Jambo moja nililojifunza kutoka kwa hawa wenzetu wa nchi zilizoendelea ni kile kinachoelezeka vizuri kwa kimombo kama not settling for less.Yaani,kwa tafsiri isiyo rasmi,ni kutokubali kuridhishwa na pungufu ya matarajio kamili.Kama ni mwanasiasa na wananachi wanaona 'unawazingua' basi usitarajie kuwa wataendelea 'kukulea'.Kama ni kwenye soka,wenye timu hawatarajii pungufu ya ushindi.
Baada ya matokeo yasiyoridhisha kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Alhamisi iliyopita,tayari 'bundi' mbaya ameshaanza kukiandama chama cha Labour.Baadhi ya wanasiasa ndani ya chama hicho wamejitokeza hadharani kutaka Gordon Brown atoswe kwa madai kuwa yeye ndio hasa chanzo cha matokeo mabaya kwenye uchaguzi huo ambapo Labour iliambulia nafasi ya pili nyuma ya chama cha wahafidhina (Conservative Party).
Japo hadi sasa Brown hajatamka kama ataachia ngazi uongozi wa chama hicho lakini dalili ni kwamba presha ikiendelea kuongezeka hatokuwa na jinsi zaidi ya kujiuzulu.Hapa sizungumzii u-waziri mkuu bali hali ya mambo ndani ya chama cha Labour.
Kukurejesha nyuma kidogo,Labour imekuwa na makundi mawili 'yasiyoiva' kwa kitambo kirefu sasa.Kwa upande mmoja ni wale wanaofahamika kama Blairites,ambao wanamhusudu Waziri Mkuu wa zamani Tony Blair,na kwa upande mwingine ni Brownites,ambao wanamhusudu Gordon Brown.Inasemekana kuwepo kwa makundi hayo kumechangia kwa kiasi flani matokeo mabaya ya chama hicho katika uchaguzi uliopita.Inadaiwa kwamba mmoja ya watu wenye nguvu kubwa ndani ya Labour,Lord Mandelson,alitumia kampeni za Brown na Labour kumuimarisha David Miliband,'Waziri' wa Mambo ya Nje wa Uingereza na chaguo la Blairites kumrithi Brown.Inaelezwa kwamba wakati Labour wanazindua kampeni zao kwa ajili ya uchaguzi huo,Mandelson (maarufu kama Malaika wa Giza-Angel of Darkness-ndani ya Labour)alifanikisha safari ya Miliband kwenda Marekani kwa mazungumzo na Rais Obama,fursa ambayo wachambuzi wa siasa wanaamini ingemwezesha Brown kuonekana kama kiongozi mwenye nguvu katika siasa za kimataifa.
Inadaiwa pia kuwa kampeni ya Brown iligeuzwa na Mandelson kuwa 'makao makuu ya Miliband' kwa maana kuwa ilikuwa ikitumika kwa namna flani kumpromoti mwanasiasa huyo (Miliband) ambaye bado ana ukaribu mkubwa na Blair.Hata meya wa zamani wa jiji la London,Ken Livingstone ameligusia hilo katika makala yake aliyoandika kwenye gazeti moja la Daily Mail.
Kwa sasa,harakati zinazoendelea chini chini ndani ya Labour ni za kumrithi Brown.Yani imekuwa kama ndugu za mgonjwa wanapoanza kugombania urithi kabla mgonjwa huyo hajaaaga dunia.Alosema siasa ni mchezo mchafu hakukosea.Baadhi ya majina yanayohusishwa na mpambano huo ni pamoja na akina Miliband,yaani David na mdogo wake Ed,ambaye ni waziri wa mazingira,Ed Ball- 'waziri' wa elimu na 'waziri' wa mambo ya ndani Alan Johnson.
Na akina Miliband wanazua mvutano ambao unavuka anga za siasa kwa vile wakati David (pichani kushoto) ni Blairite,mdogo wake (kulia) ni Brownite.Inaelezwa kuwa tayari Ed ameshamfahamisha mama yao kuwa anadhamiria kupambana na kaka yake kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Labour.Hata hivyo,inaelezwa pia kuwa bado yuko njia panda kwa vile kwa upande mmoja Brownites wenzie wanamwona kama chaguo mwafaka kwa nafasi hiyo,lakini kwa upande mwingine 'damu ni nzito kuliko maji' na anatafakari kama pengine itakuwa jambo la busara kumsapoti kaka yake.
Tukiachana na mvutano huo wa kifamilia,'vita' kubwa inatarajiwa kuwa kati ya kaka yake (David) na (Ed) Balls.Wakati David anasifika kwa upeo na akili ya hali ya juu (ni Mwingireza mwenye asili ya Kiyahudi huyu) na ufahamu wake wa siasa za kimataifa hasa kutokana na wadhifa alionao sasa,Balls ana sapoti kubwa kwenye vyama vya wafanyakazi ambavyo kimsingi vina nguvu ya kutosha kwenye chama cha Labour.Kadhalika,wakati David anaonekana kama mtu wa 'tabaka la juu' Balls yuko karibu zaidi na wana-Labour wa ngazi za chini.
Tukiweka kando kidogo matatizo yaliyo ndani ya Labour kwa sasa,huko kwa wahafidhina nako mambo si shwari sana.Kuna wanaomuona mgombea wa chama hicho,David Cameron, kama amewaangushwa kwa kushindwa kwake kupata ushindi wa jumla (overall majority).Upinzani wa chini chini dhidi ya Camron haukuanza kwenye uchaguzi huu tu bali tangu alipoweka bayana dhamira yake ya kukibadilisha chama cha Conservative kutoka mwonekano wake kama 'chama kibaya' (nasty party) kwenda chama chenye kujumuisha makundi mbalimbali katika jamii.Kabla ya harakati za Cameron,chama hicho kimekuwa kikitafsiriwa kama 'cha Waingereza Weupe wa tabaka la juu' na kinachokumbatia zaidi mabwanyenye kuliko watu wa kawaida.
Cameron amefanikiwa kwa kiasi flani kubadili taswira hiyo japo si sana.Katika uchaguzi uliopita alihamasisha uteuzi wa baadhi ya wagombea kutoka makundi ambayo kimsingi 'hayamo kwenye akili za chama hicho' kwa mfano wagombea kutoka jamii ndogo za wasio weupe (ethnic minority),shoga na mabinti kadhaa.Japo baadhi ya wagombea hao wameshinda,wengi wao wamefanya vibaya na tayari baadhi ya wahafidhina wanamlaumu Cameron kwa uamuzi huo wa 'kuwapigia debe wageni wa tamaduni za chama hicho'.
Jingine linalomwandama Cameron ni mchango wa kundi dogo la washauri wake wanaofahamika kama 'wana-Eton wa zamani' (ex-Etonian),yaani marafiki zake wa karibu aliosoma nao katika shule ya Eton yenye hadhi ya juu kabisa na chaguo la 'wateule wachache' kwa hapa.Hao ni pamoja na Kansela ('waziri wa fedha') kivuli George Osborne na mwanamikakati anayesifika kwa akili nyingi Oliver Letwin (ambaye pia ni 'waziri' kivuli).Wengine wanaotuhumiwa 'kumshika akili' Cameron ni pamoja na kiongozi wa zamani wa Conservative,William Hague,na Mkurugenzi wa Mawasiliano,Andy Coulson (ambaye kabla ya kuchukua wadhifa huo alikuwa mhariri wa gazeti maarufu kwa udaku la News of The World).Coulson anafahamika kwa uwezo wake katika 'kutengeneza fitna,majungu na kummaliza mtu' (maeneo yanayolipa umaarufu News of the World).
Washauri hao wa Cameron wanatuhumiwa 'kumshauri vibaya' mgombea hasa katika wazo la 'jamii kubwa' (Big Society) ambalo inaelezwa kuwa liliasisiwa na Letwin.Wakosoaji wanadai kuwa wazo hilo halikueleweka kwa wapiga kura na wengine wanakwenda mbali zaidi na kulieleza kama 'wazo muflisi'.Vilevile,inaelezwa kuwa Lord Ashcroft,'kibopa' aliyemwaga fedha nyingi kwa minajili ya Conservative kushinda uchaguzi huo,hajaridhishwa na matokeo ya uchaguzi huo,sambamba na 'kushindwa' kwa Cameron kusimama kidete kumtetea mhafidhina huyo tajiri (Ashcroft) alipoandamwa na skandali ya 'hadhi ya raia asiyelipa kodi kutokana na ukazi wake nje ya nchi' (non-domicile status).Lord Ashcroft anaamini kuwa suala hilo limechangia kupunguza kura za chama chao na anaamini kuwa Cameron angeweza kumtetea vizuri zaidi ya alivyofanya.Kadhalika,tajiri huyo anadaiwa kutopendezwa na wazo la Cameron kushiriki midahalo ya uchaguzi kwenye runinga,ambapo anaona kuwa ilisaidia kumuimarisha mgombea wa chama cha Waliberali (Liberal Democrats) Nick Clegg na hivyo 'kula' kura za Conservatives.
Nitaendelea kuwahabarisha kinachojiri kwenye anga za siasa za hapa kadri muda utavyoruhusu.
Matokeo ya Uchaguzi Mkuu hapa Uingereza yametuacha baadhi yetu tukiwa na majonzi baada ya chama tawala cha Labour kuambulia nafasi ya pili (viti 258) huku chama cha wahafidhina (Conservatives) waikibuka mshindi kwa kupata viti 307 (japo ni pungufu ya viti 19 kwa viti 326 vinavyohitajika kuunda serikali ya peke yao).Chama cha kiliberali (Liberal Democrats) kimeshika nafasi ya tatu kwa kuambulia viti 57.
Kila mwenye majonzi kutokana na matokeo mabaya kwa Labour ana sababu zake binafsi.Zangu ni za kibinafsi zaidi (na mambo binafsi yanapaswa kubaki binafsi).Lililo bayana ni kwamba Labour haikushindwa kwa vile ni chama kibaya au kimeboronga wakati wa utawala wake.Hapana.Tofauti kati ya hawa wenzetu na akina sie na CCM yetu ni kwamba haitoshi kuwa umefanya vizuri tu bali watu wanataka vizuri zaidi kama sio vizuri kabisa.Bahati mbaya kwa Labour ni mtikisiko wa uchumi wa dunia ambao kama ulivyoathiri sehemu nyingine ulimwenguni,umepelekea idadi kubwa tu ya Waingereza wakiwa hawana ajira sambamba na ugumu wa wastani wa hali ya maisha.Kwa lugha nyingine,hali hiyo ya uchumi (ambayo kimsingi haikusababishwa na Labour) imechangia chama hicho kuangushwa na wahafidhina.
Hadi dakika hii haijafahamika nani atakuwa Waziri Mkuu kutokana na kanuni na taratibu za uchaguzi za hapa.Tofauti na huko nyumbani ambapo wingi wa kura unatafsiri ushindi wa moja kwa moja kwa chama husika,kwa hapa ili chama kiweze kuunda serikali kinapaswa kushinda viti 326.
Nitachambua zaidi baadaye kuhusu uchaguzi huu na namna Watanzania wanavyopaswa kujifunza kwa ajili ya uchaguzi wetu hapo Oktoba mwaka huu.Ila kuna habari ya 'kuliwaza' inayokihusu chama cha kibaguzi cha BRITISH NATIONAL PARTY (BNP) ambapo mwenyekiti wake Nick Griffin ameshindwa kumuangusha mgombea wa Labour,Margaret Hodge, katika eneo la Barking lililopo mashariki mwa jiji la London.
Habari njema zaidi ni kwamba BNP imepoteza viti vyote 12 ilivyokuwa inashikilia kwenye manispaa ya Barking and Dagenham jijini London.Pengine hili linaweza kutafsiriwa kama tamko la Waingereza dhidi ya siasa za kibaguzi.BNP ilitumia suala la uhamiaji kama ajenda yake kuu kwenye uchaguzi huo lakini ni dhahiri kuwa matokeo hayo yatafikisha ujumbe kwao kuwa watu wenye akili timamu hawaafikiani na ushenzi wa wabaguzi hao.
Mengi,baadaye.Kwa sasa tusubiri matokeo ya majadiliano ya simu katika ya mgombea wa wahafidhina,David Cameron na kiongozi wa waliberali Nick Clegg yanayotarajiwa baadaye leo kuangalia uwezekano wa ushirikianio kati ya vyama hivyo.Wakiafikiana,Cameron atafanikiwa kuwa Waziri Mkuu.Lakini kama Clegg ataamua kushirikiana na Labour basi Gordon Brown ataendelea kushikilia wadhifa wake.
Leo ni siku ya uchaguzi mkuu hapa Uingereza.Vituo vya kupiga kura vilifunguliwa mapema asubuhi na inatarajiwa kuwa matokeo ya uchaguzi huo yatakuwa ya 'kukabana koo' kati ya vyama vikuu vya Labour,Conservative na Liberal Democrats.Hadi usiku wa jana,kura za maoni zilikuwa zikionyesha kwamba chama cha Conservative kingevuna viti vingi lakini visivyotosha kuunda serikali ZAIDI SOMA HAPA.
Je una ndoto za kupata shahada ya juu?Basi jaribu shahada ya uzamifu (doctorate) ya ndoto,jambo linalotarajiwa kuwa halisi nchini Saudi Arabia.
Yusuph al-Harthy,Msaudia mahiri katika kutafsiri ndoto,ana mpango wa kuanzisha taasisi ya kitaaluma itakayotoa shahada ya kwanza na ya uzalimi,na hata shahada ya uzamifu (PhD) katika ndoto na maono,kwa mujibu wa gazeti la Al-Hayat.
"Kutafsiri ndoto ni kwa asili yake ni njia ya kutoa ushauri nasaha,alisema Harthy ambaye anaendesha tovuti ya kufundisha namna ya kukokotoa maana ya ndoto.Taasisi anayotarajia kuanzisha kitashirikiana na chuo kikuu kimoja cha Uarabuni ambacho bado hakijatajwa.
Dini ya Kiislam ina historia ndefu ya kutafsiri ndoto,huku mwananzuoni wa aliyezaliwa karne ya 7,Muhammad Ibn Sirin,mwenyeji wa Basra katika Iraki ya leo,akitambulika kwa mchango wake wa kuhariri daftari (catalogue) za tafsiri za ndoto.
Harthy,ambaye hujadili ndoto kwenye vituo vya radio na shoo za runinga,haafikiani na mtizamo wa Wizara ya Saudia inayoshughulikia masuala ya Uislamu kwamba tafsiri ya ndoto sio sayansi inayoweza kufundishwa bali ni jambo linalotokana na hamasa (inspiration).
Tue, 04/05/2010 - 20:00
by Anthony Wells
Our latest daily polling figures for The Sun (fieldwork 3rd - 4th May; sample size 1,461) are:
Conservative 35%
Labour 30%
Liberal Democrat 24%
Others 11%
Marc-Anotine Fortune, outjumps Steven Smith to head Celtic in front
Rangers' Maurice Edu is felled by Celtic's Andreas Hinkel
The airspace over Scotland and Ireland was closed last night because of an ash cloud in the atmosphere. Some ascribed that to the outpourings of a certain Icelandic volcano.
Those present in the east end of Glasgow on Tuesday night know better. It came from the dying embers of the Scottish season as they flared into life with the final Old Firm derby of the campaign.
This collision incorporated enough oddities for a lively quiz, although not Mastermind. The two goalkeepers who started did not finish, Allan McGregor departing the scene after only five minutes with a medial ligament injury and Artur Boruc leaving seven minutes after the break nursing two broken fingers.
David Weir, the Rangers captain, having won the first accolades of his career at the age of 40, capped an eventful passage by colliding with McGregor at the incident which saw the keeper stretchered off. After a lengthy stoppage, play resumed with a free kick awarded to Celtic for a foul committed by Kevin Thomson on Aiden McGeady.
The script called for Lee Naylor to test Neil Alexander with some form of direct effort from 25 yards, but the twist in the plot was that the Celtic full back kept his kick low and the Rangers defenders jumped, creating the gap through which the ball sped past McGregor's replacement, helped on by a deflection off the most unfortunate Weir.
Celtic Park erupted as it has rarely done in this dismal season for the club and the players responded by controlling proceedings with a passion and guile that has also been largely absent.
Neither Celtic nor Rangers, of course, can be sure who will be in charge of them when the new season opens, but the word on the pavement has been that Neil Lennon would emerge as prime contender to raise his status from caretaker manager if he could emerge from this fixture with the Parkhead side's first derby victory of the campaign.However, just when he was entitled to believe that his men would usher their narrow lead into the interval, the contest flipped.
In another peculiarity of the evening, each side fielded a makeshift centre back. Rangers had withdrawn Lee McCulloch from midfield to make up for the absences of Madjid Bougherra and Danny Wilson, the usual partners for Weir at the heart of the Ibrox back line. Celtic, meanwhile, had drafted Mark Wilson to cover for Josh Thompson, who made up the numbers on the bench.
It was Celtic's sticking plaster that peeled off first as Steven Whittaker made ground on the right to hang a cross into the box, where Kenny Miller beat Wilson to the jump for a glanced header between Boruc and his right hand post.
The Rangers forward then tempted fate and a caution – although he escaped censure from the referee – by making towards the Celtic support while kissing his badge – but it was the home support who savoured the last laugh within seconds as their team restored its lead with an identical strike.
In this case the overlapping full back was Naylor, the man on the end of the cross was Marc Antoine Fortune and the full back asked but unable to do a centre half's job was Steven Smith. Half time was enlivened by a repeated announcement declaring that an emergency had arisen within the stadium and instructing spectators to leave the stadium in an orderly fashion.
Having spent much of the season staying away from the place because of disdain at the fare on offer, the Celtic fans responded loudly that they had no intention of heading for the exits when their team had reached such a propitious juncture, thus providing proof that Bill Shankly might have been on the mark when he uttered his famous dictum about football and life and death.
Honour was eventually satisfied, the imbroglio calmed down and Celtic were able to celebrate their first triumph over Rangers in 15 months. Enough to earn Lennon the job? That's another tale for another time.
Wiki moja baada ya kusherehekea mwaka wake wa 115 tangu azaliwe,binadamu mwenye umri mkubwa zaidi duniani amefariki katika kisiwa cha kaskazini mwa Japan cha Okinawa.Kama Chinen alizaliwa tarehe 10 ya mwezi Mei mwaka 1895 na kubahatika kushuhudia karne tatu tofauti,kwa mujibu wa wa taasisi ya utafiti wa vipengele (aspects) vya kijamii,saikolojia na baiolojia vya ukuaji wa binadamu (Gerontology Research Group)
Kikongwe huyo alifariki Jumapili iliyopita kwenye nyumba ya kutunza wazee/wagonjwa (care home)japokuwa taarifa za kifo chake hazijatolewa kwa nduguze ambao wamekuwa wakilinda faragha ya bibi hiyo kwa makini.
Kisiwa cha Okinawa kina sifa ya kuwa na wakazi wenye maisha marefu hali inayohusishwa na mlo wa asili wa mchaichai (green tea),supu ya 'miso',mbogamboga,wali na samaki.
Kama ameshikilia rekodi ya umri mkubwa duniani tangu mwezi Sptemba mwaka jana,baada ya kikongwe Gertrude Baines kufariki akiwa na umri wa miaka 115 huko Los Angeles nchini Marekani.Baada ya kifo cha Kama,rekodi yake sasa inabaki kwa bibi wa Kifaransa,Eugenie Blanchard,aliyezaliwa mwezi Februari mwaka 1896.Mwingereza Florence Emily Baldwin,wa Leeds,anashikilia nafasi ya pili akiwa na umri wa miaka 114 pia.Japo bibi huyo anasema kuwa kula sandiwichi ya mayai (egg sandwich)ndio siri ya kuishi kwake miaka yote hiyo,wataalam wanahisi maisha yasiyohusisha uvutaji sigara,unywaji pombe na kufanya kazi kwa bidii kumechangia zaidi.
Americans worry that illegal immigrants are putting a strain on schools, hospitals and the depressed job market but still are sympathetic to their plight.
Eight in 10 Americans, 84%, are very or somewhat concerned that illegal immigrants are burdening government services, and 77% worry that they are driving down wages, a USA TODAY/Gallup Poll finds.
Yet 77% are concerned that stricter immigration laws would mean illegal immigrants and their families who have lived productively in the United States for years would be forced to leave
"People seem to be more concerned about that than the hypothetical things like civil rights," Gallup pollster Jeffrey Jones said.
The seemingly contradictory sentiments reflect the difficulty in grappling with the immigration issue, said Tomas Jimenez, a fellow at the New America Foundation think tank and a sociology professor at Stanford University.
"On the one hand, they don't like the idea that people are breaking our immigration laws, that it appears we have a Southern border that is out of control," Jimenez said. "On the other hand, they think the people coming here who work hard, who have dreams of a better life, are really participating in an American tradition that is as old as this country."
The poll of 1,049 adults Saturday and Sunday has a margin of error of +/- 4 percentage points.
Waziri Mkuu wa Australia,Kevin Rudd,amekuwa akifuatilia tovuti za ngono (porn sites),kwa mujibu wa kituo cha runinga cha Sky.
Rudd,hata hivyo,amekuwa 'mfuatiliaji' wa tovuti hizo kutokana na mapungufu katika nyenzo za usalama/udhibiti (setting) katika akaunti yake ya Twitter.Kutokana na mapungufu hayo,kiongozi huyo amekuwa akifuatilia watu kama bloga wa mambo ya ngono,duka linalouza bidhaa za ngono,mwanamama aliye kifua wazi huku amjifunga pingu,na kadhalika.
Msemaji wa Waziri Mkuu ameeleza kuwa tatizo hilo lilitokana na akaunti ya Twitter ya Rudd kufuata wale wote wanaomfuata (auto-follow those who follow him)."Japo Waziri Mkuu anajitahidi kutoa majibu kwa wale wanaosema chochote kwake,kazi hiyo ni ngumu ukizingatia idadi ya watu ni 900,000", alieleza msemaji huyo.
Japo inamhitaji mtumiaji wa Twitter kuangalia kwanza wasifu wa mtu anayeomba kukufuata,kuna kipengele kinachoiwezesha akaunti imkubali moja kwa moja mtu anayeomba kumfuata pasipo haja ya mwenye akaunti kufanya hivyo.Uwezo huo unaonekana kuwa muhimu kwa watumiaji wa Twitter wenye wafuasi (followers) wengi.Katika akaunti yake KevinRuddPM,Waziri Mkuu huyo ni mfuasi wa wana-twitter wengine 200,000.
Wataalam wa teknolojia wanatahadharisha kuwa nyenzo za habari kwa jamii (social media)zinaweza kuhatarisha usalama wa mtuamiaji kama hataokuwa makini."Kuna imani kwamba kwenye vitu kama Twitter unaweza tu kufungua akaunti na mambo yakaenda mwanana",anasema Handsley,makamu mwenyekiti wa kampuni ya Young Media Australia."Tunapaswa kufahamu kwa undani kuhusu usalama wa chanzo husika cha habari kwa jamii kabla ya kuamua kukitumia",aliongeza alipoongea na gazeti la Herald Sun.
Kwa mujibu wa gazeti hilo,baadhi ya wengine 'waliofuatiliwa' na Waziri Mkuu Rudd ni pamoja na tovuti ya kamera-mtandao (webcams) za ngono na mmiliki wa kiota cha watenda ngono wa jinsia moja (gay resort) cha Phuket,Thailand.
Rudd amekuwa mtumiaji mzuri wa teknolojia ya habari huku nyakati nyingine akitumia nyenzo kama Twitter kubainisha sera zake.
Message from JESTINA: I will be hosting a brand new talk show ALL ABOUT WOMEN.It explores issues and the progress made by women of Black origin who work and live in and outside London. The show is presented by Jestina George and Kayisha.On this show, the girls talk about everything from fashion to music and general gossip. The show will start showing on Sky Channel 184 BEN TV every monday 10:30 PM. The first show goes out on Monday the 3rd of May 2010. Also the show can be watched on AILTV just log on http://www.ailtv.com or you can purchase a set top box and watch the show and many other programs on a normal television set. For more info Please contact us [email protected] or call us on 07595040952
Raia mmoja wa India amegusa hisia za jeshi la nchi hiyo kutokana na madai yake kwamba haitaji chakula wala maji kumudu kuishi.Prahlad Jani anadai yeye ni 'breatharia',yaani mtu anayeweza kuishi kwa kutumia nguvu za asili za kiimani.Anadai anapata nguvu hizo za asili kutoka kwa 'mungu wa kike' anayemmwagia kimiminika (elixir)cha miujiza katika paa la chini la mdomo wake (palate),kwa mujibu wa gazeti la Telegraph la London.
Wakati baadhi ya watu wanamwona kama 'mzushi' flani,taasisi ya maendeleo ya utafiti wa ulinzi inasema Prahlad anaweza kutoa mwangaza katika kuwasaidia wanajeshi kumudu kukaa muda mrefu bila kula,au hata wahanga wa majanga mbalimbali.Hadi sasa amekaa siku sita bila kula au kunywa chochote katika hospitali iliyopo Hyderabad,na madaktari wanasema haonyeshi dalili yoyote ya kuathiriwa na njaa.
"Ikithibitika kuwa madai yakni sahihi,basi itakuwa hatua kubwa sana kwenye sayansi ya tiba",anasema Dkt G.Ilavazhagan,Mkurugenzi wa Taasisi ya Ulinzi ya Fiziolojia na Stadi Shiriki."Itatuwezesha kuokoa maisha ya wanadamu katika nyakati za majanga,kimo cha juu,safari za majini,na mazingira mengine magumu ya kibinadamu na ya asili.Tutaweza kuwaelimisha watu kuhusu namna ya kustahimili (surviving) mazingira magumu pasipo chakula na maji au chochote kile".
Madaktari wataendelea kumchunguza kwa siku 15 kipindi ambacho wanataraji kuona misuli yake ikisinyaa,upungufu mkubwa wa maji mwilini,kupungua uzito wa mwili na baadhi ya viungo vya mwili kushindwa kufanya kazi.
Binadamu wengi hawawezi kustahimili zaidi ya siku 3 hadi 5 pasipo kunywa maji.
Imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily News la India.
NEWSWEEK: Black blogs cover a far more diverse range of stories than the rest of the media. Just ask Sandra Bullock. While Sandra Bullock's post-Oscar split from husband Jesse James may be the biggest celebrity news in the last month (or two), it's probably not surprising it's the adopted brown baby that really got the African-American blog sites going. The funny thing is, black Web sites such as MediaTakeOut.com, Bossip, and Young, Black and Fabulous have been following Bullock for years. Part of the reason is her connection to the black community. "They know about her support for victims of Katrina and Haiti so they care about what happens to her, which we thought about when we gave her coverage," says Fred Mwangaguhunga, owner of the black entertainment site MediaTakeOut.com. But part of it is that black blogs look at the world differently than the often segregated mainstream.
The US Army says that it is it is wasting far too much time preparing Powerpoint presentations and not enough time killing people.
For a while now the Army has been concerned that its officers are missing entire wars preparing Powerpoint slides and making presentations.
. TechEye has got its paws on the sort of slide they mean (see above).
Last summer Gen Stanley McChrystal, the leader of US and Nato forces in Afghanistan, said when we understand that slide that “we’ll have won the war’.
Gen James Mattis of the Marine Corps, said: "Powerpoint makes us stupid". The Marines are not renowned for being that bright in the first place, which makes them some of the US's best soldiers, but Powerpoint sucks about the direction you want to point them.
Sam Nuxoll, a platoon leader in Iraq, seems to have shaken the Pentagon with a quote that said he was spending most of the war making Powerpoint slides. Instead of spending his time dodging bullets, he was making bullet points.
What is the problem is the fact that rather than encouraging making decisions PowerPoint sucks up the time of junior officers. The idea is that they can get crappy decisions blessed if it looks good in Powerpoint. However really good tactics which are dull on screen are being mothballed.
This has been noticed in business too with some companies thinking that Powerpoint presentations are a waste of time too.
JIJI la Tanga limfeunikwa na simamzi kuu kufatia wanafunzi 18 wa Chuo cha Kiislamu cha Shamsil-Maariff kufa papo hapo na wengine 125 kujeruhiwa vibaya, baada ya lori walilokuwa wakisafiria kutoka kwenye sherehe za maulidi kupinduka.
. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Adolphina Kapufi aliliambia gazeti hli jana kuwa ajali hiyo ilitokea saa 5:30 usiku wa kuamkia jana katika eneo la njiapanda kuu ya Mabanda ya Papa jijini hapa.
Kapufi aliwataja baadhi ya waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Twalib Kunemu, Juma Idd, Faraji Habib, Jahshi Rashid, Hussein Bakari, Hajji Athumani naYussuph Hussein na kwamba, kazi ya kuwatambua maiti wengine bado inaendelea.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Paschal Kanyinyi alisema kazi ya kuwatambua waliokufa na majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo wodi ya Galanosi inaendelea.
Kanyinyi aliwataja majeruhi waliotambuliwa kuwa ni Jumaa Salim ambaye ameumia mbavu, Makame Ahmed, Ahmed Shehe, Selemani Said na Juma Akida.
Aliwataja majeruhi ambao hali zao ni mbaya, hivyo waliokimbizwa katika Hospitali Taifa ya Muhimbili, jijini Dar essalaam kuwa ni Hemed Shaaban na Hassan Adam.
Kanyinyi alifahamisha kuwa kati majeruhi 125 walifikishwa katika hospitali hiyo usiku wa kuamkia jana baada ya kupata ajali, 70 walipata matibabu na kuruhusiwa kurejea chuoni kwao.
Kwa mujibu wa Kaimu Mganga Mkuu huyo, majeruhi 55 wanaendelea kupata matibabu katika hospitali hiyo kwa msaada wa timu maalumu ya waganga na wauguzi waliokusanywa kutoka hospitali na vituo mbalimbali vya afya mkoani Tanga kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.
Mwananchi ilifika katika Hospitali hiyo ya Bombo na kukuta idadi kubwa ya wananchi waliokusanyika katika hospitali hiyo kwa lengo la kutambua miili ya waliokufa na majeruhi.
Mwalimu wa zamu wa Chuo hicho, Ustaadh Ajali Ramadhan, alisema kuwa wanafunzi hao walikuwa wakitokea Kijiji cha Kibafuta ambako walikwenda
kuhudhuria sherehe za kuzaliwa kwa Mtume Mohamad S.A.W.
Hata hivyo, Ustaadhi Ramadhan alisema anashangaa kuona idadi kubwa ya wanafunzi waliopata ajali, kwani aliowaruhusu kutoka chuoni hapo walikuwa 60 tu.
“Nashangaa sijui ni nini kimetokea, kwani niliowaruhusu kuondoka na gari
hilo ni wanachuo 60 tu, lakini idadi ya waliopata ajali imekuwa kubwa. Sijui walipandia wapi…,” alisema mwalimu huyo wa zamu.
Kanyinyi alimshukuru Mkurugenzi wa Kampuni ya Raha Leo, Seleman Abdallah kwa kutoa dawa kwa ajili ya kuwatibu majeruhi wa ajali hiyo.
“Tunashukuru Mkurugenzi wa Raha leo, ametusaidia sana kwa kutoa dawa za
kuwatibu majeruhi na pia vifaa kwa ajili ya kusaidia kuhifadhia miili ya waliokufa,” alisema Kanyinyi.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Mstaafu Said Kalembo alifika hospitalini hapo saa 5 .30 asubuhi na kuwapa pole ndugu wa wanafunzi waliokufa katika ajali hiyo.
Akiwa, akiwa katika wodi ya Galanosi Mkuu wa Mkoa huyo alimuagiza Kaimu Mganga Mkuu kuwaita waganga na wauguzi kutoka vituo vyote vya afya vya jijini hapa ili kuongeza nguvu, kwa vile waliopo katika Hospitali ya Bombo walikuwa wmezidiwa na kazi ya kuwahudumia majeruhi.
Katibu wa Bakwata wa Mkoa wa Tanga, Mohamed Riami alisema huo ni msiba
mkubwa uliwakumba Waislamu na Watanzania kwa ujumla, hivyo akaomba msaada wa hali na mali kuokoa maisha ya majeruhi waliopata ajali hiyo.
Ajali hii ni muendelezo wa ajali mbaya za barabarani zinazoendelea kutokea na kuua watu sehemu mbalimbali nchini hivi sasa.
Moja ya ajali hizo mbaya ni iliyotokea jijini Dar es Salaam mwezi uliopita na kuua watu zaidi ya 10 papo hapo baada ya lori la mafuta ya taa kuigonga na kulalia daladala maneo ya Kibamba katika Barabara ya Morogoro.
Katika ajali hiyo iliyotokea alfajiri, daladala ilisagawa na kuwa kama chapati; na miongoni mwa waliokufa ni mama mjazito aliyekuwa anakwenda kujifungua hospitalini akiwa pamoja na mumewe.
British National Party (BNP),chama cha kibaguzi cha hapa Uingereza,kimetangaza kwamba kitatoa paundi 50,000 kwa kila atakayeafiki kuhama Uingereza.Akiongea katika kipindi cha 'Today' cha kituo cha redio cha BBC4,mwenyekiti wa chama hicho,Nick Griffin (pichani) alisema kuwa mpango huo ni mahsusi kwa Waingereza wasio Weupe (non-White British) na wahamiaji wengine wasio weupe (non-White migrants).
Griffin alieleza kuwa kwa mujibu wa sera ya uhamiaji ya chama chake 'milango ya Uingereza itafungwa' kwa wageni isipokuwa tu kwa wale wenye ujuzi au taaluma maalum."Aidha unazungumzia fundi bomba wa ki-Polish au mkimbizi kutoka Afghanistan,milango ya Uingereza itafungwa kwa sababu nchi hii imejaa",aliongeza kiongozi huyo mbaguzi wa rangi.
Kiongozi huyo wa BNP alitanabaisha kuwa "Idadi ya watakaozuiwa kuingia nchi hii itakuwa yoyote na kutoka popote.Milango itafunguliwa tu pale itapokidhi mahitaji wa Waingereza na Uingereza".Akitolea mfano wa utekelezaji wa sera hiyo,Griffin alisema laiti Uingereza ikiwa na mahitaji ya wataalam wa nyukia basi chama hicho kitaruhusu,kwa mfano,mwanafikizia kutoka Japan.
Alipoulizwa kama sera hiyo itaambatana na kuvunja mikataba ya kimataifa,mbaguzi huyo alijibu: "Kabisa.Mikataba ya kimataifa haikidhi mahitaji ya Uingereza na watu wake.U-kimataifa (internationalism) ni miradi ya tabaka la wanasiasa".
Kuhusu kuwataka wasio weupe kuondoka Uingereza,Griffin alisema:"Tunasema tutatoa posho ya kuhama makazi (resettlement grants) na hili ni suala la hiari .Tunazungumzia takriban pauni 50,000 kwa kwa mtu".Alipoulizwa ni watu wangapi wanaotarajiwa kuhama Uingereza kwa mujibu wa sera hiyo alisema: "180,000 kwa mwaka,kama wataondoka katika nchi hii iliyojaa kupindukia".
Judges are set to rule whether to remove the story of the intrepid explorer's first African adventure after a Congolese man claimed it is racist.
. Bienvenu Mbutu Mondondo wants Tintin in the Congo - the second in the celebrated children's series - to be axed for its ignorant depiction of native Africans.
China has revoked a ban on people with HIV/AIDS entering the country, softening a decades-old policy that drew sharp criticism this year when an Australian writer was blocked after declaring himself HIV-positive. Until now, China's regulations formally banned foreigners entering the country with "psychiatric illness, leprosy, AIDS, sexually-transmitted diseases, active pulmonary tuberculosis or other infectious diseases."
The State Council, China's cabinet, issued amended rules late Tuesday removing the explicit ban on people who have developed AIDS or are infected with the HIV retrovirus, as well as anyone with leprosy, while leaving authorities leeway to decide which diseases could trigger an entry ban.
The United Nations welcomed the decision as an important step towards ending discrimination against people living with HIV.
"I commend President Hu Jintao for China's decision to remove travel restrictions based on HIV status," U.N. Secretary-General Ban Ki-moon said in a statement.
"Punitive policies and practices only hamper the global AIDS response. I urge all other countries with such restrictions to remove them as a matter of priority and urgency."
Travel restrictions, which are imposed in some form by dozens of countries worldwide, do not prevent transmission of the disease or protect public health, the statement added.
China's new rules, posted on the central government website (www.gov.cn), still block foreigners "with serious psychiatric illness, infectious pulmonary tuberculosis or other infectious diseases that may constitute a major threat to public health."
The amended regulations did not say whether AIDS/HIV would be among the infectious diseases that people seeking Chinese visas must declare when applying, possibly leaving officials some leeway on how to apply the rule.
But an unnamed legal affairs official for the State Council indicated that AIDS/HIV would not be a bar to entry.
"Restricting foreigners with these diseases from entering the country has played an extremely limited role in our country's disease prevention and control work, and instead has repeatedly become an impediment to our hosting a variety of international events," the official told the Legal Daily.
In March, more than 90 Australian authors signed a letter decrying China's refusal to grant a visa to one of the country's most celebrated writers, Robert Dessaix, who is HIV-positive.
Friday, Shanghai opens its World Expo, a multi-billion dollar exhibition that is China's latest effort to promote an image as a forward-looking and open country.
The HIV virus can be spread through unprotected sex, sharing of infected needles and blood, and -- without preventive drugs -- to children in the womb of infected mothers or who take milk from an infected woman.
If untreated, the virus attacks the immune system, leading to full-blown AIDS, a deadly condition.
China has 560,000 to 920,000 people infected with the HIV virus and 97,000 to 112,000 AIDS patients, according to 2009 Ministry of Health and United Nations estimates.
Matokeo ya utafiti uliofanywa na Mradi wa Utafiti na Elimu na Demokrasia Tanzania (REDET) yanaonyesha kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ni mchapakazi zaidi ya 'bosi' zake,Rais Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Ali Mohammed Shein. Kwa mujibu wa habari zilizochapishwa katika gazeti la Mwananchi,asilimia 61.2 ya wananchi waliohojiwa wameonyesha kuridhishwa na utendaji wa Pinda huku Kikwete akipata asilimia 58.8 na Dkt Shein akiwa na asilimia 46.8Kwa habari kamili soma HAPA.
Tarehe 6 ya mwezi ujao,Waingereza watapiga kura katika Uchaguzi Mkuu.Kura za maoni zinaonyesha kuwa hakuna chama kitakachopata ushindi wa kutosha kuunda serikali peke yake (hung parliament).Vyovyote itakavyokuwa,kuna mambo kadhaa mbayo Watanzania wanaweza kujifunza katika uchaguzi huu hasa kwa vile nasi tutakuwa na uchaguzi hapo Oktoba mwaka huu.
Kubwa zaidi ni namna wagombea wanavyohangaika kuwabembeleza wapiga kura.Unajua kuna kijitabia cha baadhi ya wanasiasa huko nyumbani ambao sijui ni ulevi wa madaraka au dharau kwa wapiga kura,hawajihangaishi hata kidogo kuwaonyesha wapiga kura kuwa ajira zao zinategemea ridhaa za wapiga kura hao.Pengine ni jeuri ya uwezo wao wa kununua kura katika jina la takrima au kudumisha chama.
Yani hapa ukiangalia kwenye runinga namna Waziri Mkuu wa sasa,Gordon Brown,anavyopelekeshwa na wapiga kura kwa maswali mazito kana kwamba utawala wake ulikuwa mbovu kupindukia,unapata picha kuwa kwa hawa wenzetu GOOD IS NOT ENOUGH,THEY WANT EVEN BETTER (Ubora tu hautoshi,wanataka ubora zaidi).Na si kwamba Brown na Labour yake hawajafanya mambo ya maana kwa Waingereza bali watu hawa hawapendi 'kuangushwa' kwa aina yoyote ile.
Na jingine linalovutia katika kampeni hizi ni namna wapiga kura wanavyozipa manifesto za vyama umuhimu mkubwa na pengine mwelekeo wa nani watampigia kura.Kwetu,manifesto ni sawa na waraka unaokumbukwa wakati wa chaguzi na 'kinga' ya kujitetea pale mambo yanapokwenda mrama.Wengi tunafahamu namna akina Makamba wanavyotumia manifesto ya CCM kujibu shutuma mbalimbali zinazoelekezwa kwa chama hicho tawala.Hilo sio kosa bali tatizo ni kwamba utetezi huo mara nyingi hauendani na hali halisi.Kwa mfano haitoshi kusema manifesto ya CCM inatamka bayana kuhusu 'chuki' yake dhidi ya rushwa huku in practice hadi leo hatufahamu Kagoda ni mdudu gani.Matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno,so Waswahili say.
Manifesto ya CCM kwenye uchaguzi wa mwaka 2005 iliweka bayana dhamira yake ya kupata ufumbuzi wa suala la mahakama ya kadhi lakini hadi leo suala hilo linapigwa danadana.Utafiti wangu wa shahada ya uzamili kuhusu harakati za vikundi vya waislam nchini Tanzania (unaoelekea ukingoni) ambao umegusia kwa undani suala hilo unaashiria kuwa 'kupuuzia' kero (grievances) kama hiyo ya mahakama ya kadhi na suala la OIC yana potential ya kusababisha matatizo huko mbeleni.Tatizo haliwezi kutatuliwa kwa kuliepuka bali kulikabili.We have to solve difficulties before they become problems (tunapaswa kutatua ugumu kabla haujawa tatizo).
Ni matumaini ya wapiga kura wa Tanzania kuwa watatumia haki zao za kidemokrasia kwa busara zaidi kuchagua wagombea wanaoweza kuwatumikia kwa dhati.Zama za ushabiki wa vyama zimepitwa na wakati hasa kwa vile kitakachowakomboa Watanzania kutoka kwenye lindi la umaskini na ufisadi sio ushabiki bali ufanisi wa chama.
Ujumbe kutoka kwa Executive Producer Baraka Baraka (na video ya interview hapo chini)
Kwa mara nyingine tena ningependa kuwatolea Intavyu siku tuliyotembelea rasmi na world service radio katika studio zetu za Urban Pulse hapa Mjini kusoma UK tukiwa na Presenter Fred Ili kujadili Movie ya £ovely Gamble.
Pia aliweza kukutana na baadhi ya wanatimu wa lovely gamble na pia utapata comments za Steve Kanumba mwenyewe jinsi anaitwa siku hizi.
Pia unaweza kuangalia trailer ya movie inayosubiriwa kwa hamu sana Tanzania 28.4.10 club Billcanaz na hapa mji wa kusoma UK 29.5.10
BARAKA BARAKA
EXECUTIVE PRODUCER
BUZZIE PRODUCTION UK.
Kama nilivyoahidi siku chache zilizopita kuwa blogu yako ingekuletea mahojiano mengine exclusive kutoka kwa mmoja wa Watanzania wanaotuwakilisha vema,leo natimiza ahadi hiyo kwa kuwaletea exclusive interview na msanii mahiri wa Bongoflava,anayefahamika kama Mzee wa Commercial.Huyo si mwingine bali ni Ambwene Yesaya,au AY kama anavyofahamika na wengi.Kama ilivyokuwa katika mahojiano ya Mwana FA,interview hii itapatikana pia katika sura ya Kiingereza (English version).Tuaanza kwanza na WASIFU wa AY kabla ya kuingia kwenye mahojiano kamili.Pata vitu:
MSANII TANGU UTOTONI:
AY alianza kijihusisha na fani ya muziki tangu udogoni.Alipokuwa shule ya msingi alishiriki katika mashindano mbalimbali ya kutafuta vipaji na pia alitumbuiza katika hafla mbalimbali.Mwaka 1996 akiwa high school aliunda kundi la S.O.G lililojumisha wasanii watatu (akiwemo AY) na walirekodi albamu yao ya kwanza mwaka 2000.
KUKUA KISANII:
Mwaka mmoja baadaye,AY aliamua kufanya kazi za kisanii peke yake (solo) na kufyatua albamu yake ya kwanza iliyokwenda kwa jina ‘Raha Kamili’.Wimbo wa kwanza kutambulisha albamu hiyo, ‘Raha Tupu’ ulipata mafanikio makubwa na kukamata chati za vituo vya radio na runinga,na hatimaye kumtambulisha rasmi AY katika anga za muziki nchi Tanzania.
‘Machoni Kama Watu’, single ya pili (kutoka katika albamu ya ‘Raha Kamili’) iliyomshirikisha Lady Jaydee ilifanya vizuri sana kwenye chati mbalimbali za muziki na ulisaidia sana kupaisha mauzo ya albamu hiyo katika soko.
KUJIIMARISHA KISANII:
Mwaka 2005,AY alitoa albamu yake ya pili aliyoipa jina ‘Hisia Zangu’, na ‘Yule’, single ya kwanza kutoka katika albamu hiyo, ilikamata chati mbalimbali za muziki.Katika albamu hii,AY aliwashirikisha wasanii mbalimbali maarufu katika Afrika Mashariki ikiwa ni pamoja na Prezzo,Tattuu na Dexu Vultures (wote kutoka Kenya) na msanii Maurice Kirya kutoka Uganda.Hii ilisaidia sana kumtangaza zaidi AY nje ya mipaka ya Tanzania.Single yake ya pili, ‘Binadamu’,ilifanya vizuri sana ukanda mzima wa Afrika Mashariki na hatimaye kuteuliwa kugombea Tuzo za Kora,jambo lililoandika historia kwani AY ni msanii wa kwanza wa kiume kutoka Tanzania kuteuliwa kugombea Tuzo hiyo.
KUJIKITA ZAIDI KATIKA MUZIKI
Umaarufu wa AY ulizidi kuongezeka hasa baada ya kutoa albamu hiyo ya pili,na sasa alitambulika kama mmoja wa wasanii mahiri wa Afrika Mashariki.Mwaka 2006 alifanikiwa kupata mkataba wa kutangaza kinywaji (kikali) cha ‘Konyagi’ ambacho ni maarufu ndani na nje ya Tanzania.Mkataba huo ulichangia AY kutambulika zaidi kupitia matangazo ya kinyaji hicho,na ulifungua njia kwa makampuni mengine,kama Coca Cola,Vodacom,Celtel (sasa Tigo) na Kilimanjaro Lager kuingia mikataba na msanii huyo.
STAILI:
Staili ya muziki wa AY ni hip-hop inayozungumzia ishu na maisha ya Mwafrika hivi sasa.Maudhui hayo yanawasilishwa kwa ucheshi lakini pia yanaburudisha.Muziki wa AY unawagusa watu wa rika lote.
TUZO:
Msanii huyo amefanikiwa kuteuliwa katika/kushinda tuzo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania.Tuzo hizo ni pamoja na
1 Mwaka 2005 aliteuliwa kugombea Tuzo ya Kora katika kundi (category) ya Msanii Bora wa Kiume kwa Afrika Mashariki na Kati.Wimbo ulioteuliwa ni ‘Binadamu’.
2 Mwaka 2006 aliteuliwa kugombea Tuzo za Kisima (nchini Kenya) katika kundi la Msanii Bora wa Kiume kutoka Tanzania.
3 Mwaka 2007 aliteuliza kugombea Tuzo za Kilimanjaro (Kilimanjaro Music Awards) katika kundi la single bora ya hip-hop.
4 Mwaka huohuo aliteuliwa tena kugombea Tuzo za Kisima (nchini Kenya) katika kundi la video bora ya hip-hop kutoka Tanzania.
5 Mwaka 2007 uliendelea kuwa wa mafanikio kwa AY baada ya kuteuliwa pia kugombea Tuzo za Lulu ya Afrika (Pearl of Afrika) katika kundi la single bora ya hip-hop kutoka Tanzania.
6 Mwaka 2008 AY aliteuliwa kugombea Tuzo za Kilimanjaro katika kundi la collaboration (ushirikiano wa msanii zaidi ya mmoja) bora.
7 Mwaka huohuo,msanii huyo aliteuliwa tena kugombea Tuzo za Lulu ya Afrika katika kundi la msanii bora wa kiume kutoka Tanzania.
8 Katika mwaka huo,Akon-msanii maarufu duniani kutoka Marekani,alikiri hadharani kuwa anavutiwa na staili ya muziki wa AY na akamtabiria kuwa anaweza kabisa kuwa msanii kutoka Afrika atakayefanya vizuri katika anga za muziki kimataifa.
9 Mwaka huu,AY ameteuliwa kugombea tuzo kadhaa ikiwa ni pamoja na Tuzo za Muziki za Kilimanjaro (kundi la video bora na wimbo bora wa mahadhi ya Reggae),Tuzo za Teen Extra za nchini Kenya (kundi la video bora,msanii bora wa mwaka,collaboration bora ya Afrika,wimbo bora wa mwaka Afrika Mashariki,wimbo bora wa hip-hop, na msanii bora wa kiume).
10 Na hivi karibuni AY alishinda kuwa msanii bora wa Afrika Mashariki katika Tuzo za Teenez nchini Kenya.
MAFANIKIO:
Hadi sasa msanii huyo ameshajikusanyia Tuzo sita.Pia vibao vyake 14 vimefanikiwa kukamata chati mara katika ukanda wa Afrika Mashariki.Kibao chake kinachonyanyasa zaidi ni King and Queens (Wafalme na Malkia),na kimepelekea kumpatia tuzo na umaarufu zaidi kimataifa.Wakati mahojiano haya yanafanyika,wimbo wake ‘Habari Ndio Hiyo’ ulikuwa unakamata nafasi ya 10 katika chati za muziki kwa Afrika (Radio Express-Africa Chart).AY amefanikiwa kuwa msanii pekee wa Kitanzania aliyefanya collaboration nyingi zaidi na wasanii wa nje ya Tanzania ikiwa ni pamoja na Chameleone na Ngoni (Uganda),Amani,Nameless na Juacali (Kenya), P Square na J. Martini (Nigeria) na wengineo.
Uzinduzi wa albamu za AY umekuwa wa kihistoria na wenye mafanikio makubwa chini ya udhamini wa Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) na ulifanyika wakati wa matamasha ya wasanii wa kimataifa kama vile Fat Joe,Eve,Shaggy,nk nchini Tanzania.Kadhalika msanii huyo alikuwa miongoni mwa wasanii walioshiriki tamasha kubwa la kuhamasisha vita dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi (Music Against HIV/AIDS) liliodhaminiwa na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).Pia ameshiriki Coke Side of Life Tour kwa Afrika Mashariki,Tamasha la Vijana la Afro Arab nchini Uganda,Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar (Zanzibar International Film Festival),na Tamasha la Sauti za Busara.Kadhalika,AY amewahi kualikwa kutumbuiza wakimbiki kutoka Burundi na Rwanda kwa udhamini wa Shirika la Kimataifa la Wakimbizi (UNHCR),alitumbuiza katika sherehe za kuukaribisha mwenge wa Olimpiki nchini Tanzania,na mwaka jana alialikwa kutumbuiza katika Tuzo za Muziki za MTV barani Afrika nchini Kenya.Vilevile,msanii huyo ameshatumbuiza katika nchi mbalimbali duniani ikiwa ni pamoja na eneo la Afrika Mashariki,Rwanda,Burundi,Dubai,Afrika Kusini,Marekani na Uingereza.
NINI KIPYA?
Hivi karibuni AY amezindua tovuti yake inayopatikana katika anuani www.ay.co.tz. Pia single yake ya ‘Binadamu’ itakuwa miongoni mwa nyimbo katika albamu inayoandaliwa na kampuni ya kimaifa ya muziki,Warner Music (Africa).Kadhalika,msanii huyo ameingia mkataba wa kutangaza kinywaji (kikali) cha Waragi nchini Uganda sambamba na mkataba na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.Kwa sasa anandaa ushirikiano na wasanii wa kimataifa kama J. Martin wa Nigeria na wengineo kutoka Afrika Kusini na Marekani.
JE WAJUA?
Kwamba jina halisi la AY ni Ambwene Yesaya?
Staili ya AY ni ‘simple and casual’?
AY alizaliwa Julai 5 na nyota yake ni Kansa?
Rangi aipendayo zaidi ni bluu?
Scent (harufu ya perfume au manukato) aipendayo ni DKNY?
Na msanii anayemvutia zaidi duniani ni Dr Dre?.
MAHOJIANO KAMILI YANAFUATA (BONYEZA) HAPA CHINI . KULIKONI UGHAIBUNI (K.U): Kwanza blogu hii inatoa shukrani kwa kukubali ombi la kufanya mahojiano haya maalum. Pili, hongera sana kwa kuteuliwa na hatimaye kushinda Tuzo za Teneez Kenya 2010.Wasomaji wangependa kufahamu kwanini unajulikana kama Mzee wa Commercial
A.Y: Producer P.Funk ndio alianza kuniita hiyo baada kuwa kila nikienda Bongo Records alikuwa anaweka beats za aina tofauti na tukawa tunaflow na artists wengine so akaona kila beat naenda nayo na wengine walikuwa wanashindwa katika beats nyingine so akawa ananiita mzee wa commercial ila kwa sasa nimekuwa wa commercial ya muziki wa biashara na biashara kwa ujumla.
K.U: Laiti AY asingekuwa Mzee wa Commercial (yani usingekuwa msanii) unadhani leo angekuwa nani (katika fani gani)?
A.Y: nilikuwa na ndoto sana ya kusomea urubani na naamini ningeendelea nadhani ndoto yangu ingetimia coz nikiamua kufanya kitu naakikisha nimekifanikisha
K.U:Kitu gani kilichokusukuma kuingia kwenye fani ya muziki?
A.Y: kutokana na kusikiliza nyimbo za wasanii wengine wa nje na kuona mbona naweza kujitahidi nikafanya kama wao.
K.U: Kabla hatujagusia mafanikio yako kisanii ,nini hasa kimekuwezesha kubaki kwenye chati kwa kipindi kirefu kiasi hiki?
A.Y: bidii,nidhamu na malengo katika kazi,naipenda kazi yangu na najifunza kila siku na kukubali kuwa kila kitu kinaweza kubadilika
K.U: Tuje kwenye mafanikio yako kisanii.Licha ya kuweka historia kwa kuwa Mtanzania wa kwanza wa kiume kuteuliwa kugombea tuzo za Kora na baadaye tuzo za Kisima,kuna mafanikio gani mengine unayoyahusisha na fani ya muziki?
A.Y:Ni mengi. (Zaidi angalia wasifu hapo juu)
K.U: Miongoni mwa vilio vya wanamuziki wa Tanzania ni suala la ‘wadosi’.Kama msanii mwenye mafanikio makubwa umewezaje kupambana na suala hilo?
A.Y: hili nimeliongelea sana na sasa sihusiki nao kwa sasa naweza kusema ni tatizo sugu na linaweza kumalizika au kupungua ila naona wengi wenzangu wanaendelea kufanya biashara isiyo kuwa transparent
K.U: Nilidokezwa na Mwana FA kuhusu kampuni yako inayoshughulikia usimamizi na usambazaji wa muziki ijulikanayo kama Unity Entertainment.Wasomaji wangependa kufahamu japo kwa ufupi kuhusu wazo,maendeleo na ufanisi wa mradi huu.
A.Y:(angalia wasifu hapo juu) mpaka sasa kampuni yangu imekuwa na ni wakala wa wasanii wengi ukanda huu wa afrika mashariki kama mwana fa,shaa,nameless,j.martins wa nigeria ambae nimemleta kwenye new campaign ya zain,p.square,amani,chidi benz na wengine wengi wa afrika
K.U:Tuje kwenye ushiriki wako na hatimaye kujitoa kwenye kundi la East Coast Team.Sababu zipi zilipelekea wewe kujiengua?
A.Y: kutofautiana misimamo na malengo
K.U: Wakati ukiwa na kundi la East Coast kulikuwa na beef na wasanii wa Temeke.Je unadhani beefs zinasaidia au kudumaza maendeleo ya wasanii? (nauliza hivyo kwa sababu wakati mwingine baada ya kufifia kwa beef -kama hiyo yenu-baadhi ya wasanii nao wanafifia)
A.Y: zipo zinazojenga na zipo zinazobomoa
K.U: Je makundi (kama ilivyokuwa East Coast) yanaficha udhaifu wa wasanii dhaifu na kudumaza umahiri wa wasanii bora?(nauliza hivi kwa vile baadhi ya wana-East Coast ‘walipotea’ muda mfupi baada ya wewe na Mwana FA kujitenga):
A.Y: ni kweli kabisa,makundi mengi yakivunjika ndio mnapata ukweli kuwa nani anaweza na nani hawezi kujimanage
K.U: Unatambulika kama mwakilishi bora kabisa wa Tanzania kwenye tuzo mbalimbali za kimataifa (Kora,Kisima na sasa hii ya hivi karibuni ya Teneez 2010 huko Kenya ambapo umeibuka mshindi).Wasomaji wangependa kufahamu nini siri ya mafanikio yako?
A.Y: ni kama nilivyokwambia ni bidii na nidhamu na malengo bila hivyo huwezi kwenda mbali.na si hizo tu pia nimekuwa nominated kwa mtv awards 2009 (best hip hop artist nikiwa na jay z,kanye west na m.i)kili awards (2 categories),extra teneez awards (1category) na tuzo za Ghana zinaitwa moma (5categories-artist of the year- Africa,best male,collaboration,east African song,hip hop artist) nawaomba watanzania waweze kuvote online na kwa simu kwa walio Tanzania niweze kunyakua tuzo hizo,unaweza kugogle then upate informations
K.U: Kumekuwepo malalamiko kutoka kwa baadhi ya wasanii kuhusu baadhi ya tuzo za hapo nyumbani hususan suala la upendeleo na mapungufu katika upangaji makundi (categories).Nini mawazo yako katika suala hili?
A.Y:zingine naweza kusema kweli na kuna wakati wasanii wanatakiwa kukubali matokeo maana ukikubaki kuingia katika mashinda jua kuna kushinda na kushindwa
K.U: Ukiwa kama msanii uliyedumu kwenye fani kwa muda mrefu,unaonaje maendeleo ya bongoflava ndani na nje ya Tanzania?
A.Y: inazidi kwenda mbele na kwa sasa wanaoipeleka mbele si wengi so nawaomba wenzangu tuongeze bidii na kutengeneza network zaidi ndani na nje ya nchi
K.U: Baadhi ya kazi zako zimetengenezwa na producers wa nje ya Tanzania.Je kuna tofauti yoyote kati ya kazi zako zinazotengenezwa na producers wa nyumbani na hizo zinazotengenezwa nje?
A.Y: ni ladha hazifanani,napenda sana kuchange plava mara kwa mara kwa audio na hata video
K.U: Swali linaloshabihiana na hilo lililopita.Je kufanya kazi na producers wa nje kunaweza kumsaidia msanii kufanya vyema katika nchi anayotoka producer huyo?
A.Y: sana tu mfano mzuri ni mimi mwenyewe na producer naofanya nao na nafurahi kuona wasanii wengine wa tz wameanza kufuata nyao zangu kwa kuanza kusafiri kurecord sehemu mbali mbali na kushirikiana na wasanii wa nje maana soko limeanza kuwa la afrika na si vile zamani kuwa la kibongo tu,angalia hata charts za redio records nyingi za nje na ndani zinaingia kwa pamoja
K.U: Umewahi kushiriki kwenye fani ya filamu (ambapo ulihusika kwenye filamu ya Girlfriend).Je una mpango wa kuendelea na fani hiyo huko katika siku za usoni?
A.Y:bado sijafikiria kwa kweli kama nitafanya movie
K.U:Vipi kuhusu umodo hasa ushiriki wako kwenye matangazo mbalimbali ya biashara.Je una mpango wa kuwa full-time model licha ya muziki?
A.Y:hapana ila muda wote huwa wananunua image au sauti yangu kwa ajili ya products zao au campaign zao.
K.U: Unawezaje kumudu majukumu yote hayo (muziki, umodo, biashara) pasipo kuathiri ufanisi wako?
A.Y:na masomo pia,nasomea business administration ktk chuo cha Learn IT,mi ni mtu wajukumu tangu zamani sana so najua kuhandle pressure zote na huwa naishi kwa ratiba maalumu ambazo naziweka kwa simu na calendar yangu.
K.U: Umefanikiwa sana kuteka soko la bongoflava katika eneo la Afrika Mashariki.Nini mipango yako ya baadaye kutanua mafanikio hayo maeneo mengine ya Afrika na nje ya bara hilo?
A.Y:Nimeanza kupata bookings za S.A,DJIBOUTI,NIGERIA na ZAMBIA na pia Ethiopia so nazidi kusogea zaidi.pia natoa wimbo wangu mpya niliomshirikisha J.MARTINS kutoka Nigeria so najua itanijenga zaidi.
K.U:Kwa uzoefu wako,na kwa kuzingatia mafanikio unayopata nje ya mipaka ya Tanzania,unadhani ni jambo gani linalopelekea wasanii wengine wengi wa hapo nyumbani kushindwa kufanya vizuri kwenye anga za kimataifa?
A.Y: wengi ni wagumu kujifunza,kufanya networking.maana vile wengine wengi wa nje ya tz wanavyojituma ndio maana natumia style wazotumia wao.
K.U: Moja ya mambo yanayoisumbua Tanzania kwa sasa ni ufisadi lakini wasanii wengi wa bongoflava wamekuwa wakikwepa kuzungumzia suala hili kwenye tungo zao.Je ni sahihi kuyumkinisha kuwa mnaistarehesha jamii kwa vibao vyenu ‘vikali’ lakini mnawatenga kwa kutolipa kipaumbele suala la ufisadi kwenye tungo zenu?
A.Y: sidhani kama ukiimba ufisadi utaisha, nilichongundua ni kuwa watu hawaipendi nchi yetu ndio maana tunawafumbia macho wanaofanya ufisadi na tuna ile hulka ya kulalamika tu then hakuna hatua tunazochukua ndio maana ktuna matatizo mengi sugu tunayalalamikia tu halafu tunanyamaza
K.U: Nini mipango yako ya baadaye katika fani ya sanaa?
A.Y:kuna surprise kubwa nitawatangazia muda si mrefu naakika nitasogea/tutasogea kisanaa
K.U: Mwisho,una ujumbe gani kwa mashabiki wako na wapenzi wa bongoflava kwa ujumla?
A.Y: tuthamini na kuvipenda vya kwetu kwanza kabla ya vya wengine cz hata wao mnaona jinsiwanavyosupport vya kwao kwanza hata kama ni vibaya ila ni vyao na wanavipush sana mpaka wengine wanavikubali..
Blogu hii inakushukuru sana kwa kutumia muda wako kujibu maswali haya mengi.Pia inakutakia kila la heri na mafanikio katika shughuli zako.Na ni matarajio ya blogu na wasomaji wake kuwa tutapata fursa nyingine ya kuongea huko mbeleni.Asante sana.
ANGALIZO KUTOKA KWA AY: Nyimbo zangu na video zangu zitaanza kupatikana very soon online kupitia moja ya kampuni kubwa duniani,pia May hii nafungua duka la nguo mchanganyiko lipo sinza madukani.karibuni sana na kwa mawasiliano tutaweza kuwasiliana katika email yangu ya [email protected]. Na hapa chini ni wasifu wa kampuni ya Unity Entertainment
Waungwana,ni MwanaFA hapa..i dont usually do this kwenye blogs na sites (ku'post maoni) but naona nichangie this time since naona concerns zimekuwa za kistaarabu hapa na zina lengo la kujua tu na si vinginevyo...
Yes,nimefanya masters degree ya finance,Coventry University,ilianza January 2009 na ikamalizika January 2010,natakiwa kufanya mahafali aidha July ama November(kwa jinsi ntakavyoamua)...
Sichukui maoni yeyote kati ya haya vibaya,na pengine yanamaanisha kitu nilichofanya sio kidogo mpaka kufika mahali waungwana wanashindwa kuamini nimeweza kukifanya...
NB: na yes,nikijaliwa uhai na uwezo wa kuhudhuria mahafali ntawaletea picha...
Wasalaam...nawasilisha!!
KULIKONI UGHAIBUNI: Asante Mwana FA kwa hope ufafanuzi huu.
This day last year,at 1400,I received my miracle from the Lord.Two months earlier,I was introduced to a Houston,TX-based powerful woman of God,Apostle Esther.She taught me that when praying,I should ask the Lord for receiving,rather than seek for, my miracle because it was already there.She also gave recommended the ever powerful Psalm 91 to read every day for a number of days.And guess what,as she assured me,I eventually got something that has people waiting for up to a decade to get it, if they at all are successful.God is really Great,and this particular miracle is a living example.I would also like to thank Christha, the woman whose love and care comes only second to my mother's,for introducing me to the Apostle,and for her tirelessly efforts in praying with me.Praise the Lord,Ameen.For Christa,I dedicate the following video (though I know you don't fancy secular music).