20 Sept 2008

Ukiona watu wameshaanza kutoleana macho kabla hata mafuta yenyewe hayajapatikana basi ujue pindi yakipatikana itakuwa balaa.Upatikaji wa mafuta ni neema inayoweza kuwa balaa pia pindi tamaa zinapowekwa mbele kuliko maslahi ya jamii nzima.Zaidi SOMA HAPA

19 Sept 2008


Ni jambo lililo wazi kwamba miongoni mwa wasiotaka kumuona Obama akiingia White House ni pamoja na wale wanaompinga sio kwa sera au uwezo wake bali asili yake (weusi wake).Katika hili kuna weupe wengi na weusi wachache,lakini wote ni wabaguzi wa rangi.Kwa weupe hao,kuongozwa na mtu mweusi ni jambo lisilofikirika kwao.Akilini mwao,mtu mweusi hajafikia hatua ya kuongoza taifa hilo.Kwa weusi wachache,Obama si mwenzao.Ni mtu wa tabaka tofauti na wao.Ukaribu wake na weupe unamtenga na wao.Makundi yote haya mawili yanaongozwa zaidi na hisia kuliko akili.Ni wazembe flani.Hata hivyo,hawa si wa kupuuzwa japo ni vigumu kuwabadili misimamo yao.Kuhusu namna suala la race linavyoweza kumuathiri Obama,SOMA MAKALA HII.Soma na HII kuhusu McCain anavyochomekea ishu za race.

Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi

Wawakilishi Zanzibar wachachamaa kuambiwa hakuna mafuta

Salma Said, Zanzibar
KAULI ya Mtaalamu kutoka Scotland, David Reading, kwamba kuna uwezekano mdogo wa kupata mafuta na gesi asilia katika visiwa vya Unguja na Pemba imewakera mawaziri na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na kumta aifute.

Lakini mtaalamu huyo alisisitiza kwamba yeye akiwa mshauri ni lazima awaeleze ukweli wa mambo, kwani hata makampuni yaliofanya utafiti siku za nyuma kuhusu mafuta walitoa ripoti ambayo haikueleza uhakika wa kuwepo kwa nishati hiyo.

Reading pia alisema kuwa gharama za utafutaji wa mafuta hayo ambayo hayana uhakika ni kubwa mno.

Mtaalamu huyo alikuwa akizungumza katika semina ya siku moja kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi iliyofanyika jana mjini Ugunja.

Reading alisema katika sehemu nyingi zilizogunduliwa mafuta au kuwepo kwa fununu za kuwapo kwa nishati hiyo, gharama yake ilikuwa ni kubwa ambapo ililazimu makampuni kusitisha kazi kwa sababu hiyo.

Matamshi hayo yalionekana kuwachukiza zaidi wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ambapo walimtaka mtaalamu huyo kufuta matamshi yake kwa maelezo kuwa tafiti nyingi zilizofanywa katika miaka ya mwanzoni mwa 1950 zilionesha kuwa yapo mafuta ya kutosha ya kibiashara Zanzibar.

Hoja hiyo iliibua hisia za wajumbe hao za siku nyingi na waalipopata nafasi ya kuchangia, walisema kuwa mafuta ya Zanzibar ni kwa Wazanzibari na kamwe yasifanywe kuwa ya Muungano na kusisitiza msimamo wa kutaka kuondolewa kwa sheria inayoelezea kuwa mafuta na gesi asilia kuwamo katika orodha ya mambo ya Muungano.

Wajumbe hao walisema kuwa huenda suala hilo la mafuta linaweza kusababisha machafuko visiwani, kwani uozefu unaonyesha kwamba nchi nyingi zenye mafuta kuzuka mapigano, hivyo wakashauri suala hilo lisiwe chanzo cha machafuko kwa Wazanzibari.

Waziri wa Utalii, Biashara na Uwekezaji, Samia Suluhu Hassan, alionekana kushangazwa na taarifa za Mshauri Mwelekezi na kuhoji: “Kama uwezekano wa kupatikana mafuta Zanzibar ni mdogo kwa nini serikali ya Muungano ilikataa wazo la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwenye kamati ya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi katika kugawana mapato ya mafuta?”

Hata hivyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma, aliwataka wananchi kuipuuza kauli hiyo ya Mshauri Mwelekezi na kuongeza kuwa ikiwa mafuta hayataondolewa katika orodha ya mambo ya Muungano hatajutia kuona Muungano unayumba.

“Kuna msemo wa kihindi…ipasuke ngoma au ichanike lakini tujue moja kuwa mafuta ya Zanzibar ni kwa Wazanzibari na sio ya Muungano,” alisisitiza waziri huyo.

Kiongozi wa Upinzani katika Baraza la Wawakilishi, Abubakar Khamis Bakari kama walivyo wajumbe wengine waliochangia alisema mafuta yasiwe mambo ya Muungano kwani hata kuingizwa kwake haukufuatwa utaratibu unaofaa.

Mwakilishi wa Jimbo la Gando, Said Ali Mbarouk alisema kwamba Wazanzibari wamezoea kukosa, hivyo haitokuwa jambo la kushangaza ikiwa hakutakuwa na mafuta wakati jambo hilo litakapoondolewa katika orodha ya Muungano, kwani hivi sasa hainufaiki na lolote katika suala la gesi asilia.

Waziri Kiongozi Shamsi Vuai Nahodha akifungua semina hiyo aliwasihi wajumbe hao kutumia busara katika kumpa ushauri mtaalamu huyo ili aweze kupata maoni mwafaka na aweze kuzishauri serikali mbili namna bora ya kugawana mapato yatokanayo na utafutaji na ushimbaji wa mafuta.

Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi, Ali Mzee Ali alisema Wazanzibari wanapochangia kwa ajili ya kutetea nchi yao wasionekane kama ni wasaliti au wana nia ya kugombea urais bali wanatelekeza ahadi yao kwa wananchi ya kuwatetea katika baraza hilo.

Akifunga semina hiyo Waziri wa Maji, Ujenzi Nishati na Ardhi, Mansoor Yussuf Himid aliungana na wajumbe wengine wote kwa kutaka kuwa mafuta yaondolewe katika orodha ya Muungano kwani tokea asili hayakuwa hivyo.

Na leo tena,gazeti hilo linaripoti vituko zaidi vya Wazenji

Mafuta Zanzibar: Hata kidogo katika kinibu tutagawana na mengine kujipaka
Na Salma Said, Zanzibar


Wawakilishi wa Zanzibar wamesema "hata kama ujazo wa mafuta yanayoweza kupatikana Zanzibar ni sawa na glasi ndogo ya kupimia pombe (kinibu), mafuta hayo ni mali ya Wazanzibari watagawana ili watakaoweza wajipake mwilini".


Kauli hiyo ilitolewa jana baada ya mshauri, David Reading, kueleza kuwa mafuta yanayowezekana kupatikana kisiwani humo ni kidogo na kupatikana kwake ni kwa gharama kubwa.


Mtaalamu huyo kutoka Uingereza aliitwa kwa ajili ya kuishauri Serikali ya Mapinduzi (SMZ) na serikali ya Muungano namna bora ya kugawana rasilimali itokanayo na gesi na mafuta.


Kauli hiyo ya Reading pia imesababisha wawakilishi kuingiwa na chuki dhidi ya Wazanzibari walio kwenye serikali ya Muungano, wakiwaita kuwa ni vigeugeu mithili ya vinyonga na wasiojali maslahi ya Wazanzibari.


Akitoa maoni yake kuhusu suala la mafuta na gesi asilia kwa mshauri huyo mwelekezi, mwakilishi kutoka Chama cha Wananchi (CUF), Najma Khalfan Juma alisema kuwa hata kama mafuta ya Zanzibar yatakuwa madogo kiasi cha ujazo wa glasi ndogo ya kupimia pombe ya haramu ya gongo (kinibu), Wazanzibari watagawana hata ikiwa kwa ajili ya kujipaka mwilini.


"Hata kama watajipaka mwilini au wengine watatumia kama dawa ya kuchulia misuli, itakuwa bora zaidi kuliko suala la mafuta kuwa la Muungano," alisema.


Naye mwakilishi wa kuteuliwa na rais, Ali Mzee Ali, ambaye pia ni mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi, alisukumia shutuma zake kwa mawaziri walio kwenye serikali ya Muungano ambao ni Wazanzibari, akiwaita kuwa ni wanafiki na wanaobadilika kama kinyonga.


“Mheshimiwa mwenyekiti kuna wenzetu ambao wamo katika serikali ya Muungano. Wakija hapa (Zanzibar) wanajifanya ni watetezi sana wa Zanzibar, lakini kumbe ni wanafiki,” alilalamika mwakilishi huyo.


"Tabia ya viongozi hao haiwanufaishi Wazanzibari. Viongozi wa Zanzibar wasiwatilie maanani watu wa aina hiyo kwa kuwa wanatanguliza maslahi binafsi.


Baadaye mwakilishi huyo mteule aligeukia vyombo vya habari vya Zanzibar na kusema:


"Kitu cha kushangaza ni gazeti la Asumini ambalo limesajiliwa hapa Zanzibar. Gazeti hili liliwahi kuandika makala ndefu kuelezea umuhimu wa nishati ya mafuta kuwa ya Muungano. 


Jambo hili si sahihi kwani Zanzibar hainufaiki na lolote na mapato ya gesi inayozalishwa Tanzania Bara," alisema.


“Ninalo hapa, waheshimiwa wajumbe, gazeti la Zanzibar Leo ambalo limechapisha makala kama ile iliyotolewa katika gazeti la Asumini. Sijui makala hii imepenya vipi mpaka ikatolewa humu; hilo anajua mheshimiwa (Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Ali Juma) Shamhuna.”


Gazeti la Asumini na Radio ya Zenj Fm zinamilikiwa na Kampuni ya Zanzibar Media Corporation, ambayo Mkurugenzi wake ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano, Muhammad Seif Khatib.


Mwakilishi huyo alisema mara nyingi wanaojitokeza kutetea maslahi ya Zanzibar wanaonekana wanafanya kampeni ya urais kwa mwaka 2010, huku wengine wakishambuliwa kwa maneno kuwa hawautaki Muungano ama kuwa na ajenda ya siri jambo ambalo anaamini si sahihi.


Ali Mzee aliwataka wananchi na hasa wajumbe wa baraza la wawakilishi kuungana kuwa kitu kimoja katika kutetea maslahi ya Zanzibar na kuachana na watu aliowaita kuwa 'Wazanzibari Maslahi' kwenye serikali ya Muungano.


Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma aliwataka viongozi wa Zanzibar kutoogopa kufukuzwa serikalini kwa kuitetea Zanzibar kwani mara nyingi mtu anapojitokeza kutetea maslahi ya visiwa hivyo, huambiwa kuwa amechafua hali ya hewa kama ilivyokuwa kwa rais wa zamani wa Zanzibar na Makamu wa Kwanza wa Rais, Aboud Jumbe Mwinyi.


“Waheshimiwa tusiogope kunyang'anywa magari," alisema. "Wakitunyang'anya sawa, tutatembea hata kwa miguu lakini lazima tuitetea nchi yetu kwa sababu sisi tumeapa kwa katiba hii (katiba ya Zanzibar) na sio ya Jamhuri ya Muungano.”


Akichangia hoja hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- Fedha na Uchumi, Dk. Mwinyihaji Makame alishabihiana na wenzake, akieleza kuwa katika suala la mafuta hakuna dhamira njema kwa Wazanzibari.


Mwakilishi wa Viti Maalumu (CUF), Zakia Omar Juma alisema umefika wakati sasa kwa Wazanzibari kujikomboa kiuchumi kwa kuungana kutetea mafuta yao kwani mara nyingi Zanzibar inapotaka kujikwamua kiuchumi huwekewa vikwazo na serikali ya Muungano.


Mwakilishi wa Jimbo la Ziwani (CUF), Rashid Seif alisema kwamba inaonekana Zanzibar kuna mafuta ya kutosha na ndio maana watu wa Tanzania Bara (Tanganyika) wanang'ang'ania suala la mafuta kuwa la Muungano licha ya kuwa Wazanzibari wenyewe hawataki.













According to the latest Gallup polls,Obama now leads McCain by 5 points.Sounds good,doesn't it?

(Picha kwa hisani ya Tambaza.blogspot.com

Unajua unaweza kuona kama habari ya hapo chini inahusu watu ni machizi wanaotangaza hatua za kubana matumizi kwa kuzima taa za mtaani.In fact,sisi ndio tunaonekana watu wa ajabu zaidi kwa kuwa na matumizi ya kifahari ilhali uchumi wetu unategemea zaidi huruma ya  wafadhili.Hivi ni jeuri ya kutumia ovyo fedha za wafadhili au ni uzembe wa wafadhili kufuatilia fedha zao zinatumikaje?Enewei,waungwana hawa wameamua kubana matumizi kwa njia ya kuchekesha kidogo.Bonyeza HAPA kusoma habari kamili. 

18 Sept 2008

KIDATU MACHANICAL AU MECHANICAL?

Ustaadh mmoja mwenye msimamo mkali huko Saudi Arabia ametoa fatwa dhidi ya kikatuni-kipanya Mickey Mouse,akidai kuwa "kipanya" huyo ni askari wa shetani.Huu sio utani,BONYEZA HAPA kusoma habari hiyo ya kuchekesha.

Watundu flani (au wahalifu?) wamefanikiwa ku-hack e-mails za Sarah Palin.Habari kamili na picha BONYEZA HAPA

Mlimbwende hapo juu anauza bikra (virginity) yake kwa Euro MILIONI 1 (takriban Dola za Kimarekani Milioni 1.43  au Pauni za Kiingereza Laki 7 na ushee au Shilingi za Kibongo Bilioni 1 na milioni mia 6).Tamaa ya fedha au ndio kuthamini assets zake?Stori nzima BONYEZA HAPA









Picha ya hapo juu inafurahisha.Ndio namna jamaa wa The Huffington Post wanavyo-summarize masahibu yanayomkumba John McCain.Kwa mujibu wa Gallup polls,Barack Obama amefanikiwa kumwengua McCain kwenye kura za maoni ikiwa ni mara ya kwanza tangu mgombea huyo wa Republicans apande chati kufuatia convention ya chama hicho hivi karibuni.Zaidi,angalia video hii hapa chini


17 Sept 2008

Chama cha siasa huzaliwa,hukua na kinaweza kufa pengine hata kabla hakijakua.Tofauti nachama nchi ikishazaliwa ni lazima iishi milele,tena kwa gharama yoyote ile.Lakini kuna wenzetu wengine hawataki kuelewa ukweli huo.Kwao,chama cha siasa ni kila kitu hata kama kinaipeleka nchi ahera.Angalia mfano huu mwepesi: chama kinapewa dhamana ya kuongoza nchi,lakini kinaendesha mambo yake kihuni na kupeleka nchi mrama.Ni dhahiri kwamba chama cha aina hiyo kinaamsha vurugu ambazo zitalekea mmomonyoko wa amani katika nchi husika.Kwa bahati mbaya au makusudi,kuna wenzetu hawataki kuamini kwamba ni vigumu kujenga na kudumisha amani kuliko kuivunja.Sote tunawajibika kuhakikisha nchi yetu haipelekwi kusikofaa badala ya kunyoosheana vidole tunapotofautiana namna ya kuboresha ustawi wa Tanzania yetu.

Katika toleo la wiki hii la gazeti mahiri la Raia Mwema,pamoja na mkusanyiko wa habari na makala motomoto,kuna hababari kuhusu the man of the moment,Nape Nnauye.Kuna wanaodai kuwa huyu jamaa aanashupalia ishu za ufisadi ndani ya UVCCM kwa minajili ya kutafuta umaarufu utakaopelekea apate nafasi ya juu kwenye jumuiya hiyo.Sina uhakika kuhusu hilo lakini binafsi naamini kwamba hata kama malengo yake ya ni kupata umaarufu au uongozi,jitihada zake kuushikia bango ufisadi ndilo lililo muhimu zaidi kuliko motives zake.Na wanaokemea ufisadi,hata kama kwa njia zisizo sahihi,wanapaswa kuungwa mkono badala ya kunyanyaswa.Enewei,habari ya Nape ni hii HAPA na mambo mengine motomoto yanapatikana ndani ya gazeti hili la RAIA MWEMA.


Kigoma.Mwaka 1976.Nyumba kadhaa maeneo na NHC Mnarani zinaonekana zikiwa na magamba (outer cases) ya betri yaliyobandikwa vikaratasi vyenye maandishi ya Kiarabu.Habari zilizozagaa wakati huo ni kwamba pasipo kuweka "kinga" hiyo maafa yangeikumba nyumba husika.Weka usalimike,usiweke uone kitachokutokea.Kwa vile takriban kila nyumba katika mtaa naoukumbuka ilikuwa na "kinga" hizo,haikuwa rahisi kubaini nini kingetokea kwa waliopuuza.

Ifakara.Mwaka 1982.Watoto tunaangaliwa kwa karibu na wazazi kwa hofu ya kuchukuliwa na "wanyonya damu" au maarufu kwa jina la mumiani.Nakumbuka nyumba moja iliyokuwa eneo la Kwa Shungu ambayo nadhani mmiliki wake aliamua tu kuiwekea urembo wa msalaba kwa kutumia chokaa ilikuwa ikituhumiwa kwamba ndio kituo cha kukusanyia damu zinazonyonywa na mumiani.Hadi leo sijui kama kuna mtoto au mtu aliyenyonywa damu na mumiani waliodaiwa kuvamia Ifakara.

Tanga.Mwaka 1993.Madereva wanataharishana kuhusu jini la kike linalodaiwa kuonekana nyakati za usiku katika barabara ya Ngamiani.Jini hili linadaiwa kujibadili kama mwanamke mrembo sana,na  pindi dereva akithubutu kutoa lifti akidhani "ameopoa mzigo" basi ndio mwisho wake.Pia nyumba moja maeneo ya Makorora ambayo mmiliki wake amefuga mbuzi kadhaa inadaiwa kuhifadhi majini lukuki.Wajuzi wa mambo wanatahadharisha kupita maeneo hayo usiku mkubwa,na wengine wanakwenda mbali zaidi kwa kushauri kwamba hata ukipita mchana usiangalie sana nyumba hiyo,majini yanaweza kukuvuta.Hadi naondoka Tanga mwaka 1995 sikuweza kuthibitisha ukweli au uongo wa habari hizo.

Nyanda za Juu Kusini.Miaka ya hivi karibuni.Taarifa zinatapakaa kwamba kuna biashara ya uchunaji ngozi za binadamu.Inadaiwa kwamba ngozi hizo hutumiwa na waganga kwenye masuala ya baishara.Pia inadaiwa kuwa ngozi hizo zina faida kubwa katika nchi moja jirani.Tarehe 8 mwezi Mei mwaka 2006 Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya inawakumu watu wawili,Dickson Shapwata na Nelson Mwazembe, kunyongwa baada ya kupatikana na tuhuma za kumuua na kumchuna ngozi Marehemu Loti Nzowa mnamo mwaka 2001.

Kanda ya Ziwa.Miaka ya hivi karibuni.Mauaji ya vikongwe wenye macho mekundu yanazidi kushika hatamu.Tuhuma dhidi ya vikongwe hao ni uchawi.Mtani wangu mmoja Msukuma wa Shinyanga ananinong'oneza kwamba amemshauri babu yake aache kuvuta ugoro ili macho yake yasiwe mekundu.Mtani wangu mwingine anadai kwamba vikongwe wenye macho mekundu wanauawa kwa sababu wekundu huo ni matokeo ya wao kukesha wakiwanga usiku.Utani kando,mauaji ya vikongwe bado yanaendelea japo hadi sasa ni vigumu kuelewa kwanini yashamiri Kanda ya Ziwa pekee.

Sehemu mbalimbali Tanzania.Mwaka 2008.Taarifa zinatapakaa kwamba maalbino wanawinda na wanauawa na watu wanaodaiwa kuhitaji viungo kutoka miilini mwa maalbino hao kutengenezea dawa za baishara.Mwandishi wa BBC,VIcky Ntetema,anapata vitisho wakati anatengeneza documentary kuhusu mauaji ya maalbino.Kwa mujibu wa mwandishi huyo,mwaka huu tayari maalbino 25 wameshauawa maeneo ya Mwanza,Shinyanga na Mara.Mwezi Machi mwaka huu,chama cha maalbino mkoani Tanga chatangaza sensa ya maalbino.Mwezi huohuo Serikali mkoani Mwanza inatangaza kuangalia uwezekano wa polisi kuwapatia ulinzi maalbino.

Hii ndio Tanzania yetu ambayo ushirikina unazidi kushamiri.Wapo watakaonipinga lakini ukweli ndio huo.Wanaofuatilia nyendo zisizo rasmi za siasa za nyumbani wanadai kwamba hata baadhi ya wanasiasa wanaosimama majukwaani kukemea mauaji ya vikongwe au maalbino nao wanategemea sana ndumba katika maisha yao ya kisiasa.Wengi tunakumbuka yaliyojiri katika kikao cha Bunge kilichopita ambapo mheshimiwa mmoja alituhumiwa kumwaga ndumba bungeni japo ishu hiyo iliisha kimyakimya.

Kwenye sosholojia ya dini tulifundishwa kwamba kabla ya ujio wa dini za kimapokeo (Ukristo,Uislamu,nk) jamii za Kiafrika zilikuwa zikifuata dini zao za asili (African Traditional Religions-ATRs).Na hadi sasa,dini za asili zina ushawishi mkubwa kwa waumini wa dini za kimapokeo.Tunafahamu Wakristo au Waislam wengi ambao pamoja na kwenda makanisani au misikitini hawasahau kuomba mizimu ya kale.Kwa waliozaliwa na kukulia Dar,sio rahisi sana kuelewa hili nalozungumzia lakini hilo linajulikana sana kwa "wakuja" wenzangu.Sasa,tatizo lipo katika kuchora mstari unaotenganisha dini za asili na ushirikina.Kule kwetu Undambani kuna mababu (wanaitwa "mambuyi" kwa Kindamba) wanaoaminika kufanya miujiza (kutibu,kuepusha ukame/njaa,nk) wanapoombwa kwa dhati.Inaaminika pia kwamba "mambuyi" hao wana uwezo wa kumduru mtu.

Tukirudi kwenye sosholojia ya dini tunaambiwa kuna roho mfu za aina mbili,dead-dead na living-dead.Marehemu wanaokufa na kuenziwa,hubaki kuwa mzimu yenye inayotarajiwa kuleta mema.Marehemu wanaotelekezwa (kwa mfano wanaokufa ajalini na maiti zao kuzikwa na jiji) hugeuka kuwa mzimu yenye uwezo wa kuleta mabaya kwa vile wamesahaulika.Pengine hapa ni vizuri kushauri wazazi kutosahau kutoa "sadaka" ya jina la marehemu babu,bibi,baba,mama au yeyote yule katika ukoo ili kuwaenzi kwa minajili hiyo ya baraka za mbeleni.

Ni vigumu kubashiri iwapo mauaji ya maalbino yatakwisha kwani hata hayo ya vikongwe bado yanaendelea.Tatizo kubwa zaidi linalozikabidili jamii zetu za Kiafrika ni watu kutafuta njia za mkato katika kutimiza malengo au matakwa yao.Ushirikina unashamiri zaidi kwa namna hiyo.Mtu anatafuta dawa ya kufaulu mtihani,anakwenda kwa mganga na kutakiwa apeleke kichwa cha mtu mwenye kipara.Huyu ni mzembe ambaye anataka kupata njia ya mkato ya kufaulu badala ya kusoma kwa bidii.Mheshimiwa flani anataka kurejea bungeni lakini anakabiliwa na upinzani mkali kwa vile hajaonekana jimboni tangu achaguliwe katika uchaguzi uliopita.Anakwenda kwa mganga anaambiwa alete moyo wa albino.Unategemea nini hapo?

Haya ya vikongwe wenye macho mekundu na maalbino ni mwendelezo tu wa ushirikina katika jamii zetu.Yayumkinika kuamini kuwa huko mbele wenye vipara,vitambi,matege,makengeza na pengine hata wenye mustachi wanaweza kuwa wawindwa wa hawa wanaotaka mafanikio kwa njia ya mkato.Mbinde itakuwa pale washirikina hao watakapoanza kuwinda watu wenye fedha nyingi katika akaunti zao ambazo hazikupatikana kihalali!Pengine ndio utakuwa mwisho wa ufisadi.Just thinking aloud!


15 Sept 2008

Came accross this interesting examination of Sarah Palin



Sarah Palin may not have known what the Bush Doctrine was, but we're getting a pretty good idea of what the Palin Doctrine is. Or will be -- because it's still currently under construction. And what is it going to look like? Let's just say, it's going to seem familiar.

According to London's Daily Telegraph, the architects of the Palin Doctrine are a group of people who have been singularly wrong about virtually everything in the last decade -- the neocons, who have been briefing Palin for weeks.

As predicted, the fact that she didn't know anything wasn't a bug, it was a feature. She's perfect for the neocons: likeable on the outside, a blank slate on the inside. To borrow from an old cliché, if Sarah Palin didn't exist, the neocons would have had to invent her.

In fact, this is how one former White House aide describes her: "She's bright and she's a blank page. She's going places and it's worth going there with her."

Of course, the place her neocon mentors hope she's going is the White House. Given their dismal track record, they're smart enough to figure that the American public wouldn't be too keen on letting them in the front door again, so they are trying to sneak in hidden behind Palin's skirt. The Trojan Moose approaches.

The Daily Telegraph details how the neocon talent scouts spotted their political Eliza Doolittle back in the summer of '07. The love connection began, appropriately enough, on a love boat:

"Sources in the McCain camp, the Republican Party and Washington think tanks say Mrs. Palin was identified as a potential future leader of the neoconservative cause in June 2007. That was when the annual summer cruise organised by the right-of-centre Weekly Standardmagazine docked in Juneau, the Alaskan state capital, and the pundits on board took tea with Governor Palin."

So nice to meet you, Governor. And don't forget, cucumber sandwiches and preemptive invasions on the Lido Deck at four!

Not surprisingly, Palin's biggest fan is Bill Kristol, who describes her as the "specter of a young, attractive, unapologetic conservatism" that "is haunting the liberal elites."

Among her other Henry Higginses is neo-neocon Joe Lieberman, who is reportedly helping prep Palin for the big ball -- her debate with Joe Biden.

She's already passed her first test with flying colors: being willing to link 9/11 with Iraq, something not even the president is still willing to do. Last week, she told a group of Iraq-bound soldiers that they were going to "defend the innocent from the enemies who planned and carried out and rejoiced in the death of thousands of Americans."

By George (Bush), I think she's got it! Congratulations, Professor Kristol, your student is coming along just fine.

Of course, the neocons know they already have an ally at the top of the GOP ticket. McCain may have been a reformer on campaign finance, but when it comes to foreign policy, he has always been solidly in the neocon club. He loves to burnish his foreign policy bona fides by talking about how he wanted to fire Donald Rumsfeld months before Bush did. But he doesn't talk a lot about how, in the days immediately after 9/11, he was part of the neocon crowd itching to get into Iraq.

Just a few days after the attack, McCain was already talking about "some other countries" that helped Bin Laden. Countries like Syria, Iran, and...Iraq. And a few weeks later, during an October 18, 2001 appearance on David Letterman, McCain answered a question about how the war in Afghanistan was going by announcing that the invasion of Iraq would be "the second phase" of the war on terror (how prescient of him to know that Saddam wouldn't give up those nonexistent WMD). What's more, he tried to buttress the case for attacking Iraq by claiming that the recent spate of anthrax attacks "may have come from Iraq." Or Fort Detrick.

Six years later, demonstrating how little he's learned from the debacle in Iraq, McCain hired Randy Scheunemann, a neocon darling who helped form The Committee for the Liberation of Iraq in 2002, as his campaign's chief foreign policy advisor.

As TPMMuckraker noted in July, "Of all the hawkish Washington foreign-policy types pushing both before and after 9/11 for war with Iraq -- a war that an overwhelming majority of Americans now considers a mistake -- Scheunemann, though not a marquee name, was among the most energetic and influential. And in the invasion's aftermath, he consistently opposed steps that might have helped stabilize the country."

And now, according to the Daily Telegraph, Scheunemann is briefing Sarah Palin.

McCain's selection of Palin may have been reckless, but it was anything but random. The neocons' view of the world may be disastrous, dangerous, discredited, and deadly -- but it's far from dead. Their patron saint, Dick Cheney, the scowling embodiment of the Neocon Doctrine, had way too much baggage -- and way too low approval ratings -- to mount a run for the White House.

That's why the Palin pick was so brilliant. On the outside, she's exponentially more likable and talented at connecting with people than Cheney ever was. But on the inside, once she graduates from the neocon finishing school, she'll be a complete and total Dick. Cheney. With lipstick.



Some political analysts argue that ruling parties in Africa never lose elections,and if they do,which is rarely,it is likely not because they failed to deliver to the people who put the parties in power but rather either due to their internal conflicts or laxity.One could easily blame majority of opposition parties in Africa for their failures in organizing themselves in quest to remove ruling parties from power.But the fact is,in most African countries,the idea of an opposition party coming into power spells inexplicable uncertainty to the rulers,largely due to their "sins" during their terms of leadership.

In Tanzania,opposition parties have consistently cried foul during elections accusing the ruling party,CCM,of sabotaging them by either inciting conflicts in the parties or "bribing" their leaders to defect.CCM has also been accused of reluctance to reform the electoral system,which the opposition parties,see as unfair and biased.

I strongly believe that our nation's interest should come first,mainly because political parties may come and go but the nation should always remain intact,peacefully and flourishing.Had every Tanzanian looked beyond partisan politics,it is fair to conclude that those who criticize the ruling party for its perceived failure to deals with mafisadi (economic saboteurs),for instance,would not be considered as giving ammunitions to opposition parties but instead they would be given enormous support.

A while ago,I came across this story which in my view would stir trouble in Tanzania's opposition politics.
Mtikila atamka mazito kifo cha Wangwe

Na Waandishi Wetu 

WAKATI mazingira ya kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime marehemu Chacha Wangwe yakiendelea kuwa tete, Mwenyekiti wa Democratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila, ameibuka na kile alichodai, taarifa za mpango kamili hadi mauaji ya mwanasiasa huyo. 

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mchungaji Mtikila alidai mipango ya kumuua marehemu Wangwe ilianza kusukwa mkoani Dodoma na baadaye vikao vya kukamilisha mkakati huo, vilifanyika jijini Dar es Salaam wilayani Kinondoni. 

Aliongeza kuwa wahusika baada ya kukamilisha mpango huo na jinsi utakavyotekelezwa, walikwenda nchini Kenya kukodi watu wawili ambao alidai walilipwa sh. milioni 120 kama ujira wa 'kazi' hiyo. 

Mchungaji Mtikila alidai kuwa wauaji hao, ndio walioshirikiana na Bw.Deus Mallya ambaye anadaiwa wakati huo alikuwa amejenga uhusiano mzuri na marehemu Wangwe. 

Alidai siku ya tukio, marehemu Wangwe hakutaka kusafiri lakini alishinikizwa zaidi ya mara tatu na Bw. Mallya ambaye hadi sasa anashitakiwa kwa kosa la kusababisha ajali na kuendesha gari bila leseni.

"Baada ya kushinikizwa sana, marehemu Wangwe alikubali kuanza safari ambapo Bw. Mallya aliwasiliana na washirika wake ambao muda huo walikuwa eneo la tukio wakiwasubiri," alidai Mchungaji Mtikila na kuongeza kuwa; 

"Wakati huo ilikuwa bado mapema hivyo walimshauri apoteze muda japo wa nusu saa, ndipo alipozusha hitilafu ndani ya gari na kurudi gereji na baada ya muda huo kupita ndipo walianza safari kuelekea jijini Dar es Salaam." 

Huku akidai kuwa ana ushahidi wa tukio hilo na yupo tayari kutoa ushirikiano kwa Rais Jakaya Kikwete, Mchungaji Mtikila alizidi kueleza kuwa Bw. Mallya aliendelea kuwasiliana na washirika wake hadi walipofika eneo Pandambili, wilayani Kongwa na kusimamisha gari. 

"Baada ya kusimamisha gari, washirika wa Mallya walipanda na kumpulizia dawa ya usingizi usoni mara nne na hapo hapo alipoteza fahamu," alieleza Mchungaji Mtikila na kuongeza kuwa baada ya hapo ndipo alipigwa kwa kitu cha ncha kali kisogoni. 

"Kwa kuwa Mungu alimpenda sana hakukata roho, aliendelea kuhema ndipo alipopigwa na nyundo na kummalizia kabisa," alidai. Aliongeza kuwa baada ya kutimiza hilo waliweka jiwe kwenye kiongeza mwendo gari likaondoka kwa kasi na lilipindua ili kuonesha kuwa marehemu alikufa kwa ajali lakini muda huo Mallya alikuwa hayuko kwenye gari," 

Alidai kuwa kabla ya kupindua gari hilo, walimfunga marehemu mkanda na kumwibia sh. milioni tisa alizokuwa nazo pamoja na kompyuta yake ndogo 'Lap top' ambayo ilikuwa na nyaraka zake za siri. 

Alidai kuwa baada ya kufanikisha mauaji hayo, Bw. Mallya alitoa 'line' yake ya simu ambayo alikuwa akiitumia kuwasiliana na washirika wake na kuitupa. Alidai kuwa hadi anakamatwa simu yake haikuwa na 'line' yoyote. 

Kwa mujibu wa Mchungaji Mtikila mauaji hayo yalifanyika kati ya 1.30 hadi saa 2.00 usiku, muda mfupi baada ya kumaliza kuwasiliana na familia yake saa 1.27. 

Huku akijata majina ya watu wanaodaiwa kuhusika kwenye mpango huo, alieleza kuwa kipindi cha mchakato wa mpango wa kumuua, Bw. Wangwe, walikuwa wakisafiri kwenda nchini Kenya kusuka mpango huo. 

Mchungaji Mtikila alielekeza lawama zake kwa askari wote waliohusika na uchunguzi wa mauaji hayo kwa akidai kuwa hawakusema ukweli hivyo nao wanastahili kuunganishwa kwenye kesi hiyo. 

Kutokana na mazingira ya kifo cha marehemu Wangwe kugubikwa na maswali mengi, Mchungaji Mtikila amemuomba Rais Kikwete kuunda tume ya kuchunguza mazingira ya kifo chake kama alivyofanya kwa wafanyabiashara wa madini wa Mahenge, Morogoro ambao wanadaiwa kuuawa na Polisi. 

Alidai kwa wadhifa aliokuwa nao marehemu Wangwe katika jamii akiwa Mbunge wa Tarime, Rais ana nafasi ya kuunda tume. "Naupongeza uamuzi wake wa kuunda tume ya kuchunguza vifo vya wafanyabiashara lakini na kwa hili aunde tume na mimi nitakuwa tayari kutoa ushirikiano,"alisisitiza. 

Aliongeza kuwa kama Rais hatafanya hivyo, yeye ataleta wataalam wake kutoka nje kufanya uchunguzi kwani ameishafanya mazungumzo na ubalozi wa nchi moja ambao hakuutaja. 

Mchungaji Mtikila alidai kuwa atakwenda jimboni Tarime wakati huu wa kampeni ili kuwaeleza wananchi ukweli kuhusu kifo cha marehemu Wangwe. Alisema amesimamisha mgombea kupitia chama chake, Bw. Benson Makanya, ili apate jukwaa la kueleza ukweli kuhusiana na kifo hicho. 

Marehemu Wangwe alikufa kwa ajali ya gari iliyotokea eneo la Pandambili mkoani Dodoma Julai 28 mwaka huu lakini tangu kifo chake, yameibuka maswali mengi huku baadhi ya watu wakidai kuwa aliuawa. 

Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na madaktari wawili kwa nyakati tofauti ulionesha kuwa hakupigwa risasi bali kifo chake kilisababishwa na ajali ya gari.

According to one local paper,the suspects are Freeman Mbowe,Dr Wilbroad Slaa and Tindu Lissu.This is how I look at the picture:If the accused trio decide to ignore Mtikila,it goes without saying that the public would buy the story,and it could bring their political careers to an abrupt end.Going to the court might be the only option left on their table,but Mtikila has a long history of winning charges brought against him in various courts.It should be all smiles in the ruling party's quarters as a Swahili saying goes "adui yako mwombee mabaya" (wish evil things to your enemy)

14 Sept 2008

John McCain would definitely say "Yes it Does",and so would Sarah Palin,and most,if not all,of the Republicans.However,it is claimed that violence is down in Iraq,not because of the surge,but rather the domination of the Shia and Iran in the country.HERE is the story.

Let me make a confession:Until when Hillary Clinton withdrew from the Democrat presidential campaign,and eventually endorse Barack Obama,I strongly believed that the latter's nomination could lead to another 4 yrs of a Republican in the White House ie a win for John McCain.It's not that I didnt want to see Obama making history by becoming the first Black president of the US of A,but I was rather scared of  the Republican dirty tricks (known in Bongo as "Siasa za Majitaka") on an easy target as Obama.I imagined how the GOP smear machine would assassinate Obama's character,bearing in mind how they successfully made John Kerry's bid to the White House a nightmare.

Perhaps I was wrong.Obama is now on the verge of making history.Given the unpopularity of Bush's presidency,the Dem's road to victory should have been easier.Unfortunately,the Republicans certainly know the odds against them.As I have always suspected,when the going gets tough in politics,any option on the table could be usefull.Of recent,McCain has been accussed of lies and deception,a possible sign that all might not be going well for the GOP candidate.And it seems he will soon receive support from same old groups that focuses on producing emotional rather than rational responses from voters.

HERE they come! (CLICK TO READ THE STORY)



Rais Jakaya Kikwete amewataka Watanzania kutambua kuwa njia pekee itakayowakwamua kiuchumi na kuwaletea maisha bora ni kujishughulisha na shughuli mbalimbali za maendeleo na si kukaa tu vijiweni na kulalamika. 
Kauli hiyo aliitoa jana wakati akijibu malalamiko ya wananchi wa kijiji cha Nyumba ya Mungu, kilichopo katika kata ya Lang`ata, tarafa Msitu wa Tembo, wilayani Simanjiro, ikiwa ni siku yake ya kwanza ya ziara yake ya kikazi mkoani Manyara. 

Wananchi hao waliokuwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali, walimweleza Rais Kikwete kuwa bado wanashindwa kuishi maisha bora kama walivyokuwa wametarajia na badala yake wanakabiliwa na matatizo sugu ya kupata huduma bora ya afya na mitaji ya biashara na ukosefu wa ajira. 

Rais Kikwete alielezwa hayo na wananchi wa kijiji cha Lemkuna, muda mfupi kabla ya kuzindua bonde la umwagiliaji la kijiji hicho, ambapo pia walilalamikia bei kubwa ya pembejeo za kilimo na umbali wa upatikanaji wake, hasa mbolea. 

Akizungumza mara baada ya kuwasikiliza wananchi hao, Rais Kikwete, aliwaeleza kuwa wanapaswa kujiajiri wenyewe kupitia utaratibu wa kupata mikopo na kujiunga kwenye vikundi vya kuweka na kukopa (SACCOS) ili waweze kuanzisha miradi ya maendeleo. 

``Jamani msitarajie maisha bora kama yatadondoka kutoka juu, utaratibu uliopo ni wa mikopo tuliyoianzisha ili muweze kufanya shughuli za maendeleo, awamu ya kwanza imekwishapita wengine wamepata wengine hawajapata ila tutaendelea kuhakikisha kuwa mikopo zaidi inatatolewa ili wale ambao hawajapata waweze kupata`` alisema. SOURCE:ippmedia.com

Kauli hiyo inashabihiana na hii iliyotolewa na Waziri Mkuu wa zamani,Edward Lowassa

2007-05-10 15:55:28 
Na Radio One Habari

Waziri Mkuu, Mheshimiwa Edward Lowassa amesema maisha bora kwa kila Mtanzania hayawezi kuja kwa kukaa vijiweni na kunywa kahawa bali kwa kufanyakazi kwa bidii na hasa kuendeleza kilimo. 

Amefafanua kuwa maisha bora kwa kila Mtanzania yanayosemwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ni matokeo ya kazi na hayaji kwa kukaa vijiweni kutwa nzima kunywa Kahawa na kutaka wananchi wa Pwani wafanye kazi kwa bidii kujiletea maendeleo. 

Akihutubia mkutano wa hadhara kijijini Maneromango Wilayani Kisarawe Mkoani Pwani Waziri Mkuu amesema watu wa mkoa huo lazima wabadili pato la mwaka la kila mtu ili liwe kubwa kama katika mikoa mingine. 

Aidha ameagiza mashambapori yaliyopo Kisarawe na wilaya nyingine Mkoani Pwani yaorodheshwe, yapelekwe Wizara ya Ardhi ili hatimaye yafikishwe kwa Rais yatwaliwe na kuwagawia vijana wafanye kazi za kilimo. 
Waziri Mkuu anakamilisha ziara yake ya siku sita ya Mkoa wa Pwani leo kwa kutembelea Wilaya ya Bagamoyo. 
SOURCE: Radio One


13 Sept 2008

Moja ya mambo hatari sana ambayo kwa kiasi kikubwa ni kama yamefumbiwa macho huko nyumbani ni matangazo yaliyotapakaa kwenye magazeti na mitaani kuhusu tiba ya Ukimwi.Waganga wengi wa jadi,wa kweli na "wasanii",wamekuwa wakijitangaza kuwa wanatibu ugonjwa huo hatari.Ni vigumu kupata takwimu sahihi za watu wanaopoteza maisha kwa kufuata tiba hizo badala ya ARVs,lakini yayumkinika kuamini kuwa utapeli wa aina hii inagharimu maisha ya waathirika wengi.Nimekutana na habari ya usanii kama huo uliokuwa ukiendelea nchini Afrika ya Kusini.Kibaya zaidi ni kwamba mtu aliyesimamia shughuli hiyo,Matthias Rath, alikuwa akijigamba kuwa mkombozi wa Afrika na dunia dhidi ya Ukimwi.Simulizi kamili ya video iko HAPA

12 Sept 2008

Suala la Health and Safety ni miongoni mwa vipaumbele vikubwa kwa hawa wenzetu wa nchi zilizoendelea.Lakini inapofikia hatua ya kung'oa kwa makaburi in the name of health and safety,yayumkinika kuamini kuwa hawa wenzetu nao wakati mwingine wana maamuzi as if vichwani mwao kuna mapovu badala ya ubongo.Hebu soma KIOJA HIKI CHA HAPO LONDON

Kama kioja hicho hakijakuchekesha,vipi kuhusu hiki cha Mmasai aleyekwenda Mombasa kwa matarajio ya kudaka mwanamama mtalii mzungu amuoe lakini akajikuta akiishia kuwa msusi!Bingirika na kioja hiki HAPA

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.