19 Jan 2010


DAILY NEWS Reporter, 18th January 2010 @ 12:13,

IN an interesting twist of events, President Jakaya Kikwete failed to hand over two ambulance vehicles today, after controversy ensued over the rightful identity of the targeted receivers.

The confusion ensued after a representative from Ngorongoro District in Arusha Region turned up instead of an official from Longido, whom documents indicated was supposed to receive the donation.

The twist happened at the State House grounds before officials and journalists, when the president seemed confused after he discovered it was a representative from Ngorongoro and not from the targeted Longido, who had turned up.

A representative from Mbozi District in Mbeya Region who was meant to receive the second vehicle on behalf of his district had not yet arrived, prompting the president to hand it over to someone else who was present.

When he approached the two cars recently donated by CMC Automobiles Limited, Chief Executive Officer, Mr Abdul Haji, President Kikwete was introduced to the receiver as the Executive Director of Ngorongoro District Council, Kayange Jacob when he suddenly stood back.

“You are….. (as he was being introduced by the State House Comptroller), ahh, you are from Loliondo, this car is not yours, I won’t hand it over to you. It’s not yours. It’s for the people of Longido and not Loliondo.

Turning to State House officials, he asked: What is this. This is scandalous. Apologise to those you invited to witness this”, said the president.

“This one car is to cater for the people of Longido, not Loliondo, who sent you here?’

The Executive Director of Ngorongoro District Council who introduced himself as Kayage, explained to the president that he had been sent by his Regional Commissioner, to come and receive the vehicle as a donation to carry sick people in Ngorongoro.

But the president explained that records show that one of the two cars was supposed to go to Engarinaibo Village in Longido District, following his promise to them when he toured Arusha last year.

“I personally promised the villagers I would give them an ambulance, when I receive a donation of vehicles after witnessing their difficulty in transporting their sick people to hospital. Now what is this? This is scandalous,” he repeated.

Efforts by the State House officials to explain to the president that he hands over the car to the Ngorongoro Director, as there was no other were in vain as he (president) walked back to his office.

After the drama that lasted for approximately 20 minutes, the Assistant Director of Communications at the State House, Premy Kibanga, told journalists that there was negligence on the part of some officials who had verified the documents, subsequently messing up issues.

“There has been a problem of communication here at State House, as all documents including the letter to presiding secretary in Arusha, show that those entitled to the donation is Engarinaiko village in Longido and not Loliondo,”said Kibanga.

Ms Kibanga attributed the anomaly to negligence on the part of the State House official, who was supposed to verify the documents of the director before the handing over, also blaming it on the late arrival of the two officials by ten minutes and that of Mbozi by 20 minutes.

She said the letter from State House to the presiding secretary in Arusha, dispatched at the end of last year, was clear that that the donation was for Engarinaiko village in Longido and had asked the official to release a municipal driver, to get a short course on how to use the facility at CMC.

However, it is not clear to this evening as to whether it was the driver of Longido or Ngorongoro who had received the short training prior to yesterday’s event.

The director of Ngorongoro told journalists that he had been sent by the Regional Commissioner to receive the donation, after a phone call came from the State House asking them to send a representative to receive it.

Efforts to reach the Arusha Regional Commissioner, Isidori Shirima, were futile as his phone went unanswered.

But information sent by the Communication Directorate of State House, said the president handed over one vehicle to the Director of Mbozi District, Levison Chilewa, to cater for citizens of Kamsamba as ambulance.

It was part of the president’s pledge to the area when he visited last year. Earlier, Mr Chilewa told journalists that it would support 26 wards in Mbozi with special target at Kamsamba, Ivuna, Chilulumo, Chitete and Msangano wards.

The two vehicles - Land Rover Defender 110 Hard Top - worth 108,000 US dollars (about 130m/-), were donated by CMC in honour of the manager’s wife, who lived in the country for 30 years before passing away.

15 Jan 2010


The US Government has released a new age-enhanced photograph of al-Qaeda leader Osama bin Laden as he may look now without his trademark long beard...MORE

5 Jan 2010


Naomba kuiwasilisha kama ilivyo

Zitto Kabwe: Kumbikumbi huruka na kuliwa na kunguru

TAFAKURI

Mwanahalisi Toleo Na. 168

.
Na Nkwazi Mhango

ZITTO Kabwe mbunge wa Kigoma Kaskazini, amekiri kumpa magari matatu ofisa habari za zamani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), David Kafulila.

Magari hayo anayatoa kama msaada kwa Kafulila ili aweze kushinda kampeni za ubunge katika jimbo la Kigoma Kusini. Hizi ni habari zinazozua maswali mengi, ikiwamo utajiri na uwezo wa Zitto kiuchumi.

Je, inakuwaje Zitto aweze kumiliki magari matatu wakati kipato chake kinajulikana? Lakini la pili, Kafulila na Zitto wanawezaje kuanza kampeni za ubunge wakati Tume ya Taifa ya Uchaguzi haijatangaza?

Tayari Zitto amekaririwa akisema, “Ni jambo la msingi kupunguza idadi ya wabunge wa CCM…ndiyo maana nimeamua kumsaidia Kafulila katika chama alichopo (NCCR-Mageuzi). Nipo tayari kujitolea kwa kijana mwingine anayegombea, hata kwa chama kingine, isipokuwa CCM.”

Kwa maneno ya Zitto ni kwamba anamuunga mkono Kafulila, ingawa bado anadai yuko CHADEMA. Ni ajabu kidogo. Je, kama CHADEMA wataamua kusimamisha mgombea Kigoma Kusini wakati Zitto ana mtu wake, atamuunga mkono nani kati ya mgombea wa chama anachodai kimemlea na kumkuza na kumfikisha hapo alipo na rafiki yake kipenzi?

Si vizuri kumsemea Zitto wala Kafulila. Kuna haja ya CHADEMA kuuliza swali hili kabla mambo hayajafika huko. Kwa sasa, Zitto ama kwa kujua au vinginevo, anaanza kujiona maarufu kuliko chama, kama Jakaya Kikwete-kwa mujibu wa maneno ya katibu mkuu wa CCM, Yusufu Makamba.

Ifahamike. Kumbikumbi akaribiapo mauti huotesha mbawa na kuruka na kuishia kuliwa na kunguru.

Inapofikia mtu akafikia kujiona bora kuliko chama, huyu bila shaka hakifai chama wala chama hakimfai. Na lazima kuna tatizo, tena kubwa tu. Hivyo, uwezekano wa kukitosa chama wakati mbaya, hasa ule wa uchaguzi, ni mkubwa. CHADEMA wasingoje kufika huko.
Siasa za Tanzania zina bahati mbaya. Chama kinamlea mtu hadi kufikia umaarufu kama alivyo Zitto Kabwe sasa. Halafu mtu huyu aliyefinyangwa na kulelewa na chama, analewa sifa kiasi cha kujiona bora kuliko chama.

Mwisho wake huwa mbaya kwa mhusika na chama. Daniel arap Moi wa Kenya alifikia hatua ya kulewa sifa hizi pale alipoitwa profesa wa siasa. Alifanya ubabe hadi akakikosesha dola chama chake cha KANU.

Kuna haya ya wanasiasa kuchagua kati ya chama na urafiki. Tumekuwa tukimshutumu Kikwete na CCM kwa kuendekeza urafiki na kujuana. Hata wapinzani wanamlaumu kwa hili, hasa kwa kusema anaendesha nchi “kishikaji.” Hili sina mjadala nao wala sitaki kuingia undani wake. Lakini CHADEMA waangalie wasitoe kibanzi kwenye jicho la mwenzao wakaacha boriti kwao.

Zitto kwa watu wa nje ya chama chake anaonekana kuwa mguu mmoja ndani na mwingine nje. Ushahidi ni shaka juu ya msimamo wake. Kwenye mkutano wa Opesheni Sangara kule Tanga watu wanataka kujua kama Zitto bado yumo chamani au la.

Ni rahisi mtu kukanusha, lakini ushahidi wa mazingira unaweza kupaaza sauti kuliko mwenye kukanusha. Ingawa Zitto anasisitiza kuwa yuko CHADEMA, matendo husema zaidi ya maneno matupu.

Inakuwaje Kafulila awe mali kuliko chama? Zitto anapaswa kubanwa ajibu swali hili kwa usahihi na majibu yanayoingia akilini siyo kupiga siasa. Je, kwa kumuunga mkono Kafulila, hata dhidi ya uamuzi wa CHADEMA, Zitto hadhihirishi asivyokubaliana na hukumu aliyopewa Kafulila?

Kama chama kilimuona Kafulila ana makosa na kikafuata taratibu zote za kumtimua, naye akaamua kujitoa na kutoa kashfa nyingi, maana yake ni kwamba kuna mgongano hata kama wahusika hawataki kulikubali hili.

Litakuwa jambo la ajabu kwa mtu wa cheo na elimu ya Zitto kutoliona hili. Wenzake wamekaa chini wakamtimua Kafulila na kutaja makosa yake-kuvujisha siri za CHADEMA.
Yeye bado anamtetea. Je, huku si kutetea madhambi yake au kuonyesha kuwa kipenzi chake kimeonewa? Kwanini asimtetee kwa namna inayoeleweka badala ya kuendelea kukidhoofisha chama?

Ifahamike. Tunaelekea kwenye uchaguzi mwakani. Kwa uzoefu wangu, wanasiasa nyemelezi watavitelekeza vyama vyao, hasa baada ya kuahidiwa vinono na CCM. Nani mara hii amesahau akina Masumbuko Lamwai, Tambwe Hiza, Walid Aman Kabourou, Shaib Akwilombe, Salum Msabaha na wengine wengi? Kwanini uone ubaya wa chama baada ya kutimuliwa?

Ingawa kuhama vyama ni haki ya wahusika, wengi wa wanasiasa, hasa waliojirejesha CCM baada ya kukosa ukuu kwenye vyama vyao, wameonyesha kuwa nyemelezi na “changudoa.”
Ukiwaondoa watu kama Wifred Rwakatare na wengine wachache, wengi wamedhihirisha wanavyosaka madaraka badala ya kutumikia umma. Wamejivua nguo hata kama baadhi yao wanapewa madaraka ya kufinyangwa kama ilivyo sasa ofisi ya propaganda ya CCM, ambayo imegeuka dampo la wanasiasa nyemelezi.

Hivyo basi, CHADEMA wangembana Zitto wajue msimamo wake kwamba ni nani hasa atamuunga mkono kati ya mgombea wa chama chake na rafiki yake Kafulila.
Ni heri CHADEMA wakamkosa Zitto mapema kuliko kuwachenga saa za mwisho. Huu si wakati wa kucheza pata potea.

Bado Zitto ni mdogo kisiasa na kiumri. Ubunge wa kipindi kimoja hauwezi kumfanya awe yote katika yote hadi kuwa maarufu kuliko chama. Na chama kinapozidiwa umaarufu na mtu mmoja, kama CCM, kijue kinaelekea kuzimu. Nisingetaka CHADEMA wafike huko ingawa dalili zinaonyesha ukomavu wa hali ya juu katika kuyakata mawimbi haya na majaribu makubwa.
Zitto kaamua kumuunga mkono Kafulila wazi wazi, hata kabla ya chama chake kuamua kumsimamisha mgombea Kigoma Kusini. Anajiona si mchezaji bali mwamuzi. Je, alitaka kujenga mtandao ndani ya chama ili baadaye apate madaraka?
Na ikumbukwe. Hii si mara ya kwanza kwa Kabwe kupimana misuli na chama. Nani amesahau mvutano uliotokea hivi karibuni kwenye uchaguzi wa mwenyekiti wa chama? Je, Kabwe anatingisha kiberiti kwa ajili ya kuchukua uamuzi katika chaguzi ujao?

Kwa makala zaidi kutoka kwa MPAYUKAJI tembelea blogu yake HAPA


ASEMA SIASA SI CHAGUO LAKE

Salim Said na Fidelis Butahe

NAIBU Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe ameibuka tena na kutonesha majeraha ya mgogoro uliokuwapo ndani ya chama chake, akisema haridhiki na uamuzi wa chama hicho kuwaengua David Kafulila na Danda Juju.

Ingawa Kabwe hakutaja jina, kauli yake kupinga maamuzi ya kuwavua madaraka wanachama hao; imeonyesha kumzungumzia Katibu Mkuu wa Chadema Dk Willibrod Slaa kwa vile ndiye aliyesema Kafulila na Danda si kitu ndani ya chama hicho na kwamba, anaweza kuwashughulikia bila vikao vya chama.

"Mimi sipendi siasa za kinafiki, uamuzi wa kuwavua nyadhifa zao kina Kafulila haukuniridhisha kwa sababu haukuwa mzuri, ingawa ulipitishwa na mamlaka husika, katika vikao husika," alisema Kabwe katika kipindi cha Jambo Tanzania kilichorushwa na Televisheni ya Taifa (TBC1) jana asubuhi na kuongeza:

"Unajua unaweza ukawa na maamuzi yaliyofanywa katika vikao halali, lakini yasikuridhishe, pia unaweza ukawa na maamuzi katika vikao hivyo hivyo yakakuridhisha. Lakini mimi sikuridhishwa na mamuzi ya kina Kafulila kuvuliwa nyadhifa zao."...INAENDELEA HAPA

PAMOJA NA HESHIMA KUBWA NILIYONAYO KWA ZITTO LAKINI NADHANI KUENDELEA KWAKE KUNG'ANG'ANIA ISHU YA AKINA KAFULILA KUNAMPOTEZEA HAIBA YAKE YA KISIASA MIONGONI MWA WAPENDA MABADILIKO YA KISIASA HUKO NYUMBANI NA WANANCHI KWA UJUMLA.

HAYA MALALAMIKO YATAENDELEA HADI LINI?NA YANAENDELEA KWA FAIDA YA NANI?KAFULILA NA NA MWENZIE WALIKUWA WAAJIRIWA WA CHADEMA.MWAJIRI ANAWEZA KUMPANDISHA AU KUMSHUSHA CHEO MWAJIRIWA WAKE KULINGANA NA TARATIBU NA KANUNI ZA AJIRA HUSIKA.NA IWAPO MWAJIRIWA ATASHUSHWA CHEO KINYUME NA KANUNI HUSIKA BASI ANA HAKI YA KUPELEKA MALALAMIKO HAYO SEHEMU HUSIKA KAMA SI KUCHUKUA HATUA YA KUACHA KAZI KAMA WALIVYOFANYA WANASIASA HAO.HADI HAPO TATIZO LIKO WAPI?

JE ZITTO HADHANI KWAMBA KUTOAFIKIANA NA MAAMUZI YA NGAZI ZA JUU KATIKA CHAMA CHAKE NI SAWA NA KUTAFIKIANA NA CHAMA CHENYEWE AMBACHO YEYE NI KIONGOZI PIA?JE ZITTO SI SEHEMU YA UONGOZI ULIOFIKIA MAAMUZI YA KUWASHUSHA VYEO AKINA KAFULILA (HATA KAMA SI YEYE BINAFSI ALIYEFANYA HIVYO)?HIVI HAKUNA COLLECTIVE RESPONSIBILITY NDANI YA CHADEMA?

PENGINE BADALA YA KUENDELEA KULALAMIKA PASIPO DALILI YA MALALAMIKO HAYO KULETA MABADILIKO NI VEMA KWA MH ZITTO KAMA CHADEMA BADO INAFAA KUWA MAKAZI YAKE KISIASA.VINGINEVYO ITAKUWA KAMA KELELE ZA AKINA MWAKYEMBE KULALAMIKIA UFISADI NDANI YA CCM ILHALI WAO NAO NI SEHEMU YA CHAMA KILICHOGEUZA UFISADI KUWA SERA YAKE.IT SIMPLY DOESN'T MAKE SENSE.

NADHANI KUNA UMUHIMU WA KUIGA BUSARA ZA MKE (RASMI) WA TIGER WOODS KATIKA NAMNA ANAVY-HANDLE SKANDALI ZA UZINZI ZINAZOMKABILI MUMEWE.MWANAMAMA HUYO AMEKUWA MAHIRI KUKWEPA VYOMBO VYA HABARI LICHA YA TETESI KUWA ATAMBWAGA MUMEWE.ANAACHA WANAHABARI NA WAMBEYA WENGINE KUENDELEA NA SPECULATIONS ZAO LAKINI MAAMUZI YAKE YA MOYONI ANAYAJUA YEYE.AKIMTALIKI MUMEWE AU AKIENDELEA NAE,SIFA MOJA KUU ITAKAYOMWANDAMA NI UMAHIRI WAKE KATIKA KU-DEAL NA MATUKIO MAZITO KAMA HILO LA MUMEWE.


4 Jan 2010


Je mama Kikwete ameanza kampeni kwa ajili ya mumewe?

na Nkwazi Mhango

Siku hizi mke wa rais, Salma Kikwete, anaonekana kwenye kurasa za mbele za magazeti karibu kila siku akiwa mikoani akihamasisha hili na lile. Wengi wanahoji. Kwanini sasa na si tangu mwanzo mume wake alipoingia ikulu? Na kwanini asiseme wazi kuwa anampigia kampeni mumewe? Maana, inajulikana alivyo mwana CCM damu damu tena mjumbe wa vikao vyake?

Watetezi wake wanaweza kusema anafanya kazi ya shirika lake lisilo la kiserikali la WAMA. Haiwezekani mumewe akawa mkuu wa serikali naye akawa na shirika lisilo la kiserikali kusiwe na mgongano wa kimaslahi kisheria. Uzoefu tulioupata toka kwa Anna Mkapa ungetosha kumsaidia rais Jakaya Kikwete kuondokana na aina hii ya ufisadi sugu na unyemelezi kwa kutumia mgongo wa ikulu kama angekuwa ni mtu wa kujifunza na kudhamiria kutenda haki kwa taifa.

Ngo yake ni ya mashaka-kwanini ianzishwe baada ya mumewe kuwa rais? Kuanzisha NGO baada ya mume kuwa rais ni ishara tosha ya ufisadi na usasi wa ngawira. Mbona hatuoni wake wa viongozi wa vyama vingine wakiwa na NGOs? Hata wakiwa nazo nani atazichangia iwapo wanaochangia NGOs za wake wa marais wanatafuta kuwa karibu na ikulu ili waihujumu nchi kwa kupata upendeleo kama ilivyokuwa kwa EOTF ambayo ilitumiwa na watu wengi kuliibia taifa? Mke wa Kaisari hapaswi kutenda tendo lenye kuweza kutia shaka au doa utawala wa mumewe.

Tuliishi na kumuona baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere. Mkewe-mama Maria-hakuwahi kujihusisha na upuuzi mdogo mdogo wa kutafuta pesa kwa mgongo wa mumewe.

Niliwahi kuwaandikia barua EOTF na WAMA kuwaonya juu ya hatari ya kuitumia ikulu. Hawakuwahi kunijibu zaidi ya kufumba macho na kuendelea kutengeneza pesa kwa mgogo wa ikulu. Ila nafurahi. WAMA wamefanya jambo moja (la maana la kuondoa aibu)-kuondoa maneno yasemayo WAMA Foundation the office of the First Lady of the United Republic of Tanzania kwenye wavuti wao. Niliandika baruapepe ifuatayo kwa WAMA tarehe 3 Septemba 09:

Kama mzalendo, nimejaribu kukusanya baadhi ya maoni kuhusiana jinsi ufisadi unavyoingia ikulu kiasi cha kututatiza. Kwa sasa Anna Mkapa mke wa rais wa zamani na mumwe wako msambweni. Ukiangalia kinachofanywa na WAMA hakina tofauti na Fursa sawa kwa Wote (Wake za wakubwa).
Kuondoa aibu, nimejitolea kuwasiliana nanyi ili angalau mjue tunavyojihisi kwenye wimbi hili la ufisadi wa kutumia madaraka ya waume zenu. Mama Salma NGO yako ni ulaji mtupu kusema ukweli. Acha kuna kesho. Ni uamuzi wako kuamua. Kuna kesho wakati madaraka yatakuwa mikononi mwa wengine. Hasa nikizingatia kilichompata Regina Chiluba ambacho kinapaswa kumpata hata Anna Mkapa, nimeona bora niseme hata kama nitapuuziwa. Ila najua ujumbe utafika. Someni alama za nyakati na mjue kuwa madaraka yana mwisho na yanalevya. Kuna siku mtakumbuka mchango huu.
Kila la heri,

Bahati mbaya sana , hata wavuti wa Kurungenzi ya habari Ikulu unaonekana kutangaza biashara ya WAMA badala ya wizara za serikali! Ajabu hakuna anayestuka wala kupiga kelele!

Kama umma ukishupaa NGO hii inaweza kufutwa hata na mahakama kutokana na mgongano wa maslahi ukiachia mbali kuwa kichaka cha ufisadi kutokana na uwezekano wa kuchangiwa pesa chafu kutokana na kutokuwapo sheria makini ya kuchuja na kutangaza wafadhili wa WAMA.

Hata hivyo nimefarijika kuwa sauti yangu imesikika na fedheha imeondoka. Maana neno Jamhuri ya Muungano, kisheria, halipaswi kutumiwa na mtu au taasisi yoyote isipokuwa mihimili mitatu ya dola yaani Bunge, Mahakama na Utawala. Cheo cha Ofisi ya First lady hakimo katika katiba yetu.

Kwanini mapenzi kwa wanawake na watoto yaanze baada ya kuupata urais kama siyo gea ya kuitumia vibaya ikulu? Ina maana rais na washauri wake hawalioni hili au wameridhia kwa sababu NGO ya mke wa rais inaweza kutumika kama kivuli cha kuanza kampeni hata kabla ya tume kutanganza hivyo? Inabidi tustuke. Ajabu hata wapinzani hawajaliona hili!

Tanzania inaweza kuwa nchi pekee ambapo rais na mkewe wote ni marais. Kikwete ni rais wa jamhuri huku mkewe akiwa rais wa WAMA. Ukitaka kujua hili jikumbushe mapokezi anayopewa na coverage anayopata Salma kwenye vyombo vya habari. Ajabu ukitafuta uhalali wake kikatiba haupo!

Hata kama anajulikana kwa ubabe na upayukaji wake, bado mke wa rais wa Kenya Lucy Kibaki hana mamlaka kama aliyo nayo Salma ambaye anaweza kuingia mkoa wowote kwa kisingizio cha NGO yake na kufanya shughuli za kisiasa kama kulakiwa na viongozi wa mikoa na kukagua miradi ya maendeleo ukiachia mbali kutoa kauli mbiu zinazoonyesha wazi kumpigia debe mumewe.

Salma anchomzidi Lucy ni ile hali ya kufanya kitu waitacho waingereza one woman show. Kwani kila lilipo jina WAMA yupo yeye. Hii maana yake ni kwamba yeye ni dikteta na mpenda madaraka anayetaka kufanya kila kitu peke yake. Kwanini hatuoni makamu wake au hata wasaidizi wengine wakifanya shughuli za WAMA kama kweli ni ya umma kama anavyodai? Kuthitibitisha hili, tembelea tovuti ya WAMA uone ukweli huu. Hii haiwezi ikawa taasisi ya wanawake na watoto wa Tanzania .

Kuonyesha kuna namna ya kampeni na kutumia mamlaka ya mume wake, hivi karibuni, Mama Kikwete amewahi kutoa namba yake ya simu ya mkononi ambayo ni 0754-294450 kwa wanawake mkoani Singida ili waweze kumpigia au kumtumia ujumbe mfupi wa maneno pindi waume zao watakapowanyanyasa kutokana na kitendo cha wao kwenda kupima kwaajili ya kujua afya zao. Japo kwa juu hili linaweza kuonekana ni jambo bora, kwa mtu anayejua mipaka ya mamlaka yake na utaratibu wa utawala kisheria, angeshauri wahusika waelekeze madai yao kunakohusika-polisi, vituo vya kutetea haki za binadamu hata wizarani.
Licha ya kuwa ubabe, hii ni kampeni ya wazi kuonyesha wahusika wanawajali wananchi jambo ambalo si kweli. Kwanini hasira zake zisielekezwe kwenye kumshauri mumewe kupambana na ufisadi kama ana uchungu na nchi hii? Yaani hajui kuwa ujinga na umaskini ndivyo vyanzo vya haya yote? Sijui hata kwenye kupokea misaada anauliza usafi wa mtoaji.

Kwa nijuavyo upenzi wa sifa wa watawala wetu na watu wao, kama utafanyika uchunguzi huru juu ya matumizi ya MAWA, ushingae pesa inayotumiwa kwenye ziara ikawa kubwa kuliko hiyo inayowafikia walengwa. Bahati mbaya sijwahi kusoma popote taarifa ya mahesabu ya mwaka ya si WAMA wala EOTF.

Wengi wanaweza kuona kama tunamuandama mke wa rais au kutotambua umuhimu wa kupigania haki za akina mama. Kwanini mke wa rais wakati tuna wizara yenye watendaji wanaolipwa pesa ya kodi yetu? Kwanini misaada hiyo anayopokea isipelekwe wizarani au kwenye mashirika huru kama kweli ana uchungu na walengwa na si kujipatia umaarufu, pesa na kubwa zaidi kutumia ikulu kwa manufaa binafsi yawe yake au mumewe na marafiki zake?

Je Salma Kikwete ameanza kampeni kwa ajili ya mumewe hata kabla ya kipenga kupulizwa? Je akina mama wa Tanzania wataingia mkenge wake huku waume na kaka zao wakizidi kuteswa na sera za Kikwete za kuvumilia mafisadi? Je atawalainisha wasahau kuwa Kikwete hajatimiza ahadi hata moja? Je watahoji uhalali wa NGO yake na kumwambia ukweli kuwa ni ya mashaka na ulaji?

2 Jan 2010

31 Dec 2009

BLOGU HII INAWATAKIA NYOTE HERI NA BARAKA KWA MWAKA 2010.NAAMINI TUTAENDELEA KUSHIRIKIANA KWA MICHANGO YA MAWAZO NA KUKOSOA PALE INAPOBIDI,NAMI NAAHIDI KUWEKA MABANDIKO ZAIDI KATIKA MWAKA UJAO.

ASANTENI SANA

30 Dec 2009


THE NATION

AND BEYOND

THE Publishers of

MwanaHALISI,

your enviable Kiswahili weekly

in Tanzania,

wish to convey to you, our

warmest Season Greetings

that bring with them

a New Year – 2010.

We have always done

our piece in Investigative

and Public Journalism;

we are now engaged in

marshalling more skills,

improving methods and

producing quality copy

for IMPACT.

We continue to rely

on your readership;

appreciation of our efforts

to produce a copy worthy

your money; attempt at becoming

a real people’s voice;

and your kind and material

support already rendered

and anticipated.

We pledge to do more

to your satisfaction.

Happy New Year!

Hali Halisi Publishers Limited, Tel/Fax 022 - 2760560

Kasaba Street, Plot 57/31A Kinondoni e-mail: [email protected]

P. O. Box 67311 Dar es Salaam, TANZANIA website:www.halihalisi.com.tz

Cel: 0784 440 073/0777 773347


25 Dec 2009


There will always be bad,or even worse,Santas.Look at THIS,for example.

ANYWAYS,WISHING YOU ALL MERRY CHRISTMAS.

19 Dec 2009


Ahadi za urais 2005 zamtesa Kikwete uchaguzi wa mwakani

Rais Jakaya Kikwet, mzigo mzito wa ahadi zake za mwaka 2005 unamkabili uchaguzi ujao 2010.
Na Mwandishi Wetu
MIEZI michache ikiwa imebaki kabla ya kuanza kwenda kwa wananchi kuomba ridhaa ya kuongoza nchi kwa kipindi kingine cha miaka mitano, Rais Jakaya Kikwete anaonekana kukabiliwa na mzigo mzito wa kutekeleza ahadi nyingi alizozitoa wakati wa kampeni za mwaka 2005.

Kikwete alipata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 baada ya kunyakua takriban asilimia 80 ya kura, akiwa pia ameshinda kwa kishindo dhidi ya wapinzani wake kwenye uteuzi wa mgombea wa CCM.

Lakini kadri muda unavyokwenda ndivyo umaarufu wake unaonekana kupungua huku tafiti mbalimbali zikionyesha kuwa umaarufu aliokuwa nao wakati akiingia madarakani unaendelea kuporomoka, ikiwa ni miezi tisa kabla ya uchaguzi mkuu wa mwakani.

Wakati akizunguka sehemu mbalimbali nchini kuomba kura za wananchi, Kikwete alikuwa akitoa ahadi kem kem ambazo alizielezea kwa kifupi kwenye kauli mbiu yake ya â€Å“Naisha Bora kwa Kila Mtanzania” ambayo mkakati wake wa kuitekeleza ulikuwa ni â€Å“ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya”.

Mbali na ahadi ambazo alikuwa akizitoa kwa wananchi kila sehemu alipoelezwa tatizo, ikiwa ni pamoja na matatizo sugu ya maji, miundombinu, huduma za afya na pembejeo, Rais Kikwete pia alitoa ahadi za ujumla kabla na baada ya kushinda uchaguzi kumrithi Benjamin Mkapa.

Baadhi ya ahadi hizo za Rais Kikwete kabla na baada ya kuingia madarakani ni pamoja na kuweka kipaumbele katika kilimo, akitumia kaulimbiu ya Kilimo Kwanza, kupitia upya mikataba ya madini ili inufaishe nchi na wawekezaji, na kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi wa elimu ya juu anayekosa masomo kwa kukosa karo.

Ahadi nyingine ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za umma, kuumaliza mgogoro wa Zanzibar, kuimarisha uhusiano wa kimataifa, kukomesha tatizo la ufisadi, kupambana na tatizo la uhalifu, ikiwa ni pamoja na biashara ya dawa za kulevya na ujambazi, kuandaa mdahalo wa kitaifa wa michezo kwa lengo la kuinua michezo na ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma....INAENDELEA HAPA

17 Dec 2009


Waziri wa Sheria adai Bunge la sasa halina ubavu kwa serikali
Na Leon Bahati
WAZIRI wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe amezidi kutoa kauli tata baada ya kuligeukia Bunge la Jamhuri ya Muungano, akisema halina nguvu ya kuilazimisha serikali kufanya mambo na kwamba kazi yake ni kuishauri.

Hiyo ni kauli ya pili ya waziri huyo katika kipindi kisichopungua wiki moja baada ya kukaririwa Jumatatu akisema kuwa Rais Jakaya Kikwete hana uwezo wa kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi kwa kuwa mfumo wa utawala wa sheria hauruhusu vitendo kama hivyo.

Kauli hizo mbili zinazohusu mamlaka ya kisheria zimetolewa katika kipindi ambacho mjadala mkubwa wa hatua zinazostahili kuchukuliwa dhidi ya watuhumiwa katika kashfa ya utoaji zabuni ya uzalishaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development (LLC) ukiwa umemgeukia rais.

Pia Chikawe ametoa kauli hiyo wakati Bunge likiishinikiza serikali kutoa taarifa ya utekelezaji wa maazimio yake 23 dhidi ya wahusika kwenye kashfa hiyo kubwa iliyotikisa nchi baada ya Edward Lowassa kujiuzulu wadhifa wake wa uwaziri mkuu kutokana na ushauri uliotolewa na kamati teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza kashfa hiyo....INAENDELEA HAPA

16 Dec 2009


Prof Shivji asema Rais Kikwete ana mamlaka kisheria kuwabana mafisadi
*WENGINE WAMTAKA WAZIRI CHIKAWE AACHE KUKURUPUKA
Na Sadick Mtulya

SIKU moja baada ya Waziri wa Sheria na Katiba Mathias Chikawe kusema Rais Jakaya Kikwete hawezi kutumia mamlaka yake kuwabana mafisadi, baadhi ya wanasheria nchini, akiwamo Profesa Issa Shivji, wamepinga kauli hiyo kwa kusema sio kweli.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana wanasheria hao walisema rais anaweza kuwabana mafisadi kwa kutumia mamlaka yake ndani ya chama na serikali.

Profesa Issa Shivji alisema Rais Kikwete anaweza kupambana na watuhumiwa wa ufisadi kwa kuwavua madaraka walionayo katika chama au serikali.

Gwiji hilo la Sheria na Mwenyekiti wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere, alisema kama watuhumiwa watakuwa watumishi wa serikali au watendaji katika mashirika ya umma, rais anaweza kuwawajibisha kwa kutumia sheria na kanuni za utumishi wa umma.

"Kumwajibisha mtuhumiwa sio iwe kumpeleka mahakamani, unaweza kuchukua hatua za awali ikiwemo kumvua nyadhifa zote. Kama ni mwanasiasa au mtumishi katika serikali na mashirika ya umma, unaweza kumwajibisha kwa mujibu wa sheria za umma," alisema Profesa Shivji.

Alisisitiza Kusema Rais Kikwete hana uwezo wa kuwabana mafisadi sio kweli na Watanzania wanatakiwa kuelewa hivyo kwamba rais anaweza.

Kauli ya Profesa Shivji iliungwa mkono na Profesa Abdallah Safari, aliyetia ngumu akisema sheria za nchi ikiwemo ya utawala, inampa uwezo na mamlaka rais kupambana na vitendo vya ufisadi ndani ya serikali yake na hata katika chama chake.

Rais kukasimu mamlaka yake kwa Takukuru (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ) na kwa DPP haimaanishi kwamba sasa yeye hana uwezo wa kupambana na watu wanaojihusisha na ufisadi. Bado anao, alisema Profesa Safari....INAENDELEA HAPA

Alifafanua kwamba, Rais Kikwete anayewajibika katika kupambana na ufisadi kwa kuwa yeye ndiye anayewajibika moja kwa moja kwa wananchi wa Tanzania.

14 Dec 2009



Waziri Chikawe asema Kikwete hawezi kuwabana mafisadi
*Asema Rostam, Dk Hoseah hawakamatiki
*Asikitika DPP, DK Hoseah kuparuana

Na Leon Bahati

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe amesema Rais Jakaya Kikwete hana uwezo kutumia mamlaka yake kuwapeleka mahakamani watuhumiwa wa ufisadi kwani hilo ni jukumu la vyombo alivyoviteua kuchunguza na kuchambua nani afikishwe huko baada ya kujiridhisha kwa ushahidi.

"Huu ni utawala wa sheria, Rais Kikwete hawezi kutoa amri za kukamata watu wakati kuna vyombo alivyoviteua kuchunguza na kuchukua hatua." Waziri Chakawe alisema hayo jana alipokuwa katika mahojiano maalumu na gazeti hili ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Alisema kitendo cha baadhi ya Watanzania kumshinikiza Rais Kikwete awafikishe mahakamani watuhumiwa wa ufisadi kinaashiria kuwa wanataka aamuru watuhumiwa hao wapelekwe mahakamani bila kutumia vyombo husika jambo ambalo haliwezekani katika mfumo wa kibepari.

"Enzi zile za mfumo wa ujamaa na chama kimoja cha siasa, hilo lingewezekana lakini wakati huu ambao nchi inatumia mfumo wa kibepari, haiwezekani," alisema Chikawe.

Hivi karibuni, wanasiasa na hata baadhi ya viongozi waliowahi kuwa serikalini awamu zilizopita, wakichangia mada ya mustakabali wa taifa kwenye kongamano la taasisi ya Mwalimu Nyerere, waliitaka CCM imtose Rais Kikwete asigombee tena ili kumalizia ngwe ya miaka mingine mitano, iwapo atashindwa kufanya maamuzi magumu ya kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi.

Alionya kwamba Rais Kikwete akikurupuka katika hilo, kesi nyingi zitakwaa kisiki mahakamani na itabidi hao wanaoitwa mafisadi kulipwa mabilioni ya fedha kama fidia ya usumbufu.

Chikawe alisema mawazo ya namna hiyo yanatokana na watu wengi kuendelea kuwa na mtazamo wa mfumo wa kijamaa na chama kimoja na kusahau kuwa tayari nchi imeingia katika mfumo wa kibepari.

Waziri Chikawe alitumia mfano wa enzi za waziri mkuu, hayati Edward Sokoine alipopambana na wahujumu uchumi kwa kutoa amri ya kukamatwa watu ovyo na kutaifishwa mali zao kuwa moja ya mifano ya uongozi katika mfumo wa ujamaa.

Alisema amri hizo zilikubalika kulingana na mazingira ya wakati lakini, ulipoanza kuingia mfumo wa kibepari waliopoteza mali kupitia operesheni hiyo walidai haki kupitia mahakama na walishinda hivyo serikali ikabidi iwafidie pamoja na usumbufu.

Waziri huyo mwenye dhamana ya kusimamia katiba na sheria za nchi, ambaye amekuwa kimya licha ya kuwepo na mijadala mingi inayokosoa utendaji wa vyombo vya sheria nchini hasa suala la ufisadi, alisema polisi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wana haki ya kuchunguza makosa ya jinai, lakini pia mkurugenzi wa mashtaka (DPP) ana mamlaka ya kutoruhusu kesi hizo zisiende mahakamani kama hakutakuwa na ushahidi wa kutosha.

Alitoa mfano wa Mbunge wa Igunga, Rostam Azizi (CCM) ambaye wengi wamekuwa wakimtuhumu kwa ufisadi kupitia kashfa ya kampuni tata ya Richmond iliyopewa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura mwaka 2006, akisema hakuna ushahidi wa kumfikisha mahakamani.

"Wewe jaribu kuipitia ile ripoti ya Kamati Teule ya Bunge ya (Dk Harrison) Mwakyembe, hata uipitie mara 10. Mimi nimeipitia mara nane, sijaona sehemu ya kupata ushahidi wa kumshtaki," alisema Chikawe.

Kuhusu anwani ya barua pepe ya kampuni ya Caspian ambayo inamilikiwa na Rostam kutumiwa na kampuni iliyoirithi Richmond, alisema: "Ni sawa, lakini hadi sasa hakuna mahali popote ambapo kampuni ya Dowans inatuhumiwa. Yenyewe ilipokea jukumu ambalo Richmond ilishindwa lakini wao wakatekeleza. Ingekuwa Dowans wana matatizo, basi hata Rostam angeweza kuhusishwa."

Alizungumzia shinikizo la kutaka Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hoseah awajibishwe kwa madai ya kuficha madhambi ya Richmond ambayo kamati ya Dk Mwakyembe iliyaweka wazi, alisema:

"Takukuru ilichunguza mwenendo wa utoaji wa zabuni kwa Richmond na kwenye ripoti yake ikaeleza haikuona fedha zilizotumika kurubuni mtu yeyote. Na hata kamati ya Dk Mwakyembe haikubaini kitu cha namna hiyo.

"Kamati ya Dk Mwakyembe imebaini udhaifu wa serikali kuchunguza Richmond kabla ya kuingia mkataba na hili ndilo lililofanya Lowassa na wenzake kujiuzulu na Baraza la Mawaziri kuvunjwa."

"Lakini uzuri ni kwamba Rais Kikwete alikuwa ameagiza wasipewe fedha hadi wawe wameleta mitambo nchini na hilo lilifanyika. Kampuni ya Richmond haikuchukua hata senti ya serikali. Kama ilihonga watu kwa siri huko, ilikula kwao. Ila tunachojua walishindwa kuleta mitambo ya kuzalisha umeme wakatoa kazi hiyo kwa Dowans ambao walifanikisha."

Pamoja na hali hiyo, Chikawe alisema Mtanzania yeyote mwenye ushahidi unaoweza kuwashtaki wanaotuhumiwa ni vyema akawasiliana na Mpelelezi Mkuu wa Makosa ya Jinai (DCI) au Takukuru.

Kuhusu majibizano yaliyotokea hivi karibuni baada ya Dk Hosea kumlaumu DPP, Elieza Feleshi kwa kukalia mafaili zaidi ya 60 ya kesi za ufisadi na baadaye Feleshi kumjibu kuwa ni muongo, Chikawe alisema ni jambo ambalo halikumpendeza.

"Kwa kweli imekuwa bahati mbaya vyombo hivi vya serikali kulumbana vyenyewe, lakini nafikiri ilikuwa ni bahati mbaya tu, wakati mwingine hilo halitatokea," alisema Chikawe.

Hata hivyo, alisema huenda lilichangiwa pia na vyombo vya habari kwa kuchokonoa mambo hayo hivyo kuwafanya kutoa kauli ambazo pengine zilionekana kuhitilafiana.

Chikawe ambaye ni Mbunge wa Nachingwea alisisitiza kwamba DPP amekuwa akipelekewa mafaili mengi na anapoona hayana ushahidi wa kutosha huwashauri wahusika mambo ya kufanya na pengine kuwaeleza kwamba hakuna kesi ya kujibu.

CHANZO: Mwananchi

13 Dec 2009


Mara Sophia Simba dhidi ya Anne Kilango,mara Rostam Aziz dhidi ya Mwakyembe,mara tunaambiwa Kamati ya Mwinyi nako "hakieleweki",na sasa watendaji wakuu na wateuliwa muhimu wa Rais,Mkurugenzi wa TAKUKURU Dr Edward Hosea na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) Eliezer Feleshi nao wameingia kwenye malumbano,kama linavyoripoti jarida la Mwananchi

DPP amvaa Dk Hoseah, ataka mdahalo majalada kesi za kifisadi

Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah ambaye jana alidai kuwa DPP amekalia kesi 60 tuhuma za rushwa

James Magai

KWANZA ilikuwa ni ndani ya chama tawala CCM, lakini malumbano baina ya vigogo sasa yamehamia serikalini baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Eliezer Feleshi kujibu mashambulizi ya mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah, akitaka uitishwe mdahalo baina ya wawili hao ili ajibu tuhuma dhidi yake.

Pendekezo hilo la Feleshi limekuja wakati malumbano baina ya viongozi wa CCM hayajapoa baada ya kutuhumiana kwa ufisadi na wivu wa nafasi mbalimbali zilizotokana na uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

Dk Hoseah, ambaye amekuwa akirusha makombora kwa taasisi tofauti, juzi alitoa tuhuma nzito alipokaririwa na gazeti moja akisema kuwa ameshawasilisha kesi zaidi ya 60 za tuhuma za rushwa kwa DPP na akashangaa sababu za mteule huyo mwenzake wa rais kukalia mafaili hayo badala ya kufungua kesi dhidi ya watuhumiwa.

Lakini jana Feleshi alikuwa mbogo na akasema kuwa ili ukweli uwekwe bayana kuna haja ya kuandaa mdahalo baina yake na Hoseah.

DPP Feleshi, akizungumza na gazeti dada la Mwananchi la The Citizen baada ya hafla ya mafunzo ya kamati ya kitaalamu ya mawakili wa serikali iliyofanyika Kunduchi jijini Dar es Salaam, alisema njia pekee ya kuweka sawa rekodi ni kuwepo kwa mdahalo huo wa wazi.

"Ninataka mdahalo na Hoseah katika masuala haya yanayoendelea hata kama utakuwa wa simu tena iwekwe ‘loud speaker (kipaza sauti)’ ili tujadili masuala haya na kumaliza kiu ya wananchi," aliweka msimamo DD Feleshi.

"Kama mtu anasema kuna majalada 60 ofisini kwangu, then (kisha) tunamuuliza yamefika lini? Yeye pia atajibu, kwa kufanya hivyo tutatoa mwanga mzuri kwa wananchi ambao ofisi hizi zipo kwa ajili yao tu."

DPP Feleshi alisema anataka mdahalo huo ufanyike mbele ya waandishi wa habari ili jamii ijue masuala mbalimbali yanayoelekezwa ofisini kwake.

Hoseah pia aliwahi kuirushia kombora mahakama akisema inaendesha taratibu kesi za ufisadi, hivyo kupunguza kasi ya taasisi hiyo kushughulikia watuhumiwa wa rushwa.

Miongoni mwa kesi ambazo zilifunguliwa kwa wingi hivi karibuni na Takukuru ni pamoja na kesi zaidi ya 20 zinazohusu wizi kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), matumizi mabaya ya madaraka na uzembe na tuhuma za kula njama na kuisababishia hasara serikali.

Hata hivyo, mwenendo wa kesi nyingi umekuwa wa kasi ndogo kutokana na upande wa mashtaka kutokamilisha ushahidi.

Akizungumzia madai hayo ya Hoseah, Feleshi aliweka bayana kwamba hayajui majalada hayo na anachojua ni kwamba ofisini kwake kuna majalada ya kesi ambayo yanaingia na kutoka kila siku na anayashughulikia kwa mujibu wa sheria.

Feleshi, ambaye aliwahi kurejesha Takukuru baadhi ya majalada kutokana na kuonekana udhaifu katika ushahidi, alimtaka Dk Hoseah kutoa ufafanuzi kwa kueleza ni majalada gani yanayokaliwa na ofisi yake na yamefika lini.

Alifafanua kwamba ofisi yake haiwezi kukalia majalada kwa kuwa inafanya kazi kwa mujibu wa sheria na kwa maslahi ya umma na kusisitiza hayajui majalada hayo 60 anayodai Dk Hoseah kwamba yamekaliwa ofisini hapo.

"Hayo mafaili (majalada) ya vigogo mimi siyajui. Ninachojua ni kwamba tuna majalada yanaingia kila siku ya Watanzania wanaotuhumiwa. Tunapokea na kuyafanyia kazi... na hatubagui kuwa haya ni ya PCCB (Takukuru) , TRA( Mamlaka ya Mapato) au ya Polisi. Katiba ya nchi inatoa haki sawa kwa wote kufikishwa mbele ya sheria ili kupata haki," aliongeza DPP.

"Tunafanya kazi kwa maslahi ya umma na tunaendesha shughuli zetu kisheria wala si kwa kuzingatia jambo lolote kwa kuwa hatuna maslahi yoyote kumshtaki mtu bila kuwa na ushahidi wala hatuna maslahi yoyote kumwachia mtu kama kuna ushahidi. Ndiyo maana nasema hakuna kukalia majalada."

Feleshi, ambaye ana mamlaka ya kufunga au kufungua mashtaka kwa watuhumiwa, alisema katika hali hiyo ni vigumu kusema kuna majalada yana muda mrefu kwani hajui hayo yanayosemwa yaliingia lini ofisini kwake.

"Labda kama angekuwepo mwenyewe (Dk. Hoseah) angeeleza zaidi hayo majalada anayodai tumeyakalia. Ni vema mkamuuliza hilo," alisema.

Hizi ni dalili za wazi kwamba kuna ombwe la uongozi wa kitaifa.Yaani kila mtu anaropoka anavyopenda hasa kwa vile mwenye jukumu la kukemea yuko usingizini fofofo.Nidhamu imekuwa zero kwa vile anayepaswa kuwaadabisha watovu wa nidhamu yuko bize na mambo mengine yasiyo na umuhimu kwa taifa.

Tunaelekea pabaya japo Watanzania wengi hawaonekani kuguswa na hali hii.

Ni vema tukaamua kuchukua maamuzi mazito kabla hali haijafikia mahala tusipoweza kurekebisha.Tusipoziba ufa tujajenga ukuta.Unfortunately,baada ya ukuta kuanguka kutokana na nyufa zilizopo tunaweza kushindwa kujenga ukuta huo baada ya matofali yote na tanuru zima kuuzwa na mafisadi.

2010 INAKUJA.IT'S THEN OR NEVER!

5 Dec 2009


TOFAUTI na alivyojigamba kwamba ni mlipaji mzuri wa madeni anayodaiwa na serikali, Mbunge wa Igunga, Rostam Azizi anadaiwa Sh. 2,576,583,013 tokea mwaka 1993, MwanaHALISI limegundua.

Alikopeshwa Sh. 2 bilioni (2,025,739,660) mwaka 1993 na 1997 na Mfuko wa Kuwezesha Uagizaji Bidhaa (CIS) uliokuwa ukifadhiliwa na serikali ya Japan na kusimamiwa na Wizara ya Fedha na Uchumi.

Alitumia makampuni ya Africa Tanneries Ltd, Tanzania Leather Industries Ltd na Africa Trade Development.

Fedha nyingine alizokopeshwa ni Sh. 1,516,024,125. Hizi alikopeshwa na serikali ili kuagiza mchele kupitia mpango wa Counterpart Fund. Alitumia Kampuni ya African Trade Development.

Imethibitika kwamba Rostam ameshindwa au hataki kulipa deni hilo lililodumu kwa miaka 16 sasa.

Akizungumza na vyombo vya habari 3 Mei 2009, siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani, kwenye Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski jijini Dar es Salaam, Rostam alitamba kuwa ni mlipaji mzuri wa madeni yake kwa serikali.

Alikuwa akijibu tuhuma mbalimbali za ufisadi anaodaiwa kufanya kwa kutumia makampuni yake mbalimbali. Gazeti hili lina kumbukumbu za jinsi alichukua fedha hizo, zilizokusudiwa kuboresha biashara nchini.

Uchunguzi umebaini kuwa mwaka 1993 alichukua Sh. 280 milioni kupitia Kampuni ya African Tanneries Limited. Mwaka 1997 alitumia Kampuni ya Tanzania Leather Industries Limited kuchukua Sh. 725,943,120.

Mwaka huohuo Rostam alitumia Kampuni yake nyingine ya African Trade Development kubeba Sh. 1,019,796,540 kutoka mfuko huo.

Mwishoni mwa mwaka jana, baada ya ‘mshike mshike nguo kuchanika,’ Rostam alilipa Sh. 500 milioni akikusudia kupunguza deni la “mchele.”

Lakini kutokana na kuwepo deni jingine la zaidi ya Sh. 1bilioni katika mfuko wa CIS, mamlaka husika zikaamua kutumia kiasi hicho kupunguza madeni hayo.

Kwa sasa anadaiwa na mfuko huo Sh. 1.060,558,888. Deni hilo likijumlishwa na deni alilokopa kuagiza mchele, Rostam anadaiwa jumla ya Sh. 2,576,583,013. Katika mazungumzo yake na serikali kwa nyakati tofauti, alikiri na kuahidi kulipa ingawa hadi sasa ameendelea kukaidi kulipa.

MwanaHALISI limebaini kuwa tayari mmoja wa wanasheria jijini Dar es Salaam, anayeshughulikia suala la kukusanya madeni hayo anaandaa taarifa ya kisheria itakayokabidhiwa kwa wadeni sugu wakati wowote kuanzia sasa.

Jukumu jingine analotekeleza mtaalamu huyo wa sheria ni kumshauri Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, kufanya mpango wa kutumia mamlaka ya Kamishna Mkuu wa TRA ili kutekeleza azma ya kufilisi mali za Rostam na vigogo wenzake wanaodaiwa.

Pamoja na Rostam, wadeni sugu wengine ambao walizungumza na serikali, wakakiri kudaiwa na wakaahidi kulipa madeni kwa kadri walivyoomba lakini badala ya kulipa wakaingia ‘mitini’ ni pamoja na Mbunge wa Temeke, Abass Mtemvu (CCM).

Mbunge huyo mwaka 1998 alitumia Kampuni ya A.M. General Agency kukopa Yen 20,000,000 sawa na Sh. 280 milioni. Ingawa alikiri kudaiwa na kuahidi kulipa deni, hadi sasa hajalipa hata shilingi moja.

Aliyewahi kuwa Waziri wa Utumishi na Mbunge wa Mlangege, Zanzibar, Fatma Said Ali (CCM), mwaka 1998 alitumia Kampuni ya Tanzania Save Way Co. Ltd., kukopa Yen 20,000,000 lakini akakopeshwa Yen 10,000,000 sawa na Sh.140 milioni. Aliwahi kupunguza Sh. 23,400,000 tu.

Aliyewahi kuwa mkuu wa mkoa wakati wa serikali ya awamu ya pili na ya tatu, ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Henry Shekiffu, mwaka 2000.

Alitumia kampuni ya Shemshi & Sons Limited kukopa Sh. 399,560,000. Amewahi kupunguza Sh. 65,340,051. Hadi sasa anadaiwa Sh. 279,653,794.

Nicodemas Banduka, mwaka 2000 alitumia kampuni ya Kadolo Investment kukopa Yen 105,210045 sawa na Sh. 147,294,630. Aliwahi kulipa Sh. 22,500,000. Hadi sasa anadaiwa Sh.124,794,630.

Mwingine ambaye arobaini zake zimekaribia ni aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), David Mattaka, aliyetumia kampuni ya Petmon Investment, mwaka 2000. Alikopa Sh. 140 milioni, aliwahi kupunguza Sh. 24,712,200. Hadi sasa anadaiwa Sh. 115.287,800.

Ufuatiliaji unabainisha kuwa idadi kubwa ya makampuni yaliyotumiwa na vigogo hao yalianzishwa kwa lengo la kuchota fedha hizo. Mengi kati ya hayo hayapo tena.

Vigogo wengine waliobainika kukopeshwa na CIS lakini taarifa hazielezi kama mali wanazomiliki pia zitafilisiwa, ni aliyekuwa mbunge wa Sengerema, Dk. William Shija ambaye sasa ni Katibu wa Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola.

Alikopa Sh. 140 milioni kwa kutumia kampuni ya Pyramid Investments Limited, mwaka 2000. Amewahi kupunguza Sh. 22,650,000.

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wassira, naye jina lake limo kwenye orodha ya wanaodaiwa ingawa taarifa muhimu, mathalani alikopa kiasi gani, lini na amelipa au bado hazionyeshwi katika kumbukumbu hizo.

Ingawa serikali inaelezwa kuwa kwenye hatua za kukamilisha mipango ya kufilisi mali za wadeni wake hao na wengine, bado inasuasua.

Mkataba wa kufanikisha mikopo hiyo unaruhusu serikali kupitia kwa Kamishna Mkuu wa TRA kufilisi mali za asiyetekeleza mkataba katika kipengele cha kulipa, tena bila kulazimika kwenda mahakamani. Haijafahamika kwa nini TRA haijachukua hatua hiyo.

Dhana inajengeka kwamba huenda “kigugumizi” hicho katika kukusanya madeni ya walipa kodi wa Tanzania, kinatokana na wadaiwa wengi kuwa vigogo ambao miongoni mwao bado wapo kwenye nyadhifa za juu serikalini.

CIS ilianzishwa kwa nia njema ya kukuza sekta ya biashara nchini, kwa kuwasaidia wafanyabiashara kufanya biashara za kimataifa. Kuagiza bidhaa mbalimbali kutoka nchi tofauti, zilizofadhili mpango huo.

Mpango huo ulikuwa ukitekelezwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na Uchumi. Hata hivyo taarifa zinaonyesha kuwa jumla ya Sh. 44 bilioni zilichotwa na wizara nane katika mazingira ambayo hadi sasa serikali haijafafanua.

CHANZO: Mwanahalisi

INAUDHI,INAUMA NA KUSONONESHA LAKINI IT LOOKS AS IF NCHI HAINA WENYEWE KWANI WALIOIBIWA WAKO KIMYA KANA KWAMBA WAMERIDHIKA.JE TUMEKUBALI UFISADI KUWA SEHEMU YA MAISHA YETU YA KILA SIKU?

3 Dec 2009


Sijui tuiweke CCM katika kundi gani maana kila kukicha ni songombingo moja baada ya nyingine.Of course,migongano ni jambo la kawaida kwani hata ukiweka glasi katika boksi moja zinaweza kugongana kama si kuvunjika kabisa.Ndio maana maboksi yaliyosheheni glasi huwa na tahadhari "handle with care" au "fragile".

Pengine kabla sijaendelea na mada yangu kuhusu utovu wa nidhamu unaoendelea ndani ya chama tawala CCM,huku Katibu Mkuu Yusuph Makamba akitoa kauli zisizoendana na hadhi yake katika jamii,ni vema ukasoma habari ifuatayo kisha tujadili kidogo:

Makamba awatukana wanaoshauri Kikwete asigombee 2010

Rais Kikwete kongamano la Nyerere limemweka katika lawama za kutokuwa na maamuzi na kuwa asipendekezwe kugombea awamu ya pili.

Na Leon Bahati
KATIBU mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, ambaye katika miezi ya karibuni amekuwa akihaha kutoa ufafanuzi, kukanusha au kujibu tuhuma mbalimbali dhidi ya chama hicho tawala, jana alikuwa na kazi nyingine ya kumtetea Jakaya Kikwete baada ya waziri katika serikali ya awamu ya tatu kushauri asiteuliwe kugombea urais 2010 iwapo atashindwa kufanya maamuzi magumu dhidi ya mafisadi.

Safari hii, Makamba alitumia maneno makali kumjibu waziri huyo, Matheo Qares akisema watu wenye fikra kwamba CCM inaweza kumtosa mwenyekiti wake kwenye mbio za urais wakati wa uchaguzi mkuu wa mwakani, "ni wehu".

Qares, ambaye aliwahi kushika wadhifa nyeti wa Waziri wa Menejimenti ya Utumishi wa Umma, alitoa rai hiyo juzi kwenye kongamano la kumuenzi muasisi wa taifa la Tanzania aliposema kuwa CCM haina budi kutafuta mwanachama mwingine wa kugombea nafasi ya urais mwaka 2010 iwapo Kikwete atashindwa kufanya maamuzi magumu dhidi ya mafisadi, ambao alisema hawakijui chama na wengine uraia wao una utata.

Lakini jana, Makamba alisema watu wenye fikra hizo ni wehu kwa kuwa uteuzi wa wagombea ndani ya CCM ni mchakato usiotoa ruhusa kwa mawazo binafsi ya watu.

"Mtu mwenye akili nzuri hawezi kusema kwamba Rais Kikwete ameshindwa kutekeleza wajibu wake. Anayefikiria hivyo, ni mwehu," alisema Makamba alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu kauli hizo.

Alisema ni vyema watu hao wakafahamu kuwa mgombea urais wa CCM anateuliwa kwa mujibu wa taratibu za chama kupitia vikao mbalimbali hivyo, wazo binafsi halina nafasi.

Alipoulizwa kuhusu shutuma zinazoelekezwa kwa Rais Kikwete, Makamba alisema asingependa kujibu hoja zilizotolewa na mjumbe mmoja mmoja kwenye kongamano hilo.

Lakini akaeleza kwamba yupo tayari kutoa maoni yake binafsi baada ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere kuwasilisha kwake mapendekezo waliyofikia kwenye kongamano hilo.

"Mimi mwenyewe sikuwepo kwenye kongamano hilo. Wala sijui mapendekezo yao. Siwezi nikatolea maoni hoja za mtu mmoja mmoja alizotoa kwenye Kongamano hilo. Nitakapopata mapendekezo ya jumla ya taasisi hiyo, nitakawa katika nafasi nzuri ya kutoa maoni yangu."

Katika kongamano hilo, Rais Kikwete amekuwa akilaumiwa kwa kutochukua hatua dhidi ya watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wengi wao wakielezwa kuwa ni wafanyabiashara ambao wanatuhumiwa kukiteka chama kwa kutumia nguvu zao za pesa.

Wakati fulani Joseph Butiku, mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere ambayo iliandaa kongamano hilo, alisema Rais Kikwete amezungukwa na mafisadi ambao wanaitafuna nchi.

Akizungumza kwenye kongamano hilo juzi, Qares alisema rais hana budi kufumba macho na kuwashughulikia hao watuhumiwa ambao wanadai Kikwete hakujuana nao barabarani na kama atashindwa basi ashauriwe kuwa miaka yake mitano inamtosha.

Kabla ya Qares, Musa Nkangaa, ambaye aliwahi kuwa waziri kwenye serikali ya awamu ya pili, aliituhumu CCM kuwa imepoteza hadhi na kujikuta ikikumbatia matajiri wachafu.

Kwa mujibu wa Nkangaa, CCM imekuwa si chama cha wakulima na wafanyakazi tena, bali kimebaki kuwa chama cha matajiri.

"Ndiyo maana imekuwa ikiweweseka kuwashughulikia watuhumiwa wa Richmond na Kagoda," alisema akimaanisha kashfa ya utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa Richmond Development Company LLC na tuhuma za wizi wa mabilioni ya fedha kutoka BoT.

CHANZO: Mwananchi

Tatizo kubwa la watawala wetu ni yale mazowea waliyojijengea ya kupigiwa makofi na vigeregere hata wanapoongea pumba.Ni katika mstari huohuo,kauli na mawazo mbadala huchukuliwa kuwa ni mithili ya kosa la uhaini.Sidhani kama kuna ubaya kwa wana-CCM kumpa changamoto mwenyekiti wao kama ambavyo Mtanzania yeyote mwenye mapenzi ya dhati anavyostahili haki ya kukemea mwelekeo mbovu wa nchi yetu.

Japo naafikiana na Makamba anapokumbusha wana-CCM wenzie kwamba chama hicho kikongwe kina utaratibu wake wa kumpata mgombea urais lakini hiyo sio sababu ya kuwaziba midomo wale wanaodhani mwanachama mwenzao waliyempitisha kugombea urais katika uchaguzi uliopita,na kushinda,yaani Jakaya Kikwete,ameshindwa kukidhi matarajio ya wana-CCM hao (kama Matheo Qareshi).Sio tusi kutoa mawazo kuwa flani ameshindwa hasa pale kauli kama hiyo inapoambatana na mifano hai kadhaa.

Sidhani kama Makamba anafanya hivyo kwa ile anaamini kuwa Qaresi ni mwehu (ikumbukwe Mtanzania huyo alishawahi kushika nyadhifa za juu ikiwa ni pamoja na uwaziri katika ofisi ya rais) bali ni muendelezo wa kasumba ya kujikomba.Kwa Makamba kumhukumu Qaresi kuwa ni mwehu amekwepa ujasiri wa kujadili hoja badala ya kumjadili mtu.

Ni muhimu tuwe wakweli na wawazi katika kujadili hatma ya taifa letu.Ni dhahiri kuwa vita dhidi ya ufisadi inakwamishwa na mwenye jukumu la kuchukua hatua.Hatuwezi kufanikiwa katika mapambano dhidi ya rushwa (kama yapo at all) ilhali ilishashauriwa kwamba Mkurugenzi wa TAKUKURU,Edward Hosea,ang'olewe madarakani kutokana na kuhusishwa na utapeli wa Richmond.Ushauri huo ulitolewa pia kuhusa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Johnston Mwanyika.Huwezi kuwalaumu Hosea na Mwanyika kwa vile hawakujiteua kushika nyadhifa hizo.Aliyewateua yupo na amesikia yaliyosemwa dhidi yao lakini kaamua kupuuza.

Kwa hakika kama tunataka kuiona Tanzania ikijikomboa kutoka katika lindi la umasikini unaochangiwa kwa kiasi kikubwa na ufisadi,basi ni dhahiri tunahitaji kuangalia makosa yaliyofanyika mwaka 2005 na kuhakikisha hatuyarudii katika uchaguzi mkuu ujao hapo mwakani.Haya mambo ya kuangalia haiba ya mtu na pasipo kujali kama haiba hiyo inaendana na uwezo wa kazi yameshatufikisha hapa,na tukizubaa yatatupeleka pabaya zaidi,

Kinachisikitisha ni mwamko mdogo mingoni mwa Watanzania wa tabaka la kati (the middle class).Tabaka hili lina nafasi nzuri ya kuunganisha nguvu na tabaka la walalahoi ili kulibana tabaka tawala ambalo so far limeji-identify kama sehemu muhimu ya ustawi wa ufisadi na mafisadi.

Inawezekana kabla hatujachelewa.






Honorable office of Senate
Federal Republic of Nigeria
Senate Building Wuse Abuja


FROM; Senator. David Mark,
Senate President Federal Republic of Nigeria.

Dear Beneficiary,

SENATE COMMITTEE ON OUTSTANDING FOREIGN PAYMENT.

May i use this juncture to notify you that our new Government have Paid the bills
which was the cause of the delay of your Payments, and the Office of presidency in conjuction with Senate Commette on outsatnding Foreign Payment have Concluded arrangement with Central Bank of Nigeria and BCEAO to raise International Certified Bank Draft in the tone of $1,000,000.00 (One Million United Staes Dollars) and send across to you upon receipt of the bellow informations through, there Accredited Attoney.

WARNNING/ADVISE: Please note carefully that any fee of any kind DOCUMENTATIONS, COURIER, BRIBE OR GIFT requested from you by anybody, office,banks or group of people from Africa/Nigeria or any part of the world to receive your payment,Except legal fee of the R.E.D.L of FORCE OF NATURE which is just $150.00. is at your OWN RISK, so stay away from any other office, person or group of people and commence communication with only the Central Bank of Nigeria Carredited Attorney till you receive your Certified Bank Draft Deposit With your Bank and Confirm your part payment within Three Bank Working days.

We are really sorry for all the incoviniences you have suffered in the cost of receiving your funds from our Government. Also we assure you that we are doing everything possible to release the Balance of your payment to you by Janaury 2010. we wish to effect this part payment of $1,000,000.00 through the International Certified Draft system to avoid another stress of K.T.T and so on with our banks.and our Government has mandated and paid the FEDEX COURIER SERVICE for the services of delivery the Draft to you.

Therefore, YOU have to get in touch with Central Bank of Nigeria Acredited Attorney Barr. Mike Obi via email or telephone immediately. Below are his contacts

Contact Attorney In-charge : Barr. Mike Obi Tel: 234-1-7652522 EMAIL:([email protected])

Fill bellow informations and Send back to him with R.E.D.L FORCE OF NATURE fee of $150 only. to enable him proceed with the procument of your R.E.D.L FORCE OF NATURE PERMIT from the Legal Department and submit to the Central Bank of Nigeria for onward issuance of your International Certified Draft.

* Full Names.................
* Address. (not P.O.Box)..............
* City..................
* State.................
* Postal Code...........
* Phone.................
* Fax.......................
* Email................
* Age...................
* Marital Status...............
* Sex...............


CHEERS ,
Senator David Mark
Senate President Federal Republic of Nigeria.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.