27 Jul 2011



From: Andrew Bomani
Subject: TAMKO LA KIHISTORIA NA HALI YA KUHUZUNISHA NCHINI!
Date: Monday, July 25, 2011, 3:26 AM

Ndugu msomaji,

Kufuatia ombwe la uongozi la kutisha nchini ambalo karibu kila Mtanzania anakiri ndiyo tatizo mama, baadhi yetu tumeona ni vyema tukawafikishia tamko ambalo liliwahi kutolewa mwaka 1995 na Jaji Bomani. Ni jambo la kusikitisha kwamba wananchi wengi wanadhani kwamba viongozi waliokuwepo wakati huo na waliopo sasa pengine ndiyo waliokuwa bora. Jambo hili ni hatari. Haiwezekani nchi yoyote ikakosa watu makini. Soma na tafakari namna mizengwe katika kupata viongozi makini inavyoweza kulifikisha taifa lolote mahali pabaya.

Mungu Ibariki Tanzania.

Tamko la Kihistoria



Barua ya UVCCM Kwa Jaji Bomani Kumwomba Agombee Urais 2005

25 Jul 2011


Nchi ipo kizani,Rais Kikwete yupo bize kuzurura nje ya nchi,na akirejea ni kama hayupo.Binafsi sielewi kwanini huyu mtu aligombea urais mwaka 2005 na baadaye 2010.Je ni kuweka historia tu hata kama historia yenyewe ni ya kukinai?Je ni kutopima kina kabla ya kujitosa bwawani?

Kitu kimoja cha wazi ni kwamba kama kuna mtu anayetegemea Kikwete na CCM yake wataleta ufumbuzi wa matatizo ya Tanzania,basi anaweza pia kutarajia kugema damu kwenye jiwe.Kulalamika peke yake hakuwezi kuleta ufumbuzi wa matatizo.Mkoloni,Makaburu,Nduli Idi Amini hawakuondoka kwa vile tuliwatukana au kuwalalamikia,bali tulijiunga kwa umoja wetu na kupambana nao (hata kwa nguvu ilipobidi).

Anyway,soma habari hii hapa chini inayodhihirisha kuwa wababaishaji hawa (Kikwete na chama chake cha Magamba) wapo too busy katika vita vyao vya kimaslahi to care about matatizo ya Watanzania 

Gamba laivuruga CCM 
Monday, 25 July 2011 08:47


Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Benno Malisa

WENYEVITI MIKOA WALIPINGA, BARAZA KUU UVCCM LAUNGA MKONO ZIARA ZA KINA NAPE
Waandishi Wetu
MPANGO mkakati wa kujivua gamba kwa lengo la kurejesha uhai ndani ya CCM unaelekea kuwa bomu la maangamizo kwa chama hicho, baada ya baadhi ya wenyeviti wa mikoa kuupinga huku wakiagiza wafuasi wao kuwashusha majukwaani makada wanaoupigia debe.
Wakati wenyeviti hao wakiupinga, Baraza Kuu la Umoja wa Vijana CCM (UVCCM), jana limetoa tamko rasmi la kuunga mkono ziara hizo zinazofanywa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa chama hicho, Nape Nnauye za kutekeleza mkakati huo.

Mpango huo wa kujivua gamba ulitangazwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete katika maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa chama hicho kikongwe barani Afrika, lakini jana baadhi ya wenyeviti wake wa mikoa akiwamo, John Guninita wa Dar es Salaam na Hamis Mgeja wa Shinyanga, waliupinga wakisema unamwaga sumu kali dhidi ya chama.

Msimamo wa UVCCM
Baraza Kuu la UVCCM limetoa msimamo wake kuunga mkono ziara za mikoani zinazoongozwa na Nnauye za kujivua gamba huku likiweka bayana kuwa huo ni msimamo wa Halmashauri Kuu (Nec) ya chama na si wa Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi.

Mbali na Nape, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka wamekuwa wakifanya ziara mikoani hasa katika mwisho wa wiki ambazo pamoja na mambo mengine, wamekuwa wakifanya mikutano ya kukipa uhai chama huku wakitangaza uvuaji gamba.

Kaimu Mwenyekiti wa UVCCM, Benno Malisa alisema UVCCM ilipongeza uamuzi wote wa NEC: "Kila kinachofanyika ni sahihi na sisi tunaunga mkono kabisa."

Guninita awatangazia vita
Wakati vijana wakiuunga mkono ziara hizo, juzi Guninita aliwaambia wanaCCM wa Tawi la Sinza kwamba watakapomuona kiongozi yeyote mkubwa wa chama hicho anakikiponda katika wasisite kumshusha jukwaani.
Guninita alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na wanachama hao kuhusu matatizo mbalimbali ya chama hicho na kusisitiza kwamba Waziri Sitta asipojibiwa kauli zake atajiona kuwa ni mkubwa zaidi.

Wiki iliyopita Mwenyekiti huyo alimtupia kijembe Sitta akidai kwamba waziri huyo ana mpango wa kuhakikisha kuwa Serikali ya chama hicho inaondolewa madarakani kwa kuwa bado ana hasira za kupoteza wadhifa wa Spika wa Bunge.

“Chama chetu kinazidi kupoteza sifa, hii ndiyo sababu ya mimi kufanya ziara katika majimbo ambayo yalishindwa katika ngazi zote kukipatia chama ushindi wakati wa uchaguzi. Kumekuwa na viongozi wakubwa wa chama hicho wanaozunguka nchi nzima na kuchochea ili Serikali iondolewe madarakani, nawaambieni mkiwaona viongozi hao wanakiponda chama washusheni majukwaani, wanataka kujiona wao ndiyo wakubwa zaidi ya wengine.”

Alisema chama hicho kinajipanga kikamilifu ili kuhakikisha uchaguziwa mwaka 2015, kinashinda kwa kishindo ikiwa ni pamoja na kupambana na tatizo la rushwa lililokitawala.

Guninita ambaye amekuwa akipingana hadharani na wapambanaji hao wa ufisadi ndani ya CCM, alisema katika uchaguzi huo hawatahitaji ushahidi kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (Takukuru) na kuwa mtu atakapobainika anajihusisha na rushwa atachukuliwa hatua hapohapo.

“Tatizo la rushwa katika chama lipo hasa wakati wa uchaguzi. Ninachotaka kuwahakikishia ni kwamba tunajipanga na katika uchaguzi ujao hatutahitaji ushahidi wa PCCB (Takukuru), tutakapombaini mtu tutampeleka mahakamani wenyewe. Hatutaki aibu ya mwaka huu itukumbe tena.”

Alisema tayari chama kimewabainisha viongozi wote walioingia madarakani kwa rushwa na kuwa wanaendelea kujadiliana hatua za kinidhamu dhidi yao.

Guninita alisema katika uchaguzi wa mwaka 2015, chama hicho hakitapeleka majina ya watu watakaobainika kutoa rushwa kwa ngazi za juu ili wakubalike katika kura za maoni.

Mgeja atoa tahadhari
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja alisema juzi kwamba licha ya kuwakaribisha wapambanaji hao na mkakatio wao wa kujivua gamba katika mkoa wake, waende na majibu ya kero za wananchi.

Alisema viongozi wa chama chake wanatakiwa kwenda na majibu ya kero zilizopo katika mkoa huo za wakulima kuuziwa dawa feki za pembejeo, rushwa, umasikini na rasilimali kama madini kushindwa kuwanufaisha, badala ya kutumia ziara hiyo kuwapaka matope wenzao.

“Ziara za kusafisha chama siyo mbaya, kama zitatumika vyema, lakini hali ambayo imeanza kujitokeza ni wazi haijengi chama, bali inaendelea kumwaga sumu,” alisema.

Millya, Porokwa waponda ziara hizo
Mbali ya Guninita na Mgeja, Mwenyekiti wa UVCCM, mkoani Arusha, James Ole Millya naye ameziponda ziara hizo za kujivua gamba akisema hazina tija kwa chama na Serikali kwa kuwa Sitta, ni waziri ndani ya Serikali hiyohiyo anayoituhumu na kueleza kwamba anaona kuna uchafu ndani yake ni vyema akatoka.

Millya aliwatuhumu Sitta, Nape, Ole Sendeka na Dk Mwakyembe kuwa wamekuwa wakitumia mwanya wa ziara hizo kuichafua Serikali na chama tawala huku akisisitiza: "Kama wanaona Serikali hiyo haifai ni bora wangeondoka. Sitta ni waziri, Mwakyembe ni waziri na wengine wako ndani ya Serikali na chama hawa wote ni viongozi, sasa kitendo cha wao kuzunguka na kuisema vibaya Serikali na chama tawala hakifai.”

Alisema viongozi hao wameamua kuanza mashambulizi dhidi ya Serikali kwa kuwa ni wabinafsi, huku akikitahadharisha chama hicho kuwa makini na ziara hizo kwa kuwa huenda zikakiingiza katika hatua mbaya.

Naibu Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Daniel Porokwa naye aliziponda ziara za viongozi hao akisema zimejaa unafiki kwa kuwa Sitta na Nape walikuwa waanzilishi wa Chama cha Jamii (CCJ) na kuwaita wasaliti ndani ya CCM.

Alisema pamoja na kutoa tuhuma mbalimbali dhidi ya viongozi hao kuwa ni waasisi wa CCJ, anashangaa hadi leo uongozi wa chama chake haujawahi kumwita au kumwomba udhibitisho juu ya madai aliyoyasema.


Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Nape akutana na mabango Moshi
Ziara ya Nape, juzi mkoani Kilimanjaro ilikumbana na upinzani mara baada ya kiongozi huyo kupokewa kwa mabango mbalimbali wakati akishuka kwenye gari lake katika Kituo cha Mabasi Moshi Mjini tayari kwa kuhutubia mkutano wa hadhara katika eneo hilo.

Hata hivyo, tofauti na mikutano mingine kama ule wa mkoani Mbeya, huo ulihudhuriwa na watu wachache huku wengine walionekana wakishuka kutoka kwenye mabasi uwanjani hapo.

Nape aliyefika kituoni hapo mnamo a saa 9:00 mchana akitokea Mwika katika ufunguzi wa Tawi la CCM Chuo Kikuu cha Tumaini (Smmuco), alikutana na mabango yaliyokuwa yameshikiliwa na vijana wa CCM wilayani Moshi ambayo yalikuwa yamebeba ujumbe mbalimbali.

Baadhi ya mbango hayo yalikuwa yakisomeka: ”CCJ nao wajivue gamba,” “Hatutaki makundi ndani ya CCM,” ”Vijana tumechoka na wana CCJ, wana CCJ ondokeni mtuachie CCM yetu.”.

Wakati vijana hao wakibeba mabango hayo mbalimbali yaliyolenga kufikisha ujumbe kwa Nape, vijana wa ulinzi wa CCM maarufu kama “Green Guard,” iliwabidi kutumia nguvu za ziada kuzima juhudi za vijana hao waliobeba mabango hayo na waliyakamata na kisha kuyachana baadhi yao huku mengine yakiwasilishwa katika Ofisi ya Katibu wa CCM wilayani Moshi.

Akimkaribisha Nape jukwaani, Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi Mjini, Amos Shimba aliyaponda vikali mabango hayo huku akisema vijana walioyabeba siyo wakazi wa Mji wa Moshi, bali wanatoka mkoani Arusha huku akiwaonya, kamwe wasithubutu kuleta mambo hayo mkoani Kilimanjaro.

“Kuna vijana wanaotaka kutuletea vurugu na tunajua wanatoka tu Arusha, tunawaambia tafadhali sana msituletee mambo yenu ya vurugu za Arusha hapa mkoani kwetu,” alionya Shimba.

Akihutubia mkutano huo, Nape alisema lengo la ziara yake mkoani Kilimanjaro ni kuleta matumaini kwa wanachama wa CCM sanjari na kufafanua falsafa ya kujivua gamba ambayo alidai inapotoshwa na watu wachache hapa nchini.

Alikishambulia Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) hususan viongozi wake kwamba wanapenda vurugu na maandamano huku akionya kwa kutumia mifano na nahau mbalimbali ya kuwa kamwe Serikali ya CCM haitakubali amani ya nchi ichezewe.

Aliendelea kumshambulia vikali Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa akidai kuwa ameamua kukishinikiza chama chake kumlipa kiasi cha Sh7 milioni ihali alikuwa kinara wa kupinga mishahara minono na marupurupu ya wabunge.

“Namtaka Dk Slaa aishi kama anavyoongea, alinituhumu nahusika na EPA mkiniangalia mimi sura yangu inafanania na EPA? Mbona yeye amekishinikiza chama chake kimlipe Sh7milioni wakati alikuwa akipinga mishahara na marupurupu ya wabunge? Huyu ni mnafiki,” alisema Nape.

Alisema falsafa ya kujivua gamba ndani ya CCM imekuwa ikipotoshwa na baadhi ya watu hususan wapinzani na kuuita kuwa ni dhana ya kishetani kwa kuwa imetumia mfano wa nyoka na kuwabeza watu hao kwa kuwataka wasome biblia na msaafu na kuwaeleza kuwa nyoka ametajwa ndani ya vitabu hivyo.

Akizungumzia kauli za wanaCCM wanaoipinga dhana hityo, alisema asingependa kujibizana na watu wanaouzungumza barabarani kwani chama kina vikao ambavyo vitawahukumu.

Alichokisema Sitta
Akizungumza Dar es Salaam juzi, Sitta alisema Serikali makini lazima ikiri mapungufu kutokana na makosa yake: "Nilichokisema Mbeya ni kuwaambia Watanzania ukweli na nitaendelea kuwaambia ukweli."

Alisema serikali makini haiwezi kuwadanganya wananchi wake na kusisitiza, "Watanzania wa leo ni watu wenye akili huwezi kuwambia habari nzuri za umeme wakati umeme ni tatizo."

"Kule Mbeya nilieleza ule umati ukweli kuhusu upungufu wetu serikalini na wananchi walituelewa. Kuna upungufu tumeukiri na tunajipanga kuupatia ufumbuzi. Umeme ni tatizo kubwa huwezi kueleza uongo kwa Watanzania wakakuelewa, waambie wananchi ukweli watakuelewa. Sasa huu ndiyo upungufu wetu, lakini wanatokea baadhi ya watu wenye upeo mdogo ndani ya CCM wanaoendekeza siasa za ufuasi, wanakaa na kuzungumza mambo ya hovyo."

Imeandaliwa na Ramadha Semtawa, Minael Msuya, Dar, Habiel Chidawali, Dodoma, , Moses Mashalla, Moshi

Chanzo: Mwananchi 


CLICK THE PICTURE TO ZOOM

SOURCE: The Economist

24 Jul 2011


Nimepokea kwa masikitiko kifo cha Mhadhiri wangu wa zamani Profesa Samuel Mushi.Nilikuwa mwanafunzi wa Profesa Mushi tangu nilipojiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Septemba 1996 hadi nilipomaliza mwaka wa kwanza July 1997.Profesa Mushi alinifundisha Utangulizi kwa Stadi ya Sayansi ya Siasa (PS100: Introduction to the Study of Political Science).Marehemu ni miongoni mwa wanataaluma wa mwanzo walionipa uelewa na mwamko wa stadi za siasa,japokuwa mwaka wa pili na wa tatu nilichukua mchepuo wa Sosholojia.

Bwana Ametoa Bwana Ametwaa.
Jina la Bwana Lihimidiwe Milele,
Amen 

23 Jul 2011


FAMILIA YA TULLY NGONYA(MAMA MARIA) NA IKUPA NGONYA WANASIKITIKA KUWAARIFU MSIBA WA BABA YAO MPENZI MZEE J.D. NGONYA ALIEFARIKI LEO ASUBUHI 23.7.11.
KAMA ILIVYOKUWA DESTURI YETU TUNAWAOMBA WOTE TUKUTANE TUWAFARIJI WAFIWA WAKATI WA KIPINDI HIKI KIGUMU.
MSIBA UPO 38 TRELLECK ROAD, READING RG1 6EN. 
BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA JINA LAKE LITUKUZWE MILELE. AMEN.
TAFADHALI MJULISHE NA MWENZAKO

Imetumwa na Urban Pulse Creative


Hili sio ombwe tena bali mkusanyiko wa wababaishaji walioteuliwa na mtu asiyejua kwanini aliwateua,na ndio maana wanaendesha mambo kama kwenye mchezo maarufu wa watoto ujulikanao kama kombolela.Watu wazima ovyoo!Lakini ni wazi wanapata jeuri ya kufanya ubabaishaji huo kwa vile wanafahamu fika kuwa aliyewateua hana jeuri ya japo kuwawajibisha,let alone kuwakemea.

Anyway,hebu soma madudu yao hapa chini:

DPP amkana Hoseah  
Friday, 22 July 2011 20:27

ASEMA HAJAPATA JALADA LA CHENGE, AAMBIWA AKAANGALIE MASJAJA
Nora Damian
SIKU moja baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah, kusema kwamba ofisi yake imekamilisha uchunguzi wa madai ya kumiliki Dola za Marekani 1.2 milioni katika Kisiwa cha Jersey, Uingereza yanayomkabili Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge na kwamba imekabidhi faili lake kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kwa ajili ya kumfungulia mashtaka, kiongozi wake, Eliezer Feleshi amejitokeza na kusema kwamba hawahi kuliona jalada hilo.

"Niko safarini subiri hadi wiki ijayo… kwanza ashtakiwe kwa kosa gani? Acheni siasa nyie,” alisema DPP alipotakiwa kuthibitisha kama jalada hilo limefika mezani kwake na lini Mwanasheria huyo Mkuu wa zamani wa Serikali atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili... “Aseme ni tarehe gani alileta jalada hilo kwangu?”

Kutokana na majibu hayo ya DPP, Mwananchi lilimtafuta Dk Hoseah kupata ukweli juu ya kauli yake hiyo aliyoitoa juzi huko Arusha na kusisitiza kuwa jalada hilo limepelekwa katika Ofisi ya DPP na kumtaka mkuu huyo wa Mashitaka nchini asiharakishe kusema hajaliona, kwani siyo lazima kila kitu akabidhiwe mikononi... “Kwani kila kitu kinachopelekwa kwake lazima akione? Ameangalia registry (masjala)?. Suala hili nimeshaliongea nanyi vya kutosha hivyo muulizeni zaidi DPP.”

Juzi, Dk Hoseah alisema taasisi yake imekamilisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili Chenge na kwamba jalada lake limepelekwa kwa DPP kwa hatua zaidi. Alisema Chenge atashtakiwa chini ya Kifungu cha 27 cha Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007. Kwa mujibu wa kifungu hicho, mtu akiwa na mali ambazo hazilingani na kipato chake alichokipata akiwa madarakani au baada ya kuondoka ni kosa kisheria.

Chenge anadaiwa kukutwa na kiasi hicho cha fedha mwaka 2008 baada ya uchunguzi wa kashfa ya ununuzi wa rada uliofanywa na Taasisi ya Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza (SFO). Tuhuma hizo ndizo zilizomfanya alazimike kujiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu mwaka huo.

Malumbano kati ya Dk Hoseah na Feleshi siyo ya kwanza. Mwaka jana waliwahi kulumbana baada ya mkuu huyo wa Takukuru kusema kuna majalada takriban 50 ya kesi za rushwa ambayo yamekaliwa na DPP.

Pia Dk Hoseah aliwahi kumshutumu DPP mbele ya wabunge wakati wa semina elekezi mapema mwaka huu akidai kwamba amekuwa kikwazo cha kesi kubwa za ufisadi kupelekwa mahakamani kwa kukwamisha majalada.

CHANZO: Mwananchi 



Kalapina on politics, Freemasons, war, peace, Rostam, Drugs etc.
More from Kalapina and kikosi http://www.reverbnation.com/tunepak/3387426

Click the banner titled CHEUSI DAWA TV (FID-Q) (see the sidebar) for previous episodes of Fridstyle Friday and much more!


Tunasikitika kuwatangazia kifo cha
Machira  NYITAMBE

Kilichotokea mchana leo huko  MUSOMA-TANZANIA

Mazishi yatafanyika huko Kirongwe, Shirati, katika mkoa wa Mara.


Marehemu ni baba mzazi wa:

Mrs Veronica Dibogo Nyitambe
Mrs Beatrice Nyitambe(Baba Mdogo)
Mr Soni Nyitambe (Baba Mdogo) ,


ambao wote wapo hapa Uingereza.

Msiba upo
14 Rothwell Walk
Caversham
Reading

RG4 5DB

Kwa mawasiliano zaidi tumia simu zifuatazo:
Bernard Chisumo
Mob: (0) 787 612 6862
Home: (0) 118 954 5890 
---------------------------------------------------------------- 

POLENI SANA WAFIWA.SIE TULIMPENDA MAREHEMU LAKINI BWANA ALIMPENDA ZAIDI

22 Jul 2011

Samuel Sitta mwenyewe anayepigwa mkwara na Guninita yupo hoi kwa usingizi.Labda hapo anaota yeye bado Spika

Guninita ‘amvaa’ Sitta
Posted By admin On July 22, 2011 @ 7:59 am In Habari kuu,Mtanzania |

• Adai ni mzigo, anawadanganya na kuwapotosha wananchi
• Asisitiza ni sehemu ya tatizo la mgawo wa umeme
• Asema si mgeni serikalini, ni mchochezi, mnafiki na mfitini
• Aonya anaigawa, anaitumbukiza CCM kwenye shimo
• Asema mambo yakiendelea hicho mwaka 2015 CCM itaambulia patupu

Na Habakuki Urio

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita amemlaumu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta akidai ni mnafiki na mchochezi anayetumika kuigawa CCM na kukitumbukiza chama hicho kwenye shimo.

“Sitta ni sehemu ya serikali na si mgeni serikalini. Alikuwapo tangu kipindi cha Mwalimu Nyerere, na pia alikuwa Spika wa Bunge. Kwa nafasi hizi yeye ni sehemu ya tatizo na siyo kuwadanganya wananchi na kuwapotosha kwa kuirushia serikali lawama.

‘Anaudanganya umma. Anataka kujenga umaarufu ambao siyo wa kwake. Kama ni kuharibu waliharibu wote na siyo kusema tatizo ni la serikali.
‘Sitta amekuwa mchawi wa CCM… chama kinajimaliza chenyewe tena kwa kutumia viongozi wa nafasi za juu.,” alisema Guninita.

Guninita alikuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara Mbezi na Mbezi kwa Msigani katika jana, katika ziara ya kutekeleza agizo la Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete la kuleta mageuzi ndani ya chama hicho na ‘kujivua gamba’.

Alisema hali ya siasa ndani ya chama hicho si shwari kutokana na mgawanyiko mkubwa wa baadhi ya viongozi ambao wanazungumza wanavyojisikia bila kujali maslahi na ukweli ndani ya Chama hicho.

“Kilichotufikisha hapa tulipo leo ni unafiki na fitina za viongozi kama Sitta ambao hawaeleweki wanafanya nini ndani ya chama chetu. Ndiyo maana viongozi wanajiuzulu ovyo, kitu ambacho siyo sahihi, chama kinapoteza makada muhimu na kuwaacha watu mizigo na wafitini.

“Namshangaa Waziri Sitta, ana uwezo wa kwenda kwa Rais muda anaojisikia na pia alikuwa na nafasi ya kuyasema mambo yale katika vikao vya chana “party caucus”, na pia kwenye vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) lakini anaropoka mambo kama hayo mbele ya umma wa watanzania na kuwapa umaarufu wapinzani.

“Amekosa busara kwa kuwa amekiuka maagizo ya Rais. Tunajua hakutumwa na Rais, bali alikurupuka tu, na bila kujijua anaiponda Ilani ya Uchaguzi ya CCM ambayo ndiyo muongozo wa kutekeleza majukumu yetu.
‘Mawaziri na wabunge wanasema tofauti na Rais anavyosema kuhusu matatizo ya umeme kwa sasa,” alisema Guninita

Alisema kauli mbovu za baadhi ya viongozi ambazo hazina ukweli zinabomoa chama, na kama CCM haitakauwa makini na kuwaonya wapotoshaji hao katika uchaguzi mkuu wa 2015 chama hicho kitaambulia patupu.

“Upinzani wanajipanga vizuri katika kuhakikisha mwaka 2015 wanachukua nchi, na kwa hali hii tulio nayo … kwa kauli za akina Sitta watafanikiwa kwa kuwa chama kitakuwa kimeyumba na kukosa imani kwa wapigakura wake.

“Haya siyo maneno ya Waziri, huyu jamaa ana mambo yake anayotekeleza… haiwezekani Sitta leo kuyasema haya, labda ana hasira za kukosa Uspika wakati yalikuwa makubaliano ya CCM kumuondoa kwa mafanikio ya chama na kutimiza sera ya 50 kwa 50.

‘Nilimsikia akisema kuwa atatembea mikoa yote kulisema hilo, lakini nawahakikishia kuwa hatafika Dar es Salaam labda aje na barua ya Mwenyekiti au Katibu Mkuu wa CCM kuwa wamemruhusu kupotosha jamii. Nasema kuwa hatutakubaliana na uongo wake,” alisisitiza Guninita.

Hivi karibuni, katika mkutano wa hadharani mjini Mbeya, Sitta pamoja na mambo mengine, alikaririwa akishauri serikali iwaombe radhi wananchi kutokana na tatizo la mgawo wa umeme unaoendelea nchini hivi sasa.

Guninita alisema mkutano wa jana ni matunda ya makubaliano ya kujivua gamba kama alivyoagiza Mwenyekiti Kikwete na kuwataka viongozi wote wa CCM kutembelea matawi na mashina katika maeneo yao kuyajua matatizo ya wapiga kura wao na kuimarisha mizizi ya chama ambayo ipo katika mashina na matawi.


 
Who Needs Humans?
As if American workers don’t have it rough enough, with unemployment skyrocketing and jobs moving overseas, now there’s another threat: robots.
by Daniel Lyons, July 18, 2011
Amid all the job losses of the Great Recession, there is one category of worker that the economic disruption has been good for: nonhumans.
From self-service checkout lines at the supermarket to industrial robots armed with saws and taught to carve up animal carcasses in slaughter-houses, these ever-more-intelligent machines are now not just assisting workers but actually kicking them out of their jobs.
Automation isn’t just affecting factory workers, either. Some law firms now use artificial intelligence software to scan and read mountains of legal documents, work that previously was performed by highly paid human lawyers.
“Robots continue to have an impact on blue-collar jobs, and white-collar jobs are under attack by microprocessors,” says Edward Leamer, an economics professor at UCLA’s Anderson School of Management and director of the UCLA Anderson Forecast, a survey of the U.S. and California economies. Leamer says the recession permanently wiped out 2.5 million jobs. U.S. gross domestic product has climbed back to pre-recession levels, meaning we’re producing as much as before, only with 6 percent fewer workers. To be sure, robotics are not the only job killers out there, with outsourcing stealing far more gigs than automation.
Jeff Burnstein, president of the Robotics Industry Association, a trade group in Ann Arbor, Mich., argues that robots actually save U.S. jobs. His logic: companies that embrace automation might use fewer workers, but that’s still better than firing everyone and moving the work overseas.
It’s not that robots are cheaper than humans, though often they are. It’s that they are better. “In some cases the quality requirements are so stringent that even if you wanted to have a human do the job, you couldn’t,” Burnstein says. He cites General Motors, which uses robots to lay a bead of sealant on windshields, because humans can’t do the job as precisely.
Same goes for surgeons, who are using robotic systems to perform an ever-growing list of operations—not because the machines save money but because, thanks to the greater precision of robots, the patients recover in less time and have fewer complications, says Dr. Myriam Curet, chief medical adviser at Intuitive Surgical in Sunnyvale, Calif. The surgery bots don’t replace surgeons—you still need a surgeon to drive the robot. And they’re not cheap. Prices go as high as $2.2 million. Nevertheless, Intuitive sold 400 of them just last year. If you’ve had a prostatectomy recently, chances are a robot was involved.

Surgeons may survive the robot invasion, but others at the hospital might not be so lucky, as iRobot, maker of the Roomba, a robot vacuum cleaner, has been showing off Ava, a three-foot-tall droid on wheels that carries a tablet computer. iRobot reckons Ava could be used as a courier in a hospital. And once you’re home, recovering, Ava could let you talk to your doctor, so there’s no need to send someone to your house. That “mobile telepresence” could be useful at the office. If you’re away on a trip, you can still attend a meeting. Just connect via videoconferencing software, so your face appears on Ava’s screen.

Is any job safe? I was hoping to say “journalist,” but researchers are already developing algorithms that can gather facts and write a news story. Which means that a few years from now, a robot could be writing this column. And who will read it? Well, there might be a lot of us hanging around with lots of free time on our hands.

SOURCE: Newsweek 


















Picha zote hizo kwa hisani ya gazeti la Daily Mail zilidakwa na kamera dakika ambapo waogeleaji (pichani) walipokuwa wanajirusha kutoka jukwaani.Ashakum si matusi,hutolaumiwa ukidhani baadhi yao wanajikakamua msalani kushusha "kubwa".

Appeal for Support How to Register


Moja ya matatizo mengi yanayomkabili mtu tuliyemchagua kuwa Rais wetu,Jakaya Kikwete,ni kutokuwa serious.Yeye ni mwepesi wa kuchekacheka hata kwenye mambo yanayohitaji kuwa serious.Anyway,kwanini nimesema hatuna rais?Sio siri,nimepatwa na kichwa kuuma baada ya kusoma mahojiano yafuatayo kati ya Kikwete na mwandishi wa BBC.Angalia majibu yake,angalia vicheko vyake...na kwa hakika unaweza kuafikiana nami kuwa huyu mtu sio tu mbabaishaji bali yawezekana hajui kwanini ni Rais wetu.Anyway,soma mwenyewe

BBC: Suala la Umeme Mheshimiwa Rais Kikwete ungependa kulizungumzia nini?

Rais Kikwete: Tatizo la umeme kimsingi ni suala la ukame tu. Kwa sababu mabwawa yetu ya kuzalisha umeme yanayotoa umeme karibu MW600 sasa hivi yanatoa umeme kidogo sana. Maji pungufu ndio maana kuna tatizo hilo.

BBC:Mheshimiwa, hili suala si la leo wala si la jana limekuwepo kwa muda mrefu, kwanini serikali haina njia mbadala ya kuweza kutatua suala hili? Tanzania ina raslimali nyingi mheshimiwa Kikwete!

Rais Kikwete: Kwanza serikali haina uwezo wa kufanya mvua inyeshe, unajua unajua hivyo, Kwa sababu (kicheko) ingekuwa na uwezo wa kufanya mvua inyeshe mabwawa yale yangejaa. Ni kweli kuwa Tanzania inazo raslimali za kutosha na katika kipindi hiki - toka wakati ule - sisi tulipoingia tumekuta suala la Ukame na mwaka 2007 tukapata matatizo ya kwanza.

Baada ya pale tukafanya uamuzi kwamba sasa tuanze kuwekeza katika vyanzo vingine; tuongeze uzalishaji wa umeme kutoka vyanzo vingine. Tuongeze uzalishaji wa umeme kutoka vya vya kutumia gesi asilia twende kwenye makaa ya mawe. Kutoka vyanzo vya gesi asilia tayari tuna mtambo pale Ubungo, na toka mwaka 2009 mpaka sasa tumeshaongeza MW145, itakapofika Disemba tutakuwa tumeongeza MW160 nyingine. Tutakuwa tumeongeza MW300 siyo kidogo.

BBC: Mhe. Kikwete Mmoja katika wabunge Bw. John Mnyika ambaye ni Mbunge wa upinzani ambaye ni Waziri Kivuli wa Nishati amekuwa akilalamika na kwamba amewahi kusema kwamba hili tatizo ni tatizo linalowahusu Watanzania wote na amesema mje pamoja na kuona vipi mtakavyotatua tatizo hili. Na sasa hivi Bungeni wamesimamisha mswada, wa kutoa bajeti ya nishati ya Tanzania. Wewe unachukulia vipi matamshi kama haya kutoka kwa Wabunge?

Rais Kikwete: Mimi nasema hivi yeye si Mbunge atoe maarifa yake tu; anayo maarifa gani na anapendekeza kitu gani. Kwa sababu toka Uhuru mabwawa tuliyotengeneza ni Kidatu MW200, Mtera MW80, Kihansi MW 165 mimi nilipokuwa Waziri wa Nishati, pale Pangani tumeongeza.

Sasa ufikirie kwamba toka Uhuru tumeweza kuzalisha umeme wa MW600, lakini toka 2009 mpaka Disemba mwaka huu tutakuwa tumeongeza MW300! Ni jitihada kubwa. Mimi nasema kwamba usipozitambua hizo ni kwamba wewe mwenyewe siyo mkweli.

Sasa ni hivi, unajua hii mitambo ya umeme si mitambo unaenda kununua kama unavyonunua jaketi lako hili. Ni kwamba ukitaka mitambo ya umeme, lazima uweke order wakutengenezee. Huu mtambo unaofika mwaka huu Disemba order tuliweka mwezi wa Juni mwaka jana. Inachukua muda huo kutengeneza. Sasa ingekuwa mnaenda kutafuta mitumba, mitumba ya mitambo tu ya kununua iko mingi kweli. Tukasema hatuwezi kufanya hivyo.

Mimi nasema hivi, kitu kikubwa ni kuwa na subira. Tumefanya jitihada kubwa. Ni lazima watu watambue kuwa tumefanya jitihada kubwa katika miaka hii toka 2009 mpaka sasa hivi 2011 Disemba tutakuwa tumeongeza MW300 kulinganisha na MW600 ambazo tumeziongeza katika miaka yote hii. Nasema ni lazima watu watambue hivi. Sasa kama kuna mtu ana maarifa ya haraka zaidi nasema mtu atoe maarifa hayo na sisi kama yapo tutayafanyia kazi.

BBC: Kuna njia kama umeme wa jua, umeme wa kutokea ardhini wa mvuke, kwanini serikali haitafuti njia mbadala kuzalisha umeme kwa njia hizo?

Rais Kikwete: Nasema hivi, hata umeme wa jua lazima ujenge, umeme wa mvuke lazima ujenge, si kitu cha mwezi mmoja. Nasema huo ndio ukweli wenyewe na wakati mwingine na nyinyi mjifunze hayo mambo ya kitaalamu kulikoni kuuliza tu hivi hivi. Unajua ungekuwa na wewe unauliza kwa hoja - “unajua kwamba hiki kitu hiki ingekuwa umeme wa jua miezi miwili tu upo” - tungeweza kufanya hivyo.

Sisi sasa hivi kwa mfano tunajiandaa kuzalisha umeme wa kutumia Upepo, pale Singida. Tuna mwaka wa tatu sasa tuna mipango na Wakorea wa Kusini, umeme haujakuwepo. Kwa hiyo nasema hayo ni maelezo rahisi. Wanasema “mbona jua lipo?” katengeneze umeme wa jua kama jua lipo! (kicheko).

BBC: Watanzania wamekuwa wakisema (mwisho kabisa) kwamba Tanesco ingebinafsishwa ili waweze kupata makampuni kufanya kazi hiyo ya umeme?

Rais Kikwete: Aah! Kwani ukitaifisha kesho ndio utapata mitambo kesho? Nasema hivi ni vizuri kuelewa tu - kwanza tatizo la msingi - ni maji kukauka kwenye mabwawa. Maji yasingekauka kwenye mabwawa tatizo hili halipo. Maji yamekauka kwenye mabwawa kwa sababu ya ukame. Hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzuia ukame usiwepo. Sasa hiki ndicho kiini cha tatizo. Sasa nasema sisi jitihada ambayo tumeifanya ni kupunguza sasa kutegemea umeme unaotakana na nguvu ya maji.

Toka mwaka 2009 tumewekeza adi Disemba 2011 tutakuwa tumeongeza MW 310, yenyewe hiyo ni hitihada kubwa, ni vizuri ukaitambua jitihada hiyo. Kulikoni kusema kitu tu nasema hata kama huna majawabu rahisi utuambie tu.

MSIKILIZE HAPA


Usanii wa Wachina katika kufoji umekwenda hatua ya juu zaidi baada ya bloga mmoja kugundua maduka makubwa (malls) matatu ya bidhaa za kampuni ya Apple (inayotengeneza iPhone,iPads,nk).Kichekesho ni kwamba maduka hayo ni feki kwa vile hayana kibali cha kampuni ya Apple.Lakini to make matter even worse,biahdaa zote za Apple zinazouzwa kwenye maduka hayo nazo ni feki pia.Kama hiyo haitoshi,hata wafanyakazi wa maduka hayo nao "waliingizwa mjini" kwani siku zote walikuwa wanaamini kuwa wao ni waajiriwa wa Apple ya Marekani.

Halafu hawa ndio watu tunaowaamini kama mapatna wetu wa maendeleo katika jitihada zetu za kujiweka mbali na "Wazungu"!! Angalia picha hizi na video








Mwanamama mmoja na mumewe huko Aberdeen,Scotland walikumbwa na kiwewe baada ya kukumbana na bonge la dude kwenye ufukwe wa Bahari ya Kaskazini.Well,dude hilo halikuwa hai bali kiufasaha ni masalia ya "sea monster" (sijaui tafsiri yake kwa Kiswahili ni ipi)?Pata picha ndio ungekuwa wewe peke yako...Hadi sasa haijafahamiaka masalia hayo ni ya kiumbe gani wa baharini lakini wataalam wanabashiri kuwa inawezekana ni ya papa muuaji (killer whale) au papa rubani (pilot whale)

Papa muuaji  

Papa rubani

20 Jul 2011



Majaribio yameanza ya kinga inayotokana na mimea kutumika kama kinga dhidi ya virusi vinavyosababisha upungufu wa kinga ya mwili (UKIMWI).Kinga hiyo inatengenezwa kwa kutumia majani ya tumbaku iliyozalishwa maabara,ikitarajiwa kuwa ufanisi wake utapunguza gharama ya dawa za kurefusha maisha ya waathirika wa ugonjwa huo,na kwa muda mrefu kupata tiba ya kudumu ya ugonjwa huo.

Vidonge vilivyotengenzwa kutokana na mimea vinafanyiwa majaribio kwa kundi la wanawake hapa Uingereza,hasa kuangalia ufanisi wake.Watengenezaji wa vidonge hivyo wanategemea vitasaidia kupatikana kwa kinga dhidi ya maambukizo ya virusi vinavyosababisha ukimwi lakini mafanikio makubwa yanatarajiwa kwenye ukweli kwamba molekyuli zinazotarajiwa kuwa na ufanisi ni nafuu zaidi kwa minajili ya gharama.

Majaribio hayo katika miili ya binadamu yameidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Madawa na Huduma za Afya ya hapa Uingereza,na inafanyika huko Guildford katika taasisi ya utafiti wa afya ya Chuo Kikuu cha Surrey.

"Pharma-Plant" ni mradi ulioanzishwa miaka saba iliyopita ukiwa na lengo la kutumia mimea iliyozalishwa maabara kupunguza gharama ya uzalishaji wa vidonge kwa ajili ya tiba mbalimbali.Wanasayansi wanadhamiria kutengenza madawa yenye ufanisi lakini kwa gharama nafuu,na kuzisaidia nchi masikini duniani.

Habari hii imetafsiriwa kutoka katika gazeti la Guardian.Kwa habari kamili soma HAPA

19 Jul 2011


Rais Kikwete kutembelea Afrika Kusini 
Monday, 18 July 2011 21:28

Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete, jana alianza ziara ya kihistoria ya kidola nchini Afrika Kusini, ikiwa ni ziara ya kwanza ya aina yake, kufanywa na Rais wa Tanzania katika nchi hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, Rais Kikwete anafanya ziara hiyo kwa mwaliko wa Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ambaye utawala wake umekuwa uhusiano wa karibu na Tanzania, tangu aliposhika madaraka ya kuongoza taifa hilo kubwa kiuchumi kuliko mengine, katika Afrika.

Rais Kikwete na ujumbe wake unaojumshia pia mkewe, Mama Salma Kikwete, uliondoka nchini jana mchana kwenda Pretoria, kwa ziara hiyo ya siku nne.Pamoja na kwamba marais wa Tanzania waliomtangulia Rais Kikwete wametembelea Afrika Kusini mara nyingi kwa shughuli mbalimbali, lakini hakuna kiongozi aliyepata kualikwa kufanya ziara rasmi, ya kiserikali ama ya Kidola, tangu nchi hiyo ilipoingia katika mfumo wa demokrasia mwaka 1994.

Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, Rais Kikwete na ujumbe wake, watapokelewa rasmi leo asubuhi katika Jumba la Serikali, mjini Pretoria.Tayari Rais Zuma na mkewe walikwishajipanga kwa sherehe za makaribisho zitakazofuatiwa na mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati ya Tanzania na Afrika Kusini.

Mazungumzo hayo, yatafuatiwa na utiaji saini wa mikataba na makubaliano katika nyanja mbalimbali kati ya nchi hizo mbili.Baadaye, viongozi hao wawili watahutubia mkutano wa waandishi wa habari na baada ya hapo, Rais Kikwete atatembelea Uwanja wa Uhuru akiandamana na Rais Zuma.

Mchana viongozi hao watahudhuria chakula cha mchana kikiwashirikisha pia wafanyabiashara wa Tanzania na Afrika Kusini ambao watazungumza na kuelezea umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.Jioni, Rais Zuma ataandaa dhifa ya kitaifa kwa ajili ya Rais Kikwete na ujumbe wake .

Keshokutwa, Rais Kikwete na ujumbe wake watakwenda Cape Town, ambako miongoni mwa mambo mengine ujumbe huo utatembelea Kisiwa cha Robben ambako wapigania uhuru maarufu wa Afrika Kusini, akiwamo Rais Mstaafu Nelson Mandela, walifungwa kwa miaka mingi na makaburu. Rais Kikwete atarejea nyumbani keshokutwa asubuhi.

CHANZO: Mwananchi 

LABDA AKIREJEA KUZURURA TATIZO LA UMEME LITAKUWA LIMEPATA UFUMBUZI. 




Kama kuna kosa ambalo Watanzania watalijutia kwa muda mrefu sana ni lile walilofanya mwaka 2005 na kisha kulirudia mwaka jana kumchagua Jakaya Kikwete kuwa Rais wa nne wa Tanzania.Tusiume maneno,mengi ya matatizo yanayoikabili nchi yetu kwa sasa ymesababisha,yanasababishwa au yamechangiwa au yanachangiwa na ubabaishaji wa Kikwete.

Ni nani mwenye akili timamu asiyefahamu kuwa wakati kelele dhidi ya ufisadi zinaelekezwa kwa "mapacha watatu" waliobaki wawili (ie Lowassa na Chenge,na Ristam aliyejiuzulu),Kikwete ni sehemu muhimu kabisa ya tuhuma zinazoelekezwa kwa wanasiasa hao.Hapa simaanishi kuwatetea mafisadi hao bali ninachojaribu kupigia mstari ni ukweli kwamba Kikwete hana tofauti na Lowassa,Chenge au Rostam.Na hilo halihitaji ufafanuzi.Yeye anajua,mapacha watuatu waliobaki wawili wanajua,na kila Mtanzania mwenye akili tiammu anajua.Kwanini hadi leo Kikwete bado ni Rais wetu ni swali gumu kulijibu just like lile la kwanini alichaguliwa mara ya kwanza mwaka 2005 na baadaye 2010 ilhali wanamjua walikuwa wanatambua bayana kuwa hana sifa za kushika wadhifa huo mkubwa kabisa katika nchi yetu.

Anyway,lengo la makala hii sio kujadili ubabaishaji wa Kikwete katika utendaji kazi wake bali lengo ni kukemea kwa nguvu kubwa uhuni uliofanywa na Kikwete wa kufanya harusi ya mdogo wake kwenye Ikulu ndogo ya Bagamoyo.Hivi kwa kuwa Rais,Kikwete anadhani kuwa Watanzania wametoa urais kwa ukoo wake mzima?Kwanini asikodi ukumbi kwa fedha zake kisha akamfanyia sherehe mdogo wake?

Kama huelewi kwanini ninalamika,Ikulu iwe ile ya Magogoni au hizo ndogo za wilayani na mikoani ni mahala patakatifu-kama alivyowahi kusema Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.Si mahala ambapo kila Tom,Harry and Dick anaweza kufanya atakalo.Lakini licha ya utakatifu huo wa Ikulu,ifahamike kuwa mahala hapo panaendeshwa kwa fedha za walipakodi.Kwa mantiki hiyo,kufanyia sherehe mahala hapo ni sawa na kuwabebesha gharama Watanzania kwa ajili ya harusi ya ndugu wa Kikwete.Sidhani hata waliompigia kura mwaka jana au 2005 walitamani kuona kura waliyompigia Jakaya inageuzwa kuwa mithili ya kuupigia kura ukoo wake mzima.

Huu ni uhuni unaopaswa kukemewa vikali.Rais anaweza kuzurura nje ya nchi atakavyo (inaelekea kama hakuna namna ya kumwelewesha kuwa safari zake za mara kwa mara nje ya nchi ni mzigo mkubwa kwa Watanzania) lakini kamwe tusiruhusu nafasi ya Urais ikageuzwa kuwa kama cheo cha kifamilia.

Madhara ya kumwacha Kikwete aendelee na madudu yake ni kwamba anaweza kumaliza muda wake hapo 2015 na kuiacha Tanzania ikiwa jina tu-haina maadili,haina raslimali,na kibaya zaidi,nafasi ya urais ikaishia kuwa na heshima ndogo kuliko ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa.

PICHA: Kwa hisani ya Global Publishers

18 Jul 2011


BRILLIANT BUDGET SPEECH, HONGERA SANA! 
Nd. Mnyika,
Nimesoma hotuba yako bungeni hapa chini kwa makini sana na kupata faraja kubwa – hongera nyingi, na kama wasemavyo wataliano – BRAVISSIMO!  Pia nimefurahi zaidi baada ya kuona baadhi ya yale ninayoandika na kushauri, hususan maswala ya urani (uranium), kupewa hisa watanzania, STAMICO na TPDC, maswala ya kulinda na kuhufadhi vizuri mazingira ya nchi wakati wa uchumbaji wa madini, haja ya kuchunguza na kubadilisha mikataba mibovu ya madini ikiwa ni pamoja na ulaghai wa kampuni kama Williamson Diamonds, TanzaniteOne, uzembe uliofanyika kuingia mikataba mibovu ya gesi asilia n.k., haya mambo yote umeyachambua ipasavyo na hata kwenda mbele zaidi kwa kuweka bayana baadhi ya mambo mengine ambayo mimi kama mtaaalamu sikuwa nayafahamu kuwa yanatendeka Tanzania hivyo kuweza kunipa habari ambazo zitanisaidia kuyachambua kitaalamu, tena kwa kina. Nimepaka rangi baadhi ya sehemu kwenye hotuba yako kuonyesha yale ambayo yamenigusa zaidi na mambo ambayo niliwahi kuyakemea na kusisitiza yachunguzwe na kubadilishwa kwa muda mrefu.
Nadhani utakuwa umesoma barua zangu za hivi karibuni zinazohusu maswala ya madini nchini Mongolia na Sudani Kusini – ziko hapa. Ni matumaini yangu mtazichambua barua hizi pamoja na wenzako wa kambi ya upinzani Bungeni na muangalie namna gani mnaweza kuhakikisha yale muhimu kwa taifa letu yanaweza yakatekelezwa Tanzania. Ndani ya barua hizo utaona pia maoni yangu kuhusu mauaji ya Tarime uliyoniuliza hapo awali ingawa msimamo wangu kuhusu hili jambo niliwahi kuzungumzia vikali kwenye baadhi ya barua zangu zikiwezo hizi hapa: 1 (soma kuhusu mamillionea wa kimya kimya - Silent Millionaires – walivyowadanganya watu wetu Bulyanhulu. Baadhi ya hawa mamillionea ni/au walikuwa wafanyakazi wa serikali). Soma pia hapa 2, pamoja na hapa 3.
Pia hapa chini nakutumia tovuti za makala kadhaa ambazo nadhani ni muhimu kuzisoma hasa baada ya kuona kuwa ni mambo ambayo uliyazungumzia kwenye hotuba yako na mimi pia nimekuwa nikisisitiza kwa muda mrefu yafanyiwe kazi na serikali. Ni matumaini yangu utaendela na msimamo wako imara wa kuibana serikali ifanye marekebisho pale ambapo inaonekana kuwa rasilimali za taifa haziwanufaishi watanzania, na wale waliongia nchini kama wawekezaji wa kigeni, na hata raia na makampuni yetu ya Tanzania, wanakiuka na kuvunja sheria za sekta ya madini. Ni muhimu makosa makubwa tunayoyafanya kwenye sekata ya madini, gesi asilia na petroli yarekebishwe, tena haraka sana. Kama ulivyoeleza kwenye hotuba yako, hakuna sababu yeyote ya msingi watanzania waishi kwenye umaskini wa kutupwa huku wakiwa na utajiri mkubwa wa madini kama tulionao, utajiri ambao serikali yetu inautoa, hata niseme, kuutupa kwa wageni – hii si sahihi hata kidogo. Nitashukuru kama utakuwa unaniarifu mara kwa mara maendeleo ya jitihada zenu kufanikisha azma hii.
Ahsante, na pongezi nyingi kwa ujasiri na uimara wako Bungeni.
Shaaban
Moscow, Urusi.     


MNAKARIBISHWA NYOTE KWENYE SABATO YA WAGENI TAREHE 23/07/2011

Kanisa la wasabato ( Angaza Swahil UK)  linapenda kuwakaribisha  watu wote    kutoka sehemu mbali mbali za Uingereza katika sabato ya wageni itakayofanyika tarehe 23/07/2011 kuanzia saa 3.00 asb hadi saa 11.00 jioni.
Siku hiyo itakuwa ya pekee kweli kwani vikundi mbali mbali vya nyimbo vitakaribishwa kuimba kutoka kwenye kila dhehebu  .Pia watoto wataonyesha programme mbali mbali.

 THEME: NJOO UJUE UNA NINI MKONONI MWAKO

Baada ya ibada ya mchana tutakusanyika pamoja kwa ajili ya chakula na vinywaji.Usipange kukosa lete rafiki yako .Kama hauna usafiri i wasiliana nasi.KARIBU NYOTE

ANUANI
St Barnabas C Of E Church
Elm Road, Reading, RG6 5TS


 


16 Jul 2011


School of Public Policy Building Bridges
Tanzanian Student Wins Research Award
Most young people in Tanzania have never heard of the Maryland School of Public Policy. But through the generosity of those who saw the promise in Emmanuel Sulle, he has completed his first year of studies at the School and has also won the Conservation Research in Eastern Africa’s Threatened Ecosystems (CREATE) Research Award from the Frankfurt Zoological Society. Sulle will study the impact of microcredit institutions (in this case Community Conservation Banks) which are in place within the Serengeti ecosystem in Tanzania. Sulle will conduct the field research in Tanzania during the winter break of 2011-2012.
"Emmanuel is a wonderful example of the School's bridge across the oceans--of using the tools of public policy to improve the quality of life and to make a big impact on the world," says MSPP Dean Don Kettl.
Sulle was working as a Research Associate at the Tanzania Natural Resource Forum when he was encouraged by Professor Robert Nelson to apply to the MSPP program. Nelson’s son Fred, who worked 12 years in Tanzania on wildlife conservation, had worked with Sulle on two research studies – most recently the published report on “Biofuels, land access and rural livelihoods in Tanzania”.
“We need more people like Emmanuel,” said Bob Nelson, who also serves as Sulle’s informal mentor.
  “Unfortunately, they are hard to identify.”
Sulle is currently in Tanzania collaborating with the Maliasili Initiatives to undertake two research projects on “Wildlife Management Areas and Pastoralist Livelihoods: An Assessment,” and “Analysis from Northern Tanzania and Community-based Conservation in the Tarangire-Manyara Corridor: An Assessment of Existing Models and Experiences.”
“Emmanuel is in a position to take his MSPP education and make a serious policy impact in Tanzania,” says MSPP Student Affairs Assistant Director, Taryn Faulkner.
Sulle earned his BA in Economics from St. Augustine University of Tanzania (SAUT) in 2008. He has carried out a variety of research projects commissioned by, or in collaboration with MISERIOR-Germany, Fulbright, Tanzania Natural Resource Forum, Sand County Foundation, and Health and Development International Consultants. He has authored and co-authored a number of research reports on tourism revenue transparency, wildlife management areas, as well as biofuels, land access, and rural livelihoods in Tanzania.
“I am interested to see rational use of natural resources as a tool for poverty reduction in developing countries,” Sulle said.

HONGERA SANA,NDUGU EMMANUEL.KILA LA HERI.

12 Jul 2011


Ndugu zangu wapendwa,kwa niaba ya familia ya Chahali naomba kuwasilisha shukrani za dhati kwa wote ambao kwa namna moja au nyingine mmeungana nasi kwa maombi kwa baba Mzee Philemon Chahali ambaye hali yake bado ni mahututi kufuatia ajali ya kugongwa na pikipiki huko Ifakara,Alhamisi iliyopita.

Ningetamani sana kutoa shukrani kwa kutaja jina la kila mmoja wenu lakini naomba nitoe shukrani za jumla.Nawashukuru sana bloggers wenzangu ambao licha ya kunisaidia kuweka tangazo la maombi ya sala kwa baba mmekuwa mkinitumia meseji na barua pepe za kunipa moyo pamoja na sala/dua zenu.Katika kuonyesha upendo wa hali ya juu,dada yangu blogger wa hapa UK Rachel Siwa aliweka maombi kwenye misa ya Jumapili iliyopita huko Coventry.Tunakushukuru sana dada Rachel na Mungu akubariki.Bloga mwenzangu Miss Jestina naye amekuwa akitujulia hali ya Mzee mara kadhaa kwa siku,bila kuwasahau wadogo zangu Jackie Lawrence (La Princessa) na Faith Charles Hillary (Candy1World) ,na Mtakatifu Simon Kitururu,bloga Malkiory  Matiya na Nova Kambota

Huko Twitter nimekuwa nikipata sapoti ya kutosha tangu zilipojiri habari za ajali.Dada zangu Maria Sarungi na Lilly  Melody,pamoja na wasanii wetu mahiri kabisa Hamisi Mwinjuma (Mwana FA) na Joseph Haule (Profesa Jay) ni miongoni mwa wana-Twitter wenzangu ambao wamekuwa mstari wa mbele kunifariji.

Kwa bahati mbaya,ukweli mchungu kuhusu maisha ni kwamba mpaka upate tatizo ndio unaweza kufahamu upendo wa watu wanaokuzunguka.Kuna watu nilikuwa sifahamiani nao kabisa lakini baada ya kusikia habari za ajali iliyomkumba baba wamekuwa ni nguzo muhimu kutusapoti.Kwa kweli ninawashukuru sana na Mungu awabariki sana kwa upendo wenu.Ni imani ya familia yetu kuwa sala zenu na zetu zitamsaidia Mzee Chahali sio tu kupata nafuu bali kupona kabisa.

Kwa vile inaniwia vigumu kublog kutokana na tatizo linalonikabili,naomba pia kutumia fursa hii kuwashukuru wasomaji wote wa blogu hii na watu wengineo walionipigia kura katika Tuzo la Blogu za Kitanzania (Tanzanian Blog Awards) ambapo japo sikuibuka mshindi lakini nimepata matokeo ya kupigiwa mstari.Kwa kifupi,blogu hii imeshika nafasi ya pili katika categories za Best Inspiration Blog na Best News Blogs na imeshika nafasi ya tatu katika category ya Best Political Blog.Ukiangalia kwenye hizo categories mbili za mwanzo utagundua kuwa aliyeshika nafasi ya kwanza ni bloga ambaye blogu yake imeshatembelewa na wasomaji zaidi ya milioni 12 wakati blogu hii "inasuasua" na wasomaji 424538 hadi dakika hii.Kwangu hayo ni mafanikio makubwa sana lakini si mafanikio yangu pekee bali ya wadau wote wa blogu hii.Namshukuru kila aliyenipigia kura,na japo hatukuibuka washindi wa jumla,kushiriki kwenye tuzo hizo na kukamata nafasi za juu ni tuzo kubwa sana.

Naomba nimalizie kwa kurejea tena shukrani zangu na za familia yangu kwenue nyote mnaoshirikiana nasi kwenye maombi kwa ajili ya Mzee Philemon Chahali.Ni matumaini yetu kuwa Bwana anasikiliza sala/dua zetu na atamjalia baba uponyaji kwa vile Mungu ni mwema na mwenye upendo.

ASANTENI SANA

7 Jul 2011


Nasikitika kuwafahamisha kuwa baba mzazi Mzee Philemon Chahali amepata ajali mbaya asubuhi hii huko Ifakara.Amegongwa na pikipiki ambazo ndio usafiri mkuu wa huko.Kwa mujibu wa habari nilizonazo hadi muda huu,hali yake ni mbaya,ambapo licha ya kuvnjika mguu pia ameumia kichwani.Kibaya zaidi ni kwamba umri wake ni kwenye miaka ya 80 kwa hiyo mshtuko tu wa ajli unaweza kumwathiri sana.

Basi naomba kutumia fursa hii kuomba sala zenu.Sie Wakristo tunaamini kuwa wanapojumuka wengi kufanya sala basi Mungu naye anakuwepo.Natumaini kwa sala zenu na za familia yetu Mungu atamjalia baba apone na kurejea katika hali yake ya kawaida.

Natanguliza shukrani zangu za dhati.Asanteni 


Na Nova Kambota,

Rais wa awamu ya tatu Mzee Benjamin Mkapa aliwahi kusema kuwa maisha bila vipaumbele ni ujinga mtupu, bilashaka hili halina ubishi kabisa taifa lolote linaloishi bila vipaumbele hugeuka taifa la wahuni, waporaji, mafisadi, wajinga,duni na zaidi huwa taifa legelege na dhaifu.

Wageni mbalimbali kutoka Ulaya, Marekani ,Asia na sehemu nyingine za ulimwengu waliowahi kufika nchini huwa wanashangazwa sana na umasikini wa kutisha unaowaandama wananchi wa taifa hili. Wageni wanatushangaa sana na wataendelea kushangaa kuanzia Mlima Kilimanjaro,Mlima Meru, Udzungwa, Usambara, Ziwa Tanganyika, Victoria, Bahari ya Hindi mbuga nzuri za wanyama kama Mikumi na Ngorongoro lakini pia misitu ya kumwaga tu,mito mingi, mabonde ndiyo usiseme na ardhi yenye rutuba na

ya kutosha lakini bado miaka hamsini baada ya uhuru mamilioni ya watanzania bado ni masikini wa kutupwa.

Kwa mtiririko huu wa mantiki hapa ndiyo inaibuka hoja kuwa watanzania hawafanani na nchi yao hata kidogo kwa maana ni watu mafukara waliozungukwa na utajiri wa kutisha , hakika kuna utofauti mkubwa kati ya watanzania na utajiri wa taifa lao, hata ukifika pale mbuga ya Ngorongoro wanyama wanacheza na kufurahi na ndege wanarukaruka kwa furaha kubwa, nenda kandokando ya bahari ya Hindi uone mawimbi yanavyopanda na kushuka kwa furaha kisha angalia samaki walivyo na furaha kisha sasa rudi katika maisha ya walalahoi wa nchi hii, kweli inahuzunisha kuona wanyama wana furaha kushinda watanzania, inauma sana!

Kuna kisa kimoja cha kuhuzunisha sana ambacho nadhani watoto wetu wanapaswa kufundishwa madarasani. Inaelezwa kuwa mwaka jana 2010 wakati wa uchaguzi mkuu mwangalizi mmoja wa kimataifa kutoka nje alitembelea Tunduru akaona watu wanavyoogelea kwenye umasikini wa kutisha kisha akatupa macho kwa mbali akaona misitu mizuri na mto Ruvuma kisha akahoji kuwa inakuwaje watu hao ni masikini sana? Wananchi hawakuwa na la kujibu baadaye mzungu huyo akasema kuwa “siamini kabisa na hainiingii akilini kuwa CCM huwa inashinda kihalali kwa maana haiwezekani watu masikini kama hawa waichague CCM”

Hivi nani atanishawishi kuwa CCM inashinda kihalali? Hapa uhalali unaozungumzwa sio wa kura tu bali hata wa kuwaacha watu huru, kwa maana haiwezekani watu wanakuwa masikini, wanafanywa wajinga na mifumo mibovu kiasi kwamba hawajui umuhimu wa kura halafu wanajiandikisha watu milioni 19 kupiga kura lakini siku ya kupiga kura wanajitokeza milioni 5 na CCM wanashinda! Kisha uniambie hapo kuna ushindi? Ushindi gani? wakati milioni 14 nzima hawajapiga kura? Idadi hii inaweza kubadili matokeo, kwa maana nyingine yule mwangalizi wa kimataifa yupo sahihi kabisa kuwa watanzania hawaichagui CCM badala yake inajichagua yenyewe na kujipa madaraka, ajabu sana!

Watanzania wanalia kwa mengi, heri wote wangekuwa masikini lakini kuna wenzao “wajanja wachache” wanaishi kama wafalme kwa jasho la watanzania. Cha ajabu katika umasikini huu wa kutisha wa watanzania kuna baadhi ya watanzania wachache wamejigeuza “miungu watu” wamejimilikisha utajiri wote huu wakisaidiana na waporaji mabeberu kutoka Ulaya na Marekani, hawa hawajui njaa ni nini? hawafahamu masikini anafananaje? Wenyewe wanajua kuvaa suti na tai na mwisho wa mwaka wanaenda kwenye maduka makubwa ya nguo huko London na Dubai ili kuwafanyia “shopping” wake zao na watoto wao wapendwa.

Nchi imekuwa ya matabaka kiasi kwamba mpaka taifa linayumba . Leo hii imefika mahali kuna watu wana nguvu za kutisha kwenye nchi mpaka mkurugenzi wa TAKUKURU anakiri kwenye mtandao wa Wikileaks kuwa Tanzania kuna “untouchables” hawagusiki hawa. Katika mazingira haya bado CCM inahubiri usawa, usawa gani? hata mtoto mdogo hawezi kushawishika kuwa kuna hata chembe ya huo usawa kwenye nchi hii, labda kidogo CCM waje na hoja ya kuwa na nchi mbili za kimatabaka kwenye taifa moja ndiyo! Kuna Tanzania ya tabaka la juu na Tanzania ya tabaka la chini.

Huu ndiyo ukweli wa mambo , na matabaka haya mwanzo wake ni kuwa kuna wale walioshikilia utajiri wa taifa na wale waliotengwa na utajiri huo. Cha kusikitisha zaidi serikali inapigia chapuo mpasuko huu wa kitabaka kiasi kwamba imejenga shule za kata maalumu kwa masikini ili wakafeli na kuna mashule ya kimataifa yenye ubora haya ni maalumu kwa ajili ya watoto wao na maswahiba zao. Serikali haijaishia hapo tu sasa hivi Tanzania fedha iko juu ya sheria , nani asiyefahamu ukiwa na fedha nchi hii unaweza kupindisha sheria? Zaidi ya yote kuonyesha kuwa serikali yetu ni legelege ni jinsi inavyozitekeleza hospitali za serikali kiasi kwamba ni kama majengo tu bila dawa na ili kuonyesha kweli ubaguzi ni mfumo rasmi kwenye nchii hii hakuna “mkubwa” anaayekwenda kwenye hospitali za serikali huko ni kwa kapuku na walalahoi, ubaguzi wa kutisha!

Viongozi hawaishii hapo tu kwenye juhudi zao za kuwafukarisha wananchi na kuwaibia mali zao, sasa wameanzisha soko huria la kura na wapiga kura na mnada kila baada ya miaka mitano. Hivi kwanini viongozi wasiwaache huru watanzania? Kwanini wasiwaache wakajichagulia watu wanaowaamini ni viongozi bora? Huu kama sio ujambazi wa haki za masikini ni nini? yaani hao walioko madarakani mwaka jana tu walipambana kununua kura kama sio kwenye ngazi ya chama basi kwenye uchaguzi kamili lakini ndiyo hivyo ukweli ni kuwa wamenunua kura kwa pesa nyingi na sasa wapo madarakani wanashindana kupora mali za wavuja jasho.

Taifa limekosa vipaumbele , limehalalisha rushwa, uporaji na ufisadi, taifa linapepesuka kwa uhuni na tamaa za viongozi , dola imedhoofika sana hata kamanda mkuu Rais Jakaya Kikwete analifahamu hili lakini tatizo “kupe” wamejaa kuanzia huko CCM mpaka serikalini. Kile alichokitabiri Mwalimu Nyerere sasa kinatokea kweli, Mwalimu aliwahi kusema “serikali isiyojali wananchi wake haina uhalali hata kama imepigiwa kura” sitaki kuamini kuwa serikali ya CCM haina uhalali ila nashawishika kuwa haijali wala kuthamini wananchi wake hivyo kwa maana nyingine imeanza kupoteza uhalali wake.

Imefika sehemu sasa watanzania wanapaswa kufanana na utajiri wa nchi yao, viongozi inabidi wafahamu kuwa watanzania hawana sababu ya kuwa masikini kama walivyo sasa. Watanzania lazima wafanywe kujivunia utanzania wao tofauti na hivi sasa ambapo kuna watanzania wanajilaani kwa kuwa watanzania yote kwasababu ya ubabaishaji wa viongozi wao ambao badala ya kuwatumikia wananchi wao wako “busy” kutumikia matumbo yao na familia zao.

Lakini kama kawaida ya viongozi wetu wana tabia ya kuweka pamba masikioni hawataki kusikia bilashaka hata hili watapuuzia lakini nawapa angalizo kuwa watanzania wanafahamu kuwa hawakuumbwa walivyo bali umasikini wao umetengenezwa hivyo ni swala la muda tu lakini siku ikifika uvumilivu utakapowashinda basi watawang’oa wababaishaji wote wanaojineemesha na mali zao tena kwa njia yoyote ile, hizi ni zama za ukweli na uwazi ni wakati sahihi wa kuwa na mgawanyo sawa wa keki ya taifa…..Allutacontinua!

Nova Kambota Mwanaharakati,



+255717 709618

Tanzania, East Africa

07/07/2011, Alhamisi

Naomba kura yako kwenye tuzo za blog Tanzania kwenye category ya best collaboration/group blog, best informative political blog na best political blog kunipigia kura nenda http://www.tanzanianblogawards.com/


 

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.