26 Jan 2009

Gavana wa zamani wa "Benki Kuu" ya Marekani,Allan Greenspan
Rais Mstaafu wa Marekani,George W Bush
Rais Mstaafu wa Marekani,Bill Clinton

Waziri Mkuu wa Uingereza,Gordon Brown
Bonyeza HAPA kwa orodha kamili na maelezo.

25 Jan 2009


Hatimaye katika kukabiliana na wimbi la mauaji ya albino,Waziri Mkuu Mizengo Pinda ameagiza leseni za waganga wa jadi wote zifutwe.Majuzi,Pinda alikaririwa akiagiza wananchi kuchukua sheria mkononi kwa kuwaua "wauaji wa maalbino".Hatua zote mbili zinaweza kutofanikiwa kwa vile inaelekea kana kwamba zimechukuliwa pasipo kufanyiwa utafiti wa kina.


Kuruhusu wananchi wafanye "jino kwa jino" dhidi ya wanaoua maalbino kunaweza kulipeleka Taifa mahala pabaya.Taasisi pekee yenye mamlaka ya kuhukumu ni mahakama zetu,na hizo ndio zinazoweza kuhakiki makosa halasi tofauti na majungu,chuki,visasi,nk na haki inatarajiwa kuwa imetendeka pindi hukumu itapokuwa ya kifo au mshtakiwa kuachiwa huru kulingana na ushahidi uliowasilishwa mahakamani.Hilo haliwezekani katika "mahakama za jino kwa jino mitaani".Si ajabu watu waliokosana kwa sababu zao binafsi wakishia kupigana mapanga kwa kisingizio cha "kudhibiti mauaji ya maalbino".Ikumbukwe kuwa ni rahisi kuruhusu uvunjifu wa sheria lakini ni zaidi ya vigumu kurejesha heshima na utiifu kwa sheria.


Tuje kwa hili la kufuta leseni za waganga wa jadi.Je amri hii inamaanisha ni marufuku kwa mtu yeyote kujihusisha na uganga wa jadi au...?Sijaelewa vizuri hapo lakini nahisi inamaanisha hivyo kwani katika hali ya kawaida,kufanya shughuli inayohitaji leseni pasipo kuwa na leseni husika ni uvunjifu wa sheria.Swali la kwanza,hivi ni waganga wa jadi wangapi wenye leseni (tukiachana na hao Maprofesa wanaojitangaza kwenye magazeti kuwa wanatibu ukimwi,wanawezesha kufaulu pasipo kusoma,na miujiza mingine)?Nauliza hivyo kwani haitaleta mnaana yoyote kumfutia mtu leseni ambayo hajawahi kuwa nayo hata siku moja.Swali la pili,je utekelezaji wa amri hiyo utasimamiwa vipi?Polisi watazungukia mganga mmoja hadi mwingine nchi nzima kuhakikisha kuwa hafanyi uganga?
Swali la tatu,je tumefikia hatua ya kufanya maamuzi kwa kigezo cha "samaki mmoja akioza basi wote wameoza"?Nauliza hivyo kwani tafsiri ya moja kwa moja ya kuwafutia leseni masangoma ni kwamba wao ndio wahusika muhimu katika suala la mauaji ya maalbino.Hii "overgeneralization" inatoka wapi?Mbona wale wazembe wa Muhimbili walipompasua kichwa mgonjwa wa goti na wa goti akapasuliwa kichwa walioadhibiwa ni madaktari husika tu na sio kada nzima ya madaktari hapo Muhimbili au nchi nzima?Au mbona ilipobainika kwamba kuna uhuni umefanyika pale BoT kwenye ishu ya EPA,aliyefukuzwa kazi ni Ballali pekee na wengine wameendelea kuwa madarakani hadi leo?Au mbona aliyekuwa balozi wetu huko Italy alipokumbwa na tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma haikupelekea kutimua mabalozi wote?Sasa iweje "uhuni" wa baadhi ya waganga wa jadi upelekee hukumu kwa wote wanaohusika kwenye taaluma hiyo (na yayumkinika kusema kuwa wengi wao-hususan vijijini-ni waadilifu katika kazi yao)?


Naomba nisisitize kwamba hapa simaanishi two wrongs make a right.Hapana,najaribu kuangalia approaches za nyuma katika kukabiliana na matatizo mbalimbali na namna zinavyokinzanna na hii ya ku-revoke leseni za waganga wa jadi.


Kwa wanaofahamu umuhimu wa tiba asili katika jamii husasan katika kipindi hiki cha uchangiaji wa gharama kwenye public health facilities,ni dhahiri hatua ya kuwafutia leseni waganga wote wa jadi itaathiri Watanzania wengi wanaotegemea huduma hizo (aidha kutokana na imani,nature ya maradhi yao au uwezo duni katika kumudu gharama za huduma za afya hospitalini).


Japo ni muhimu sana kutafuta ufumbuzi wa haraka kukomesha mauaji dhidi ya maalbino,ni muhimu zaidi kutumia common sense and viable approaches kuliko hatua ambazo pamoja na nia zake nzuri zinaweza kutuletea matatizo zaidi.Tukirihusu sheria zivunjwe kwa kuruhusu kuua wanaoua maalbino (badala ya kuwafikisha kwenye vyombo vya dola) basi tusishangae pindi baadhi ya wananchi watakapoamua kuchukua sheria mkononi dhidi ya mafisadi,kwa mfano,badala ya kusubiri kesi zilizoko mahakamani,ripoti za tume,nk

23 Jan 2009



CLICK HERE for more on this story.

Salaam,
Tunakukaribisha www.TanzaniaYetu.com ambapo tovuti zote zinazohusu TANZANIA zinaandikishwa bure.
Wako,
Uongozi
http://www.tanzaniayetu.com/
------------------------------------------------------------------------------------------------- Dear Sir/Madam,
We sincerely welcome you to www.TanzaniaYetu.com where websites concerning TANZANIA are listed and you can list yours for free.
Kindest Regards,
Team,www.TanzaniaYetu.com


KATIKA hali ya isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu Mizengo Pinda jana aliwaambia wananchi kuwa wanaoua watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) pamoja vikongwe ni hawana budi kuuawa kwa kuwa wakisubiri mahakama kuwahukumu, watakuwa wanakosea.

Waziri Pinda, ambaye ameanza ziara katika mikoa ya Kanda ya Ziwa yenye lengo la kuhamasisha vita dhidi ya mauaji ya vikongwe na albino, aliutaka Umoja wa Vijana wa CCM kuongoza vita hiyo, akisema lina jeshi zuri. Mauaji ya albino yamekuwa ni tatizo kubwa nchini na hasa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Pamoja na serikali kutangaza hatua kadhaa za kupambana na wauaji hao, bado matukio ya kuuawa kwa watu hao wenye ulemavu wa ngozi yamekuwa yakiendelea kuripotiwa,
lakini Waziri Pinda ameenda mbali zaidi katika kukabiliana na tatizo hilo alipotaka wauaji hao wauawe badala ya kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.


Kauli ya Pinda, ambayo inaweka maswali katika suala la utawala bora, imekuja wakati ambao wananchi wamekuwa wakijichukulia sheria mkononi na kuua vikongwe kutokana na imani za uchawi. Akihutubia wakati wa kufungua mkutano wa 16 wa Shirikisho la Vyama vya Kuweka na Kukopa (SCCULT) kwenye ukumbi wa Chuo cha Utumishi Umma mkoani hapa, Waziri Pinda alisema iwapo wananchi wataendelea kuwahurumia wauaji hao ambao wanatafuta viungo vya albino wakitegemea mahakama itatenda haki huku nao wakiongeza kasi ya mauaji kwa Watanzania, watakuwa wanakosea.


Hivyo alisema kwamba kuanzia sasa mtu yeyote atakayemuona mtu amemkata shingo au mkono mweziwe basi naye auawe papo hapo hii itakuwa ndiyo dawa kwani vingozi wote tumechoka na mauji hayo.


"
Mkimuona mtu akamkata mwingine shingo naye muueni kwani sasa viongozi wote tumechoka... no more, I can't tolerate anymore (imetosha, siwezi kuvumilia tena)," alisema Pinda huku akiwaacha watu midomo wazi.


Aliviomba vyama vya siasa kushirikiana na wananchi kuhakikisha suala hili la mauji linakwisha kwani wauji "tunaishi nao na ni rahisi kulimaliza iwapo tutakuwa kitu kimoja katika kuondoa kashifa hii ambayo imekuwa mbaya kwa nchi yetu".


Aliuagiza Umoja wa Vijana wa CCM kuhakikisha mauaji hayo yanatokomezwa kabisa, akisema kuwa ni jeshi zuri ambalo likiamua kutokomeza kabisa mauaji ya vikongwe na ndugu zetu maalbino inawezekana.


"Umoja wa vijana mna jeshi zuri ambalo naamini mkiamua mnaweza kutokomeza mauaji ya wazee wetu pmoja na ndugu zetu maalbno na kazi hiyo nawaagiza muanze leo msisubri auawe mwingine tena
," alisema waziri mkuu.


Baada ya kumalizika kwa mkutano huo, baadhi ya watu wanaoonekana kuwa ni wa "serikali" waliwafuata baadhi ya waandishi wa habari, akisihi suala hilo lisiripotiwe magazetini kwa madai kuwa kauli hiyo ya Waziri Pinda inaweza kusababisha matatizo.



Rais Jakaya Kikwete, ambaye pia amekuwa mstari wa mbele kupiga vita mauaji hayo, alitofautiana na Waziri Pinda katika moja ya hotuba zake aliposema kuwa adhabu ya kuua haitofautishi muuaji wa albino na muuaji mwingine na kwamba watakaopatikana na hatia ya kuua albino, atakabiliana na adhabu ya kifo kama ilivyo kwa muuaji mwingine.


Waziri Pinda alionekana kukerwa na mauaji ya albino wakati alipopata taarifa kwamba kuna mama mwingine aliuawa usiku wa kuamkia juzi.


"Nimeambiwa kuwa juzi wilayani Sengerema kuna mama mmoja ambaye ni mlemavu wa ngozi amekatwa mkono na wauaji wakaondoka na mkono huo na tayari mama huyo amekufa," alisema Pinda na kusisitiza kushughulikia wauaji hao. Akitoa takwimu za mauaji ya vikongwe na malbino alisema mwaka 2003 waliuwawa vikongwe 517, mwaka 2004 waliuawa vikongwe 444, mwaka 2005 (494), 2006 (vikongwe 386), mwaka 2007 (vikongwe 526) na albino sita na mwaka 2008 (vikongwe 526 na albino 28). Alisema tayari mwaka huu wameuawa albino watatu hivyo kufanya albino na vikongwe waliouawa kufikia kuwa jumla 2,900.


Waziri mkuu ameanza ziara ya siku nne kutembelea mikoa ya Shinyanga, Tabora na Mwanza ili kuhamasisha wananchi watokomeze vitendo vya mauaji ya vikongwe na watu weye ulemavu wa ngozi.


CHANZO: Mwananchi

WHILE NOT CONDONING THE EVIL DEEDS BY THOSE WHO KILL THE ALBINOS ,I JUST DON'T SEE HOW THIS "AN-EYE-FOR-AN-EYE STYLE OF RULE OF LAW" COULD BE EFFECTIVE IN ELIMINATING THIS PROBLEM!I'M EVEN MORE SCARED OF A POSSIBILITY THAT UVCCM MIGHT TURN THIS THING INTO A POLITICAL CRUSADE...CLAIMING CHADEMA ARE BEHIND THE ALBINO KILLINGS,FOR INSTANCE...WE ALL KNOW HOW DIRTY OUR POLITICS GETS WHEN THE YOUTH WINGS OF OUR PARTIES ARE MOBILIZED TO EXHAUST WHATEVER MEANS THEY HAVE TO ADDRESS SOME SENSITIVE ISSUES IN OUR SOCIETY...

22 Jan 2009

Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wakifanya patrol hapo Mlimani (UDSM).Picha kwa hisani ya MICHUZI JR.

Nilimaliza ngwe yangu hapo Mlimani (UDSM) takriban miaka kumi iliyopita.Kuna yaliyobadilika kwa kipindi cha miaka mitatu niliyokuwa hapo,na kuna mengine yamebaki kama yalivyo.Kwa kifupi sana,katika miaka hiyo mitatu,sikumbuki kama kuna academic year iliyopita pasipo mbinde ya aina moja au nyingine kati ya wanafunzi na serikali.Na kila mara chanzo kilikuwa kilekile:FEDHA.

Binafsi nadhani chanzo cha matatizo ya migogoro kati ya wanavyuo na serikali ni mapungufu katika sera nzima ya uchangiaji gaharama za elimu ya juu.Kwa nchi masikini kama yetu,haihitaji busara kufahamu kwamba kuna wanafunzi lukuki wanaotoka katika familia ambazo kumudu gharama za maisha ya kila siku ni mgogoro,achilia uwezo wa kumudu gharama za kumsomesha mtoto chuo kikuu.Kwa mantiki hiyo,ajenda ya kulipa ada na gharama nyingine kwa silimia 100 ni suala lisilowezekana kwa wanafunzi wanaotoka familia za aina hii,ambao kwa hakika ni wengi zaidi.

Kinachohitajika ni usimamizi mzuri wa mikopo kwa wanafunzi wa aina hiyo.Hii ni investment nzuri kwa future ya taifa letu.Iwapo serikali itakuwa na nia ya dhati kuhakikisha kuwa wakopeshwaji wanarejesha fedha hizo,ni dhahiri itajitahidi kuwatengenezea mazingira mazuri ya ajira pindi watapohitimu masomo yao...kwa vile ajira hiyo ndio inayotarajiwa kuwawezesha kulipa mikopo hiyo ya serikali.

Kama tunaweza kuwakopesha wabunge mashangingi yenye thamani ya mamilioni ya shilingi,naamini kabisa kuwa kuwakopesha wanavyuo wetu ni swala linalowezekana pasipo kusababisha hizi mbinde za kila mwaka au muhula wa masomo.Tatizo sio sera ya uchangiaji gharama per se bali,kama ilivyo kwenye maeneo mengine mengi,ni utekelezaji wa sera hiyo.FFU wanaweza kutuliza ghasia chuoni hapo kwa muda lakini hawawezi kuwa ufumbuzi wa tatizo hilo.

19 Jan 2009

16 Jan 2009





Pichani,ni KEZIA OBAMA-mama wa kambo wa Barack Obama-akiwa uwanja wa ndege wa Heathrow,London hapa Uingereza tayari "kukwea pipa" kuelekea Marekani kuhudhuria kuapishwa kwa mwanae hapo Jumanne ijayo.Kezi,ambaye kwa sasa anaishi Bracknell, Berkshire,aliwahi kuolewa na marehemu baba yake Rais Mteule Obama.Mama huyo aliondoka siku ambapo sanamu (waxwork) ya mwanae ilizinduliwa katika musemum ya Madame Tussaud jijini London.





14 Jan 2009

WARNING: Very Graphic

Osama bin Laden has called for Muslims to wage a holy war against Israel over the invasion of Gaza. Skip related content

The al-Qaeda leader called for jihad in an audio tape that appeared on Islamist websites. In response, the US said it demonstrated bin Laden's isolation and it was merely an effort to raise money.

The news came as United Nations Secretary-General Ban Ki Moon visited the Middle East to press for an immediate ceasefire in the Gaza Strip.

The Hamas-run Health Ministry in Gaza has said 1,010 Palestinians - including over 670 civilians - have been killed in the offensive which began on December 27. Around 4,700 people have been wounded.

t
Ten Israeli soldiers and three civilians hit by rockets fired from the Gaza Strip have been killed in the violence. Israel has continued to drop bunker-busting bombs on around 35 smuggling tunnels under the Gaza-Egypt border in a bid to halt Hamas re-arming.

Meanwhile, in Cairo, Mr Ban renewed his call for "an immediate and durable ceasefire" between the warring sides. An unnamed Israeli official has said Egypt, which is trying to broker a truce, is pushing for a deal by the weekend.

The official said "there has been progress" on talks over border controls to prevent Hamas from replenishing its arsenal. But he said Israeli leaders were non-committal about the prospect of reaching a ceasefire accord in the next few days. Elsewhere, three rockets launched from Lebanon hit fields outside
the Israeli town of Kiryat Shmona, the second such attack in less than a week.
SOURCE: ITN



13 Jan 2009

Venance George, Morogoro
BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kauli iliyotolewa juzi na baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu kupinga oparesheni Sangara inayoendeshwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), si kauli ya waislamu wote.
Akizungumza mjini Morogoro kwa niaba ya Kaimu Mufti wa Tanzania,
Shekhe Suleiman Gorogosi, mratibu wa habari wa Bakwata, ustadhi Issa Mkalinga alisema kauli hiyo ni ya waislamu wachache ambao wamekuwa wakitumiwa na viongozi wa kisiasa kwa manufaa binafsi.
Ustadhi Mkalinga pamoja na Mkurugenzi wa Utawala, ustadhi Karim Mataliwa, aakizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara ya kaimu mufti huyo ya kutembelea mikoani kuhamasisha uhai wa baraza, alisema baraza halitambui kauli hiyo na wala halijihusishi na mambo ya siasa.
"Ujue tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu hapo mwakani, hivyo wako baadhi ya wanasiasa wanatumia mwanya wa majukwaa ya dini kupeleka ujumbe wao," alisema.
Akizungumzia ziara ya kaimu mufti mkoani Morogoro, Mkurugenzi wa Utawala alisema kuwa ziara hiyo ni sehemu ya utaratibu aliyojiwekea kaimu mufti ya kutembelea baraza katika mikoa yote Tanzania na kwamba kaimu mufti ametembelea Dodoma na Morogoro na atatembelea mikoa mingine.
Ustadhi Mataliwa alisema lengo la ziara hizo ni kutaka kujua uhai wa baraza na matatizo yanayolikabili baraza katika ngazi hizo ikiwa ni pamoja na kuhimiza kufanya maandalizi ya uchaguzi wa viongozi kuanzia ngazi ya msikiti hadi taifa utakaoanza kufanyika mwezi April mwaka huu.
Wakati huo huo, katika mahojiano na baadhi ya waumini wa dhehebu hilo, mkoani Morogoro wameunga mkono kauli ya Bakwata na kudai kuwa viongozi wa dini ni vema wakafanya shughuli zao za kiroho na kuwaacha wanasiasa kufanya kazi zao za siasa.
Mmoja wa waumini hao, Ismael Rashid, alisema tamko lililotolewa na waislamu katika kongamano la jijini Dar es Salaam la kudai kuwa Chadema haina manufaa na msaada wowote kwa uislamu si maneno ya kiungwaana na si vema kukipakazia chama hicho kwamba ni kikabila na cha kibinafsi.
Rashid ambaye pia ni kiongozi wa chama cha Jahazi asilia mkoani Morogoro alisema hatua iliyochukuliwa na Chadema ya kuacha kuunga mkono vyama vya CUF na Sauti ya Umma (SAU) ilikuwa ni sahihi kwa sababu chadema walisimamisha mgombea ubunge katika jimbo la Mbeya vijijini lakini vyama hivyo vilimwekea pingamizi mgombea huyo na kuenguliwa.
"Pingamizi hilo lilisababisha mgombea ubunge wa Chadema akaenguliwa kugombea
nafasi hiyo, sasa iweje chadema iwaunge mkono?" alihoji Rashid .
Alisema chama cha Chadema hakiungi mkono kampeni za mgombea wa CUF kwa mdai kuwa chama hicho, mwakani inakusudia kusimamisha mgombea wake katika jimbo hilo kwa hiyo kama Chadema ikiunga mkono CUF itashindwa kusimamisha mgombea wake hapo mwakani.


CHANZO:Mwananchi

12 Jan 2009

KWANZA,SAMAHANI KWA KUPOTEA ANGANI GHAFLA.HIYO NI KUTOKANA NA SABABU ZILIZOKUWA NJE YA UWEZO WANGU.PILI,NIMEKUTANA NA HABARI IFUATAYO KATIKA GAZETI LA MWANANCHI,NA IMEVUTA HISIA ZANGU.ISOME KWANZA KISHA TUIJADILI KIDOGO


WAUMINI wa dini ya kiislam wamepinga oparesheni sangara
inayoendeshwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa madai kuws
chama hicho na operesheni hiyo, haina manufaa kwa uisalam kwa kuwa imejaa
ukabila, ubinafisi na udini
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye
kongamano la kiisilamu, lililofanyika jana jijini Dar es Salaam, walisema
oparasheni Sangara imekuwa ikimchafua rais Jakaya Kikwete bila sababu licha ya
mambo mengi mazuri, aliyoyafanya kwa taifa.
Shekhe Saidi Mwaipopo aliwataka
waisalamu kutambua kuwa chama hicho, hakina msaada wowote wa maendeleo ya
uislamu kutokana na chama hicho kujaa ukabila udini na ubinafisi.
"Napenda
waislamu muelewe kuwa chama cha Chadema hakina msaada wowote juu ya uislamu na
kimekumbatia udini, ukabila na ubinafisi kutokana na sababu hiyo, tutatembea
nchi nzima kuwaeleza wanachi ukweli wa jambo hili na kuwataka wasikiunge mkono
chama hicho,"alisema Mwaipopo...
ENDELEA


HISIA ZANGU ZA HARAKA NI KWAMBA KUNA KUNDI LA MAFISADI AMBAO KATIKA KUTAPATAPA KWAO WAMEAMUA KUTUMIA TURUFU YA UDINI.KUNA VUGUVUGU LA UDINI LINALOENDELEA KIMYAKIMYA HUKO NYUMBANI.KUNA WATU WANATUMIWA KUTETEA MASLAHI YA MAFISADI,AIDHA WAKATI WANAFAHAMU KUWA WANATUMIWA AU HAWAFAHAMU KABISA.




HIVI INAINGIA AKILINI KWELI KWA WAUMINI WA DINI INAYOSIMAMIA HAKI (UISLAM) KUPINGA HARAKATI ZA KUSIMAMIA HAKI?JE IWAPO OPERESHENI SANGARA ITAZAAA MATUNDA KWA KUFANIKISHA UDHIBITI DHIDI YA MAFISADI,WAISLAMU NCHINI HAWATONUFAIKA?HAPA KUNA MIKONO YA WATU WANAOMWAGA FEDHA ZXAO ZA KIFISADI KWA WALE WALIO TAYARI KUSEMA LOLOTE ALIMRADI MKONO UENDE KINYWANI.




TUSIPOKUWA MAKINI,UFISADI UTAIFIKISHA TANZANIA MAHALA PABAYA ZAIDI YA HAPA TULIPO.

7 Jan 2009

Padre Privatus Karugendo amekuwa akisimulia mkasa ulisababisha yeye kusimamishwa,na hatimaye kuvuliwa,daraja la upadre.Kma nilivyoeleza katika post hii,japo sifahamiani personally na Mtumishi huyu wa Bwana,alikuwa columnist mwenzangu katika jarida la Raia Mwema hadi nilipolazimika kuchukua "sabbatical leave" ya uandishi wa makala.Pia,maandiko mbalimbali ya Padre Karugendo yalinipa changamoto kubwa hadi nikaamua kujiingiza katika anga za uandishi wa makala kwenye magazeti mbalimbali huko nyumbani.

Unaweza kusoma SIMULIZI kuhusu chanzo cha mkasa uliopelekea Padre huyo kusimamishwa na hatimaye kuvuliwa upadre kwa KUBONYEZA HAPA (Sehemu ya Kwanza) na HAPA (Sehemu ya Pili) na HAPA (latest).Blogu hii itaendelea kuwaletea simulizi hizo kadri zinavyochapishwa gazetini.Mkasa uliomkumba Padre huyu unanigusa sio tu kwa vile napenda makala zake au kwa sababu tuliwahi kuandikia gazeti moja,bali pia kwa vile kwa namna flani yeye,kama mie,ni majiruhi wa mfumo uliozowea kupongezwa na kunyenyekewa lakini usiotaka kusikia criticism au mawazo mbadala.
NYONGEZA: Nimekutana na post katika blogu ya Pambazuko ambapo Askofu (anayetajwa kwenye Simulizi za Karugendo) ANADAIWA KUWA NA MTOTO NA ANATAKIWA AKAMCHUKUE. (Bonyeza link kuisoma)




MWANGALIE MZAZI HUYU ASIYE NA AIBU KATIKA PICHA HII ILIYOPATIKANA KWA HISANI YA Father Kidevu.AMEJAWA NA TABASAMU WAKATI ANAMPELEKEA BIA MWANAE AMBAYE KWA MAKISIO HAZIDI MIAKA MITANO.TENA BIA YENYEWE NI SAFARI,AMBAYO HATA WANYWAJI SUGU WANAELEWA INAVYOMPELEKESHA MNYWAJI.INGEKUWA KWENYE NCHI ZINAZOJALI HAKI YA MTOTO NA WAJIBU WA WAZAZI,HUYU FISADI WA MALEZI ANGESHACHUKULIWA HATUA.KWANINI AMRITHISHE MWANAE ULEVI BADALA YA VITU VYA MUHIMU ZAIDI KWA FUTURE YA DOGO HUYO?HEBU ANGALIA VIDEO HII HAPO CHINI YENYE HABARI KUHUSU MZAZI ALIYECHUKULIWA HATUA KWA KILICHOELEZWA KUWA NI KOSA LA KUMPA SAPOTI MWANAE APIGANE.
KAMA WENZETU WANAWEZA,WHY NOT US?




CLICK HERE to read more about Orgasmic childbirth


6 Jan 2009

Picha kwa hisani ya Mjengwa.

Habari hiyo ni kwa mujibu wa gazeti la  Sunday Citizen.Pia,mwanablogu BWAYA ameichambua kwa undani habari hiyo ya kusikitisha.Makala za Padre Karugendo ni miongoni mwa maandiko yaliyonishawishi nami njiingize kwenye fani ya uandishi wa makala.Nahisi Kanisa Katoliki limechukua hatua hiyo kutokana na msimamo makini na wa uwazi wa Padre Karugendo kuhusiana na mambo mbalimbali ya Kanisa hilo.Japo mie ni Mkatoliki pia,lakini sipendezwi na namna Kanisa hili lisivyopenda kukosolewa.Nalinganisha tukio hili na lie la Father Nkwera (na wanamaombi) ambaye kimsingi kosa lake kubwa ni kutumia karama kama ile aloyokuwanayo Bwana Yesu ya kuponyesha wagonjwa.Yayumkinika kubashiri kwamba hatma ya Kanisa letu sio ya kuleta matumaini sana kama litaendeleza UKALE na kujifanya halitambua dunia inavyobadilika.

5 Jan 2009


ALIYEKUWA Mkuu wa Majeshi Nchini, Meja Jenerali, Robert Mboma, amesema anaamini kitambi alicho nacho kimesababisha kushindwa katika kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) za ubunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini.

Mboma aliyasema hayo juzi wakati akiwashukuru wananchi katika uzinduzi wa kampeni za chama hicho za kinyang'anyiro cha ubunge wa jimbo hilo.Alisisitiza kuwa anaamini kilichochangia kutopata kura nyingi zaidi ni kitambi hicho alichokuwa nacho na kwamba hali hiyo itamkomaza kisiasa.

Mboma ambaye aliwashangaza baadhi ya watu walioshuhudia uzinduzi wa kampeni hizo uliofanywa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi katika kijiji cha Ilembo Mbeya vijijini.Alisema kkuanguka kwake katika jimbo hilo kumetokana na wananchama wa chama hicho kumnyima kura.

Alisema kitendo hicho hakiotamuathiri bali wanamkomaza kisiasa na kwamba endapo kama angeteuliwa kuwa Mbunge wa jimbo hilo angelepeleka maendeleo."Kwa kweli nanawashukuru wananchi mlionipigia kura nilizozipata ingawa hazikuwa ndogo lakini ninasikitika na ninawashukuru ambao hawakunipigia kura na kuniangusha wakati wakijua wazi kuwa mimi ni mzaliwa na hapa na mngenichagua ningewaletea wananchi maendeleo katika jimbo la Mbeya vijijini," alisema.

Aliendelea kusema kuwa sio mbaya hata kama wamemchagua Mchungaji Mwanjali kwa sababu anaimani atawaletea Maendeleo na kurithi yale yote aliyatarajia kuyafanya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Marehemu Richard Nyaulawa katika kuboresha huduma za jamii hususan maji, umeme na kuboreshea miundombinu...HABARI HII INAENDELEA HAPA.

NILIDHANI WANAJESHI WANASTAHILI KUJIWEKA FIT HATA BAADA YA KUSTAAFU MAJUKUMU YAO.HOW COME MKUU WA MAJESHI AMEJIACHIA KIASI CHA KUWA NA KITAMBI KIKUBWA "KILICHOPELEKEA KUANGUSHWA KWAKE KWENYE KINYANG'ANYIRO HICHO"? BY THE WAY I DONT BUY HIS LAME EXCUSE.NADHANI HAKUFANYA RESEARCH YA KUTOSHA KABLA YA KUJIINGIZA KWENYE COMPETITIVE POLITICS.WATANZANIA WAMEANZA KUTOFAUTISHA KATI YA UMAARUFU WA MTU NA UWEZO WA KUWALETEA MAENDELEO.AND IT'S THE LATTER THAT LED TO MBOMA'S FAILURE TO WIN HIS PARTY'S NOMINATION.

HII DHANA YA KWAMBA ANGEPATA UBUNGE ANGEWEZA KUWALETEA MAENDELEO WANA MBEYA VIJIJINI SIO TU POTOFU BALI PIA MUFILISI.KWANI ILI KULETA MAENDELEO YA WANANCHI WENZIO NI LAZIMA UWE KIONGOZI WAO?ALISHINDWAJE KUWALETEA MAENDELEO ALIPOKUWA KIONGOZI WA KITAIFA (MKUU WA MAJESHI) LAKINI AWEZE ATAPOPATA UBUNGE?NI UKOSEFU WA WASHAURI WAZURI AMBAO WANGEPASWA KUMKUMBUSHA HISTORIA YA MA EX-CDF WENZIE.

Magazeti mbalimbali ya leo huko nyumbani yameongozwa na habari za uzinduzi wa kampeni za CCM katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Mbeya Vijijini unaotarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu.Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi ndiye aliyezindua kampeni hizo na kufanya kila ambacho kwa muda mrefu kimekuwa adimu katika duru za siasa za vyama vingi huko nyumbani.Kwa mujibu wa habari hizo,Mwinyi,maarufu kama Mzee Ruksa,alitumia sehemu kubwa ya hotuba yake kuzungumzia maslahi ya wana-Mbeya Vijijini katika uchaguzi huo badala ya kuipigia debe CCM pekee.

"Mwinyi...hakuonyesha unazi kwa CCM wala mgombea wake wakati alipozindua kampeni za chama hicho jana katika kata ya Kijiji cha Ilembo kilicho tarafa ya Isangati wilayani Mbeya Vijijini.Badala yake, Mwinyi alisisitiza amani, mshikamano na maendeleo ya wilaya ya Mbeya Vijijini, akiwataka wananchi wa eneo hilo kuhakikisha wanabakia na mshikamano wakati wanasiasa watakapoondoka jimboni humo baada ya purukushani za uchaguzi...linaandika gazeti la Mwananchi.

Tanzania Daima linamnukuu Mwinyi akisema kwamba "Vyama vya siasa vishindane kwa sera, visitumie lugha za matusi, kejeli, dharau na uongo wakati wa kampeni, uungwana wenu viongozi wa siasa utawapa matumaini wananchi kuchagua chama au mtu wanayemtaka ili kuhakikisha kuwa maendeleo ya nchi yanakua kwa kasi".

Akionyesha kuthamini zaidi maslahi ya wananchi wa Mbeya vijijini kuliko ya kisiasa,Rais huyo mstaafu aliwausia wapiga kura jimboni humo "kumsikiliza kila mgombea kwa makini na baadaye kila mmoja amchague yule anayeona sera za chama chake zinakidhi matumaini ya wananchi wa Mbeya Vijijini, " na kuhakikisha "kwamba wakati wanasiasa wetu wanapoondoka Mbeya Vijijini baada ya kampeni nyinyi mnabaki kuwa kitu kimoja katika umoja wenu," linaeleza Habari Leo.

MIONGONI MWA MAMBO YANAYOKWAZA MAENDELEO NI KUWEKA MBELE MASLAHI YA KISIASA BADALA YA YALE YA WANANCHI.OF COURSE,VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WANAPASWA KUSIMAMIA MASLAHI YA VYAMA VYAO LAKINI NI MUHIMU KWAO KUTAMBUA KUWA JUKUMU KUU LA VYAMA HIVYO NI KUWAHUDUMIA WANANCHI NA NI WANANCHI HAOHAO WANAOWEZESHA KUWEPO HAI KWA CHAMA IN THE FORM OF WANACHAMA.KWA MANTIKI HIYO,WANANCHI,REGARDLESS YA POLITICAL AFFILIATIONS ZAO,WANA NAFASI NA UMUHIMU WA KIPEKEE KWA VYAMA VYA SIASA HASA IKIZINGATIWA PIA KWAMBA WAO NDIO PIA CHIMBUKO LA UONGOZI KATIKA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA.

BAADA YA KUNG'ATUKA KATIKA ACTIVE POLITICS,BABA WA TAIFA ALIJITAHIDI KUCHUKUA NAFASI YA UANASIASA WA KITAIFA BADALA YA KICHAMA AMBAPO MARA KADHAA ALIWEKA MKAZO KATIKA MASUALA YANAYOHUSU TAIFA KWA UPANA BADALA YA YALE YA CHAMA CHAKE CHA CCM PEKEE,LICHA YA KUWA YEYE NDIO ALIKUWA MIONGONI MWA WAASISI WAKUU WA CHAMA HICHO TAWALA.KWA UPANDE MWINGINE,MWINYI NAFASI YA MWINYI BAADA YA KUSTAAFU UENYEKITI WA CCM IMEPEWA ATTENTION NDOGO NA WACHAMBUZI WA SIASA PAMOJA NA MEDIA KWA KUTOFANYA REFERENCE YA NAMNA KIONGOZI HUYO WA ZAMANI ANAVYOJITAHIDI KUFUATA FOOTSTEPS ZA BABA WA TAIFA KATIKA KUTANGULIZA ZAIDI MASLAHI YA WANANCHI NA TAIFA KWA UJUMLA BADALA YA KUENDEKEZA UNAZI WA KISIASA PEKEE.

NI MATUMAINI YA WATANZANIA WOTE WAPENDA MAENDELEO KWAMBA MFANO HUU WA MZEE MWINYI UTAIGWA NA WANASIASA WETU WOTE KAMA KWELI NIA YAO NI KUTUHUDUMIA KUPITIA VYAMA VYAO.LAKINI PIA WANANCHI NAO WANAPASWA KUFUMBUKA MACHO NA KUTAMBUA KWAMBA UNAZI WA KISIASA HAUPASWI KUWA INFRONT OF MASLAHI YAO KAMA WANANCHI,NA KWA MANTIKI HIYO TOFAUTI ZETU ZA KIITIKADI HAZIPASWI KULETA MGAWANYIKO AU KUPELEKEA KUCHAGUA VIONGOZI WABOVU KWA VILE TU WANATOKA KATIKA VYAMA TUNAVYOSHABIKIA.

HONGERA SANA MZEE RUKSA.YOU TRULY HAVE SHOWN THE RIGHT WAY.



4 Jan 2009

Ghana's peaceful presidential election was a rare example of a functioning democracy in Africa and should be a model for the continent, African leaders and voters have said. Skip related content

Much attention in Africa and elsewhere was focused on the Ghanaian vote after a year of political crises, many of them violent, tarnished Africa's democratic credentials.

Opposition candidate John Atta Mills was declared the winner on Saturday after the closely fought election was settled by a run-off.

Kenya's prime minister Raila Odinga said: "John Atta Mills' victory and the conduct of the people of Ghana provides a rare example of democracy at work in Africa."

While the contest raised tensions and some violent incidents were reported, international observers say the vote was mostly peaceful. The conduct of the election contrasted with many other African countries, where democracy was battered in 2008.

More than 1,000 people were killed in post-election violence in Kenya at the start of the year and in Zimbabwe President Robert Mugabe and opposition leader Morgan Tsvangirai have been deadlocked for months over a power-sharing agreement after disputed elections.

SOURCE: ITN

3 Jan 2009

Maelfu ya waandamanaji wanatarajiwa kuandamana baadae leo jijini London kupinga mashambulizi ya Israel dhidi ya Wapalestina.Inakadiriwa takriban watu 20,000 watashiriki maandamano hayo yatakayowajumuisha watu maarufu kama Mbunge wa chama cha Respect,George Galloway na mwanamuziki mkongwe Annie Lennox.Picha ya mwanzo inaonyesha akinamama wa Kiislam walioandamana jana jijini Dar kupinga mashambulizi hayo,na picha za chini zinaonyesha hali ilivyo na uharibifu uliosababishwa na makombora ya Israel huko Gaza.




VYANZO:Sky News,Habari Leo ,The Washington Post na The Guardian.


2 Jan 2009

Soma stori kamili HAPA.

1 Jan 2009

FASHIFASHI LONDON EYE JIJINI LONDON,UINGEREZA

FIREWORKS ST ANDREWS STREET,EDINBURGH,SCOTLAND.

WARSAW,POLAND.

VILNIUS,LITHUANIA.


SALA YA MWAKA MPYA POPE BENEDICT KATIKA MISA YA MKESHA WA MWAKA MPYA HUKO VATICAN CITY,VATICAN.

SHAMRASHAMRA JIJINI VALENCIA,SPAIN.

TAIPEI,TAIWAN.

SOFIA,BULGARIA.

RED SQUARE,MOSCOW

MANILA,PHILIPPINES.

POLISI WAKIDHIBITI WAANDAMANAJI WA KIPALESTINA MKESHA WA MWAKA MPYA HUKO ATHENS,UGIRIKI

GISBORNE,NEW ZEALAND.

CHAMPS ELYSEE,JIJINI PARIS,UFARANSA.

BERLIN,UJERUMANI.

FASHIFASHI JIJINI ATHENS,UGIRIKI.

MALAYSIA.

HONGKONG


SYDNEY,AUSTRALIA.

AUCKLAND,NEW ZEALAND.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.