8 Mar 2009

Bonyeza HAPA kwa habari na video.

5 Mar 2009

SAKATA la ununuzi wa mitambo ya ufuaji umeme wa dharura ya kampuni ya Dowans Tanzania Limited, jana lilimgusa spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta na kuamua kutoa tamko kali la kuitahadharisha serikali dhidi ya azma yake ya kutaka kuinunua mitambo hiyo yenye utata.

Spika Sitta pia ameonya kuwa mkasa wa kampuni tata ya Richmond Development (RDC) LLC uliotikisa kiasi cha kusababisha Edward Lowassa awajibike kwa kujizulu wadhifa wake wa waziri mkuu, lisifufuliwe upya kwa kutumia Dowans, ambayo ilirithishwa mkataba wa miaka miwili wa kufua umeme wa dharura.


Richmond ilishinda zabuni ya kufua umeme wa dharura kwa njia iliyojaa utata kabla ya matatizo ya usajili wake kuzua maswali mengi na kusababisha Dowans warithishwe mkataba huo mwaka 2006.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Sitta alieleza nafasi ya Bunge katika kuisimamia na kuishauri serikali katika utekelezaji wa majukumu yake, huku akitaka ushauri wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini wa kuizuia serikali isinunue mitambo hiyo uheshimiwe.

Sitta pia alisema Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma haikustahili kufuatwa katika kutaka ushauri kuhusu suala hilo kwa kuwa suala hilo lipo kwenye Kamati ya Nishati na Madini na kwamba kama kuna sababu mbadala, wasi ililazimika kuliwasilisha upya kwa kamati hiyo.

"Naitahadharisha serikali juu ya athari zinazoweza kujitokeza iwapo itaamua kuendelea na mchakato wa ununuzi wa mitambo ya Dowans kwa kupuuza ushauri uliotolewa na Kamati ya Nishati na Madini," alisema Spika Sitta.

Alisema: "Isisahaulike kwamba Dowans ni kampuni iliyopatikana kwa kurithishwa mradi na kampuni ya Richmond katika mazingira yenye utata ambao hadi leo ni kitendawili."

Spika Sitta alifafanua kuwa uhalali wa utaratibu wa Richmond kumkabidhi mradi Dowans ulitiliwa mashaka na kamati teule ya Bunge, na kuongeza kuwa Dowans na Richmond ni kama kitu kimoja.

"Dowans na Richmond ni mtu na binamu yake na si vigumu kukubali kuwa bado wao ni wabia hadi sasa: Pamoja na yote mkasa wa Richmond haufai kufufuliwaaa upya kupitia Dowans," alisisitiza Sitta.

Aliongeza kuwa kama kweli Tanesco na serikali inazo Dola 69 milioni za Kimarekani (sawa na Sh90 bilioni za Kitanzania) ambazo ni bei ya mtambo wa Dowans, ingezitumia fedha hizo kama sehemu ya malipo ya kununua mitambo mipya. Alisema Tanesco ingetafuta ushauri kutoka Mamlaka ya Ununuzi Serikalini (PPRA) ili taratibu za dharula zitumike kununua mitambo mipya kukabiliana na "dharula inayotabiriwa".

Sitta alihoji mantiki itakayotumiwa na Tanesco kutaka kununua mitambo ambayo inamilikiwa na kampuni ambayo imeishtaki kwenye Baraza la Usuluhishi ambalo makao yake makuu yako Paris, Ufaransa.

"Gharama za mitambo na gharama za kuikodi haviwezi kuepukwa kuwa ni sehemu ya shauri lililo Paris," anasema Sitta. "NI kwa mantiki ipi kesi baina yao iendelee na hapo hapo mdaiwa (Tanesco) anunue mitambo kutoka kwa mdai (Dowans.

"Tanzania ilikuwa ikilipa Dowans shilingi za Kitanzania milioni 152 kwa siku (Dola 120,000) sawa na Dola 42 milioni kwa mwaka).

"Pamoja na yote, mkasa wa Richmond haufai kufufuliwa upya kupitia Dowans. Tanesco/serikali waelekeze nguvu zao katika njia mbadala za kulipatia taifa umeme wa dharura, badala ya njia hii ya Dowans iliyojaa utata."

Kuhusu mvutano kati ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Mashirika ya Umma na ile ya Nishati na Madini, Spika Sitta amsema si sahihi kwa kamati yoyote ya Bunge isiyo ya sekta husika, kutoa maoni yake hadharani na kuishawishi jamii kwamba Bunge lina ushauri unaopingana kuhusu suala husika.

"Si sahihi kwa Kamati yoyote ya Bunge isiyo ya sekta kutoa maoni yake hadharani na kujenga taswira kwa umma kwamba, Bunge lina ushauri unaokinzana kuhusu suala lililo mbele yake. Kamati nyingine, haina budi kupitisha ushauri na maoni yake kwenye kamati ya kisekta," alisema Sitta.

Zitto Kabwe, ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, alikaririwa na vyombo vya habari akieleza msimamo wa kamati yake kuunga mkono Shirika la Umeme (Tanesco), kuinunua mitambo ya Dowans kwa maelezo kuwa hatua itasaidia kulinusuru taifa katika janga kubwa la kukosa umeme na kwamba sheria ya manunuzi si msahafu, hivyo inaweza kubadilishwa.

Lakini Kamati ya Nishati na Madini, ambayo mwenyekiti wake ni William Shelukindo, inapinga hatua hiyo ikieleza kuw ainakiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma, inayokataza serikali kununua vitu ambavyo tayari vimetumika.

Alisema ushauri kwa serikali kuhusu Tanesco kununua au kutonunua mitambo ya Dowans ulikwishatolewa kwa Wizara ya Nishati na Madini na Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini Desemba 14 mwaka uliopita.

"Huo ndiyo ushauri rasmi na sahihi wa Bunge ninaoutambua. Kwa msingi huo hoja ya kuzikutanisha Kamati hizi mbili (ya Nishati na Madini na ya Hesabu za Mashirika ya Umma) ili kurejea uamuzi au maoni yaliyokwishatolewa na Kamati inayohusika, haina msingi," alisema Sitta.

Alisema mkondo rasmi wa ushauri kwa serikali uliokusudiwa kwenye Ibara ya 63 (2) ya katiba ikisomwa na pamoja na kanuni za Bunge za mwaka 2007 ni kupiti Bunge zima au kamati zake za kisekta kila kamati na sekta yake.

Wakati Spika Sitta akibainisha msimamo wake na wa Bunge, mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba ameunga mkono ununuzi wa mitambo hiyo huku akisema kauli ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa jana inaweza kukwamisha mchakato wa ununuzi wa mitambo hiyo.

Lipumba alisema katika mfumo wa utawala bora wakati kamati za bunge zinazohusika na mambo hayo na bodi za mashirika zipo, rais hapaswi kujiingiza mapema katika mijadala.

“Katika mfumo wa utawala bora ambao una kamati za bunge zinazohusika na sekta ya umeme na manunuzi, kwa rais kujiingiza kunaweza kuwa ni kikwazo cha mchakato mzima wa ununuzi wa mitambo,” alisema Profesa Lipumba.

Alifafanua kuwa, sheria ya manunuzi ya Serikali ina upungufu kwa kuwa inalazimisha ununuzi wa mitambo mipya, jambo ambalo haliwezekani kwa nchi zinazoendelea kama Tanzania.

“Ununuzi wa mitambo ya kibiashara katika sekta ya biashara huwezi kulazimisha ununuzi wa mitambo mipya hususan katika nchi zinazoendelea kama ya kwetu. Jambo la msingi ni kuangalia uwezo wa mitambo katika kufanya kazi na si kwamba ni mipya au mikongwe,” alifafanua Lipumba na kuongeza:

“Sheria yetu ya manunuzi ni nzuri na inafaa sana kwa kununua vitu vya huduma za serikali, kama magari na vifaa vingine.”

Aliitaka Tanesco kuwa wazi kwa kuwa ni wao waliosema mitambo hiyo hawaitaki hivyo kuamuwa kuvunja mkataba na Dowans iweje leo wanageuka na kusema mitambo hiyo ni mizuri na kuitaka serikali iinunuwe.

“Tanesco walituambia kuwa mitambo hiyo hawaitaki na walivunja mkataba na Dowans, sasa inakuaje leo wanageuka na kusema kwamba mitambo hiyo ni mizuri na inunuliwe kwa ajili ya kuzalishia umeme? Tunahitaji uwazi zaidi kutoka Tanesco,” alihoji Profesa Lipumba.

Naye Stephen Menad ambaye ni mshauri wa masuala ya nishati na mazingira, alisema hakuna kitu kipya kwenye mitambo hiyo ya Dowans hivyo isinunuliwe na badala yake itafutwe mipya ili kuondoa mvutano baina ya wananchi na serikali.

Mussa Hassan, mkazi wa jijini Dar es Salaam ambaye ni mfanyabiashara, alisema ni aibu kwa serikali kula matapishi na kwamba viongozi wasisahau yaliyotokea wakati mitambo ya Richmond ilipokuja na mwisho wake kuwaweka pabaya viongozi waliokuwa serikalini.

Anthony Chambi, ambaye ni mfanyabiashara katikati ya jiji la Dar es Salaam, alisema hataki kusikia kuhusu mitambo hiyo kwa kuwa tayari ilishaiabisha serikali. Alisema anasikia kuna kesi Ufaransa kuhusu mitambo hiyo kitu kinachomshangaza kwa nini serikali inataka kununua mitambo ambayo ina kesi.
CHANZO: Mwananchi
BIG UP,MHESHIMIWA SPIKA.
BINAFSI HADI MUDA HUU SIELEWI HAO WANAOTAKA MITAMBO YA DOWANS INUNULIWE WANA AJENDA GANI!NACHANGANYWA ZAIDI NAPOSIKIA WATU KAMA ZITTO KABWA NA PROFESA LIPUMBA NAO WAKIPIGA DEBE MITAMBO YA DOWANS INUNULIWE.HUU NI UNAFIKI WA MCHANA KWEUPE.WHY?BECAUSE KUNUNUA MITAMBO HIYO NI KUHALALALISHA UJAMBAZI WA DOWANS NA KAKA YAKE RICHMOND.HIVI INAINGIA AKILINI KWELI PALE TAPELI ANAPOKUUZIA MALI FEKI KISHA UKAMKALIA KOONI MPAKA AKAKIRI KUWA KWELI ALICHOKUUZIA NI FEKI,HALAFU UKAISHIA KUONGEZA FEDHA KUNUNUA MALI HIYO FEKI!?
I WOULD ONLY SUPPORT MATUMIZI YA MITAMBO YA DOWANS LAITI INGEKUWA IMETAIFISHWA (NA SIJUI KWANINI HADI MUDA HUU HAIJATAIFISHWA...WE MISS YOU BABA WA TAIFA).ETI AKINA KABWE WANASEMA TUWEKE MBELE UTAIFA KWANZA!UTAIFA KWANZA KWA MANUFAA YA AKINA RICHMOND?HAWA WAMEINGIZWA MKENGE NA VITISHO VYA TANESCO KUWA ETI NCHI IKO HATARINI KUINGIA KIZANI!YALEYALE YA RICHMOND!
WIZI MTUPU!

Picha kwa hisani ya Mjengwa
MWAKA 2006,MANISPAA YA TEMEKE ILITANGAZA AZMA YAKE YA KULIBORESHA SOKO LA TEMEKE.LAKINI KATIKA HALI YA KUSTAAJABISHA,KUNA TAARIFA KWAMBA SASA SOKO HILO LIMEUZWA KWA MWEKEZAJI.KWA MWENENDO HUU,SI AJABU SIKU YA SIKU MTU AKAAMKA NA KUKUTA MTAA ANAOISHI UMEUZWA KWA MWEKEZAJI.

4 Mar 2009

A controversial Italian doctor known for his work allowing post-menopausal women to have children has claimed in an interview to have cloned three babies who are now living in eastern Europe.

"I helped give birth to three children with the human cloning technique," Severino Antinori, a prominent gynaecologist, told Oggi weekly in an interview to appear Wednesday."It involved two boys and a girl who are nine years old today. They were born healthy and they are in excellent health now."He did not provide proof of his claims, but said cells from the three fathers, who were sterile, allowed the cloning to be carried out.

The women's egg cells were impregnated in a laboratory through a method called "nuclear transfer," he said.Antinori, who became famous after allowing a 63-year-old woman to have a child in 1994, said "respect for the families' privacy does not allow me to go further."He added that the method used was "an improvement" over the technique used to clone Dolly the sheep in 1996.

Reminded by the journalist that such cloning is prohibited in heavily Catholic Italy, the doctor said he preferred to "speak of innovative therapies" or "genetic recoding" rather than cloning.Two weeks ago, Antinori sparked controversy by announcing that he would artificially impregnate a woman whose husband is in an irreversible coma following a brain tumour.It would be the first procedure of its kind in Italy if successful.
SOURCE: AFP

3 Mar 2009

RAIS Jakaya Kikwete amesema ana majina ya watu wa kitengo cha maktaba cha Bandari ya Dar es salaam wanaofanya ufisadi unaolikosesha taifa mamilioni ya fedha na kuahidi kuyakabidhi kwa wahusika ili washughulikiwe. Kikwete alisema hayo jana baada ya kufanya ziara ya kushitukiza kwenye Bandari ya Dar es salaam kukagua utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa Januari 15 mwaka huu kwa wakuu wa Mamlaka ya Bandari (TPA).

Alisema kitengo cha maktaba kimekuwa kikifanya mchezo mchafu bandarini hapo kwa kushirikiana na wasafirishaji na kwamba, vibarua vya watu wa kitengo hicho viko hatarini.

“Waambieni watu wa kitengo cha maktaba kuwa mchezo wao unajulikana na orodha ya majina yao inajulikana, lakini bado kuwaumbua tu,” alisema Kikwete baada ya kumaliza ziara yake.

“Ndugu zangu sitawataja hadharani wala kwenye magazeti, bali nitakachofanya nitawaletea orodha ya majina, muwafukuze kazi. Kama wameshindwa kazi tutaleta watu wengine ambao wako tayari kufanya kazi kwa uaminifu.”

Alisema watu hao wamekuwa wakiwasiliana na wasafirishaji na kufanya ujanja wakati wa kujaza fomu za makontena yanayoingia nchini kwa kuandika mizigo tofauti na ile iliyomo ndani ya makontena hayo, ili yasipitishwe katika mashine ya uchunguzi ...ENDELEA

CHANZO: Mwananchi

HIVI KAMA MAJINA YA MAFISADI YANAJULIKANA (NA KINACHOSUBIRIWA NI "KUWAUMBUA") KWANINI WASICHUKULIWE HATUA?WAZIRI MWENYE MAMLAKA NA BANDARI YUKO WAPI NA ANAFANYA NINI?MKURUGENZI NA BODI YA BANDARI WANAFANYA NINI?NA,HIVI HATUA MWAFAKA DHIDI YA MAFISADI NI KUWAUMBUA AU KUWAFIKISHA MBELE YA VYOMBO VYA SHERIA?

2 Mar 2009

UAMUZI WA SERIKALI KUHUSU KURA YA MAONI DHIDI YA WAUAJI WA ALBINO-ULIOTANGAZWA NA RAIS JK KWENYE HOTUBA YAKE YA MWISHO WA MWEZI FEBRUARI- UMEPOKELEWA KWA HISIA TOFAUTI NA BAADHI YA WANANCHI KAMA INAVYOELEZWA KATIKA HABARI NAMBARI 2 HAPO CHINI.KWA MTAZAMO WANGU,NADHANI WANANCHI WANA KILA SABABU YA KUHOJI UAMUZI HUO WA SERIKALI HASA KWA VILE IMEKUWA NI KAMA DESTURI KWA NCHI YETU KUTANGAZA HATUA KALI ZA KISIASA AMBAZO HUISHIA KUBAKI HISTORIA TU PASIPO MAFANIKIO.WENGI TUNAKUMBUKA KUHUSU DEADLINE WALIYOPEWA WALA RUSHWA MWANZONI MWA MWAKA 2006 NA ORODHA YA MAJINA YA WANAOJIHUSISHWA NA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA ILIYOKABIDHIWA KWA (ALIYEKUWA )WAZIRI BAKARI MWAPACHU....LAKINI HADI LEO HAKUNA HATUA YOYOTE ILIYOCHUKULIWA.KWANZA SOMA HABARI HUSIKA KISHA TUJADILI ZAIDI:

Kikwete:Wanaoua albinokuanza kutajwa kwa kura
mwezi huu

Claud Mshana

RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa, maandalizi ya zoezi la upigaji kura za maoni za kung'amua wauaji wa albino na vikongwe, limekamilika na litazinduliwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda. Akizungumza jana kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi wa Februari, Rais Kikwete alisema kuwa maandalizi ya kutekeleza zoezi hilo yamekamilika na kwamba, waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi huu.

Alisema kuwa alitoa maagizo ya kufanyika kwa zoezi hilo mwezi Desemba mwaka jana kwamba wananchi wapige kura kutaja majina ya waovu hao, akiwa na dhamira ya kuwapa nafasi wananchi kushiriki kikamilifu.

"Maandalizi ya kutekeleza uamuzi wangu huo yanaelekea kukamilika, mheshimiwa waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi Machi, 2009 na zoezi lenyewe la kupiga kura kufanyika kuanzia wiki ya pili ya Machi, 2009."

Alifafanua kuwa katika zoezi hilo pia wauaji wa vikongwe, majambazi wa kutumia silaha na wauzaji wa dawa za kulevya nao watahusishwa. Alitaja utaratibu wa kuendesha zoezi hilo utakuwa ni kufuata kanda na kwamba mikoa imegawanywa katika kanda saba ambazo ni Kanda ya Ziwa inayojumuisha mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza na Shinyanga.

Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yenye mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa na Ruvuma; Kanda ya Kati (Dodoma na Singida), Kanda ya Kusini (Lindi na Mtwara), Kanda ya Magharibi (Kigoma na Tabora), Kanda ya Kaskazini (Arusha, Kilimanjaro, Tanga na Manyara), na Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na Morogoro).
Wakuu wa mikoa yote nchini wameshapewa mwongozo wa jinsi ya kutekeleza zoezi hilo na kutaja miongoni mwa mambo watakayotakiwa kuzingatia ni pamoja na kuelimisha na kuhamasisha wananchi kushiriki katika zoezi hilo, upigaji kura ufanyike mwezi Machi kwa tarehe zitakazopangwa kwa kuzingatia kanda hizo.

"Kamati za ulinzi na usalama za mikoa zikiongozwa na wakuu wa mikoa zisimamie zoezi hili kwa makini. Kadhalika, kamati za ulinzi na usalama za wilaya zikiongozwa na wakuu wa wilaya zitaongoza utekelezaji katika wilaya zao na kushirikisha serikali za vijiji na mitaa," alisema Rais Kikwete.

"Napenda kuitumia fursa hii kuwasihi Watanzania; wake kwa waume; vijana na wazee tujitokeze kwa wingi kuwataja watu wanaojihusisha na maovu hayo katika jamii. Kura ni siri, hakuna atakayejua umemtaja nani. Hata msimamizi wa kituo hawezi kujua," alisema......
CHANZO: Mwananchi

NA IFUATAYO NI HABARI KUHUSU REACTION YA BAADHI YA WANANCHI JIJINI DAR ES AALAAM KUHUSIANA NA UAMUZI HUO WA KURA YA MAONI KUWATAMBUA WAUAJI WA MAALBINO.


Dar wataka serikali iweke wazi chanzo cha mauaji ya
albino


Na Boniface Meena

WANANCHI wa Mkoa wa Dar es Salaam wameiomba serikali itafute na kuewaleza chanzo cha mauaji ya albino, badala ya kuendelea kutoa kauli za kisiasa wakati hali inaendelea kuwa mbaya.

Pia wamesema hawadhani kama upigaji kura kuhusu mauaji hayo kama utasaidia kwa kuwa hata kesi za waliokamatwa kwa kuhusishwa na mauaji hayo hazijasikika. Mbali na hilo wameitaka serikali kuanzisha mahakama maalum kwaajili ya kusikiliza kesi za mauaji hayo ili waweze kujua maamuzi yanayotolewa na mahakama. Wakizungumza mbele ya Mkuu wa wilaya ya Temeke ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Kihato wananchi hao walidai serikali inaoneka kutokuwa makini na suala hilo kwa kuwa hakuna hata kesi moja ya mauaji ya albino iliyotolewa hukumu hadi hivi sasa.

Mbunge wa kuteuliwa, Al-Shaimar Kweiger alidai kuwa kuna mtandao mkubwa wa matajiri unaohusika na mauaji hayo ambao alisema hadhani kama unaweza kuishinda serikali katika kupambana nao. "Hili suala limeshazungumziwa sana, tumezunguka na Waziri Mkuu sehemu nyingi, lakini hawakomi nadhani kuna mtandao mkubwa wa watu wenye fedha uko nyuma ya jambo hili," alisema Kweiger.

Josephat Torner ambaye ni mwanaharkati wa kupinga mauaji ya albino alisema suala hilo linaonekana kuwa la kisiasa kwa kuwa hakuna hatua za haraka zilizochukuliwa kuwasaisdia wahanga wa mauaji hayo. "Tunataka kujua serikali imefikia wapi tangu suala hili lilipotangazwa kuwa ni la kitaifa," alihoji Torner. Torner ambaye ni albino alisema hawadhani kama upigaji kura utasaidia, kwani wanaona kama ni mchezo wa kisiasa hivyop wangependa kujua wako katika hali gani hivi sasa kuhusu mauaji hayo.

Christopher Andendekisye ambaye ni Mkurugenzi wa Shirikisho la Vyama vya Walemavu Tanzania (Shivyawata) alisema, kama serikali haitakuwa makini na mauaji hayo yanaweza kuendelea kwa muda mrefu kwa kuwa chanzo chake bado hakijajulikana. "Itabidi tuwe na wiki maalum au mahakama maalumu kwaajili ya kusikiliza kesi za mauaji haya na kama haiwezekani tuambiwe chanzo ni nini," alisema Andendekisye. Maria Chale ambaye ni albino alidai kuwa inaonekana serikali mpaka sasa haijui chanzo kitu ambacho kinatia wasiwasi kama zoezi hilo litafanikiwa.

Steven pascal ambaye ni katibu wa Albino muungano Investiment Trust(Amit), alisema ni bora jeshi (JWTZ) watumike kuwaska wanaohusika na mauaji hayo. "Ni bora Jeshi lihusishwe kwani hawa jamaa (wanajeshi) akipigwa mwenzao mmoja kijiji kizima kinazingira mpaka wapatikane wahusuka," alisema Pascal. Wananchi hao walisemas hayo jana wakitoa maoni yao mbele ya DC Kihato ambaye alikutana nao kuwaeleza juu ya uzinduzi wa upigaji kura za maoni dhidi ya mauaji ya albino utakaofanyika jijini Dar es Salaam Machi 5, mwaka huu.

Akijibu baadhi ya maoni yaliyotolewa na wananchi hao, Kihato ni kweli serikali haijatatua tatizo hilo kama wananchi wanavyotaka lakini inajitahidi kuhakikisha mauaji hayo yanatokomezwa, ndiyo maana wameitisha kura ya maoni.


CHANZO: Mwananchi

KATIKA HABARI YA KWANZA,KUNA MANENO NIMEYAONYESHA KWA RANGI NYEKUNDU KWA SABABU MAALUMU.PAMOJA NA NIA NZURI YA SERIKALI KUTAFUTA UFUMBUZI WA KUDUMU WA MAUAJI YA MAALBINO,WAZO LA KURA YA MAONI LINAWEZA LISIWE NA MAFANIKO YANAYOKUSUDIWA.KWANZA,KAMA MANENO YENYE RANGI NYEKUNDU YANAVYOONYESHA "...Alifafanua kuwa katika zoezi hilo pia wauaji wa vikongwe, majambazi wa kutumia silaha na wauzaji wa dawa za kulevya nao watahusishwa..." KUTANUA WIGO WA WALENGWA KUNALIFANYA ZOEZI HILO KUWA PANA ZAIDI ILHALI MAANDALIZI YAKIWA DUNI.ZAIDI,IWAPO KWELI DHAMIRA NI KUWASAKA WAUAJI WA MAALBINO,KUNA HAJA GANI KUINGIZA HABARI ZA WAUZA MADAYA YA KULEVYA,KWA MFANO,AMBAO HUKO NYUMA TULISHAAMBIWA KUWA ORODHA YAO ILIKABIDHIWA KWA WAZIRI MWAPACHU NAE AKADAI KUWA AMEIKABIDHI KWA RAIS?

JINGINE AMBALO LINAHITAJI TAFAKURI NI UTATA KATIKA KAULI ZA VIONGOZI WETU.RAIS ANASEMA ALITOA AGIZO MWEZI DESEMBA,LAKINI TUNAKUMBUKA KAULI ZA WAZIRI MKUU HAPO KATIKATI KWAMBA WAUAJI WA MAALBINO NAO WAUAWE (JAPO BAADAYE ALIOMBA MSAMAHA KWA MACHOZI HUKO BUNGENI)....INA MAANA AGIZO LA DESEMBA LILIPUUZWA NA KUBADILISHWA KUWA "JINO KWA JINO" KABLA HALIJAFUTWA KUFUATIA KELELE ZA WADAU KUHUSU HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA WA SHERIA?

NA KAMA AGIZO LILITOLEWA DISEMBA,KWANINI BASI ICHUKUE MIEZI MITATU MIZIMA KUTOA UAMUZI HUU AMBAO KWA HAKIKA UNAHITAJI MAANDALIZI MAZURI NA YA KUTOSHA (HUSUSAN UHAMASISHAJI)?JE WIKI MBILI ZINATOSHA ?RAIS ANASEMA "...maandalizi ya kutekeleza zoezi hilo yamekamilika na kwamba, waziri mkuu atafanya uzinduzi rasmi wa zoezi hilo mwishoni mwa wiki ya kwanza ya mwezi huu...zoezi lenyewe la kupiga kura kufanyika kuanzia wiki ya pili ya Machi, 2009."ARE WE ARE WE REALLY SERIOUS?KURA YA MAONI WIKI MOJA BAADA YA UZINDUZI!?JE MAANDALIZI YANAYODAIWA KUKAMILIKA HAYAKUPASWA KUJUMUISHA UHAMASISHAJI WA WANANCHI?PASIPO UMAKINI,ZOEZI HILI LITAISHIA KUTUNISHA POSHO ZA WAHUSIKA NA WAUAJI WA MAALBINO,WAUZA UNGA NA MAJAMBAZI WAKAENDELEA "KUPETA."

SWALI JINGINE LA MSINGI NI KUHUSU MATOKEO YA KURA HIYO YA MAONI.HIVI KWA MFANO BLOGU HII IKIPIGIWA KURA NYINGI KUWA NDIO SPONSOR WA WAUAJI WA MAALBINO (GOD FORBID),NINI KINAFUATA?MHUSIKA ATAKAMATWA NA KUHOJIWA KWA VILE KURA NYINGI ZIMESEMA HIVYO?MHUSIKA ATATAKIWA AJIELEZE KWANINI WANANCHI WENGI WAMEMPIGIA KURA "ZA CHUKI"?AU WAPELELEZI WATAINGIA UWANJANI KUANZA UCHUNGUZI?VIPI ILE TASK FORCE ILIYOUNDWA HUKO NYUMA?

KWA NCHI INAYOHESHIMU UTAWALA WA SHERIA INATARAJIWA KUWA MATOKEO YA KURA HIYO HAYATACHUKULIWA KUWA NDIO HUKUMU DHIDI YA WATAJWA.HIYO ITAMAANISHA KUFANYIA UCHUNGUZI MAJINA YA WALIOPATA KURA NYINGI.KISHA UCHUNGUZI UTAPOKAMILIKA NA USHAHIDI WA KUTOSHA KUPATIKANA NDIPO ZIANZE HATUA ZA KISHERIA KWA VILE,KWA MUJIBU WA SHERIA, NI MAHAKAMA PEKEE (NA SIO MATOKEO YA KURA YA MAONI) INAYOWEZA KUMTIA MTUHUMIWA HATIANI AU KUMWACHIA HURU.

MWISHO,NI MUHIMU PIA KUKUMBUKA NAMNA UTAMADUNI WA RUSHWA UNAVYOATHIRI MWENENDO WA MAISHA YA MTANZANIA KILA SIKU.HIVI KAMA BAADHI YA WAHESHIMIWA WANAWEZA KUNUNUA KURA ILI WATUWAKILISHE HUKO BUNGENI,KWA MFANO,ITASHINDIKANA VIPI KWA MATAJIRI WANAOFADHILI MAUAJI YA MAALBINO KUNUNUA KURA "ZA KUPENDWA" NA WAPIGA KURA?VIPI IWAPO MATOKEO YA KURA YATAONYESHA MAJINA YA BAADHI YA WAHUSIKA WA KAMPUNI YA KAGODA?HAKUTAKUWA NA KIGUGUGMIZI KAMA KILICHOPO KWENYE UFISADI WA KAMPUNI HIYO KWENYE FEDHA ZA EPA?

NA VIPI IWAPO WANYONGE WATAPIGIWA KURA ZA CHUKI?

MASWALI NI MENGI KULIKO MAJIBU.KWA HAKIKA DHAMIRA KUHUSU KURA YA MAONI NI NZURI LAKINI WASIWASI WANGU MKUBWA NI KATIKA UTEKELEZAJI WAKE.NA KAMA WALIVYOSEMA BAADHI YA WAKAZI WA DAR KATIKA STORI NAMBA 2,MAFANIKIO KATIKA HARAKATI ZA KUKOMESHA MAUAJI YA ALBINO YANAHITAJI JITIHADA ZA ZAIDI YA KAULI ZA KISIASA.

26 Feb 2009


MKUU wa wilaya ya Maswa, James Yamungu, amempongeza aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, Albert Mnali, akimwita kuwa ni shujaa kutokana na kitendo chake cha kuchapa viboko walimu wa shule tatu za msingi na kusababisha atimuliwe kazi na Rais Jakaya Kikwete.

Mnali, ambaye hakujutia kitendo chake cha kuchapa walimu akisema alikuwa tayari kwa uamuzi wowote toka juu, aliwachapa viboko walimu wa shule za Kansenene, Katerero na Kanazi kwa madai ya utoro kazini, kuchelewa na uzembe na kusababisha kushuka kwa kiwango cha elimu kwenye wilaya hiyo. Kitendo chake kililaaniwa na wadau mbalimbali, ikiwa ni pamoja na serikali na kufuatiwa na uamuzi wa Rais Kikwete kumvua ukuu wa wilaya.

Lakini jana, mkuu wa wilaya ya Maswa alionekana kuchukulia kitendo hicho kuwa sahihi na kumuita Mnali kuwa ni shujaa. Akizungumza wakati akifungua mkutano mkuu wa tatu wa chama cha kuweka na kukopa cha Nyalikungu uliofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya hiyo, kapteni huyo mstaafu wa jeshi alisema kuwa Mnali ni shujaa ambaye alikuwa akiwatetea Watanzania licha ya kitendo chake kusababisha atimuliwe. ..
ENDELEA


CHANZO: Mwananchi


YAYUMKINIKA KUAMINI KWAMBA KUNA TATIZO KATIKA UTEUZI WA BAADHI YA WATENDAJI WA SERIKALI HASA KATIKA NGAZI ZA MIKOA NA WILAYA.SIJUI NI KUJISAHAU,SIJUI NI KULEWA MADARAKA,AU SIJUI NDIO ILE "MIE NDIO RAIS WA WILAYA,KIJIJI,NK" INAYOWAPA BAADHI YA MA-RC,MA-DC,NA VIONGOZI WENGINEO KATIKA NGAZI MBALIMBALI KUJIONA WAKO JUU YA SHERIA,WAKO SAHIHI KATIKA KILA WAFANYACHO,NA PENGINE KUJIONA WAKO SAHIHI KULIKO HUYO ALIYEWATEUA (RAIS).HIVI HUYU DC ANAYEMWITA MWENZIE ALIEFUKUZWA NA RAIS KUWA NI SHUJAA HAFANYI DHIHAKA KWA RAIS?SI VIGUMU KUJUA WANAPATA WAPI JEURI HII....

25 Feb 2009

21 Feb 2009

ULE MCHEZO WA KUIGIZA KUHUSU "KUTOWEKA" KWA LIYUMBA BADO UNAENDELEA.LATEST EPISODE INAHUSU TAKUKURU KUTANGAZA DONGE NONO KWA ATAYEFANIKISHA KUKAMATWA KWA NDUGU LIYUMBA.

Na Boniface Meena

TAASISI ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini(Takukuru) imetangaza kutoa donge nono kwa mtu yeyote atakayefanikisha kukamatwa kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi (DPA) wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba ambaye hadi hivi sasa hajulikani halipo.

Wakati Takukuru ikifikia hatua hiyo, tayari kuna wananchi ambao wametoa taarifa kwenye baadhi ya vyombo vya habari kuwa wanaweza kutoa taarifa za alipo Liyumba. Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani alisema wameamua kutangaza doge nono ambalo hakulitaja ni kiasi gani cha fedha ili wananchi wasaidie kupatikana kwa Liyumba. Alisema Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru Dk Edward Hoseah ,anakaribisha watu ambao wanaweza kutoa taarifa au kusaidia alipo Liyumba ili aweze kukamatwa.

"Kuna wananchi tumesikia wako tayari kuisaidia Takukuru, tunawakaribisha na Dk Hoseah anawakaribisha ili waweze kutusaidia na donge nono litatolewa kwa atakayesaidia kukamatwa kwa Liyumba," alisema Kapwani.

Wakati Takukuru ikifikia maamuzi hayo Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imesema kama Takukuru itahitaji msaada wa Wizara hiyo kumtafuta Liyumba iko tayari kutoa msaada huo.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili Waziri wa Wizara hiyo, Lawrance Masha alisema wakipewa maombi ya kumtafuta Liyumba, watasaidia kumtafuta kwa kuwa wote ni Serikali. "Juzi nilitoa tamko kuwa hatujaletewa maombi ya kumtafuta, lakini Takukuru wakituletea tutafanya hivyo, kwa kuwa sisi ni Serikali," alisema Masha.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilifuta dhamana ya Liyumba Februari 19 na kutoa amri ya kuwakamata wadhamini wake ambao walikamatwa siku hiyohiyo na baadaye kuachiwa. Wadhamini hao ni wafanyakazi wa BoT Benjamin Nduguru (mhasibu wa benki hiyo) na Agaterus Oto (Afisa Usalama wa ndani wa benki hiyo).

Hata hivyo, licha ya mahakama kufuta dhamana kuwakamata wadhamini hao, ilitoa amri ya kumtafuta na kumkamatwa Liyumba.Liyumba pamoja na aliyekuwa Meneja Miradi wa BoT, Deogratius Kweka wameshitakiwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia vibaya madaraka yao katika mradi wa ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo na kuisababishia hasara serikali jumla ya Sh221 bilioni.

Liyumba alipewa dhamana na Hakimu Mkaazi wa Kisutu, Hadija Msongo kwa kutumia hati ya nyumba yake iliyoko Mbezi Juu, jijini Dar es Salaam yenye thamani ya Sh800 milioni, ambayo hata hivyo ililalamikiwa na upande wa mashitaka kwamba imetolewa katika mazingira tata kwa kuwa haijafikisha kiwango cha Sh50 bilioni walizotakiwa kutoa

Juzi Wakili wa serikali, Prosper Mwangumila aliileza mahakama kwamba, Liyumba bado hajapatikana. Hakimu alisema amri ya kumkamata Liyumba bado inaendelea na ya kuwakamata wadhamini imesitishwa hadi kesi itakapotajwa Februari 24, mwaka huu.

Katika hatua nyingine Mawakili wanaomtetea mtuhumiwa huyo waliulalamikia upande wa mashitaka kwa kitendo chake cha kuwanyanyasa ndugu wa mtuhumiwa huyo ambapo walidai kuwa uliwanyang’anya baadhi ya mali zao.

Mmoja wa mawakili hao wa utetezi, Majura Magafu aliiomba mahakama kutoa amri ya kuutaka upande wa mashitaka kuacha kuinyanyasa familia ya Liyumba na kwamba warudishe gari ya mmoja wa wadhamini ambayo waliikamata. Akijibu hoja hiyo, Hakimu Msongo aliutaka upande wa utetezi kama una maombi yoyote kuyapeleka kwa utaratibu wa mahakama kwa kuwa juzi haikuwa tarehe ya kesi.

Wakati akitoa dhamana hiyo Februari 17, mwaka huu, Hakimu Msongo alisema mshitakiwa huyo, atakuwa nje kwa dhamana ya Sh882 milioni wakati mahakama inajiridhisha na hati nyingine zilizopingwa na upande wa mashitaka. Alisema mshitakiwa atatakiwa kutimiza masharti ya dhamana ya kiasi kilichobaki cha Sh54,417,344,800.23 endapo mahakama itabaini kuwa hati hizo zina kasoro.

Hata hivyo baada ya kutolewa maamuzi hayo Wakili wa serikali Justus Mulokozi alisema hawajaridhika na maamuzi yaliyotolewa na kwamba watakaa kuyajadili na kuyatolea maamuzi. Upande wa mashitaka ulipinga kupokelewa kwa hati 10 kati ya 11 zilizowasilishwa mahakamani hapo na upande wa utetezi kwa madai kuwa zina kasoro, zikiwemo za kuwa na mali zisizokuwa za kudumu kama mbuzi, ng’ombe na kuku.

Siku mbili baada ya mtuhumiwa huyo kuachiwa huru na mahakama kutokana na kutimiza masharti, mahakama ilitoa amri ya kukamatwa tena jambo lilosababisha wadhamani wake kushikiliwa kwa muda na kisha kuachiwa.

Liyumba na Kweka walipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza , Januari 27, mwaka huu kwa tuhuma za kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia hasara serikali kiasi cha Sh 221 bilioni. Kweka bado hajapata dhamana.



TATIZO KUBWA LA VYOMBO VYETU VYA HABARI NI KURIPOTI HABARI AU MATUKIO BADALA YA KWENDA NDANI ZAIDI NA KUCHUNGUZA YALIYOJIFICHA KATI YA MISTARI.KWA MFANO,KWANINI HATUJIULIZI SABABU WA WADHAMINI WA LIYUMBA KUKAMATWA KISHA KUACHIWA?JE WADHAMINI HAO NAO "WAKITOWEKA" SI ITAMAANISHA "KIFO CHA ASILI" CHA KESI HIYO?

HIVI HATUWEZI KUJIULIZA SABABU ZA HAKIMU KUTOA DHAMANA KWA MSHTAKIWA JAPO DHAMANA HIYO ILIKUWA NA MAPUNGUFU?NAFAHAMU NI HAKI KWA MSHTAKIWA KUPATIWA DHAMANA LAKINI SHARTI ATIMIZE MASHARTI YA DHAMANA HIYO.

WIZI MTUPU!

20 Feb 2009




HAYA NDIO MAJIBU YA CCM.CHINI YA MAJIBU HAYO NI HABARI YENYE MATAMSHI YA DR KITINE.


CCM yamjibu Dk. Kitine

na Edward Kinabo

SIKU moja baada yaMkurugenzi mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa nchini, Dk. Hassy Kitine, kudai nchi inaendeshwa kienyeji na kukilalamikia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuendelea kuwakumbatia wanachama wake wanaokabiliwa na kesi za ufisadi, chama hicho
kimesema hakiwezi kuwavua nyadhifa hizo, kwa sababu kesi zao bado ni tuhuma tu.

Sambamba na hilo, CCM imesema kauli ya Dk. Kitine kwamba nchi inaendeshwa kienyeji ni maoni yake binafsi, kwani hayana ukweli. Msimamo huo wa CCM ulitolewa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati, alipozungumza na Tanzania Daima, akijibu shutuma nzito zilizotolewa juzi na Dk. Kitine dhidi ya serikali.

“Sisi tunasema, yeye kama raia ana haki ya kutoa mawazo yake, na hiyo ndiyo demokrasia. Lakini si lazima kila anayetoa mawazo yake yawe sahihi. Mtu anaweza kujiuzulu nafasi yake kupisha uchunguzi ufanyike, hiyo haimaanishi kwamba hilo jambo amelifanya kweli.

“Uchunguzi unapofanyika kuna mambo mawili yanaweza kutokea, la kwanza huyo mtu anaweza kubainika alifanya hicho kitu na la pili anaweza kuonekana hana hatia.

“Hatuwezi kuwavua watu uanachama au nyadhifa zao ndani ya chama kwa sababu hiyo tu. Yeye aliyesema hivyo atutajie ni kiongozi gani wa serikali ambaye pia ni kiongozi wa chama, ameshathibitika kuwa hana maadili halafu kama chama tumeendelea kumwacha. Atuambie…..hakuna,” alisema Chiligati.

Alipoulizwa kwanini CCM isiwafukuze uanachama na kuwavua nyadhifa zao za kichama na ubunge, baadhi ya viongozi wake, ambao tayari serikali ya chama hicho ilisharidhika kwamba walikiuka maadili ya uongozi kwa kutumia vibaya madaraka yao, hata ikaamua kuwafungulia kesi, alisema: “Hatuwezi kuwachukulia hatua kwa sababu kesi zao bado ni tuhuma tu. Wakithibitika kama kweli walifanya hivyo, hatutawaacha,” alisema Chiligati.

Chiligati alipinga madai ya nchi kuongozwa kienyeji na kusisitiza kuwa kauli ya Dk. Kitine, haina ukweli wowote.

Alisema nchi inaongozwa vizuri kwa kufuata utawala wa sheria na mihimili yote ya dola, ikiwemo utawala, Bunge na Mahakama, inafanya kazi zake vizuri. Alibainisha kuwa kielelezo kuwa nchi haiongozwi kienyeji, ni amani na utulivu vilivyopo nchini, kwani kama nchi ingekuwa inaongozwa kienyeji kusingekalika.

“Kwa mfano, hilo alilosema nchi inaongozwa kienyeji, maana yake nini? Nchi kuongozwa kienyeji maana yake hakuna mfumo wa utawala kabisa, hakuna utawala wa sheria. Mahakama hazipo wala Bunge halipo…serikali haipo.

“Kungekuwa na hali hiyo, ingekuwa sawa na kusema nchi inaongozwa kienyeji. Lakini sisi hatujafikia hatua hiyo. Bunge lipo, Mahakama ipo, Serikali ipo. Utawala wa sheria. Nchi haiongozwi kienyeji, ndiyo maana kuna amani na
utulivu,” alisema Chiligati.

Mbali ya CCM kutoa kauli hiyo, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), aliunga mkono kauli ya Dk. Kitine.

“Mzee Kitine ameongea jambo ambalo ninaliongea kila siku kwamba, kuna tatizo kubwa serikalini. Tuhuma za ufisadi zimeshamiri sana, watendaji hawachukui maamuzi, wanasiasa wenye nyadhifa serikalini wamejaza nafasi na hawako tayari kuwajibika. Tunahitaji muafaka wa kitaifa kwenye mambo mengi,” alisema Zitto. Alisema ili mambo yaende vizuri, Tanzania inahitaji kelele za wazee wastaafu kama Dk. Kitine, wasimamie kunena na kushauri na hata kukemea na wananchi wawapigie kura wabunge wengi wa upinzani ili Bunge liwe na meno.

Juzi, Dk. Kitine alisema taifa linakabiliwa na tatizo la uongozi, ambalo halijawahi kutokea katika historia ya nchi. Kada huyo wa siku nyingi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), aliyewahi kuwa mbunge wa Makete, mkoani Iringa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, chini ya uongozi wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, alisema nchi imekuwa ikiendeshwa kienyeji, kwa sababu ya kuporomoka kwa maadili ya uongozi.

“Hali tuliyofikia si nzuri, tena niseme ni mbaya sana. Kuna kuporomoka kwa kiasi kikubwa kwa maadili ya uongozi. Na hii nawaambia, nchi haijawahi kuwa katika hali mbaya huko nyuma kama ilivyo sasa. Kwa hali tuliyofikia ni ngumu kurekebisha maadili ya uongozi."

“Tatizo kubwa ni viongozi kukosa integrity (uadilifu). Kwanza ni integrity ya viongozi wenyewe, pili ni commitment (wito), tatu ni nationalism (utaifa). Haya ndiyo yalikuwepo wakati wa Mwalimu,” alisema Dk. Kitine. Alisema baadhi viongozi wa serikali wamepoteza sifa kuu tatu za uongozi ambazo ni kuwa na uadilifu, wito na kuweka mbele
utaifa, sifa ambazo alisema ndizo zilikuwa nguzo ya uongozi wakati wa Serikali
ya Awamu ya Kwanza, chini ya Baba wa Taifa, hayati, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Alisema uteuzi mbaya wa viongozi hususan uteuzi wa mawaziri, umechangia
kupatikana kwa viongozi wasio waadilifu, wengi wao wakijihusisha na vitendo vya rushwa

CHANZO: Tanzania Daima



IFUATAYO NI HABARI ILIYOBEBA MATAMSHI YA DR KITINE.

MKURUGENZI Mkuu mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Dk. Hassy Kitine, amesema taifa linakabiliwa na tatizo kubwa la uongozi, ambalo halijawahi kutokea katika historia ya nchi.

Kitine ambaye aliiongoza idara hiyo nyeti kwa karibu miaka 30 zama za Serikali ya Awamu ya Kwanza na ya Pili, alisema ukosefu huo wa uongozi umesababisha nchi iongozwe kienyeji.

Kachero huyo namba moja kwa miaka mingi, ambaye alilazimika kujiuzulu wadhifa wa uwaziri wa nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) wakati wa utawala wa Benjamin Mkapa, mwishoni mwa miaka ya 1990 kutokana na kuhusishwa na kashfa ya mkewe kufuja fedha za umma kiasi cha shilingi milioni 40, alirejea kutoa kilio chake cha miaka mingi cha kuporomoka kwa maadili ya uongozi nchini.

Kitine ambaye aliwahi pia kuwa Mbunge wa Makete kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alitoa matamshi hayo mazito katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam jana, alipozungumza na waandishi wa vyombo kadhaa vya habari.

“Hali tuliyofikia si nzuri, tena niseme ni mbaya sana. Kuna kuporomoka kwa kiasi kikubwa kwa maadili ya uongozi.Na hii nawaambia, nchi haijawahi kuwa katika hali mbaya huko nyuma kama ilivyo sasa. Kwa hali tuliyofikia, ni vigumu kurekebisha maadili ya uongozi.

“Tatizo kubwa ni viongozi kukosa integrity (uadilifu). Kwanza ni integrity ya viongozi wenyewe, pili ni commitment (wito), tatu ni nationalism (utaifa). Haya ndiyo yalikuwepo wakati wa Mwalimu,” alisema Dk.Kitine.

Akizungumza kwa kujiamini kama ilivyo kawaida yake, Kitine alisema viongozi wengi wa serikali wamepoteza sifa kuu tatu za uongozi ambazo ni kuwa na uadilifu, wito na kuweka mbele utaifa, sifa ambazo alisema ndizo zilikuwa nguzo ya uongozi wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, chini ya Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

“That was possible (hilo liliwezekana) chini ya Mwalimu. Kama alikuwa akifanya kosa, basi kosa hilo lilikuwa likitokea tu wakati akifanya jambo kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania. "

“Philosophy (falsafa) ya Mwalimu, ilikuwa kwanza Mungu, pili Tanzania, halafu yeye binafsi. Kila kiongozi anayetofautiana na Mwalimu tu hulifikisha taifa hili kubaya, if you differ with him, utaishia kubaya,” alisema Dk. Kitine akionyesha hali ya masikitiko.

Alisema uteuzi mbaya wa viongozi, hususan ule wa mawaziri, umechangia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa viongozi wasio
waadilifu, wengi wao wakijihusisha na vitendo vya rushwa. “Haiwezekani viongozi wakateuliwa kwa misingi ya mitandao …sijui, kwa msingi wa politics of division (siasa za makundi) ndani ya chama. Haiwezekani nchi ikaendeshwa kienyeji. Integrity should be number one (uadilifu unapaswa kuwa kitu cha kwanza kuzingatiwa). "

“Mtu anajiuzulu, anafukuzwa uwaziri kwa sababu ya kashfa, kwa sababu ya kukosa maadili, halafu anabakia kuwa mbunge na mjumbe wa kamati kuu ya chama, nini hii? Hii haifai. Waziri akikosa uadilifu anatakiwa aondolewe mara moja nyadhifa nyingine zote alizobakiwa nazo. Nadhani hii itasaidia,” alisema Dk. Kitine pasipo kutaja jina la kiongozi yeyote.

Kitine ambaye wakati wote wa mazungumzo yake alisema alikuwa anataka kujadili masuala muhimu na si watu, alieleza namna asivyo na imani na hatua zinazochukuliwa na serikali katika kukabiliana na tatizo la rushwa kubwa. Kwa mujibu wa kachero, mwanasiasa na mwanazuoni huyo, hatua hizo ambazo zinahusisha baadhi ya watu wenye majina makubwa kufikishwa mahakamani, zimechukuliwa kwa ajili tu ya maandalizi ya uchaguzi ujao.

“Nilikuwa kiongozi wa kwanza kuzungumzia rushwa kubwa miaka 10 iliyopita. Nilisema ndiyo inayovuruga uchumi kuliko hata rushwa ya
nesi, hakimu, polisi,.… hakuna hata mkubwa mmoja aliyekamatwa. Ilinigharimu sana, na mimi nilipata adhabu ya kuzuiliwa kikao kwa miezi miwili, kama huyu nani huyu, Zitto (Kabwe). Wakati huo ilikuwa ndani ya CCM".

“Mimi nadhani hatua hizi zinazochukuliwa hazilengi kukomesha tatizo la rushwa, ni siasa tu za uchaguzi,” alisema Dk. Kitine.

Alipoulizwa nini kifanyike ili kukabiliana na tatizo hilo la uongozi mbaya, pamoja na mambo mengine, alielekeza changamoto zake kwa Idara ya Usalama wa Taifa.

“Usalama wa Taifa should be completely clean (unapaswa kuwa safi kabisa). Idara hii inatakiwa kuwa, juu ya mambo ya rushwa, iwe safi kabisa. Usalama wa Taifa ndiyo unayoteua viongozi, ndiyo inayoshirikiana na rais kwa kumshauri katika kuteua mawaziri. Sasa kama Usalama wa Taifa ukiwa mchafu ndio tunapata viongozi wala
rushwa. Nafikiri vigezo vinavyotumika kuteua viongozi pia vina matatizo,” alisema Dk. Kitine.

Kada huyo wa CCM ambaye kitaaluma ni mchumi na mwanasheria, akizungumzia hali ya uchumi nchini, alisema kwa kiasi kikubwa uchumi umeshikiliwa na wageni kuliko wazawa, na kuelezea kusikitishwa kwake juu ya kuwepo kwa pengo kubwa kati ya matajiri na maskini.

Akitoa mfano alisema, miongoni mwa mambo yanayoonyesha kuparaganyika kwa mambo ni kukithiri kwa idadi ya ombaomba mitaani. “Mwalimu asingeruhusu watu hawa waombeombe barabarani. Kazi za Watanzania ni udereva teksi, daladala, mabasi, kazi ya uboi ndani ya nyumba na kazi ya kufagia barabarani. Hizi ndizo kazi za Watanzania na hawa ndio wenye mali."

“Uchumi huu wa Watanzania si wa kwao. Watanzania ambao ni matajiri hawazidi hata watano. Hakuna sera bora za kusaidia kutumia
maliasili zetu ili zitupe fedha ya kujenga shule, madaraja, hospitali…..”
alisema Dk. Kitine. Akizungumzia utendaji wa kazi wa Bunge katika kusimamia utendaji wa serikali, Kitine alisema kazi inayofanywa na taasisi hiyo hivi sasa ni kubwa kuliko ilivyopata kuwa wakati wowote huko nyuma.

Hata hivyo katika kuusifia utendaji wa kazi wa Bunge, aliupongeza mchango mkubwa na muhimu wa wabunge wa upinzani katika kuiimarisha taasisi hiyo muhimu. “Ni Bunge zuri kuliko lilivyowahi kuwa huko nyuma. Linaonyesha kila dalili za uhuru. Upinzani unafanya kazi nzuri. Bunge liko wazi zaidi na wabunge wanatoa michango mingi yakinifu, yenye manufaa kwa taifa. Likiendelea hivi tutafika mahali pazuri,” alisema
.

CHANZO :Tanzania Daima



WELL SAID!

Picha kwa hisani ya KENNEDY.
HUU NI USANII WA MCHANA MWEUPE.UNFORTUNATELY,VYOMBO VYETU VYA HABARI VIMEKUWA MAKINI ZAIDI KATIKA KURIPOTI MATUKIO BADALA YA KUYAFANYIA UCHUNGUZI HABARI.WELL,HII NDIO BONGO BWANA.


PENGINE UTASEMA NI MAPEMA MNO KUWA PESSIMIST,LAKINI YAYUMKINIKA KUAMINI KWAMBA NI VIGUMU SANA KWA MTUHUMIWA MWENYE UWEZO WA KIFEDHA KUHUKUMIWA KWA KOSA LOLOTE ALILOTENDA,HATA KAMA KUNA USHAHIDI WA WAZIWAZI.


HIVI INAINGIA AKILINI KWELI KWAMBA TUHUMA DHIDI YA LIYUMBA NI PAMOJA NA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA KATI YA MWAKA 2001 HADI 2006?KAMA HUJAELEWA MANTIKI YA SWALI LANGU NI KWAMBA HUU NI MWAKA 2009.SO,INA MAANA MATUMIZI HAYO MABAYA HAYAKUWEZA KUGUNDULIKA KWA KIPINDI CHOTE HICHO CHA MIAKA MITANO?HIVI BENKI KUU HAIFANYIWI UKAGUZI WA MAHESABU KILA MWAKA?IF SO,KWANINI WAKAGUZI HAO WASIULIZWE KUHUSU TAARIFA ZA MWAKA 2001-2006?OK,TUACHANE NA WAKAGUZI.VIPI KUHUSU INTERNAL SECURITY NDANI YA BENKI KUU?HAWA WATU WANALIPWA KWA AJILI YA KAZI GANI IWAPO FEDHA ZILIKUWA ZIKITUMIKA KWA MIAKA MITANO MFULULIZO PASIPO WAO KUSHTUKA.


PENGINE JIBU LA SWALI HILO LA MWISHO LINAWEZA KUPATIKANA KWENYE TAARIFA KWAMBA MMOJA YA WADHAMINI WA LIYUMBA NI AFISA USALAMA WA BENKI HIYO.DOES THIS MAKE ANY SENSE?AFISA USALAMA WA BENKI ANAMDHAMINI MTUHUMIWA ANAYAYESHTAKIWA KWA UBADHIRIFU WA FEDHA KATIKA BENKI HIYOHIYO!?


HAYA TWENDE KWENYE SUALA ZIMA LA DHAMANA.KAMA LIYUMBA ALIKUWA HAJATIMIZA MASHARTI YOTE YA DHAMANA KWANINI BASI HAKIMU ALITOA DHAMANA HIYO?INAELEZWA KWAMBA DHAMANA ILIYOTOLEWA ILIKUWA NA MAPUNGUFU YA MAMILIONI KADHAA.HALAFU ETI KWA USANII,WAENDESHA MASHTAKA WALINUKULIWA WAKIDAI HAWAJARIDHISHWA NA DHAMANA HIYO.


HUU NI MCHEZO WA KUIGIZA.NA NDIO MAANA UKISOMA MAGAZETI KADHAA UTAGUNDUA STORI ZINALINGANA.HII BUZZ IS MOST LIKELY ENGINEERED BY SOMEONE WHO'S BEHIND ALL THIS FRAUD.WANATANGAZA KWA SAUTI KUWA LIYUMBA KATOWEKA (JAPO TUNAAMBIWA ETI PASSPORT YAKE ILIKUWA IMEZUILIWA) ILI BAADAE WATANZANIA WASAHAU KAMA WALIVYOSAHAU KUHUSU BALLALI,MAJAMBAZI WA RICHMOND,MAFISADI WA KAGODA,NK.

WANAFANYA HIVI KWA VILE WANAFAHAMU BAYANA KUWA WATANZANIA NI WAPOLE,HAWAKAWII KUSAMEHE NA KUSAHAU MABAYA.

HII NDIO BONGO YETU!AU KAMA WANAVYOSEMA SIKU HIZI, WIZI MTUPU

19 Feb 2009


CLICK HERE to read more about this wonder kid.

16 Feb 2009


A drug which appears to erase painful memories has been developed by scientists. The astonishing treatment could help sufferers of post-traumatic stress disorder and those whose lives are plagued by hurtful recurrent memories.


But British experts said the breakthrough raises disturbing ethical questions about what makes us human. They also warned it could have damaging psychological consequences, preventing those who take it from learning from their mistakes...MORE
SOURCE: Daily Mail

14 Feb 2009

Some casting sheets actually said ‘No Blacks,”’ the 19-year-old model Shawn Sutton was saying on Friday, backstage at the Duckie Brown show in the Bryant Park tent. He was referring to the model castings at the recent men’s wear shows in Milan. “It was pretty brutal and, yeah, it was racist,” he added. “But things opened up a lot by Paris, so I paid it no mind.”Mr. Sutton was one of 24 models in a show whose casting, for once, reflected some ethnic diversity. It is early days in New York’s Fashion Week, but already there are signs that the recent industry habits of exclusion may be undergoing a shift. Call it the Obama effect, if you will...MORE


SOURCE: NYTimes


WAKATI serikali ikiendelea na mchakato wa zabuni ya vitambulisho vya uraia ya Sh222 bilioni, imebainika kwamba kiasi hicho cha fedha ni kikubwa mno na kama wangemtumia Mpigachapa wa Serikali kazi hiyo ingetumia Sh95 bilioni tu. Habari zilizopatikana zinaeleza kwamba, ingawa mpigachapa wa serikali alishaomba zabuni hiyo kufanya kazi hiyo, lakini hajachaguliwa bila ya sababu maalumu.

Siri hiyo ilifichuka juzi wakati Kamati ya Bunge ya Mabadiliko ya Sheria Mbalimbali (Miscellaneous Amendments) ilipotembelea ofisi ya Mpigachapa Mkuu kujionea utendaji kazi ikiongozwa na Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Benson Mpesya ambaye ni Mbunge wa Mbeya mjini kupitia CCM na kugundua kuwa ofisi hiyo ya serikali ina uwezo wa kufanya hiyo kazi kwa bei nafuu zaidi.

Mbunge wa Moshi mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Philimon Ndesamburo ambaye ni mjumbe wa kamati hiyo aliiambia Mwananchi Jumapili jana kuwa serikali, itoe sababu za kuikatalia Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wake, kuandaa vitambulisho vya uraia kwa gharama ya Sh95 bilioni badala yake kung'ang'ania zabuni itakayogharimu Sh222 bilioni.

Akifafanua hoja yake mbunge huyo, alisema akiwa kwenye ziara hiyo, alimuuliza Mpigachapa Mkuu wa Serikali, Cassian Chibogoyo, kama Ofisi yake inao uwezo wa kuchapa vitambulisho vya taifa na aliwajibu wajumbe wa Kamati ya Bunge kwamba, ofisi yake inaweza kutengeneza vitambulisho hivyo kama itapatiwa fedha.

Mbunge huyo alimkariri Chibogoyo akisema kwamba, ofisi yake ilishaomba kazi ya kuchapa vitambulisho hivyo kwa gharama ya Sh95 bilioni miaka miwili iliyopita, lakini hadi sasa hajui kinachoendelea. Ndesamburo alisema kauli ya Mpiga Chapa iliwashitua wajumbe wote wa kamati hiyo iliyoambatana na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu.

"Mimi ninachotaka kujua kutoka serikalini ni kwa nini isiimarishe zaidi ofisi yake ambayo mpaka sasa inachapa siri nyingi za serikali kwa kuipatia kazi hiyo hata kama ni Sh150 bilioni kwa sasa, ili kuondokana na utata unaoendelea?" alihoji.

Mbunge huyo alisema mpigachapa mkuu alieleza kwamba, kabla ya kuomba kazi hiyo alifanya utafiti katika nchi kadhaa ikiwamo Ujerumani na kuona wazi kwamba, kazi hiyo ingefanyika kwa kiwango cha kimataifa kwa gharama ya Sh95 bilioni.

"Serikali ingepunguza gharama na kuondoa malumbano yanayoendelea kama ingetoa kazi kwa Ofisi yake (mpiga chapa), ambayo inaongozwa na mtu ambaye alikuwa Rais wa Shirikisho la Wapigachapa wakuu duniani," alisema na kuongeza:

"Mpigachapa Mkuu anasema sehemu ya fedha hizo zitatumika kununua mtambo wa kisasa ambao baada ya kuchapa vitambulisho utabaki hapa hapa nchini."

Chibogoyo alipopigiwa simu jana ili kufafanua taarifa hizo, alikataa katakata kuzungumzia suala hilo kwa maelezo kwamba, mambo ya wabunge yanatolewa na wabunge wenyewe. Naye Mpesya licha ya kukiri kwamba kamati yake ilitembelea ofisi hiyo ili kupata maelezo mbalimbali hususan jinsi ya kuchapa sheria, hakutaka kufafanua zaidi juu ya yaliyojitokeza.

Akizungumzia hali hiyo jana, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha, alisema kwa sasa bado mchakato huo unaendelea, hivyo hawezi kuzungumza lolote juu ya suala hilo kwa kuwa kila mmoja ameomba tenda na serikali bado inaendelea kuzichambua.

“Kwa kuwa mchakato wenyewe bado haujaanza, siwezi kusema lolote juu ya hilo, hivyo basi nakuomba usubiri mpaka zoezi hilo litakapokamilika ndipo ujue ni nani ameshinda tenda hiyo na kuniuliza swali lako,” alisema Masha. Aliongeza kuwa kuchelewa kwa mchakato wa kutengeneza vitambulisho vya uraia, kunatokana na kumtafuta mzabuni mwenye sifa anayeweza kusimamia kazi hiyo kwa umakini.

Kazi ya kuchapisha vitambulisho vya uraia imekuwa chanzo cha mvutano mkubwa miongoni mwa wanasiasa na baadhi ya watendaji wa serikali. Katika mkutano wa bunge uliomalizika wiki hii mjini Dodoma, Mbunge wa Karatu, Dk Wilibrod Slaa alitaka kuwasilisha hoja binafsi akidai kuwa waziri Masha ameingilia kati mchakato wa kuchapisha vitambulisho hivyo kinyume cha taratibu. Hata hivyo, hoja hiyo ilishindwa kujadiliwa na wabunge baada ya Spika kuizuia kwa maelezo kwamba, kufanya hivyo ni kuingilia kati mchakato mzima wa zabuni hiyo unaoendelea.

Suala la kuchapisha vitambulisho vya uraia nchini, limekuwa likiingia utata mara kwa mara kutokana na baadhi ya wakubwa kudaiwa kutaka kujinufaisha na zabuni hiyo. Mchakato wake wa zabuni ya kuchapa vitambulisho hivyo ulianza mwaka 2004 na kwamba, umekuwa ukisuasua kutokana na kuzingirwa na mizengwe.

Mradi huo ulioanza kuzungumzwa miaka ya katikati ya 1970 na ambao utagharimu kiasi cha Sh222 bilioni, unaelezwa kwamba umo katika hatua za mwisho za kutaka kutekelezwa japo taarifa zinaonyesha kwamba, ni mpango mwingine mkubwa wa ulaji fedha za umma.

CHANZO: Mwananchi

NENO MCHAKATO LIMETOKEA KUWA OFFICIAL SUBSTITUTE YA "UJANJAUJANJA WA KIFISADI".ETI MCHAKATO UNAENDELEA KUMPATA MZABUNI MWENYE SIFA ANAYEWEZA KUSIMAMIA KAZI KWA UMAKINI!HIVI KAMA OFISI YA MPIGACHAPA MKUU WA SERIKALI HAINA SIFA HIZO,KWANINI BASI INAENDELEA KUWEPO?TUACHE HILO,HIVI KATIKA UCHAPISHAJI WA NYARAKA NYETI KAMA VITAMBULISHO VYA URAIA,KUNA MZABUNI MWENYE SIFA ZA MASLAHI YA TAIFA KIUSALAMA ZAIDI YA GOVERNMENT PRINTER?WELL,KWENYE KUSAKA UPENYO WA KUFISADI,KILA EXCUSE ITATOLEWA.

PENGINE WAKATI UMEFIKA WA KUACHANA KABISA NA WAZO HILI LA VITAMBULISHO VYA TAIFA MAANA DANADANA ZINAZOCHOCHEWA NA UFISADI ZIMEKUWA ZIKIENDELEA MIAKA NENDA MIAKA RUDI.

HEBU KWANZA MSIKILIZE KIONGOZI HUYU WA UMMA HUKO ZENJI ANAVYOJITETEA DHIDI YA WITO WA KUMTAKA AJIUZULU KISHA TUJADILI KIDOGO:



WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Haroun Ali
Suleiman, amesema haoni sababu ya kujiuzulu wadhifa huo kwa madai ya wanafunzi
wengi Zanzibar kufanya vibaya katika mitihani yao ya kidato cha nne.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, alisema utamaduni kama huo haupo Zanzibar na
wangejiuzulu mawaziri wengi wa elimu waliopita akiwamo Katibu Mkuu wa CUF,
Maalim Seif Sharif Hamad.

Waziri Suleiman ametoa kauli hiyo huku kukiwa
na malalamiko kutokana na matokeo mabaya ya mitihani, huku baadhi ya wanasaisa
wakimtaka awaombe radhi Wazanzibari na kutangaza kuwajibika kutokana na
kusimamia vibaya sekta hiyo.

Alisema
kimsingi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) inapaswa kupongezwa kutokana na
mafanikio inayopata katika sekta ya elimu, ikiwamo kuongezeka kwa shule za
serikali kutoka sita kabla ya Mapinduzi hadi 134 hivi sasa
.

Inashangaza kuona watu wamekuwa wepesi wa
kulaumu pale matokeo yanapokuwa mabaya, lakini yanapokuwa mazuri hushindwa kumpa
sifa anazostahili.
Tangu kushika wadhifa huo mwaka 2001, kuna
mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa vile kiwango cha kufaulu kimeongezeka
kutoka asimilia 77.3 mwaka 2000 hadi asilimia 84.6 mwaka 2007.

Matokeo mabaya yaliyojitokeza mwaka huu si jambo
geni
kwa vile wanafunzi wamekuwa wakifanya vizuri katika baadhi
ya wakati na mara nyingine kufanya vibaya. Akiwa ameshikilia takwimu za kufaulu
wanafunzi tangu mwaka 1971, alisema hata yeye hakufurahishwa na kiwango cha
kufaulu kuanguka mwaka huu kutoka asilimia 84. 6 hadi 77.3.

Mwaka 1982
wakati Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, akiwa Waziri wa Elimu
Zanzibar, kiwango cha kufaulu kilishuka zaidi hadi asilimia 64.4.

Haroun
alisema hivi sasa kuna sababu mbalimbali zinazochangia wanafunzi kutofanya
vizuri ikiwamo upungufu wa vitendea kazi, uhaba wa vifaa vya sayansi pamoja na
walimu wa masomo hayo.

Hata hivyo, alisema Serikali ya Zanzibar kwa
kushirikiana na Serikali ya Marekani imeanza kuchukua hatua za kuondoa uhaba wa
vifaa, ikiwamo vitabu vya sayansi na kujenga shule za sekondari 19 ambazo kila
wilaya itanufaika hapa Zanzibar.

Hadi ifikapo mwaka 2010 tatizo kwa
baadhi ya wanafunzi kukaa chini litakuwa limekwisha pamoja na kuwapo uwiano kati
ya idadi ya wanafunzi na walimu katika darasa. Hivi sasa serikali inaendelea na
programu ya kusomesha walimu katika ngazi mbalimbali ambao watatumika kufundisha
katika shule za sekondari.

Hata hivyo, ni kweli Zanzibar inakabiliwa na
wimbi la walimu wanaomaliza katika viwango vya shahada kukimbilia ajira binafsi
zenye maslahi zaidi. Ili kukabiliana na tatizo hilo, serikali imeamua kupitia
utaratibu wa malipo kwa walimu kuyaboresha zaidi.

Juzi Chama cha
Wananchi (CUF) kilisambaza taarifa kwa vyombo vya habari kikimtaka waziri huyo
kuwaomba radhi wazee na vijana wa Zanzibar kwa kushindwa kwake kuinua na kukuza
elimu Zanzibar.



JAPO SIAFIKIANI NA HOJA ZILIZOTOLEWA NA MHESHIMIWA HUYU KUTETEA UNGA WAKE,NASHAWISHIKA KUKUBALIANA NAE KWENYE KAULI YAKE KUWA UTAMADUNI WA KUJIUZULU HAUPO (SI ZANZIBAR TU BALI TANZANIA KWA UJUMLA).HEBU TUANGALIE MFANO WA CHAPCHAP HUKO ATCL,UNADHANI KWANINI HADI MUDA HUU HAKUNA ALIYEJIUZULU?MAJUZI MMOJA WA MANAIBU GAVANA BOT AMETAJWA MAHAKAMANI KUWA ANAHUSIKA KWA NAMNA FLANI KWENYE SKANDALI LA EPA,KWANINI HAJAJIUZULU KUPISHA UCHUNGUZI?BAADHI YA WATENDAJI WALIOTAJWA KWENYE TUME YA MWAKYEMBE HAWAJAJIUZULU HADI LEO,KWANINI?JIBU LISILOHITAJI TAFAKURI NI HILO ALOTOA MUUNGWANA HUYO WA ZENJE:HAKUNA UTAMADUNI WA KUJIUZULU.JE CHANZO NI NINI?KWA MTIZAMO WANGU TATIZO LIKO KWA WALIOWATEUA WA HAO WANAOPASWA KUJIUZULU.UTAMADUNI HUU UMELELEWA NA UKWELI MCHUNGU KWAMBA MTU ANAWEZA KUAMUA KUJIUZULU PINDI ANAPOBORONGA JUKUMU FLANI LAKINI ALIYEMTUA HAONI UMUHIMU WA KUFANYA HIVYO.FRANKLY SPEAKING,UKOSEFU WA UWAJIBIKAJI KATIKA MAONEO MBALIMBALI UNACHNGIWA ZAIDI NA TABIA YA KULEANA NA KUBEMBELEZANA KATI YA MABOSI NA WALIO CHINI YAO.LAITI KUNGEKUWA NA KANUNI KWAMBA "UKIBORONGA ,UNAWAJIBIKA.USIPOWAJIBIKA UNATIMULIWA" BASI SI AJABU TUNGESHUHUDIA WABABISHAJI WENGI WAKIACHIA NGAZI KUEPUKA FEDHEHA YA KUTIMULIWA AMBAYO MARA NYINGI HUAMBATANA NA KUNYIMWA MARUPURUPU YA KUMALIZA AJIRA.



INACHEKESHA (JAPO INAUDHI BAADA YA KICHEKESHO HICHO) KUMSIKIA MUUNGWANA HUYU WA KIZANZIBARI AKIDAI PONGEZI ZA "kuongezeka kwa shule za serikali kutoka sita kabla ya Mapinduzi hadi 134 hivi sasa".HUU NI UGONJWA MWINGINE UNAOSHAMIRI KILA KUKICHA;KUTUMIA TAKWIMU NZURI ZA IDADI NA KUFUMBIA MACHO TAKWIMU MBAYA ZA VIWANGO (QUANTINTY vs QUALITY).HIVI KUONGEZEKA KWA IDADI YA SHULE NI MUHIMU ZAIDI YA UBORA WA ELIMU INAYOTOLEWA KWENYE SHULE HUSIKA HATA KAMA NI CHACHE?




ANASEMA "watu wamekuwa wepesi wa kulaumu pale matokeo yanapokuwa mabaya, lakini yanapokuwa mazuri hushindwa kumpa sifa anazostahili" KANA KWAMBA PAMOJA NA MATOKEO YA MWAKA HUU KUWA MABAYA BADO WIZARA ILISTAHILI PONGEZI KWA VILE ILIFANYA VIZURI MWAKA JANA.UGONJWA ULEULE WA TAKWIMU ZA MAZURI ZINAZOTUMIKA KUFICHA TAKWIMU ZA MABAYA.




SAFARI YA MAENDELEO YA KWELI BADO NI NDEFU SANA HASA KUTOKANA NA MENTALITY YA BAADHI YA WALIOPEWA JUKUMU LA KUTONGOZA KWENYE SAFARI HIYO,KAMA HUYU MUUNGWANA WA ZENJI.

13 Feb 2009



12 Feb 2009

Ni kweli nimewachapa, mara hii nimewachapwa wakiwa wamefungiwa, wakati mwingine watachapwa hadharani.” Ni kauli ya MKUU wa Wilaya ya Bukoba, Albert Mnali kuthibitisha habari kwamba aliamuru polisi mmoja kuwachapa viboko walimu katika shule tatu za msingi zilizo Bukoba, kutokana na wilaya hiyo kuwa ya mwisho katika matokeo ya darasa la saba. Huu sio udikteta bali DC huyo yaelekea haelewi aliteuliwa kufanya nini wilayani humo.Kwa habari kamili,BONYEZA HAPA

Soma zaidi HAPA.

Madaktari wamefanikiwa kuondoa virusi vya ukimwi katika mwili wa mgonjwa kwa kutumia bone marrow transplant,hatua inayoonekana kuwa ya mafanikio zaidi kuelekea kupatikana kwa tiba ya kudumu ya ugonjwa huo.Kwa habari kamili,BONYEZA HAPA.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.