15 May 2011


Wakati wenzetu mnasherehekea timu "zenu" kama Manchester United kuchukua ubingwa,akina sie bado tupo na Simba na Yanga zetu licha ya ubabaishaji wao wa hali ya juu.Kanuni nyepesi ya kumudu kuzipenda klabu hizi kongwe za Tanzania ni kuweka hisia mbele ya busara/akili (putting emotions in front of common sense).

Kwa bahati ya mtende,wana Msimbazi tumepata fursa ambayo laiti tukiitumia vema basi tutapiga hatua kubwa ya kushiriki Ligi ya Mabingwa.Kwa sasa sitaki hata kufikiria itakuwaje kwenye Ligi hiyo,iwapo tutafanikiwa,maana timu zilizopo huko ni hatari.Anyway,kwa muda huu ngoja tushangilie habari hizi njema (hata kama ni ushindi wa mezani)

Simba yawang’oa Mazembe Afrika
• Sasa kuwavaa Wamorocco jijini Khartoum

na Mwandishi wetu, CAIRO, Misri


WEKUNDU wa Msimbazi, Simba ya jijini Dar es Salaam, imeshinda rufaa yake iliyokata dhidi ya mabingwa mara mbili mfululizo wa Ligi ya Mabingwa Afrika 2009 na 2010, TP Mazembe ya DR Congo.

Sasa TP Mazembe imeondoshwa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa kwa kosa la kumchezesha mchezaji batili.

Huo ni uamuzi wa Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Soka (CAF), baada ya kupitia rufaa iliyokuwa imewasilishwa na Simba, kupinga TP Mazembe kumchezesha Janvier Besala Bokungu.

Bokungu (22), beki aliyezaliwa Kinshasa, akiwa mchezaji wa TP Mazembe mwaka 2007, alihamia Esperance ya Tunisia kabla ya kurejea mwaka huu.

Kwa mujibu wa CAF, Kamati ya Mashindano iliamua kushughulikia suala la nyota huyo baada ya Simba kuwasilisha pingamizi kwamba amechezeshwa isivyo halali.

Kamati hiyo imebaini kuwa kwa TP Mazembe kumchezesha Bokungu, ilifanya kosa kwa mujibu wa kifungu namba VIII kinachohusiana na ulaghai. Aidha, kifungu kingine kilichoipa Simba ushindi ni ibara ya 24 na 26 inayohusu uhalali wa mchezaji na ibara ya 29 ya kanuni za michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kwamba TP Mazembe ilimchezesha Bokungu ambaye bado ni nyota wa Esperance, kwani mkataba wake na wakali hao wa Tunisia, utafikia ukomo Juni mwaka huu, ingawa TP Mazembe wanasisitiza ni mchezaji wao halali.

“Janvier alifuata taratibu zote kuvunja mkataba wake na si Esperance wala Mazembe yenye tatizo na mchezaji huyu, kwa sababu amejiunga nasi kwa maridhiano,” alisema Meneja Mkuu wa Mazembe, Frederic Kitengie.

Simba chini ya Mwenyekiti wake Ismail Aden Rage, ilimkatia rufaa Bokungu, licha ya kung’olewa katika raundi ya kwanza ya michuano hiyo kwa jumla ya mabao 6-3.

Katika mechi ya kwanza ambayo ilichezwa mjini Lubumbashi, Simba ilifungwa mabao 2-1 kabla ya kupigwa 4-1 kwenye marudiano Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Kutokana na maamuzi hayo, sasa Simba itakipiga na mabingwa wa Morocco, Wydad Casablanca jijini Khartoum, Sudan, ambako itapigwa mechi moja tu ili kumpata atakayeingia katika kapu la timu nane bora, ambazo zitacheza ligi ndogo.

Tayari zilizotinga nane bora ni Ahly ya Misri, Raja Casablanca ya Morocco, Enyimba ya Nigeria, Esperance ya Tunisia, MC Alger ya Algeria, Al Hilal ya Sudan na Coton Sport ya Cameroon.

Wakati Simba wakifurahia kushinda rufaa, wakali hao wa Morocco, nao wanafurahia kurejea kwenye michuano hiyo kwani tayari walishang’olewa na TP Mazembe kwa jumla ya mabao 2-1.

Wakati hali ikiwa hivyo, leo Wekundu wa Msimbazi Simba, wanatarajiwa kufanya mkutano mkuu wa mwaka kwenye bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam, ikiwa ni mwaka mmoja tangu uongozi wa Mwenyekiti Ismail Aden Rage kuingia madarakani.

Kwa mujibu wa Rage, mkutano huo utakuwa na ajenda za mawasilisho ya mapato na matumizi ya fedha za mwaka, sambamba na kuwasilishwa kwa bajeti ya mwaka ya Kamati ya Utendaji na mengineyo.

Alisema ni mara ya kwanza Simba kuwasilisha taarifa za mahesabu ya mwaka mapema, jambo ambalo walijiandaa kabla ya uchaguzi mkuu, ikiwa ni mojawapo ya mapendekezo yaliyomo ndani ya katiba.

Uongozi wa Rage uliingia madarakani Mei 9 mwaka jana, baada ya uongozi wa mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Hassan Dalali, kumaliza miaka mitatu ya uongozi wake.

CHANZO: Tanzania Daima

14 May 2011


Victoria Climbié (RIGHT) and her killer aunt Marie Therese Kouao

Hundreds of children being accused of witchcraft 'as belief in demonic possession spreads across the UK'
By Rob Cooper

Last updated at 12:36 PM on 14th May 2011

Hundreds of witchcraft abuse cases are going unreported across the country each year, it has been revealed.

Officials believe child protection officers are only tipped off in the most extreme cases when a child's life has been put in danger.

Just 38 cases have been reported in the last five years - and it is feared that they represent just the tip of the iceberg.Hundreds of children may be left to starve, beaten and having chili rubbed into their eyes.

Youngsters born with physical and mental difficulties are most at risk from abuse.Relatives often believe that the children are 'possessed' and the torture is carried out as a form of exorcism.

Extreme evangelical Christian churches - most prevalent in the Democratic Republic of Congo - have grown significantly in recent years and their influence is thought to have spread to groups in the UK.

A decade ago the death of Victoria Climbie suffered appalling injuries at the hands of her aunt and boyfriend who believed she was possessed by the devil, sparking huge public anger.
Victoria

The eight-year-old had 128 injuries on her body in a case described by a pathologist as one of the worst ever child abuse cases.

She tied up, hit with bike chains and attacked with lighted cigarettes.

As officials try to combat the extreme beliefs, social services have been issued with a new set of guidelines to help them deal with youngsters from religious and ethnic minority backgrounds who could suffer abuse, The Times revealed.

The Metropolitan Police are working on their scheme to deal with religious-based child abuse to place extra emphasis on dealing with tackling witchcraft and abuse.

Witchcraft is most often found in the Democratic Republic of Congo and surrounding countries.

Romain Matondo, who works at the safeguarding children programme at the Congolese Family Centre, north London, said often it is not biological parents who are the abusers.

He told The Times: 'At first maybe it is swearing and shouting at the child, what we would call emotional abuse.

'But if there is church involvement, it sometimes means it doesn't stop there, but becomes physical and very violent as the church tries to get rid of the evil spirit.'

He added that children can be slapped, starved or beaten with spoons all to get the spirit out.

A report yesterday revealed that it is the poorest children that are most at risk of beind told they are 'possessed' because relatives are more likely to be influenced by faith leaders.

SOURCE: The Daily Mail

13 May 2011


Napenda kuwafahamisha badiliko la anwani ya blogu
Blog title: SAUTI YA MNYONGE:

Asante
Malkiory William Matiya,
B.Ed.(Hons) (UDSM); M.Sc, P/Health (UTA, Finland)
Mobile: +358404623776



11 May 2011




Africa here we come! Birmingham set to tour Tanzania ahead of new season

By Sportsmail Reporter

Last updated at 11:11 AM on 11th May 2011

Birmingham are planning a pre-season trip to Tanzania in July.

The details have not yet been finalised but first-team coach Andy Watson and chief medical officer Ian McGuinness have travelled to Africa to inspect facilities

Birmingham are expected to undertake a four-day trip, with Tanzanian top-flight sides Simba or Yanga, or possibly both, providing the opposition at the National Stadium in Dar-es-Salaam.

Watson told the club's website: 'The people of Tanzania that we have met have been very hospitable and kind, and from what we've seen of the country so far it looks an amazing place.
'We have been made aware of just how much the Tanzanian people love their football - especially the Barclays Premier League - and when everything is fully in place we look forward to coming back in July and playing.'

SOURCE: The Daily Mail

Mwangalie huyo kijana (well,may be mzee.You can't tell the difference,can you?) wa kwanza kulia.Sidhani kama anayoongea Nape yanamwingia akilini.Na wa tatu kutoka kulia,mwanamama aliyeshika tama,ni kama aliamrishwa kuhudhuria mkutano huo.Sio kashfa au dharau,lakini ni wazi kuwa sura za wahudhuriaji zinatia huzuni.Zimejaa mawazo,hazionyeshi matumaini....yet wamehudhuria.Ukiwaangalia akinamama hao hapo chini,japo kuna kijitabasabu cha kujipa matumaini,lakini hizo flana za njano na khanga zimeficha mengi...ngozi zao zinaonyesha waziwazi namna maisha yao ya kila siku yalivyo magumu katika harakati za kupeleka mkono kinywani.


Lakini bado wanahudhuria mikutano ya porojo.Wanajua wanadanganywa,kwani huhitaji kwenda shule kujua una njaa ilhali anayepiga porojo ameshiba.Mng'aro tu wa ngozi ya Nape as opposed to msinyao wa ngozi za wasikilizaji wake unaelezea mengi.Wanaambiwa kuwa CCM imejivua magamba,sasa itaendeshwa kisayansi,sijui imekuwa mpya...lakini hawaambiwi ni kwa namna gani ugumu wa maisha ya walalahoi hao utapungua...ni lini nao watapata fursa ya kunawiri kama akina Nape....

Lakini bado wanahudhuria mikutano hii ya porojo.Ndio maana katika kichwa cha habari nimehoji: WAMEROGWA?

Picha kwa hisani ya Jamii Forums

10 May 2011



Kwa walioamini usanii wa CCM kuwa imeamua kujivua magamba wahesabu wameliwa.Sio tu ukweli kwamba joka linalojivua magamba linakuwa hatari zaidi bali pia ufahamu wetu wengi kuwa joka likijivua magamba haligeuki kuwa mjusi.Na kama baadhi ya wanasiasa wa upinzani walivyoelezea suala hilo la magamba,tatizo la CCM ni mithili ya kansa ya damu.Dawa yake pekee ni kifo,and sure will CCM die,sio kwa vile kimezeeka vibaya bali kwa sababu ni mkusanyiko wa walafi,waroho,majambazi,matapeli na mabazazi wa kisiasa.Putting it bluntly,ushirika wa wachawi kamwe hauwezi kudumu.Let's wait and see!

VIONGOZI wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameshindwa kuwaondoa katika chama hicho wale wanaowaita watuhumiwa wakuu wa ufisadi nchini, imefahamika.

Viongozi ambao waliotajwa kuwa wanatakiwa kujiondoa kwenye uongozi au chama ndani ya siku 90 kwa kuwa ni “mafisadi wanaochafua sura ya chama mbele ya jamii,” ni Edward Lowassa, Rostam Aziz na Andrew Chenge.

Kinyume na majigambo ya viongozi wa juu wa chama hicho, kuwa sharti watuhumiwa hao waondolewe kwenye vikao vya maamuzi, hadi sasa chama kimeshindwa kuwapa barua za kuwajulisha juu ya suala hilo.

Katibu Mkuu Wilson Mukama, katibu wa itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara, John Chiligati wamekuwa wakishindilia kuwa “mafisadi lazima waondoke.”

Hata hivyo, Mukama aliwaambia waandishi wa habari juzi Jumatatu, jijini Dar es Salaam, “…hakuna mahali popote katika maazimio ya NEC panapotaja siku 90.”

Alisema, “Kama ni muda basi ni pale mwenyekiti wetu aliposema NEC ijayo. NEC hukutana kila baada ya miezi minne na kwa hiyo kama ni siku, basi ni 120 na siyo 90,” alieleza Mukama akijibu swali la mmoja wa waandishi waliotaka kufahamu ni lini chama hicho kitaandika barua na kukabidhi watuhumiwa.

Kauli ya Mukama kwamba hakuna mahali ambapo NEC imeagiza Lowassa, Rostam na Chenge waondoke ndani ya chama katika muda wa siku 90 zijazo, imekuja wiki moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kukutana kwa faragha na Lowassa.

Taarifa za ndani ya chama na kutoka baadhi ya viongozi wa CCM, zinasema mazungumzo ya viongozi hao wawili yalijikita katika kile kilichoitwa “kujivua gamba” na kwamba Lowassa anamtuhumu Nape kusambaratisha chama chao kwa kuendeleza tuhuma katika mikutano ya hadhara.

Lowassa na Kikwete walikutana ikulu jijini Dar es Salaam, 25 Aprili 2011 baada ya kushindwa kukutana mjini Dodoma, 3 Aprili 2011 kama ambavyo Kikwete alikuwa ameahidi.

Katika mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari, Mukama alisema, “NEC ilitoka na maazimio 26. Azimio mojawapo linasema chama kiendelee na mapambano yake dhidi ya ufisadi na kwamba watuhumiwa wakitafakari, wajipime na kuchukua hatua.”

Alisema, “Sehemu ya hotuba ya mwenyekiti wakati akifunga mkutano ilisema tunatambua athari ya kukosekana maadili katika chama na tuendelee kupambana; na katika hili hakuna ajizi. Viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajitafakari, wajipime na wachukue hatua,” alisema Mukama akinukuu kauli ya mweneykiti wa CCM, Rais Kikwete.

Alipoulizwa ni watuhumiwa gani wa ufisadi kwa kuwa chama hicho hakijawahi kuwa na orodha yake, badala yake orodha inayofahamika kwa wengi ni ile iliyotolewa na kiongozi mkuu wa upinzani nchini, Dk. Willibrod Slaa, Mukama alisema, “…CCM ni taasisi kubwa yenye mfumo wake na miongozo yake; hivyo haitegemei orodha ya CHADEMA.”

Mukama alikuwa akijibu swali la Manyerere Jackton wa New Habari House. Alitaka kufahamu vigezo vinavyotumika kutambua mafisadi; na iwapo wataweza kumwondoa Kikwete ndani ya chama hicho kwa vile naye ametajwa katika orodha ya Dk. Slaa ya tarehe 15 Septemba 2007.

Hata hivyo Mukama aliendelea kushikilia kuwa chama chake hakiwezi kufuata orodha za vyama vingine, hasa CHADEMA.

Kwa upande mwingine Lowassa amenukuliwa akimtaka Kikwete kumdhibiti Nape kwa kuwa “anakivuruga chama” kwa hatua yake ya kusisitiza kuwa NEC ilipitisha maamuzi ya kuwataka wajiuzulu, wakati akijua fika kwamba hilo si kweli.

“Mkutano kati ya Lowassa na rais ulikuwa mfupi sana. Lowassa alimueleza Bwana Mkubwa (rais Kikwete), jinsi asivyofurahishwa na mwenendo wa Nape hasa jinsi anavyowatuhumu ufisadi. Alimsihi Rais Kikwete kumweleza hilo katibu wake mwenezi, Nape…,” ameeleza mtoa taarifa.

Kikwete, taarifa zinasema, alimhakikishia Lowassa kuwa “…hakuna lolote litakalotokea,” kauli ambayo imethibitishwa na Mukama katika mazungumzo yake na wahariri.

“Yule bwana (Lowassa) alimuuliza Kikwete, mnataka kunipa barua kwa kosa lipi? Nimefanya nini? Nini ambacho wewe hukifahamu,” anasema mtoa taarifa wa MwanaHALISI.

Gazeti hili limejulishwa na vyanzo vyake vya ndani ya serikali kuwa uamuzi wowote utakaochukuliwa na Lowassa, unaweza kuzidisha mgawanyiko ndani ya CCM.

Mara baada ya Lowassa kukutana na Kikwete, taarifa zinasema mbunge huyo wa Monduli alikutana na kufanya mazungumzo marefu na Peter Kisumo, mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya chama hicho.

Katika mazungumzo yao, Lowassa alionya kuwa CCM kiko hatarini kupasuka kutokana na kauli za Nape na mwenzake John Chiligati juu ya ufisadi na watuhumiwa wake.

“Huyu bwana anaua chama. Nakuhakikishia mzee Kisumo, hawa watu wakiendelea kunishutumu bila sababu, nitatoka hadharani na kujibu mapigo,” anaeleza mtoa taarifa akimnukuu Lowassa katika mazungumzo yake na Kisumo.

Naye Kisumo anaripotiwa kumhoji Lowassa, “Mbona ninyi marafiki wawili mnataka kusambaratisha chama?” Naye Lowassa alijibu, “Kheri iwe hivyo…”

Mwandishi wa gazeti hili alimtafuta Lowassa ili kuthibitisha walichojadili na Kikwete, lakini simu yake iliita bila kupokelewa.





Leo ni tarehe 10/05/2011,na deadline aliyotoa Ridhiwani Kikwete,mtoto wa Rais Jakaya Kikwete,kwa Katibu Mkuu wa Chadema,Dkt Willibroad Slaa,na Mwenyekiti wa DP,Mchungaji Christopher Mtikila,imemalizika jana.Ridhiwani alitoa dealine ya siku saba kuwataka Dkt Slaa na Mtikila wamwombe radhi kufuatia tuhuma zao dhidi yake kuwa amekuwa bilionea kwa njia za kutilia shaka.

Ni mapema mno kubashiri chochote lakini habari ifuatayo inaweza kutoa mwangaza kuhusu uwezekano wa Ridhiwani kwenda mahakamani kama livyotishia au kutokwenda (which would imply tuhuma hizo dhidi yake ni za kweli).Soma kwanza habari yenyewe


Mtoto wa Rais Kikwete ang’aka

na Janet Josiah

MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, amesema hataki kufuatiliwa maisha yake na wanasiasa hasa wanaomtuhumu kuwa ni bilionea huku akisisitiza kuwashughulikia waolimchafua.

Ridhiwani, alisema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima akitakiwa kueleza hatua atakazochukua baada ya muda wa siku saba aliowapa Mwenyekiti wa Demokratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willbrod Slaa kupita.

Awali, mtoto huyo wa Rais aliwataka wanasiasa hao wamwombe radhi katika kipindi cha siku saba vinginevyo angewapeleka mahakamani kwa kuwa wamemchafua pamoja na familia yake.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwa njia ya simu, ili kujua lini angekwenda mahakamani kuwafungulia mashtaka viongozi hao, alijibu kwa jazba kwamba jambo hilo linahusu maisha yake hivyo haoni sababu ya kufuatiliwa na vyombo vya habari.

“Jambo la kuwafikisha wanasiasa hao mahakamani si jambo lenu, hilo ni jambo linalonihusu mimi na maisha yangu hivyo nitachokifanya nakijua mwenyewe,” alisema Ridhiwani huku akisisitiza kwamba hata alipozungumza na waandishi wa habari juma lililopita alisema lengo lake ni kuueleza umma na sio kufuatiliwa maisha yake.

Kwa nyakati tofauti Mchungaji Mtikila na Dk. Slaa, walimtuhumu Ridhiwani kwa ukwasi huku wakiitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kumchunguza.



Pasipo nia ya kufanya hitimisho lolote,nashindwa kumwelewa Ridhiwani anaposema "jambo la kuwafikisha mahakamani wanasiasa hao si jambo lenu..."Hivi sio Ridhiwani huyuhuyu aliyeitisha mkutano na waandishi wa habari,ambapo pamoja na mambo mengine alikanusha tuhuma zilizotolewa na wanasiasa hao,na akawataka wamwombe rahdi vinginevyom angewafikisha mahakamani?Sasa kama jambo la kuwafikisha mahakamani wanasiasa hao si jambo lao (wanahabari) kwanini basi aliitisha mkutano nao na kuwaelezea same thing anachodai hakiwahusu?

Waandishi wa habari wana kila sababu ya kumhoji kama atawafikisha Slaa na Mtikila mahakamani au la.Kwanini?Kwa sababu,kwanza,alitamka hayo mbele ya waandishi hao hao wa habari,na pili,yeye ni mtoto wa Rais na ametuhumiwa kuwa bilonea kwa mgongo wa baba yake.Sasa hakuna Mtanzania asiyependa kujua kama madai ya wanasiasa hao ni zushi mtupu au yana ukweli ndani yake.

Wito wangu kwa Ridhiwani ni huu:TIMIZA AHADI YAKO YA KWENDA MAHAKAMANI.Tuhuma za wanasiasa hao dhidi yako si ndogo,kwani licha ya kukugusa wewe binafsi zinamgusa pia baba yako ambaye ni Rais wetu (na ambaye siku za karibuni ametangaza kuwa anadhamiri kuukalia kooni ufisadi).Usipokwenda mahakamani itaonyesha kuwa tuhuma hizo zina ukweli.

And to make matter even worse,Dkt Slaa na Mtikila wanaweza kukufungulia kesi ya kuwakashifu,kwani ulidai ni wazushi tu.Sasa kama sio wazushi then go to the court as you promised,bearing in mind kwamba wewe ni mwanasheria.

Enewei,tunasikiliza WHAT'S NEXT!

Ngoma inogire!



Ama kweli chozi limepata mliaji.Kila mara tunasikia Rais wetu kalia na watendaji hawa,au kasikithswa na watendaji wale.Kichekesho ni kwamba watendaji hao hawakujiteua wenyewe kuwa madarakani bali waliteuliwa na huyhuyo anayelalama.

Binafsi,nadhani tatizo sio watendaji dhaifu wanaopelekea Rais "kulia" nao kila mara bali tatizo la msingi ni Rais mwenyewe.Kiongozi dhaifu haishiwi visingizio.Kiongozi dhaifu haishiwi lawama.Na kiongozi dhaifu hakawii kudai hili limeshindikana kwa vile yule hakufuata maagizo.Kwanini asiwatimue?

Hizi semina elekezi ni mzigo mwingine kwa Watanzania,ambao hawastahili kubebeshwa gharama za posho za waheshimiwa hao kwa ajili ya semina kama hizo ilhali aliyawateua ana kila sababu ya kuwatimua,lakini hana nia wala uwezo (wa kibinadamu,sio uwezo anaopewa na Katiba).

Yaani hadi tutapofika hapo 2015 sijui hali itakuwaje.Lakini moja ambalo tuna uhakika wa kulikumbuka kuhusu Kikwete ni hivi "vilio" vyake dhidi ya watendaji aliowateua yeye mwenyewe.

Enewei,soma habari husika hapo chini:

Kikwete alia na mawaziri mizigo 
Monday, 09 May 2011 21:54


Habel Chidawali, Dodoma
RAIS Jakaya Kikwete amewataka mawaziri na makatibu wakuu kujiamini katika utendaji wao wa kazi badala ya kutegemea maelekezo ya mamlaka zilizo juu yao.Alisema hayo jana alipokuwa akifungua semina elekezi kwa viongozi na watendaji wakuu wa Serikali iliyofanyika katika Ukumbi wa St Gasper nje kidogo ya Manispaa ya Dodoma.“Hadi leo sijui kwa nini hasa watu (mawaziri) wanashindwa kuzungumza mambo yaliyofanywa na Serikali na kuwapa uwanja mpana wenzetu wa upande wa pili (wapinzani) ambao wanajua kweli kuvitumia vyombo vya habari. Sisi tunaendelea kulalamika kila siku kwamba hatuandikwi, nani atakuandika wakati hutoi taarifa,” alisema Kikwete.

Kuna wakati waziri mmoja aliwahi kunipigia simu na kusema 'Mheshimiwa Rais habari hii tuikanushe?' Nilichokifanya nilimwambia pima wewe baada ya hapo nikakata simu,” alisema

Rais Kikwete alisema kitendo cha mawaziri kukataa kutoa habari na kuwafanya maofisa habari wa wizara kuwa kama waandishi wa habari ni hatari kwa serikali.

Katika hotuba yake, Rais Kikwete aliwataka watendaji hao kufanya kazi kwa kufuata misingi ya Katiba, sheria, kanuni na taratibu ili kukwepa hasara inayoweza kutokana na uamuzi usiofuata kanuni na kuiaibisha Serikali.
"Ni muhimu kwenu kama viongozi mkajielimisha juu ya Katiba, sheria, kanuni na taratibu mbalimbali zinazoongoza utendaji kazi katika sehemu zenu za kazi. Uhalali wa maamuzi mtakaoyafanya hupimwa na sheria," alisema Kikwete na kuongeza:
"Ukifanya uamuzi unaokinzana na sheria utahojiwa wewe binafsi lakini pia utaibebesha Serikali mzigo wa hasara na fedheha itakayotokana na uamuzi huo. Uamuzi usiofuata sheria unaweza kuwa na madhara kwa wananchi.

"Heshimuni Katiba na fuateni sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika utekelezaji wa majukumu yenu. Katika semina hii masuala hayo yatafafanuliwa na kuzungumzwa. Kadhalika, uhusiano wa Serikali na mihimili mingine ya dola yaani, Bunge na Mahakama utafafanuliwa."

Rais Kikwete pia aliwataka watendaji hao kuepuka kauli na vitendo vinavyoweza kuwafarakanisha na kuleta mgawanyiko katika Serikali ili kulinda dhana ya uwajibikaji wa pamoja.

"Viongozi na watendaji wakuu wa wizara hamna budi kujenga uhusiano mzuri na uwajibikaji wa pamoja. Haifurahishi kuona waziri na katibu mkuu au waziri na naibu waziri; naibu waziri na katibu mkuu au katibu mkuu na naibu katibu mkuu hawaelewani."

"Wanasemana na hata wanapingana hadharani, yaani mbele ya wafanyakazi. Baya zaidi ni pale wanapopingana katika vyombo vya habari kuhusu uamuzi au utendaji wa wizara au serikali kwa jumla. Hayo si maadili mema katika taasisi yoyote.

"Kama unaona vigumu kuuafiki ni bora kutoka. Hairuhusiwi kupinga taasisi ambayo wewe umo ndani kama mmoja wa viongozi wake. Ni vyema hili likaeleweka. Msitupe tabu ya kuulizana maswali na kuwasemea."
Rais Kikwete pia aliwataka watendaji hao kuwa mstari wa mbele kuzungumzia mafanikio ya Serikali ili kuziba midomo ya wapinzani wanaopita kila kona nchini na kuwaeleza wananchi kuwa haijafanya chochote.

"Sijui kwa nini hatuwi wepesi kuyasemea mafanikio mengi tuliyoyapata tukaacha wasiotutakia heri wanaosema hatukufanya kitu wasikike mpaka waonekane wanasema kweli," alisema.

Alisema hajui na hana majibu mazuri ya kwa nini Serikali imekuwa ikishindwa kuzungumza mambo mazuri yaliyofanywa katika kipindi cha miaka mitano na hata wakati mwingine kushindwa kuzungumza jambo hadi wampigie simu, kitu ambacho ni aibu.

Alisema kuna udhaifu katika kujipanga kwa wasemaji kutokana na kuchelewa kutoa taarifa au kukanusha habari ambazo zimekuwa zikitolewa na upinzani, jambo linalowafanya wananchi waamini kuwa ni kweli, kwani uongo ukizungumzwa mara nyingi hugeuka na kuwa ukweli.

“Unajua mimi sijui hadi leo ni kwa nini hasa watu wanashindwa kuzungumza mambo yaliyofanywa na serikali na kuwapa uwanja mpana wenzetu wa upande wa pili ambao wanajua kweli kuvitumia vyombo vya habari huku sisi tunaendelea kulalamika kila siku kwamba hatuandikwi, nani atakuandika wakati hutoi taarifa,” aliuliza Kikwete.

Alikanusha madai kuwa baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika habari za upinzani na kuacha habari nzuri za serikali na badala yake akasema woga na urasimu uliowajaa wasemaji katika serikali, ndilo tatizo hasa kwa kuwa hawajui kuwa vyombo vya habari vinatafuta habari na kama wao hawatoi habari ni lazima waandike zile zinazotolewa na upande wa pili.

Katika hatua nyingine, Kikwete alisema kuwa anategemea kuona Serikali yake ikifanya kazi kwa umoja na ushirikiano mkubwa katika kipindi hiki cha miaka mitano na kwamba kushirikishana na kupeana habari iwe ndiyo dira ya maendeleo yao.

Sikuteua mawaziri wa kusoma mafaili ofisini
Aliwataka viongozi hao kuacha umangimeza, badala yake watoke ofisini kujionea matatizo ya wananchi.
"Mawaziri na makatibu wakuu lazima mtoke. Hiyo ndiyo njia bora zaidi ya kujua mambo yahusuyo wizara zenu na ndiyo njia bora ya kuongoza: kuona wenyewe na kutenda," alisema Rais Kikwete na kuongeza: "Hii itawafanya mjiamini kuelekeza na pia mnaposimama mbele za watu na kusema. Msiwe mamangimeza. Tokeni, tembeeni kuona shughuli zenu. Tembeleeni wananchi muwafahamu, wawafahamu, mjue shida zao muwatatulie."

Alikemea tabia ya viongozi hao kushinda kwenye mitandao kila siku na kusoma ujumbe badala ya kwenda kuwatumikia wananchi vijijini.Alisema tabia hiyo haipaswi kuvumiliwa hata kidogo na akaonya viongozi wa namna hiyo wataishia kuwa wababaishaji na hatakwenda nao katika kipindi chake cha uongozi.

Mimi sikuteua mawaziri wa kusoma mafaili ofisini, bali niliteua watu wanaoweza kukimbizana kwa kasi zaidi, ari zaidi pamoja na nguvu zaidi, kwani nataka kuwasikia mkichakarika huko kwenye miradi mlikopeleka fedha, siyo kupokea taarifa ofisini bila ya kujua fedha za walipa kodi zinatumikaje huko.”

Dawa ya mawaziri hawa ipo jikoni
Rais Kikwete pia aliwatahadharisha mawaziri ambao wamekuwa wakipinga kauli na miswada ya mawaziri wenzao, huku wengine wakiwa wanatoa siri za Serikali.Alisema kuwa watu wa namna hiyo dawa yao iko jikoni kwa kuwa kitendo wanachokifanya si kizuri ndani ya Serikali.

Alisema anayo mamlaka ya kuchagua na ya kumwondoa waziri wakati wowote akiamua, hasa kama haoni umuhimu wa kuendelea na mtu wa aina hiyo.

“Katika hili nawaambia mapema kabisa kuwa waziri anayeishi kwa kupinga miswaada ya Serikali ajue kuwa anaipinga Serikali na hivyo sitakuwa tayari kufanya kazi na mtu wa aina hiyo. Sehemu kubwa ya kazi zenu mawaziri nataka ziwe za Serikali na zile za jimbo mtajua namna mtakavyojipanga bila ya kuharibu kazi za Serikali,” alisema.

Pato la Mtanzania litakua miaka mitatu ijayo
Rais Kikwete alisema kasi ya kukua kwa pato la Mtanzania ni ndogo na kwamba kunahitajika juhudi za makusudi katika kuongeza pato hilo. Hata hivyo, alitamba kuwa pato la Mtanzania litaongezeka katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia sasa kutokana na baadhi ya nchi wahisani kuahidi kuongeza misaada kwa Tanzania.

Alisema katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake, umaskini umepungua kwa asilimia mbili tu hivyo, akaahidi kuwa katika kipindi cha miaka mitano ya awamu ya pili ya uongozi wake, umaskini utapungua kwa kiasi kikubwa.

Alisema mkakati uliopo hivi sasa serikalini ni kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2025, Tanzania inakuwa nchi yenye uchumi wa kati pato la Mtanzania wa kawaida likitarajiwa kufikia Dola za Marekani 2,500 hadi 3,000. Sasa ni Dola 600. Kuhusu kipindi cha miaka mitatu, alisema kuwa, ipo mipango mizuri kutoka kwa wahisani, ikiwamo Benki ya Dunia ambayo imekubali kuisaidia Tanzania kiasi cha Dola 2.8 milioni ambazo zinaweza kusaidia katika kutengeneza ajira na kupambana na umaskini.

Semina hiyo ilihudhuriwa na watendaji wote wa Serikali wakiwamo Waziri Mkuu, Jaji Mkuu, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, mawaziri na manaibu waziri, makatibu na naibu makatibu wakuu, Mwanasheria Mkuu na naibu wake, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na viongozi wastaafu, akiwamo Spika wa zamani na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya

CHANZO: Mwananchi

9 May 2011


Baada ya Rais Jakaya Kikwete kuonekana kituko kwa kupokea hundi yenye tarakimu zinazokinzana na thamani ya hundi hiyo kwa maandishi,na yeye kuonekana akitoa tabasamu la nguvu (trademark yake),sasa imekuwa zamu ya mkewe.

Ukiangalia hundi anayokabidhiwa Mama Salma Kikwete (pichani juu) utabaini kuwa thamani ya hundi kwa maandishi ni shilingi milioni tatu na laki nane,ambayo kwa tarakimu inapasa kuwa 3,800,000.Sasa sijui ni umaimuna au uzembe tu,tarakimu za hundi hiyo zimeandikwa kichakachuaji- TZS 3,800,00.Unaweza kudhani ni shilingi elfu tatu mia nane (3,800.00) lakini maelezo ya hundi yatakusuta kwani yametamka bayana kuwa ni SHILINGI MILIONI TATU NA LAKI NANE.

Na hapa chini tunamwona mtu tuliyemkabidhi dhamana ya kutuongoza Watanzania takriban milioni 50 akikenua meno kwa furaha huku hundi imeandikwa TWO HUNDRED THOUSAND lakini tarakimu ni 300,000



Hivi kabla ya hafla hizi, hao jamaa wa  PSU  hawakagui vitu anavyokabidhiwa Rais au mkewe?Au nao hadithi ni hiyohiyo?

Na haya ni madudu nadra tunayobahatika kuyaona hadharani.Je yanayofanyika kwa kwa faragha ua sirini inakuwaje?Npatwa na wasiwasi kuwa hadi Kikwete anaondoka madarakani hapo 2015 (kama hatoombwa na mafisadi kugombea tena ili aendelee kuwalinda) tunaweza kushtukia Tanzania ishauzwa zamani hizo.Unashangaa nchi inawezaje kuuzwa?Waulize "Zaire" (DRC Kinshasa)!!!!

Chanzo: Nimkutana na habari hii kwa ndugu yangu MPAYUKAJI MSEMAOVYO

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.