20 Feb 2011








Picha hizi za kutisha zinajieleza zenyewe.Hakuna maelezo yanayotosheleza kueleza kwa ufasaha kuhusu janga hili.Lakini kwa vile kamwe hatutoelezwa chanzo cha milipuko ya mabomu huko Gongo la Mboto,kama ambavyo hatukuelezwa chanzo cha milipuko iliyotokea mwaka juzi huko Mbagala,ni muhimu kwa kila Mtanzania kudai haki yake ya kikatiba ya usalama wa maisha yake.


Ni wazi kuwa wahusika wanapata jeuri ya kutangaza hadharani kuwa hawatajiuzulu kwa vile wanafahamu bayana kuwa aliyewateua kushika madaraka hayo ni mzembe,dhaifu na asiyejua kinachoendelea.Kwa lugha nyingine,YUPO YUPO TU.

Nilighadhibika sana niliposoma kauli ya Mkuu wa Usalama na Utambuzi wa JWTZ Brigedia Jenerali Paul Meela kuwa hakuna atakayejiuzulu kwa sababu uongozi jeshini sio nafasi za kisiasa.Haya ni matusi kwa Watanzania.Kwani Amatus Liyumba alipohukumiwa kwenda jela kwa ubadhirifu wa fedha za umma hapo Benki Kuu alikuwa mwanasiasa?

Kwa akili finyu ya Brigedia Meela,ni wanasiasa pekee wanaopaswa kuwajibika wanapoboronga.Lakini kwa vile kamanda huyo alikuwa anamwakilisha Mkuu wa Mwajeshi Jenerali Davis Mwamunyange,yayumkinika kuamini kuwa kauli hiyo pia ni msimamo wa mkuu huyo wa majeshi.

Tuliowahi kupitia mambo ya kijeshi tunafahamu kasumba ya jeuri na u-mungu mtu ilivyokomaa vichwani mwa viongozi jeshini.Hii inaimarishwa zaidi na utaratibu wa kawaida jeshini kwamba amri ina mwelekeo mmoja tu: kutoka juu kwenda chini,na haihojiwi.

Kwahiyo,wakati Kamanda Meela anaongea na waandishi wa habari,akilini mwake alikuwa kama anaongea na makuruta ambao ni dhambi kuu kwao kuhoji lolote lile.Na kwa vile Meela alikuwa anawakilisha mabosi wake,mtu pekee ambaye angeweza kumwadabisha ni Amiri Jeshi Mkuu,Rais Jakaya Kikwete.

Lakini takriban miezi mitano tangu baadhi ya Watanzania wenzetu watusaliti kwa kumrejesha Kikwete madarakani (tukiweka kando uchakachuaji wa Tume ya Uchaguzi),naamini kila Mtanzania anafahamu fika kuwa ombwe la uongozi wa taifa lililojiokeza wakati wa awamu ya kwanza ya utawala wa Kikwete,sio tu limezidi kukua bali pia limeifanya Tanzania kuishi kwa kutegemea kudra za Mwenyezi Mungu.Ni kama hatuna Rais wala serikali.

Na taasisi muhimu kwa ustawi wa taifa kama Idara ya Usalama wa Taifa ziko katika usingizi mzito unaosababishwa zaidi na marupurupu makubwa licha ya utendaji kazi duni na wa chini ya kiwango.Sijui kama watu hawa wanasumbuliwa na mwenendo wa nchi yetu,kwani ingekuwa hivyo tusingeshuhudia mazingaombwe ya kuruhusu mtu kama Edward Lowassa kuwa Mwenyekiti wa kamati nyeti ya bunge ya Ulinzi na Usalama,leave alone ishu kama za Dowans,EPA,nk.

Na kwa kuonyesha watu wa Usalama wamegubikwa na usingizi,wameshindwa hata kumshauri bosi wao Kikwete kuwa safari yake kwenda Mauritania kusaka ufumbuzi wa mgogoro huko Ivory Coast,sio mwafaka wakati huu wa majonzi makubwa kwa Watanzania.Kikwete na washauri wake wanajifanya hawajui kuwa janga la Gongo la Mboto linawagusa zaidi Watanzania kuliko matatizo ya wa-Ivory Coast.Ni rahisi kwa baadhi ya watu kuhisi kuwa Kikwete anakwepa majukumu na kuamua kwenda kuzurura huko ng'ambo.

Tukirejea kauli za wanajeshi wetu,Brigedia Jenerali Meela anasema taarifa za milipuko iliyopita ni kwa matumizi ya jeshi.Kwani JWTZ limegeuka jeshi la mtu binafsi?Sote tunafahamu kuwa hilo ni Jeshi la Wananchi wa Tanzania.Sasa iweje madudu wanayofanya na yanayopelekea kuwaathiri wananchi wasio na hatia yaishie kuchungiuzwa na wao wenyewe kisha findings nazo zibaki kuwa siri yao?

Jibu la maswali haya na mengineyo mengi ni rahisi:Rais tuliyenae ni dhaifu na asiye na uwezo wa kuwawajibisha hata wale aliowateua yeye mwenyewe.Sasa kwa wanaotegemea Kikwete anaweza kudili na maharamia kama wa Dowans (ambao hakuwateua,na sanasana wanamdai fadhila) watakuwa wana jibu la msingi kuhusu kusuasua kwake kuwashughulikia mafisadi.

Picha kwa hisani ya Rev Masanilo wa Jamii Forums


Tunaendelea kuwaletea updates za tukio la milipuko ya mabomu jijini Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali,hadi sasa inakadiriwa zaidi ya watu 20 wamepoteza maisha katika tukio hilo.

Tovuti ya Shirika la Habari la Uingereza (BBC) Idhaa ya Kiswahili inaripoti:
Hali ya taharuki imetanda mji wa Dar Es Salaam, nchini Tanzania, huku wakaazi wakiamka kuomboleza vifo vya zaidi ya watu kumi na zaidi ya wengine 60 kujeruhiwa kufuatia milipuko iliyotokea kwenye ghala la kuhifadhi silaha za kijeshi, lililo karibu na uwanja wa kimataifa wa ndege.

Wakaazi wa eneo la Gongo la Mboto lililo karibu na ghala hilo wamekesha nje baada ya makaazi yao kubomoka kutokana na mtikisiko wa milipuko hiyo iliyodumu kwa saa kadhaa. Milipuko hiyo ilisikika kwa umbali wa zaidi ya kilomita ishirini kutoka kituo hicho cha kijeshi.

Inaarifiwa kuwa milipuko hiyo ilianza mwendo wa saa mbili usiku.

Msemaji mmoja wa jeshi amesema kuwa kuna watu wengi ambao wamepoteza maisha yao lakini idadi kamili haijajulikana.

Kamanda wa polisi jijini Dar-es-Salaam, Suleiman Kova, ametoa wito kwa raia wa mji kuwa huo watulivu huku maafisa wa ulinzi wakiendelea na mikakati ya kurejesha hali ya uthabiti.

Kova amesema uchunguzi wa awali umebainisha kuwa mlipuko huo ni ajali na wala sio shambulio la kigaidi.

Ni hii mara ya pili kwa milipuko kama hiyo kutoka jijini Dar es Saalam katika kipindi cha miaka miwili iliyopita mwaka wa 2009 zaidi ya watu ishirini waliuawa na wengine 300 kujerihiwa

Kadhalika,Rais Jakaya Kikwete amewaasa wananchi kuepuka maelezo ya "redio mbao" na badala yake wasubiri taarifa rasmi kutoka serikalini na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).Hata hivyo inawezekana Kikwete hajajiuliza kwanini wananchi wanategemea taarifa za "radio mbao" kwani ni dhahiri kuwa penye ombwe la taarifa rasmi,wananchi wanalazimika kugeukia vyanzo vya habari visivyo rasmi.



Hadi muda huu,hakuna kiongozi yeyote aliyewajibika au kuwajibishwa.Watanzania wanatarajia kuona Waziri wa Ulinzi Dkt Hussein Mwinyi,Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama,Jenerali Davis Mwamunyange na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi hilo,Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo,wakiwajibishwa mara moja.Lakini kwa namna tunavyofahamu udhaifu wa Rais Kikwete katika kuwashughulikia watendaji wake,kuna uwezekano mkubwa wa Dkt Mwinyi,Mwamunyange na Shimbo kuendelea na madaraka yao

Kilicho wazi ni kuwa serikali itapoteza fedha za walipa kodi kuunda tume kama ile ya milipuko ya Mbagala mwaka 2009,na kisha ripoti ya tume hiyo kuishia kuwa karatasi za kufungia vitafunio.

Japo hakuna anayetaka kutumia janga hili la milipuko kama mtaji wa kuwahukumu watawala wetu,lakini kuna umuhimu mkubwa wa kuunganisha matukio yaliyopita na tukio hili na uwajibikaji duni wa serikali iliyopo madarakani.

Ni muhimu pia kutafakari dhamira ya serikali kuilipa kampuni ya kitapeli ya Dowans,sambamba na mpango wa kuwapatia wabunge shilingi bilioni 90 kila mmoja,huku mipango endelevu ya kuepusha na kukabiliana na majanga ikipuuzwa.

Ukweli ulio bayana ni kwamba serikali ya Kikwete na CCM yake haisumbuliwi na hali ya kutokuwa na uhakika na usalama wa wananchi.

Endelea kutembelea tovuti hii kwa habari na uchambuzi zaidi kuhusu tukio hili la kusikitisha.

16 Feb 2011




Habari kutoka Dar es Salaam zinaeleza kuwa milipuko kadhaa imetokea maeneo ya Gongo la Mboto.Hata hivyo habari nyingine zinadai kuwa milipuka hiyo imetokea maeneo ya Kisarawe

Bado hakuna taarifa rasmi kuhusu eneo na chanzo cha milipuko hiyo japokuwa habari zilizopo zinadai milipuko hiyo imetokea kwenye kambi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

Mtandao wa Jamii Forums umemnukuu Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Brigedia Jenerali Abdulrahman Shimbo akisema "Hali ni mbaya Kikosi namba tano maghala yamelipuka ni hatari, watu wahame, maghala yako karibu karibu sana, tunaomba wananchi wahame sasa hivi, tunajitahidi kuzuia moto unaotokana na hilo unaweza kwenda mbali sana hadi Kilomota kumi, wananchi walioko karibu na maghala ya kikosi Gongo la Mboto wasogee mbali sasa hivi."

Hadi sasa hakuna taarifa kamili kuhusu idadi ya majeruhi japokuwa picha zilizotumwa na baadhi ya watumiaji wa huduma ya mtandaoni ya Twitter zinaonyesha majeruhi wakiwa katika hali mbaya



Tukio hili la kusikitisha linatokea wakati Serikali ikiwa haijaweka hadharani ripoti ya vyanzo vya milipuko iliyotokea kwenye Kambi ya JWTZ Mbagala mwezi Aprili na Mei mwaka juzi.

Wakati huo,aliyekuwa Waziri wa Ulinzi Dokta Hussein Mwinyi aliahidi kuwa angewajibika iwapo ingebainika amezembea.Lakini simulizi hizo ziliishia hapo baada ya vile Serikali kupitia Wizara inayoongozwa na Mwinyi kuamua kuiweka ripoti hiyo 'kapuni'

Wakati tovuti hii inaendelea kukusanya habari za uhakika kuhusiana na milipuko hiyo ni muhimu kwa Watanzania kudai haki zao za msingi za usalama wa maisha yao na mali zao.Haiyumkiniki kuona 'intelijensia' ya vyombo vya dola ikiwa na 'ufanisi mkubwa' katika kukandamiza haki za kikatiba za wananchi lakini ikishindwa kuepusha majanga kama haya.

Upatikanaji wa taarifa sahihi unakuwa mgumu hasa kutokana na vyombo 'rasmi' vya habari nchini Tanzania kutowajibika ipasavyo kuwajulisha wananchi kinachoendelea.Tovuti zote za magazeti 'makubwa' hazina breaking news hadi wakati naweka habari hii.

(Video kwa hisani ya Dedichjr na Picha kwa hisani ya Jamii Forums)



Pichani ni Mbunge John Komba wa CCM 'akiwa makini' kwa kuuchapa usingizi Bungeni Dodoma.Hata huyu naye anastahili 'zawadi' ya milioni 90?

Hivi kweli inaingia akilini kusikia kwamba Serikali ya Kikwete ina mpango wa kuwapatia wabunge shilingi milioni 90 kila mmoja "kwa sababu inazojua yenyewe?Majuzi tu tumesikia habari kwamba Serikali hiyo hiyo inatembeza bakuli kwa wahisani ili wasaidie 'kuokoa jahazi' la hali mbaya ya Bajeti ya 2010/11.

Lakini pia tunakumbuka Kikwete alivyokuwa mkali kwa watumishi wa umma walipotishia kugoma kushinikiza kulipwa mishahara inayoendana na hali halisi ya maisha.Sasa kama ilishindikana kuwalipa wafanyakazi wa umma mishahara bora haya mabilioni ya kuwazawadia wabunge yanatoka wapi?

Naona kuna kila jitiahada za watawala wetu kukaribisha yanayojiri huko Arabia na Mashariki ya Kati.Japo inauma kuona mabilioni ya shilingi yakizawadiwa kwa waheshimiwa kama huyo anayechapa usingizi,lakini hatua hiyo inaweza kuwa blessing in disguise kwa maana kwamba huenda ikawahamasisha Watanzania kuiga mifano ya 'walalawima' wenzao wa Tunisia na Misri,na hatimaye kufanikiwa kuleta 'Uhuru wa Pili' (wa kwanza ulikuwa wa kumwondoa mkoloni.Wa pili ni wa kuwaondoa mafisadi)



My sista Jestina,a top-notch fashion blogger,with her exquisitely beautiful daughter Princess Iman .

.



15 Feb 2011


Hatimaye mmoja wa wanasoka mahiri kabisa duniani,Ronaldo wa Brazili,ameamua kuundika madaluga.Staa huyo mwenye kipaji cha hali ya juu ametangaza kustaafu rasmi soka.

Katika makala hii nawaletea video za kumbukumbu ya nguli huyo wa kandanda.Picha zote hizo ni kwa hisani ya gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza






















14 Feb 2011


Leo ni Siku ya Mtakatifu Valentine,maarufu kama Siku ya Wapendanao,au Valentine's Day kwa kimombo. Pengine ni vema kuadhimisha siku hii kwa kutafakari umuhimu wa upendo.

Binafsi,si muumini mzuri wa siku zinazoambatana na matukio.Kwa mfano,mara nyingi huwa naadhimisha siku yangu ya kuzaliwa kwa sala na tafakuri ya miaka iliyopita na ijayo,Mungu akinijalia.Kwa wengine,siku ya kuzaliwa ni wakati wa kuingia gharama zisizo na umuhimu kwa sherehe kubwa zinazowaacha wakiwa na hali ngumu baadaye.Japo ni muhimu kufanya maadhimisho ya siku muhimu kama ya kuzaliwa lakini kuna umuhimu gani kama siku hiyo inabaki kuwa "siku muhimu" tu pasipo kuangalia wapi umetoka,ulipo na unakoelekea?

Na katika mantiki hiyohiyo,Siku ya Wapendanao inakuwa tu na umuhimu kama upendo utatafsiriwa kwa dhamira na vitendo.Kuna umuhimu gani wa kuadhimisha Siku ya Wapendanao kwa kadi za gharama na vinywaji ilhali umewasahau wanaohitaji upendo wako?

Wengi tunaelewa namna baadhi ya wenzetu wanavyoiogopa siku hii kutokana na kuwa na ma-Valentine wengi.Na miongoni mwa hawa ni wale wanaoadhimisha siku hii na "nyumba ndogo" huku wakiacha visingizio kwa wapenzi wao halisi.Hali hiyo inapoteza maana nzima ya siku hii.Haiwezekani mtu kudai anaadhimisha Siku ya Wapendanao kwa kumsaliti mpenzi wake.

Vinginevyo,nawatakia Siku njema ya Wapendanao nikiamini kuwa maadhimisho ya siku hii yatakuwa ya dhamira zaidi kuliko vitendo pekee.

13 Feb 2011



Kumekuwa na tetesi za muda mrefu kuwa hali ya uchumi wa Tanzania ni mbaya.Hata hivyo,kama ilivyozoeleka,wahusika serikalini wameendelea kuwanyima Watanzania haki yao ya msingi ya kufahamishwa hali ya uchumi wa taifa lao. 

Hivi karibuni Gavana wa Benki Kuu,Profesa Benno Ndulu,alizungumza na waandishi wa habari kuhusu ubora wa noti mpya.Licha ya kuonekana kufahamu kuwa wananchi hawaridhishwi na kiwango duni cha noti hizo,Gavana Ndulu alizitetea kwa nguvu zote.Akemee ili ifahamike kuwa 'zimechakachuliwa'?

Akiichambua hali ya uchumi, gavana huyo alisema kwa sasa hali ya uchumi ni nzuri na kwamba nchi ina uwezo wa kulipa huduma kwa miezi sita bila kutegemea sehemu yoyote.Lakini katika kile kinachoweza kiashirikia kiwa kauli hiyo ilikuwa ya kisiasa zaidi kuliko ya kitaalamu,Gavana alidai kuwa mwenye dhamana ya kueleza athari za mgao wa umeme kwa uchumi ni Waziri wa Nishati na Madini.Huku sio tu kukwepa majukumu bali mwendelezo wa danadana za kibabaishaji zinazoeleka kuunda mfumo wa utendaji wa viongozi wengi wa taasisi za umma.Na kwa vile 'Mteuzi Mkuu' Serikalini,yaani Rais,anaonekana kama yupo usingizini kubaini mapungufu ya baadhi ya watendaji aliowateua,ni dhahiri utendaji kwa mfumo wa 'bora liende' utaendelea kuwepo kwa muda mrefu.

Kwa hapa Uingereza,Benki Kuu imekuwa ikitoa taarifa kuhusu viwango vya riba kila mwezi.Taarifa hiyo huambatana na maelezo ya kutosha kuhusu mwenendo wa uchumi wa nchi hii.Na kila baada ya miezi michache,ofisi ya takwimu nayo hutoa taarifa yenye takwimu zinzoashiria kupanda,kutuama au kushuka kwa uchumi.Kadhalika,vielekezo muhimu kuhusu uchumi wa nchi kama vile idadi ya wasio na ajira,mfumuko wa bei,wastani wa thamani ya sarafu,nk vimekuwa vikiwekwa wazi kwa umma.

Na huko nchini Marekani,Serikali ya Rais Barack Obama,imekuwa ikitoa taarifa za hali ya uchumi wa nchi hiyo mara kwa mara,hata kama kufanya hivyo kufanya hivyo kunaathiri namna wananchi wanavyoridhishwa au kutoridhishwa na serikali hiyo.Huku sio tu kutambua haki ya wananchi kuhabarishwa bali pia kuelewa kuwa kuficha ukweli kuhusu hali ya uchumi hakuwezi kuufanya uchumi husika kuboreka.

Na ndio maana licha ya kuwaficha Watanzania kuhusu hali ya uchumi wa nchi yao,sambamba na kauli mbalimbali za kisiasa kuwa 'hali cha uchumi ni poa' gazeti la Mwananchi katika toleo lake la leo linaripoti kuwa Serikali imelazimika kufumua bajeti yake ya mwaka wa fedha 2010/11 kwa kupunguza matumizi ya Wizara ili kufidia upungufu wa Sh670.4 bilioni zilizotegemewa kupatikana kutokana na makusanyo ya kodi katika mwaka huu wa fedha.

Hata hivyo,gazeti hilo lilipomtaka Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustaffa Mkullo, kuihusina na hali hiyo alisema taarifa ya hali ya uchumi wa nchi alishaitoa hivi karibuni kwenye chombo kimoja nchini, hivyo hahitaji kuitoa tena."Nilitoa taarifa kwa wenzenu wa gazeti (sio Mwananchi) sasa siwezi tena kuirudia," alisema.Ni dhahiri kuwa laiti hali ingekuwa nzuri,Mkulo asingefanya dharau hiyo hasa kwa vile viongozi dhaifu huwa wepesi sana kumwaga hadharani habari njema wakiamini zitawaletea sifa.

Wakati Watanzania wanasubiri 'waletewe' Katiba mpya,ni muhimu kuangalia tatizo hili la ukandamizwaji wa makusudi wa haki ya kuhabarishwa.Nchi mbalimbali zina sheria zinazoilazimisha Serikali na taasisi za umma kutoa au kuruhusu upatikanaji wa taarifa.Japo tunafahamu kuwa taarifa nyingi nchini 'zinachakachuliwa' kwa minajli ya kufisadi,kudanganya wapiga kura,kughilibu wafadhili,au sehemu tu ya utamaduni wa kutowajibika,uwepo wa sheria ya Haki ya Habari (Freedom of Information act) utakomesha tabia kama hiyo ya dharau Waziri Mkulo kupuuza kuwaeleza Watanzania kuhusu hali ya uchumi wa nchi yao

12 Feb 2011

Zoezi la ujenzi wa jarida kamili mtandaoni linaendelea vema.Lakini kama ilivyo pindi mtu anapohama kutoka sehemu moja kwenda nyingine,kuna vitu vinavyochukua muda kuwa timilifu.

Naomba nichukue fursa hii kuwashukuru wanahabari-mtandaoni wenzangu waliokubali ombi langu kwao kunitundikia katika blogu zao tangazo la mabadiliko ya anwani ya mtandao huu.Nawashukuru sana.Na pia nawakaribisha sana kushirikiana nami katika tovuti hii shirikishi.

Kwa wale niliowatumia ombi kama hilo lakini wakapuuza,sina maneno nao as such.Kuna baadhi yao ambao nina uhakika wa asilimia kubwa kuwa hawakuona barua pepe niliyowatumia.Nina uhakika huo kwa vile nawafahamu kuwa si watu wenye tabia ya dharau,jeuri au husda.Labda wako bize sana kiasi hawakuwa na muda hata wa kusoma barua-pepe iliyokuwa na ombi hilo.

Lakini kuna wengine ambao nadhani walikuwa na sababu zao "binafsi".Labda hawakupendezwa na uhamaji huu wa kutoka blogu kuelekea jarida kamili mtandaoni (wanasema ukitaka ufarakane na Waswahili basi piga hatua japo nusu).Au labda wao ni viumbe muhimu kabisa ambao hawakupaswa kubughudhiwa na ombi kama hilo.Na kwa baadhi ya waswahili,wanaamini dharau na maringo ni viungo (recipes) vya "umuhimu" wao katika jamii.

Enewei,natambua wametumia haki yao ya kikatiba na kidemokrasia lakini hio haiondoi ukweli kuwa walichofanya si uungwana.Na kwa vile binafsi naamini kwenye kuelezana ukweli,nimeona ni vema kuwashutumu japo naelewa fika haitobadili chochote.

Mwisho,nakaribisha maoni kuhusu tovuti hii hususan yaliyomo na mwonekano.Pia naomba wanahabari-mtandaoni ambao awali nilijumuisha anwani za blogu zao kwenye blogroll yangu lakini kwa sasa hazipo,wasifikiri nimewatelekeza.Naendelea na zoezi la kukusanya viungo vyote vya awali ambavyo kwa bahati mbaya vilifutika wakati wa uhamaji huu unaoendelea.

Tupo pamoja


Serikali ya Uswisi imetangaza kutaifisha mali zote za Dikteta Hosni Mubarak,ambaye jioni hii ameng'olewa madarakani na nguvu ya umma.Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa,haijafahamika iwapo serikali za Uingereza,Marekani na nchi nyingine za Magharibi ambako Mubarak ana mali zake (na kujichumia utajiri unaokadiriwa kufikiwa dola za Kimarekani Bilioni 70) nazo zitachukua hatua kama hiyo ya Uswisi au la.Je mafisadi wetu huko nyumbani wanajifunza lolote katika sakata hili?
I just hope they do!

11 Feb 2011

Habari zaidi baadaye

10 Feb 2011







BLOGU HII YA Kulikoni Ughaibuni INAPENDA KUWAFAHAMISHA KUWA INAHAMIA KATIKA ANWANI MPYA MTANDAONI.AWALI BLOGU HIYO IMEKUWA IKIPATIKANA KATIKA ANWANI http://chahali.blogspot.com/
 LAKINI SASA INAHAMIA KATIKA ANWANI MPYA YA http://www.blogger.com/goog_939388498
.
http://www.chahali.com

PAMOJA NA MABADILIKO HAYO,AMBAYO NI SEHEMU TU YA MABADILIKO MAKUBWA ZAIDI YA UBORESHAJI NA HATUA YA KUELEKEA KUWA TAASISI KAMILI YA HABARI NA UTAFITI,ANWANI YA AWALI ITAENDELEA KUWA HEWANI KWA MUDA WOTE WA ZOEZI HILI LA UHAMAJI (MIGRATION).SAMAHANI SANA KWA USUMBUFU WOWOTE UTAKAOJITOKEZA

ASANTENI NA KARIBUNI SANA http://www.chahali.com/








Mlolongo wa ushahidi kuwa Kikwete ni sehemu muhimu ya ustawi na mafanikio ya ujambazi wa Dowans,na uthibitisho kuwa nchi imemshinda.

www-freemedia-co-tz

www-mwananchi-co-tz

www-freemedia-co-tz (1)

www-mwananchi-co-tz (1)

www-freemedia-co-tz (2)

Www Uhurupublications Com

9 Feb 2011



So CCM has turned 34!

It's almost certain that you'll end up in confusion,if not a severe headache,or to make matter even worse feeling nauseated when you take time to reflect  on where this exceedingly corrupt party came from.I remember back in the days when CCM used to be as important as one's religious faith.Of course,people were coerced into having a blind faith in the sole party by then but that does not diminish the fact that the party was to a larger extent serving the masses regardless of their bank balances.

But,any sensible discussion on how CCM transformed itself from a people's party to a clique of political thugs should not try to avoid the role of Baba wa Taifa in getting all of us to this unknown destination.I have great respect to Mwalimu but his failure,intentionally or short-sightedly,to realise that some of his closest allies were actually wolves in sheep skin.You don't have to be a political analyst to discover that the likes of Kingunge Ngombale Mwiru,who were like Nyerere's brothers,were preaching to the public about Ujamaa na Kujitegemea while they were secretly praying for Mwalimu to disappear so that they could tunr our country into shamba la bibi.And shmba la bibi we truly are now!

Some scholars have gone further to a point of claiming that Nyerere's decision to ng'atuka in 1985 was actually a vailed admission of his failure to turn Tanzania into a socialist state.They also contend that his decision to appoint Ali Hassan Mwinyi as a successor was a calculated move to obscure Nyerere's own failures.And that move seemed to have paid dividends as it is the Mwinyi-era,and not Nyerere's, that is often portrayed as a the starting point of Tanzania's journey to nowhere.

It could as well be argued that in choosing Mwinyi as his successor,Nyerere was continuing his tradition of appointments based on personal allegiance rather than being merit-driven.Let's be honest.What convinced him that Tanzania would have been in safe hands under Mwinyi's leadership,bearing in mind that the country's fragile and aid-dependent economy was in shambles?

Do I think  Nyerere's leadership  was as poor as his predecessors?Not really.The major issue I have with the way he ruled the country is his blind faith in some crooks who  surrounded him,fooling him and the masses that they had strong faith in Ujamaa na Kujitegemea while in fact the were worse than the Mob.

However,at least Nyerere seemed to be concerned about the welfare of the nation and the people he led.And although he retired without making a public apology for his failure in realising the Ujamaa na Kujitegemea dream,his commitment to Tanzanians of all walks of life was truly unsurpassed.

Fast forward two decades later,and we have a political party that not lacks strong leadership but also has willingly made itself a hostage to the worst kind of characters.When you have a weak party leader like Jakaya Kikwete,sitting in midst of crooks who bankrolled their dirty money between 1995 to 2005 to assure he becomes the 4th President of Tanzania,come what may,the Judiciary comprised of a substantially high number of appointees who hold their allegiance to Kikwete as a person,and a Legislative body full of people who bought their way into power by splashing illegally amassed funds,the result is no better than having a Mafia state.

To make matter even worse,the instruments for good governance and public service are also severely infected with a congregation of unscrupulous people whose only mission is to multiply their number of nyumba ndogos,mansions,fleets of luxury cars and deposits in their fat bank accounts.

And contrary to popular belief that age comes with wisdow,the older CCM gets the more corrupt and useless it becomes.And as every young and old sinner seems to realise that the ruling party offer a safe haven as long as one is ready to buy ukamanda wa vijana,CCM's coming birthdays will continue to bring painful memories to every mlalahoi while the fisadis laugh their way to the bank.



Due to the growing demand and popularity of the hit reality show "Growing Up African" there have been several inquiries pertaining to television access. Growing Up African has become a huge success in several countries including the United States and U.K through the internet especially on their youtube channel. In order to translate this success to the general public especially those in Tanzania, the cast have chosen to take a direct approach. In a statement released by the family, Johnson the oldest son will be traveling to Dar es salaam for the month of February. On this trip, he will meet with several executives from the entertainment and television realm in order to make the show available to the average person. At the current moment, internet based entertainment is only vastly avalaible to those overseas. The purpose of this trip is to select a host television network for the reality show so it can become available to a much wider audience throughout East Africa.

Please visit the youtube channel to view the new episodes and previews of the show from 2011.











For more information please send all questions or concerns to [email protected] or sms to 845-518-5559.

4 Feb 2011


Kuna jitihada zinazofanyika huko nchini Misri katika jitihada za kumaliza machafuko yaliyodumu kwa zaidi ya siku 10 sasa kushinikiza kung'oka madarakani kwa Rais Hosni Mubarak.Jitihada hizo zinafanywa na kundi linalojumisha "Kamati ya Watu wa Busara" (ni kama Wazee wa Busara lakini sio kama wale walioimbwa na kundi la Wachuja Nafaka ).Watu hawa wenye heshima zao katika taifa hilo wanajaribu kuepusha maafa zaidi ambapo inaelezwa kuwa hadi sasa zaidi ya watu 300 wameshauawa.Kwa mfano,miongoni mwa mambo waliyojaribu kuishauri Serikali ya Mubarak ni kuangalia uwezekano wa Rais huyu kubaki na cheo cha heshima (figure head) lakini majukumu ya kuendesha nchi yakabidhiwe kwa Makamu wa Rais.Kadhalika,walidai kuwa wanaweza kushawishi kundi la Muslim Brotherhood lisisimamishe mgombea iwapo Serikali ya Mubarak itakubali kuitisha uchaguzi.

Ukiangalia mwenendo wa mambo huko nyumbani,ni dhahiri nasi tunahitaji Wazee wa Busara wa kukutana na Rais Jakaya Kikwete,angalau kumwamsha katika lindi la usingizi unaomkabili na kumfahamisha kuwa taifa letu linaelekea kusikostahili.Tunaweza kujidanganya kuwa yanayotokea Misri hayawezi kutokea kwetu lakini ukweli ni kwamba mazingira yaliyopelekea mbinde huko Misri,Tunisia,na sasa Yemen na Sudan (kwa kiasi flani) pia yapo huko nyumbani.Umasikini wa kupindukia ambao unapuuzwa na watawala wanaozidi kujirundikia utajiri,sambamba na kupora raslimali za umma;ukosefu wa ajira;utawala wa kibabe (rejea mauaji ya raia wasio na hatia huko Arusha na Mbeya,sambamba na nguvu kubwa kupita kiasi zinazotumiwa na vyombo vya dola kudhibiti maandamano ya amani),to mention but a few.

Unfortunately,wazee aliotuachia Baba wa Taifa ndio dizaini ya akina Kingunge-watetezi wakubwa wa ufisadi.Kuna watu kama Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi,Mawaziri Wakuu Wastaafu kama Warioba na Cleopa Msuya,na wanasiasa kama akina Joseph Butiku lakini hawa wote wanakwazwa na tatizo lilelile linaloikwamisha Tanzania yetu: kuweka maslahi ya kisiasa mbele ya maslahi ya taifa.Angalau Warioba amejaribu mara kadhaa kuzungumza "kwa niaba ya umma" lakini mafisadi wakaanza kumuundia zengwe.

Nalazimika kupigia mstari umuhimu wa kuwatumia Wazee wa Busara kumwamsha Kikwete kwa vile inaelekea Rais wetu anajifanya haelewi kinachoendelea kwenye maisha ya Watanzania wengi.Yoote aliyoahidi wakati wa kampeni zake za mwaka 2005,na kisha kuyarejea tena wakati za kampeni za mwaka jana yanaelekea kuwa yamesahaulika kama sio kupuuzwa.

Majuzi nilityumiwa comment na msomaji mmoja aliyenishutumu kwa kile alichoita "kuchochea vurugu" na kudai mie nahamasisha yanayotokea Misri na Tunisia yatokee Tanzania pia ilhali mie mwenyewe niko nje ya nchi.Mpuuzi huyu anajifanya haelewi kwamba kuwa nje ya nchi hakumaanishi Utanzania wangu unakuwa nusu.Afterall,nina ndugu,jamaa na marafiki wanaoteseka kutokana na hayo nayopigia kelele kila siku.

Na hata blogu hii ikikaa kimya,au wazalendo wa mtandao kama Jamii Forums nao wakinyamaza,ukweli unabaki kuwa siku moja Watanzania wanaweza kusema this is too much,liwalo na liwe.Mwanafalsafa Karl Marx aliwahi kutuasa kuwa masikini hana cha kupoteza (akiamua liwalo na liwe) except minyororo anayobebeshwa na watawala dhalimu.

Tuna uchaguzi mmoja tu: kubadilisha hali ya mambo kwa njia za amani ama sivyo yanayojiri mahala kwingineko yanaweza kutokea kwetu pia.Sio suala la kuombea au unabii wa maangamizi bali huo ni ukweli mchungu.Hakuna namna ya kumaliza ugonjwa pasipo tiba.

Na kwa Kikwete na jamaa zake,ni muhimu kujifunza katika yanayoendelea huko Tunisia,Misri,Jordan,Yemen na Sudan.Kuendelea kuwakumbatia mafisadi wanaokwangua uchumi wetu kila kukicha ni jambo lisilokubalika hata chembe.

TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA

3 Feb 2011



Dear all our Valued, Fans we are pleased to introduce to you our New track named Jiachie by Victor Mrisho (Producer Kita) Rama Records enjoy the song as we are approaching to Valentine enjoy.


On Behalf of Umabe Arts Company
Fredy Njeje
Project and Design Manager.


Kwa pamoja Tunaendeleza Burudani

29 Jan 2011


Katika siku za hivi karibuni,gazeti la Tanzania Daima limeonekana kama linafanya juhudi za wazi kuiweka profile ya Edward Lowassa machoni na masikioni mwa wasomaji wa gazeti hilo.

Ukidhani observation hii ni ya majungu,basi nakushauri uanze na habari zilizo kwenye toleo la kesho Jumapili (mbalo tayari lipo mtandaoni katika tovuti ya gazeti hilo) kisha fanya assessment yako Jumapili ijayo,na nyingineyo.

Je hizi ni sehemu ya kampeni za kumrithi Kikwete 2015?

Nimechokoza tu udadisi,hitimisho nakuachia wewe msomaji



TWELVE years is an eternity in music - but it's taken hip-hop legend DR. DRE that long to return.

The reclusive veteran producer, who launched SNOOP DOGG and EMINEM, finally issued his comeback single, I Need A Doctor, yesterday.

Dr. Dre f. Eminem I Need A Doctor CDQ

Its crashing rock drums and squealing guitars are far from the electro beats he's known for. And the lyrics are gushing, as Dre and Eminem swap verses saying they would be nothing without each other.

Dre also has a foul-mouthed pop at his critics, which is par for the course.

Universal insist his follow-up album to 1999 collection 2001, will come this year. I'll not hold my breath - but it's intriguing.

SOURCE: The Sun

Prior to the release of this joint,Dr Dre had earlier dropped another track,Kush, featuring his protege Snoop Dogg and Akon.As usual,it's as exceedingly explicit as blunt-themed.Check the video below.





Mourners for hire
Saturday, 29 January 2011 08:17

By Polycarp Machira
The Citizen Reporter
Dar es Salaam. Would you cry at the funeral of somebody you don’t even know, a person you never met during his or her lifetime? How would anybody work himself into a sombre mood at the funeral of a total stranger and break into sobs, shedding lots of tears?Well, faced with economic hardships and lack of jobs, some young people in Dar es Salaam are doing something that would never have been imagined only a few years ago. In fact, the traditionalists would have been shamed to death in the face of such a scenario.

But the young people are going to extremes to earn some money, and in some cases doing what to many would consider rather weird, such as offering to cry at funerals for a fee.

And this is not a scene from a stage play about death and funerals. It is the real thing – a new profession, mourning for hire, is taking root in Dar es Salaam.

While death has always been a source of income for funeral homes in the urban centres, coffin makers, transporters, grave diggers, and providers of other services, including catering, to give the dead a grand send-off, the idea of “professional mourners” is a brand new one.

But the rather morbid business of professional mourners is gaining popularity, with many families hiring strangers to cry at their relatives’ funerals.

The Umoja wa Waombolezaji Misibani (UWAMI), a group of ‘professional mourners’ in Dar es Salaam is already gaining ground by offering what is increasingly becoming a major part of funerals in the city. They charge Sh150,000 for a day’s service, which ends when the person is buried.

The business is fast catching on as the greater society opens up to adopt the traditional rites of communities or things that happen in other countries.

Some traditions demand the holding of grand funerals, where loud crying by close relatives, acquaintances, friends or associates, is meant to demonstrate deep love for the deceased.

The gift of acting (crying) among the UWAMI group members has been nurtured by their daily activities of making and selling coffins in the Manzese suburb of the city.

Comprising six members, the group was established in October last year to provide “crying services” at funerals for a fee.
Speaking to The Citizen of Saturday, UWAMI chairperson Frank Anthony said the members had been inspired by the search for a livelihood amid hardships due to lack of steady jobs to find an alternative source of income.

He said the idea was born, when, as they sold coffins, they would ask some of their customers to consider hiring some “readymade” mourners, as well.

A customer, who told them that he had heard on radio that such groups were already operating in Kenya, got them to turn their idea into reality.

They started out as a group of three, but as more city residents heard about the service and demand increased, more members joined.

In less than six months, the group has provided mourners for hire at three funerals, but is looking forward to a business boom as more people get to know about the service.

“We hope to provide well organised funeral crying services based on the needs of our customers from different ethnic and cultural backgrounds,” said Mr Anthony.

But the chairman conceded that the group would have to work hard to cope with the different requests for their services.
He said that at some funerals, relatives asked them not to cry, but to “joyously sing along with the family members”. He quipped: “It is serious business…crying.”

To prepare for a job, they need information on the age, sex and occupation of the dead person. They should also know about where he or she used to work, relations with the neighbours, workmates and family members.

The group must find out what exactly the family expects them to do. “In some communities, they do not cry all the time, but just sit waiting for relatives who come in crying, and they join in.”

UWAMI members cry along with funeral music.
The professional mourners are served with ugali and meat and provided with alcoholic drinks to stimulate their crying.
For a session, a crate of beer, konyagi and banana, a local alcoholic drink, are sufficient.

Group member Faida Yassin said that judging from the income earned in the short time they have been offering the services, the future is promising.

Mr Yassin, a father of three children, said he was able to pay school fees for his son in secondary school with his earnings.

“This service will really change our lives if the society responds positively,” he said.

However, he conceded that it had not been easy at the beginning, as they learned how to cry for pay.
A lecturer in psychology at the University of Dar es Salaam, Prof Issa Omari, said the phenomenon was part of society’s development, and should be viewed positively.

“It is not a new thing, as it started in Kenya almost a decade ago. It is just a money making enterprise for jobless youth,” he said. “There is nothing strange in a money-dominated society about allowing people to buy anything they want.”

But Dar es Salaam residents have received the news of the “professional mourners” with mixed reactions.

Some of those interviewed said the emergence of such groups “simply shows the levels of frustration in the society due to lack of job openings”.

Mr Stephen Maina, a 70-year-old resident of Mabibo, said it “is not part of Tanzanian culture”.

He added: “Crying in a funeral is an act that close relatives or friends of the deceased can do. Having some hired people crying is shameful and unethical.”

He said that in some traditions, having a stranger crying at a funeral was seen as an act that could result in a bad omen in the bereaved family.

“In Germany, France, China and England, where I’ve lived, the practice is quite different. They hire people to perform at funerals but not to cry.”

He added: “I think even those who hire mourners must have some problems.”
Mr Rashid Juma, a businessman at Kariakoo Market, said: “Tanzanians should not just copy anything, including services that add no value to our norms.”

The vice-chairman of the Christian Council of Tanzania, Bishop Peter Kitala, dismissed UWAMI’s services as ungodly, adding that crying at a funeral was a way of sharing the grief of the bereaved and should not be for financial gain.

“I urge the public to shun the services of the professional mourners. I find it really sorrowful that Tanzanians can go to that level of pretending just to get money,” he said.

The clergyman said it was sinful to pretend to be in a certain state for personal gain.

SOURCE: The Citizen

28 Jan 2011












Chanzo: The Guardian

KAMA TUNISIA WALIFANIKIWA,MISRI NAO WANAWEZA KUFANIKIWA.KAMA TUNISIA NA MISRI WAMEDIRIKI,WAANZANIA NAO WANAWEZA.PENYE NIA PANA NJIA.IT CAN BE DONE IF WE ALL PLAY OUR PARTS.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.