28 Mar 2009

(Photo credit:JIJI LA DAR)

Mayor threatens legal action against street name changers

SEBASTIAN MRINDOKO
Dar es Salaam

A TOP local government official in Dar es Salaam has roundly rebuked the ongoing trend of people clandestinely changing street names in the city without following proper channels, including getting the blessing of the City Fathers.

According to the Mayor of the Ilala Municipality, Abuu Jumaa, legal action will certainly be taken against such people once sufficient proof is obtained.

Referring specifically to a query by THISDAY on the name-change applied to one of the city’s most historically famous thoroughfares Kisutu Street, now apparently going by the name of ’PRAMUKH SWAMI’, Mayor Jumaa stated unequivocally:

’’My office has never received an official application to change the Kisutu Street name into an Indian name. Therefore, such an action is an insubordination to the city authority.’’

The mayor’s statement is a direct contradiction of that made last year by the former deputy mayor of the same Ilala Municipality, Mohamed Yakoub, who asserted in an interview with THISDAY that the Kisutu Street name-change had been given a formal stamp of approval.

’’All the (Ilala) municipality legal procedures were properly followed in changing the name of not only Kisutu Street, but also some other streets around the city centre,’’ Yakoub said.

But according to current mayor Jumaa, there are no records whatsoever showing the change of the traditional Kisutu name to ’PRAMUKH SWAMI.’

THISDAY last year ran a series of articles on the increasing trend of various streets within Dar es Salaam’s central business district, suddenly acquiring bizarre-sounding new names in highly mysterious circumstances.

It has been noted that skepticism is on the rise amongst members of the general public over the supposed ’secrecy’ shrouding the whole exercise, with open suggestions that corruption at certain local government levels may be involved.

The Dar es Salaam City Director, Bakari Kingobi, has conceded in the past that such street name changes could very easily cause confusion particularly for tourists who may be trying to find their way around the metropolis using officially-approved city maps.

According to Kingobi, only the city authorities have the mandate to administer such street name changes.

’’There is only one city authority - not two - responsible for administering such name-changes to the city streets. Anyone who tries to do so without informing this city authority, is violating the law and is liable for prosecution,’’ he said.

Speaking to THISDAY yesterday, Ilala Municipality mayor Jumaa said it amounted to sacrilege for anyone to change a street name on the basis of racial, tribal, or religious beliefs.

’’There are some basic criteria used to endorse suggestions for street name changes. Bias of any sort is not one of them,’’ he asserted.

He also said streets with traditionally famous names like Kisutu should be left alone, while anyone wanting to recommend a street name to suit their own needs should look for streets with no names at all � of which apparently there are still many.

According to Jumaa, the municipal authorities will seek explanations from the local government authorities regarding the Kisutu Street name-change in particular.

Any official found to have been responsible for wrongdoing in the whole episode will be taken to task through legal channels, he added.

SOURCE: ThisDay


Aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge (61), amewekwa chini ya ulinzi katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar es Salaam, kwa zaidi ya saa saba baada ya kuhusishwa na ajali ya gari na bajaj ambayo imeua watu wawili. Waliokufa ni wanawake wawili ambao ndugu amejitokeza na kudai kuwa wote ni wageni, waliwasili juzi Dar es Salaam kutoka Mwanza na mmoja alikuwa njiani kwenda Zanzibar kuolewa. Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, ajali hiyo ilitokea saa 10 alfajiri usiku wa kuamkia jana wakati Chenge akiendesha gari namba T 512 ACE aina ya Toyota Hilux na kuigonga bajaj hiyo namba T 736 AXC iliyokuwa na abiria hao wawili wanawake.

Chanzo hicho kilidai kuwa baada ya ajali hiyo, Chenge alikwenda kwanza nyumbani kwake na kuripoti kituoni hapo saa moja asubuhi jana na kuwekwa chini ya ulinzi na kuhojiwa hadi saa saba mchana, huku nje akisubiriwa na ndugu zake. Gazeti hili lilimshuhudia mbunge huyo wa Bariadi Magharibi akiingizwa kwenye gari la Polisi namba PT 0217 na kwenda eneo la tukio karibu na shule ya msingi ya Oysterbay katika makutano ya barabara za Karume na Haile Selassie, ambako alieleza namna ajali hiyo ilivyotokea.

Wakati mbunge huyo akitolewa katika kituo cha Polisi, kulitokea vurugu baina ya ndugu zake na waandishi wa habari, ndugu hao wakitaka kuzuia Chenge kupigwa picha, hali iliyosababisha kusukumana na kurushiana maneno makali. “Ninyi mmezidi kumwonea huyu kwani ni lazima mumpige picha ndio muuze? Hebu tokeni hapa,“ alisikika mwanamke ambaye alikuwa mstari wa mbele kusukuma waandishi, huku akilia na almanusra wapigane na mmoja wa wapigapicha waliokuwa kazini.

Hata hivyo, vurugu hizo zilimalizika baada ya waandishi kuwazidi nguvu ndugu hao na kung’ang’ania kumpiga picha mbunge huyo ambaye awali alikuwa akifunikwa magazeti na nduguze, lakini aliyatoa na kupisha waandishi wampige picha vizuri. Akiwa katika eneo la tukio, Chenge alimwelezea Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Peter Kivuyo, namna ajali hiyo ilivyotokea na alidai ilitokea baada ya bajaj hiyo kutaka kupita gari jingine kwa kasi.

“Bajaj ile ilikuwa inataka kupita gari jingine lililokuwa likitoka Morogoro Stores, bahati mbaya kukawa na gari lingine linakuja, ile bajaj ikabana upande wangu na mimi nilikuwa katika mwendo wa kati ya kilometa 80 hadi 100 kwa saa,“ alidai Chenge. Alidai kuwa baada ya kuona bajaj ile inakwepa gari la mbele wasigongane uso kwa uso, alirudi upande wa kulia ndipo alipoigonga ubavuni kushoto. "Gari la nyuma lingesimama, dereva wake angeweza kueleza vizuri, ila baada ya ajali nikasikia watu wanaita 'Chenge! Chenge!’ nikajua niko salama, nikashuka,“ alidai.

Aliendelea kudai kuwa aliposhuka, alikuta abiria wawili wanawake wakiwa bado wanapumua ingawa kwa shida, lakini walipofika trafiki hali zao zilizidi kuwa mbaya na katika kipindi hicho chote, dereva wa bajaj alikuwa haonekani. Naye askari wa usalama barabarani aliyefika katika ajali hiyo, Mustafa Salum, alimweleza Kivuyo juu ya tukio hilo, ambapo alisema alipata taarifa za ajali hiyo saa 10.30 alfajiri na alipofika eneo la tukio, alikuta tayari abiria hao wawili wameshafariki dunia. “Niliipeleka miili ya marehemu hospitali ya Mwananyamala, ila kwa mujibu wa watu waliokuwa eneo la tukio, waliowaona marehemu hao wawili katika ukumbi wa Maisha Club,“ alisema.

Naye kaka wa mmoja wa marehemu hao, January Constantine, alisema alipata taarifa za kifo cha dada yake, Beatrice Constantine (34) asubuhi na alikwenda kutambua mwili wake hospitalini, lakini kutokana na alivyopondeka alimtambua kwa alama za mwili. Alisema dada yake ni mfanyabiashara na mkazi wa Mwanza na kwamba aliwasili Dar es Salaam, akiwa na rafiki yake huyo na ilikuwa aondoke jana alfajiri kwenda Zanzibar kwa ajili ya harusi ya rafiki yake huyo. Gazeti hili lilishuhudia gari la Chenge kwa mbele likiwa na damu, nywele na mabaki ya ubongo ambao unasadikiwa kuwa wa mmoja wa marehemu hao. Polisi pia iliokota kipande cha fuvu la mtu katika eneo la tukio.

Gari hilo lilikuwa na stika ya Bima ambayo ilikatwa Juni 6, 2006 na kumaliza muda wake Juni 6, mwaka juzi. Naye Theopista Nsanzugwanko anaripoti kuwa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu Dar es Salaam, Suleiman Kova, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema mmiliki wa bajaj hiyo ni Zuwena Nassoro na anatakiwa kuripoti katika kituo chochote cha Polisi huku wakiwa wanamshikilia Chenge Oysterbay ili kuisaidia Polisi. Alisema uchunguzi wa tukio hilo unafanywa chini ya Kivuyo na wataalamu mbalimbali ili kuondoa dhana ya upendeleo kwa kuwa Chenge ni mtu maarufu.

Chenge (62) alijiuzulu uwaziri wa miundombinu Aprili 20 mwaka jana, kutokana na kashfa ya rushwa ya dola milioni moja kutoka kampuni kubwa ya uuzaji vifaa vya kijeshi duniani ya BAE Systems. Alijiuzulu baada ya kudaiwa kupokea rushwa ili kuwezesha ununuzi wa rada ya kijeshi ya pauni milioni 20 za Uingereza na kwamba fedha hizo ziliwekwa katika akaunti yake ya kisiwa cha Jersey.

Baada ya kujiuzulu, alikaririwa akisema pamoja na tuhuma hizo, mapenzi kwa nchi yake na chama chake, ndivyo vilimlazimisha achukue uamuzi huo na kuongeza kuwa fedha zilizokutwa katika akaunti yake hiyo hazina uhusiano wowote na BAE Systems. Tuhuma hizo za rushwa zilichochea kelele pale alipohojiwa na waandishi wa habari na kujibu kuwa fedha anazotuhumiwa nazo ni 'vijisenti (fedha kidogo)'.

CHANZO: HabariLeo

I SMELL DITOPILE-LIKE ADMINISTRATION OF JUSTICE......KWA UBINADAMU WA KAWAIDA TU,GARI LAKO LIKIHUSIKA KATIKA AJALI INAYOPELEKEA HATARI YA MAISHA YA MAJERUHI PRIORITY INAKUWA KWENYE KUOKOA MAISHA YA MAJERUHI HAO (KWA MUJIBU WA HABARI HII MZEE WA VIJISENTI ALIKWENDA ZAKE NYUMBANI HADI SAA 1 ASUBUHI ALIPORIPOTI KITUO CHA POLISI NA KUHOJIWA KWA MASAA 7-(DOES IT REALLY MATTER HOW LONG THE INTERROGATION LASTED WHEN TWO PEOPLE HAD ALREADY LOST THEIR LIVES?).

ANYWAY,LET'S GIVE THE POLICE A BENEFIT OF DOUBT HOPING THAT THIS TIME HAKUTAKUWA NA USANII KAMA KATIKA ISHU YA MAREHEMU DITO.

27 Mar 2009


DNA tests on Alfie Patten, the 13-year-old boy who was alleged to have become a father when he was just 12, show that he not the baby girl’s actual dad.

The 300-pound test was conducted on him after half a dozen boys claimed to have slept with schoolgirl pal Chantelle Stedman, 15.

Although Alfie was convinced he was the dad after a single night of unprotected sex with Chantelle, the DNA test proved the 4ft-tall pupil was not the father of her seven-week-old tot Maisie Roxanne.

According to The Mirror, Chantelle had told her half-sister Jodie O’Neill, 17, that her daughter’s father could have been one of the boys she slept with at her parents’ home in Eastbourne, East Sussex.

The paper further reveals that the teen girl also said that her mother Penny had ordered her to keep saying that she has been a virgin when she slept with Alfie.
SOURCE: ThisIs50.com


Brazil’s President Luiz Inácio Lula da Silva on Thursday blamed the global economic crisis on “white people with blue eyes” and said it was wrong that black and indigenous people should pay for white people’s mistakes.

Speaking in Brasília at a joint press conference with Gordon Brown, the UK prime minister, Mr Lula da Silva told reporters: “This crisis was caused by the irrational behaviour of white people with blue eyes, who before the crisis appeared to know everything and now demonstrate that they know nothing.”

He added: “I do not know any black or indigenous bankers so I can only say [it is wrong] that this part of mankind which is victimised more than any other should pay for the crisis.”

Mr Brown appeared to distance himself from Mr Lula da Silva’s remarks. “I’m not going to attribute blame to any individuals,” he said.

Mr Brown was visiting Brazil as part of a five-day tour of Europe, the US and South America in preparation for the G20 summit to take place in London next Thursday. He made a joint appeal with Mr Lula da Silva for the world’s biggest economies to provide $100bn to boost global trade.

“I’m going to ask the G20 summit next week to support a global expansion of trade finance to reverse a slide in world trade,” Mr Brown said.

Mr Lula da Silva also spoke out strongly against raising trade barriers in response to the global crisis. “I compare protectionism to a drug,” he said. “Why do people use drugs? Because they are in crisis and they think the drug will help them. But its effects pass quickly.”

The two leaders’ remarks demonstrate the desire each will have to secure the other’s support during the G20 meeting.

Brazil – which has long campaigned unsuccessfully to be given a permanent seat on the United Nations Security Council – will argue for a bigger voice for Brazil and other emerging nations in multilateral organisations such as the International Monetary Fund and the Financial Stability Forum, a group of central banks and national supervisory authorities established in 1999.

Brazil is one of many nations calling for increased regulation of global financial markets and greater powers for multilateral regulators.

It will also call for a resumption and conclusion of the Doha round of talks at the World Trade Organisation.

In return for supporting such initiatives, Mr Brown will expect Brazil to endorse calls for fiscal stimulus in a bid to mitigate the impact of the global crisis, such as the proposed $100bn in trade finance.


SOURCE: FT


KWA MTU YEYOTE MWENYE AKILI TIMAMU,HATA AKIAMSHWA USINGIZINI AU AKIWA BWII KWA ULEVI,HAIINGII KICHWANI KUSIKIA HOJA ZA KIFISADI ZA KUNUNUA MITAMBO ILIYONGIZWA NCHI KITAPELI NA MAJAMBAZI WA RICHMOND NA HATIMAYE KURITHISHWA KISANII KWA WENZAO WA DOWANS.TUKIRUHUSU HILI LITOKEE,KUNA MAHALA ITAFIKA NCHI YETU NAYO ITAUZWA NA KISHA TUTATAKIWA KUINUNUA BACK....


Tausi Mbowe na Elias Msuya

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk Wilbroad Slaa ameitaka serikali kuitaifisha mitambo ya Kampuni ya kuzalisha umeme ya Dowans badala ya kujadili manunuzi yake.

Dk Slaa aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada yakutopa taarifa ya kamati kuu kilichokutana kwaajili ya kuandaa mkutano wa baraza kuu.

Alisema kuwa mitambo ya Dowans ilirithiwa kutoka kwenye kampuni ya Richmond ambayo ilibainika bungeni kuwa ni ya kifisadi kwahiyo hakuna haja ya kuinunua tena bali kuitaifisha.

“Msimamo wangu siku zote ni kutaifishwa kwa mitambo ile na siyo kuinunua. Naishangaa serikali, kutaka kuinunua mitambo ya Dowans wakati mitambo ile ilishabainishwa Bungeni kuwa ni ya kifisadi. Kama mtu umekamata kitu chako cha wizi utakinunua tena?" alihoji

Akizungumzia malumbano kati ya Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, Dk Slaa alisema,

“Mradi wa kuzalisha umeme nimeushughulikia kwa miezi minane. Nilikwenda hadi kijiji cha Kisesida mkoni Singida ambako ndiko kampuni mbili za Power Pool East Africa ya Dk Mwakyembe na wenzake na Wind East Africa ya Rostam Aziz zimewekeza.

Kampuni ya Power Pool East Afrika ni ya wazalendo na imeshalipa fidia kwa wakazi wa kijiji cha Kisesida lakini ile ya Wind East Africa haijafanya hivyo, badala yake inabebwa na kiongozi wa ngazi za juu mkoani ambaye amekuwa akiwakejeli wanakijiji wa Kisesida. Ndiyo maana kuna kuwa na malumbano kati ya Rostam Aziz na Dk Mwakyembe,” alisema Dk Mwakyembe.

Akizungumzia tatizo la mgawo wa umeme ambalo litangazwa na Tanesco hivi karibuni, Dk Slaa alisema,"Baada ya kubainika kwa kashfa ya Richmond, Rais Kiwete alitangaza kuwa suala la mgawo wa umeme litakuwa historia katika nchi hii, sasa mgawo huu unatoka wapi tena? nendeni mkamwulize,” alisema Dk Slaa.

Aidha alimshangaa Rais Kikwete kwa kuendelea kumwacha madarakani Mkurugenzi wa Tanesco, Idriss Rashid wakati anatuhumiwa kwa ufisadi.

"Dk Rashid (PICHANI JUU) alihusishwa na ufisadi alipokuwa Gavana wa Benki kuu. Tumeshatoa vilelezo vyote kuthibitisha jinsi alivyoshiriki kwenye ununuzi wa rada na ndiyo maana sasa hivi anashirkiana na Dowans ili kununua mitambo yake kiufisadi. Tunashangaa kwanini Rais Kikwete hamchunguzi, wala kumwajibisha. Eti wanasema Serikali ya Uingereza inachunguza, wakati si kweli. Uingereza wanachunguza ushiriki wa BAE system siyo watu wetu,” alisema Dk Slaa.



CHANZO: Mwananchi
IT MAKES A LOT OF SENSE,DOESN'T IT?UNAMKAMATA KIBAKA NA MALI YAKO,BADALA YA KUMKWINDA AKUREJESHEE NA HATIMAYE KUMFIKISHA POLISI ETI UNAKUBALI AKUUZIE ALICHOKUIBIA!IT COULD ONLY HAPPEN IN TANZANIA,I SUPPOSE!

26 Mar 2009


YAANI HADI INATIA KIZUNGUZUNGU.HEBU SOMA HABARI IFUATAYO KISHA TUSHIRIKIANE KUJIBU MASWALI NILIYOWEKA BAADA YA HABARI HII

Bunge mradi wa ulaji

na Mwandishi Wetu

WAKATI baadhi ya wabunge wakiendelea kulumbana kupitia katika vyombo vya habari kuhusu masuala mbalimbali yanayogusa maslahi ya taifa,imebainikawamekuwa wakichuma mamilioni ya fedha kupitia katika malipo yao halali ya mishahara, posho na fedha nyingine zisizotokana na malipo yao rasmi wanayostahili.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano umethibitisha pasipo shaka kwamba, fedha ambazo wabunge wamekuwa wakichuma kwa njia mbalimbali kwa kutumia nafasi zao za uwakilishi, zinaweza zikawa sababu mojawapo muhimu ya kuibuka kwa makundi yanayosigana ndani ya Bunge na hususan miongoni mwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, gazeti hili limefikia hatua ya kutilia shaka kwamba, mzozo wa hivi karibuni, kati ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe na mwenzake wa Igunga, Rostam Aziz, kwa kiwango kikubwa unakuzwa kutokana na sababu za maslahi binafsi zaidi kuliko madai ya uzalendo na maslahi ya taifa.

Shaka hiyo ya Tanzania Daima Jumatano inatokana na ukweli kwamba, wabunge hao wawili ambao wote wawili ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kwa namna moja au nyingine wamepata kuwa au wanayo maslahi ya wazi na ya moja kwa moja katika sekta ya nishati.

Kauli ya hivi karibuni ya mmiliki wa Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd, Mohammed Al Adawi, kukiri kwamba aliwekeza katika sekta ya nishati kwa ushawishi wa Rostam sambamba na ile ya kubainisha kuwa kampuni ya mbunge huyo ilipata kuingia katika zabuni ya kutaka kufanya kazi za ujenzi katika mradi wa kuzalisha umeme wa dharura, ni ushahidi wa wazi wa namna mwanasiasa huyo alivyo na maslahi ya moja kwa moja katika sekta ya nishati.

Kama ilivyo kwa Rostam, taarifa za hivi karibuni, zilizothibitishwa na Mwakyembe mwenyewe
kuwa ni mmoja wa wakurugenzi waanzilishi wa Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd yenye malengo ya kuzalisha umeme wa upepo kutoka mkoani Singida, ni ushahidi kwamba naye anayo maslahi ya moja kwa moja katika sekta ya nishati.

Kuingia kwa Rostam na Mwakyembe katika sekta ya nishati, kwa kiwango kikubwa kunaonyesha namna wabunge, hususan wale wa CCM walivyojizatiti kutumia fursa zao za kisiasa kujinufaisha kiuchumi, nyuma ya kivuli cha uwekezaji
kupitia sheria ya soko huria.

Kama hiyo haitoshi, mzizi wa fitina kuhusu ukweli kwamba Bunge limekuwa likitumiwa kama kiota cha wanasiasa kuvuna mamilioni, zilithibitishwa mkoani Kilimanjaro juzi na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilibrod Slaa ambaye alisema mshahara anaolipwa mbunge kwa mwezi unafikia sh. milioni saba, hiyo ikiwa mbali na posho nyingine.

Dk. Slaa alitaja kiwango hicho cha mshahara wake wakati akihutubia wakazi wa mji mdogo wa Hedaru, wilayani Same katika mfululizo wa mikutano ya Operesheni Sangara inayoendeshwa na CHADEMA.

Wakati Dk. Slaa akibainisha ukweli huo, uchunguzi wa Tanzania Daima Jumatano umebaini pia kuwa wabunge wanaweza kujikusanyia mamilioni ya shilingi kwa kuhudhuria vikao mbalimbali vya kamati za kudumu za Bunge, semina na safari za ndani na nje ya nchi.

“Ndugu zangu, afadhali msijue mshahara anaolipwa Dk. Slaa kama mbunge, mkijua nalipwa shilingi ngapi mnaweza hata kunipiga mawe,” alisema Dk. Slaa wakati akihutubia mkutano huo na kuitikiwa na sauti za wananchi wakimtaka ataje mshahara wake.

“Mnataka kuujua mshahara wangu, ninalipwa sh milioni saba kwa mwezi. Haki iko wapi? Mimi nalipwa milioni saba, na posho yangu kwa siku ni sh 135,000. Haya ni malipo makubwa mno, fedha ninayopata kwa siku inaweza kuzidi hata mshahara wa mwezi mzima wa polisi. Muulizeni yule polisi pale analipwa shilingi ngapi msikie.

“Juzi nimetaja posho za wabunge na kusema zipunguzwe, lakini Spika wa Bunge analalamika eti naingilia haki na madaraka ya Bunge, sasa leo nasema ninalipwa jumla ya shilingi milioni saba kwa mwezi, acha posho za bungeni. Kweli hii ni haki?” alisema Dk. Slaa.

Alisema kuwa akiwa raia huru, ana haki ya kutaja kwa hiari yake kiwango cha mshahara wake, hasa pale anapoona kuwa kulipwa kiwango hicho ni kutowatendea haki mamilioni ya Watanzania maskini wanaolipa kodi zao wakitegemea serikali iwakomboe kutoka kwenye lindi la umaskini.

Dk. Slaa alisema wabunge wengi wa CCM akiwamo Spika wa Bunge, Samuel Sitta, hawawezi kuunga mkono hoja hiyo kwa vile wapo bungeni kwa ajili ya kutafuta maslahi yao binafsi.

“Wafanyakazi wengi na Watanzania wanateseka kwa mishahara midogo na maisha duni, mamilioni haya ya fedha kwenda mifukoni mwa watu ni aibu kwa nchi na CHADEMA tunasema hapana, fedha hizi ziende katika masuala ya kusaidia jamii na kuongeza mishahara ya walimu, polisi, mahakimu na watendaji wengine,” alisema Dk. Slaa huku akishangiliwa na mamia ya wakazi wa Hedaru waliohudhuria mkutano huo.

Alirejea kauli yake ambayo amekwishakaririwa akiitoa mara kadhaa kuwa Spika Sitta, anapaswa kujiuzulu nyadhifa alizonazo katika CCM, ili awe huru kuliongoza Bunge kwa maslahi ya Watanzania badala ya kushinikizwa na maslahi ya chama chake.

Dk. Slaa alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba, kushangazwa na hatua ya Rais Jakaya Kikwete kuendelea kuwateua wabunge wa CCM kuwa wajumbe katika bodi za mashirika ya umma.

Akizungumza wiki iliyopita katika mkutano uliondaliwa na Jukwaa la Wahariri, Prof. Lipumba alisema, hatua hiyo ya Rais Kikwete mbali na kuwahalalishia wabunge ulaji, inazoretesha utendaji wao katika kuyasimamia ipasavyo mashirika hayo ambayo utendaji wake wa kazi unapaswa kusimamiwa na taasisi hiyo muhimu ya dola.

Wakati hali ikiwa hivyo katika mishahara ya wabunge, Tanzania Daima Jumatano limebaini kuwa wabunge wamekuwa wakilipwa mamilioni ya fedha wakati wanapokutana na baadhi ya taasisi za umma ambazo kamati za Bunge zinazisimamia shughuli zake.

Taarifa za hivi karibuni ambazo gazeti hili limezipata zinaonyesha kuwa, Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (Tanesco) lilitumia jumla ya sh milioni 16 kwa ajili ya kulipa posho na usafiri wabunge kutoka majimboni mwao, pamoja na makatibu wawili waliohudhuria kikao cha dharura kilichowakutanisha Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Kamati ya Bunge ya Kamati ya Nishati na Tanesco.

Taarifa kutoka ndani ya ofisi ya Bunge, zinaeleza kuwa licha shirika hilo kuwa na hali mbaya kifedha, lililazimika kuingia gharama hizo baada ya ofisi ya Bunge kuitaka Wizara ya Nishati na Madini kuwagharamia wabunge hao kwa sababu Bunge halikuwa na fedha katika kikao chake cha Desemba mwaka jana.

Katika hali ya kushangaza, habari za wanakamati hao wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kulipwa posho na gharama zao nyingine na Tanesco wakati wakihudhuria kikao hicho zimewafanya wabunge, Katibu wa Bunge na Spika kutofautiana.

Spika Sitta, jana alilithibitishia Tanzania Daima Jumatano kuwa, wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini walilipwa posho na gharama za usafiri kwa sababu Bunge halikuwa na fedha wakati Waziri wa Nishati na Madini, Ngeleja alipotaka kukutana na kamati hiyo ili kupata ushauri.

Lolote linaweza kutokea kutegemea na nani amewaita, kama wameitwa kusaidia jambo ambalo halimo kwenye utaratibu wa Bunge wanalipwa na aliyewaita. Na katika hili ilikuwa hivyo, ninalifahamu vizuri sana, waziri aliomba kukutana na kamati wakati muda wa Bunge ukiwa umepita, Katibu wa Bunge alimuandikia akimueleza kuwa Bunge halina fedha ila kama wizara yake inaweza, basi ilipe posho na gharama za wabunge hao kusafiri hadi Dar ili aweze kukutana
nao.

“Hivyo ndivyo ilivyokuwa, sasa mimi sijui kama ililipa wizara, Tanesco au nani, la msingi hawakulipwa na Bunge, na kama wabunge ambao ni wanakamati wanakanusha hili, ni watu wa ajabu kwa sababu sijui wanaogopa nini kueleza ukweli,” alisema Spika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo (CCM), alipozungumza na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani, alikana kupokea senti tano kutoka Tanesco wakati wakihudhuria kikao hicho na kueleza kuwa, kamati yake iliitwa na Spika na malipo yalifanywa na Bunge.

Hatukumuomba mtu hela, sielewi lolote, sisi tuliitwa na Spika na malipo yetu yalishughulikiwa na Bunge,” alisema Shellukindo na kusisitiza kuwa, kanuni za Bunge zinaeleza wazi kuwa wabunge wanapokuwa katika vikao vilivyo na baraka za Spika, iwe bungeni au nje ya Bunge, posho na gharama zao nyingine zinalipwa na Bunge na si taasisi nyingine yoyote.

Alipoulizwa kuhusu hilo, Waziri wa Nishati na Madini, Ngeleja alieleza kuwa Tanesco ililazimika kulipa gharama hizo kwa wabunge licha ya kikao hicho kufanyika kwa ridhaa ya Spika, baada ya Bunge kueleza kuwa halikuwa na fedha kwa ajili ya kulipa posho na gharama za usafiri kwa wabunge.

Wakati wanasiasa hao wakivutana kuhusu mfumo huo wa ulipaji posho, Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashillilah, alipotafutwa na Tanzania Daima Jumatano
ili kutoa ufafanuzi wa jambo hilo, alieleza kuwa wabunge wote wanapokuwa katika shughuli za Bunge, ikiwamo vikao vya kamati za kudumu za Bunge, posho na gharama
zao nyingine zinalipwa na ofisi ya Bunge, na si vinginevyo.

Alisisitiza kuwa, Tanesco haiwezi kuliwalipa posho wabunge wakiwa katika kikao cha kamati ya kudumu ya bunge na kuongeza kuwa katika utumishi wake ndani ya taasisi hiyo, hajawahi kuona fedha za Tanesco zikitolewa kwa ajili ya kulipa posho wa wabunge.

CHANZO: Tanzania Daima

MHESHIMIWA SPIKA ANASEMA WABUNGE WA KAMATI HUSIKA WALILIPWA NA TANESCO.WAZIRI NGELEJA NAE ANATHIBITISHA HILO.MBUNGE SHULIKINDO ANAKATAA TAARIFA KUWA WALILIPWA JAPO SENTI TANO,NA KATIBU WA BUNGE ANAWEKA BAYANA TARATIBU ZA MALIPO KWA WANAKAMATI ZA BUNGE.
JE NANI MKWELI NA NANI ANAONGOPA?
JE ANAYEONGOPA ANAFANYA HIVYO KWA SABABU GANI?
SHERIA NA TARATIBU ZINASEMAJE KUHUSU KUONGOPA KWA AINA HIYO?
NA ADHABU GANI INATOLEWA KWA KOSA LA AINA HIYO?

24 Mar 2009


NAKUOMBA SOMA HABARI MBILI ZIFUATAZO KISHA TUJADILI DHANA YA KULAZIMISHA UWAJIBIKAJI.KWA KIFUPI,KATIKA HABARI YA KWANZA,PAMOJA NA MAMBO MENGINE,DR SLAA ANAONYESHA KUWA CHADEMA INA USHAHIDI WA KUTOSHA KUIHUSISHA CCM NA WIZI WA EPA.KATIKA HABARI YA PILI,MWANASHERIA TINDU LISSU ANAMTAKA MKUU WA MKOA WA SINGIDA,MHESHIMIWA KONE,AOMBE RADHI HADHARANI KUTOKANA NA MADAI KUWA ALIWATUKANA HADHARANI BAADHI YA WANANCHI ANAOWAONGOZA.MJADALA UTAKAOFUATA BAADA YA HABARI HIZO UNAANGALIA MANTIKI YA DR SLAA NA CHADEMA KUENDELEA KUTUELEZA KWAMBA WANA USHAHIDI WA KUTOSHA UNAOIHUSISHA CCM NA UFISADI WA EPA,LAKINI KIONGOZI HUYO NA CHAMA CHAKE WAMEKUWA KANA KWAMBA WANATINGISHA KIBERITI VILE...KWA MAANA KWAMBA KAMA USHAHIDI UPO,KWANINI WASIFUNGUE KESI MAHAKAMANI KWA NIABA YA WANANCHI BADALA YA KUENDELEA KUDAI USHAHIDI TUNAO,USHAHIDI UPO...IRONICALLY,TINDU LISSU,MWANASHERIA ANAYEWATETEA BAADHI YA WAKAZI WA SINGIDA DHIDI YA MH. KONE,SIO TU NI MWANASHERIA WA CHADEMA BALI PIA NI MIONGONI MWA VIONGOZI WAANDAMIZI WA CHAMA HICHO.

ANYWAY,HEBU SOMA KWANZA HABARI HUSIKA

Chama tawala chaambiwa kuacha kutisha wananchi kuhusu ufisadi

Na Mussa Juma, Same.

KATIBU mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amemtaka katibu mwenezi wa CCM, John Chiligati, kuacha vitisho dhidi ya upinzani, akisema kuwa wataendelea kufichua ufisadi uliotanda kwenye chama hicho tawala.

Chiligati alivionya vyama vya upinzani kuwa visitumie ufisadi kama ngazi ya kujipatia umaarufu, huku akionya kuwa kuendelea kuishutumu CCM kunaweza kuhatarisha amani kwa sababu kama watu milioni nne watachukia (akimaanisha wana-CCM), hakutakuwa na amani.

Lakini Dk Slaa, mmoja wa wabunge ambao wamesimama imara katika kufichua na kupiga vita ufisadi, alisema hakuna ubishi kuwa CCM imeingia madarakani kwa kuchotewa fedha kutoka Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) na kama kinapinga, basi kiende mahakamani. Kauli hiyo ilitolewa jana na Dk Slaa wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika kata ya Hedaru na Makayanya wilayani Same na baadaye kukutana na waandishi wa habari.

Dk Slaa alisema Chadema ina ushahidi wa maandishi jinsi CCM ilivyokuwa inachotewa fedha za EPA kupitia kampuni ya Kagoda, hivyo kama inaona inapakwa matope, inaweza kwenda mahakamani kulalamika na sio kutoa vitisho kupitia vyombo vya habari.

“Tunamshangaa sana Chiligati na tunamuomba aache vitisho. Tunao ushahidi hadi muhtasari wa kikao kilichoongozwa na rais mstaafu kikielezea jinsi walivyokuwa wanajichotea fedha za EPA na pia ujumbe mfupi kutoka kwa katibu mkuu wa CCM kwenda Benki Kuu kuomba fedha hizo. Sasa wanaposema hawahusiki na EPA tunawashangaa,” alisema Dk Slaa.

CHANZO: Mwananchi
HABARI YA PILI :


RC atakiwa kuwaomba radhi wananchi

na Deogratius Temba

MKUU wa Mkoa wa Singida, Vincent Parseko Kone, ametakiwa kuitisha mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kisasida, Wilaya ya Singida na kuomba radhi kwa wanachi na mwenyekiti wa kijiji hicho, kwa kuwatukana hadharani na kuwalipa fidia ya sh milioni moja.

Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Mwenyekiti wa kijiji hicho, Ramadhani Mwankumbi, kutoa taarifa kuwa anakusudia kumfikisha mkuu huyo wa mkoa mahakamani kutokana na kumtukana hadharani wakati akiwa katika mkutano wa hadhara kijijini hapo.

Kwa mujibu wa barua aliyoandikiwa jana, Mkuu wa mkoa huyo, kutoka kwa Kampuni ya uwakili ya M/S TUNDU A.M. LISSU Advocates, yenye kumbukumbu namba TAML/SDG/RSM/KSSD/09/01, na kusaniwa na wakili wa kujitegemea Tindu Lissu, ilieleza Februari 24, mwaka huu, mkuu huyo wa mkoa alienda katika kijiji hicho na kutumia cheo chake kwa lengo alilodai kuwa ni kukagua mradi wa kilimo cha umwagiliaji. Badala ya kutembelea mradi huo, kama alivyodai, aliomba kumwona Mwenyekiti wa Kijiji Mwankumbi, na kuanza kumfokea mbele ya wanakijiji wenzake, viongozi wa mkoa na wananchi wengine wengi kwa madai kuwa ameshirikiana na mtu mwingine aitwaye, Josephat Isango, kumchafulia jina lake.

“Mteja wetu alipoomba nafasi ya kujieleza juu ya tuhuma ulizokuwa unamrushia ulikataa na badala yake ulianza kumtukana matusi mazito, baada ya kumtukana ukaondoka na kurudi Singida,” ilieleza sehemu ya barua hiyo. Pia barua hiyo ilieleza kisheria maneno hayo, ambayo yalitolewa na mkuu huyo wa mkoa ni kosa na ni kashfa dhidi ya mteja wao, na yamemdhalilisha, kumnyanyasa, kumvunjia heshima aliyokuwa nayo mbele ya wanakijiji waliomchagua na kumpa dhamana.

“Maagizo kutoka kwa mteja wetu ni kukutaka wewe Parseko Kone, utembelee tena Kijiji cha Kisasida na kuitisha mkutano wa hadhara wa wanakijiji wote na uwaombe radhi hadharani kwa maneno ambayo sisi tutakuelekeza.

“Aidha, tunakuagiza ufanye ziara ya mkutano huo wa kuomba radhi ndani ya siku 14, kutokea leo (jana), pia mteja wetu anadai umlipe sh milioni moja kama gharama za ufuatiliaji kwetu,” ilieleza barua hiyo.

Lissu, alidai kuwa mkuu huyo wa mkoa, endapo atashindwa kufanya hivyo, au kupuuza kutekeleza matakwa yao watamfungulia kesi ya madai katika mahakama watakayoichagua wao. Aliongeza pia kama Kone atashindwa kutekeleza madai yao, hawatasita kumdai fidia zaidi ya fedha na nafuu nyinginezo za kisheria dhidi yao.

Mwishoni mwa wiki iliyopita Kone alizungumza na Tanzania Daima, alikanusha tuhuma hizo zinazomkabili na kudai kuwa alikwenda katika kijiji hicho kukagua mradi wa umwagiliaji na hakumtukana kiongozi yeyote.


MLOLONGO WA KULALAMIKA,KUTOA VITISHO AU HATA KULIA HAUWEZI KUKOMESHA UFISADI AU KUWAKUMBUSHA WAJIBU BAADHI YA VIONGOZI WANAOJIONA MIUNGU WATU.DR SLAA NA CHADEMA WAMEKUWA WAKITUAMINISHA KWAMBA CCM INAHUSIKA MOJA KWA MOJA KATIKA KUFANIKISHA UJAMBAZI WA EPA.JAPO NAFAHAMU KUWA HUKUMU YA UMMA INA MADHARA ZAIDI YA HUKUMU YA MAHAKAMA ZA KISHERIA,SOTE TUNAJUA NAMNA HUKUMU YA UMMA INAVYOWEZA KUPINDISHWA NA ZAWADI ZA KHANGA,FLANI,KILO YA SUKARI,NK KAMA VIVUTIO WAKATI WA UCHAGUZI.

NGOJA NIFAFANUE KAMA HUJANIELEWA VIZURI.YAYUMKINIKA KUAMINI KUWA CHADEMA INAPOITUHUMU CCM KWENYE MIKUTANO YA HADHARA KWAMBA CHAMA HICHO TAWALA KINA MAHUSIANO NA UFISADI/MAFISADI INATARAJIWA KUWA WANANCHI WATATOA HUKUMU DHIDI YA CCM (HUKUMU YA UMMA) WAKATI WA UCHAGUZI.HILO LINAWEZEKANA KATIKA MFUMO HURU WA DEMOKRASIA,NA MIFANO HAI NI NAMNA HUKUMU YA UMMA ILIVYOFANYA KAZI KATIKA CHAGUZI HUKO HISPANIA MWAKA 2004 NA MAREKANI MWAKA JANA.KATIKA CHAGUZI ZINAZOFANYIKA KATIKA MAZINGIRA YA DEMOKRASIA HURU,HASIRA ZA WAPIGA KURA (AU KURIDHISHWA KWAO) NI MIONGONI MWA MAMBO MUHIMU KATIKA KU-DETERMINE MATOKEO YA UCHAUZI HUSIKA.

SASA SOTE TUNAJUA MAZINGIRA YA CHAGUZI NYINGI ZA "DUNIA YA TATU".KANUNI ISIYO RASMI KUHUSU CHAGUZI ZETU INADAI KWAMBA CHAMA TAWALA HAKIWEZI KUSHINDWA UCHAGUZI.KIKISHINDWA BASI AIDHA KILIZEMBEA KUTUMIA MBINU ZAKE ZA AWALI ZA KUBAKI MADARAKANI AU KILIPIGIWA KURA ZA CHUKI NA WAFUASI WAKE AU KULITOKEA MPASUKO NDANI YA CHAMA TAWALA AMBAO ULIZAA MAKUNDI MAWILI YENYE TAKRIBAN NGUVU SAWA,KILA MOJA LIKIFAHAMU MBINU SAFI NA CHFU ZA KUSHINDA CHAGUZI,NK.WAPO WANAOAMINI KUWA HATA KANU YA MOI HAKIKUSHINDWA UCHAGUZI WA 2002 KWA VILE WAPIGA KURA WALIKUWA WAMEICHOKA (WHICH WAS TRUE i.e. kweli walikuwa wameichoka) BALI NI UTEUZI MBOVU WA MGOMBEA UHURU KENYATA.

VINGI VYA VYAMA TAWALA KATIKA NCHI ZA TATU HUSHIKILIA DOLA KWA MAANA HALISI YA KUSHIKILIA,YAANI WANAITUMIA IPASAVYO KUHAKIKISHA UTAWALA UNAENDELEA MILELE.HAKUNA DHAMBI KWA CHAMA KUWA MADARAKANI MUDA MREFU AS LONG AS KINAWAHUDUMIA WANANCHI IPASAVYO.KWA BAHATI MBAYA,U-KING'ANG'ANIZI WA BAADHI YA VYAMA TAWALA KATIKA NCHI ZA DUNIA YA TATU HAUTOKANI NA MAPENZI YAO KWA NCHI AU WANANCHI BALI HOFU YA KUADHIBIWA KWA MADHAMBI YALIYOWAFANYWA WAKATI VYAMA HIVYO VIKIWA MADARAKANI.KADRI MADHAMBI YANAVYOZIDI KUONGEZEKA NDIVYO KADRI VYAMA HIVYO VINAVYOZIDIWA NA HOFU YA NINI KITATOKEA PINDI VIKITOLEWA MADARAKANI,NA MATOKEO YAKE NI KUTUMIA KILA NJIA KUHAKIKISHA VINATAWALA MILELE.NA KWA VINASHIKILIA DOLA,HILO LINAKUWA SIO JAMBO GUMU.

KWAHIYO,KAMA DR SLAA,CHADEMA NA WENGINEO WANADHANI KELELE KUWA CCM INAHUSIKA KATIKA WIZI WA EPA ZITAFANIKISHA KUPATIKANA KWA HUKUMU YA UMMA KATIKA UCHAGUZI WA 2010 AU BAADAYE,THEY REALLY NEED TO THINK AGAIN.KUFANYA HIVYO NI SAWA NA KUTARAJI KUWA HUYO RC ANAYETUHUMIWA KUWATUKANA WANANCHI ANGEAMUA YEYE MWENYEWE KWA HIARI YAKE KUOMBA RADHI BADALA YA KULAZIMISHWA KUFANYA HIVYO (KAMA ANAVYOTAKIWA NA WAKILI LISSU).NAMNA PEKEE YA CHADEMA,ET AL WANAWEZA KUFANIKIWA KATIKA TUHUMA ZAO DHIDI YA CCM NI KWENDA MAHAKAMANI WAKIWA NA USHAHIDI WANAODAI KUWA NAO.

KUITAKA CCM IENDE MAHAKAMANI (INAPOTUHUMIWA KUWA NA UHUSIANO NA MAFISADI) NI SAWA NA KUMTAKA MTU UNAYEMTUHUMU KUTEMBEA NA MKEO/MUMEO (KUTEGEMEA JINSI YAKO MSOMAJI) AENDE POLISI/MAHAKAMANI.....KWA KIFUPI,ATAENDELEA KUKUIBIA NA HATOTIA MGUU POLISI/MAHAKAMANI.COMMON SENSE INATUELEZA KUWA MWENYE TUHUMA NDIO ANAYEPASWA KUWA NA UHARAKA WA KUZIDHIBITISHA AU KUWA NA DHAMIRA YA KUZITOKOMEZA KABISA.MTUHUMIWA ANAWEZA KUWA NA UHARAKA HUO IWAPO ANAONA ZINAMCHAFULIA JINA.LAKINI WHAT IF TUHUMA DHIDI YA MTUHUMIWA NI ZA KWELI?BADO TUTATEGEMEA MTUHUMIWA AJIEPELEKE KWENYE HUKUMU YAKE?

NAHISI CHADEMA WANACHELEA KWENDA MAHAKAMANI SIO KWA VILE WANAHOFIA KUTOPATA HAKI BALI WANAZITUMIA TUHUMA HIZO KUWA MTAJI WA KISIASA.NA-HYPOTHESIZE KUWA CHAMA HICHO KITAZITUMIA TUHUMA HIZO KWENYE KAMPENI ZAKE ZA UCHAGUZI MKUU WA 2010 KIKIAMINI KUWA ZITAKISAIDIA KUPATA USHINDI KWA HUKUMU YA UMMA DHIDI YA CCM.JAPO LOLOTE LINAWEZEKANA KATIKA SIASA,NA MBINU HIYO YA CHADEMA INAWEZA KUFANIKIWA,WAZOEFU WA SIASA WANAWEZA KUAFIKIANA NAMI KWENYE HYPOTHESIS YANGU YA PILI KUWA MKAKATI HUO HAUTOFANIKIWA.KINACHONIPELEKA KUAMINI HIVYO NI UZOEFU KUHUSU NAMNA CCM INAVYOELEWA UDHAIFU WA MPIGA KURA WA KITANZANIA,FAIDA ZA KILOJISTIKI ZINAZOELEMEA UPANDE WA CHAMA TAWALA,MILKI NA SAPOTI YA DOLA BILA KUSAHAU "MBINU CHAFU."

UCHAGUZI MKUU WA 2010 UNAWEZA KABISA KUPITA NA CCM KUIBUKA KIDEDEA HUKU CHADEMA IKIWA "IMEDODEWA" NA USHAHIDI WAKE DHIDI YA CCM.HILO SIO BAO LA KISIGINO BALI NI MITHILI YA KIBAKA KUKUPORA KISHA ANAKUPIGIA KELELE KUWA WEWE NDIO MWIZI....(AND WE ALL VERY WELL KNOW MOB JUSTICE HUKO NYUMBANI ZILIVYO...WATU WAKISKIA UKELELE WA MWIZI,MWIZI HAWAULIZI ILIKUWAJE.NI KIPIGO TU....PASIPO KUJUA KUWA WANAYEMPIGA NDIO ALOPORWA NA KIBAKA).

BONYEZA HAPA kusoma kimbwanga hiki.

23 Mar 2009


KADA maarufu wa Chama cha Mapinduzi, Nape Nnauye, amesema malumbano yanayoendelea sasa nchini ni ishara kwamba mafisadi wamejipanga kuifanya nchi isitawalike.

Nape alitoa kauli hiyo jana alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu hali ya kisiasa nchini, hususani malumbano yanayoendelea sasa kati ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.

Bila kutaja majina ya watu, Nape alisema chimbuko la malumbano hayo aliyoyaita ya kipuuzi ni kashfa nzima ya kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, iliyosababisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na aliyekuwa Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha, kujiuzulu.

Huku akiwa makini kuchangua maneno ya kuzungumza, Nape alisema malumbano hayo yanaonyesha kuna baadhi ya watu hawakuridhika na taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Mwakyembe, hivyo kuna ulazima wa hoja hiyo kurudishwa tena bungeni ili kukata mzizi wa fitna.

“Kuna kila dalili kuwa mafisadi wamejipanga kuhakikisha nchi haitawaliki, ndiyo maana mijadala isiyo na kichwa wala miguu inaibuka kila kukicha hata kwa mambo ambayo yamekwishaamuliwa na chombo kikubwa kama Bunge,” alisema.

Katika kuthibitisha kauli yake, Nape alisema ana taarifa za siri kuwa kuna baadhi ya mafisadi wamekuwa wakifanya mikutano ya faragha ambapo pamoja na mambo mengine, wamepanga kuhakikisha nchi haitawaliki kwa kuibua hoja na mijadala kupitia baadhi ya vyombo vyao vya habari.

“Tunakoenda ni kubaya, ila naamini serikali iko imara na CCM kama chama tawala, tutaomba tulizungumze kwenye vikao vyetu kwa nia njema ya kuliokoa taifa linalovurugwa na watu wachache wenye fedha,” alisema Nape.

Nape alisema ili kuhakikisha Tanzania haiyumbishwi, aliwataka wananchi kupuuzia mjadala wa sasa kwa madai kuwa hauna tija na una lengo la kuhatarisha amani na utulivu uliopo nchini.

Kuhusu mjadala wa ununuzi wa mitambo ya kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans iliyorithi kutoka Kampuni ya Richmond, kada huyo wa CCM alisema anashangazwa na uamuzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kuomba kibali cha Bunge au kamati zake.

“Kwani TANESCO wanapoenda kununua transfoma na vifaa vingine, wanaomba kibali cha Bunge? Kama si hivyo, kwa nini wanataka kuhalalisha ununuzi wa mitambo ya Dowans kupitia kamati za Bunge? Hata hivyo, Bunge lilishatoa msimamo wake juu ya hilo, kama kuna mtu hakuridhika, alirudishe bungeni na si kuwagawa Watanzania kwa mijadala isiyoisha na vitisho,” alisema Nape.

Mwanasiasa huyo machachari aliwataka mafisadi kutambua kuwa hata wakiibua mijadala ya kuwagawa Watanzania kama ilivyo sasa, hakutabadili ukweli kwamba Richmond na hata mrithi wake Dowans, ndio waliolifikisha taifa hapa lilipo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Maswa, John Shibuda, alisema malumbano yanayoendelea sasa kati ya Dk. Mwakyembe na Rostam kumetokana na upepo wa kisiasa ambao wakati mwingine huleta tija katika kukuza demokrasia.

Hata hivyo, Shibuda ambaye hupenda kuzungumza kwa mafumbo, alisema mjadala huo umejikita kwenye hila na visa vya kufunika mema na mazuri ya mtu.

“Mimi naona hayo ni mapepo ya kisiasa na mtenguko wa fikra ambao umeleta mng’atuko dhidi ya dhulma, lakini ni mjadala wa heri kwa maana kuwa unawafanya watu kutoa manung’uniko yao, bila hivyo hali ingekuwa mbaya siku moja, kwa hiyo naona mjadala uendelee,” alisema Shibuda.

Mbunge wa zamani wa Morogoro Vijijini, Semindu Pawa (CCM), aliiambia Tanzania Daima jana kuwa, mjadala huo sasa umechacha na kuwataka waandishi wa habari kuachana nao.

“Mimi sitaki kusema nani yuko sahihi, lakini nasema mjadala huo umechacha, umepitwa na wakati, wanahabari mkiacha tu, hautausikia tena, lakini naweza kusema wanahabari ndio mnaoukuza, waacheni,” alisema Semindu Pawa.

Mwishoni mwa wiki, Dk. Mwakyembe alijibu tuhuma zinazomhusisha na kumiliki kampuni binafsi ya kuzalisha umeme kuwa ni kazi mahususi inayofanywa na majeruhi wa vita ya ufisadi, ambao waliumizwa na matokeo ya kazi ya Kamati Teule ya Bunge ya kuchunguza mkataba wa Kampuni ya Richmond, ambayo yeye alikuwa mwenyekiti wake.


Hatua ya Mwakyembe kujibu tuhuma hizo, ilikuja baada ya magazeti mawili ya kila siku, (si Tanzania Daima) kuchapisha habari zinazomhusisha yeye na umiliki wa hisa 1,000,000 zenye thamani ya jumla ya sh bilioni 1.5 katika Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd.

Mbali ya habari hizo kuandikwa katika magazeti hayo mawili; moja la binafsi na jingine la serikali, nyaraka kadhaa zinazomhusisha Mwakyembe na kampuni hiyo, zimesambazwa katika mtandao wa intaneti.

Taarifa hizo pia zinamtaja Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya TANESCO, kuwa miongoni mwa wanahisa wa kampuni hiyo binafsi ambayo wakati fulani Mwakyembe alipata kuwa mtendaji mkuu wake.

Taarifa hizo zinajaribu kujenga hoja zinazojaribu kumuondolea Mwakyembe uhalali wa kuendelea kudai kupambana na ufisadi ndani na nje ya Bunge ilhali yeye mwenyewe akionekana kuwa na ukwasi mkubwa unaotiliwa shaka.

Pia zinaonyesha kuwa, Mwakyembe licha ya kuwa na hisa nyingi katika kampuni hiyo, ameisaidia katika mambo mbalimbali ambayo hata hivyo hayakufafanuliwa, wakati akiwa katika wadhifa wa mtendaji mkuu.

Kwa mujibu wa uchunguzi wetu, lengo kuu la kusambaza nyaraka hizo ni kujaribu kumnyoshea kidole Mwakyembe na kujaribu kumuondolea uhalali wa kuendelea kupigania sekta ya nishati ilhali yeye mwenyewe akijua kuwa na maslahi.

Mwakyembe ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alisema kuwa katika Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd, hakuwezi kukamsababishia akaingia katika mgogoro wowote wa kimaslahi kutokana na ukweli kwamba, kampuni hiyo iliyosajiliwa kwa Wakala wa Usajili wa Makampuni (BRELA), bado ipo katika hatua ya awali ya mradi ambao bado haujaanza kuzalisha.

Alipotakiwa kueleza ni kwa nini wakati alipoteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyoichunguza Richmond kuanzia Oktoba mwaka juzi na kuwasilisha ripoti yake mwaka jana, hakueleza lolote kuhusu kuwa na kampuni ya kuzalisha umeme, Mwakyembe alisema asingeweza kufanya hivyo wakati mkakati wao wa kikampuni ukiwa katika hatua ya mradi tu.

‘‘Kwa mujibu wa sheria ya makampuni, majina yanakuwapo mpaka hapo kampuni itakapoanza ‘ku-take off’ (kuanza kazi). Sikuweza kuitaja kuwa ni sehemu ya makampuni yangu, kwa kuwa bado ilikuwa katika hatua ya mradi,” alisema Mwakyembe.

Mwanasiasa huyo alikwenda mbele zaidi na kuwaeleza wanahabari hao ambao miongoni mwao walionekana dhahiri kukabiliana naye kwa njia ya malumbano kuwa, hata wakati akiandikisha mali anazomiliki chini ya sheria ya viongozi kutangaza mali wanazomiliki, hakuitaja kampuni hiyo ya Power Pool kwa sababu hizo hizo za kutoanza kwake kazi.

Akifafanua tuhuma hizo dhidi yake, alimgeukia mbunge mwenzake wa CCM, Rostam Aziz na kumtuhumu kuwa nyuma ya habari zote mbaya zinazoandikwa dhidi yake.

Huku akilitaja jina la Rostam mara kadhaa, Mwakyembe alisema ni jambo ambalo haliingii akilini kwa mtu ambaye amechafuka kuamua kutumia maji taka kujisafisha.


WALA TUSINGEFIKA HAPA TULIPO IWAPO SHERIA INGEFUATA MKONDO WAKE.VINARA WALIOTUINGIZA MKENGE KWENYE UTAPELI WA RICHMOND HAWAJACHUKULIWA HATUA BAADA YA KUJIUZULU,NA SASA WAMEPATA JEURI YA KUTAKA KUTULIZA MARA YA PILI KWA KUTUUZIA MITAMBO MITUMBA ILEILE ILE YA RICHMOND a.k.a DOWANS.HUU MTINDO WA KULINDANA UTALIPELEKA TAIFA MAHALA PABAYA.

HOWEVER,LET IT BE KNOW TO MAFISADI AND THOSE WHO SHIELD THEM THAT IF THEY TURN OUR BELOVED COUNTRY INTO ANOTHER MADAGASCAR THEY TOO WOULDNT BE SAFE!

22 Mar 2009


Tanzania has condemned the forced resignation of Madagascar President Marc Ravalomanana and said it does not recognise the regime of his successor, Andry Rajoelina...MORE

SOURCE: Guardian


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.