23 Jun 2009

Pichani,Mwanasoshojia akimuaga Mzaa chema.

BLOGU HII INATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUTOKANA NA KIFO CHA MAMA MZAZI WA BLOGA MWANASOSHOLOJIA.HAKUNA MANENO MWAFAKA YANAYOWEZA KUKULIWAZA WEWE BINAFSI NA FAMILIA YENU KWA UJUMLA,LAKINI TUAMINI KUWA MUNGU AMEMPENDA MAREHEMU ZAIDI YETU,NA NDIO MAANA AMEMCHUKUA.NA KWA VILE MUNGU NI WA UPENDO,BASI TUNA HAKIKA ATAMPATIA MAREHEMU PUMZIKO LA AMANI NA RAHA YA MILELE.

POLE SANA,MWANASOSHOLOJIA.

Dunia haina dogo.Kuna wambeya wanaodai eti huyo "nzi" alikuwa ni skadi lililotumwa na Dick Cheney kwa Obama.Kuna wengine wanadai huyo wala hakuwa "nzi" bali roboti lilotengenezwa na majasusi wa Kimarekani kupeleka ujumbe kwa Kim Jong Ill na mikwara yake ya nyuklia.Wapo wanaomhusisha "nzi" huyo na uchaguzi wa Irani..... Alimradi burudani!

ELEKEZO: Neno "nzi" limetumika kama tafsiri isiyo rasmi ya "fly" (BAKITA mko wapi?)


Inakera ati!hususan kwa simu vimeo zinazokula chaji kama hazina akili nzuri.Wajuzi wa simu wanadai kwamba baadhi ya simu "zina allergy na full charge",yaani chaji haidumu.

Taarifa zinaeleza kwamba maabara ya Kampuni ya Nokia hapo Cambridge wanatafiti ujio wa simu itakayokuwa ikijichaji yenyewe.Badala ya kutumia chaja za kawaida,simu hiyo itakuwa ikijichaji kwa kugema nishati kutoka kwa mawimbi ya radio (radio waves) yanayotoka kwenye antena,milingoti ya televisheni,Wi-Fi transmitters,nk.

CHANZO: The Guardian


The British National Party could face legal action over its 'whites only' membership policy, a watchdog said yesterday.The party could be taken to court for three counts of discriminating on grounds of colour, the Equalities and Human Rights Commission said.

If the BNP refuses to allow non-whites to join the party, it could face heavy fines, or its assets could be seized - making it almost impossible for them to fight elections effectively.

Senior party members, such as leader Nick Griffin, could even be imprisoned, if the courts so decided. The move comes two weeks after the BNP won its first seats in the European Parliament following a collapse in Labour support. The party has around 60 councillors across the country.

Their constitution says only those with 'indigenous Caucasian' racial backgrounds can become members of the party. It is believed to be the first time that race watchdogs have threatened a political party with legal action.

The commission said the party appeared to be guilty of three breaches of the Race Relations Act: not allowing non-whites to join the party, not allowing them to take jobs at the party, and not providing equal services to constituents based on the colour of their skin.

They said this amounted to discrimination on the grounds of race and colour, which is banned under the act.The EHRC called on the BNP to provide written undertakings by 20 July that it will make the required changes or it could face a legal injunction. If not they could bring a civil action against them at the High Court.
If the party still did not comply, judges could find it guilty of contempt of court, which could lead to fines or even jail for BNP leaders.

A spokesman for the watchdog said: 'This exclusion is contrary to the Race Relations Act which the party is legally obliged to comply with. The commission therefore thinks that the BNP may have acted, and be acting, illegally.

'The commission has required the BNP to provide a written undertaking that it will not discriminate contrary to the Race Relations Act in its employment and recruitment policies, procedures and practices.'

The commission said it was also concerned that the BNP's elected representatives may not intend to offer or provide services on an equal basis to all their constituents and members of the public irrespective of race or colour.

John Wadham, the Commission's legal director, said: 'The legal advice we have received indicates that the British National Party's constitution and membership criteria, employment practices and provision of services to constituents and the public may breach discrimination laws which all political parties are legally obliged to uphold.

'We await a response from the BNP to our letter before deciding what further action we may take. Litigation or enforcement action can be avoided by the BNP giving a satisfactory response to our letter.'
The commission has received around 50 calls from members of the public recently about the BNP's membership policy, although it is believed that officials were already looking into the issue.

But last night BNP leader Nick Griffin, who was elected as an MEP for the north west of England earlier this month, said the party's rules were 'entirely legal', adding: 'We are not discriminating on the grounds of colour'.

He claimed the party was an exempted organisation under the Race Relations Act, which protected organisations which represented minority groups.Mr Griffin said this meant 'ethnic groups who need special protection such as the English in their own country, who are now second class citizens' were 'entitled to discriminate on that basis and not on the grounds of colour'.

A spokesman for the BNP said: 'We are not going to respond to threats like this. We will look at it, but it is an entirely politically-motivated attack. 'I don't think we should be bullied by outside forces. They are asking us to change our whole political ideology.'




Pengine siendi na wakati.Pengine mgumu wa kuelewa.Pengine....well,pengine sina hoja bali naibua tu cha kuropoka.All in all,mie ni miongoni mwa sijui wengi au wachache ambao hizi SIKU MAALUM hazina umuhimu kihivyo.Tuanze na siku ya kuzaliwa (BIRTHDAY).Mie nilizaliwa tarehe inayofanana na siku ya Uhuru na Jamhuri,yaani 9 Desemba (mwaka sabini na kitu).Excuse yangu kubwa ya "kuipuuza" birthday yangu huwa "tayari taifa linasherehekea pamoja nami".Si unajua 9 Desemba huwa ni mapumziko huko home?Halafu maswala ya gwaride na vikorombwezo vingine.Well,inatosha kuwa kiji-excuse cha namna flani.La muhimu kwangu katika kila 9 Desemba ni kumshukuru Mungu kwa kunifikisha siku hiyo,kisha kuongea na wazazi.Baba na marehemu mama walijenga utaratibu wa kutuimbia wimbo wa hepi bethdei to yuuu...That's it.Sala,wimbo na dua za wazazi,siku imekamilika.Hizo habari za birthday parties ni msamiati ambao haujaingia kwenye kamusi yangu.


Kuna kitu inaitwa MAHAFALI.Well,sikumbuki vyema kuhusu mahafali ya kumaliza darasa la saba lakini natambua kuwa ilikuwa mbinde hapo Ifakara.Uchumi wa familia haukuruhusu anasa zisizo na msingi,na wakati huo (1985) taifa nalo lilikuwa katika wakati mgumu vilevile.Si zamani kihivyo.lakini mengi ya yanayoonekana leo hayakuwepo zama hizo.

Nadhani kitu pekee nachokumbuka kuhusu mahafali ya kumaliza kidato cha nne ni uamuzi nilokuja kuujutia baadaye wa kuonja kilevi cha kiwandani.Nilijaribu bia aina ya Safari Lager kwa mara ya kwanza maishani.Of course,kabla ya hapo nilishawahi kujaribu kilevi cha asili cha pombe ya mpunga.Ili nisije sahau,ni vema nikujulishe kidogo kuhusu pombe hii inayonukia kama wali.Kwa kifupi,ukiinywa saa 10 jioni basi inakuwa kichwani hadi kesho saa 10 jioni.Well,at least kwa "vichwa panzi" kama nilivyokuwa siku hizo.

Basi hiyo Safari Lager ilinipelekesha kupita maelezo.Nadhani nilifanya vituko kadhaa lakini kumbukumbu zaidi niliyonayo ni kuugua kwa takriban wiki hivi.Ungetegemea kuwa hiyo ndio ingekuwa mara yangu ya kwanza na ya mwisho kugusa kilauri.Wapi!Ukiniuliza namna gani niliweza kuji-transform kutoa mnywaji anayeugua wiki nzima baada ya kunywa bia moja hadi kufikia hatua kummudu John Mtembezi (John Walker),sidhani kama nitakuwa na jibu sahihi.

Anyway,mahafali ya kidato cha sita hata sikumbuki yalikuwaje.Shule yenyewe ilikuwa ya kijeshi (Tabora Boys) halafu nilikuwa miles away from home.Mahafali kwa maana ya mahafali yalikuwa ya kuhitimu Mlimani (UDSM).Kuna waungwana walishauri nitengeneze kadi za mchango wa sherehe ya mahafali.Well,it worked.Watu wakapiga donation,likapatikana fungu la kufanya sherehe ya maana mtaa wa Isisi,Kinondoni.Na kuna mahala flani walinisaidia bia za bei nafuu.

Hapa Aberdeen nilijichukulia tu vyeti vyangu hapo 2003 na 2004.Ila nikikamilisha libeneke hili la sasa,huenda nikajumuika na watu wawili watatu maana hii ya sasaa ni shughuli nzito kwa kiasi kikubwa.

Back to the topic.Sijui Father's Day ni leo au kesho au ishapita.Honestly,muda huu naoandika post hii sina hakika,na sitaki kuhakikisha kwa ku-google.Kwangu,siku ya Baba yangu (na kama ilivyokuwa kwa Mama yangu) ni kila siku.Najua kwanini kuna siku moja maalumu,lakini kwa mie kila siku ni maalum.Yaleyale ya siku ya Wapendanao.Nikimpenda mwandani wangu basi ni suala la kila siku na Ferbuari 14 inakuwa siku kama siku nyingine tu.Of course,nimeshawahi kuonekana kichekesho huko nyuma lakini hainisumbui.

Vipi,huu mtazamo wangu unaouonaje?Ukale,uzembe wa kwenda na wakati,sahihi au you dont even care?


Na Ramadhan Semtawa, Dodoma

SERIKALI imesisitiza kuwa haiwezi kuruhusu suala la kampuni ya Buhemba Goldmine (Meremeta), kujadiliwa hadharani kwa kuwa inahusu mambo ya usalama wa taifa, lakini ikaeleza kuwa suala la ukaguzi wa Mwananchi Gold linasubiri wakati mwafaka kwa kuwa kwa sasa inafilisiwa.

Kauli hiyo ilitolewa Bungeni jana na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari wakati akijibu swali la mbunge wa Karatu, Dk Willbrod Slaa, aliyetaka kujua sababu za kampuni hizo kutokaguliwa.

Kauli hiyo pia imetolewa siku moja baada ya kuripotiwa kwa taarifa kuwa, Bunge limemwagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG), kuyakagua mashirika hayo tata yanayohusishwa na upotevu wa mabilioni ya fedha za walipakodi.

Swali hilo lilitakiwa kujibiwa Ijumaa iliyopita, lakini Spika Samuel Sitta aliliahirisha hadi jana.

Akitoa majibu ya serikali, Waziri Sumari alisema msimamo kuhusu Kampuni ya Meremeta ulishawekwa bayana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati wa kikao cha Bunge cha mwaka jana aliposema kuwa, suala hilo haliwezi kujadiliwa kwenye chombo hicho cha kutunga sheria kwa sababu linahusu usalama wa nchi.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema yuko tayari kusulubiwa kuliko kuizungumzia Meremeta kwa kuwa inahusu usalama wa taifa.

Waziri Sumari alirejea kauli hiyo ya Pinda akitaka iheshimiwe na kwamba asingeweza kueleza chochote kuhusu Meremeta na badala yake angetoa majibu ya Kampuni ya Mwananchi Gold peke yake.

Hatua hiyo ya serikali kutangaza uamuzi huo inaonekana kwenda kinyume na Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2008 inayompa CAG, ambaye anawajibika kwa Bunge, mamlaka ya kufanya ukaguzi bila ya kuagizwa.

Sumari pia alisema: “Makampuni mengine yote yenye uhusiano na Maremeta kama alivyosema mheshimiwa waziri mkuu hayatajadiliwa hadharani na serikali haioni sababu ya kufanya ukaguzi."

Baada ya majibu hayo, Dk Slaa alisimama tena kuulizwa swali la nyongeza na kudai kuwa hakuwa amejibiwa chochote na wakati akiendelea kuuliza kuhusu Meremeta, Spika Sitta alisimama na kumzima.

“Mheshimiwa Dk Slaa, suala la Meremeta linahusu jeshi. Tulikaa kwenye Kamati ya Uongozi tukakubaliana kwamba suala hili lisizungumzwe hadharani. Waziri Mkuu alishalisema; nafikiri na wewe ulikuwepo, kwa hiyo sitakuruhusu kuuliza chochote kuhusu Meremeta. Uliza makampuni hayo mengine ya Mwananchi Tangold," alisema Spika Sitta na kuipa serikali ahueni.Lakini Dk Slaa akajibu na kusema: “Siulizi Jeshi, nauliza wizi.” Lakini Sumari akamjibu kwa kusema: "Na wewe pia (Dk Slaa) tafuta hoja nyingine..."

Taarifa zinadai kuwa, Meremeta ni kampuni ambayo ilianzishwa ikimilikiwa kwa asilimia 50/50 baina ya serikali na kampuni ya Trinnex na kuna tuhuma kuwa Benki Kuu (BoT) ililipa zaidi ya Sh155 bilioni kupitia benki moja ya kigeni bila ya kufuata taratibu, kwa mujibu wa taarifa ya ukaguzi ya CAG ya kipindi kinachoishia Juni 30, 2006.

Kuhusu Mwananchi Gold, Sumari, alisema kwa sasa iko katika mchakato wa kufilisiwa.Hata hivyo, alisema ni mapema mno kuzungumzia mchakato huo, bali alitaka wabunge, akiwemo Dk Slaa kuvuta subira na muda mwafaka utakapofika wataelezwa.

Mwishoni mwa wiki, CAG aliiambia Mwananchi kuwa amepata barua kutoka Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma inayomtaka azikague kampuni hizo tata, lakini akasema bado hajapanga ataanza lini kuzikagua.

Barua hiyo yenye kumbukumbu BC.50/155/06/98 inamtaka CAG afanye ukaguzi maalumu ili kubaini thamani ya mtaji na hisa za serikali katika makampuni hayo tata na pia aieleze kamati sababu za kampuni hizo kutokaguliwa.

Awali, Dk Slaa alimuuliza Waziri wa Fedha na Uchumi ni sababu gani za msingi zilizofanya kuchukua muda mrefu kuanza ukaguzi kwa kampuni hizo hata pale tuhuma hizo zilizopigiwa kelele na jamii na hata kamati mbalimbali zilizoundwa kuchunguza tuhuma hizo.

Katika swali hilo namba 76, Dk Slaa alisema kwa kuwa katika hotuba ya waziri mkuu kivuli kwa Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), aliyoitoa bungeni Juni, 2007, alieleza juu ya ubadhirifu mkubwa uliofanywa kwa kutumia makampuni ya Meremeta na Tangold.

Dk Slaa alifafanua kwamba ubadhirifu huo ulibainika kwenye Makampuni ya Mwananchi na Deep Green Finance Co, ambao kiasi kinachodaiwa kufanyiwa ufisadi ni zaidi ya Sh215 bilioni.

Alihoji: “Ni lini kampuni hizo zitafanyiwa ukaguzi maalumu kama ilivyofanyika kwa Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) ili kubaini ubadhirifu huo uliohusisha uhamisho wa fedha kutoka Benki Kuu (BoT) na vyombo vya umma kupitia NBC Corporate Branch DSM na Ned Bank ya Afrika Kusini.

Akizungumzia majibu hayo ya serikali, mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe alisema serikali imepotoka.Zitto alisema CAG anawajibika kwa bunge na si serikali kwa kuwa ndiyo inayokaguliwa. "Serikali ndiyo inakaguliwa na CAG, huyo waziri kakosea kusema serikali haijaamua kufanya ukaguzi huo," alifafanua Zitto.

Zitto aliongeza kuwa kauli hiyo ya waziri ni sawa na kutangaza kujiingiza katika mgogoro na bunge kwa kuwa CAG anafanya kazi kwa niaba ya bunge.Utata mkubwa uliopo Meremeta ambayo inamiliki mgodi wa dhahabu wa Buhemba, pamoja na tuhuma za ufisadi ni utata wa wanahisa.Wakati serikali ikisema kampuni hiyo inahusu masuala ya ulinzi na usalama wa nchi, ndani yake kuna wanahisa ambao ni kampuni ya Uingereza ya British Law Associate.


CHANZO: Mwananchi

22 Jun 2009


Katika MAKALA HII nilionyesha wasiwasi wangu kuhusu hatua ya Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo kutangaza kufutwa kwa misamaha ya kodi kwa taasisi za dini.Katika makala hiyo,nilieleza hivi (najinukuu)

Lakini binafsi natafsiri kuwa hatua hii ina ajenda mbalimbali zilizofichika
ikiwa ni pamoja na kuonyeshana nani mwenye nguvu zaidi: mamlaka za kidunia au za kiroho.Usisahau kauli za hivi karibuni kutoka kwa madhehebu mbalimbali ya Kikristo kwamba mafisadi wameteka nchi....na kuandaa mkakati wa kupata viongozi bora katika uchaguzi mkuu wa 2010.
Toleo la leo la gazeti la Majira lina habari inayothibitisha hypothesis hiyo.Kwa mujibu wa gazeti hilo,kauli zilizoikera Serikali hadi kufikia hatua ya kutoa "kibano" hicho ni pamoja na ile ya Kanisa Katoliki kuanzisha program maalum ya kuelimisha waumini wake kuhusu masuala mbalimbali ya demokrasiapamoja na namna ya kuchagua viongozi bora.

Kwa mujibu wa Majira,kauli nyingine ni ile iliyotolewa na na Jumuiya ya Kikristo Tanzania kwenye Mkutano wake mjini Dodoma ambapo ulitolewa wito kwa waumini wa madhehebu hayo kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu hapo mwakani.




Picha ya gazeti la Majira kwa Hisani ya KENNEDY.

Najiuliza,hivi hapa nimejisifu au nimejipongeza?


20 Jun 2009


Ahadi tupu za kiwete zaelekea kutengeneza kitanzi cha CCM 2010

Na Mwandishi Wetu

IKIWA imesalia takriban miezi 18 kabla ya Uchaguzi Mkuu Oktoba mwakani, sasa ni dhahiri kuwa Rais Jakaya Kikwete ana kibarua kigumu cha kukamilisha ahadi lukuki alizotoa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.

Mazingira hayo pia yanawaweka njiapanda wabunge wengi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika kutetea tena nafasi zao.

Baadhi ya wabunge tayari wameliona hilo na miongoni wamelisema bungeni wakiwashutumu mawaziri ambao wamekuwa wakilimbikiza miradi ya maendeleo kwa upendeleo kwenye maeneo yao bila kuzingatia vipaumbele vya taifa, hata baadhi yao walifikia hatua ya kutishia kukwamisha bajeti iliyopitishwa Alhamisi iliyopita.

Kauli kali zaidi ilitoka kwa Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii aliyeomba dua kwa Mungu awalaami mawaziri hao.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa, ahadi kadhaa alizozitoa Rais Kikwete bado hazijatekelezwa na kwa kipindi kilichosalia ni vigumu kufanya hivyo.

Miongoni mwa ahadi alizotoa Rais Kikwete na hazijaonekana matunda yake dhahiri ni zile zilizoandamana na kaulimbiu yake ya Ari Mpya, Nguvu Mpya, Kasi Mpya na mpango wa ‘Maisha bora kwa kila Mtanzania’.

Kigogo mmoja ndani ya CCM amelieleza gazeti hili kwamba ahadi hiyo ya maisha bora ndiyo ilimpatia Kikwete kura za kishindo na isipotengenezewa mkakati maalumu inaweza kuwa ndio kitanzi chake na wabunge wengi wa CCM.

Alisema ahadi hiyo imesababisha baadhi ya vigogo wa chama na serikali kubadili kauli, na kusema kwamba maisha bora hayatawafuata wananchi kama hawafanyi kazi kwa bidii.

Kwa mujibu wa watu mbalimbali waliozungumza na Mwananchi Jumapili, na hata kauli za wabunge wanapochangia bungeni, Watanzania walio wengi bado wana hali duni ya kimaisha, jambo ambalo litakuwa gumu kulieleza kwa wapigakura hapo mwakani.

Kutokana na ahadi hiyo serikali ilitoa Sh30 bilioni ambazo zilipewa jina la mabilioni ya Kikwete, lakini hazikufika kwa maskini walio wengi kutokana na masharti yake kuwa magumu, na kuangukia kwenye mikono ya wasio wajasiriamali wadogo, hivyo kukwamisha mpango huo wa rais.

Ahadi nyingine zinazoelekea kushindikana ni ya mwafaka wa kisiasa wa Zanzibar ambao Rais Kikwete aliuweka kwenye kipaumbele, lakini hadi sasa hakuna mafanikio yoyote na tayari Chama cha Wananchi (CUF), kimetangaza kujitoa katika mazungumzo.

Ahadi nyingine ni ujenzi wa madaraja ya Kilombero mkoani Morogoro na Kigamboni, jijini Dar es Salaam ni miongoni mwa ahadi kubwa alizotoa Kikwete na hadi sasa hakuna dalili zinazoweza kuashiria kuwa ipo nia ya utekelezaji.

Hata hivyo, Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawambwa alipoulizwa alisema kwamba daraja la Kilombero limetengewa fedha katika bajeti ya mwaka 2009/10.

Kuhusu daraja la Kigamboni, alirudia kauli za muda mrefu kuwa hilo limo kwenye mkakati wa kuanza kujengwa wakati wowote chini ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali.

Ahadi nyingine ambazo hazijatekelezwa, zimeelezwa kuwa ni kilio cha mahakama nchini juu ya suala la masilahi ya watumishi na vifaa vya kazi.

Hivi karibuni, Jaji Mkuu, Augustino Ramadhan alisikika akilalamika kuwa kiwango cha mafungu yanayoahidiwa kutengwa kwa mahakama hufika kwao kikiwa pungufu.

Suala jingine limeelezwa kuwa ni uboreshaji wa mashirika ya umma ambayo bado yako mikononi mwa serikali, lakini kila kukicha yamekuwa na matatizo na kuzua malalamiko mengi.

Kwa upande wa barabara ambazo ziliahidiwa kujengwa kwa kiwango cha lami na ambazo bado ni Tabora-Nzega, Bunda-Ukerewe na Marangu-Mkuu Rombo-Tarakea-Kamwanga.

Aliahidi pia kulifanya jimbo la Rorya mkoani Mara kuwa wilaya, lakini utekelezaji wake umekuwa ukisuasua.

Mambo mengine ilikuwa ni kupambana na rushwa, lakini pamoja na hali hiyo kuonekana kuzaa matunda kwa mambo mengi yaliyokuwa yamejificha kuchimbuliwa na kuwekwa hadharani, malalamiko yanayoibuka ni baadhi ya watuhumiwa kutofikishwa mahakamani.

Rais Kikwete pia aliahidi kuondoa kero nyingi za Muungano lakini licha ya kuunda kamati ya kuzijadili na kuzishughulikia chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais, zipo dalili za baadhi ya wananchi kutoridhika.

Tatizo kubwa linalojitokeza ni baadhi ya Wazanzibari, wakiwamo viongozi wa SMZ kutoa kauli zinazoonyesha dalili za waziwazi kwamba wanadhulumiwa ndani ya Muungano.

Pamoja na hali hiyo, Rais Kikwete atajivunia kwa kutekeleza ahadi yake ya kulifanya Bunge kuwa huru kwani limeonyesha dhahiri kuwa na meno kwa kufichua udhaifu wa baadhi ya vigogo serikali bila kuwa na woga.

Ameonyesha mafanikio pia katika ahadi yake ya kuendesha dola kwa misingi ya utawala bora na uwajibikaji; utawala wa sheria unaoheshimu na kulinda haki za binadamu.

Hata hivyo, katika kipengele hicho kuna manung’uniko kadhaa kama vile baadhi ya viongozi wanaotuhumiwa kuendelea na nyadhifa zao wakati taratibu za utumishi wa umma ziko wazi kwamba wangepaswa kusimamishwa au kupewa likizo ama kuhamishiwa sehemu nyingine, ili uchunguzi huru ufanyike.

Mafanikio mengine ni kutekeleza ahadi ya kuongeza nafasi za elimu ya juu baada ya kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dodoma.

Ahadi nyingine ambayo Rais Kikwete ameonekana wazi kuivalia njuga ni kuboresha kilimo; na tayari mikakati kadhaa ikiwepo ya pembejeo za kilimo imewekwa, ingawa kuna malalamiko ya pembejeo kutofika kwa wakulima na wakulima wa karafuu na kahawa kutokuwa huru kutafuta masoko yao nje ya nchi.

Nguvu kubwa ya serikali yake kuielekeza kwenye kilimo imechagizwa na mtikisiko wa uchumi duniani ambao umetishia uchumi wa nchi nyingi hasa maskini ambazo zinategemea chakula kutoka nje.

Licha ya mafanikio hayo, serikali ya Kikwete inakabiliwa na changamoto kadhaa hasa za wananchi kutoridhika na mambo mbalimbali yanayotendwa na serikali yake.

Lingine ni wananchi kuona kuwa bado serikali ina matumizi makubwa ya fedha na wakati huo huo inawabidi kufunga mkanda ili kuihudumia huku wakikabiliwa na mazingira magumu ya kipato.

Malalamiko mengine ni baadhi ya watendaji serikalini kuendelea kutumia magari ya kifahari na kutenga Sh19 bilioni kwa ajili ya chai maofisini.

CHANZO: Mwananchi


Orodha ya wabunge bubu bungeni yawekwa hadharani

Na Leon Bahati

WAKATI tukielekea mwaka wa lala salama wa Bunge la mwaka 2005-2010, huku baadhi ya wabunge wakiibuka mashujaa kwa kutoa michango mizito inayoitingisha serikali, imebainika kuwa baadhi yao hadi sasa hawajawahi kuuliza hata swali moja wala kuchangia.

Uchunguzi huo umefanywa na Mwananchi Jumapili kwa msaada wa tovuti ya bunge ambako kila mchango wa mbunge hurekodiwa kwa kuonyesha swali la msingi au la nyongeza alilouliza, majibu yake na mchango aliotoa.

Kati ya wabunge 319 walioko katika Bunge la sasa ambao hawajawahi kuuliza maswali ya msingi wanakadiriwa kufikia 50 na wasiouliza maswali ya msingi wala nyongeza ni zaidi ya 30.

Mawaziri na wabunge ambao pia ni wakuu wa mikoa, hawajahusishwa kwenye hesabu hizo kwa sababu wapo upande wa serikali na wote wamekuwa hawaulizi maswali. Wengine ambao hawakuhusishwa kwenye vipengele hivyo ni Spika na Naibu Spika, lakini wote wameonyeshwa kuwahi kuchangia hoja mbalimbali.

Kwa mujibu wa mtandao huo, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz ndiye pekee ameonyeshwa kuwa hajawahi kuuliza swali lolote wala kuchangia jambo lolote tangu Bunge limeanza.

Wabunge wengine ambao wameonyeshwa hawajawahi kuuliza maswali, lakini wamekuwa wakichangia hoja mbalimbali nao ni Yusuf Makamba (Katibu Mkuu wa CCM); John Shibuda, Harith Mwapachu, Ali Haji Ali, Omar Sheha Musa, Abdallah Sumry, Gideon Cheyo, Juma N’hunga, Nazir Karamagi, Anna Abdalah, Ali Haji Ali, Thomas Mwang’onda, Salum Khamis Salum, Hassan Rajabu Khatibu na Felix Mrema.

Wengine ni Philemon Sarungi, Edward Lowassa, Andrew Chenge, Abdisaalam Issa Khatib, Dk Ibrahim Msabaha, Zakia Meghji, Kingunge Ngombale Mwiru, Salimu Yusufu Mohamed, Salum Ahamed Sadiq, Omar Sheha Mussa, Manju Msambya na Benedict Ole-Nangoro.

Wabunge ambao pia ni wakuu wa mikoa ufanisi wao wa kuchangia bungeni ni mdogo ni Abdul Aziz – Iringa (7); Dk James Msekela – Dodoma (6); Monica Mbega – Kilimanjaro (3); Dk Christine Ishengoma-Ruvuma (4) na William Lukuvi – Dar es Salaam (3). Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba aliwahi kutoa michango bungeni mara mbili tu.

Katika Kundi la wabunge 13 wanaoongoza kwa kuuliza maswali ya msingi linaongozwa na Mgana Msindai (CCM) mwenye maswali 34 na kufuatiwa na William Shellukindo (29); Diana Chilolo (28), Paschal Degera (28), George Lubelege (25), Raphael Mwalyosi (24) na Mhoga Ruhwanya (23).

Wabunge wengine kwenye kundi hilo wana maswali 22 kila mmoja nao ni, James Msalika, Job Ndugai, Zitto Kabwe, Herbert Mtangi, Victor Mwambalaswa na Lucy Owenya.

Wabunge 11 vinara wa kuuliza maswali ya nyongeza ni Dk Wilbrod Slaa (71), Hamad Rashid Mohamed (71), Mgana Msindai (67), Esther Nyawazwa (58), George Lubelege (56), Diana Chilolo (54), Hafidh Ali Tahir (52), Geofrey Zambi (50) na wawili waliofungana kwa kuuliza 49, Jenista Mhagama na John Kilimba (49).

Katika kundi la kutoa michango mbalimbali kwenye vikao vya bunge linaongozwa na Naibu Spika Anne Makinda (495); akifuatiwa na Spika, Samweli Sita (494). Wengine ni Jenister Mhagama (193); Job Ndugai (147); Zitto Kabwe (125); Dk Slaa (106); Andrew Chenge (89); Suzan Lyimo (87); William Shelukindo (77); Geofrey Zambi (73); John Kilimba (69) na mawaziri wawili waliofungana kwa kufikisha michango 67 ambao ni Shamsa Mwangunga, Waziri wa Maliasili na Utalii na Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawambwa.

Mawaziri wengine wanaofuatia ni Dk Mary Nagu (64); Profesa David Mwakyusa (59); William Ngeleja (50); Mwanasheria Mkuu wa Serikali; Johnson Mwanyika (47); Dk Makongoro Mahanga (45); Profesa Jumanne Maghembe (45); Stephen Wasira (41) na John Chiligati (40).

Akizungumzia kuhusu kumbukumbu hizo wiki iliyopita, Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alisema kuwekwa kwa taarifa hizo hakuna maana zaidi ya kuweka kumbukumbu za michango ya wabunge, lakini akasema kulikuwa na marekebisho kwa wakati huo.

Alipotafutwa tena jana, alisema tovuti hiyo ya Bunge imefanyiwa marekebisho makubwa ili wananchi waweze kupata kwa undani kumbukumbu mbalimbali za vikao vya Bunge.

Pamoja na maboresho hayo, Dk Kashililah alisema: "Tuna mpango wa kuongeza maboresho zaidi yakiwepo ya kuwezesha watu kufuatilia vikao vya Bunge kupitia tovuti hiyo."

Licha ya baadhi ya wabunge kuwa na mchango hafifu, Bunge la sasa limeonekana kuwa mwiba mkali kwa viongozi serikalini hususan mawaziri, kutokana na baadhi ya wabunge kuwabana katika mambo mbalimbali ya utendaji mbovu na ufisadi, huku kufupishwa kwake kukipunguza nafasi ya kuuliza maswali na kuchangia kwa baadhi yao ambao walikuwa hawajafanya hivyo.

Katika kipindi hicho miongoni mwa hoja nyingine zilizosisimua ni mjadala wa Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe kuhusu utoaji wa zabuni ya umeme wa dharura iliyotolewa kwa kampuni ya Richmond Development Limited (LLC); na kusababisha Rais Jakaya Kikwete kuvunja baraza la mawaziri baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kujiuzulu pamoja na mawaziri wengine wawili.


CHANZO: Mwananchi

19 Jun 2009


18 Jun 2009



Hivi karibuni watunga sheria (wabunge) wetu watatu "waliungana" kuandika kitabu walichokipa jina "BUNGE LENYE MENO".Ukiangalia sehemu ndogo tu ya wasifu wa wabunge hao utamaizi kuwa "muungano huo wa uandishi" ulikuwa ni mithili ya "ndoa za makaratasi" (marriages of inconvenience).

Dkt Wilbroad Slaa,Spika Samuel Sitta na John Momose Cheyo!Nadhani kitu pekee kinachoweza kuwafanya wafanane ni "wote ni wabunge",and the similarity stops there.Wakati Dkt Slaa amejijengea jina kubwa kama kinara wa mapambano ya ufisadi,ni vigumu kum-define Spika Sitta linapokuja suala la mapambano dhidi ya ufisadi.Lakini si vigumu kukumbuka kuwa ni Sitta huyuhuyu aliyempa kadi nyekundu Zitto Kabwe alipombana ex-waziri Nazir Karamagi kuhusu sakata la Buzwagi.Na ni Sitta huyuhuyu aliyetishia kumshtaki Dkt Slaa alipoibua tuhuma ufisadi ndani ya Benki Kuu akidai kuwa ni ushahidi wa kufoji!Eti leo tunaambiwa Spika huyuhuyu nae ni kinara wa mapambano ya ufisadi!


Tukija kwa John Cheyo,nadhani amebaki kuwa UDP,kwa maana ya one-man party.Sera yake ya mapesa ilijaa utani ambao ungekuwa na maana zaidi kwenye sanaa za maigizo kuliko katika siasa makini.Amebaki kuwa jina tu.Sidhani kama kunamfano wowote hai unaoweza kutumika kumtambulisha Cheyo kama mwanaharakati wa mapambano dhidi ya ufisadi.


Sasa hao ndio waandishi wa kitabu BUNGE LENYE MENO.Lakini kwa vile nafahamu kwamba uchambuzi makini unahitaji kwenda mbali zaidi ya kuangalia personalities,naomba kugeukia hoja yangu ya kupingana na ya akina Sitta kuwa bunge la sasa lina meno.Binafsi nasema kama ni meno basi ni ya plastiki.Nadhani unafahamu mtoto mchanga anapoanza kuota meno huwa yanaota meno ambayo yanaitwa meno kwa vile tu yamekaa sehemu yalipo meno.Ukimnywesha uji wa moto basi kilio chake hapo ni balaa!Ni meno machanga yasiyomudu kutafuna vitu vigumu.


Na ndio bunge letu lilivyo.Utasikia kelele,vitisho,na vitu kama hivyo kila waheshimiwa wanapokutana hapo Dodoma ambapo mwisho wa siku akaunti zao zinaingiza kipato cha zaidi ya mwezi mzima kwa Mtanzania wa kawaida,huku kila mwisho wa mwezi wakiondoka na mamilioni lukuki.Basi angalau kipato chao kingeendana na hali halisi ya uchumi wa nchi yetu.


Wabunge wa CCM,ambao wanatengeneza zaidi ya robo tatu ya bunge letu,ndio vichekesho zaidi.Utamsikia huyu akisema hili kabla ya mwenzie kumkalia kooni akitaka mwongozo wa Spika kwa madai ya "kukiuka kanuni za bunge".Lakini ukifuatilia kwa makini,mara nyingi mwongozo huo huombwa pale anapojitokeza mbunge mmoja kuelezea yale yanayozungumzwa na Watanzania wengi mitaani,kwa mfano ishu ya ufisadi.Sasa kwa vile kuna wabunge wenye deni kubwa zaidi kwa CCM na vigogo wake,njia pekee ya kulipa deni hilo ni kuomba mwongozo wa Spika ili kuwaziba midomo wale wanaoongea yasiyopendeza masikioni mwa watawala.


Majuzi,Mbunge wa Nzega Lukas Selelii amemwomba Mungu awalaani mawaziri kwa madai kwamba wamekuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya ufisadi nchini.Mbunge wa Pangani Mohammed Rished akaomba mwongozo....sijui kuonyesha anafahamu zaidi sheria za Bunge au kwa vile yaliyoongelewa na Selelii hayakumpendeza mbunge Rished.Kwani si kweli kwamba maamuzi mengi yaliyopelekea skandali za ufisadi yalipitishwa na Baraza la Mawaziri?Kabineti ingetimiza wajibu wake tungekuwa na Richmond?au Kiwira?Au TICTS?au Buzwagi?Au IPTL?Orodha ni ndefu.Sasa Rished alihitaji mwongozo kwa vile Selelii kumuomba Mungu awalaani watu waliofanya maamuzi yaliyopelekea ufisadi ni kosa la jinai au?Halafu tunaambiwa tuna "bunge lenye meno"!In this case,haya wala si meno ya plastiki bali ni mapengo kabisa.


Fuatilia kwa karibu mjadala wa Bajeti unavyoendelea huko Dodoma.Kuna kauli za uchungu kutoka kwa baadhi ya wabunge kama Selelii,Mwambalaswa,Mpendazoe na,kama kawaida,wabunge wa upinzani kama vile Dkt Slaa.Lakini kauli pekee hazimsaidii Mtanzania masikini asiyejua hatma ya maisha yake.Kelele hizi zimekuwepo tangu bunge hili linaanza.Ndio,zimesaidia kuundwa kwa kamati mbalimbali kama ile ya Mwakyembe.Lakini kuunda kamati kisha kutofanyia kazi mapendekezo yake ni sawa na ufisadi tu.Ikumbukwe kuwa kamati hizo hutumia mamilioni ya fedha za walipa kodi.Ukubwa wa gaharama za kuendesha kamati za aina hiyo ungeweza kupunguziwa maumivu laiti mapendekezo yanayotolewa yangekuwa yanafanyiwa kazi.Hadi leo wahusika wa Richmond (achana na yule decoy mwenye kesi mahakamani) wanaendelea "kupeta".


Laiti Bunge lingekuwa na meno,isingetosha kwa Lowassa,Msabaha na Karamagi kujiuzulu tu.Walipaswa wakabidhiwe kwa vyombo vya dola.Kadhalika,watendaji wa serikali waliotajwa kuhusika walipaswa kuwajibishwa mara moja.Badala yake,hadithi zimeendelea kila kinapojiri kikao kingine cha bunge,huko waandishi wetu mahiri wa kunukuu wakija na vichwa vya habari kama "Moto kuwaka Bungeni","Ishu ya EPA kuibuliwa tena Bungeni"...Huwezi kuwalaumu sana kwa vile vyombo vya habari vinaendeshwa kibiashara na kichwa cha habari chenye mvuto kinauza gazeti!


Bunge lenye meno lisingekuwa linapigwa danadana na Waziri Ngeleja kuhusu ishu ya Kiwira.Bunge lenye meno lisingekubali mkataba wa TICTS uendelee kuwa hoja ya moto kila kikao lakini inayoishia kuwa ya moto pasipo mabadiliko,only for it kuwa ya moto tena kwenye kikao kingine.Yayumkinika kusema kuwa kama ni moto wa hoja,basi ni wa njiti ya kiberiti kwenye upepo mkali;hudumu kwa sekunde tu.


Sintajadili zaidi kwa vile itakuwa sawa na kupre-empty muswada wa chapisho naloandaa kama mapitio (majibu?) ya kitabu hicho cha wabunge hao.Ila kwa kifupi,si rahisi kuwa na bunge lenye meno wakati wabunge wenyewe wanaishi maisha tofauti na hao wanaopaswa kuwawakilisha bungeni (nikimaanisha maslahi yao).Tusidanganyane,mtu anayelipwa milioni 6 na ushee kwa mwezi hawezi hata chembe kuwa mwakilishi mzuri wa mtu asiye na uhakika wa kukamata angalau shs 10,000 kwa mwezi.Haya ni matabaka mawili tofauti,na japo kinadharia wabunge wanapaswa kuwa sehemu ya tabaka tawaliwa kwa maana ya uwakilishi wa wananchi,maslahi yao makubwa yanawaingiza kwenye tabaka tawala na hivyo kuwaweka kwenye mgongano wa moja kwa moja direct confrontation) na tabaka tawaliwa la wananchi wa kawaida.Katika hali hiyo,serikali kwa maana ya the executive branch of the government,inapata free pass kwani wanaopaswa kuihoji nao wanajikuta wakihojiwa na wanaowawakilisha.Kiuhalisia,mpiga kura is hardly represented bungeni.


Lakini tukiweka kando suala la kipato na matabaka,tatizo la msingi zaidi kwenye bunge hili ni kutanguliza mbele maslahi ya chama badala ya maslahi ya nchi.Umoja na mshikamano ndani ya CCM unatafsiriwa kuwa ni muhimu zaidi kuliko umoja na mshikamano wa kitaifa.Wengi wa wabunge wa CCM wanahofia kuzungumzia baadhi ya masuala yanayolihusu taifa ambayo kwa namna moja au nyingine yanaifanya CCM inyooshewe kidole.Hakuna mbunge wa CCM anayeweza kuzuia bajeti ya wizara flani,hata kama ni mbovu namna gani,kwa vile akifanya hivyo atatafsiriwa kuwa anavunja mshikamano wa chama.Mbunge katika bunge lenye meno hawezi kuogopa tafsiri ya chama chake,bali wapigakura wake.

Kwa anayehitaji nakala ya bure ya kitabu hicho cha BUNGE LENYE MENO (as an ebook),tuwasiliane.

17 Jun 2009


Ni dua pekee linaloweza kubadili viumbe wa aina hii.Sijui ni kujikomba,sijui uhaba wa tafakari au...!!!Soma kwanza stori hii kisha utafakari

Chenge asimikwa utemi

na Sitta Tumma, Magu

MBUNGE wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, ambaye amekuwa akiandamwa na kashfa mbalimbali, ametawazwa kuwa mtemi wa kabila la Wasukuma-Bagole, Kanda ya Itilima, wilayani Bariadi.

Chenge alichaguliwa katika sherehe maarufu za kabila hilo, maarufu kama Bolabo, mwishoni mwa wiki, wilayani hapa, ambazo mbali naviongozi wa kimila, Mkuu wa Mkoa, Abbas Kandoro, alikuwa ni miongoni mwa waliohudhuria.

Baadhi ya watu waliokuwepo kwenye sherehe hizo, waliuelezea utemi wa Chenge kwa mtazamo tofauti, huku baadhi wakidai kaupata ili kuweka mambo yake sawa, na wengine wakidai anastahili kupata nafasi hiyo kwa kuwa ni miongoni mwa watu wa kabila hilo.

Mbunge huyo ambaye alilazimika kujiuzulu nafasi yake ya uwaziri alisema, utemi huo ni karama aliyopewa na Mungu na kwamba wajibu huo ni sawa na daraja la kuunganisha jamii ya kabila husika.

"Utemi niliopewa naweza kusema ni karama iliyotoka kwa Mwenyezi Mungu! Kazi hii ya utemi ni nzito kwa sababu ina masuala yake yanayohusiana na mambo ya kimila pamoja na kuunganisha jamii ya kabila husika," alisema Chenge.




Ndio maana wakati mwingine hawa "wazungu" wanapata wakati mgumu kutuelewa.Hivi inaingia akilini kweli kwa mtuhumiwa wa ufisadi wa zaidi ya shilingi bilioni moja,Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge,kutunikiwa utemi?Watoto wanaozaliwa leo na kesho na kukuta mtemi wao ni miongoni mwa watu waliochuma utajiri kwa njia za miujiza kabisa (fedha alizonazo haziwezi kuwa zimepatikana kwa njia halali,piga ua) watawaelewa kweli wazazi wao?

Mtemi wa nini?Au wanamaanisha utemi wa kuifanya sheria imwogope?Maana kesi yake ya kuua ni vituko vitupu.Mara iundiwe tume,mara iahirishwe kwa hili na lile!Mtu kasababisha ajali huku gari ikiwa na bima iliyoisha muda wake,mnamuundia tume ya nini?Na kwanini hiyo tume iwe kimya kama haikuundwa vile?

Mtuhumiwa huyu wa ufisadi ameendelea pia kuwa kwenye kamati ya maadili ya CCM.Halafu ukisema CCM chama cha kifisadi kuna waungwana wananuna!

Kaaazi kwelikweli

16 Jun 2009

Posing for GQ,Sacha as BRUNO

In Paris at the premiere of his latest movie BRUNO


Red carpet queer style

Cohen's (real-life) other half ISLA FISHER.With Cohen,it seems necessary to state clearly if something about him is real or sheer comedy.


As a Kazakh reporter BORAT.


As a Staines gangsta Ali G (AKA Alistair Leslie Graham)


Ali G: Gangsta or Chav?
PICS FROM The Daily Mail and the Web.




Please copy the sample letter and write to your representatives in the government, asking them not to recognize the presidency of Mr. Ahmadinejad. Please also ask others to do the same.

Dear Sir or Madam:

On June 12, 2009, the Iranian people went to the polls in record numbers to choose the next president of the Islamic Republic of Iran. Only four candidates were allowed to compete: the incumbent President Mahmoud Ahmadinejad, Mir Hussein Mousavi, MehdiKaroubi, and Mohsen Rezaie. The Iranian reform movement was united behind Mr. Mousavi’s
candidacy.

Based on numerous polls carried out a few days before the elections, Mousavi had a commanding lead over Ahmadinejad. Unfortunately, in total disregard for the people’s choice, the interior ministry haphazardly declared Mr. Ahmadinejad the winner, giving him 63.62% of the votes. The absurdity of the government’s election engineering is that none of the candidates managed to get more than a fraction of the votes even in their hometowns! In his birthplace, the village of Lali, Rezaie received fewer than 70 votes of the total of 900 votes cast, while 830 votes went to Ahmadinejad. Likewise, Karoubi did not do much better in his birthplace Aligoudarz, garnering only 14,512 votes, while Ahmadinejad received 39,690 votes. Finally, Mousavi, in his birthplace, Shabstar, was given only 2,000 of the total of 7,000 votes cast, while the rest went to Ahmadinejad.

How could all these candidates get defeated in their own hometowns, while we know that in the past presidential elections, all the candidates got the majority of the votes in their hometowns? Evidently, those who manufactured these figures got their lesson from Nazi propaganda minister Joseph Goebbels that the bigger the lie, the more believable it is. They must have thought that if Ahmadinejad is declared the winner even in his rivals’ hometowns, the Iranian people would believe his victory everywhere.

The unofficial results from the interior ministry tell quite a different story. Accordingly, Mr. Mousavi was the absolute winner with 54% of the votes, followed by Karoubi and Ahmadinejad with 31% and 13% of the votes,respectively.

Given that days before the election the Revolutionary Guards made a scarcely veiled threat to the followers of the reform movement that they will stifle swiftly any attempt at a “velvet revolution,” that a day before the elections the SMS network of mobile users were disconnected in the country, and that the websites belonging to the reformist candidates were filtered—all were indicative of the fact that the regime had staged a political coup. If Ahmadinejad was so popular, why should the Revolutionary Guards be so concerned about an impending velvet revolution? Why should they be compelled to disconnect the SMS network of mobile users?

The Iranian people do not accept the shenanigans engineered by the regime. They are demanding an investigation. They demand an honest and objective counting of the votes. Without their demands being met, the result has no validity.

Please do not recognize the official results of the elections. Please do not recognize the presidency of Mr. Mahmoud Ahmadinejad.

Democracy in Iran means peace in the Middle East. I appreciate your support.

Below are links to more information and report on Iran’s elections.

http://www.nytimes.com/2009/06/15/opinion/15iht-edcohen.html?_r=1&th&emc=th

http://garysick.tumblr.com/

www.truthout.org/061409Z?print

Miongoni mwa nukuu muhimu kuhusisna na Mwenyekiti Mao wa China ni hii: usiseme kitu kama hujakitafiti (tafsiri yangu isiyo rasmi kwenye usemi no research,no right to speak).Sasa sijui tumweleweje huyu Sekulu MUSTAFA MKULO anapodai kwamba kuna baadhi ya taasisi za dini zimekuwa zikitumia vibaya misamaha ya kodi,lakini hakuweza kutaja angalau jina la taasisi moja.Hizi ni dalili za ubabaishaji na uoga.Uoga huo wa kutaja hadharani watumishi wa Mungu wanaotuhumiwa kuvunja sheria unasababishwa na mtoa tuhuma kutokuwa mkamilifu.Ni mithili ya mama anayechelea kutaja madhambi ya bintie kwa kuwa naye yumo katika mchezo huohuo.



Kama kuna wachunga kondoo wa Bwana walikuwa wakitumia misamaha ya kodi vibaya lakini hawakuchukuliwa hatua,inamaanisha chombo kinachoitwa Mamlaka ya Mapato kiko kwenye usingizi wa pono.Kwanini wahusika hawakuchukuliwa hatua?Au kulikuwa na utatu usio mtakatifu wa vigogo serikalini,wafadhili ughaubuni na watumishi wa Mungu?

Hata kama tukiafikiana na maelezo za Mheshimiwa Mkulo kuhusu hako kamchezo kasikopendeza ,ni dhahiri kwamba vitendo vya watenda dhambi hao wachache havimaanishi kuwa dhehebu lote analotoka mtenda dhambi nalo lina makosa.Kuwepo kwa viongozi kadhaa wa dini ambao wamekuwa wakitumia vibaya misamaha ya kodi hakumaanishi kwamba mantiki nzima ya mpango huo imepoteza maana.


Na lini utaratibu huu wa "akikosea mmoja basi wamekosea wote" ulianza?Mbona hapo Benki Kuu palipozaliwa ufisadi wa EPA na nduguye wa Maghorofa Pacha bado wahusika wameendelea "kupeta"?Kama Ballali ndio kinara cha wizi huo,kwanini basi wasaidizi wake (ikiwa ni pamoja na huyu gavana wa sasa) wameachwa kuendelea na kazi?Je Liyumba anapotuhumiwa kufanya ubadhirifu wa fedha za Maghorofa Pacha,kwanini basi menejimenti yote ya Benki Kuu nayo isipandishwe kizimbani kwa vile,kwamujibu wa Mkulo,akikosea mmoja basi wamekosea wote!Mbona Mattaka kalikoroga ATCL kapelekwa NIC,Peter Noni anahusishwa na EPA kapewa ulaji TIB,Mzee wa Vijisenti na mabilioni yake visiwani Jersey bado yuko kwenye kamati ya maadili ya chama tawala!

Kwa madhambi haya,dnio maana hutosikia yeyote akidiriki kutaja jina la kiongozi wa dini anayetuhumiwa kufuja misamaha ya kodi (kama yupo).Mtu asiye msafi hawezi kuonyesha uchafu wa mwenzie.

Lakini binafsi natafsiri kuwa hatua hii ina ajenda mbalimbali zilizofichika ikiwa ni pamoja na kuonyeshana nani mwenye nguvu zaidi: mamlaka za kidunia au za kiroho.Usisahau kauli za hivi karibuni kutoka kwa madhehebu mbalimbali ya Kikristo kwamba mafisadi wameteka nchi....na kuandaa mkakati wa kupata viongozi bora katika uchaguzi mkuu wa 2010.



Wizara ya Fedha na Uchumi imesema, siasa za Tanzania ni nzuri na kuna mipango mizuri ya maendeleo ndiyo maana umasikini wa kipato unapungua. Hata hivyo Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Omar Yussuf Mzee amesema, bungeni mjini Dodoma kuwa, kuna watanzania wengi wanaishi kwa kula mlo mmoja. Kiongozi huyo wa Serikali amesema leo kuwa, umasikini ni mchakato, unapungua siku hadi siku.

Mzee ameyasema hayo wakati anajibu maswali ya Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya aliyetaka kufahamu ni kwa nini watanzani wengi bado ni masikini wakati nchi imepata uhuru miaka 48 iliyopita.

Mbunge huyo pia alidai bungeni kuwa, watanzania wengi bado ni masikini kabisa kwa kuwa hakuna siasa safi, na pia hakuna mipango mizuri ya kuwawezesha wananchi wapate maendeleo.

Naibu Waziri Mzee amewaeleza wabunge kuwa kuna umasikini wa aina tatu ukiwamo wa elimu, afya na kipato.Amesema, kama Tanzania isingekuwa na siasa safi na mipango mizuri ya maendeleo, takwimu zisingeonyesha kupungua kwa umasikini wa kipato nchini.


Amewaeleza wabunge kuwa, mwaka 1991, asilimia 21.6 ya watanzania wote milioni 24.8 walikuwa masikini kabisa. Kwa mujibu wa kiongozi huyo, mwaka 2001, Tanzania ilikuwa na watu milioni 31.9, asilimia 18.7 kati yao walikuwa masikini kabisa, na mwaka 2007, asilimia 16.5 ya watanzania milioni 38.3 walikuwa masikini kabisa.

Mzee amelieza Bunge kuwa, watanzania wengi bado ni masikini kwa kwa wengi wao ni wakulima wanaotumia jembe la mkono, bei za pembejeo za kilimo zimepanda, na pia mabadiliko ya hali ya hewa yanathiri uzalishaji kwa kuwa sehemu kubwa ya kilimo nchini hutegemea mvua. Ametaja sababu nyingine kuwa ni ukuaji mdogo wa sekta ya viwanda, wakulima kukosa mitaji, na pia ukosefu wa ajira.


CHANZO: Habari Leo

Wizi mtupu!


Professor Duncan Rice, Principal and Vice Chancellor of the University of Aberdeen, has been honoured with a Knighthood in the Queen’s Birthday Honours.

Professor Rice has been awarded the honour for services to higher education.

Professor Rice said: "On a personal level this is a wonderful honour, and I'm very proud of it. But I know it's intended to recognise all the University has achieved in the last decade. I am just the vehicle, and the real congratulations go to the whole of our community. It is being transformed by the commitment, quality and vision of all my colleagues, and my knighthood is a way of honouring them."

He added: "By the standards of where we were a decade ago, we have manoeuvred ourselves into being one of the top handful of universities in Scotland. That makes this something of a minor golden age. What we really want to do now is to advance into a real golden age, where we are one of the top handful of universities in the world."



14 Jun 2009


Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu has announced he will back a Palestinian state - but only if it is completely demilitarised.

He said a Palestinian state must have no army, no control of its air space and no way of smuggling in weapons.

And a Palestinian state must recognise Israel as a Jewish nation, he said.

Mr Netanyahu's speech, laying out his plans for regional peace, came a month after US President Barack Obama urged him to accept a two-state solution.

The BBC's Paul Wood says Mr Netanyahu broke ground by accepting the principle of a demilitarised Palestinian state, albeit with conditions, and this will be what the White House is looking for.

But our correspondent says the question is whether this will be enough to make up for the lack of movement on the issue of Jewish settlements in the occupied West Bank.

Mr Obama has stressed that he wants all settlement activity to stop.

But in his speech Mr Netanyahu said settlers were not "enemies of peace" and did not move from his position of backing "natural growth" in existing settlements.

Guarantee needed

The Israeli leader offered to talk to the Palestinians immediately and with "no preconditions".

"We want to live with you in peace as good neighbours," he said.

Mr Netanyahu also said he was willing to go to Damascus, Riyadh and Beirut in pursuit of a Middle East peace deal.

He said Israel would "be prepared for a true peace agreement [and] to reach a solution of a demilitarised Palestinian state alongside the Jewish state".

But only if "we receive this guarantee for demilitarisation and the security arrangements required by Israel, and if the Palestinians recognise Israel as the nation of the Jewish people.


SOURCE: BBC


Majuzi,Watanzania wametahadharishwa kuhusu athari za mdodoro wa uchumi wa dunia na madhara yake kwa nchi yetu.Kadhalika,bajeti ya mwaka ujao wa fedha imeandaliwa kwa kuzingatia tahadhari hiyo huku kukitangazwa mpango wa kuchochea uchumi (economic stimulus plan).

Hata hivyo,kama nilivyojadili HAPA,uwezekano wa bajeti na stimulus plan hiyo kufanikiwa,sambamba na umuhimu wa tahadhari iliyotolewa,utategemea zaidi hatua kali na za makusudi dhidi ya ufisadi na mafisadi.Yayumkinika kubashiri kwamba pamoja na imani kwamba mipango hiyo inalenga kulinusuru taifa,wanaufaika wakubwa wanweza kuwa mafisadi wanaojua vema namna ya kubuni mikakati ya ulaji huku wakiwa hawana hofu ya kuchukuliwa hatua yoyote kutokana na siasa za kulindana na kishkaji.

Hebu soma kwanza habari ifuatayo,kisha tujadili kidogo mwishoni.

Wingu zito fedha za EPA
• Chegeni: Zimekwenda kusikojulikana

na Mwandishi Wetu

UTATA umegubika mahali zilipo na matumizi ya fedha zilizorejeshwa na kampuni zilizoshiriki katika wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), uliofanyika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akilihutubia Bunge mjini Dodoma Agosti mwaka jana, alibainisha fedha hizo zilizorejeshwa na baadhi ya kampuni si mali ya serikali lakini zitawekwa kwenye akaunti maalumu kabla ya kupelekwa katika Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) kwa ajili ya kufungua dirisha dogo la kuwakopesha wakulima wakati nchi ikielekea katika mchakato wa kuanzisha Benki ya Kilimo.

Ingawa Rais Kikwete na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, kwa nyakati tofauti walieleza kuwapo kwa fedha hizo katika akaunti maalumu, taarifa ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata zinasema hadi sasa fedha hizo hazijaingia katika Benki ya TIB, licha ya kuwapo kwa taarifa kuwa fedha hizo zimetumika kununulia mbolea iliyotolewa kwa mfumo wa vocha kwa baadhi ya wakulima hapa nchini.

Chanzo kimoja cha habari kilichomo ndani ya TIB kimedai fedha hizo wamekuwa wakizisikia kupitia katika vyombo mbalimbali vya habari kutoka kwa wanasiasa, ambao wamekuwa wakijinadi kuwa fedha hizo zitatumika kunyanyua kilimo ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wananchi.

Chanzo hicho kilibainisha kuwa hadi sasa dirisha la kilimo lililosemwa bado halijaanza kufanya kazi iliyotarajiwa, ingawa maneno ya watu mbalimbali yamekuwa yakibainisha kuanza kazi kwake ambako kungetarajiwa kuwasaidia wakulima kupata mikopo ya muda mrefu, baada ya kuikosa fursa hiyo kwa kipindi kirefu kutokana na kutokopeshwa na taasisi za fedha za hapa nchini.

“Haya mambo huwa tunayasoma, kuyasikia na kuyaona kwenye hivyo vyombo vyenu vya habari, lakini kwenye makaratasi hali ni tofauti, sasa sijui niseme siasa inatawala au muda bado haujafika,” kilisema chanzo hicho.

Tanzania Daima Jumapili, ilifanya juhudi za kumtafuta Mkurugenzi Mtendaji wa TIB, Peter Noni, ambaye ameteuliwa hivi karibuni kushika wadhifa huo na Rais Jakaya Kikwete, lakini Ofisa Mwanadamizi wa Mambo ya Uhusiano wa benki hiyo,Catherine Magambo, alisema mkurugenzi wake hawezi kutoa ufafanuzi hivi sasa, kwa kuwa ameanza kazi siku si nyingi na ni busara akapewa wiki moja ili aweze kujipanga.

Catherine, alipotakiwa kueleza kama ana taarifa zozote za kutokuwapo kwa fedha zilizoahidiwa na rais kupelekwa katika benki hiyo, alisema anachokifahamu ni kile kilichoelezwa wakati fulani na Mkurugenzi aliyestaafu, William Mlaki, kuwa hawajapokea fedha hizo na kama kungekuwa na mabadiliko vyombo vya habari vingejua kama walivyofanya hapo awali.

“Nyinyi Tanzania Daima Jumapili, habari kama hii unayoniuliza au unayotaka mkurugenzi wangu akujibu, najuakwamba hakuna kitu ambacho kimebadilika lakini kama mnataka habari zaidi msubiri mkurugenzi mpya azoee ofisi kwa muda wa wiki, halafu ndipo uje kumuuliza maswali yako,” alisema Magambo.

Pia alibainisha kuwa hajaona mabadiliko yoyote juu ya ahadi iliyotolewa pia na Rais Kikwete ya kutoa kiasi cha sh bilioni 15 kwa ajili ya kuendeleza benki hiyo ili iweze kutoa mikopo kwa wakulima.

“Jamani maswali yenu mbona yamezidi, si nimewaambia hakuna mabadiliko na hayo maswali yenu msubirini mkuu? Mbona mnanibana kwa mambo nisiyo na uwezo wa kutoa majibu? Kwani kila ofisi ina utaratibu wake,” alisema Magambo.

Wakati fedha hizo zikionekana kugubikwa na utata, baadhi ya watu wamekuwa wakiiona hatua ya serikali kutangaza kurejeshwa kwa fedha hizo ni kiini macho au zimetumika katika matumizi mengine badala ya kupelekwa katika kilimo kama ilivyoahidiwa, kwa kuwa viwanda vingi vya mbolea kwa mwaka huuvimejikuta vikishindwa kujiendesha baada ya kuzalisha bidhaa hiyo na kukosa wanunuaji.

Dhana hiyo inachagizwa na baadhi ya wakulima ambao wamekuwa wakilalamikia kutokupata mbolea hiyo, licha ya serikali kutangaza kutenga fungula fedha kwa ajili ya kutoa ruzuku ya mbolea kwa wakulima ili kukuza kilimo na kuleta mapinduzi ya kijani.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa na wanasiasa mbalimbali wa hapa nchini walikuwa wakihusisha wizi huo wa fedha na mkakati maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwaagiza baadhi ya makada wake na wanachama wakwapue fedha hizo kwa ajili ya matumizi ya kampeni za uchaguzimkuu wa mwaka 2005 uliokiwezesha chama hicho kuibuka na ushindi wa ‘kishindo.’

Hisia hizo zilipata nguvu baada ya kuwapo tetesi kuwa kampuni iliyochota kiasi cha sh bilioni 40 ya Kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, inadaiwa kumilikiwa na baadhi ya vigogo wa chama hicho, jambo lililochangia ugumu wa kukamatwa kwa wamiliki wa kampuni hiyo ambayo inaaminika ndiyo iliyosuka mpango wa uchotaji wa fedha hizo.

Tuhuma hizo mara kadhaa zimekuwa zikikanushwa na viongozi waandamizi wa chama hicho, akiwamo Katibu Mkuu wake, YusufMakamba, ambaye aliweka bayana kuwa CCM haijamtuma mwanachama wake afanye wizi huo na kama kuna mwanachama amehusika na wizi huo apewe lawama hizo binafsi na si chama.

Naye Mbunge wa Busega, Dk. Raphael Chegeni, katikati ya wiki alinukuliwa na vyombo vya habari mjini Dodoma akisema kuwa fedha za EPA zinaonekana kwenda sehemu zisizoonekana kirahisi kwa wananchi, ingekuwabusara kama zingetumika katika ujenzi wa barabara ambayo ingepewa jina la EPA, ili kila
mwananchi aweze kuamini kinachosemwa na viongozi wa serikali.

Alisema mazingira ya fedha hizo tangu awali yalionyesha utata, hivyo ingekuwa busara hata matumizi yake yakafanyika bila kuwapo kwa usiri, ili kuondoa fikra potofu kuwa hakuna fedha iliyorejeshwa.

“Hizi fedha za EPA mimi nafikiri zingetumika kujengea barabara na tukaziita barabara za EPA, ili yeyote anayetaka kuzusha lake ashindwe kufanya hivyo au tumuonyeshe vithibitisho,” alisema Chegeni.

Alisema sekta ya kilimo ni pana na hata fedha zinazotumbukizwa huko ni lazima ziandaliwe mipango mizuri na mapema ili ziweze kufikia walengwa na zilete tija inayotakiwa kuliko inavyoonekana sasa ambapo serikali inasema imetoa mbolea ya ruzuku kwa wingi, lakini wakulima wanalalamika kutoipata mbolea hiyo kwa kiwango kinachohitajika.

Wizi wa fedha za EPA ulibainika baada ya Kampuni ya ukaguzi ya kimatifa ya Ernst &Young kubaini wizi wa sh bilioni 133, ambapo baada ya uchunguzi huo, Rais Kikwete aliamua kumfukuza kazi aliyekuwa Gavana wa benki hiyo, marehemu Daudi Ballali na kuagiza mamlaka husika kufanya uchunguzi kwa maofisa wa benki hiyo ili kufikishwa mbele ya vyombo vyasheria.


CHANZO: Tanzania Daima.

Katika mazingira kama haya,itakuwa kosa kweli kuyamkinisha kwamba hiyo stimulus plan inaweza kuishia kutengeneza dili ya kuifanya EPA ionekane "cha mtoto"?

Halafu,habari hiyo hapo juu ina kitu kingine cha ziada,nacho ni kuhusu PETER NONI.Huyu jamaa anahusishwa kwa karibu na skandali la EPA.Awali wasiwasi wangu ulikuwa kwenye kuteuliwa kwake kuwa Mkurugenzi wa TIB.Kilichonifumbua macho katika habari hii ni ukweli kwamba marejesho ya fedha za EPA yalipangwa kupelekwa TIB.You see the connection?NONI anahusishwa na ishu ya EPA kwa wadhifa aliokuwa nao BoT.Sasa anapokwenda TIB ambako tunaambiwa ndiko zitakapopelekwa marejesho ya fedha za EPA ni mithili ya "kula denge" kuelekea lilipo fungu hilo.

Ndio Tanzania yetu hiyo!

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.