24 Dec 2010


Majuzi,msomaji mmoja wa blogu hii alinitumia maoni ambapo pamoja na mambo mengine aliashiria kuwa nina chuki dhidi ya Rais Jakaya Kikwete.Msomaji huyo aliyejitambulisha kuwa mkazi wa hapa Glasgow alidai (namnukuu) "...I know you hate JK because whatever happens to him you have a negative view, even a tyre puncture...",yaani kwa Kiswahili,"najua unamchukia JK kwa vile chochote kinachotokea kwake wewe una mtizamo hasi,hata pancha ya tairi".Hii ndio mitizamo ya Watanzania wenzetu ambao licha ya kubahatika kuwa nje ya nchi,hususan nchi zilizoendelea kama hapa Uingereza,bado wana mitizamo mgando ambayo kwa kiasi kikubwa imechangia kutufanya hata miaka 49 baada ya uhuru kutamani mkoloni arejee.

Yah,huwezi kuwalaumu wanaotama mkoloni arejee japo mie si mmoja wao.Hivi tunawezaje kuelezea namna Watanzania wanavypelekeshwa kama watoto wadogo tena yatima siku chache tu baada ya Kikwete na CCM yake kupita huku na kule kuahidi neema,only for madudu and more madudu kuibuka kila kukicha?Unajua,angalau mkoloni alipotupelekesha alikuwa na excuse (japo isiyokubalika) kwamba yeye hakuwa Mtanganyika,na hakuwa na uchungu na nchi yetu.Na kwa wanaokumbuka vizuri somo la historia wanafahamu bayana kuwa ujio wa mkoloni ulikuwa kwa minajili ya kuendeleza nchi zao za asili,yaani kukwapua raslimali zetu kwa ajili ya viwanda vyao,kupata masoko ya bidhaa zao na eneo la makazi kwa nguvukazi ya ziada katika nchi hizo za wakoloni.Sasa ondoa neno mkoloni kisha weka neno FISADI,na yayumkinika kuhitimisha kuwa angalau mkoloni alikuwa na ajenda ya maendeleo huko kwao japo at our expense.Mafisadi nao wana ajenda za maendeleo pia,ila ni katika kutunisha akaunti zao kwenye mabenki ya hukohuko kwa wakoloni,kuongeza idadi ya nyumba ndogo zao (isomeke ufuska au uzinzi),kuongeza idadi ya mahekalu yao na magari ya kifahari,na sasa ajenda mpya ya kuimarisha himaya zao kwa kutumbukiza kila mwanafamilia na ndugu wa karibu kwenye siasa ili pindi baba akiondoka madarakani basi mwana amrithi kuzuia uwezekano wa baba mtu kukaliwa kooni kwa madudu aliyofanya akiwa madarakani.

Nimelazimika kuandika makala hii sio kwa minajili ya kumjibu huyo msomaji wangu wa hapa Glasgow bali ni baada ya kusoma toleo la mtandaoni la gazeti la Mwananchi ambapo kuna habari kuwa Tanesco wametangaza tena mgao wa umeme nchi nzima.Hivi sio majuzi tu shirika hilo lilitangaza mwisho wa mgao wa umeme?Tuwe wakweli,hivi uhuni huu wa Tanesco,ambao mie natafsiri kuwa ni uhuni wa serikali iliyopo madarakani,utaendelea hadi lini?So far,hakuna taarifa za wazi kuhusu athari za mgao wa umeme lakini haihitaji sayansi ya roketi au dissertation ya quantum physics kumaizi kwamba mgao huo una madhara makubwa mno kwa uchumi wa taifa na kwa maisha ya walalahoi kwa ujumla (vigogo licha ya kunufaika na ufisadi unaowawezesha kuuza jenereta kila mgao unapotangazwa lakini pia hawaathiriki kwa vile majumbani na maofisini kwao kuna jenereta zinazoendeshwa na fedha za kodi za walalahoi).

Hatuwezi kuilaumu Tanesco pekee kuhusiana na uhuni huu kwani ni siri ya wazi kuwa shirika hilo na sekta ya nishati kwa ujumla vimegeuzwa kitegauchumi kizuri kwa mafisadi.Majuzi tu tumesikia majambazi wa Richmond wakijiandaa kurejeshewa fedha walizotuibia ambapo watalipwa fidia ya mabilioni kwa mgongo wa binamu zao wa Dowans.Hatuwezi kumwepusha Kikwete na CCM yake na ufisadi huu kwa vile licha ya madudu hayo kushika hatamu wakati wa utawala wake,sasa tunafahamu kuwa amekuwa akiwakingia kifua mafisadi wasichukuliwe hatua za kisheria (thanks to nyaraka za siri za kidiplomasia zilizovujishwa na mtandao wa WikiLeaks).Kwa wale ambao hawajabahatika kusoma habari hizo,kuna nyaraka kutoka ubalozi wa Marekani hapo Dar zilizobeba maongezi kati ya bosi wa Takukuru Edward Hoseah na afisa ubalozi wa Marekani ambapo Hoseah alinukuliwa akieleza bayana kwamba Kikwete alishinikiza baadhi ya mafisadi wasichukuliwe hatua.Japo bosi huyo wa Takukuru amejaribu kuruka kimanga na kukana tuhuma hizo,kila mwenye akili timamu anafahamu kuwa ufisadi unashamiri Tanzania kwa vile Kikwete ameshindwa kuwachukulia hatua mafisadi papa licha ya madaraka lukuki aliyorundikiwa na Katiba.

Baadhi yetu tuliwaasa Watanzania wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita majuzi kwamba kuirejesha tena madarakani serikali ya Kikwete ni sawa na kumwaga chumvi kwenye kidonda kibichi,na matokeo yake ndio haya.Wakati tunaelekea mwezi wa pili tangu Kikwete atangazwe mshindi,hakuna lolote la maana lililokwishafanyika kuashiria kuwa kiongozi huyo ana ajenda mpya tofauti na zile zilizotawala miaka mitano iliyopita,kubwa ikiwa na kushamiri kwa ufisadi na uimarishaji himaya za mafisadi huko nyumbani.

Sawa,makosa yameshafanyika kwa kumrejesha Kikwete na CCM yake madarakani lakini hiyo isiwe sababu ya kuendelea kunung'unika kimoyomoyo huku nchi yetu ikizidi kuteketea.Umefika wakati Watanzania wasikubali kupelekeshwa namna hii.Kwanini Kikwete asibanwe kuhusu tatizo la umeme licha ya ahadi zake za mara kwa mara kuwa tatizo hilo lingekuwa historia?Au alimaanisha kuwa tatizo hilo litaendelea kuwa la kihistoria?

Nimesikia taarifa za mpango wa Chadema kuandaa maandamano ya nchi nzima kupinga kuongezwa bei ya umeme.Yaani licha ya mgao wa kila kukicha bado Tanesco wanataka kuongeza bei?Yayumkinika kuhisi kuwa wazo hilo la ongezeko la bei ya umeme ni la kifisadi lenye lengo la kupata fedha za kuwafidia mafisadi wa Richmond/Dowans.Ni muhimu kwa kila Mtanzania mzalendo kuunga mkono mpango huo wa maandamano ya amani ili kufikisha ujumbe kwa Kikwete na serikali yake kuwa Watanzania wamechoka kupelekeshwa.Hata hivyo,kama maandamano ya kuwapongeza wabunge wa upinzani yalizuiliwa na polisi,sidhani kama serikali itaridhia maandamano hayo ya kupinga ongezeko la bei ya umeme.

Mwisho,tuna choices mbili tu:kuchukua hatua sasa kabla hatujafika mahala ambapo hata tukichukua hatua itakuwa sawa na kutwanga maji kwenye gunia,au tusubiri kusoma rambirambi kuhusu nchi yetu hapo 2015.

22 Dec 2010



Picha kwa Hisani ya Mjengwa

Japo haipendezi kuona jeshi la polisi likitumia nguvu kubwa kuzuwia haki ya kikatiba ya wananchi kuandamana au kugoma kwa amani,lakini nashawishika kutowaonea huruma wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma kufuatia kichapo walichopewa na askari wa FFU.Hivi sio hawa wana UDOM waliochangisha fedha kwa ajili ya kampeni za Jakaya Kikwete?Na sio hawa waliotoa tamko la kukemea haki ya kikatiba ya wabunge wa Chadema kususisa hotuba ya Kikwete huko Bungeni?

Najua si vyema kutoa lawama za jumla kwani si kila mwana-UDOM aliafiki wazo la kujikomba kwa Kikwete lililopelekea wanafunzi hao kuchangia fedha zao za ngama ili kumwezesha mwanasiasa huyo aliyekuwa mgombea wa CCM arejee madarakani.

Na kama tulivyoandika baadhi yetu wakati wa kampeni za uchaguzi wakati tunaonya madhara ya kuirejesha CCM madarakani,haijachukua muda kwa  Kikwete na serikali yake kuwalipa fadhila wasomi hao wa Dodoma.

Majuzi nilimsuta mwanahabari mkongwe Dunstan Tido Mhando baada ya kupata taarifa kuwa serikali imemtosa ubosi wa TBC.Nilimsuta kwa vile naamini wakati Tido anaombwa na WALIOMUOMBA kuja kuendesha TBC alikuwa anafahamu fika kuwa aidha anapanda mchicha au bangi,na mavuno yangekuwa mchicha au bangi,respectively.Ukikubali kutumiwa lazima ukubali kitachotekea itapojiri "expiry date" yako.

Sasa tunashuhudia kundi jingine la walioingizwa mkenge.Hawa wasomi watarajiwa wa UDOM walijikomba kwa Kikwete na CCM na kuchangia kampeni zake,sijui wakitarajia kuwa pindi mwanasiasa huyo akirejea Ikulu angewapatia muujiza gani sijui!

MLIPANDA BANGI SASA MNATARAJIA KUVUNA MPUNGA?

17 Dec 2010



So the infamous Dunstan Tido Mhando is gone!I was a bit shocked to learn that,not because he did or did not deserbe the boot,but rather the fact the the guy had been running TBC as if it were an extension of the CCM-owned Radio Uhuru.You wouldn't blame him,would you?He had to serve his masters in the government who shamelessly disregard the fact that state-run bodies are funded by all Tanzanian taxpayers (minus mafisadi,of course) regardless of their politicwl affiliations.

Tido has simply been used and abused.I'm sorry to say this but anyone,journalists included,who allow themselves to be used by some unscrupulous politicians could find themselves deemed useless once their service is no longer required.We all are aware of how,for instance, our artists attract inexplicable attention from our politicians come elections,only to hear the same cries of "tumesahauliwa" after the elections.Our ever important politicians can't afford to be seen sorrounded by a bunch of wana bongoflava.They had afterall done their job and got paid,so no more reasons for them to hang around with such important people in our society.

Of course we could blame such selfish crooks who never shy away from taking for a long ride whoever willing to attend to their needs but I think the latter deserve a share of such blames simply because they wouldnt be on the receiving end of such dirty games had they resisted being manipulated in the first place.Njaa?kujikomba?Blind faith?or sheer stupidity?

Back to poor Tido,he just reaped what he had sewn.I simply don't get it when I hear some people suspecting that his removal would bring TBC back to the 'Radio Tanzania era'.What they overlook is the fact that before he took the TBC post,Tido was working with one of the best,and hugely transparent,media house in the world,The British Broadcasting Corporation (BBC).Some people.Some of us expected that Tido would have brought "the BBC effect" to Tanzanian media but you and I know how he fared.Of course,I understand it wouldn't have been easy for him to transform an exceedingly biased,pro-ruling party state-owned media into an independent,fair and balanced organisation but at least he could have tried.Praising him for allowing opposition parties candidates to take part in "Jimbo kwa Jimbo" is totally missing the point.Why?Because that's actually what a public funded media organisation is supposed to do.Let us not forget what TBC behaved when Chadema inaugurated their general election campaign.And who was TBC's top boss when that was happening?

Rumour has it that Tido was brought to TBC by a certain bigwig who's currently not in the government.If such rumours are true,then why should we feel sorry for someone who got the job not on merit but rather because someone out wanted Tido at the helm of TBC for the bigwig's personal interests to be realised?

I just hope Tido has learned a lesson that political conmen would never hesitate to use and abuse anyone who is willing to be manipulated.For these cons,any tesource is like a condom: needed before and during sex,but something to disposed of immediately after the act.It's my hope that a decorated professional like him would never again allow any politician to take him for a stepping stone.There were some rumours that a certain fisadi who's aspiring to vie for the presidency in 2015 was planning to recruit Tido as his proposed TV/radio chief.If the rumours eventually turn out to be true in the future,and Tido grabs the offer,then we surely haven't seen the end of saddening chapters in Tido's professional life.

16 Dec 2010

Soma stori yake HAPA

15 Dec 2010

NIMETUMIWA NA WADAU,NAMI NAIWASILISHA

Kwanza napenda kukusalimu sana na kukupa hongera sana kwa kazi ambayo umeendelea kuifanya katika blog site yako big up sana...Tulikua tunaomba ututambulishie hii trak yetu mpya ni ya X-mas and New year special. Natanguliza shukurani zangu kwako. Asante sana.



UMABE GENERAL MANAGER: AZMA MPONDAPRODUCED BY: KITA
STUDIO: RAMA RECORDS
PROJECT AND DESIGN: FREDY NJEJE
COUNTRY:TANZANIA
+255712738888
MAY GOD BLESS U ALL!! PAMOJA SANA.
EMAIL: [email protected] &[email protected]
WEBSITE:  http://umabeartscompany.blogspot.com

Tunatanguliza shukurani
 Zetu....

12 Dec 2010



Majuzi kulifanyika uzinduzi wa kitabu kinachoelezea wasifu wa Rais Jakaya Kikwete.Tukio hilo linaelekea kuwa na uzito wa kipekee kwani baadhi ya picha zilionyesha sehemu kubwa ya familia ya mkuu huyo wa nchi ilihudhuria uzinduzi huo.Sina hakika kuhusu kilichomo kwenye kitabu hicho lakini yayumkinika kuamini kuwa laiti wasifu huo ungegusia masuala kama "Wanamtandao na mchango wao katika ushindi wa Kikwete 2005",au "Uswahiba kati ya Kikwete,Lowassa na Rostam Aziz na jinsi unavochangia kufilisika kwa Tanzania", au "wasifu wa wateuliwa mbalimbali wa Kikwete na namna wanavyohusiana nae",nk isingekuwa rahisi kwa Rais Kikwete kujitokeza kwenye uzinduzi huo.

Mwandishi wa kitabu hicho ni Profesa Julius Nyang'oro.Wakati mwingine najiuliza kama baadhi ya maprofesa wa aina hii wameishiwa na mada za muhimu kwa jamii na badala yake wanageukia kujikomba kwa watawala kwa kuandika wasifu mithili ya pambio.Unaweza kunilaumu kwa kutoa tuhuma kabla sijasoma kilichomo katika kitabu hicho.Hata hivyo,huhitaji upeo wa juu kubashiri yaliyomo katika kitabu hicho,maana laiti ingekuwa ni wasifu wa Kikwete huyu ambaye utawala wake umetuzalishia msamiati wa "ufisadi",sambamba na kugubikwa na ishu za Kagoda,EPA,Dowans,Richmond na uzururaji njeya nchi,basi si mkulu huyo wala wanafamilia yake wangetia mguu kwenye uzinduzi huo.

Sasa sijui Profesa Nyang'oro kajaza nini kwenye wasifu huo!Mamia ya ahadi za Kikwete na kisha kuichambua moja baada ya nyingine ( kwa mtizamo chanya usiomuudhi mtawala) au ni hadithi za namna Jakaya alivyozaliwa katika familia ya kawaida,akajiendeleza pasipo makeke,akashika hatamu za uongozi lakini akiendelea kuwa "mtu wa watu" na hatimaye akapata urais ( bila kutaja mchango wa wanamtandao) na ameendelea kuwa mwenye upendo na upole sio kwa walalahoi pekee bali hata mafisadi.

Huenda wasifu huo pia ukagusia udaktari wa falsafa (wa heshima) wa Rais Kikwete.Inawezekana atapomaliza miaka yake 10 hapo 2015 (na kama hatafanya mbinu za kutaka aongezewe muda madarakani) ataweka historia nyingine ( on top ya ile ya kumpiku Vasco da Gama kwa safari) ambapo atakuwa kiongozi pekee aliyezawadiwa shahada nyingi za uzamifu kuliko mwingine duniani.Sijui mpaka sasa ana PhD ngapi,ila nakumbuka ile ya Uturuki,nyingine sijui ya Uganda kama sio Kenya,hii ya juzijuzi Dodoma na Muhimbili nao wamemzawadi shahada ya Afya ya Jamii.


Na kwa vile utawala wa Kikwete umetawaliwa na usanii wa namna flani,yayumkinika kuhisi kuwa hizo PhDs zinatolewa baada ya wahusika "kupigwa somo" au "kupewa kilicho chao".Ungeweza kuhisi kuwa ilikuwa hivyo hata Profesa Nyang'oro,lakini "mnyonge mnyongeni haki yake mpeni" hapo itakuwa mtu tu kaamua kujikomba.

Na kama ilivyozoeleka,wanahabari wetu (pamoja na baadhi ya mabloga) walichokumbuka ni picha za tukio na maelezo ya picha hizo (captions) tu,utadhani kwa kuangalia picha hizo msomaji atapata summary ya jumla ya kilichomo katika kitabu hicho.Hapa "simpigi mtu dongo" ila natoa changamoto kwa wenzetu mliobobea kwenye picha,mkumbuke kuwa picha pekee si habari kamili.Hivyo,inapowezekana mtupatie habari zaidi ya picha husika.Ni ushauri tu,tena wa bure buleshi.

Nakumbuka mwaka 2005 kulikuwa na kitabu cha wasifu wa Kikwete.Nahisi hapa katikati kuna waliojipendekeza na kuja na wasifu mwingine.Sasa tuna wasifu huu "mpya" kutoka kwa Profesa Nyang'oro na huenda hapo 2015 kutakuwa na wasifu mwingine wa "miaka 10 ya mafanikio ya kihistoria chini ya utawala wa Jakaya Kikwete".Mtu mmoja wasifu kibao!

Enewei,hiyo ndio Tanzania yetu.Na ukiwa na kiongozi mpenda sifa basi wajanja hawachelewi kumpamba kwa sifa hii au ile.Na kwa vile hawagusii yale yatakayomfanya mtawala atambue kuwa "hajafunga zipu" basi kwa upande mmoja watoa sifa hao wanapata wanachotegemea kupata (sifa,hela,kupiga picha na rais,kualikwa ikulu,na pengine kuzawadiwa U-DC) na kiongozi mpenda sifa anaendelea kuamini yeye ni chaguo la Mungu ndio maana sifa zinaendelea kumiminika kumhusu yeye.



WAKATI biashara ya magogo ikiendelea kutikisa vichwa vya viongozi wa serikali, imebainika kuwa mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, kada wa CCM, wakuu wa polisi na maafisa wa Takukuru ndio wanaomiliki vibali vya kuvuna magogo katika msitu wa serikali wa Sao Hill ulio wilayani Mufindi.Biashara ya magogo ambayo ilishamiri mwaka 2005/06 ilipigwa marufu baada ya kuonekana kasoro kwa wasafirishaji magogo nje ya nchi ambao walionekana kukiuka masharti ya leseni zao na wiki iliyopita Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige alisema marufuku hiyo inaendelea kwa kuwa ni kinyume cha sheria za nchi.
Lakini msimamo huo wa Waziri Maige utakuwa mgumu kuutekeleza baada ya Mwananchi kubaini kuwa wanaomiliki vibali vya kuvuna magogo ni baadhi ya viongozi wa serikali ambao badala ya kuvitumia kwa malengo waliyoombea, wamekuwa wakivikodisha kwa wafanyabiashara.

Baadhi ya vigogo mbao majina ambayo yamo kwenye orodha watu wanaomiliki vibali hivyo ni pamoja na Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Cyril Chami, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera, Uratibu na Bunge-, William Likuvi, mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Evalista Kalalu, mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita na wengine waliotumia majina ya jamaa zao.

Wengine ni Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene na kampuni ya Rombo Green View inayomilikiwa na mmoja wa mawaziri wa zamani katika serikali za awamu tofauti. Katika orodha hiyo pia yamo majina ambayo ubini wake unafanana na baadhi ya viongozi kama vile Selemani KIKWETE, Aneth P. Msekwa na Juma Abdallah Zombe.

Hata hivyo, haikufahamika mara moja kama watu hao wana uhusiano wa moja kwa moja na watu ambao majina yao ya ubini yanafanana na ya viongozi wa serikali.Vyanzo vyetu vya habari vimebainisha kuwa vigogo walioficha majina yao wanafahamika na kwamba itakapohitajika watatajwa hadharani na raia wema walioapa kuwa tayari kufanya hivyo.
Habari za kiuchunguzi zimebaini kuwa kuwepo kwa watumishi hao wa serikali katika biashara ya magogo kumezua mgogoro mkubwa wa kimaslahi kati yao na wavunaji wadogo wanaolalamika kupunjwa kwenye mgao wa vitalu vya uvunaji.

Uchunguzi umebaini kuwa mgao wa kitaifa unaelekeza meneja mradi wa Sao Hill kugawa magogo yasiyozidi mita za ujazo (cubic metre) milioni moja kwa mwaka.Hata hivyo, katika hali inayoweka mashaka, mgao huo unaonekana kuwapendelea zaidi vigogo hao wanaotumia nyadhifa zao kupata vibali bila kuwa na sifa za kupata mgao huo, huku wengine wanaonufaika wakitajwa kuwa ni baadhi ya wawekezaji wakubwa.Imeelezwa kuwa masharti yaliyowekwa na serikali kwa kila kibali ni kwamba lazima muombaji awe na vifaa kama malori makubwa ya kukokota magogo (break down), mashine zenye uwezo mkubwa wa kuchana magogo na lazima muomba kibali awe ameajiri wataalamu toka chuo cha misitu kinachotambuliwa na serikali, masharti ambayo Mwananchi imedokezwa kuwa hayajatekelezwa na vigogo hao.

Katika kipindi ambacho Rais Jakaya Kikwete amewataka mawaziri na wasaidizi wao kuwa tayari kutoa habari kwa wananchi, katibu mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk Ladslaus Komba hakuweza kuzungumzia suala hilo kila mara Mwananchi ilipowasiliana naye kuanzia Jumatano iliyopita.Badala yake, katika simu zote sita alizopigiwa kati ya Jumatano na jana jioni, Dk Komba alipokea lakini baada ya mwandishi kujitambulisha na kueleza kile anachotaka kufahamu kutoka kwake, alijibu:
"Kwa sasa niko kwenye kikao nitakutafuta baadaye.Hata hivyo, hakutekeleza ahadi hiyo hata mara moja.

Katika moja ya simu hizo, Dk Komba alisema: “Kuna kitu hapa nakinukuu, naomba unipe muda nitakujulisha.”
Hata hivyo alipotafutwa baadaye simu yake ilikuwa haipatikani.
Hata alipofuatwa ofisini kwake, katibu muhtasi wake alieleza kuwa Dk Komba alikuwa ameenda kikazi nje ya ofisi na kumtaka mwandishi amsubiri.

Mmoja wa vigogo waliotajwa kwenye orodha ya mgao wa magogo, WaziriLukuvi alikiri kupokea mgao huo, lakini akasema aliomba kwa ajili ya ujenzi wa shule za sekondari zilizo jimboni kwake Isimani na si kwa nia ya biashara.

Kwenye mgao huo, Lukuvi amepewa kibali cha kuvuna magogo yenye mita za ujazo 1,000, kulingana na orodha iliyobandikwa kwenye ubao wa matangazo wa Sao Hill Mufindi. Katika  orodha hiyo Lukuvi ni mtu wa 564.
“Ni kweli niliomba na nikapewa kibali cha kuvuna magogo. Lakini, si kwa nia ya biashara bali kwa ajili ya kupata mbao za ujenzi wa sekonda zilizopo jimboni kwangu, ikiwemo ile iliyoungua moto ya Idodi,” alisema.

Mbunge wa jimbo la Kibakwe, George Simbachawene alipoulizwa kuhusu suala hilo alikiri kuomba mgao wa uvunaji magogo katika msitu huo, lakini akasema lengo lake si kwa ajili ya kufanya biashara bali ni ujenzi wa madarasa.
"Ni kweli niliomba wala sibishi, lakini si kwa ajili ya kufanya biashara. Ilikuwa ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya shule zetu zilizo katika halmasahauri yetu, kwa sababu kununua mbao zikiwa zimeshaandaliwa ni gharama kuliko kuomba kuvuna magogo na kuchana mwenyewe," alisema Simbachawene.

Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni jitihada za kumpata Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Cyril Chami na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita zilishindikana.

Taarifa zinasema kuwa licha ya kujipatia vibali vinavyotolewa bure na Wizara ya Maliasili na Utalii, wamekuwa hawavitumii kwa uvunaji bali huvikodisha kwa wavunaji wadogo kwa gharama ya Sh5 milioni hadi Sh7 milioni kwa kibali kimoja huku ikielezwa kuwa wapo wanaomiliki vibali zaidi ya 10 na wanavitumia kwa majina tofauti.
Hali hiyo imefanya wavunaji wadogo kupunjwa mgao wa uvunaji magogo tofauti na ilivyokuwa kabla ya watumishi hao wa umma na vigogo kuvamia sekta hiyo.

Hivi sasa wavunaji wadogo zaidi ya 400 wanaambulia mgao kiduchu na wengine kukosa kabisa, hivyo wengi wamelazimika kufunga viwanda vyao kutokana na kukosa malighafi.
“Kama watoa vibali ndio wahusika katika biashara hii je, haki itatendeka kwa wavunaji wadogo?,” kilihoji chanzo kimoja.

9 Dec 2010



JAMAA mmoja ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Joseph, leo asubuhi alikutwa na kamera yetu akiwa ameanguka katika Barabara ya Forest mjini Morogoro, pembezoni mwa uzio wa Hospitali Kuu ya Mkoa wa Morogoro, akidai kwamba alikuwa ametokea katika hospitali hiyo na kwamba hali yake ilikuwa imezidi kuwa mbaya.

Akizungumza na mtandao huu, Joseph alisema: "Nimetoka humu ndani (hospitali) kutibiwa na baada ya kupewa dawa niliruhusiwa kurudi nyumbani, nilipofika hapa nimezidiwa na njaa pamoja na ukali wa dawa hizo na kujikuta nikiishiwa nguvu na kuanguka.

Kama kuna mtu ana shilingi elfu moja anisaidie nikanunue walau uji," alisema Joseph huku akionekana akitetemeka kwa njaa pamoja na ukali wa dawa hizo.



Alipoulizwa anasumbuliwa na ugonjwa gani alidai ni homa ya matumbo (typhoid) iliyoambatana na homa kali.

Mwandishi wetu alimpatia kiasi hicho cha fedha ambapo pia baadhi ya watu waliokuwa eneo hilo walimuunga mkono mpiga picha wetu kwa kumuongezea kiasi cha fedha na baadaye kumwinua hadi kwenye mgahawa uliopo jirani na Shule ya Sekondari ya Morogoro.

Baada ya kupata hudumu hizo, Joseph alizinduka na kauli yake ya kwanza ilikuwa ni kuushukuru mtandao huu na wananchi wengine kwa kumpatia msaada huo.

Picha na Habari kwa Hisani ya Global Publishers



WAKATI HALI IKIWA HIVYO KWA MLALAHOI HUYU,GAZETI LA Mwananchi LILIRIPOTI HABARI IFUATAYO.ISOME KISHA ULINGANISHE NA HABARI HIYO YA KUSIKITISHA HAPO JUU,KISHA TAFAKARI KUHUSU MIAKA 49 YA UHURU WETU

Mashangingi ya mawaziri yazua utata 
Sunday, 28 November 2010 21:05

Sadick Mtulya

WAKATI mawaziri na manaibu wawaziri wakikabidhiwa magari mapya, baada ya kuapishwa Jumamosi iliyopita, serikali imeibuka na kusema sio mapya ni ya zamani.Kauli hiyo inaibua utata kutokana na kuwa baada ya kuapishwa viwanja vya Ikulu na Rais Jakaya Kikwete, kila waziri alikabidhiwa dereva mpya na gari jipya aina ya Toyota GX V8, badala ya gari aina ya Toyota VX V8 iliyokuwa ikitumiwa na mawaziri waliopita.

Ununuzi wa Toyota GX V8 mpya, unashiria serikali bado haijawa tayari kuunga mkono msimamo wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambaye amekuwa akisikika akitaka kusitishwa ununuzi wa magari ya kifahari ili kupunguza matumizi ndani ya serikali.

Toyota GX V8 moja huuzwa kati ya Sh210 milioni hadi Sh240 milioni, hukuToyota VX V8 moja inauzwa sio chini ya Sh180 milioni.Akizungumza na Mwananchi jana, Katibu Mkuu wa iliyokuwa Wizara ya Miundombinu, Omari Chambo, alisema magari hayo sio mapya na kwamba, yaliyotumiwa na mawaziri waliopita.Rais Jakaya Kikwete ameigawanya iliyokuwa Wizara ya Miundombinu na kuwa wizara mbili; Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Uchukuzi.

“Yale magari sio mapya, yalikuwepo. Kwanza uliyaona au unasema tu, hamjayachunguza vizuri jamani, fanyeni uchunguzi,’’ alisema Chambo na kukata simu.
Mawaziri wote na baadhi ya manaibu walikabidhiwa magari hayo (GX V8), huku manaibu wengine wakikabidhiwa VX V8.Sababu ya baadhi ya manaibu mawaziri kukabidhiwa VX V8 badala ya GX V8, ni kutokana na kutokamilishwa kwa taratibu za kutokamilika.

Mmoja wa manaibu mawaziri (jina tunalo), alikabidhiwa VX V8 iliyokuwa ikitumiwa na aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Mifungo na Uvuvi, John Magufuli, ambaye sasa ni Waziri wa Ujenzi.Gazeti moja la kila siku (si Mwananchi) limeeleza kuwa ununuzi wa magari hayo, umegharimu serikali Sh9.3 bilioni na kwamba, takwimu za iliyokuwa Wizara ya Miundombinu zinaonyesha kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwaka wa fedha wa 2005/06 magari makubwa ya kifahari yapatayo 6,000 yalikuwa yamenunuliwa na serikali kwa gharama inayokadiriwa kufikia Sh160 bilioni.

Miongoni mwa magari hayo ni Toyota Land Cruiser (VX/ GX V8, Prado) yapatayo 1,655, Nissan Patrol na Land Cruiser 885, Mitsubishi Pajero 400 na mengineyo.

Tangu kipindi cha serikali ya awamu ya tatu chini ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, kumekuwepo na mjadala kuhusu matumizi makubwa ya serikali hasa katika ununuzi wa magari ya kifahari kutokana na kuendeshwa kwa gharama kubwa.Wadau wengi wanataka viongozi watumie magari ya kawaida kama ilivyo kwa nchi ya Kenya na Rwanda




Leo ni siku yangu ya kuzaliwa.Kwanza sina budi kumshukuru Muumba kwa kunileta duniani tarehe 9 Desemba miaka thelathini na kitu iliyopita (30 plus yrs ago).Pili,nawashukuru wazazi wangu wapendwa,Baba Mzee Philemon Chahali na Mama mpendwa Marehemu Adelina Mapango (Mungu Akulaze Mahali Pema Peponi Amen).Tatu,nawashukuru wanafamilia wenzangu katika familia yetu-kaka na dada na wadogo zangu.Na nne nawashukuru wale woote nilio/ninaofahamiana nao katika muda wote huo.

Makala hii sio kwa ajili ya kuzungumzia birthday yangu.Kwa bahati nzuri (au mbaya?) tarehe ya siku yangu ya kuzaliwa inarandana na tarehe ya Uhuru wa Tanzania.Inapendeza kusherehekea siku ya kuzaliwa inayoambatana na tukio jingine muhimu la kihistoria.Lakini historia pekee sio muhimu kama haina manufaa stahili kwa jamii husika.

Wakati tunaadhimisha miaka 49 ya uhuru wa Tanzania tunalazimika kujiuliza mara mbili mbili umuhimu wa uhuru huo.Je uhuru wetu uliishia tu kwenye kumwondoa mkoloni au ulipaswa kutuweka huru katika nyanja zote?Naamini hilo la pili ndilo dhamini na maana halisi ya uhuru: uhuru wa kupata huduma tunazostahili (elimu,afya,maji,barabara,umeme,maji,nk),uhuru wa kuchagua na kukataa viongozi kwa njia halali (sio uchakachuaji),uhuru wa habari pamoja na uhuru wa kutoa maoni hata kama habari na maoni hayo hayawapendezi watawala),uhuru wa kuabudu pasipo kuwa kikwazo kwa waumini wa imani tofauti,uhuru wa kuishi ikiwa ni pamoja na kuepusha vifo vinavyoepukika (ajali zinazochangiwa na ufisadi wa polisi trafiki,ukosefu wa madawa unaochangiwa na ufisadi kwenye misaada/manunuzi kwenye sekta ya afya),uhuru wa kuishi bila kubaguliwa (mafisadi vs walalahoi,vigogo vs makabwela,watawala vs watawaliwa,nk),na KILA UHURU ambao ni HAKI ya msingi kwa mwanadamu.

Japo haipendezi kuzungumizia,ukweli mchungu ni kwamba miaka 49 ya uhuru wetu inatuacha na maswali mengi kuliko majibu.Na kama mzaha mbaya,siku chache kabla ya kusherehekea umri huu tumeshuhudia namna uchaguzi mkuu uliojaa kasoro lukuki na uchakachuaji ukitupatia "serikali mpya" (denti yuleyule lakini katika yuniformu mpya...ni dhahiri kuwa kama denti huyo ni "kichwa panzi" yunifomu hizo mpya hazitomsaidia lolote kimasomo).Na siku chache zilizopita tumeshindiliwa msumari wenye kutu katika kidonda kibichi pale kampuni ya Dowans "iliposhinda" kesi dhidi ya Tanesco (serikali) na sasa inastahili kulipwa mabilioni ya shilingi.Hiyo ndio salamu ya happy birthday kutoka kwa mafisadi.Tukio hilo halina tofauti na vitendo vya vibaka (hususan mitaa ya Mwananyamala karibu na hospitali kama unatokea Mwananyamala Kwa Kopa) ambapo vibaka wanakupiga roba ya mbao kisha wanakupigia ukelele wa "mwiz,mwizi".Kuporwa uporwe,na kipigo ukipate.Naam,ndivyo Dowans na wamiliki wake mafisadi wanavyotutenda.Huu ni ubakaji wa hadharani tena mchana kweupe.

Anyway,mie nasherehekea birthday yangu kibinafsi.Kama kuna mafanikio au mapungufu yaliyojiri katika miaka thelatini na kitu tangu nizaliwe yanabaki kuwa masuala binafsi.Lakini kwa vile Tanzania ni yetu sote,hatuna budi kusherehekea birthday yake kwa kufanya tafakuri kuhusu mantiki nzima ya "kuzaliwa" na kuwepo kwake.Ni kwa namna hiyo tu ndipo tutaweza kuendelea kusherehekea siku kama ya leo kwa "amani na utulivu" (tukumbuke mwenye njaa hana amani kama ilivyo kwa mgonjwa asiyeweza kupewa tiba stahili,au msafiri asiyeweza kufika aendako kwa vile barabara hazipitiki,au mlipakodi anayekwamishwa kimaisha na mgao usioisha wa maji na umeme,au mlalahoi asiye na haki mbele ya matakwa ya vigogo na mafisadi).

Happy birthday to me.Happy birthday Tanzania

4 Dec 2010



The founder of WikiLeaks, Julian Assange, answers The Guardian readers' questions about the release of more than 250,000 US diplomatic cables

Fwoggie
I'll start the ball rolling with a question. You're an Australian passport holder - would you want return to your own country or is this now out of the question due to potentially being arrested on arrival for releasing cables relating to Australian diplomats and polices?

Julian Assange:
I am an Australian citizen and I miss my country a great deal. However, during the last weeks the Australian prime minister, Julia Gillard, and the attorney general, Robert McClelland, have made it clear that not only is my return is impossible but that they are actively working to assist the United States government in its attacks on myself and our people. This brings into question what does it mean to be an Australian citizen - does that mean anything at all? Or are we all to be treated like David Hicks at the first possible opportunity merely so that Australian politicians and diplomats can be invited to the best US embassy cocktail parties.

girish89
How do you think you have changed world affairs?
And if you call all the attention you've been given-credit ... shouldn't the mole or source receive a word of praise from you?

Julian Assange:
For the past four years one of our goals has been to lionise the source who take the real risks in nearly every journalistic disclosure and without whose efforts, journalists would be nothing. If indeed it is the case, as alleged by the Pentagon, that the young soldier - Bradley Manning - is behind some of our recent disclosures, then he is without doubt an unparalleled hero.

Daithi
Have you released, or will you release, cables (either in the last few days or with the Afghan and Iraq war logs) with the names of Afghan informants or anything else like so?
Are you willing to censor (sorry for using the term) any names that you feel might land people in danger from reprisals??
By the way, I think history will absolve you. Well done!!!
Julian Assange:
WikiLeaks has a four-year publishing history. During that time there has been no credible allegation, even by organisations like the Pentagon that even a single person has come to harm as a result of our activities. This is despite much-attempted manipulation and spin trying to lead people to a counter-factual conclusion. We do not expect any change in this regard.

distrot
The State Dept is mulling over the issue of whether you are a journalist or not. Are you a journalist? As far as delivering information that someone [anyone] does not want seen is concerned, does it matter if you are a 'journalist' or not?
Julian Assange:
I coauthored my first nonfiction book by the time I was 25. I have been involved in nonfiction documentaries, newspapers, TV and internet since that time. However, it is not necessary to debate whether I am a journalist, or how our people mysteriously are alleged to cease to be journalists when they start writing for our organisaiton. Although I still write, research and investigate my role is primarily that of a publisher and editor-in-chief who organises and directs other journalists.

achanth
Mr Assange,
have there ever been documents forwarded to you which deal with the topic of UFOs or extraterrestrials?
Julian Assange:
Many weirdos email us about UFOs or how they discovered that they were the anti-christ whilst talking with their ex-wife at a garden party over a pot-plant. However, as yet they have not satisfied two of our publishing rules.
1) that the documents not be self-authored;
2) that they be original.
However, it is worth noting that in yet-to-be-published parts of the cablegate archive there are indeed references to UFOs.

gnosticheresy
What happened to all the other documents that were on Wikileaks prior to these series of "megaleaks"? Will you put them back online at some stage ("technical difficulties" permitting)?
Julian Assange:
Many of these are still available at mirror.wikileaks.info and the rest will be returning as soon as we can find a moment to do address the engineering complexities. Since April of this year our timetable has not been our own, rather it has been one that has centred on the moves of abusive elements of the United States government against us. But rest assured I am deeply unhappy that the three-and-a-half years of my work and others is not easily available or searchable by the general public.

CrisShutlar
Have you expected this level of impact all over the world? Do you fear for your security?
Julian Assange:
I always believed that WikiLeaks as a concept would perform a global role and to some degree it was clear that is was doing that as far back as 2007 when it changed the result of the Kenyan general election. I thought it would take two years instead of four to be recognised by others as having this important role, so we are still a little behind schedule and have much more work to do. The threats against our lives are a matter of public record, however, we are taking the appropriate precautions to the degree that we are able when dealing with a super power.

JAnthony
Julian.
I am a former British diplomat. In the course of my former duties I helped to coordinate multilateral action against a brutal regime in the Balkans, impose sanctions on a renegade state threatening ethnic cleansing, and negotiate a debt relief programme for an impoverished nation. None of this would have been possible without the security and secrecy of diplomatic correspondence, and the protection of that correspondence from publication under the laws of the UK and many other liberal and democratic states. An embassy which cannot securely offer advice or pass messages back to London is an embassy which cannot operate. Diplomacy cannot operate without discretion and the
protection of sources. This applies to the UK and the UN as much as the US.
In publishing this massive volume of correspondence, Wikileaks is not highlighting specific cases of wrongdoing but undermining the entire process of diplomacy. If you can publish US cables then you can publish UK telegrams and UN emails.
My question to you is: why should we not hold you personally responsible when next an international crisis goes unresolved because diplomats cannot function.
Julian Assange:
If you trim the vast editorial letter to the singular question actually asked, I would be happy to give it my attention.

cargun
Mr Assange,
Can you explain the censorship of identities as XXXXX's in the revealed cables? Some critical identities are left as is, whereas some are XXXXX'd. Some cables are partially revealed. Who can make such critical decisons, but the US gov't? As far as we know your request for such help was rejected by the State department. Also is there an order in the release of cable or are they randomly selected?
Thank you.
Julian Assange:
The cables we have release correspond to stories released by our main stream media partners and ourselves. They have been redacted by the journalists working on the stories, as these people must know the material well in order to write about it. The redactions are then reviewed by at least one other journalist or editor, and we review samples supplied by the other organisations to make sure the process is working.

rszopa
Annoying as it may be, the DDoS seems to be good publicity (if anything, it adds to your credibility). So is getting kicked out of AWS. Do you agree with this statement? Were you planning for it?
Thank you for doing what you are doing.
Julian Assange:
Since 2007 we have been deliberately placing some of our servers in jurisdictions that we suspected suffered a free speech deficit inorder to separate rhetoric from reality. Amazon was one of these cases.

abbeherrera
You started something that nobody can stop. The Beginning of a New World. Remember, that community is behind you and support you (from Slovakia).
Do you have leaks on ACTA?
Julian Assange:
Yes, we have leaks on the Anti-Counterfeiting Trade Agreement, a trojan horse trade agreement designed from the very beginning to satisfy big players in the US copyright and patent industries. In fact, it was WikiLeaks that first drew ACTA to the public's attention - with a leak.

people1st
Tom Flanagan, a [former] senior adviser to Canadian Prime Minister recently stated "I think Assange should be assassinated ... I think Obama should put out a contract ... I wouldn't feel unhappy if Assange does disappear."
How do you feel about this?

Julian Assange:
It is correct that Mr. Flanagan and the others seriously making these statements should be charged with incitement to commit murder.

Isopod
Julian, why do you think it was necessary to "give Wikileaks a face"? Don't you think it would be better if the organization was anonymous?
This whole debate has become very personal and reduced on you - "Julian Assange leaked documents", "Julian Assange is a terrorist", "Julian Assange alledgedly raped a woman", "Julian Assange should be assassinated", "Live Q&A with Julian Assange" etc. Nobody talks about Wikileaks as an organization anymore. Many people don't even realize that there are other people behind Wikileaks, too.
And this, in my opinion, makes Wikileaks vulnerable because this enables your opponents to argue ad hominem. If they convince the public that you're an evil, woman-raping terrorist, then Wikileaks' credibility will be gone. Also, with due respect for all that you've done, I think it's unfair to all the other brave, hard working people behind Wikileaks, that you get so much credit.
Julian Assange:
This is an interesting question. I originally tried hard for the organisation to have no face, because I wanted egos to play no part in our activities. This followed the tradition of the French anonymous pure mathematians, who wrote under the collective allonym, "The Bourbaki". However this quickly led to tremendous distracting curiosity about who and random individuals claiming to represent us. In the end, someone must be responsible to the public and only a leadership that is willing to be publicly courageous can genuinely suggest that sources take risks for the greater good. In that process, I have become the lightening rod. I get undue attacks on every aspect of my life, but then I also get undue credit as some kind of balancing force.

tburgi
Western governments lay claim to moral authority in part from having legal guarantees for a free press.
Threats of legal sanction against Wikileaks and yourself seem to weaken this claim.
(What press needs to be protected except that which is unpopular to the State? If being state-sanctioned is the test for being a media organization, and therefore able to claim rights to press freedom, the situation appears to be the same in authoritarian regimes and the west.)
Do you agree that western governments risk losing moral authority by
attacking Wikileaks?
Do you believe western goverments have any moral authority to begin with?
Thanks,
Tim Burgi
Vancouver, Canada
Julian Assange:
The west has fiscalised its basic power relationships through a web of contracts, loans, shareholdings, bank holdings and so on. In such an environment it is easy for speech to be "free" because a change in political will rarely leads to any change in these basic instruments. Western speech, as something that rarely has any effect on power, is, like badgers and birds, free. In states like China, there is pervasive censorship, because speech still has power and power is scared of it. We should always look at censorship as an economic signal that reveals the potential power of speech in that jurisdiction. The attacks against us by the US point to a great hope, speech powerful enough to break the fiscal blockade.

rajiv1857
Hi,
Is the game that you are caught up in winnable? Technically, can you keep playing hide and seek with the powers that be when services and service providers are directly or indirectly under government control or vulnerable to pressure - like Amazon?
Also, if you get "taken out" - and that could be technical, not necessarily physical - what are the alternatives for your cache of material?
Is there a 'second line' of activists in place that would continue the campaign?
Is your material 'dispersed' so that taking out one cache would not necessarily mean the end of the game?
Julian Assange:
The Cable Gate archive has been spread, along with significant material from the US and other countries to over 100,000 people in encrypted form. If something happens to us, the key parts will be released automatically. Further, the Cable Gate archives is in the hands of multiple news organisations. History will win. The world will be elevated to a better place. Will we survive? That depends on you.
That's it every one, thanks for all your questions and comments. Julian Assange is sorry that he can't answer every question but he has tried to cover as much territory as possible. Thanks for your patience with our earlier technical difficulties

SOURCE: The Guardian

2 Dec 2010














Utawala wa URBAN PULSE CREATIVE MEDIA Unapenda kuwashukuru wale wote ambao walijitolea kufika, kushiriki na kutoa support ya namna moja au nyingine wakati wa URBAN TOUR ili kusaidia kuchangia fedha za kupambana na vita dhidi ya Malaria Tanzania. Tour hii ilifanikiwa kwa kiwango kikubwa sana kuweza kupata publicity duniani kote na kuhamasisha watu mbalimbali ili kutambua umuhimu na namna ya kufanya ili kutokomeza ugonjwa huu kama ambapo kila mtu ataamua kuchukua majukumu na kufanya sehemu yake.

Itakuwa ni vigumu kutoa shukrani kwa kila mtu ila URBAN PULSE ingependa kutoa shukrani za dhati kwanza kabisa kwa Mwenyezi MUNGU ambaye alisaidia kufanikisha tour hii, Ubalozi wa Tanzania hapa UK Pamoja na staff wake,ASET(ASHA BARAKA; BARAKA MSILWA) Bloggers Wote waliosadia kutangaza show yetu ukianzia na MICHUZI,JIACHIE,MISS JESTINA,DJ CHOKA,TZ UK, HAKI NGOWI,GLOBAL PUBLISHERS, ABDALLAH MRISHO,KULIKONI UGHAIBUNI,HUNGA,MASHUGULI,KANUMBA,VINCENT KIGOSI,JENGATZ,MASHUGHULI,TA READING,LADY JAYDEE,MJENGWA,MTAA KWA MTAA,BONGO WIKEND na wengine wote.TV ; RADIO STATION zikiwepo BBC, BEN TV, BET,MTVBASE,AILTV, PRESENTERS: SPORAH, AYOUB MZEE, FRED MTOI, FRED MACHA, SAFINA,IDD SAFE, CHRIS GOLDFINGER NA JJ. MA DJZ; CHAMBI,ASH,ANDREW,10 TONNES,JCOM,MOJA PAMOJA NA CHRIS GOLD FINGER

Hiyo basi Imeandaa party ya kutoa shukrani na kusherekea anniversary ya kwanza ya URBAN PULSE kwa wote jumamosi hii kuanzia 10pm- 4am. DJZ on the deck DJ CHAMBI ;ANDREW


4th November 2010
CLUB AMBASSADOR
20 LONDON ROAD
BARKING, 1G11 8AJ


WOTE MNAKARIBISHWA
ASANTENI
URBAN PULSE CREATIVE



Nimetumiwa na mdau,nami nawasilisha

Nadhani kwa wakaazi wa Arusha na vitongoji vyake watakuwa wameshaona kwenye mabango mbalimbali barabarani ama kupitia redio ama magazeti ya kuwa iliyokuwa inaitwa Novotel Mount Meru Hotel inafunguliwa tena upya ikijulikana kama New Mount Meru Hotel.

Kikubwa nachotaka kuwafikishia watanzania wenzangu ni kuwa nimestaajabika sana ile maana kamili ya uwekezaji kuendelea kutupwa kapuni. Huwezi amini moderator na watanzania kwa ujumla, Hotel hii hadi maua na mchanga vyote vimetoka South Africa ambapo ndipo ilipo kampuni iliyopewa jukumu la kuindesha hotel hii ijulikanayo kama Zabulan.

Nachokiona hapa ni kuwa wasauzi afrika wao wanathamini vyao hata kama wako nje ya kwao, itakumbukwa watu walishapiga kelele kuhusu bidhaa zipatikanazo shoprite ya kuwa hadi nyanya na vitunguu hata mchicha vinatoka hukohuko SA, sasa ambacho watu watajionea hapa ni kuwa mchanga, maua, mbolea, signboards, tisheti, viatu, sabuni, vitambaa, computer, curtains na vyooote vinatoka sauzi afrika, hivi ina maana hapa hatuna hivyo vitu; vingine itasemekana labda viwango na jee hata mbolea na mchanga??

Kali zaidi ni kuwa Senior staffs woote ni ndani ya sauzi afrika ama asia au kwa watani wa jadi, ina maana hapa hatuna mameneja wazuri wakuendesha hotel? hatuna mashefu wazuri hapa tz?

Ikumbukwe walisema katika ajira wataweka mbele wazawa...hii imefia wapi??

Kama uwekezaji ndo hivi jamani bora tufie na tai shingoni.

Kali nyingine ni kuwa Raisi wetu yuleyule aliyeifunguaga Snow Crest Hotel then kesho yake ikaja kuvunjwa ukuta ndio anakuja tarehe 17 Dec kuifungua hii ambayo ilikuwa mali ya watanzania then Mkapa na Magufuli wakaiuza na sasa watanzania hawana hata percent moja hapa, hilo moja pili ni kuwa wafanyakazi woote ni wametoka kenya ama sauzi afrika ma bara asia na pia waliopewa tenda za ku-supply vyakula ni wakenya tupu na vyote vinatoka hukuhuko kenya kuanzia kuku, maharage hadi matunda, jamani rais hana washauri wakamfungua kwenye hili na jee watanzania tutakuwa wapole hadi lini watu wanakuja kupora malighafi zetu na kukimbia??


Ama ndio kichwa cha mwendawazimu??


TUAMKE WATANZANIA NA TULIANGALIE HILI SWALA LA MOUNT MERU KWA JICHO LATATU.


NGUVU YA UMAA IFANYE KAZI JAMANI............

28 Nov 2010


Waislam wakiwa kwenye swala.Picha hii haihusiani moja kwa moja na habari ifuatayo
Waislam wenye msimamo mkali wanashukiwa kuyachoma moto majengo mawili ya kanisa huko Zanzibar,tukio lililotokea Jumapili iliyopita huku waumini wa makanisa hayo wakipokea vitisho vya kuuawa.

Majengo hayo ya Kanisa la Assemblies of God (TAG) na Evangelical Assemblies of God Zanzibar (EAGZ) katika kijiji cha Masingini kilichopo kilomita 5 kutoka mjini-kati Zanzibar yalichomwa moto takriban saa 2 usiku,kwa mujibu wa Askofu Fabien Obeid wa EAGZ.Polisi wa Mwera walipata taarifa ya tukio hilo kesho yake asubuhi.

Matukio hayo ni mwendelezo wa vitendo vya kuwatisha Wakristo katika eneo hilo lenye Waislam wengi,na kuibua hofu kwamba Waislam wenye msimamo mkali wanaweza kudiriki kufanya lolote lile kuzuwia ustawi wa Ukristo.

“Muislam mmoja alisikika akisema, ‘Tumesafisha eneo letu kwa kuharibu makanisa mawili,na sasa tuna mpango wa kuwaua waumini wa makanisa haya mawili-hatutaruhusu kanisa kujengwa tena,’” alisema muumini mmoja wa kanisa ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe.

Jengo hilo la matofali la TAG lilikuwa katika hatua za mwisho za ujenzi,na kwa mara ya kwanza Jumapili hiyo waumini walifanya ibada katika jingo hilo jipya.Jengo la EAGZ ambalo waumini takrban 30 walihudhuria ibada lilikuwa la udongo.

Pasta Michael Maganga wa EAGZ na Pasta Dickson Kaganga wa TAG walieleza hofu yao kuhusu hatma ya kanisa hapo Masingini.Mapasta wa Zanzibar walitarajiwa kukutana jana (Jumamosi) kujadili namna ya kukabiliana na uharibifu huo,alieleza Mwenyekiti wa Usharika wa Mapasta Zanzibar,Askofu Lonard Masasa wa Kanisa la EAGT.

Kwa muda mrefu Waislam wenye msimamo mkali visiwani Zanzibar,wanaoungwa mkono na baadhi ya viongozi wa serikali katika maeneo husika,wamekwaza uwezekano wa Wakristo kupata ardhi kwa minajili ya ujenzi wa majengo ya ibada.Kuna nyakati ambapo wamebomoa majengo yaliyopo na badala yake kuanzisha ujenzi wa misikiti.

Huku wakikanganywa na kutopata ushirikiano wa serikali katika kuwashughulikia wahusika wa matukio hayo,viongozi wa makanisa wameeleza kuwa uwezekano wa waliochoma moto majengo hayo kukamatwa ni mdogo.Mara nyingi,serikali huegemea upande wa wanaofanya matukio hayo,kuchelewesdha uchunguzi kwa hofu ya kuwaudhi Waislam walio wengi ambao wanapinga kuenea kwa Ukristo.

Mwaka jana,maafisa wa serikali katika eneo la Mwanyanya-Mtoni waliungana na Waislam wa eneo hilo kujenga msikiti katika eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa kanisa la EAGZ,alieleza Pasta Paulo Kamole Masegi.

Pata Masegi alinunua ardhi mwezi Aprili mwaka 2007 kwa ajili ya ujenzi wa kanisa katika eneo hilo la Mwanyanya-Mtoni,na kufikia mwezi Novemba mwaka huohuo tayari kulikuwa na jengo lililotumika kama sehemu ya ibada kwa muda.Muda si mrefu Waislam wa eneo hilo walipinga hatua hiyo.

Mwezi Agosti mwaka jana,Waislam hao walianza ujenzi wa msikiti futi tatu tu kutoka kitalu cha kanisa.Mwezi Novemba mwaka huohuo,Pasta Masegi alianza ujenzi wa kanisa la kudumu.Waislam wenye hasira walivamnia eneo hilo na kubomoa msingi wa jengo hilo,alieleza Pasta huyo.

Viongozi wa kanisa waliripoti tukio hilo kwa polisi,ambao hawakuchukua hatua yoyote- na walikataa kutoa ripoti ya tukio,hivyo kukwamisha suala hilo kufikishwa mahakamani,alisema Pasta Masegi.

Wakati huohuo,ujenzi wa msikiti ulikamilika mwezi Desemba (mwaka jana).Hatma ya mpango wa ujenzi wa kanisa ilielekea kufikia ukomo mapema mwaka huu baada ya Mkuu wa Wilaya Ali Mohammed Ali kumfahamisha Pasta Masegi kuwa hana haki ya kufanya ibada katika jengo husika.

Kihistoria, wafanyabiashara wa Kiislam kutoka Ghuba ya Uajemi walifika visiwani Zanzibar mapema karne ya 10 baada ya kusukumwa na pepo za monsoon katika Ghuba ya Aden.Muungano wa visiwa hivyo na Tanganyika mwaka 1964 (na kuunda Tanzania) uliwaacha Waislam visiwani humo wakiwa na hofu kuhusu Ukristo,wakiuona kama njia inayoweza kutumiwa na Tanzania Bara kuwatawala,na tangu wakati huo kumekuwa na hali ya mashaka.


27 Nov 2010


Image and video hosting by TinyPic
Ni matumaini yangu kuwa muwazima na mnaendelea na majukumu yenu ya kujenga Taifa au ustawi wa familia zenu popote mlipo.

Ni kitambo kidogo nilitoweka katika ulimwengu wa Kublog, na hiyo ilitokana na majukumu yangu ambayo yalinifanya nihamie Arusha kwa muda ambapo nilijikuta nikiwa na wakati finyu sana kuutenga kwa ajili ya kublog.

Najua kwa wale wapenzi wa Blog ya VUKANI, watakuwa wame-miss makala zangu ambazo kwa kweli zilikuwa zikiibua mijadala mipana ambayo ilikuwa ikifurahisha kuchangamsha na wakati mwingine kukera kidogo.......lakini yote kwangu yalikuwa ni heri tu... lakini pia kwa wale waliokuwa wakifuatilia maoni yangu popote pale nilipokuwa nikichangia mada mbalimbali nao pia walikuwa wanani-miss kwa kuwa napo huko nilikuwa siishi uchokozi.

UCHAGUZI UMEKWISHA!

katika kipindi kizima cha kampeni za uchaguzi karibu blog zote zilikuwa zimedorora, nadhani sikuwa peke yangu, nawapongeza sana wale walioendelea kutupasha habari mbalimbali wakati wa kampeni hususan kaka zangu Evarist Chahali, Mubelwa Bandio,Prof. Matondo,Prof Mbele, Mzee wa Karibu Iringa, Magid Mjengwa Simon Kitururu, Chacha Wambura, Kamala Fadhy Dada yangu Subi, Yasinta na wengine ambao sikuwataja hapa, lakini nilikuwa napitia blog zenu na kujifunza japo mawili matatu.

sasa baada ya uchaguzi kwisha ni vyema wote turejee na nguvu mpya tukiwa na fikra pevu za kuijenga nchi yetu, kuna haja sasa ya kuwa na sauti moja yaani wanablog na wasomaji wa blog kuwahamasisha viongozi wa serikali wasome blog zetu hizi kwani kuna mawazo mengi yanayotolewa katika eneo hili la blog lakini yameachwa tu yapotee bila sababu.

Ni vyema kuunganisha nguvu zetu bila kujali vyama, maana najua wengi tumeumia mioyoni mwetu baada ya kuona yule tuliyemtegemea hakutangazwa na tume kuwa ndiye mshindi, lakini mimi naamini kuwa kwa kiasi kikubwa vyama vya upinzani vimeshinda uchaguzi wa mwaka huu, kwani kwa nguvu ndogo walizokuwa nazo kwa maana ya nguvu ya kifedha, lakini wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuzoa wabunge na madiwani wengi nchini na hivyo kuonyesha kuwa wananchi wamewakubali.

Tunahitaji sasa kuonesha mshikamano, na kumsaidia bwana mkubwa aliyeko madarakani ili aweze kutuvusha katika miaka mitano hii aliyobakiza salama.Tunatakiwa kukosoa kwa nia ya kujenga na kuelekeza na ikibidi kufundisha........katika tasnia hii ya wanablog naamini kuna vichwa vilivyojaa hekima na mawazo mapya, na ninaamini hata wao wanalitambua hilo

Nimerejea lakini sidhani kama nitakuwa na nguvu kama ile ya kipindi kilichopita kwa sababu ya kutingwa na mambo ya kujiimarisha kiuchumi......

nawatakia kila la kheri na mafanikio mema katika kipindi hiki cha kuumaliza mwaka huu wa 2010.

Ni mie Koero Japhet Mkundi

ASANTE SANA DA KOERO.NAMI NAKUTAKIA HERI NA MAFANIKIO MEMA KATIKA KIPINDI HIKI KILICHOSALIA KABLA YA KUMALIZA 2010 NA SIKU ZOTE.

26 Nov 2010


Kwa mara nyingine,shule ya Sekondari ya Wavulana ya Tabora (Tabora Boys')imezalisha kiongozi mwingine baada ya Mheshimiwa Mahadhi Juma Mahadhi (pichani kulia anayehojiwa) kuteuliwa kuwa Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa.Mahadhi pia alishinda ubunge wa jimbo la Muyuni kwa tiketi ya CCM huko Zanzibar.

Ushindi wako wa kiti cha ubunge na kuteuliwa kuwa Naibu Waziri ni sifa kubwa kwako na kwa Tabora Boys kwa ujumla,a inadumisha rekodi ya shule hiyo kama kitalu cha kuzalisha viongozi wa baadaye wa taifa.

Hongera sana,Mheshimiwa Naibu Waziri.

Image and video hosting by TinyPic

Msanii wa kizazi Kipya Diamond aka Mzee wa Mbagala ametengeneza kibao kipya mapema wiki hii ndani ya Studio za URBAN PULSE CREATIVE maalum kwa ajili Urban Tour war on Malaria. Kibao hicho cha kusisimua kinaitwa LALA SALAMA kimeangushwa na Producer Young Josh na Salim kutoka URBAN PULSE. Ili kuwapa mafans wake burudani ya ukweli Diamond ataperfom LALA SALAM kwa mara ya kwanza kwenye show zake za mwisho ambazo zitafanyika:


CLUB AMBASSADOR
20 LONDON ROAD
BARKING, 1G11 8AJ



BARAKA, FRANK NA DIAMOND WAKIJADILI MWELEKEO WA NYIMBO MPYA YA DIAMOND.
Image and video hosting by TinyPic
DIAMOND AKITUNGA NYIMBO MPYA NA URBAN PULSE
Image and video hosting by TinyPic
URBAN PULSE SECRET WEAPON SALIM AKIWA JIKONI NA DIAMOND
Image and video hosting by TinyPic
YOUNG JOSH NA SALIM WAKIAWA WANAKAMUA
Ratiba zaidi:
27 November 2010
116 GAR GOSFORD STREET
PALMS BAR
COVENTRY
CV1 5 EA

Kiingilio ni £10 kabla ya saa sita usiku.
Tafadhali wahi mapema na pia tunaomba mpe taarifa mwenzako.

WOTE MNAKARIBISHWA

Asanteni sana,
URBAN PULSE CREATIVE

24 Nov 2010

Important: The pill was found to lessen infection chances in conjunction with education and condoms

A pill which prevents people from getting HIV has come a step closer after medication already available in pharmacies was shown to lessen the chances of infection.
.Scientists gave the pill, which is currently used to treat people who have contracted the virus, to healthy gay and bisexual men during the three-year global trial.

They discovered daily doses of the pill, Gilead Science's Truvada cut the risk of infection when given with condoms, counselling and other prevention services.

Breakthrough: Truvada, pictured being held by Gilead Sciences Inc. Chief Executive John Martin, was found to lessen the chances of infection among gay men
The drug lowered the chances of infection by 44 per cent, and by 73 per cent or more among men who took their pills most faithfully.

Researchers had feared the pills might give a false sense of security and make men less likely to use condoms or to limit their partners, but the opposite happened - risky sex declined.

The results are 'a major advance' that can help curb the epidemic in gay men, said Dr. Kevin Fenton, AIDS prevention chief at the U.S. Centers for Disease Control and Prevention.

But he warned they may not apply to people exposed to HIV through male-female sex, drug use or other ways. Studies in those groups are under way.

Because Truvada is already on the market, the CDC is rushing to develop guidelines for doctors who want to use it to prevent HIV, and urged people to wait until those are ready.

However, high prices of the pills which cost $5,000 to $14,000 a year in the United States could be prohibitive.

They are sold for roughly $140 a year in some poor countries where they are produced in generic form.

Whether insurers or government health programs should pay for them is one of the tough issues to be sorted out, said Dr. Anthony Fauci, director of the National Institute of Allergy and Infectious Diseases.
Historic: The Vatican, led by Pope Benedict XVI, has indicated it now supports condom use in the fight against AIDS
'This is an exciting finding,' but it 'is only one study in one specific study population,' so its impact on others is unknown, Fauci said.

His institute sponsored the study with the Bill & Melinda Gates Foundation.

It was the second piece of good news in a day for the fight against AIDS after U.N. officials said new HIV cases are dropping dramatically worldwide.

The U.N. report said that new cases dropped nearly 20 percent over the last decade and that 33.3 million people are living with HIV now.

And earlier, the Pope, in a shift from historic teachings, said that using a condom is a lesser evil than infecting a sexual partner with HIV.

Gilead Sciences Inc. donated Truvada for the study, which involved about 2,500 men at high risk of HIV infection in Peru, Ecuador, Brazil, South Africa, Thailand and the United States.

The foreign sites were chosen because of high rates of HIV infection and diverse populations.

The men were given either Truvada or dummy pills. All had monthly visits to get HIV testing, more pills and counselling.

Every six months, they were tested for other sexually spread diseases and treated as needed.

After a median follow-up of just over a year, there were 64 HIV infections among the 1,248 men on dummy pills, and only 36 among the 1,251 on Truvada.

Among men who took their pills at least half the time, the risk of infection fell by 50 per cent. For those who took pills on 90 per cent or more days, risk fell 73 per cent.

Tests of drug levels in the blood confirmed that more consistent pill-taking gave better protection, and in one subgroup, the reduction in risk was 92 per cent.



Mwandishi Wetu
Novemba 24, 2010
Polisi Uingereza wamchunguza mwanawe
Washitushwa na uhamishwaji wa Sh.bil. moja
MTOTO wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa anayeitwa Frederick Lowassa anachunguzwa na Kitengo Maalumu cha Polisi wa Kimataifa wa Uingereza wanaofuatilia utata wa uhamishaji fedha kutoka Tanzania, Raia Mwema limedokezwa.

Fedha hizo zinahusishwa na ununuzi wa nyumba yenye thamani ya pauni za Uingereza 475,000 (takriban Shilingi bilioni moja) katikati ya Jiji la London, .

Hata hivyo, watu walio karibu na Frederick wameelezea kwamba kijana huyo hakuwahi kununua nyumba; bali aliwahi kutaka kupanga kwa ajili ya kuishi akiwa masomoni nchini Uingereza na fedha nyingine alizituma kwa ndugu yake aishie nchini humo.

Nyumba ambayo inatajwa katika maelezo ya awali iko mtaa wa Leinster Gardens, jijini London.

Hata hivyo, hakuna ofisa yeyote wa Serikali ya Tanzania aliyekuwa tayari kuzungumzia suala hilo, pamoja na kuwapo taarifa kwamba tayari vyombo vya dola vya Tanzania vimekwisha kuhusishwa katika uchunguzi huo.

Maofisa wa Polisi wa Idara ya Upelelezi wa Jinai (CID) wanaohusika na uchunguzi wa fedha haramu, wamekwepa kuzungumzia suala hilo na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Robert Manumba, hakuweza kupatikana, na alielezwa kuwa nje ya nchi kikazi.

Ofisa wa CID aliyeelezwa kuongoza kitengo kinachochunguza makosa ya uhalifu wa fedha na nyaraka, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Samson Kasala, alikanusha kufahamu chochote kuhusiana na suala hilo, kabla ya kukata simu alipohojiwa na Raia Mwema kuhusu taarifa hizo.

Taarifa zinaeleza kwamba Kitengo cha Ufuatiliaji wa Fedha Haramu (Financial Intelligence Unit-FIU) kilichopo chini ya Wizara ya Fedha nchini, kilipokea taarifa kutoka Polisi wa Kimataifa wa London, Uingereza, wakitaka taarifa muhimu kuhusiana na Frederick, kabla ya kitengo hicho kuomba msaada wa polisi.

Hata hivyo, Kamishna wa FIU, Herman Kessy, hakuweza kupatikana wiki iliyopita akielezwa kuwapo nchini Afrika Kusini kikazi, lakini hata aliporejea wiki hii Raia Mwema ilikosa ushirikiano kutoka kitengo hicho Jumatatu wiki hii.

FIU imeanzishwa chini ya Sheria ya Udhibiti wa Fedha Haramu ya mwaka 2006 (Anti-Money Laundering Act-2006) kwa kuundiwa kanuni mwaka 2007, lakini hadi sasa kitengo hicho kimekuwa kikiendeshwa na maofisa watano tu, Kamishna Kessy, mchambuzi mmoja, mtaalamu wa mawasiliano na wasaidizi wawili wasio wataalamu, kitengo kilichopaswa kuendeshwa na watu wengi zaidi kutokana na unyeti wake.

Habari zinaeleza kwamba hata ofisa wa Polisi aliyewahi kuhamishiwa FIU kwa kazi maalumu alijikuta akitengwa na kutopangiwa kazi na maofisa hao ambao wengi wanatoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), baada ya kuwa ‘wameaminiwa’ sana na uongozi wa juu wa serikali.

Kwa mujibu wa taarifa hizo ambazo bado zinafanyiwa kazi, Frederick ambaye baba yake alijiuzulu Waziri Mkuu kwa kuhusishwa na kashfa ya ununuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme iliyokabidhiwa kwa kampuni tata ya Richmond Development LLC, anadaiwa kufanya mawasiliano kupitia kampuni ya uwakala iliyotajwa kwa jina la ‘Mishcon’.

Nyaraka alizowasilisha, zilidai kuwapo ubia kati ya mtuhumiwa huyo na kampuni tatu ikiwamo Integrated Property Investment(T) Ltd na Barare Ltd Company.

Mkataba huo unaonyesha kuwa Frederick Lowassa ana hisa kwenye kampuni hizo, na kwamba fedha za ununuzi wa nyumba hizo zinatokana na fedha za malipo ya hisa anazopata kutokana na kampuni hizo.

Hata hivyo, mkataba huo unaonyesha kusainiwa Machi 25 mwaka 2009 siku moja baada ya Frederick Lowassa kusaini mkataba kati yake na kampuni ya Mishcon kama wakala wake katika ununuzi wa jengo hilo.

Pia aliwasilisha nyaraka zinazoihusisha kampuni ya Alphatel kama moja ya kampuni ambayo pia yeye ni mkurugenzi wake ambayo pia ni chanzo chake kingine cha fedha anazotumia kununua jengo hilo.

Taarifa zimedokeza kuwa ununuzi huo ulikwama baada ya kushindwa kutoa malipo hayo kwa mujibu wa mkataba kati yake na wakala wa ununuzi wa nyumba hiyo (kampuni ya Mishcon) ambao ulimtaka awe amekamilisha kulipa fedha hizo kabla ya Aprili 14, mwaka 2009.

Hata hivyo, siku chache baadaye ndani ya mwezi huo wa Aprili, Frederick aliipelekea Mishcon kiasi cha pauni za Uingereza 199,940 zikitokea kwenye kampuni ya ununuzi fedha ya Wall Street Exchange.

Aidha kiasi cha pauni 100,000 kiliingizwa kwenye akaunti ya kampuni hiyo hiyo ya Mishcon kwa fedha taslimu katika mikupuo 12 tofauti zikitokea kwenye matawi tofauti ya benki ya NatWest Bank plc iliyoko Kaskazini mwa Jiji la London.

Raia Mwema limeelezwa kuwa mazingira ya kuingizwa fedha hizo kwenye akaunti ya wakala huyo ( Mishcon) ndiyo yameifanya Taasisi ya SCD 6 Economics and Specialist Proceeds of Corruption Unit ya Uingereza inayosimamia uchunguzi wa sakata hilo kuwa na mashaka makubwa kuhusu uhalali wa fedha hizo.

Kutokana na mazingira hayo, SCD 6 Economic and Specialist Crime Proceeds of Corruption Unit yenye ofisi zake Victoria Block, New Scotland Yard, London, ililazimika kuwasiliana na FIU ikitaka maelezo ya awali kuwezesha kufanyika kwa uchunguzi kuhusu fedha hizo.

Raia Mwema iliwasiliana na Fred ambaye alikana kununua nyumba Uingereza lakini alikiri kuwahi kutuma fedha huko. Aliliambia Raia Mwema pia kwamba hajawahi kuhojiwa na yeyote kuhusu suala hilo, na pia kwamba hana taarifa kuwa polisi wa Uingereza wanampeleleza.

Hata hivyo kwa upande mwingine, gazeti hili limebaini kuwa, maelezo ya awali ambayo yalitakiwa kutoka Tanzania na makachero hao wa Uingereza, ni pamoja na kutaka kufahamu kama kweli Frederick Edward Lowassa amezaliwa Agosti 26, 1977, Mwanza Tanzania na anamiliki hati ya kusafiria yenye namba AB 109402 iliyotolewa Tanzania na kwamba anwani yake nchini Uingereza ni 71 Hendrix Drive, Milton Keynes, MK8 0DY.

Pia makachero hao waliitaka Serikali ya Tanzania kutoa ufafanuzi wakitaka kujua kama Frederick Lowassa ni mbia katika kampuni za Alphatel Partnership (Tanzania) Barare Ltd na Intergrated Tanzania Limited, kampuni ambazo zimefahamika kumilikiwa na familia ya Lowassa.

Asasi hiyo ya Uingereza pia imeomba kujua kama FIU wana taarifa zozote za uhalifu dhidi ya Frederick Lowassa na kama baba yake Edward Lowassa anachunguzwa kwa tuhuma yoyote ya rushwa na mamlaka za uchunguzi wa rushwa nchini Tanzania kuhusu fedha haramu.

Uchunguzi wa awali uliofanywa na vyombo vya dola, ulielezwa na taarifa hizo kwamba Frederick Lowassa si mbia katika kampuni hizo na kwamba Barare Ltd wenye hisa ni Edward Ngoyai Lowassa mwenye hisa 500 na Regina Mumba Lowassa mwenye hisa 500 huku wakurugenzi wakiwa ni hao hao.

Ofisa wa Uingereza anayesimamia uchunguzi huo, George Simpson, ameliambia Raia Mwema kupitia barua pepe kwamba kanuni za uchunguzi kuhusiana na kesi zenye mguso wa kisiasa huwazuia kukanusha au kuthibitisha kuhusu uchunguzi unaoendelea hadi pale wanapofikia hatua ya kukamata mtuhumiwa ama anapofikishwa mahakamani.

CHANZO: Raia Mwema

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.