Showing posts with label OBAMA. Show all posts
Showing posts with label OBAMA. Show all posts

23 May 2011




BONYEZA PICHA HAPO JUU KUSOMA HABARI KAMILI






CHANZO : Daily Mail

1 May 2011


Wanasema "kisasi ni sawa na chakula ambacho ladha yake inaongezeka kinapokuwa kimepoa".Maana ya msemo huo ni kwamba kisasi kinamuumiza zaidi mkosaji pale mkosewa anapomvutia muda mkosaji hadi anasahau kuwa alishawahi kumkosea mtu,kisha mkosewa analipiza kisasi.Inakuwa kama kuchonokoa kidonda kilichokwishapona.

Lakini inaelekea Rais Barack Obama hakutaka kusubiri hadi Donald Trump asahau kuwa alikuwa kinara wa fitna kwamba Obama si raia wa Marekani.Na jana alipata fursa mwanana ya "kumfanyizia" tajiri huyo wa uwekezaji kwenye majengo.

Katika hafla ya kila mwaka ya Waandishi wa Habari wanaoripoti habari kutoka Ikulu ya Marekani ambapo mgeni rasmi huwa Rais,Obama alimrushia Trump vijembe vikali lakini katika hali ya utani,kama ilivyo desturi ya halfa hiyo.

Hikuwa siku nzuri kwa Trump aliyehudhuria hafla hiyo kwa mwaliko wa gazeti la Wahington Post.Alipowasili tu alikumbana na sauti za kuzomewa.Lakini alikuwa Obama aliyemnyong'onyeza tajiri huyo kwa vijembe vikali vya utani wenye ukweli.

Obama alimkebehi Trump kwa kijembe kwamba ana furaha suala la wanaodadisi uraia wake sasa limekwisha kwahiyo Trump atapata wasaa wa kuchunguza kama kweli wataalamu wa anga walifika kweli mwezini,na iwapo Tupac na Biggie (Notorious B.I.G) kweli waliuawa.

Lakini kimbembe kwa tajiri huyo hakikuishia kwa vijembe vya Obama pekee kwani mchekeshaji maarufu Seth Meyer hakubaki nyuma katika "kummaliza" Trump.Alimgalagaza kwa kutanabaisha kuwa "Donald Trump amekuwa akieleza kuwa atagombea urais kwa tiketi ya chama cha Republican,jambo ambalo ni la kushangaza...nilidhani jambo pekee analoweza kugombea ni kuwa kituko".

Kadhalika,Obama aliwatania pia baadhi ya wagombea urais watarajiwa wa Republicans kwa kusema tetesi zinaonyesha kuwa Michelle Buchmann,mwanamama kipenzi cha wahafidhana wa Tea Party Movement,alizaliwa Canada na sio Marekani (na kumkumbusha kuwa majungu huwa yanaanza kihivyo).Pia alimtania mgombea mwingine mtarajiwa Tim Pawlenty kwa kudai amesikia kwamba jina kamili la mwanasiasa huyo ni Tim HOSNI Pawlenty (akimaanisha pengine ana asili ya Misri kwa akina HOSNI Mubarak).

Sio siri.Kwa mara ya kwanza kabisa nilimwonea huruma Trump alipokuwa akipigwa vijembe na Obama na Meyer huku ukumbi ukilipuka kwa mayowe.Lakini ndio hivyo,mkuki mtamu kwa nguruwe lakini kwa binadamu mchungu.

Angalia clip ifuatayo kisha jiburudishe kwa video za Tupac na Biggie (kwa vile walitajwa katika hafla hiyo)




9 Dec 2008


WASHINGTON — The first sign of cracks in President-elect Barack Obama's foreign policy team of rivals emerged on Monday as his choices for secretary of state and U.S. ambassador to the United Nations visited the State Department.

As Secretary of State-pick Hillary Rodham Clinton and U.N. envoy-choice Susan Rice separately visited the diplomatic agency's headquarters in Washington's Foggy Bottom neighborhood, persons familiar with the transition said that Rice wants to install her own transition team inside the department.

Such a move by an incoming U.N. ambassador is rare, if not unprecedented, because the job is based at the United Nations in New York, where Rice already has a small transition staff, the sources familiar with the incoming administration.

The push by Rice, an early Obama supporter whose position the President-elect wants to elevate to a cabinet post, is also a signal that she intends to use her influence with the new president to play a more significant role than previous U.N. envoys, they said. The transition sources spoke on condition of anonymity to discuss internal deliberations.

Officials with Clinton's transition team declined to comment on the matter, and aides to Rice could not immediately be reached. State Department officials declined to comment on issues related to the transition.

It was not clear if Clinton and Rice _ who had strained relations during the Democratic primaries because of Rice's steadfast backing of Obama _ saw each other at the State Department as Clinton left the building shortly after Rice arrived.

During the presidential campaign, some Clinton aides saw Rice's early decision to back Obama as a betrayal because of her previous role as a high State Department official during President Bill Clinton's administration. Rice's desire to place her own team in Washington could fuel speculation that those tensions will carry into the new administration.

The officials could not say if Clinton's team had formally objected to Rice's plan, or even if Rice would be able to install a separate transition team inside the State Department. But they noted that dueling transition teams could complicate the handover by blurring lines of authority.

Technically, the job of U.N. envoy falls under the authority of the secretary of state, although some previous U.N. ambassadors have held cabinet rank. The last U.N. ambassador to be part of the president's cabinet was Richard Holbrooke, who had a famously icy relationship with then-Secretary of State Madeleine Albright during the Clinton administration.

Albright, who was President Clinton's first ambassador to the United Nations, was a mentor to Rice. But the two had a falling out when Albright, America's first female secretary of state, lined up behind Hillary Clinton for the Democratic presidential nomination and Rice backed Obama.

Hillary Clinton, meanwhile, was to dine Monday evening with the nation's current and second female secretary of state, Condoleezza Rice, at Rice's apartment in the exclusive Watergate complex. The two Rices are not related and Condoleezza Rice said on Sunday that she thought Clinton would do a great job.

Also Monday, Clinton was to meet privately with Sen. John Kerry, D-Mass. and the incoming chairman of the Senate Foreign Relations Committee, according to a Democratic official. Kerry, once a contender for the secretary of state job, will oversee Clinton's confirmation. Kerry has pledged to hold "swift and fair" confirmation hearings.


11 Nov 2008






7 Nov 2008


Barack Obama's motorcade had an unexpected occurrence while ferrying the president-elect to a security briefing at Chicago FBI headquarters Thursday morning.

As the motorcade pulled onto Van Buren, towards the Loop, a couple in a tan sedan tried to drive around the heavily-armed line of vehicles, wrote pool reporter P.J. Hufstutter of the Los Angeles Times:

The SUV cut the car off immediately, and the security team aimed their weapons at the car. The driver and passenger in the sedan stopped, and looked stunned -- until the male driver appeared to understand what was happening (your pool reporter could see him mouth "Obama"). The motorcade continued on. The sedan remained stopped, near the side of the road. [...] Some of the drivers here in Chicago do not seem to understand that a) the Chicago police car at the end of the president-elect's motorcade is serious about having traffic pull over when the officers flash their lights and hit their sirens, and b) it's not a great idea to jump ahead of traffic by trying to cut around the black SUV filled with five heavily-armed secret service CAT members.


5 Nov 2008


YESTERDAY,KARL ROVE PREDICTED OBAMA WOULD HAVE WON BY 338 VOTES.AND THAT'S EXACTLY WHAT OBAMA HAS SO FAR GOT AT THIS VERY MOMENT.I WISH HE WOULD HAVE BEEN A DEMOCRAT!I REALLY ADMIRE THIS GUY (EXCEPT FOR HIS ASSOCIATION WITH BUSH,OF COURSE).CLICK HERE TO SEE  THE LINK SHOWING HIS PREDICTION.

16 Oct 2008


Beware an October surprise from bin Laden
By Joseph Nye
Published: October 15 2008 19:31 | Last updated: October 15 2008 19:31

Americans are transfixed by the aftermath of the September surprise in financial markets. Could there be a very different surprise coming in October?

The public thinks Democrats do better on economic issues, and the financial crisis erased the bounce in the polls that John McCain received from the Republican convention. After the second presidential debate, Mr Obama widened his lead, but dangers remain. Polls show that Republicans do better on the issue of terrorism. Last June, McCain adviser Charlie Black was reprimanded for having the temerity to point out that the intrusion of a terrorist event into the campaign would “certainly be a big advantage” for Mr McCain. Mr Black may have been politically incorrect but an objective analysis suggests he might be right.

On October 29 2004, four days before the last election, Al Jazeera aired an 18 minute video tape in which Osama bin Laden addressed the American people and threatened further retaliation and a desire to bankrupt the US. In the first poll after that tape was released, President George W. Bush opened up a six point lead over Senator John Kerry. The deputy director of the CIA commented that “Bin Laden certainly did a nice favour today for the president”.

Since the election turned on 120,000 votes in Ohio, it is plausible Mr bin Laden was able to affect the election. From the al-Qaeda leader’s point of view, Mr Bush’s policies were more useful for his efforts to recruit supporters than Mr Kerry’s might have been. Mr bin Laden is involved in a civil war within Islam. He wants the US to pursue policies that create the appearance of a clash of civilisations. Anything that polarises the mainstream of Muslim opinion helps his recruiting. As the deputy director for analysis at the CIA commented at the time: “Certainly, he would want Bush to keep doing what he’s doing for a few more years.”

From that point of view, Barack Obama must be unsettling for Mr bin Laden. An African-American with a father born in Kenya and a childhood spent partly in Indonesia presents a very different face to the world. A recent BBC poll of 22 countries found that if the world could vote, Mr Obama would win in a landslide. The pro-Obama margin varied from 82 percentage points in Kenya to 9 points in India.

Of course, Americans do not like outside interference in their elections. When Mr Obama attracted a crowd of 200,000 to a speech in Berlin last summer, Republican critics portrayed him as an elitist who appeals overseas but not to blue collar workers at home. On the other hand, in a recent poll that asked Americans to rate a series of foreign policy goals for the next president, 83 per cent ranked “improving America’s standing in the world” as most important. Certainly, the election of the first African-American as president would do wonders to restore the soft power that the Bush administration has squandered over the past eight years. That is why Mr Obama is such a threat to Mr bin Laden.

Some voters worry that even though Mr Obama might be good for US soft power, he might not understand hard power. Mr Obama’s statements in the two presidential debates suggest that he gets it. He has promised to give priority to finding and killing Mr bin Laden but there is more to the story. Niccolò Machiavelli said that it is more important for a prince to be feared than to be loved but we sometimes forget that the opposite of love is not fear, but hatred. Machiavelli made it clear hatred is something a prince should avoid at all costs. Smart power is the ability to combine hard and soft power into an effective strategy.

Both Mr McCain and Mr Obama have impressive hard power political and organisational skills, or they would not be where they are today. After all, Mr McCain has a military background and Mr Obama came up through the rough and tumble of Chicago politics. More over, Mr Obama’s campaign has set a new standard for political organisation. But on the crucial soft power skills of emotional intelligence, vision and communication, Mr Obama has the edge as reflected in the global polls and that must be giving Mr bin Laden a headache. In the next few weeks, as the remaining undecided voters have to make up their minds, Mr bin Laden may again be tempted to enter the fray. Given the scale of the financial crisis, it might take more than a video tape to refocus the attention of the American electorate this year but we should be alert to Mr bin Laden’s temptation and the danger it presents.

The writer is a professor at Harvard University and author most recently of The Powers to Lead

SOURCE: FT

8 Oct 2008

CLICK HERE to read the story.

6 Oct 2008



CLICK HERE to read the story.

18 Sept 2008









Picha ya hapo juu inafurahisha.Ndio namna jamaa wa The Huffington Post wanavyo-summarize masahibu yanayomkumba John McCain.Kwa mujibu wa Gallup polls,Barack Obama amefanikiwa kumwengua McCain kwenye kura za maoni ikiwa ni mara ya kwanza tangu mgombea huyo wa Republicans apande chati kufuatia convention ya chama hicho hivi karibuni.Zaidi,angalia video hii hapa chini


22 Mar 2008

Jana nilishuhudia kituko cha mwaka.Mwanzoni nilidhani ni porojo tu lakini asubuhi hii nimeona tukio hilo limekuwa gumzo mtandaoni.Ilikuwa takriban saa 6 mchana za hapa (hapa saa zitabadilika mwishoni mwa mwezi huu),nikaamua kupoteza muda kwa kuangalia kipindi cha Fox&Friends.Nasema kupoteza muda kwa vile waendesha kipindi hicho huwa wananikera sana kutokana na kauli zao za upendeleo wa wazi kwa wahafidhina na upinzani wao mkubwa dhidi ya Democrats na liberals.Sikujutia uamuzi wa "kupoteza muda" kwani huku watangazaji Steve Doocy na Gretchen Carlson wakishikia bango kauli ya Obama kwamba grandmom wake ni like typical White person,mwenzao Brian Kilmeade aliamua kuondoka kwa muda studioni kutokana na kukerwa na namna wenzie walivyokuwa wakimsakama Obama.Kama hiyo haitoshi,muda mfupi baadaye,mtangazaji mwandamizi wa kituo hicho,Chris Wallace,alionekana hewani wakati Fox&Friends inaendelea ambapo alielezea waziwazi kwamba alikuwa akiangalia kipindi hicho na hakupendezwa na namna kauli ya Obama kuhusu bibi yake ilivyokuwa ikipotoshwa.Wallace alieleza wazi kwamba yeye si msemaji wa kambi ya Obama lakini angependa kuona kipindi hicho kinazungumzia suala hilo ndani ya context,na kwenda mbali zaidi kwa kuwashauri wana-Fox&Friends kuangalia pia habari nyingine za muhimu kuhusu Obama kama vile endorsement ya Bill Richardson na hotuba zake mbili kuhusu uchumi na vita ya Irak.





15 Mar 2008



OBAMA:On My Faith and My Church. (CLICK THE LINK TO READ THE ARTICLE)

24 Jan 2008

Siku chache zilizopita Wamarekani waliadhimisha siku ya Dakta Martin Luther King Jr,mmoja wa wapigania haki za Waamerika Weusi.Historia inamkumbuka Dkt King (aliyezaliwa mwaka 1929 na kuuawa kwa risasi mwaka 1968)kama nguzo muhimu katika kupigania haki za Waamerika Weusi nchini humo.Pengine kilichomfanya wanaharakati huyo akubalike zaidi ni imani yake ya kudai haki kwa njia za amani.

Miaka mitano kabla ya kuuawa,mwaka 1963,Dkt King alitoa hotuba ambayo hadi leo imeendelea kuwa na mvuto mkubwa sio nchini Marekani pekee bali pia sehemu mbalimbali duniani katika mapambano ya kudai usawa.Katika hotuba hiyo iliyopewa jina “I Have a Dream” (“Nina Ndoto”,kwa tafsiri isiyo rasmi),Dkt King alieleza matamanio yake kuona Waamerika Weusi na Weupe wakiishi pamoja kwa amani na usawa.Hotuba hiyo iliyotolewa mbele ya watu zaidi ya laki mbili,inakubalika miongoni mwa wengi kama moja ya hotuba za muhimu kabisa katika historia ya Marekani.Mwaka 1999,hotuba hiyo ilichaguliwa na wasomi kuwa ni hotuba bora kabisa za karne ya 20.

Miongoni mwa nukuu muhimu katika hotuba hiyo ni pamoja na (kwa tafsiri yangu isiyo rasmi) “…nina ndoto kwamba siku moja taifa hili litasimama na kuishi kama inavyotamkwa kwenye imani yake….nina ndoto kwamba siku moja watoto wangu wanne wataishi katika taifa ambalo hawatahukumiwa kutokana na rangi ya ngozi zao bali tabia/utu wao….nina ndoto kwamba siku moja watoto wa waliokuwa watumwa na watoto wa waliokuwa wamiliki watumwa watakaa pamoja katika meza ya undugu…”

Msukumo uliotokana na uongozi wa harakati za Dkt King ulisaidia sana kubadili historia ya Marekani hususan usawa kwa (Wamarekani) Weusi, na kupelekea mabadiliko mbalimbali dhidi ya sheria za kibaguzi.Miongoni mwa sheria hizo ni pamoja na “Civil Rights Act” ya mwaka 1964 iliyoharamisha ubaguzi kwenye sehemu mbalimbali katika jamii.Mwaka uliofuata, “Voting Rights Act” ilipitishwa na kufuta kipengere kilicholazimisha wapiga kura watarajiwa kufanya testi za kupima uwezo wa kusoma na kuandika (wengi wa waathirika wa kipengere hicho walikuwa Wamarekani Weusi ambao walikuwa na maendeleo duni kielimu kutokana na kubaguliwa).

Maadhimisho ya siku ya Dkt King yamekuwa yakitoa changamoto nzuri kwa jamii ya Wamarekani kutafakari mahusiano kati ya Weupe na Weusi.Wengi hujiuliza iwapo ndoto za Dkt King zimetimia kweli,zinaelekea kutimia au hazina dalili ya kutimia kabisa.Ni maswali magumu ambayo yanahitaji uchambuzi wa kina kuyajibu,na pengine hata kwa uchambuzi wa kina bado inaweza kuwa vigumu kupata jawabu moja linalokubalika.Kingine kinacholeta ugumu wa kupata jawabu ni tofauti ya vizazi.Kwa walioishi nyakati za ubaguzi wa rangi na kushuhudia harakati za Dkt King wanaweza kuwa na mtizamo tofauti kuhusu kutimia kwa ndoto za mwanaharakati huyo ukilinganisha na kizazi cha hivi karibuni ambacho kinamwelewa Dkt King kupitia kumbukumbu za historia tu.

Hata hivyo ni rahisi kukubaliana kwamba harakati za Dkt King na wenzie zimesaidia kuleta mabadiliko makubwa ikiwa ni pamoja na hayo ya kisheria niliyotaja awali.Wapo wanaokwenda mbali zaidi na kutoa mifano ya mafanikio ya Waamerika Weusi maarufu kama Jenerali Colin Powell na Condoleeza Rice ambao wameshika nafasi nyeti katika uongozi wa taifa hilo.Lakini mfano mzuri zaidi ni Barack Obama,seneta Mweusi anayewania kuteuliwa kugombea urais wa nchi hiyo kupitia chama cha Democrats.Akiteuliwa kuwa mgombea,ataweka historia ya pekee nchini humo,na akifanikiwa kushinda urais basi hiyo itakuwa zaidi ya kuweka historia (tuite kuandika historia upya).Hata kama atashindwa,mafaniko aliyokwishafikia hadi sasa ni hatua muhimu katika kutimia kwa ndoto za Dkt King.

Afrika nayo imetoa akina Dkt King kadhaa,na kwetu Tanzania tunajivunia Baba wa Taifa marehemu Julius Nyerere ambaye (kama Dkt King) alikuwa na ndoto zake kadhaa ambazo kimsingi zilihusu kuwa jamii yenye usawa.Ndoto za Mwalimu zilivuka mipaka ya Tanzania kuhakikisha kuwa Afrika yote inakuwa huru.Mchango wa Mwalimu katika mapambano ya ukombozi kusini mwa Afrika utaendelea kukumbukwa milele.Na pengine hapo ndipo baadhi yetu tunagundua mabadiliko ya vizazi yanavyochangia kusahaulisha historia.

Mara nyingi napokutana na vijana Waafrika wenzangu (wanaoishi hapa Uingereza) kutoka nchi kama Zimbabwe,Zambia,Angola,Msumbiji,Afrika Kusini,Namibia na Uganda,nabaini kwamba wengi wao aidha wamesahau au wanapuuza mchango wetu katika ukombozi wa nchi zao (kwa Uganda ni kumng’oa Nduli Idi Amini).Angalau Wazimbabwe wanaweza kuwa na kisingizio kwamba kutokana na ubabe wa Mugabe,baadhi yao wanaweza kutoona faida ya kumkimbiza mkoloni na kujipatia uhuru.

Lakini pengine si busara sana kuwalaumu wanaopuuza mchango wa Mwalimu na Tanzania kwa ujumla katika ukombozi wa nchi zao kwani inawezekana kabisa wanafuatilia kinachoendelea nchini mwetu na kugundua kwamba baadhi yetu tumetupilia mbali kabisa jitihada za Baba wa Taifa kuhakikisha tunajenga jamii yenye usawa.Kwa vile dunia ni kama kijiji,katika zama hizi za utandawazi,majirani zetu hao watakuwa wanasoma na kusikia habari kuhusu ufisadi nchi mwetu,na pengine kubaki wanajiuliza “hivi hawa si ndio waliokuwa wanapigania usawa barani Afrika?Mbona wenyewe wako sasa wanafanyiana hivi?”.

Mwalimu alifariki huku baadhi ya ndoto zake zikiwa hazijatimia.Wachambuzi wazuri wa siasa wanadai kwamba baadhi ya ndoto hizo zilishindikana hata kabla hajang’atuka (kwa mfano upinzani wake wa awali dhidi ya ushirikiano na mashirika ya fedha ya kimataifa).Lakini nadhani Mwalimu aliumia zaidi kuona Azimio la Arusha likizikwa hai na Azimio “la kimyakimya” la Zanzibar (naliita hivyo kwani sijawahi kuona “document” yoyote rasmi inayoelezea kilichomo kwenye Azimio hilo).

Wakati Dkt King anaweza kufarijika huko aliko iwapo angeweza kufahamu baadhi ya mambo yanayoendelea sasa nchini Marekani (hususan kuhusu Obama) nashindwa kuhisi ni lipi litakalokuwa linampa furaha Mwalimu huko aliko tukiweka pembeni suala la amani na utulivu.Na hata katika hilo (la amani na utulivu) wapo wanaodai kuwa ni ya kufikirika zaidi kwani ni ukweli usiopingika kwamba masikini ni wengi zaidi kuliko matajiri,na yayumkinika kusema kwamba matumbo ya masikini hao hayana amani wala utulivu.

Kadhalika,kuna wanaodai kwamba kigezo cha amani na utulivu kimekuwa kikitumiwa vizuri zaidi na mafisadi wanaoamini kwamba Watanzania ni wapole sana na hawako tayari kuchezea lulu ya amani na utulivu kwa vile tu flani kakwiba mabilioni ya umma.Pengine mafisadi hao wako sahihi kwani tumekuwa tukishuhudia baadhi ya watu wakiua,wakapewa dhamana za chapchap na kuendela na maisha yao kama kawaida huku hatima ya kesi zao ikisubiri isahaulike akilini mwa watu.Wakati hayo yakitokea,magereza yetu yamejaa wamachinga wanaotafuta ridhiki mitaani na wafungwa wengine ambao inawezekana kabisa walijiingiza kwenye wizi wa nyanya au kuku kwa vile tu hawakuwa na njia nyingine ya kujipatia kipato.Uhalifu ni uhalifu,na kila mhalifu anastahili adhabu lakini inatatiza kuona wahalifu wengine wakiendelea kula raha kana kwamba waliyofanya si kinyume cha sheria.

Tofauti kubwa kati ya ndoto ya Dkt King na Mwalimu ni kwamba wakati Wamarekani Weusi wanafanya kila jitihada kuenzi jitihada za Dkt King kwa kuendeleza mapambano dhidi ya ubaguzi na kupigania usawa,sie tuko kwenye mgawanyiko mkubwa kati ya wachache walionacho wasiosubiri kuongezewa bali wanapora, na wengi wasio nacho ambao hata kile kidogo walicho nacho kinaporwa.Hili ndio tishio kubwa,sio tu kwa ndoto za Mwalimu,bali hata kwa hiyo lulu yetu ya amani na utulivu.

16 Jan 2008


Wiki iliyopita ilitawaliwa na surprises mbili:huko New Hampshire,Marekani,Hillary Clinton aliibuka mshindi kwenye primaries za chama cha Democrats,kinyume kabisa na utabiri wa awali wa waendesha kura za maoni na wachambuzi wa siasa za nchi hiyo.Na huko nyumbani,ugavana wa Daudi Balali ulitenguliwa.Wakati ili kuelewa nini kinaweza kuwa chanzo cha tofauti kati ya utabiri (kwamba Hillary angeshindwa) na matokeo (ambapo mwanamama huyo alishinda) kunahitaji upeo wa namna flani kuhusu siasa za Marekani na tabia ya chaguzi katika nchi hiyo (kwa mfano phenomenon kama Bradley effect),utenguzi wa ugavana wa Balali haukuhitaji hata short course ya uchambuzi wa siasa kubaini kwamba he had to go,pengine mapema zaidi ya wiki iliyopita.

Makala yangu ndani ya gazeti la Raia Mwema wiki hii inazungumzia surprises hizo mbili.Inakwenda mbali zaidi kwa kuhoji iwapo ufisadi uliopelekea Balali kupoteza unga wake ulihusisha mtu mmoja pekee.Kadhalika,inahitimisha kwamba kufanikiwa kwa ufisadi huo ni failure kwa TAKUKURU na jeshi la Polisi,taasisi ambazo kimsingi zilipaswa kuchukua hatua mapema kuzuia na/au kupunguza uhalifu huo.

Pamoja na makala nyingine zilizokwenda shule ndani ya Raia Mwema,bingirika na makala hiyo hapa.

9 Jan 2008


Baada ya Barack Obama kuibuka kidedea huko Iowa,kuna wengi walioanza kuamini kwamba sura mpya imefunguliwa katika siasa za Marekani.Mimi sikuwa mmoja wao,na ushahidi unapatikana kwenye makala zangu zilizopita kuhusu ushindi huo wa Obama.Katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema nimejaribu kuangalia namna imani na matumaini ya Obama yalivyomfikisha hapa alipo sasa.Napenda kusisitiza kwamba makala hiyo iliandaliwa kabla ya matokeo ya primaries huko New Hampshire ambapo Hillary Clinton ameibuka mshindi na kuwafanya baadhi ya wachambuzi wa siasa na waendesha kura za maoni "kulamba matapishi yao".

Nikipata muda mwafaka nitachambua kwa kirefu nini nachodhani kimechangia kugeuza upepo uliokuwa ukivuma kuelekea kwa Obama huko New Hampshire.Lakini kwa kifupi,nadhani waendesha kura za maoni waliokuwa wakimpa Obama nafasi kubwa ya ushindi huku wakitabiri kuwa Hillary ataanguka walisahau namna Bradley effect inavyoweza kuwazuga watu pindi panapokuwa mgombea Mweupe na Mweusi.Kwa kifupi kabisa,Bradley effect ni tabia katika chaguzi za Marekani  ambapo  wapiga kura watarajiwa ambao hawajafikia uamuzi watampa nani kura zao (undecided voters) hutoa mtizamo tofauti na namna watakavyopiga kura.Kimsingi,tabia hii huchochewa na ubaguzi wa rangi ambapo undecided voters Weupe huweza kudai kuwa hawajaamua wampe nani kura au kudai kuwa watampa kura mgombea Mweusi lakini huishia kumpa kura mgombea Mweupe.

Kama nilivyosema awali,makala yangu kwenye Raia Mwema inahusu namna imani inavyoweza kuyapa nguvu matumaini ili kufikia malengo flani.Nafasi ya Obama imetumiwa kama kielelezo tu cha namna imani mbalimbali huko nyumbani (kwa mfano,kwamba maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana) zinavyoshindwa kuleta matumaini yanayokusudiwa kutokana na ufisadi,uzembe na ubabaishaji.Pamoja na makala nyingine zilizokwenda shule katika gazeti la Raia Mwema,bingirika na makala yangu hapa.

Baada ya kusoma makala hii sio vibaya ukiburudika na warembo hawa wa Blu3 na kitu chao Hitaji


7 Jan 2008


Kuna mengi yanasemwa kuhusu mwelekeo mzuri wa Barack Obama katika harakati zake za kuingia Ikulu ya Marekani baadaye mwaka huu.Lakini,je mafanikio ya Obama yanamaanisha kukubalika kwa asilimia 100 kwa mtu mweusi katika jamii ya Waamerika au ni matokeo ya kukwepa kile "weusi wenzie" kama Jesse Jackson na Al Sharpton wamekuwa wakikipigia kelele?
Nimekutana na makala hii katika toleo la leo la gazeti la Guardian la hapa Uingereza na nimeona ni vema nikakupa nafasi msomaji mpendwa wa blogu hii nafasi ya kuisoma na kutoa hukumu yako wewe mwenyewe.

Binafsi napenda kumuona mtu mweusi (au hata half-caste) akiwa White House,na kwa maana hiyo ingependeza endapo Januari mwakani Bush angempokea Obama kama "mkazi mpya" katika jumba hilo maarufu hapo 1600 Pennsylvania Avenue NW.Lakini sioni dalili ya hilo kutokea.Na kumbe siko peke yangu mwenye mtazamo wa namna hiyo.Naendelea kuamini kuwa White America bado haiko tayari kumuona mtu mweusi akiwa Rais wa Taifa hilo.Na pengine ndio sababu muhimu ya Republicans "kusherehekea" mafanikio ya Obama (wahenga wanatuonya kwamba ukiona adui yako anasherehekea ushindi wako basi ujue ushindi huo utamnufaisha).Wana sababu kuu mbili,moja,wanafahamu ugumu wa kumzuia Hillary Clinton kuingia Ikulu,na pili,wanafahamu wepesi wa kumwangusha Obama pindi akipitishwa kuwa mgombea wa Democrats.Niite prophet of doom lakini amin nakuambia,pindi Obama akishinda kuwa mgombea,basi shehena zote za White America za kumbomoa mwanasiasa zitaelekezwa kwake.Na atakuwa target rahisi kwao:watapigia mstari jina lake la kati la Hussein na kulikuza utadhani linamaanisha ugaidi (baadhi yao walishajifanya kuteleza ulimi na kumwita Barack Osama),watakumbushia confession yake kwamba zamani hizo alishawahi kubwia unga na kuvuta bangi.Anyway,ndani ya The Huffington Post kuna makala inayoelekea kurandana na mtizamo wangu kuhusu Obama.

Ukimaliza kusoma jipoze na clip hii ya Common featuring Dwelle iendayo kwa jina The People

12 Sept 2007

Asalam aleykum,

Katika makala yangu iliyopita,nilizungumzia kuhusu kile ambacho wachambuzi wa siasa za kimataifa wanakiona kama kurejea kwa kasi kwa mbio za silaha (arms race) zenye uwezo mkubwa na wa kisasa zaidi kuliko hapo awali au sasa.Nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani zimeonekana kuguswa na namna Russia inavyoongeza kasi katika teknolojia na uzalishaji wa silaha za kisasa.Muda mfupi kabla ya kuandaa makala hii,nimeona taarifa moja inayoeleza kuwa Russia imefanikiwa kufanya majaribio ya kile inachokiita “Baba wa Mabomu Yote” (Father of all Bombs).Teknolojia hiyo mpya inaelezwa kuwa na uwezo mara nne zaidi ya ile ya Marekani inayojulikana kama “GBU-43 Massive Ordnance Air Blast” (MOAB) au “Mother of all Bombs” (yaani “Mama wa Mabomu Yote”) ambayo ilifanyiwa majaribio yenye mafanikio mwaka 2003.Tofauti na teknolojia ya awali ya mabomu,hilo la kisasa la Russia ni la “thermobaric,” yaani linatumia oksijeni iliyopo hewani (atmospheric oxygen) kusababisha mlipuko badala ya kutumia kemikali nyingine (oxidizing agent) kuleta matokeo hayo (mlipuko).Silaha za ki-“thermobaric” zina tabia ya kutoa nishati kubwa zaidi kuliko zile zisizotumia teknolojia hiyo,na inaelezwa kwamba bomu hilo jipya la Russia lina uwezo wa kuteketeza kabisa maisha katika eneo mzunguko la maili nne.

Kinachochochea mbio za silaha ni sawa na kile wanafalsafa wanachokiita “domino effect” yaani badiliko (change) moja linapelekea badiliko jingine jirani,nalo linapekea badiliko jingine,na jingine kwa jingine,na kadhalika.Yaani ni kama kugongwa gari la kwanza kwenye foleni ndefu ambapo la kwanza litaligonga la pili,la pili litaligonga la tatu,na kadhalika,na kadhalika.Kwa Russia kutambulisha mafanikio yake hayo,ni dhahiri kwamba Wamarekani nao watakuna vichwa ili waibuke na teknolojia kali zaidi ya hiyo ya Russia (pengine wataamua kuiita “babu wa mabomu yote” maana tayari tuna “baba” na “mama,” na si ajabu Russia nao watajibu mapigo kwa kuja na “bibi wa mabomu yote”).Wajuzi wa mambo wanadai kuwa miongoni mwa mambo yanayoichochea Russia kuelekeza nguvu zake kwenye uboreshaji wa teknolojia ya silaha ni faida kubwa inayopata nchi hiyo kwenye biashara ya mafuta na gesi,na ukweli kwamba Rais Putin alikuwa shushushu mwandamizi ndani ya shirika la kijasusi la uliokuwa Muungano wa Jamuhuri za Kisovieti (USSR) ambapo shirika hilo lilikuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya teknolojia ya silaha.
Habari nyingine “nyepesi” kutoka Russia zinasema kwamba jiji la Ulyanovsk nchini humo limetoa “off” kwa wafanyakazi wote ili wapate fursa ya kufanya tendo la ndoa katika maadhimisho ya “Siku ya Kutunga Mimba jijini Ulyanovsk” (the Day of Conception in Ulyanovsk).Ruhusa hiyo ya mapumziko imetolewa kama sehemu ya mpango wa manispaa ya jiji hilo ujulikanao kama “Give Birth to a Patriot” (Zaa Mzalendo) ambapo watakaofanikiwa kudunga au kudungwa wanaweza kuibuka na zawadi ya gari,fedha au friji.Jiji hilo ndipo alipozaliwa Vladmir Lennin, na mpango huo wa kuhamasisha uzazi ni sehemu ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Lenin mwezi huu.Washindi wanatarajiwa kupatikana kwa kuzingatia heshima ya ndoa yao pamoja na sifa bora kama wazazi,na watapatikana kutokana na maamuzi ya jopo la majaji.Mambo hayo!!

Kabla ya kugeukia masuala ya huko nyumbani,ngoja nizungumzie suala moja ambalo mie binafsi linanigusa.Nilipokuwa Mlimani (UDSM) nilibahatika kuchukua somo liitwalo “Gender and Family Relations” (yaani Jinsia na Mahusiano ya familia).Naomba kukiri kwamba kabla ya hapo,sikuwa na uelewa wa kutosha kuhusu nafasi ya mwanamke katika jamii na picha nzima ya usawa wa kijinsia katika jamii mbalimbali.Sasa majuzi nilisoma gazeti la Guardian la hapa Uingereza na kukutana na habari isemayo kwamba serikali (ya hapa) ina mpango wa kuwachukulia hatua wanaume wanaonunua huduma ya ngono.Kimsingi,huduma nyingi,ikiwemo ngono,huhusisha mtoaji huduma na mpokeaji huduma,lakini katika dunia yetu ambayo tumezowea kuyaona makosa ya wanawake pekee ilhali yetu wanaume yakionekana ni ya “ya kishujaa,” suala la ukahaba limeendelea kwa kiasi kikubwa kuwa kosa la wanawake wanaojihusisha na biashara hiyo kuliko wateja wao ambao ni wanaume (hapa sizungumzii ukahaba kati ya watu wa jinsia moja).Neno “malaya” ni maarufu zaidi kuliko neno “fuska” na baadhi ya wachambuzi wa mahusiano ya jamii wanadai hiyo inasababishwa na tabia ya kuona matendo hasi (negative) ya mwanamke kuwa mabaya zaidi ya yale hasi ya mwanaume.Hata linapokuja suala la nyumba ndogo,tunashuhudia kuwa ni rahisi kwa mwanaume kuwa nazo hata 10 kama ana uwezo wa kuzimudu lakini mwanamke akijaribu hilo basi muda si mrefu anaweza kujikuta anafungashiwa virago vyake.Nchi za Magharibi zimepiga hatua flani katika kuleta usawa wa kijinsia,na miongoni mwa mitihani mikubwa katika eneo hilo ni ugombea (candidacy) wa Hillary Clinton kwenye kinyang’anyiro cha kuteuliwa kuwa mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Democrat.Na mshawasha zaidi unaeletwa na mgombea mwingine kutoka jamii ambayo hadi sasa bado inaonekana ni ya kuongozwa zaidi badala ya kuongeza,yaani watu weusi (Blacks).Historia inasubiri kuandikwa iwapo Hillary atafanikiwa kuwa mwanamke wa kwanza kuwa rais wa Marekani,au Barack Obama atafanikiwa kuwa Mweusi wa kwanza kuwa rais.Bibi,mama na dada zetu wanastahili pongezi (au hukumu) sawa na sie akina kaka,baba na babu.

Sasa mambo ya huko nyumbani.Nilipigwa na butwaa niliposoma habari katika gazeti moja la nyumbani kuwa huko Mwanza kampeni za kugombea uongozi wa CCM ziligeuka kuwa uwanja wa vita pale washabiki wa kambi za wagombea flani walipoamua “kufanyiana kweli” na kutupiana mawe.Sijui wangapi walijeruhiwa katika patashika hiyo lakini nachoshindwa kuelewa ni namna kila raslimali,ikiwemo vurugu,inavyotumika kutafuta uongozi wa kisiasa.Hivi kuna nini huko kwenye uongozi hadi watu watake kutoana roho?Yaani ukereketwa umekolea namna hiyo hadi watu wawe tayari kuweka rehani usalama wao kwa ajili ya mgombea flani?Cha kusikitisha ni kwamba si ajabu wapambe hawa hawa ndio watakuwa wa kwanza kulalamika kuwa mgombea wao “hafai” pale atapowatelekeza baada ya kupata anachohitaji (uongozi).Pasipo busara za haraka kutumika tunaweza kujiwekea katika mahali pabaya sana kama tutawaruhusu baadhi ya watu kuhatarisha amani kwa vile tu wanataka kupata uongozi.

Nimesoma pia ushauri wa aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM,Philip Mangula,ambaye baada ya kubwagwa huko Iringa alitahadharisha kwamba kuna wakati itafika uongozi wa chama hicho utagombewa kwa mfumo wa tenda (bid) na “bidder” mkubwa ndiye atakayeibuka kidedea.Pengine ana hoja ya msingi hapo,lakini inaweza kufunikwa na ukweli kwamba haya anayoyaona sasa yamekuwa yakitokea kwa muda mrefu,na kipindi hicho alikuwa katika nafasi nzuri zaidi ya sio tu kukosoa bali hata kukomesha matumizi ya “takrima” kwenye kusaka uongozi.Hata wazo lake kwamba ni vema kwa wanachama wa CCM wenye madaraka mengine (kama ubunge au uwaziri) wakatoa mwanya kwa wale wasio na madaraka (japo sio kosa,si ajabu baada ya uchaguzi huu kumkuta mtu akiwa na vyeo zaidi vitano) mawazo hayo yangekuwa na “mwangwi” mkubwa zaidi iwapo yangetolewa katika kipindi ambacho Mangula alikuwa madarakani.Yayumkinika kusema kuwa ni vigumu kurekebisha mapishi pindi ukiwa nje ya jiko,na majaribio ya kufanya hivyo nje ya jiko yanaweza kutafsiriwa tofauti na baadhi ya watu.

Na huko Morogoro,baada ya kushindwa kwenye uchaguzi wa miongoni mwa nafasi katika mkoa huo,Waziri Ngasongwa nae “aliwatolea macho” TAKUKURU kwa kile alichodai walishindwa kuzuwia baadhi ya wagombea kutoa “takrima” kwa wapiga kura.Swali pana zaidi ni je waziri anadhani taasisi hiyo ilishindwa (kwa mujibu wake) kutekeleza majukumu yake kwa vile ni sehemu ya mapungufu yake ya kila siku au ni katika tukio hilo tu?Iwapo jibu ni hilo la pili basi wapo wanaoweza kuhisi kuwa waziri ameweza kuona matatizo hayo kwa vile tu yamemgusa yeye binafsi. “Bottom line” ni kwamba iwapo mlolongo wa vimbwanga vinavyoendelea kwenye uchaguzi wa CCM vitachukuliwa kuwa ni mambo ya kawaida tu basi tunaweza kufika mahala tukajilaumu huku tukisema “laiti tungejua wakati ule…”Bahati mbaya,kwa wakati huo tutakuwa tumechelewa kuweza kufanya mabadiliko yoyote ya msingi.Ushauri huu sio wa kupandikiza chuki bali ni kwa ajili ya hatma ya taifa letu kwa manufaa yetu sasa na kwa vizazi vijavyo.

Neno la mwisho kabisa ni kuungana na wapenzi na mashabiki wa msanii maarufu anti Shenaz ambaye alikutana na mauti kwenye ajali ya basi huko Mbeya.Kwa tunaomfahamu,dada huyo alikuwa akipendezesha kila shughuli aliyokuwepo.Na tofauti na umaarufu wake,alikuwa mcheshi na asiye na chembe ya dharau.Mungu airehemu roho ya marehemu,Amina.

Alamsiki


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.