17 Sept 2009


HIZI SIO HARAKATI ZA SIASA BALI NI UTOTO.NA UTOTO HUU UNAENDELEA KWA VILE CHAMA TAWALA KINA IMANI YA KUTOSHA KUWA WANAOCHEZEWA SHERE (WAPIGA KURA) BADO WAKO USINGIZINI,NA KINACHOENDELEA (UTOTO HUO) NI SAWA NA NJOZI.

HEBU SOMA HII,KISHA TAFAKARI:

Makamba amfuata Spika Sitta Urambo, ampigia magoti

*ASEMA HANA UGOMVI NAYE, ASEMA ALIKUWA MLEZI WA NDOA ZA WANAYE

Na John Dotto, Tabora

KATIKA kile kilichoelezwa kwamba, ni kujisafisha mbele ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, CCM imesema ipo pamoja naye katika kutekeleza majukumu yake kama Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa CCM, Yusufu Makamba; ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kuondoa utata uliotokana na maazimio ya Halmashauri Kuu ya chama hicho ulioonyesha kuwa wabunge wanaopiga kelele dhidi ya ufisadi, wanakichafua chama na serikali yake.

Akizungumza na viongozi wa CCM wilaya ya Urambo kwenye mkutano wa ndani uliohudhuriwa na Spika Sitta, Makamba, alitumia muda mwingi kumsifia Sitta kwamba ni mtu muelewa, asiyetetereka na wala kuyumbishwa na mtu yeyote na kwamba anachokifanya ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho.

Makamba aliwaambia wanaCCM hao kwamba, hana chuki na Sitta, kwani hata alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alimkaribisha katika ndoa za wanawe na akapewa nafasi ya kuzungumza kama baba mlezi, heshima ambayo alisema hataisahau katika maisha yake.

Alisema wana CCM wanatakiwa kupuuza maneno ya watu wanaodai chama kina mgogoro na Spika, kwasababu hakuna kitu kama hicho na yote anayoyatekeleza kwenye Bunge ni kwa niaba ya chama chake.

Hata hivyo, baada ya kikao cha NEC, Makamba alikuwa mstari wa mbele kudai kuwa kikao kile kina uwezo wa kumuhoji mbunge yoyote hata Sitta kama anakwenda tofauti na chama.

Makamba alinukuliwa akisema NEC ni mama na akina Spika ni watoto hivyo ina mamlaka ya kuhoji mienendo yao.

Mara baada ya kikao cha NEC, Sitta alifanya ziara mkoani Tabora na kulalamika kwamba, CCM makao makuu wamewakataza viongozi wa chama hicho mkoani kumpokea.

Hatua ya Makamba kwenda Urambo kuhutubia na Sitta, inatafsiriwa kama njia ya kuweka mambo sawa na kufuta makovu ya huko nyuma baina yake na Spika.

Kwa upande wake, Sitta alimshukuru Makamba kwa kutembelea jimboni kwake na mkoa wa Tabora kwa ujumla.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika baada ya kikao cha ndani kumalizika, Makamba aliwahakikishia wananchi wa Urambo kwamba CCM kipo pamoja na mbunge wao Sitta, ndiyo maana wanatekeleza ahadi zote ikiwemo ujenzi wa barabara ya Urambo Kaliua mpaka Tabora Mjini.

Akizungumzia suala la ufisadi, Makamba alisema kuwa wanaCCM wote kuanzia ngazi ya matawi wanapaswa kuungana na wabunge wanaopiga vita ufisadi, kwani vita dhidi ya rushwa ni ya wanaCCM wote.

Alisema anakerwa na watu wanaosema CCM ni chama cha mafisadi kwani ufisadi wa mtu mmoja si wa CCM na akatoa mfano kuwa dhambi ya Mkatoliki mmoja si dhambi ya Askofu Kilaini wala kanisa lote.

Makamba alimaliza ziara yake jana mkoani Tabora na juzi alipokuwa akizungumza na viongozi wa CCM wakiwemo makatibu wote wa wilaya za Tabora kwenye ukumbi wa mikutano wa CCM mkoa, aliwalaumu viongozi hao kukaa kimya wakati wapinzani wanakishambulia chama hicho kwa kukipakazia maneno machafu.

Aliwataka waamke na kukipigania chama na kuacha kukaa kimya na kusubiri makao makuu ama Makamba kujibu mashambulizi.

Baada ya kikao cha Nec kilichofanyika Dodoma mwezi uliopita, Makamba na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chilligati kwa nyakati tofauti walisema CCM imeunda kamati ya watu watatu, inayoongozwa na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi kuwachunguza wabunge wenye tabia ya kuishambulia serikali nje ya vikao vya chama.

Habari za ndani ya kikao hicho ambazo baadaye zilivuja kwa vyombo vya habari, zilieleza kuwa Nec ilimweka kitimoto Spika Sitta kwa madai kuwa anaruhusu mijadala inayokichafua chama na serikali, huku baadhi ya wajumbe wakishinikiza anyang'anywe kadi ya CCM kwa madai kuwa anawapa uhuru bungeni watu wanaoishambulia serikali kwa ufisadi.

Hata hivyo, mwanzoni mwa wiki hii baada ya hotuba ya Rais, Chilligati alisema chama hicho hakina ugomvi wala uadui na wabunge wake wanaoongoza vita dhidi ya mafisadi nchini.

Kabla ya hapo, Mwenyekiti wa Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita ambaye alisemekana kumwandama Spika Sitta katika kikao cha NEC na akamwita faru aliyejeruhiwa anayetakiwa kumalizwa kabla hajasababisha madhara zaidi, naye alibadili msimamo na kuwaunga mkono wapiganaji wa ufisadi pamoja na Spika Sitta kwamba, wanatekeleza ilani ya CCM, hivyo wanastahili kuungwa mkono.

Mabadiliko haya ya siasa ndani ya chama hiki tawala na mfululizo wa matukio ya aina hiyo likiwemo la Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile ambaye amekaririwa katika vyombo vya habari akisema hana ugomvi na Mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe, anayesemekana kuwa ni hasimu wake kisiasa.

CHANZO: Mwananchi


NA HAWA NDIO TUNAOTARAJIA WAREJEE KUTUTAWALA 2010!

13 Sept 2009


Lowassa Tishio Ndani ya CCM

Nguvu ya kundi lake yatawala ndani ya NEC

KUNA kila dalili kwa aliyekuwa Waziri Mkuu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa, kupitishwa na vikao vya juu vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa mgombea urais wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu ujao, mwaka 2010.

Taarifa za kuaminika kutoka kwa vigogo kadhaa ndani ya CCM na kwa baadhi ya wabunge wa chama hicho kikongwe nchini, zimethibitisha nia ya Lowassa kuwania kiti hicho, huku kukiwa na uwezekano mkubwa wa kupitishwa na vikao vya juu kuwa mgombea pekee badala ya Rais Jakaya Kikwete, anayetarajiwa kuomba tena nafasi hiyo ili kumalizia kipindi kingine cha miaka mitano cha kuliongoza taifa.

Taarifa hizo zimefafanua kuwa nafasi ya Kikwete kupitishwa na CCM kuwa mgombea urais haitabiriki iwapo Lowassa ataamua kuwania nafasi hiyo ambayo pia humpa nafasi kiongozi kuwa mwenyekiti wa chama.

Ikiwa imesalia miezi 13 kabla ya kufanyika kwa uchaguzi huo, tayari Lowassa anaonekana kuwa na nguvu kubwa ndani ya chama, huku akiungwa mkono na wajumbe wengi wa vikao vya juu, hususan wale wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC).

Siku moja tu baada ya Rais Kikwete, kuzungumza na wananchi kwa staili mpya ya kujibu maswali ya papo kwa papo, Tanzania Daima Jumapili, ilizungumza na mbunge mmoja maarufu wa CCM, juu ya mustakabali wa chama hicho kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010, kwa sharti la kutotajwa jina lake.

“Kwa NEC hii niliyoiona kwenye kikao kilichopita, Lowassa anaweza kabisa kupitishwa kuwa mgombea urais wa CCM 2010 badala ya Bwana Mkubwa (Kikwete). Maana kwanza urais anautaka na jinsi nilivyoiona hii NEC, wajumbe wengi tayari wamesha declare interests kwa Lowassa …wengi wanamuunga mkono na ndiyo maana tumekuwa na vita kali ya makundi ndani ya chama.

“Kwa kweli Bwana Mkubwa sijui hali itakuwaje, nafasi ya kupitishwa kwake eti kwa sababu ni rais anayemaliza muda wake itakuwa ngumu sana, niseme tu kwamba haitabiriki,” alisema mbunge huyo aliyejizolea umaarufu kwa kupambana na ufisadi.

Nguvu ya Lowassa ndani ya NEC ndiyo inayodaiwa nusura imwangushe Spika wa Bunge, Samuel Sitta, baada ya wajumbe wengi kudai kwamba anaihujumu serikali bungeni, hivyo kupendekeza avuliwe uanachama, hali inayotafsiriwa kuwa walikusudia kulipiza kisasi dhidi ya hatua ya spika huyo kuunda Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza sakata la Richmond na ripoti yake kusababisha Lowassa kujiuzulu.

Kwa upande mwingine, baadhi ya vigogo kadhaa wa CCM wamekanusha kauli ya Rais Kikwete aliyoitoa wiki hii kwamba kuna uadui miongoni mwa wabunge na baina ya wabunge na mawaziri, na kufafanua kuwa uadui uliopo ni baina ya baadhi ya wabunge na chama chao.

“Alichosema rais kwamba wabunge wana uadui hata wanafikia hatua ya kuogopana, kwamba wanaweza kuwekeana sumu, kwa kweli si sahihi, uadui uliopo si kati ya wabunge na wabunge, bali ni kati ya baadhi ya wabunge na chama chenyewe. Kwani waliotaka kumsulubu Sitta kwenye NEC ni wabunge wenzake? Si wabunge wenzake, walikuwa ni wajumbe tu wa kikao kile cha chama, ambao wengi wako upande wa Lowassa. Wao bado wana kisasi na lile suala la Richmond na wako wengi kweli,” alisema kigogo huyo wa CCM.

Lowassa ambaye inaaminika kuwa ni rafiki wa siku nyingi wa Rais Kikwete, alijiuzulu uwaziri mkuu Februari 2007, kutokana na kuhusishwa na kashfa ya kutoa zabuni ya kufua umeme wa dharura kwa kampuni ‘hewa’ ya Richmod Development Company LLC.

Baadhi ya watu walio karibu na watu hao wanadai tangu kujiuzulu kwake, amekuwa katika kundi tofauti na Kikwete, huku akiwa na nguvu kubwa ya kichama inayodaiwa kuzidisha uhasama wa kimakundi ndani ya chama hicho.

Mbali ya nguvu hiyo ya kichama, wadadisi wa mambo waliozungumza na gazeti hili, walisema uwezekano wa Lowassa kuwania nafasi hiyo ya juu kabisa serikalini unatokana na ukweli kuwa mwenendo wa hivi karibuni wa utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu sakata la Richmond umeonekana kumsafisha mwanasiasa huyo kuwa hakuhusika kabisa katika sakata hilo, kwani tayari serikali yenyewe imeshatangaza kutowachukulia hatua baadhi ya watendaji waliokuwa chini yake kwa sababu ya kile kilichoelezewa kuwa hawakuhusika katika sakata hilo.

Katika mkutano wa 16 wa Bunge, serikali ilitangaza kuwa haijawachukulia hatua baadhi ya watumishi wake kadhaa ilioagizwa na Bunge, kwa sababu ya kutobainika kuhusika na mazingira ya rushwa na kuwafanya waipe ushindi wa zabuni ya kuzalisha umeme Kampuni ya Richmond.

Miongoni mwa watumishi ambao kamati teule ya Bunge iliyokuwa chini ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, ilipendekeza wachukuliwe hatua za kinidhamu na kisheria lakini hawakuchukuliwa hatua kama ilivyopendekezwa na Bunge ni Mwanasheria Mkuu, Johnson Mwanyika, huku Mkurugenzi wa Tume ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Edward Hosea, akichukuliwa hatua ndogo ya kuonywa.

“Lowassa anaweza kabisa kugombea urais, kwa sababu tayari jina lake limeshatakata, maana serikali yenyewe imeshasema kwamba kina Mwanyika hawakuwa na makosa yoyote katika suala la Richmond. Sasa kama Mwanyika hakuwa na kosa basi ni dhahiri kuwa kwa mtazamo wa watu Lowassa alionewa tu, kwa hiyo anaweza kabisa kufufuka kisiasa na kugombea urais,” alisema.

Wakati hali ikiendelea hivyo, hatima ya vita hiyo ya makundi sasa inaonekana kumtegemea Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, ambaye ndiye Mwenyekiti wa kamati maalumu iliyoundwa na Kikwete ili kufanya kile kinachoelezewa na baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa kama utafiti wa kutafuta suluhu ya kuinusuru CCM kutoka kwenye vita hiyo.

Wakati kamati hiyo ina wajumbe wengine kama Abdulhaman Kinana na Pius Msekwa, ni Mwinyi pekee anayeonekana kuungwa mkono na wana CCM wa makundi yote, hivyo kuwa tegemeo pekee katika kutafuta suluhu, kwani wajumbe wenzake bado wanaonekana kuwa ni sehemu ya watu wanaochochea vita hiyo ya makundi.




Na Mwandishi Wetu
KUNA kila dalili kwamba Rais Jakaya Kikwete ameamua kuwakana marafiki zake wa karibu baada ya kuueleza umma kuwa, hana urafiki wala udugu katika vita vya kupambana na ufisadi nchini.

Akizungumza na taifa kwa staili mpya ya kuwasiliana moja kwa moja na wananchi Alhamisi wiki hii, Kikwete alionya kuwa katika masuala ya rushwa, hasa ya Richmond na Kagoda, hana udugu wala urafiki.

“Mimi niseme kwamba, katika mapambano ya rushwa hakuna udugu wala urafiki, na suala la kuamua nani ashtakiwe au nani asishtakiwe halipo katika mamlaka yangu, hilo ni la Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP),” alifafanua Rais Kikwete.

“DPP akiridhika kwamba, mtu fulani ana la kujibu mahakamani wanastahiki kumfikisha mahakamani bila ya ushauri kutoka , kwa sababu katika vita hii hakuna rafiki wala ndugu."

Rais Kikwete alikuwa akijibu swali la msikilizaji aliyejitambulisha kwa jina la Joseph Machumu, aliyetaka kujua kwamba kashfa za Richmond na Kagoda zinachelewa kushughulikiwa kutokana na Rais Kikwete kuwa na urafiki na watu wanaotuhumiwa kuhusika.

Kauli hiyo ya Rais Kikwete iliibua maswali miongoni mwa wachunguzi wa mambo ya kisiasa, wakihoji kama ni kweli ameamua kwa dhati kuwatosa marafiki zake wa karibu waliohusishwa na Richmond au ililenga tu kufurahisha wananchi.

Kamati ya Bunge iliyokuwa ikichunguza kashfa ya Richmond ilimhusisha katika kashfa hiyo aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz na watumishi wengine wa serikali.

Wengine waliotajwa kuhusika katika kashfa hiyo ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, aliyekuwa Waziri wa Afrika Mashariki, Ibrahim Msabaha na watendaji wengine wa serikali, wakiwamo wanaoteuliwa na rais.

Baadhi ya watendaji hao ni Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Edward Hosea, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Athur Mwakapugi na wengineo.

Lowassa, Karamagi na Msabaha walijiuzulu mara tu baada ya kamati hiyo iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe kuwasilisha bungeni ripoti yake, Februari mwaka jana.

Miongoni mwa waathirika hao wa kashfa ya Richmond, ni Lowassa na Rostam pakee ambao Rais Kikwete aliwahi kukiri kuwa ni rafiki zake wakati akichukua fomu za kuwania uteuzi wa CCM kugombea urais mwaka 2005 mjini Dodoma.

Kikwete aliwataja maswahiba wake hao baada ya kuulizwa swali kwamba, alikuwa anajiamini nini hadi akateua baraza la mawaziri kabla ya kuteuliwa kugombea, jambo alilolipinga akifafanua kuwa akina Lowassa na Rostam walikuwa wanatajwa kwa kuwa ni marafiki zake na yeye kama mgombea hakuwa anazuiliwa kuwa na marafiki.

Baada ya uteuzi huo kumpitisha yeye na baadaye kunyakua urais, alimteua Lowassa kuwa Waziri Mkuu na Rostam akawa Mweka Hazina wa CCM na wawili hao walishiriki kwa kiwango kikubwa katika kampeni zilizomweka Rais Kikwete madarakani.

Lakini mara kwa mara Rais Kikwete amekuwa akieleza bayana kuwa hana ubia kwenye urais wake, isipokuwa Makamu wake, Dk Ali Mohamed Shein aliyekuwa mgombea wake mwenza.

Vilevile kitendo cha Rais Kikwete kukubali kupokea barua ya kujiuzulu kwa Lowassa kutoka kwenye nafasi hiyo ya juu, na kuondolewa kwa Rostam katika uweka hazina wa CCM kunawafanya baadhi ya watu waamini kuwa kweli Rais Kikwete hakuwa na ubia naye na kukubali maneno yake kuwa, kwenye suala la Richmond na kashfa nyingine za ufisadi hana urafiki wala udugu.

Pamoja na ufafanuzi huo wa Rais Kikwete suala la Richmond limekuwa ni tete tangu kuibuka kwake, huku likiwa limewagawa wabunge katika mapande mawili, moja likiwatetea washirika wa kampuni hiyo na jingine lenye nguvu likitaka watoswe kabisa.

Pia mgongano huo umehamia kwenye vikao vya CCM ambapo pande hizo zimeendelea kukamiana huku lile la watetezi wa Richmond likiwa na nguvu kuliko jingine linalotaka watoswe kwenye chama

Kutokana na mpambano uliopo kwenye suala hilo limekuwa likiibuka kila kukicha na ndio maana wasikilizaji waliamua kutumia nafasi hiyo adimu kumuuliza rais wao.

Akifafanua zaidi kuhusu suala hilo, Rais Kikwete alisema kampuni hiyo iliteuliwa na Tanesco katika mchakato wao. "Mimi nilipoambiwa nilisema kwamba, ni jambo zuri kumpata mwekezaji huyo."

Lakini Rais alikiri kwamba, ripoti za uchunguzi wa Richmond zinaonyesha kulikuwa na uzembe katika mchakato wa kuipata kampuni hiyo ya kufua umeme kwa sababu mchakato ulifanyika bila ya kamati kuthibitisha uwezo wa kampuni.

“Ingefanya utafiti wa kutosha, ikiwa ni pamoja na kutembelea ofisi za kampuni hiyo ili kujua uwezo wao na kurudisha ripoti kwa waziri na baadaye kwa waziri mkuu, lakini hilo halikufanyika. Yangefanyika haya matatizo yote yangeepukika,” alisema.

Alisema ukiachia mawaziri waliowajibika kwa kujiuzulu, maofisa wa chini waliofanya mchakato huo kushughulikiwa kwake hakujaridhisha.

“Tunapenda kuona kwamba, maofisa hawa washughulikiwe na mambo haya bado yanaendelea, katika vikao vijavyo tutapata taarifa nzuri kwa sababu hawa ndio tuliotegemea watuepushe na hasara hii, hivyo walistahili wachukuliwe hatua zinazostahili,” alisisitiza.

CHANZO: Mwananchi

TATIZO LA WENGI WA WAANDISHI WETU WA HABARI NI UVIVU WA KUCHAMBUA HABARI,SAMBAMBA NA KUJIKOMBA/KUJIPENDEKEZA KWA WATAWALA.UCHAMBUZI WENYE MANUFAA UNAPASWA KWENDA BEYOND RHETORICS NA KUNUKUU.UZEMBE WA KUSOMA "KATI YA MISTARI" UNASABABISHA UCHAMBUZI MWINGI KUWA RIPOTI YA KILICHOSEMWA NA FLANI.

8 Sept 2009


RAIS Jakaya Kikwete leo ataanza staili mpya ya kuwasiliana moja kwa moja na wananchi kwa njia ya simu na barua pepe, akisikiliza hoja, kujibu maswali na kupata maoni yao juu ya mustakabali wa nchi , Ikulu imesema jana.

Kikwete, ambaye alizungumza na taifa kwa mara ya mwisho Juni 11 alipozungumza na wazee wa mkoani Dodoma, atafanya mazungumzo hayo ya dakika 90 kwa njia ya televisheni kuanzia saa 2:30 usiku wakati atakapopokea simu na kusikiliza maswali, ushauri, maoni na kujibu moja kwa moja.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais inaeleza kuwa katika staili hiyo ya aina yake, Rais Kikwete pia atapokea ushauri kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu (sms) kutoka kwa watazamaji na ujumbe wa barua pepe, ikiwa ni mpango wa kusikiliza matarajio ya wananchi katika jitihada zao za kuboresha maisha yao kwa kujiletea maendeleo.

"Rais atatumia aina mpya ya kuwasiliana na wananchi kwa kusikiliza hoja zao, kwa kujibu maswali yao, kusikiliza ushauri wao na kupata maoni juu ya mambo yanayohusu mustakabali wa nchi yetu, serikali yetu na maendeleo yetu," inaeleza taarifa hiyo.

"Mazungumzo hayo yatakachukua muda wa dakika 90 kuanzia saa mbili unusu usiku (saa 2:30 usiku) hadi saa nne kamili usiku."

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, chini ya mpango huo rais atazungumza moja kwa moja kupitia vituo vya redio na televisheni vya Shirika la Utangazaji (TBC) na vyombo vingine vya utangazaji nchini.

Kurugenzi hiyo ya Mawasiliano Ikulu, ilifafanua kwamba "mbali na TBC, televisheni nyingine za ITV, TVZ, Mlimani TV, Tumaini TV na Channel Ten zinatarajiwa kuonyesha mazungumzo hayo".

Taarifa ya kurugenzi hiyo imevitaja vituo vitakavyotangaza moja kwa moja mazungumzo hayo kuwa ni TBC-Taifa, Sauti ya Tanzania Zanzibar (STZ), Radio Mlimani, Radio Clouds, Radio Tumaini, na Radio Uhuru.

Ikulu pia imetaja namba zitakazotumika kwa ajili ya maswali, maoni, hoja, ushauri utakaotolewa moja kwa moja kupitia TBC. Namba hizo ni +255-22-2772448, +255-22-2772452 na +255-22-2772454.

Pia kwa watakaotaka kutuma ujumbe mfupi wa simu watatakiwa kutuma kwenda namba 0788-500019, 0714-591589 na 0764-807683, huku wale watakaotaka kutumia barua pepe watatuma kwenda anuani ya [email protected].

Hii ni mara ya kwanza kwa Rais Kikwete kutumia aina hiyo ya mazungumzo na wananchi baada ya viongozi wengine waliomtangulia kutumia hotuba za mwisho wa mwezi kwa kupitia redio na televisheni na pia mikutano na wazee au na waandishi wa habari.

Kikwete anaanza utaratibu huo akionekana kufuata nyayo za aliyekuwa Rais wa Philippines, hayati Gloria Macapagal Arroyo, ambaye amekuwa alikuwa na utaratibu wa kuruhusu wananchi kupiga simu na kuuliza maswali.

Lakini Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ana utaratibu tofauti. Kiongozi huyo wa muda mrefu wa Uganda ana kawaida ya kuingilia mijadala inayoendeshwa moja kwa moja na vituo vya redio na kujibu tuhuma dhidi ya serikali yake au kutoa ufafanuzi.

Rais wa Marekani, Barack Obama husikiliza maoni, ushauri na kujibu maswali ya wananchi kupitia barua pepe.

Utaratibu huo mpya utamfanya rais apokee maswali ya aina tofauti na kumuwezesha kujua kero hasa za wananchi tofauti na vilio vya wanasiasa, hali ambayo itafanya muda wa dakika 90 kuwa mfupi kuweza kukidhi utashi.

Katika hotuba yake ya Juni 11, Rais Kikwete alizungumzia athari za mtikisiko wa uchumi na kutangaza mpango mkubwa wa kutenga Sh1.7 trilioni kwa ajili ya kunusuru uchumi.


CHANZO: Mwananchi

HIVI MPAKA LEO KIONGOZI WETU HAJUI MUSTAKABALI WA TAIFA LETU HADI AOMBE MAONI KUTOKA KWA WANANCHI?HIZO DAKIKA TISINI ZINATOSHA KWELI KUMFAHAMISHA KUWA NCHI INAELEKEA PABAYA?
JE INA MAANA ZIARA ZA KILA KUKICHA ZA VIONGOZI WETU HAZIJAFANIKIWA KUWAFAHAMISHA KERO ZA WANANCHI NI ZIPI?
NAULIZA HAYO KWA VILE HUU NI MWAKA WA 4 TANGU AWAMU YA NNE IINGIE MADARAKANI.SASA KAMA HADI LEO HAWAFAHAMU KINACHOIANGAMIZA TANZANIA....
LAKINI KUBWA ZAIDI YA KWAMBA LICHA YA UFINYU WA MUDA ULIOTOLEWA KWA WAULIZA MASWALI/ATOA USHAURI,NA LICHA YA UKWELI KWAMBA UTARATIBU HUO UNAWAPENDELEA WACHACHE WENYE ACCESS NA SIMU AU KOMPYUTA (KUTUMA BARUA-PEPE),KUNA UHAKIKA GANI KUWA KERO ZITAKAZOTOLEWA ZITAFANYIWA KAZI?KAMA USHAURI WA KITAALAM WA KAMATI YA AIKNA MWAKYEMBE KUWA WASHIRIKI WA UTAPELI WACHUKULIWE HATUA NA HADI LEO "BADO WANAPETA" KERO NA VILIO VYA WALALAHOIKWENYE SIMU/SMS/E-MAIL ZITABADILISHA KITU GANI?
KADRI 2010 INAVYOJONGEA NDIVYO KADRI VITUKO VINAVYOONGEZEKA.NA TUTASHUHUDIA MENGINE MENGI.

7 Sept 2009


Unaweza kupatwa na hasira nikikuambia kuwa wewe (na mie) kwa namna flani tunahusika na kushamiri kwa biashara ya filamu za ngono, au kwa lugha mwafaka sekta ya filamu za ngono.” Najua utakuwa tayari kushika kitabu kitakatifu kuapa kwamba kamwe hujawahi kujihusisha na “uchafu wa aina hiyo.”

Katika sehemu ya pili ya kipindi cha BBC2 nilichokizungumzia wiki iliyopita kuhusu Utandawazi na Filamu za Ngono kumebainishwa mambo ambayo kwa hakika yanatuhisisha wengi wetu na kukua kwa sekta ya filamu za ngono. Tukiweka kando namna tunavyohusishwa kwa kuwa wateja wa makampuni yanayonufaika kwa ushiriki wao katika sekta hiyo (kwa mfano makampuni ya simu za mikononi, vituo vya runinga vyenye idhaa za filamu za ngono, mahoteli yanayotoa huduma ya “luku” ya filamu za ngono, nk) kuna uthibitisho kuwa baadhi ya taasisi za dini, hususan za Kikristo, zinawekeza fedha zao katika sekta ya ngono, japo sio moja kwa moja (directly).

Tunafahamu kuwa makanisa mengi yanategemea ufadhili kutoka mashirika mbalimbali ya kidini hapa Ulaya na huko Amerika.Lakini ili wafadhili hao waweze kuendelea na usamaria wema huo ni lazima wawekeze fedha zao katika mifuko au makampuni katika mfumo wa hisa.Mfano hai ulioonyeshwa katika kipindi hicho ni namna shirika moja kubwa la kidini huko Marekani lilivyowekeza mamilioni ya dola kwa mfumo wa hisa katika kampuni moja maarufu ya simu za mikononi, ambayo kama zilivyo kampuni nyingi za aina hiyo, hufanya biashara ya kuonyesha filamu za ngono kwa mfumo wa kulipia premium content.

Kwa lugha nyingine, misaada inayotolewa na shirika hilo inatokana na sehemu ya faida iliyopatikana kwa kuwekeza kwenye kampuni ya simu inayotengeneza sehemu ya faida yake kwa kuonyesha filamu za ngono. Naamini kwamba hadi hapo si vigumu kwako msomaji kuona uhusiano kati ya shirika hilo la kidini na filamu za ngono.

Lakini kuna namna nyingine ambavyo wengi wetu tunahusishwa na ustawi wa sekta ya filamu za ngono pasipo kuelewa waziwazi.Chukulia mfano huu mwepesi wa huko nyumbani. Vyama vingi vya kuweka na kukopa (Saccos) huzalisha faida zao kwa kuwekeza hisa kwenye mabenki, mifuko ya jamii (kama NSSF) au makampuni yaliyoandikishwa kwenye soko letu la “kichovu” la hisa.Kadhalika, Saccos hizo huwa na akaunti katika mabenki mbalimbali kwa vile sote tunafahamu kuwa kulaza mamilioni katika ofisi ya Saccos ni mithili ya kutangaza tenda ya kuvamiwa na majambazi.

Sote tunafahamu katika kutoa mikopo, mabenki mengi hayajihangaishi na maadili ya biashara ya mkopaji as long as ametimiza masharti ya kupata na kurejesha mkopo.Na hapo ndipo fedha zako kule Saccos zinapoweza kujikuta zikiishia kwenye akaunti ya mkopaji anayejishughulisha na filamu za ngono.

Lakini mfano mwepesi zaidi kwa mabenki ni akaunti zetu. Fedha tunazoweka katika akaunti hizo hazikai kama matangazo huko benki bali hutumika kibiashara aidha kwa kuwekeza au kukopesha.Na miongoni mwa wakopeshwaji hao ni haohao wanaojihusisha na filamu za ngono. Kwa huko nyumbani, fedha zako unazoweka benki zinaweza kabisa kuishia kwenye akaunti ya mkopaji mwenye gesti bubu wanakotengeza filamu za ngono kama sio gesti hiyo sio danguro bubu.

Njia nyepesi ya “kuua” makampuni ya filamu za ngono ni aidha kususia bidhaa zao (jambo ambalo ni rahisi kufikirika lakini almost impossible kutekelezeka kwa vile kilicho haramu kwako na kitakatifu kwa mwenzako) au kuyakatia mirija ya fedha, yaani kwa mfano kwa mabenki kukataa kutoa mikopo au kwa makampuni yanayowekeza huko kuacha kufanya hivyo au kwa biashara zinazotumia huduma za makampuni ya filamu za ngono kuachana na mtindo huo.

Ili hayo mawili ya mwisho yawezekane kunahitajika kitu kiitwacho uwekezaji wa kimaadili (ethical investment).Lakini hilo si rahisi kwa vile lengo kuu la uwekezaji, kama yalivyo maudhui ya ubepari, ni kutengeneza faida.Ni dhahiri basi kuzingatia maadili kutakwaza upatikanaji wa faida “rahisi” kama hiyo inayopatikana katika mahusiano ya kibiashara na makampuni ya ngono.

Na kwa masikini kama sie tunaotarajia misaada katika ustawi wa takriban kila sekta ya maisha yetu, ni dhahiri hatuna jeuri ya kuhoji msaada tuliopewa umepatikana kutokana na fedha za baishara ya filamu ya ngono au la.

3 Sept 2009


Kikwete awapa mafisadi ahueni

Asaini marekebisho yaliyopitishwa na Bunge kimya kimya

Ufisadi sasa si uhujumu uchumi

Kesi za ufisadi kuwa kiini macho?

RAIS Jakaya Kikwete amesaini kuridhia mabadiliko ya sheria zinazohusu rushwa na uhujumu uchumi, hatua ambayo wanaharakati wa vita dhidi ya ufisadi nchini wanaitafsiri kwamba ina lengo la kupunguza makali kesi za uhujumu uchumi na rushwa zinazowakabili baadhi ya vigogo nchini, RAIA MWEMA limeambiwa.

Katika hatua hiyo, inayoashiria kupunguza makali ya sheria zinazotumika kuendesha kesi za uhujumu uchumi na rushwa nchini, kesi ambazo baadhi zinaendelea kusikilizwa mahakamani zikiwahusisha waliowahi kuwa viongozi wa kitaifa, Rais Kikwete, Machi, mwaka huu, alisaini marekebisho hayo ya sheria yaliyopitishwa na Bunge katika kikao chake cha Januari mwaka huu.

Hatua hiyo inatokana na kuwasilishwa bungeni kwa Mabadiliko ya Sheria Mbalimbali, ndani yake kikiwamo kipengele kinachoingiza makosa ya rushwa katika Sheria namba 200 ya Uhujumu Uchumi ya mwaka 2002 (Economic and Organized Crime Act Cap 200 R.E. 2002).

Kwa kutia saini kwa Rais Kikwete kuridhia marekebisho hayo, rushwa sasa si kosa la kuhujumu uchumi.

Raia Mwema imefahamishwa kwamba mabadiliko hayo ya sheria yaliyopitishwa na Bunge Januari, yalisainiwa na Rais Jakaya Kikwete, Machi 12, mwaka huu na kutangazwa katika Gazeti la Serikali Machi 20, 2009. Habari kwamba Rais ameridhia marekebisho hayo kwa kutia saini zilifahamika hivi karibuni tu kwa wanaharakati wa vita dhidi ya ufisadi nchini.

Uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kwamba Mabadiliko hayo ya Sheria hiyo yamewashitua wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi ambao wanasema wakati sheria hiyo inapitishwa walipata nafasi ya kuchangia maoni, hali ambayo haikujirudia wakati wa kuifanyia mabadiliko.

“Tulikuwa tunafikiria Serikali iongeze makali katika sheria ili tuweze kuwadhibiti zaidi mafisadi na wahujumu uchumi, badala yake sasa tunalegeza sheria ili kuwasaidia, ” alihoji mdau wa mapambano dhidi ya ufisadi aliyeko serikalini ambaye anasema ameshitushwa na mabadiliko ya sheria hiyo.

Mabadiliko hayo yamo katika kifungu cha 38 na 39 cha Sheria namba 3 ya Mabadiliko ya Sheria Mbalimbali ya mwaka 2009, kifungu kinachofuta kifungu cha kwanza na cha pili katika jedwali la kwanza la makosa ya uhujumu uchumi kinachoingiza makosa ya rushwa na ufisadi.

Vifungu vilivyofutwa vilikuwa vinasomeka hivi:“Mtu yeyote atakuwa ametenda kosa (la uhujumu uchumi) ikiwa atakuwa ametenda kosa chini ya Sheria ya Kuzuia Rushwa” na “atakuwa ametenda kosa (la uhujumu uchumi) ikiwa atakuwa ametenda kosa la rushwa zaidi ya makosa yanayotajwa katika kifungu cha nne cha Sheria ya Kuzuia Rushwa.”

Kuondolewa kwa vifungu hivyo kunatoa nafuu kubwa kwa watu ambao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa makosa ya ufisadi, lakini pia mabadiliko hayo yanawavunja nguvu wapambanaji wa ufisadi ikiwa ni pamoja na vyombo vya dola vikiongozwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Habari za ndani ya Serikali zinaeleza kwamba hakuna uhakika wa moja kwa moja kwamba TAKUKURU ilishirikishwa katika mchakato wa kuifanyia mabadiliko sheria hiyo ambayo ndiyo imekuwa kwa muda mrefu msingi wa mashauri mengi inayopeleka mahakamani na kwa ajili hiyo marekebisho hayo yanagusa moja kwa moja utendaji kazi wa kila siku wa taasisi hiyo inayopigana dhidi ya rushwa nchini.

“Kama TAKUKURU wameshirikishwa basi itakuwa ni juu juu sana, lakini ninavyofahamu ni kwamba hawajashirikishwa katika hili bali Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliandaa muswada na kuupeleka bungeni kimya na wabunge wetu bahati mbaya sana hawakugundua hilo,” ameeleza mdau mmoja muhimu wa mapambano dhidi ya rushwa.

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Dk. Edward Hosea, hakuweza kupatikana kuzungumzia Mabadiliko hayo ya Sheria yanayoipunguzia ofisi yake ‘makali’ kutokana na kile Raia Mwema ilichoambiwa ya kuwa amekuwa na vikao na kufanya kazi za nje ya ofisi.

Mabadiliko hayo ya Sheria ndogo ndogo yaliwasilishwa bungeni yakiwa na marekebisho katika sheria mbalimbali 11 ikiwamo hiyo ya uhujumu uchumi na inawezekana kwamba wabunge wengi walikosa nafasi ya kupitia sheria zote zilizoguswa na mabadiliko hayo.

Sheria nyingine zilizounganishwa katika muswada huo ambao tayari umekuwa sheria ni pamoja na ya Administrator-General (Powers and Function) Act, ya Usajili wa Vizazi na Vifo, ya Chuo cha Sheria (Law School of Tanzania), Utumishi wa Umma, Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Afya, National Prosecution Service Act, Sheria ya Uchawi, Penal Code, Sheria ya Leseni za Usafirishaji na Sheria ya Ardhi.

Madhumuni ya awali ya kutungwa kwa sheria ya rushwa yalikuwa ni pamoja na kukuza na kuchochea utawala bora na kutokomeza rushwa na ufisadi kwa kutoa msingi wa kitaasisi na kisheria ambao ni muhimu katika mapambano hayo.

Mabadiliko haya yamekuja baada ya hatua kadhaa za Serikali ya Awamu ya Nne iliyofungua, baada ya muda mrefu, kesi kadhaa, zikiwagusa vigogo mbalimbali, karibu zote zikitumia kipengele cha makosa ya uhujumu uchumi ambacho kilisababisha wengi wao kukwama kupata dhamana.

Miongoni mwa walioshitakiwa kwa makosa hayo ni pamoja na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, mawaziri wa zamani, Daniel Yona na Basil Mramba na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha kwa muda mrefu, Gray Mgonja.

Mbali ya viongozi hao waandamizi, kuna mlolongo wa watuhumiwa wengine wa ufisadi ambao TAKUKURU imewashitaki kwa kutumia Sheria ya Uhujumu Uchumi, wakiwamo watuhumiwa wa EPA na ujenzi wa majengo pacha ya BoT, wote wakibanwa na sheria hiyo katika kupatiwa dhamana.

Wakati kesi hizo zikifunguliwa hasa baada ya vigogo kuanza kupandishwa kizimbani, baadhi ya watu walisema kwamba kesi hizo zimefikishwa mahakamani kama njia ya kufunika baadhi ya mambo ya ndani ya serikali.

Japo baadhi ya Watanzania walifurahia hatua hiyo ya Serikali kufikisha mahakamani baadhi ya vigogo, kumekuwa na maoni kwamba hakukuwa na mantiki ya kuwatia nguvuni watu ambao maamuzi yao yalikuwa ni ya kimchakato na kwamba kesi hizo zilikuwa ni kama mzaha katika utendaji kazi wa serikali.

“Nashangaa ninyi mnafurahia (vyombo vya habari).. Tena inaelekea kila mara wanapopelekwa mahakamani mlikuwa mnajulishwa mapema. Huu ni mzaha. Ni masuala ya kisiasa. Ni kesi zilizojaa siasa. Ukitaka kuwashitaki watu kama hawa basi itabidi ama ushitaki baraza la mawaziri au kundi zima la makatibu wakuu wa wakati huo,” alisema msomaji mmoja wa Raia Mwema.

Aliongeza: “ Haya ni matumizi mabaya ya sheria kwa maslahi ya kisiasa. Nadhani hizi ni jitihada za kufunika kesi nyingine nyeti. Nia ni wananchi wazisahau hizo.

Mramba, Yona na Mgonja, walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu wakishtakiwa kwa makosa ya kutumia vibaya madaraka na kuisababishia Serikali hasara ya Sh 11,752,350,148 kutokana na kile kilichodaiwa mahakamani kwamba walitumia madaraka vibaya kwa kusababisha kusamehewa kodi Kampuni ya M/S Alex Stewart (Assayer) Government Business Corporation.

Makosa yote hayo yaliegemea zaidi katika Notisi za Serikali (GN) zilizotangazwa kati ya mwaka 2003 na 2005, notisi ambazo ndizo zilihalalisha msamaha wa kodi kwa kampuni ya M/S Alex Stewart (Assayer) Government Business Corporation.

CHANZO: Raia Mwema

1 Sept 2009




Jana nilibahatika kuangalia kipindi flani cha kuvutia katika kituo cha runinga cha BBC2.Mada kuu ilikuwa ni namna makampuni makubwa, katika jina la utandawazi, yanavyosaka faida kupitia biashara ya ngono.Tangu mwanzo wa kipindi hicho ilionekana bayana kwamba kuna mahusiano ya karibu, japo yasiyo waziwazi, kati ya makampuni yanayotengetengeneza filamu za ngono na makampuni ya biashara nyingine katika nyanja zisizohusiana na ngono.

Kwa mfano, hoteli nyingi zina huduma ya idhaa (channels) za kulipia kadri inavyoangalia zinazoonyesha ngono kwa wateja wanaohitaji.Kwa namna utaratibu huo ulivyosambaa sehemu nyingi ulimwenguni ni dhahiri biashara hiyo ina faida nono.

Mfano mwingine ni kwa makampuni ya simu za mikononi.Japo jambo hilo linaweza kuonekana geni huko nyumbani, takriban makampuni yote makubwa ya simu za mikononi yana huduma zinazomwezesha mteja kuchungulia kile kinachojulikana kama ngono nyepesi (soft-core porn).

Lakini kama kuna mahala ambapo biashara ya filamu za ngono imeshamiri vilivyo basi ni kwenye mtandao wa kompyuta yaani intaneti.Ni kutokana na kushamiri kwa filamu za ngono kwenye intaneti, hususan huduma zinazowezesha watumiaji kuweka filamu (uploading) wao wenyewe,kumekuwapo hisia kwamba intaneti “itaua” makampuni ya filamu za ngono.

Watetezi wa hoja hiyo wanadai kuwa urahisi, kwa maana ya gharama na access, wa kuona filamu za ngono kwenye intaneti unaweza kabisa kupelekea wateja wazoefu wa filamu za ngono kuacha kununua filamu hizo madukani kwa vile zinapatikana (mara nyingi pasipo kulipia senti moja) mtandaoni.

Wapinzani wa hoja hiyo wanadai kuwa kama ambavyo watu hawaachi kwenda hotelini au migahawani kwa vile tu wanaweza kujipikia nyumbani ndivyo ambavyo filamu “halisi” za ngono madukani zitakavyoendelea kuvutia wateja licha ya upatikanaji wake kirahisi mtandaoni.

Kuna hoja ya ziada kwamba wakati filamu “halisi” za ngono hutengeneza kwa kuzingatia ubora wa hali ya juu katika studio zilizo tayari kwa shughuli ya aina hiyo, nyingi ya filamu za “ridhaa” kama hizo zilizotapakaa mtandaoni zina ubora duni. Lakini hoja hiyo inavutia upinzani mwingine (kutoka kwa watetezi) kwamba nyingi ya filamu za “ridhaa” mtandaoni zina uhalisia zaidi, kwa mfano pale wapenzi wanapoamua “kuweka mambo yao binafsi hadharani” mtandaoni. Watetezi hao wanakwenda mbali zaidi na kudai kuwa filamu za “ridhaa” mtandaoni zina ladha mithili ya “kupiga kozi” (u-peeping tom).

Mfano mwingine ulioonyeshwa kwenye kipindi hicho ni namna makampuni makubwa ya ku-process malipo ynanavyorahisisha upatikanaji wa huduma ya filamu za ngono.Na hili ni maarufu zaidi kwenye tovuti za ngono mtandaoni. Mara nyingi, ili mtumiaji aweze kulipia huduma hiyo analazimika kutumia credit au debit card yake katika tovuti maalumu za ku-process malipo. Kwa mara nyingine, ni dhahiri kwamba kushamiri kwa makampuni ya aina hiyo kunaashiria faida nono kwao kwani kinyume chake yasingekubali “fedha chafu”.

Kilichonigusa zaidi katika kipindi hicho ni namna filamu za ngono, whether zile halisi kutoka studio au hizo za “ridhaa” mtandaoni zinavyochangia kubadili sexual behaviours sehemu mbalimbali duniani.Na pasipo kutarajia, mtangazaji alitoa mfano wa athari za filamu hizo kwa sexual behaviours huko nyumbani. Guess what? Ni kile ambacho wengi wanakihusisha na u-Magharibi: tendo la ndoa kinyume cha maumbile! Kwa mujibu wa kipindi hicho, wataalam wetu wa sexual behaviours huko nyumbani wanaamini kwamba filamu za ngono zimechangia sana kulifanya tendo la ndoa kinyume cha maumbile kuwa mithili ya jambo la kawaida (mainstream).


Binafsi nadhani moja ya eneo lililopewa attention pungufu tunapoangalia athari za mageuzi mbalimbali yaliyojitokeza miaka ya 80 (1980s) ni mageuzi katika tabia za kujamiiana.Hivi ni mie pekee ninayeshtushwa na kukua “kwa ghafla” kwa interest kwenye umbile halisi la mwanamke wa Kiafrika? Na swali la nyongeza, je kwanini “ghafla”, ashakum si matusi, makalio ya mwanamke wa Kiafrika yaonekane kuwa na umuhimu wa kipekee katika ku-describe shepu yake? Wapo wanaohusisha interest hiyo na kukua kwa interest kwenye tendo la ndoa kinyume cha maumbile.

La kusikitisha ni kwamba hakuna namna tunavyoweza kukabiliana na nguvu kubwa ya utandawazi. Filamu za ngono zinazoendelea kuonyeshwa katika “Drive-Inn, Avalon na Empress za uswahilini” zinazidi kusambaza tabia ambazo kimsingi zinakinzana na maadili yetu. Kipindi nachokizungumzia kilionyesha namna vijana flani huko Ghana walivyoishia kuambukizwa ukimwi baada ya kujifunza “mbinu za kisasa za kufanya tendo la ndoa” mtandaoni.Ni dhahiri pia kuwa filamu za ngono zinazoonyeshwa kwenye “majumba yasiyo rasmi ya filamu za ngono” (tukiweka kando mfumuko wa kasi wa madanguro bubu) unazidi sio tu kubomoa mila na desturi zetu bali pia kutapakaza maambukizo ya gonjwa la ukimwi.

Pengine mahala mwafaka kubaini kuwa tendo la ngono kinyume cha maumbile limekamata kasi katika jamii yetu ni pale kwa Dada Dina.Lakini hiyo si kusema kwamba suala hili linajadiliwa kwa uwazi zaidi. Kama kawaida yetu, baadhi ya mambo yanaonekana kama mwiko kuyajadili hata kama yanaathiri jamii yetu. Yayumkinika kuhitimisha kuwa unafiki ni kikwazo kikubwa kwa mijadala ya aina hiyo. Wapo “waliobobea” kwenye matendo kama hayo lakini aidha wanakwazwa na “kuonekana wa ajabu” iwapo watadiriki kuzungumzia ishu ya namna hiyo au “wanaruka kimanga” pale wanapoulizwa licha ya umahiri wao.

TAFAKARI!

28 Aug 2009


Pengine ushasikia kuhusu Perfect Storm.Sijui tunaweza kuiitaje kwa Kiswahili lakini kwa kifupi ni hivi: kadri idadi ya watu inavyoongezeka duniani,mahitaji ya chakula,maji na nishati nayo yanaoongezeka.Pasipo jitihada za makusudi na za haraka kufanyika,inatarajiwa kufikia wakati flani bei za vyakula zitakuwa hazikamatiki,watu lukuki watakabiliwa na njaa kutokana na uhaba wa chakula,na idadi wa "wakimbizi" kuongezeka kutoka mahala kwenye uhaba kuelekea kwenye nafuu (ambayo itapelekea sehemu hizo zenye nafuu nazo kujikuta zikishindwa kuhimili mahitaji ya "wakimbizi" hao).


Kwa mujibu wa takwimu zilizopo,inatarajiwa kwamba kufikia mwaka 2030 idadi ya watu duniani itafikia bilioni 8 kutoka bilioni 6 ya sasa,mahitaji ya chakula yatapanda kwa asilimia 50,mahitaji ya maji yatapanda kwa asilimia 30 na ya nishati nayo asilimia 50.

Kama ilivyo kawaida ya majanga makubwa,nchi masikini huwa waathirika wakubwa zaidi kutokana na uwezo duni unaochangiwa pia na viongozi mafisadi walio maarufu zaidi kwa ngonjera kuliko vitendo.Kabla ya hiyo 2030,tayari kumeanza kujitokeza kinachoitwa "ukoloni mpya wa ardhi" ambapo baadhi ya makampuni ya katika nchi zilizoendelea yamekuwa yakinunua ardhi kwa kasi katika nchi masikini.Hali hiyo inajionyesha zaidi huko Ulaya Mashariki,lakini kuna kila dalili kuwa upepo unaelekea kwenye "shamba la bibi",yaani bara letu la Afrika.Urahisi wa Afrika unachagizwa zaidi na mitizamo mifupi ya baadhi ya viongozi wetu kuwa hatuwezi kuendelea pasipo ushiriki wa "wawekezaji" katika mipango yetu ya maendeleo (kana kwamba "wawekezaji" hao ni wazalendo wenzetu).

Itakumbukwa kuwa miezi michache iliyopita viongozi wetu waliwashawishi "masikini wa ardhi" kutoka Saudi Arabia kuja kuwekeza Tanzania huku wakihakikishiwa umilikishwaji ardhi wa muda mrefu.Nawaita Wasaudi "masikini wa ardhi" kwa vile asilimia kubwa ya nchi za Ghuba,Arabia na Mashariki ya Kati zina uhaba mkubwa wa ardhi ya kilimo (sehemu kubwa ni jangwa) japo wana utajiri wa mafuta.Tatizo sio kuwakaribisha Wasaudia au Makaburu,bali ni udhaifu sugu tulionao kwenye udhibiti wa raslimali zetu.Uzoefu tulionao katika namna madini yanavyokombwa kwa pupa na " wawekezaji" huku tukiambulia mrahaba " cha mtoto" ambao asilimia kubwa unaishia mifukoni mwa mafisadi,ni dhahiri kukodisha ardhi kwa wageni kutapelekea kuiweka rehani nchi yetu,achilia mbali wakulima kuporwa ardhi yao kama inavyoshuhudiwa kwenye maeneo yenye madini.

2005 CCM iliahidi Maisha Bora kwa Kila Mtanzania,lakini kabla hatujapewa tathmini ya utekelezaji wa wimbo huo,kunakuja hadithi nyingine ya Kilimo Kwanza.Huu ni usanii wa kisiasa.Kilimo Kwanza mwaka mmoja kabla ya uchaguzi?Kwanini haikuwa kwenye Ilani ya 2005?Na kwa aliyepata muda wa kusoma kilichomo kwenye "kibwagizo" hicho cha Kilimo Kwanza atabaini kuwa ni muendelezo uleule wa kupiga risasi kisha kulenga (shooting then aiming).Yaani,watu wanakurupuka na mawazo ya ajabu ajabu,yanashindikana kisha zinaanza semina elekezi za kujadili kwanini mkakati ulishindwa.

And these people can't be serious kwa vile wakati wanakuja na Stimulus Package (sijui imeishia wapi) "walisahau" kuwa kilimo bado ni uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania,with exception of mafisadi ambao uti wa mgongo wa uchumi wao ni ufisadi.

Ni katika mazingira hayo tunalazimika kujiuliza itakuwaje hapo 2030 tunapotarajia hiyo Perfect Storm.Of course,sie tushazowea storms mbalimbali miaka nenda miaka rudi.Tunaambiwa taifa letu changa lakini tunamudu kuongeza maradufu mishahara ya wabunge huku walimu wakitishia kugoma kutokana na madai yao ya malimbikizo ya mishahara yao kiduchu.

Kitakachotunusuru ni kudra za Mwenyezi Mungu pekee kwa vile sote tunajua nini kitatukumba come hiyo Perfect Storm tukiwa na wababaishaji kama hawa waliopo sasa.

24 Aug 2009


EITHER ex-prime minister Edward Lowassa or ex-attorney general Andrew Chenge were on the short list to take over the Speaker’s seat in the National Assembly had the attempted ouster of incumbent Samwel Sitta succeeded last week, THISDAY can reveal today.

According to a senior Chama Cha Mapinduzi (CCM) official privy to details of the reported plotting and scheming during last week’s high-level CCM meetings in Dodoma, a good number of ruling party regional branch chairmen had been "compromised" to push for either of the two ex-government leaders to assume the Speakership after Sitta’s envisaged ejection.

It has been confirmed that the entire plan to remove Sitta and put in place a smooth replacement system was hatched and finalized during a series of secret meetings in Dodoma, Dar es Salaam and Mbeya ahead of the Dodoma meetings involving CCM’s central committee and national executive committee (NEC).

”The plotters not only sought Sitta’s removal as Speaker and expulsion from the party...they also took it a step further and earmarked who exactly should immediately replace him (as Speaker),
” the CCM official, also a NEC member, said.

He continued: ”The names that came up were Lowassa or Chenge. But would either of them have actually agreed to have their names nominated for election as Speaker, had the plot to remove Sitta succeeded? Of that I am not sure.”

It is also unclear if either Lowassa or Chenge were even aware that they were in line to replace Sitta at short notice, if it had come to that.

Lowassa was forced to resign from the post of prime minister in February last year, after being heavily implicated by a parliamentary team probing the infamous Richmond power generation scandal.

Hardly a couple of months later, Chenge - the country’s attorney-general for ten years until 2005, and thereafter a senior Cabinet minister - was similarly compelled to quit his government position after being named as an official suspect in the radar deal corruption investigation.

While both have yet to be formally charged with criminal wrongdoing, they remain active as members of both the parliamentary backbench and the various CCM caucuses.

Apart from Lowassa and Chenge, another name floated as a potential replacement for Sitta is the incumbent deputy Speaker of the National Assembly, Anna Makinda, who political insiders say is seen as more inclined to ”defend CCM interests” in parliament.

The Speakership of the National Assembly is seen as a powerful and pivotal post within the ruling party and the national political scenario as a whole.

As such, according to various CCM insiders, Sitta’s continued occupation of that post and anti-corruption stance represents a perceived large thorn in the flesh of a powerful group of corrupt politicians with vast personal business interests, who more or less control the party at will through its secretariat.

According to one ruling party insider speaking to THISDAY:"These politicians are now desperate to also control the parliament...and they regard the removal of Sitta as a key necessity towards that goal.”

The said group of politicians is believed to number about five or six, most of them incumbent members of parliament whose public images have in recent years become heavily tainted by serious allegations of grand corruption.

”They want to use the Bunge to clean up their own battered images, so that they emerge smelling like roses ahead of next year’s general elections,” said another CCM insider.

According to THISDAY findings, the plot to remove Sitta from the post of Speaker is understood to have involved large sums of money exchanging hands within the CCM-NEC ranks.

It is also understood that party leaders at various levels within mainland Tanzania were targeted to be roped in, while emissaries were also dispatched to Zanzibar to garner similar CCM grassroots leadership support for the plot over there.

Sources say some NEC members received between 3m/- and 5m/- "to ensure that the plan to get rid of Sitta succeeded."

Speaker Sitta was on Saturday accorded a hero’s welcome on returning to his Urambo parliamentary constituency in the wake of the failed plot to oust him. He vowed to soldier on with his work in the National Assembly, to ensure greater transparency and accountability in government.

SOURCE: ThisDay

20 Aug 2009


Labda CCM imekaa madarakani kwa muda mrefu mno hadi imefikia hatua ya kusahau wajibu wake. Pengine ni matokeo ya mafisadi kushika hatamu ndani ya chama hicho, au pengine ni CCM imesharidhika kwamba Watanzania wamezowea kunyanyaswa, kupuuzwa na kuchezewa kama watoto wadogo pasipo kuchukua hatua yoyote.

Najiuliza hivyo baada ya kusoma habari kwamba chama hicho tawala “kimechimba mkwara mzito” kwa baadhi ya viongozi na wanachama wake wanaodiriki kunyooshea vidole ufisadi na mafisadi.Ungetegemea CCM ingekuwa mstari wa mbele kuhamasisha mapambano dhidi ya ufisadi na mafisadi kwa vile so far ndio kikwazo kikubwa katika utekelezaji wa kauli-mbiu Maisha Bora kwa Kila Mtanzania. Lakini kwa vile mafisadi ni watu muhimu sana kwa chama hicho, jaribio lolote la kuwakemea ni sawa na kusigina katiba ya CCM.

Kana kwamba kushindwa ku-meet matarajio ya wapigakura (waliokipa dhamana chama hicho mwaka 2005 kututawala tena) sio jambo linaloinyima CCM usingizi, chama hicho kimeanza kuonyesha dalili za udikteta tukirejea kauli zake nzito za hivi karibuni. Siku chache zilizopita, kiongozi mkongwe na miongoni mwa waasisi wa CCM,Kingunge Ngombale Mwiru,aliwakemea viongozi wa Kanisa katika lugha inayoweza kutafsiriwa kuwa ni ya kidikteta,alipoonyesha dhahiri kukerwa na kitendo cha viongozi wa dini kutumia uhuru wao wa kikatiba kutoa maoni yao kuhusu hatma ya taifa letu.Na sasa tunaambiwa kwamba chama hicho kimeamua kuwafunga midomo wabunge wake wanaojaribu kuwakemea mafisadi, sambamba na kunyamazisha kelele dhidi ya tuhuma zinazomwandama Benjamin Mkapa, Rais wa Awamu ya Tatu.

CCM imefikia hatua ya kulitukana Bunge la Jamhuri ya Muungano na kulifananisha na kikundi cha vichekesho cha Ze Komedi.Jaribu ku-imagine kauli kama hiyo ingetoka kwa mtu kama Dkt Wilbroad Slaa au Zitto Kabwe! Ni dhahiri watu kama George Mkuchika, anayechanganya majukumu yake ya u-Katibu Mwenezi wa CCM na u-Waziri wa Habari, au Yusuph Makamba wangekurupuka na vitisho kuwa “wapinzani wanaikosea heshima Katiba ya Jamhuri.” Kulilinganisha Bunge na Ze Komedi kwa vile tu limejikongoja kuruhusu sauti zisizopendeza masikioni mwa mafisadi na watetezi wao ni kitendo kinachoashiria utovu wa nidhamu wa hali ya juu.

Bunge la Jamhuri ya Muungano ni taasisi nyeti na inayopaswa kuenziwa na kuheshimiwa na kila Mtanzania including hao wanaoifananisha na kikundi cha vichekesho. Kama unadhani kauli ya “Bunge ni mithili ya Ze Komedi” haina uzito, tafakari upya. Mtu anapokufananisha na mchekeshaji (comedian) anafikisha ujumbe kwamba hupaswi kuchukuliwa seriously. Kauli na matendo yake pia yanapaswa kuchukuliwa kama mambo yasiyopaswa kupewa umuhimu au kutekelezwa kwa vile ni ya “kusukuma muda” tu. Japo vichekesho vingi huwa na ujumbe uliofichika katika maneno au matendo ya kuchekesha, mara nyingi kauli au matendo hayo hayapaswi kuchuliwa seriously.

Kwa CCM kulifananisha Bunge na Ze Komedi inatueleza kwamba taasisi hiyo yenye jukumu la kutunga sheria za nchi haistahili kuchukuliwa serious katika kauli, maamuzi na matendo yake. Lakini hilo si geni kwa vile hata maamuzi ya baadhi ya kamati za Bunge, kama ile ya Mwakyembe, yameendelea kupuuzwa katika kile kinachothibitisha kuwa CCM imekuwa ikiliona Bunge kama genge la wachekeshaji,with exception of wabunge kama Kingunge,Serukamba,Mkuchika ,Lowassa,Rostam,Karamagi,Chenge na “wateule wengine wachache” wenye umuhimu wa kipekee kwa chama hicho.

La kusikitisha ni kwamba bado mamilioni ya Watanzania wenye akili zao timamu wataipigia kura CCM hapo mwakani irejee madarakani kuendeleza nyodo kama hizi.Na hicho ndicho kinawapa jeuri watu kama Mkuchika kusema lolote pasi hofu ya kukigharimu chama hicho ushindi hapo mwakani.CCM inajivunia knowledge yake kuhusu Watanzania kwamba ni kama wamezowea kupuuzwa (wao na baadhi ya wawakilishi wao wachache wanaopiga kelele Bungeni kutetea maslahi ya walalahoi),kunyanyaswa,kuburuzwa na kudanganywa kama watoto wadogo.

La kusikitisha zaidi ni namna uongozi wa juu (with exception of Makamba na Mkuchika wanaofahamika bayana wanaoelemea upande gani kati ya watetezi na wapinzani wa ufisadi) walivyo kimya japo kila siku wanasikika majukwaani wakiahidi Maisha Bora kwa Kila Mtanzania. Taarifa za vyombo vya habari kuhusu yaliyojiri kwenye vikao vya juu vya chama hicho zinatuthibitishia bayana kuwa uongozi wa juu wa CCM hauna dhamira ya dhati ya kukomesha ufisadi kwa vile badala ya kuwakemea wanaowakwaza wapambanaji dhidi ya ufisadi wanadaiwa kuleta ngonjera za “kujadili mambo ndani ya chama.”Yaani wanataka kutuambia hawajui kuwa ndani ya chama kuna watu kama Lowassa, Rostam, Chenge na wengineo ambao kwa namna yoyote hawako tayari kuruhusu mjadala huru dhidi ya ufisadi kwa vile wao ni watuhumiwa?

Ungetarajia busara za watu kama Mzee Ali Hassan Mwinyi ziwafumbue macho CCM kwamba kuzuia demokrasia katika kujadili mambo yanayowakera na kuwaumiza Watanzania kutapelekea kifo cha mende kwa chama hicho. Lakini pengine wanafahamu nguvu za mafisadi ndani ya chama hicho, na hivyo kuhofia kuwaudhi katika kipindi hiki ambacho CCM inawahitaji mafisadi more than ever ili iendelee kututawala.Wanatupuuza kwa vile wanajua hatuna jeuri ya kuwaadhibu kwa madhambi yao.

They could be right, though! However, they fooled us in 2005.They possibly will fool us again in 2010, but let them rest assured that they will never fool us forever. They are simply buying time to finish digging their own graves.


14 Aug 2009


Kingunge Ngombale Mwiru ni mkingwe,kiumri,kisiasa na kimadaraka.Japo umri si kigezo muhimu cha kuwa na busara,ukongwe katika fani flani unatarajiwa kuambatana na busara.Lakini hali si hivyo kwa Kingunge.Kuna nyakati baada ya kifo cha Nyerere baadhi ya watu walitarajia kuwa Kingunge angefanikiwa kuendeleza mema ya Mwalimu hasa kwa vile tuliaminishwa kwamba mwanasiasa huyu (Kingunge) ana damu ya Ujamaa kiasi cha kuachana na mambo ya imani ya kidini.Tuliambiwa dini ya Kingunge ni Ujamaa.

Pamoja na mapungufu ya hapa na pale,Nyerere anaendelea kukumbukwa kwa jitihada zake za kujenga jamii yenye kukaribia usawa na kuchukia unyonyaji.Sijui Kingunge akifa tutamkumbuka kwa lipi zaidi ya kuzeekea kwake kwenye siasa pasipo tija na hili jukumu jipya alilojipachika la u-Baba wa Taifa wa Mafisadi.Kingunge ni mnafiki mkubwa kwa vile wakati anadai kuwa viongozi wa kanisa "wangeufyata" laiti Mwalimu angekuwa hai,sijui yeye Kingunge angemwambia nini anaposimama kidete kutetea mafisadi.

Haya ndio madhara ya kuviacha vikongwe madarakani hadi vinapoteza uwezo wa kufikiri.Na huyu ni mshauri wa kiongozi wa nchi!Kama uwezo wake binafsi wa kufikiri umefikia kikomo atawezaje kumshauri mtu mwingine,achilia mbali kiongozi wa nchi?

Kwanini adai waraka wa kanisa utawagawa Watanzania lakini akae kimya pale chama chake cha CCM kilipocheza karata-tatu ya kisiasa kilipoahidi (katika manifesto yake ya uchaguzi 2005) uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kwa Waislam?Binafsi,sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama ya kadhi iwapo mambo flani muhimu yatazingatiwa,lakini kwa uendeshaji wa mambo kwa mtindo wa zima moto,au pata potea,ni dhahiri uamuzi huo wa mahakama ya kadhi unaweza kulipeleka pabaya taifa.Narudia,tatizo sio uanzishwaji au kuwepo kwa mahakama hiyo,bali ni ubabaishaji wa viongozi wetu katika kushughulikia uanzishwaji na uwepo wake pasipo kuathiri umoja wa kitaifa.

Na kikongwe huyu (Kingunge) mbona yuko kimya hadi leo baada ya chama chake kusuasua katika utekelezaji wa ahadi hiyo ya uanzishwaji wa mahakama ya kadhi?Kama uamuzi wa CCM kutaja katika manifesto yake juu ya suala hilo ulikuwa hatari (kwa mujibu wa wanaodhani hivyo),kitendo cha chama hicho kurushiana mpira kila kinapoulizwa na waahidiwa (Waislam) kuhusu utekelezaji ni cha hatari zaidi.

Tatizo la Kingunge kuhusu waraka wa kanisa haliko kwenye kile anachodai "kuijua vizuri nchi yetu" bali wasiwasi wake kwamba pindi waraka huo ukitekelezwa kwa vitendo basi yeye na mafisadi anaowatetea watakuwa katika wakati mgumu.Kwa lugha nyingine,Kingunge anatetea maslahi ya tabaka alilomo na analoliwakilisha (mafisadi).

Hivi ni lini umewahi kumsikia Kingunge akikemea ufisadi?Hivi Kanisa lingetoa wapi wazo la kujana waraka huo laiti kikongwe hiki cha siasa kingesimama kidete kuendeleza harakati za Mwalimu kupambana na unyonyaji?Badala ya kutueleza yeye anafanya nini kuhakikisha nchi inakwenda vizuri anakimbil;ia kukosoa wengine kuwa wanataka kuipeleka nchi pabaya.

Halafu inakera zaidi kumskikia babu huyu akijifanya kama yeye ndio mwenye hatimili ya historia,mwelekeo na chochote kuhusu Tanzania.Eti anakemea wenzake "wanaodakia hoja pasipo kujua vema tumefikaje hapa..."Tumefika hapa tulipo kwa sababu ya watu kama Kingunge,wanafiki waliojifika kwenye ngozi wa kondoo wakati wa Mwalimu kumbe ni mbwa mwitu wa kifisadi waliokuwa wakisubiri Mwalimu aondoke kwenye ulingo wa siasa kisha watufisadi.

Kingunge ni mtu hatari sana,na asipodhibitiwa ataiingiza nchi katika machafuko.Kishajizeekea,hajali litakalotukumba kwa vile ashachuma vya kutosha na anamsubiri Muumba amrejeshe mbele ya haki (na huko atakuwa na maswali lukuki ya kujibu atapokutana na Mwalimu).Ni muhimu kwa wanaomlea kikongwe huyu wakamhurumia kwa kumpatia pumziko haraka,la sivyo "atazidi kulikoroga".

Mungu ibariki Tanzania na waangamize mafisadi na watetezi wao,hususan wale wanaotaka ligi
na wachunga kondoo wako.

11 Aug 2009


Kuna tamasha kubwa la kimataifa linaloendelea jijini Glasgow.Wenyewe wanaliita World Pipe Band Championships.Ni mashindano ya bendi za kupuliza filimbi kama zile za brass band (pipes).Kumejitokeza mgogoro wa kiplomasia baada ya Wakala ya Mipaka ya Uingereza (UK Border Agency) kuwanyima viza wanabendi ya kupuliza filimbi kutoka Pakistan.Licha ya bendi hiyo inayojulikana kama Lahore Piping Band,msafara wa wafanyabiashara kutoka Pakistan nao umenyimwa viza.Kinachochochea zaidi songombingo hilo ni ukweli kwamba Glasgow na Lahore ni miji pacha (twin cities).

7 Aug 2009



Kwa mfumo wa tarehe za "kwetu" tunaanza na tarehe kisha mwezi,tofauti na wenzetu wa kwa Obama ambao wanaanza na mwenzi kisha tarehe.Yaani,kwa hapa,na kama ilivyo huko nyumbani TZ,ni tarehe 07/08/09 japo kwa wenzetu wa US itaandikwa 08/07/09.Basi,leo mchana kulikuwa na tukio adimu katika uhai wa wengi.Kama inavyoonekana pichani juu,kuna muda saa na kaelnda ilisomeka 1-2-3-4-5-6-7-8-9,yaani saa 12 na dk 34 na sekunde 56 tarehe 7 mwezi wa nane mwaka 2009 (12:34:56 7/8/9).Ulikumbuka kuhusu tukio hili?

MHAMASISHA VITA DHIDI YA MAFUA YA NGURUWE NAYE AAMBUKIZWA....


Na the funny side ya "maadhimisho" hayo ni habari hapa Uingereza kwamba jamaa aliyetumika katika tangazo la "Wizara" ya Afya katika runinga kuhamasisha jamii dhidi ya mafua ya nguruwe (swine flu) nae ameambukizwa ugonjwa huo.Msanii Davidi McCusker (pichani juu).Hata hivyo,lililo dhahiri ni kwamba maambukizo hayo hayana mahusiano na ushiriki wa msaanii huyo David McCusker katika tangazo hilo.

6 Aug 2009


IMMIGRANTS who come to live and work in Scotland could have a better chance of earning full UK citizenship, it was revealed yesterday.

The Home Office unveiled plans for an Australian-style points systems for foreigners who want to settle in Britain.

Workers from overseas will receive extra points based on their skills and qualifications. Once they have enough points, they will be able to move to Britain permanently.

It also emerged yesterday that extra points will be given to migrants who settle in parts of the UK where population is set to fall - such as Scotland.

The move would build on the Fresh Talent Initiative, set up by former first minister Jack McConnell to let foreign students stay after graduation.

A Home Office spokesman said: "There are parts of the country where spaces in the workforce aren't being filled by UK residents and could very easily be filled by hard-working migrants."

Scottish Secretary Jim Murphy last night said he was "pleased" at the move.

He added:"Our need for a growing population is ranked alongside the need to recruit to occupations where we have a shortage."

SNP MP Pete Wishart gave the plans a cautious welcome. He said:"The Home Office must demonstrate the new points based immigration system is fit for Scottish purpose.

"Scotland's population and immigration requirements are completely different from the rest of the UK and this has to be recognised when points are added up."



Na Awila Silla, Singida

RAIS Jakaya Kikwete ametangaza vita dhidi ya askari wa usalama barabarani ili waweze kufanya kazi kwa kufuata sheria na kanuni za nchi.

Kikwete alitoa kauli hiyo nzito mkoani Singida alipozungumzia kero kubwa ya ajali nchini ambayo alisema inakwamisha juhudi za serikali kuleta maendeleo kwa wananchi.

"Na nyie watu wa usalama barabani manaendekeza urafiki na madereva wa nini badala ya kukagua gari mnazunguka nyuma ya gari na makonda kufanya nini? huku umeona kabisa gari bovu na dereva hana leseni, nawambia, safari hii naanza na nyie," alisema Rais akionyesha ukali

"Msinilazimishe sana niendelee kufoka kila siku wimbo umekuwa huo huo nimechoka jamani , Wizara mnafanya nini fanyeni kazi yenu fukuzeni hawa watu kama hawataki kufuata sheria warudi nyumbani kufua au wakafanye kazi nyingine" alisisitiza .

Mbali ya kauli hiyo nzito pia alisema haoni sababu ya kuendelea kufoka kuhusu baadhi ya matatizo ya ajali na badala yake aliitaka pia Wizara ya Mambo ya Ndani kuchukua hatua mathubuti kutatua matatizo hayo.

Alisema jukumu la sasa kwa Wizara hiyo ni pamoja na kuweka mpango mkakati wa utaratibu mpya wa sheria ya usalama barabarani juu utoaji leseni kwa madereva na kufanya marekebisho ya adhabu ambazo alisema zimepitwa na wakati.

Rais alisema hatua ambazo zinaweza kuchukuliwa chini ya wizara hiyo ni unyang'anywaji wa leseni bandia kwa madereva wasio na taaluma au wanaokiuka sheria na masharti ya usalama barabarani.

Kutokana na hilo aliitaka Wizara hiyo kuongeza ukali na kuondoa urafiki na ulegevu kwenye mambo yanayozuika ili kuboresha usalama wa barabara na kulinda uhai wa watu.

Akifafanua juu ya hilo Kikwete alisema licha ya matatizo mengi yanayojitokeza kwenye miundombinu hiyo, lakini utafiti unaonyesha kuwa asilimia kubwa ya ajali nyingi inatokana na matatizo ya kibinadamu ikiwemo uzembe wa madereva hao.

Kwa mujibu wa utafiti huo takribani asilimia 88 ya vifo hivyo kwa mwaka vilisababishwa na uzembe wa madereva,ulevi wa kupindukia na mwendo kasi.

Katika hatua nyingine alitoa mfano wa kusikitishwa na ajali mbaya ya basi la Kampuni ya Mohamedi iliyotokea hivi karibuni Wilayani Korogwe mkoani Tanga na kusababisha vifo vya watu vya zaidi ya watu 28,jambo alilokemea kutohitaji lisikia tena.

Alisema badala ya serikali kufanya ubinadamu mwema kwa wananchi lakini imekuwa ikilazimika kutuma salamu za rambirambi kwa vifo vinavyotokana ama kusababishwa na uzembe wa wachache huku ikiwa na majukumu mengi hatua aliyosema kuwa imechangia kuzorotesha maendeleo.

Aidha ametaja sababu nyingine kuwa ni pamoja na mashindano ya uendeshaji baina ya magari unaotokana na matajiri wa magari hayo hususani wa mabasi kutaka madereva hao kufika mapema kwenye vituo lengwa kwa kile kinachodaiwa cha kuwapa takrima ama posho nzuri nje ya mshahara anaopata.

Rais Kikwete alisema hayo jana kwenye uzinduzi wa miradi mikuu 3 ya barabara iliyofanyi kwenye eneo la Kititimo yenye urefu wa km 224 ya mikoa ya Singida, Manyara na Arusha (Singida, Babati na Minjingu) iliyoko kwenye mchakato wa ujenzi kwa kiwango cha lami kwa miaka 3.

CHANZO: Mwananchi

KATIKA KUMSAIDIA MHESHIMIWA RAIS,AMBAYE PIA NI AMIRI JESHI MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NA USALAMA,KIINI CHA TATIZO NI RUSHWA NA UFISADI.LAITI AHADI ZA 2005 ZA KUPAMBANA NA RUSHWA ZINGETIMIZWA NI DHAHIRI TATIZO LA AJALI ZINAZOSABABISHWA NA TRAFIKI KUTOTEKELEZA MAJUKUMU YAO IPASAVYO (BAADA YA KUSHIKISHWA KITU KIDOGO) LINGEPUNGUA KWA KIASI KIKUBWA.

RAIS ALIKASIRISHWA NA UFISADI KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM NA KUELEZA KUWA ANAWAJUA WAHUSIKA NA ANGEWASILISHA MAJINA YAO KWA MAMLAKA HUSIKA ILI WACGHUKULIWE HATUA.YOU AND I KNOW WHAT TRANSPIRED....JUST LIKE ALIVYOSEMA 2006 ANAWAJUA WALA RUSHWA NA KUWAPA MUDA WA KUJIREKEBISHA...SOUNDS LIKE AN UNDEFINITE DEADLINE.

KUFOKA AU KUONGEZA UKALI HAKUWEZI KUWA UFUMBUZI WA AJALI ZA KILA KUKICHA,ESPECIALLY PALE UKALI WENYEWE UNAPOKUWA NI MITHILI YA KUTEKELEZA WAJIBU TU.YEAH,KWANI WANAOKARIPIWA HAWANA MASIKIO AU MACHO YA KUMAIZI KUWA KUFOKA NA UKALI KWA RAIS HUKO NYUMA HAKUJABADILI CHOCHOTE?

4 Aug 2009


Mkutano mwingine wa Bunge umamilizika huko Dodoma huku danadana ziliendelea kuhusu ufisadi wa Richmond.Wakati Watanzania wakiendelea kumwagiwa "changa la macho",gazeti la Mwananchi linaripoti kuwa Mwanasheria Mkuu,Johnston Mwanyika,ambaye anahusishwa kwa karibu na ufisadi huo,anatarajiwa kustaafu kabla ya kuanza kwa kikao kijacho cha Bunge.Na akistaafu ndio habari imekwisha!Kama unabisha,jiulize kwanini uamuzi wa Lowassa,Msabaha,Karamagi na Chenge ndio ulikuwa mwisho wa kuhusishwa kwao na tuhuma zote zinazowakabili.Yaani mtu anaiba,au anawezesha wizi,au kwa lugha mwafaka ANAFISADI kisha anajiuzulu!Kwa lugha nyingine,anahitimisha utumishi wake uliotukuka kwa heshima zote.


Kwa wale wanaotarajia jipya kwenye kikao kijacho cha Bunge hapo Novemba wanapoteza muda wao.Ngonjera zitakuwa zilezile za "Bunge kuwaka moto kuhusu Richmond","Wabunge wampania Masha","Ngeleja kuwekwa kitimoto",na uzushi mwingine.Kikao kitaanza,wahehimiwa watalambishwa mamilioni yao ya mishahara (huku Watanzania wenzao waliokodoshwa kwa wahindi wa TRL wakizungungushwa kila kukicha na wawekezaji hao feki),na hatimaye kikao kitafikia ukingoni kwa ahadi kuwa "ishu x,y na z zitajadiliwa katika kikao kijacho"


Na bado itapojiri 2010 utaskia watu wazima na akili zao wamefungiwa baa au shuleni (na mgombea mmoja) ili wasinunuliwe na mgombea mwingine!Wawakilishi wetu wanafahamu kuwa hata wakizembea namna gani bado siasa itaendelea kuwa shughuli yenye mvuto mkubwa miongoni mwa wananchi kuliko jambo lolote lile.


Halafu tunaambiwa eti tuna BUNGE LENYE MENO!Labda ya plastiki!

31 Jul 2009


Ushaskia kuhusu political conmanship?Hebu soma kwanza habari ifuatayo kisha tujadili




Spika Sitta aomba ulinzi zaidi, adai nguvu ya mafisadi inahatarisha maisha yake

Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muuangano wa Tanzania sasa anahofia maisha yake kutokana na vitisho vya mafisadi

Spika Sitta aomba ulinzi zaidi, adai nguvu ya mafisadi inahatarisha maisha yake

Kizitto Noya, Dodoma na Boniface Meena

SPIKA wa Bunge Samuel Sitta ameiomba Serikali kumwongezea ulinzi kwa kuwa mafisadi wameongeza nguvu ya vita dhidi yake.

Spika Sitta alisema hayo alipokuwa akizungumzia tuhuma dhidi yake, zilizoripotiwa jana na baadhi ya vyombo vya habari (sio Mwananchi) kuwa anafanya njama kuchoma nyaraka za Bunge.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Spika anadaiwa kula njama ili kuchoma ofisi ya mhasibu wa Bunge ili kuharibu nyaraka muhimu zinazomhusisha na ubadhirifu wa fedha za Bunge.

Lakini Spika Sitta alijibu tuhuma hizo bungeni akisema taarifa hizo zina mkono wa wabaya wake, wenye lengo la kumchafua katika utendaji wake.

“Hivi kama kweli nataka kuficha faili la Bunge nani anaweza kunizuia humu ndani?” alihoji Spika Sitta na kuongeza:

“Hizi ni taarifa za wabaya wangu, wanachofanya ni kuziweka kwenye internet kwanza halafu wanazisambaza kwenye vyombo vyao maalum, magazeti manne; gazeti la Tazama, Tanzania Daima na mengine mnayoyaona," alisema Spika na kuongeza:

“Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba mnipe ulinzi zaidi, hii vita ni ngumu na kubwa sasa. Ulinzi mnaonipa naona hautoshi,” alilalamika Spika Sitta na kuwaponda wanaomwandama kuwa hata iweje, ataendelea kushinda ubunge jimboni kwake na kuwa Spika kama bado atakuwa hai mwakani.

Alifafanua kuwa fedha wanazopeleka maadui zake jimboni kwake Urambo zinasaidia kuimarisha maendeleo, lakini hazitomng’oa madarakani.

"Wananchi wangu wanajua ninachokifanya jimboni kwangu, hata wakipeleka pikipiki bado nitashinda," alisema Sitta.

Mara kwa mara Spika Sitta amekuwa akidai kwamba anaandamwa na mafisadi ambao wanataka aache kufichua maovu yao.

Spika Sitta alisema hayo muda mfupi baada ya kumaliza kutoa mwongozo kwa mbunge wa Micheweni (CUF), Shoka Khamis Juma, kwamba chama fulani kina tabia ya kununua shahada za kura wakati wa chaguzi.

Katika mwongozo wake, Spika alimtaka mbunge huyo kufuta kauli yake bungeni kwa kuwa ushahidi aliotoa kuthibitisha kauli hiyo ni dhaifu.

“Madai ya Shoka ni tuhuma kama tuhuma zozote zinazotolewa na wanasiasa wengine,” alisema.

Akifafanua kuwa Shoka ameshindwa kuthibitisha tuhuma zake kwa kuwa ametoa ushahidi wa magazeti ambayo sio yote yanaweza kuaminika.

“Magazeti yanaweza kuwa chanzo cha taarifa kwa wabunge katika kuchangia hoja zao, lakini sio kigezo pekee cha kumwezesha Spika kutoa mwongozo,” alisema Sitta na kuendelea:

“Hivyo mheshimiwa Shoka hawezi kulindwa na kifungu namba 63 (2), kwa mantiki hiyo namtaka kwa kanuni namba 63 (1) afute kauli yake humu bungeni kabla ya kumalizika kikao hiki cha Bunge”.

Juni 12 mwaka huu mbunge huyo wa CUF alitamka bungeni alipokuwa akiuliza swali la nyongeza kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimekuwa na tabia ya kuiba shahada za kupigia katika maeneo ambayo kinaona hakiungwi mkono.

Naibu Spika Anne Makinda ambaye alikuwa anaongoza kikao cha Bunge siku hiyo, alimtaka mbunge huyo athibitishe kauli yake, naye alifanya hivyo Juni 17, mwaka huu kwa kuwasilisha kwa Spika nakala za magazeti yaliyoripoti uchaguzi wa Jimbo la Busanda.

Hata hivyo, Spika Sitta alisema kwa kuwa hakuna ushahidi wa hukumu kuhusu tuhuma hizo, madai ya Shoka ni tuhuma kama tuhuma zingine zinazotolewa na wanasiasa majukwaani, hivyo kumtaka afute madai yake.




CHANZO: Mwananchi

Nadhani sasa kuna umuhimu wa kuangalia kama Spika huyu wa Viwango na Spidi bado anastahili kuendelea na wadhifa wake ambao ni wa nne kitaifa.Natoa hoja hiyo kwa vile kuna kila dalili kuwa Spika Samwel Sitta sasa anaogopa kivuli chake mwenyewe.




Ni hatari kwa kiongozi wa kitaifa kama Spika kutoa madai mazito namna hiyo pasipo kuwa na uthibitisho wowote.Hivi hao mafisadi wanaohatarisha maisha yake ni akina nani?Nauliza hivyo kwa vile kwa mujibu wa maelezo yake inaonyesha anawafahamu hata kwa majina.Sasa tunapokuwa na kiongozi wa kitaifa ambaye pindi maisha yake yanapokuwa hatarini (kama unaamini anachosema) anakimbilia kuomba aongezewe ulinzi hadharani,then hapo kuna mushkeli.



Ni hatari zaidi kumsikia Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,taasisi tukufu yenye jukumu la kutunga sheria za nchi,akiuliza bila aibui wala uoga "Hivi kama kweli nataka kuficha faili la Bunge nani anaweza kunizuia humu ndani?” You can't be serious,Mzee wa Spidi na Viwango!Yaani unatuambia kuwa kwa wadhifa wako unaweza kuficha nyaraka muhimu za Taifa (mfano faili la Bunge) na hakuna mwenye uwezo wa kukuzuia?Nadhani unatafsiri vibaya madaraka yako.Uspika ni nafasi inayoongozwa kwa taratibu na sheria,za nchi na za Bunge unaloongoza.Sasa unapotuambia kuwa hakuna wa kukuzuia ndani ya Bunge kuficha faili (ukijiskia kufanya hivyo) unatuaminisha kuwa aidha huelewi mipaka ya kazi yako,au unadhani Uspika ni kuwa juu ya sheria za nchi na Bunge,au kulewa madaraka.



Tukiwa hapohapo kwenye hoja yako ya "hakuna wa kukuzuia...",na tukiamini kuwa ni kweli hakuna wa kukuzuia,je utalalamika kuwa mafisadi wanakuwinda wakikuzushia zengwe kwamba umeficha nyaraka muhimu zaidi ya faili la Bunge?Sawa utasema wanakuandama lakini ushawapa hoja kwamba "ukitaka kuficha faili la bunge hakuna wa kukuzuia".Well,wao wanaweza kuja na tuhuma kubwa zaidi ya kuficha faili.Laiti busara zingetumika,ungeishia tu kukanusha tuhuma za kwamba una mpango wa kuchoma moto ofisi za bunge,na sio kukurupuka kudai una uwezo wa kuficha faili la bunge pasipo kuwapo wa kukuzuwia.



Ni rahisi kwa Spika kuomba aongezewe ulinzi (kwa kigezo kuwa ulinzi alionao sasa hautoshi) kwa vile gharama za kuongezewa ulinzi zitabebwa na walipa kodi na si kutoka mfukoni mwa Spika.Hoja hii ya Spika Sitta pia inaweza kufanya tujiulize iwapo licha ya nafasi yake ya Uspika,Mheshimiwa Sitta pia ni mtaalam wa mambo ya ulinzi wa viongozi,na review aliyofanya katika protection anayopewa hivi sasa imempelekea kuhitimisha kuwa ulinzi alionao hautoshi.Hii ni sawa na kuwadharau professionals wenye jukumu hilo,ambao naamini wangetambua mapungufu hayo kabla hata ya Spika Sitta kutamka hadharani.



Lakini twende mbali zaidi kwenye hili la "ulinzi alionao Spika hautoshi"Je anaweza kututhibitishia japo tukio moja linaloashiria kutotosha kwa ulinzi alionao hivi sasa?Yaani kutuhumiwa kuwa anataka kuchoma moto ofisi za bunge, na "maadui zake kumwaga fedha jimboni kwake" vimekuwa matishio ya kiusalama yanayotosheleza kufikia uamuzi wa kumuongezea ulinzi?



Kichekesho ni kwamba wakati Spika akimtaka Mbunge wa Cuf (Mheshimiwa Shoka Hamis Juma) afute kauli yake kwa kuwa "ushahidi aliotoa-katika madai kuwa kuna chama flani kinanunua shahada wakati wa chaguzi-ni dhaifu",yeye mwenyewe anafanya kilekile cha kutoa madai dhaifu kuwa nguvu ya mafisadi inahatarisha usalama wake ilhali hajaweza kutoa uthibitisho wowote zaidi ya "kauli za kisiasa" kuwa maadui zake wanapeleka pesa jimboni kwake ili asirejee bungeni.Ana uhakika gani kuwa hao anaowaita maadui zake si wananchi wenye dhamira ya kuleta maendeleo katika jimbo hilo pasipo kuwa na ajenda za kisiasa?Au Spika Sitta anataka kutuambia kuwa ni yeye tu aliye na hatimiliki ya kupeleka misaada katika jimbo hilo?Jamani,yaani hadi maendeleo ya jimbo yanafanywa kuwa mithili ya maamuzi ya mtu binafsi!?



Kuna mengi ya kujadili kuhusu kauli za Spika Sitta,lakini lililo wazi ni kwamba nafasi anayojipachika ya ukinara wa mapambano dhidi ya ufisadi ni sawa na political conmanship.Kwa lipi hasa?Sio Sitta huyu aliyempa "kifungo" Zitto Kabwe kwa "kosa" la kumkalia kooni Karamagi kuhusu Buzwagi?Sio Spika Sitta huyu aliyetishia kumfungulia mashtaka Dkt Wilbroad Slaa pale mbunge huyo wa Karatu aliposhikilia bango kuhusu ishu za ufisadi?Ni lipi alilofanya Samweli Sitta,kama Spika wa Bunge la Jamhuri au Mbunge wa Urambo linaloweza kumjumuisha kwenye kundi la vinara wa mapambano dhidi ya ufisadi?Yaani Watanzania wenzake kutamani jimbo la Urambo imekuwa ufisadi?Au mtu kutamani nafasi ya uspika imekuwa ufisadi?



Lakini kwa vile siasa zetu kwa sasa zinaruhusu mambo ya ajabu kabisa kutokea,kauli hizi za Spika Sitta hazitawahangaisha wenye dhaman ya uchambuzi wa kauli hatari kama hizi na kuchukua hatua za haraka.Ni business as usual,kauli imetolewa,siku imepita,and life goes on!



Na kwa vile magazeti yetu yako bize zaidi kuripoti habari badala ya kuchambua mantiki ya habari husika,yayumkinika tutasikia makubwa zaidi ya kauli hizi za wanasiasa wanaoogopa vivuli vyao wenyewe.Na kwa vile kilio,kicheko,kuchafua hewa na hata kukoroma kwa mwanasiasa kunatosha kuwa leading news kwenye magazeti yetu,basi tutarajia vimbwanga zaidi.



Trust me,tutashuhudia vituko vingi zaidi na zaidi kadri siku zinavyoyoyoma kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010.By the way,si ndio tunaelekea kile kipindi cha usanii wa kisiasa ambapo watu wazima hupiga magoti majukwani na wengine kutoa shikamoo hata kwa watoto wadogo alimradi wahakikishiwe kura?




30 Jul 2009


Tume huru inayochunguza uhusika wa Uingereza katika vita ya Iraki imetangaza kuwa itamhoji Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair.


Atakayenuna na anune,lakini ni dhahiri kuwa Rais wetu mstaafu ( wa awamu ya tatu),Benjamin William Mkapa,amekuwa akiandamwa na tuhuma za ufisadi wakati akiwa jengo takatifu la Ikulu.Hoja kubwa ya wanaomtetea Mkapa ni maneno kama "Mwacheni Mzee wetu apumzike".

Ni wazo zuri kutosumbua wazee wetu,lakini ingeleta maana kama wazee wote,na si Mkapa pekee,wangekumbukwa katika "maombi" hayo kuwa waachwe wapumzike.Mbona "busara" hizo hazijatumika kuwakumbuka wazee (halisi) wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki?Wamesumbuliwa,wamezungushwa,wametishiwa FFU,na kufanyiwa kila aina ya vituko...tofauti na Mkapa-ambaye hajaomba atetewe au ajitetee-wastaafu hao wanadai stahili yao halali.Hawakutumia ofisi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kununua japo vifusi vya kokoto au kuanzisha chama cha kuweka na kukopa,tofauti na Mkapa ambaye pamoja na mambo mengine anayetuhumiwa kujiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei ya kishkaji na pia kuhusishwa na kuanzisha benki.

Hivi njia bora zaidi ya kumwacha Mkapa apumzike ni kwa wanasiasa kumsafisha katika tuhuma za ufisadi zinazomkabili au kwa mahakama-chombo chenye mamlaka ya kikatiba kutoa haki-kufanya kazi hiyo?Wanasiasa wetu ni wavivu wa kufikiri.Wao ni binadamu,kwa maana hiyo leo wapo kesho hawapo-aidha kiuhai au kimadaraka.Utetezi wao leo unaweza kabisa kuondoka pindi nao watakapoondoka.Uzuri wa taasisi-kama mahakama-ni kwamba inastahili kuwepo kwa muda mrefu au hata milele ikibidi.Na hata ikibadilishwa,misingi yake itaendelea kuwepo.Kwa mantiki hiyo,namna pekee ya "kumwacha Mkapa apumzike" ni kumburuza mahakamani kisha haki itendekee huko.Kupuuza ushauri huu kunaweza kupelekea mzee huyo kuburuzwa kwa nguvu kwenda kujibu tuhuma zake wakati watetezi wake wa sasa hawako madarakani au nao wakiwa wanakabiliwa na tuhuma za kujibu.Hebu chukua mfano mwepesi kama huu.Unadhani Charles Taylor huko aliko anakumbuka flani aliyekuwa anamtetea?Hapo ni kila mtu anabeba mzigo wake.

Sawa,Tanzania sio Uingereza.Na ni kweli kwamba sio kila wafanyalo Waingereza lazima sie pia tulifanye.Lakini mfano wa Blair kufikishwa kwenye tume hiyo ya vita ya Irak inapswa kuwa changamoto nzuri kwa mamlaka zetu kuangalia umuhimu wa kuzingatia sheria na taratibu badala ya kuendekeza ushakaji na kubebana.By the way,si kila mtuhumiwa anayefikishwa kwenye vyombo vya sheria lazima aonekane ana hatia.

Mzee wetu Mkapa hatoweza kupumzika hadi sheria itakapochukua mkondo wake kumsafisha au kumtia hatiani.Kuzembea kufanya hivyo ni kuiachia "mahakama ya umma" (court of public opinion) kumhukumu pasipo kumpatia nafasi ya kujitetea.Na kwa vile mahakama hiyo ya umma haina utaratibu wa kukata rufaa pindi hukumu ikishatolewa,tuhuma dhidi ya Mkapa zitaendelea kuwepo hadi hapo......God knows!Kama wanaomtetea wanampenda kwa dhati (au hata kinafiki) basi ni vema wakamwepusha na hatari ya kuburuzwa mahakamani akiwa na mkongojo wake,say miaka 20 au zaidi kutoka sasa.

Binafsi siamini kuwa wanaomtetea Mkapa wanafanya hivyo kwa vile wanamheshimu sana au wanaamini kuwa tuhuma hizo ni uzushi.Badala yake,wanachelea kwamba wakiruhusu sheria ichukue mkondo wake,kesho wao nao watajikuta wakikabiliwa na hali hiyohiyo kama ya Mkapa.Waadilifu hawaogopi sheria bali wanaiheshimu na kuilinda,lakini wenye mapungufu kwenye maadili yao huiogopa sheria kama kirusi cha mafua ya nguruwe (japo huitumia kuwakandamiza wabaya wao).

Naamini pia kuwa ipo siku Mkapa na watuhumiwa wengine wa ufisadi watafikishwa kwenye vyombo vya sheria.Inaweza kuwa sio kesho au mwaka kesho lakini siku hiyo itafika.Na hapa nazungumzia mahakama za kidunia na sio ile ya kwenye wimbo niupendao wa "na kila mtu atatoa habari zake mwenyewe mbele ya Mungu,siku hiyo itafika...."

Kuendeleza ushkaji katika mambo yanayopaswa kushughulikiwa kisheria kunaweza pia kusambaza kirusi cha "ah mbona yule fisadi anatetewa na kusafishwa,what's wrong with me kufisadi pia?Si nami nitatetewa kama fisadi X..."Hapo tunafanya reproduction ya ufisadi katika jamii.Yayumkinika kuhisi kuwa kwa namna watuhumiwa wa ufisadi wa EPA,Richmond na maskandali mengine wanavyoendelea kuogopwa,tayari mafisadi hao wameshaambukiza virusi vya ufisadi kwa Watanzania wengine chungu mbovu.Thing is,kama wenye maamuzi wameamua kuhalalisha visivyo halali,then visivyo halali vinageuka kuwa halali.

Na kama kuna mzembe ataona wazo langu la kuchukua hatua dhidi ya Mkapa ni ukosefu wa nidhamu,then they can simply shove it up kunakostahili.


Kizitto Noya, Dodoma


SASA ni wazi kwamba sakata la Richmond limeingia katika hatua nyingine baada ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ofisi Rais kutangaza kwamba, Rais Jakaya Kikwete hahusiki kwa namna yoyote na kashfa hiyo ambayo inaendelea kulitikisa taifa kwa muda sasa.

Hatua ya Rais Kikwete kutotaka kuhusishwa na kashfa hiyo ya Richmond kunazidi kuibua maswali mengi kutoka kwa wananchi kwamba, ni nini hatima ya mjadala huo ambao unazidi kupamba moto kila kukicha nje na ndani ya Bunge.

Wakati Rais Kikwete akijivua kutoka katika sakata hilo, Kamati ya Nishati na Madini imetoa maazimio ya kupinga jinsi serikali inavyotekeleza maazimio ya Bunge kuhusu ripoti ya Richmond. Jana jioni Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, ilitoa taarifa ikimuepusha rais na kashfa hiyo.

"Tumepata kusema huko nyuma, na tunapenda kusisitiza kwa mara nyingine kuwa, Rais hana mkono katika Richmond na hata Ripoti ya Bunge iliyotolewa kufuatia uchunguzi katika suala hilo la Richmond, haikumhusisha Rais Kikwete," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa ya Ikulu, imetolewa huku Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba akidai kwamba, Rais Kikwete anahusika na Richmond kwa kuwa maamuzi yalifanyika chini ya serikali anayoiongoza.

Habari kutoka Dodoma zinadai kuwa kutokana na kusuasua kwa utekelezaji wa maazimio ya Bunge kutaka maafisa wa serikali waliohusika kwa njia moja au nyingine na mchakato wa kampuni hiyo kupewa zabuni Tanesco, wachukuliwe hatua.

Kundi mojawapo la wabunge limeeleza kutoridhishwa na ripoti ya serikali iliyotolewa bungeni hivi karibuni kuwasafisha. Kundi hilo limepanga kumchukulia hatua kubwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye ndiye kiongozi mkuu wa serikali bungeni, kutokana na kuwanusuru maafisa waliotuhumiwa kuhusika na kashfa hiyo.

Wakati kamati hiyo ikitoa msimamo huo, wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walikutana jana usiku katika Ukumbi wa Pius Msekwa kutafakari sakata hilo.

Ingawa tangazo la Mwenyekiti wa Bunge, Job Ndugai jana mchana halikueleza agenda za kikao hicho, vyanzo huru vya habari vililidokeza gazeti hili kuwa wabunge hao wangejadili ripoti ya Richmond na kuweka mkakati wa kuinusuru serikali.

Mjumbe wa Kamati ya Nishati na Madini ambaye hakutaka kutajwa gazetini akihofia kuvunja Kanuni za Bunge kwa kutoa siri za vikao, alisema kamati haikuridhishwa na ripoti ya serikali hasa katika suala la kuwasafisha Mkurugenzi wa Takukuru, Dk Edward Hoseah na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika.

"Kamati haikubaliani na ripoti hiyo hasa pale iliposema Dk Hoseah na Mwanyika hawana hatia. Tumekuwa na vikao kwa siku mbili jana (juzi), leo (jana) na bado tunaendelea kesho (leo),”alisema.

Alisema mapendekezo ya kamati ya Bunge kuhusu Richmond yalijitosheleza kimaamuzi na serikali ilitakiwa kuyatekeleza tu na sio kuendesha uchunguzi mwingine.

"Uchunguzi ulishafanywa na Bunge, serikali ilitakiwa kutekeleza tu. Ilikuaje ifanye tena uchunguzi kwa muda zaidi ya ule uliopangwa na Bunge badala ya kufanya utekelezaji?" alihoji.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, William Shelukindo na Makamu wake, Dk Harrison Mwakyembe hawakupatikana jana kuzungumzia suala hilo na simu zao za mikononi kutopatikana kabisa.

Mjumbe wa kamati iliyoundwa na Bunge kuchunguza suala la Richmond, Habib Mnyaa alikiri kuwa na taarifa ya kamati ya kisekta kukutana na kujadili ripoti hiyo, lakini akaeleza kuwa kikao hicho kilichokaa juzi na jana, kinamalizika leo.

"Kikao kimekuwapo, lakini hakijafikia maamuzi hayo unayosema," alisema Mnyaa akirejea hoja ya mwandishi wa habari aliyetaka kuthibitisha taarifa kwamba, kikao hicho kimejenga hoja ya kutokuwa na imani na serikali katika suala la Richmond.

Hata hivyo, habari nyingine zinadai kuwa kamati hiyo leo inatarajia kumweka kiti moto Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja ili awaeleze ni kwanini serikali imeshindwa kutekeleza mapendekezo ya Bunge.

Hata hivyo, mjumbe mwingine, Lucas Selelii alilieleza gazeti hili kuwa vikao vyote vilivyojadili Richmond, vimemaliza kazi na kuwasilisha hoja zake kwa spika wa Bunge Samuel Sitta ambaye leo atatoa mwongozo bungeni.

"Mjadala wa Richmond umemalizika na mambo yote kesho (leo) yako hadharani. Kamati ya kisekta imekaa na kuandaa taarifa ambayo amekabidhiwa spika wa Bunge leo (jana). Kikubwa jamii ijue kwamba, kamati iko makini, haimwonei wala kumpendelea mtu," alisema Selelii.

Alipotakiwa kuthibitisha kama amepokea hoja za kamati hiyo kuhusu Richmond na kwamba ataruhusu mjadala wake bungeni leo, Spika Sita alisema: "Haijanifikia bado".

Alifafanua kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini anatarajia kuwasilisha hoja za Kiwira na Richmond kesho, siku ambayo pia wenyeviti wa kamati za Miundombinu, Ardhi, Maliasili na Mazingira watawasilisha hoja zao.

Alibanwa zaidi aeleze kama endapo angeipata jana jioni angekuwa tayari kuiwasilisha leo kama ilivyoelezwa, alijibu:

"Hata kama nitaipata sasa, siwezi kuitable kesho (leo) kwani nahitaji muda kuisoma na kuielewa".

Awali mbung wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alisema suala la Richmond limeanza kuligawa taifa na njia pekee ya kuirudishia jamii imani na serikali, ni Rais kwa mamlaka ya kuwa mkuu wa nchi kuunda jopo la majaji kupitia upya hoja zote na kutoa maamuzi.

"Suala hili limeonekana kuigonganisha mihimili mikuu miwili ya dola, Bunge na Serikali, dawa yake sasa ili liishe, ni Rais kama mkuu wa nchi nasisitiza, mkuu wa nchi sio serikali kuunda tume ya majaji wapitie Maazimio ya Bunge, utekelezaji wa serikali na watoe maamuzi," alisema.

Alisema: "Inavyoonekana kila upande unavutia kwake, wakati Bunge likitaka serikali itekeleze mapendekezo yake ndani ya miezi mitatu, serikali imetumia karibu mwaka na nusu na bado inakuja na majibu ya kubabaisha.
CHANZO: Mwananchi

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.