30 Apr 2010

Mtakatifu au mzushi?

Raia mmoja wa India amegusa hisia za jeshi la nchi hiyo kutokana na madai yake kwamba haitaji chakula wala maji kumudu kuishi.Prahlad Jani anadai yeye ni 'breatharia',yaani mtu anayeweza kuishi kwa kutumia nguvu za asili za kiimani.Anadai anapata nguvu hizo za asili kutoka kwa 'mungu wa kike' anayemmwagia kimiminika (elixir)cha miujiza katika paa la chini la mdomo wake (palate),kwa mujibu wa gazeti la Telegraph la London. 


Wakati baadhi ya watu wanamwona kama 'mzushi' flani,taasisi ya maendeleo ya utafiti wa ulinzi inasema Prahlad anaweza kutoa mwangaza katika kuwasaidia wanajeshi kumudu kukaa muda mrefu bila kula,au hata wahanga wa majanga mbalimbali.Hadi sasa amekaa siku sita bila kula au kunywa chochote katika hospitali iliyopo Hyderabad,na madaktari wanasema haonyeshi dalili yoyote ya kuathiriwa na njaa.

"Ikithibitika kuwa madai yakni sahihi,basi itakuwa hatua kubwa sana kwenye sayansi ya tiba",anasema Dkt G.Ilavazhagan,Mkurugenzi wa Taasisi ya Ulinzi ya Fiziolojia na Stadi Shiriki."Itatuwezesha kuokoa maisha ya wanadamu katika nyakati za majanga,kimo cha juu,safari za majini,na mazingira mengine magumu ya kibinadamu na ya asili.Tutaweza kuwaelimisha watu kuhusu namna ya kustahimili (surviving) mazingira magumu pasipo chakula na maji au chochote kile".

Madaktari wataendelea kumchunguza kwa siku 15 kipindi ambacho wanataraji kuona misuli yake ikisinyaa,upungufu mkubwa wa maji mwilini,kupungua uzito wa mwili na baadhi ya viungo vya mwili kushindwa kufanya kazi.

Binadamu wengi hawawezi kustahimili zaidi ya siku 3 hadi 5 pasipo kunywa maji.

Imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily News la India.

29 Apr 2010

NEWSWEEK: Black blogs cover a far more diverse range of stories than the rest of the media. Just ask Sandra Bullock. While Sandra Bullock's post-Oscar split from husband Jesse James may be the biggest celebrity news in the last month (or two), it's probably not surprising it's the adopted brown baby that really got the African-American blog sites going. The funny thing is, black Web sites such as MediaTakeOut.com, Bossip, and Young, Black and Fabulous have been following Bullock for years. Part of the reason is her connection to the black community. "They know about her support for victims of Katrina and Haiti so they care about what happens to her, which we thought about when we gave her coverage," says Fred Mwangaguhunga, owner of the black entertainment site MediaTakeOut.com. But part of it is that black blogs look at the world differently than the often segregated mainstream.
. CLICK HERE TO READ THE FULL STORY

The US Army says that it is it is wasting far too much time preparing Powerpoint presentations and not enough time killing people.

For a while now the Army has been concerned that its officers are missing entire wars preparing Powerpoint slides and making presentations.

. TechEye has got its paws on the sort of slide they mean (see above). 

Last summer Gen Stanley McChrystal, the leader of US and Nato forces in Afghanistan, said when we understand that slide that “we’ll have won the war’.

Gen James Mattis of the Marine Corps, said: "Powerpoint makes us stupid". The Marines are not renowned for being that bright in the first place, which makes them some of the US's best soldiers, but Powerpoint sucks about the direction you want to point them.

Sam Nuxoll, a platoon leader in Iraq, seems to have shaken the Pentagon with a quote that said he was spending most of the war making Powerpoint slides. Instead of spending his time dodging bullets, he was making bullet points.

What is the problem is the fact that rather than encouraging making decisions PowerPoint sucks up the time of junior officers. The idea is that they can get crappy decisions blessed if it looks good in Powerpoint. However really good tactics which are dull on screen are being mothballed.

This has been noticed in business too with some companies thinking that Powerpoint presentations are a waste of time too.

.SOURCE: Tech Eye

JIJI la Tanga limfeunikwa na simamzi kuu kufatia wanafunzi 18 wa Chuo cha Kiislamu cha Shamsil-Maariff kufa papo hapo na wengine 125 kujeruhiwa vibaya, baada ya lori walilokuwa wakisafiria kutoka kwenye sherehe za maulidi kupinduka.

. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Adolphina Kapufi aliliambia gazeti hli jana kuwa ajali hiyo ilitokea saa 5:30 usiku wa kuamkia jana katika eneo la njiapanda kuu ya Mabanda ya Papa jijini hapa.

Kapufi aliwataja baadhi ya waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Twalib Kunemu, Juma Idd, Faraji Habib, Jahshi Rashid, Hussein Bakari, Hajji Athumani naYussuph Hussein na kwamba, kazi ya kuwatambua maiti wengine bado inaendelea.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Paschal Kanyinyi alisema kazi ya kuwatambua waliokufa na majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo wodi ya Galanosi inaendelea.

Kanyinyi aliwataja majeruhi waliotambuliwa kuwa ni Jumaa Salim ambaye ameumia mbavu, Makame Ahmed, Ahmed Shehe, Selemani Said na Juma Akida.

Aliwataja majeruhi ambao hali zao ni mbaya, hivyo waliokimbizwa katika Hospitali Taifa ya Muhimbili, jijini Dar essalaam kuwa ni Hemed Shaaban na Hassan Adam.

Kanyinyi alifahamisha kuwa kati majeruhi 125 walifikishwa katika hospitali hiyo usiku wa kuamkia jana baada ya kupata ajali, 70 walipata matibabu na kuruhusiwa kurejea chuoni kwao.

Kwa mujibu wa Kaimu Mganga Mkuu huyo, majeruhi 55 wanaendelea kupata matibabu katika hospitali hiyo kwa msaada wa timu maalumu ya waganga na wauguzi waliokusanywa kutoka hospitali na vituo mbalimbali vya afya mkoani Tanga kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.

Mwananchi ilifika katika Hospitali hiyo ya Bombo na kukuta idadi kubwa ya wananchi waliokusanyika katika hospitali hiyo kwa lengo la kutambua miili ya waliokufa na majeruhi.

Mwalimu wa zamu wa Chuo hicho, Ustaadh Ajali Ramadhan, alisema kuwa wanafunzi hao walikuwa wakitokea Kijiji cha Kibafuta ambako walikwenda
kuhudhuria sherehe za kuzaliwa kwa Mtume Mohamad S.A.W.

Hata hivyo, Ustaadhi Ramadhan alisema anashangaa kuona idadi kubwa ya wanafunzi waliopata ajali, kwani aliowaruhusu kutoka chuoni hapo walikuwa 60 tu.

“Nashangaa sijui ni nini kimetokea, kwani niliowaruhusu kuondoka na gari
hilo ni wanachuo 60 tu, lakini idadi ya waliopata ajali imekuwa kubwa. Sijui walipandia wapi…,” alisema mwalimu huyo wa zamu.

Kanyinyi alimshukuru Mkurugenzi wa Kampuni ya Raha Leo, Seleman Abdallah kwa kutoa dawa kwa ajili ya kuwatibu majeruhi wa ajali hiyo.

“Tunashukuru Mkurugenzi wa Raha leo, ametusaidia sana kwa kutoa dawa za
kuwatibu majeruhi na pia vifaa kwa ajili ya kusaidia kuhifadhia miili ya waliokufa,” alisema Kanyinyi.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Mstaafu Said Kalembo alifika hospitalini hapo saa 5 .30 asubuhi na kuwapa pole ndugu wa wanafunzi waliokufa katika ajali hiyo.

Akiwa, akiwa katika wodi ya Galanosi Mkuu wa Mkoa huyo alimuagiza Kaimu Mganga Mkuu kuwaita waganga na wauguzi kutoka vituo vyote vya afya vya jijini hapa ili kuongeza nguvu, kwa vile waliopo katika Hospitali ya Bombo walikuwa wmezidiwa na kazi ya kuwahudumia majeruhi.

Katibu wa Bakwata wa Mkoa wa Tanga, Mohamed Riami alisema huo ni msiba
mkubwa uliwakumba Waislamu na Watanzania kwa ujumla, hivyo akaomba msaada wa hali na mali kuokoa maisha ya majeruhi waliopata ajali hiyo.

Ajali hii ni muendelezo wa ajali mbaya za barabarani zinazoendelea kutokea na kuua watu sehemu mbalimbali nchini hivi sasa.

Moja ya ajali hizo mbaya ni iliyotokea jijini Dar es Salaam mwezi uliopita na kuua watu zaidi ya 10 papo hapo baada ya lori la mafuta ya taa kuigonga na kulalia daladala maneo ya Kibamba katika Barabara ya Morogoro.

Katika ajali hiyo iliyotokea alfajiri, daladala ilisagawa na kuwa kama chapati; na miongoni mwa waliokufa ni mama mjazito aliyekuwa anakwenda kujifungua hospitalini akiwa pamoja na mumewe.

CHANZO: Mwananchi
.

British National Party (BNP),chama cha kibaguzi cha hapa Uingereza,kimetangaza kwamba kitatoa paundi 50,000 kwa kila atakayeafiki kuhama Uingereza.Akiongea katika kipindi cha 'Today' cha kituo cha redio cha BBC4,mwenyekiti wa chama hicho,Nick Griffin (pichani) alisema kuwa mpango huo ni mahsusi kwa Waingereza wasio Weupe (non-White British) na wahamiaji wengine wasio weupe (non-White migrants).

Griffin alieleza kuwa kwa mujibu wa sera ya uhamiaji ya chama chake 'milango ya Uingereza itafungwa' kwa wageni isipokuwa tu kwa wale wenye ujuzi au taaluma maalum."Aidha unazungumzia fundi bomba wa ki-Polish au mkimbizi kutoka Afghanistan,milango ya Uingereza itafungwa kwa sababu nchi hii imejaa",aliongeza kiongozi huyo mbaguzi wa rangi.

Kiongozi huyo wa BNP alitanabaisha kuwa "Idadi ya watakaozuiwa kuingia nchi hii itakuwa yoyote na kutoka popote.Milango itafunguliwa tu pale itapokidhi mahitaji wa Waingereza na Uingereza".Akitolea mfano wa utekelezaji wa sera hiyo,Griffin alisema laiti Uingereza ikiwa na mahitaji ya wataalam wa nyukia basi chama hicho kitaruhusu,kwa mfano,mwanafikizia kutoka Japan.

Alipoulizwa kama sera hiyo itaambatana na kuvunja mikataba ya kimataifa,mbaguzi huyo alijibu: "Kabisa.Mikataba ya kimataifa haikidhi mahitaji ya Uingereza na watu wake.U-kimataifa (internationalism) ni miradi ya tabaka la wanasiasa".

Kuhusu kuwataka wasio weupe kuondoka Uingereza,Griffin alisema:"Tunasema tutatoa posho ya kuhama makazi (resettlement grants) na hili ni suala la hiari .Tunazungumzia takriban pauni 50,000 kwa kwa mtu".Alipoulizwa ni watu wangapi wanaotarajiwa kuhama Uingereza kwa mujibu wa sera hiyo alisema: "180,000 kwa mwaka,kama wataondoka katika nchi hii iliyojaa kupindukia".

Imetafsiriwa kutoka Yahoo! News


Judges are set to rule whether to remove the story of the intrepid explorer's first African adventure after a Congolese man claimed it is racist.

. Bienvenu Mbutu Mondondo wants Tintin in the Congo - the second in the celebrated children's series - to be axed for its ignorant depiction of native Africans.


Creator Hergé defended his book, first published in 1930, in later life and said any stereotypes merely reflected contemporary colonialist views.

The Belgian courts may follow a recent compromise decision in Britain and place a sticker warning of offensive content instead.

That was the result when the UK's Commission for Racial Equality called for the comic to be banned in 2007.

Mr Mondondo has put his case to Belgian and French judges before, but his latest legal challenge faces some scepticism.

Online comic magazine actubd.com accused him of lying about his profession, amid other doubts that he will be unable to pay his own lawyers.

SOURCE: Skynews

28 Apr 2010

China has revoked a ban on people with HIV/AIDS entering the country, softening a decades-old policy that drew sharp criticism this year when an Australian writer was blocked after declaring himself HIV-positive. Until now, China's regulations formally banned foreigners entering the country with "psychiatric illness, leprosy, AIDS, sexually-transmitted diseases, active pulmonary tuberculosis or other infectious diseases."


The State Council, China's cabinet, issued amended rules late Tuesday removing the explicit ban on people who have developed AIDS or are infected with the HIV retrovirus, as well as anyone with leprosy, while leaving authorities leeway to decide which diseases could trigger an entry ban.

The United Nations welcomed the decision as an important step towards ending discrimination against people living with HIV.

"I commend President Hu Jintao for China's decision to remove travel restrictions based on HIV status," U.N. Secretary-General Ban Ki-moon said in a statement.

"Punitive policies and practices only hamper the global AIDS response. I urge all other countries with such restrictions to remove them as a matter of priority and urgency."

Travel restrictions, which are imposed in some form by dozens of countries worldwide, do not prevent transmission of the disease or protect public health, the statement added.

China's new rules, posted on the central government website (www.gov.cn), still block foreigners "with serious psychiatric illness, infectious pulmonary tuberculosis or other infectious diseases that may constitute a major threat to public health."

The amended regulations did not say whether AIDS/HIV would be among the infectious diseases that people seeking Chinese visas must declare when applying, possibly leaving officials some leeway on how to apply the rule.

But an unnamed legal affairs official for the State Council indicated that AIDS/HIV would not be a bar to entry.

"Restricting foreigners with these diseases from entering the country has played an extremely limited role in our country's disease prevention and control work, and instead has repeatedly become an impediment to our hosting a variety of international events," the official told the Legal Daily.

In March, more than 90 Australian authors signed a letter decrying China's refusal to grant a visa to one of the country's most celebrated writers, Robert Dessaix, who is HIV-positive.

Friday, Shanghai opens its World Expo, a multi-billion dollar exhibition that is China's latest effort to promote an image as a forward-looking and open country.

The HIV virus can be spread through unprotected sex, sharing of infected needles and blood, and -- without preventive drugs -- to children in the womb of infected mothers or who take milk from an infected woman.

If untreated, the virus attacks the immune system, leading to full-blown AIDS, a deadly condition.

China has 560,000 to 920,000 people infected with the HIV virus and 97,000 to 112,000 AIDS patients, according to 2009 Ministry of Health and United Nations estimates.

SOURCE: Reuters

.

Matokeo ya utafiti uliofanywa na Mradi wa Utafiti na Elimu na Demokrasia Tanzania (REDET) yanaonyesha kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ni mchapakazi zaidi ya 'bosi' zake,Rais Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Ali Mohammed Shein. Kwa mujibu wa habari zilizochapishwa katika gazeti la Mwananchi,asilimia 61.2 ya wananchi waliohojiwa wameonyesha kuridhishwa na utendaji wa Pinda huku Kikwete akipata asilimia 58.8 na Dkt Shein akiwa na asilimia 46.8Kwa habari kamili soma HAPA.

27 Apr 2010

Tarehe 6 ya mwezi ujao,Waingereza watapiga kura katika Uchaguzi Mkuu.Kura za maoni zinaonyesha kuwa hakuna chama kitakachopata ushindi wa kutosha kuunda serikali peke yake (hung parliament).Vyovyote itakavyokuwa,kuna mambo kadhaa mbayo Watanzania wanaweza kujifunza katika uchaguzi huu hasa kwa vile nasi tutakuwa na uchaguzi hapo Oktoba mwaka huu. 


Kubwa zaidi ni namna wagombea wanavyohangaika kuwabembeleza wapiga kura.Unajua kuna kijitabia cha baadhi ya wanasiasa huko nyumbani ambao sijui ni ulevi wa madaraka au dharau kwa wapiga kura,hawajihangaishi hata kidogo kuwaonyesha wapiga kura kuwa ajira zao zinategemea ridhaa za wapiga kura hao.Pengine ni jeuri ya uwezo wao wa kununua kura katika jina la takrima au kudumisha chama.

Yani hapa ukiangalia kwenye runinga namna Waziri Mkuu wa sasa,Gordon Brown,anavyopelekeshwa na wapiga kura kwa maswali mazito kana kwamba utawala wake ulikuwa mbovu kupindukia,unapata picha kuwa kwa hawa wenzetu GOOD IS NOT ENOUGH,THEY WANT EVEN BETTER (Ubora tu hautoshi,wanataka ubora zaidi).Na si kwamba Brown na Labour yake hawajafanya mambo ya maana kwa Waingereza bali watu hawa hawapendi 'kuangushwa' kwa aina yoyote ile.

Na jingine linalovutia katika kampeni hizi ni namna wapiga kura wanavyozipa manifesto za vyama umuhimu mkubwa na pengine mwelekeo wa nani watampigia kura.Kwetu,manifesto ni sawa na waraka unaokumbukwa wakati wa chaguzi na 'kinga' ya kujitetea pale mambo yanapokwenda mrama.Wengi tunafahamu namna akina Makamba wanavyotumia manifesto ya CCM kujibu shutuma mbalimbali zinazoelekezwa kwa chama hicho tawala.Hilo sio kosa bali tatizo ni kwamba utetezi huo mara nyingi hauendani na hali halisi.Kwa mfano haitoshi kusema manifesto ya CCM inatamka bayana kuhusu 'chuki' yake dhidi ya rushwa huku in practice hadi leo hatufahamu Kagoda ni mdudu gani.Matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno,so Waswahili say.

Manifesto ya CCM kwenye uchaguzi wa mwaka 2005 iliweka bayana dhamira yake ya kupata ufumbuzi wa suala la mahakama ya kadhi lakini hadi leo suala hilo linapigwa danadana.Utafiti wangu wa shahada ya uzamili kuhusu harakati za vikundi vya waislam nchini Tanzania (unaoelekea ukingoni) ambao umegusia kwa undani suala hilo unaashiria kuwa 'kupuuzia' kero (grievances) kama hiyo ya mahakama ya kadhi na suala la OIC yana potential ya kusababisha matatizo huko mbeleni.Tatizo haliwezi kutatuliwa kwa kuliepuka bali kulikabili.We have to solve difficulties before they become problems (tunapaswa kutatua ugumu kabla haujawa tatizo).

Ni matumaini ya wapiga kura wa Tanzania kuwa watatumia haki zao za kidemokrasia kwa busara zaidi kuchagua wagombea wanaoweza kuwatumikia kwa dhati.Zama za ushabiki wa vyama zimepitwa na wakati hasa kwa vile kitakachowakomboa Watanzania kutoka kwenye lindi la umaskini na ufisadi sio ushabiki bali ufanisi wa chama.

26 Apr 2010

Ujumbe kutoka kwa Executive Producer Baraka Baraka (na video ya interview hapo chini)


Kwa mara nyingine tena ningependa kuwatolea Intavyu siku tuliyotembelea rasmi na world service radio katika studio zetu za Urban Pulse hapa Mjini kusoma UK tukiwa na Presenter Fred Ili kujadili Movie ya £ovely Gamble.




Pia aliweza kukutana na baadhi ya wanatimu wa lovely gamble na pia utapata comments za Steve Kanumba mwenyewe jinsi anaitwa siku hizi.


Pia unaweza kuangalia trailer ya movie inayosubiriwa kwa hamu sana Tanzania 28.4.10 club Billcanaz na hapa mji wa kusoma UK 29.5.10


BARAKA BARAKA
EXECUTIVE PRODUCER
BUZZIE PRODUCTION UK.



25 Apr 2010




Kama nilivyoahidi siku chache zilizopita kuwa blogu yako ingekuletea mahojiano mengine exclusive kutoka kwa mmoja wa Watanzania wanaotuwakilisha vema,leo natimiza ahadi hiyo kwa kuwaletea exclusive interview na msanii mahiri wa Bongoflava,anayefahamika kama Mzee wa Commercial.Huyo si mwingine bali ni Ambwene Yesaya,au AY kama anavyofahamika na wengi.Kama ilivyokuwa katika mahojiano ya Mwana FA,interview hii itapatikana pia katika sura ya Kiingereza (English version).Tuaanza kwanza na WASIFU wa AY kabla ya kuingia kwenye mahojiano kamili.Pata vitu:


MSANII TANGU UTOTONI:
AY alianza kijihusisha na fani ya muziki tangu udogoni.Alipokuwa shule ya msingi alishiriki katika mashindano mbalimbali ya kutafuta vipaji na pia alitumbuiza katika hafla mbalimbali.Mwaka 1996 akiwa high school aliunda kundi la S.O.G lililojumisha wasanii watatu (akiwemo AY) na walirekodi albamu yao ya kwanza mwaka 2000.

KUKUA KISANII:
Mwaka mmoja baadaye,AY aliamua kufanya kazi za kisanii peke yake (solo) na kufyatua albamu yake ya kwanza iliyokwenda kwa jina ‘Raha Kamili’.Wimbo wa kwanza kutambulisha albamu hiyo, ‘Raha Tupu’ ulipata mafanikio makubwa na kukamata chati za vituo vya radio na runinga,na hatimaye kumtambulisha rasmi AY katika anga za muziki nchi Tanzania.
‘Machoni Kama Watu’, single ya pili (kutoka katika albamu ya ‘Raha Kamili’) iliyomshirikisha Lady Jaydee ilifanya vizuri sana kwenye chati mbalimbali za muziki na ulisaidia sana kupaisha mauzo ya albamu hiyo katika soko.

KUJIIMARISHA KISANII:
Mwaka 2005,AY alitoa albamu yake ya pili aliyoipa jina ‘Hisia Zangu’, na ‘Yule’, single ya kwanza kutoka katika albamu hiyo, ilikamata chati mbalimbali za muziki.Katika albamu hii,AY aliwashirikisha wasanii mbalimbali maarufu katika Afrika Mashariki ikiwa ni pamoja na Prezzo,Tattuu na Dexu Vultures (wote kutoka Kenya) na msanii Maurice Kirya kutoka Uganda.Hii ilisaidia sana kumtangaza zaidi AY nje ya mipaka ya Tanzania.Single yake ya pili, ‘Binadamu’,ilifanya vizuri sana ukanda mzima wa Afrika Mashariki na hatimaye kuteuliwa kugombea Tuzo za Kora,jambo lililoandika historia kwani AY ni msanii wa kwanza wa kiume kutoka Tanzania kuteuliwa kugombea Tuzo hiyo.

KUJIKITA ZAIDI KATIKA MUZIKI
Umaarufu wa AY ulizidi kuongezeka hasa baada ya kutoa albamu hiyo ya pili,na sasa alitambulika kama mmoja wa wasanii mahiri wa Afrika Mashariki.Mwaka 2006 alifanikiwa kupata mkataba wa kutangaza kinywaji (kikali) cha ‘Konyagi’ ambacho ni maarufu ndani na nje ya Tanzania.Mkataba huo ulichangia AY kutambulika zaidi kupitia matangazo ya kinyaji hicho,na ulifungua njia kwa makampuni mengine,kama Coca Cola,Vodacom,Celtel (sasa Tigo) na Kilimanjaro Lager kuingia mikataba na msanii huyo.

STAILI:
Staili ya muziki wa AY ni hip-hop inayozungumzia ishu na maisha ya Mwafrika hivi sasa.Maudhui hayo yanawasilishwa kwa ucheshi lakini pia yanaburudisha.Muziki wa AY unawagusa watu wa rika lote.

TUZO:
Msanii huyo amefanikiwa kuteuliwa katika/kushinda tuzo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania.Tuzo hizo ni pamoja na
1 Mwaka 2005 aliteuliwa kugombea Tuzo ya Kora katika kundi (category) ya Msanii Bora wa Kiume kwa Afrika Mashariki na Kati.Wimbo ulioteuliwa ni ‘Binadamu’.
2 Mwaka 2006 aliteuliwa kugombea Tuzo za Kisima (nchini Kenya) katika kundi la Msanii Bora wa Kiume kutoka Tanzania.
3 Mwaka 2007 aliteuliza kugombea Tuzo za Kilimanjaro (Kilimanjaro Music Awards) katika kundi la single bora ya hip-hop.
4 Mwaka huohuo aliteuliwa tena kugombea Tuzo za Kisima (nchini Kenya) katika kundi la video bora ya hip-hop kutoka Tanzania.
5 Mwaka 2007 uliendelea kuwa wa mafanikio kwa AY baada ya kuteuliwa pia kugombea Tuzo za Lulu ya Afrika (Pearl of Afrika) katika kundi la single bora ya hip-hop kutoka Tanzania.
6 Mwaka 2008 AY aliteuliwa kugombea Tuzo za Kilimanjaro katika kundi la collaboration (ushirikiano wa msanii zaidi ya mmoja) bora.
7 Mwaka huohuo,msanii huyo aliteuliwa tena kugombea Tuzo za Lulu ya Afrika katika kundi la msanii bora wa kiume kutoka Tanzania.
8 Katika mwaka huo,Akon-msanii maarufu duniani kutoka Marekani,alikiri hadharani kuwa anavutiwa na staili ya muziki wa AY na akamtabiria kuwa anaweza kabisa kuwa msanii kutoka Afrika atakayefanya vizuri katika anga za muziki kimataifa.
9 Mwaka huu,AY ameteuliwa kugombea tuzo kadhaa ikiwa ni pamoja na Tuzo za Muziki za Kilimanjaro (kundi la video bora na wimbo bora wa mahadhi ya Reggae),Tuzo za Teen Extra za nchini Kenya (kundi la video bora,msanii bora wa mwaka,collaboration bora ya Afrika,wimbo bora wa mwaka Afrika Mashariki,wimbo bora wa hip-hop, na msanii bora wa kiume).
10 Na hivi karibuni AY alishinda kuwa msanii bora wa Afrika Mashariki katika Tuzo za Teenez nchini Kenya.

MAFANIKIO:
Hadi sasa msanii huyo ameshajikusanyia Tuzo sita.Pia vibao vyake 14 vimefanikiwa kukamata chati mara katika ukanda wa Afrika Mashariki.Kibao chake kinachonyanyasa zaidi ni King and Queens (Wafalme na Malkia),na kimepelekea kumpatia tuzo na umaarufu zaidi kimataifa.Wakati mahojiano haya yanafanyika,wimbo wake ‘Habari Ndio Hiyo’ ulikuwa unakamata nafasi ya 10 katika chati za muziki kwa Afrika (Radio Express-Africa Chart).AY amefanikiwa kuwa msanii pekee wa Kitanzania aliyefanya collaboration nyingi zaidi na wasanii wa nje ya Tanzania ikiwa ni pamoja na Chameleone na Ngoni (Uganda),Amani,Nameless na Juacali (Kenya), P Square na J. Martini (Nigeria) na wengineo.

Uzinduzi wa albamu za AY umekuwa wa kihistoria na wenye mafanikio makubwa chini ya udhamini wa Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) na ulifanyika wakati wa matamasha ya wasanii wa kimataifa kama vile Fat Joe,Eve,Shaggy,nk nchini Tanzania.Kadhalika msanii huyo alikuwa miongoni mwa wasanii walioshiriki tamasha kubwa la kuhamasisha vita dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi (Music Against HIV/AIDS) liliodhaminiwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).Pia ameshiriki Coke Side of Life Tour kwa Afrika Mashariki,Tamasha la Vijana la Afro Arab nchini Uganda,Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar (Zanzibar International Film Festival),na Tamasha la Sauti za Busara.Kadhalika,AY amewahi kualikwa kutumbuiza wakimbiki kutoka Burundi na Rwanda kwa udhamini wa Shirika la Kimataifa la Wakimbizi (UNHCR),alitumbuiza katika sherehe za kuukaribisha mwenge wa Olimpiki nchini Tanzania,na mwaka jana alialikwa kutumbuiza katika Tuzo za Muziki za MTV barani Afrika nchini Kenya.Vilevile,msanii huyo ameshatumbuiza katika nchi mbalimbali duniani ikiwa ni pamoja na eneo la Afrika Mashariki,Rwanda,Burundi,Dubai,Afrika Kusini,Marekani na Uingereza.

NINI KIPYA?
Hivi karibuni AY amezindua tovuti yake inayopatikana katika anuani www.ay.co.tz. Pia single yake ya ‘Binadamu’ itakuwa miongoni mwa nyimbo katika albamu inayoandaliwa na kampuni ya kimaifa ya muziki,Warner Music (Africa).Kadhalika,msanii huyo ameingia mkataba wa kutangaza kinywaji (kikali) cha Waragi nchini Uganda sambamba na mkataba na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.Kwa sasa anandaa ushirikiano na wasanii wa kimataifa kama J. Martin wa Nigeria na wengineo kutoka Afrika Kusini na Marekani.


JE WAJUA?
Kwamba jina halisi la AY ni Ambwene Yesaya?
Staili ya AY ni ‘simple and casual’?
AY alizaliwa Julai 5 na nyota yake ni Kansa?
Rangi aipendayo zaidi ni bluu?
Scent (harufu ya perfume au manukato) aipendayo ni DKNY?

Na msanii anayemvutia zaidi duniani ni Dr Dre?.

MAHOJIANO KAMILI YANAFUATA (BONYEZA) HAPA CHINI .

KULIKONI UGHAIBUNI (K.U): Kwanza blogu hii inatoa shukrani kwa kukubali ombi la kufanya mahojiano haya maalum. Pili, hongera sana kwa kuteuliwa na hatimaye kushinda Tuzo za Teneez Kenya 2010.Wasomaji wangependa kufahamu kwanini unajulikana kama Mzee wa Commercial




A.Y: Producer P.Funk ndio alianza kuniita hiyo baada kuwa kila nikienda Bongo Records alikuwa anaweka beats za aina tofauti na tukawa tunaflow na artists wengine so akaona kila beat naenda nayo na wengine walikuwa wanashindwa katika beats nyingine so akawa ananiita mzee wa commercial ila kwa sasa nimekuwa wa commercial ya muziki wa biashara na biashara kwa ujumla.

K.U: Laiti AY asingekuwa Mzee wa Commercial (yani usingekuwa msanii) unadhani leo angekuwa nani (katika fani gani)?
A.Y: nilikuwa na ndoto sana ya kusomea urubani na naamini ningeendelea nadhani ndoto yangu ingetimia coz nikiamua kufanya kitu naakikisha nimekifanikisha

K.U:Kitu gani kilichokusukuma kuingia kwenye fani ya muziki?
A.Y: kutokana na kusikiliza nyimbo za wasanii wengine wa nje na kuona mbona naweza kujitahidi nikafanya kama wao.

K.U: Kabla hatujagusia mafanikio yako kisanii ,nini hasa kimekuwezesha kubaki kwenye chati kwa kipindi kirefu kiasi hiki?
A.Y: bidii,nidhamu na malengo katika kazi,naipenda kazi yangu na najifunza kila siku na kukubali kuwa kila kitu kinaweza kubadilika

K.U: Tuje kwenye mafanikio yako kisanii.Licha ya kuweka historia kwa kuwa Mtanzania wa kwanza wa kiume kuteuliwa kugombea tuzo za Kora na baadaye tuzo za Kisima,kuna mafanikio gani mengine unayoyahusisha na fani ya muziki?
A.Y:Ni mengi. (Zaidi angalia wasifu hapo juu)

K.U: Miongoni mwa vilio vya wanamuziki wa Tanzania ni suala la ‘wadosi’.Kama msanii mwenye mafanikio makubwa umewezaje kupambana na suala hilo?
A.Y: hili nimeliongelea sana na sasa sihusiki nao kwa sasa naweza kusema ni tatizo sugu na linaweza kumalizika au kupungua ila naona wengi wenzangu wanaendelea kufanya biashara isiyo kuwa transparent

K.U: Nilidokezwa na Mwana FA kuhusu kampuni yako inayoshughulikia usimamizi na usambazaji wa muziki ijulikanayo kama Unity Entertainment.Wasomaji wangependa kufahamu japo kwa ufupi kuhusu wazo,maendeleo na ufanisi wa mradi huu.





A.Y:(angalia wasifu hapo juu) mpaka sasa kampuni yangu imekuwa na ni wakala wa wasanii wengi ukanda huu wa afrika mashariki kama mwana fa,shaa,nameless,j.martins wa nigeria ambae nimemleta kwenye new campaign ya zain,p.square,amani,chidi benz na wengine wengi wa afrika
K.U:Tuje kwenye ushiriki wako na hatimaye kujitoa kwenye kundi la East Coast Team.Sababu zipi zilipelekea wewe kujiengua?
A.Y: kutofautiana misimamo na malengo 

K.U: Wakati ukiwa na kundi la East Coast kulikuwa na beef na wasanii wa Temeke.Je unadhani beefs zinasaidia au kudumaza maendeleo ya wasanii? (nauliza hivyo kwa sababu wakati mwingine baada ya kufifia kwa beef -kama hiyo yenu-baadhi ya wasanii nao wanafifia)
A.Y: zipo zinazojenga na zipo zinazobomoa

K.U: Je makundi (kama ilivyokuwa East Coast) yanaficha udhaifu wa wasanii dhaifu na kudumaza umahiri wa wasanii bora?(nauliza hivi kwa vile baadhi ya wana-East Coast ‘walipotea’ muda mfupi baada ya wewe na Mwana FA kujitenga):
A.Y: ni kweli kabisa,makundi mengi yakivunjika ndio mnapata ukweli kuwa nani anaweza na nani hawezi kujimanage

K.U: Unatambulika kama mwakilishi bora kabisa wa Tanzania kwenye tuzo mbalimbali za kimataifa (Kora,Kisima na sasa hii ya hivi karibuni ya Teneez 2010 huko Kenya ambapo umeibuka mshindi).Wasomaji wangependa kufahamu nini siri ya mafanikio yako?
A.Y: ni kama nilivyokwambia ni bidii na nidhamu na malengo bila hivyo huwezi kwenda mbali.na si hizo tu pia nimekuwa nominated kwa mtv awards 2009 (best hip hop artist nikiwa na jay z,kanye west na m.i)kili awards (2 categories),extra teneez awards (1category) na tuzo za Ghana zinaitwa moma (5categories-artist of the year- Africa,best male,collaboration,east African song,hip hop artist) nawaomba watanzania waweze kuvote online na kwa simu kwa walio Tanzania niweze kunyakua tuzo hizo,unaweza kugogle then upate informations

K.U: Kumekuwepo malalamiko kutoka kwa baadhi ya wasanii kuhusu baadhi ya tuzo za hapo nyumbani hususan suala la upendeleo na mapungufu katika upangaji makundi (categories).Nini mawazo yako katika suala hili?
A.Y:zingine naweza kusema kweli na kuna wakati wasanii wanatakiwa kukubali matokeo maana ukikubaki kuingia katika mashinda jua kuna kushinda na kushindwa

K.U: Ukiwa kama msanii uliyedumu kwenye fani kwa muda mrefu,unaonaje maendeleo ya bongoflava ndani na nje ya Tanzania?
A.Y: inazidi kwenda mbele na kwa sasa wanaoipeleka mbele si wengi so nawaomba wenzangu tuongeze bidii na kutengeneza network zaidi ndani na nje ya nchi

K.U: Baadhi ya kazi zako zimetengenezwa na producers wa nje ya Tanzania.Je kuna tofauti yoyote kati ya kazi zako zinazotengenezwa na producers wa nyumbani na hizo zinazotengenezwa nje?
A.Y: ni ladha hazifanani,napenda sana kuchange plava mara kwa mara kwa audio na hata video






K.U: Swali linaloshabihiana na hilo lililopita.Je kufanya kazi na producers wa nje kunaweza kumsaidia msanii kufanya vyema katika nchi anayotoka producer huyo?
A.Y: sana tu mfano mzuri ni mimi mwenyewe na producer naofanya nao na nafurahi kuona wasanii wengine wa tz wameanza kufuata nyao zangu kwa kuanza kusafiri kurecord sehemu mbali mbali na kushirikiana na wasanii wa nje maana soko limeanza kuwa la afrika na si vile zamani kuwa la kibongo tu,angalia hata charts za redio records nyingi za nje na ndani zinaingia kwa pamoja

K.U: Umewahi kushiriki kwenye fani ya filamu (ambapo ulihusika kwenye filamu ya Girlfriend).Je una mpango wa kuendelea na fani hiyo huko katika siku za usoni?
A.Y:bado sijafikiria kwa kweli kama nitafanya movie 
K.U:Vipi kuhusu umodo hasa ushiriki wako kwenye matangazo mbalimbali ya biashara.Je una mpango wa kuwa full-time model licha ya muziki?
A.Y:hapana ila muda wote huwa wananunua image au sauti yangu kwa ajili ya products zao au campaign zao.

K.U: Unawezaje kumudu majukumu yote hayo (muziki, umodo, biashara) pasipo kuathiri ufanisi wako?
A.Y:na masomo pia,nasomea business administration ktk chuo cha Learn IT,mi ni mtu wajukumu tangu zamani sana so najua kuhandle pressure zote na huwa naishi kwa ratiba maalumu ambazo naziweka kwa simu na calendar yangu.

K.U: Umefanikiwa sana kuteka soko la bongoflava katika eneo la Afrika Mashariki.Nini mipango yako ya baadaye kutanua mafanikio hayo maeneo mengine ya Afrika na nje ya bara hilo?
A.Y:Nimeanza kupata bookings za S.A,DJIBOUTI,NIGERIA na ZAMBIA na pia Ethiopia so nazidi kusogea zaidi.pia natoa wimbo wangu mpya niliomshirikisha J.MARTINS kutoka Nigeria so najua itanijenga zaidi.

K.U:Kwa uzoefu wako,na kwa kuzingatia mafanikio unayopata nje ya mipaka ya Tanzania,unadhani ni jambo gani linalopelekea wasanii wengine wengi wa hapo nyumbani kushindwa kufanya vizuri kwenye anga za kimataifa?
A.Y: wengi ni wagumu kujifunza,kufanya networking.maana vile wengine wengi wa nje ya tz wanavyojituma ndio maana natumia style wazotumia wao.

K.U: Moja ya mambo yanayoisumbua Tanzania kwa sasa ni ufisadi lakini wasanii wengi wa bongoflava wamekuwa wakikwepa kuzungumzia suala hili kwenye tungo zao.Je ni sahihi kuyumkinisha kuwa mnaistarehesha jamii kwa vibao vyenu ‘vikali’ lakini mnawatenga kwa kutolipa kipaumbele suala la ufisadi kwenye tungo zenu?
A.Y: sidhani kama ukiimba ufisadi utaisha, nilichongundua ni kuwa watu hawaipendi nchi yetu ndio maana tunawafumbia macho wanaofanya ufisadi na tuna ile hulka ya kulalamika tu then hakuna hatua tunazochukua ndio maana ktuna matatizo mengi sugu tunayalalamikia tu halafu tunanyamaza

K.U: Nini mipango yako ya baadaye katika fani ya sanaa?
A.Y:kuna surprise kubwa nitawatangazia muda si mrefu naakika nitasogea/tutasogea kisanaa

K.U: Mwisho,una ujumbe gani kwa mashabiki wako na wapenzi wa bongoflava kwa ujumla?
A.Y: tuthamini na kuvipenda vya kwetu kwanza kabla ya vya wengine cz hata wao mnaona jinsiwanavyosupport vya kwao kwanza hata kama ni vibaya ila ni vyao na wanavipush sana mpaka wengine wanavikubali..





Blogu hii inakushukuru sana kwa kutumia muda wako kujibu maswali haya mengi.Pia inakutakia kila la heri na mafanikio katika shughuli zako.Na ni matarajio ya blogu na wasomaji wake kuwa tutapata fursa nyingine ya kuongea huko mbeleni.Asante sana.


ANGALIZO KUTOKA KWA AY: Nyimbo zangu na video zangu zitaanza kupatikana very soon online kupitia moja ya kampuni kubwa duniani,pia May hii nafungua duka la nguo mchanganyiko lipo sinza madukani.karibuni sana na kwa mawasiliano tutaweza kuwasiliana katika email yangu ya [email protected]. Na hapa chini ni wasifu wa kampuni ya Unity Entertainment
Unity Entertainment Profile 2010

24 Apr 2010

Waungwana,ni MwanaFA hapa..i dont usually do this kwenye blogs na sites (ku'post maoni) but naona nichangie this time since naona concerns zimekuwa za kistaarabu hapa na zina lengo la kujua tu na si vinginevyo...

Yes,nimefanya masters degree ya finance,Coventry University,ilianza January 2009 na ikamalizika January 2010,natakiwa kufanya mahafali aidha July ama November(kwa jinsi ntakavyoamua)...

Sichukui maoni yeyote kati ya haya vibaya,na pengine yanamaanisha kitu nilichofanya sio kidogo mpaka kufika mahali waungwana wanashindwa kuamini nimeweza kukifanya...

NB: na yes,nikijaliwa uhai na uwezo wa kuhudhuria mahafali ntawaletea picha...

Wasalaam...nawasilisha!!

KULIKONI UGHAIBUNI: Asante Mwana FA kwa  hope ufafanuzi huu.

This day last year,at 1400,I received my miracle from the Lord.Two months earlier,I was introduced to a Houston,TX-based powerful woman of God,Apostle Esther.She taught me that when praying,I should ask the Lord for receiving,rather than seek for, my miracle because it was already there.She also gave recommended the ever powerful Psalm 91 to read every day for a number of days.And guess what,as she assured me,I eventually got something that has people waiting for up to a decade to get it, if they at all are successful.God is really Great,and this particular miracle is a living example.I would also like to thank Christha, the woman whose love and care comes only second  to my mother's,for introducing me to the Apostle,and for her tirelessly efforts in praying with me.Praise the Lord,Ameen.For Christa,I dedicate the following video (though I know you don't fancy secular music).

23 Apr 2010

Majuzi Rais Jakaya Kikwete alimteua Doug Pitt,mdogo wa staa wa filamu Brad Pitt,kuwa balozi wa heshima (goodwill ambassador) kusaidia kuitangaza Tanzania hususan kwenye sekta ya utalii.Kwa kuzingatia wasifu wa Doug,na umuhimu wa kuitangaza nchi yetu,uteuzi huo unastahili pongezi za kutosha.Hat hivyo,ili Doug awe na umuhimu kwa Tanzania,au uteuzi wake uzae matunda yanayotarajiwa,kuna mambo kadhaa tunayopaswa kuyaangalia kwa makini 
Kwa hakika hatuna kisingizio cha kwanini nchi yetu inahitaji nguvu za ziada (kama akina Doug) katika kujitangaza.Tuna kila aina ya utajiri na vivutio ambavyo laiti tungejibidiisha kuvitangaza kwa bidii basi huenda tungekuwa mbali sana kimaendeleo.Kwa mtizamo wangu,kikwazo kikubwa ni uhaba wa uzalendo.Baadhi ya wateule wanaopaswa kuwajibika ipasavyo kulitangaza taifa letu na raslimali zake wako bize zaidi kuangalia maslahi yao binafsi badala ya kufanya kile wanacholipwa mshahara kukifanya.

Lakini kama unadhani hilo ni tatizo dogo basi kuna suala la mazingira yanayopaswa kuboreshwa ili jitihada za Doug ziweze kuwa na maana au zilete ufanisi unaotarajiwa.Kwa mfano,Doug anaweza kuhamasisha watalii waje kwa wingi Tanzania,lakini kwa ufisadi unaoendelea kila kukicha katika sekta ya umeme,ni dhahiri kuwa watalii watakaoitikia wito wa Doug wanaweza kuhisi 'wameingizwa mkenge' baada ya kukutana na adha za mgao wa umeme ambao unazidi kuzoeleka kwa Watanzania wengi.Danadana zinaendelea kuhusu kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo sugu la umeme.Na kikwazo kikubwa katika kupatikana ufumbuzi huo ni wahusika kutanguliza maslahi yao binafsi badala ya yale ya taifa.Ni katika mazingira hayo ndipo matapeli wa Richmond na Dowans walifanikiwa kutufisadi.

Kwa Watanzania walio nje watakubaliana nami kwamba kwa hawa wenzetu,'holidays' ni suala lenye umuhimu wa kipekee katika kalenda na ratiba zao.Ni matarajio ya wengi kwamba holidays walizozihangaikia kwa muda mrefu zitaacha kumbukumbu nzuri maishani mwao,na sio kugeuka 'holidays from hell'.

Kuna tatizo jingine katika suala la udokozi.Pale Mwalimu Nyerere International Airport panahitaji tahadhari kubwa ili mizigo ya msafiri itoke eneo hilo salama.Sasa kama kweli tunataka jitihada za akina Doug ziwe na maana ni vema tukafahamu kuwa pasipo kudhibiti wahuni hawa wa airport ambao inaonekana dhamira yao kuu ni kutoa 'karibu Tanzania ya majonzi' tutaishia kukimbiza watalii badala ya kuwafanya wawashiwishi ndugu na jamaa zao nao waende Tanzania kutalii.Wadokozi wengine mahiri wako Posta.Kwa vile mawasiliano yetu bado si ya kisasa sana,umuhimu wa Posta unabaki kuwa mkubwa,na si ajabu kwa baadhi ya potential watalii kutumia huduma hiyo kabla ya kwenda Tanzania,au wakati wakiwa hapo.Sasa it seems as if baadhi (au pengine most) ya watumishi wa Posta wana 'allergy' na kitu chochote chenye address ya ng'ambo.Ni lazima wafungue na wakikuta chochote 'wanakitaifisha'.

Tuna matatizo ya miundombinu.Tumeruhusu wahuni wa TRL wafanye usanii wao pasipo kuleta mabadiliko yoyote ya muhimu zaidi ya kuandika historia ya kuwa wawekezaji wa kwanza kusaidiwa na serikali kulipa mishahara ya wafanyakazi wao.Ni dhahiri kuwa laiti waliosaini mkataba wa wababaishaji hao angekuwa mzalendo wa dhati angetambua kuwa wangekuja kuikongoroa zaidi Reli ya Kati kuliko walikvyoikuta.Je watalii wakitaka kutumia usafiri wa treni kutalii inakuwaje?Huko TAZARA nako hadithi ni ileile.Na hii ni njia muhimu kwa mtalii anayetaka 'kuifaidi' hifadhi ya Selous.

Kuna tatizo la barabara zetu.Na hapa kuna suala la barabara za msimu ambazo kupitika kwake kunatarajia msimu wa mwaka.Nyingi ya barabara hizi hufanyiwa ukarabari pale tu panapokuwa na ujio wa kiongozi.Uelekeo wa kule kwetu Ifakara tuna hifadhi ya msitu asilia,lakini kufikika kwake ni mbinde msimu wa masika.

Kwa kifupi,nachojaribu kupigia mstari hapa ni umuhimu wa kuboresha mazingira yatakayopelekea watalii kuhitimisha kuwa hawakufanya makosa kukubali ushauri wa Doug kuitembelea Tanzania.Pasipo mazingira bora basi tunaweza kuteua mabalozi Hollywood nzima lakini itakuwa kazi bure.

Na jingine la muhimu zaidi ni manufaa ya ujio wa watalii kwa Watanzania.Sote tunashuhudia jitihada za kuvutia wawekezaji na mwitikio wao lakini pia sote twafahamu namna uwekezaji ulivyoshindwa kuwa na manufaa kwa Watanzania walio wengi.Makampuni ya madini yanazidi kumaliza raslimali zetu huku sie wenye utajiri huo tukibaki na mashimo matupu.Sasa Doug anaweza kulivalia njuga suala la kuhamasisha watalii,nao wakaitikia wito lakini kitakachopatikana kikaishia kwenye ununuzi wa ma-vogue,ujenzi wa mahekalu au kuongeza idadi ya nyumba ndogo za mafisadi.

Ndio maana basi,pamoja na kupongeza uteuzi wa Doug Pitt kuwa balozi wa hisani wa Tanzania huko Marekani,ni muhimu kuwekeza zaidi katika uzalendo utakaopelekea kuzalisha akina Doug wa ndani (na hakutokuwa na gharama ya kuwafuata ng'ambo) na, cha muhimu zaidi,kuchangia maendeleo ya taifa letu 'changa'.

22 Apr 2010

Dressed to kill.Our sisters looking good.Picture courtesy of Miss Jestina's Blog.(1st left ).

'SOS' Appeal!

Yea,I normally blog about politics and such stuffs,but,well,there's no harm in touching some other  issues that make the world go around.I'm talking about fashion.If you happen to visit as many blogs each day as I do you certainly would appreciate that our sisters are doing quite an excellent job in blogging about different stuffs in our lives,especially fashion.However,unfortunately,most of them tend to 'forget' including men's fashion trends in their blogs.They justifiably could 'defend' themselves by arguing that it's not up to them to make sure that we look as good as they normally do.But,honestly,when you have the likes of me whose taste for fashion is as good as a blind man in a dark alley,that spells trouble,and calls for an urgent need for help.Arguably,I'm not an exceptional case as there's probably a whole bunch of guys out there who seriously need help.So,come on sisters,we all know that if what a man dresses pleases you it certainly would please the rest of the world.Could you kindly please think of us,at least once a month, when you keep your audience posted about latest fashion trends?

21 Apr 2010







Picha zote hapo juu zinaonyesha maadhimisho ya 'Siku Ya Bangi Kitaifa' (National Weed Day) almraaduf '4/20' (April 20) nchini Marekani.ANGALIA HAPA kwa habari kamili na picha zaidi

20 Apr 2010

Hapa chini kuna habari ambayo kama ni ya kweli basi hatma ya nchi yetu iko mashakani.Lakini kabla hujaisoma,angalia picha ifuatayo na inaweza kukusaidia kukupa uelewa wa namna tulivyofika tulipo.






KUMBE Rais Jakaya Kikwete hakusoma sheria aliyosaini kwa mbwembe. Sasa baada ya kugundua kasoro zake anataka ikarabatiwe kwa njia ya kanuni, MwanaHALISI limeelezwa.

Hilo liligundulika katika mkutano wa wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wenyeviti na makatibu wa wilaya uliomalizika wiki iliyopita mjini Dar es Salaam.

Taarifa za ndani zinasema, bila aibu na hasa kwa ujasiri wa kiongozi mkuu wa nchi, Rais Kikwete alimuuliza Philip Marmo, waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, maana ya baadhi ya vifungu katika sheria hiyo.

Lakini katika hali ambayo haikutegemewa, Marmo alijibu kana kwamba anamkejeli rais, jambo ambalo lilistua wajumbe wa kikao hicho cha juu cha utekelezaji wa sera za chama.

MwanaHALISI limeelezwa kwamba Rais Kikwete alistushwa na kifungu cha sheria kinachotaka mgombea kuwasilisha katika ofisi za msajili, taarifa ya fedha atakazotumia.

Kifungu hicho kinatoa siku saba kabla ya siku ya mwisho ya NEC kutangaza majina ya wagombea.

Kifungu kingine kinachodaiwa kumstua kinahusu idadi ya wajumbe wa kampeni. Kwa CCM, yenye hata vikundi vya ngoma na nyimbo kama ToT, kuweka timu ndogo kunaweza kupunguza shamrashamra na kuathiri kampeni.

Kwa mujibu wa mtoa taarifa, ilikuwa baada ya rais kupitia maeneo hayo, alimuuliza Waziri Marmo iwapo kile alichokuwa akifafanua kimetokana na sheria iliyopitishwa.

Naye Marmo, akiongea kwa sauti ya unyenyekevu alijibu, “…hiki ndicho ulichosaini.”

Kwa kauli ya Marmo, Rais Kikwete alionekana kustuka na kusema, kama hali ni hivyo, basi sheria itakuwa imeingilia hata mchakato wa wagombea ndani ya vyama, kimeeleza chanzo chetu.

Taarifa zinamnukuu rais akihoji kwa nini “sheria imekwenda mbali mno” na kuagiza papohapo kuwa wahusika waangalie ambapo sheria inaingiliana na watengeneze kanuni zitakazoleta nafuu.

Rais amenukuliwa akimwagiza Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutengeneza “kanuni vizuri” ili kuondoa mwingiliano unaoleta ugumu wa utekelezaji.

Hoja ya maelekezo ya sheria mpya ya gharama za uchaguzi ilikuwa moja ya ajenda za kikao cha NEC, wenyeviti na makatibu wa CCM wilaya kutoka kote nchini.

Tarehe 17 Machi mwaka huu, Rais Kikwete alisaini hadharani na kwa mbwembwe Sheria ya Gharama za Uchaguzi, ikulu Dar es Salaam ambapo hafla hiyo ilihudhuriwa na majaji, wabunge, viongozi wa serikali na vyama vya siasa, mabalozi na waandishi wa habari.

Hata hivyo, sheria hii imekuwa ikilalamikiwa na vyama vya siasa na wanaharakati, kabla na baada ya kusainiwa kuwa itakuwa ya udhibiti kwa wenye msimamo tofauti na watawala.

Aidha, siku tatu baada ya sheria hiyo kusainiwa, mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa alitupa kombora kwa kusema sheria aliyosaini rais ilikuwa na vipengele ambavyo havikujadiliwa bungeni na kwamba “viliingizwa kinyemela.”

Ubishi wa Mwanasheria Mkuu wa serikali, Jaji Frederick Werema kwamba hakukuwa na chochote kilichofanywa kinyemela ndio umekuza hoja ya Dk. Slaa na kufanya achimbue zaidi kshfa hiyo.

Katika kufukua, Dk. Slaa amekwenda hadi kwenye kumbukumbu za bunge (Hansard) na kuthibititisha kuwa Kifungu 7 (3) ambacho kimo katika sheria aliyosaini rais hakikujadiliwa bungeni na hivyo hakikurekodiwa katika hansard.

Mtunga sheria huyo kutoka Karatu amesema pia kuwa chochote kilichojadiliwa bila kuamuliwa na bunge kilikuwa kinatarajiwa tu katika kanuni au fafanuzi za au ainisho za maneno na taratibu lakini siyo katika vifungu vya sheria.

Katika majibu yake kwa kauli za Dk. Slaa, Jaji Werema alitetea serikali na kuthibitisha kuwa kifungu hicho kiliwekwa na waziri Marmo.

Dk. Slaa amesema katika andishi maalum, “Hakuna mwenye mamlaka, hata rais hana mamlaka hayo, sembuse waziri.

“Baada ya mjadala katika Kamti ya Bunge zima, maneno yakikubaliwa ndiyo hayo yanaingia kwenye sheria na serikali haina mamlaka ya kwenda kuyarekebisha inavyotaka. Ndiyo maana ya kusema ‘kifungu kimepitishwa,’ ” ameeleza Dk. Slaa.

Akiweka msisitizo, Dk. Slaa anasema, “Kitendo cha kuchomeka kinyemela ni kitendo kibaya sana na kinapaswa kulaaniwa, kwa sababu, kwa utaratibu huu wataalam wanaweza kuipeleka nchi pabaya kwa kupenyeza jambo lolote wanalotaka wao hata kama halijajadiliwa au limekataliwa na Bunge.”

Dk. Slaa anafafanua hatua ya serikali ya kuingiza mambo kinmyemela katika sheria kuwa ni kosa la jinai na kusema hata kifingu walichochomeka kinyemela kina madhara makubwa.

Kifungu kilichoongezwa na serikali kinataka timu ya kampeni kukaguliwa na watendaji wa serikali ya CCM.

“Kampeni ndiyo inayobeba mikakati na siri yote ya uchaguzi. Haiingii akilini kabisa kuwa serikali (pengine unayotaka kuiondoa kwenye uchaguzi ambayo ndio haki ya msingi ya kila mgombea) ndiyo inaweka mkono wake kwenye udhibiti wa mikakti hiyo,” anafafanua Dk. Slaa.

Anasema kuweka kifungu kama hicho ni “wenda wazimu, kwa mtu yeyote aliyefikiria jambo hilo, au anaandika tu kutoka mezani na au hajui maana halisi na majukumu yake.”

Kutokana na kuibuka kwa kashfa hii, serikali sasa imeamua sheria hiyo irejeshwe bungeni ili kufanyiwa marekebisho yanayostahili.

Naye Dk. Slaa tayari ametoa pendekezo: “Namna pekee ya kuepukana na athari hiyo ni kwa serikali kukiri imefanya makosa, na ndio ustaarabu bila kutafuta visingizio.”

Anasema serikali iwasilishe kwenye Mkutano wa 19 wa Bunge hili ulioanza jana, kitu kinachoitwa “Miscellaneous Amendment” – marekebisho ya sheria mbalimbali – na au ikichelewa sana katika Bunge la Bajeti.

Wachunguzi wa mambo wanasema Rais Kikwete atakuwa amesikitishwa sana na hatua ya wasaidizi wake ya “kumchomekea” vitu ambavyo baadaye vinamomonyoa hadhi yake kama mkuu wa nchi.

Miongoni mwa wanaotajwa kuwa wamempotosha au wameshindwa kumsaidia rais, ni pamoja na Jaji Werema ambaye ametetea uingizaji kinyemela kipengele ambacho hakikujadiliwa bungeni.

Mwingine anayetajwa ni waziri Marmo ambaye ambaye nduye hasa ametajwa kubuni na kuingiza maneno ya kifungu kinacholaaniwa.

CHANZO: Mwanahalisi.



19 Apr 2010

Ni dhahiri unapokutana na kitangulizi 'http://...' unafikiri kuwa kinachofuata ni anuani ya tovuti flani.Lakini je 'http://' (kifupisho cha Hypertext Transfer Protocal)bado ina umuhimu katika mazingira ya sasa ambapo unaweza kuitambua anuani ya tovuti hata bila kitangulizi hicho? . 
Wanateknolojia wa Google Chrome hawadhani kama kitangulizi hicho bado ni muhimu na wameamua kukificha katika toleo jipya la browser hiyo.

Hata hivyo,ufumbuzi huo sio rahisi kama inavyoonekana kwani unaweza kuficha kitangulizi hicho unapoandika anuani ya tovuti lakini bado kipo.Pia inatarajiwa kuwa maendeleo hayo yanaweza kuzua mkanganyiko kwa baadhi ya watumiaji wa intaneti.

Makala hii imetafsiriwa (katika tafsiri isiyo rasmi) kutoka mtandao wa Mashable

Kuna busara moja inayotuasa kuwa mpuuzi husema kwa vile anajiskia kusema (hata kama ni upuuzi) ilhali mwenye busara husema tu pale anapokuwa na kitu cha kusema (ikimaanisha kama hana cha kusema,au haoni umuhimu wa kusema kitu,atakaa kimya. Busara zaidi zinatuasa kuwa makini na tunayosema hadharani kwa vile mara nyingi jamii humtambua zaidi mtu kwa kauli zake.Sema upuuzi,utaonekana mpuuzi.Sema ya busara,utaonekana mwenye busara.Sasa kuna huyu msomi,Dokta Benson Bana,ambaye licha ya kuwa mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam,ni mkuu wa idara ya Sayansi za Siasa na Uongozi na pia ni Mwenyekiti Mwenza wa REDET.Yayumkinika kusema Dkt Bana amekuwa mahiri zaidi wa kutoa kauli zisizoendana na wasifu wake kitaaluma kuliko umahiri wa wa usomi wake

Na leo,kwa mujibu wa habari katika gazeti la Mwananchi,msomi huyo 'amelipuka' tena kwa kauli kwamba tuhuma zilizokithiri dhidi ya ufisadi zinaweza kusababisha taifa kukosa viongozi wazuri wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba.Huhitaji kuwa na hata asilimia moja ya kiwango cha elimu ya Dkt Bana kutambua kuwa tuhuma zilizotapakaa kuhusu ufisadi ni matokeo ya kuwepo kwa ufisadi.Msomi huyu anaishi Tanzania lakini yaelekea hafahamu mazingira yanayomzunguka,na hilo linaleta wasiwasi mkubwa kuhusu mchango wa wanataaluma katika maendeleo ya nchi yetu.

Katika habari hiyo Dk Bana aliwataka watu "waaache siasa chafu za kuhubiri na kudai kuwa watuhumiwa wa ufisadi hawafai kupewa kura au kuchaguliwa katika nafasi mbalimbali za uongozi kana kwamba wameshathibitika".Huu ni zaidi ya ubabaishaji wa kitaaluma,na kwa kiasi flani inaaibisha Udaktari wa Filosofia tunaohenyea akina sie.Kwanza,Dkt Bana amepata wapi mamlaka ya kuwataka wananchi waache kulalamikia ufisadi?Usomi hautoi mamlaka ya kuizuia jamii kulalamikia maovu yanayoisumbua.Pili,kwa mtizamo wa msomi huyu,kwa vile tuhuma za ufisadi hazijathibitika basi watu wakae kimya hadi 'miujiza itapotokea kwa watawala wetu kuamua kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mafisadi'!Hii ni sawa na kuingiliwa ndani na kibaka halafu ukakaa kimya kwa vile tu wewe sio chombo cha sheria.Ukifanya hivyo,hata hao polisi watakuona mpumbavu na unawapotezea muda.La kufanya ni kumdhibiti kibaka au kupiga kelele kuwashtua majirani wakusaidie kumdhibiti.

Binafsi,pamoja na kuheshimu uhuru wa kutoa mawazo,nadhani tatizo kubwa la Dkt Bana ni tabia yake ya 'kusema chochote' hata kama hana cha kusema.Inaelekea aidha hafahamu athari za tabia hiyo au anapuuza tu.Matokeo yake ni kuonekana mbabaishaji wa namna flani.Si lazima jina lake lionekane magazetini au kusikika radioni kama hana la muhimu kuieleza jamii.Eti anatuasa kuwa "si vizuri kwa watu kunyimwa kura kwa sababu ya kutuhumiwa kwa ufisadi hadi hapo watakapothibitika na kutaka wanasiasa waache kuhukumu wenzao bila kosa".Kwanini hajiulizi inakuwaje watu hao wanatuhumiwa ufisadi in the first place?Kwanini ni wao na si Dokta Bana,kwa mfano?

Hivi lipi lililo muhimu zaidi kwa Tanzania kama taifa: kukosa viongozi bora kwa vile wanatuhumiwa kwa ufisadi au kupata viongozi bora watakaowajibika kulitumikia taifa kupambana na ufisadi?Wasiwasi wa Dkt Bana ulipaswa kuwa kwenye athari za ufisadi kwa jamii na sio tuhuma za wananchi dhidi ya mafisadi.Ni mlevi tu atakayeshindwa kuelewa kuwa kinachoumiza Watanzania kwa sasa ni UFISADI na sio TUHUMA DHIDI YA MAFISADI.

Mwanataaluma huyu anaongoza taasisi ya REDET ambayo mara imekuwa ikishutumiwa kwa upendeleo inapotoa taarifa za kura zake za maoni (opinion polls) kuhusu CCM na vyama vingine vya siasa.Sina hakika kuwa matokeo ya kura hizo huwa 'yanapikwa' ili kuridhisha watawala lakini kinachozua maswali dhidi ya polls hizo ni kutoendana na hali halisi na dalili za upendeleo.

Wito wangu kwa Dkt Bana ni huu: wakati mwingine jaribu kuitendea haki taaluma yako kwa kukaa kimya pale usipokuwa na cha kuongea.Kwa kufanya hivyo,utawatendea haki pia wasomi wenzako,taasisi unazoongoza na fani nzima ya usomi.Ni muhimu pia unapotoa matamshi mazito ukajitahidi kutumia theories za kusapoti matamshi hayo badala ya kutoa hisia zenye mwelekeo wa kijiweni.


.

Tanzania leads the list of East African states that have lost billions of dollars to money laundering, tax evasion, government graft and other illegal operations, according to a report by a US-based financial watchdog group.


The report “Illicit Financial Flows from Africa: Hidden Resources for Development,” by Global Financial Integrity, states that the country has lost $8.9 billion over the past four decades through the illicit means. Kenya lost $7.3 billion while Uganda lost $6.4 billion over the same period.


The three East African countries thus lost a total of $22.6 billion, money that would be sufficient to wipe out their combined outstanding external debt while leaving several billion dollars available for fighting poverty and spurring economic growth.

The study points out that the impact of these losses is felt most acutely by the poorest Africans. The illicit outflow of money also “drains hard currency reserves, heightens inflation, reduces tax collection, cancels investment and undermines free trade,” the study says.

Tanzania is ranked 13th among the top 15 countries with cumulative illicit outflows after Angola, Republic of Congo, Cameroon, Côte d’Ivoire, Ethiopia, Gabon, Ghana, Madagascar, Mozambique, Nigeria, South Africa and Sudan. Zambia and Zimbabwe take the 14th and 15th positions respectively.

Already, Global Financial Integrity has started collecting signatures to petition the G20 Transparency at the G20 summit this June. The organisation is looking for 100,000 signatures from all over the world to forward to Canadian Prime Minister Stephen Harper, the current president of the G20. “Our goal is to show him the names of 100,000 people from all over the world who support ending banking secrecy, increasing financial transparency, and finally attacking the root causes of poverty.”

The report says: “So long as illicit capital continues to haemorrhage out of poor African countries over the long term at a rapid pace, efforts to reduce poverty and boost economic growth will be thwarted as income distribution becomes ever more skewed, leading to economic and political instability.”

Tanzania’s Finance and Economy Minister Mustafa Mkulo told The EastAfrican from Dodoma that in order to reverse this situation, the country has set up a Financial Intelligence Unit within the ministry to join international community in fighting money laundering and financing of terrorism.

“This problem indeed exists. At regional level, within the East African Community and the Southern African Development Community, we have seen this problem thrive for a long time and decided to jointly act against it,” he said. (See related story, “Will electronic tax registers stem the tide of pilfering?”)

The report says that the figure for Uganda likely understates the true volume of illicit outflows. It notes that civil strife in the Great Lakes region during parts of the 1970-2008 study period resulted in “incomplete and poor quality data” for Uganda, Rwanda, Burundi and Congo.

In all cases, adds the study that encompassed all of Africa, actual losses due to systematic looting are likely to be far greater than the study estimates.

Researchers Dev Kar, a former senior economist at the International Monetary Fund, and Devon Cartwright-Smith, an economist at Global Financial Integrity, note that their figures do not take account of proceeds from smuggling and some of the ways in which trade and services are mis-priced by commercial swindlers.

The actual totals might be more than double the $22.6 billion listed in the report for the three East African countries if those other sorts of illicit outflows were included in the computations, a Global Financial Integrity spokeswoman told The EastAfrican.

Bribery and theft involving government official accounts for only a three per cent share of the money that moves across borders illicitly, the study says.

“Criminal proceeds generated through drug trafficking, racketeering, counterfeiting and more are about 30 to 35 per cent of the total,” the study adds. “The proceeds of commercial tax evasion, mainly through trade mis-pricing, are by far the largest component at some 60 to 65 per cent of the global total.”

Trade mis-invoicing, described in the report as “a significant problem for Kenya,” involves the overpricing of imports and the underpricing of exports on Customs documents, the study explains.

For Africa as a whole, total illicit outflows are said to have amounted to at least $854 billion across the 39 years encompassed in the study.

The top five countries with the highest outflow measured were: Nigeria ($89.5 billion) Egypt ($70.5 billion), Algeria ($25.7 billion), Morocco ($25 billion), and South Africa ($24.9 billion). Most of that money has gone into Western financial institutions, the study says.

“This massive flow of illicit money out of Africa is facilitated by a global shadow financial system comprising tax havens, secrecy jurisdictions, disguised corporations, anonymous trust accounts, fake foundations, trade mis-pricing and money laundering techniques,” Mr Kar and Mr Cartwright-Smith write. “The impact of this structure and the funds it shifts out of Africa is staggering.”

The researchers argue that the existing global financial system, shaped by liberalisation and deregulation of financial markets, has ended up generating ever-rising illicit flows and losses in government revenues. Economic growth without credible reform could lead to more, not less, capital flight, as the increase in incomes would simply finance the increased accumulation of foreign assets.

According to the United Nations’ Millennium Development Goals, $348 billion will be needed to cover MDG costs by 2010 and $529 billion by 2015. The United Nations report World Economic Situation and Prospects 2010 notes that a large gap still separates Africa from its MDGs.

By all accounts, official donor aid commitments will probably fall well short of the required funding of MDGs, leaving open the serious possibility that related targets will recede even further.


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.