo zimeathiriwa na mtikisiko wa uchumi duniani.
Nipashe: Sungusungu wawavua nguo walimu na kuwachapa viboko



NA ANCETH NYAHORE



14th April 2010

Walimu watatu wa kike na mke mmoja wa mwalimu wa kijiji cha Sakasaka, tarafa ya Kisesa wilayani Meatu, wamevuliwa nguo na kucharazwa viboko na walinzi wa jadi sungusungu wa kijiji hicho kwa madai ya kutohudhuria mkutano uliokuwa umeitishwa na jeshi hilo.

Imedaiwa kuwa walimu hao walishindwa kwenda kwenye mkutano huo kwa sababu ni wajawazito jambo ambalo sungusungu hao walipinga na kuwalazimisha wavue nguo kuthibitisha kama kweli ni wajawazito mbele ya mkutano huo.

Tukio hilo la aina yake na udhalilishaji kijinsia, lilitokea AprilI 7, mwaka huu kati ya saa na 4:00 na 5:00 asubuhi kijijini hapo.Katibu wa Chama cha Walimu (CWT) wa wilaya ya Meatu, Baraka Owawa, aliiambia Nipashe kuwa walimu hao walikamatwa na sungusungu hao na kuanza kuwapiga, kuwavua nguo kwa madai ya kutohudhuria mkutano.Owawa alisema walimu hao hawakuwa na jinsi yoyote ya kukabiliana na sungusungu hao bali walitii amri hiyo ya askari hao wa jadi kunusuru maisha yao.

Mara baada ya walimu hao kufanyiwa unyama huo, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Julius Mtuli, alitoa taarifa kwa uongozi wa juu wilayani hapa ikiwemo polisi na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Meatu na timu maalum kuundwa kwenda kijijini hapo kufuatilia suala hilo.

12 Apr 2010



Kama nilivyoahidi jana, leo nawaletea mahojiano maalum (exclusive interview) na msanii mahiri wa Bongoflava,Hamis Mwinjuma,almaaruf Mwana F.A.Pamoja na mambo mengine,blogu hii ilionelea umuhimu wa kufanya mahojiano na msanii huyo kwa sababu kuu mbili.Kwanza,yayumkinika kum-describe MwanaFA kama mmoja wa wasanii wenye elimu ya hali ya juu baada ya kuhitimu masomo yake hapa Uingereza.Pili,ilitarajiwa kwamba kwa kuwa kwake nje ya nchi kwa muda mrefu kimasomo atakuwa katika nafasi nzuri ya kutupa mwanga kuhusu nafasi ya bongoflava ndani na nje ya Tanzania.Basi nisimalize ladha bali tiririka na mahojianio hayo hapa chini. 









KULIKONI UGHAIBUNI (K.U.):Kwanza,blogu hii inatoa shukrani kwa kukubali ombi la kufanya mahojiano nawe.Pili ni pongezi kwa kuhitimu masomo yako ya Shahada ya Uzamili nchini Uingereza.


Umekuwa ukifahamika zaidi kwa jina la Mwanafalsafa,na wakati mwingine Binamu.Je nini asili au maana ya majina hayo?


MwanaF.A: Nashukuru ndugu yangu.



Mwanafalsafa nilipewa na producer wangu wa kwanza,Dj Boniluv..nilikuwa na wimbo unaitwa ‘mwanafalsafa’(upo kwenye album yangu ya kwanza) na Boni akadhani itakuwa busara nikilitumia jina hilo sababu ya aina ya uandishi wa mashairi nnaoufanya(kujaribu kuzungumzia vitu kwa uzito)..Binamu lilikuja baadae,na linaelezea mahusiano yangu na hadhira nnayoongea nayo,kwamba nawaambia watu vitu ambavyo kaka na dada zao wangeshindwa kuwaambia,pengine sababu ya heshima za kindugu walizonazo,lakini mimi kwa ukaribu na urafiki wa ki’binamu naweza kuwawasilishia.




K.U:Ukiwa mmoja wa wasanii wakongwe wa bongoflava,je ni kipi kinachokuwezesha kubaki kwenye form kwa muda mrefu kiasi hiki?


MwanaF.A:ah,kitu cha kwanza najua nimekuwa mwenye bahati,na namshukuru Mungu kwa hilo..sababu naamini kuna wengi walikuwa na vipawa vya kuweza kubaki lakini hawapo kwa sababu moja ama nyingine..huwa najaribu kusema vitu watu wanavyotaka kuvisikia,na pengine hawakuvitegemea,natafuta namna ya kuzunguka na ideas na kuzijengea hoja..then kilichobaki ni siasa za mziki.

K.U:Tuje kwenye maisha yako nje ya Tanzania.Kama msanii unaonaje nafasi ya bongoflava kwenye anga za kimataifa?:


MwanaF.A:sio kubwa kwa kweli,ina safari ndefu SANA..kuna mambo ambayo kimsingi tunatakiwa kuanza kwa kuyakubali kwanza,mathalani mipaka ya lugha..hili sio suala dogo,na nasema hivyo sababu ili kufanya vizuri nyumbani itakubidi kufanya kwa Kiswahili,ambapo nje ya nyumbani ni shida kukivusha..ubora wa mziki wetu na kukosa kwake uhalisi(kuna hiphop,r&b,afro pop,zouk,kwaito,lingala nk kwenye bongo flava) vinaiweka kwenye hali ngumu sana wakati wa kuutafutia nafasi.Pengine,tungeanza kwa kufanyia kazi vitu viwili hivi,lugha na uhalisi.







K.U: Je katika kipindi ulichokuwa nje ya Tanzania ulifanya kazi zozote za kisanii kushirikiana na wasanii wa nje au una mpango wa aina hiyo?:


MwanaF.A:sikuweza kwa kweli..nilikaribia kufanya kazi na producer Amit,lakini ratiba zangu na zake zikawa zinapishana mno so sikuweza tena..nna mpango wa kufanya kazi na wasanii wan je ndio lakini bado naifikiria Africa kwanza..so nawaza Nigeria na South Africa kwa kuanzia.




K.U: Umaarufu unaambatana na usumbufu.Je wakati uko masomoni Uingereza,ulimudu vipi kukabiliana na hali hiyo (i.e. muingiliano wa umaarufu wako katika masomo yako)?


MwanaF.A:nimekuwa nikisoma kwa muda sasa wakati najulikana julikana na watu(siuiti umaarufu)..see,nimekuwa nafanya mziki wa kusikika na kuonekana kwa takriban miaka 9 sasa na nimezoea kukabiliana na vikwazo nnapotaka langu liwe..nilisoma IFM kwa miaka kadhaa na bado niliweza kukabana na mazingira ya kujulikana na shule,so nje ilikuwa rahisi zaidi,sababu watu wachache zaidi wananijua kulingana na nyumbani.

K.U: Ni dhahiri kuwa kutokana na kiwango chako cha juu kitaaluma,utakabiliwa na majukumu mengine kama kikazi,nk.Je unataraji kubalansi vipi maisha yako kama msanii na majukumu mengine ya kimaisha (mfano kikazi)?:


MwanaF.A:kwa kuanzia nimempa AY majukumu ya kusimamia sehemu kubwa ya kazi zangu za mziki ili nipate nafasi ya kumudu kufanya mambo mengine kwa kuwa yeye ana kampuni inayojihusisha na masuala ya mziki(Unity Entertainment)..hii inanibakisha na kufanya mziki na shows tu ambapo ni maisha niliyoyazoea..bado naendelea kufikiri namna bora zaidi ya kutogonganisha majukumu..najaribu kutoweka mipaka kwenye idadi ya vitu nnavyoweza kuvifanya,napigana na haya maisha na najaribu kunyoosha mambo kwa kadri nnavyoweza.





K.U:Je unadhani hatua uliyopiga kitaaluma inaweza kuzaa matarajio mapya kwa washabiki wako hususan kwenye ujumbe uliomo kwenye tungo zako?


MwanaF.A:yeah,naishi najifunza..kila hatua ya maisha nnayopitia ni somo kwangu na nadhamiria kuwaambia watu wangu vingi nnavyojifunza..so hata hatua za kitaaluma nnazopiga zinaniongeza uelewa wa vitu na nimepanga kushiriki na hadhira yangu,sio kwa namna ya kishule,bali kwa namna ambayo mitaa itaelewana nayo.








K.U:Swali linaloshabihiana na hilo lililotangulia.Je kwa hatua uliyopiga kitaaluma,jamii itarajie mtazamo mpya kwenye tungo zako?


MwanaF.A:jibu lake ni exactly kama lililopita.


Nnachoweza kuking’arisha hapa ni kuwa sitaki kuchanganya sana shule yangu na huu mziki isipokuwa kwenye namna ya biashara na vitu vichache vitakavyohitaji mawili matatu nnayojifunza kila kukicha...huhitaji masters degree kutengeza mziki mzuri....huu ni wa mtaa na ntaendelea kuufanya kwa ajili ya mitaa,kama unanielewa vizuri..mara nyingi nyumbani unaweza kuhukumiwa kwa kujua.



K.U:Kama msanii msomi kabisa una ushauri gani kwa wasanii wengine kuhusu suala la kujiendeleza kielimu?


MwanaF.A:namna pekee ya kuliangalia hili kwa wasanii ni kuwa,tusiache maisha yetu yakawa sehemu ya mziki tunaoufanya,bali mziki wetu uwe sehemu ya maisha tunayoishi..niliamua kurudi shule sababu nilikuwa nataka kubaki kuwa mtoto wa mama Hamis,na kwa kufanya kile ambacho ningekifanya kama nisingekuwa mwanamuziki...mziki,HASA HUU WETU, una siasa nyingi na hautoi ahadi ya kukupa uwezo wa kuyamudu maisha yako yote yaliyobaki na familia yako,hivyo ni busara kuwa na mipango ya ziada.





K.U: Kwa uzoefu wako baada ya kuwa nje ya Tanzania kwa muda mrefu,una ushauri gani kwa wasanii wenzio kuhusu uwezekano wao kuvusha kazi zao za sanaa nje ya mipaka ya Tanzania?




MwanaF.A:ni kama nilishajibu na hili mkuu..tunapaswa kuondoka kwenye denial state kwanza..tukubali kuufanyia marekebisho ya kimsingi mziki wetu then tukimbizane na chochoro za kuuvusha..vinginevyo tutaendelea kuimbia wa’Tz 200-300 kwenye maonyesho yetu ya nje kila wakati.




K.U: Mwisho,una ujumbe gani kwa mashabiki wako.Je wategemee vitu vipya hivi karibuni?


MwanaF.A:yeah,maskio yakae wazi..nawadondokea punde tu.








Blogu hii inakutakia kila la heri katika shughuli zako.


MwanaFA: Ahsante sana,nashukuru..na pole kwa kuchukua muda mwingi kujibu..mbio za maisha tena..na naamini wewe na watembeleaji wa blogu mtanielewa.


.

11 Apr 2010

Kama nilivyoahidi awali,blogu yako itakuwa ikikuletea mahojiano na Watanzania 'wanaowakilisha' (representing) nchi yetu kwa namna moja au nyingine.Na sasa nafurahi kukujulisha kuwa blogu imekamilisha mahojiano na supastaa big name wa bongoflava.Could you make a guess?Hint: Ni msanii mwenye kipaji cha hali ya juu katika kupangilia verses na lyrics zake,sambamba na uwezo mkubwa wa 'kucheza na maneno' na kwa sasa ni mwana bongofleva mwenye elimu ya kiwango cha juu kabisa. Na hapa chini (video) inakupa hint zkubwa zaidi.
Mahojiano kamili yatawekwa hapa kesho katika versions mbili:Kiingereza na Kiswahili.USIKOSE

10 Apr 2010

Kama Mtanzania mzalendo na mwenye kupenda nchi yangu nawajibika kuwa na heshima kubwa kwa Rais wangu Jakaya Kikwete.Hata hivyo,heshima inapaswa kuendana na matendo ya mheshimiwa.Kwa maana hiyo,naamini simkosei heshima Rais wangu nikihoji baadhi ya busara zake.Mpaka muda huu sielewi nini kinaendelea kati ya JK,Husna Mwilima na Sophia Simba!Awali,Sophia Simba kama Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM alisimama kidete kuhakikisha Mwilima 'anapigwa chini'.Tuhuma zilizotolewa dhidi yake ni 'mapungufu katika utendaji wake wa kazi.'Sasa kama tukiamini kuwa ni kweli Mwilima alishindwa kumudu majukumu ya uongozi huko UWT,how come JK ameamua kumpa ukuu wa Wilaya? Na kwa kuonyesha kuwa mambo yanaendeshwa kienyeji,Mwilima hakuchelewa 'kutoa mipasho kwa wabaya wake' pale alipotamka bayana kuwa kuteuliwa kwake na JK kuwa DC wa Tandahimba ni 'majibu ya JK kwa akina Sophia Simba'.Huwezi kumlaumu kuwa 'ameropoka' kwa vile hakujiteua.

Lakini swali la msingi ni kwamba je ni kweli JK ameamua kumteua Mwilima kumwonyesha Sophia Simba na UWT yake kuwa mwanamama huyo (Mwilima)aliondolewa katika wadhifa wake huko UWT kwa mizengwe na si mapungufu ya utendaji kazi?Lakini kama jibu la swali hilo ni ndio,hivi JK si ndio Mwenyekiti wa CCM ambayo UWT ni jumuiya yake,na kwa maana hiyo alikuwa na uwezo wa kusimamia mtizamo wake kuwa Mwilima ni mtendaji kazi hodari?Kwanini aliacha mwanamama huyo adhalilishwe huko UWT kabla ya kuamua 'kumsafisha' kwa kumpa u-DC?

Katika picha kubwa zaidi,je inawezekana utoaji wa baadhi ya vyeo unafanyika sio kwa maslahi ya wananchi bali kusafishana na 'kupunguza maumivu ya kisiasa'?Nauliza hivyo kwa vile naamini kwamba kama Mwilima alikuwa ameonewa huko UWT,JK alikuwa na uwezo mkubwa wa 'kumlinda' kama alivyoamua 'kumlinda sasa' kwa kumpa u-DC.Kwa kukaa kwake kimya wakati Mwilima 'anapelekeshwa' huko UWT,inatafsiriwa kuwa alikuwa anaafikiana na maamuzi ya akina Sophia Simba.Lakini kwa uamuzi huu 'mpya' wa kumpa Mwilima u-DC,inatafsiriwa (kama anavyosema Mwilima) kuwa anafikisha ujumbe kwa akina Sophia Simba kuwa Mwilima 'alionewa tu huko UWT kwani bado ana sifa za kuongoza wananchi huko Tandahimba kama DC'!

Nilisema mwanzoni kuwa namheshimu Rais wangu JK lakini nadhani aidha ana washauri wabovu au yeye mwenyewe maamuzi yake ni dhaifu.Na bahati yake ni kwamba Watanzania wengi hawana muda wa kuhoji au 'kukomalia' baadhi ya maamuzi yake.Ni aibu kwa Rais wetu kugeuka sehemu ya mipasho ya akinamama hao (Mwilima na Sophia Simba).Ni dhahiri kinachofanyika hapo ni kupoza pande zote mbili,yaani JK kama Mwenyekiti wa Taifa wa CCM aliamua kukaa kimya pale Sophia Simba na wenzake walipomtimua Mwilima,lakini katika kumpoza Mwilima akaamua kumpatia 'zawadi' ya u-DC.

Halafu kwa mtindo huu tutarajie Maisha Bora kwa Kila Mtanzania?

9 Apr 2010

Yea,I know,it's none of my business but,man,this story left me quite perplexed.Lots of stuff's already been said about what you might call 'the foreign arms of our ruling party CCM.And much of it isn't funny to read,but I personally don't have any issues with people exercising their democratic rights by forming or joining 'matawi ya CCM nje ya Tanzania'.However,as I once wrote,these branches and their members could surely be so instrumental in reforming the old party especially at times when it's perceived by many as the godfather of 'ufisadi'.Our bothers and sisters in the form of 'wanachama wa CCM nje ya nchi' could use their foreign experience to make CCM return to its root as a party of peasants and workers instead of leaving it being hijacked by and put in control of some unscrupulous tycoons (mafisadi). All I could ask our CCM friends in Russia is to settle their differences amicably and avoid tarnishing their party's and own images by the on-going infighting.I sincerely understand that this is a private party affair but wisdom could easily prevail by keeping this matter private instead of making it public.That's,however, not suggesting that the Moscow Branch of CCM should not make use of the web to keep the public informed of whatever they are up to.We have had enough of the thuggery of our local politics,and surely we wouldn't wish to see the same be replicated in the party's 'overseas branches'.The best thing to do with private problems is to see them stay private

A discovery about the way HIV attacks the immune system could pave the way for the development of new treatments. Researchers have identified a new method in which the human immunodeficiency virus, which causes Aids, is able to prevent tetherin - a protein found naturally in human cells - from doing its job of blocking the invaders.

This highly-skilled study has been carried out by a team based in Montreal in Canada.

The hope now is that this information will help scientists to target certain aspects of the virus and therefore develop new anti-HIV drugs.

At the moment, there is no way of knowing how much of a difference this discovery will make to HIV therapy and any such developments could take decades.

Almost 33 million people around the world are thought to be living with HIV and AIDS.

SOURCE: ITN

JK alisaini sheria hiyo kwa mbwembe kama alivyoahidi.Siku chache baadaye,Dkt Wilboard Slaa akaibua hoja kuhusu 'usanii' uliofanyika kuongeza vipengere katika Sheria hiyo.Spika na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakatetea 'usanii' huo.Licha ya mlolongo wa matukio hayo kuashiria kuwa sheria hii yenye nia njema itabaki kuwa maandishi tu,walengwa wakuu wa sheria hiyo wameamua kuipuuza na 'misaada' inatolewa kama kawaida katika kujitengenezea mazingira ya ushindi kwenye uchaguzi. Dk. Nkya kujitosa ubunge Morogoro Kusini Mashariki

na Joseph Malembeka, Morogoro

NAIBU Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Lucy Nkya, ametangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo la Morogoro Kusini Mashariki.
Dk. Nkya alitangaza nia hiyo akiwa katika ziara ya kukagua maenndeleo na utekelezaji wa ahadi alizotoa baada ya kuchanguliwa kuwa mbunge wa Viti Maalum.

“Nawatakeni wanachama wenzangu ndani ya CCM muelewe kuwa na mimi nakuja huku mbali na kuwa kuna wenzangu waliotangaza nia hii,” alisema Dk.Nkya.

Dk. Nkya ambaye kwa nyakati tofauti alikabidhi vitu mbalimbali yakiwemo mabati, vipaza sauti, saruji, vyerehani, misumari, baiskeli na fedha taslimu sh 1,500,000 kwa wananchi na wana CCM katika kata mbalimbali aliwataka wana CCM kukiimarisha chama na wao kiuchumi.

“Sasa hivi tunakwenda kwenye hekaheka za uchaguzi ila nawatakeni mbali na siasa jiimarisheni kiuchumi kwa kulima mazao yanayokomaa kwa muda mfupi na yanayostahimili ukame tuepukane na janga la njaa,” alitahadharisha Dk. Nkya.

Dk. Lucy Nkya anakuwa miongoni mwa watu saba walioonyesha nia ya kuwania ubunge katika jimbo hilo. Wengine ni mbunge wa sasa wa jimbo hilo (Samir Lotto), Jamira Mohamed, Amani Mwenigoha, Gabriel Mkwawe, Semindu Pawa na Salumu Salum Mkangala.

CHANZO: Tanzania Daima.

Takriban nusu karne tangu tupate uhuru tunakutana na takwimu zinazopaswa kuchochea mjadala wa umuhimu wa kumuondoa mkoloni.Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi,zaidi ya asilimia 90 ya uchumi wa Tanzania unamilikiwa na wageni.Kwa bahati mbaya (au makusudi) habari hiyo haikuingia kwa undani kujadili impacts zinazosababishwa na hali hiyo lakini kilicho wazi ni kwamba uhuru wetu uko mashakani.Katika zama hizi ambapo nguvu za kiuchumi zina athari kubwa kwenye siasa,ni dhahiri kuwa hata huo uhuru wetu wa kisiasa unabaki kuwa wa kinadharia zaidi kuliko uhalisia..Habari husika ni hii hapa
Na Ramadhan Semtawa
ZAIDI ya asilimia 90 ya uchumi wa Tanzania unaendelea kumilikiwa watu wenye asili ya Asia na Ulaya, takwimu zinaonyesha.

Takwimu hizo zimetolewa huku kukiwa na kilio kikubwa cha Watanzania wazawa, kutaka wajengewe mazingira mazuri ya uwezeshaji ili kumiliki uchumi wa nchi kupitia migodi mikubwa ya madini na maeneo nyeti ya kiuchumi.

Lakini wakati kilio hicho kikiwa hakijapata ufumbuzi, Taarifa ya Utendaji ya Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, iliyowasilishwa katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi jana, ilisema watu wenye asili ya mabara ya nje wanaomiliki uchumi wa Tanzania ni sawa na asilimia moja ya Watanzania.

Takwimu hizo zilifafanua kwamba, asilimia hiyo 90 ya uchumi wa nchi umeshikwa na watu wenye asili ya Asia na Ulaya, wakati asilimia 99 ya Watanzania wazawa, hawana kitu.

Kwa mujibu wa takwimu hizo zilizowasilishwa katika kikao hicho kilichohudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Omar Yusuph Mzee, tatizo la Watanzania weupe kumiliki uchumi, lilianza tangu wakati wa ukoloni.

"Wakati wa enzi za ukoloni na hata baada ya uhuru Watanzania wengi hawakuwa wakishiriki kikamilifu katika kumiliki uchumi wa nchi yao. Uchumi wa nchi umeendelea kutawaliwa na wageni wakishirikiana na Watanzania wachache," inasema sehemu ya ripoti hiyo.

Ripoti hiyo inasema "asilimia 99 ya wananchi ni Watanzania weusi na asilimia 1 iliyobaki inajumuisha Waasia na Wazungu ambao wana miliki zaidi ya asilimia 90 ya uchumi wa nchi hii (Msambichaka, 2008).

"Hii ina maana asilimia 99 ya Watanzania halisi wanamiliki asilimia 10 tu ya uchumi wa taifa lao," inasisitiza ripoti.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali za kurekebisha kasoro zilizoko, ikiwa ni pamoja na kuanzisha (lililokuwa) Azimio la Arusha, Vijiji vya Ujamaa, Elimu ya Kujitegemea, Serikali za Mitaa, Vyama vya Ushirika, Sera ya Uwekezaji na Sera ya Ubinafsishaji wa Mashirika ya Umma.

Inasema hata hivyo,juhudi hizo hazijazaa matunda yaliyotarajiwa na kwamba na kwamba kushindikana kwa juhudi za kuwawezesha Watanzania kushiriki kikamilifu katika kujenga uchumi wa nchi yao, ndilo chimbuko la kubuniwa kwa mkakati wa kuwawezesha wananchi kiuchumi, katika ilani ya CCM ya mwaka 2000."

CHANZO: Mwananchi

5 Apr 2010

Ukifuatilia kwa karibu namna nchi yetu ilivyogeuzwa 'shamba la bibi' unaweza kupata shinikizo la damu siku si zako.However,shinikizo la damu or not,tutaendelea kufahamishana namna ufisadi unavyoiteketeza nchi kwa kasi,ari na nguvu kubwa.Na haya yanatokea wakati kuna watu wanalipwa mishahara kuhakikisha hayatokei. Nimekutana na habari moja kwenye gazeti la Mwananchi ikieleza kwamba Jeshi la Magereza limekumbwa na kashfa ya ufisadi wa shilingi milioni 300.Ufisadi huo umewekwa hadharani na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kwa Kamati Ya Bunge ya Hesabu za Serikali.Yaani taasisi iliyopewa jukumu la kuwahifadhi na kuwarekebisha tabia wafungwa nayo inafanya yaleyale yaliyopelekea wengi wa wafungwa kuwa jela in the first place.Well,namaanisha wale waliofanya uhalifu lakini hawakuwa na majina ya kuwalinda au hawakuwa na uwezo wa kuhonga ili kesi zao zife kienyeji.

Kichekesho ni kwamba wezi wa mamilioni hayo walifikishwa mahakamani (pengine katika kutuzuga kuwa sheria inachukua mkondo wake) lakini wakaachiwa huru katika kile kinachofahamika kisheria kama want of prosecution.Kichekesho kingine ni kwamba licha ufisadi huo,Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi imelipa jeshi la magareza 'hati safi'.Yani ni kama wanapongwezwa kwa kuiba mamilioni badala ya mabilioni kaka wenzao huko Benki Kuu,TRA,nk.Na kikubwa zaidi ya kichekesho ni kauli ya Mbunge Mudhihir Mudhihir,ambaye ni mjumbe wa Kamati hiyo ya Bunge,kwamba "Pamoja na kwamba mna hati safi, lakini upotevu huu wa fedha unasikitisha sana..."Hivi kusikitika sana kunasaidia nini?Kwanini badala ya kupoteza muda kusikitika,Mbunge huyo na Kamati yake wakaagiza hatua zaidi za kisheria?Rais anasikitika,mawaziri wanasikitika,wabunge wanasikitika!Yani utadhani kwa kusikitika kwao mafisadi watapatwa na huruma na kusitisha ujambazi wao.

Well,makala hii inauliza Mdhibiti na Mkaguzi wa nini nikimaanisha ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali inavyofanya kazi ya kujaza maji kwenye gunia.Ikumbukwe kuwa uandaaji wa ripoti za ofisi hiyo unahisisha matumizi ya fedha za walipakodi.Kinachokasirisha ni ukweli kwamba taarifa za ofisi hiyo zimeendelea kuwa kama utaratibu tu wa kusukuma siku kwani wenye mamlaka ya kuzifanyia kazi hawaonekani kuguswa kwa namna yoyote na wingi wa tarakimu katika fedha zilizofisadiwa.

Picha hapo juu inamwonyesha Rais Kikwete akipokea ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu,Ludovic Utouh.Unaweza kupata matumaini kuwa labda ripoti hiyoi inaweza kufanyiwa kazi mwaka huu kwa vile kuna uchaguzi,au kwa vile CCJ imezaliwa...kalagabaho,huo ni utaratibu tu.Utouh katimiza wajibu wake,na JK nae katimiza wajibu wake wa kupokea taarifa,na kupigwa picha inayoashiria kuwa tuna Tanzania ina uongozi unaoguswa sana na matumizi ya fedha za umma!

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.