26 Jun 2009

Ifakara katika picha niliyopiga mwezi Mei mwaka jana.

Mji una neema ya ardhi yenye rutuba inayokubali kilimo cha mpunga,mahindi,na mazao mengine lukuki.Ungetegemea mapinduzi ya kijani yaanzie sehemu kama hizi lakini kama kawaida ya wanasiasa wetu,maneno meeengi huku vitendo vikiishia kwenye michakato,mikakati,vipaumbele,semina elekezi na ubabaishaji mwingine kama huo.Habari hii hapo chini licha ya kunigusa kutokana na ukweli kwamba wilaya ya Kilombero ndio nyumbani,pia inawakilisha matatizo yanayowakabili mamilioni ya Watanzania wanaotegemea kilimo kama njia pekee ya kuwawezesha kuishi.Isome kwanza:

Kilombero, Ulanga wahofia njaa

na Joseph Malembeka, Kilombero

BAADHI ya
wananchi wanaoishi katika wilaya za Kilombero na Ulanga mkoani Morogoro wameiomba serikali kuingilia kati ununuzi holela wa mazao ya chakula unaofanywa na walanguzi sasa.

Ombi hilo limekuja kutokana na ongezeko kubwa la wafanyabiashara kuingia wilayani humo na kununua kwa kasi mpunga ukiwemo uliovunwa na uliopo mashambani.

Wakizungumza na Tanzania Daima juzi, John Lyapi na Selemani Kinana walisema kama serikaliikifumbia macho suala hilo kuna hatari ya wakazi wengi wa wilaya hizo kupata baa la njaa mwaka huu.

Lyapi alisema kwa sasa walanguzi hao wamevamia zaidi katika tarafa za Malinyi na Mtimbira na kuwarubuni wananchi kuwauziampunga wao kwa sh 5,000 kwa debe na huku wakiwafuatilia hadi mashambani.

Alisema kutokana na wengi wa wakulima kwa kipindi hiki wanatokea mashambani inawawia vigumu kukataa kupokea fedha hizo, kwani wengi wao huwa kama wanaanzamaisha mapya majumbani baada ya kuhamia mashambani kwa muda mrefu.

Naye Kinana mkazi wa Kilombero alisema kila kukicha bei ya mazao ya chakulaimekuwa inapanda na kushuka kutegemeana na kuongezeka kwa walanguzi hususanwakubwa.

Alisema endapo serikali itakabiliana kikamilifu na walanguzi haoitasaidia kuondoshwa chakula kingi wilayani humo na kunusuru janga la njaa.

Kwa mujibu wa wakuu wa wilaya hizo Evarist Ndikilo (Kilombero) na DkRajabu Rutengwe (Ulanga) kwa nyakati tofauti walisema tayari halmashauri zimeagizwa kuwatangazia wananchi kuacha mtindo huo.

Walisema mbali na kupiga marufuku kwa wananchi kuuza vyakula pia wanakusudia kuweka sheria itakayowasaidia, iliwaweze kujikwamua na janga la njaa kwa kutouza vyakula hivyo.

CHANZO: Tanzania Daima

Mkuu wa wilaya ya Kilombero anaweza hata kuamuru jeshi la polisi likamate wanaouza chakula,lakini haitokuwa ufumbuzi wa tatizo hilo.Bottom line is,watu wanauza akiba ya chakula chao ili kukabiliana na ugumu wa maisha.Unadhani kuna mkulima anayependa kula mbegu?

Hivi kwanini hizo trilioni moja na ushee zilizotengwa kukabailiana na msukosuko wa uchumi zisiangalie walalahoi kama hawa?Katika mpango huo ambao bado nina wasiwasi unaweza kuishia kuwa-bailout mafisadi kama si kuzua EPA nyingine,wakulima wa kawaida wamepewa kisogo licha ya hadithi za KILIMO KWANZA.

Ukitembelea Ifakara katika kipindi hiki cha mavuno utapata picha moja ya kusikitisha.Wakulima wa mji huo wanatumia takriban robo tatu ya mwaka kulima mpunga (na kilimo cha mpunga kiko very demanding huku kikitegemea kudra za Mungu kwenye hali ya hewa).Baada ya mavuno,mji huo unafurika wanunuzi wa mpunga na mchele,huku wengine wakiufuata hukohuko mashambani.Kwa vile muda huu wengi wa wakulima huwa hoi kiuchumi,bei ya mpunga na mchele huwa ni karibu na bure.Pia baadhi ya wakulima wenye mahitaji mengine muhimu kama vile nguo,sukari,nk huamua kupokea bidhaa hizo badala ya fedha (barter trade) alimradi siku ziende mbele.Na muda si muda,wakulima hao hujikuta wameuza hadi mbegu na kurejea mahala palepale walipoanzia: hawana hela,hawana chakula.

Tuna wizara ya wajibu wa kushukulikia kilimo,na tuna wizara yenye wajibu wa kuwasaidia wakulima kupata masoko ya kuaminika ya mazao yao.Pia tuna wizara inayowajibika na masuala ya ushirika.Kwa makusudi,wizara hizi zimebaki majina tu japo utasikia zinatengewa mamilioni kama sio mabilioni,sio tu kwa ajili ya "kuleta ufanisi" bali pia huduma za ukarimu-chai,chakula,nk.

Tuna takriban Watanzania wenzetu 50 wenye wadhifa wa uwaziri au unaibu waziri.Sehemu kubwa tu ya fedha za walipa kodi inatumika kuwahudumia waheshimiwa hawa.Lakini ni ukweli usiopingika kuwa utendaji kazi wao ni chini ya kiwango.Walikabidhiwa dhamana ya kutekeleza kaulimbiu ya MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA lakini yayumkinika kuhitimisha kuwa sanasana wamefanikiwa kujitengenezea maisha bora wao wenyewe na "wafadhili wao wa kisiasa".


Kwa mmiliki wa makazi hayo pichani juu,habari za Maisha Bora kwa Kila Mtanzania ni kama utani mbaya kwake.Japo amezungukwa na ardhi kijani yenye rutuba,hajui jioni itakuwaje let alone hiyo kesho au msimu ujao wa kilimo na mavuno.Ukimwambia kuwa kuna kaulimbiu mpya ya
KILIMO KWANZA anaweza kukushushia ngumi!



On Nixon Tapes, Ambivalence Over Abortion, Not Watergate

By CHARLIE SAVAGE

WASHINGTON — On Jan. 22, 1973, when the Supreme Court struck down laws criminalizing abortion in Roe v. Wade, President Richard M. Nixon made no public statement. But the next day, newly released tapes reveal, he privately expressed ambivalence.

Nixon worried that greater access to abortions would foster “permissiveness,” and said that “it breaks the family.” But he also saw a need for abortion in some cases — like interracial pregnancies, he said.

“There are times when an abortion is necessary. I know that. When you have a black and a white,” he told an aide, before adding, “Or a rape.”

Nine months later, Nixon forced the firing of the special prosecutor looking into the Watergate affair, Archibald Cox, and prompted the resignations of Attorney General Elliot L. Richardson and Deputy Attorney General William D. Ruckelshaus. The next day, Ronald Reagan, who was then governor of California and would later be president, told the White House that he approved.

Reagan said the action, which would become known as the “Saturday Night Massacre,” was “probably the best thing that ever happened — none of them belong where they were,” according to a Nixon aide’s notes of the private conversation.

Those disclosures were among the revelations in more than 150 hours of tape and 30,000 pages of documents made public on Tuesday by the Nixon Presidential Library, a part of the National Archives. The audio files were posted online, as were a sampling of the documents.

The tapes were recorded by the secret microphones in the Oval Office from January and February 1973. They shed new light on an intense moment in American history, including Nixon’s second inauguration, the Vietnam War cease-fire, and the trial of seven men over the break-in at the Democrats’ headquarters at the Watergate complex amid mounting revelations about their ties to the White House.

The tapes also capture more mundane details of life in the White House — conversations about what to pack for a trip, when to schedule a trip to the barber, whether the president’s wife would enjoy going to Trader Vic’s for dinner.

Most segments of the tapes relating to the Watergate scandal, which would lead to Nixon’s resignation 20 months later, have already been released. But there are some new materials that were previously held back because the audio quality was so poor that archives officials could not be certain whether they contained discussion of any classified topics. Improvements in audio technology have allowed archives staff to clear additional ones.

They include a Jan. 5, 1973, conversation between Nixon and his aide Charles W. Colson in which they discussed the possibility of granting clemency to E. Howard Hunt Jr., one of the Watergate conspirators, according to a log compiled by archives staff. Scholars say the same topic was addressed in several other tapes that were previously made public.

The documents also include nine pages of handwritten notes by a domestic policy aide about plans for what the White House would say about the dismissal of the Watergate special prosecutor, Mr. Cox.

The tapes also provide new material about the circumstances surrounding the Paris treaty to end the United States’ military involvement in Vietnam.

A call between Nixon and Mr. Colson just after midnight on Jan. 20 showed that Nixon anticipated, when the treaty was announced, that he would be vindicated for continuing to bomb North Vietnam. He especially relished the hit that he believed members of Congress who opposed the war — whose public statements he pronounced “treasonable” — would suffer.

Several conversations center on the pressure Nixon placed on South Vietnam’s president, Nguyen Van Thieu, to accept the cease-fire agreement. Ken Hughes, a Nixon scholar and research fellow at the Presidential Recordings Project at the University of Virginia, said he was struck by listening on one of the new tapes to Nixon’s telling his national security adviser, Henry A. Kissinger, that to get Thieu to sign the treaty, he would “cut off his head if necessary.”

Mr. Hughes said the conversation bolstered his view that Nixon, Thieu and Mr. Kissinger knew at the time that the cease-fire could not endure, and that it was not “peace with honor,” as Nixon described it, so much as a face-saving way for the United States to get out of the war. In 1975, North Vietnam would violate the cease-fire and conquer South Vietnam.

The tapes also include a phone call from February 1973 between Nixon and the evangelist Billy Graham, during which Mr. Graham complained that Jewish-American leaders were opposing efforts to promote evangelical Christianity, like Campus Crusade. The two men agreed that the Jewish leaders risked setting off anti-Semitic sentiment.

“What I really think is deep down in this country, there is a lot of anti-Semitism, and all this is going to do is stir it up,” Nixon said.

At another point he said: “It may be they have a death wish. You know that’s been the problem with our Jewish friends for centuries.”

The documents also include three newly declassified pages from a National Security Council brief discussing secret Israeli efforts to build a nuclear weapon.

SOURCE: The New York Times


Ana umri wa miaka miwili tu,lakini anavuta pakti zima la sigara kwa siku.Huyo ni Tong Liangliang,mkazi wa mji wa Tianjin nchini China.Dogo huyo anaaminika kuwa ndio mvuta fegi mdogo zaidi duniani,at least miongoni mwa waliojitambulisha kama watumiaji wa tumbaku.

Tong alianza kuvuta fegi akiwa na umri wa miezi 18 baada ya baba yake kumpatia mche kwa minajili ya kupunguza maumivu ya henia aliyozaliwa nayo dogo huyo.Kwa sasa hakuna dalili za yosso huyo kuachana na sigara kwani amekataa katakata ushauri wa kumtaka a-quit.Pia kiserengeti boy hicho hakioni aibu kuomba sigara pindi kikutanapo na mvutaji mwingine,na husononeka anaponyimwa sigara.

Mwaka 2005,mkazi mmoja wa China alituma maombi kwenda Kitabu cha Rekodi za Guinness akitaka atambuliwe kama mtu aliyeanza uvutaji sigara akiwa na umri mdogo zaidi (duniani),ambapo alianza kuvuta fegi akiwa na miaka mitatu.Japo ombi lake lilikataliwa kwa minajili kwamba "rekodi" hiyo ingechochea tabia mbaya,ni dhahiri kwamba hata ingekubaliwa ingekumbana na upinzani kutoka kwa Tong.


Just in case sura ya mwenye gwanda la jela na pingu mkononi ni ngeni kwako,basi huyo ni bilionea Sir Allen Stanford.Unadhani kuna siku majambazi wa kampuni ya Kagoda watakuwa katika hali kama hii?Sijui wewe unaonane,lakini mie sidhani kama hilo litatokea hasa ukizingatia kwamba wanufaika wa ufisadi (kisiasa) wameshaanza kutembeza mabakuli kwa maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwakani.And guess what,wafadhili wakubwa ni haohao tunaowaita akina Kagoda.Nani mwenye jeuri ya kukata mkono unaomlisha?



Kwa mujibu wa TMZ.COM (katika tafsiri isiyo rasmi)

Kufuatia habari za kifo cha Michael Jackson,watu luluki walikimbilia kwenye intaneti kiasi kwamba mfumo mzima (the World Wide Web) ulisimama.Social networks kama Facebook,Twitter,MySpace,AIM-zilikuwa miongoni mwa maeneo ya mtandao yaliyozidiwa na wingi waliotembelea maeneo hayo.Japo zote ziliendelea kufanya kazi (kufunguka) lakini kasi yake ilikuwa ni ndogo mno kutokana na wingi huo wa watu waliokuwa wakizitembelea.Mara ya mwisho kwa mtandao kukumbwa na idadi kubwa namna hiyo ni tukio la kuapishwa Barack Obama.


Kwa mujibu wa MZEE WA CHANGAMOTO,Hasheem Thabeet amenyakuliwa na klabu ya mpira wa kikapu ya Memphis Grizzlies katika draft ya NBA.

Hii ni miongoni mwa njia mwafaka-na nafuu-za kuitangaza Tanzania.Kila la kheri Hasheem.Mafanikio yako ni zaidi ya kufanikiwa kimichezo,umeingia kwenye orodha ya vitambulisho vya Tanzania kama vile Mlima Kilimanjaro,madini ya Tanzanite (japo mafisadi wamepania kuyamaliza kama walivyomaliza dhahabu ilivyo huko Tulawaka),Hifadhi ya Selous na vivutio vinginevyo.Kuna cha zaidi kuhusu mafanikio yako.Umevunja "utamaduni" wa Kitanzania wa ku-settle for less.Angalia timu yetu ya taifa,kwa mfano.Tumekuwa na Maximo kwa muda sasa,na wajuzi wa michezo wanatuambia tumepiga hatua.Kupiga hatua kwa kutoka sare na Senegal?Angalia Simba na Yanga,kila msimu wanahangaika na "wachezaji wa kimataifa",lakini huhitaji kuwa mtaalam wa soka kumaizi kuwa ma-pro" hao ni wababaishaji tu na hawajasaidia kuzifanya klabu hizo zitambe katika anga za soka la kimataifa (na tunaambiwa kocha wa Yanga ni profesa wa soka!Lakini msimu wa pili huu hakuna kombe la kimataifa na wana-Yanga wameridhika,sio na mafanikio ya klabu yao bali kuwa na kocha mgeni "profesa wa soka").Angalia baadhi ya mitazamo yetu.Shangwe na vigelegele tukisikia Zeutamu kakamatwa ilhali majambazi wa Kagoda bado wanapeta,na huku tukizugwa kuwa eti ufisadi wa Meremeta na Tangold ni siri za taifa! (Na kweli ni siri maana ni nadra kwa wizi kufanyika hadharani).

Mafanikio yako yanaweza kuwa chachu kwa Watanzania wengine kuondokana na unyonge wa kifikra kwamba kila baya linalotusibu ndio destiny yetu.Na ni kwa namna hiyo ndio mafisadi wanazidi kutufisadi kwa vile wanatambua unyonge na udhaifu wetu wa kukubali matokeo kirahisi.

Hongera sana,Hasheem.Sote tunajivunia jina lako.


Hili ndio "BUNGE LENYE MENO"!Juzijuzi mbunge mmoja wa CCM kaomba Mungu alilaani Baraza la Mawaziri kwa kushindwa kutimiza majukumu yake.Mwingine kadai serikali ina ugonjwa na inahitaji maombezi (na kwa kawaida magonjwa yanayohitaji maombezi ni yale yasiyotibika kama vile ukimwi,nk).Jana mbunge mwingine wa chama hicho tawala amewafananisha mawaziri na mbwa.Na pengine moja ya mambo yatakayokumbukwa zaidi katika historia ya bunge letu tukufu ni jinsi kikao hiki cha bajeti kinavyoonekana "mwiba mkali" kwa mawaziri,at least according to walio mahiri katika kuripoti pasipo kusoma kati ya mistari (reading between the lines).

Sina maneno ya huruma kwa baadhi ya wabunge hawa wa CCM.Ni wanafiki wanaohangaika kutumia vizuri nafasi hizi za mwisho mwisho kujitengenezea mazingira ya kurejea bungeni hapo mwakani.Lakini ili haki itendeke,ni vema kuwatofautisha wanafiki hawa kwa makundi.Kuna kundi la wabunge waliojitokeza mapema (kabla hata ya joto la uchaguzi wa mwakani halijaanza kupanda) kukemea ufisadi na vitendo vingine vinavyokwaza maendeleo ya taifa letu.Sio siri kwamba wabunge kama Selelii,Kimaro,Killango,Mwambalaswa,Mwakyembe na wengineo wamejitokeza kuwa sauti adimu ndani ya CCM dhidi ya ufisadi.Na tunafahamu vituko wanavyofanyiwa na watu walewale wanaopaswa kuwaunga mkono.

Kundi la pili ni la wababaishaji walio njia panda; upande mmoja hawana nia ya dhati ya kupambana na ufisadi au pengine ni sehemu ya mfumo unaodumisha ufisadi,upande mwingine wanafahamu fika kwamba miongoni mwa ajenda za uchaguzi mkuu ujao ni ufisadi na namna wawakilishi wetu walivyoshiriki katika mapambano dhidi ya ufisadi.

Pia kuna makundi mengine mawili: la kwanza linajumuisha wababaishaji wanaokwenda bungeni kwa vile tu ndio mahala pao pa kuchuma shs 7,000,000/= za mshahara kiulaini.Hawachangii hoja,hawaongei lolote japo si mabubu,wapo wapo tu.Kuwepo au kutokuwepo kwao bungeni hakutambuliki kwa vile wanaongeza tu idadi ya wabunge.Kundi la pili ni la watetezi wa ufisadi.Hawa ni wepesi wa kuomba mwongozo wa Spika kila maslahi yao au ya wadau wenzao wa ufisadi yanapoguswa.Nadhani mmesikia "Dokta" Mzindakaya alivyotumia Maandiko Matakatifu kutetea ufisadi .Ila hawa wanaocheza na vitabu vya Mungu,nadhani ndio wanaostahili kulaaniwa zaidi kwani wamevigeuza kama manifesto za usanii wao wa kisiasa!

Uzuru wa makundi haya mawili ya mwisho-la tatu na la nne-ni kwamba angalau yanajumuisha wabunge tunaofahamu wanaposimamia.Aidha ni wazembe na mabubu wasioongea (aidha kwa aibu ya kuongea,au "heri mie sijasema",au uzembe tu) au ni watetezi wa mafisadi.Hawa si wanafiki as such kwa vile wameji-identify kwetu kuwa ni viumbe wa namna gani.

Tofauti kati ya makundi hayo ni ndogo mno contrary to inavyosomeka na kusikika kwenye vyombo vya habari.Hapa nataka kuzungumzia makundi mawili ya mwanzo-la kwanza na la pili.Hawa wote ni wana CCM,na kwa namna yoyote ile hawawezi kujitenganisha na matatizo yanayosababishwa na chama hicho tawala.Na hili si la kufikirika kwa sababu tayari wengi wa wabunge wa kundi la kwanza wamekuwa wakikumbana na kadhia mbalimbali kutokana na msimamo wao dhidi ya ufisadi,na guess what,kadhi hizo ni kutoka kwa wenzao ndani ya CCM.

Mawaziri wanaolaaniwa na kufikia hatua ya kuitwa mbwa wanatoka CCM pia.Hii sio vita ya wenyewe kwa wenyewe kama inavyoweza kutafsiriwa kiuzembe.Huu ni unafiki,period.CCM isingefika hapo ilipo laiti "wapambanaji hawa" wangekuwa na mkakati wa dhati wa kuleta mabadiliko ya kweli.Wanachofanya muda huu ni cha kibinafsi zaidi kuliko kitaifa.Wanaweza kurudi bungeni hapo mwakani baada ya wapiga kura wao "kuzugika" na CVs za wawakilishi wao tangu 2005 hadi 2010.Kurudi kwao bungeni kutapelekea CCM kuendelea kuwa yenye wabunge wengi bungeni,na hivyo kupelekea kuendelea kwa haya tunayopigia kelele kila siku.

Siamini kama kuna mkakati kwa Selelii na wenzake kuleta mageuzi ndani ya CCM.So far,kelele zao hazijasaidia kukitenganisha chama hicho na ufisadi,implying that kelele zao zimebaki kuwa kelele tu.Wana options mbili: waendelee kupiga kelele lakini wabaki kuwa sehemu ya chama kinachohusishwa na ufisadi au wajondoe ndani ya chama hicho na hivyo kubainisha kuwa kuwa kwao ndani ya CCM ilikuwa ni sehemu tu ya maisha yao ya kisiasa lakini cha muhimu zaidi kwao ni Tanzania na ustawi wa Tanzania.Yes,si lazima kuwa mbunge wa CCM ili kupata fursa ya kupigania maslahi ya taifa.Mifano hai ipo;Dkt Slaa,Zitto Kabwe,nk sio wabunge wa CCM,lakini sote tunafahamu michango yao katika kupambana na ufisadi.

Unafiki wa wabunge hao wa CCM unasababishwa na kitu kimoja kisicho na msingi: UBINAFSI WA KISIASA.Ni hivi,kwa CCM,umoja na mshikamano ndani ya chama hicho ni muhimu zaidi kuliko umoja na mshikamano wa taifa.Na hilo ni matokeo ya chama hicho kuamini kwamba ni chenyewe tu kinachoweza kudumisha mshikamano na umoja wetu.Kwa lugha nyingine,kimebinafsisha uwezo,dhamira,jitihada na nguvu za Watanzania zaidi ya milioni 35 ambao si wanachama wa chama hicho (takwimu za karibuni zinaonyesha idadi ya wanachama wa CCM ni takriban milioni 4 tu).Japo ni kweli kwamba chama hicho kimetoa uongozi uliosaidia kudumu kwa amani na mshikamano huo,Watanzania wenyewe ndio waliofanya kazi ya msingi zaidi kufanikisha hilo.Upendo na upole wetu (ambao mara nyingi umeishia kutumiwa vibaya na wanasiasa walafi) ndio sababu kuu ya kwanini tumeendelea kubaki kisiwa cha amani (kwa maana ya kutokuwa vitani).

Ni ubinafsi wa kisiasa unaopelekea CCM kuweka mbele maslahi ya kisiasa badala ya maslahi ya taifa.Sote tumeshuhudia mara kadhaa wabunge wa chama hicho tawala wakiitisha vikao "vya kuwekana sawa" kila zinapojiri hoja nzito bungeni.Kuwekana sawa kwa maslahi ya nani?Hivi cha muhimu ni hoja ipite tu au ipite ili ilete mabadiliko chanya kwa wananchi?

Lakini ili upate mfano sahihi zaidi kuhusu ubinafsi wa wabunge hawa ni pale Dkt Slaa alipotamka bayana kwamba mishahara ya wabunge ni mikubwa mno kulinganisha na hali halisi ya uchumi wetu.Kwa umoja wao (huku wakipata sapoti kutoka kwa wabinafsi wengine waliojificha kwenye vyama vya upinzani) walimzomea Dkt Slaa na kumzongazonga kana kwamba kawatukana.Hivi ina maana wabunge hawa wanaotuzuga kuwa wanatetea maslahi yetu hawaelewi kuwa wakati wao wanazawadiwa takriban shilingi 7,000,000/= mwezi (wastani wa shilingi laki 230,000/= kwa siku sawa na takriban shs 10,000/= kwa saa) takriban Watanzania 36,000,000 wanaoishi kwa chini ya shilingi 3000/= kwa siku?

Hadi kufikia tamati yake na mabiloni kadhaa kutumika,kikao hiki cha bajeti kitashuhudia kila aina ya vituko kutoka kwa wanafiki hawa.Ukidhani hizo dua dhidi ya mawaziri na "matusi" ya kuwaita mbwa ndio hatua kali kabisa,subiri usikie "makombora" zaidi.Na kama kawaida ya vyombo vyetu vya habari,kurasa zitapambwa na maneno mazito kama "Bunge moto juu","Wabunge wachachamaa",na ubabaishaji mwingine kama huo.Lakini pamoja na yote hayo,makadirio ya wizara za mawaziri wanaoombewa dua mbaya na kuitwa mbwa yatapitishwa na wabunge haohao wanaotuzuga kuwa "wana hasira na mawaziri".

25 Jun 2009


Breaking News hii ni kwa mujibu wa TMZ.COM ambapo wanaeleza
Michael Jackson Dies

Posted Jun 25th 2009 5:20PM by
TMZ Staff

We've just learned Michael Jackson has died. He was 50.
Michael suffered a cardiac arrest earlier this afternoon at his Holmby Hills home and paramedics were unable to revive him. We're told when paramedics arrived Jackson had no pulse and they never got a pulse back.

A source tells us Jackson was dead when paramedics arrived. A cardiologist at UCLA tells TMZ Jackson died of cardiac arrest.

Once at the hospital, the staff tried to resuscitate him but he was completely unresponsive.
We're told one of the staff members at Jackson's home called 911.La Toya ran in the hospital sobbing after Jackson was pronounced dead.Michael is survived by three children: Michael Joseph Jackson, Jr., Paris Michael Katherine Jackson and Prince "Blanket" Michael Jackson II.

Story developing...

24 Jun 2009

Pichani,Berlusconi akijifuta jasho baada ya kutwanga swali kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga kuhusu tuhuma zinazoweza kuotesha nyasi ndoa yake na mkewe anayeonyeshwa kwenye background.

Waziri Mkuu wa Italia,Silvio Berlusconi,amekanusha madai kwamba alinunua huduma ya tendo la ndoa kwa changudoa mmoja,Patrizia D'Addario.Kiongozi huyo machachari na mwingi wa vituko,anakabiliwa na shinikizo la kisiasa kufuatia madai hayo ya kujimwayamwaya na kimada aliyekuwa miongoni mwa waliohudhuria pati iliyoandaliwa na Berlusconi.

Hadhi ya mwanasiasa huyo tajiri imekumbwa na migogoro lukuki,na hivi karibuni alikuwa na tuhuma za kuvunja amri ya sita na binti wa miaka 18,Noemi Letizia (pichani chini)


Kwa jeuri,Berlusconi amekanusha madai ya kununua ngono huku akikisitiza kwamba "Sijawahi kuona raha ya kununua ngono badala ya ujasiri wa kutongoza".
Vyama vya upinzani pamoja na Kanisa Katoliki wanamtaka Berlusconi kujieleza kuhusiana na skandali hiyo iliyoibuliwa na tume moja ya kuchunguza rushwa huko Italia ya kusini,ambapo inaelezwa kwamba kimada mhusika (kushoto,pichani chini) aliieleza tume hiyo kuwa alilipwa na Berlusconi ili kumpa huduma ya ngono na ana mkanda uliorekodi tukio hilo.

Yote haya yanajiri wakati mke wa Waziri Mkuu huyo akiwa kwenye taratibu za kuomba talaka huku akimtuhumu mumewe kwamba anapendelea sana dogodogo.

CHANZO: itn

Na sie tungekuwa na uhuru wa kuweka ishu kama hizi hadharani,sijui nani angesalimika among vingunge wetu!

Kontebo wa Polisi,Tariq Dost (pichani juu) amefungua mashtaka dhidi ya mwajiri wake na Mamlaka ya Polisi ya eneo la Midlands,hapa Uingereza, kutokana na matamshi ya mwaka 2007 kwamba anafanana na gaidi nambari wani Osama bin Laden (pichani chini).Nadhani kisa ni huo "mzuzu".Je wanafanana?
CHANZO: The Daily Mail


Slaa up in arms on 'silencing' in House
By Faraja Jube Dodoma

Karatu MP Willibrod Slaa has threatened to "go public" with what he said were issues of national interest the Parliament blocked him from tabling in the august House on Monday.

Some MPs heckled the firebrand opposition leader as he stood up in parliament on Monday to give a speech on the Prime Minister's Office 2009/10 Budget.

Dr Slaa had reportedly prepared a vitriolic attack on former President Benjamin Mkapa and the Government over alleged mismanagement of funds.

Before giving his speech, the Chadema leader was reminded to respect the Parliamentary Standing Orders and warned not to breach the law in his presentation.

But in an interview with The Citizen yesterday, Dr Slaa said the National Assembly Speaker, Mr Samwel Sitta, had no right to block debate on sensitive public issues.

He said: "I have written to the Speaker asking him why unnecessary restrictions are being imposed on MPs who want to discuss matters of public interest in parliament."

He threatened to go public with the same issues he was barred from presenting in parliament saying he had the right to let people know about matters that affected them.

"If they don't want us to speak in parliament, it will reach a point where the only reasonable thing to do is table the agenda to the people," said Dr Slaa.

CCM MPs accused the opposition legislator of attempting to use the platform to launch a verbal attack against Mr Mkapa.

Mr Mudhihir Mudhihir (Mchinga-CCM) defended the former president saying he had done "a lot of good things but people want to see the negative only".

"It was under his leadership that this country recorded significant increases in Government revenue," the MP said, praising Mr Mkapa's administration for containing inflation and opening a number of trade opportunities.

Another CCM legislator, Dr Chrisant Mzindakaya (Kwela), tried to have Dr Slaa blocked from presenting his speech at all.

But even when he finally gave his speech, the opposition leader was forced to skip tabling his prepared questions on controversial deals the Mkapa administration allegedly signed.

And in an apparent reference to Dr Slaa, Dr Mzindakaya lashed out at "jealousy hypocrites and good-for-nothing crusaders against corruption".

"Those who criticise Mr Mkapa are agents of the Devil and loafers who have done nothing in life, but are motivated by jealousy and hatred. They are themselves corrupt people," he said.

But Dr Slaa insisted he would not relent on the issues he was barred from talking about saying the Constitution and Parliamentary Immunities and Privileges Act guarantee MPs the freedom to challenge the Government in the parliament.

"I will not accept such moves by anyone any more. This is all compromising principles. But I will stand up for my principles and for justice. We all have the right voice our concerns," he said.

Dr Slaa, who had prepared his disputed speech as a shadow minister, said the Government was obliged to respond to all queries raised by MPs in parliament.

"Even if the issues are sensitive, this is the whole purpose of raising them so that people can know and be informed about what is going on," he said.

"But there has been a tendency to block all sensitive issues from being discussed in parliament," he added.

Before he gave his controversial speech, Mr Sitta told the opposition MP he had read the speech and warned him against making statements that breached parliamentary regulations.

The Speaker had also ordered Dr Slaa not to use abusive language against a former president or discuss issues that had been lined for debate during the session.

Earlier, the chairman of the Parliamentary Committee on Justice, Constitutional Affairs and Governance, Mr George Lubeleje, a CCM MP, had tabled the committee's position against Dr Slaa's speech.

However, the opposition leader retorted: "Why must I have any confidence in the committee or Speaker's office if they insist on imposing on us?"

He questioned the Speaker's application of the Parliamentary Standing Orders to the contentious issues of Meremeta, Tangold, Mwananchi and Deep Green Finance companies.

Last Friday, Dr Slaa asked the Government to respond to allegations of funds mismanagement involving the four companies that have become subjects of public debate.

"I was just questioning the Government over the embezzlement of Sh155 billion in Meremeta and not about the issues pertaining to national security," he said.

Mr Sitta postponed the debate to this Monday saying the Government should be given time to prepare its response.

But Dr Slaa also questioned the Parliament barred debate on the CAG report. "Where does the Speaker obtain the directive to block the debate?"

On the PMO's 2009/10 Budget estimates, the Chadema leader queried the allocation of billions of shillings to entertainment and hospitality, which he said had nothing to do the welfare of people.

He had to put up with sporadic interventions, mainly from Mr Philip Marmo, the minister of State in the President's Office (Good Governance), who also serves as coordinator of parliamentary activities.

Mr Marmo wanted, among other things, the Speaker to reprimand Dr Slaa for his reference to the amount of funds set aside for particular votes in the Government's Budget.

However, Mr Sitta said there was nothing wrong with the MP debating the Government's budget priorities.


SOURCE: The Citizen


Kama hujawahi kuhudhuria matamasha au maonyesho ya wasanii wetu huko Bongo,wala usidhani ume-miss raha pekee.Kuna karaha pia,hususan ile inayotokana na mastaa wetu kudekezwa kupita kiasi na vyombo vya dola.Kwa kifupi,huko ni bangi nje nje,wasanii hugeuka madikteta wanaoweza kufanya lolote lile hadharani ikiwa pamoja na unyanyasaji wa waziwazi dhidi ya dada zetu.Na baada ya "unga" kugeuka "kilevi cha kawaida",wengi wa wasanii hao hujitundika madawa hayo vya kutosha pasipo hofu ya kuchukuliwa hatua na vyombo vya dola.

Nadhani wapo wanaokumbuka msanii mmoja wa bongefleava aliyekamatwa na bangi katika mkoa mmoja wa nyanda za juu kusini.Ni Daz Baba wa kundi lililokuwa likijulikana kama Daz Nundaz.Iliishia kuwa amekamatwa tu,wala hakukuwa na taarifa za msanii hiyo kufikishwa mahakamani au hata kupewa onyo (si lazima kila kosa limaanishe kifungo).

Twende kwa baadhi ya marapa maarufu Msafiri Diouf na Banza Stone.
Haihitaji upelelezi kujua kuwa wanatumia kilevi haramu,lakini dola haijihangaishi kuwachukulia hatua ambazo licha ya kuwaadhibu zingesaidia pia kuokoa maisha yao kwani ni dhahiri kwamba mwisho wao sio mzuri.

Kuna msanii anaitwa Chid Benz.

Licha ya sifa yake ya kufanya vizuri zaidi anaposhirikishwa kwenye nyimbo za wasanii wengine (wanaita "kolabo" as corruption ya neno collaboration) zaidi ya nyimbo zake mwenyewe,mwanabongofleva huyo ni maarufu pia kwa vurugu na vipigo kwa wasanii wenzie.Dola imeendelea kumwangalia tu,hali inayoweza kupelekea Chid Benz kuamini kuwa yuko juu ya sheria kutoa kipondo kwa yeyote yule anapojiskia kufanya hivyo.

Leo,kwenye tovuti ya Global Publishers kuna habari kwamba msaanii Khaleed Mohammed,almaaruf T.I.D,amemjeruhi mwanafunzi mmoja wa kike baada ya kumshushia kipigo cha nguvu.Kwa mujibu wa tovuti hiyo,T.I.D nasakwa na polisi na "hajulikani alipo".Nisingependa kutoa hukumu kwa vile mie si mahakama,lakini napenda kukiri kwamba nilishangazwa na habari kwamba msanii huyo alikuwa miongoni mwa waliopewa msamaha na Rais katika maadhimisho ya siku flani ya kitaifa.

Sikushangaa kwa vile aliyesamehewa ni T.I.D,bali vigezo vilivyotumika kumpa msamaha huo.Kwa tunaofahamu ukweli kuhusu kesi hiyo,yayumkinika kuwa maombi ya msahama ya mtenda kosa kwa waliotendewa kosa yalisikilizwa,na kwa vile waliotendewa kosa ni "wenye kuwezesha jua liwake au lisiwake",yaani "the powers-that-be",msanii huyo akajumuishwa kwenye msamaha wa Rais.

Tukio hili la sasa ambapo T.I.D amerejea kosa lilelile lililompeleka jela in the first place,sio tu linazidisha hisia kuwa wengi wa wasanii na mastaa wetu wanaringia ugoigoi wa wanadola wetu katika kuchukua hatua inapostahili,bali pia ni fedheha na aibu kwa suala zima la msamaha wa rais.Navyofahamu,msamaha huo huzingatia tabia ya mfungwa,afya yake,idadi ya siku zilizosalia katika kifungo chake,na pengine kikubwa zaidi,mwenendo wake pindi akipewa msamaha huo.

Ni dhahiri kwamba jinsi jeshi la Magereza "lilivyojichokea" si rahisi kwake kukamilisha vigezo hivyo vyote.Na katika jamii ambayo mwenye fedha ni mithili ya mungu-mtu huku ufisadi ukishamiri kila kukicha,yayumkinika kuamini iwamba misamaha ya rais imekuwa ikitumika ndivyo sivyo.

Hivi tunajenga jamii ya aina gani?Wkati wenzetu katika nchi zilzoendelea wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa kudhibiti uvutaji wa sigara katika maoneo ya mikusanyiko,sie tunaelekea kuruhusu uvutaji wa bangi kana kwamba ni kitu halali.Nilisoma mahala flani kwamba msanii mmoja wa filamu za kibongo alichomoa bastola hadharani kisa wapita njia walimlalamikia kwa kupaki gari lake barabarani.

Jeuri hii wanaipata wapi?

Hypothesis yangu ni hii: itikadi ya ujamaa iliifanya sehemu kubwa ya Watanzania kuwa wanyonge wasio na stahili ya kuwa karibu na makundi yenye nguvu au mvuto kwenye jamii hiyo e.g. wanasiasa,wasanii,nk.Japo tunadai kuwa ujamaa umekufa,mentality ya itikadi hiyo bado iko hai na inatuathiri katika namna tunavyodili na watu hao walio kwenye "makundi maalumu" kwa mfano "mastaa wetu".Polisi wa trafiki anajiuliza mara mbilimbili "kuipiga mkono" Benz au Vogue,kwa vile akilini mwake,dereva wa gari hilo ola thamani anaweza "kuhatarisha ajira yake".Mtaani,msanii anageuka "mungu-mtu",wananchi wanatamani kuwa karibu nae,angalau kugusana mabega nae,wanadola wanachelea kumchukulia hatua (pengine kwa kudhani kuwa kwa vyovyote vile msanii hiyo atakuwa na connection na mtoto wa kigogo flani),na upuuzi mwingine kama huo.

Sio kwamba ujamaa ni mbaya per se.Kuna mazuri flani,ila hapa nimezungumzia legacy ya itikadi ya ujamaa katika upande hasi.Pengine kunahitajika mjadala wa kitaifa kutafakari mambo kama haya.

UNAONAJE?

23 Jun 2009

Pichani,Mwanasoshojia akimuaga Mzaa chema.

BLOGU HII INATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUTOKANA NA KIFO CHA MAMA MZAZI WA BLOGA MWANASOSHOLOJIA.HAKUNA MANENO MWAFAKA YANAYOWEZA KUKULIWAZA WEWE BINAFSI NA FAMILIA YENU KWA UJUMLA,LAKINI TUAMINI KUWA MUNGU AMEMPENDA MAREHEMU ZAIDI YETU,NA NDIO MAANA AMEMCHUKUA.NA KWA VILE MUNGU NI WA UPENDO,BASI TUNA HAKIKA ATAMPATIA MAREHEMU PUMZIKO LA AMANI NA RAHA YA MILELE.

POLE SANA,MWANASOSHOLOJIA.

Dunia haina dogo.Kuna wambeya wanaodai eti huyo "nzi" alikuwa ni skadi lililotumwa na Dick Cheney kwa Obama.Kuna wengine wanadai huyo wala hakuwa "nzi" bali roboti lilotengenezwa na majasusi wa Kimarekani kupeleka ujumbe kwa Kim Jong Ill na mikwara yake ya nyuklia.Wapo wanaomhusisha "nzi" huyo na uchaguzi wa Irani..... Alimradi burudani!

ELEKEZO: Neno "nzi" limetumika kama tafsiri isiyo rasmi ya "fly" (BAKITA mko wapi?)


Inakera ati!hususan kwa simu vimeo zinazokula chaji kama hazina akili nzuri.Wajuzi wa simu wanadai kwamba baadhi ya simu "zina allergy na full charge",yaani chaji haidumu.

Taarifa zinaeleza kwamba maabara ya Kampuni ya Nokia hapo Cambridge wanatafiti ujio wa simu itakayokuwa ikijichaji yenyewe.Badala ya kutumia chaja za kawaida,simu hiyo itakuwa ikijichaji kwa kugema nishati kutoka kwa mawimbi ya radio (radio waves) yanayotoka kwenye antena,milingoti ya televisheni,Wi-Fi transmitters,nk.

CHANZO: The Guardian


The British National Party could face legal action over its 'whites only' membership policy, a watchdog said yesterday.The party could be taken to court for three counts of discriminating on grounds of colour, the Equalities and Human Rights Commission said.

If the BNP refuses to allow non-whites to join the party, it could face heavy fines, or its assets could be seized - making it almost impossible for them to fight elections effectively.

Senior party members, such as leader Nick Griffin, could even be imprisoned, if the courts so decided. The move comes two weeks after the BNP won its first seats in the European Parliament following a collapse in Labour support. The party has around 60 councillors across the country.

Their constitution says only those with 'indigenous Caucasian' racial backgrounds can become members of the party. It is believed to be the first time that race watchdogs have threatened a political party with legal action.

The commission said the party appeared to be guilty of three breaches of the Race Relations Act: not allowing non-whites to join the party, not allowing them to take jobs at the party, and not providing equal services to constituents based on the colour of their skin.

They said this amounted to discrimination on the grounds of race and colour, which is banned under the act.The EHRC called on the BNP to provide written undertakings by 20 July that it will make the required changes or it could face a legal injunction. If not they could bring a civil action against them at the High Court.
If the party still did not comply, judges could find it guilty of contempt of court, which could lead to fines or even jail for BNP leaders.

A spokesman for the watchdog said: 'This exclusion is contrary to the Race Relations Act which the party is legally obliged to comply with. The commission therefore thinks that the BNP may have acted, and be acting, illegally.

'The commission has required the BNP to provide a written undertaking that it will not discriminate contrary to the Race Relations Act in its employment and recruitment policies, procedures and practices.'

The commission said it was also concerned that the BNP's elected representatives may not intend to offer or provide services on an equal basis to all their constituents and members of the public irrespective of race or colour.

John Wadham, the Commission's legal director, said: 'The legal advice we have received indicates that the British National Party's constitution and membership criteria, employment practices and provision of services to constituents and the public may breach discrimination laws which all political parties are legally obliged to uphold.

'We await a response from the BNP to our letter before deciding what further action we may take. Litigation or enforcement action can be avoided by the BNP giving a satisfactory response to our letter.'
The commission has received around 50 calls from members of the public recently about the BNP's membership policy, although it is believed that officials were already looking into the issue.

But last night BNP leader Nick Griffin, who was elected as an MEP for the north west of England earlier this month, said the party's rules were 'entirely legal', adding: 'We are not discriminating on the grounds of colour'.

He claimed the party was an exempted organisation under the Race Relations Act, which protected organisations which represented minority groups.Mr Griffin said this meant 'ethnic groups who need special protection such as the English in their own country, who are now second class citizens' were 'entitled to discriminate on that basis and not on the grounds of colour'.

A spokesman for the BNP said: 'We are not going to respond to threats like this. We will look at it, but it is an entirely politically-motivated attack. 'I don't think we should be bullied by outside forces. They are asking us to change our whole political ideology.'




Pengine siendi na wakati.Pengine mgumu wa kuelewa.Pengine....well,pengine sina hoja bali naibua tu cha kuropoka.All in all,mie ni miongoni mwa sijui wengi au wachache ambao hizi SIKU MAALUM hazina umuhimu kihivyo.Tuanze na siku ya kuzaliwa (BIRTHDAY).Mie nilizaliwa tarehe inayofanana na siku ya Uhuru na Jamhuri,yaani 9 Desemba (mwaka sabini na kitu).Excuse yangu kubwa ya "kuipuuza" birthday yangu huwa "tayari taifa linasherehekea pamoja nami".Si unajua 9 Desemba huwa ni mapumziko huko home?Halafu maswala ya gwaride na vikorombwezo vingine.Well,inatosha kuwa kiji-excuse cha namna flani.La muhimu kwangu katika kila 9 Desemba ni kumshukuru Mungu kwa kunifikisha siku hiyo,kisha kuongea na wazazi.Baba na marehemu mama walijenga utaratibu wa kutuimbia wimbo wa hepi bethdei to yuuu...That's it.Sala,wimbo na dua za wazazi,siku imekamilika.Hizo habari za birthday parties ni msamiati ambao haujaingia kwenye kamusi yangu.


Kuna kitu inaitwa MAHAFALI.Well,sikumbuki vyema kuhusu mahafali ya kumaliza darasa la saba lakini natambua kuwa ilikuwa mbinde hapo Ifakara.Uchumi wa familia haukuruhusu anasa zisizo na msingi,na wakati huo (1985) taifa nalo lilikuwa katika wakati mgumu vilevile.Si zamani kihivyo.lakini mengi ya yanayoonekana leo hayakuwepo zama hizo.

Nadhani kitu pekee nachokumbuka kuhusu mahafali ya kumaliza kidato cha nne ni uamuzi nilokuja kuujutia baadaye wa kuonja kilevi cha kiwandani.Nilijaribu bia aina ya Safari Lager kwa mara ya kwanza maishani.Of course,kabla ya hapo nilishawahi kujaribu kilevi cha asili cha pombe ya mpunga.Ili nisije sahau,ni vema nikujulishe kidogo kuhusu pombe hii inayonukia kama wali.Kwa kifupi,ukiinywa saa 10 jioni basi inakuwa kichwani hadi kesho saa 10 jioni.Well,at least kwa "vichwa panzi" kama nilivyokuwa siku hizo.

Basi hiyo Safari Lager ilinipelekesha kupita maelezo.Nadhani nilifanya vituko kadhaa lakini kumbukumbu zaidi niliyonayo ni kuugua kwa takriban wiki hivi.Ungetegemea kuwa hiyo ndio ingekuwa mara yangu ya kwanza na ya mwisho kugusa kilauri.Wapi!Ukiniuliza namna gani niliweza kuji-transform kutoa mnywaji anayeugua wiki nzima baada ya kunywa bia moja hadi kufikia hatua kummudu John Mtembezi (John Walker),sidhani kama nitakuwa na jibu sahihi.

Anyway,mahafali ya kidato cha sita hata sikumbuki yalikuwaje.Shule yenyewe ilikuwa ya kijeshi (Tabora Boys) halafu nilikuwa miles away from home.Mahafali kwa maana ya mahafali yalikuwa ya kuhitimu Mlimani (UDSM).Kuna waungwana walishauri nitengeneze kadi za mchango wa sherehe ya mahafali.Well,it worked.Watu wakapiga donation,likapatikana fungu la kufanya sherehe ya maana mtaa wa Isisi,Kinondoni.Na kuna mahala flani walinisaidia bia za bei nafuu.

Hapa Aberdeen nilijichukulia tu vyeti vyangu hapo 2003 na 2004.Ila nikikamilisha libeneke hili la sasa,huenda nikajumuika na watu wawili watatu maana hii ya sasaa ni shughuli nzito kwa kiasi kikubwa.

Back to the topic.Sijui Father's Day ni leo au kesho au ishapita.Honestly,muda huu naoandika post hii sina hakika,na sitaki kuhakikisha kwa ku-google.Kwangu,siku ya Baba yangu (na kama ilivyokuwa kwa Mama yangu) ni kila siku.Najua kwanini kuna siku moja maalumu,lakini kwa mie kila siku ni maalum.Yaleyale ya siku ya Wapendanao.Nikimpenda mwandani wangu basi ni suala la kila siku na Ferbuari 14 inakuwa siku kama siku nyingine tu.Of course,nimeshawahi kuonekana kichekesho huko nyuma lakini hainisumbui.

Vipi,huu mtazamo wangu unaouonaje?Ukale,uzembe wa kwenda na wakati,sahihi au you dont even care?


Na Ramadhan Semtawa, Dodoma

SERIKALI imesisitiza kuwa haiwezi kuruhusu suala la kampuni ya Buhemba Goldmine (Meremeta), kujadiliwa hadharani kwa kuwa inahusu mambo ya usalama wa taifa, lakini ikaeleza kuwa suala la ukaguzi wa Mwananchi Gold linasubiri wakati mwafaka kwa kuwa kwa sasa inafilisiwa.

Kauli hiyo ilitolewa Bungeni jana na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari wakati akijibu swali la mbunge wa Karatu, Dk Willbrod Slaa, aliyetaka kujua sababu za kampuni hizo kutokaguliwa.

Kauli hiyo pia imetolewa siku moja baada ya kuripotiwa kwa taarifa kuwa, Bunge limemwagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG), kuyakagua mashirika hayo tata yanayohusishwa na upotevu wa mabilioni ya fedha za walipakodi.

Swali hilo lilitakiwa kujibiwa Ijumaa iliyopita, lakini Spika Samuel Sitta aliliahirisha hadi jana.

Akitoa majibu ya serikali, Waziri Sumari alisema msimamo kuhusu Kampuni ya Meremeta ulishawekwa bayana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati wa kikao cha Bunge cha mwaka jana aliposema kuwa, suala hilo haliwezi kujadiliwa kwenye chombo hicho cha kutunga sheria kwa sababu linahusu usalama wa nchi.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema yuko tayari kusulubiwa kuliko kuizungumzia Meremeta kwa kuwa inahusu usalama wa taifa.

Waziri Sumari alirejea kauli hiyo ya Pinda akitaka iheshimiwe na kwamba asingeweza kueleza chochote kuhusu Meremeta na badala yake angetoa majibu ya Kampuni ya Mwananchi Gold peke yake.

Hatua hiyo ya serikali kutangaza uamuzi huo inaonekana kwenda kinyume na Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2008 inayompa CAG, ambaye anawajibika kwa Bunge, mamlaka ya kufanya ukaguzi bila ya kuagizwa.

Sumari pia alisema: “Makampuni mengine yote yenye uhusiano na Maremeta kama alivyosema mheshimiwa waziri mkuu hayatajadiliwa hadharani na serikali haioni sababu ya kufanya ukaguzi."

Baada ya majibu hayo, Dk Slaa alisimama tena kuulizwa swali la nyongeza na kudai kuwa hakuwa amejibiwa chochote na wakati akiendelea kuuliza kuhusu Meremeta, Spika Sitta alisimama na kumzima.

“Mheshimiwa Dk Slaa, suala la Meremeta linahusu jeshi. Tulikaa kwenye Kamati ya Uongozi tukakubaliana kwamba suala hili lisizungumzwe hadharani. Waziri Mkuu alishalisema; nafikiri na wewe ulikuwepo, kwa hiyo sitakuruhusu kuuliza chochote kuhusu Meremeta. Uliza makampuni hayo mengine ya Mwananchi Tangold," alisema Spika Sitta na kuipa serikali ahueni.Lakini Dk Slaa akajibu na kusema: “Siulizi Jeshi, nauliza wizi.” Lakini Sumari akamjibu kwa kusema: "Na wewe pia (Dk Slaa) tafuta hoja nyingine..."

Taarifa zinadai kuwa, Meremeta ni kampuni ambayo ilianzishwa ikimilikiwa kwa asilimia 50/50 baina ya serikali na kampuni ya Trinnex na kuna tuhuma kuwa Benki Kuu (BoT) ililipa zaidi ya Sh155 bilioni kupitia benki moja ya kigeni bila ya kufuata taratibu, kwa mujibu wa taarifa ya ukaguzi ya CAG ya kipindi kinachoishia Juni 30, 2006.

Kuhusu Mwananchi Gold, Sumari, alisema kwa sasa iko katika mchakato wa kufilisiwa.Hata hivyo, alisema ni mapema mno kuzungumzia mchakato huo, bali alitaka wabunge, akiwemo Dk Slaa kuvuta subira na muda mwafaka utakapofika wataelezwa.

Mwishoni mwa wiki, CAG aliiambia Mwananchi kuwa amepata barua kutoka Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma inayomtaka azikague kampuni hizo tata, lakini akasema bado hajapanga ataanza lini kuzikagua.

Barua hiyo yenye kumbukumbu BC.50/155/06/98 inamtaka CAG afanye ukaguzi maalumu ili kubaini thamani ya mtaji na hisa za serikali katika makampuni hayo tata na pia aieleze kamati sababu za kampuni hizo kutokaguliwa.

Awali, Dk Slaa alimuuliza Waziri wa Fedha na Uchumi ni sababu gani za msingi zilizofanya kuchukua muda mrefu kuanza ukaguzi kwa kampuni hizo hata pale tuhuma hizo zilizopigiwa kelele na jamii na hata kamati mbalimbali zilizoundwa kuchunguza tuhuma hizo.

Katika swali hilo namba 76, Dk Slaa alisema kwa kuwa katika hotuba ya waziri mkuu kivuli kwa Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), aliyoitoa bungeni Juni, 2007, alieleza juu ya ubadhirifu mkubwa uliofanywa kwa kutumia makampuni ya Meremeta na Tangold.

Dk Slaa alifafanua kwamba ubadhirifu huo ulibainika kwenye Makampuni ya Mwananchi na Deep Green Finance Co, ambao kiasi kinachodaiwa kufanyiwa ufisadi ni zaidi ya Sh215 bilioni.

Alihoji: “Ni lini kampuni hizo zitafanyiwa ukaguzi maalumu kama ilivyofanyika kwa Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) ili kubaini ubadhirifu huo uliohusisha uhamisho wa fedha kutoka Benki Kuu (BoT) na vyombo vya umma kupitia NBC Corporate Branch DSM na Ned Bank ya Afrika Kusini.

Akizungumzia majibu hayo ya serikali, mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe alisema serikali imepotoka.Zitto alisema CAG anawajibika kwa bunge na si serikali kwa kuwa ndiyo inayokaguliwa. "Serikali ndiyo inakaguliwa na CAG, huyo waziri kakosea kusema serikali haijaamua kufanya ukaguzi huo," alifafanua Zitto.

Zitto aliongeza kuwa kauli hiyo ya waziri ni sawa na kutangaza kujiingiza katika mgogoro na bunge kwa kuwa CAG anafanya kazi kwa niaba ya bunge.Utata mkubwa uliopo Meremeta ambayo inamiliki mgodi wa dhahabu wa Buhemba, pamoja na tuhuma za ufisadi ni utata wa wanahisa.Wakati serikali ikisema kampuni hiyo inahusu masuala ya ulinzi na usalama wa nchi, ndani yake kuna wanahisa ambao ni kampuni ya Uingereza ya British Law Associate.


CHANZO: Mwananchi

22 Jun 2009


Katika MAKALA HII nilionyesha wasiwasi wangu kuhusu hatua ya Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo kutangaza kufutwa kwa misamaha ya kodi kwa taasisi za dini.Katika makala hiyo,nilieleza hivi (najinukuu)

Lakini binafsi natafsiri kuwa hatua hii ina ajenda mbalimbali zilizofichika
ikiwa ni pamoja na kuonyeshana nani mwenye nguvu zaidi: mamlaka za kidunia au za kiroho.Usisahau kauli za hivi karibuni kutoka kwa madhehebu mbalimbali ya Kikristo kwamba mafisadi wameteka nchi....na kuandaa mkakati wa kupata viongozi bora katika uchaguzi mkuu wa 2010.
Toleo la leo la gazeti la Majira lina habari inayothibitisha hypothesis hiyo.Kwa mujibu wa gazeti hilo,kauli zilizoikera Serikali hadi kufikia hatua ya kutoa "kibano" hicho ni pamoja na ile ya Kanisa Katoliki kuanzisha program maalum ya kuelimisha waumini wake kuhusu masuala mbalimbali ya demokrasiapamoja na namna ya kuchagua viongozi bora.

Kwa mujibu wa Majira,kauli nyingine ni ile iliyotolewa na na Jumuiya ya Kikristo Tanzania kwenye Mkutano wake mjini Dodoma ambapo ulitolewa wito kwa waumini wa madhehebu hayo kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu hapo mwakani.




Picha ya gazeti la Majira kwa Hisani ya KENNEDY.

Najiuliza,hivi hapa nimejisifu au nimejipongeza?


20 Jun 2009


Ahadi tupu za kiwete zaelekea kutengeneza kitanzi cha CCM 2010

Na Mwandishi Wetu

IKIWA imesalia takriban miezi 18 kabla ya Uchaguzi Mkuu Oktoba mwakani, sasa ni dhahiri kuwa Rais Jakaya Kikwete ana kibarua kigumu cha kukamilisha ahadi lukuki alizotoa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.

Mazingira hayo pia yanawaweka njiapanda wabunge wengi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika kutetea tena nafasi zao.

Baadhi ya wabunge tayari wameliona hilo na miongoni wamelisema bungeni wakiwashutumu mawaziri ambao wamekuwa wakilimbikiza miradi ya maendeleo kwa upendeleo kwenye maeneo yao bila kuzingatia vipaumbele vya taifa, hata baadhi yao walifikia hatua ya kutishia kukwamisha bajeti iliyopitishwa Alhamisi iliyopita.

Kauli kali zaidi ilitoka kwa Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii aliyeomba dua kwa Mungu awalaami mawaziri hao.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa, ahadi kadhaa alizozitoa Rais Kikwete bado hazijatekelezwa na kwa kipindi kilichosalia ni vigumu kufanya hivyo.

Miongoni mwa ahadi alizotoa Rais Kikwete na hazijaonekana matunda yake dhahiri ni zile zilizoandamana na kaulimbiu yake ya Ari Mpya, Nguvu Mpya, Kasi Mpya na mpango wa ‘Maisha bora kwa kila Mtanzania’.

Kigogo mmoja ndani ya CCM amelieleza gazeti hili kwamba ahadi hiyo ya maisha bora ndiyo ilimpatia Kikwete kura za kishindo na isipotengenezewa mkakati maalumu inaweza kuwa ndio kitanzi chake na wabunge wengi wa CCM.

Alisema ahadi hiyo imesababisha baadhi ya vigogo wa chama na serikali kubadili kauli, na kusema kwamba maisha bora hayatawafuata wananchi kama hawafanyi kazi kwa bidii.

Kwa mujibu wa watu mbalimbali waliozungumza na Mwananchi Jumapili, na hata kauli za wabunge wanapochangia bungeni, Watanzania walio wengi bado wana hali duni ya kimaisha, jambo ambalo litakuwa gumu kulieleza kwa wapigakura hapo mwakani.

Kutokana na ahadi hiyo serikali ilitoa Sh30 bilioni ambazo zilipewa jina la mabilioni ya Kikwete, lakini hazikufika kwa maskini walio wengi kutokana na masharti yake kuwa magumu, na kuangukia kwenye mikono ya wasio wajasiriamali wadogo, hivyo kukwamisha mpango huo wa rais.

Ahadi nyingine zinazoelekea kushindikana ni ya mwafaka wa kisiasa wa Zanzibar ambao Rais Kikwete aliuweka kwenye kipaumbele, lakini hadi sasa hakuna mafanikio yoyote na tayari Chama cha Wananchi (CUF), kimetangaza kujitoa katika mazungumzo.

Ahadi nyingine ni ujenzi wa madaraja ya Kilombero mkoani Morogoro na Kigamboni, jijini Dar es Salaam ni miongoni mwa ahadi kubwa alizotoa Kikwete na hadi sasa hakuna dalili zinazoweza kuashiria kuwa ipo nia ya utekelezaji.

Hata hivyo, Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawambwa alipoulizwa alisema kwamba daraja la Kilombero limetengewa fedha katika bajeti ya mwaka 2009/10.

Kuhusu daraja la Kigamboni, alirudia kauli za muda mrefu kuwa hilo limo kwenye mkakati wa kuanza kujengwa wakati wowote chini ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali.

Ahadi nyingine ambazo hazijatekelezwa, zimeelezwa kuwa ni kilio cha mahakama nchini juu ya suala la masilahi ya watumishi na vifaa vya kazi.

Hivi karibuni, Jaji Mkuu, Augustino Ramadhan alisikika akilalamika kuwa kiwango cha mafungu yanayoahidiwa kutengwa kwa mahakama hufika kwao kikiwa pungufu.

Suala jingine limeelezwa kuwa ni uboreshaji wa mashirika ya umma ambayo bado yako mikononi mwa serikali, lakini kila kukicha yamekuwa na matatizo na kuzua malalamiko mengi.

Kwa upande wa barabara ambazo ziliahidiwa kujengwa kwa kiwango cha lami na ambazo bado ni Tabora-Nzega, Bunda-Ukerewe na Marangu-Mkuu Rombo-Tarakea-Kamwanga.

Aliahidi pia kulifanya jimbo la Rorya mkoani Mara kuwa wilaya, lakini utekelezaji wake umekuwa ukisuasua.

Mambo mengine ilikuwa ni kupambana na rushwa, lakini pamoja na hali hiyo kuonekana kuzaa matunda kwa mambo mengi yaliyokuwa yamejificha kuchimbuliwa na kuwekwa hadharani, malalamiko yanayoibuka ni baadhi ya watuhumiwa kutofikishwa mahakamani.

Rais Kikwete pia aliahidi kuondoa kero nyingi za Muungano lakini licha ya kuunda kamati ya kuzijadili na kuzishughulikia chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais, zipo dalili za baadhi ya wananchi kutoridhika.

Tatizo kubwa linalojitokeza ni baadhi ya Wazanzibari, wakiwamo viongozi wa SMZ kutoa kauli zinazoonyesha dalili za waziwazi kwamba wanadhulumiwa ndani ya Muungano.

Pamoja na hali hiyo, Rais Kikwete atajivunia kwa kutekeleza ahadi yake ya kulifanya Bunge kuwa huru kwani limeonyesha dhahiri kuwa na meno kwa kufichua udhaifu wa baadhi ya vigogo serikali bila kuwa na woga.

Ameonyesha mafanikio pia katika ahadi yake ya kuendesha dola kwa misingi ya utawala bora na uwajibikaji; utawala wa sheria unaoheshimu na kulinda haki za binadamu.

Hata hivyo, katika kipengele hicho kuna manung’uniko kadhaa kama vile baadhi ya viongozi wanaotuhumiwa kuendelea na nyadhifa zao wakati taratibu za utumishi wa umma ziko wazi kwamba wangepaswa kusimamishwa au kupewa likizo ama kuhamishiwa sehemu nyingine, ili uchunguzi huru ufanyike.

Mafanikio mengine ni kutekeleza ahadi ya kuongeza nafasi za elimu ya juu baada ya kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dodoma.

Ahadi nyingine ambayo Rais Kikwete ameonekana wazi kuivalia njuga ni kuboresha kilimo; na tayari mikakati kadhaa ikiwepo ya pembejeo za kilimo imewekwa, ingawa kuna malalamiko ya pembejeo kutofika kwa wakulima na wakulima wa karafuu na kahawa kutokuwa huru kutafuta masoko yao nje ya nchi.

Nguvu kubwa ya serikali yake kuielekeza kwenye kilimo imechagizwa na mtikisiko wa uchumi duniani ambao umetishia uchumi wa nchi nyingi hasa maskini ambazo zinategemea chakula kutoka nje.

Licha ya mafanikio hayo, serikali ya Kikwete inakabiliwa na changamoto kadhaa hasa za wananchi kutoridhika na mambo mbalimbali yanayotendwa na serikali yake.

Lingine ni wananchi kuona kuwa bado serikali ina matumizi makubwa ya fedha na wakati huo huo inawabidi kufunga mkanda ili kuihudumia huku wakikabiliwa na mazingira magumu ya kipato.

Malalamiko mengine ni baadhi ya watendaji serikalini kuendelea kutumia magari ya kifahari na kutenga Sh19 bilioni kwa ajili ya chai maofisini.

CHANZO: Mwananchi


Orodha ya wabunge bubu bungeni yawekwa hadharani

Na Leon Bahati

WAKATI tukielekea mwaka wa lala salama wa Bunge la mwaka 2005-2010, huku baadhi ya wabunge wakiibuka mashujaa kwa kutoa michango mizito inayoitingisha serikali, imebainika kuwa baadhi yao hadi sasa hawajawahi kuuliza hata swali moja wala kuchangia.

Uchunguzi huo umefanywa na Mwananchi Jumapili kwa msaada wa tovuti ya bunge ambako kila mchango wa mbunge hurekodiwa kwa kuonyesha swali la msingi au la nyongeza alilouliza, majibu yake na mchango aliotoa.

Kati ya wabunge 319 walioko katika Bunge la sasa ambao hawajawahi kuuliza maswali ya msingi wanakadiriwa kufikia 50 na wasiouliza maswali ya msingi wala nyongeza ni zaidi ya 30.

Mawaziri na wabunge ambao pia ni wakuu wa mikoa, hawajahusishwa kwenye hesabu hizo kwa sababu wapo upande wa serikali na wote wamekuwa hawaulizi maswali. Wengine ambao hawakuhusishwa kwenye vipengele hivyo ni Spika na Naibu Spika, lakini wote wameonyeshwa kuwahi kuchangia hoja mbalimbali.

Kwa mujibu wa mtandao huo, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz ndiye pekee ameonyeshwa kuwa hajawahi kuuliza swali lolote wala kuchangia jambo lolote tangu Bunge limeanza.

Wabunge wengine ambao wameonyeshwa hawajawahi kuuliza maswali, lakini wamekuwa wakichangia hoja mbalimbali nao ni Yusuf Makamba (Katibu Mkuu wa CCM); John Shibuda, Harith Mwapachu, Ali Haji Ali, Omar Sheha Musa, Abdallah Sumry, Gideon Cheyo, Juma N’hunga, Nazir Karamagi, Anna Abdalah, Ali Haji Ali, Thomas Mwang’onda, Salum Khamis Salum, Hassan Rajabu Khatibu na Felix Mrema.

Wengine ni Philemon Sarungi, Edward Lowassa, Andrew Chenge, Abdisaalam Issa Khatib, Dk Ibrahim Msabaha, Zakia Meghji, Kingunge Ngombale Mwiru, Salimu Yusufu Mohamed, Salum Ahamed Sadiq, Omar Sheha Mussa, Manju Msambya na Benedict Ole-Nangoro.

Wabunge ambao pia ni wakuu wa mikoa ufanisi wao wa kuchangia bungeni ni mdogo ni Abdul Aziz – Iringa (7); Dk James Msekela – Dodoma (6); Monica Mbega – Kilimanjaro (3); Dk Christine Ishengoma-Ruvuma (4) na William Lukuvi – Dar es Salaam (3). Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba aliwahi kutoa michango bungeni mara mbili tu.

Katika Kundi la wabunge 13 wanaoongoza kwa kuuliza maswali ya msingi linaongozwa na Mgana Msindai (CCM) mwenye maswali 34 na kufuatiwa na William Shellukindo (29); Diana Chilolo (28), Paschal Degera (28), George Lubelege (25), Raphael Mwalyosi (24) na Mhoga Ruhwanya (23).

Wabunge wengine kwenye kundi hilo wana maswali 22 kila mmoja nao ni, James Msalika, Job Ndugai, Zitto Kabwe, Herbert Mtangi, Victor Mwambalaswa na Lucy Owenya.

Wabunge 11 vinara wa kuuliza maswali ya nyongeza ni Dk Wilbrod Slaa (71), Hamad Rashid Mohamed (71), Mgana Msindai (67), Esther Nyawazwa (58), George Lubelege (56), Diana Chilolo (54), Hafidh Ali Tahir (52), Geofrey Zambi (50) na wawili waliofungana kwa kuuliza 49, Jenista Mhagama na John Kilimba (49).

Katika kundi la kutoa michango mbalimbali kwenye vikao vya bunge linaongozwa na Naibu Spika Anne Makinda (495); akifuatiwa na Spika, Samweli Sita (494). Wengine ni Jenister Mhagama (193); Job Ndugai (147); Zitto Kabwe (125); Dk Slaa (106); Andrew Chenge (89); Suzan Lyimo (87); William Shelukindo (77); Geofrey Zambi (73); John Kilimba (69) na mawaziri wawili waliofungana kwa kufikisha michango 67 ambao ni Shamsa Mwangunga, Waziri wa Maliasili na Utalii na Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawambwa.

Mawaziri wengine wanaofuatia ni Dk Mary Nagu (64); Profesa David Mwakyusa (59); William Ngeleja (50); Mwanasheria Mkuu wa Serikali; Johnson Mwanyika (47); Dk Makongoro Mahanga (45); Profesa Jumanne Maghembe (45); Stephen Wasira (41) na John Chiligati (40).

Akizungumzia kuhusu kumbukumbu hizo wiki iliyopita, Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alisema kuwekwa kwa taarifa hizo hakuna maana zaidi ya kuweka kumbukumbu za michango ya wabunge, lakini akasema kulikuwa na marekebisho kwa wakati huo.

Alipotafutwa tena jana, alisema tovuti hiyo ya Bunge imefanyiwa marekebisho makubwa ili wananchi waweze kupata kwa undani kumbukumbu mbalimbali za vikao vya Bunge.

Pamoja na maboresho hayo, Dk Kashililah alisema: "Tuna mpango wa kuongeza maboresho zaidi yakiwepo ya kuwezesha watu kufuatilia vikao vya Bunge kupitia tovuti hiyo."

Licha ya baadhi ya wabunge kuwa na mchango hafifu, Bunge la sasa limeonekana kuwa mwiba mkali kwa viongozi serikalini hususan mawaziri, kutokana na baadhi ya wabunge kuwabana katika mambo mbalimbali ya utendaji mbovu na ufisadi, huku kufupishwa kwake kukipunguza nafasi ya kuuliza maswali na kuchangia kwa baadhi yao ambao walikuwa hawajafanya hivyo.

Katika kipindi hicho miongoni mwa hoja nyingine zilizosisimua ni mjadala wa Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe kuhusu utoaji wa zabuni ya umeme wa dharura iliyotolewa kwa kampuni ya Richmond Development Limited (LLC); na kusababisha Rais Jakaya Kikwete kuvunja baraza la mawaziri baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kujiuzulu pamoja na mawaziri wengine wawili.


CHANZO: Mwananchi

19 Jun 2009


18 Jun 2009



Hivi karibuni watunga sheria (wabunge) wetu watatu "waliungana" kuandika kitabu walichokipa jina "BUNGE LENYE MENO".Ukiangalia sehemu ndogo tu ya wasifu wa wabunge hao utamaizi kuwa "muungano huo wa uandishi" ulikuwa ni mithili ya "ndoa za makaratasi" (marriages of inconvenience).

Dkt Wilbroad Slaa,Spika Samuel Sitta na John Momose Cheyo!Nadhani kitu pekee kinachoweza kuwafanya wafanane ni "wote ni wabunge",and the similarity stops there.Wakati Dkt Slaa amejijengea jina kubwa kama kinara wa mapambano ya ufisadi,ni vigumu kum-define Spika Sitta linapokuja suala la mapambano dhidi ya ufisadi.Lakini si vigumu kukumbuka kuwa ni Sitta huyuhuyu aliyempa kadi nyekundu Zitto Kabwe alipombana ex-waziri Nazir Karamagi kuhusu sakata la Buzwagi.Na ni Sitta huyuhuyu aliyetishia kumshtaki Dkt Slaa alipoibua tuhuma ufisadi ndani ya Benki Kuu akidai kuwa ni ushahidi wa kufoji!Eti leo tunaambiwa Spika huyuhuyu nae ni kinara wa mapambano ya ufisadi!


Tukija kwa John Cheyo,nadhani amebaki kuwa UDP,kwa maana ya one-man party.Sera yake ya mapesa ilijaa utani ambao ungekuwa na maana zaidi kwenye sanaa za maigizo kuliko katika siasa makini.Amebaki kuwa jina tu.Sidhani kama kunamfano wowote hai unaoweza kutumika kumtambulisha Cheyo kama mwanaharakati wa mapambano dhidi ya ufisadi.


Sasa hao ndio waandishi wa kitabu BUNGE LENYE MENO.Lakini kwa vile nafahamu kwamba uchambuzi makini unahitaji kwenda mbali zaidi ya kuangalia personalities,naomba kugeukia hoja yangu ya kupingana na ya akina Sitta kuwa bunge la sasa lina meno.Binafsi nasema kama ni meno basi ni ya plastiki.Nadhani unafahamu mtoto mchanga anapoanza kuota meno huwa yanaota meno ambayo yanaitwa meno kwa vile tu yamekaa sehemu yalipo meno.Ukimnywesha uji wa moto basi kilio chake hapo ni balaa!Ni meno machanga yasiyomudu kutafuna vitu vigumu.


Na ndio bunge letu lilivyo.Utasikia kelele,vitisho,na vitu kama hivyo kila waheshimiwa wanapokutana hapo Dodoma ambapo mwisho wa siku akaunti zao zinaingiza kipato cha zaidi ya mwezi mzima kwa Mtanzania wa kawaida,huku kila mwisho wa mwezi wakiondoka na mamilioni lukuki.Basi angalau kipato chao kingeendana na hali halisi ya uchumi wa nchi yetu.


Wabunge wa CCM,ambao wanatengeneza zaidi ya robo tatu ya bunge letu,ndio vichekesho zaidi.Utamsikia huyu akisema hili kabla ya mwenzie kumkalia kooni akitaka mwongozo wa Spika kwa madai ya "kukiuka kanuni za bunge".Lakini ukifuatilia kwa makini,mara nyingi mwongozo huo huombwa pale anapojitokeza mbunge mmoja kuelezea yale yanayozungumzwa na Watanzania wengi mitaani,kwa mfano ishu ya ufisadi.Sasa kwa vile kuna wabunge wenye deni kubwa zaidi kwa CCM na vigogo wake,njia pekee ya kulipa deni hilo ni kuomba mwongozo wa Spika ili kuwaziba midomo wale wanaoongea yasiyopendeza masikioni mwa watawala.


Majuzi,Mbunge wa Nzega Lukas Selelii amemwomba Mungu awalaani mawaziri kwa madai kwamba wamekuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya ufisadi nchini.Mbunge wa Pangani Mohammed Rished akaomba mwongozo....sijui kuonyesha anafahamu zaidi sheria za Bunge au kwa vile yaliyoongelewa na Selelii hayakumpendeza mbunge Rished.Kwani si kweli kwamba maamuzi mengi yaliyopelekea skandali za ufisadi yalipitishwa na Baraza la Mawaziri?Kabineti ingetimiza wajibu wake tungekuwa na Richmond?au Kiwira?Au TICTS?au Buzwagi?Au IPTL?Orodha ni ndefu.Sasa Rished alihitaji mwongozo kwa vile Selelii kumuomba Mungu awalaani watu waliofanya maamuzi yaliyopelekea ufisadi ni kosa la jinai au?Halafu tunaambiwa tuna "bunge lenye meno"!In this case,haya wala si meno ya plastiki bali ni mapengo kabisa.


Fuatilia kwa karibu mjadala wa Bajeti unavyoendelea huko Dodoma.Kuna kauli za uchungu kutoka kwa baadhi ya wabunge kama Selelii,Mwambalaswa,Mpendazoe na,kama kawaida,wabunge wa upinzani kama vile Dkt Slaa.Lakini kauli pekee hazimsaidii Mtanzania masikini asiyejua hatma ya maisha yake.Kelele hizi zimekuwepo tangu bunge hili linaanza.Ndio,zimesaidia kuundwa kwa kamati mbalimbali kama ile ya Mwakyembe.Lakini kuunda kamati kisha kutofanyia kazi mapendekezo yake ni sawa na ufisadi tu.Ikumbukwe kuwa kamati hizo hutumia mamilioni ya fedha za walipa kodi.Ukubwa wa gaharama za kuendesha kamati za aina hiyo ungeweza kupunguziwa maumivu laiti mapendekezo yanayotolewa yangekuwa yanafanyiwa kazi.Hadi leo wahusika wa Richmond (achana na yule decoy mwenye kesi mahakamani) wanaendelea "kupeta".


Laiti Bunge lingekuwa na meno,isingetosha kwa Lowassa,Msabaha na Karamagi kujiuzulu tu.Walipaswa wakabidhiwe kwa vyombo vya dola.Kadhalika,watendaji wa serikali waliotajwa kuhusika walipaswa kuwajibishwa mara moja.Badala yake,hadithi zimeendelea kila kinapojiri kikao kingine cha bunge,huko waandishi wetu mahiri wa kunukuu wakija na vichwa vya habari kama "Moto kuwaka Bungeni","Ishu ya EPA kuibuliwa tena Bungeni"...Huwezi kuwalaumu sana kwa vile vyombo vya habari vinaendeshwa kibiashara na kichwa cha habari chenye mvuto kinauza gazeti!


Bunge lenye meno lisingekuwa linapigwa danadana na Waziri Ngeleja kuhusu ishu ya Kiwira.Bunge lenye meno lisingekubali mkataba wa TICTS uendelee kuwa hoja ya moto kila kikao lakini inayoishia kuwa ya moto pasipo mabadiliko,only for it kuwa ya moto tena kwenye kikao kingine.Yayumkinika kusema kuwa kama ni moto wa hoja,basi ni wa njiti ya kiberiti kwenye upepo mkali;hudumu kwa sekunde tu.


Sintajadili zaidi kwa vile itakuwa sawa na kupre-empty muswada wa chapisho naloandaa kama mapitio (majibu?) ya kitabu hicho cha wabunge hao.Ila kwa kifupi,si rahisi kuwa na bunge lenye meno wakati wabunge wenyewe wanaishi maisha tofauti na hao wanaopaswa kuwawakilisha bungeni (nikimaanisha maslahi yao).Tusidanganyane,mtu anayelipwa milioni 6 na ushee kwa mwezi hawezi hata chembe kuwa mwakilishi mzuri wa mtu asiye na uhakika wa kukamata angalau shs 10,000 kwa mwezi.Haya ni matabaka mawili tofauti,na japo kinadharia wabunge wanapaswa kuwa sehemu ya tabaka tawaliwa kwa maana ya uwakilishi wa wananchi,maslahi yao makubwa yanawaingiza kwenye tabaka tawala na hivyo kuwaweka kwenye mgongano wa moja kwa moja direct confrontation) na tabaka tawaliwa la wananchi wa kawaida.Katika hali hiyo,serikali kwa maana ya the executive branch of the government,inapata free pass kwani wanaopaswa kuihoji nao wanajikuta wakihojiwa na wanaowawakilisha.Kiuhalisia,mpiga kura is hardly represented bungeni.


Lakini tukiweka kando suala la kipato na matabaka,tatizo la msingi zaidi kwenye bunge hili ni kutanguliza mbele maslahi ya chama badala ya maslahi ya nchi.Umoja na mshikamano ndani ya CCM unatafsiriwa kuwa ni muhimu zaidi kuliko umoja na mshikamano wa kitaifa.Wengi wa wabunge wa CCM wanahofia kuzungumzia baadhi ya masuala yanayolihusu taifa ambayo kwa namna moja au nyingine yanaifanya CCM inyooshewe kidole.Hakuna mbunge wa CCM anayeweza kuzuia bajeti ya wizara flani,hata kama ni mbovu namna gani,kwa vile akifanya hivyo atatafsiriwa kuwa anavunja mshikamano wa chama.Mbunge katika bunge lenye meno hawezi kuogopa tafsiri ya chama chake,bali wapigakura wake.

Kwa anayehitaji nakala ya bure ya kitabu hicho cha BUNGE LENYE MENO (as an ebook),tuwasiliane.

17 Jun 2009


Ni dua pekee linaloweza kubadili viumbe wa aina hii.Sijui ni kujikomba,sijui uhaba wa tafakari au...!!!Soma kwanza stori hii kisha utafakari

Chenge asimikwa utemi

na Sitta Tumma, Magu

MBUNGE wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, ambaye amekuwa akiandamwa na kashfa mbalimbali, ametawazwa kuwa mtemi wa kabila la Wasukuma-Bagole, Kanda ya Itilima, wilayani Bariadi.

Chenge alichaguliwa katika sherehe maarufu za kabila hilo, maarufu kama Bolabo, mwishoni mwa wiki, wilayani hapa, ambazo mbali naviongozi wa kimila, Mkuu wa Mkoa, Abbas Kandoro, alikuwa ni miongoni mwa waliohudhuria.

Baadhi ya watu waliokuwepo kwenye sherehe hizo, waliuelezea utemi wa Chenge kwa mtazamo tofauti, huku baadhi wakidai kaupata ili kuweka mambo yake sawa, na wengine wakidai anastahili kupata nafasi hiyo kwa kuwa ni miongoni mwa watu wa kabila hilo.

Mbunge huyo ambaye alilazimika kujiuzulu nafasi yake ya uwaziri alisema, utemi huo ni karama aliyopewa na Mungu na kwamba wajibu huo ni sawa na daraja la kuunganisha jamii ya kabila husika.

"Utemi niliopewa naweza kusema ni karama iliyotoka kwa Mwenyezi Mungu! Kazi hii ya utemi ni nzito kwa sababu ina masuala yake yanayohusiana na mambo ya kimila pamoja na kuunganisha jamii ya kabila husika," alisema Chenge.




Ndio maana wakati mwingine hawa "wazungu" wanapata wakati mgumu kutuelewa.Hivi inaingia akilini kweli kwa mtuhumiwa wa ufisadi wa zaidi ya shilingi bilioni moja,Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge,kutunikiwa utemi?Watoto wanaozaliwa leo na kesho na kukuta mtemi wao ni miongoni mwa watu waliochuma utajiri kwa njia za miujiza kabisa (fedha alizonazo haziwezi kuwa zimepatikana kwa njia halali,piga ua) watawaelewa kweli wazazi wao?

Mtemi wa nini?Au wanamaanisha utemi wa kuifanya sheria imwogope?Maana kesi yake ya kuua ni vituko vitupu.Mara iundiwe tume,mara iahirishwe kwa hili na lile!Mtu kasababisha ajali huku gari ikiwa na bima iliyoisha muda wake,mnamuundia tume ya nini?Na kwanini hiyo tume iwe kimya kama haikuundwa vile?

Mtuhumiwa huyu wa ufisadi ameendelea pia kuwa kwenye kamati ya maadili ya CCM.Halafu ukisema CCM chama cha kifisadi kuna waungwana wananuna!

Kaaazi kwelikweli

16 Jun 2009

Posing for GQ,Sacha as BRUNO

In Paris at the premiere of his latest movie BRUNO


Red carpet queer style

Cohen's (real-life) other half ISLA FISHER.With Cohen,it seems necessary to state clearly if something about him is real or sheer comedy.


As a Kazakh reporter BORAT.


As a Staines gangsta Ali G (AKA Alistair Leslie Graham)


Ali G: Gangsta or Chav?
PICS FROM The Daily Mail and the Web.




Please copy the sample letter and write to your representatives in the government, asking them not to recognize the presidency of Mr. Ahmadinejad. Please also ask others to do the same.

Dear Sir or Madam:

On June 12, 2009, the Iranian people went to the polls in record numbers to choose the next president of the Islamic Republic of Iran. Only four candidates were allowed to compete: the incumbent President Mahmoud Ahmadinejad, Mir Hussein Mousavi, MehdiKaroubi, and Mohsen Rezaie. The Iranian reform movement was united behind Mr. Mousavi’s
candidacy.

Based on numerous polls carried out a few days before the elections, Mousavi had a commanding lead over Ahmadinejad. Unfortunately, in total disregard for the people’s choice, the interior ministry haphazardly declared Mr. Ahmadinejad the winner, giving him 63.62% of the votes. The absurdity of the government’s election engineering is that none of the candidates managed to get more than a fraction of the votes even in their hometowns! In his birthplace, the village of Lali, Rezaie received fewer than 70 votes of the total of 900 votes cast, while 830 votes went to Ahmadinejad. Likewise, Karoubi did not do much better in his birthplace Aligoudarz, garnering only 14,512 votes, while Ahmadinejad received 39,690 votes. Finally, Mousavi, in his birthplace, Shabstar, was given only 2,000 of the total of 7,000 votes cast, while the rest went to Ahmadinejad.

How could all these candidates get defeated in their own hometowns, while we know that in the past presidential elections, all the candidates got the majority of the votes in their hometowns? Evidently, those who manufactured these figures got their lesson from Nazi propaganda minister Joseph Goebbels that the bigger the lie, the more believable it is. They must have thought that if Ahmadinejad is declared the winner even in his rivals’ hometowns, the Iranian people would believe his victory everywhere.

The unofficial results from the interior ministry tell quite a different story. Accordingly, Mr. Mousavi was the absolute winner with 54% of the votes, followed by Karoubi and Ahmadinejad with 31% and 13% of the votes,respectively.

Given that days before the election the Revolutionary Guards made a scarcely veiled threat to the followers of the reform movement that they will stifle swiftly any attempt at a “velvet revolution,” that a day before the elections the SMS network of mobile users were disconnected in the country, and that the websites belonging to the reformist candidates were filtered—all were indicative of the fact that the regime had staged a political coup. If Ahmadinejad was so popular, why should the Revolutionary Guards be so concerned about an impending velvet revolution? Why should they be compelled to disconnect the SMS network of mobile users?

The Iranian people do not accept the shenanigans engineered by the regime. They are demanding an investigation. They demand an honest and objective counting of the votes. Without their demands being met, the result has no validity.

Please do not recognize the official results of the elections. Please do not recognize the presidency of Mr. Mahmoud Ahmadinejad.

Democracy in Iran means peace in the Middle East. I appreciate your support.

Below are links to more information and report on Iran’s elections.

http://www.nytimes.com/2009/06/15/opinion/15iht-edcohen.html?_r=1&th&emc=th

http://garysick.tumblr.com/

www.truthout.org/061409Z?print

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.