29 Jul 2009

(Picha kwa hisani ya MJENGWA)

Wenzetu wa huku Magharibi wanasifika kwa kuwajali watoto. Licha ya serikali zao kutunga sheria zenye kulenga kuzuia na kukomesha uonevu, unyanyasaji, ukatili na unyama mwingine dhidi ya watoto, kuna mlolongo wa taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali zinazojihusisha na suala hilo. Hiyo sio kusema watoto wote wako salama.Ni vigumu katika ubinadamu wetu kufanya kitu kiwe absolutely perfect.

Pamoja na sifa hiyo ni shutuma kwamba upendeleo huo wa hali ya juu kwa watoto unachangia “kuwaharibu” watoto hao. Yayumkinika kusema kwamba miongoni mwa time bombs katika jamii za Magharibi ni watoto wanaodekezwa kupita kiasi. Kama ilivyo kwenye nyanja nyingine, uhuru usipokuwa na mipaka unaweza kupelekea matokeo yasiyopendeza.Hatahivyo, katika hili, uzuri (kuwajali watoto) unazidi ubaya (kuwadekeza).

Ni katika minajili hiyo kunajitokeza hofu kwa baadhi ya watu kutoa misaada kwa watoto kwa kuhofia misaada hiyo inaweza kutafsiriwa tofauti. Hivi karibuni niliona kwenye runinga mtunzi mmoja wa vitabu akilalamikia utaratibu wa kufanyiwa background checks (uchunguzi wa kiusalama,kwa tafsiri isiyo rasmi) kila anapokwenda kwenye shule za watoto kuwasomea vitabu anavyotunga.Mtunzi huyo analalamika kwamba kitendo hicho kinamfanya ajisikie kama mhalifu licha ya ukweli amekuwa akijihusisha na usomaji vitabu kwa watoto kwa miaka kadhaa sasa. Mamlaka husika zinajitetea kwamba utaratibu huo unalenga kuwalinda watoto.

Zamani kidogo niliwahi kukutana na simulizi moja kwamba jamaa flani (mwanaume) alimwona mtoto wa kike anakaribia kuzama kwenye bwawa la kuogelea.Kwa huruma, akajitosa majini kumwokoa mtoto huyo ambaye kwa bahati mbaya chupi yake ilimvuka katika hekaheka hiyo ya kukaribia kuzama.Alipomwokoa na kumpeleka mtoto huyo kwa mama yake akapigwa swali la kutatanisha: “Chupi ya mtoto iko wapi?”Kabla hajatafakari jibu akatandikwa kigongo kingine, “Hivi lini mibaba kama wewe mtaacha kunyemelea watoto wetu kwenye sehemu za kuogelea huku mkisubiri wakumbwe na matatizo kisha muwatomasetomase kwa kisingizio cha kuwaokoa? Hebu nipe chupi ya mwanangu kabla sijakuripoti kwa polisi”.Sijui ungekuwa wewe ungefanyaje!

Tafiti zisizo rasmi zinadokeza kwamba wanaume wengi wamekuwa waoga kusaidia watoto, hususan wa kike, kwa kuhofia kwamba ukarimu na msaada wao usije kuwaingiza matatizoni kwa tuhuma za child molestation.

Nadhani kufikia hapa unajiuliza naelekea wapi! Well, nataka kuzungumzia namna mamlaka zetu zinavyowadekeza mafisadi, lakini nataka kwanza nikupe mifano ya kuiweka akili yako vema kabla hatujaivaa hoja ya ufisadi.Twende kwenye mfano mwingine. Katika miaka ya hivi karibuni baadhi ya watu wanaoporwa na vibaka wameishia kupata vipigo kutoka kwa raia baada ya washirika wa kibaka aliyepora kupiga ukelele wa “mwiz,mwizi...” dhidi ya aliyeporwa.Na kama kanuni za mob justice zilivyozoeleka,hakuna muda wa kuhakiki iwapo aliyepigiwa ukelele ni kibaka halisi au victim.

Back to hoja kuhusu mafisadi. Inaelekea mamlaka husika huko nyumbani zimeamua kuwalinda mafisadi mithili jamii za Magharibi zinavyowalinda watoto dhidi ya suspected/potential/career child molesters.Na anayediriki kupiga kelele dhidi ya mafisadi anakumbana na yaleyale ya anayeporwa na kibaka na kisha kupigiwa ukelele wa “mwizi,mwizi...” na washirika wa kibaka mhusika, na kuishia kupewa kipigo cha haja katika mtindo wa mob justice.

Wachunga kondoo wa Bwana walipobaini kwamba kondoo wao wanakamuliwa hadi damu baada ya maziwa kumalizika miilini mwao wakaamua kuja na kinachoitwa roughly muongozo wa kanisa kuhusu elimu ya uraia hususan uchaguzi wa viongozi. Tuliyekuwa tukimwamini kuwa swahiba wa karibu wa Baba wa Taifa, Kingunge Ngombale Mwiru,akatuthibitishia his true colours kwa kuwakemea wachunga kondoo wa Bwana.Hata kama Kingunge aliasi Nyumba ya Bwana (tukiaminishwa kuwa ni matokeo ya kuamini Ujamaa kupitiliza hadi kuufanya kuwa dini yake) tunapaswa kumshangaa babu huyu ambaye hivi karibuni ameibuka kuwa mtetezi mahiri wa mafisadi. Gazeti la Taifa Letu limemnukuu mtumishi mmoja wa Mungu akim-describe Kingunge kama BABA WA TAIFA WA MAFISADI.

Walioliibia taifa kwa kununua mgodi wa Kiwira kwa bei ya kutupa kana kwamba wanachonunua ni kifusi wameishia sio tu kusafishwa bali kufidiwa kwa wizi wao. This is more than crazy! Yaani tunawafidia majambazi!?Tunalipeleka wapi taifa letu? Wakati hatujui hizo milioni kadhaa walizotumia kununulia mgodi huo walizitoa wapi (lakini kwa vile hawakuwa wafanyabiashara basi yayumkinika kuhisi ni fedha za kifisadi),tuna uhakika wa asilimia zaidi ya 1000 kwamba hayo mabilioni watakayolipwa kama “fidia za kutufisadi” ni fedha zangu, zako na zetu walalahoi,walalawima,walala kichwa-chini miguu-juu, na wanyonge wengineo.

Kinachosikitisha ni kwamba kuna waungwana wanalipwa mishahara minono kuzuia upuuzi wa namna hii lakini badala ya kutumia nguvu za kikatiba walizonazo kustopisha ujambazi wa aina hii, wanakuwa bize zaidi na wale wanaowasaidia (waungwana hao) kupiga kelele dhidi ya ufisadi na mafisadi. Kama hufahamu basi naomba nikujulishe kwamba shughuli ya hatari kabisa kwa Mtanzania ni kudiriki kukemea ufisadi.Utaandamwa,utatishwa,utafanywa ujione mhaini,na kufanyiwa kila anachopaswa kufanyiwa Osama bin Laden pindi akikamatwa!Na shughuli yenye uhakika wa kipato, heshima na ulinzi kuliko zote ni ufisadi. Correct me if I’m wrong!

Siku zote nimekuwa nafahamu kwamba kimbelembele changu (according to how those in the know describe it) dhidi ya mafisadi ni kujiingiza kwenye kundi la dead men walking. I know, you’re thinking I’m scared of my own shadow. Kwa vile hapa si mahala mwafaka kutoa ushuhuda wangu, then ni bora tuliache hilo kwa sasa. Hata hivyo, naamini kwa nguvu zote kwamba ukimya sio suluhisho la matatizo yetu. Silence is not an option at all.

Kinachonisikitisha zaidi ni namna baadhi ya wenzetu wenye nguvu, uwezo na sababu wanapokosa nia au ujasiri wa kuendeleza kelele hizi. Inasikitisha zaidi unapoona wasomi wenye uwezo mkubwa wa uchambuzi wanageuka vibaraka wa kusifia pasipo kugeuza upande wa pili wa shilingi kukemea mwenendo tete wa taifa letu.Hate me or love me, ninachofanya ni kinachopaswa kufanywa na kila Mtanzania mwenye uchungu wa dhati wa taifa letu, na anayefahamu kwamba it’s no use crying over spilled milk. Imani kwamba “hata tukipiga kelele hatuwezi kubadili kitu” ni hatari sana kwa vile japo Ukimwi umekuwepo kwa miongo kadhaa sasa bado jamii inaendelea kuhamasisha vita dhidi ya gonjwa hilo hatari.

Kinachopaswa kuwaamsha wanaochelewa kujiunga kwenye mapambano dhidi ya ufisadi ni ukweli ufuatao.Katika utafiti wangu wa kitaaluma unaoelekea ukiongoni,kuna ushahidi wa kutosha unaoonyesha kwamba vurugu za kidini (utafiti wangu unahusu dini) na nyinginezo katika jamii zinachangiwa sana na jamii kukatishwa tamaa na mwenendo wa watawala kushughulikia matatizo yanayozikabili jamii hizo.Na kwa vile watawala wa aina hiyo hufanya kila wawezalo kuzuia “sauti zisizopendeza masikioni mwao”,kimbilio pekee hubaki kwa nyumba za ibada na dini kwa ujumla.

Tatizo ni kwamba masuala ya dini yanaelemea zaidi kwenye hisia kuliko reasoning. Sote tunafahamu, kwa mfano, kuwa piga ua huwezi ku-reason na Mkatoliki kuhusu ishu “ngumu kuelezeka” kama Utatu Mtakatifu, namna Bikira Maria alivyomzaa Yesu pasipo “kukutana” na Josefu, na maswali mengine kama hayo.Na katika masuala ya dini, ambapo mara nyingi emotions tend to come in front of common sense, hakuna taratibu kama za jeshini kwamba amri ya jenerali lazima iheshimiwe na brigedia, au ya kanali iheshimiwe na meja, au ya kapteni kwa lance corporal. Kwenye dini, kauli ya askofu au shehe haina nguvu sana katika kutuliza hamasa za waumini pindi wanapoamua kupambana na mamlaka za kidunia kwa jina la Mungu.

Kinachoniogopesha zaidi ni vuguvugu linaloendelea huko nyumbani ambapo ishu kama ahadi hewa za CCM kuanzisha mahakama ya kadhi,mwongozo wa Kanisa kuhusu uchuguzi wa viongozi waadilifu,mwendelezo wa madai kuwa Wakristo wanapendelewa na Waislam wanaonewa,nk zimetawala anga za habari. Kibaya zaidi, hayo yanatokea katika kipindi ambacho mafisadi wako tayari kufanya lolote alimradi wafanikiwe kuendelea kutufisadi. Yayumkinika kuamini kwamba hawawezi kusita kutumia fursa hii ya “kuwachanganya Watanzania” kwa misingi ya dini na hivyo ku-deflect attention yao (Watanzania) kuhusu ufisadi na mafisadi kwa vile watakuwa bize zaidi kunyoosheana vidole kwa misingi ya udini.

Tukiunyamazia ufisadi, utatumaliza!

It can be done if you play your part.

It’s now or never!

28 Jul 2009

Picha kwa Hisani ya MJENGWA.Uchambuzi zaidi kesho,panapo majaliwa.

23 Jul 2009







Hiyo sio sanamu,bali "msanii" mmoja ambaye kila wikiendi anavizia mtaa ulio bize na "kuganda kama sanamu" kisha kutoa vijishara vya kuvunja mbavu.Hulazimishwi kutoa asante bali "mchango wako utathaminiwa".Ni mchanganyiko wa ubunifu na "usanii" (i.e. ujanja-ujanja wa kuishi mjini)

Huyu nae ni mtaalam wa cover versions,or sort of off.Ukiskia muziki wake pasipo kumtia machoni unaweza kudhani The Killers,Coldplay,au rockers flani wanafanya concert mtaani minus makelele ya kawaida ya rock stars.Kipaji?Usanii? Well,katika zama hizi za recession,credit crunch na vitu kama hivyo,si serikali na taasisi za fedha pekee zinazohitaji kuwa na mikakati ya kujinusuru.Nahisi "wasanii" hawa wanatumia vipaji-au ujanja ujanja-kukabiliana na hali hiyo.At the end of the day,kinacho-matter ni kono kwenda kinywani.

22 Jul 2009



Riot police have broken up a tense standoff between black and white protesters in a town in Texas.


The conflict began with a march by 100 mostly African-American activists, who were unhappy at the state̢۪s handling of the case of 24-year-old Brandon McClelland who was run over and killed by a vehicle.

Speaking to US television network ABC, Brandon's mother Jacquiline said: "The reason for today's rally is to let everybody know how the justice system around here is really doing things."
When the protesters reached the town square, the crowd of black demonstrators ballooned to around 200 people on one side of the street.

Approximately a dozen white supremacists, including four skinheads carrying Nazi swastika flags, gathered on the other side.

A skinhead and another white man were arrested on suspicion of disorderly conduct, before the protesters separated peacefully.

No blows were exchanged.


SOURCE: Yahoo! News

15 Jul 2009


na Charles Mullinda

IMEBAINIKA kuwa, Ofisi ya Bunge imetumia vibaya mamilioni ya shilingi yaliyotolewa na serikali kwa ajili ya uendeshaji wa ofisi hiyo katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2007/2008.

Hayo yamebainishwa na baadhi ya wabunge wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) katika mahojiano yao na Tanzania Daima Jumatano yaliyofanyika wiki iliyopita mjini Dodoma kwa wakati tofauti.

Wakizungumza kwa sharti la majina yao kutoandikwa gazetini, kwa kile walichoeleza kuwa ni kuogopa kuandamwa na baadhi ya wabunge wenzao, walisema ushahidi wa maelezo yao umo katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CGA) ya mwaka wa fedha wa 2007/2008.

Mmoja wa wabunge hao alieleza kuwa licha ya ripoti ya CGA kubainisha matumizi mabaya ya mamilioni ya fedha katika Ofisi ya Bunge, Mwenyekiti wa PAC, John Cheyo, alizuia kujadiliwa kwa ripoti hiyo baada ya kushauriana na baadhi ya vigogo wa Ofisi ya Bunge, jambo ambalo linazuia kuchukuliwa hatua zozote za kisheria au kurekebisha hali hiyo hadi sasa.

Alisema Ofisi ya Bunge imekuwa ikifanya jitihada za makusudi kuhakikisha ripoti hiyo haijadiliwi na PAC, kwa hofu kwamba inaweza kusababisha baadhi ya watendaji kuwajibishwa na baadhi ya wanasiasa kuchafuka majina yao.

Cheyo, Mwenyekiti wa PAC na Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP), alipoulizwa na gazeti hili kuhusu madai hayo, alisema ni kweli ripoti ya CAG kuhusu matumizi ya fedha za serikali katika Ofisi ya Bunge si nzuri, kwa sababu inaonyesha upungufu mkubwa wa urejeshaji masufuru pamoja na matumuzi mengine mabaya ya fedha za ofisi hiyo.

Hata hivyo, alikana kuikalia ripoti hiyo kwa namna yoyote na kueleza kuwa, aliamua kuiweka pembeni baada ya kushauriana na kukubaliana na wajumbe wote wa kamati hiyo kuwa hawawezi kuijadili, kwa sababu walishindwa kumhoji Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah, ambaye wakati kamati hiyo akikutana kujadili ripoti mbalimbali za CGA kuhusu hesabu za taasisi za serikali, alikuwa hajaapishwa na rais kushika wadhifa huo.

“Ni kweli ripoti ya CAG kuhusu matumuzi ya fedha katika Ofisi ya Bunge si nzuri, inaonyesha upungufu mkubwa katika urejeshaji wa masurufu, na ripoti zote ambazo zinaonyesha hivyo kihasibu huwa ni mbaya. Sasa kwa Spika hii si nzuri, inamtia doa, anaweza asiaminike tena iwapo itawekwa wazi, kwa sababu ataonekana hafanani na kauli zake.

“Siyasemi haya kwa sababu nina kisasi na Spika, bali ni kwa sababu umeniuliza. Unajua Spika amenijeruhi hivi karibuni, sasa sitaki nionekana kama ninalipa kisasi. Lakini ukweli unabaki pale pale kwa sababu umeandikwa vitabuni kuwa kuna kasoro katika Ofisi ya Bunge ambayo inasimamiwa na Spika,” alisema Cheyo.

Spika Sitta alipoulizwa kuhusu kauli hiyo ya Cheyo, alisema hahusiki kwa namna yoyote na uchukuaji wa masurufu, hivyo hapaswi kunyooshewa kidole iwapo imebainika kuwapo kwa kasoro zozote za matumuzi mabaya ya fedha za serikali katika ofisi yake.

Spika alisema taratibu ziko wazi kuwa wanaochukua masufuru kwa ajili yake ni wasaidizi wake wanaohusika kumuandalia safari zake zote, ndani na nje ya nchi.

“Mimi sihusiki kuchukua masurufu, wanaohusika ni wasaidizi wangu, sasa kama kuna kasoro, wao ndio wanajua. Nina ofisi yangu binafsi kama viongozi wengine wakuu wa kitaifa, sitembei na fedha mfukoni, wasaidizi wangu wa ofisi hiyo ndio wanaoniandalia safari na ziara zangu zote. Wao ndio wanaonilipia kila kitu, walinzi, maradhi, kila kitu, ndio wanaochukua fedha za masurufu kwa niaba yangu,” alisema Spika Sitta.

Alipoulizwa kuhusu madai kuwa alitumia fedha nyingi za Ofisi ya Bunge kugharamia vikao na tafrija zilizokuwa zikifanyikia nyumbani kwake wakati mkewe, Margaret Sitta, ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, akiwania nafasi ya kuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), alisema madai hayo inabidi yafafanuliwe.

“Ninachokijua mimi kuhusu hili, ni kweli kulikuwa na vitu vya aina hiyo wakati huo, lakini ninachokumbuka ni kwamba gharama nyingi za mikusanyiko hiyo nilikuwa ninatumia fedha zangu za mfukoni, nilikuwa nalipa mwenyewe. Lakini hili ili nilielewe vizuri, inabidi lifafanuliwe,” alisema.

Naye Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah alipoulizwa kuhusu hali hiyo, alisema hawezi kuzungumza jambo hilo, kwa sababu alipoingia katika wadhifa huo alikuta hali hiyo imeshatokea.

Alibainisha kuwa ni kweli hakuhojiwa na Kamati ya PAC kwa sababu alikuwa hajaapishwa na rais, lakini kwa sasa kamati hiyo inaweza kuendelea na kazi zake kama kawaida, bila kupata kipingamizi kutoka kwa mtu yeyote.

“Mimi nilipoingia katika ofisi hii, hali hiyo niliikuta, hivyo siwezi kusema kitu, kwa sababu sikuwapo, siwezi kuizungumzia. Ninachoweza kukitolea maelezo ni kile ambacho kimefanyika wakati wa kipindi changu.

“Lakini suala la ripoti hiyo kukaliwa halipo, PAC ikitaka kukaa kuijadili hata kesho ni sawa tu, hakuna tatizo, waje wakae, wao wana ratiba zao za vikao, kuna ripoti nyingi tu hazijajadiliwa, hizi hazijakaliwa, naomba kwa sababu linahusu Ofisi ya Spika, isichukuliwe kuwa linazimwa,” alisema Dk. Kashililah.

Ripoti ya CAG, ambayo Tanzania Daima Jumatano imeiona, katika ukurasa wake wa 43, fungu la 42, inaitaja Ofisi ya Bunge katika orodha ya taasisi za serikali zilizopewa hati zenye shaka, kwa kukiuka taratibu za kihasibu.

Ripoti hiyo inabainisha kuwa Ofisi ya Bunge ilifanya malipo ya matibabu nje ya nchi ya zaidi ya sh milioni 101 bila kuidhinishwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, uhamisho wa fedha wa zaidi ya sh milioni 63 kutoka kifungu kimoja kwenda kingine bila kibali na malipo yenye thamani ya sh milioni 7.8 yalifanyika bila kibali.

Upungufu mwingine uliotajwa katika ripoti hiyo ni malipo yenye nyaraka pungufu ya sh milioni 526, malipo yasiyo halali ya sh milioni 102.5, malipo yenye shaka ya sh milioni 63.9, mishahara isiyolipwa na ambayo haikurejeshwa Hazina sh milioni 17.1, sh milioni 3.4 za mishahara ya watumishi walioachishwa kazi inayoendelea kulipwa kwenye akaunti zao benki na usuluhisho wa tofauti ya sh milioni 1.1 kati ya bakaa ya benki na bakaa inayoonyeshwa katika daftari la mapato na matumizi haukufanyika.

Marekebisho yasiyostahili yaliyojumuishwa kwenye hundi ambazo hazijawasilishwa benki ni sh milioni tano, masurufu maalumu ya sh milioni 50.2


KINACHOKWAMISHA VITA DHIDI YA UFISADI NI HUU MTINDO WA KUENDESHA MAMBO KISHKAJI.UKITAFAKARI KAULI YA CHEYO KUHOFIA KUHUSISHA HABARI ZA UFISADI HUO NA HATUA YA SPIKA KUMTOA NJE YA BUNGE HIVI KARIBUNI UTAGUNDUA KUWA BADALA YA MBUNGE HUYO KUSHUGHULIKIA SUALA HILO KAMA MWENYEKITI WA KAMATI HUSIKA,YEYE ANAJIONA KAMA JOHN MOMOSE CHEYO ALIYETOLEWA NJE NA SAMUEL SITTA,BADALA YA OFISI YA BUNGE ILIYO CHINI YA SPIKA NA WATENDAJI KADHAA.

NA UNAFIKI MWINGINE NI WA HAO WABUNGE WALIONUKULIWA KATIKA HABARI HII AMBAYO HAWATAKI KUTAJWA MAJINA KISA WANAOGOPA KUANDAMWA NA WABUNGE WENZAO.KWANI WALIINGIZWA BUNGENI NA HAO WABUNGE WENZAO WANAOWAOGOPA AU WANANCHI HUKO MAJIMBONI?

WIZI MTUPU!


12 Jul 2009


Kizitto Noya na Habel Chidawali, Dodoma

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Shamsa Mwangunga, amekiri kukithiri wizi wa nyara za serikali hasa pembe za ndovu na kueleza kuwa sio rahisi kudhibiti vitendo hivyo kwa kuwa vinafanywa na mtandao wa watu wenye fedha nyingi.

Mwangunga alisema hayo bungeni jana alipokuwa akihitimisha mjadala wa bajeti ya wizara yake mjini na kufafanua wizi wa makontena mawili ya pembe za ndovu yaliyokamatwa Machi, mwaka huu nchini Vietnam.

“Kukithiri kwa wizi huo kumetokana na Wizara ya Maliasili na Utalii kutohusishwa na ukaguzi wa mizigo bandarini na soko kubwa la nyara hizo liko katika nchi za Asia. Mtandao wa watu wenye fedha nyingi ndio unaendesha biashara hiyo kwa kushirikiana na maafisa wa bandari,” alisema Mwangunga.

“Ninasema maafisa wa bandari wanahusika kwa sababu bandarini ndiko kwenye lango la kupitisha nyara hizo na maafisa wake ni miongoni mwa watuhumiwa katika matukio hayo.”

Mwangunga alikuwa akijibu hoja ya mbunge wa Same Mashariki Anne Kilango Malecela ambaye juzi alitishia kutoa hoja binafsi kutaka iundwe Kamati teule ya Bunge kuchunguza wizi wa makontena hayo yaliyokamatwa Machi 25, mwaka huu nchini Vietnam.

Mbunge huyo alitaka kamati hiyo ichunguze jinsi makontena hayo yalivyopita kwenye bandari za hapa nchini baada ya kukaguliwa na mamlaka husika na kufika Vietnam bila kujulikana kuwa yalibeba pembe za ndovu.

"Mheshimiwa Spika, naomba nizungumzie kuhusu jambo ambalo kwa kweli limenisikitisha sana ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii ambao ni wizi wa nyara; wizi wa pembe za ndovu. Wizi huu Mheshimiwa Spika, unafanyika kama vile nchi yetu hakuna ulinzi," alilaumu Kilango na kuongeza:

"Nimefanya utafiti nina faili zima; Mheshimiwa Spika nilikwenda kufanya utafiti, baada ya kusoma kwenye magazeti kuhusu makontena mawili yaliyokamatwa Vietnam, nikaona nisiishie hapo niende ndani mpaka nipate faili zima.

"Nasikitika sana. Nilikwenda kuhoji; nikaelezwa; nikapewa na faili; nikasoma kontena zile mbili zilipitia bandari yetu kama kawaida".

Kilango aliomba atumie kanuni ya 117 ya Bunge kuwasilisha hoja binafsi kutaka iundwe kamati teule kwa ajili ya kuchunguza jambo hilo.

Hata hivyo, jana Spika wa Bunge Samuel Sitta ambaye juzi aliahidi kufanyia kazi suala hilo, alitupa hoja hiyo baada ya Kilango kushindwa kuwasilisha kusudio lake hilo kwa maandishi kwa wakati.

”Kulikuwa na hoja ya kuundwa kamati teule jana, lakini niseme kwamba, hoja hiyo sijaipata hapa kwa maandishi, nimwombe Katibu aendelee na shughuli za leo,” alisema Sitta muda mfupi kabla ya bunge kukaa kama kamati.

Kabla ya Sitta kusema hivyo, aliingia bungeni akikimbia akiwa ameshika bahasha ya kaki ambayo ilisemekana kuwa ilikuwa na hoja yake hiyo kimaandishi ambayo alitarajia kuiwasilisha.

”Naona kuna kitu kinataka kunifikia sijui kama ndio hiyo hoja, ah, lakini kwa mujibu wa kanuni za Bunge siwezi kuipokea hoja hiyo na kusema kweli itakuwa ndiyo basi, sitaipokea tena hivyo tunaendelea waheshimiwa,” alisema Sitta.

Akizungumza na gazeti hili katika viwanja vya Bunge jana, Kilango alisema alichelewesha kupeleka hoja yake baada ya awali kushauriwa na Spika kuwa suala hilo liachwe liendelee kushughulikiwa na Polisi wa Interpol chini ya makubaliano ya Lusaka (Lusaka Agreement).

”Mimi hoja nilishaandaa, lakini Spika alinishauri kuwa kwa vile suala hilo linashughulikiwa na Interpol, tuache kwanza.

Lakini hii haina maana kwamba, hoja imekufa. Nitaiibua tena wakati wowote baada ya interpol kumaliza kazi yake,” alisema.

Awali akizungumzia wizi huo Mwangunga alisema ulitokea Machi 25 mwaka huu na tayari watu tisa wamekamatwa na kuhojiwa.

”Kati yao, watu wanne wamefunguliwa kesi mahakamani mkoani Tanga,” alisema Mwangunga na kutaja majina ya watuhumiwa hao.

Alisema mbali na tukio hilo, kontena lingine lilikamatwa Machi Mosi, mwaka huu katika Bandari ya Manila Ufilipino ambako pembe za ndovu zenye uzito wa tani tano lilikamatwa.

Siku nne baadaye maafisa Forodha wa Vietnam walikamata kontena lingine namba ESU 1174 lililokuwa na tani 6.2 za pembe za ndovu.

Hata hivyo, Mwangunga alishindwa kusema pembe hizo za ndovu zilitoka wapi kama alivyotakiwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe.

Kabwe alitaka waziri huyo aeleze endapo shehena hiyo ni ndovu wanaoendelea kuuawa au zimekwapuliwa kutoka kwenye ghala la serikali.

”Siwezi kusema kuwa zilitoka wapi kwani katika ghala za serikali hakuna wizi uliotokea na namna zilivyopangwa na kama ingechukuliwa hata moja ni rahisi sana kujua, hivyo inawezekana zilitoka katika maeneo yetu au hata nchi jirani waliamua kusafirisha kwa kupitia bandari zetu kutokana na udhaifu uliopo katika bandari za hapa nchini,” alisema Mwangunga.

CHANZO: Mwananchi

INA MAANA WIZARA INGEWEZA KUWADHIBITI MAFISADI HAO LAITI MTANDAO WAO UNGEKUWA NA FEDHA KIDOGO AU HOHEHAHE?HII WIZARA IMEKUWA KICHAKA CHA MAFISADI MIAKA NENDA MIAKA RUDI.BY THE WAY,KAMA MAFISADI WANAWEZA KUTUIBIA BENKI KUU (THRU EPA,etc) AMBAPO KUNA ULINZI WA HALI YA JUU,TUTEGEMEE NINI HUKO MBUNGANI?TUTAJUA MENGI PINDI IKIFANYIKA "SENSA" YA RASLIMALI ZETU HUKO MBUGANI.HOPEFULLY,BY THEN MAFISADI HAWA HAWATAKUWA WAMEKOMBA KILA KITU!


<

11 Jul 2009


Pamoja na sifa zake nyingi ikiwa ni pamoja na kuwa jiji la tatu kwa ukubwa (kwa idadi ya watu idadi ya watu,nyuma ya London na Birmingham) hapa UK,Glasgow,unabeba historia ya "Simba na Yanga" za Scotland,yaani klabu mbili za soka zenye upinzani wa kupindukia:Glasgow Rangers (almaaruf RANGERS) na Celtic.Tofauti na upinzani wa Simba na Yanga,au Manchester City na Manchester United,au kwingineko kwenye "mafahali wawili wanaopigania ubabe kwenye mji mmoja",upinzani kati ya Celtic na Rangers umevuka mipaka ya soka.Wakati Celtic ni,generally speaking,Wakatoliki,Rangers ni Waanglikana.Zamani hizi,ilikuwa jambo lisilowezekana kabisa kwa mchezaji Mkatoliki kusajiliwa na Rangers,au Muanglikana kusajiliwa na Celtic.

Sasa,moja ya tahadhari wanazopewa wageni katika jiji la Glasgow ni rangi za timu hizo mbili.Ukirogwa kuvaa "jezi" za Rangers kwenye maeneo ya wapenzi wa Celtic,au kutinga rangi za Celtic kwenye maeneo ya kujidai ya Rangers,tarajia yasiyotarajiwa.






In his first visit to Africa since taking office, Barack Obama said today that the continent of his ancestors must overcome tyranny and corruption if it is to flourish.

Speaking in Ghana's parliament, Obama said the key to Africa's future prosperity was democratic and accountable government.

"Development depends upon good governance. That is the ingredient which has been missing in far too many places, for far too long. That is the change that can unlock Africa's potential," he said.

In an tough speech aimed at politicians across the continent, he gave an unsentimental account of squandered opportunities since the end of colonial rule. "No country is going to create wealth if its leaders exploit the economy to enrich themselves, or police can be bought off by drug traffickers," he said.

"No business wants to invest in a place where the government skims 20% off the top ... No person wants to live in a society where the rule of law gives way to the rule of brutality and bribery. That is not democracy, that is tyranny, and now is the time for it to end.

"Africa doesn't need strongmen, it needs strong institutions."

Obama conceded that colonialism had left a legacy of conflicts and arbitrary borders. "But the west is not to blame for the destruction of the Zimbabwean economy over the last decade, or wars in which children are enlisted as combatants.

"Africa is not the crude caricature of a continent at war," he said. "But for far too many Africans conflict is a part of life, as constant as the sun. There are wars over land and wars over resources. And it is still far too easy for those without conscience to manipulate whole communities into fighting among faiths and tribes."

Earlier, after meeting Ghana's president, John Atta Mills, Obama praised the country's record of democracy and economic growth as a rare success in a continent beset by corruption and poor governance.

"We think that Ghana can be an extraordinary model for success throughout the continent."

This morning, Obama was given a hero's welcome in the country's capital, Accra. Thousands of people wearing Obama T-shirts thronged the streets, cheering and waving as his motorcade swept past.

Walls and utility poles were plastered with posters of Obama and Mills, as well as the word "change" – the mantra of Obama's presidential election campaign. Other posters showed the president and his wife, Michelle, with the greeting "Ghana loves you".

Obama and his family arrived late last night from the G8 summit in Italy, where the world's richest nations agreed on a $20bn (£12.4bn) food security plan to help poor nations feed themselves during the global recession.

Speaking in Italy before he left, Obama said: "There is no reason why Africa cannot be self-sufficient when it comes to food."


The Obamas will visit Gold Coast Castle, a former British slave trading post. Michelle Obama is a great-great granddaughter of slaves.

The visit comes as the US plans a much more assertive policy in Africa, using both diplomacy and the threat of force to end the protracted conflicts in Democratic Republic of the Congo and Nigeria, which are seen as two of the main obstacles to the continent's progress.

"This is both a special and an important visit for him personally as president, but also for our country to articulate a vision for Africa," said Robert Gibbs, the White House spokesman.

Despite the enthusiastic reception from ordinary Ghanians, no major public events have been planned during Obama's 21-hour visit, for fear it could cause a celebratory stampede, as almost happened during a 1998 stop by Bill Clinton.


SOURCE: The Guardian

10 Jul 2009

Rais Barack Obama anaonekana kama "analipiga jicho" bunda (makalio) la binti wa Kibrazili,Mayara Tavarez,huku Rais Nicholas Sarkozy akishika tama!Yes,He can!


9 Jul 2009


A British diplomat in Russia, James Hudson, has quit after being filmed having sex with two blonde prostitutes.Hudson, 37, resigned from his posting to the Urals over the video, which is thought to have been secretly shot by Russian spies.

The footage apparently shows Mr Hudson, wearing a dressing gown, kissing the two semi-naked girls while drinking champagne in a brothel
...CONTINUES



8 Jul 2009


Neo-Nazis are plotting a 'spectacular' terrorist attack on Britain to fuel racial tension, Scotland Yard's counter-terrorism officers fear.

Senior officers have increased their surveillance of suspects to monitor their ability to carry out a deadly attack aimed at causing a 'breakdown in community cohesion'.

The chilling warning comes after last month's startling gains by the BNP in the local and European elections which many fear may 'embolden' violent Far-Right extremists.

Commander Shaun Sawyer, from the Met's specialist operations wing told a meeting of British Muslims last night: 'I fear that they will have a spectacular ...

'They will carry out an attack that will lead to a loss of life or injury to a community somewhere. They're not choosy about which community.'

His comments came after Commissioner Sir Paul Stephenson asked officers to examine what effect the recession could have on far-right violence.

And the news mirrors similar warnings of the threat from far-right sympathisers issued in America in recent months.

While countering a threat from Islamic extremists remains the priority many officers now believe that funds need to be funnelled towards preventing a possible strike by the Far-Right.

Threat level in the UK may be downgraded, says terror chief

Despite the warning, Assistant Commissioner John Yates today warned that counter terrorism police face budget cuts.

He admitted savings must be made in two years time despite the risks posed by the looming London 2012 Olympic Games.

The senior officer, who took control of Scotland Yard's specialist operations wing three months ago, said it would be "naive" to think counter terrorism work would escape the recession.

Last weekend it was revealed that a network of suspected extremists with access to 300 weapons and 80 bombs has been uncovered by counter- terrorism detectives.

Thirty-two people were questioned by police and 22 properties were raided over an alleged plot to bomb mosques.

It was the biggest terrorist arms haul since the IRA mainland bombings in the 1990s.

Sir Norman Bettison, the chief constable of West Yorkshire, said: 'The big bad wolf is still the Al-Qaeda threat.

'But my people are knocking over right-wing extremists quite regularly. We are interdicting it so that it doesn't first emerge into the public eye out of a critical incident like an explosion.'

It is more than 10 years since neo-Nazi nail bomber David Copeland attacked three targets in London in 1999.

Three people died at the Admiral Duncan gay pub in Soho.

Copeland also targeted the Muslim community in Brick Lane, east London, and a supermarket in Brixton, south London.

Abdurahman Jafar of the Muslim Safety Forum, where the concerns were raised, said:

'Muslims are the first line of victims in the extreme right's campaign of hate and division and they make no secret about that.

'Statistics show a strong correlation between the rise of racist and Islamophobic hate crime and the ascendancy of the BNP.'

Mark Gardner, of the Community Security Trust, which monitors violence against Jews, said there has been a surge in right-wing incidents.

He said: 'Ten years after the Nazi nail bombings in London, we are seeing increasing numbers of neo-Nazis being arrested in their attempts to start some kind of so-called race war.

'It is the Muslim community that appears to be most targeted, but all of society is at risk, and we are in regular discussion with police about the problem.

'Worse still, the recent electoral successes for the BNP may cause some would-be terrorists to be further emboldened in their actions.'

Last year neo-Nazi Martyn Gilleard, 31, was convicted of three terrorism offences and jailed for 16 years.

Gilleard idolised Adolf Hitler and urged sympathisers to act to preserve the 'purity of the white race'.

When police raided his flat they found bullets, swords, knives and four nail bombs under a bed used by his five-year-old child.

Officers also found DIY bomb manuals, a guide on making a sub-machine gun and internet instructions on carrying out assassinations by poison.

A speech he had recorded in a notebook mentioned 'killing Muslims, blowing up mosques and fighting back'.

No one at the Muslim Safety Forum was available for comment. The Metropolitan Police declined to comment.

Last month a white supremacist with links to the BNP shot dead a security guard at Washington's Holocaust Museum in a racially-motivated killing.

Before launching the attack, 88-year-old James von Brunn sent out an email claiming: 'It's time to kill all the Jews.'

Von Brunn was shot and wounded by museum security officers after he walked into the packed tourist attraction and began firing indiscriminately.

4 Jul 2009



KWANZA Merged

Picha kwa hisani ya KENNEDY

Wanasema siasa ni mchazo mchafu.Lakini siasa katika bara letu la Afrika ni zaidi ya mchezo mchafu.Ni mchanganyiko wa kanyaboya,songombingo,mbinde,usanii,ufisadi na what have you.Hiyo sio kumaanisha kuwa siasa katika maeneo mengine,kama Ulaya na kwingineko ni safi kihivyo.Lakini angalau hawa wenzetu check-and-balance mechanism zinafanya kazi kwa kiasi kikubwa.Sie tunazo lakini aidha wenye majukumu ya kuzitumia wako bize sana na posho au nyumba ndogo au hawajui kwa nini wapo mahala panapopaswa kufanya hiyo check na balance.

Hivi CCM walikuwa wanafikiri nini mwaka 2005 kuahidi kuwa wangeshughulikia uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi?Binafsi sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama hiyo as long as suala hilo linafanywa kwa uangalifu.Sio priority kwa sasa lakini kwa vile ni haki kwa Waislamu,then hakuna budi kuangalia uwezekano huo.Kwahiyo,CCM hawakufanya kosa "kukubali" kuanzisha Mahakama ya aina hiyo baada ya uchaguzi mkuu wa 2005.Hawakufanya kosa kwa vile wazo hilo sio baya au la hatari kama baadhi ya watu wanavyofikiria.Nitatafuta wasaa mwafaka siku nyingine kuelezea kwanini Waislam wako sahihi kudai mahakama hiyo na kwanini uanzishwaji wake hauna madhara kwa wasio waislam.In fact,suala sio "kuanzisha" bali "kurejesha" kwa vile mahakama za aina hiyo zilikuwepo wakati wa ukoloni na muda mfupi baada ya uhuru.

Kosa la jinai (yes,ni jinai) la CCM ni kutoa ahadi nyeti kama hiyo wakati inafahamu fika kwamba haina muda wa kuishughulikia.Ni kosa pia kwa vile pamoja na ahadi hiyo ya kuanzisha mahakama ya kadhi tayari chama hicho kilikuwa kimeshatoa ahadi nyingine lukuki kana kwamba kinaomba kutawala kwa miaka 100 na sio mitano (2005-2010)!Kulikuwa na ahadi za kuwakalia kooni wala rushwa,kushughulikia kero za Muungano,kuboresha maisha ya Watanzania,na ahadi nyingine kedekede.Si tu kwamba wakati tunaelekea mwishoni mwa miaka hiyo mitano rushwa imeshamiri na ku-mutate into ufisadi (kumbuka,neno hili limejitokeza katika kipindi hiki),kero za Muungano sio tu kuwa bado zipo ila tumeshuhudia "kibiriti kikitikiswa mpaka kinataka kulipuka",na hayo maisha bora kwa kila Mtanzania sanasana yamewezekana kwa mafisadi na washirika zao....

Hili la kuahidi kushughulikia masuala yanayogusa imani (ya kiroho) ilhali hakuna dhamira au uwezo wa kufanya hivyo ni jambo hatari mno.Dini ni hatari zaidi ya ukabila kwani inahusisha uhai na kifo (mtu akifa kwa ajili ya dini ni martyr,at least dini nyingi zinaamini hivyo).

Kauli za viongozi kuhusu suala hili sio tu zimekuwa za kujichanganya bali zimechangia kukuza tatizo hilo.Mara mchakato unaendelea,mara sheria za kiislam zitaingizwa kwenye sheria za mahakama za sasa (hicho tayari kinafanyika),mara hili,mara lile.Kama kawaida,wahusika wanasubiri lilipuke ndio watafute chanzo cha mlipuko.Unfortunately,milipuko mingine ikianza hata huo muda wa kutafuta chanzo hautokuwepo.Waulize Nigeria!

Tuiombee nchi yetu.












Michael Jackson mithili ya chura!?The Jacko mithili ya Bikira Maria!?Ukishangaa yanayohusu maisha na kifo cha the King of Pop basi hujakutana na "kazi za sanaa" zinazomhusu the Jacko.Picha za juu ni baadhi tu ya "kazi" hizo.Unajua,fani yenyewe ya sanaa imetawaliwa na ujanja ujanja wa namna flani.Kwa mfano nenda maeneo ya Msasani kwa wauza vinyago wa Kimakonde.Utakutana na kinyago cha Nyerere,kwa mfano,lakini zaidi ya ukweli kuwa kinyago hicho ni cha mpingo (kama alivyodai mchonga kinyago),the rest havifanani kabisa na Nyerere,unless uwe hujawahi kuona sura ya Baba wa Taifa.Pita pita mitaani,utakutana na wasanii wanaodai wanaweza kukuchora na wakikamilisha mchoro utadhani unajiangalia kwenye kioo.Of course,wapo wenye vipaji vya namna hiyo.Lakini kuna " wasanii" pia.Atakuchora,kisha akikupatia "picha yako" unaweza kuishia kutamani kumkaba loba (kabali) ya mbao!

Na kifo cha Michael kinaelekea kuwa dili la nguvu kwa WASANII kwa maana ya ARTISTS na WASANII kwa maana ya CONFIDENCE ARTISTS (con artists).Ama kweli kufa kufaana!



3 Jul 2009


Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Mufti Issa bin Shaaban Simba, amekasilishwa na uamuzi wa serikali kuhusu Mahakama ya Kadhi.

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.

Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.

Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.

Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao.

Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka .


CHANZO: Mwananchi


KWA MWENENDO HUU SI AJABU KUSIKIA HATA WATANZANIA WALIOAHIDIWA MAISHA BORA NAO WAKAJITOKEZA KUDAI HAWAITAKI CCM....HOJA IKIWA MAISHA BORA YALIYOAHIDIWA YAMEISHIA KWA KUNDI DOGO LA MAFISADI PEKEE!



In a recent interview with MTV News, The Game relayed Michael Jackson’s attempts to end the beef between him and 50 Cent. Although the rappers eventually laid the feud to rest (without Jackson’s help) the tension between the two still remained.However, The Game has finally taken it upon himself to give a formal apology, not just to 50, but to the whole Interscope label.“For 50, I’m just gonna apologize to him, just as a man,” he told MTV. “It has nothing to do with music, or beef, or nothing like that. It ain’t about being the bigger man. He can take it and say, ‘Game is apologizing,’ ‘Game’s a sucka, he’s apologizing.’ I’m apologizing for me to him, to [Dr.] Dre, to Jimmy Iovine, to Eminem, to all the fans. Because if you think about what Interscope was when we were gellin’, man we were it. We were an unstoppable force.”

He explained that while he was a member of G-Unit, there were some things he needed to do “for my career to have longevity, and for me to survive in Hip Hop music,” and this may have played a part in the dissolving relationship between himself and 50 Cent. He also expressed some regret that G-Unit and the Interscope label did not get to experience the success that it could have had, potentially.

“Now, four albums in, I can say as a man that G-Unit, Game, Aftermath, Black Wall Street, Interscope, Geffen, Eminem, Shady, from [Lloyd] Banks to [Young] Buck to [Tony] Yayo to Dre to whoever; If it woulda kept going: endless paper. Millions of albums sold. Because we were great together.”

The Game also expressed his strong belief that, had he and G-Unit (and perhaps Young Buck) not parted ways, many things would have been different.

“Me and Fif’s chemistry is what Method Man was to Redman when they get in. Red ain’t from Wu-Tang but you know when Meth gets wit' Redman it’s goin’ down… [Me and 50’s] biggest records were together. Whether I was on them or I wasn’t on them. Whether he was on them or he wasn’t on them. When we were in gellin’ writing together as a family, we had it man. If we never would have [broken] up, I think Detox would have been out and we all would have been selling millions from Banks to Buck, and Tony Yayo. I’m going to apologize for my role.”

50 Cent and the Aftermath camp have not yet issued a response.

SOURCE: Hiphopdx.com


1 Jul 2009


CCM wafanya mkutano kanisani, wampiga kiongozi wa kigango

Na Frederick Katulanda, Biharamulo

WAFUASI wa CCM juzi walivamia Kanisa Katoliki, Kigango cha Nyantakara kilicho Kata ya Lusahunga na kufanya mkutano wao, huku wakimshambulia na kumjeruhi katibu wa kanisa hilo baada ya kuwaamuru watoke.

Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 3:00 asubuhi wakati wafuasi hao wa wanawake wa CCM, wakiongozwa na mtu mmoja aliyejulikana kwa jina moja la John, walipoingia kanisani humo kwa madhumuni ya kuchukua viti kwa ajili ya mkutano wao. Badala ya kuchukua viti, waliamua kutotoka na kufanyia mkutano huo kanisani.

Akizungunza na Mwananchi katekista wa kigango hicho ambacho kipo katika parokia ya Kaniha, jimbo la Kahama, Faustine Damas alisema wafuasi hao wa CCM waliingia kanisani na kuchukua meza ya kuendeshea ibada na kuigeuza kuwa meza ya wageni wao na baadaye kuendesha mkutano wao.

Alieleza kuwa alipofika kanisani alistaajabu kusikia nyimbo wa 'Tieni, tieni' ukiimbwa na baada ya kuingia ndani alikuta wakiwa wanaendelea na mkutano wao huku wakitumia meza kuu ya ibada, jambo ambalo lilimfanya ampigie simu katibu wa kigango hicho, Festus Masumbuko ambaye baada ya kuwaomba waondoke na kuwanyang'anya meza hiyo ya ibada, wafuasi hao wa CCM walianza kumpiga.

"Waliamua kugoma kuondoka na ndipo alipowanyang'anya meza ya ibada, lakini wakamvamia na kumpiga mateke na ngumi. Wamemjeruhi vibaya na pia wamemchania shati," alieleza katekista huyo.

Alisema kutokana na hali hiyo alilazimika kupiga kelele na ndipo wananchi walipofika na kumwokoa. Lakini wakati hali hiyo ikiendelea, mfuasi mmoja wa CCM alipiga simu polisi na kuwaeleza kuwa walikuwa wakifanyiwa vurugu na ndipo polisi walipoenda eneo hilo na kuwakamata wananchi waliokuwa wanataka kumuokoa katibu.

Wananchi hao wanashikiliwa na polisi kwa kufanya vurugu katika mkutano huku wana CCM wakiachiwa huru na kuondoka zao.

Kutokana na hali hiyo paroko wa parokia ya Kaniha, Padri Isaya Bahati ambaye pia ni msaidizi wa askofu wa jimbo la Kahama, alisema muda mfupi baadaye akiwa polisi kuwa amesikitishwa na vurugu hizo na kusisitiza kuwa kanisa kama nyumba ya ibada inapaswa kuheshimika kwa vile si uwanja wala ukumbi wa mikutano.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, naibu katibu mkuu wa CCM, George Mkuchika alisema hana taarifa ya vurugu za wafuasi wake kanisani na kwamba kwa kuwa amepokea taarifa hizo, atazifuatilia kwa kina.

“Ngoja nifuatilie kwa kina kujua ni nini kimetokea,” alieleza Mkuchika.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Henry Salewi alisema kuwa hakuwa kwenye eneo la uchaguzi na kumtaka mwandishi awasiliane na kamishina Telesphol Anaclet ambaye ndiye amekuwa akishughulikia masuala hayo. Hata hivyo, kamishna huyo alisema jeshi la polisi linaendelea na masuala yake hivyo lipewe nafasi ya kufanya kazi.

“Naomba mtuache tufanye kazi yetu sina cha kukueleza kwa sasa,” alisema kamishina huyo wa oparesheni maalumu ya uchaguzi na akakata simu.

Waliokamatwa na jeshi hilo la polisi wametajwa kuwa ni Evarist Dotto, Semen Elias, Mosha Makoye, Batista na Timetheo ambao walitambulika kwa jina moja.

CHANZO: Mwananchi

HITIMISHO LISILOHITAJI TAFAKURI YA KINA NI KWAMBA CCM IMEFILISIKA KISIASA,NA KATIKA KUTAPATAPA KWAKE IKO TAYARI HATA KUWEKA REHANI AMANI NA UTULIVU WA TAIFA LETU.

NA KWA JINSI ILIVYOSHINDWA KUJINASUA NA TUHUMA KWAMBA INAKUMBATIA UFISADI NA MAFISADI,NI DHAHIRI KAMPENI ZA 2010 ZITASHUHUDIA MAZINGAOMBWE,UHUNI NA UPUUZI ZAIDI YA HUU.DINI NI KITU HATARI KINAPOTUMIWA KWA MINAJILI YA UBINAFSI WA KISIASA JAPO BINAFSI SINA KIPINGAMIZI NA KUCHANGANYA DINI NA SIASA ALIMRADI WAHUSIKA WAWE MAKINI KUTENGANISHA LIPI LA KAIZARI NA LIPI LA KIROHO.

30 Jun 2009





Kifo cha mtu maarufu huambatana na kila aina ya tetesi.Na kifo cha Michael Jackson is no exception.Ukisikiliza,kuona au kusoma kuhusu kifo cha mfalme huyo wa Pop,unaweza kumhukumu kirahisi tu kuwa alikuwa mithili ya mfu aliye hai (dead man walking).Baadhi ya vyombo vya habari vinadai Michael alikuwa akibwia madawa lukuki ya kumudu maumivu ya mwili.Mengine yanadai alikuwa amekongoroka kupita kiasi.Gazeti moja limekwenda mbali zaidi na kudai kwamba eti miezi michache iliyopita,ilibainika wazi kuwa Michael alikuwa na miezi si zaidi ya sita ya kuishi.Lakini picha hizi zilizopigwa wakati wa rehersal zake zilizopangwa kufanyika O2 Arena mwezi ujao,zinatoa taswira tofauti kabisa.


29 Jun 2009

Bwana Mapesa,John Momose Cheyo,Mbunge wa Bariadi kwa tiketi ya UDP akitoka nje ya jengo la bunge baada ya kukumbana na makali ya viwango na spidi vya Mheshimiwa Spika Samuel Sitta.Ironically,Cheyo ni mwandishi-mwenza (co-author) wa kitabu BUNGE LENYE MENO.

CHANZO: Jamii Forums

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.