16 Oct 2009


NDUGU YANGU Mpayukaji Msemaovyo anasema:

Naitwa Mchumiatumbo mwana wa Tapeli.

Ingawa wakati naandika waraka huu vijana wenzangu wapatao 166 wamo wakimenyeka toka Mwanza hadi Butiama, kama ishara ya kumbukizi ya safari yako adhimu ya ukombozi ukiliungua mkono marehemu azimio la Arusha, mimi sitafanya hivyo.

Nina sababu. Kwanza mimi ni mnafiki wala mjamaa kama wewe. Nina roho nyepesi hasa nionapo vitu kama pesa madaraka na sifa.

Mimi ni mbabaishaji na muongo; au msanii kama washikaji wasemavyo. Ni fisadi through and through. Ninanuka kiasi cha kutostahili hata kukaribia kaburi lako achia mbali nyumba yako, wanao, mkeo, watu wako hata taifa lako. Nisingependa walevi na wazinzi kufagia makaburi ya mitume mwalimu. Hivyo, kwanza nakuwa mkweli kwa nafsi yangu na kwako na umma wako.

Tatu, nitaunga mkono azimio lipi iwapo ninaoona wamenizunguka wakiwaibia watu wako ni wale wale walioliua azimio la Arusha? Nitaadhimisha vipi iwapo miiko ya uongozi na usawa wa binadamu vimetoweka na nafasi yake kuchukuliwa na ufisadi, ujambazi wa mchana, ubabaishaji na uongo?

Nne, mwalimu, sitaki kujidanganya na kukudanganya. Kile ulichopigania kwa sasa hakuna. Ulipigania uhuru na maendeleo. Sasa kuna utumwa na kuporomoka. Ulitekeleza ujamaa na kujitegemea. Sasa tuna uhujumaa na kujimegea. Ulipigania mstakabali wa nchi toka kwa wakoloni wawe wavumbuzi, wamisionari na watawala. Sasa mstakabali huo umo mikononi mwa wawekezaji, na wafadhili wa makuadi wao. Ulipigania ardhi ya Tanzania kabla haijaingia mikononi mwa vijifalme vya kifamilia. Nitakuenzi kwa udhu upi iwapo kila nipitapo Loliondo nakaribishwa kwenye falme za kiarabu utadhani hapa ni uarabuni?

Nitapata wapi mshipa wa kukuenzi wakati nakung’ong’a? Je mwalimu una habari? Yale madini uliyosema vizazi vijavyo vingeyaendeleza na kufaidika nayo yaliuzwa na jamaa yako Tunituni uliyempigia debe usijue jizi.

Tano, mwalimu siwezi kukuenzi wakati nakuchukia na kukudharau. Ningekupenda na kukuheshimu ningeshika urithi wako na kuheshimu wosia wako wa kupendana na kutohujumiana. Nakumbuka wakati ukianga dunia ulikuwa ukiwalilia watanzania wako baada ya kugundua makosa uliyofanya kuwaweka mikononi mwa nunda wala watu. Nami ni mmojawapo.

Je una habari mkoani mwako watu wameishamiminiwa risasi za moto kutokana na kukatiza kwenye ardhi ya mwekezaji na si mtanzania? Una habari mkoani mwako uchafuzi wa mazingira unatishia maisha ya ndugu zako? Hapa kweli nina sababu ya kukuenzi? Je kukuenzi ni matendo au maneno mwalimu?

Ingawa ukiwa kuzimu bado unaliletea sifa taifa langu, sifichi wala kuchelea kukwambia kuwa waliohai wanaliletea aibu na fedheha baada ya kulibinafsisha huku wakibinafsisha hata akili na roho zao. Mwalimu nilikufahamu sana . Ulikaa madarakani kwa kitambo kirefu ukiacha nyuma familia isiyo na ukwasi zaidi ya utu. Uliowawezesha wamefikia hata kuchukua ule mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira uliozawadiwa na rafiki yako Mao Tse Tung.

Mwalimu, vinyamna mwitu na mbwa hawa walitutenda kweli. Walitudanganya kuwa uwekezaji ndiyo sera na njia pekee ya kutukomboa tusijue walikuwa wakimaanisha kinyume. Wengine walituahidi maisha bora kwa wote tusijue wote ni wao washirika zao, watoto zao na wake zao hata nyumba ndogo zao. Tupo msambweni mwalimu wakati huu tunapozidi kuuzana na kuhadaana. Je unaweza kuamini kuwa kwa sasa hakuna tofauti ya polisi na kibaka? Nina ushahidi. Juzi polisi aliuawa kama kibaka na wananchi wenye hasira na kukata tamaa huku polisi tena wakubwa wakiwapiga risasi wafanyabiashara wakidai ni vibaka!

Wakati wa uongozi wako matupinkele au zeruzeru kwa lugha rahisi walikuwa salama. Baada ya kuingia pepo la utajiri usioulizwa ulivyopatikana, maskini hawa wanatolewa kafara na wanganga njaa wa kienyeji. Hivyo ndugu zetu hawa wanauawa hata zaidi ya swala mwalimu na hawana mtetezi zaidi ya vijikesi viwili vitatu vya kuondolea lawama. Tembo kwa sasa wana ulinzi madhubuti zaidi ya ndugu hawa.

Zama zako uliongoza. Uongozi ulikuwa utumishi wa umma na si uchumia tumbo na utumikishaji na uhujumu wa umma. Ikulu ilikuwa mahali patakatifu siyo pa deal. Uongozi ulikuwa uongozi na si uongo kama sasa. Siasa ilikuwa baraka si balaa kama sasa.

Wale watoto wa wachunga mbuzi na maskini wa kunuka uliowatoa kwenye umaskini na kuwasomesha sasa ni matajiri wa kutupwa. Yupo mpumbavu mmoja jizi aliyewahi kuita shilingi bilioni moja vijisenti ukiachia mbali wengine uliowaachia laana kuwa walikuwa wamejilimbikizia chumo la wizi. Na kweli maneno yako hayakuanguka. Kwani wezi wenzao waliwabeba na kuwakweza hatimaye tamaa zao na upofu vikawadondosha.

Mwalimu sitakuenzi,. Siwezi kujidanganya na kuidanganya dunia. Nitakuenzije iwapo kipato changu kinatokana na rushwa, uwekezaji, uuzaji mihadarati, uongo, ahadi hewa, uhujumu na mengine mengi yapinganayo na dhamira ya dira yako mwalimu?

Hivi kweli panya anaweza kumuenzi paka zaidi ya kufaidi ‘uhuru’ baada ya paka kuondoka? Je nune aweza kuishi nje ya kinyesi cha ng’ombe zizini? Si haki nune kuwa mwalimu wa usafi wakati mlo wake na makazi yake ni kwenye uchafu hata anenepe na kunawiri vipi.

Mwalimu naogopa kuja Butiama au kusimama mbele ya kadamnasi ya maadhimisho yako na kukupamba wakati nilisha kuvua nguo. Naogopa. Maana mama Maria hata wanao wananijua. Inawezekana nikakulamba uchogo na kukupaka mafuta kwa mgongo wa chupa kiasi cha kumkera mmojawapo akaamua kunizodoa na nikazidi kudhalilika ingawa niliishadhalilika muda mrefu.

Mwalimu ulikuwa na akili inayochemka. Yangu mimi ni bongolala. Ulikuwa msafi na mwadilifu. Mie ni mchafu sina mfano. Mkeo hakuwa akitumia ofisi yako kuubia umma. Mie wangu nami wote tu wezi. Nikiiba huku yeye anaibia kule. Hata watoto nimewaingiza. Nataka hata ikibidi wawe marais kama siyo mawaziri. Je hapa mwalimu nitakuwa na cha kukuenzi?

Mwalimu ulileta elimu bure kwa wote. Mie nashabikia kuchangia gharama ingawa kimsingi hakuna gharama za kuchangia zaidi ya kutunisha mfuko wa walaji wakubwa. Ulipigania ardhi. Mie natamani niwe rais niiuzie mbali nipate changu nifiche ughaibuni. Mwalimu ulichukia wafanya biashara wezi. Mie hawa ndiyo washitili wangu.

Mwalimu ulisisitiza usawa wa binadamu. Mie naamini binadamu si sawa wala si mfano wa Mungu kama wachungaji wasemavyo. Usawa ni mambo ya kizamani. Kwangu, heshima ya binadamu haitokani na ubinadamu wake bali pochi lake. Hukusikia wahenga wakisema mwalimu kuwa aso kitu si mtu bali kinyama mwitu? Mtu chake bwana. Kwa imani yangu mie si mfano wa Mungu bali mfano wa shetani kutokana na uroho na roho mbaya vyangu. Mungu si mwizi wala muongo wala mbabaishaji kama mimi mwalimu.

14 Oct 2009


Na Fredy Azzah

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, amesema kashfa za ufisadi zinazowakabili baadhi ya viongozi wake, zimekiumbua chama hicho pamoja na serikali yake.

Akiwahutubia wanafunzi wa matawi ya CCM ya vyuo vikuu vilivyopo jijini Dar es Salaam, wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere jana, alisema ufisadi ambao umewakumba wengi umesababishwa na tabia ya viongozi kulindana na kutosimamia kikamilifu maadili ya uongozi yaliyoainishwa ndani ya katiba ya CCM.

Alisisitiza kuwa tabia hiyo ni kinyume na misingi ambayo Baba wa Taifa, aliwaachia Watanzania....ENDELEA

WAKATI HUOHUO

WASOMI na wanazuoni nchini, wamesema nchi haina dira na kwamba kuna mpasuko mkubwa ambao usiposhughulikiwa mapema, nchi inaweza kuingia kwenye machafuko.

Wakizungumza juzi katika baraza lililopewa jina la Mbongi, lililoandaliwa na Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Julius Nyerere, walisema mpasuko hiyo ni pamoja na ya udini, ukabila, ukanda, matatizo ya vitambulisho Zanzibar pamoja na hofu ya kuvunjika muungano...ENDELEA

CHANZO: Mwananchi


Police recoup £1.4m from criminals in last two weeks as war on crime profits gathers pace



Oct 12 2009 by Rebekah Oruye, Birmingham Mail



WEST Midlands Police is driving home the message that crime does not pay after confiscating £1.4 million from criminals in the past two weeks.

In addition, nearly £100,000 in cash was seized from a car on the M6 in Birmingham, believed to have been intended for criminal use.

Det Chief Insp Simon Wallis, head of the force’s economic crime team, said: “This money has been taken from those who think crime is an easy way to make money.

“It brings West Midlands Police to a total of £15 million seized from criminals in the last 18 months.

“On many of these occasions through financial investigation and the confiscation process we are able to trace monies and give them back to victims. In cases where money is transferred abroad, it still is able to be retrieved. Crime does not pay. We will investigate those involved in criminality to ensure that they do not enjoy their ill gotten gains.”

Among the success stories for the police is the near £900,000 seized from Walsall conman Mponjoli Malakasuka, who had been stealing and exporting high powered luxury cars.

Malakasuka, aged 36, from the Yew Tree estate, was ordered to pay back the money in one month or face an additional four years in jail. He was originally sentenced to three-and-a-half years in July 2008 for conspiracy to steal.

Malakasuka had used a variety of sophisticated methods to steal prestige vehicles which he then exported out of the UK to Tanzania and Kenya. The cars were stolen both through car key burglaries and a variety of identity fraud and fake hire purchase agreements.

The cars included Mercedes Benz S320 CDi and Porsche Cayenne cars. In all over £300,000-worth of vehicles were stolen.

At the time of his arrest police discovered Malakasuka to be living a life of luxury in his four-bed house. At his address were pictures of luxury houses in Tanzania into which officers believed he had invested his fraudulent cash.

The court accepted the houses in Tanzania were proceeds of his criminality. Financial investigators were also able to show thousands of pounds passing through in excess of 70 bank accounts in the UK and Tanzania including one account which alone had £350,000. Det Sgt Jonathan Jones, who led the investigation for the Economic Crime Team, said: “This has been a great investigation, as not only have we stopped fraud and theft, but we have now recovered the profit that this man made from his criminality.”

In a separate case a money launderer from Birmingham was ordered to pay back more than £450,000 of his criminal profit.

Barrington Fulcott, aged 48, from Kingstanding, was told to pay £450,386 at the hearing in Birmingham Crown Court.

He was given six months to return the cash, or face an extra four years in prison. Fulcott was originally sentenced to 42 months in prison in February 2008 in relation to three counts of money laundering.

He had gathered considerable wealth from his criminal activity which had allowed him to purchase five properties in the West Midlands and begin the development of a large home in St Annes, Jamaica.


13 Oct 2009


WAKATI TUNAADHIMISHA KIFO CHA MWASISI WA TAIFA LA TANZANIA,MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE,TUNAPASWA PIA KUTAFAKARI MAMBO KADHAA AMBAYO KWA KIASI KIKUBWA HAYAKUPATA FURSA YA KUJADILIWA WAKATI WA UHAI WA NYERERE,NA KUYAJADILI BAADA YA KIFO CHAKE INAWEZA KUTOA TAFSIRI POTOFU YA UTOVU WA NIDHAMU.

MENGI YAMEONGELEWA KUHUSU MCHANGO WA NYERERE KATIKA HARAKATI ZA UHURU WA TANGANYIKA,NA NDOTO YAKE YA UMOJA ILIYOZAA TAIFA LA TANZANIA KWA KUUNGANA NA ZANZIBAR,PAMOJA NA MCHANGO WA TANZANIA KATIKA MAPAMBANO YA UHURU KUSINI MWA BARA LA AFRIKA.

BAADHI YA MISINGI ALIYOJENGA NYERERE BADO IPO LICHA YA JITIHADA KUBWA ZA "WANAFUNZI WAKE" KUIBOMOA.WATANZANIA BADO TUNASIFIKA KWA NAMNA TUNAVYOTHAMINI UNDUGU WETU (USHAHIDI UKIWA NENO "NDUGU" KABLA YA MAJINA YETU JAPO WAWAKILISHI WETU BUNGENI WANAITWA WAHESHIMIWA).

KAMA KATUNI YA KIPANYA INAVYOONYESHA HAPO JUU,NYERERE PIA ALITUFANYA TUWE WAPOLE KUPITA KIASI.UPOLE HUO ZAMA ZA CHAMA KIMOJA ULIIMARISHWA NA SHERIA ZILIZOTULAZIMISHA KUAMINI KUWA KIONGOZI YUKO SAHIHI WAKATI WOTE.MADHARA YA IMANI HIYO NI HUJUMA INAYOFANYA NA BAADHI YA WANASIASA KUAHIDI MAMBO WASIYOWEZA KUTEKELEZA LAKINI KWA VILE WATANZANIA NI WAPOLE,NA WANAOAMINI KILA ASEMACHO KIONGOZI,WAMEENDELEA KUTUTAWALA NA SI AJABU WAKAENDELEA KUTUTAWALA ZAIDI.WANAFAHAMU KUWA WANAOWATAWALA HAWANA JEURI YA KUHOJI AHADI ZISIZOTEKELEZEKA ACHIULIA MBALI VITENDO VYA UFISADI VINAVYOFANYWA NA WATEULE WA VIONGOZI HAO.

PAMOJA NA HESHIMA YANGU KUBWA NILIYONAYO KWA BABA WA TAIFA,NALAZIMIKA KUMLAUMU KWA UZAZI NA KULEA TABAKA AMBALO LEO HII TUNALIITA MAFISADI.SIAMINI KABISA KUWA BAADHI YA WANAFUNZI WA MWALIMU WALIKURUPUKA GHAFLA KUWA MATAJIRI KUPINDUKIA HUKUN WAKIKUMBATIA WAGENI NA MARAFIKI ZAO.NAAMINI KUWA WATU HAWA HAWAKUWAHI KUWA WAJAMAA JAPO WALIIMBA NA KUCHEZA UJAMAA MAJUKWAANI WAKIWA NA MWALIMU.

TUMWANGALIE MTU KAMA KINGUNGE NGOMBALE MWIRU.HUYU ALIKUWA SWAHIBA WA MWALIMU NA TULIAMBIWA KUWA DINI YAKE NI UJAMAA.HIVI KWELI KINGUNGE AMEBADILIKA GHAFLA KUWA MTETEZI WA MAFISADI AU ALIKUWA ANAMZUGA TU MWALIMU ZAMA ZA UTAWALA WAKE?

BAADHI YA MADUDU TUNAYOSHUHUDIA LEO YALIANZA ZAMA ZA MWALIMU.KULIKUWA NA KIJITABIA CHA MTU AKIHARIBU HAPA ANAHAMISHIWA PALE,KAMA AMBAVYO AKINA MATTAKA WALIVYOSHINDWA KUIOKOA TRC LAKINI WAKAPELEKWA BIMA.SI KWELI KWAMBA NYERERE HAKUENDEKEZA URAFIKI,MAANA ISINGEKUWA HIVYO BASI ASINGEMPIGIA DEBE MKAPA,RAIS AMBAYE BAADA YA KUTOKA IKULU AMEACHA WATANZANIA WENGI WAKISHANGAA KWA NAMNA ALIVYOTUMIA FURSA HIYO KUJITAJIRISHA (REJEA ISHU YA KIWIRA).

BAADHI YA WACHAMBUZI WA SIASA ZA AFRIKA WANAMTUHUMU MWALIMU KUWA WAKATI ANASTAAFU MWAKA 1985 ALIACHA TAIFA LIKIWA KATIKA HALI MBAYA SANA KIUCHUMI.KUNA WANAODAI KWAMBA UAMUZI WA KUNG'ATUKA UNAOPIGIWA MSTARI KAMA MFANO WA KUIGWA ULIKUWA MATOKEO YA KUKWEPA MAJUKUMU.WAPO WANAOKWENDA MBALI ZAIDI NA KUDAI KWAMBA MWALIMU ALIPASWA KUWAOMBA MSAMAHA WATANZANIA KWA KULIFIKISHA TAIFA LILIPOFIKA WAKATI ANASTAAFU.

HATA SIASA YA UJAMAA NAYO IMEZUA MJADALA KWA BAADHI YA WACHAMBUZI WA SIASA.KUNA WANAOONA KUWA NYERERE ALIKUWA MUUMINI PEKEE WA ITIKADI HIYO HUKU AKIWA AMEZUNGUKWA NA KUNDI LENYE BAADHI YA MATAPELI WA KISIASA WALIOKUWA WANAMUUNGA MKONO JAPO NAFSINI MWAO WALIKUWA NA MAWAZO TOFAUTI.NA MFANO UNAOREJEWA MARA NYINGI NI UAMUZI WA KUUA AZIMIO LA ARUSHA MARA BAADA YA MWALIMU KUTOKA MADARAKANI NA KULETA AZIMIO LA ZANZIBAR.

TATIZO JINGINE LA UJAMAA LIKO KWENYE UKWELI KWAMBA ULIKUWA MITHILI YA JARIBIO,AMBALO KWA KIASI KIKUBWA HALIKUFANIKIWA HADI MWALIMU ANAONDOKA MADARAKANI.KUTOKUFANIKIWA HUKO KULICHANGIWA NA NAMNA UJAMAA ULIVYOSAMBAZWA,AMBAPO MATUMIZI YA NGUVU YALIKUWA JAMBO LA KAWAIDA.REJEA NAMNA OPERESHENI VIJIJI VYA UJAMAA ILIVYOWAATHIRI BAADHI YA WATANZANIA KWA KUONDOLEWA MAHALA WALIPOJIJENGA NA KUPAZOWEA NA KUPELEKWA "UGENINI."HOJA HAPA SI KWAMBA WAZO LA UJAMAA LILIKUWA ZURI AU BAYA BALI KAMA LILIKUWA LINATEKELEZEKA HASA IKIZINGATIWA KWAMBA TANZANIA ILIKUWA TEGEMEZI KIUCHUMI TANGU ILIPOPATA UHURU WAKE 1961.

KUDHANI KWAMBA MAFISADI WALIIBUKA GHAFLA NI KUKWEPA KUDADISI CHANZO CHA TATIZO.MAFISADI WENGI NI TABAKA LILILOIBUKA MIAKA YA MWISHO WA HARAKATI ZA UHURU NA BAADA YA KUPATIKANA UHURU.NI KIKUNDI CHA WARASIMU WALIOTUELEKEZA NAMNA YA KUFANYA JAPO WAO WENYEWE HAWAKUFANYA HIVYO.TABAKA HILI LILIKUWA LINASUBIRI MWALIMU AONDOKE MADARAKANI LIANZE "KUFANYA VITU VYAKE",AND SURE THEY DID!

NYERERE ALIZUNGUKWA NA LUNDO LA WANAFIKI.KISICHO NA HAKIKA NI KAMA ALIFAHAMU UNAFIKI WAO NA KUWAVUMILIA AU WALIMZIDI AKILI.YOTE MAWILI HAYAMTOI LAWAMANI KWA VILE PINDI KIONGOZI ANAPOCHAGUA WASAIDIZI WENYE MAPUNGUFU,AIDHA KWA KUTOJUA AU KWA MAKUSUDI,NI LAZIMA ABEBE LAWAMA KWA UTEUZI MBOVU.

UJAMAA,REGARDLESS YA KUWA ITIKADI YA MAJARIBIO,UNGEWEZA KUZAA MATUNDA MEMA IWAPO UNGEGUSA KILA MTANZANIA PASIPO KUJALI NAFASI YAKE KATIKA JAMII.NI DHAHIRI KUWA LAITI HILO LINGETIMIA BASI TUSINGESHUHUDIA AWAMU YA PILI (BAADA YA NYERERE) IKIENDESHA TAIFA KWA MTINDO WA LAISSEZ FAIRE (BORA LIENDE) NA AWAMU YA TATU IKITUAMINISHA UJIO WA ZAMA ZA UWAZI NA UKWELI HUKU WATU WANAUZIANA MGODI WA KIWIRA KWA BEI YA KISHKAJI.YA UFISADI KILA MMOJA WETU ANAFAHAMU HALI ILIVYO.

KWA VILE MIE NI MKRISTO,NA KWA VILE MILA ZETU ZINAKATAZA KUWASEMA VIBAYA MAREHEMU,BASI NAUNGANA NA WATANZANIA WENZANGU KUMTAKIA MWALIMU PUMZIKO LA MILELE NA MWANGA WA MILELE,APUMZIKE KWA AMANI,AMINA.HATA HIVYO,KAMA SIE WAKATOLIKI TUNAVYOAMINI KUWA ROHO ZA MAREHEMU ZIKO "HAI" TUKIZIKUMBUKA KWA SALA,BILA SHAKA MWALIMU ANAJUTA KUCHAGUA "MARAFIKI" AMBAO BAADA YA KUONDOKA KWAKE WAMEGEUZA TANZANIA KUWA SHMBA LA BIBI,WANACHUMA WATAKAVYO,WANAKWIBA WATAKAVYO,LAKINI KWA VILE ALITUGEYUZA WAPOLE NA WAGUMU KUDAI HAKI ZETU,TUNAENDELEA KUVUMILIA MACHUNGU.

MWISHO,KWA VILE LAWAMA PEKEE HAZIWEZI KUSAIDIA KUTUFIKISHA TUENDAKO,JUST LIKE MAKALA NDEFU ZA KUMBUKUMBU YA MWALIMU ZISIVYOWEZA KUWAKWAMUA WALALAHOI,NI MUHIMU KUITUMIA SIKU HII KUJIULIZA SWALI HILI MUHIMU.JE NYERERE NA WAPIGANIA UHURU WENZAKE WALIPAMBANA NA MKOLONI KWA MINAJILI YA KUMUONDOA MTU MWEUPE NA KUMUWEKA MKOLONI MWEUSI (MAFISADI,et al)?

ANGALAU MKOLONI ALIKUWA NA EXCUSE YA KUTUNYONYA NA KUTUPELEKESHA.HAKUWA MTANZANIA,HAKUWA NA UCHUNGU NA NCHI HII,NA HAKUFIKISHWA ALIPOFIKIA KWA JITIHADA ZA WATANZANIA.LAKINI MAFISADI NI WATANZANIA WENZETU,WANALAZIMIKA KUWA NA UCHUNGU NA NCHI YETU KWA VILE KWA VYOVYOTE VILE BAADHI YA WAATHIRIKA WA UFISADI WAO NI NDUGU ZAO WA MBALI (WA KARIBU WAMESHATENGENEZEWA ULAJI SOMEWHERE).

NJIA BORA YA KUMUENZI MWALIMU NI KUREKEBISHA PALE ALIPOKOSEA (KWA MFANO KUWALEA VIONGOZI WALIOMZUGA KUWA NI WAJAMAA LAKINI WAKAGEUKA MAFISADI MARA BAADA YA KUONDOKA KWAKE) NA KUIANGALIA TANZANIA KAMA NCHI YETU SOTE NA SI YA WATEULE WACHACHE (AMBAO MARA NYINGI HAWATAKI KUSIKIA SAUTI TOFAUTI NA YAO UNLESS IWE NI VIGEREGERE AU MAKOFI YA PONGEZI).TUMUENZI MWALIMU KWA KUKATAA NCHI YETU KUWA SHAMBA LA BIBI HUKU WAWEKEZAJI UCHWARA WAKIJA NA BRIEF CASES TUPU NA KUONDOKA WAKIWA MAMILIONEA.TUKATAE WEZI KAMA WA KAMPUNI YA KAGODA NA MATAPELI KAMA WA RICHMOND,NA UJAMBAZI KAMA WA MEREMETA,TANGOLD,NK KUENDELEA HUKU WAHUSIKA WAKITUPUUZA KWA KUGOMA KUTUELEZA UKWELI.


BONYEZA PICHA KUIKUZA NA KUSOMA STORI



Hivi karibuni niliandika makala flani kuhusu milipuko ya mabomu huko Mbagala, jijini Dar es Salaam. Kwa kutambua kuwa blogu yangu haina idadi kubwa ya wasomaji (japo nawathamini sana wachache wanaotumia muda wao kuitembelea) niliamua kuisambaza makala hiyo kwa bloga wenzangu wawili ambao “nyumba” zao hupata “wageni” wa kutosha kila siku.

Kwa bahati mbaya, bloga hao waliamua kuiweka makala hiyo kapuni.Siwalaumu,kwa sababu kadhaa. Kwanza, blogu ni mali ya mmiliki, na hilo linampa haki ya kuchagua nini kiwepo kwenye blogu yake na nini kisiwepo.Pili, kila bloga ana mtazamo wake kuhusu mambo mbalimbali yanayotuzunguka, iwe siasa, dini au nyanja nyingine za maisha ya binadamu. Kwa maana hiyo, kama ataletewa makala inayokinzana na mtazamo huo, ana haki ya kuipuuza. Kuna sababu nyingine za kibinafsi lakini sidhani kama zina umuhimu sana.

Makala husika (isome hapa) haikuwa ya matusi, kashfa au utovu wa nidhamu kwa watawala japo ilikuwa ikizungumzia uzembe na kutowajibika kwa baadhi ya viongozi wetu unavyohusika na janga hilo la milipuko ya mabomu.Nilishauri katika makala hiyo kwamba wakati umefika kwa Watanzania kudai haki zao hasa pale zinapopuuzwa makusudi. Kwamba ripoti ya milipuko ya kwanza inaozea katika makabrasha ya Wizara husika, kisha mlipuko mwingine unatokea lakini hakuna anayewajibika, jambo linalohitaji shinikizo la kudai haki na uwajibikaji.

Naamini kwamba laiti makala hiyo ingechapishwa laiti ingekuwa ya kumsifia kiongozi flani au kukumbushia tarehe yake ya kuzaliwa. Au laiti ingekuwa ni tangazo binafsi. Yote hayo ni mazuri kwa vile ni huduma kwa umma. Hata hivyo, harakati tunazohangaika nazo wengine kuboresha future ya nchi yetu ni muhimu pia na hazipaswi kupuuzwa.

Ni rahisi kwangu kuhitimisha kwamba kinachokwanza makala za aina hiyo kuchapishwa ni uoga wa mabloga husika wakihofia kuwaudhi watawala. Japo huo ni uhuru wao kibinadamu, madhara yake kwa jamii ni makubwa kwa vile historia inaonyesha kwamba uoga ni kitalu mwafaka kwa ushamiri wa tawala dhalimu.

Lengo langu si kulaumu bali kushauriana.Kukimbilia kuweka picha za kiongozi akihutubia au akirejea Dar akiwa bukheri wa afya lakini kuchelea kujumuisha maelezo kwamba pia alikumbwa na dhahama ya kiafya ni kutowatendea haki wasomaji wetu. Hapa narejea tukio lililotokea jijini Mwanza hivi karibuni ambapo baadhi ya wenzetu walitonyesha “picha nzuri” za JK lakini “wakabania” maelezo kuhusu mkasa uliomkumba wa kushindwa kuendelea na hotuba yake katika kile kilichoelezwa kuwa “uchovu wa safari.”

Ushirikiano wetu jumuiya iliyojibebesha dhamana ya kuujulisha umma kuhusu mambo mbalimbali usiishie kwenye yanayopendeza machoni pekee bali pia yale yanayoudhi au kukera.


Hivi mwenzangu unapoiangalia CCM kwa mtazamo wa kawaida tu (yaani usiohisha uchambuzi wa kitaaluma) unaielezeaje?Pengine huafikiani na mtizamo wangu wa “kawaida” na kitaaluma kwamba pamoja na hadi lukuki za kuwakomboa Watanzania kutoka kwenye lindi la umasikini,chama hicho hakijaonyesha dhamira ya dhati kutimiza ahadi hizo.

Naamini kuwa baadhi ya ahadi hizo zilikuwa za dhati,hususani ile ya kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.Naamini hivyo kwa vile ni dhahiri kwamba chama hicho kilikuwa kinatambua hali ngumu inayowakabili Watanzania baada ya miongo kadhaa ya utawala wake.Kwa kutambua tatizo,CCM ilileta dalili za matumaini kwamba sio tu inataka kuendelea kutawala lakini pia inataka kuwa chachu ya mabadiliko.Japo chama hicho kinafahamika kwa usugu wa kukiri mapungufu ya utendaji wake,uamuzi wake kugusia maeneo yanayowakera wananchi ilikuwa ishara ya kutambua mapungufu katika awamu zilizotangulia na kudhamiri kufanya marekebisho.

Binafsi nilitarajia kwamba kama ilivyokuwa mwaka 2005 ambapo CCM “ilikiri mapungufu yake kiaina” kwa kuahidi kuboresha maisha sambamba na kukabili chanzo kikuu cha kuzorota/kudidimia kwa maendeleo (rushwa),basi safari hii pia kingepata ujasiri wa kutueleza bayana kwamba kumekuwa na mapungufu makubwa zaidi katika utekelezaji wa ahadi hizo.

Ni nani asiyejua kuwa kiwango cha rushwa kinazidi kupaa siku hadi siku?Ni nani asiyejua kuwa rushwa na uhujumu mwingine wa uchumi umechukua sura mpya kwa kuzaa tabaka “jipya” la mafisadi?Ni nani pia asiyejua kuwa kwa kiasi kikubwa ahadi ya maisha bora kwa kila Mtanzania imekuwa na maana zaidi kwa mafisadi kuliko walalahoi?Ni dhahiri kwamba Watanzania wenzetu kama wamiliki wa kampuni ya Kagoda wanaishukuru CCM kwa ukarimu na huruma yake to an extent that inaona aibu kuwataja hadharani.Matapeli wa Richmond (achana na yule Mhindi aliyegeuzwa mbuzi wa kafara mahakamani) wanaishukuru sana CCM kwa huruma yake kwao ambapo kila kikao cha bunge kinazugwa kuwa “taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya kamati ya Mwakyembe itatolewa katika kikao kijacho”,na porojo nyingine kama hizo.

Kinachokera sasa sio tu madudu yanayoendelea kufanywa na CCM bali hizi kauli za kukera kwamba eti chama hicho kimeweka rekodi ya mapambano ya rushwa kuliko nyakati yoyote ile.Hii ni sawa na kuwasanifu Watanzania.Ni mithili ya kuwafanya wajinga,wasioona madudu yanayoendelea,wasiosikia maumivu ya vibano wanavyopewa na mafisadi,na wasiofahamu kuwa watuhumiwa kadhaa wa ufisadi hawajaguswa hadi leo (na hakuna dalili kuwa wataguswa licha ya ahadi kuwa kuna kesi tatu kubwa zitafunguliwa hivi karibuni....na kila mara tunaambiwa “hivi karibuni).”

Ni kweli kwamba hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi hazipaswi kuchukuliwa kutokana na utashi wa watu flani bali kwa kuzingatia sheria na kanuni.Lakini utashi ni muhimu katika kuchukua hatua,na hapa hatuzungumzii utashi wa wananchi wasio na uwezo wa kuuamua,kwa mfano “Chenge na tuhuma za vijisenti vyake huko Jersey hastahili kuwa kwenye kamati ya maadili ya CCM.”Kwanza kuwa na utashi wa kufanya jambo jema si dhambi,kama CCM inavyotaka kutuaminisha.Kuwa na utashi wa kuchukua hatua dhidi ya mafisadi ndio itapelekea chama hicho kuwatenga mafisadi inaowakumbatia,na hivyo kuwa rahisi kwake kuchukua hatua dhidi yao.Utashi unapaswa kuepukwa ni kama ule wa wanamtandao unaoendelea kuwaangalia wana-CCM wasio wanamtandao kuwa mithili ya wahaini.

Mamlaka husika zinapozembea kuchukua hatua sahihi halafu tunaishia kuambiwa kuwa hatua haziwezi kuchukuliwa kwa utashi wa watu flani...jibu jepesi ni kwamba matatizo yetu hayawagusi wanaotuongoza.Wanaona tunapiga kelele zisizo na msingi,ndio maana kwao haki za binadamu za mafisadi ni muhimu zaidi kuliko za walalahoi walio wengi.

Hivi kweli CCM inataka kutuzuga kuwa haifahamu kwamba Watanzania wengi wangependa kuona wahusika “halisi” wa utapeli wa Richmond wakifikishwa mahakamani badala ya kile tunachoelezwa kuwa “walijiuzulu kwa maslahi ya taifa”?CCM haijui kwamba kwa kuendelea kuminya taarifa kuwa nani anamiliki Kagoda ni mithili ya kuwapuuza Watanzania?Au CCM haifahamu kuwa kuwaachia mzigo Waingereza kudili na vijisenti vya ujambazi wa rada ni kukwepa majukumu?

Au chama hicho kinapotulaghai kwamba tumwache mhusika mkuu wa ufisadi katika mgodi wa Kiwira apumzike kwa amani ni sawa na kuruhusu kila mtu aibe kisha aachwe apumzike kwa amani?Kwanini basi vibaka wanajazana magerezani ilhali wezi wakubwa wanatetewa kwa nguvu zote?

Watanzania wana kila sababu ya kuiadhibu CCM hapo mwakani.Kinachofanywa na chama hicho kinapodai kuwa “kimeweka rekodi ya kupambana na rushwa” ni mithili ya vibaka wanaokuibia kisha wanakupigia ukelele wa mwizi na kupelekea wewe mwathiriwa wa uporaji huo kushushiwa kipigo kitakatifu huku kibaka “akiyeyuka kiulaini.”Badala ya kukiri kwamba kasi yao ya kupambana na ufisadi ni ndogo, wao wanatukejeli kuwa wameweka rekodi!Halafu bado tutegemee lolote kutoka kwa wababaishaji hawa?

Hakuna haja ya kubishana au kupigiana kelele nao.Dawa yao ni hapo mwakani.Kama unataka kuendelea kuona mafisadi wakitetewa huku wanaowapinga wakikemewa basi irejeshe CCM madarakani hapo mwakani.Kama unadhani maisha bora yaliyoahidiwa 2005 yamepatikana zaidi ya matarajio yako basi hutofanya kosa kutoa kura ya ndio kwa chama hicho.

Tukiendeleza mazowea tutazidi kuumia.Kuna wanaodhani kwamba Tanzania haiwezi kuwa kisiwa cha amani pasipo utawala wa CCM.Wanachosahau kuwa hata hao CCM ni Watanzania wenzetu japo wanawathamini zaidi wageni (wawekezaji) kuliko sie wenye nchi.Wanasahau pia kuwa wingi wa wabunge wa CCM unakwaza jitihada wa wapambanaji kama akina Dokta Slaa kuwakalia kooni wababaishaji waliojazana chini ya utawala wa CCM.

Atakayenuna na anune lakini nchi hii ni yetu sote na kila Mtanzania ana haki ya kudai haki yake.Tukiruhusu kuendelea kwa ngojera za “tunaendelea na mchakato wa blah blah blah” au “kesi kadhaa zkubwa zitapelekwa mahakamani hivi karibuni...” na hadithi nyingine kama hizo basi tutaendelea kuwa watu wa kulalamika kila siku japo ni sie wenyewe tunaoweza kukomesha usanii wa kisiasa wa aina hiyo.Kama imewezekana Ghana basi hata kwetu inawezekana.Si kweli kwamba chama mbadala kitashindwa kutupeleka tunakostahili kwenda hasa ikizingatiwa kuwa hakuna uwezekano wa chama hicho mbadala kupata idadi kubwa ya wabunge zaidi ya CCM,which means itakuwa rahisi kukidhibiti iwapo kitaonyesha dalili za kurejea madudu ya CCM.

Kusanya hasira zako lakini usipigane bali pugie kura ya kujiletea maisha yako bora wewe mwenyewe kwa kuwaondoa wanaokwaza uwezekano huo.Ifike wakati tusema tumechoshwa na ahadi na maneno matamu (na mengine si matamu bali ya dharau kama hayo ya kudai wameweka historia ya kupambana na rushwa wakati wanajua waziwazi kuwa wamekuza rushwa kupindukia).

It can be done if you play your part.

Inawezekana ukiamua kutimiza wajibu wako.


10 Oct 2009


SOMA KAULI ZA BABU HUYU HAPA CHINI KISHA UELEWE KWANINI NATOA WITO AONEWE HURUMA KWA KUPUMZISHWA.

Ahofia wabunge wengi CCM kutorudi Bungeni
Na Keneth Goliama, Mbeya

MBUNGE wa kuteuliwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kingunge Ngombale Mwiru, amewashutumu viongozi wanaounda makundi ndani ya chama hicho na kuwaita waliochanganyikiwa.

Mbunge huyo aliapa kuwa matajiri wasipewe kipaumbele katika uongozi, kwani watu wakishakuwa na fedha wanajiingiza katika siasa kufanikisha malengo yao ya kibiashara.

Kingunge ambaye pia ni Naibu Kamanda UVCCM Taifa,aliyasema jana wakati akiwaapisha Makamanda wa Mkoa wa Mbeya kwenye ukumbi wa Mkapa.

Aliwataka makamanda hao kufanya kazi ya kuwashauri vijana na sio kuwaingiza vijana katika makundi yaliyopo ndani ya chama hicho.

Kingunge alisema kauli za baadhi ya viongozi kuwa, wabunge wengi wa CCM hawatarudi katika ubunge mwaka 2010 ni kweli kwa sababu kunahitajika mabadiliko katika uongozi ndani ya chama.

Hata hivyo, alisema wabunge hao wapya ni faraja kwa CCM kwa sababu watakuwa ni wakutoka ndani ya chama hicho.

Aliongeza licha ya Mkoa wa Mbeya ni mingoni mwa mikoa ambayo ilitoa watu waliokuwa mstari wa mbele kugombea uhuru , lakini sifa hiyo imeharibiwa na viongozi wachache.

Kingunge alisema baadhi ya viongozi mkoani hapa wanauhasama wa kugombea madaraka na kwamba sasa ugomvi huo unakiharibia chama.

Akiunga mkono jitihada za vijana wa mkoa huo kupambana na mafisadi, Kingunge aliwataka wasiache kutetea haki yao kwa sababu vijana ndio wenye nguvu katika maendeleo ya jamii na siasa.

Kingunge aliwaasa wanachama hao kukataa kurubuniwa na watu wenye fedha kwani kukubali kufanya hivyo ni kuua chama.

Baadhi ya viongozi wamefanikiwa kuwarubuni vijana kwa fedha ili waweze kujinufaisha wenyewe na kuharibu siasa mkoani hapa, alisema Kingunge

Alikionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa, hakijui siasa ndio maanakimejaa matatizo matupu na uchaguzi wao ni ovyo na kwamba hakina uwezo wa kupewa kuongoza dola.

CHANZO: Mwananchi

HIVI ALIYECHANGANYKIWA NI NANI KATI YA KINGUNGE NA HAO ANAOWAITA "WAMECHANGANYIKIWA."MAJUZI,MTETEZI MAHIRI WA MAFISADI,YUSUPH MAKAMBA NAE ALITOA TAMKO LINALOSHOBIHIANA NA HILI LA KINGUNGE,MWANASIASA ALIYETUZUGA ENZI ZA MWALIMU KUWA NI MFUASI MAHIRI WA UJAMAA ONLY KUIBUKA MTETEZI MAHIRI WA MAFISADI.LEO,MIEZI MICHACHE KABLA YA UCHAGUZI MKUU,NAE ANAJITUTUMUA KUKEMEA MAFISADI!?HUKU NI KUCHANGANYIKIWA KUNAKONASIBISHWA NA KUZEEKA VIBAYA.

9 Oct 2009


From its politics to its economy to its environment and way of life, California is like a patient on life support. At the start of summer the state government was so deeply in debt that it began to issue IOUs instead of wages. Its unemployment rate has soared to more than 12%, the highest figure in 70 years. Desperate to pay off a crippling budget deficit, California is slashing spending in education and healthcare, laying off vast numbers of workers and forcing others to take unpaid leave. In a state made up of sprawling suburbs the collapse of the housing bubble has impoverished millions and kicked tens of thousands of families out of their homes. Its political system is locked in paralysis and the two-term rule of former movie star Arnold Schwarzenegger is seen as a disaster – his approval ratings having sunk to levels that would make George W Bush blush. The crisis is so deep that Professor Kevin Starr, who has written an acclaimed history of the state, recently declared: "California is on the verge of becoming the first failed state in America." WRITES The Observer's Paul Harris.



Na Ramadhan Semtawa

RAIS Jakaya Kikwete aliweka hadharani matokeo ya uchunguzi wa vipimo vya afya yake, yanayoonyesha kuwa kiongozi huyo wa nchi ana afya njema baada ya tatizo la kuishiwa nguvu akiwa jukwaani mjini Mwanza Oktoba 4, kuibua mjadala.

Lakini vipimo hivyo vinaonyesha kuwa tatizo pekee linalomsumbua Rais Kikwete ni maumivu ya shingo ambayo yanatokana na kuumia nyakati za ujana au utoto.

Afya ya Rais Kikwete ilizuia mjadala baada ya kuishiwa nguvu akihutubia kwenye Uwanja wa Kirumba mjini Mwanza na kulazimika kubebwa na wasaidizi wake hadi chumba kidogo cha uwanjani hapo na ilielezwa baada ya rais kuzinduka kuwa tatizo hilo lilitokana na uchovu baada ya safari ndefu kati ya New York, Marekani na Dar es salaam na baadaye Arusha na Mwanza.

Pamoja na uchovu huo kuhusishwa na safari ndefu ya Rais Kikwete taarifa iliyopokelewa kutoka Radio Jamaica jana jioni zinasema kuwa rais atakwenda nchini Jamaica kwa ziara ya kikazi itakayoanza Novemba 24 na kumalizika Novemba 26.

Na jana daktari wa rais, Peter Mfisi alirejea tena kauli hiyo akisema uchovu, hasa wa safari, ndio uliosababisha kiongozi huyo wa nchi kuishiwa nguvu jukwaani, huku kukiwa na habari kuwa ataenda Jamaica mwezi ujao kwa safari ya kikazi.

Hii ni mara ya kwanza kwa Ikulu kuweka hadharani vipimo vya uchunguzi wa afya ya Rais Kikwete, ambaye pia aliwahi kuishiwa nguvu siku ya mwisho ya kampeni zilizomuingiza Ikulu, na kuanguka akiwa jukwaani.

Daktari wa rais, Peter Mfisi aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa vipimo hivyo ni pamoja na cha damu kwa ajili ya kuangalia virusi vya Ukimwi ambacho huchukuliwa kila baada ya miezi sita.

"Nimekuja kufafanua afya ya mheshimiwa rais kutokana na tukio la Oktoba 4, 2009 (la kuishiwa nguvu jukwaani) pale Mwanza. Tukio hilo limesababisha mshtuko kwa watu wengi na kuendelea kuwa jambo linalozua mjadala kuhusu hali ya afya ya mheshimiwa," alisema daktari huyo.

"Naelewa sababu ya wananchi kuwa na hofu na kuwepo kwa mjadala miongoni mwao. Tatizo pekee ambalo limekuwa likimsumbua rais mara kwa mara ni maumivu ya shingo yanayotokana na kuumia utotoni na wakati wa ujana.

"Baadhi ya pingili za uti wa mgongo sehemu ya shingoni ziliathirika kutokana na kuumia huko na humsababishia maumivu. Mara nyingi matatizo hayo huwapata wanamichezo na wanajeshi."

Dk Mfisi aliongeza kusema: "Tumekuwa tunamfanyia mheshimiwa rais uchunguzi wa damu yake kwa vipimo mbalimbali vinavyotumika kutambua maradhi mbalimbali yanayohusu damu yenyewe na mwili mzima wa mwanadamu. Tumekuwa tunafanya hivyo hapa nchini na hata nje kwa nia ya kulinganisha matokeo yetu na kwa vipimo ambavyo sisi tunavyo.

"Matokeo ya uchunguzi wetu yameonyesha mheshimiwa rais yuko salama, hana maradhi ya damu au kisukari, wala Ukimwi au wingi wa mafuta (Cholestrol), kiwango cha madini, tezi la kibofu wala shingo, au ya ini, au ya homoni mbalimbali zilizoko mwilini na mengine."

Dk Mfisi alifafanua kwamba, uamuzi huo wa kutoa vipimo hivyo umetokana na ridhaa ya rais mwenyewe.

"Ni ridhaa ya mheshimiwa rais mwenyewe... kutokana na kiapo changu cha udaktari na maadili yangu ya kazi, siruhusiwi kutoa hadharani undani wa habari yoyote inayohusu mgonjwa ninayemtibu bila ridhaa yake," alisema Dk Mfisi.

Kwa mujibu wa daktari huyo, baada ya Rais Kikwete kuishiwa nguvu jukwaani, alichukua vipimo muhimu wakati akiwa kwenye chumba maalumu uwanjani hapo kama ilivyo kawaida na kwamba vipimo hivyo vimeshafanyiwa uchunguzi.

Alifafanua kwamba matokeo ya vipimo vilivyochukuliwa siku ya tukio la Mwanza yalionyesha shinikizo la damu (BP) lilikuwa kati ya 130 kwa 85 (vipimo vya kitaalamu), kitu ambacho ni cha kawaida kwa mtu mwenye umri kama wa Rais Kikwete.

"Mapigo ya moyo wake yalikuwa ni 76 kwa dakika ambayo pia ni ya kawaida; sukari kwenye damu ilikuwa 5.5 ambayo nayo ilikuwa ya kiwango cha kawaida; joto la mwili lilikuwa nyuzi 37.5 ambalo ni la kawaida," alifafanua Dk Mfisi.

"Mheshimiwa Rais pia hakuwa na kiungo chochote kilichoonekana kutetereka, jambo ambalo lilithibitisha kuwa hakupata kiharusi. Mheshimiwa Rais hakuwa na matatizo yoyote ya kiafya ambayo yangeweza kuhusishwa kuwa chanzo cha tukio lile (la Mwanza)."

Hata hivyo, Dk Mfisi alisema baada ya kurejea Dar es Salaam alijaribu kuwasiliana na madaktari wenzake wa ndani na nje ya nchi ambao wamekuwa wakishirikiana nao katika kuchunguza na kufuatilia afya ya Rais Kikwete.

"Wote hao baada ya kuwasimulia kilichotokea na matokeo ya vipimo nilivyomfanyia mheshimiwa rais, kwa tafakuri zao hawakuwa na wasiwasi wowote kuwa tukio hilo lilisababishwa na jambo jingine lolote isipokuwa uchovu," alisisitiza daktari huyo wa rais.

Aliongeza kwamba mmoja wao alimuona rais siku moja kabla ya kuondoka New York ambako alipata nafasi ya kumchunguza afya ya mkuu huyo wa nchi.

Dk Mfisi, akitoa mtiririko huo wa vipimo mbalimbali na matokeo alisema: " Blood Pressure (shinikizo la damu), tunafuatilia kwa karibu sana msukumo wa damu, mwenyewe tunampa mashine ya kujipima kila siku na anafanya hivyo, kwa jumla presha yake iko kwenye viwango vya kawaida.

"Aidha, uzito wake wa mwili unaendana ipasavyo na urefu wake, mheshimiwa Rais ni mtu mwenye mazoea ya kufanya mazoezi na yuko makini katika chakula anachokula."

Daktari huyo wa rais aliweka bayana kwamba, wanahusika kwa ukamilifu na kuelekeza kuhusu chakula anachokula na kuongeza kwamba "ana nidhamu ya kujipima pamoja na mazoezi na chakula."

Kuhusu moyo, Dk Mfisi alisema tayari walishamfanyia rais vipimo vya kitaalamu vinavyofahamika kama ECHO na ECG na vingine, na kwamba matokeo yameonyesha hakuna tatizo lolote.

Akizungumzia ubongo, alisema mwaka jana Rais Kikwete alifanyiwa uchunguzi wa afya ya ubongo wake katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kutumia kipimo cha CT-Scan na matokeo yake yalionyesha kwamba, hakuwa na tatizo pia.

Dk Mfisi alisema Rais Kikwete aliwahi kufanyiwa uchunguzi wa ini, figo, bandama na kongosho kwa kutumia kipimo cha mionzi (ultra sound), uchunguzi ambao ulibaini viungo vyote hivyo viko salama.

"Kila mwaka tunapomfanyia uchunguzi wa afya ya mheshimiwa rais, tumekuwa tunafanyia uchunguzi wa viungo vyake muhimu vya tumboni kama vile ini, figo, bandama na kongosho na kwa kupima damu yake kwa vipimo vyote muhimu," aliongeza Dk Mfisi.

Kuhusu mfumo wa njia ya chakula, ambayo huhusisha koromeo la chakula, tumbo, utumbo mdogo, Dk Mfisi aliweka bayana kwamba matokeo ya uchunguzi yameonyesha hakuna tatizo lolote.

Alisema mwaka 2007 walimfanyia kipimo cha kitaalamu cha colonoscopy mjini Paris, Ufaransa, kuchunguza hali ya afya ya utumbo mkubwa na kwamba matokeo ya uchunguzi yalionyesha kuwa hana matatizo yoyote.

Alisema daktari aliyemfanyia rais kipimo hicho aliwaambia kuwa mkuu huyo wa nchi hahitaji kufanyiwa kipimo kama hicho tena mpaka baada ya miaka saba na kwamba daktari huyo alimtania rais kwa kusema kuwa "angefurahi kuazima utumbo" wake.

Kuhusu tezi la shingo, Dk Mfisi alisema kuwa akiwa mjini New York katika safari yake ya juzi, Rais Kikwete alifanyiwa uchunguzi wa afya ya tezi la shingo pamoja na kiwango chake cha utoaji wa homoni, matokeo yaliyoonyesha hakuna tatizo, hali kadhalika uchunguzi wa tezi la kibofu ulionyesha hana tatizo.

Dk Mfisi alisema rais hana tatizo la macho, masikio na pua na kwamba uvaaji miwani wa Kikwete haumaanishi kuwa ni maradhi.

"Tunapofanya uchunguzi wa macho ukiacha ile ya kuchunguza uwezo wa kuona, tunaangalia presha ya macho na hali ya viungo vya nje na ndani, mheshimiwa Rais hana matatizo yoyote," alisema.

CHANZO: Mwananchi

WAKATI DR MFISI AKITOA MAELEZO HAYO,MHADHIRI MWANDAMIZI KATIKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM DR HAJI SEMBOJA AMENUKULIWA NA JARIDA LA RAIA MWEMA AKIELEZA KUWA URAIS NI ASASI NA SI MTU BINAFSI.

Urais si Kikwete binafsi, ni mfumo wa kitaasisi. Ni wazi kuwa Rais amesema yeye ndiye hakuzingatia ushauri wa wataalamu wake kutokana na kuwaondolea lawama. Ameamua kuwalinda kwa kubeba lawama, lakini ukitazama jambo hili kwa upana wake wasaidizi wake walipaswa kutambua tangu awali kuwa urais ni system nzima Ikulu hata mlinzi wa getini. Kwa hiyo, wasaidizi ndiyo wenye kuamua na si kila kitu kifanywe na Rais kama ambavyo wanasema sasa watajaribu kumpunguzia ratiba,” ALISEMA DR SEMBOJA NA KUSISITIZA KWAMBA“Sidhani kama ni sahihi kukubali kuwa Rais ndiye alikataa ushauri, kwa taratibu za kimfumo Rais anapangiwa kila kitu ni kama anaamriwa hivi. Kwa tukio hili ameamua tu kuwa na nidhamu ya kuwalinda wasaidizi wake, namwombea afya njema lakini ni muhimu tuzingatie kuwa wengi walioamua kufanya kila kitu wenyewe walipata matatizo, Ikulu sasa ifanye kazi kama Ikulu.”

BINAFSI NAAMINI TATIZO NI LA KIMFUMO ZAIDI.KUNA TAASISI ZENYE MAMLAKA NA WAJIBU WA KUPANGA RATIBA ZA RAIS SAMBAMBA KWA KUZINGATIA UHALISIA,USALAMA NA MAMBO MENGINE KAMA HAYO.KWA WENZETU WANAOZINGATIA KANUNI NA TARATIBU ZA KITAASISI,SI RAHISI KWA RAIS KUJIAMULIA MAMBO YAKE MWENYEWE PASIPO KUZINGATIA USHAURI WA KITAALAM.SI RAHISI,KWA MFANO,BARACK OBAMA KUJIAMULIA KWENDA MAHALA FLANI KINYUME NA USHAURI WA U.S. SECRET SERVICE.UBISHI WA RAIS KAMA BINADAMU HAUNA NAFASI KATIKA UFANISI WA TAASISI INAYOZINGATIA TAALUMA NA MAADILI.IKUMBUKWE KWAMBA LAITI RAIS AKING'ANG'ANIA KUFANYA ZIARA MAHALA FLANI KINYUME NA USHAURI WA WASAIDIZI WAKE KISHA AKAPATWA NA JANGA,WATAKAOBEBA LAWAMA NI WASAIDIZI HAO NA SI RAIS.LAKINI PIA KUNA SUALA LA FEDHA ZA WALIPA KODI ZINAZOTUMIWA NA TAASISI HUSIKA KUILINDA ASASI YA URAIS NA BINADAMU ALIYEKABIDHIWA DHAMANA YA URAIS.NI DHAHIRI KWAMBA RAIS AKIPUUZA USHAURI WA WA TAASISI HUSIKA INAMAANISHA PIA UPOTEVU WA FEDHA ZA WALIPA KODI.



UTENDAJI WA AINA YA ZIMAMOTO,AU VIBAYA ZAIDI,KULENGA SHABAHA BAADA YA RISASI KUFYATUKA,UTATUGHARIMU HUKO MBELENI.LEO HII TUSINGEHITAJI DAKTARI WA RAIA KUWEKA HADHARANI TAARIFA NYETI ZA AFYA YA JK LAITI TAASISI HUSIKA ZINGEMLAZIMISHA JK KUFUATA USHAURI WA KITAALAMU KUHUSIANA NA RATIBA AU ZIARA ZAKE.TUSISUBIRI JAMBO LITOKEE NDIPO TUANZE KUTOA MAELEZO YA KITAALAMU. BY THE WAY,TAARIFA HIYO YA DAKTARI WA RAIS INAWEZA KUZUA MJADALA USIO NA TIJA KUHUSU MANTIKI YAKE.JAPO NI VEMA KUTOA UFAFANUZI KATIKA MASUALA YANAYOZUA UTATA (I WISH NA KWELI ISHU YA KAGODA INGEKUWA HIVYO) LAKINI KUNA UWEZEKANO WA "WABISHI" KUHOJI KAMA DAKTARI WA RAIS WA AFRIKA ANAWEZA KUTOA TAARIFA "MBAYA" DHIDI YA BOSI WAKE!

KWA SASA,MAMLAKA HUSIKA ZINAWEZA KUFARIJIKA BAADA YA KUPATA UTETEZI KUTOKA KWA JK.LAKINI NI VEMA ZIKATAMBUA KUWA JUKUMU LAO SI KUMWOGOPA MHESHIMIWA BALI KUFANYA KAZI ZAO KWA KUZINGATIA MAADILI NA TAALUMA.JK KAMA MTU ANAWEZA KUTOZINGATIA USHAURI WA MAMLAKA HIZO,LAKINI JK KAMA RAIS HARUHUSIWI KUJIAMULIA MAMBO YANAYOWEZA KUATHIRI ASASI YA URAIS.UOGA NA KUJIKOMBA NI MAMBO YASIYO NA NAFASI KATIKA PROFESSIONALISM.


8 Oct 2009

Mambo mengine huku Ughaibuni ni vituko vitupu.Kuna watu wanafuga majoka makubwa na kuyalea kama watoto wao,kuna wanaofuga panya mithili ya paka,na wengine wamegeuza tumbili kuwa watoto wa kambo.Na matunzo wanayopewa mbwa na paka hayatofautiani sana na anasa wanazofaidi watoto wa wabaka-uchumi wetu (mafisadi).

Kuna vijibwa flani vimekuwa kwenye chati kwa muda mrefu kutokana na kushebedukiwa na watu maarufu.Nadhani ushakiona ki-chihuahua cha Paris Hilton,kijibwa kidogo mithili ya paka.Sasa imeibuka fasheni mpya ya “kitimoto pimbi”,yaani nguruwe wadogo kupindukia.

Jioni hii kipindi cha Live From Studio Five katika kituo cha runinga cha Channel Five kimezungumzia fasheni hiyo mpya ambayo kwa hakika inaweza kuzua songombingo na maustaadhi pindi ikitua Bongo,almaaruf kwa ku-copy na ku-paste mengi ya yanayojiri anga hizi.






Manji, Jeetu wagombea matrekta

• Homa ya Kilimo Kwanza

na Mwandishi Wetu

WAFANYABIASHARA wawili maarufu hapa nchini wenye asili ya Kiasia, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel, maarufu kwa jina la Jeetu Patel, wanadaiwa kuingia katika mzozo mkubwa wa kibiashara wakati wakigombea kupata zabuni ya mradi wa kuingiza nchini na kusambaza matrekta, wenye thamani ya zaidi ya sh bilioni 50.

Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano limezipata kutoka vyanzo vyake vya habari vya kuaminika zimeeleza kuwa, Manji na Patel ambao wanadaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika kuomba zabuni hiyo, sasa wanawindana huku wakitishana kumalizana kibiashara.

Baadhi ya watu wa karibu na wafanyabiashara hao mabilionea waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti katika siku za karibuni walieleza kuwa, kumekuwa na jitihada za chini kwa chini zinazofanywa na wapambe wao kuvujisha katika vyombo vya habari mbinu zao wanazotumia kupata zabuni kubwa za serikali.

Mfanyabiashara mmoja maarufu ambaye yuko karibu na wafanyabiashara hao, alilieleza gazeti hili kuwa, mabilionea hao sasa wamekuwa mahasimu baada ya kuzidiana ujanja katika zabuni hiyo ambapo kila mmoja anatishia kutoa siri za kibiashara za mwenzake.

“Sasa wanatishana, kila mmoja anatishia kutoa siri za mwenzake kibiashara. Wote wanapata tenda kubwa kutoka serikalini, wanavyozipata wanajua wao. Kinachotushangaza kila mmoja anasema atamuanika mwenzake,” alisema mfanyabiashara huyo aliyeomba jina lake lisitajwe.

Taarifa za ndani kutoka kwa watu walio karibu na Manji, zinadai kuwa mfanyabiashara huyo hakufurahishwa na jinsi mchakato wa upatikanaji zabuni hiyo ulivyoendeshwa, na sasa anakusudia kuvujisha katika vyombo vya habari taratibu zilizokiukwa katika mchakato wa utoaji wa zabuni hiyo.

Zinadai kuwa, Manji anajiandaa kuweka wazi jinsi sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004 ilivyokiukwa wakati wa mchakato wa utoaji zabuni hiyo.

Katika mradi huo, Jeetu ambaye anatajwa kuwa mwakilishi wa Kampuni ya Escort hapa nchini, yenye makao makuu yake nchini India, ambayo imeshinda zabuni hiyo, anadaiwa kuwashawishi maofisa wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ambalo limekabidhiwa jukumu la kuutekeleza mradi huo na serikali, kuipatia kampuni hiyo.

Habari hizo zimedai kuwa, Jeetu alifanikisha mpango huo baada ya kuwaunganisha maofisa kadhaa wa ngazi za juu wa JKT na watendaji wakuu wa Escort walioko India, ambao baada ya kuhakikishiwa kupewa zabuni hiyo, waliwaalika maofisa kadhaa wa JKT kwenda nchini humo kwa ajili ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa kazi ya kusambaza matrekta hapa nchini.

Taarifa zaidi zilidai kuwa, tayari baadhi ya viongozi wa juu wa JKT wamekwisha safiri hadi India kusaini mkataba huo.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa, Manji anapinga hatua ya viongozi wa JKT kwenda kusaini mkataba huo nchini India, ikizingatiwa kuwa baadhi ya watendaji wa serikali wamekwishalalamikiwa kwa kusaini mikataba inayohusu miradi ya kitaifa nje ya nchi.

Aidha, inadaiwa kuwa, baadhi ya habari zinazotarajiwa kusambazwa zitakuwa zinahoji ukiukwaji wa taratibu kwa kutoa zabuni hiyo pasipo kuitangaza kama sheria ya manunuzi ya umma inavyoelekeza, licha ya Baraza la Mawaziri kuujadili mradi huo na kutoa baraka kwa JKT kuutekeleza.

Kwa upande wa Jeetu, taarifa zinadai kuwa, anajiandaa kujibu tuhuma za aina yoyote zitakazotolewa katika vyombo vya habari, zikiwa na lengo la kuichafua Kampuni ya Escort au zinazohusu upatikanaji wa zabuni hiyo.

Baadhi ya maofisa wa serikali waliozungumza na Tanzania Daima Jumatano kuhusu suala hilo walieleza kuwa, serikali ina taarifa kuhusu jambo hilo na inalifuatilia kwa karibu ili kuhahakisha hakuna taratibu zinazokiukwa katika utekelezaji wa mradi huo.

Mmoja wa maofisa wa ngazi za juu serikalini aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake alieleza kuwa, anafahamu kuwa Serikali ya India ilitoa mkopo usiokuwa na riba, wa zaidi ya sh bilioni 50 kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kununulia matrekta, wakati Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed Shein, alipofanya ziara nchini humo mapema mwaka huu, kwa sharti la kulipwa katika kipindi cha miaka 10.

Alisema sharti jingine lililotolewa katika kutoa mkopo huo, linaitaka Serikali ya Tanzania kuhakikisha inanunua matrekta hayo kutoka kampuni za India na si vinginevyo.

Ofisa huyo alisema, serikali iliamua kuikabidhi JKT jukumu la kusimamia utekelezaji wa mradi huo ili kuondoa mazingira yoyote ya kutokea udanganyifu katika kuutekeleza.

Hata hivyo, alieleza wasiwasi wake iwapo kuna taarifa za baadhi ya maofisa wa JKT waliokabidhiwa jukumu la kusimamia utekelezaji huo, kuzungumza na mwakilishi wa Kampuni ya Escort hapa nchini (Jeetu), kisha wakaipa kampuni anayoiwakilisha zabuni hiyo bila kufuata taratibu.

“Hili jambo linaweza kuharibu kabisa sifa ya JKT kama litakuwa kweli, kwa sababu itakuwa ni kashfa kubwa kwa jeshi kukiuka taratibu za manunuzi ya umma. Ingawa kuna imani kuwa si rahisi mambo ya kijeshi kuchunguzwa, lakini hili liko wazi mno kwa sababu ni zabuni iliyo wazi iliyokuwa ikifuatiliwa na wafanyabiashara wengi, hivyo hao hao wanaweza kuwa wametoa siri za taratibu kukiukwa,” alisema ofisa huyo.

Waziri mmoja aliyezungumza na gazeti hili hivi karibuni, alisema suala hilo lilizungumzwa katika Baraza la Mawaziri na kupatiwa baraka zote za kulitekeleza. Aliongeza kuwa, anaamini hakuna taratibu zilizokiukwa.

Hata hivyo, alionya kuwa Baraza la Mawaziri linazo taarifa za mfanyabiashara mmoja maarufu kufanya mpango wa kutoa taarifa za uongo kuhusu mchakato wa upatikanaji zabuni hiyo kwa sababu ya kisasi cha kukosa zabuni hiyo.

Tanzania Daima Jumatano lilipowasiliana na Ofisa Habari wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Nadhifa Omary, ili kupata ufafanuzi wa suala hilo, alisema jambo hilo linaweza kuzungumziwa na waziri tu kwa sababu ya unyeti wake.

Alieleza zaidi kuwa, hawezi kulizungumzia kwa sababu yuko nje ya ofisi kwa mapumziko, hivyo hana maelezo ya kina ya kulitolea ufafanuzi.

Alipoulizwa, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga, Dk. Hussein Mwinyi, alisema analifahamu vizuri suala hilo na alilihakikishia gazeti hili kuwa, hakuna utata wowote katika utekelezaji wa mradi huo, isipokuwa linaweza kufanywa ajenda ya kuchafuana na watu ambao wana malengo binafsi na mradi huo.

“Ninalijua vizuri jambo hilo, tenda zilitangazwa na zikafunguliwa, nakuhakikishia. Mimi mwenyewe niliona kampuni kama 11 hivi zilizoomba zabuni hiyo, sasa kama kuna mtu anasema kulikuwa na kasoro, ni mambo ya wafanyabiashara kutaka kuchafuana tu kwa malengo binafsi waliyonayo katika mradi huo,” alisema.

Naye Manji alipotafutwa kupitia simu yake ya kiganjani ili kuzungumzia suala hilo, kwa mara kadhaa ilikuwa ikipokelewa na wasaidizi wake na kueleza ameweka utaratibu wa kutoongea na waandishi wa habari mpaka inapobidi.

CHANZO: Tanzania Daima

NILIWAHI KUANDIKA HUKO NYUMA KWANZA HUU WIMBO WA "KILIMO KWANZA" HAUNA TOFAUTI NA USANII WA "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA."NGONJERA ZA KISIASA ZINAZOHANIKIZWA NA KAULI-MBIU MWANANA HAZIWEZI KUMKOMBOA MTANZANIA KATIKA LINDI LA UMASIKINI UNAOMKABILI.BADALA YAKE,JITIHADA KUBWA ZINAHITAJIKA KATIKA KUPAMBANA NA UFISADI NA MAFISADI,VIKWAZO VIWILI VIKUU VYA MAENDELEO YETU.HILO HALIWEZEKANI CHINI YA UTAWALA WA CCM KWA VILE CHAMA HICHO NI KITALU MWAFAKA KWA MAZALISHO NA HIFADHI YA UFISADI NA UFISADI.

HAWA WAHINDI WAMEGEUZA TANZANIA KAMA SEHEMU YA MAJARIBIO YA KILA MADUDU YANAYOWAJIA KICHWANI.WAMENABAKA UCHUMI WETU HUKU TULIOWAKABIDHI DHAMANA YA KUULINDA WANAENDELEA KUWANYENYEKEA KUTOKANA NA NJAA YAOYA TENI PASENTI.

MWAKA WA HUKUMU 2010 UNAKARIBIA.USIREJEE MAKOSA YA 2005,PLEEEEEZ!

6 Oct 2009


NILIWAHI KUBASHIRI HUKO NYUMA KWAMBA KADRI 2010 INAVYOSOGEA NDIVYO TUTAVYOZIDI KUSHUHUDIA VITUKO.LEO HII MAKAMBA NAE AMEJIUNGA KATIKA VITA DHIDI YA UFISADI!HIVI SI BINADAMU HUYU ALIYEWATAKA WATANZANIA KUACHANA NA MIJADALA YA UFISADI KWA VILE BAADHI YA WAHUSIKA WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI?

HEBU MSIKIE ALIVYOGEUKA KINYONGA KATIKA HABARI HII HAPA CHINI:

Makamba ahimiza mapambano dhidi ya ufisadi

na Jacob Ruvilo, Kigoma

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusufu Makamba, amesema ufisadi unapaswa kupigwa vita na kila Mtanzania mzalendo, kwani umechangia kwa kiasi kikubwa kudidimia maendeleo ya nchi.

Makamba alisema hayo juzi kwenye semina ya viongozi wa CCM Jimbo la Kigoma Mjini iliyofanyika katika viwanja vya Lake Tanganyika.

Alisema suala la watu kujipatia mali kinyume cha utaratibu na kuhujumu nchi havina uhusiano wowote na CCM, kwani watuhumiwa wote hawakuagizwa na chama kufanya hivyo, bali ni hulka zao binafsi.

Makamba alifafanua kuwa suala la muumini wa dhehebu fulani kwenda kinyume na maadili au amri ya vitabu vya dini, hapaswi kulaumiwa sheikh au mchungaji, badala yake ni muumini husika ambaye mwisho wa siku ndiye atakayepata adhabu kwa Mungu.

Aidha, Makamba alisema suala la vyama vya upinzani kushika bango na kuidhihaki CCM kuwa ni mafisadi kutokana na viongozi wachache wasio waaminifu, halina maana, bali suala la umoja na mshikamano katika kupinga mafisadi hao ni jukumu la watu wote, ikiwamo CCM.

Mbali na hilo, Makamba alikemea baadhi ya viongozi wa chama hicho kutumia uwezo wao wa fedha kutoa rushwa ili kupita katika chaguzi mbalimbali kuwa ni moja ya upatikana wa viongozi mafisadi na wasiofaa kwa jamii.

Alisema Tanzania haikuandaliwa kutawaliwa na wenye nacho na kwamba hali hiyo inaweka tabaka la mwenye nacho na asiyenacho, hali ambayo isipoangaliwa kwa umakini suala la rushwa litabaki kuwa ndoto.


TATIZO LETU WATANZANIA NI UWEPESI WETU KUAMINI KILA KINACHOAHIDIWA.MWAKA 2005 MAKAMBA NA CCM YAKE WALITAMBUA HILO NA KUJA NA AHADI LUKUKI IKIWEMO ILE MAARUFU YA KULETA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.SASA WANASEMA KWAMBA SUALA LA MAISHA BORA LILIANZA ZAMA ZA MWALIMU NYERERE,PENGINE KATIKA KUKWEPA KUTUELEZA HAYO MAISHA BORA WALIYOAHIDI ILIKUWA NI KWA MAFISADI PEKEE AU...?MAANA KAMA SUALA HILO LILIASISIWA NA NYERERE BASI WANGETAMKA BAYANA WAKATI ZA KAMPENI ZA 2005 BADALA YA KUIFANYA KAULI-MBIU MUHIMU ILIYOWAZUGA WATANZANIA NA KUTOA USHINDI MKUBWA KWA CCM.

NI MUHIMU KWA WAPIGA KURA KUTAMBUA KUWA WANASIASA WETU WANAWEZA KUAHIDI LOLOTE ILI WAPATE KURA KAMA ILIVYOSANIFISHWA KWENYE WIMBO WA "NDIO MZEE" WA PROFESA JAY.

TUSIREJEE MAKOSA YA 2005,PLEEEEZ!


The media as the source of information has the power influence public opinion. But before getting into how it might, it is important to know what my understanding of public opinion. I would define public opinion as the opinion shared by the majority of the public. Majority because it is almost impossible to find an absolutely agreed opinion among people with different social and economic background, racial differences, age, gender, etc. Gauging public opinion is normally done by using opinion polls, which as we all know, are merely representative of opinions shared by different groups in a given society, or in research terms, population.

If a study that is measuring public opinion on the impact of global warming finds 75% of respondents thinks that global warming possess a major threat to the future of mankind, it would then be concluded as “the study found that global warming is actually a threat to the future of mankind.”Public opinion is more about what many, and not necessarily all, think about something rather than what each of us think.

Take an example of the Loch Lomond “myth.” Majority of those who believe about the Loch Lomond monster have not even been to Scotland, let alone Loch Lomond itself. One of the reasons for the publicity of the myth has been the stories we frequently hear of read, or hear from, the media. The publicity has led to many us believing the existence of the Loch Lomond monster. If there were an opinion poll on whether people believe there is actually a monster there, the results could very likely be “yes” mainly because a larger section of the media has led us to believe that way.

As the public is made of individuals, it is difficult for each of them to make their opinions known, hence the usefulness of the media in giving a medium for a rather general collection of what each of us think about something. If manipulated, the media could as well lead us into believing that majority of us something is the way it is because many think so. Neglecting deviants, many people tend to be conformists in the sense that they normally do not want to look different from what the majority’s position. Therefore, as the Americans were led to believe by a section of the US media that the Saddam Hussein’s regime was actually linked for the 9/11 atrocities, rather than a neo-con agenda spearheaded by the likes of Donald Rumsfield, Richard Perle and Paul Wolfowitz,so does a section of the British public becomes influenced in their opinion by The Sun, The Daily Express, The Daily Telegraph and The Daily Mail that asylum seekers and refugees as actually among the causes of the country’s economic problems.

A biased media could in short or long run effectively influences public opinion because it communicates what “A” thinks in Derbyshire and “B” thinks in Lanarkshire. Or in an international perspective, what Maggie thinks in Glasgow and Evarist thinks in Dar es Salaam, Tanzania. It is even more effective in shaping public opinion in the less educated or less informed section of society that normally takes what is said by the media for granted.

During the 2005 general election campaigns in Tanzania, the ruling party courted the media to publicise a story that a neighbouring country’s army was planning to invade Tanzania. The ruling party then went on urging reminding the voters how the country emerged victorious in the 1978-79 war against Uganda under its (the ruling party’s) leadership. Some analysts believe that although the gimmick did not directly determine the outcomes of the election it all the same helped the ruling party to identify itself to voters as one they could rely on during uncertain times.

Exploiting the ineffectiveness of the Kenyan political situation in which a coalition of opposition parties successfully broke an “African political taboo” that a ruling party never loses an election, CCM-Tanzania’s ruling party-has frequently used the media during elections to tell voters that bringing an opposition into power could not solve the country’s problems, referring to the Kenyan situation. The pro-CCM media has also been telling Tanzanians that regardless of how bad they think of CCM, it still is the “devil they know”, and therefore should never try a political experience of voting an opposition party into power. Many would agree despite proving wrong in some African countries such as Ghana the trick has been very successful.

The pro-government media in Sudan has also been effective in swaying public opinion in favour of President Al-Bashir when he a warrant was made by the International Criminal Court in The Hague accusing him of being responsible for genocide in the Darfur region. The media working under the directives of the Sudanese government portrayed the warrant as an attempt by the West to re-colonise Africa.

Although public opinion could also shape opinion in the media, it is rather for commercial purposes than public interest. When The Daily Mail ran an exclusive story about an “illegal immigrant” employed by Baroness Scotland, it fair to believe that based on its strong anti-immigration stance, it did not do so to sympathise with the plight faced by those who make a choice of being in the UK illegally but rather to amass pressure to force the peer out of office.

If we agree that although the media the primary source of information broadcasted or published by the media comes from the public, and therefore a need to see the media serves the interest of the public, it still remains true that the flow information has usually been from the media to the public in terms of news consumption. The point here is that the media collects information from the public not for final consumption but rather for the public consumption. It is on such views that I argue that it is the media which shapes public opinion, and not vice versa.


5 Oct 2009


KWANGU,MISINGI MIKUU YA NYERERE ILIKUWA UJENZI WA JAMII YENYE USAWA NA INAYOTHAMINI UTU WA BINADAMU.UHURU BILA USAWA NI POROJO.UMOJA KATIKA LINDI LA UMASIKINI NI SAWA NA USINGIZI WA PONO KWENYE UTANDO WA BUIBUI.NA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA HAYAWEZI KUPATIKANA KATIKA SIASA ZA KUKUMBATIA MAFISADI SAMBAMBA KUKEMEA WAPAMBANAO NA UFISADI,KUTOJUA VIPAUMBELE VYA NCHI,NA KUENDELEZA AHADI ZA MAENDELEO ILHALI ZILE ZA AWALI HAZIJATEKELEZWA.

JK AMEKUMBUKA MISINGI YA MWALIMU.MSOME KATIKA HABARI IFUATAYO:

Mwandishi Maalum, Mwanza

RAIS Jakaya Kikwete ametaja misingi mikuu mitatu iliyowekwa na Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere katika kulijenga taifa la Tanzania, misingi ambayo rais alisema ni kumbukumbu yao kuu kwa kiongozi huyo wa harakati za Uhuru wa Tanganyika.

Rais Kikwete aliwashangaa Watanzania ambao wanabeza Uhuru wa Tanzania na kufurahia wakati jina la Tanzania linaposhambuliwa na wageni.

Aliitaja misingi hiyo mikuu kuwa ni uhuru, umoja wa taifa la Tanzania, na safari ya kujenga maisha bora kwa kila Mtanzania iliyoanza hata kabla ya Tanganyika kupata uhuru wake rasmi Desemba 9, 1961.

Rais Kikwete alisema hayo mjini Mwanza juzi alipozungumza na vijana wa CCM ambao wanaanza safari ya kuelekea kijijini Butiama mkoani Mara, ikiwa ni matembezi ya kumuezi Mwalimu Nyerere ambaye alifariki miaka 10 iliyopita baada ya kuugua saratani ya damu.

Mwalimu Nyerere alifariki Oktoba 14, 1999 akiwa amelazwa hospitali ya St Thomas jijini London, Uingereza.

Vijana 166 kutoka mikoa yote ya Tanzania wanashiriki katika matembezi hayo ya siku 10 ambayo yatapitia njia ambayo Mwalimu Nyerere alitembea mwaka 1967 katika kuunga mkono na kuhamasisha Azimio la Arusha.

Kauli mbiu ya matembezi hayo ni “Uhuru na Kazi” na miongoni mwa mambo ambayo vijana hao watafanya njiani ni kukarabati Shule ya Msingi ya Mwisenge ambako Mwalimu Nyerere alipata elimu yake ya msingi.

Rais Kikwete alisema kuwa urithi mkuu ambao Mwalimu aliwaachia Watanzania ni misingi hiyo mikuu ambayo imeendelea kulifanya Taifa la Tanzania kuwapo na kuwa imara.

Rais Kikwete alisema kuwa kila taifa duniani lina waasisi wake ambao wanastahili kuendelea kukumbukwa siyo tu kwa uasisi pekee, bali pia kwa mambo ambayo waliyasimamia, waliyaamini na waliyajenga.

"Wamarekani wanaye George Washington… sisi tunaye Mwalimu Julius Kambarage Nyerere… na kila nchi ina muasisi wake ambaye anakumbukwa kwa aliyoyasimamia," alisema JK.

"La kwanza la kumkumbuka Mwalimu ni uhuru wa nchi yetu. Huyu alikuwa ni kiongozi aliyeambiwa achague kati ya siasa ama kazi ya ualimu… huyu mzee wetu akachagua siasa na utumishi wa umma bila hata kujua atakula nini.

"Akachagua kupigania uhuru wa nchi yetu. Kama mnavyojua nyote hii kazi ya siasa ni kamari... unakwenda kugombea ukijua kuna kupata ama kukosa... lakini yeye alifanya uamuzi sahihi wa kupigania uhuru,"

Rais Kikwete alisema kuwa uhuru siyo mipaka bali ni heshima ya nchi na ndiyo maana Tanzania haitasita kumkabili yoyote ambaye atajaribu kuchezea uhuru huo.

Alisisitiza: "Mwaka 1978 yule msanii na profesa wa historia na jiografia, Idi Amin alivamia nchi yetu… na sisi tukamfurumusha ili kulinda uhuru wetu na wako wenzetu ambao walipoteza maisha yao kwa ajili ya kulinda uhuru wetu. Wamelala Kaboya (mkoani Kagera) na tutaendelea kuwaenzi kwa sababu walijitolea kulinda uhuru wetu."

Rais Kikwete pia aliwashangaa watu wote ambao wanafurahia wakati heshima ya Tanzania inapobezwa na wageni.

"Uhuru siyo mipaka kama nilivyosema. Uhuru ni heshima ya taifa letu. Wako wale wenzetu wanaofurahi wakati wageni wanaposhambulia nchi yetu. Ni wajibu wetu sote kuhakikisha kuwa uhuru wetu hauchezewi na mtu yoyote,"alisema.

Kuhusu umoja wa taifa, Rais Kikwete alisema Mwalimu alihakikisha kuwa uhuru wa nchi unazaa umoja ili nchi iwe moja na isigawanyike vipande vipande kwa sababu yoyote ile.

"Aliondoa viashiria vyote vya kuvunja umoja wa taifa tokea mwanzo kabisa. Aliondoa uchifu ili kuondoa nguvu za ukabila. Alitambua hatari ya dini na akataifisha shule zote za dini ili vijana wetu waelimishwe na kulelewa kama vijana wa taifa moja na siyo vijana wa dini tofauti,"alisema Kikwete.

Rais Kikwete alisema kuwa hata kabla ya uhuru, Mwalimu alitambua kuwa ili uhuru na umoja viweze kudumishwa ni lazima wananchi wake wapate maisha bora na ndiyo maana akawatambua maadui wakuu watatu – ujinga, maradhi na umasikini- na njia za kukabiliana na maadui hao.

CHANZO:
Mwananchi

BAADHI WANAHOJI KUHUSU MANTIKI YA UHURU ALIOPIGANIA BABA WA TAIFA NA WENZAKE.TULIMKIMBIZA MKOLONI ILI TUJITAWALE NA KUFAIDI RASLIMALI ZETU KWA HAKI NA USAWA.JAPO SIO EXCUSE,LAKINI MKOLONI HAKUTUJALI KWA VILE HAKUWA MTANZANIA.LEO HII WANAOTUTENDA VIBAYA ZAIDI YA WAKOLONI NI WATANZANIA WENZETU,WENGI WAO WAKIWA WALIOSOMOSHWA KWA SHIDA NA FEDHA ZA WATANZANIA WENZAO.KUNDI JINGINE NI LA MABWANYENYE WALIOPTA URAIA KWA VIJISENTI VYAO NA WAKOLONI -MAMBOLEO WALIOREJEA KWA JINA LA WAWEKEZAJI.NYERERE HAKUPIGANIA UHURU ILI WAGENI WAJE NA DOLA MOJA NA KUONDOKA NA MAMILIONI YA DOLA,AU AKINA LOWASSA KUTUINGIZA MKENGE KWENYE RICHMOND,NA USANII MWINGINE WA KISIASA.

UHURU PASIPO UONGOZI BORA NI SAWA NA KUWA NA VOGUE LENYE DEREVA MLEVI AU KIPOFU;LITATUMBUKIA MTARONI KAMA SI KUPORWA NA MAJAMBAZI.UHURU ILHALI TUMEBANWA NA NIRA ZA MAFISADI NI UTANI MBAYA KWA WALIOPIGANIA UHURU WA NCHI YETU.WEZI WA KAGODA WAMEHIFADHIWA HADI LEO,MASHIRIKA YA UMMA YAMEGEUKA KICHAKA CHA WATU KUHUJUMU KISHA WABADILISHIWE (REJEA MATTAKA NA ATCL),WAZEMBE WANAENDELEA KULINDWA KWA VILE TU KUWABADILISHA KTATHIBITISHA MAPUNGUFU YA ALIYEWATEUA IN THE FIRST PLACE,NA HADITHI NYINGINE ZA KUSIKITISHA.

HATUKUPIGANIA UHURU KUPATA HESHIMA FEKI MACHONI MWA JUMUIYA YA KIMATAIFA BALI AMANI NAFSINI NA MIILINI MWETU KAMA WATANZANIA.


AONDOLEWA JUKWAANI, ASEMA NI UCHOVU WA SAFARI

Frederick Katulanda, Mwanza na Exuper Kachenje, Dar

RAIS Jakaya Kikwete jana alizidiwa ghafla wakati akihutubiwa waumini wa Kanisa la African Inland (AICT) kwenye Uwanja wa CCM Kirumba na kulazimika kukatisha hotuba yake na baadaye kuondolewa uwanjani akiwa amebebwa na walinzi wake kabla ya kiongozi huyo kurejea jukwaani muda mfupi baadaye.

Rais Kikwete, ambaye alifika mkoani hapa akitokea Arusha ambako alifungua mkutano wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola, ikiwa ni siku chache tangu atoke Marekani kuhudhuria mkutano wa Baraza la Umoja wa Mataifa, alikumbwa na mkasa huo majira ya saa 6:29 mchana.

Rais Kikwete alikatisha hotuba yake wakati akianza kuelezea suala la kudumisha amani upendo na mshikamano, akisema:"Wakati nilipokuwa nikipita kuomba ridhaa yenu kuongoza nchi hii, kote nilikopita niliomba kudumishwa kwa amani upendo na mshikamano…"

Ghafla alinyamaza na baadaye ikasikika sauti kutoka kwenye kipaza sauti chake ambayo inaonekana kuwa ya mlinzi wake, iliyosema "Kakae".

Baadaye Rais Kikwete aliuliza kwa sauti akisema "naweza kuhutubia nikiwa nimekaa"na kujibiwa na mwenyeji wake, Askoku Mkuu wa AICT, Daniel Nungwana kuwa "unaweza kukaa", jibu ambalo lilifanya aondoke kwenye eneo ambalo alikuwa akitumia kuhutubia jukwaani na kwenda kukaa meza kuu ambayo ilikuwa umbali wa takriban mita mbili.

Mara baada ya kukaa na vipaza sauti kurekebishwa ili aendelee na hotuba, Rais Kikwete alitamka kwa sauti ya juu iliyoonyesha kuwa afya yake si nzuri wakati alipoeleza kuwa “nimechoka sana kwa sababu ya safari” na kisha kuendelea na hotuba yake, lakini sauti yake ilizidi kubadilika na kuwa inayokwaruza na akakatisha hotuba yake, akiacha waumini wakinong’ona.

Baadaye Rais Kikwete, ambaye aliwahi kupoteza nguvu jukwaani wakati akihitimisha kampeni zake za uchaguzi kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam, alinyamaza na kutulia huku akiwa anaangalia upande wa mashariki, shingo yake ikilalia bega la kushoto na kichwa kuegemea kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro.

Dakika chache baadaye (saa 6: 35), mlinzi wake ambaye alisimama nyuma ya kiti chake, alimtikisa kwa muda, lakini rais hakuonekana kujibu kitu na ndipo walinzi wake na maofisa wengine wa usalama walipomzunguka kumkinga kuzuia watu wasimuone na baadaye kumbeba juu na kumpeleka kwenye chumba maalumu kilicho eneo la jukwaa kubwa la Uwanja wa CCM Kirumba.

Wakati akiingizwa chumbani humo, magari yote ya msafara wake yalielekea nje ya uwanja huo na kuegeshwa nje ambako kuna mlango, jambo lililoashiria kuwa iwapo afya yake isingetengemaa, angetolewa kupitia mlango huo na kukimbizwa hospitali.

Wakati harakati hizo zikiendelea, Kandoro alirejea jukwaani na kuelekea kwenye kipaza sauti. Kandoro aliwataka wananchi kutulia kwa maelezo kuwa hali ya rais ni nzuri na kwamba amepumzika kwa muda kutokana na uchovu.

"Nawaomba mtulie, Rais wetu amepumzika tu kwa muda kutokana na uchovu wa safari na yuko salama. Nawahakikishia kuwa yuko salama na huu ni uchovu tu kwani amesafiri sana kutoka nje ya nchi hadi Arusha na baadaye kuja hapa Mwanza. Hivi sasa amepumzika na atarudi hapa," alieleza Kandoro.

Kikwete alirejea jukwaani majira ya saa 6: 45 akitembea bila ya msaada wa walinzi ambao walikuwa nyuma yake na kwenda kukaa kwenye meza kuu ambako aliomba kipaza sauti na kusema maneno machache.

"Ndugu wachungaji na waumini, nguvu imerudi; nataka kutumia fursa hii kuzindua mfuko wenu maalumu; nami nachangia shilingi milioni moja,"alisema Kikwete na kuamsha kelele za shangwe na vigelegele.

Baadaye ratiba ya sherehe hizo iliendelea kwa harambee ya kuchangia mfuko maalumu wa watu wenye ulemavu wa ngozi ambao aliombwa na Askofu Nungwana kuchangia kwa kuuzindua kabla ya hotuba yake.

Askofu Musa Mwagwesela aliwatangazia wananchi kuwataka wajitokeze kuchangia mfuko huo kwa kipindi cha dakika tano, ili wamruhusu rais aondoke uwanjani hapo. Alisema ameombwa kufanya hivyo na watu wa usalama.

Zoezi hilo la wananchi na watu mbalimbali kuchangia mfuko huo liliendelea na majira ya saa 7:08 mchana Rais Kikwete aliombwa na mwenyeji wake Askofu Daniel Nungwana kuwashukuru wananchi kabla ya kuondoka.

Aliposimama Rais Kikwete alisema: "Kwanza nawaombeni radhi kwa mshtuko niliopata. Lakini umenitokea kwa ubishi wangu; ni kwa ajili ya uchovu wa safari."

Kikwete aliendelea kusema: "Nimerudi juzi saa 7:00 usiku. Nilikuwa Arusha kwenye mkutano wa bunge, walinishauri nipumzike nikasema ahaa hawa nao ngoja niende tu; waliniambia tunaona uchovu mwingi, nikasema hawa nao ahaa… nitaweza tu; nimekuja hapa… siku nyingine nitawasikiliza wanaonishauri."

Hii si mara ya kwanza kwa Rais Kikwete kukumbwa na mikasa hadharani. Aliishiwa nguvu ghafla wakati akihutubia mkutano wa mwisho wa kampeni kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2005. Alitolewa viwanja vya Jangwani na kwenda kupatiwa matibabu.

Lakini saa chache baadaye CCM ilitoa taarifa kuwa afya ya mgombea wake wa kiti cha urais ni nzuri na kwamba, mkasa huo ulitokana na rais kuwa alifunga na uchovu wa safari nyingi za kampeni hizo.

Alikumbana na mkasa mwingine mjini Mwanza Oktoba 15, 2005 wakati akiwa kwenye kampeni za kuwania kuingia Ikulu. Alikuwa akisimikwa kuwa mtemi wa kabila la Wasukuma kabla ya mtu mmoja, Lucas Omahe Garani, 34, ambaye ni mganga wa jadi, kujipenyeza hadi jukwaani na kujaribu kumvuta miguu, lakini akawahiwa na watu waliomzunguka Kikwete.

Alikuwa akisimikwa utemi na kikundi cha waganga kutoka Kituo cha Utamaduni wa Kisukuma cha Bujora ambacho kinamilikiwa na Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Mwanza.

Garani, ambaye kwa sasa anatumikia kifungo cha miaka 13 jela kutokana na kosa hilo, alidai kuwa alifanya kitendo hicho kupinga uamuzi wa kikundi hicho cha waganga kumsimika chifu hadharani na mchana, kitu ambacho alidai kinakiuka mila za kisukuma.

Garani mkazi wa Mtaa wa Nyakabungo jijini Mwanza alikuwa anafanya kazi ya kutunza bustani ya ofisi za Dayosisi ya Victoria Nyanza ya Kanisa la Anglikana.

Kabla ya kuzidiwa na kukatisha hotuba yake jana, Rais Kikwete alilipongeza kanisa hilo kwa kutimiza miaka 100 na kwa kutoa huduma mbalimbali katika sekta ya afya na elimu.

Alisema serikali inatambua mchango wa mashirika ya dini na kusisitiza kuwa unapotaja maendeleo ya nchi hii, huwezi kukwepa mchango huu wa mashirika ya dini.

Hali haikuwa shwari kwa wananchi waliokuwa kwenye uwanja huo licha ya matangazo ya Kandoro kuwa afya ya rais ni nzuri. Kulikuwa na minong'ono mingi kutokana na kila mmoja kuuliza nini kimetokea kabla ya Askofu Mussa Magwesela kuwaambia waumini kuanza maombi maalumu kumuombea rais kutokana na hali iliyomkumba ghafla.

"Waumini wote naomba tumuombee mpendwa rais wetu; tumuombee Mungu amrejeshee afya yake,"alisema na mara moja waumini wakaanza maombi ya mmoja mmoja.

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa baadaye na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ilidai kuwa Rais Kikwete alilazimika kupumzika kwa dakika chache "baada ya kumaliza hotuba yake” katika sherehe hizo kutokana na kuzidiwa na uchovu.

"Nguvu imerudi…napenda sasa kuchukua nafasi hii kuzindua rasmi uchangiaji wa shughuli za kanisa lenu na mimi naanza na mchango wa Sh 1,000,000," taarifa hiyo ya Ikulu ilimkariri Rais Kikwete ikieleza kuwa baada ya mapumziko mafupi alirejea na kuendelea kushiriki shughuli hiyo.

Ilieleza kuwa Kikwete alianza kusikia uchovu wakati akisoma hotuba yake mbele ya maelfu ya waumini wa Kanisa hilo.

Taarifa hiyo inaeleza: "Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumapili, Oktoba 4, 2009, amelazimika kupumzika kwa dakika chache katika chumba cha mapumziko kwenye Uwanja wa Kirumba mjini Mwanza mara tu baada ya kumaliza hotuba yake wakati wa sherehe za miaka 100 tokea kuanzishwa kwa Kanisa la African Inland (AICT) nchini Tanzania.

"Mhe. Rais amelazimika kupumzika kutokana na kuzidiwa na uchovu kufuatia shughuli nyingi mfululizo katika siku za karibuni. Baada ya mapumziko hayo, Mhe. Rais aliendelea kushiriki katika shughuli hizo hadi mwisho wa shughuli hiyo ya AICT."

Taarifa hiyo inaeleza kuwa Kikwete alikiri kupata matatizo hayo, akisema kuwa yalitokana na kutofuata ushauri wa wasaidizi wake waliomtaka apumzike baada ya kurejea kutoka Marekani. Taarifa hiyo imeeleza kuwa washauri walimtaka asiende Arusha kufungua mkutano huo wa mabunge na baadaye kumzuia asiende Mwanza.

Taarifa hiyo ya Ikulu inasema: "Kwa kweli mshtuko huu wa leo ni matokeo ya ubishi wangu. Nilishauriwa na wasaidizi wangu nipumzike baada ya kurejea nyumbani kutoka Marekani. Niliambiwa nisiende Arusha ama kuja hapa. Lakini nikakataa. Siku nyingine nitawasikiliza zaidi."

Taarifa hiyo ya Ikulu imeeleza kuwa rais amekuwa na shughuli nyingi katika miezi kadhaa iliyopita na kwamba hakuwahi kupumzika kutokana na ratiba ya shughuli hizo kufuatana.

Ilisema ndani ya siku 15 zilizopita Kikwete alikuwa New York, Marekani kuhudhuria Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN), juzi na jana alikuwa mjini Arusha na jana na leo mjini Mwanza alipokutwa na tukio hilo.

Taarifa hiyo ilikumbusha kuwa Septemba 20 Rais Kikwete aliondoka kwenda nchini Marekani kuhudhuria Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) na tangu hapo hajapumzika.

Kwa mujibu wa Ikulu Kikwete alirejea nchini kutoka Marekani saa 7:00 usiku wa kuamkia Ijumaa baada ya kusafiri kwa zaidi ya saa 19 na Ijumaa asubuhi alisafiri kwenda Arusha kufungua mkutano huo wa 55 wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola.

Wakati huohuo, Ofisi Binafsi ya Rais (OBR) imetangaza kuwa itaangalia upya ratiba ya rais kwa namna ya kumpunguzia mlundiko wa shughuli hata kama yeye binafsi ni “mpenzi mkubwa wa kuchapa kazi na kutumikia wananchi”.

OBR ndiyo husimamia upangaji ratiba za rais.

CHANZO: Mwananchi

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.